ILI NIWE PAMOJA NA WAKWELI

ILI NIWE PAMOJA NA WAKWELI 0%

ILI NIWE PAMOJA NA WAKWELI Mwandishi:
Kundi: Midahalo na majadiliano kielimu

ILI NIWE PAMOJA NA WAKWELI

Mwandishi: TIJANI SAMAWI
Kundi:

Matembeleo: 35344
Pakua: 3141

Maelezo zaidi:

ILI NIWE PAMOJA NA WAKWELI
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 21 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 35344 / Pakua: 3141
Kiwango Kiwango Kiwango
ILI NIWE PAMOJA NA WAKWELI

ILI NIWE PAMOJA NA WAKWELI

Mwandishi:
Swahili

13

ILI NIWE PAMOJA NA WAKWELI

MUT'A (AU NDOA YA MUD A)

Kinachokusudiwa ni ndoa ya Mut'a au ndoa ya muda au ndoa ya wakati maalum, na ndoa hii ni sawa na ndoa ya kudumu, kwani haisihi isipokuwa kwa mafungamano yanayokusanya Qabul na I'jab, kwa mfano mwanamke aseme, "Nimekuozesha nafsi yangu kwa mahari kiasi kadhaa," Basi na mwanamume aseme "Nimekubali." Na ndoa hii inazo sharti zake ambazo zimetajwa ndani ya vitabu vya Fiqhi kwa (Madhehebu ya) Imamiya kama vile kubainisha mahari na muda, basi huwa inasihi kwa kila kile ambacho pande mbili hizi zitaridhiana, na (sharti nyingine) ni kama vile uharamu wa kutamatui (kumuona) mwanamke ambaye ni haramu kisheria kumuoa, kama ilivyo katika ndoa ya daima. Na ni juu ya mwanamke aliyeolewa ndoa ya Mut'a kukaa eda baada ya kumalizika muda wa ndoa kwa hedhi mbili na atakaa eda miezi minne na siku kumi kama mumewe atafariki (kabla ya muda kwisha).

Na wawili hawa walioowana ndoa ya Mut'a hawarithiani wala hakuna (sharti ya wajibu wa) chakula (kwa mume kumlisha mke) na mke hamrithi mume wala mume hamrithi mke, na mtoto aliyezaliwa ndani ya ndoa ya Mut'a ni sawa na mtoto aliyezaliwa ndani ya ndoa ya daima kikamilifu kabisa, katika haki za urithi, chakula na haki zote za malezi, maadili ya kimwili na mafunzo, na ni mtoto wa baba huyo. Hii ndiyo ndoa ya Mut'a kwa sharti zake na mipaka yake nayo ni kama uionavyo, siyo miongoni mwa uzinzi kwa hali yoyote ile kama wanavyodai watu.

Na Masunni kama ilivyo kwa ndugu zao Mashia wanaafikiana kuhusu sheria ya ndoa hii kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu iliyopo katika aya ya ishirini na nne ndani ya Suratun-Nisai pale Mwenyezi Mungu aliposema: "Wale mtakaostarehe nao (mtakao waoa Mut'a) miongoni mwao, wapeni mahari yao (ambayo) ni faradhi, wala si vibaya kwenu katika yale muliyoridhiana badala ya yale yaliyotajwa, bila shaka Mwenyezi Mungu ni mjuzi tena mwenye hekima." Ni kama ambavyo pia wameafikiana (Sunni na Shia) kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) aliiruhusu ndoa ya Mut'a na Masahaba walioa (kwa ndoa hiyo) zama zake Mtume.

Isipokuwa wamehitilafiana (Sunni na Shia) kuhusu kufutwa kwa ndoa hiyo au kutokufutwa, kwani Masunni wanasema imefutwa na kwamba iliharamishwa baada ya kuwa ilikuwa ni halali, na kwamba kufutwa huko ilifutwa na Sunna na siyo Qur'an. Shia wao wanasema kuwa ndoa hiyo haikufutwa na kwamba ni halali mpaka siku ya kiyama. Kwa hiyo basi uchambuzi unafungamana tu na kuhusu kufutwa kwa ndoa hiyo au kutokufutwa, na kuzichunguza kauli za pande mbili ili iweze kumbainikia msomaji wazi wazi jambo hili na kwamba wapi ndiko kunakopatikana haki, basi aifuate bila ya chuki na upendeleo.

Ama kwa upande wa Mashia wasemao kwamba haikufutwa na ni halali mpaka siku ya kiyama, hoja yao ni kuwa: Haikuthibiti kwetu sisi kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu aliikataza ndoa hiyo, na Maimamu wetu kutoka katika kizazi kitukufu cha Mtume, wao wanasema kuwa ni halali. Na lau ingekuwa imefutwa na Mtume (s.a.w.), basi Maimamu wa nyumba ya Mtume wangelilijua jambo hilo wakiongozwa na Imam Ali, kwani watu wa nyumba ya Mtume (s.a.w.) ndiyo wajuao mno yaliyomo ndani ya nyumba hiyo. Lakini kilichothibiti kwetu sisi ni kwamba Khalifa wa pili Umar bin Al-Khatab ndiye aliyeikataza ndoa hii na akaiharamisha kwa Ij-tihadi yake kama wanavyoshuhudia wanachuoni wa Kisunni wenyewe. Sisi hatuwezi kuacha hukumu ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake kwa ajili ya (kufuata) maoni na Ij-tihadi ya Umar bin Al-Khatab.

Basi huu ni muhtasari wa yale wayasemayo Mashia juu ya uhalali wa Mut'a nayo ndiyo kauli ya sawa na ni mtazamo bora. Waislamu wote wanatakiwa wafuate hukmu za Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wampinge asiyekuwa Mwenyezi Mungu na Mtume wake hata kama anacheo gani pindi Ij-tihadi yake itapokwenda kinyume cha Qur'an na Sunna. Ama Masunni wao wanasema kwamba, Mut'a ilikuwa halali na Qur'an ilishuka kuhusu Mut'a na Mtume aliiruhusu na masahaba wakaifanya, kisha baada ya hapo ilifutwa, na wanatofautiana juu ya kilichoifuta. Wapo miongoni mwao wanasema kwamba, "Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) aliizuwia kabla ya kufa kwake, na wengine wanasema kwamba Umar bin Al-Khatab, ndiye aliyeiharamisha, na kauli yake (Umar) kwetu sisi (Masunni) ni hoja (yenye nguvu) kufuatia kauli ya Mtume (s.a.w.) aliposema: "Shikamaneni na Sunna zangu na Sunna za Makhalifa wangu viongozi baada yangu zishikeni kwa nguvu.

Ama wale wasemao kuwa Mut'a ni haramu kwa kuwa Umar bin Al-Khatab aliiharamisha na kwamba kitendo cha Umar ni sunna ya lazima (kufuatwa). Basi watu hawa sisi hatuna maneno nao wala hatuna uchambuzi wowote, kwani (mtazamo wao huo) ni wa kung'ang'ania na kujikusuru. Itakuwaje Mwislamu aache kauli ya Mwenyezi Mungu na kauli ya Mtume na awapinge kisha afuate kauli ya mtu mwenye kujitahidi, anayekosea na kupatia, na hali hii ya kujitahidi kwake juu ya mas-ala fulani (inaweza kuchunguzwa) iwapo ndani ya Qur'an na sunna hakuna tamko (linalohusu ufumbuzi wa mas-ala hayo) ama kama tamko litakuwepo basi, "Haifai kwa Muumini mwanamume na Muumini mwanamke pindi Mwenyezi Mungu na Mtume wake watakapoamua jambo wawe na hiyari katika jambo lao (hilo lililoamriwa) na yeyote atakayemuasi Mwenyezi Mungu na Mtume wake bila shaka amepotea upotevu ulio wazi". (Qur'an, 33:36)

Na yeyote asiyekubaliana nami juu ya kanuni hii basi ni juu yake kuyarejea maarifa yake na ufahamu wake kuhusu (muongozo) na sheria ya Kiislamu na aisome Qur'an Tukufu na Sunna ya Mtume kwani Qur'an yenyewe binafsi imeeleza katika aya iliyotajwa hapo juu, na aya zingine mfano wa hiyo ni nyingi mno zinafahamisha juu ya kukufuru na kupotea kwa mtu yeyote asiyeshikamana na Qur'an na Sunna ya Mtume (s.a.w.). Ama kwa upande wa dalili ya Sunna tukufu ya Mtume ziko dalili nyingi vile vile, lakini tunatosheka na kauli moja ya Mtume (s.a.w.) isemayo: "Halali iliyo halalishwa na Muhammad ni halali mpaka siku ya Kiyama, na haramu iliyoharamishwa na Muhammad ni haramu mpaka siku ya kiyama. Hivyo basi hana haki mtu yeyote kuhalalisha au kuharamisha katika mas-ala ambayo ndani yake yamethibiti maandiko na ni hukumu kutoka kwa Mwenyezi Mungu au kwa Mtume wake (s.a.w.).

Na kwa yote haya tunawaambia hao wanaotaka kutukinaisha kwamba vitendo vya Makhulafaur-Rashiduna na Ij-Tihadi zao vinatulazimu, sisi tunasema: "Hivi mnajadiliana nasi juu ya jambo la Mwenyezi Mungu ambaye ni Mola wetu na ni Mola wenu, na sisi tuna matendo yetu nanyi mnayo matendo yenu, nasi kwake Mwenyezi Mungu tunajitakasa" (Qur'an, 2:139) Wanaozungumzia dalili hii (bila shaka) wanakubaliana na Mashia kwenye madai ya (kuwa Mtume hakuiharamisha Mut'a) na wanakuwa ni hoja dhidi ya ndugu zao Masunni (wasemao kuwa Mtume aliiharamisha). Hivyo basi uchunguzi wetu tunaufungamanisha tu na kundi lisemalo kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) ndiye aliyeiharamisha na akaifuta (aya ya) Qur'an kwa hadithi.

Watu wasemao hivi wanajikanganya wenyewe katika kauli zao na hoja zao zi tupu hazina msingi imara, japokuwa imepokewa kwa Muslim ndani ya sahih yake kuhusu katazo (hilo linalodaiwa), kwani lau kungekuwa na katazo litokalo kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.), basi katazo hilo lisingefichikana kwa masahaba ambao walioa Mut'a katika zama za Ukhalifa wa Abubakar na sehemu fulani ya Ukhalifa wa Umar kama alivyosimulia jambo hilo Muslim ndani ya sahih yake. Taz: Sahih Muslim Juz. 4 uk. 158. Amesema A'ta', "Jaabir bin Abdillah alikuja hali ya kuwa anafanya Umra nasi tukamfuata nyumbani kwake, watu wakamuuliza mambo mengi, hatimaye wakamuuliza juu ya Mut'a akasema ndio tuliowa zama za Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) na zama za Abubakar na Umar".

Basi lau Mtume wa Mwenyezi Mungu angekuwa ameikataza Mut'a, isingejuzu kwa Masahaba kufanya Mut'a katika zama za Abubakar na Umar kama ulivyosikia. Ukweli uliopo ni kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) hakukataza Mut'a wala hakuiharamisha, bali katazo lilitokana na Umar bin Khatab kama yalivyokuja maelezo ya jambo hilo ndani ya Sahih Bukhar. Imepokewa toka kwa Musaddad, ametusimulia Yahya kutoka kwa Imran Abu Bakr, ametusimulia Aburajaa kutoka kwa Imran bin Huswain (r.a.) amesema: "Aya ya Mut'a ilishuka ndani ya Kitabu cha Mwenyezi Mungu, basi tukaitenda wakati wa Mtume wa Mwenyezi Mungu, na haikushuka Qur'an kuiharamisha na wala Mtume hakukataza mpaka alipokufa Mtume, basi mtu fulani kwa maoni yake akasema aliyoyataka, Muhammad akasema, inasemekana mtu huyo ni Umar". Taz: Sahih Bukhar Juz. 5 uk. 158.

Ewe Msomaji unaona ya kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) hakuikataza Mut'a mpaka kufa kwake kama alivyobainisha Sahaba huyu. Na unamuona anaunasibisha huu uharamishaji kwa Umar wazi wazi bila ya kificho na anaongeza kuwa yeye Umar alisema ayatakayo kwa maoni yake. Huyu hapa Jabir bin Abdillah Al-Ansari anasema wazi wazi kama ifuatavyo:"Tulikuwa tunaoa Mut'a kwa gao la tende na unga kwa siku kadhaa, katika zama za Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) na (zama za) Abubakar mpaka Umar alipokataza kutokana na suala la A'mri bin Hurayth. Taz: Sahih Muslim Juz. 4 uk. 131. Na miongoni mwa mambo yanayotujulisha kwamba baadhi ya Masahaba walikuwa na mtazamo kama wa Umar jambo ambalo si geni ni kuwa, imetangulia katika uchambuzi wetu kuhusu msiba wa siku ya Al-Khamis ya kwamba baadhi ya Masahaba walimuunga mkono Umar katika kauli yake aliposema kuwa "Mtume wa Mwenyezi Mungu anaweweseka kinatutosha kitabu cha Mwenyezi Mungu'!! Kwa hiyo ikiwa walimtia nguvu kwenye jambo la hatari kama hili ambalo alimtuhumu Mtume (s.a.w.) basi ni kwa nini wasikubaliane naye katika baadhi ya Ij-tihadi zake?

Hebu na tuisikilize kauli ya mmoja wao (hao Masahaba wanaomuunga mkono Umar): "Nilikuwa kwa Jabir bin Abdillah, mara alimjia mtu fulani akamwambia: ibn Abbas na ibn Zubair wanahitilafiana kuhusu Mut'a mbili (Mut'a ya ndoa na Mut'a ya Hija) basi Jabir akasema zote mbili tulizifanya zama za Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) kisha akatukataza Umar basi hatukurejea tena (kuzifanya). Taz: Sahih Muslim Juz. 4 uk. 131. Kwa ajili hiyo mimi binafsi naamini kabisa kwamba kuna baadhi ya Masahaba walilihusisha kwa Mtume katazo la kuharamishwa kwa Mut'a ili kuutakasa msimamo wa Umar na (kuupitisha) kuwa ni sahihi. Kinyume chake ni kuwa haiwezekani kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) kuharamisha kilichohalalishwa na Qur'an, kwani sisi hatukuti hata hukmu moja katika hukmu zote za Kiislamu ambayo Mwenyezi Mungu ameihalalisha kisha Mtume akaiharamisha, na hapana yeyote asemaye hivyo isipokuwa ni mpinzani mwenye chuki.

Na lau tutakubali ili kupata jinsi ya kujadili ya kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) aliikataza Mut'a, basi Imam Ali bin Abi Talib ambaye ni mtu wa karibu mno kwa Mtume na mjuzi mno kuliko watu wengine asingesema kama ifuatavyo: "Bila shaka Mut'a ni rehma, Mwenyezi Mungu amewahurumia kwayo waja wake, na lau siyo Umar kuikataza, basi asingezini isipokuwa mtu duni". Taz: Ath-Tha'alabi ndani ya tafsirul-Kabir, na Tabari alipoifasiri aya ya Mut'a ndani ya tafsiri yake iitwayo Alk-Kabir. Na hii ni kwa kuwa Umar mwenyewe hakuunasibisha kwa Mtume uharamishaji wa Mut'a bali amesema wazi wazi katika kauli yake ifuatayo: "Mut'a mbili zilikuweko zama za Mtume wa Mwenyezi Mungu, nami ninazikataza na nitatoa adhabu dhidi ya mwenye kuzitenda, Mut'a ya Hija na Mut'a ya wanawake." Taz: At-Tafsirul-Kabir ya Al-Fakhrur-Razi alipokuwa akifasiri kauli ya Mwenyezi Mungu "Famastamtaatum Bihi Minhunna." Na hii hapa Musnad ya Imam Ahmad bin Hanbal ambayo ni shahidi mzuri juu ya kwamba Masunni wanahitilafiana mno katika mas-ala haya, wako miongoni mwao wanaihalalisha Mut'a na wako miongoni mwao wanaofuata kauli ya Umar bin Al-Khatab wanaiharamisha.

Imam Ahmad amethibitisha kama ifuatavyo: Imepokewa toka kwa ibn Abbas amesema: "Mtume (s.a.w.) alifanya "Tamattui" (Mut'a) 'Ur-wa ibn Zubair akasema, Abubakar na Umar walikataza Mut'a, basi ibn Abbas akasema: Kinasemaje hiki Kiur-wah akasema: anasema, Abubakr na Umar walikataza Mut'a, ibn Abbas akasema: Nawaona watu hawa wataangamia, nasema kasema Mtume nao wanasema kakataza Abubakr na Umar". Taz: Musnad lmam Ahmad bin Hanbal Juz. 1 uk. 337. Na imekuja ndani ya Sahih Tirmidhi kwamba Abdalla bin Umar aliulizwa kuhusu Mut'a ya Hija akasema:"Ni halali" basi yule muulizaji akamwambia,"Hakika baba yako aliikataza", akasema Ibn Umar:"Waonaje ikiwa baba yangu aliikataza na Mtume wa Mwenyezi Mungu aliifanya,basije nifuate amri ya baba yangu au amri ya Mtume wa Mwenyezi Mungu?" Yule mtu akasema,"Bali (ufuate) amri ya Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.)."

Taz: Sahih Tirmidhi Juz. 1 uk. 157. Masunni wamemtii Umar juu ya (kuharamisha) Mut'a ya wanawake na wamempinga kuhusu Mut'a ya Hija. Pamoja na kuwa katazo lake (alilitoa) akiwa mahala pamoja kama tulivyotanguliza kueleza. Jambo la maana katika yote haya ni kuwa Maimamu wa nyumba ya Mtume (s.a.w.) na wafuasi wao wamempinga (Umar) na wakasema kuwa Mut'a zote mbili ni halali mpaka siku ya Kiyama. Na kuna wanachuoni wa Kisunni ambao wamewafuata (Mashia) katika jambo hilo na ninamtaja miongoni mwao mwanachuoni Mtukufu wa Tunis ambaye ni kiongozi wa chuo kikuu cha "Az-Zaytuni" Mtukufu Sheikh Ta'hir bin A'shur (Mwenyezi Mungu amrehemu) yeye amesema ndani ya tafsiri yake mashuhuri kuwa Mut'a ni halali pale alipoitaja aya ya "Famastamtaatum Bihi Minhunna Faa'tuhunna-Ujurahunna Faridhah." Taz: At-Tahrir Wat-tan-wir cha Ta-hir A'shur Juz. 3 uk. 5.

Basi namna hii wanachuoni wanatakiwa wawe huru katika itikadi zao wasiathiriwe na upendeleo wala ujamaa na wala wasiogope kulaumiwa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. Baada ya uchambuzi huu mfupi hakuna hoja wala chenye kuwatakasa Masunni kutokana na kebehi na tuhuma yao dhidi ya Shia kuhusu kuhalalisha kwao ndoa ya Mut'a zaidi ya dalili madhubuti na hoja bora walizonazo Shia. Muislamu anawajibika kuiangalia kwa makini kauli ya Imam Ali (a.s.) ya kwamba:"Mut'a ni Rehma, Mwenyezi Mungu amewahurumia kwayo waja wake" Na kwa hali halisi basi, ni ukubwa ulioje wa rehma ambayo inazima moto wa matamanio yenye nguvu yanayomfunika mtu awe mwanamume au mwanamke, (mpaka) akawa kama mnyama mwenye kushambulia. Ni wajibu kwa Waislamu wote na hasa vijana, wafahamu ya kwamba Mwenyezi Mungu amewajibisha kwa mzinifu adhabu ya kuuawa kwa kupigwa mawe kwa wale wenye kuhifadhika wanaume na wanawake basi hawezi Mwenyezi Mungu kuwaacha waja wake bila huruma wakati yeye ndiye muumba wao na ndiye muumba wa maumbile yao na anafahamu kitakachowarekebisha. Iwapo Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema mwenye kurehemu amewahurumia waja wake kwa kuwaruhusu kufanya Mut'a basi hakuna atakayezini baada ya ruhusa hiyo isipokuwa mtu muovu mno. (Mfano wa hili) ni kama mwizi kukatwa mkono kwani kama kutakuwa na Baytul-Mal (Bank) kwa ajili ya kusaidiwa wenye dhiki na shida basi hakuna atakayeiba isipokuwa mtu muovu.

KAULI INAYOHUSU TAHRIFUL-QUR'AN

Kauli hii kwa maana yake halisi ni mbaya sana ambayo Muislamu yeyote aliyeuamini utume wa Muhammad (s.a.w.) hawezi kuivumilia, sawa sawa akiwa ni Shia au Sunni. Hiyo ni kwa kuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu amebeba jukumu la kuilinda pale aliposema: "Hakika sisi ndiyo tulioiteremsha Qur'an na bila shaka ni sisi ndiyo tutakao ilinda." Hivyo basi haiwezekani kwa yeyote kuipunguza au kuongeza herufi moja, na hii Qur'an ndiyo muujiza wa milele wa Mtume wetu (s.a.w.) ambao hauwezi kujiwa na batili hapo kabla au hapo baadaye. Na ukweli halisi ulivyo kimatendo kwa Waislamu ni kuwa wanapinga Tahrifu ya Qur'an, kwani Masahaba wengi walikuwa wakiihifadhi kwa moyo, na walikuwa wakishindana kuihifadhi na kuihifadhisha kwa watoto wao kwa muda wote mpaka leo, hivyo haiwezekani kwa mtu fulani au kikundi fulani wala dola fulani kuigeuza au kuibadilisha.

Na lau tutaitembelea miji ya Kiislamu Mashariki na Magharibi, Kaskazini na Kusini na kila sehemu ya dunia, basi tutaikuta Qur'an ni ile ile bila ya ziyada wala upungufu, japokuwa Waislamu wametofautiana kwenye Madhehebu na vikundi na mila na mienendo. Basi Qur'an ni msukumo pekee unaowakusanya wala hawatofautiani watu wawili kuhusu Qur'an katika umma (wa Kiislamu), isipokuwa maelezo ya tafsiri, kila kikundi hufurahia yale waliyo nayo. Na yale yanayonasibishwa kwa Mashia kusema kuwa wanaipotosha Qur'an ni wazi kabisa kwamba ni tuhuma na kebehi na wala jambo hilo haliko kabisa katika itikadi za Kishia. Na endapo tutazisoma akida za Kishia ndani ya Qur'an, basi tutakuta kauli yao ya pamoja ni kukitakasa Kitabu cha Mwenyezi Mungu kutokana na kila aina ya upotoshaji.

Anasema mwenye kitabu kiitwacho "Aqaidul-Imamiyyah Sheikh Muzaffar" "Sisi tunaitakidi kwamba Qur'an ni. ufunuo wa Mwenyezi Mungu, ulioteremshwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa ulimi wa Nabii wake Mtukufu, ndani yake (Qur'an) muna ubainisho wa kila kitu, nayo ni muujiza wa kudumu ambao watu wameshindwa kuukurubia katika balagha, ufasaha na katika mambo iliyoyakusanya miongoni mwa ukweli na maarifa ya hali ya juu. Haizukiwi na mabadiliko wala mageuzi wala upotovu, na hii Qur'an tuliyonayo mikononi mwetu tunayoisoma ndiyo ile ile Qur'an iliyoteremshwa kwa Nabii, na yeyote atakayedai kinyume cha hivyo, basi mtu huyo ni mzushi au mpotoshaji au amechanganyikiwa, na wote hao hawako katika uongofu, kwani Qur'an ni maneno ya Mwenyezi Mungu ambayo hayajiwi na ubatilifu hapo baadaye wala kabla yake. Na baada ya haya, miji yote ya Kishia inafahamika, na hukmu zao ndani ya fiqhi zinaeleweka kwa watu wote, basi lau wangekuwa na Qur'an nyingine isiyokuwa hii tuliyonayo, watu wangeliitambua.

Mimi ninakumbuka wakati nilipotembelea miji ya Kishia kwa mara ya kwanza, ndani ya mawazo yangu kulikuwa na baadhi ya habari hizi, basi nilikuwa kila nionapo kitabu kikubwa hukichunguza ili huenda nikaigundua hii Qur'an inayodaiwa (kuwa ipo), lakini mawazo haya yaliondolewa kwa haraka sana, na nilifahamu hapo baadaye kuwa hiyo ni moja ya kebehi za uongo zenye lengo la kuwafanya watu wawakimbie Mashia, lakini siku zote kumebakia watu wanaowakebehi Mashia na kutoa hoja dhidi yao kwa kitabu kiitwacho; "Faslul-Khitab Fi Ithbat Tahrifi Kitabi Rabbi'l Ar-Bab" ambacho mtunzi wake ni Muhammad Taqiyyun-Nuri At-Tabrasi aliyefariki mwaka 1320 Hijriyyah naye ni Shia, na hawa wenye kuwashinikiza Mashia wanataka kuwabebesha Mashia jukumu la kitabu hiki, na jambo hili ni kinyume cha uadilifu. Basi kwani vitabu vingapi vimeandikwa ambavyo ukweli havielezi isipokuwa maoni ya mwandishi wake, na ndani yake kuna mambo machafu na mengine yenye hekima, na kuna haki na batili na humo ndani kuna makosa na mengine ya sawa na yote hayo tunayakuta kwa kila vikundi vya Kiislamu, na wala siyo kwa Mashia peke yao na wengine ikawa hakuna hali hiyo. Basi je, inajuzu kwetu sisi kuwabebesha Masunni jukumu la yale yaliyoandikwa na waziri wa utamaduni wa Misri na mkuu wa Elimu ya Kiarabu Doctor Taha Husain kuhusu Qur'an na Mashairi ya zama za Jahiliyah?

Au yale aliyoyasimulia Bukhari, kitabu ambacho ni sahihi kwao Masunni, (yasemayo) kuwa Qur'an ina upungufu na ina ziyada, pia (namna hiyo hiyo) ndani ya Sahih Muslim na vinginevyo.[93] Hebu tutupiliye mbali hayo na tuukabili uovu kwa wema, na bora ya kauli kuhusu maudhui hii ni ile iliyoisemwa na Al-Ustadh Muhammad Al-Madini Mkuu wa Kitivo cha Sheria katika Chuo Kikuu cha Az-har pale alipoandika akasema: Amma (kusema) kwamba Mashia Imamiyyah wanaitakidi kuwa Qur'an imepungua, (sisi) tunajilinda kwa Mwenyezi Mungu (kutokana na kauli hiyo) bali hizo ni riwaya tu zilizosimuliwa ndani ya vitabu vyao, kama ambavyo kuna riwaya kama hizo zilizosimuliwa ndani ya vitabu vyetu, na wanachuoni wenye kuhakiki kutoka pande hizi mbili (Shia na Sunni) wamezipinga riwaya hizo na wakabainisha upotovu wake, na hapana Shia Imamiyyah au Zaidiyyah anayeitakidi hivyo, kama ambavyo hapana Sunni anayeitakidi hivyo.

Mwenye kutaka anaweza kurejea kwenye kitabu kama "Kitabul-It'qan" cha Suyuti ili apate kuona mfano wa riwaya kama hizi tunazozitupilia mbali. Na kuna Mmisri mmoja katika mwaka wa 1498 alitunga kitabu kiitwacho "Al-Fur-Qan ambacho alikijaza riwaya nyingi kama hizi mbovu zilizoingizwa (tu) na zinapingwa, (lakini) alizinakili kutoka kwenye vitabu na rejea za Kisunni, chuo cha Az-har kiliitaka serikali ya Misri kukipiga marufuku kitabu hiki baada ya kuwa kimebainisha dalili na uchambuzi wa kielimu namna ya upotovu na uovu uliyomo. Serikali ya Misri ilikubali ombi hili na ikakipiga marufuku kitabu hicho, lakini mwandishi wa kitabu hicho alipeleka madai ya kutaka fidia, na kikao cha serikali katika idara ya mahakama kiliyatupilia mbali madai hayo.

(Sasa basi, kutokana na hali kama hii). Je, itasemwa kwamba Masunni wanapinga utakasifu wa Qur'an? Au wanaamini kuwa imepungua kwa sababu tu ya riwaya zilizosimuliwa na fulani? Au kwa sababu tu ya kitabu kilichotungwa na fulani? Basi hali ni hiyo hiyo kwa Mashia Imamiyyah, kuna riwaya ndani ya baadhi ya vitabu vyao kama riwaya zilizomo ndani ya vitabu vyetu. Kuhusu jambo hili Al-Imam Al-Allamah Said Abul-Fadhli bin Al-Hasan At-Tabrasi ambaye ni miongoni mwa wanachuoni wakubwa wa Kishia katika karne ya sita Hijiriyyah anasema ndani ya kitabu kiitwacho, "Maj-Maul-Bay an Lil-U'lumil-Qur'an""A.m.a kuweko na nyongeza ndani ya Qur'an jambo hili limewafikiwa kuwa ni wazo batili na ama wazo la kuwepo upungufu katika Qur'an limeelezwa na jamaa katika Mashia wenzetu na baadhi ya Masunni kuwa mabadiliko na upungufu upo. Na wazo sahihi kwa mtazamo wa watu wetu ni kinyume na wazo la kuwepo badiliko au upungufu, nalo ndilo alilolinusuru Murtaza Mwenyezi Mungu aitakase roho yake. Usemi wake ulikuwa wa kutosheleza katika majibu ya MASA-ILU-TARABLOSIAT.

Ametaja katika sehemu kadhaa kuwa: Kujuwa kuwa nakala ya Qur'an nakala ni sahihi ni sawa na kujuwa kuwa kuna nchi, matukio makubwa, majanga ya kutisha, vitabu mashuhuri, na mashairi ya Kiarabu,na hiyo ni kwa sababu uangalizi ulikuwa makini, na sababu za kuinakili na kuihifadhi (Qur'an) zilikamilika, zilifikia kiwango cha juu mno yote hayo ni kwa sababu Qur'an ni muujiza wa Mtume na ndiyo chimbuko la elimu za kisheria na hukumu za kidini. Wanachuoni wa Kiislamu pia walifikia kiwango cha juu kabisa katika kuihifadhi na kuilinda, walifikia hata kujuwa kila kitu wametofautiana katika Qur'an kama Irabu yake, usomaji wake, herufi zake, na aya zake. Hivyo basi pamoja na uangalifu wa yakini na udhibiti kama huu yawezekana vipi iwe imebadilishwa au kupunguzwa?

Taz: Maqala ya Al-Ustadh Muhammad Al-Madini Mkuu Kituo cha Sheria katika Chuo Kikuu cha Az-har (iliyoandikwa katika) jarida liitwalo Risalatul-Islam toleo la nne katika mwaka wa kumi na moja uk. 382 na383. Na ili ikubainikie wazi ewe msomaji kwamba tuhuma hii (ya kupunguka kwa Qur'an au kuzidi) kuwa iko karibu mno na Masunni kuliko Mashia, ni kwamba miongoni mwa mambo yaliyonifanya nizirejee(upya) itikadi zangu zote ni kila nilipokuwa nikijaribu kuwakosoa Mashia katika jambo lolote lile na kuwapinga, wao walithibitisha kutohusika nalo na wakiliambatanisha kwangu (kama Sunni kabla kuwa Shia) na ndipo nilipofahamu kwamba wao siku zote wanazungumza kweli na kwa njia ya kufanya uchambuzi namshukuru Mwenyezi Mungu kwamba nimekinaika.

Na hapa basi nakuletea yatakayothibitisha jambo hilo katika maudhui hii: Wamethibitisha Mabwana Tabrani na Baihaqi ya kwamba, Hakika ndani ya Qur'an muna sura mbili, moja wapo ni: Bismillahir-Rahmanir-Rahim Innaa Nastainuka Wanastaghfiruka Wanuthnii A'laykal-Khaira kullahu Wala nakfuruka Wanakhlau' wanatruku Man Yajjuruka ". Maana Yake: "Kwa Jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehma Mwenye Kurehemu, Hakika sisi tunakuomba msaada na tunakuomba msamaha na tunakusifu kwa mema yote na wala hatukukatai na tunajiepusha na kumuacha yule anayekufanyia maovu." Na Sura ya pili ni: Bismillahir-Rahmanir-Rahim Allahumma Iyyaka Naabudu Walaka Nusalli Wanasjudu Wailaika Nas-a' Wanahfad, Nar-ju Rahmataka Wanakhsha Adha-Bakal-Jadda Inna Adha-baka Bil-Kafirina Mul-Haq." Maana Yake: Kwa Jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehma Mwenye Kurehemu, Ewe Mwenyezi Mungu peke yako tu tunakuabudu na tunasali na kusujudu kwa ajili yako na kwako wewe tunatumika, tunataraji rehma zako na tunaiogopa adhabu yako kali, hakika adhabu yako itawapata makafiri".

Sura hizi mbili Ar-Raghibu ndani ya Muhadharat ameziita kuwa ni Sura za Qunut nazo ni miongoni mwa zile ambazo Sayyidina Umar bin Al-Khatab alikuwa akiqunuti kwazo, zinapatikana ndani ya Mus-hafu wa ibn Abbas na Mus-hafu wa Zaid bin Thabit. Taz: Al-It-Qan cha Jalal-ud-Dinis-Suyuti pia ndani ya Ad-Durrul-Manthoor. Imam Ahmad bin Hanbal amethibitisha ndani ya Musnad yake kama ifuatavyo:- "Imepokewa toka kwa Ubayyi bin Kaab amesema:"Ni aya ngapi mzisomazo ndani ya Suratul-Ahzab? akasema:Aya sabini na kidogo hivi, akasema:Hakika mimi niliisoma pamoja na Mtume (s.a.w.) mfano wa sura Al-Baqarah au zaidi kuliko hiyo na hakika ndani yake imo aya ya Rajmi". Taz: Musnad Imam Ahmad bin HanbalJuz. 5 uk. 132. Ewe msomaji mwenye akili hebu ziangalie hizi sura mbili zilizotajwa ndani ya Al-It-Qan na Ad-Durrul-Manthoor ambavyo ni vitabu vya Suyuti, pia zimethibitishwa na Tabran na Baihaqi na zinaitwa kuwa ni sura za Qunut wakati hazimo ndani ya kitabu cha Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Hii ina maana kwamba Qur'an tuliyonayo mikononi mwetu inapungua kwa sura mbili hizi zilizomo ndani ya Msa-hafu wa ibn Abbas na Msa-hafu wa Zaid bin Thabit kama ambavyo pia inajulisha kuwa kuna Misahafu mingine isiyokuwa hii tuliyonayo. Hali hii inanikumbusha ile tuhuma dhidi ya Shia kwamba wanao Msa-hafu wa Fatmah, basi yajuwe haya. Na (inajulisha) kwamba Masunni huzisoma sura hizi katika dua ya Qunut kila asubuhi, nami binafsi nilikuwa nimezihifadhi na kuzisoma katika Qunut ya sala ya alfajiri (nilipokuwa sunni). Ama riwaya ya pili ambayo ameithibitisha Imam Ahmad ndani ya Musnad yake, ni riwaya inayosema kuwa, Suratul-Ahzab imepungua robo tatu nzima, kwani Suratul-Baqarah ina aya 286 wakati ambapo Suratul-Ahzab haizidi aya 73 na tukizingatia hesabu ya Qur'an kwa hizbu, basi bila shaka Suratul-Baqarah ina hizbu tano wakati Suratul-Ahzab ina hizbu moja. Na kauli ya Ubayyi bin Kaa'b aliposema: "Nilikuwa nikiisoma pamoja na Mtume wa Mwenyezi Mungu kama ilivyo Suratul-Baqarah au zaidi" wakati ambapo ni miongoni mwa wasomaji mashuhuri waliokuwa wakihifadhi Qur'an katika zama za Mtume (s.a.w.) na huyo ndiye aliyechaguliwa na Umar[94] kuwasalisha watu sala ya Tarawehe, basi kauli yake hii inazusha mashaka na wasi wasi kama inavyoonekana wazi.

Na amethibitisha Imam Ahmad bin Hambal ndani ya Musnad yake[95] mapokezi toka kwa Ubayyi bin Kaab amesema: "Hakika Mjumbe wake alisema, Mwenyezi Mungu Mtukufu ameniamuru nikusomee Qur'an akasoma: "Lam Yakunil-ladhiina Kafaruu min ahlil-Kitabi", ndani yoke akasoma; "Walau anna ibn Adama Saala Wa-diyan min malin Faa A'taytuhu Lasaala Thaaniyan Falau Saala Thaniyan Faataytuhu Lasaala Thalithan, Wala-Yamlau Jaufa ibn Adama Illat-Turabu Wayatubullahu ala Man Taaba, Wainna dhalikad-Dinul-Qayyimu Indallahil-Hanafiyyah Gharyul-Mushrikah Walal-Yahudiyah Walan-Nasraniyyah Woman Yaf-alu Khayran Falan Yukfarah." Na amethibitisha Al-Hafidh ibn Asakir alipokuwa akitoa Tarjuma ya Ubayyi bin Kaab ya kwamba Abud-Dar-Dai alikwenda Madina akiwa pamoja na jamaa fulani miongoni mwa watu wa Dimishq, akamsomea Omar bin Khatab huko Madina aya hii: "Idh'jaalal-Ladhiina Kafaru Fi Qulubihim Al-Hamiyata Hamiyatal-Jaahiliya Walau Hamaitum kama hamau La Fasadal-Masjidul-Haram."

Umar bin Khatab akasema:"Nani alikusomesheni kisomo hiki"? Wakasema, "Ubayyi bin Kaab" akamwita, na akawaambia "Someni (mlivyosoma)" wakasoma:"Walau hamaltum kama hamau lafasadal-Masjidul-haraam " Ubayyi bin Kaab akamwambia Umar bin Khatab "Ndiyo, ni mimi niliyewasomesha (hivyo)" Umar akamwambia Zaid bin Thabit "Soma ewe Zaid" Zaid akasoma kama wasomavyo watu wote, basi Umar akasema, "Sifahamu kisomo kingine isipokuwa hiki"! Ubayyi bin Kaab akasema: "Ewe Umar namuapa Mwenyezi Mungu ya kwamba hakika wewe unafahamu kwamba mimi nilikuwa nikihudhuria (mbele ya Mtume) na wao hawahudhurii na nikikurubia (kwa Mtume) wao hujificha, na namuapa Mwenyezi Mungu lau utapenda (nisisome hivi nisomavyo) basi nitabakia nyumbani mwangu wala sitamsomea yeyote mpaka nife" Umar akasema, Samahani, bila shaka wewe unafahamu kwamba, Mwenyezi Mungu amekujaalia elimu, basi wasomeshe watu kile ukijuacho".

Amesema:(Kuna siku) Umar alipita kwa kijana fulani akiwa anasoma ndani ya msahafu kama ifuatavyo: "Annabiyyu aula Bil-Muuminina Mina anfusihim Wa'az-Wajuhu Ummahatuhum Wahuwa Abun-lahum". Umar akasema:"Ewe kijana (imekuwaje) hebu eleza", yule kijana akasema:"Huu ni msahafu wa Ubayyi bin Kaab" Basi Umar akaenda akamuuliza Ubayyi naye akamwambia: "Bila shaka mimi ilikuwa ikinishughulisha Qur'an nawe ulikuwa ukishughulishwa na biashara sokoni." Taz: Tarikh Dimishq ya Al-Hafidh ibn Asakir Juz. 2 uk. 228. Nao ibn Al-Athir ndani ya Jamiul-Usul na Abu Dawud ndani ya Sunan yake na Al-Hakim ndani ya Mustadrak yake wamesimulia mfano wa riwaya kama hii (iliyotangulia).

Mara hii nakuachia ewe ndugu msomaji ufafanue mwenyewe riwaya kama hizi zilizojaa ndani ya vitabu vya Kisunni, hali yakuwa wao hawana habari nazo (kwamba zimo vitabuni mwao) na wanawatuhumu Mashia ambao kwao haipatikani kiasi kama hiki. Lakini huenda baadhi ya watu wakorofi miongoni mwa Masunni wakazikwepa riwaya kama hizi na kuzikataa kama ilivyo kawaida yao. Si hivyo tu bali watampinga Imam Ahmad kwa kuandika uzushi kama huu na Sanad zake kuwa ni dhaifu. Isitoshe wataiona Musnad ya Imam Ahmad bin Hanbal na Sunan ya Abi Dawud kwao Masunni kwamba hazina kiwango cha usahihi kama ule wa Bukhar na Muslim, lakini (inawapasa wafahamu kwamba) riwaya kama hizi zinapatikana pia ndani ya sahih Bukhar na sahih Muslim.

Imam Bukhar amethibitisha ndani ya Sahih yake[96] katika mlango wa Manaqib Ammar na Hudhaifah (r.a.) kutoka kwa Il-Qimah amesema:

"Nilifika Sham nikasali rakaa mbili kisha nikasema,"Ewe Mwenyezi Mungu nisaidie mwenza mwema, basi nikaenda kwa jamaa fulani nikakaa kwao, mara alikuja mzee mmoja hivi akakaa pembeni yangu, nikasema ni nani huyu"? Wakasema:"Abud-dar-dai" Nikasema:"Hakika nilimuomba Mwenyezi Mungu anisaidie mwenza mwema, amenisaidia wewe". Akasema: "Ni nani wewe"? Nikasema, "Mimi ni miongoni mwa watu wa Kufah" Akasema:"Hivi huko kwenu hayuko mwana wa Ummi Abdi mwenye viatu viwili, mto na birika ya kujitaharishia? Na kwenu yuko mtu ambaye Mwenyezi Mungu amemlinda kutokana na shetani kwa mujibu wa kauli ya Nabii wake (s.a.w.), mtu ambaye hapana mwingine ila yeye, hayuko kwenu mwandani wa Nabii (s.a.w.) ambaye hakuna mwingine ajuaye isipokuwa yeye. Kisha akasema namna gani Abdallah aisomavyo;(Wallayli Idha-Yaghsha)." Basi nikamsomea "Wallayli Idha Yaghsha, Wannahari ldha-Tajalla-Wad-Dhakari Wal-Untha) Akasema:"Wallahi ndivyo alivyonisomea Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) kutoka kinywani mwake kuja kinywani mwangu".

Kisha ameongeza kwenye riwaya nyingine amesema, "Watu hawa hawakuniachia mpaka karibu waniondoshe kwenye jambo nililolisikia toka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.)". Taz: Sahih Bukhar Juz. 4 uk. 216. Na katika riwaya nyingine amesema: (Wallayli Idha Yaghsha Wannahari,Idha-Tajalla Wad-Dhakari Wal-Untha) Akasema: "Amenisomea Mtume toka kinywani mwake kuja kinywani mwangu basi watu hawa hawakuniacha mpaka karibu wanirudishe." Taz: Sahih BukharJuz. 4 uk. 218 (Babu Manaqib Abdillah, ibn Mas-ud).

Basi riwaya zote hizi zinafidisha kwamba Qur'an tuliyonayo imezidishwa neno lisemalo, "Wamakhalaqa". Na amethibitisha Bukhar ndani ya sahih yake kwa isnadi yake kutoka kwa ibn Abbas ya kwamba Umar ibn Al-Khtab amesema:"Bila shaka Mwenyezi Mungu amemtuma Muhammad (s.a.w.) kwa ukweli na akamteremshia kitabu, miongoni mwa aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu ni aya ya Rajmi, tuliiisoma na tukaifahamu na kuizingatia, na kwa ajili hiyo Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) alirujumu (kupiga mawe wazinifu) nasi baada yake tulirujumu, mimi nachelea iwapo zitapita siku nyingi kwa watu atakujasema msemaji, Wallahi hatuioni Ayatur-Rajmi ndani ya kitabu cha Mwenyezi Mungu,watapotea kwa kuiacha faradhi aliyoiteremsha Mwenyezi Mungu, na kurujumiwa kulikomo ndani ya kitabu cha Mwenyezi Mungu ni stahiki ya aliyezini iwapo amehifadhika miongoni mwa wanaume na wanawake pindi ushahidi ukithibitishwa au ikapatikana mimba na akakiri (kuzini). Kisha tulikuwa tukisoma miongoni mwa yale tuyasomayo ndani ya Kitabu cha Mwenyezi Mungu kwamba:"Msiwachukie wazee wenu kwani kuwachukia wazee wenu ni kufru kwenu, au hakika kufru kwenu ni kuwachukia wazee wenu".

Taz: Sahih Bukhar Juz. 8 uk. 26 Babu Rajmil-Hubla Minaz-Zina Idhaa uh-Sinat. Naye Imam Muslim amethibitisha ndani ya Sahih yake mlango wa Lau anna libni Adama Wadiyan Labtagha Thalithan Juz. 3 uk 100, Amesema:"Abu Musa Al-ash-ari alituma ujumbe kwa wasomaji wa Qur'an wa huko Basra wakaingia kwake watu mia tatu ambao wamekwisha soma Qur'an, akasema: Ninyi ndiyo watu wema huko Basra na ni wasomaji wao, basi isomeni (mara kwa mara) isije kukupitieni muda mrefu mioyo yenu itakuwa migumu kama ilivyokuwa migumu mioyo ya waliokuwa kabla yenu, nasi tulikuwa tukisoma sura tukiifananisha kwa urefu na ugumu na sura (isemayo):"Laukana Libni Adama Wadiyaani Min Malin Labtagha Wadiyan Thalithan Wala Yamlau Jaufa bni Adama Illat-Turaab". Tulikuwa tukisoma sura tunayoifananisha na moja ya Musabbihat nimesahaulishwa isipokuwa nimehifadhi sehemu yake (isemayo): "Ya Ayyuahal-Ladhiina A'manu Lima Taquluna Mala Taf-Aluna Fatuktabu Shahadatu Fii Aa'naqikum Fatus-Aluna An-haa yaumal-Qiyamah ". Taz: Sahih Muslim Juz. 3 uk. 100.

Na hizi sura mbili zinazodaiwa ambazo Abu Musa Al-ash-ari amezisahau, moja wapo inafanana na Suratu Baraa yaani aya 129 na ya pili inafanana na mojawapo ya Musabbihat yaani aya ishirini, sura hizi hazipo isipokuwa zimo ndani ya mawazo ya Abu Musa, basi soma na ustaajabu nami nakuachia uamuzi ewe mchunguzi muadiliru. Sasa basi ikiwa vitabu vya Masunni, Musnad zao na Sihahi zao zimejazwa riwaya kama hizi ambazo zinadai kuwa Qur'an imepungua na wakati mwingine imezidi, basi kebehi hizi ni za nini dhidi ya Mashia ambao wameungana kubatilisha upotovu wa madai haya kwa kauli moja? Na kama yule Shia mwenye kitabu kiitwacho; "Fas-Lulkhitab Fi Ith-Bati Tahrif Kitabi Rabbil-Ar-Bab", aliyefariki mwaka 1320 A.H. aliandika kitabu chake karibu miaka mia iliyopita, yeye alitanguliwa na Msunni kutoka Misri yule mwenye kitabu kiitwacho "Al-Fur-Qan" kwa karibu karne nne kama alivyoonesha jambo hilo Shekh Muhammad Al-Madani mkuu wa kitivo cha sheria katika Azhar.

Jambo la muhimu katika yote haya ni kwamba wanachuoni wa Kisunni na wanachuoni wa Kishia miongoni mwa wahakiki wamezibatilisha riwaya kama hizi na wakazizingatia kuwa potovu na wamethibitisha kwa dalili zinazotosheleza kwamba Qur'an iliyoteremshwa kwa Mtume wetu Muhammad (s.a.w.) hakuna ziyada ndani yake wala upungufu wala mabadiliko wala mageuzi. Je, ni vipi Masunni wanawakebehi Mashia kwa sababu tu ya riwaya zisizokubalika kwa Mashia na wao Masunni wajitakase wakati ambapo sihahi zao zinathibitisha juu ya usahihi wa riwaya hizo?

Nami huzikumbuka riwaya hizi kwa uchungu mkubwa na huzuni nyingi, kwani hakutusaidii kitu leo hii kuzinyamazia na kuzitupa ndani ya kapu la takataka, lau siyo shinikizo la hujuma iliyoenezwa na baadhi ya watunzi na waandishi miongoni mwa wale wanaodai kuwa wameshikamana na sunna ya Mtume na hali ya kuwa nyuma yao kuna msukumo unaowatikisa na kuwatia nguvu wawatukane Mashia na kuwakufurisha na hasa baada ya ushindi wa mapinduzi ya Kiislamu ya Iran. Basi watu kama hawa nawaambia: "Muogopeni Mwenyezi Mungu kuhusu ndugu zenu, na mshikamane na dini ya Mwenyezi Mungu nyote wala msifarakane, na ikumbukeni neema ya Mwenyezi Mungu iliyoko juu yenu, pindi mlipokuwa maadui (Mwenyezi Mungu) akaziunganisha nyoyo zenu mkawa kwa neema yake (nyote) ni ndugu.