ILI NIWE PAMOJA NA WAKWELI

ILI NIWE PAMOJA NA WAKWELI 20%

ILI NIWE PAMOJA NA WAKWELI Mwandishi:
Kundi: Midahalo na majadiliano kielimu

ILI NIWE PAMOJA NA WAKWELI
  • Anza
  • Iliyopita
  • 21 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 37848 / Pakua: 4636
Kiwango Kiwango Kiwango
ILI NIWE PAMOJA NA WAKWELI

ILI NIWE PAMOJA NA WAKWELI

Mwandishi:
Swahili

1

2

3

4

5

6

7

11

ILI NIWE PAMOJA NA WAKWELI

ISMAH

Mashia wanasema:"Tunaitakidi kwamba Imam ni kama Nabii, ni wajibu awe Maasum (mwenye kuhifadhika) kutokana na machafu yote na maovu yenye kudhihiri na yenye kufichikana tangu miaka ya utotoni mpaka kufa (asiyafanye hayo) kwa kukusudia au kusahau. Kama ambavyo ni wajibu Imam awe amehifadhiwa kutokana na kusahau, kukosea na kughafilika, kwa sababu Maimamu ndiyo walinzi wa sheria na ndiyo wenye kuisimamia, hivyo hali yao katika jambo hilo ndiyo hali ya Mtume. Dalili ambayo imetupelekea tuitakidi Ismah ya Manabii ndiyo hiyo hiyo iliyotupelekea tuitakidi Ismah ya Mamimau bila tofauti yoyote. Taz: Aqaidul-Imamiyah uk. 67. Naam hivi ndivyo tunavyoona, haya ni maoni ya Mashia kuhusu maudhui ya Ismah basi je, ndani ya itikadi hii kuna kitu kinachopinga Qur'an na Sunna? Au kuna ambacho akili inakipinga? Au kuna ambacho kinauharibu Uislamu na kuuvuruga, au kipo kinachoshusha heshima ya Mtume au Imam?

Hapana, kamwe hatukukuta ndani ya kauli hii isipokuwa ni kukiunga mkono kitabu cha Mwenyezi Mungu na sunna ya Mtume wake, na mambo ambayo yanakubaliana na akili iliyo salimika na wala hakuna kinachoipinga, na yamo mambo ambayo yananyanyua heshima ya Mtume na Imam na kumtukuza. Basi hebu na tuanze utafiti wetu kwa kuisoma Qur'an Tukufo. Mwenyezi Mungu amesema: "Hakika Mwenyezi Mungu anataka kukuondoleeni uchafu na kukutakaseni sana enyi watu wa nyumba (ya Mtume)". Qur'an, 33:33 Iwapo kuondoshewa uchafu ambako kunakusanya mambo mabaya, na kutakaswa kutokana na kila dhambi hakufidishi Ismah, basi ni nini maana yake? Mwenyezi Mungu anasema: "Hakika wale wanaomuogopa (Mwenyezi Mungu) zinapowagusa pepeso za shetani hukumbuka, basi mara huwa wamekwishaiona njia". (Qur'an, 7:201) Ikiwa Muumini mcha Mungu, Mwenyezi Mungu humuhifadhi kutokana na vitimbi vya Shetani pindi anapojaribu kumwita na kumpotosha, Muumini hukumbuka na kuiona haki kisha huifuata, hivyo basi unafikirije kwa yule ambaye Mwenyezi Mungu amemteua na akamuondoshea uchafu na kumtakasa sana sana?

Na anasema Mwenyezi Mungu: "Kisha tumewarithisha (tumewapa) kitabu wale tuliowachagua miongoni mwa waja wetu". (Qur'an, 35:32) Na yeyote achaguliwaye na Mwenyezi Mungu Mtukufu bila shaka anakuwa ni Maasum (aliyehifadhiwa) kutokana na makosa. Aya hii ndiyo aliyoitolea hoja Imam Ridhaa ambaye yeye ni miongoni mwa Maimamu wa nyumba ya Mtume (s.a.w.) dhidi ya wanachuoni aliowakusanya Khalifa wa Kibani Abbas aitwaye Maamum bin Harun Rashid. Imam aliwathibitishia kwamba wao Maimamu wa nyumba ya Mtume ndiyo waliokusudiwa kwenye aya hii, na kwamba Mwenyezi Mungu amewachagua na kuwarithisha wao elimu au Kitabu (Qur'an), na hao wanachuoni walimkubalia juu ya jambo hilo. Taz: Al-I'Qdul-Farid cha ibn Abdirabbih Juz. 3 uk. 42.

Hii ni baadhi ya mifano iliyokuja ndani ya Qur'an Tukufu, na ziko aya nyingine zinazofidisha juu ya Ismah ya Maimamu, kama vile kauli yake Mwenyezi Mungu isemayo: "Maimamu wanaoongoza kwa amri yetu." Na nyinginezo, lakini tunatosheka kwa kiasi hiki kwa nia ya kufupisha maelezo. Na baada ya Qur'an Tukufu hebu angalia maelezo yaliyokuja ndani ya sunna ya Mtume. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) amesema: "Enyi watu hakika mimi ninaacha kwenu vitu ambavyo mkivichukua hamtapotea, Kitabu cha Mwenyezi Mungu na kizazi changu watu wa nyumba yangu": Taz: 1). Sahih Tirmidhi Juz. 5 uk. 328. 2). Al-Hakim ndani ya Mustadrak Juz. 3 uk. 148. 3). Al-Imam Ahmad bin Hambal ndani ya Musnad yake Juz. 5 uk. 189. Kama unavyoona bayana kwamba Maimamu kutoka nyumba ya Mtume (s.a.w.) wamehifadhiwa. Kwanza: Ni kwa kuwa Kitabu cha Mwenyezi Mungu kimehifadhiwa, hakifikwi na upotofu kabla au baadaye ni maneno ya Mwenyezi Mungu, na mwenye kukitilia shaka basi amekufuru. Pili: Ni kwamba mwenye kushikamana navyo "Kitabu na kizazi cha Mtume" atasalimika kutokana na upotofu. Hivyo basi hadithi hii imejulisha kwamba kitabu na kizazi cha Mtume haiwezekani kuwa vinamakosa. Na amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.): "Bila shaka mfano wa watu wa nyumba yangu ni kama Safina ya Nuhu, atakayeipanda ataokoka na mwenye kuiacha ataangamia".

Taz: Mustadrak Al-Hakim Juz. 2 uk. 343, Kanzul-Ummal Juz. 5 uk. 95, As-sawaiqul-Muhriqah cha ibn Hajar uk. 184. Kama uonavyo ubainifu kuwahusu Maimamu kutoka nyumba ya Mtume (s.a.w.) kwamba wao ni Maasum (wamehifadhiwa) kutokana na makosa, na kwa ajili hiyo husalimika kila apandaye Safina yao na kila atayeacha kupanda Safina hiyo ataangamia katika upotofu. Na amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.): "Yeyote atakayependa kuishi maisha niliyoishi mimi na afe kifo nilichokufa mimi na aingie ndani ya pepo ambayo Mola wangu ameniahidi nayo ni pepo ya milele, basi na amtawalishe Ali na watoto wake baada yake, bila shaka wao hawatakutoweni nje ya mlango wa uongofu na hawatakuingizeni ndani ya mlango wa upotofu". Taz:

1) Kanzul-Ummal Juz. 6 uk. 155.

2). Maj-Mauz-Zawaid cha Al-Haithami Juz. 9 uk. 108.

3). Al-isabah cha Ibn Hajar Ai-As-Qalani.

4). At-Tabrani ndani ya Al-Jamiul-Kabir.

5). Tarikh Ibn AsakirJuz. 2 uk. 99.

6). Mustadrak Al-Hakim Juz. 3 uk. 128

7). Hilyatul-Auliyai Juz. 4 uk. 349. 8). Ihqaqul-Haqi Juz. 5 uk. 108.

Kama uonavyo ya kwamba Maimamu kutoka katika nyumba ya Mtume (s.a.w.) ambao ni Ali na wanawe,

wamehifadhiwa kutokana na makosa kwani wao kamwe hawatawaingiza watu waliowafuata katika mlango wa upotofu. Na hapana upinzani kwamba mtu anayekosea haiwezekani kwake kuwaongoa watu.

Na amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.):

"Mimi ni muonyaji na Ali ni muongozaji, na kwako ewe Ali wataongoka wenye kuongoka baada yangu:

Taz: 1). Tafsir At-Tabari Juz. 13 uk. 108.

2). Tafsir Ar-Razi Juz. 5 uk. 271.

3). Tafsir ibn Kathir Juz. 2 uk. 502.

4). Tafsir Ash-Shaukani Juz. 3 uk. 70.

5) Ad-Durrul-Manthoor cha Suyuti Juz. 4 uk. 45.

6). Nurul-Ab-Sar uk. 71.

7). Mustadrak Al-Hakim Juz. 3 uk. 129.

8). Tafsir ibn JauziJuz. 4 uk. 307.

9). Shawahidut-TanzilJuz. 1 uk. 293.

10). A 1-Fusulul-Muhimmah Na yanabiul-Mawaddah.

Hii ni hadithi nyingine iliyo bayana kabisa kuhusu Ismah ya Imam kama ambavyo haifichikani kwenye akili. Imam Ali kwa nafsi yake mwenyewe ameithibitisha Ismah kwake mwenyewe na kwa Maimamu miongoni mwa wanawe pale aliposema: "Mnakwenda wapi na ni vipi mnadanganywa hali ya kuwa muongozo upo na aya ziko wazi na minara imesimikwa, basi vipi mnapotoshwa bali ni jinsi gani mnapotea hali yakuwa miongoni mwenu kimo kizazi cha Nabii wenu ambao ni walinzi wa haki, na ndiyo muongozo wa dini na ndimi za ukweli, basi waheshimuni kwa heshima nzuri ya Qur'an na muwafuate kama ngamia mwenye kiu kali afuatavyo (maji). Enyi watu kichukuweni kutoka kwa Mtume wa mwisho (s.a.w.), hakika hufariki mwenye kufariki miongoni mwetu (sisi watu wa nyumba ya Mtume) lakini anakuwa hajafariki, na huchakaa mwenye kuchakaa miongoni mwetu lakini siyo kwamba amechakaa, basi msiseme msiyoyajua, kwani haki imo ndani ya vile mnavyovikanusha. Na toshekeni kwa mtu ambaye ninyi hamna hoja yoyote dhidi yake, nami ndiye huyo mtu, basi je, sikukitumia ndani yenu kizito kikubwa na ninakuachieni kizito kidogo nami nimesimika kwenu bendera ya Imani..."[92]

Taz: Nahjul-Balaghah ya Imam Ali Juz. 1 uk. 155. Na baada ya ubainifu huu kutoka ndani ya Qur'an Tukufu na sunna tukufu ya Mtume na kauli za Imam Ali ambazo zote zinajulisha juu ya Ismah yao (a.s.) basi hivi kweli akili itapinga Ismah ya wale aliowachagua Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa ajili ya uongofu? Jawabu ni kwamba, kamwe haiwezi kupinga, kinyume chake ni kwamba akili inasema kuwa, kuna ulazima wa kuwepo hiyo Ismah kwani yeyote ambaye amewakilishwa wajibu muhimu wa uongozi na kuongoa watu haiwezekani awe ni mtu wa kawaida anayezukiwa na makosa, kusahau na kisha kushehenezwa madhambi na makosa halafu aaibishwe na akosolewe na watu. Bali akili inaona ni lazima awe mjuzi mno kuliko wengine katika zama zake na muadilifu, mchamungu, na shujaa kuliko wote, sifa ambazo zinapandisha cheo cha kiongozi na kumtukuza mbele za watu na kumletea heshima kwa wote na utukufu na hatimaye wakamtii bila ya woga.

Ikiwa hali ya mambo iko namna hiyo, basi yanini kebehi yote hii na vitisho dhidi ya wanao itakidi hivyo? Bila shaka imasikia na kusoma Masunni wanavyoikosoa maudhui ya Ismah kwa kusema kwamba, Mashia ndiyo wanaomvisha nishani ya Ismah yule wampendaye, au yeyote azungumzaye kuhusu kuthibiti kwa Ismah (kwao wao) huwa amesema jambo bay a na la kufru, basi si hili wala lile, bali Ismah kwa Mashia ni kuwa huyo Maasum awe amezungukwa na uangalizi na uhifadhi wa Mola ili shetani asiweze kumpoteza, na wala nafsi inayoamrisha maovu isiweze kuishinda akili yake ikampeleka kwenye maasi. Jambo hili Mwenyezi Mungu hakuliharamisha kwa waja wake wamchao kama ilivyotangulia katika ay a isemayo: "Wale ambao wamchao Mwenyezi Mungu unapowapata upepeso wa Shetani hukumbuka, basi mara huiona haki". Na hii Ismah iliyokadiriwa kwa waja wa Mwenyezi Mungu huenda ikaondoka kwa kukosekana sababu zake ambazo ni ucha Mungu kwa hiyo mja atakapokuwa mbali na ucha Mungu Mwenyezi Mungu hawezi kumuhifadhi. Ama Imamu ambaye Mwenyezi Mungu amemchagua, huyo hapotoki wala kulegalega kwenye ucha Mungu na kumuogopa Mwenyezi Mungu Mtukufu.

- Bila shaka imekuja ndani ya Qur'an simulizi juu ya Bwana wetu Yusuf (a.s.): "Kwa'hakika mwanamke huyo alimkusudia (Yusuf) na (Yusuf) naye angemkusudia mwanamke yule, lau kama asingeona dalili toka kwa Mola wake, tumefanya hivyo ili tumwepushie kila jambo la ubaya na la uovu. Hakika yeye (Yusuf) ni miongoni mwa waja wetu waliotakaswa". (Qur'an, 12:24) Na kwa sababu Bwana wetu Yusuf hakukusudia kufanya zinaa kama walivyofasiri baadhi ya wafasiri, kwani haiwezekani kabisa kwa Manabii wa Mwenyezi Mungu kufanya tendo hili baya.

IDADI YA MAIMAMU (NI KUMI NA WAWILI)

Mashia wanasema kwamba idadi ya Maimamu Ma'asum baada ya Mtume (s.a.w.) hi kumi na wawili, hawazidi wala kupungua, na Mtume wa Mwenyezi Mungu amewataja kwa majina yao na idadi yao. Taz: Yanabiul-Mawaddah cha Al-Qanduzi Al-Hanafi uk. 99 Juz. 3. Nao ni hawa wafuatao:

1) Imam Ali bin Abi Talib

2) Imam Hasan bin Ali

3) Imam Husein bin Ali

4) Imam Ali bin Husein (Zainul-Abidin)

5) Imam Muhammad bin Ali (Al-Baqir)

6) Imam Ja'afar bin Muhammad (As-Sadiq)

7) Imam Musa bin Ja'afar (Al-Kadhim)

8) Imam Ali bin Musa (Ar-Ridha)

9) Imam Muhammad bin Ali (Al-Jawad)

10) Imam Ali bin Muhammad (Al-Hadi)

11) Imam Al-Hasan bin Ali (Al-Askari)

12) Imam Muhammad bin Al-Hasan (Al-Mahdi)

Basi hawa ndiyo Maimamu kumi na wawili ambao Mashia wanazungumza kuhusu Ismah yao ili baadhi ya Waislamu wasijegubikwa na vitimbi. Hivyo basi Mashia hawaitambui hapo zamani wala sasa hivi Ismah nyingine isiyokuwa ya Maimamu hawa ambao Mtume wa Mwenyezi Mungu aliwataja kabla hata hawajazaliwa, na baadhi ya wanachuoni wa Kisunni wameyathibitisha majina yao (hao Maimamu) kama ilivyotangulia (kuelezwa). Nao Bukhar na Muslim wamethibitisha ndani ya Sahih zao hadithi inayohusu Maimamu kwa idadi yao ambayo ni kumi na wawili na wote ni kutokana na Qur'aish. Taz: 1). Sahih Bukhar Juz. 8 uk. 127. 2). Sahih Muslim Juz. 6 uk. 3. Na hadithi hizi hazisimami wala hazisihi isipokuwa tutakapozifasiri kuwahusu Maimamu wa nyumba ya Mtume ambao Mashia Imamiyah ndiyo wanaowazungumzia, na Masunni wao ndio wanaotakiwa kutatua utata huu, kwani idadi ya Maimamu kumi na wawili ambayo wameithibitisha ndani ya vitabu vyao mpaka sasa kwao imebakia kuwa ni fumbo ambalo hawalipatii jawabu!

ELIMU YA MAIMAMU

Na miongoni mwa mambo ambayo Masunni huwakebehi Mashia ni kauli ya Mashia isemayo kwamba: "Maimamu kutoka katika nyumba ya Mtume (s.a.w.), Mwenyezi Mungu amewahusisha na elimu ambayo hakuwashirikisha pamoja na yeyote miongoni mwa watu, na kwa kuwa Imamu ni mjuzi mno kuliko watu wote wa zama zake, basi haiwezekani kwa yeyote kumuuliza Imam kisha akashindwa kutoa jawabu!! Basi je, madai haya yanayo dalili? Na tuanze na Qur'an kama ilivyo kawaida yetu katika kila uchambuzi tunaoufanya.. Mwenyezi Mungu anasema: "Kisha tumewarithisha (tumewapa elimu ya) kitabu wale ambao tumewateua miongoni mwa waja wetu". (Qur'an, 35:32) Aya hii inajulisha dalili iliyo wazi kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu ameteua waja miongoni mwa watu na akawarithisha elimu ya Kitabu.

Basi je, tunaweza kuwafahamu waja hawa walioteuliwa? Hapo kabla tumeeleza kuwa Imamu wa nane miongoni mwa wale Maimamu wanaotoka katika nyumba ya Mtume (s.a.w.) ambaye ni Ali bin Musa Ar-Ridhaa alitoa ushahidi ya kuwa aya hii ilishuka kuwahusu wao, na hali hii (aliisema) pindi Maamuni (Khalifa wa Banu Abbas) alipomkusanyia Imam (huyu) Maqadhi arobaini miongoni mwa Maqadhi mashuhuri, na kila mmoja wa Maqadhi hawa aliandaa mas-ala arobaini ili kumuuliza Imam Ali Ar-Ridhaa. Basi Imam (a.s.) aliwanyamazisha (alipowajibu wote bila kubabaika) na wao wakakiri kuwa yeye Imam ni mjuzi mno. ; Taz: Al-Iqdul-Farid cha ibn Abd Rabbih Juz. 3 uk. 42. Hivyo basi, ikiwa Imam huyu wa nane ambaye alikuwa hata hajafikia umri wa miaka kumi na minne wakati wa majadiliano kati yake na wanachuoni hao ambao walikiri juu ya elimu yake, basi vipi ishangaze (na kuwa ngeni) kauli ya Mashia isemayo kuwa Maimamu ni wajuzi mno, maadamu wanachuoni wa Kisunni wanakiri kuhusu hali hiyo kwa Maimamu. Ama tukitaka kufasiri Qur'an kwa Qur'an, basi tutapata aya nyingi zinazoelekeza maana moja, na zinabainisha kwamba Mwenyezi Mungu kwa hekima yake amewahusisha Maimamu kutoka ndani ya nyumba ya Mtume (s.a.w.) kwa elimu itokayo kwake, amewapa ili wawe ni Maimamu wa uongofu na taa za kuondosha kiza.

Mwenyezi Mungu anasema: "Humpa hekima amtakaye, na yeyote aliyepewa hekima, basi bila shaka amepewa kheri nyingi, na hawakumbuki ila wenye akili". (Qur'an, 2:269) Na amesema vile vile: "Basi ninaapa kwa maangukio ya nyota, na bila shaka hicho ni kiapo kikubwa lau kama mngejuwa, hakika hii ni Qur'an Tukufu, iliyowekwa ndani ya Kitabu kilichohifadhiwa (madhubuti) hapana atayekigusa (kukifahamu vyema) isipokuwa wale waliotakaswa". (Qur'an, 56:75-79) Mwenyezi Mungu ameapa katika aya hii kwa kiapo kikubwa ya kwamba Qur'an Tukufu inazo siri na maana za ndani zilizodhibitiwa, hawawezi kutambua maana zake na uhakika wake isipokuwa wale waliotakaswa, na hao waliotakaswa ni wale ambao Mwenyezi Mungu amewaondolea uchafu na amewatakasa sana sana.

Pia aya imejulisha kwamba, Qur'an ina undani ambao Mwenyezi Mungu amewahusisha kwa undani huo Maimamu wa nyumba ya Mtume (s.a.w.) na wala haiwezekani kwa asiyekuwa wao kuufahamu undani huo isipokuwa kupitia kwao. Hivyo basi Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) ameelekeza juu ya ukweli huu akasema: "Msiwatangulie (Maimamu) mutaangamia, na wala msiwapuuze mtaangamia, na wala msiwafunze kwani wao ni wajuzi mno kuliko ninyi". Taz:

1). As-sawa'iqul-Muhriqah cha ibn HajarAsh-Shqfti uk. 148.

2). Ad-Durrul-Manthoor cha Suyuti Juz. 2 uk. 60.

3). Kanzul-UmmalJuz. 1 uk. 168.

4). Usudul-Ghabah Fii Maa'rifatis Sahabah Juz. 3 uk. 137.

Na kama alivyosema Imam Ali mwenyewe:

"Wako wapi wale waliodai kuwa wao wamebobea katika elimu kuliko sisi, huo ni uongo na ni dhulma dhidi yetu, Mwenyezi Mungu ametunyanyua sisi na wao akawatweza, na ametupa sisi wao akawanyima, na ametuingiza sisi wao akawatoa, kwetu sisi ndiko kunakoombwa uongofu na upotofu huondoka... Hakika Maimamu wanatokana na Quraish wamepandikizwa ndani ya tumbo hili toka kwa Hashim, haukubaliki Uimamu kwa asiyekuwa wao wala utawala haukubaliki toka kwa asiyekuwa wao." Taz: Nahjul-Balaghah Juz. 2 uk. 143, Muhammad Abdoh, Khutba namba 143. Na amesema Mwenyezi Mungu: "Waulizeni wenye kumbukumbu iwapo ninyi hamujui" (Qur'an, 16:43 na 21:7). Aya hii vile vile imeshuka kuwahusu Ahlul-Bait (a.s.).

Taz: 1). Tafsirut-Tabari Juz. 14 uk. 134. 2). Tafsir ibn Kathir Juz. 2 uk. 570. 3). Tafsirul-Qur-tubi Juz. 11 uk: 272. ;,. 4). Shawahidut-Tanzil cha Al-Haskani Juz.luk. 334. 5). Yanabiul-Mawaddah. 6). Ih-Qa-Qul-Haqq cha At-Tustari Juz. 3 uk. 482. Na inafidisha kwamba umma (wa Kiislamu) baada ya kuondoka kwa Mtume wake hauna budi kuwarejea Maimamu wanaotoka katika nyumba ya Mtume (s.a.w.) ili kuufahamu ukweli, na bila shaka Masahaba (r.a.) walimrejea Imam Ali bin Abi Talib ili awabainishie yaliyokuwa yakiwatatiza, kama ambavyo watu walivyowarejea Maimamu wa nyumba ya Mtume kwa miaka mingi ili wapate kufahamu halali na haramu na wapate (kunywa) elimu yao na mwenendo wao. Na iwapo Abu Hanifah anasema: "Lau si miaka miwili, basi Nuu'man angeangamia" akikusudia miaka miwili aliyoitumia kusoma kwa Imam Jaa'far Sadiq (a.s.) Na Imam Malik naye anasema: "Jicho halijaona wala sikio halijasikia, wala halijapita wazo katika moyo wa mtu yeyote (kuwa kuna) mbora kuliko Jaafar As-Sadiq kwa utukufu, elimu, ibada, na ucha Mungu" Taz: Kitabu Manaqib Ali bin Abi Talib kuhusu mazingira ya Imam Jaafar As-Sadiq. Kama mambo yako namna hii, Maimamu wa Kisunni wanakiri, basi ni za nini kebehi zote hizi na upinzani huu ni wa nini baada ya kuwepo dalili zote hizi na (hasa) baada ya historia ya Waislamu wote (kukubali) kwamba Maimamu toka katika nyumba ya Mtume (s.a.w.) walikuwa ni wajuzi mno kuliko watu wote wa zama zao? Basi ajabu iko wapi kwa Mwenyezi Mungu kuwahusisha mawalii wake aliowachagua (akawahusisha) kwa hekima na elimu, akawafanya kuwa ni kigezo cha waumini na kuwa viongozi wa Waislamu?

Lau Waislamu wangelifuatilia dalili za wao kwa wao, bila shaka wangetosheka na kauli ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wangekuwa umma mmoja unaopeana nguvu na pasingekuwa na tofauti wala madhehebu mengi. Lakini hapana budi yatokee yote hayo ili Mwenyezi Mungu apate kupitisha jambo ambalo lilikuwa lazima litendeke:"Kusudi aangamiae, aangamie kwa dalili iliyo wazi na anayezindukana azindukane kwa dalili iliyo wazi na Mwenyezi Mungu ni msikivu mjuzi" (Qur'an 8:42)

AL-BADA'U

Al-Bada'u: Ni kumdhihirikia kitu katika jambo fulani alilotaka kulifanya kisha rai yake kubadilika kuhusu jambo hilo na akafanya kitu ambacho hakuwa ameazimia kukifanya hapo kabla. Ama kauli ya Mashia kuhusu Al-Bada'u na kuinasibisha kwa Mwenyezi Mungu, na kebehi dhidi yao kwamba (Al-Bada'u) inawajibisha kutokujuwa na upungufu kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu kama watakavyo Masunni kuichukulia kwa maana hii, basi tafsiri hii ni potofu na wala Mashia hawasemi hivyo kamwe, na yeyote mwenye kuwanasibishia hilo bila shaka amewazulia. Zifuatazo ndizo kauli zao zinazowashuhudia tangu hapo zamani mpaka sasa. Amesema Sheikh Muhammad Ridha Al-Mudhaffar ndani ya kitabu chake kiitwacho "Aqaidul-Ima 'miyyah': "Al-Bada'u kwa maana hii ni muhali kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu kwani (itakuwa) ni kutokujua na ni upungufu, na hili haliwezekani kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu (kutokujuwa na kuwa mpungufu wa sifa) na wala Mashia hawasemi hivyo". Imam Jaa'far As-Sadiq amesema: "Mwenye kudai kwamba Mwenyezi Mungu amedhihirikiwa na kitu mdhihiriko wa majuto, basi mtu huyo kwetu sisi (atakuwa) amemkufuru Mwenyezi Mungu Mtukufu" Na amesema pia kwamba: "Mwenye kudai kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu amedhihirikiwa na kitu ambacho jana alikuwa hakukifahamu basi mimi niko mbali naye".

Kwa hiyo basi "Al-bada'u" waisemayo Mashia haivuki mipaka ya Qur'an kama ilivyo katika kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu aliposema: "Mwenyezi Mungu hufuta ayatakayo na huyathibitisha (ayatakayo) na kwake ndiko kwenye msingi wa Kitabu" (Qur'an, 13:39). Na kauli hii Masunni wanaisema kama waisemavyo Mashia, basi ni kwa nini wanaumbuliwa Mashia na wala Masunni hawaumbuliwi ambapo wao (Masunni) wanasema Mwenyezi Mungu anabadilisha hukumu na kugeuza muda na riziki? Ibn Mar-Dawaih na ibn Asakir wamethibitisha (mapokezi) toka kwa Ali (a.s.) kwamba yeye alimuuliza Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) kuhusu aya hii isemayo: "Mwenyezi Mungu hufuta ayatakayo na huyathibitisha (ayatakayo) na kwake ndiko kwenye msingi wa kitabu." Mtume wa Mwenyezi Mungu akamwambia: "Nitakutuliza kwa tafsiri ya aya hii, na nitawatuliza umma wangu baada yangu kwa tafsiri yake, (Mtume akasema) Kutoa sadaka kwa namna inayostahiki na kuwatendea wema wazazi wawili, na kutenda mema (ni mambo) yanayobadilisha maovu kuwa mema, na yanaongeza umri (wa kuishi) na yanakinga misukosuko ya maovu"

Naye ibn Al-Mindhir na ibn Abi1 Hatim na Al-Baihaqi ndani ya Ash-Shuabi toka kwa Qais bin Ubba'd (r.a.) amesema: "Kuna jambo Mwenyezi Mungu hulitenda katika kila usiku wa kumi wa miezi mitukufu, ama katika usiku wa kumi wa mwezi wa Rajab, ndani yake Mwenyezi Mungu huyafuta ayatakayo na huyathibitisha ayatakayo. Na amethibitisha Abd bin Hamid, ibn Jarir na ibn Mundhir toka kwa Umar bin Al-Khatab (r.a.) kwamba yeye Umar alisema hali yakuwa anatufu Al-Qaaba: "Ewe Mwenyezi Mungu ikiwa umeniandikia uovu au dhambi basi ifute, hakika wewe unafuta ukitakacho na unakithibitisha ukitakacho, na kwako ndiko kwenye msingi wa kitabu hivyo basi fanya iwe ni wema na ni msamaha".

Taz: Ad-Durrul-Manthoor Juz. 4 uk. 661. Naye Bukhar ndani ya sahihi yake juzuu ya nne ukurasa sabini na nane (Kitabu Bad'il-Khalqi Babu Dhikri L-Malaikah) amethibitisha kisa cha ajabu kinachosimulia miiraji ya Mtume (s.a.w.) na kukutana na Mola wake; miongoni mwa aliyoyasema Mtume (s.a.w.) ni kama ifuatavyo: "Kisha nikafaradhishiwa sala khamsini, nikaondoka mpaka nikafika kwa Musa akasema: Je, kuna nini ulichofanya? Nikasema nimefaradhishiwa sala khamsini, akasema: Mimi nawajua mno watu kuliko wewe nimeshughulika na wana wa Israel sana, hakika ummati wako hautaweza, basi rudi kwa Mola wako umuombe (akupunguzie), nikarudi nikamuomba na akazifanya kuwa arobaini. Nikarudi tena kwa Musa akaniambia kama alivyoniambia kwanza nikarudi kwa Mola naye akanipunguzia zikawa thelathini, Ishirini, Kumi, kisha tano, nikaja kwa Musa akasema umefanya nini? Nikasema amezifanya kuwa sala tano, akasema kama kwanza. Nikamwambia, Nimesalimu amri. Pakanadiwa Hakika mimi nimepitisha faradhi zangu na nimewapunguzia waja wangu na nitakuwa nalipa kwa kila tendo jema moja thawabu kumi." Na ndani ya riwaya nyingine vile vile Bukhari ameinakili riwaya hiyo ameandika, Na baada ya Muhammad (s.a.w.) kurudi kwa Mola wake mara nyingi baada ya kufaradhishiwa sala tano, Musa (a.s.) alimtaka Muhammad (s.a.w.) arudi kwa Mola wake ili ampunguzie, kwani ummati wake hawawezi (kutekeleza) japo sala tano, lakini Muhammad (s.a.w.) alimjibu Musa; "Namuonea haya Mola wangu".

Taz: Sahih BukharJuz. 4 uk. 250 Babul-Miiraj, Sahih Muslim Juz. 1 uk. 101 mlango wa Israi ya Mtume na kufaradhishwa swala. Naam (msomaji) soma na uone maajabu ya itikadi hizi zisemwazo na wasimuliaji wa Kisunni, lakini pamoja na hayo Masunni wanawatukana Mashia ambao ni wafuasi wa Maimamu kutoka katika nyumba ya Mtume kuhusu kauli ya Al-Bada'u. Na hawa Masunni ndani ya kisa hiki wanaitakidi kwamba Mwenyezi Mungu alimfaradhishia Muhammad (s.a.w.) sala khamsini kisha baada ya Muhammad kumrudia Mwenyezi Mungu (mara nyingi) ikamdhihirikia azifanye kuwa arobaini kisha ikamdhihirikia baada ya Muhammad kumrejea mara ya pili akazifanya kuwa thelathini, kisha ikamdhihirikia baada ya kurejea mara ya tatu akazifanya zikawa ishirini kisha baada ya kumrejea mara ya nne akazifanya kuwa kumi, kisha ikamdhihirikia baada ya kumrejea mara ya tano Mwenyezi Mungu akazifanya zikawa sala tano.

Na tukifumbia macho suala la kukubali riwaya hii au kutoikubali, ni kweli kabisa kwamba kauli ya "Al-Bada'u" ni Aqida madhubuti inayokubaliana na mafunzo ya dini ya Kiislamu na msingi wa Qur'an. "Bila shaka Mwenyezi Mungu habadilishi mambo ya watu mpaka wabadilishe yaliyoko katika nafsi zao". Na lau siyo itikadi yetu - Masunni na Mashia - kwamba Mwenyezi Mungu anabadilisha na kugeuza, basi sala zetu na dua zetu zisingekuwa na faida wala sababu wala maana, kama ambavyo sote tunaamini kwamba Mwenyezi Mungu hubadilisha hukmu na kufuta sheria kutoka kwa Nabii mmoja hadi mwingine, na hata katika sheria ya Mtume wetu (s.a.w.) kuna nasikh na mansukh (aya inayofuta na inayofutwa), hivyo basi kauli kuhusu "Al-Bada'u" siyo kufuru wala siyo kutoka katika dini na haiwafalii Masunni kuwaumbuwa Mashia kwa ajili ya itikadi hii, kama ambavyo haiwafalii Mashia vile vile kuwaumbuwa Masunni. Na ukweli ulivyo mimi naiona hii riwaya ya miraji kuwa inawajibisha kumnasibishia ujinga Mwenyezi Mungu Mtukufu na inaitia dosari heshima ya mtu Mtukufu aliyetambulikana katika historia ya wanaadamu naye ni Mtume wetu Muhammad (s.a.w.), pale inaposema kwamba Musa alimwambia Muhammad "Mimi nawajua mno watu kuliko wewe", na pia riwaya hii inamfanya Musa kuwa ni mbora ambapo lau si yeye, basi Mwenyezi Mungu asingeupunguzia ummati Muhammad.

Nami nashindwa kufahamu ni vipi Musa alifahamu kwamba ummati Muhammad hawawezi hata sala tano wakati ambapo Mwenyezi Mungu hakulijua hilo na anawakalifisha waja wake jambo wasiloliweza akawafaradhishia sala khamsini? Na hebu Ewe ndugu msomaji, wewe na mimi kwa pamoja tupime ni vipi zitafaradhishwa sala khamsini kwa siku moja, basi hapatakuwa na shughuli yoyote wala kazi yoyote wala hakuna kusoma hata kutafuta riziki wala harakati yoyote au jukumu lolote, (na kama ni hivyo) basi mtu atakuwa kama Malaika aliyekalifishwa kwa sala na ibada tu. Na hebu fanya mahesabu mepesi ili none uongo wa riwaya hii. Ukizidisha dakika kumi ambazo ni muda unaokubalika kiakili kutekeleza faradhi moja ya sala ya jamaa (uzidishe) mara khamsini utakuja muda uliofaradhishwa (kwa ajili ya sala) ni masaa kumi, hivyo basi ni juu yako uvumilie au uikatae dini hii inayowakalifisha wafuasi wake mambo zaidi ya uwezo wanaoweza kuumudu na kuwafaradhishia wasiyoyaweza.

Basi ikiwa Masunni wanawakebehi Mashia kwa kusema kwao juu "Al-Bada'u", na kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu hubadilisha na kugeuza vile apendavyo, hivyo ni kwa nini wao wenyewe hawajikosoi kuhusu kauli yao kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu amegeuza na kubadilisha hukumu mara tano katika faradhi moja ndani ya usiku mmoja ambao ni usiku wa miraji? Mwenyezi Mungu ailaani chuki ya upofu na upinzani mbaya ambao unafunika ukweli na kuugeuza chini juu. Basi mtu mwenye chuki anamshinikiza anayemkhalifu katika maoni na kumpinga kwa mambo yaliyo wazi, kumkebehi, kueneza uzushi dhidi yake na vitisho kutokana na mambo ya kawaida ambayo yeye anayo makubwa kuliko hayo. Hali hii inanikumbusha yale aliyoyasema Bwana wetu Isa (a.s.) kuwaambia Wayahudi aliposema: "Ninyi mnatazama kapi kwenye macho ya watu, na wala hamtazami boriti lililoko machoni kwenu". Au kwa mfano wa msemaji aliposema: "Alinitupia maradhi yake na akatokomea"

Na huenda mtu fulani anaweza akapinga (akasema) kwamba tamko la "Al-Bada'u" halikutoka kwa Masunni, na kwamba kisa hiki (baina ya Mtume Muhammad na Mtume Musa) pamoja na kuwa maana yake kinajulisha juu ya kuweko mabadiliko katika hukmu, lakini haiwezekani kukata shauri kuwa lilimdhihirikia Mwenyezi Mungu. Nami ninasema hivi, kwa kuwa ni mara nyingi nilikuwa nikikieleza kisa cha Miiraji ili kutolea ushahidi wa kauli ya "Al-Bada'u" kwa Masunni, basi baadhi yao walinipinga juu ya rai hii, lakini baadaye waliikubali na niliwasimamisha kwenye riwaya nyingine kutoka ndani ya Sahih Bukhari inayoitaja "Al-Bada'u" kwa tamko lililo wazi bila ya utatanishi. Bukhari ameeleza maelezo yaliyotoka kwa Abu Hurairah kwamba, Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) amesema: "Hakika kulikuwa na watu watatu miongoni mwa Bani Israeli mwenye mbaranga, kipofu na mwenye upara, Mwenyezi Mungu akaona awape mtihani, akawatumia Malaika, Malaika akamuendea mwenye mbaranga akamwambia, ni kitu gani ukipendacho mno, akasema, (napenda) rangi nzuri na ngozi nzuri (ya mwili) watu wamenichukia (kwa ubaya wa ngozi yangu) basi Malaika akampangusa na ugonjwa ule ukamuondokea, akampa rangi nzuri na ngozi nzuri, kisha akamwambia ni mali ipi uipendayo, akasema, ngamia, basi akapewa ngamia mwenye mimba. Kisha Malaika yule akamwendea mwenye kipara akamwambia, ni kitu gani ukipendacho mno, akasema, nywele nzuri na hiki kipara kiniondokee, watu wamenichukia (kwa ajili hii) basi Malaika akampangusa na kipara kikaondoka na akapewa nywele nzuri, kisha Malaika akamwambia, ni mali gani uipendayo, akasema ngombe, basi akampa ngombe mwenye mimba. Halafu Malaika akamwendea kipofu akamwambia, ni kitu gani ukipendacho mno, akasema, Mwenyezi Mungu ayarudishe macho yangu, basi akampangusa na Mwenyezi Mungu akamrudishia macho yake akamwambia ni mali gani uipendayo, akasema, mbuzi, basi akampa mbuzi mwenye kuzaa...

Ulipita muda fulani, yule Malaika alirudi baada ya ngamia, ng'ombe na mbuzi walipokuwa wengi kwa watu hawa kiasi kila mmoja wao akawa anamiliki kikundi (cha wanyama hao) basi akawaendea mwenye mbaranga na mwenye kipara na yule kipofu na kila mmoja wao akiwa katika hali yake, na akamtaka kila mmoja wao ampe alicho nacho, basi yule mwenye kipara na mwenye mbaranga wakamkatalia, na Mwenyezi Mungu akawarudisha katika hali yao waliyokuwa nayo hapo zamani, (ama) yule kipofu yeye akampa (Malaika alichokitaka) Mwenyezi Mungu akamzidishia na akambakishia macho yake. Taz: Sahih Bukhar Juz. 2uk. 259.

Na kwa sababu hii basi mimi nawaambia ndugu zangu (Masunni) ile kauli ya Mwenyezi Mungu isemayo: "Enyi mlioamini (watu fulani) wanaume wasiwakebehi wanaume (wengine) huenda wakawa bora kuliko wao, wala wanawake fulani wasiwakebehi wanawake (wengine) huenda wakawa bora kuliko wao, wala msijiaibishe wenyewe na wala msiitane majina mabaya, jina baya la ufasiki ni lile (aitwalo mtu) baada ya imani, na wasiotubu hao ndio madhalimu." (Qur'an, 49:11) Ni kama ambavyo natamani kwa moyo wangu wote kwamba Waislamu wangerejea kwenye muongozo wao, na waipuuze chuki (iliyojengeka baina yao) na waache ushabiki ili akili ipate kutulia mahala pake katika kila uchambuzi (unaofanywa) hata kama (uchambuzi huo) utafanywa na mpinzani wao, na wajifunze kutoka ndani ya Qur'ani Tukufu taratibu za uchambuzi na majadiliano kwa njia iliyo bora zaidi.

Bila shaka Mwenyezi Mungu alimpelekea ufunuo Mtume wake (s.a.w.) awaambie wapinzani, "Bila shaka ni sisi au ninyi, (kuna ambaye) yuko juu ya uongofu au katika upotofu uliodhahiri" (Qur'an, 34:24). Basi Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) anaipandisha daraja ya washirikina hawa, naye anajiteremsha na kuwapa sehemu fulani itakayowafanya walete dalili zao na hoja zao ikiwa wanasema kweli. "Basi sisi tuko wapi kutokana na hii tabia tukufu (ya Mtume (s.a.w.)?

12

ILI NIWE PAMOJA NA WAKWELI

TAQIYYAH

Kama tulivyotangulia kusema kuhusu kauli ya "Al-Bada'u, basi Taqiyyah nayo vile vile ni miongoni mwa mambo yanayopingwa kwa Masunni, na wao huwakejeli ndugu zao Mashia kwa hilo na kuwaona kuwa ni wanafiki, kwani hukidhihirisha ambacho sicho walichokificha...!! Na ni mara nyingi nimezungumza na baadhi yao na nikajaribu kuwakinaisha kwamba Taqiyyah siyo unafiki, lakini hawakukinaika, bali wakati mwingine utamkuta anayesikiliza jambo hili anachukia na wakati mwingine anashangaa, na hali yakuwa anadhani kuwa itikadi hii imezushwa katika Uislamu na kama kwamba ni miongoni mwa yaliyofanywa na Shia na uzushi wao. Lakini pindi mwenye kufuatilia atapofanya uchambuzi na akawa muadilifu, atakuta kwamba itikadi hii yote ni katika uti wa mgongo wa Uislamu na imetokana na Qur'an Tukufu na Sunna Tukufu ya Mtume (s.a.w.), bali mafunzo ya dini tukufu ya Kiislamu na hii sheria madhubuti havisimami ila kwa Taqiyyah.

Na jambo la kushangaza kwa Masunni ni kwamba, wao wanazipinga itikadi ambazo wanazitaja (ndani ya vitabu vyao) na vitabu vyao na sihahi zao na Musnad zao zimejaa mambo hayo na zinashuhudia dhidi yao. Hebu tuyasome kwa pamoja yale wayasemayo Masunni kuhusu Taqiyyah: Ibn Jarir na ibn Abi Hatim wamethibitisha kwa njia ya Al-Au'fi kutoka kwa ibn Abbas katika kauli ya Mwenyezi Mungu isemayo: "Isipokuwa kwa ajili ya kujilinda kutokana na shari zao" (Qur'an, 3:28) Amesema ibn Abbas "Taqiyyah (kujilinda) ni kwa ulimi, yeyote atakayelazimishwa jambo fulani aliseme hali ya kuwa jambo hilo ni la kumuasi Mwenyezi Mungu, naye akalisema kwa kuwachelea watu, na moyo wake umetulizana kwa imani, basi hali hiyo haitamdhuru kwani Taqiyyah ni kwa ulimi"

Taz: Ad-Durrul-Manthoor Fi Tafsir Bil- Maathur cha Jalalud-Din Suyuti. Na Al-hakim ameandika hadithi na kuisahihisha, na Al-Baihaqi ndani ya Sunan yake kwa njia ya A'taa1 kutoka kwa ibn Abbas amesema kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu isemayo:"Isipokuwa kwa ajili ya kujilinda kutokana na shari zao" Kwamba: "At-Tuqah" yaani Taqiyyah ni kusema kwa ulimi na hali yakuwa moyo umetulizana (umethibiti) kwa imani: Taz: Sunanul-Baihaqi na Mustad-Rak Al-Hakim. Na amethibitisha Abdu bin Hamid kutoka kwa Al-Hasan amesema:"Taqiyyah inajuzu hadi siku ya Kiyama." Taz: Ad-Durrul-Manthoor cha Jalalud-Dinis-Suyuti Juz. 2 uk. 176.

Naye Abdur-Razzaq, ibn Saad, ibn Jabir, ibn Abi-hatim na ibn Mar-dawaih wamethibitisha na Al-Hakim amesahihisha ndani ya Mustadrak yake na Al-Baihaqi ndani ya Ad-Dalail amesema: "Washirikina walimuadhibu Ammar bin Yaasir hawakumwachia mpaka alipomtukana Mtume (s.a.w.) na akawataja Miungu yao kwa wema ndipo walipomuachia, alipofika kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) Mtume akasema, kuna nini huko? Ammar akasema shari tupu, kwani sikuachiwa mpaka nilipokutukana na nikawataja miungu wao kwa wema, Mtume akasema, wauonaje moyo wako, Ammar akasema, umetulizana (umethibiti) kwa imani, Mtume akasema, basi wakirudia tena nawe rudia tena, basi hapo ikashuka (aya isemayo) "Isipokuwa yule aliyelazimishwa na hali moyo wake umetulizana kwa imani" (Qur'an, 16:106) Na amethibitisha ibn Saa'd kutoka kwa Muhammad bin Siriin kwamba Mtume (s.a.w.) alimkuta Ammar hali yakuwa analia, basi Mtume akawa anampangusa macho yake huku akisema "Wamekuadhibu makafiri wakakuzamisha ndani ya maji nawe ukasema kadha wakadha, basi iwapo watarudia tena waambie hivyo hivyo (ulivyowaambia kwanza). Taz: Atabaqatul-Kubra cha ibn Saad.

Na wamethibitisha ibn Jarir, ibn Mundhir, ibn Abi-Hatim na Al-Baihaqi ndani ya sunan yake kwa njia ya Ali kutoka kwa ibn Abbas kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu isemayo: "Mwenye kumkufuru Mwenyezi Mungu ..." Amesema: "Mwenyezi Mungu ameeleza kwamba, yeyote mwenye kumkufuru Mwenyezi Mungu baada ya kuwa amemuamini, basi mtu huyo ghadhabu toka kwa Mwenyezi Mungu zimshukie na atapata adhabu kali, ama yule mwenye kushurutishwa akasema kwa ulimi wake na moyo wake uko kinyume (cha hivyo) kwa kuwa na imani, (lakini akakufuru) kwa kujiokoa tokana na maadui zake, basi huyo hana makosa, kwani Mwenyezi Mungu Mtukufu huwaadhibu waja kwa yale waliyoamini mioyoni mwao". Taz: Sunan Al-Bayhaqi.

Na wamethibitisha mabwana ibn Abi Shaibah, ibn Jabir, Ibn Mundhir na ibn Abi Hatim kutoka kwa Mujahid amesema: "Aya hii ilishuka kwa watu wa Maka walioamini, basi baadhi ya Masahaba kutoka Madina wakawaandikia (wakasema), Hameni, hakika sisi hatuoni kwamba ninyi ni miongoni mwetu mpaka muhame mje kwetu, basi wakatoka kuelekea Madina, ghafla Maqurayshi wakawakamata njiani wakawatesa, wakakufuru hali ya kulazimishwa kufanya hivyo, basi kwa ajili yao ilishuka aya hii, "Isipokuwa yule aliyelazimishwa na hali moyo wake umethibiti kwa imani", Taz: Ad-Durrul-Manthoor cha Jalakud-Dinis-Suyuti Juz. 2uk 178. Naye Bukhar amethibitisha ndani ya sahih yake katika Babul-Mudaarati Maan-Nas, na ameeleza kutoka kwa Abud-Dar-dai amesema: "Hakika sisi tunaonyesha meno mbele ya nyuso za watu na hali yakuwa nyoyo zetu zinawalaani". Taz: Sahih Bukhar Juz. 7 uk. 102.

Naye Al-Halabi amethibitisha ndani ya Sira yake amesema: "Pindi Mtume wa Mwenyezi Mungu alipoushinda mji wa Khaybar, Hajjaj bin Ala-t alimwambia Mtume, Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu mimi ninazo mali huko Maka na ninao jamaa huko, nami nataka kuwatembelea, basi je, ninayo ruhusa ikiwa nitakutukana na nikasema jambo fulani? Mtume wa Mwenyezi Mungu alimruhusu aseme alitakalo". Taz: As-Si'ratul-Halabiyyah Juz. 3 uk. 61. Na imekuja ndani ya Kitabu kiitwacho Ihyau-Ulum cha Imam Ghazali amesema: "Hakika kuhifadhika damu ya Muislamu ni jambo la wajibu basi wakati wowote itakapokuwa makusudio ya kumwaga damu ya Muislamu yamefichikana ndani ya dhalimu, kumwambia uongo ni wajibu." Taz: Ihyau Ulumid-Din cha Hujjatul-Islam Abu Hamid Al-Ghazali.

Na amethibitisha Jalalud-Din As-Suyuti ndani ya kitabu kiitwacho Al-Ash-Ba'hu Wan-Nadhair amesema: "Inaruhusiwa kula mzoga wakati wa njaa (hakuna chakula kingine) na kunywa funda la pombe na kutamka neno la kufru (wakati wa matatizo) na lau haramu itaenea katika sehemu fulani kiasi kwamba haipatikani halali katika sehemu isipokuwa kwa nadra, basi inaruhusiwa kutumia (haramu) kwa kiasi cha Haja". Na amethibitisha Abubakr Ar-Razi ndani ya kitabu chake Ahkamul-Qur-an katika kufasiri kauli ya Mwenyezi Mungu isemayo: "Illa Antat-Taqu Minhum Tuqatan" Yaani (isipokuwa kwa ajili ya kujilinda kutokana na shari zao) amesema ina maana kuwa mtakapochelea kuzidhuru nafsi au baadhi ya viungo basi mtajilinda kutokana nao kwa kudhihirisha kuwafuata bila ya kuyaamini hayo yao, na hii ndiyo bayana inayokubaliana na tamko hilo na ndiyo msimamo wa kongamano la wanachuoni, kama ilivyokuja kutoka kwa Qatada juu ya kauli ya Mwenyezi Mungu isemayo:

"Waumini wasiwafanye makafiri kuwa wandani wao (watawala) kinyume cha Mwenyezi Mungu". Amesema (Qatadah) haifai kwa Muumini kumfanya kafiri kuwa mtawala katika dini yake, na kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu isemayo, "Isipokuwa kwa kujilinda na shari zao inapelekea ruhusa ya kudhihirisha kufru wakati wa Taqiyyah Taz: Ahkamul-Qur'an cha Ar-Razi Juz. 2 uk. 10,

Naye Bukhari amethibitisha ndani ya sahih yake kutoka kwa Qutaibah bin Said, kutoka kwa Sufiyan, kutoka kwa Al-Mukandar, amemsimulia toka Ur-Wah bin Zubair kwamba bibi Aisha alimueleza yakuwa, "Kuna mtu alibisha hodi nyumbani kwa Mtume (s.a.w.), Mtume akasema mkaribisheni, Oh! Mwana wa Al-Ashira ni muovu, au alisema ni muovu ndugu wa Al-Ashira. Alipoingia Mtume alizungumza naye kwa maneno laini, basi mimi nikasema (Yaani Aisha) Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu umesema uliyoyasema kisha umemfanyia upole katika mazungumzo? Mtume (s.a.w.) akasema: Ewe Aisha hakika watu wenye daraja ya shari kwa Mwenyezi Mungu ni mtu yule waliyemuacha watu au kumtelekeza ili kujilinda na uovu wake." Taz: Sahih Bukhari Juz. 7uk.81.

Na hii inatutosha kuwa ni dalili baada ya kuwa tumeonesha ndani ya maelezo yaliyotangulia ya kwamba masunni wanaamini kuwepo ruhusa ya Taqiyah mpaka kwenye mipaka yake ya mbali kwamba Taqiyah inaruhusiwa hadi siku ya qiyama kama maelezo yaliyopita hapo kabla, na kuwa ni wajibu kusema uongo kama alivyosema Ghazali, na kudhihirisha kufru nayo ni mwenendo na makubaliano ya wanachuoni, kama alivyolikubali jambo hilo Arrazi, na pia kujuzisha Tabasamu kwa dhahiri na kulaani kwa ndani, kama alivyokiri Bukhar. Na ruhusa ya mtu kusema atakavyo na kumtia dosari Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa kuchelea mali yake kama alivyobainisha jambo hilo mwenye Sira tul-Halabiyyah, na mtu kusema mambo ambayo ndani yake ni maasi kwa Mwenyezi Mungu kwa kuwachelea watu kama alivyokiri jambo hili Suyuti.

Basi hapana litalo halalisha kebehi ya Masunni na upinzani wao dhidi ya Mashia kwa ajili ya itikadi ambayo wao wenyewe wanaisema na kuisimulia ndani ya Sihahi zao na Musnad zao. (Vitabu vyao) ya kwamba itikadi hiyo (ya Taqiyyah) inaruhusiwa bali ni wajibu. Na Mashia hakuna chochote walichoongeza juu ya vile wasemavyo Masunni isipokuwa wao (Mashia) wametambulikana mno kuliko wengine katika matumizi ya Taqiyyah, kutokana na mateso, dhulma, na maudhi waliyoyapata toka kwa watawala wa Kibanu Ummayyah na Banu Abbas, kwani katika zama hizo ilikuwa inatosha kabisa kwa mtu kusema kwamba: "Huyu ni mfuasi wa Ahlul-Bayt" ili apambane na kifo chake na kuuliwa kwa mauaji mabaya akiwa mikononi mwa maadui wa watu wa nyumba ya Mtume (s.a.w.). Hivyo basi ilikuwa hapana budi kwa Mashia kuitumia Taqiyyah kwa kufuata maelekezo ya Maimamu wa nyumba ya Mtume (s.a.w.). Imepokewa kutoka kwa Imam Jaafar As-Sadiq (a.s.) amesema:"Taqiyyah ni dini yangu na ni dini ya wazazi wangu" na amesema: "Asiyekuwa na Taqiyyah basi huyo hana dini".

Na bila shaka Taqiyyah ilikuwa ni kielelezo cha Maimamu wa Nyumba ya Mtume kwa kujikinga na madhara wao wenyewe na wafuasi wao na wawapendao pia kuhifadhi damu yao na kusuluhisha hali ya Waislamu waliofitiniwa katika dini yao kama alivyofitiniwa Ammar bin Yasir (r.a.) na wengine. Ama Masunni, wao walikuwa mbali na balaa hilo, kwani wao kwa kipindi kirefo walikuwa wakikubaliana na watawala, hivyo basi hawakusumbuliwa si kwa kuuawa wala kuporwa mali (zao) na dhulma (yoyote dhidi yao haikuwepo) basi moja kwa moja hali hiyo ikawafanya wawe wapinzani mno wa Taqiyyah na kuwakejeli wanaoitumia. Kwa hakika watawala wa Kibanu Umayyah na Kibanu Abbas walitoa mchango mkubwa kuwafanya Mashia watambulikane mno kuitumia Taqiyyah.

Na kwa kuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu ameteremsha Qur'an (ikazungumzia) Taqiyyah, (Qur'an ambayo) inasomwa na hukmu zinatekelezwa, na kwa kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) yeye mwenyewe aliitumia Taqiyah kama ilivyokudhihirikia ndani ya Sahih Bukhar. Kadhalika Mtume alimruhusu Ammar bin Yasir amtukane na akufuru iwapo makafiri watarudia tena kumuadhibu. Si hivyo tu bali wanachuoni wa Kiislamu wameruhusu jambo hilo kwa kufuata kitabu cha Mwenyezi Mungu na Sunna ya Mtume wake, sasa basi ni kejeli gani na ni upinzani gani baada ya yote haya utakaokubalika kuelekezwa kwa Mashia? Bila shaka Masahaba watukufu walitumia Taqiyyah katika zama za watawala waovu mfano wa Muawiyah ambaye alikuwa akimuuwa kila aliyekataa kumlaani Ali bin Abi Talib, na kisa cha Hujri bin Adiyyi Al-Kindi na jamaa zake ni mashuhuri. Na mfano (watawala waovu) ni kama vile kina Yazid, ibn Ziyad na Abdul-Malik bin Marwan na wengine kama hao. Na lau ningetaka kukusanya ushahidi wa matendo ya Masahaba kuhusu Taqiyah, basi ingelazimu kitabu kamili, lakini ushahidi niliouleta miongoni mwa dalili za Masunni unatosha, shukrani zote ni zake Mwenyezi Mungu. Na sitaiacha fursa hii ipite ila niwasimulie kisa kizuri kilichonitokea mimi binafsi (nikiwa) pamoja na mwanachuoni mmoja miongoni mwa wanachuoni wa Kisunni ambaye tulikutana naye ndani ya ndege. Tulikuwa tumealikwa kuhudhuria mkutano wa Kiislamu huko Uingereza, na tukawa tunazungumza juu ya Ushia na Usunni kwa kipindi cha masaa mawili. Huyu mwanachuoni alikuwa miongoni mwa watu wanaolingania umoja (miongoni mwa Waislamu) na nilipendezwa naye, isipokuwa sikupendezwa na kauli yake aliposema kwamba: "Inabidi Mashia waziache baadhi ya itikadi ambazo zinasababisha Waislamu wahitilafiane na kukebehiana wao kwa wao."

Mimi nilimuuliza: "Kama itikadi gani"? Kwa haraka sana akajibu: "Kama vile Mut'a na Taqiyyah." Mimi nilijaribu kumkinaisha kwa uwezo wangu ya kwamba Mut'a ni ndoa ya kisheria na Taqiyyah ni ruhusa toka kwa Mwenyezi Mungu, lakini aliendelea na mtazamo wake na haikumkinaisha kauli yangu wala hoja zangu, akidai kwamba yote niliyoyaleta ni sahihi lakini inabidi kuyaacha kwa ajili ya Maslahi muhimu ambayo ni umoja wa Waislamu. Nilishangazwa sana na hekima hii inayoamuru kuacha hukumu za Mwenyezi Mungu kwa ajili ya umoja wa Waislamu na nikamwambia kwa kumfurahisha tu ya kwamba: "Lau umoja wa Waislamu utasimama juu ya jambo hili basi nitakuwa wa mwanzo kuitikia".

Tulishuka uwanja wa ndege wa London, nami nilikuwa nikitembea nyuma yake, na pindi tulipowafikia askari wa uwanja wa ndege yeye aliulizwa sababu za yeye kuja Uingereza na akawajibu kwamba amekuja kwa ajili ya matibabu, nami nilidai kwamba nimekuja kuwatembelea jamaa zangu fulani. Basi tukapita kwa salama bila ya kucheleweshwa mpaka tukafika mahala pa kukaguliwa mizigo na hapo ndipo nilipomnong'oneza nikamwambia, "Waonaje, Taqiyyah ni jambo linalofaa katika nyakati zote"? Akasema, "Kwa vipi"? Nikamwambia "Hapana shaka sisi tumewadanganya askari hawa, mimi kwa mujibu wa kauli yangu nimesema kuwa nimekuja kuwatembelea jamaa zangu, nawe kwa mujibu wa kauli yako umesema kuwa umekuja kwa ajili ya matibabu, wakati ambapo sisi tumekuja kwa ajili ya mkutano".

Basi alitabasamu na akagundua kwamba amesema uongo mbele yangu hali ya kuwa ninamsikia, hivyo akasema: "Kwani katika mkutano wa Kiislamu si kuna matibabu ya nafsi zetu"? Mimi nilicheka huku nikisema: "Je, ndani ya mkutano huo si kuna kuwatembelea ndugu zetu"? Sasa ninarejea kwenye maudhui na ninasema kwamba, "Taqiyyah ilivyo, siyo kama wanavyodai Masunni kwamba eti ni namna fulani ya unafiki, bali kinyume chake ndiyo sahihi. Kwani unafiki ni kudhihirisha imani na kuficha ukafiri, wakati ambapo Taqiyyah ni kudhihirisha kufru na kuficha imani, na misimamo hii miwili iko mbali mbali kabisa. Msimamo huu yaani wa unafiki ni ule ambao Mwenyezi Mungu Mtukufu ameusema (kama ifuatavyo):

"Na wanapokutana na wale walioamini husema tumeamini, na wanapokuwa faragha kwa mashetani wao husema sisi tuko pamoja nanyi, hakika sisi tunawacheza shere." Basi hii ndiyo imani kwa nje na ni kufru kwa ndani "Unafiki." Ama namna ya pili ya Taqiyyah ambayo Mwenyezi Mungu ameieleza (kama ifuatavyo): "Na akasema mtu mmoja muumini kutoka katika watu wa Firaun anayeficha imani yake." Hii ina maana ya kufru kwa nje na ni imani kwa ndani "Taqiyyah." Basi bila shaka muumini wa watu wa Firaun alikuwa akificha imani yake kwa ndani na hakuna aliyejua isipokuwa Mwenyezi Mungu na alikuwa akijidhihirisha kwa Firauni na watu wote kwamba yeye yuko kwenye msimamo wa dini ya Firaun. (Mwenyezi Mungu amemtaja ndani ya Kitabu choke kwa kuitukuza heshima yake). Ewe msomaji Mtukufu hebu twende pamoja ili upate kufahamu kauli ya Mashia juu ya Taqiyyah usije ukadanganyika na maneno ya uzushi na uongo yasemwayo juu ya Mashia.

Amesema Sheikh Muhammad Ridhaa Al-Mudhaffar ndani ya kitabu chake kiitwacho, "Aqaidul-Imamiyyah ". Ufuatao ndio usemi wake: "Taqiyyah inazo hukumu zake katika hali ya kuwa ni wajibu na kutokuwa wajibu kufuatana na tofauti ya mahala penye khofu ya madhara, (hukumu hizo) zimetajwa katika milango yake ndani ya vitabu vya wanachuoni wa Fiqh. Na Taqiyyah siyo wajibu katika kila hali, bali huenda ikajuzu au ikawajibika kinyume chake katika baadhi ya nyakati, kama vile itakapokuwa wakati wa kuidhihirisha haki na kuionesha kwa ajili ya kutetea dini na kuutumikia Uislamu na kuupigania katika njia yake, basi wakati huo mali hupuuzwa haipewi kima na wala nafsi hazipewi heshima (yaani haitoruhusiwa Taqiyyah ili kuokoa mali au kuokoa nafsi na dini iangamie). Na huenda Taqiyyah ikawa haramu katika matendo ambayo yanalazimisha kuua nafsi zinazo heshimika au (watu) kuzama katika batili au uovu ndani ya dini au madhara makubwa kwa Waislamu kwa kuwapotosha na kueneza dhulma na ujeuri miongoni mwao. Kwa vyovyote vile maana ya Taqiyyah kwa Shia siyo kuifanya Taqiyyah miongoni mwao kuwa ni Jumuiya ya siri kwa lengo la kuvunja na kuharibu - kama wanavyoidhania baadhi ya maadui zao wasio na upeo wa kufahamu mambo kwa mwelekeo wake na wala hawajilazimishi nafsi zao kufahamu mtazamo uliosahihi.

Kama ambavyo maana ya Taqiyyah siyo kuifanya dini na hukmu zake viwe ni mambo ya siri miongoni mwa siri ambazo haifai kuzitangaza kwa asiyefuata dini hiyo. Sasa basi inakuwaje (kudhaniwa vibaya) wakati Mashia wameandika ndani ya tunzi zao mambo yanayohusu Fiqhi, hukumu na uchambuzi wa maneno na itikadi zimejaa mashariki na magharibi na zimevuka mipaka inayotarajiwa na umma wowote unaofuata dini yake. Nawe msomaji bila shaka unaona ya kwamba, hakuna unafiki wala udanganyifu au uongo wala hadaa kama wanavyodai maadui wa Mashia.

2

MUANDAMO WA MWEZI

SURA YA PILI

JAWABU KWA WANAFUNZI WA BACHOO JAWABU YA UTANGULIZI

Wahusika ndugu zetu wa Masjid Al-Sunna Zanzibar, wameanza kitabu chao hicho kwa utangulizi wenye kumshukuru na kumuhimidi Allah na kumtakia rehema na amani Bwana wetu Muhammad (s.a.w.) kama zilivyo khutuba na vitabu vya kiislamu. Na hayo yote yamefanyika chini ya utangulizi wenye anwani:

UKWELI JUU YA KUANDAMA KWA MWEZI

Na hii ndio sehemu ya kwanza ya kitabu chao. Wakasema katika utangulizi huo: Msisitizo wetu mkubwa katika kitabu hiki ni ile nukta muhimu ya kwamba suala la kufunga na kufungua kwa muandamo mmoja kwa dunia nzima si jambo jipya kama wanavyodhani baadhi ya watu, ni jambo la kale mno ambalo linaweza kutekelezeka na kwamba huo ndio uliokuwa msimamo wa 'Jamhur' ya wanavyuoni.

Jawabu Nakubali kuwa hili ni jambo la zamani, lakini kudai kuwa hii ni kauli ya Jumhuri ni madai hewa: hayana ushahidi. Leo hii duniani hakuna madhehebu yoyote ambayo inaitendea kazi kauli hio kama ni madhehebu nzima, bali kuna baadhi ya watu tu katika kila madhehebu ambao wanafata kauli hio. Hata zile madhehebu ziliotajwa kuwa ni zenye kufata kauli hio kama vile Malik, Hanbal na Hanafi, basi hawaitendei kazi kauli hio ila baadhi yao tu. Libya, Algeria na nchi nyengine za Afrika Kaskazini na Magharibi - kwa mfano - ni nchi za wafuasi wa madhehebu ya Malik, nao wanafata miandamo yao wenyewe. Kwa hivyo, dai kuwa hii ni kauli ya Jumhur ya wanavyuoni, si dai sahihi.

SEHEMU YA PILI

Katika sehemu ya pili, ndugu waandishi wanasema:

2. Si Fikra Za Shaykh Naaswir Bachuu "Ndugu yetu Juma Muhammad Rashid Al-Mazrui amejitahidi kuandika kitabu alichokiita: "Ushahidi Uliowekwa Wazi Katika Suala La Miandamo Ya Mwezi. Makusudio yake yalikuwa ni kutaka kukijibu kitabu kilichoandikwa na Shaykh Naaswir Abdullah Bachuu kinachojulikana kwa jina la "Ufafanuzi Wa Mgogoro Wa Kuandama Kwa Mwezi."

Jawabu Kidogo na mimi naomba niweke wazi kwamba kitabu changu hakikuwa kabisa na lengo la kujibu kitabu cha Sheikh Nassor Bachoo. Hili la kunukuu maneno yake na kuyajadili lilikuwa ni jambo la kutokea tu baada ya mtu Fulani kuniletea kitabu chake. Kwa havyo, kama mulivyosema nyinyi katika kitabu chenu kwamba: Kitabu hiki ni kama nasaha kwa Waislamu wote ili kuweza kudumisha umoja wetu hususan pale ambapo pamejitokeza misimamo tofauti katika mambo ya ibada. Wala lengo la kitabu hiki sio kuendeleza malumbano baina ya Waislamu wenyewe kwa wenyewe hata kwa wale wenye misimamo tofauti. Kutajwa ndugu yetu Juma Muhammad Rashid lilikuwa ni jambo lisilobudi wala hapakuwa na lengo la kumkashifu au kumuumbua bali ni kutokana na kuwa hapakuweza kupatikana njia mbadala kwa vile ameshaandika kitabu ambacho ameshakichapisha chapa ya kwanza na ya pili.

Basi na mimi nakuombeni munielewe hivyo hivyo, kwamba wakati mimi naikubali fikra Fulani na kuikataa fikra Fulani, hakuna budi ninukuu fikra pinzani na kuonesha kwanini siikubali; na kwa upande wa pili ni lazima nioneshe kwanini naikubali fikra ninayoikubali. Na nitaposema kuwa kuna watu wana fikra hii, basi nadhani haitokuwa jambo la busara kama watu hao sikuwataja na nikiwataja ni lazima nitaje marejeo. Kwa sababu hii ndio maana nimekuwa nikinukuu maelezo ya Sheikh wetu Nassor Bachoo na kumjadili mule nisimokubaliana naye. Naomba musihuzunike kwani kujibizana katika kutafuta ukweli ni suala mashuhuri katika uwanja wa elimu. Wanavyuoni wakubwa wa kale na wa sasa wamekuwa wakijibizana ili kutafuta ukweli na hatimae huwabainikia woa pamoja na wasomaji. Kwa hivyo, hamukuwa na haja ya kutumia lugha: "Wala hapakuwa na lengo la kumkashifu": hii si kashfa hata kidogo: hii ni elimu.

Lakini, hakuna haja ya kufichana; kitabu chenu mumeandika kwa kujibu kitabu changu. Hamuna haja ya kusema: "Wala lengo la kitabu hiki sio kuendeleza malumbano baina ya Waislamu wenyewe kwa wenyewe hata kwa wale wenye misimamo tofauti. Kutajwa ndugu yetu Juma Muhammad Rashid lilikuwa ni jambo lisilobudi wala hapakuwa na lengo la kumkashifu au kumuumbua bali ni kutokana na kuwa hapakuweza kupatikana njia mbadala kwa vile ameshaandika kitabu ambacho ameshakichapisha chapa ya kwanza na ya pili", kwani kitabuchenu kimeanza kwa kunitaja mimi mwanzo hadi mwisho na kuniaga kwa kunipa nasaha mimi. Ama mimi naandika jawabu hii kukujibuni nyinyi: sikufichini wala sisemi uwongo.

Munasema Kutokana na jambo hilo , sisi kwa upande mmoja tunashukuru kwa juhudi yake hiyo na kwa upande wa pili tunatuma masikitiko yetu kwake kwa kutokuwa makini na muadilifu katika kulifafanua jambo hilo muhimu. Kwani kitabu chake hicho kimeandikwa katika mfumo wa chuki, kibri, kejeli na malumbano huku akisisitiza kwa mara nyingi kauli chafu ambazo muandishi hapaswi kuzitumia katika kitabu au katika mijadala ya Dini. Jawabu Hizi chuki, kibri na kejeli, mimi nimezisoma kwenu, kwa hivyo na iwe kama msemo wa Waswahili: "Papa akipea mafuta huwapa wanawe". Je nyinyi munayakumbuka haya:

1) Munaukumbuka muhadhara wa Sheikh Bachoo ambao alisema kuwa wasionyanyua mikono katika sala wanasali kama mipopoo? Jamani! Hii si kejeli? Je katika nyinyi yuko aliyetoa muhadhara au kuandika kitabu ili kumjibu Sheikh wetu. Sasa uadilifu uko wapi?

2) Je munaukumbuka muhadhara wa Sheikh Bachoo aliozungumzia mas-ala ya udhu kasha akasema: "Wengine wakitia udhu kiungo hiki huomba dua hii na kiungo hiki huoma dua hii; upumbavu mtupu". Je haya si matusi? Je hii si kejeli?

3) Siku moja palikuwa na maziko. Maiti alisaliwa msikiti wa wajiitao "Watu wa Sunna". Kijana mmoja akasimama akasema: "Leo tunataka kukuonesheni vipi Mtume (s.a.w.) kamsalia maiti: si kama wanavyofanya Ibadhi na Shia.

4) La nne ni kuwa ikiwa nyinyi mumethubutu kunita mjeuri, mwenye kibri na kejeli; maneno ambayo mimi sikukwambieni wala kumwambia Sheikh Nassor; mimi nimemtoa makosa tu Sheikh wetu: na hii ni kawaida katika uwanja wa elimu; sasa je na nyinyi pia ni majeuri, wenye kibri na kejeli? Katika uwandishi wenu, pia mumesema: "Hatujui dhana hii potofu ameitoa wapi." Mwenye dhana potufu naye ni mpotufu, kwa hivyo na nyinyi hamukutoa nasaha bali mumetukana. Nakupeni mifano hii mitatu ya Sheikh wetu na mmoja wenu nyinyi wenyewe enyi wenye kuandika Radan mardudan na mifano iko mingi. Inatosha kuwaita kwenu watu wengine kuwa ni watu wa bidaa na nyinyi ndio watu wa Sunna. Kwa hivyo, hii hali mumeiuda nyinyi wenyewe: Zanzibar bali Afrika Mashariki na Dunia kwa ujumla haikuwa hivi. Chuki mumeziunda nyinyi; mukijirekebisha kwa kutumia lugha nzuri nadhani hakuna atayekwambieni jambo kwa lugha nzito.

Mnasema Mfano wa kauli zake mbaya ni kama zifuatazo:

(vuta-nikuvute) [uk. 6]

(hii ni ajabu katika ajabu za dunia!) [uk. 124]

(Kwa hivyo, uwezekano huo alioutoa Sheikh hauwashi wala hauzimi [uk. 124]

(Ninasema: Enyi walimwengu wenzangu tazameni hoja za kielimu hizo!!!!!!! Kwani nyinyi Wazanzibari kabla ya kuja fikra hio ya Sheikh Nassor Bachoo ya kufunga kwa muandamo mmoja,)

(Utaona kwamba masuala yote haya si yenye kima katika soko la elimu, bali ni masuala ya kuwababaisha watu wasiojua nini cha kujadiliwa katika mas-ala haya ya funga) [uk. 167]

(Hoja nyengine - nayo pia ni hoja ya mitaani - ni kuwa watu wengi wa kawaida wanapouona mwezi mkubwa husema: "E basi ule ndio mwezi wa leo ule?!!!")

(Jawabu hii ya mwisho, inaufanya upinzani mzima wa Sheikh Bachoo kuwa hauna maana yoyote.) [uk. 132]

(Kwa ufupi ni kuwa hicho walichokidai watetezi wa rai pinzan) [uk. 32]

(utaona jinsi gani mwanamume alivyokuwa bingwa wa kubadilika! Na hili si jengine bali ni lile Waswahili wanalolisema: "Mfa maji hukamata maji.") [uk. 128]

(Hakuna hapa kinachoonesha mas-ala ya kufunga kwa muandamo mmoja wala kumi na moja.)) [uk. 125] (haina maana kwamba usiku ukiingia sehemu moja ndio umeingia dunia nzima. Kwa ufupi ni kuwa hii ni hoja ambayo haina faida yoyote ya kielimu, lakini tunaijadili kwa ajili ya watu wa mitaani tu.)

Jawabu Sikubaliani na nyinyi kwamba humu muna maneno mabaya. Lakini hata nikikubali basi nasema kwamba lugha ya namna hii sababu ni nyinyi, na kwa hivyo, utaona kwamba ninapojadiliana na watu wengine basi lugha yangu hubadilika. Kwa hivyo, tujirekebisheni sote na tujadili tafauti zetu kwa lugha ya kiungwana. Ama ukinita mpopoo, basi usinilaumu na wewe nikikwita mnazi: unanilaumu nini na wewe unakifanya kile kile nikifanyacho?! Bali hata katika kitabu hiki munachonijibu, basi nanyi mumetumia lugha hizo hizo. Katika baadhi ya sehemu umesema: "Kwa hakika katika kitabu chake hicho kwenye uk 6, anajionyesha alivyo na kauli mbili tofauti..". Na mwishoni mwa kitabu mumesema: "Dhana ya pili ya ndugu Juma imejengeka katika msingi dhaifu wala haina nafasi katika uwanja wa fani (kitaalamu) nao ni kule kusukuma kwake juu ya elimu ya Jiografia". Na yamo mengi katika kitabu chenu. Sasa nyinyi mwasema nini na mwatenda nini?

Munasema "Kwa hakika katika kitabu chake hicho kwenye uk 6, anajionyesha alivyo na kauli mbili tofauti: Kwanza anakubali kwamba suala la muandamo wa mwezi lina ikhtilafu katika kufunga kwa kumuelezea Shaykh Naaswir Bachuu kwamba: (Tunampongeza kwa juhudi) Kisha pale pale anageuka kwa kusema: (madamu hili ni suala la khilafu - basi i likuwa ni kutolizungumza kabisa,) Sasa hebu tumuulize ndio anapongeza nini? Na ni nani aliyemwambia kwamba jambo lenye khitilafu halizungumzwi? Yeye angezungumza nini katika kitabu chake kama si masuala ya ikhtilafu? Pia anatwambia haya ni katika mambo ya furui (matawi) za Kidini, kwa hivyo zisizungumzwe. Kwani ni nani aliyemwambia kuwa furui za Kidini hazizungumzwi?"

Jawabu Ikiwa lugha hii ndogo hamukuweza kuifahamu, vipi mutaweza kufahamu kitu chenye kuhitaji fani za lugha na usuli na mengineo. Ikiwa mimi niliingia msikitini kwenu Raha Leo nikakuta juu ya ubao wenu munawasomesha vijana na katika darsa hio Mubtadaa mumemwita Fa'il (vipi mutaweza kujadili masuala haya?!!! Mimi nimempongeza Sheikh Bachoo kwa juhudi au moyo wake; na sikumpong eza kwa kulikuza suala ambalo:

1) Ni la furuu'i

2) Lina khilafu. Na hii haina maana kuwa Furu'i zisizungumzwe; suala la Furu'i huwa halishadidiwi; bali unawaacha watu kama walivyo tu. Lakini yeye anapenda kushadidia katika mas-ala kama haya; ndio maana akashadidi hata katika suala la kufunga mikono hata kuwaita watu mipopoo bali na kuwambia kuwa hawana Sala. Kwa hivyo, nieleweni kwamba ninachokipinga ni kushadidia au kuwakoroga watu katika kitu ambacho ni furu'i za dini ilhali yeye kawakuta na msimamo tafauti tangu zamani. Katika mas-ala ya furu'i, wanavyuoni huwa hawashadidi juu ya Mas-ala kama haya. Mimi leo nikisimama nikaanza kufanya kampeni kwamba watu wasiitikie amina wa kisali, nalo ni jambo la furu'i, si nitakuwa natia fitna tu? Jambo kama hili huwachwa wasomi wakalitafiti kaiha kila mmoja akafanya vile ilivyombainikia. Lakini kufanya kampeni maalumu na da'awa kana kwamba waliotangulia wote ni wapotovu, hili ndilo jambo la kulaumiwa.

Ama kauli yenu: "Kwanza anakubali kwamba suala la muandamo wa mwezi lina ikhtilafu katika kufunga kwa kumuelezea Shaykh Naaswir Bachuu kwamba: (Tunampongeza kwa juhudi) Kisha pale pale anageuka kwa kusema: (madamu hili ni suala la khilafu - basi ilikuwa ni kutolizungumza kabisa,) Sasa hebu tumuulize ndio anapongeza nini?" Mwisho wa kunukuu. Na mimi nikuulizeni nyinyi mumenishukuru kwa juhudi yangu kisha mwisho wa kitabu mukaniambia: "Mwisho tunachukua fursa hii kumuonya ndugu Juma kuwa amuogope Mwenyezi Mungu hususan katika mas-ala ya kielimu. Akumbuke kuwa Mwenyezi Mungu Ameonya juu ya mtu kusema jambo au kufanya asilolijua. Aelewe kwamba ataulizwa juu ya hilo. Lingekuwa jambo la busara kama ndugu Juma angalikubali kuuliza na kufanya utafiti zaidi juu ya mas-ala haya kama agizo la Mwenyezi Mungu linavyotutaka". Sasa na nyinyi munanishukuru nini?

Munasema "Sisi tunapenda kumfahamisha kuwa suala hili la kwamba mwezi ukiandama sehemu moja unatosheleza kufuatwa kwa kufunga au kufungua ulimwengu mzima, si suala jipya bali ni jambo la kale. Tunasikitika kwamba hakuangalia vizuri maoni ya Wanavyuoni wakubwa walivyoelezea msimamo huo. Angalia katika kitabu cha Shaykh Naaswir Bachuu uk 51-58. Hapa tunanukuu baadhi ya kauli hizo:

Imamun-Nawawy aliyekisherehesha Kitabu cha Sahihi Muslim anasema:

"Na jambo lililo sahihi kwa wenzetu (Mashaffi) ni kuwa muandamo mmoja hauwahusu watu wote bali unawahusu wale walio karibu kwa kiasi ambacho hawaruhusiki kupunguza Sala (Sala ya safari). Pia imesemwa kuwa iwapo matlai ni mamoja watalazimika (watu) kufunga pamoja. Pia imesemwa kuwa ikiwa (wanaishi) katika eneo la Iklimu moja (maili 72 au km 89) (watalazimika kufunga pamoja) vyenginevyo kila mmoja atafunga kwa muandamo wake. Na wakasema wenzetu wengine (Mashaffi) kuwa muandamo katika sehemu moja utawahusu wote wa dunia nzima".

Shaykh Jaadul Haq wa chuo kikuu cha Al-Azhar katika kitabu chake "Bayaanullinnas" J. 2 uk 203 - 204 ameandika yafuatayo juu ya kauli hiyo ya Imamun-Nawawy:

"Hapa Imamu An-Nawawy ametaja kwa mukhtasari kauli zilizomo katika madhehebu ya Kishaffi (juu ya kuandama kwa mwezi) na ambazo pia zimo katika madhehebu mengine ya Kiislamu. Kauli hizo tunaweza kuzigawa katika maf ungu matatu makuu: "...Hapo Imamu An-Nawawy ametaja kwa mukhtasar kauli zilizomo katika madhehebu ya Shaffi (juu ya kuandama kwa mwezi) na ambazo pia zimo katika madhehebu nyengine za Kiislam. Kauli hizo tunaweza kuzigawa katika mafungu matatu makuu: Kauli ya kwanza: "Kila nchi iwe na matlai yake, wala muandamo wa nchi moja hautalazimu nchi nyengine ya mbali wala karibu". Kauli ya pili: "Muandamo wa nchi moja unalazimu nchi zote za dunia hata kama ziko mbali".

Kauli ya tatu: "Muandamo wa nchi moja unalazimu nchi iliyo karibu nayo au inayowafikiana kimatlai". Kisha, Shaykh Jaadul-Haq akaendelea kusema kwamba:

"Na (kauli) zote hizo ni maoni yatokanayo na Ijtihaadi ambazo hazikusimama juu ya hoja kat-ii, si sanad wala matni. Kwa hivyo ingefaa ichaguliwe kauli ambayo inakubaliana na maslahi ya (Waislam wote wa) dunia nzima kwa jumla"."

Jawabu Sikubaliani na mtazamo wa Sheikh Shaykh Jaadul Haq wa chuo kikuu cha Al-Azhar, kwamba zote hizi ni rai na itihad kwani kanuni ni kuwa "Hakuna ijtihadi mbele ya andiko" Ijtihad mwahala mwake ni musimo andiko. Wakatika katika suala hili, utaona kwamba asemaye kuwa tufunge kwa muandamo mmoja, hoja yake ni Hadithi "Fungeni kwa kuuona"; na anayesema kuwa kila mahala na muandamo wake, anatoa ushahidi wake ni Hadithi ya Ibn Abbaas na Kuraib. Kwa hivyo, ijtihad ni katika kuyafahamu maandiko: si ijtihad kwa maana ya rai tupu pasi na andiko kama alivyosema Sheikh. Kilichobaki ni kuzijadili riwaya mbili hizi zina maana gani?

Munasema Tungependa kumueleza ndugu yetu kwamba hata hapa Afrika ya Mashariki jambo hili hakulianzisha Shaykh Naaswir Bachuu kama alivyodai mwenyewe (Nd. Juma) kwamba: (Muafrika wa Mashariki wa kawaida kusikia sauti ya mgogoro)) Inasikitisha hakuweza kuangalia katika kitabu cha Shaykh Naaswir Bachuu uk 161-163 wametajwa walioonyesha kwa vizuri kabisa misimamo hiyo tofauti. Mashaykh wenyewe ni hawa wafuatao: Al-marhuum Shaykh Juma Abdul Waduud (wa Zanzibar), Shaykh Abdillahi Naaswir ( Nairobi Kenya ), na Shaykh Naaswir Khamis Abdul Rahman ( Mombasa Kenya ).

Jawabu Kwani wapi katika kitabu changu nilisema kuwa Sheikh Nassor Bchoo ndiye aliyeanzisha fikra hii hapo Afrika ya Mashariki hata mukaleta dai hili? Mimi nimeeleza kuwa zamani Afrika Mashariki watu wote wakifata muandamo mmoja. Nilisema: Karne zimepita bila ya sikio la Muafrika wa Mashariki wa kawaida kusikia sauti ya mgogoro juu ya suala la muandamo wa mwezi. Harakati za elimu zilipobadilika na kuelekea zaidi - kwa kujua au bila kujua - katika mrengu wa Kihanbali na Kiwahabi, pakajitokeza mapinduzi ya ghafla ya fikra na matendo. Dr. Ramadhan Al-butti - miongoni mwa wanavyuoni wakubwa wa ulimwengu wa sasa - anaona kwamba harakati hizi hazisifiki kama ni madhehebu: bali ni hatua (phase) katika mapito ya Historia.

Na katika uk. 97, nimesema:

Kwa kwetu - Afrika Mashariki - kusema kwamba mwezi muandamo wa nchi moja ni muandamo kwa nchi nyengine zote za dunia ni kitu kipya. Kwa hivyo, ni wazi kwamba mimi nazungumzia Afrika Mashariki. Na mfano wa hilo pia kalisema Sheikh Nassor Bachoo, lakini yeye hamukumjibu. Anasema: "Pamoja na kuwa mgogoro wa kuandama kwa mwezi umeanza kuonekana hadharani katika jamii za Waislam wa hapa Afrika ya Mashariki katika miaka ya hivi karibuni". Inasikitisha kwamba hata maneno yangu mumeyakata na kuchukua yale ambayo hayakamilishi maana nilioilenga. Maneno "Karne zimepita" hamukuyataka kwani hayakufikisheni kule mutakako!

Pili narejea tena kusema kwamba hao wanavyuoni aliowataja Sheikh Nassor, hawajathibitisha habari za kuwa watu wafunge au wakifunga kwa muandamo mmoja Africa Masharik, ukimtoa Sheikh Nassir Khamis wa Mombasa ambaye naye pia ni mtu wa sasa. Ama sheikh Juma Abdu-Wadood yeye, kwa mujibu wa nakala hio ya Sheikh Nassor Bachoo, kasema hivi: Kuona huku kwa mwezi kumekusudiwa kuonekana na Waislam, na kuonekana na Waislamu huko, sio lazima kuonekana na Waislamu wote. Bali inatosha shahada ya mtu mmoja muadilifu".

Pia inampasa mtu mmoja pekee kama ameuona mwezi yeye afunge na kila aliyemuamini; hata akiwa haijakubaliwa shahada yake. Haya ndio maneno ya Sheikh Juma Abdu-Wadood kwa mujibu wa alivyomnukuu Sheikh Bachoo. Sasa ikiwa ndugu zetu mumeshindwa kuyafahamu maneno haya ya Sheikh Juma Abdu-Wadood, bado mutaendelea kupoteza watu bila ya elimu?! Sheikh Juma Abdul-Wadood hapa anazungumzia mas-ala ya ushahidi kwamba si lazima - katika suala la kuonekana kwa mwezi - kwamba kila mmoja auone: bali akiona mtu mmoja basi inatosha kwa wengine kufunga. Hii ndio kauli ya Sheikh Juma Abdul-Wadood na hili nimelieleza kwa urefu katika kitabu changu.

Kisha Sheikh Juma Abdul-Wadood akazungumzia suala la kufunga kwa muandamo mmoja akasema: "Rai za Maimamu wengine wameifasiri hadithi isemayo: (Fungeni kwa kuuona Mwezi) kwamba ukionekana popote mashariki au magharibi (watu) wafunge; hapana kutazama masafa fulani au nini. Hii ni rai nayo na wengi wamesema (hivyo) kama Imamu Malik , Ahmad na kundi kubwa la Hanafi. Inakurubia kuwa n dio rai ya Jamhuri - kufata rai hii ni kuhakikisha umoja wa dunia nzima. Wala hatuwezi kusema kwamba rai ya Shaffiy ndio ya Jamhur". Hapa Sheikh Juma anasimulia rai za Maimamu wengine: si rai za Maulamaa wa Afrika Mashariki. Mimi dai langu nililodai ni kuwa jambo hili la kufunga kwa muandamo mmoja, napenda munifahamu: ni jipya kwa Africa Mashariki. Mimi sikusudii jambo la wanazuoni kuzungumzia rai mbali mbali: bali nazungumzia jambo la watu kufata muandamo mmoja kwamba karne zimepita ya sikio la Muafrika Mashariki wa Kawaida halijiapata kusikia. Na nimetumia maneno "Muafrika wa Mashariki wa kawaida" ili kuwatoa wanavyuoni wao hata kama walikuwa hawafati kauli hio, lakini wanaijua. Kwa hali yoyote ile:

1) Sheikh Juma Abdul-Wadoo hajazungumzia kwamba Afrika Mashariki watu walikuwa wakifunga au wafunge kwa muandamo mmoja, bali kazungumzia rai za wanavyuoni wasio wa Afrika Mashariki - Al-Imamu Shafi, Hanbal n.k. Na mimi sijakanusha tafauti hizi.

2) Kauli yake ilikuwa ni kuhusu suala la mashahidi.

Ama Sheikh Abdillahi Nassir, yeye ni mwanachuoni wa sasa. Na mimi sijasema kuwa sasa hakuna rai hizo. Pili ni kuwa nakala alizotupa Sheikh Bachoo za kitabu cha Sheikh Abdillahi utaona kwamba Sheikh Abdillahi hazungumzii kuwa kauli ya kufatwa ni ile ya muandamo mmoja; bali yeye kasema kuwa hili ni suala la khilafu kwa hivyo tusigombane kila mtu afate rai anayoiona kuwa ni sawa. Sheikh Abdillah kayasema haya baada ya kutokea mizozo hii ya sasa. Kwa hivyo tunarudi pale pale kwamba "Karne zimepita bila ya sikio la Muafrika wa Mashariki wa kawaida kusikia sauti ya mgogoro juu ya suala la muandamo wa mwezi. Harakati za elimu zilipobadilika na kuelekea zaidi - kwa kujua au bila kujua - katika mrengu wa Kihanbali na Kiwahabi, pakajitokeza mapinduzi ya ghafla ya fikra na matendo". Kwa hivyo, nukta hii hamukuuijibu: na wala sioni kuwa kuna haja ya kuijibu kwani haina umuhimu katika maudhui yetu. Bali kitabu chenu chote, munachagua mambo yasio na umuhimu "Juma kantutukana; Juma kanfanya hivi" nyinyi ndio munajibu baada ya kuzungumzia dalili za kielimu.

Ama Sheikh Nassor: yeye pia ni mtu wa sasa na ni mfuasi wa skuli hio hio munayoifuata nyinyi, kwa hivyo kusema kwake alivyosema hakujapindua nilioyasema kuwa - kimatendo - hili ni suala jipya kwa kwetu Afrika ya Mashariki. Wala mimi sikusema kuwa Sheikh Nassor Bachoo ndiye muasisi wa fikra hio huko kwetu. Naomba munifahamu ninachokisema kwanza kisha ndio munijibu. Na sijui munapinga nini kitu ambacho watu wote wanakijua. Bila ya kusahau kwamba mimi sikusudii kusema kuwa kitu sahihi ni kilichofanywa zamani au kilichofanywa leo: laa! Bali kitu sahihi ni chenye ushahidi sahihi uliojengeka juu ya misingi sahihi ya kielimu. Na kielimu, suala la kuzingatia muandamo mmoja - hamutoweza kulithibitisha.

MNASEMA

Pia Shaykh Ahmad Al Khalil, Mufti wa Omani amethibitisha kwamba Ikhtilaf hii ya muandamo wa mwezi katika hukmu ya kufunga au kufungua ipo na kwamba ni jambo la kale. Kama alivyosema maneno yake yaliyotafsiriwa na Shaykh Muniir Sulayman 'Aziz kwamba: "Hakuna madhehebu iliyokuwa imesalimika na kuwa na Khitilafu baina ya Wanavyuoni wake juu ya suala la kutafautiana miandamo ya mwezi." Jee ndugu Juma anataka kusema kwamba Shaykh Naaswir Bachuu ndiye mwalimu aliyeanzisha madhehebu zote? Au ndiye aliyeanzisha mtafaruku huu kama alivyouita mwenyewe ndugu Juma?

JAWABU

Suala hilo jiulizeni wenyewe; mujijibu wenyewe; kwani nyinyi ndio mulioliunda: mimi sikusema hivyo kamwe bali nilichokisema ni hiki: "Kwa kwetu - Afrika Mashariki - kusema kwamba mwezi muandamo wa nchi moja ni muandamo kwa nchi nyengine zote za dunia ni kitu kipya". Nami sikusudii kusema kwamba upya huo ni katika kuzungunzwa au kusomwa suala hilo katika vitabu; nakusudia kimatendo sula hili lilikuwa halipo Afrika Mashariki. Sasa ili muwe mumenijibu, twambieni nani alikuwa akifata muandamo mmoja hapa Afrika Mashariki. Jamani! Tafuteni hoja mujadili: musijadili kitu kisichokuwa na umuhimu. Kama hamuna hoja nyamzeni musijitie aibu!

MNASEMA

Katika kudhihirisha udhaifu wake wa kumuandama mtu fulani; Ndugu Juma anasema: (Kama tunavyojua kwamba Sheikh Nassor Bachoo, ni mmoja wa wenye kusisitiza ulazima wa kuwa na muandamo mmoja.) Sisi kwa upande wetu tunasema: Katika kitabu cha Shaykh Naaswir Bachuu hakuna pahala alipolazimisha watu wafuate huo aliouita ndugu Juma (msimamo wa Shaykh Naaswir). Bali yeye ameonesha mitizamo ya Wanavyuoni kwa kutumia Aya za Qur-aan, Hadiythi na vitabu vinavyokubalika. Lugha aliyotumia Shaykh Naaswir katika huo unaonekana ni msimamo wake ni maneno yaliyozimuliwa kilugha (polite language) kama vile: (inawezekana) ((inaonyesha) .

JAWABU

Na mimi hapa sijasema kuwa Sheikh Nassir Bachoo kalazimisha watu wafunge kwa muandamo mmoja. Nimesema "Anasisitiza ulazima" yaani yeye analingania msimamo huo kwani kwake ndio msimamo sahihi na ndio wajibu kuufata. Naomba tena tuelewane musiseme kitu kinyume na nilivyosema. Wala musitafute kitu kisicho na maana mukajadili eti ndio jawabu! Pili maneno yenu: "Katika kudhihirisha udhaifu wake wa kumuandama mtu fulani". Sasa je na nyinyi pia munaonesha udhaifu huo huo kwa kumuandama mtu fulani katika kitabu chenu?

MNASEMA

Aliyelazimisha rai ni ndugu Juma mwenyewe kama anavyosema: (Lakini kilicho lazima na ambacho tunatakiwa tukubaliane ni kuwa muandamo wa mbali hautendewi kazi mbali) [uk. 112]

JAWABU

Bali hata Sheikh Bachoo pia kalazimisha kwani ukidai kuwa huu ndio msimamo wa haki au ndio msimamo sahihi au ndio wajibu kufatwa, bila kusema kuwa rai zote zinafaa basi na wewe huwa umelazimisha rai yako. Sasa je Sheikh Bachoo anakubali hivyo kuwa rai zote ni sawa? Mimi kweli sisemi kuwa rai zote ni sawa: nasema kuwa nyinyi mumekosea na sahihi ni kinyume na munavyofanya, na kwa hivyo bado nipo katika msimamo wangu huo huo kwamba: "Kilicho lazima na ambacho tunatakiwa tukubaliane ni kuwa muandamo wa mbali hautendewi kazi mbali".

MUNASEMA

"Kisha katika uk 85 ndugu Juma anataja kwamba msimamo huu wa muandamo mmoja kwa dunia nzima ni ((kitu kipya)) na kwamba jambo hilo halitekelezeki na ni kauli iliyobaki vitabuni tu baada ya kutaja baadhi ya nchi zinazofuata miandamo yao - yaani kila nchi na muandamo wake kama Al-yaman , Oman , Misri na Saudia. Kisha hapo hapo akataja: ((isipokuwa Imarati katika miaka ya mwisho wamekuwa wakifata Saudia.)) Inafaa ndugu Juma aulizwe masuala yafuatayo:

i) Kama ni jambo lisilotekelezeka vipi tena Imarat wanalitekeleza?

ii) Je hawa wa Imarat nao ni wanafunzi wa Shaykh Naaswir Bachuu?

iii) Kwani hiyo sio kauli ya Jamhuur ambayo ndio msimamo wa maimamu wakubwa wakiwemo Ahmad bin Hanbal, Malik na Abu Hanifa? (Angalia pia sehemu ya 11 na 13 za kitabu hiki)

JAWABU

Kwanza mumemefanya ghushi: maneno yangu hamukuyanukuu yote. Mimi nimesema: "Kwa kwetu - Afrika Mashariki - kusema kwamba mwezi muandamo wa nchi moja ni muandamo kwa nchi nyengine zote za dunia ni kitu kipya". Nyinyi maneno "Kwa kwetu Afrika Mashariki" mumeyatoa ili ionekane kuwa mimi nasema kuwa hili ni suala jipya kila pahala. Watu kama nyinyi vipi tutakuamini katika dini yenu na uadilifu wenu, ikiwa munaghushi maandiko hivi? Hii ndio kamati ya Msikiti Sunna na hii ndio suna yenyewe?! Halafu mukaendelea na tadlis (ghushi) yenu mukasema: "Na kwamba jambo hilo halitekelezeki na ni kauli iliyobaki vitabuni tu". Mimi sikusema hapa kuwa "Halitekelezeki", bali nimesema:

Lakini ukweli ni kuwa hata katika nchi nyengine zote za dunia taqriban kauli kwamba tufunge kwa muandamo mmoja, ni kauli ilioishia katika vitabu tu, kimatendo (practically) kauli hio haitumiwi isipokuwa na mtu mmoja mmoja. Hadi leo hii: watu Al-yaman wanafata muandamo wao, Oman wanafata muandamo wao, Saudia wanafata muandamo wao, Misr wanafata muandamo wao na nchi zote taqriban ni hivyo, isipokuwa Imarati katika miaka ya mwisho wamekuwa wakifata Saudia.

Haya nionesheni hapa maneno "Halitekelezeki". Mimi nimesema kuwa kimatendo kauli hii, hadi leo haitendewi kazi isipokuwa na baadhi ya watu. Nyinyi mumebadilisha na kuweka ghushi yenu mukasema nimesema halitekelezeki. Kwa hivyo, hilo Sula (a na b) jibuni wenyewe kwani mumesema kinyume na nilivyosema. Suala (d), najibu kuwa sio: hio si kauli ya jumhur bali jumhur kauli yao ni kinyume na hivyo na hili nimelithibitisha katika uk. 189-193 wa chapa ya pili ya kitabu changu au uk. 171 wa kitabu hicho chapa ya kwanza. Na Al-Imamu Malik riwaya zake zimegongana na riwaya kwamba kila watu na muandamo wao ndio ilio bora kwani ni riwaya ya Madina aliko kuweko Al-Imamu Malik, wakati riwaya nyengine ni ya watu wa Irak kulikokuwa na viwanda vya kutunga riwaya!

MNASEMA

Na sisi tunamuongezea habari moja ambayo ni vyema kuielewa, kwamba nchi ya Uganda iliyo katika Afrika ya Mashariki pia inafuata rasmi muandamo mmoja wa duniani. Pia aelewe kwamba huo msimamo wa kila nchi na mwezi wake huku Afrika ya Mashariki haukuwepo tokea zamani. Mashaykh wote wa huku wanakubaliana mwezi ukionekana popote katika nchi hizi tatu ( Kenya , Uganda na Tanzania ) wanafunga pamoja. Yeye anaendelea kushika msimamo wake: (Al-yaman wanafata muandamo wao, Oman wanafata muandamo wao, Saudia wanafata muandamo wao). Lile analoliona yeye halitekelezeki, basi ndio linatekelezeka.

JAWABU

1) Kitu rasmi Uganda hakizingatiwi kwani Uganda kimsingi sin chi ya Kiislamu wala ya Waislamu: Waislamu ni wachache ukilinganisha na Wasio Waislamu. Kwa hivyo, hakuna kitu rasmi. Na jambo hilo ni jambo la sasa. Na mimi sijapinga kwamba sasa fikra hio ipo Afrika Mashariki.

2) Ama kauli yenu: "Mashaykh wote wa huku wanakubaliana mwezi ukionekana popote katika nchi hizi tatu ( Kenya , Uganda na Tanzania ) wanafunga pamoja". Ndio maana nikatumia lafdhi "Kwa kwetu Afrika Mashariki" nikijua kuwa wanavyuoni wote wa kwetu Afrika Mashariki wana msimamo huo. Ama kauli yenu: "Yeye anaendelea kushika msimamo wake: ((Al-yaman wanafata muandamo wao, Oman wanafata muandamo wao, Saudia wanafata muandamo wao,)). Lile analoliona yeye halitekelezeki, basi ndio linatekelezeka". Mwisho wa kunukuu. Inaonesha kuwa kitabu changu mumekijibu bila ya kukifahamu. Nilichosema ni kuwa, ijtihadi ifanywe katika kubainisha wapi hadi wapi watu wafunge pamoja. Kwa vile, hakuna andiko lililobainisha hivyo. Ama muandamo mmoja kwa dunia nzima hili ni kinyume na andiko. Kwa hivyo, wakiwa wanavyuoni wa zamani wamefanya ijtihad hio, sisi tunafata ijtihad yao kwa vile hapa ni mahala pa ijtihad na haikugongana na andiko. Ama madai yenu nyinyi ni kinyume na andiko lilivyoonesha.

MNASEMA

"Kuna suala moja la nyongeza tunapenda tumuulize ndugu yetu Juma: Hata kama hizo nchi alizozitaja ( Al-Yaman , Oman , Misri na Saudia) hazijakubaliana kufuata muandamo mmoja, je hakuna uwezekano (japo wa sadfa) unaoweza kutokea kufunga siku moja ijapokuwa kila mmoja ameona mwezi katika nchi yake? Sasa tuseme kila nchi katika hizo imeona mwezi usiku wa Alkhamisi kuamkia Ijumaa - Wote si watafunga siku moja ya Ijumaa? Basi huo ndio utekelezaji aliosema hautekelezeki. Ni wazi kuwa unatekelezeka.

JAWABU

Munaendelea kuuliza masula haya kwa sababu masuala yenu mumeyajenga katika kitu nisichokisema kamwe. Wapi nimesema kuwa "Hilo halitekezeki" hata mukauliza masuala haya?

2

MUANDAMO WA MWEZI

SURA YA PILI

JAWABU KWA WANAFUNZI WA BACHOO JAWABU YA UTANGULIZI

Wahusika ndugu zetu wa Masjid Al-Sunna Zanzibar, wameanza kitabu chao hicho kwa utangulizi wenye kumshukuru na kumuhimidi Allah na kumtakia rehema na amani Bwana wetu Muhammad (s.a.w.) kama zilivyo khutuba na vitabu vya kiislamu. Na hayo yote yamefanyika chini ya utangulizi wenye anwani:

UKWELI JUU YA KUANDAMA KWA MWEZI

Na hii ndio sehemu ya kwanza ya kitabu chao. Wakasema katika utangulizi huo: Msisitizo wetu mkubwa katika kitabu hiki ni ile nukta muhimu ya kwamba suala la kufunga na kufungua kwa muandamo mmoja kwa dunia nzima si jambo jipya kama wanavyodhani baadhi ya watu, ni jambo la kale mno ambalo linaweza kutekelezeka na kwamba huo ndio uliokuwa msimamo wa 'Jamhur' ya wanavyuoni.

Jawabu Nakubali kuwa hili ni jambo la zamani, lakini kudai kuwa hii ni kauli ya Jumhuri ni madai hewa: hayana ushahidi. Leo hii duniani hakuna madhehebu yoyote ambayo inaitendea kazi kauli hio kama ni madhehebu nzima, bali kuna baadhi ya watu tu katika kila madhehebu ambao wanafata kauli hio. Hata zile madhehebu ziliotajwa kuwa ni zenye kufata kauli hio kama vile Malik, Hanbal na Hanafi, basi hawaitendei kazi kauli hio ila baadhi yao tu. Libya, Algeria na nchi nyengine za Afrika Kaskazini na Magharibi - kwa mfano - ni nchi za wafuasi wa madhehebu ya Malik, nao wanafata miandamo yao wenyewe. Kwa hivyo, dai kuwa hii ni kauli ya Jumhur ya wanavyuoni, si dai sahihi.

SEHEMU YA PILI

Katika sehemu ya pili, ndugu waandishi wanasema:

2. Si Fikra Za Shaykh Naaswir Bachuu "Ndugu yetu Juma Muhammad Rashid Al-Mazrui amejitahidi kuandika kitabu alichokiita: "Ushahidi Uliowekwa Wazi Katika Suala La Miandamo Ya Mwezi. Makusudio yake yalikuwa ni kutaka kukijibu kitabu kilichoandikwa na Shaykh Naaswir Abdullah Bachuu kinachojulikana kwa jina la "Ufafanuzi Wa Mgogoro Wa Kuandama Kwa Mwezi."

Jawabu Kidogo na mimi naomba niweke wazi kwamba kitabu changu hakikuwa kabisa na lengo la kujibu kitabu cha Sheikh Nassor Bachoo. Hili la kunukuu maneno yake na kuyajadili lilikuwa ni jambo la kutokea tu baada ya mtu Fulani kuniletea kitabu chake. Kwa havyo, kama mulivyosema nyinyi katika kitabu chenu kwamba: Kitabu hiki ni kama nasaha kwa Waislamu wote ili kuweza kudumisha umoja wetu hususan pale ambapo pamejitokeza misimamo tofauti katika mambo ya ibada. Wala lengo la kitabu hiki sio kuendeleza malumbano baina ya Waislamu wenyewe kwa wenyewe hata kwa wale wenye misimamo tofauti. Kutajwa ndugu yetu Juma Muhammad Rashid lilikuwa ni jambo lisilobudi wala hapakuwa na lengo la kumkashifu au kumuumbua bali ni kutokana na kuwa hapakuweza kupatikana njia mbadala kwa vile ameshaandika kitabu ambacho ameshakichapisha chapa ya kwanza na ya pili.

Basi na mimi nakuombeni munielewe hivyo hivyo, kwamba wakati mimi naikubali fikra Fulani na kuikataa fikra Fulani, hakuna budi ninukuu fikra pinzani na kuonesha kwanini siikubali; na kwa upande wa pili ni lazima nioneshe kwanini naikubali fikra ninayoikubali. Na nitaposema kuwa kuna watu wana fikra hii, basi nadhani haitokuwa jambo la busara kama watu hao sikuwataja na nikiwataja ni lazima nitaje marejeo. Kwa sababu hii ndio maana nimekuwa nikinukuu maelezo ya Sheikh wetu Nassor Bachoo na kumjadili mule nisimokubaliana naye. Naomba musihuzunike kwani kujibizana katika kutafuta ukweli ni suala mashuhuri katika uwanja wa elimu. Wanavyuoni wakubwa wa kale na wa sasa wamekuwa wakijibizana ili kutafuta ukweli na hatimae huwabainikia woa pamoja na wasomaji. Kwa hivyo, hamukuwa na haja ya kutumia lugha: "Wala hapakuwa na lengo la kumkashifu": hii si kashfa hata kidogo: hii ni elimu.

Lakini, hakuna haja ya kufichana; kitabu chenu mumeandika kwa kujibu kitabu changu. Hamuna haja ya kusema: "Wala lengo la kitabu hiki sio kuendeleza malumbano baina ya Waislamu wenyewe kwa wenyewe hata kwa wale wenye misimamo tofauti. Kutajwa ndugu yetu Juma Muhammad Rashid lilikuwa ni jambo lisilobudi wala hapakuwa na lengo la kumkashifu au kumuumbua bali ni kutokana na kuwa hapakuweza kupatikana njia mbadala kwa vile ameshaandika kitabu ambacho ameshakichapisha chapa ya kwanza na ya pili", kwani kitabuchenu kimeanza kwa kunitaja mimi mwanzo hadi mwisho na kuniaga kwa kunipa nasaha mimi. Ama mimi naandika jawabu hii kukujibuni nyinyi: sikufichini wala sisemi uwongo.

Munasema Kutokana na jambo hilo , sisi kwa upande mmoja tunashukuru kwa juhudi yake hiyo na kwa upande wa pili tunatuma masikitiko yetu kwake kwa kutokuwa makini na muadilifu katika kulifafanua jambo hilo muhimu. Kwani kitabu chake hicho kimeandikwa katika mfumo wa chuki, kibri, kejeli na malumbano huku akisisitiza kwa mara nyingi kauli chafu ambazo muandishi hapaswi kuzitumia katika kitabu au katika mijadala ya Dini. Jawabu Hizi chuki, kibri na kejeli, mimi nimezisoma kwenu, kwa hivyo na iwe kama msemo wa Waswahili: "Papa akipea mafuta huwapa wanawe". Je nyinyi munayakumbuka haya:

1) Munaukumbuka muhadhara wa Sheikh Bachoo ambao alisema kuwa wasionyanyua mikono katika sala wanasali kama mipopoo? Jamani! Hii si kejeli? Je katika nyinyi yuko aliyetoa muhadhara au kuandika kitabu ili kumjibu Sheikh wetu. Sasa uadilifu uko wapi?

2) Je munaukumbuka muhadhara wa Sheikh Bachoo aliozungumzia mas-ala ya udhu kasha akasema: "Wengine wakitia udhu kiungo hiki huomba dua hii na kiungo hiki huoma dua hii; upumbavu mtupu". Je haya si matusi? Je hii si kejeli?

3) Siku moja palikuwa na maziko. Maiti alisaliwa msikiti wa wajiitao "Watu wa Sunna". Kijana mmoja akasimama akasema: "Leo tunataka kukuonesheni vipi Mtume (s.a.w.) kamsalia maiti: si kama wanavyofanya Ibadhi na Shia.

4) La nne ni kuwa ikiwa nyinyi mumethubutu kunita mjeuri, mwenye kibri na kejeli; maneno ambayo mimi sikukwambieni wala kumwambia Sheikh Nassor; mimi nimemtoa makosa tu Sheikh wetu: na hii ni kawaida katika uwanja wa elimu; sasa je na nyinyi pia ni majeuri, wenye kibri na kejeli? Katika uwandishi wenu, pia mumesema: "Hatujui dhana hii potofu ameitoa wapi." Mwenye dhana potufu naye ni mpotufu, kwa hivyo na nyinyi hamukutoa nasaha bali mumetukana. Nakupeni mifano hii mitatu ya Sheikh wetu na mmoja wenu nyinyi wenyewe enyi wenye kuandika Radan mardudan na mifano iko mingi. Inatosha kuwaita kwenu watu wengine kuwa ni watu wa bidaa na nyinyi ndio watu wa Sunna. Kwa hivyo, hii hali mumeiuda nyinyi wenyewe: Zanzibar bali Afrika Mashariki na Dunia kwa ujumla haikuwa hivi. Chuki mumeziunda nyinyi; mukijirekebisha kwa kutumia lugha nzuri nadhani hakuna atayekwambieni jambo kwa lugha nzito.

Mnasema Mfano wa kauli zake mbaya ni kama zifuatazo:

(vuta-nikuvute) [uk. 6]

(hii ni ajabu katika ajabu za dunia!) [uk. 124]

(Kwa hivyo, uwezekano huo alioutoa Sheikh hauwashi wala hauzimi [uk. 124]

(Ninasema: Enyi walimwengu wenzangu tazameni hoja za kielimu hizo!!!!!!! Kwani nyinyi Wazanzibari kabla ya kuja fikra hio ya Sheikh Nassor Bachoo ya kufunga kwa muandamo mmoja,)

(Utaona kwamba masuala yote haya si yenye kima katika soko la elimu, bali ni masuala ya kuwababaisha watu wasiojua nini cha kujadiliwa katika mas-ala haya ya funga) [uk. 167]

(Hoja nyengine - nayo pia ni hoja ya mitaani - ni kuwa watu wengi wa kawaida wanapouona mwezi mkubwa husema: "E basi ule ndio mwezi wa leo ule?!!!")

(Jawabu hii ya mwisho, inaufanya upinzani mzima wa Sheikh Bachoo kuwa hauna maana yoyote.) [uk. 132]

(Kwa ufupi ni kuwa hicho walichokidai watetezi wa rai pinzan) [uk. 32]

(utaona jinsi gani mwanamume alivyokuwa bingwa wa kubadilika! Na hili si jengine bali ni lile Waswahili wanalolisema: "Mfa maji hukamata maji.") [uk. 128]

(Hakuna hapa kinachoonesha mas-ala ya kufunga kwa muandamo mmoja wala kumi na moja.)) [uk. 125] (haina maana kwamba usiku ukiingia sehemu moja ndio umeingia dunia nzima. Kwa ufupi ni kuwa hii ni hoja ambayo haina faida yoyote ya kielimu, lakini tunaijadili kwa ajili ya watu wa mitaani tu.)

Jawabu Sikubaliani na nyinyi kwamba humu muna maneno mabaya. Lakini hata nikikubali basi nasema kwamba lugha ya namna hii sababu ni nyinyi, na kwa hivyo, utaona kwamba ninapojadiliana na watu wengine basi lugha yangu hubadilika. Kwa hivyo, tujirekebisheni sote na tujadili tafauti zetu kwa lugha ya kiungwana. Ama ukinita mpopoo, basi usinilaumu na wewe nikikwita mnazi: unanilaumu nini na wewe unakifanya kile kile nikifanyacho?! Bali hata katika kitabu hiki munachonijibu, basi nanyi mumetumia lugha hizo hizo. Katika baadhi ya sehemu umesema: "Kwa hakika katika kitabu chake hicho kwenye uk 6, anajionyesha alivyo na kauli mbili tofauti..". Na mwishoni mwa kitabu mumesema: "Dhana ya pili ya ndugu Juma imejengeka katika msingi dhaifu wala haina nafasi katika uwanja wa fani (kitaalamu) nao ni kule kusukuma kwake juu ya elimu ya Jiografia". Na yamo mengi katika kitabu chenu. Sasa nyinyi mwasema nini na mwatenda nini?

Munasema "Kwa hakika katika kitabu chake hicho kwenye uk 6, anajionyesha alivyo na kauli mbili tofauti: Kwanza anakubali kwamba suala la muandamo wa mwezi lina ikhtilafu katika kufunga kwa kumuelezea Shaykh Naaswir Bachuu kwamba: (Tunampongeza kwa juhudi) Kisha pale pale anageuka kwa kusema: (madamu hili ni suala la khilafu - basi i likuwa ni kutolizungumza kabisa,) Sasa hebu tumuulize ndio anapongeza nini? Na ni nani aliyemwambia kwamba jambo lenye khitilafu halizungumzwi? Yeye angezungumza nini katika kitabu chake kama si masuala ya ikhtilafu? Pia anatwambia haya ni katika mambo ya furui (matawi) za Kidini, kwa hivyo zisizungumzwe. Kwani ni nani aliyemwambia kuwa furui za Kidini hazizungumzwi?"

Jawabu Ikiwa lugha hii ndogo hamukuweza kuifahamu, vipi mutaweza kufahamu kitu chenye kuhitaji fani za lugha na usuli na mengineo. Ikiwa mimi niliingia msikitini kwenu Raha Leo nikakuta juu ya ubao wenu munawasomesha vijana na katika darsa hio Mubtadaa mumemwita Fa'il (vipi mutaweza kujadili masuala haya?!!! Mimi nimempongeza Sheikh Bachoo kwa juhudi au moyo wake; na sikumpong eza kwa kulikuza suala ambalo:

1) Ni la furuu'i

2) Lina khilafu. Na hii haina maana kuwa Furu'i zisizungumzwe; suala la Furu'i huwa halishadidiwi; bali unawaacha watu kama walivyo tu. Lakini yeye anapenda kushadidia katika mas-ala kama haya; ndio maana akashadidi hata katika suala la kufunga mikono hata kuwaita watu mipopoo bali na kuwambia kuwa hawana Sala. Kwa hivyo, nieleweni kwamba ninachokipinga ni kushadidia au kuwakoroga watu katika kitu ambacho ni furu'i za dini ilhali yeye kawakuta na msimamo tafauti tangu zamani. Katika mas-ala ya furu'i, wanavyuoni huwa hawashadidi juu ya Mas-ala kama haya. Mimi leo nikisimama nikaanza kufanya kampeni kwamba watu wasiitikie amina wa kisali, nalo ni jambo la furu'i, si nitakuwa natia fitna tu? Jambo kama hili huwachwa wasomi wakalitafiti kaiha kila mmoja akafanya vile ilivyombainikia. Lakini kufanya kampeni maalumu na da'awa kana kwamba waliotangulia wote ni wapotovu, hili ndilo jambo la kulaumiwa.

Ama kauli yenu: "Kwanza anakubali kwamba suala la muandamo wa mwezi lina ikhtilafu katika kufunga kwa kumuelezea Shaykh Naaswir Bachuu kwamba: (Tunampongeza kwa juhudi) Kisha pale pale anageuka kwa kusema: (madamu hili ni suala la khilafu - basi ilikuwa ni kutolizungumza kabisa,) Sasa hebu tumuulize ndio anapongeza nini?" Mwisho wa kunukuu. Na mimi nikuulizeni nyinyi mumenishukuru kwa juhudi yangu kisha mwisho wa kitabu mukaniambia: "Mwisho tunachukua fursa hii kumuonya ndugu Juma kuwa amuogope Mwenyezi Mungu hususan katika mas-ala ya kielimu. Akumbuke kuwa Mwenyezi Mungu Ameonya juu ya mtu kusema jambo au kufanya asilolijua. Aelewe kwamba ataulizwa juu ya hilo. Lingekuwa jambo la busara kama ndugu Juma angalikubali kuuliza na kufanya utafiti zaidi juu ya mas-ala haya kama agizo la Mwenyezi Mungu linavyotutaka". Sasa na nyinyi munanishukuru nini?

Munasema "Sisi tunapenda kumfahamisha kuwa suala hili la kwamba mwezi ukiandama sehemu moja unatosheleza kufuatwa kwa kufunga au kufungua ulimwengu mzima, si suala jipya bali ni jambo la kale. Tunasikitika kwamba hakuangalia vizuri maoni ya Wanavyuoni wakubwa walivyoelezea msimamo huo. Angalia katika kitabu cha Shaykh Naaswir Bachuu uk 51-58. Hapa tunanukuu baadhi ya kauli hizo:

Imamun-Nawawy aliyekisherehesha Kitabu cha Sahihi Muslim anasema:

"Na jambo lililo sahihi kwa wenzetu (Mashaffi) ni kuwa muandamo mmoja hauwahusu watu wote bali unawahusu wale walio karibu kwa kiasi ambacho hawaruhusiki kupunguza Sala (Sala ya safari). Pia imesemwa kuwa iwapo matlai ni mamoja watalazimika (watu) kufunga pamoja. Pia imesemwa kuwa ikiwa (wanaishi) katika eneo la Iklimu moja (maili 72 au km 89) (watalazimika kufunga pamoja) vyenginevyo kila mmoja atafunga kwa muandamo wake. Na wakasema wenzetu wengine (Mashaffi) kuwa muandamo katika sehemu moja utawahusu wote wa dunia nzima".

Shaykh Jaadul Haq wa chuo kikuu cha Al-Azhar katika kitabu chake "Bayaanullinnas" J. 2 uk 203 - 204 ameandika yafuatayo juu ya kauli hiyo ya Imamun-Nawawy:

"Hapa Imamu An-Nawawy ametaja kwa mukhtasari kauli zilizomo katika madhehebu ya Kishaffi (juu ya kuandama kwa mwezi) na ambazo pia zimo katika madhehebu mengine ya Kiislamu. Kauli hizo tunaweza kuzigawa katika maf ungu matatu makuu: "...Hapo Imamu An-Nawawy ametaja kwa mukhtasar kauli zilizomo katika madhehebu ya Shaffi (juu ya kuandama kwa mwezi) na ambazo pia zimo katika madhehebu nyengine za Kiislam. Kauli hizo tunaweza kuzigawa katika mafungu matatu makuu: Kauli ya kwanza: "Kila nchi iwe na matlai yake, wala muandamo wa nchi moja hautalazimu nchi nyengine ya mbali wala karibu". Kauli ya pili: "Muandamo wa nchi moja unalazimu nchi zote za dunia hata kama ziko mbali".

Kauli ya tatu: "Muandamo wa nchi moja unalazimu nchi iliyo karibu nayo au inayowafikiana kimatlai". Kisha, Shaykh Jaadul-Haq akaendelea kusema kwamba:

"Na (kauli) zote hizo ni maoni yatokanayo na Ijtihaadi ambazo hazikusimama juu ya hoja kat-ii, si sanad wala matni. Kwa hivyo ingefaa ichaguliwe kauli ambayo inakubaliana na maslahi ya (Waislam wote wa) dunia nzima kwa jumla"."

Jawabu Sikubaliani na mtazamo wa Sheikh Shaykh Jaadul Haq wa chuo kikuu cha Al-Azhar, kwamba zote hizi ni rai na itihad kwani kanuni ni kuwa "Hakuna ijtihadi mbele ya andiko" Ijtihad mwahala mwake ni musimo andiko. Wakatika katika suala hili, utaona kwamba asemaye kuwa tufunge kwa muandamo mmoja, hoja yake ni Hadithi "Fungeni kwa kuuona"; na anayesema kuwa kila mahala na muandamo wake, anatoa ushahidi wake ni Hadithi ya Ibn Abbaas na Kuraib. Kwa hivyo, ijtihad ni katika kuyafahamu maandiko: si ijtihad kwa maana ya rai tupu pasi na andiko kama alivyosema Sheikh. Kilichobaki ni kuzijadili riwaya mbili hizi zina maana gani?

Munasema Tungependa kumueleza ndugu yetu kwamba hata hapa Afrika ya Mashariki jambo hili hakulianzisha Shaykh Naaswir Bachuu kama alivyodai mwenyewe (Nd. Juma) kwamba: (Muafrika wa Mashariki wa kawaida kusikia sauti ya mgogoro)) Inasikitisha hakuweza kuangalia katika kitabu cha Shaykh Naaswir Bachuu uk 161-163 wametajwa walioonyesha kwa vizuri kabisa misimamo hiyo tofauti. Mashaykh wenyewe ni hawa wafuatao: Al-marhuum Shaykh Juma Abdul Waduud (wa Zanzibar), Shaykh Abdillahi Naaswir ( Nairobi Kenya ), na Shaykh Naaswir Khamis Abdul Rahman ( Mombasa Kenya ).

Jawabu Kwani wapi katika kitabu changu nilisema kuwa Sheikh Nassor Bchoo ndiye aliyeanzisha fikra hii hapo Afrika ya Mashariki hata mukaleta dai hili? Mimi nimeeleza kuwa zamani Afrika Mashariki watu wote wakifata muandamo mmoja. Nilisema: Karne zimepita bila ya sikio la Muafrika wa Mashariki wa kawaida kusikia sauti ya mgogoro juu ya suala la muandamo wa mwezi. Harakati za elimu zilipobadilika na kuelekea zaidi - kwa kujua au bila kujua - katika mrengu wa Kihanbali na Kiwahabi, pakajitokeza mapinduzi ya ghafla ya fikra na matendo. Dr. Ramadhan Al-butti - miongoni mwa wanavyuoni wakubwa wa ulimwengu wa sasa - anaona kwamba harakati hizi hazisifiki kama ni madhehebu: bali ni hatua (phase) katika mapito ya Historia.

Na katika uk. 97, nimesema:

Kwa kwetu - Afrika Mashariki - kusema kwamba mwezi muandamo wa nchi moja ni muandamo kwa nchi nyengine zote za dunia ni kitu kipya. Kwa hivyo, ni wazi kwamba mimi nazungumzia Afrika Mashariki. Na mfano wa hilo pia kalisema Sheikh Nassor Bachoo, lakini yeye hamukumjibu. Anasema: "Pamoja na kuwa mgogoro wa kuandama kwa mwezi umeanza kuonekana hadharani katika jamii za Waislam wa hapa Afrika ya Mashariki katika miaka ya hivi karibuni". Inasikitisha kwamba hata maneno yangu mumeyakata na kuchukua yale ambayo hayakamilishi maana nilioilenga. Maneno "Karne zimepita" hamukuyataka kwani hayakufikisheni kule mutakako!

Pili narejea tena kusema kwamba hao wanavyuoni aliowataja Sheikh Nassor, hawajathibitisha habari za kuwa watu wafunge au wakifunga kwa muandamo mmoja Africa Masharik, ukimtoa Sheikh Nassir Khamis wa Mombasa ambaye naye pia ni mtu wa sasa. Ama sheikh Juma Abdu-Wadood yeye, kwa mujibu wa nakala hio ya Sheikh Nassor Bachoo, kasema hivi: Kuona huku kwa mwezi kumekusudiwa kuonekana na Waislam, na kuonekana na Waislamu huko, sio lazima kuonekana na Waislamu wote. Bali inatosha shahada ya mtu mmoja muadilifu".

Pia inampasa mtu mmoja pekee kama ameuona mwezi yeye afunge na kila aliyemuamini; hata akiwa haijakubaliwa shahada yake. Haya ndio maneno ya Sheikh Juma Abdu-Wadood kwa mujibu wa alivyomnukuu Sheikh Bachoo. Sasa ikiwa ndugu zetu mumeshindwa kuyafahamu maneno haya ya Sheikh Juma Abdu-Wadood, bado mutaendelea kupoteza watu bila ya elimu?! Sheikh Juma Abdul-Wadood hapa anazungumzia mas-ala ya ushahidi kwamba si lazima - katika suala la kuonekana kwa mwezi - kwamba kila mmoja auone: bali akiona mtu mmoja basi inatosha kwa wengine kufunga. Hii ndio kauli ya Sheikh Juma Abdul-Wadood na hili nimelieleza kwa urefu katika kitabu changu.

Kisha Sheikh Juma Abdul-Wadood akazungumzia suala la kufunga kwa muandamo mmoja akasema: "Rai za Maimamu wengine wameifasiri hadithi isemayo: (Fungeni kwa kuuona Mwezi) kwamba ukionekana popote mashariki au magharibi (watu) wafunge; hapana kutazama masafa fulani au nini. Hii ni rai nayo na wengi wamesema (hivyo) kama Imamu Malik , Ahmad na kundi kubwa la Hanafi. Inakurubia kuwa n dio rai ya Jamhuri - kufata rai hii ni kuhakikisha umoja wa dunia nzima. Wala hatuwezi kusema kwamba rai ya Shaffiy ndio ya Jamhur". Hapa Sheikh Juma anasimulia rai za Maimamu wengine: si rai za Maulamaa wa Afrika Mashariki. Mimi dai langu nililodai ni kuwa jambo hili la kufunga kwa muandamo mmoja, napenda munifahamu: ni jipya kwa Africa Mashariki. Mimi sikusudii jambo la wanazuoni kuzungumzia rai mbali mbali: bali nazungumzia jambo la watu kufata muandamo mmoja kwamba karne zimepita ya sikio la Muafrika Mashariki wa Kawaida halijiapata kusikia. Na nimetumia maneno "Muafrika wa Mashariki wa kawaida" ili kuwatoa wanavyuoni wao hata kama walikuwa hawafati kauli hio, lakini wanaijua. Kwa hali yoyote ile:

1) Sheikh Juma Abdul-Wadoo hajazungumzia kwamba Afrika Mashariki watu walikuwa wakifunga au wafunge kwa muandamo mmoja, bali kazungumzia rai za wanavyuoni wasio wa Afrika Mashariki - Al-Imamu Shafi, Hanbal n.k. Na mimi sijakanusha tafauti hizi.

2) Kauli yake ilikuwa ni kuhusu suala la mashahidi.

Ama Sheikh Abdillahi Nassir, yeye ni mwanachuoni wa sasa. Na mimi sijasema kuwa sasa hakuna rai hizo. Pili ni kuwa nakala alizotupa Sheikh Bachoo za kitabu cha Sheikh Abdillahi utaona kwamba Sheikh Abdillahi hazungumzii kuwa kauli ya kufatwa ni ile ya muandamo mmoja; bali yeye kasema kuwa hili ni suala la khilafu kwa hivyo tusigombane kila mtu afate rai anayoiona kuwa ni sawa. Sheikh Abdillah kayasema haya baada ya kutokea mizozo hii ya sasa. Kwa hivyo tunarudi pale pale kwamba "Karne zimepita bila ya sikio la Muafrika wa Mashariki wa kawaida kusikia sauti ya mgogoro juu ya suala la muandamo wa mwezi. Harakati za elimu zilipobadilika na kuelekea zaidi - kwa kujua au bila kujua - katika mrengu wa Kihanbali na Kiwahabi, pakajitokeza mapinduzi ya ghafla ya fikra na matendo". Kwa hivyo, nukta hii hamukuuijibu: na wala sioni kuwa kuna haja ya kuijibu kwani haina umuhimu katika maudhui yetu. Bali kitabu chenu chote, munachagua mambo yasio na umuhimu "Juma kantutukana; Juma kanfanya hivi" nyinyi ndio munajibu baada ya kuzungumzia dalili za kielimu.

Ama Sheikh Nassor: yeye pia ni mtu wa sasa na ni mfuasi wa skuli hio hio munayoifuata nyinyi, kwa hivyo kusema kwake alivyosema hakujapindua nilioyasema kuwa - kimatendo - hili ni suala jipya kwa kwetu Afrika ya Mashariki. Wala mimi sikusema kuwa Sheikh Nassor Bachoo ndiye muasisi wa fikra hio huko kwetu. Naomba munifahamu ninachokisema kwanza kisha ndio munijibu. Na sijui munapinga nini kitu ambacho watu wote wanakijua. Bila ya kusahau kwamba mimi sikusudii kusema kuwa kitu sahihi ni kilichofanywa zamani au kilichofanywa leo: laa! Bali kitu sahihi ni chenye ushahidi sahihi uliojengeka juu ya misingi sahihi ya kielimu. Na kielimu, suala la kuzingatia muandamo mmoja - hamutoweza kulithibitisha.

MNASEMA

Pia Shaykh Ahmad Al Khalil, Mufti wa Omani amethibitisha kwamba Ikhtilaf hii ya muandamo wa mwezi katika hukmu ya kufunga au kufungua ipo na kwamba ni jambo la kale. Kama alivyosema maneno yake yaliyotafsiriwa na Shaykh Muniir Sulayman 'Aziz kwamba: "Hakuna madhehebu iliyokuwa imesalimika na kuwa na Khitilafu baina ya Wanavyuoni wake juu ya suala la kutafautiana miandamo ya mwezi." Jee ndugu Juma anataka kusema kwamba Shaykh Naaswir Bachuu ndiye mwalimu aliyeanzisha madhehebu zote? Au ndiye aliyeanzisha mtafaruku huu kama alivyouita mwenyewe ndugu Juma?

JAWABU

Suala hilo jiulizeni wenyewe; mujijibu wenyewe; kwani nyinyi ndio mulioliunda: mimi sikusema hivyo kamwe bali nilichokisema ni hiki: "Kwa kwetu - Afrika Mashariki - kusema kwamba mwezi muandamo wa nchi moja ni muandamo kwa nchi nyengine zote za dunia ni kitu kipya". Nami sikusudii kusema kwamba upya huo ni katika kuzungunzwa au kusomwa suala hilo katika vitabu; nakusudia kimatendo sula hili lilikuwa halipo Afrika Mashariki. Sasa ili muwe mumenijibu, twambieni nani alikuwa akifata muandamo mmoja hapa Afrika Mashariki. Jamani! Tafuteni hoja mujadili: musijadili kitu kisichokuwa na umuhimu. Kama hamuna hoja nyamzeni musijitie aibu!

MNASEMA

Katika kudhihirisha udhaifu wake wa kumuandama mtu fulani; Ndugu Juma anasema: (Kama tunavyojua kwamba Sheikh Nassor Bachoo, ni mmoja wa wenye kusisitiza ulazima wa kuwa na muandamo mmoja.) Sisi kwa upande wetu tunasema: Katika kitabu cha Shaykh Naaswir Bachuu hakuna pahala alipolazimisha watu wafuate huo aliouita ndugu Juma (msimamo wa Shaykh Naaswir). Bali yeye ameonesha mitizamo ya Wanavyuoni kwa kutumia Aya za Qur-aan, Hadiythi na vitabu vinavyokubalika. Lugha aliyotumia Shaykh Naaswir katika huo unaonekana ni msimamo wake ni maneno yaliyozimuliwa kilugha (polite language) kama vile: (inawezekana) ((inaonyesha) .

JAWABU

Na mimi hapa sijasema kuwa Sheikh Nassir Bachoo kalazimisha watu wafunge kwa muandamo mmoja. Nimesema "Anasisitiza ulazima" yaani yeye analingania msimamo huo kwani kwake ndio msimamo sahihi na ndio wajibu kuufata. Naomba tena tuelewane musiseme kitu kinyume na nilivyosema. Wala musitafute kitu kisicho na maana mukajadili eti ndio jawabu! Pili maneno yenu: "Katika kudhihirisha udhaifu wake wa kumuandama mtu fulani". Sasa je na nyinyi pia munaonesha udhaifu huo huo kwa kumuandama mtu fulani katika kitabu chenu?

MNASEMA

Aliyelazimisha rai ni ndugu Juma mwenyewe kama anavyosema: (Lakini kilicho lazima na ambacho tunatakiwa tukubaliane ni kuwa muandamo wa mbali hautendewi kazi mbali) [uk. 112]

JAWABU

Bali hata Sheikh Bachoo pia kalazimisha kwani ukidai kuwa huu ndio msimamo wa haki au ndio msimamo sahihi au ndio wajibu kufatwa, bila kusema kuwa rai zote zinafaa basi na wewe huwa umelazimisha rai yako. Sasa je Sheikh Bachoo anakubali hivyo kuwa rai zote ni sawa? Mimi kweli sisemi kuwa rai zote ni sawa: nasema kuwa nyinyi mumekosea na sahihi ni kinyume na munavyofanya, na kwa hivyo bado nipo katika msimamo wangu huo huo kwamba: "Kilicho lazima na ambacho tunatakiwa tukubaliane ni kuwa muandamo wa mbali hautendewi kazi mbali".

MUNASEMA

"Kisha katika uk 85 ndugu Juma anataja kwamba msimamo huu wa muandamo mmoja kwa dunia nzima ni ((kitu kipya)) na kwamba jambo hilo halitekelezeki na ni kauli iliyobaki vitabuni tu baada ya kutaja baadhi ya nchi zinazofuata miandamo yao - yaani kila nchi na muandamo wake kama Al-yaman , Oman , Misri na Saudia. Kisha hapo hapo akataja: ((isipokuwa Imarati katika miaka ya mwisho wamekuwa wakifata Saudia.)) Inafaa ndugu Juma aulizwe masuala yafuatayo:

i) Kama ni jambo lisilotekelezeka vipi tena Imarat wanalitekeleza?

ii) Je hawa wa Imarat nao ni wanafunzi wa Shaykh Naaswir Bachuu?

iii) Kwani hiyo sio kauli ya Jamhuur ambayo ndio msimamo wa maimamu wakubwa wakiwemo Ahmad bin Hanbal, Malik na Abu Hanifa? (Angalia pia sehemu ya 11 na 13 za kitabu hiki)

JAWABU

Kwanza mumemefanya ghushi: maneno yangu hamukuyanukuu yote. Mimi nimesema: "Kwa kwetu - Afrika Mashariki - kusema kwamba mwezi muandamo wa nchi moja ni muandamo kwa nchi nyengine zote za dunia ni kitu kipya". Nyinyi maneno "Kwa kwetu Afrika Mashariki" mumeyatoa ili ionekane kuwa mimi nasema kuwa hili ni suala jipya kila pahala. Watu kama nyinyi vipi tutakuamini katika dini yenu na uadilifu wenu, ikiwa munaghushi maandiko hivi? Hii ndio kamati ya Msikiti Sunna na hii ndio suna yenyewe?! Halafu mukaendelea na tadlis (ghushi) yenu mukasema: "Na kwamba jambo hilo halitekelezeki na ni kauli iliyobaki vitabuni tu". Mimi sikusema hapa kuwa "Halitekelezeki", bali nimesema:

Lakini ukweli ni kuwa hata katika nchi nyengine zote za dunia taqriban kauli kwamba tufunge kwa muandamo mmoja, ni kauli ilioishia katika vitabu tu, kimatendo (practically) kauli hio haitumiwi isipokuwa na mtu mmoja mmoja. Hadi leo hii: watu Al-yaman wanafata muandamo wao, Oman wanafata muandamo wao, Saudia wanafata muandamo wao, Misr wanafata muandamo wao na nchi zote taqriban ni hivyo, isipokuwa Imarati katika miaka ya mwisho wamekuwa wakifata Saudia.

Haya nionesheni hapa maneno "Halitekelezeki". Mimi nimesema kuwa kimatendo kauli hii, hadi leo haitendewi kazi isipokuwa na baadhi ya watu. Nyinyi mumebadilisha na kuweka ghushi yenu mukasema nimesema halitekelezeki. Kwa hivyo, hilo Sula (a na b) jibuni wenyewe kwani mumesema kinyume na nilivyosema. Suala (d), najibu kuwa sio: hio si kauli ya jumhur bali jumhur kauli yao ni kinyume na hivyo na hili nimelithibitisha katika uk. 189-193 wa chapa ya pili ya kitabu changu au uk. 171 wa kitabu hicho chapa ya kwanza. Na Al-Imamu Malik riwaya zake zimegongana na riwaya kwamba kila watu na muandamo wao ndio ilio bora kwani ni riwaya ya Madina aliko kuweko Al-Imamu Malik, wakati riwaya nyengine ni ya watu wa Irak kulikokuwa na viwanda vya kutunga riwaya!

MNASEMA

Na sisi tunamuongezea habari moja ambayo ni vyema kuielewa, kwamba nchi ya Uganda iliyo katika Afrika ya Mashariki pia inafuata rasmi muandamo mmoja wa duniani. Pia aelewe kwamba huo msimamo wa kila nchi na mwezi wake huku Afrika ya Mashariki haukuwepo tokea zamani. Mashaykh wote wa huku wanakubaliana mwezi ukionekana popote katika nchi hizi tatu ( Kenya , Uganda na Tanzania ) wanafunga pamoja. Yeye anaendelea kushika msimamo wake: (Al-yaman wanafata muandamo wao, Oman wanafata muandamo wao, Saudia wanafata muandamo wao). Lile analoliona yeye halitekelezeki, basi ndio linatekelezeka.

JAWABU

1) Kitu rasmi Uganda hakizingatiwi kwani Uganda kimsingi sin chi ya Kiislamu wala ya Waislamu: Waislamu ni wachache ukilinganisha na Wasio Waislamu. Kwa hivyo, hakuna kitu rasmi. Na jambo hilo ni jambo la sasa. Na mimi sijapinga kwamba sasa fikra hio ipo Afrika Mashariki.

2) Ama kauli yenu: "Mashaykh wote wa huku wanakubaliana mwezi ukionekana popote katika nchi hizi tatu ( Kenya , Uganda na Tanzania ) wanafunga pamoja". Ndio maana nikatumia lafdhi "Kwa kwetu Afrika Mashariki" nikijua kuwa wanavyuoni wote wa kwetu Afrika Mashariki wana msimamo huo. Ama kauli yenu: "Yeye anaendelea kushika msimamo wake: ((Al-yaman wanafata muandamo wao, Oman wanafata muandamo wao, Saudia wanafata muandamo wao,)). Lile analoliona yeye halitekelezeki, basi ndio linatekelezeka". Mwisho wa kunukuu. Inaonesha kuwa kitabu changu mumekijibu bila ya kukifahamu. Nilichosema ni kuwa, ijtihadi ifanywe katika kubainisha wapi hadi wapi watu wafunge pamoja. Kwa vile, hakuna andiko lililobainisha hivyo. Ama muandamo mmoja kwa dunia nzima hili ni kinyume na andiko. Kwa hivyo, wakiwa wanavyuoni wa zamani wamefanya ijtihad hio, sisi tunafata ijtihad yao kwa vile hapa ni mahala pa ijtihad na haikugongana na andiko. Ama madai yenu nyinyi ni kinyume na andiko lilivyoonesha.

MNASEMA

"Kuna suala moja la nyongeza tunapenda tumuulize ndugu yetu Juma: Hata kama hizo nchi alizozitaja ( Al-Yaman , Oman , Misri na Saudia) hazijakubaliana kufuata muandamo mmoja, je hakuna uwezekano (japo wa sadfa) unaoweza kutokea kufunga siku moja ijapokuwa kila mmoja ameona mwezi katika nchi yake? Sasa tuseme kila nchi katika hizo imeona mwezi usiku wa Alkhamisi kuamkia Ijumaa - Wote si watafunga siku moja ya Ijumaa? Basi huo ndio utekelezaji aliosema hautekelezeki. Ni wazi kuwa unatekelezeka.

JAWABU

Munaendelea kuuliza masula haya kwa sababu masuala yenu mumeyajenga katika kitu nisichokisema kamwe. Wapi nimesema kuwa "Hilo halitekezeki" hata mukauliza masuala haya?


11

12

13

14

15