• Anza
  • Iliyopita
  • 12 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 10685 / Pakua: 4474
Kiwango Kiwango Kiwango
UKWELI WA USHIA

UKWELI WA USHIA

Mwandishi:
Swahili

UKWELI WA USHIA

TAMKO LA MUASSASATUR-RASULIL-AKRAM (S.A.W)

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHMA MWENYE KUREHEMU

Sifa zote njema ni za Mwenyezi Mungu Mola wa viumbe wote na sala na salam (rehma na amani) ziwe juu ya muongozaji kwenye njia ya haki na mtoa bishara na taa yenye kuangaza Muhammad na Ahli zake walio watwaharifu. Ama baada, wapinzani na maadui wa madhehebu ya Shia bado wanaendelea kati ya kipindi na kipindi kingine na kazi yao ya kuamsha na kueneza shubha zao na kusambaza maneno yao ya uzushi na yasiyo na ukweli wowote dhidi ya madhehebu ya Ahlul-bayti(a.s) na kwa kufanya hivyo hutarajia ya kuwa huenda wakafanikiwa kuziyumbisha na kuzitia shaka itikadi za watu wenye mustawa mdogo wa kielimu na kuwatoa kwenye itikadi zao za asili.

Lakini ukweli ni kwamba usaidizi wa pekee wa Mwenyezi Mungu mtukufu autoao kwa madhehebu ya haki wakati wote na bila kukoma huwa ni kizingiti na kizuizi kikubwa cha kuyafikia malengo yao hayo.

Pamoja na shubha zote na uzushi wote utolewao na uenezwao dhidi ya Ushia, tunakuta kwamba ukweli na haki daima ni yenye kudhihiri na haifichiki kamwe, na imekuwa ni yenye kudhihiri kupitia mikononi mwa wateule kati ya wafuasi wema ambao wamejitolea nafsi zao kwa ajili ya kuyanusuru madhehebu ya haki ambayo aliyaanzisha Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w .w) tangia kudhihiri na kuchomoza kwa Uislaam.

Na katika uwanja huu kuna vitabu vingi sana vilivyo andikwa na vilivyo madhubuti na vizuri, na kati ya vitabu hivyo ni kitabu kiitwacho (Haqaaiqu ani Shia) kilicho andikwa na mheshimiwa Ayatullahil-udhmaa Sayyid Swadiq Shirazy Mwenyezi (Mungu amrefushie umri) alicho kiandika katika masiku ya ujana wake, na kuthibitisha kwa dalili madhubuti haki na ukweli wa madhehebu ya Ahlul-bayti(a.s) .

Na kitabu hiki kimetofautiana na vitabu vingine na kuvipituka kutokana na umadhubuti pia umakini wa dalili zake na mfumo wake ulio mzuri na madhubuti na mwepesi ambao humfikisha msomaji kwenye kina cha shubha zitolewazo na kubainisha ubatilifu wake kwa njia nyepesi na rahisi na kwa umakini wa hali ya juu kabisa.

Na kauli ya mwisho ni kuwa: Hakika kitabu hiki pamoja na kuwa hajmu yake ni ndogo na ibara zake kuwa nyepesi, ukweli ni kwamba wakati huo huo ni kijitabu chenye faida na chenye undani katika maana, kwa hivyo basi hapana budi na inawapasa waumini wakisome na kukipitia au kuzitwalii bahthi zake na kufaidika na maudhui yake yenye kina na madhubuti, tukimtaraji Mwenyezi Mungu awape tawfiq (awawafikishe) kwa yale ayapendayo na kuyaridhia yeye Muumba subhanah.

1 UKWELI WA USHIA

KUENEZA ITIKADI YA USHIA NI FURSA YA THAMANI SANA KATIKA UMRI WA MTU

YAPANGENI VEMA MAMBO YENU NA WALA MSIYAACHE HORERA [1]

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHMA MWENYE KUREHEMU.

Sifa zote njema zinamstahiki Mola wa viumbe wote na sala na salam ziwe juu ya bwana wetu Muhammad na Aali zake walio watwaharifu, na laana ya Mwenyezi Mungu iwe juu ya maadui zao wote hadi kitakapo simama kiama.(Mlivyonavyo vitakwisha na vilivyoko kwa Mwenyeezi Mungu ndivyo vitakavyo bakia) [2]

Aya hii ni miongoni mwa aya nyingi za kitabu kitukufu cha Allah na maana yake ni kuwa kila mlicho nacho ni chenye kutoweka na kumalizika bila shaka yoyote, na yaliyoko kwa Mwenyezi Mungu ni yenye kubakia milele. Kwa hakika katika usiku huu mmetekeleza na kusali sala mbili Maghribi na Isha, na Shekh Tusy (Radhi za Allah ziwe juu yake) alifariki na kuiaga dunia kabla ya zaidi y miaka elfu moja iliyo pita, lakini sehemu fulani ya thawabu za sala ya Magharibi na Isha mlizo zisali na kuzitekeleza ataandikiwa yeye, kwa sababu yeye alikuwa ni sababu ya kusaliwa sala hizi, kwani mas'ala mengi, pia Hadithi nyingi zilizo tufikia sisi zimetufikia kupitia kwake na kutokana na juhudi zake,Na mwenye kuwaongoza watu kwenye kheri ni kama mfanyaji wa kheri hiyo (katika thawabu)

Ni watu wangapi walio fanikiwa kusali katika usiku huu wa leo?! Bila shaka yoyote ni mamilioni kadhaa, sasa angalieni kiasi cha thawabu ambazo atazipata Shekh Swaduq kutokana na sala hizi pekee. Si vibaya kueleza kuwa Marhum Shekh Tusy alikuwa na ndugu ambae alifahamika kwa wema wake na kwamba alikuwa ni mtu alie shikamana na dini vema, lakini ndugu yake huyo hakutuachia athari yoyote,(kumbukumbu yoyote) na wote wawili walikuwa ni watoto wa baba mmoja na wakiishi wakati mmoja, lakini mamilioni haya ya thawabu yanamfikia Shekh Tusy kila siku wakati ambapo ndugu yake hapati thawabu hizo, kwa sababu hakuacha athari wala chembe yeyote katika dunia kama alizo ziacha ndugu yake wa tumbo moja.

Na jaribuni kuangalia(fanyeni Taswawwur) ya kuwa baada ya miaka elfu moja tokea sasa ni nani utajo wake utabakia na nani atasahaulika na kuto kumbukwa kabisa, kwa hivyo basi nyinyi mnaweza hivi sasa kufanya mambo au matendo ambayo yatakuwa ndio sababu ya kubakia utajo wenu na mkawa ni wenye kukumbukwa kwa muda wa maelfu kadhaa ya miaka na mkajipatia thawabu zisizo koma na kumalizika na zenye kuendelea milele na bila kukatika.

Kwa hakika Mwenyezi Mungu alikadiria kuwa nchi ya India ibadilike na yote kugeuka na kuwa nchi ya Kiislaam, (yaani watu wake wote wabadilike na kuwa Waislaam), katika siku za usoni, na vizazi vyote vijavyo visilimu, vizazi vitokanavyo na waabudu masanamu, kama vile wenye kuabudu Ng'ombe, panya na wenye kuabudu jua. Kwa mfano kabla ya miaka mia moja iliyopita nchi ya Iran yote ilikuwa ni nchi ya kikafiri na baada ya miaka mia moja ili badilika yote na wakazi wake wote wakawa ni Waislaam wa madhehebu ya sunni, kisha wananchi wake wakaongoka na wengi wao au asilimia kubwa kati yao hivi leo wakawa ni wafuasi wa Madhehebu ya Ahlul-bayti(a.s) , na haya ndio yatakayo tokea katika nchi ya India vilevile, kwa utashi wake Allah.

Na hapa linajitokeza swali moja nalo ni kuwa: Baada ya miaka kadhaa, ni ipi nafasi yenu na dauru lenu katika mabadiliko hayo yatakayo tokea?! Inasemekana kuwa katika nchi ya India kuna zaidi ya watu milioni 600 wenye kuabudu masanamu, sasa ikiwa mmoja wenu atachukua jukumu la kusoma vizuri kitabu kitukufu cha watu wenye kuabudu masanamu kisha baada ya kufanya hivyo akachukua jukumu la kukusanya vijana na mabarobaro ambao ni watoto wa wenye kuabudu masanamu katika nchi ya India na akawafafanulia yaliyomo kwenye kitabu chao kitukufu na akawatolea mihadhara, pia akawakusanya wanafunzi wa vyuo vikuu na walimu, pia wasomi, wabunge, mawaziri na watawala kwa kutumia mantiki ya akili na akasema: Je nyinyi mmekinaika na mafundisho haya yaliyomo kwenye kitabu chenu kitakasifu?!

Na je mnafahamu ya kuwa mambo haya ya kutunga ni sehemu moja wapo ya itikadi yenu ya dini?! Niswadikisheni ya kuwa mmoja wenu anaweza kwa kufanya hivi kuziyumbisha Imani za maelfu miongoni mwao. Nitakutajieni baadhi ya mifano hai kati ya mambo yaliyomo kwenye kitabu chao kitakatifu, na kati ya hayo ni kuwa:Ikiwa mwanamume ataoa mwanamke na baada ya muda mrefu mwanamke yule asifanikiwe kuzaa au asimzalie mtoto na baada ya kuonana na madaktari na kumsisitizia au kumthibitishia ya kuwa mwanamume hana kizazi yaani ni tasa, inajuzu kwa mwanamke yule kulala na ndugu wa kiume wa mumewe ili aweze kupata mtoto mmoja tu na si zaidi, na mtoto yule hunasibishwa na kuambatanishwa na mumewe! Na jambo hili ni lenye kupingwa na nafsi ya kila kiumbe na ghera (wivu) inapinga kitu kama hicho, pia elimu inapinga kitu kama hicho.

Na katika mahala pengine kitabu hicho kitakatifu kina sema: Wakati mwingine hutokea mwanadamu kubadilika na kuwa Mungu kiasi kwamba yeye mwenyewe hahisii hivyo au bila ya yeye kuhisia! Na jambo hili ni jambo la batili na lisilo na maana yoyote kwa kiwango kikubwa.

Hakika kitabu chao hiki kimejawa na mambo ya kutunga na ya batili na ngano zisizo na maana, na anaweza mmoja wenu kuyafuatilia kwa karibu zaidi na kujua idadi yake na kuyaeleza wazi wazi bila kutumia matusi na kejeli. Kwa hivyo basi mas'ala muhimu kabisa katika dunia ni kuwaongoza viumbe, na Mtume(s.a.w.w) alimwambia Imam Amiril-muuminiin(a.s) :Ewe Ali ikiwa Mwenyezi Mungu alie takasika atamuongoza mtu mmoja kupitia kwako ni bora kwako (ni kheri kwako) kuliko vitu vyote vichomozewavyo na jua (vipatavyo mwanga wa jua) .[3]

Na ninakunukulieni kisa kingine, Imepokelewa katika moja wapo kati ya kitabu cha historia nacho ni (Atharul-bilaad wa Akhbaarul-ibaad) ya kuwa mtawala mmoja wa kisunni aliekuwa akitawala Iran alitengeneza muhuri wa chuma na akachonga kwenye muhuri huo Ibara hii (Abubakar wa Omar) na alikuwa akiwaonea na kuwadhulumu Mashia na akiwatawala kwa mabavu pia alikuwa akiwapiga muhuri huo kwenye mapaji ya nyuso zao baada ya kuuchemsha kwa moto, na kitabu hicho kinasimulia ya kuwa baadhi ya Mashia ambao walipigwa mhuri huo kwenye mapaji ya nyuso zao walikuwa hawatoki majumbani mwao kwa muda wote wa maisha yao na hawakutoka wala kuyahama majumba yao kutokana na aibu ya ibara hiyo kwa ndugu zao waumini ambao ni Mashia, na wakihofia masunni wasijekoge kupitia kwao.

Hebu jaribuni kuangalia na kuifikiria hali na mazingira magumu kama hayo wakati huo, lakini pamoja na yote hayo na mazingira hayo magumu na maonevu kama hayo, ugumu wa mazingira kama huu wa hali ya juu, Mashia walikuwa wakisindikiza majeneza ya masunni, hadi hivi leo Iran ikawa ni yenye itikadi ya Ushia, kwani mateso na maonevu yale hayakuwazuia kutekeleza majukumu yao bali waliendelea na juhudi za kuwaongoza waja na likathibiti na kuwa lile walilo litaka.

Na hapana shaka ya kuwa nyinyi nyote mmesikia jina la Allamah Al-majlisiy, kwa hakika alikuwa ni mwanazuoni mkubwa, na baba yake alikuwa ni miongoni mwa maulamaa wakubwa pia, na katika kizazi chake Allamah Al-majlisiy ambae tangu kufariki kwake hadi sasa kumepita miaka 300 walijitokeza wanazuoni na maulamaa wengi na marajiut- taqlidi na waandishi wa vitabu wakubwa na watoa mawaidha kwa watu, illa tunakuta kuwa babu wa juu kabisa wa Allamah alikuwa ni mfuasi wa madhehebu ya sunni, na vijana wa kishia wa Isfahani waliweza kumkinaisha na yeye kuamua kujiunga na madhehebu ya Shia, pamoja na kuwa zama zile zilikuwa na taasubi kubwa kabisa ya kimadhehebu, lakini ukweli ni kuwa vijana wale walikuwa na hima ya hali ya juu na wakaweza kuwafanya mashia vijana wengine wa kisunni. Nanyi ni juu yenu kufanya kama walivyo fanya waumini na wapigana jihadi hao, na ni wajibu juu yenu kwa ajili ya kulifikia na kulithibitisha lengo hilo au malengo hayo, kwanza kabisa mjifunze vema na muwe ni miongoni mwa maulamaa wakubwa ili muweze kufanya mahojiano na majadiliano na kuwakinaisha.

Na sikilizeni kisa hiki ambacho kilitokea kabla ya miaka arobaini iliyo pita. Wakati huo tulikuwa Karbalaa, jarida moja la wakati huo liliandika ya kuwa mwanazuini mmoja wa kisunni amekuwa Shia, na walipo muuliza kwa nini umebadilisha madhehebu yako? Akasema: Nimebadilisha kwa sababu ya herufi moja kati ya herufi za jarri iliyotajwa katika Qur'an tukufu! Wakamuuliza ni herufi ipi hiyo?

Akawajibu: Hakika mimi nimesoma Qur'ani mara nyingi sana na mara ya mwisho suratul-fatiha ikanifanya nisite na kusimama katika aya ya mwisho ya sura hiyo, na nilipo anza kusoma suratu (Inna fatahnaa laka fathan mubiinaa) hadi nikafika mwisho wa surat (Muhammad rasulullah walladhina maahu.) na ambayo inamaanisha maswahaba wa Mtume rehma na amani ziwe juu yake, na kuona ya kuwa sura inawazungumzia maswahaba wa Mtume na imewataja mara kumi kwa swigha ya jam'u (mfumo wa wingi) au kwa dhamiri za wingi ambazo d hamiri hizo zinawakusudia wao, lakini sura hiyo inapozungumzia ya kuwa malipo na jazaa zao walizo ahidiwa kuwa ni pepo na msamaha na malipo makubwa inasema:(Mwenyezi Mungu amewaahidi wale ambao wameamini na wa kafanya amali njema miongoni mwao)

Kwa hivyo basi herufi ya (Mim) inamaana ya (Baadhi), na herufi hii ilinifanya nifikirie na kujiuliza: Kwa nini Maswahaba wote hawaingii peponi kama tulivyo fundishwa?

Nikajisemea moyoni mwangu: Niwajibu niende na kufanya utafiti na udadisi kuhusu suala hili, na jambo hilo likanipa picha ya kuwa inawezekana suala hili likawa ni miongoni mwa mifumo ya Qur'an, lakini mimi nimeiona aya hii na kuikuta ikiwa wazi kabisa kwani herufi hiyo inamaana ya (Baadhi) ya (Maswahaba) na (sio wote) laa sivyo hakika Qur'an imewataja wote katika aya nyingi tofauti na katika aya hii, kwa hivyo nadharia ya uadilifu wa Maswahaba ikiwa imetenguka kwangu, na utafiti wangu ukanifikisha katika natija hii ya kuwa hawa (Baadhi) ya walio tajwa ni wafuasi wa Ali bin Abi Twalib (a.s) na wale walio shikamana na wilaya (utawala) yake na kutokana na utafiti huo nikawa Shia.

Kwa hivyo basi ni juu yenu kuyaandaa vema mambo yenu, na fanyeni juhudi kubwa na wala msipoteze fursa hii ya umri wenu, na someni vizuri na mtwalii sana (someni sana vitabu mbali mbali) mpaka muwe ni miongoni mwa watu wenye elimu, kwani watu wa batili hawana elimu na kila walicho nacho ni njozi za mashetani.

Imam Swaadiq (a.s) amesema: Ni juu yako kuwa na vijana (wenye umri mdogo) hakika wao ni wepesi sana kuelekea kwenye kila la kheri[4]

Na Al-ahdaath walo tajwa kwenye hadithi ni kizazi kipya, kwani vijana bado akili zao hazija oshwa, na wao ni wepesi zaidi katika kufanya kheri kuliko wengine. Kwa hivyo fanyeni harakati na nashati ili India na ulimwengu wote wawe ni Mashia watupu..insha allah.

2 UKWELI WA USHIA

WAOKOENI WATU KUTOKANA NA UJINGA UPOTOVU NA DHULMA KAMA IMAM HUSEIN (A.S) ALIVYO WAOKOA [5]

MANENO YA MHESHIMIWA AYA TULLAHIL-UDHMAA IMAM SAYYID SWADIQ SHIRAZIY (Mungu amzidishie umri) ALIYO YATOA KWA MNASABA WA KUMBUKUMBU ZA ASHURA SIKU ALIYO UWAWA SHAHIDI SAYYID SHUHADAA IMAM HUSEIN (A.S)

Kwa jina la Mwenyezi Mungu mwingi wa rehma mwenye kurehemu. Sifa zote njema na himidi ni za Mola wa viumbe wote na sala na salam ziwe juu ya Mtume wake alie muaminifu Muhammad(s.a.w.w) na Aali zake watwaharifu na laana iwe juu ya maadui zao wote. Ama baada, hakika Mwenyezi Mungu alie takasika alitaka kwa kufa shahidi Imam Hussein (a.s) kuweka mazingatio, kilio, ibra na kigezo kizuri, si kwa kizazi kilicho fuatia baada yake pekee, bali hata kwa Mitume na Manabii(a.s) ambao Imam Hussein alikuja baada yao(a.s).

Ama kuhusu mazingatio na kilio, kwa hakika alianza kutekeleza mambo hayo Muumba wa viumbe pale alipo muumba Adam(a.s) kwani Jibrilu alimtajia(a.s) watwaharifu watano ambao ni Muhammad, Ali, Fatima, Hassan, Hussein(a.s) na Adam akamwambia: Nina nini mimi kila ninapo mkumbuka Hussein macho yangu hutokwa na machozi, kisha kuamsha huzuni na majonzi yangu, na Mwenyezi Mungu mtukufu akamuambatanisha pamoja na manabii katika visa vyao kupita kwao katika ardhi tukufu ya Karbalaa na matatizo waliyo kumbana nayo katika ardhi hiyo, na hali hiyo ikaendelea katika muda wote mpaka Imam Hussein aliposema(a.s)

(Mimi ni muuliwa mwenye Ibra (mazingatio) hanikumbuki muumini yeyote isipokuwa hulia). Ama kuwa kwake ni mazingatio na kigezo, kwa hakika Imam Swadiq(a.s) aliashiria katika ziyara yake aliyo msomea babu yake Hussein(a.s) siku ya kumbukumbu ya Arobaini ya Imam Hussein huku akimzungumzia Mwenyezi Mungu mtukufu kwa kumuashiria Hussein(a.s) : Na akajitolea damu yake katika njia yako ili awaokoe waja wako kutoka katika ujinga na utata wa upotovu (njia ya upotovu).

Na waja hapa: Haimaanishi kikundi fulani, au umma fulani, au kizazi fulani. Na Kuokoa: Ni kuashiria kwenye mambo waliyo tihaniwa nayo watu wale. Na bado mtihani huo upo. Kama kutumbukia katika mabalaa ya aina tofauti na mambo ya kila aina ambayo msingi wake ni ujinga na upotovu. Na Kubabaika: Ambako kumewakumba watu wengi katika mwendo mzima wa maisha yao na mwisho wao (yaani akhera yao). Hizi ndio nukta ambazo zinaunda sehemu fulani kati ya malengo ya Imam Hussein(a.s) katika kauli zake na matendo yake katika historia ya Ashura.

Ni uzuri ulioje kwa waumini kila mahala walipo na kila mmoja wao kusimama na kutekekeza jambo hilo la kheri katika nyanja mbali mbali. Na kufanya awezalo kulifanya kama kufanya maandalizi ya kuwafikishia walimwengu wote habari zihusianazo na upande wa kufanya mazingatio na kulia kwa ajili ya Imam, kwa kufanya majlisi ya kumbukumbu za kufa shahidi kwa Imam Husein na kudhihirisha alama na shiari za Imam Hussein ambazo ndio kitu cha kuendeleza na kudhihirisha alama na shiari za Mwenyezi Mungu alie takasika, na kwa hakika Qur'an tukufu amelisifia jambo hili kuwa ni katika uchaji wa Mwenyezi Mungu

Na haya ndio ambayo yaliifanya hali ya kulia kwa mfazaiko kusiko kwa kisheria na kuliko kemewa kisheria katika misiba yote, liwe ni jambo lenye kusifika na kuamrishwa kulifanya na kupewa malipo juu ya jambo hilo ikiwa litafanyika kwa ajili ya Ashura, na katika njia ya bwana wa mashahidi Imam Husein(a.s).

Na haya ndio mazingatio na kilio vitu viwili ambavyo vimekuwa mutawaatir na mashuhuri na kupokelewa kwa wingi kutoka kwa Watu wa nyumba ya utume na ujumbe wa Allah (a.s) hadi macho yao yakapatwa na vidonda, na kuhusiana na hilo Imam Ridhaa(a.s) amesema katika hadithi iliyo pokelewa kutoka kwake na Rayyaan bin Shabiib ya kuwa:

(Hakika siku ya Husein Imeyatia vidonda macho yetu)([6] ) . Na haya ndio yaliyo sababisha kutokwa machozi macho yale matwaharifu ya walii mtukufu wa Mwenyezi Mungu Imam Mahdi mwenye kusubiriwa (rehma za Mwenyezi Mungu zowe juu yake na Mwenyezi Mungu aharakishe kudhihiri kwake na faraja yake tukufu) kama ilivyo pokelewa katika ziara ya (An-nahiyatul-muqaddasa):

(Na kwa hakika nitakulili damu badala ya machozi). Na kuhusu mazingatio na kigezo, mambo ambayo Imam Husein(a.s) aliyatangaza na kuyadhihirisha mara kadhaa wa kadhaa tangu alipotoka katika mjiwa wa babu yake Mtume wa Mwenyezi Mungu na kuyarudia katika mji mtukufu wa Makka, na katika muda wote alipokuwa njiani akielekea Karbalaa tukufu, na katika Karbalaa, na katika Usiku wa Ashura, na siku ya Ashura, katika hotuba yake barua zake na maneno yake mbali mbali, na kupitia muamala wake katika mwendo huu wa ushindi, na mazingatio yale ni kusimama kidete kwa kufanya juhudi kubwa kwa ajili ya kuwatenga pia kuwaepusha watu wote na ujinga na upotovu.

Na haliwezi kuthibitika hilo isipokuwa kwa kufanya juhudi kubwa na kuwa na ikhlaas kwa ajili ya Mwenyezi Mungu alie takasika. Na kujitolea muhanga kwa kiwango kikubwa na cha hali ya juu katika njia ya kuwaelimisha watu na waja wa Mwenyezi Mungu mtukufu, na kuieneza nuru ya Ahlul bayti(a.s) kila upande na kila mahala na katika kila mji na kijiji, na katika kila nyumba na vibanda vya makuti, na kuifikisha kwa kila mtu wanamume kwa wanamke, mabinti kwa vijana.

Na kutekeleza mfumo na mwenendo wa Imam Husein(a.s) katika kuitumia Ashura kwa ajili ya kuwaokoa waja wa Mwenyezi Mungu mtukufu kutokana na dhuluma na mauaji yaliyopo katika zama hizi, umwagaji wa damu, na kuonekana kuwa ni kikundi kidogo chenye kufuata batili na kuadhibiwa, na kudharauliwa kwa mambo matukufu ambayo watu wengi katika siku hizi wamekuwa wakiyavunjia heshima yake, na hasa hasa waislaam katika sehemu tofauti za Ardhi hii.

Na kwa ajili ya kueneza misingi ya Uislaam na matawi yake. Kupitia vyombo vyote vya habari na tabligh. Katika nyanja mbali mbali za maisha. Na Mwenyezi Mungu ndie mwenye kuombwa msaada awawafikishe wote kupata mazingatio haya na kigezo hiki, na awawafikishe kupata mazingatio pia kutokwa na machozi, nae ndie mwenye kutegemewa.

3 UKWELI WA USHIA

SISI SI KATIKA MASHIA WA ALI (A.S) IKIWA HATUKUZIHESABIA NAFSI ZETU KILA SIKU [7]

MIONGONI MWA MANENO YA MHESHIMIWA AYATULLAHIL-UDHMAA SAYYID SWADIQ SHIRAZIY(Mwenyezi Mungu amzidishie umri)

Hakika Amirul-muuminiin Imam Ali bin Abi Twalib(rehma za Allah ziwe juu yake) alikuwa na orodha ya majina ya watu fulani wanaume kwa wanawake na orodha hiyo ikiwa imeandikwa juu yake (Si katika sisi), na kwa hakika Amirul-muuminiin aliwasifia na kuwaelezea watu hao ya kuwa watu hao ni miongoni mwa watu ambao hawakuzihesabia nafsi zao na wala hawakuya angalia matendo yao).

Kwa hivyo basi muumini yeyote akitaka asiwe katika hawa ni juu yake kila usiku unapo ingia aweke angalau dakika tano maalum, na katika dakika hizo ayarejee matendo yake yote aliyo yatenda katika siku ile, je yalikuwa ni matendo mazuri ? na akiyakuta matendo yake aliyo yatenda ni mazuri basi amshukuru Mwenyezi Mungu alie takasika juu ya hilo, na ikiwa matendo yake ni mabaya, basi amuombe Mwenyezi Mungu alie takasika msamaha na aazimie ya kuwa hatorudia tena kufanya matendo hayo.Kwani Imam Kaadhim(a.s) anasema:

(Si katika sisi mtu ambae haihesabii nafsi yake katika kila siku, akifanya mema humuomba Mwenyezi Mungu amuwafikishe kutenda mema zaidi, na akifanya maovu humuomba Mwenyezi Mungu msamaha kutokana na maovu hayo na kurejea kwake)[8] .

Hakika kila mtu anatabia maalum na ana matakwa maalum, kwa hivyo maisha yanapo mzonga na matatizo ya kimaisha kumtatiza, basi tabia yake hubadilika na kuwa mbaya, kwa hivyo Qur'ani tukufu na Ahlul-bayti(a.s) wamesisitiza na kusema ya kuwa mtu mwenye tabia njema ataingia peponi ama mtu mwenye tabia mbaya kwa hakika mtu huyo ataingia motoni.

Imepokelewa katika riwaya ya kwamba mwanamke mmoja katika zama za Mtume(s.a.w.w) tangu asubuhi hadi jioni alikuwa akijishughulisha na ibada bila kupumzika, na katika masiku mengi ya mwaka alikuwa akifunga, lakini mwanamke huyo alikuwa na kasoro moja, nayo ni kuwa tabia yake ilikuwa ni mbaya na alikuwa akimuudhi jirani yake kwa ulimi wake mbaya, Mtume(s.a.w.w) akasema kuhusina na mwanamke huyo: (Hakuna kheri yoyote kwa mwanamke huyo, yeye ni mtu wa motoni)([9] ) Kwa hivyo ni juu ya kila mtu kufanya juhudi kwa ajili ya kujipamba na tabia njema kati ya jamaa zake, watu wake wa karibu, majirani zake na watu walioko pembezoni mwake. Hakika Mwenyezi Mungu anampenda mtu mwenye kutoa huduma na ambae anawasaidia watu na kutatua matatizo yao.

Ninawausia wanaume kwa wanawake usia mbili: Usia wa kwanza, Mkumbukeni Imam Husein(a.s) wakati wote, kuomboleza kifo cha Imam Husein ni tawfiki ya Mwenyezi Mungu ambayo huipata Muumini, na maombolezo hayo huwa ni wasila na nyenzo ya kutatua matatizo yote ya kidunia, kwa hivyo basi ni wajibu kuwe na vikao vya kila wiki kwa ajli ya kukumbuka mauaji ya Imam Husein(a.s) katika majumba yenu.

Na ninakumbuka ya kuwa kulikuwa na mtu mmoja alikuwa akija kumtembelea marehemu kaka yangu, na kaka yangu kama ada yake anapokutana na waumini alikuwa daima akimhimiza na kumsisitizia kuweka vikao na kufanya majlisi za kumkumbuka za Imam Husein katika nyumba yake, na bwana yule alikuwa akitoa udhuru ya kuwa nyumba yake ni ndogo na haitoshi kuweza kufanya hivyo kwa sababu nyumba yake ina chumba kimoja chenye ukubwa wa mita kumi na mbili tu, Marehemu Imam akamwambia:

Fanya majlisi katika chumba hicho kila wiki kwa muda wa saa moja. Yule bwana akaitikia wito na kufanya vile na kutokana na baraka za vikao vya kila wiki alivyo kuwa akivifanya katika chumba kile kidogo, na akisomea kwenye chumba hicho maombolezo ya msiba wa Imam Husein(a.s) , baadae bwana yule akawa ni katika wafanya biashara wakubwa kabisa kiasi kwamba akawa ni mwenye kumiliki majumba na akawa ni mwenye kumiliki vitu vingi visivyo kuwa na hesabau ( yaani akawa tajiri mkubwa).

Ama usia wa pili ni kutekeleza usia wa Imam Swadiq(a.s) kwa Mashia (wafuasi) wake ambao alisema katika usia huo:

Ni juu yenu enyi ndugu zangu waumini kuzitilia umuhimu itikadi za vijana na kufanya juhudi kubwa katika kuzirekebisha na kuziweka sawa zisiyumbe, na ziimarisheni dhidi ya watu wa batili na itikadi za batili na mbaya.

Fanyeni juhudi ya kufuatana nao na kuwa nao wakati wote mnapokwenda katika vikao vya Imam Husein(a.s) , na wasikilizieni na muwafahamishe pia muangalie ni kitu gani wanacho fikiria na vipi wanafikiri, na wala msikabiliane nao kwa ukali na msiwafanyie ugumu, ikiwa mtaweza kujibu ishkali na maswali yao basi jambo hilo ni zuri sana, laa sivyo fuataneni nao kwa mtu anae weza kujibu mswali yao na kubatilisha ishkali zao, kwa mfano katika zama za Mtume mtukufu(s.a.w.w) na katika zama za maima watwaharifu(juu yao sala na sala zilizo bora kabisa) vijana wengi waliongoka katika itikadi zao na tabia zao, na Abu dharri alikuwa ni mmoja wa vijana hao, kwani Abu dharri alikuwa ni mshirikina lakini alisilimu na kuamini na akawa ni mtu mwenye kupigiwa mfano na akawa mfano mwema na wa aina ya pekee, na Bwana Othumani bin Affan alifanya kile kitendo cha kumfukuza na kumpekeleka kaskazini mwa nchi ya lebanoni ili asiufedhehi utawala wake na asieneze fadhila za Ahlul-bayti(a.s) , lakini Aba Dharri kwa maneno yake na ushupavu wake na tabia yake aliweza kuwaongoa vijana wengi sana wa miji ile ambao baadae wakawa ni miongoni mwa watu wenye kuwatawalisha Ahlul-bayti(a.s) na wao wakaweza kuueneza Ushia katika miji ya Jabal Aamil na kaskazini mwa Lebanoni hadi hivi leo.

Na nyinyi mtokao katika mji wa Isfahani.. je mnafahamu ya kuwa Allamah Al-majlisiy alie zikwa katika mji wenu wa Isfahani babu yake wa juu kabisa hakuwa ni Shia?! Lakini kijana wa kawaida wa kishia aliweza kumkinaisha babu yake juu ya ukweli wa Ushia na itikadi ya Ahlul-bayti na Allamah Al-majlisiy akawa ni Shia mwenye Kuwatawalisha Ahlul-Bayti? Na sisi Mashia bado tunafaidika na Athari zake na elimu zake pia vitabu vyake mbali mbali, na huenda nyinyi nyote mmesikia kitabu chake cha riwaya kilicho kikubwa (Buharul-anwaar) ambacho alikusanya ndani yake maneno mazuri na maneno ya Maimam watwaharifu yenye nuru (rehma za mwenyezi Mungu ziwe juu yao wote).

Kwa hivyo ni juu yetu, enyi ndugu waumini, tuwe kama kijana yule ambae aliongoka kupitia kwake babu yake Allamah Al-majlisiy, hadi tuweze kuwapata watu mfano wa Allamah Al-majlisy. Ni juu yetu kuwangoza viumbe na hasa vijana miongoni mwao ili Ushia ubakie ukiwa ni wenye nguvu na ukiwa imara na wafuasi wake wawe ni wenye kuongezeka siku hadi siku. Na mwisho ninakuombeeni tawfiq na kila la kheri na namuomba Mwenyezi Mungu ayakubali matendo yenu na msitusahau katika dua zenu.

4 UKWELI WA USHIA

KUSUJUDU JUU YA UDONGO

SAMI : Ewe Ali kwa hakika nyinyi Mashia mnamshirikisha Mwenyezi Mungu, kwa kusujudu kwenu juu ya udongo, je udongo huo sio kiasi kidogo cha udongo ulio kauka mnao uabudu kinyume cha Mwenyezi Mungu?

ALI: Niruhusu nikuulize swali moja.

SAMI: Bila wasi wasi wowote uliza.

ALI : Je ni wajibu kusujudu juu ya kiwiliwili cha Mwenyezi Mungu mtukufu? SAMI: Hakika kauli yako hii ni kufru, kwa sababu Mwenyezi Mungu hana kiwiliwili, haonekani kwa macho, wala haguswi kwa kiwiliwili, na mwenye kuitakidi ya kuwa Mwenyezi Mungu ana kiwiliwili basi yeye ni kafiri. Hakika sijda ni wajibu ifanyike kwa ajili ya Mwenyezi Mungu pekee, yaani lengo la kusujudu na kunyenyekea inabidi liwe ni Mwenyezi Mungu alie takasika, ama kusujudu juu ya Mwenyezi Mungu hiyo ni kufru (huo ni ukafiri).

ALI : Kutokana na maneno yako haya imethibiti kuwa kusujudu kwetu juu ya udongo si shirki, kwa sababu sisi tunasujudu juu ya udongo, si kwamba tunausujudia udongo. Na tujaalie jambo lililo muhali ya kuwa, lau kama tunge kuwa tunaitakidi kwa mfano ya kuwa udongo ndio (Mwenyezi Mungu) basi ilikuwa ni lazima kuusujudia, si kusujudu juu yake, kwa sababu hakuna mtu yeyote anaesujudu juu ya Mola wake.

SAMI : Hakika ni mara ya kwanza kwangu kusikia uchambuzi kama huu, na kwa hakika ni uchambuzi ulio sahihi, kwani lau kama nyinyi mnge kuwa mnauzingatia (Udongo) kuwa ni Mungu msinge sujudu juu yake, na kusujudu kwenu juu yake ni dalili ya kuwa ninyi hamuuzingatii udongo huo kuwa ni Mungu. SAMI: Basi niruhusu nikuulize swali.

ALI : Uliza.

SAMI: Basi ni sababu ipi iwafanyayo muendelee kusujudu juu ya udongo kwa wakati wote, na kwa nini hamsujudu juu ya vitu vingine, kama mnavyo sujudu juu ya udongo?

ALI: Kuna hadithi tukufu iliyo pokelewa kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) kwa makubaliano ya madhehebu zote za Waislaam ya kuwa Mtume(s.a.w.w) alisema:

(Kwa hakika ardhi imefanywa kwangu iwe ni mahala pa kusujudia na mahala pa kujitwahirishia)[10] Kwa hivyo basi udongo halisi ndio ambao inajuzu kusujudu juu yake kwa makubaliano ya makundi yote ya Waislaam, kwa sababu hiyo sisi wakati wote husujudu juu ya udongo ambao waislaam wote wamekubaliana juu ya kuwa inajuzu kusujudu juu yake.

SAMI : Wamekubaliana vipi Waislaam wote juu ya jambo hilo?

ALI: Mwanzo kabisa alipo kuja Mtume(s.a.w.w) katika mji wa madina, na kujenga msikiti katika mji huo, je msikiti huo ulikuwa umetandikwa kwa mazulia?

SAMI: Hapana.. haukuwa umetandikwa kwa mazulia.

ALI: Basi Mtume(s.a.w.w) na Waislaam walikuwa wakisujudi juu ya nini?

SAMI : Walikuwa wakisujudu juu ya ardhi yenye udongo au mchanga.ALI : Kwa hivyo sala zote za Mtume(s.a.w.w) zilikuwa zikifanyika juu ya ardhi, na alikuwa akisujudu juu ya udongo, vile vile Waislaam katika zama zake na baada yake walikuwa wakisujudu juu ya udongo. Kwa hivyo kusujudu juu ya udongo bila shaka yoyote ni jambo lililo sahihi, na kwa maana hiyo sisi tunasujudu juu ya udongo kwa kufuata sira na sunna ya Mtume na kwa kufuata nyendo za Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) , na kwa maana hiyo sala zetu bila shaka ni sahihi

SAMI : Basi nyinyi Mashia kwa nini hamsujudu juu ya kitu kingine tofauti na udongo muuchukuao na kuubeba pamoja nanyi kutoka katika ardhi nyingine, au kwa nini hamsujudu kwenye udongo mwingine?

ALI : Kwanza kabisa: Mashia wanasema kuwa inajuzu kusujudu juu ya kila ardhi sawa iwe ni ile iliyo shikamana na kuwa kama jiwe au mchanga. Pili: Nisharti sehemu ya kusujudia iwe twahara, yaani isiwe na najisi, kwa hivyo basi haijuzu kusujudu juu ya ardhi iliyo najisika, au mchanga usio twahara, kwa maana hiyo ndio maana tunabeba kipande cha udongo mkavu ulio twahara, na kwa kufanya hivyo tunaepukana na hali ya kusujudu juu ya udongo ambao hatujui ya kuwa ni twahara au laa. Na kwa kuongezea ni kuwa, sisi tunasema kuwa inajuzu kusujudu juu ya udongo wa ardhi au ardhi ambayo hatujui kuwa ni najsi au laa.

SAMI : Ikiwa kwa kufanya hivyo mnataka kusujudu juu ya udongo halisi ulio twahara.. kwa nini hambebi mchanga ili muweze kusujudu juu yake?ALI : Kwa sababu kubeba mchanga husababisha kuchafuka kwa nguo, kwani mahala popote utakapo wekwa katika nguo nilazima nguo hiyo itachafuka, kwa sababu hiyo sisi huuchanganya na kiasi fulani cha maji kisha tunauacha ukauke, ili tunapo ubeba usisababishe kuchafuka kwa nguo.

Kisha kusujudu juu ya kipande cha udongo ulio kauka kuna dalili zaidi juu ya unyenyekevu na khushui kwa ajili ya Mwenyezi Mungu mtukufu. Hakika sijda ndio mwisho wa unyenyekevu, kwa sababu hiyo haijuzu kukisujudia kitu kingine tofauti na Mwenyezi Mungu alie takasika. Kwa hivyo basi ikiwa lengo la kusujudu ni kwa ajili ya kumnyenyekea Mwenyezi Mungu, kila sijda ambayo itakuwa ni yenye kuonyesha na kudhihirisha unyenyekevu zaidi, hakuna shaka yoyote kuwa itakuwa ni nzuri sana.

Kwa ajili hiyo imekuwa ni sunna sehemu ya kusujudia iwe chini zaidi kuliko sehemu ya mikono na miguu, kwani kufanya hivyo ni dalili zaidi juu ya unyenyekevu kwa Mwenyezi Mungu mtukufu. Na vilevile ni sunna kuipakaza pua kwa udongo wakati wa sijda. Kwa sababu kufanya hivyo kuna dalili zaidi juu ya unyenyekevu na khushuu'i kwa ajili ya Mwenyezi Mungu.

Kwa maana hiyo kusujudu juu ya ardhi, au juu ya kipande cha udongo ulio mkavu ni vizuri zaidi kuliko kusujudu juu ya vitu vingine tofauti na vitu viwili hivyo kati ya vitu ambavyo inajuzu kusujudu juu yake, kwani kufanya hivyo ni kuweka sehemu ya mwili iliyo tukufu zaidi- ambayo ni paji la uso- juu ya ardhi- kwa ajili ya kumnyenyekea Mwenyezi Mungu mtukufu na kudhalilika mbele ya utukufu wake Mwenyezi Mungu.

Ama mwanadamu-katika hali ya sijda- kuweka paji lake la uso juu ya zulia lenye thamani ya juu na lililo tengenezwa na kupambwa kwa madini kama Fedha, Akiki, Dhahabu na mengineyo, au juu ya nguo yenye thamani kubwa. jambo hilo ni kati ya mambo yanayopunguza hali ya unyenyekevu na khushuu 'i, na huenda kufanya hivyo kukapelekea kuto dhalilika mbele ya Mwenyezi Mungu mtukufu.

Kutokana na hayo je inawezekana kusujudu juu ya kitu kinacho mzidishia mtu unyenyekevu mbele ya Mola wake kikazingatiwa kuwa ni shirki na kufru? Na kusujudu juu ya kitu kinacho ondoa unyenyekevu kwa ajili Mwenyezi Mungu mtukufu kikazingatiwa kuwa ni kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu? Hakika hiyo si jambo lingine bali ni kauli ya uzushi na uongo.

SAMI : Basi ni maneno gani haya yalipo juu ya udongo ambao mnasujudu juu yake?

ALI: Kwanza kabisa: si kweli kuwa sehemu zote za udongo huo zimeandikwa juu yake, kwa hakika kuna udongo mwingi ambao haukuandikwa hata herufi moja. Pili: Udongo ulio andikwa katika upande fulani ni udongo ulio chukuliwa katika ardhi tukufu ya Karbalaa.[11] [2] je katika hilo kuna shirki? Na je hilo linautoa udongo huo katika hukumu ya kujuzu kusujudu juu yake? Hapana kamwe.

SAMI : Je udongo wa ardhi ya(Karbalaa) unakhususiya gani kwani tunawaona Mashia wengi wanajifunga tu na kusujudu juu ya udongo huo vyovyote itakavyo kuwa?

ALI : Sababu ya kufanya hivyo ni kuwa imepokelewa katika Hadithi tukufu:

(Kusujudu juu ya udongo wa kaburi la Husein kunavuka vizuizi saba)[12] Yaani kusujudu juu ya udongo huo kunapelekea kukubaliwa kwa sala, na sala hiyo kupanda kwa Mwenyezi Mungu mtukufu juu ya mbingu saba. Na haikuwa hivyo isipokuwa ni kwa kufahamu ubora wa udongo huo, ubora ambao haupatikani katika udongo mwingine tofauti na udongo mtukufu wa Karbalaa.

SAMI : Je kusujudu juu ya udongo wa kaburi la Husein kunaifanya sala iwe ni yenye kukubaliwa mbele ya Mwenyezi Mungu mtukufu hata kama sala hiyo itakuwa batili?

ALI : Mashia wanasema kuwa sala ambayo haikutimiza masharti ya kusihi kwake ni batili, haikubaliwi. Lakini sala iliyo timiza masharti yote ya kusihi kwake ni yenye kukubalika mbele ya Mwenyezi Mungu, na huenda isikubaliwe, kwa maana kuwa hapewi thawabu mtu kwa sala hiyo, kwa hivyo sala iliyo saliwa juu ya udongo wa kaburi la Imam Husein ikiwa ni sahihi, hukubaliwa na kupewa thawabu juu ya sala hiyo, kwa hivyo basi kusihi ni kitu, na kukubaliwa kwa sala ni kitu kingine.

SAMI : Je ardhi (tukufu ya Karbalaa) ni tukufu zaidi kuliko ardhi yote hata ardhi ya Makka na Madina, hadi kusujudu juu yake kuwe bora?

ALI: Kuna kizuizi gani katika hilo?

SAMI: Hakika udongo wa(Makka tukufu) ambao tangu kutelemka kwa Adam(a.s) bado ni ardhi ya Kaaba, na ardhi ya (Madinatu- lmunawwarah) ardhi ambayo ndani yake kunakiwiliwili cha Mtume mtukufu(s.a.w.w) zinakuwa na daraja la chini zaidi kuliko daraja la ardhi ya Karbalaa? Hili ni jambo la ajabu! Na je Husein bin Ali ni bora kuliko babu yake Mtume wa Mwenyezi Mungu?

ALI: Hapana. hakika utukufu wa Husein ni chembe ndogo ya utukufu wa Mtume(s.a.w.w) , na utukufu wa Husein ni sehemu ndogo ya utukufu wa Mtume(s.a.w.w) , na nafasi ya Husein mbele ya Mwenyezi Mungu mtukufu si kwa ajili ya jambo lingine bali ni kwa sababu ya kuwa yeye ni Imam alie fuata dini ya babu yake Mtume wa Mwenyezi Mungu hadi kufa shahidi katika hilo. Hapana, daraja ya Husein si chochote isipokuwa ni sehemu ndogo tu ukilinganisha na daraja ya Mtume(s.a.w.w). Lakini.. kutokana na ukweli kuwa Husein aliuliwa yeye na Ahli-bayti wake, na answari wake katika njia ya kuusimamisha Uislaam, na kuimarisha kanuni zake, na kuulinda usichezewe na watu wenye kufuata matamanio ya nafsi zao, Mwenyezi Mungu mtukufu kwa kufa kwake shahidi alimpa badala yake mambo matatu:

1-Kujibiwa kwa maombi chini ya kuba la kaburi lake.

2-Maimamu kutokana na kizazi chake.

3- Udongo wa kaburi lake kuwa ni dawa na tiba ya maradhi mbali mbali.

Kwa hivyo Mwenyezi Mungu akautukuza udongo wa kaburi lake kwa sababu yeye aliuwawa katika njia yake kwa mauaji yaliyo mabaya sana na ya kikatili, na wanawake wake wakachukuliwa mateka,, Maswahaba wake kuuwawa, na mabalaa mengi tofauti na hayo yaliyomfika kwa ajili ya dini..je katika hilo kuna kizuizi chochote? Na je kuufadhilisha udongo wa Kaarbalaa juu ya udongo wa sehemu nyingi ya ardhi hata juu ya ardhi ya Madina maana yake ni kuwa Husein(a.s) ni bora kuliko Mtume(s.a.w.w) ? bali suala ni kinyume chake. Kwani kuutukuza udongo wa kaburi la Husein ni kumtukuza Husein, na kumtukuza Husein(a.s) ni kumtukuza Mwenyezi Mungu na Mtume wake(s.a.w.w).

SAMI : Haya ni kweli, na mimi nilikuwa nikidhania ya kuwa mnamfadhilisha Husein(a.s) hata kuliko Mtume(s.a.w.w) , na hivi sasa nimefahamu ukweli kuhusu suala hili, na ninakushukuru kwa maneno yako haya mazuri ambayo umenifahamisha na kunizindua kwayo, na wakati wote nitachukua na kubeba kipande cha ardhi tukufu ya Karbalaa ili nikitumie kusujudu juu yake popote nitakapo kwenda kusali.. kama ambavyo nitaacha kusujudu juu ya kitu chochote mfano wa zulia na madini.

ALI : Kwa hakika mimi nilitaka kukubainishia ya kuwa tuhuma hizi zielekezwazo kwetu sisi Mashia, hazina ukweli wowote, bali ni uongo mtupu ulio pangwa na kuelekezwa kwetu na watu waovu kati ya maadui wa Waislaam, wanao jiita kuwa ni waislaam, huenda ukajipamba na ukweli wakati wote, na wala usijali na kujishughulisha na utakayo yasikia dhidi ya Mashia bila kufanya utafiti kuhusu ukweli wa madai hayo na ukweli wake.

ambao walimuamini Nuhu katika tufani na kupanda juu ya kuba hiyo.

Na Abu jaafar Imam Baaqir(a.s) amesema: Al-ghaadhiriyyah ni kipande cha ardhi ambacho Mwenyezi Mungu alizungumza na Musa(a.s) bin Imran katika sehemu hiyo na ni sehemu alipo muokolea Nabii Nuhu, na sehemu hiyo ni sehemu tukufu sana kati ya ardhi ya Mwenyezi Mungu, lau kama si hivyo basi Mwenyezi Mungu asinge ipa amana ya kuvihifadhi viwiliwili vya mawalii wake na watoto wa Mtume wake, (Hakika wamekufa katika ardhi ya Karbalaa manabii mia mbili na mawasii mia mbili) basi yazuruni makaburi yetu katika ardhi ya Ghaadhiriyyah. Na Mwenyezi Mungu ameifanya ardhi ya Karbalaa kuwa ni haram yenye amani na yenye baraka kabla Mwenyezi Mungu haja iumba ardhi ya kaaba na akaifanya kuwa ni haram (sehemu tukufu) kwa muda wa miaka ishirini na nne elfu, na ardhi ya Karbalaa na maji ya mto Furati ni ardhi ya kwanza na maji ya mwanzo kabisa yaliyo takaswa na Mwenyezi Mungu na yaliyo barikiwa)

Rejea ziara: Kaamiluz-ziyaarat cha Ibnu Qawlawaihi Jaafar bin Muhammad Al-qumiy (368 hijiria) ukurasa 444-445 mlango wa 88 kuhusu ubora wa Karbalaa. Na imepokelewa kutoka kwa Alaa bin Abi Aathah amesema: Nimehadithiwa na Ra'asi Jaaluut, kutoka kwa baba yake amesema: Sikupita Karbalaa isipokuwa nilikuwa nikimkimbiza mnyama wangu hadi ninapo ivuka sehemu hiyo, amesema: nikamuuliza kwa nini? Akasema: Tulikuwa tukizungumza ya kuwa mtoto wa nabii atauwawa katika sehemu hiyo. Akasema: Na nilikuwa nikiogopa nisije nikawa ni mimi, wakati alipo uliwa Husein tukasema: haya ndio tuliyo kuwa tukiyazungumza. Akasema: Na baada ya tukio hilo nilikuwa kila nipitapo sehemu hiyo nilikuwa nikipita kwa kutembea taratibu na sikuwa ni mwenye kukimbia)

Tariikhut-twabariy juzu ya 5 393. matukio ya mwaka 60 hijiria,

Al-kaamil fit-tarikh juzu ya 4 90. Matukio ya mwaka 61 hijiria.

5 UKWELI WA USHIA

KUYAJENGEA MAKABURI

FUADI : Ewe Jaafar, je unaniruhusu nikuulize kuhusiana na maudhui ya Shia na Sunni?[13]

JAAFAR : Uliza kwani nina penda sana kila mtu awe ni mwenye kufahamu mambo, mwenye elimu na anae fahamu mambo kutokana na utafiti na kwa kupata yakinina hawi ni mwenye msimamo legelege na mwenye kufuata kila akisikiacho na kipepeacho angani, au kila sauti ijitokezayo na kutangaa anganibila ya kufahamu usahihi wake na ubatilifu wake au ufisadi wake.

FUADI : Je maneno yangu utayaamini ikithibitika kuwa sisi (Ahli sunna) ndio wenye haki?

JAAFAR : Kwa hakika mimi niko msitari wa mbele kati ya wale wenye kuamini mambo ya kweli haraka pale wanapo yafahamu, na mimi sikushikamana na ushia isipokuwa ni baada ya kuuona kuwa ni haki na wewe unafahamu ya kuwa baba yangu na mama yangu na ndugu zangu na watu wa kabila langu wote ni masunni na kati yao hakuna Shia hata mmoja, na mimi sikufuata Ushia isipokuwa ni kwa ajili ya ukweli nilio uona na kuukuta ndani ya madhehebu hayo.. na lau nitafahamu usahihi wa maneno yako mimi ni wa mwanzo kuyaamini.

FUAD : Nyie Mashia mnayajengea makaburi ya Manabii, Maimamu, Maulamaa na watu wemamajengo makubwa, mnasali kwenye makaburi, wakati jambo hilo ni shirki, kama washirikina wanavyo abudu masanamu nanyi Mashia mnaaabudu majengo ya makaburi ya mawalii.

JAAFAR : Ni wajibu sisi tuwe wakweli na tunao kwenda sambamba na uhakika wa mambo, tusiwe ni watu wachukuao maganda na kuacha kiini, tusiangalie yasemwayo na fulani au fulani, bali tuangalie ukweli ulio wazi katika kitabu cha Mwenyezi Mungu na Sunna ya Mtume wake(s.a.w.w) , na mwenendo wa watu wema walio tangulia.

FUAD : Ndio, nami ni hivyo hivyo, ninapenda kufahamu ukweli wa mambo kupitia njia za kielimu na ufahamu sahihi, si kufuata mambo ufuataji wa kipofu.

JAAFAR : Kwanza kabisa: Sio sisi Mashia pekee tuhusikao na suala la kuyajengea makaburi, kwani waislaam wote wanayajengea makaburi ya Manabii na Maimam na wanazuoni wakubwa au viongozi wao, na ifuatayo ni mifano juu ya hayo: Kaburi la Mtume(s.a.w.w) na makaburi ya makhalifa wawili bado hadi hivi sasa yamejengewa kwa jengo kubwa na yenye kuba kubwa na ya hali ya juu kabisa.

Makaburi ya Mitume kadhaa, kama vile kaburi la Nabii Ibrahim(a.s) lililoko Jodan katika mji wa (Al-khaliil) makaburi hayo yana dharihi (yamejengewa) na juu yake kuna kuba na majengo makubwa. Kaburi la Nabi Mussa(a.s) lililoko Jodan kati ya mji wa (Qudsi) na (Omman) lina jengo kubwa. Kaburi la Abi Hanifa lililoko Baghdad hadi leo bado limejengewa kwa jengo kubwa, na juu yake kuna kuba. Kaburi la Abi Hurairah katika (Misri) hufanyiwa ziara na limejengewa na juu yake kuna kuba. Kaburi la Abdul-qaadir lililoko (Baghdaad) kaburi hilo lina uwanja mkubwa na dharihi na juu yake kuna kuba.

Na makaburi mengine ya Mitume, na makaburi ya Maimamu na wanazuoni wakubwa wa madhehebu, yote hayo yana majengo na juu yake kuna kuba, na yana waqfu maalum ambapo waqfu hizo faida zake hutumika kuyaimarisha na kuyakarabati makaburi hayo na kuyalinda yasiharibike.

Na Miji ya kiislaam imejawa na majengo kama hayo.. na Waislaam wote pamoja na tofauti za madhehebu yao tangu siku ya kwanza hadi leo huyapenda mambo hayo, na huwaamrisha watu kuyatekeleza hayo, na hawakukataza kufanya hivyo hata siku moja, kwa hivyo si sisi Mashia pekee tuhusikao na hukumu hii, bali wanakubaliana nasi na kuwafikiana nasi Waislaam wengine wote, na wao pia huyajengea makaburi ya maimamu wao na wakati wote huyatembelea.

Pili: Sisi- Mashia- au waislaam wengine wakati tunapo Sali pembezoni mwa makaburi ya mawali, hatusali kwa ajili ya mawalii hao bali tunasali kwa ajili ya Mwenyezi Mungu pekee. Na liwezalo kukujulisha hilo ni kuwa sisi tunapokuwa katika sala huelekea kibla na wala hatuyaelekei makaburi hayo, na lau kama tunge kuwa tukiyasalia makaburi yale, na kuelekea kwenye ibada zatu kwenye dharihi zile (majengo yale ya makaburi), ingewajibika kuyaelekea, na tusinge elekea kwenye kibla.

FUAD : Kwa nini mnasali nyuma ya makaburi hayo, mpaka mkayafanya kuwa ni kibla chenu?

JAAFAR : Hakika sisi wakati tunapo Sali nyuma ya makaburi, tunaelekea kibla na wala hatuyaelekei makaburi, bali makaburi yale-imetokea tu- yakawa mbele yetu, bila ya sisi kukusudia kuyaelekea.

Na hili halitokei isipokuwa kwa mtu anae Sali akiwa ameelekea kibla katika sehemu fulani na ikatokea kwa mfano kukawa na jengo kubwa mbele yake, je kusali katika sehemu hiyo kunamaanisha kuwa mwenye kusali anaabudu jengo hilo?! Na zaidi ya hayo Maulamaa wote wa Waislaam wanasema kuwa: Inajuzu kusalia katika majumba ya ibada za washirikina hali ya kuwa umeelekea kibla hata kama mbele ya mwenye kusali kutakuwa na sanamu lenye kuabudiwa kinyume cha Mwenyezi Mungu, Kwani mwenye kusali humuelekea Mwenyezi Mungu na wala halielekei sanamu. Je hii inamaana kuwa mwenye kusali analiabudu sanamu lile?

FUAD : Ikiwa kuyajengea makaburi si shirki- kama unavyo sema- na waislam wote wanasema ya kuwa inajuzu kufanya hivyo, ilikuwaje wakavunja madharihi (majengo ya makaburi) na makuba yaliyo jengwa juu ya makaburi ya maimamu na wengineo, kwa hoja ya kuwa kufanya hivyo ni shirki na ni kumuabudu asie kuwa Mwenyezi Mungu, na maulamaa wa Hijazi wakatoa fat'wa ya kufanya hivyo?

JAAFAR : Kwa hakika ni baadhi tu walio toa fat'wa kama hiyo kati ya maulamaa wa Hijazi katika zama zile, kwani kuna baadhi ya Mashekhe waishio katika mji wa Madina walio nihadithia na kunisimulia kwa kusema: Kwa hakika wakati huo walipo toa amri ya kubomoa makuba na majengo ya makaburi, maulamaa wenyewe wa Hijazi walipinga amri hiyo, wakitoa hoja kuwa hilo si shirki bali vitu kama hivyo ni sunna katika sheria ya kiislaam, kutokana na kauli yake Mwenyezi Mungu mtukufu:jambo lililo pelekea kufukuzwa kwa maulamaa wale, na kuwauz ulu wengine katika nyadhifa zao na kuwatenga. Kwa hivyo basi: Fat'wa hiyo haikutolewa isipokuwa na baadhi tu ya maulamaa wa Hijaz.

FUAD: Kwa hakika mimi nilikuwa nikifikiria na kujiuliza ya kuwa: Ikiwa kujenga madharihi na makuba ni haram na shirki, kwa nini maulamaa wa Waislaam hawakuzinduka na kuliona hilo tangu zama za Mtume(s.a.w.w) hadi leo, na kwanini hawakuzuwia kufanya hivyo? Na ilikuwaje Waislaam wasilifahamu hilo kwa muda wa karne kumi na tatu?

JAAFAR: Nitakuongezea elimu na maarifa: Hakika Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) alikiri na kukubali kujengea makaburi, madharihi na makuba na hakukataza kufanya hivyo. Kwa mfano hili ni jengo la hijri Ismail mahala alipo zikwa Nabi (Ismail) na sehemu alipo zikiwa mama yake Haajar. Na haya hapa makaburi ya Manabii wengine-kama Ibrahim Musa na wengineo- walio zikiwa pembezoni mwa baytul-maqdas, yalikuwa ni yenye majengo makubwa katika zama za Mtume(s.a.w.w) na hadi zama zetu hizi, na wala hakuzuwia yeyote si Mtume Mwenyewe (s.a.w) wala mmoja wapo kati ya makhalifa wake.

Na lau kama tendo hilo linge kuwa haram au linge kuwa ni shirki basi Mtume ange amuru kuvunjwa na kubomolewa kwa majengo na makuba hayo, na ange kataza kufanya hivyo. Na kutokana na ukweli kuwa hakufanya hivyo tunafahamu na kuwa na yakini ya kuwa mfano wa vitu kama hivyo au kufanya hivyo ni kitu kinacho juzu na kinafaa.

Hivyo hivyo baada ya kufariki Mtume(s.a.w.w) , kwani Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo chukuliwa roho yake alizikwa katika chumba chake, na mlango wa chumba kufungwa, na kaburi lake likawa katikati ya chumba kilicho jengewa kuta na dari, na lau kama sahaba yeyote ange sikia kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) kuwa tendo kama hilo ni haram basi wasinge thubutu kumzika Mtume katika chumba hicho kilicho jengewa, na lau kama ingelazimika kumzika chumbani mwake basi ingekuwa wajibu kubomoa chumba hicho ili kaburi hilo lisiwe na jengo au lisiwe ni lenye kujengewa.

Na kutokana na kutofanya kwao hivyo, tukafahamu ya kuwa kujenga juu ya makaburi si haram, sasa vipi itakuwa ni shirki?.

FUAD: Ninakushukuru kwa wema wako kwani umeniongoza kwenye ukweli (haki), na kunijulisha ya kuwa kujenga juu ya makaburi si haram wala shirki, na kwamba wale ambao wanaharamisha jambo hilo hawana dalili yoyote katika sheria wawezayo kuitegemeza kwayo kauli yao.Na kwa hakika mimi nitakushukuru daima juu ya hili.

JAAFAR: Nami ninakushukuru kwa kukubali kwako ukweli na haki baada ya kuifahamu, na kuufuata kwako uongofu pale ulipo uona, kwani wewe ni mwenye kufuata muongozo wa akili na mantiki sahihi, kwa hivyo basi ninapenda kukuzidishia maarifa zaidi kuhusiana na haki na ukweli, na kukupatia maarifa mbali mbali katika dini, je unawakati zaidi ili niweze kuzungumza na wewe?

FUAD: Kwa hakika mimi ninapenda sana maneno ya kweli, zungumza ulitakalo, hakika mimi niko tayari kukusikiliza na kuyajaza masikio yangu kwa maarifa.

JAAFAR: Kutokana na mazungumzo yetu yaliyo pita imethibiti kuwa kujenga juu ya makaburi ya mawalii wa Mwenyezi Mungu ni jambo linalo faa na inajuzu kufanya hivyo, na jambo hilo si haram.

FUAD: Ndio.. nami niko pamoja nawe katika hilo.

JAAFAR : Hivi sasa nataka kusema hivi: Hakika kujenga juu ya makaburi ya mawalii wa Mwenyezi Mungu na kuweka madharihi juu yake na kujenga makuba.. yote hayo ni sunna, hupewa thawabu mwenye kuyafanya hayo yote, si tu kwamba inajuzu.

FUAD : Vipi inakuwa sunna?

JAAFAR : Mwenyezi Mungu mtukufu amesema:( Na anayeziheshimu alama za Mwenyeezi Mungu basi hayo ni katika unyenyekevu wa nyoyo). Kwa hivyo kila kitu ambacho huzing atiwa na kuhesabiwa kuwa ni katika shiari za Mwenyezi Mungu kukitukuza ni sunna katika Uislaam.

FUAD: Ndio..lakini vipi itakuwa kujenga juu ya makaburi ya mawalii wa Mwenyezi Mungu ni katika shiari za Mwenyezi Mungu?

JAAFAR: Shiari ni vitu ambavyo huitukuza dini katika mtizamo wa ulimwengu bila kuwepo dalili juu ya uharamu wake.

FUAD: Je dini hutukuzwa kwa majengo na makuba hayo?

JAAFAR : Ndio.

FUAD: Ki vipi?

JAFAAR: Kujengea makaburi ya maulamaa na viongozi watukufu wa kiislaam, na kujenga makuba juu yake, na kuyahifadhi yasiharibike na yasibomoke, ni kuwatukuza watukufu hao bila shaka yoyote. Kwa mfano: Akijitokeza mtu fulani na kupanda uwa waridi kwenye kaburi la mtu alie kufa, je mtu huyu haonekani kuwa amemtukuza maiti yule, na kuwa amemuenzi?

FUAD : Ni sahihi.

JAAFAR : Vipi ikiwa atajenga juu ya kaburi lake jengo kubwa na kuweka kuba juu yake, hakika kufanya hivyo ni kumtukuza na kumuenzi maiti huyo bila shaka yoyote. Na kuwatukuza viongozi na maulamaa wa kiislaam pia maimamu na mawalii.. ni kuutukuza Uislaam, na kuitukuza na kuienzi dini ambayo watu hawa walikuwa wakiilingania, na wakiwaelekeza watu kwenye dini hiyo. Je mtu fulani anapo mtukuza Raisi wa chama fulani, au walinganiaji wa itikadi za chama hichohuzingatiwa kuwa ni mwenye kukitukuza chama kile na itikadi ile au laa?

FUAD: Ndio ni kama usemavyo.

JAAFAR: Kwa hivyo basi kuyajengea makaburi ya mawalii wa Mwenyezi Mungu ni kuwatukuza wao na kumtukuza Mwenyezi Mungu, na ni kuuinua na kuutukuza Uislamm, na kila kitu ambacho kukifanya kutakuwa ni kumtukuza Mwenyezi Mungu na ndani yake kuna kuuinua Uislaam, kitu hicho ni katika shiari za Mwenyezi Mungu ambazo anahimiza kuzifanya, kwani anasema:Suratul- haji aya 32.

FUAD: Kwa hivyo..kuvunja na kubomoa maka buri ya mawalii na Mitume na maimam, inakuwa ni kuidhalilisha dini, na kuutia dosari utukufu wa kiislaam.. kwani kuyabomoa ni kuwadharau viongozi wetu, na ni kuwahini wao.. na kuwahini wao ni kuihini dini, na kuutia dosari utukufu wao ni kuutia dosari utukufu wa Uisalaam.

JAAFAR: Na mimi pia nimekuwa Shia, na nimefuata madhehebu ya Ahlil-bayti (a.s) na nimebadilisha jina kutoka jina la Waliid na kuwa Jaafarkwa sababu hii hii? Kwa hakika mimi wakati nilipo kuwa nikifuata rai za watu wengine sikuwa nikidha nia ya kuwa hakuna alie kwenye haki kinyume changu mimi, lakini nimeitafuta haki na kuifuata hadi kuifikia. Na mtu wakati wote anapo acha nyuma na kuzitupilia mbali asabia za madhehebu, na kukifungua kifua chake kwa ajili ya kuikubali haki, na kuitafuta haki.. hapana budi ataifikia haki hiyo na kuipata.

FUAD: Mimi, na baada ya msimamo na mawkifu haya, nitakuwa makini katika mambo mbali mbali, na nitakuwa ni mwenye kuitafuta haki, mpaka niweze kuifuata haki kokote nitako ikuta. Na kwa hakika nitakushukuru kwa muda wote.. Basi niruhusu nende zangu kwani nina ahadi na mtu fulani.

JAAFAR: Nenda, Mwenyezi Mungu akulinde.

FUAD : Fii amani llahi.

JAAFAR : Uwe katika amani ya Mwenyezi Mungu.

Abu haatam Ar-raziy katika kitabu chake (Az-ziinah) anasema: Kwa hakika jina la kwanza lililo dhihiri katika zama za Mtume wa Mwenyezi Mungu ni Shia, na jina hili ndilo lililo kuwa jina mashuhuri (Laqab) la masahaba wane nao ni: Abu Dharri Salman Miqdaad na Ammar.

Na Shekh Mohammad Husein Kaashiful-Ghitaa katika kitabu chake kiitwacho (Aslush-shia wa Usuuliha) anasema: Hakika mbegu ya mwanzo ya Ushia iliwekwa na kupandikizwa na Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) tangu zama za mwanzo kuanza kueneza Uislaam bila ya kutofautisha kati ya vitu viwili hivyo na vikiwa sawa.

Na ushahidi ni hadithi zake tukufu si kupitia njia za Mashia na upokezi wa wapokezi wa Kishia Imamiyyah pekee bali ni hadithi za maulamaa wa kisunni na wanazuoni wao na kupitia njia zao wanazo ziamini ambazo hazidhaniwi kuwa zina chembe ya uongo, na katika hadithi hizo ni hadithi iliyo pokelewa na Suyuut katika kitabu chake (Ad-durrul-manthuur fii tafsiri kitabillahi bil-ma'athur) katika kuitafsiri kauli yake Mwenyezi Mungu mtukufu:(Hao ndio viumbe bora) (suratul bayyinah aya 7). Ame sema: Ametoa hadithi Ibn Asakir kutoka kwa Jaabir bin Abdillahi amesema: Tulikuwa kwa Mtume(s.a.w.w) mara akatokea Ali na kuingia na Mtume(s.a.w.w) akasema: Nina apa kwa haki ya yule ambae nafsi yangu iko mikononi mwake hakika huyu na wafuasi (Mashia) wake ndio walio faulu na kufuzu siku ya kiama. Na hapo ikatelemka aya isemayo:(Hakika wale ambao waliamini na kufanya matendo mema hao ndio viumbe bora). (Suratul-bayyinah aya 7). Ibnu Hisham katika Siir atun-nabawiyyah anasema:Hakika umma wa kiarabu uligawanyika katika makundi mawili Masunni na Mashia tangu siku ya Sakifa.

Muhammad Abu Zuhra anasema katika kitabu chake kiitwacho Taarikhul-madhaahibil-islaamiyyah:(Ushia ni madhehebu ya kiislaam ya kisiasa ya tangu muda mrefu na Mashia walidhihiri na madhehbu yao hayo tangu mwishoni mwa zama za Uthuman na kukua na kupata nguvu katika zama za ukhalifa wa Ali, kwani kila alipo pata nafasi ya kuchanganyika na watu walizidi kupendezewa na kuvutiwa kutokana na kipawa chake na kutokana na nguvu ya Imani yake ya dini na elimu yake).

Ibnu Abil-hadiid anasema katika kitabu chake Sharhu Nahjul-balagha:(Hakika Mashia katika zama za dola na utawala wa Muawia walikuwa wakifadhilisha kuitwa Al-kitabiy na wasiitwe Shia. Kwani Ushia anwani yake na shiari yake ni kushikamana na Ahlul-bayti na kufuata elimu yao na kujiepusha na watu wa Bidaa (Uzushi) na kushikamana na kizazi kitwaharifu na kilicho pambika na tabia njema na bora kabisa) (Rejea kitabu Taarikhul-firaqil-islaamiyyah cha Shekh Muhammad Khaliil Az-zayni ukurasa wa 108-109).

Neno Sunnah: Lenye shadda, asili ya neno hilo ni njia, na neno hilo limepanuka maana yake katika makundi tofauti, na linapo tumika huwa lina maana ya aliyo yafanya Mtume (s.a.w) kama kauli vitendo au aliyo yakataza na kuyakemea, na hutumika katika maana hizo kupitia ndimi za wanazuoni na hadithi za Mtume(s.a.w.w) . Na katika zama za hivi karibuni neno Sunnah limekuwa likitumika katika mukabala wa neno Shia, na Husemwa: As-sunnatu wal-jamaah katika mukabala wa watu maalum, na katika ufahamu wa Shekh wa madhehebu ya Hanbali Ibnu Taimiyyah: Neno Sunnah: lina maana ya kumpenda Ali Uthmani na kumtanguliza Abubakar na Omar kwa wawili hao walio tangulia.

Na madhehebu yalipokithiri na makundi kuwa mengi, baadhi wakashikamana na rai isemayo kuwa tamko Sunni lilikuwa likitumika kwa mtu ambae anafuata dini kwa kuwapenda na kuwatawalisha mashekhe wawili, (Abubakar na Omar), na ilikuwa ikisemwa Sunaatul-umariyyh) Rejea kitabu Tariikhul-firaqil-islaamiyyah ukurasa 44-45).

6 UKWELI WA USHIA

KUPAMBWA KWA MAKABURI YA MAIMAM

KHALID : Salaamun alaykum.

BAAQIR : Wa alaykumus-salaam warahmatullahi wabarakatuhu.KHALID : Umefanya vizuri umekuja lini?

BAAQIR : Nimekuja kumtembelea mtoto wa ami yangu anaishi hapa.KHALID : Nakuomba leo hii ukaribie nyumbani kwetu.

BAAQIR : Kwa hakika ninakazi nyingi nilizo ziacha kwa ajili ya kuwatembelea ndugu (kuunga udugu) na kuomba unisamehe sana kwa wito huo.

KHALID : Haiwezekani..marafiki wawili baada ya kutengana kwa muda wa miaka kumi wanakutana kisha wasibakie na kufuatana walau kwa muda wa saa moja. Hakika mimi -pia nina haki ya udugu wa kiislaam. Kisha kulitokea mazungumzo kati yangu na ndugu yangu mmoja muumini kuhusiana na maudhui ya Shia na Sunna na kutokana na kuwa mimi ninamatumaini na imani na wewe ninataka na ninakusudia kufanya mazungumzo na wewe kuhusu maudhui hayo ili niweze kuelewa ukweli na uhaki katika maudhui hayo.

BAAQIR : Hakuna shaka. Walifuatana pamoja hadi nyumbani kwa Khalid, na kufika nyumbani kwake, na kila mmoja akaketi pembezoni mwa mwenziwe. Na baada ya kuzungumza kuhusiana na mambo yanayo wahusu na yaliyo maalum kwa ajili yao wawili, Baaqir akamuwahi mwenzie kwa kumuuliza swali na kusema: Ni mazungumzo gani yaliyo fanyika kati yenu?

KHALID : Mazungumzo yalikuwa yakihusiana na kuyapamba makaburi ya Manabii, maimam, maulamaa, waumini na watu wema na mfano wa hao, kwa Dhahabu na Fedha na mapambo mengineyo.

BAAQIR : Ni tatizo gani lililopo kuhusiana na jambo hilo?

KHALID : Je kufanya hivyo si haram?

BAAQIR : Kwanini iwe haram?

KHALID : Je maiti anafaidika na mapambo hayo?

BAAQIR : Hapana, hafaidiki nayo.

KHALID : Kwa hivyo, hayo yote ni Israfu na matumizi mabaya, na Mwenyezi Mungu anasemaWala usitawanye (mali yako) kwa ubadhirifu. Hakika watumiao kwa ubadhirifu ni ndugu za mashetani. suratul- israai aya 26-27.

BAAQIR : Unasemaje kuhusiana na nguo ifunikwayo juu ya Kaaba na mapambo yake, na Dhahabu Fedha na vitu ambavyo vipo juu ya Kaaba na ndani ya Kaabah?

KHALID: Sijui.

BAAQIR : Ndio, Kaaba ina nguo ambayo hufunikwa juu yake, na kuna Dhahabu nyingi, ambayo watu huitoa zawadi kwa ajili ya Kaaba kutoka sehemu tofauti za Dunia tangu zama za ujahilia hadi katika zama zetu hizi. Ibnu Khaladuni[14] anasema katika utangulizi wa kitabu chake:

[15] Kwa hakika tangu zama za Ujahilia kaumu mbali mbali walikuwa wakiitukuza Kaaba, na wafalme walikuwa wakituma mali na vitu vya thamani kwenye nyumba hiyo kama vile Kisraa na wengineo, Na kisa cha mapanga na nguo zilizo fumwa kwa dhahabu, vitu ambavyo Abdulmutwalib alivikuta chini alipo chimba kisima cha Zamzam ni maarufu sana).

Na Mtume(s.a.w.w) alipo ikomboa Makka alikuta katika kisima kirefu kukiwa na Awqiyah sabini elfu za Dhahabu vitu ambavyo wafalme walikuwa wakizitoa zawadi kwa ajili ya nyumba ya Allah. Na kulikuwa na dinari milioni moja, yaani zenye uzito wa Kintwari milioni mbili. Na Ali(a.s) alisema kumwambia Mtume: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu unaonaje ukitumia mali hii ikakusaidia katika vita vyako? Mtume hakufanya hivyo. Kisha akamwambia Abubakar nae hakuzitoa. (hadi akasema)

(Amesema Abu waail): Niliketi kwa Shaibah bin Othuman nae akasema Aliketi kwa Omar bin Khattab, akasema: Niliazimia nisibakishe katika nyumba hiyo chembe yoyote ya Dhahabu wala Fedha isipokuwa nitaigawa kati ya Waislaam. Nikasema Hutafanya hivyo?

Akasema: Kwanini nisifanye hivyo?

Nikasema: Sahiba wako hakufanya hivyo.

Akasema: Hao wawili ndio ambao hufuatwa nyendo zao.[16]

Je Kaabah ilikuwa ikifaidika na Dhahabu na Fedha hizo ewe Khalid?

Au -Mwenyezi Mungu -ametakasika na hili- alikuwa akifaidika na vitu hivyo viwili?

KHALID : Hapana.

BAAQIR : Pamoja na hayo Mtume(s.a.w.w) hakuunyoosha mkono wake kwenye mali hiyo iliyo kuwa imelimbikizana, wala hakutumia hata chembe moja ya mali hiyo, pamoja na kuwa wakati ule Uislaam ulikuwa ukihitajia sana mali na pesa nyingi wakati ambapo hazina ilikuwa imejaa, kwa ajili ya kuimarisha nguzo zake katika miji na nchi mbali mbali. Kwa nini hakufanya hivyo? Ni kwa sababu mali hiyo nyingi ilikuwa ni mali ya Kaabah na huiongezea Kaabah utukufu na heba yake machoni mwa watu, japokuwa utukufu na daraja yake ya kweli iko kwa Mwenyezi Mungu mtukufu, utukufu ambao haupungui wala kuongezeka, sawa iwe na mali zote za dunia, au isiwe na chochote.

Na maneno ni hayo hayo kuhusiana na makuba ya Dhahabu, na milango ya Dhahabu na Fedha, na nguo ifunikwayo juu yake na mapambo yatolewayo zawadi na kupambwa nayo makaburi ya mawalii wa Mwenyezi Mungu mtukufu kama vile: Amirul-muuminiin, Imam hasan na Imam Husein, Imam Ridhaa na wengineo juu yao rehma na amani. Watu hawa cheo na daraja yao ya kweli waliyo pewa na Mwenyezi Mungu haipungui wala kuzidi kwa kuwepo madini hayo ya thamani kwenye makaburi yao, na wala haipungui ikiwa hayakuwepo, kwa mfano Imam Hasan bin Ali(a.s) ni bora kuliko nduguye Husein(a.s) japokuwa kaburi la Imam Hasan(a.s) hupigwa na jua katika jangwa la Bakii'i likiwa halikujengewa juu yake au juu yake kukiwa hakuna jengo lolote, na likiwa halikupambwa na pambo la aina yoyote, na kaburi la Imam Husein(a.s) lilikuwa na majengo makubwa makubwa ya dhahabu halisi iangazayo angani na kuyaondoa mawingu.

Lakini tumeyafanya hayo kwa ajili yao, na kutoa zawadi ya mapambo ya Dhahabu kwenye makaburi yao, na makuba ya makaburi yao kuyatia dhahabu na mengineyo, yote hayo kwa ajili ya kuwaenzi na kuwatukuza wao.

KHALID : Je vitu hivi vinawapatia hawa utukufu katika macho ya watu?BAAQIR : Ndio. Na hivi sasa nitakufanya ukiri jambo hilo. Kwa mfano ukienda kwa Mayahudi na kuyaona makaburi ya maulamaa wao yakiwa yameharibika, yakipigwa na jua, hakuna kizuizi chochote juu yake au chumba ambacho mwenye kuyatembelea anaweza kujikinga jua kwenye kivuli chake. Kisha ukenda kwa Wakiristo, na ukakuta makaburi ya maulamaa wao yakiwa yamejengewa vizuri na kuhifadhika, yakiwa yamejengewa makuba na yakiwa yamepambwa kwa dhahabu na fedha, na mapambo mengine ya madini mbali mbali. Je ni maulamaa gani utakao waona kuwa ni wenye utukufu, ni maulamaa wa Mayahudi au Wakiristo, pamoja na kuwa unafahamu ya kuwa wewe ni Muislaam na unafahamu ya kuwa wote wawili wako kwenye batili?

KHALID : Bila shaka kutokana na mandhari ya makaburi ya pande mbili niliyo yaona nitachukua picha fulani ya utukufu wa maulamaa wa Wakiristo, na picha ya udhalili wa maulamaa wa Mayahudi.

BAAQIR : Kwa hivyo basi wayafanyayo Mashia na Masunni kwa kujenga madharihi juu ya makaburi, na kujenga haram na makuba na mengineyo juu ya makaburi ya maimamu na Mitume.. ni kwa ajili ya kuwatukuza wao na kuwaenzi, kwa sababu hiyo huyapamba kwa Dhahabu Fedha na mapambo mengine ya madini mbali mbali.

KHALID : Yote hayo ni sahihi lakini je jambo hilo linakitoa kitendo hicho kwenye sifa ya israfu na matumizi mabaya na yasiyo ya lazima?.BAAQIR : Ndio, na zaidi ya hapo. Ikiwa itathibiti kuwa matendo haya ni kuwatukuza mawalii wa Mwenyezi Mungu, wakati huohuo ni kuutukuza Uislaam, kwani kuwatukuza viongozi na watukufu wa Uislaam ni kuutukuza Uislaam, na kila kitu ambacho ndani yake kuna kuutukuza Uislaam basi kitu hicho ni katika shiari za Mwenyezi Mungu ambazo Mwenyezi Mungu amesema kuhusiana nazo:Kwa hivyo basi kuyapamba makaburi ya mawalii wa Mwenyezi Mungu ni katika shiari za Mwenyezi Mungu ambazo ni sunna kuzifanya na kufanya kazi kwa ajili yake, na mtu mwenye kufanya hivyo hupewa thawabu kwa matendo yake hayo. KHALID : Nakuomba samah ani, kwa kuchukua kiasi hiki cha wakati wako lakini mbele ya Mwenyezi Mungu ni mwenye malipo, kwani umenitoa kwenye kiza cha ujinga na kuniweka kwenye nuru ya elimu na ufahamu, ni kwa kiasi gani nilikuwa nikifikiria kuhusiana na upambaji huu wa makaburi na nisielewe siri yake na faida yake na usahihi wake, kwa hakika hivi leo-wewe- umenitia nuru kwa elimu yako hii, na umenifikisha niliko kuwa nikipakusudia.

BAAQIR : Sasa shaka yote uliyo kuwa nayo kuhusiana na kupamba makaburi imetoweka?

KHALID : Ndio.. hakuna shaka yoyote niliyo bakia nayo kwani kufanya hivyo ni sunna na jambo lililo himizwa na Qur'ani tukufu kwa kauli yake Mwenyezi Mungu:

BAAQIR : Alaa ayyi hal (Kwa hali yoyote ele):Hakika mimi niko tayari kufahamiana nawe katika maudhui kama haya ili niweze kufaidika, au wewe pia ufaidike, na wote kwa pamoja tuwe ni wenye kuyafahamu mambo kwa ufahamu mzuri na wenye mazingatio.

KHALID : Ninakushukuru sana sana, na ninamuomba Mwenyezi Mungu mtukufu akuwafikishe kwa yale ayaridhiayo.

7 UKWELI WA USHIA

KUBUSU MADHARIHI (MAKABURI)

MAALIK: Ewe Swaadiq ni sababu gani iwafanyayo kubusu Dharihi ya kaburi la Mtume na maimam na kutoacha kitendo hicho?

SWAADIQ: Je kuna tatizo (ishkali) lolote kufanya hivyo?

MAALIK: Inasemekana kuwa kufanya hivyo ni miongoni mwa matendo ya shirki.

SWADIQ: Nani asemae kuwa kufanya hivyo ni shirki?

MAALIK: Waislaam ndio wasemao hivyo.

SWADIQ: Ajabu! Basi ni watu gani ambao wanabusu madharihi?MAALIK: Inasemekana kuwa ni kikundi kidogo cha Mashia.

SWADIQ: Je umewahi kwenda hija?

MAALIK: Ninamshukuru Mwenyezi Mungu.. ndio nimefanikiwa kwenda hija.

SWADIQ: Je umelitembelea kaburi la Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w) katika mji wa Madinah?

MAALIK: Ninamshukuru Mwenyezi Mungu nimefanikiwa kulitembelea.SWAADIQ: Je hukuwaona maelfu ya waislaam wa madhehebu ya sunni wakikusudia na kutaka kulibusu dharihi la kaburi la Mtume wa Mwenyezi Mungu na huku wakipigwa na walinzi wa kikundi cha (Hay'atu amri bil-maarufi)?!!

MAALIK: Ndio..

SWAADIQ: Kwa maana hiyo si sisi Mashia pekee tunao busu madharihi ya Mitume wa Mwenyezi Mungu, bali waislaam wote huyabusu.

MAALIK: Sasa kwanini baadhi wanasema kuwa kufanya hivyo ni haram, na kwamba kufanya hivyo ni kumshirikisha Mwenyezi Mungu mtukufu?

SWAADIQ: Hawa ni watu wachache wa kikundi fulani kati ya makundi ya waislaam, wajionao kuwa wao ndio wenye haki, na kwamba wao ndio waislam wa kweli na wanawaona waislaam wengine kuwa ni makafiri na washirikina wanamuabudu asie kuwa Mwenyezi Mungu, na hawawaoni watu wengine kuwa ni waislaam walio kosea, kwa hivyo ndio maana huwaona wakiyakufurisha madhehebu (makundi) mengine yote ya kiislaam. Je hukuona ile kamati ya (Al-amri bil-maarufi)!! katika nchi ya Hijazi wakimpiga anaekusudia na kutaka kubusu dharihi la kaburi la Mtume(s.a.w.w) na kumwambia:Ewe kafiri! Ewe mshirikina! Ewe zindiki! Ewe nguruwe! Ewe mbwa! Na mengineyo kati ya aina mbali mbali za matusi na tuhuma zilizo mbaya kabisa.

Na matusi hayo humuelekea kila mtu: Sawa awe Shia, Hanafiy, Maalikiy, Shafiiy, Hanbaliy, Zaydiah, na waislaam wengine..[17]

MAALIK: Ndio.. yote hayo nimeyaona, na yaliyo mabaya zaidi kuliko hayo: Kwa hakika mimi niliwaona wakimpiga kichwani mtu mmoja alie ng'ang'ania kufanya hivyo kwa fimbo kiasi kwamba huenda pigo hilo lilipelekea kumpasua na kutoka damu, na wakati mwingine huwapiga kwa mikono yao-kwa nguvu- na wakiwapiga vifuani waislaam walio kuja kufanya ziara mapigo ambayo huwaumiza na kuwadhuru vifua vyao na kuwasababishia maumuvu na maradhi miili yao! Na ni kwa kiwango gani niliumia kwa kuyao mambo hayo na vitendo hivyo!!.

Hija ambayo Mwenyezi Mungu ameifanya kuwa ni kongamano la waislaam wote ulimwenguni ili waweze kuzungumza katika kongamano hilo kuhusu mambo yao mbali mbali, hivi leo imekuwa ni mahala pa kutia tofauti kati ya waislaam kutokana na matendo ya kikundi hicho kidogo kinacho jiita kuwa ni (hay'atul-amri bil-maaruf wannahyi anil-munkar)!!!.SWAADIQ: Ala ayyi hal, ewe Maalik.. je wewe unambusu mwanao?MAALIK: Ndio!

SWADIQ: Je unamshirikisha Mwenyezi Mungu mtukufu kwa kumbusu mwanao?

MAALIK: Hapana, hapana.. kamwe simshirikishi Mwenyezi Mungu.SWADIQ: Vipi usimshirikishe Mwenyezi Mungu kwa kumbusu mwanao?MAALIK: Kwa hakika mimi ninambusu mwanangu kwa ajili ya mapenzi yangu kwake, na hilo si shirki.

SWADIQ: Je wewe unaibusu Qur'ani?

MAALIK: Ndio.

SWADIQ: Je kwa kufanya kwako hivyo humshirikishi Mwenyezi Mungu?

MAALIK: Hapana.

SWADIQ: Je jalada la Qur'ani unalo libusu si ngozi ya mnyama?MAALIK: Ndio.

SWADIQ: Kwa hivyo wewe unamshirikisha Mwenyezi Mungu, na unaifanya ngozi ya mnyama kuwa ni mshirika wa Mwenyezi Mungu.. ametakasika Mwenyezi Mungu na hilo.

MAALIK: Si hivyo. Kwa hakika mimi ninaibusu Qur'ani kwa sababu imekusanya maneno ya Mwenyezi Mungu, kutokana na mapenzi ya maneno ya Mwenyezi Mungu ndio maana ninalibusu jalada lililo ifunika Qur'ani hiyo, na hii ni kutokana na mapenzi mengi, na wingi wa shauku yangu kwa Qur'ani, ni tofauti iliyoje kati ya kitendo hiki na kumshirikisha Mwenyezi Mungu?

Kisha ninapo ibusu Qur'ani ninapata thawabu kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa kufanya hivyo, kwa sababu kuibusu Qur'ani ni kuitukuza na kuienzi na kuiinua daraja yake, na kuitukuza Qur'ani kuna thawabu na malipo mbele ya Mwenyezi Mungu, kwa hivyo ni tofauti iliyoje iliyopo kati ya tendo hili na kumshirikisha Mwenyezi Mungu?

SWADIQ: Kwa nini maneno kama hayo usiyasema katika kubusu dharihi la Mtume(s.a.w.w) na madharihi ya maimam(a.s) [18] au unadai ya kuwa wale ambao wanabusu madharihi huvifanya vyuma hivyo kuwa ni washiriki wa Mwenyezi Mungu mtukufu?! Ikiwa ni hivyo kwanini hawabusu vyuma mbali mbali vilivyoko huku na kule katika ardhi? Lakini..kutokana na ukweli kuwa dharihi hilo limefunika kaburi la Mtume(s.a.w.w) au kaburi la mmoja wapo kati ya maimamu(a.s) , kutokana na mapenzi ya Mtume(s.a.w.w) na maimamu na kutokana na shauku yao kwao ndio maana wanalibusu dharihi la kaburi lake kwa sababu wao hawawezi kumfikia Mtume na imamu mwenyewe(a.s).

Pamoja na kufanya kwao hivyo hakika wao hupata malipo kwa Mwenyezi Mungu mtukufu, na hupawa thawabu kwa kufanya hivyo, kwani kulibusu dharihi la mtu fulani ni kumtukuza mtu yule. Na kumtukuza Mtume(s.a.w.w) au mmoja wapo kati ya maimamu(a.s) , ni kuutukuza Uislaam ambao huyu alikuwa ni Mtume wake(s.a.w.w) au alikuwa ni imamu wake alie kuwa akilingania watu kwenye Uislaam huo.

Na jambo lolote litakapo kuwa na sura ya kuutukuza Uislaam basi jambo hilo ni katika shiari za Mwenyezi Mungu ambazo amezizungumzia kwa kusema:suratul-haji aya 32.

MAALIK: Ikiwa ukweli ni huo basi kwanini baadhi ya watu wanasema kuwa nyinyi ni wenye kumshirikisha Mwenye zi Mungu?

SWAADIQ: Imepokelewa katika Hadithi tukufu kama ifuatavyo:(Kwa hakika matendo hufanyika kutokana na Nia) [19] ikiwa mtu yeyote anabusu dharihi na katika kubusu kwake huko anakusudia kumshirikisha Mwenyezi Mungu bila shaka mtu huyo ni mwenye kumshirikisha Mwenyezi Mungu (mshirikina). Na ikiwa kubusu huku kunatokana na mapenzi mengi, na kwa ajili ya kupata thawabu kwa ajili ya kuadhimisha na kutukuza shiari za Mwenyezi Mungu kwa kufanya hivyo, basi hupewa thawabu yule mwenye kuyatekeleza matendo hayo. Na wewe waulize wote wale ambao wanayabusu madharihi kati ya Mashia na Masunni kama ifuatavyo: Kwa nini mnabusu madharihi?

Hata kujibu yeyote kati yao isipokuwa kwa kusema tunafanya hivyo kutokana na mapenzi makubwa na shauku kubwa tuliyo nayo na kwa ajili ya kupata thawabu, na huwezi kumsikia yeyote kamwe-bila shaka yoyote- akisema ya kuwa anabusu dharihi kwa ajili ya jambo lingine tofauti na hili tulilo litaja.

MAALIK: Ni kweli, maneno yako ni sahihi.

SWADIQ: Na ikiwa kubusu peke yake bila kukusudia kumshirikisha Mwenyezi Mungu kunamfanya mtu kuwa mshirikina, bila shaka huwezi kumpata mwanadamu yeyote asie mshirikina, kwani waislaam imma wanabusu madharihi, au wanabusu Qur'ani.. kwa msingi wa hali mbili hizi wao-wote-ni washirikina. Sasa ikiwa hali ni kama hiyo Muislaam ni nani?

MAALIK: Ninakushukuru sana, na kwa hakika mimi nitafanya mazungumzo na majadiliano na baba yangu alie kuwa akinilisha na kunifundisha mambo kama haya ya asabia yasiyo na maana yoyote, na sinto sikiliza maneno ya mtu yeyote wa madhehebu mengine, kwa hakika nimefahamu ya kuwa haki na ukweli uko pamoja nanyi-nyinyi Mashia- na wewe unahaki juu yangu milele, kwa sababu umenionyesha njia, si katika jambo hili tu bali katika mambo yote, ili nisifuate kila kinifikiacho masikioni mwangu, bila ya kufikiria kuhusu usahihi wake na ubatilifu wake.


3

4