ILI NIWE PAMOJA NA WAKWELI

ILI NIWE PAMOJA NA WAKWELI 20%

ILI NIWE PAMOJA NA WAKWELI Mwandishi:
Kundi: Midahalo na majadiliano kielimu

ILI NIWE PAMOJA NA WAKWELI
  • Anza
  • Iliyopita
  • 21 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 37839 / Pakua: 4635
Kiwango Kiwango Kiwango
ILI NIWE PAMOJA NA WAKWELI

ILI NIWE PAMOJA NA WAKWELI

Mwandishi:
Swahili

4

ILI NIWE PAMOJA NA

UFAFANUZI

Pamoja na kwamba Imam Muslim amelifupisha tukio hili na hakulisimulia kikamilifu, lakini Al-Hamdulillah inatosheleza na labda ufupisho huu ulitoka kwa Zaid bin Ar-Qam mwenyewe pale hali halisi ya kisiasa ilipomlazimisha kuificha hadithi ya Ghadir na hili tunalifahamu kutokana na mfumo wa hadithi ulivyokuja kwani msimuliaji anasema:

"Mimi, Husain bin Sabrah o na Umar bin Muslim tulikwenda kwa Zaid bin Ar-Qam, tulipokaa Husain akamwambia Zaid, Bila shaka ewe Zaid umepata kheri nyingi, umemuona Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) umesikia hadithi zake na umepigana vita pamoja naye na umesali nyuma yake, kwa hakika umepata kheri nyingi mno, hebu tusimulie ewe Zaidi yale uliyoyasikia kwa Mtume (s.a.w.)". Zaid akasema, "Ewe mtoto wa ndugu yangu nimekwisha kuwa mzee sasa na umekuwa mrefu muda wangu, nimesahau baadhi ya mambo ambayo nilikuwa nikiyahifadhi toka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) basi yale nitakayokusimulieni yakubalini na yale nisiyokusimulieni msinilazimishe, kisha akasema: Mtume wa Mwenyezi Mungu siku moja alisimama kwenye maji yaitwayo Khum akahutubia..."

Kutokana na mtiririko wa hadithi inadhihiri kwamba, Husain alimuuliza Zaid bin Ar-Qam tukio la Ghadir naye Zayd akalitoa jibu la suali hili mbele ya wote waliohudhuria, hivyo basi hapana shaka Zaid alikuwa akitambua kwamba kutoa jawabu la wazi wazi juu ya suali hilo ingemsababishia matatizo mbele ya serikali ambayo ilikuwa ikiwalazimisha watu kumlaani Ali bin Abi Talib, na kwa ajili hii tunamkuta anajitetea kwa muulizaji ya kuwa sasa amekuwa mtu mzima na muda mrefu umempitia na ameyasahau baadhi ya mambo aliyokuwa akiyahifadhi, kisha anaongeza kwa kuwataka waliohudhuria wakubali yale anayowasimulia na wala wasimlazimishe kuyasimulia yale anayotaka kuyanyamazia.

Pamoja na woga wake na kulifupisha kwake tukio hili bila shaka Zaidi bin Ar-Qam (Mwenyezi Mungu amlipe Kheri) ameubainisha ukweli mwingi na akaichenga hadithi ya Ghadir hakuitaja ile kauli yake isemayo "Mtume (s.a.w.) alisimama akatuhutubia kwenye bonde la Khum liliko kati ya Maka na Madina," kisha baada ya hapo akataja ubora wa Ali (a.s.) na kwamba yeye ni mshirika wa Qur'ani katika hadithi ya vizito viwili, kitabu cha Mwenyezi Mungu na watu wa nyumba yangu", na hakulitaja jina la Ali (a.s.) akawaachia waliohudhuria hapo hapo watumie akili zao kwani Waislamu wote wanafahamu kwamba Ali(a.s.) ndiyo kiongozi wa watu wa nyumba ya Mtume.

Na ndiyo maana tunamuona hata Imam Muslim mwenyewe alifahamu kutokana na hadithi hiyo kile ambacho sisi tumekifahamu, kwani ameiandika hadithi hii katika mlango wa Fadhail za Ali bin Abi Talib(a.s.) ingawaje hadithi haikutaja jina la Ali bin Abi Talib!! Taz: Sahih Muslim Juz. 7 uk. 122 Babu Fadhail Ali. 5) At-Tabrani amethibitisha ndani ya Muujamul-Kabir kwa sanad iliyo sahihi toka kwa Zaid bin Ar-Qam na Hudhaifah bin Usayd Al-Ghifari amesema: "Mtume wa Mwenyezi Mungu alihutubia huko Ghadir Khum chini ya miti akasema:

"Enyi watu yakaribia nitaitwa na nitaitika, nami nitaulizwa nanyi mtaulizwa, ni nini mtakachokisema?" Wakasema, "Tunashuhudia ya kwamba wewe umefikisha na umepigania (dini) na umetoa nasaha Mwenyezi Mungu akulipe mema". Mtume akasema, "Je, hivi hamushuhudii ya kwamba hapana Mola wa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu na kwamba Muhammad ni Mtume wake, na kwamba pepo yake ni kitu cha kweli na moto wake ni kitu cha kweli, na kuwa mauti ni kitu cha kweli na kwamba kufufuliwa baada ya kufa ni kitu cha kweli. Na kwamba kiyama kitakuja bila ya shaka yoyote na kwamba Mwenyezi Mungu atawafufua waliomo makaburini?

Wakasema, tunashuhudia yote hayo," Mtume akasema: "Ewe Mwenyezi Mungu shuhudia" kisha akasema, "Enyi watu hakika Mwenyezi Mungu ni mtawalia mambo yangu na ni mtawalia mambo ya waumini nami ni bora mno kuliko nafsi zao, basi yeyote ambaye mimi ni mtawalia mambo yake huyu hapa ni mtawala wake (yaani Ali.) ewe Mwenyezi Mungu msaidiye atakayemsaidia na umfanye adui atakayemfanya adui kisha akasema, "Enyi watu hakika mimi nakutangulieni nanyi mutanifikia kwenye haudh, haudh ambalo upana wake ni kati ya Basra na San-aa, kwa hakika nitakuulizeni mtaponifikia kuhusu vizito viwili ni vipi mtanifuata katika vizito hivyo, kizito kikubwa ni kitabu cha Mwenyezi Mungu Mtukufu sehemu ya ncha yake iko mikononi mwa Mwenyezi Mungu na nyingine iko mikononi mwenu, shikamaneni nayo msipotee wala msibadilishe, na (kizito cha pili) ni kizazi changu watu wa nyumba yangu, hapana shaka Mwenyezi Mungu mjuzi amenijulisha mimi ya kwamba viwili hivi havitatengana mpaka vinifikie kwenye Haudh."

Taz: Ibn Hajar ndani ya Sawaiq uk. 25 amenakili kwa Tabrani, Al-Hakim na Tir-midhi. 6) Kama ambavyo amethibitisha Imam Ahmad kwa njia ya Al-Barraa bin Azib kwa njia mbili amesema: "Tulikuwa pamoja na Mtume wa Mwenyezi Mungu tukafika Ghadir-Khum, ikanadiwa sala ya jamaa Mtume akaandaliwa mahali chini ya miti miwili akaswali sala ya adhuhuri na akaushika mkono wa Ali kisha akasema: "Je, hamjui kwamba mimi ni bora mno kwa waumini kuliko nafsi zao" Wakasema kwa nini (twalijua hilo), akaushika mkono wa Ali(a.s.) kisha akasema, yeyote ambaye mimi ni mtawala wa mambo yake basi Ali ni mtawala wa mambo yake, Ewe Mwenyezi Mungu msaidie atakaye msaidia na mfanye adui atakayemfanyia uadui." Baada ya tukio hilo Umar akamkuta Ali akamwambia, "Hongera Ewe mwana wa Abu Talib umekuwa mtawalia mambo ya kila muumini mwanaume na mwanamke". Taz: Musnad Ahmad bin Hanbal Juz. 4 uk. 281 Kanzul-Ummal Juz. 15uk. 117. Fadhailul-Khamsah Minas-Sihahis-Sittah. Juz. 1 uk. 350.

Na kwa kifupi hadithi ya Ghadir (wameisimulia) wanachuoni wengi wa Kisunni zaidi kuliko tuliowataja, k.m Tirmidhi, Ibn Asakir, Abunuaim, Ibnul-Athir, Al-Khawar-Zami na Suyuti. Wengine ni Ibn Al-Haithami, Ibnus-Sabbagh Al-Maliki, Al-Al-Hanafi, Ibnul-Maghazili, Al-Humuwaini, Al-Haskani, Al-Ghazali na Bukhari ndani ya tarikh yake. Al-Allamah Al-Amin mwenye kitabu cha Al-Ghadir amewataja wanachuoni wa Kisunni walioisimulia hadithi hii ya Ghadir na wakaithibitisha ndani ya vitabu vyao, pamoja na tofauti zao za kimadhehebu tangu karne ya kwanza Hijiriyyah mpaka karne ya kumi na nne. Idadi yao ilikuwa inazidi wanachuoni mia tatu na sitini, na yeyote mwenye kutaka ushahidi basi ni juu yake kukirejea kitabu cha Al-Ghadir.[35]

Basi Je baada ya yote haya inawezekana akasema mwenye kusema kwamba hadithi ya Ghadir ni miongoni mwa uzushi wa Kishia?

Kinachoshangaza ni kuwa, wengi wa Waislamu wakati unapowatajia hadithi ya Ghadir hawaifahamu au unaweza kusema kuwa hawajaisikia.La kushangaza zaidi kuliko hili ni kwamba, ni vipi basi wanachuoni wa Kisunni baada ya kuwepo kwa hadithi hii ambayo imekubaliwa usahihi wake wanadai kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu hakuacha Khalifa (aliyembainisha) bali aliacha jambo hili liwe la mashauriano miongoni mwa Waislamu?

Basi je, kuna hadithi iliyotoa maana ya wazi kuhusu Ukhalifa na ikabainisha kuliko hii enyi waja wa Mungu? Kwa hakika mimi nayakumbuka majadiliano yangu na mmoja wa wanachuoni kutoka Az-Zaitunah nchini kwetu pale nilipomtajia hadithi ya Ghadir nikiitolea ushahidi juu ya Ukhalifa wa Ali (a.s.), basi alikiri kuwa hadithi hiyo ni sahihi bali aliiongezea nguvu akanionyesha tafsiri ya Qur'an aliyoiandika yeye mwenyewe, tafsiri ambayo ndani yake ameitaja hadithi ya Ghadir na kuwa ni sahihi na baada ya hapo akasema ndani ya tafsiri yake:

"Mashia wanadai kwamba hadithi hii ni tamko linalohusu Ukhalifa wa Ali Karrama Llahu Waj-hahu na madai hayo ni batili kwa Masunni kwani yanapingana na ukhalifa wa bwana wetu Abubakar As-Siddiq na bwana wetu Umar Al-Faruq na bwana wetu Uthman Dhin-Nurain, basi hapana budi kulipa tafsiri nyingine tamko la Al-Maula (mtawalia mambo) lililokuja ndani ya hadithi hii liwe na maana ya mpenzi na msaidizi kama ilivyokuja ndani ya Qur'an na hivi ndivyo walivyolifahamu Makhalifa waongozi na Masahaba watukufu Mwenyezi Mungu awawie radhi wote, na hivi ndivyo walivyochukua toka kwao waliofuatia na wanachuoni wa Kiislamu. Basi hapana mazingatio yoyote kwa tafsiri ya Marafidhi (Mashia) kuhusu hadithi hii kwani wao hawakubali ukhalifa wa makhalifa (Abubakar, Umar, Uthman) na wanawatukana Masahaba wa Mtume na hili peke yake linatosha kuupinga uzushi wao na kuyabatilisha madai yao" Mwisho wa maneno yake yaliyomo ndani ya kitabu chake.

Basi mimi nilimuuliza: "Je, tukio hili lilitokea huko Ghadir Khum?"

Akajibu "Lau lingekuwa halikutokea wanachuoni na wataalam wa hadithi wasingelisimulia"!! Nikasema:

"Hivi kweli inakubalika kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) kuwakusanya Masahaba wake katika jua kali linalounguza na kuwahutubia hotuba ndefu ili tu awaambie kuwa Ali ni mpenzi wenu na mtetezi wenu? Hivi kweli munaridhia tafsiri hii?" Akajibu:

"Bila shaka wako baadhi ya Masahaba walio mlalamikia Ali na walikuwepo wenye kumchukia na kumbughudhi hivyo basi Mtume (s.a.w.) alitaka aizidishe chuki yao ndipo alipowaambia kwamba Ali ni mpenzi wenu na ni mtetezi wenu ili tu wampende na wasimkere." Mimi nikasema:

"Basi kama jambo lenyewe ni hilo, halihitaji kuwasimamisha wote na kuwasalisha kishaa kuanza kuwahutubia kwa kuwaambia: "Je, mimi siye bora kwenu kuliko nafsi zenu." Ili Mtume aifafanue maana ya Maula, na kama mambo yatakuwa kama unavyosema basi ilikuwa inawezekana kwake Mtume kuwaambia wale waliomlalamikia Ali (kumshitakia kwa Mtume) kwamba: "Ali ni kipenzi chenu na ni mtetezi wenu" na mambo yakaisha bila ya yeye Mtume kulizuwia katika jua kali kundi hilo kubwa ambalo lilikuwa na watu zaidi ya laki moja wakiwemo wazee na wanawake. Mtu mwenye akili hawezi kabisa kukubaliana na hivyo (usemavyo).

Akasema: "Je, mtu mwenye akili ataamini kwamba Masahaba laki moja hawakuifahamu maana uliyoifahamu wewe na Mashia?" Nikasema: "Kwanza wengi wao walikuwa hawakai Madina, pili hakika wao moja kwa moja walifahamu kama nilivyofahamu mimi na Mashia na ndiyo maana wanachuoni wamesimulia kwamba, Abubakr na Umar walikuwa miogoni mwa waliompongeza Ali waliposema: "Hongera Ewe mwana wa Abu Talib umekuwa mtawalia mambo ya kila muumini". Akasema: "Basi ni kwa nini hawakumpa baia baada ya Mtume kufariki? Unawaona kwamba wao waliasi na kwenda kinyume cha amri ya Mtume (Astaghfirullah) Mwenyezi Mungu anisamehe kutokana na kauli hii". Mimi nikasema:"Ikiwa wanachuoni wa Kisunni wanashuhudia ndani ya vitabu vyao kwamba baadhi yao yaani Masahaba walikuwa wakienda kinyume cha maamrisho ya Mtume zama za uhai wake tena mbele yake[36] basi siyo ajabu kuyaacha maamrisho yake baada ya kufariki kwake, na ikiwa wengi wao walimtuhumu Mtume kwa kumpa uamirijeshi Usamah bin Zaid kutokana na umri wake kuwa mdogo pamoja na kuwa jeshi hilo la Usama lilikuwa ni kwa muda mfupi basi ni vipi wao watakubali Ali awe amiri juu yao tena mwenye umri mdogo kisha kwa muda wa uhai wao (au wake) na Ukhalifa wake ni kwa kila kitu, nawe umeshuhudia mwenyewe kwamba baadhi yao walikuwa wakimchukia Ali na kumkera?

Alinijibu huku akiwa amekasirika: "Lau kama Imam Ali Karrama Llahu Waj-hahu angekuwa anafahamu kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu amemtawalisha Ukhalifa, basi asingenyamazia haki yake naye alikuwa mtu shujaa isitoshe Masahaba wote walikuwa wakimuogopa" Mimi nikasema: "Bwana wangu hii ni maudhui nyingine nami sitaki kuiingia kwani wewe hukutosheka na hadithi za Mtume zilizosahihi na unajaribu kuziawili na kuzibadilisha maana yake ili tu ulinde utukufu wa viongozi waliopita, basi mimi nitakukinaisha- namna gani suala la kunyamazia kwa Imam Ali au kutoa hoja kwake dhidi yao kuhusu haki yake ya Ukhalifa?

Yule bwana alitabasamu huku akisema: "Wallahi mimi ni miongoni mwa watu wanaomtukuza Bwana wetu Ali Karrama llahu Waj-hahu juu zaidi kuliko wengine, na lau ningekuwa na uwezo nisingemtanguliza juu yake Sahaba yeyote, kwani yeye (Ali) ndiye mlango wa mji wa elimu na ndiye simba wa Mwenyezi Mungu aliyemshindi, lakini matakwa ya Mwenyezi Mungu yanamtanguliza amtakaye na kumbakisha nyuma amtakaye, haulizwi (Mwenyezi Mungu) kile akifanyacho nao viumbe wataulizwa".

Nami nilitabasamu na nikasema: "Na hii pia ni maudhui nyengine inatutaka tuzungumzie Qadhaa na Qadar na hapo kabla tumetangulia kuizungumzia na kila mmoja wetu akawa amebakia kwenye mtazamo wake, kwa hakika ninashangaa ewe bwana wangu ni kwa nini kila ninapozungumza na mwanachuoni wa Kisunni na ninapomshinikiza kwa hoja haraka sana huikimbia maudhui tuliyonayo na kushika maudhui nyingine ambayo haina uhusiano na utafiti tunao ulenga".

Akasema: "Nami nabakia kwenye mtazamo wangu siwezi kuubadilisha." Basi nilimuaga nikaondoka, na nikabaki ninafikiri saa zote, ni kwa nini simpati mwanachuoni miongoni mwa wanachuoni wetu atakayekamilisha pamoja nami mazungumzo haya na ausimamishe mlango mguuni kwake kama isemavyo methali mashuhuri huku kwetu. Baadhi yao huanza mazungumzo na pale anapojikuta hawezi kusimamisha hoja juu ya maneno yake huepa kwa kusema, "Hao ni umati uliokwisha pita, wanayo yao waliyoyachuma nanyi munayo yenu mliyoyachuma", na baadhi yao husema: "Tunahaja gani ya kuzusha fitna na chuki, la muhimu ni kuwa Masunni na Mashia wanaamini Mungu mmoja na Mtume mmoja basi hii inatosha" Na wengine husema kwa kifupi tu, "Ewe ndugu yangu muogope Mwenyezi Mungu juu ya Masahaba". Basi je, kuna nafasi yoyote inayobakia kwa watu hawa kutafiti, kuchunguza kielimu, kuing'arisha njia na kurejea kwenye haki ambayo hapana baada yake isipokuwa upotofu? vipi) mbinu za Qur'an ambazo zinawataka watu kusimamisha dalili "Waambie leteni hoja zenu ikiwa ninyi mnasema kweli." Pamoja na kufahamu kwamba lau wao wataacha kuwashutumu na kuwahujumu Mashia basi tusingelazimika kujadiliana nao hata kwa yale yaliyo mema.

AYA YA KUKAMILISHA DINI

AYA YA KUKAMILISHA DINI PIA INAHUSIANA NA SUALA LA UKHALIFA

Kauli ya Mwenyezi Mungu isemayo: "Leo nimekukamilishieni dini yenu na nimekutimizieni Neema yangu na nimeuridhia kwenu Uislamu kuwa ndiyo dini" (Qur'an, 5:3) Mashia wanakubaliana kuwa ilishuka hapo Ghadir Khum baada ya Mtume (s.a.w.) kumsimika Imam Ali kuwa ni Khalifa wa Waislamu, na hiyo ni riwaya iliyopokelewa toka kwa Maimamu wa kizazi kitakatifu, na ndiyo maana utawaona (Mashia) wanauhesabu Uimamu kuwa ni miongoni mwa "Misingi ya Dini" (Usulud-Din). Pamoja na kwamba wengi wa wanachuoni wetu wa Kisunni wanaisimulia aya hii kuwa ilishuka hapo Ghadir Khum baada ya kusimikwa Imam Ali nami ninataja miongoni mwao kama mfano:

1). Tarikh Dimishq ya ibn Asakir Juz. 2 uk. 75.

2). Manaqib Ali bin Abi Talib cha Ibn Maghazili As-Shafiiuk.19.

3). Tarikh Baghaad cha Al-Khatib Al-Baghdadi Juz.8 uk. 290.

4). Al-It-Qan cha SuyutiJuz. 1 uk. 31.

5). Tadhikiratul-Khawas cha ibn Al-Jauzi uk. 30.

6). Al-Manaqib cha Al-Khawar-Zami Al-Hanafi uk. 80.

7). Tafsir ibn KathirJuz. 2 uk. 14.

8). Ruhul-Maani ya Al-Alusi Juz. 6uk. 55.

9). Al-Bidayatu Wan-Nihayah ya Ibn Kathir Juz.5 uk. 213.

10). Ad-Durrul-Manthur ya Suyuti Juz. 3 uk. 213.

11). Yanabiul-Mawaddah cha Al-Qanduzi Al-Hanafi uk. 115.

12). Shawahidut-Tanzil cha Al-Haskani Juz. 1 uk. 157.

Mimi nasema, pamoja na yote hayo wanachuoni wa Kisunni wamelazimika kuibadilisha aya hii na kuiweka kwenye munasaba mwingine, na kufanya hivyo ni kwa ajili ya kulinda heshima ya viongozi waliopita miongoni mwa Masahaba, vinginevyo kama wangekubali kwamba aya hiyo imeshuka hapo Ghadir Khum na wangekiri kwamba kutawazwa kwa Imam Ali ndiyo jambo ambalo kwalo Mwenyezi Mungu aliikamilisha dini na akawatimizia Waislamu kwa jambo hilo neema yake, na pia ungelitoweka Ukhalifa wa Makhalifa watatu ambao walimtangulia Imam Ali na ungeporomoka uadilifu wa Masahaba na hadithi nyingi zingeyeyuka kama chumvi inavyoyeyuka ndani ya maji. Lakini jambo hili haliwezekani na ni jambo zito kwani lahusika na itikadi ya umma mkubwa wenye historia yake na wanachuoni wake na watukufu wake, hivyo basi imeshindikana kwetu sisi kumpinga Bukhari na Muslim ambao wanasimulia ya kwamba aya hiyo ilishuka Ijumaa jioni ya siku ya Arafa.

Na kwa riwaya hizo za kina Bukhari zile riwaya za mwanzo zinaonekana kuwa ni uzushi wa Kishia na hazina msingi wowote wa usahihi, na kuwashutumu Mashia inakuwa ni bora mno kuliko kuwashutumu Masahaba, kwani Masahaba hawa wamehifadhika kutokana na makosa[37] na wala hapana uwezekano wa mtu yeyote kuyakosoa matendo yao na maneno yao. Amma hao Mashia wao ni majusi, makafiri, wazandiki, na ni walahidi na muasisi wa madhehebu yao ni Abdallah bin Saba[38] ambaye ni Myahudi aliyesilimu zama za Uthmani bin Affan ili kuwavuruga Waislamu na Uislamu. Kufanya hivyo ni jambo jepesi mno ili kuupotosha umma ambao umeleleka juu ya msingi wa kuwatukuza na kuwaheshimu Masahaba (yaani Sahaba yeyote yule japokuwa alimuona Mtume mara moja) basi itawezekana vipi kwetu sisi kuwakinaisha watu kwamba riwaya hizo siyo uzushi wa Kishia bali ni hadithi za Maimamu kumi na wawili ambao Mtume wa Mwenyezi Mungu alitamka kuhusu Uimamu wao, Maimamu ambao serikali za Kiislamu katika karne ya kwanza zilifanikiwa kupandikiza mapenzi na kuwaheshimu Masahaba dhidi ya Ali na wanawe juu ya Mimbar na kuwafuatilia Mashia wao kwa kuwauwa na kuwafukuza, na hapo ndipo ilipoanzia chuki na karaha dhidi ya kila Shia kutokana na mambo yaliyosambazwa na vyombo vya habari katika zama za Muawiyah ikiwa ni pamoja na itikadi mbaya dhidi ya Shia, na leo hii Mashia wanaitwa kuwa ni kundi la upinzani ili tu kuwatenga na kuwamaliza.

Na kwa ajili hiyo tunawakuta hata waandishi na wanahistoria katika zama hizo wakiwaita Mashia kuwa ni Ar-Rawafidhi" (yaani wapinzani) na huwakufurisha na kuwauwa ili tu kujipendekeza kwa watawala. Ulipoanguka utawala wa Banu Umayyah na ukafuatiwa na dola ya Banu Abbas baadhi ya wanahistoria walibadili muelekeo wao, baadhi yao wakaitambua haki ya watu wa nyumba ya Mtume hiyo ni kwa sababu ya Maimamu wa nyumba ya Mtume nafsi zao zilishikamana na Akhlaq yao njema na elimu zao ambazo zilijaa ulimwenguni, na uchamungu wao na utukufu aliowapa Mwenyezi Mungu.

Kutokana na mazingira haya wanahistoria hao wakajaribu kufanya uadilifu na ndipo walipomuunganisha Ali kwenye Makhalifa waliomtangulia, lakini pamoja na hayo hawakuthubutu kuiweka wazi haki yake, na ndiyo maana utawaona hawakuandika ndani ya vitabu vyao isipokuwa sehemu ndogo tu ya ubora wa Ali na tena wanatoa zile sifa ambazo hazipingani na Ukhalifa wa waliomtangulia. Baadhi yao wameweka hadithi nyingi zinazohusu ubora wa Abubakar, Umar na Uthman kwa kupitia ulimi wa Ali mwenyewe ili wapate kukata njia ya Mashia wanaosema kuwa Ali ni bora zaidi.

Kwa kupitia uchunguzi wangu nimegundua kwamba umashuhuri wa watu na utukufu wao ulikuwa ukipimwa kwa kiwango cha kumchukia Ali bin Abi Talib, kwani Banu Umayya na Banu Abbas walikuwa wakimkurubisha na kumtukuza kila yule ambaye alikuwa akimpiga vita Imam Ali au akisimama dhidi yake kwa upanga au ulimi, ndiyo maana utawaona wanawatukuza baadhi ya Masahaba na kuwatweza wengine. Si hivyo tu bali (Banu Umayya na Banu Abbas) wakiwasheheneza kwa mali nyingi baadhi ya washairi na kuwauwa wengine, na huenda mama Aisha Ummul-Muuminina asingekuwa na hadhi kwa kiwango hicho kwa Masunni lau siyo kumchukia[39] kwake Ali na kumpiga vita.

wanaonekana wamefikia kiwango cha upuuzi na ujinga wa akili na maoni potofu kwa vile wanaitakidi juu ya Uimamu wa Mahdi anayengojewa ambaye ataujaza ulimwengu uadilifu na usawa kama ambavyo umejazwa dhulma na ujeuri. Na sasa tunarudi kuzijadili kauli za pande mbili kwa Sasa hebu turudi na tuzijadili kauli za pande mbili kwa utulivu bila ya chuki ili tufahamu ni munasaba upi na ni sababu ipi ya kushuka kwa aya ya kukamilisha dini ili itupambanukie haki na tuifuate. Hapo sasa hatuwajibiki kukubaliana na ridhaa ya hawa au chuki ya wale maadam kabla ya chochote tunaikusudia radhi ya Mwenyezi Mungu Mtukufu na kujiokoa kutokana na adhabu yake siku ambayo haitamfaa mtu mali yake wala watoto ila yule atakayemjia Mwenyezi Mungu na moyo uliosalimika. Siku ambayo nyuso zitang'ara na nyuso zingine zitakuwa nyeusi, ama wale ambao nyuso zao zitakuwa nyeusi, je, mlikufuru baada ya kuamini? Basi ionjeni adhabu kwa yale muliyokuwa mukikufuru. Na ama wale ambao nyuso zao zitang'ara basi hao watakuwa katika Rehma za Mwenyezi Mungu wao wataingia humo. (Qur'an, 3:106)

3

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA SABA

﴿جَعَلَ اللَّـهُ الْكَعْبَةَ الْبَيْتَ الْحَرَامَ قِيَامًا لِّلنَّاسِ وَالشَّهْرَ الْحَرَامَ وَالْهَدْيَ وَالْقَلَائِدَ ذَٰلِكَ لِتَعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ يَعْلَمُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ وَأَنَّ اللَّـهَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ﴾

97.Mwenyezi Mungu amefanya Al-Kaaba nyumba tukufu, kuwa ni kisimamo cha watu na miezi mitukufu na wanyama wa kuchinja na vigwe; hayo ni kwa sababu mjue kuwa Mwenyezi Mungu anayajua yaliyomo mbinguni na yaliyomo ardhini na kwamba Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.

﴿اعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ شَدِيدُ الْعِقَابِ وَأَنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ﴾

98. Jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni mkali wa kuadhibu na kwamba Mwenyezi Mungu ni mwingi wa maghufira, Mwingi wa kurehemu.

﴿مَّا عَلَى الرَّسُولِ إِلَّا الْبَلَاغُ وَاللَّـهُ يَعْلَمُ مَا تُبْدُونَ وَمَا تَكْتُمُونَ﴾

99.Haimlazimu Mtume ila kufikisha tu, na Mwenyezi Mungu anajua mnayo yadhihirisha na mnayoyaficha.

NYUMBA TAKATIFU

Aya 97-99

MAANA

Mwenyezi Mungu ameifanya Al-Kaaba, nyumba takatifu, kuwa ni kisimamo cha watu na miezi mitakatifu na wanyama wa kuchinja na vigwe.

Kisimamo cha watu; yaani mahali pa ibada na ibada za Hijja. Miezi mitakatifu ni ile minne Rajab, Dhul-qa'da, Dhul-Hijja na Muharram[5] Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameharamisha kupigana huko na katika miezi hiyo; ispokuwa kutetea nafsi au mali. Anasema:

﴿وَلَا تُقَاتِلُوهُمْ عِندَ الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ حَتَّىٰ يُقَاتِلُوكُمْ فِيهِ﴾

"Wala msipigane nao karibu na Msikiti Mtakatifu mpaka wakupigeni huko" (2:191) Na akasema tena:

﴿الشَّهْرُ الْحَرَامُ بِالشَّهْرِ الْحَرَامِ وَالْحُرُمَاتُ قِصَاصٌ فَمَنِ اعْتَدَىٰ عَلَيْكُمْ فَاعْتَدُوا عَلَيْهِ بِمِثْلِ مَا اعْتَدَىٰ عَلَيْكُمْ ﴾

"Mwezi mtakatifu kwa mwezi mtakatifu; na vitu vitakatifu vina kisasi. Basi wanaowachokoza, pia nanyi wachokozeni kwa kadiri walivyowachokoza" (2:194)

Mnyama wa kuchinja, ni wale wanaochinjwa Makka. Na kigwe ni ukambaa anaofungwa nao mnyama wa kuchinja kuwa ni alama ya kufahamisha kuwa ni wa Al-Kaaba ili asitaradhiwe na yeyote. Kwa hiyo kuunganisha vigwe kwa wanyama ni kuunganisha maalum katika ujumla.

Makusudio ya kutaja chinjo pamoja na Nyumba takatifu na miezi mitakatifu ni kwamba mnyama wa kuchinja inapasa awe salama yeye na anayemchunga, kwa sababu yeye anakusudia Haram tukufu.

Bali ni kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewapa amani ndege na wanyama walio katika haramu yake; isipokuwa mwewe, kipanga, kunguru, panya, nge, mbwa anayeuma watu na kila tunayemuona anaudhi.

Hayo ni kwa sababu mjue kuwa Mwenyezi Mungu anayajua yaliomo mbinguni na yaliyomo ardhini na kwamba Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa kila kitu.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kubainisha miko ya Al-Kaaba, miezi mitukufu na wanyama wa kuchinja, anaashiria kwamba hekima ya sharia hii ni kuwa watu wajue kwamba Mwenyezi Mungu anajua ufafanuzi wa mambo katika ardhi na katika mbingu; na ambayo yana masilahi kwa watu katika dini yao na dunia yao.

Kuna masilahi gani makubwa zaidi ya usalama wa maisha ya mtu na mali yake ijapokuwa ni kwa kipindi fulani. Tumeyaona mataifa makubwa yanayotwangana, wakati huu, yakiafikiana kuwa baadhi ya miji iwe ni maeneo maalumu ya amani, haijuzu kwa taifa linalopigana kuishirikisha katika vita wala kuweka vituo vya kijeshi katika ardhi hiyo au kupita wanajeshi wake.

Jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni mkali wa kuadhibu na kwamba Mwenyezi Mungu ni mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amekutanisha adhabu na rehema na maghufira ili mja awe anahofia adhabu yake na kutaraji rehema yake. Kwa sababu mja, akiwa na hofu atajiepusha na maasi na akiwa na matarajio atajitahidi katika twaa.

Razi anasema: "Mwenyezi Mungu (s.w.t) ametaja kuwa yeye ni mkali wa kuadhibu, kisha akafuatishia kwa wasifu wa rehema na maghufira. Na huu ni uzinduzi juu ya undani kuwa kupatikana kiumbe ni kwa ajili ya rehema. Na kwa dhahiri ni kuwa mwisho hauwi ila kwa rehema" Hiyo ni kweli kabisa.

Haimlazimu Mtume ila kufikisha tu.

Hatakiwi jingine zaidi ya hilo, ambapo hapana udhuru baada ya kufikisha kwa anayepuuza na kupetuka mpaka. Ama hisabu na adhabu hiyo ni juu ya Mwenyezi Mungu pekee Yake. Mwenyezi Mungu anasema:

"Hakika ni juu yako kufikisha tu, na ni juu yetu hisabu." (13:40)

Mwenyezi Mungu anayajua mnayoyadhihirisha katika kauli na vitendo na mnayoyaficha. Haya ni makemeo kwa anayeinyamazia haki, na hasa yule anayeifanyia biashara kwa kujipanua na jina la dini na la nchi.

﴿قُل لَّا يَسْتَوِي الْخَبِيثُ وَالطَّيِّبُ وَلَوْ أَعْجَبَكَ كَثْرَةُ الْخَبِيثِ فَاتَّقُوا اللَّـهَ يَا أُولِي الْأَلْبَابِ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ﴾

100.Sema: Hawi sawa habithi na mwema, hata ukikupendeza wingi wa habith, Basi mcheni Mwenyezi Mungu enyi wenye akili ili mpate kufaulu.

WINGI WA MWOVU

Aya 100

MAANA

Aya hii inarudufu Aya ile isemayo:

﴿لَا يَسْتَوِي أَصْحَابُ النَّارِ وَأَصْحَابُ الْجَنَّةِ أَصْحَابُ الْجَنَّةِ هُمُ الْفَائِزُونَ﴾

"Hawawi sawa watu wa Motoni na watu wa Peponi, watu wa Peponi ndio wenye kufuzu" (59:20)

Wingi wa habithi ni anayoyamiliki miongoni mwa jaha na mali. Mwenye akili hawezi kumweka sawa habithi, na mwema hata kama ana mali nyingi na jaha kubwa. Kwa sababu jaha na mali hazimfanyi mwovu kuwa mwema; wala ufakiri na udhaifu haumfanyi mwema kuwa mwovu.

Mtu habith katika kipimo cha dini ni yule anayeasi hukumu za Mwenyezi Mungu katika kitabu chake na Sunna za Mtume wake. Na katika desturi ya watu ni yule wanayemhofia kwa shari yake na wasiyemwamini kwa jambo lolote na kutomsadiki katika kauli au vitendo vyake. Kimsingi ni kwamba mwenye sifa hizi, ni mbaya pia mbele ya Mwenyezi Mungu. Mtume wa Mwenyezi Mungu anasema:"Utukufu zaidi wa imani ni kuaminiwa na watu." Ama mtu mwema ni yule aliye kinyume cha mtu habithi katika sifa zake zote.

JE RIZIKI NI BAHATI AU MAJAALIWA?

Unaweza kuuliza : Ikiwa habithi anachukiwa na Mwenyezi Mungu na mwema anaridhiwa na Mwenyezi Mungu, kwa nini basi habithi anafaulu katika maisha haya na kuneemeshwa kwa jaha na utajiri, na mwema anaanguka na wala hapati matakwa yake?

Jibu : Maisha yana desturi na kanuni zinazokwenda nayo, na hazigeuki kwa hali yoyote ile. Kwa sababu hisia na uoni unakataa mkorogano katika ulimwengu. Desturi na kanuni hizi ni katika matengenezo ya Mwenyezi Mungu Mtukufu: Kwa sababu yeye ni muumbaji wa asili na vilivyomo katika asili.

Kimsingi ni kuwa desturi ya kawaida ya tabia inakataa kuwa mali, afya na ilimu, vishuke tu kutoka mbinguni. Isipokuwa vitu hivi na mfano wake vinakuja kwa njia zake na sababu zake za kimaumbile. Elimu inatokana na kujifundisha, afya inatokana na lishe na kinga, na mali inatokana na kazi. Kwa hiyo mwenye kujifunza hujua, mwenye kujiepusha na visababishi vya maradhi husalimika, mwenye kujinyonga atakufa tu; awe mwema au mwovu, mumin au kafiri.

Kwa hiyo wema au imani hauoteshi ngano wala hauponeshi ugonjwa wala haumfanyi asiyejua kuwa mjuzi, Yote haya na mfano wake yanakwenda kwa desturi ya tabia na desturi ya tabia inakwenda kwa matakwa ya Mwenyezi Mungu, hilo halina shaka.

Kwa sababu yeye ndiye aliyejaalia kujifundisha ndio sababu ya elimu na kujikinga ndio sababu ya afya na kupanda kuwa ndio sababu ya kuvuna. Yeye ni Muumba wa kila kitu na kwake yeye ni mwishilio wa kila jambo.

Ndiyo! kuchuma mali kuna njia nyingi, na milango mingi, nyingine Mwenyezi Mungu amezihalalisha na nyingine akaziharamisha. Mwenyezi Mungu (s.w.t) amehalalisha biashara, kilimo na viwanda; na akaharamisha riba, utapeli, rushwa, kupora na ulanguzi.

Mwenye kuchuma mali kwa njia ya halali hunasibishwa chumo lake kwake, kwa sababu yeye amejitahidi na kufanya bidii kuitafuta, na vilevile hunasabishwa kwa Mwenyezi Mungu. Kwa sababu yeye ndiye aliyepitisha sababu hizi na kuzihalalisha kwa kila azitakaye, awe mwema au mwovu.

Ama mwenye kuchuma mali kwa njia za haramu; kama vile riba na unyang'anyi; chumo lake litanasibishwa kwake na kwa hali aliyoitumia, wala halinasibishwi kwa Mwenyezi Mungu, kwa sababu yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu ameharamisha njia hizi kwa mwema na mwovu.

Utasema : Haya yote ni kweli, lakini hayajibu swali wala hayatatui mushkeli. Tumewahi kumuona mwema na mwovu wote wakifuata njia za sharia za riziki, na kuzitafuta riziki kwa njia zile alizozihalalisha Mwenyezi Mungu na kuziharamisha, lakini pamoja na hayo, riziki inakuwa zaidi kwa mwovu aliye habith na kuwa dhiki kwa mwema, pengine huyu mwema ametoa juhudi maradufu ya yule mwovu, bali mara nyingine riziki humjia mwovu bila ya kutazamia wala maandalizi au juhudi, na inazuilika kumwendea mwema anapoitazamia na kuifanyia maandalizi na juhudi?

Jibu : Baadhi ya watu wanakimbilia kulifasiri hilo kwa kusema ni sadfa au bahati. Hakuna kinachofahamika kutokana na maelezo hayo zaidi ya kushindwa kwao kutoa tafsiri sahihi. Vinginevyo wasingelikimbilia kwenye maelezo ya kubahatisha tu.

Kwa hiyo sisi tunapinga Sadfa na bahati na tunaamini kwa imani ya mkato kwamba kuna chaguo la juu linajiingiza kwa sababu tusizozijua. kwa vile elimu katika masuala hayo na mfano wake, bado ni changa. Na kushindwa kwa elimu hakumaanishi kuwa kitu hakiko. Imani yetu hii inatiliwa mkazo na kauli zake Mwenyezi Mungu zifuatazo:

﴿وَاللَّـهُ فَضَّلَ بَعْضَكُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ فِي الرِّزْقِ﴾

"Na Mwenyezi Mungu amewafadhilisha baadhi yenu kuliko wengine katika riziki" (16:71)

﴿اللَّـهُ يَبْسُطُ الرِّزْقَ لِمَن يَشَاءُ وَيَقْدِرُ﴾

"Mwenyezi Mungu hukunjua riziki kwa amtakaye na huidhikisha (13:26) Ay a hii imekuja kwa herufi zake katika 17:30, 28:82, 29:62, 30:37, 34: 36, 34: 39, 39:52, 42:12.

Kwa hiyo basi aliyesema au anayesema: Mwenyezi Mungu amemtajirisha fulani kwa kuwa yeye ni mwema basi atakuwa anazungumza mantiki ya Firaun na kupima kwa kipimo cha Shetani. Hekima yake Mwenyezi Mungu Mtukufu imetaka kumlipa mwema malipo mazuri na kumwadhibu mwovu katika akhera inayobakia sio katika hii dunia inayokwisha. Hii ni Nyumba ya matendo na ile ni Nyumba ya Hisabu. Zaidi ya haya ni kuwa wingi wa mali wa mwovu huenda ukawa ni balaa kwake na sababu ya kuadhibiwa kwake. Mwenyezi Mungu anasema:

﴿ذَرْهُمْ يَأْكُلُوا وَيَتَمَتَّعُوا وَيُلْهِهِمُ الْأَمَلُ فَسَوْفَ يَعْلَمُونَ﴾

"Waache wale na wafurahi na iwazuge tamaa, watakuja jua." (15:3)

﴿يَتَمَتَّعُونَ وَيَأْكُلُونَ كَمَا تَأْكُلُ الْأَنْعَامُ وَالنَّارُ مَثْوًى لَّهُمْ﴾

"Hujistarehesha na hula kama walivyo wanyama, na moto ndio makazi yao." (47:12)

Kwa ufupi ni kwamba riziki inategemea mambo mawili. Kuhangaika na matakwa ya Mwenyezi Mungu. Asiyehangaika ataishi omba omba; na mwenye kuhangaika Mwenyezi Mungu humruzuku kutokana na bidii yake, akitaka humpa nyingi na akitaka humpa chache.

Uhakika huu umo katika maumbile ya binadamu na anaufanya bila ya kujitambua. Mfanya biashara humwomba Mwenyezi Mungu (s.w.t) amruzuku kupata soko zuri la bidhaa zake na watu wazikubali. Mkulima anamwomba Mungu aiteremshie mimea yake mvua; wala hamuombi kumwoteshea mimea bila ya mvua.

Mimi hapa namwomba Mwenyezi Mungu ampe tawfiq mwanangu katika masomo yake na kufaulu mtihani; wala si mwombi akipe mawazo chuo kikuu kimpatie shahada bila ya kusoma na kufanya mtihani. Iko methali isemayo: Mgaagaa na upwa hali wali mkavu.

Pengine inawezekana mahangaiko yasiambulie kitu, lakini pamoja na hayo inatakikana kupanga mipango na kuongeza juhudi. Kwa sababu kuongeza juhudi, kutumia mipango, na kuvumilia tabu ni sababu ya matakwa ya kufaulu kutoka kwake Mwenyezi Mungu Mtukufu.

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَسْأَلُوا عَنْ أَشْيَاءَ إِن تُبْدَ لَكُمْ تَسُؤْكُمْ وَإِن تَسْأَلُوا عَنْهَا حِينَ يُنَزَّلُ الْقُرْآنُ تُبْدَ لَكُمْ عَفَا اللَّـهُ عَنْهَا وَاللَّـهُ غَفُورٌ حَلِيمٌ﴾

101.Enyi Mlioamini! Msiulize mambo ambayo mkidhihirishiwa yatawachukiza. Na mnapoyauliza inapoteremshwa Qur'an mtabainishiwa. Mwenyezi Mungu ameyasamehe hayo. Na Mwenyezi Mungu ni mwingi wa maghufira Mpole.

﴿قَدْ سَأَلَهَا قَوْمٌ مِّن قَبْلِكُمْ ثُمَّ أَصْبَحُوا بِهَا كَافِرِينَ﴾

102.Waliyauliza watu waliokuwa kabla yenu kisha wakawa makafiri kwayo.

MSIULIZEULIZE MAMBO

Aya 101-102

MAANA

Enyi Mlioamini! Msiulize mambo ambayo mkidhihirishiwa yatawachukiza.

Kauli yake Mwenyezi Mungu 'Msiulize' inaishiria kuwa baadhi ya Masahaba walikuwa waking'ang'ania kuuliza mambo yasiyokuwa na dharura yoyote kuyajua na huenda jibu lake likawaudhi waulizaji. Kuna riwaya isemayo kuwa mtu mmoja alimuuliza Mtume(s.a.w.w) : "Ni nani baba yangu?" Mtume akamwambia, "baba yako ni Fulani" Mwingine akauliza "Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Baba yangu yuko wapi? Mtume akajibu: "Yuko motoni," ndipo ikashuka Aya hiyo.

Riwaya nyingine inasema kuwa Mtume alisema: "Mwenyezi Mungu amewafaradhishia kuhiji, basi hijini." Wakauliza: "Kila mwaka ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?" Mtume akanyamaza. Wakarudia kuuliza, akasema La; lau ningelisema naam, ingelikuwa wajib." Ndipo ikashuku Aya hii. Riwaya hii ndiyo yenye nguvu kuliko ile ya kwanza.

Na mnapoyauliza inapoteremshwa Qur'an mtabainishiwa.

Yaani msijikalifishe kuuliza mambo ila baada ya kuteremshwa Qur'an. Mtakapoanza kuuliza Mtume(s.a.w.w) atawadhirishia mliyokuwa mkiyauliza.

Kwa hali hii, inatubainikia kuwa riwaya ya Hija ndiyo yenye nguvu katika sababu ya kushuka Aya, kuliko riwaya ya kuuliza mababa na wahenga wa Masahaba. Kwa sababu Qur'an inaanza kuleta itikadi na sharia na wala sio kuanzia kwa mababa na mababu wa Masahaba. Katika Hadith imeelezwa:"Hakika Mwenyezi Mungu ameweka mipaka msiikiuke; amewafaradhishia faradhi msizipoteze; ameharamishia vitu msivifanye; na ameacha vitu vingine si kwa kusahau, lakini ni kwa kuwahurumia, basi vikubalini wala msivifanyie utafiti".

Mwenyezi Mungu amesamehe hayo

Yaani maswali yenu yaliyotangulia, kwa hiyo msiyarudie. Imesemekana kuwa maana yake ni amezuia kutaja vitu mlivyoviulizia, basi nanyi jizuieni wala msijikalifu kuviulizia. Tafsir zote mbili zina uwezekano hazikataliwi na dhahiri ya tamko.

Na Mwenyezi Mungu ni mwingi wa maghufira, Mpole.

Humsamehe mkosaji akikosea tena.

Waliyauliza watu waliokuwa kabla yenu kisha wakawa makafiri kwayo.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kuwakataza kuuliza mambo wasiyokuwa na haja nayo, anawapigia mfano wa watu waliokuwa kabla yao, waliuliza wakang'ang'ania kuuliza. Walipobainishiwa na Mwenyezi Mungu walichukia wakaasi na wakastahiki adhabu. Lau wangeliacha kuuliza ingelikuwa bora kwao.

Wafasiri wamerefusha maneno katika kubainisha makusudio ya watu waliouliza, kisha wakawa makafiri kwa sababu ya kuuliza, lakini Aya haikubainisha. Pamoja na hivyo, tunaweza kusema kuwa watu waliouliza wakawa makafiri kwa sababu ya kuuliza ni wana wa Israil, kwa sababu ya kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu akiwasimulia:

﴿فَقَدْ سَأَلُوا مُوسَىٰ أَكْبَرَ مِن ذَٰلِكَ فَقَالُوا أَرِنَا اللَّـهَ جَهْرَةً ﴾

"Hakika walimtaka Musa makubwa kuliko hayo, Walisema: Tuonyeshe Mwenyezi Mungu waziwazi" (4:153)

﴿مَا جَعَلَ اللَّـهُ مِن بَحِيرَةٍ وَلَا سَائِبَةٍ وَلَا وَصِيلَةٍ وَلَا حَامٍ وَلَـٰكِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا يَفْتَرُونَ عَلَى اللَّـهِ الْكَذِبَ وَأَكْثَرُهُمْ لَا يَعْقِلُونَ﴾

103.Mwenyezi Mungu hakujaalia Bahira wala Saiba wala Waswila wala Hami; Lakini waliokufuru wanamzulia Mwenyezi Mungu uwongo na wengi wao hawafahamu.

﴿وَإِذَا قِيلَ لَهُمْ تَعَالَوْا إِلَىٰ مَا أَنزَلَ اللَّـهُ وَإِلَى الرَّسُولِ قَالُوا حَسْبُنَا مَا وَجَدْنَا عَلَيْهِ آبَاءَنَا أَوَلَوْ كَانَ آبَاؤُهُمْ لَا يَعْلَمُونَ شَيْئًا وَلَا يَهْتَدُونَ﴾

104.Wakiambiwa njooni katika yale aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu na kwa Mtume, husema: Yanatutosha yale tuliyowakuta nayo babu zetu. Je hata kama baba zao walikuwa hawajui kitu wala hawakuongoka?

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا عَلَيْكُمْ أَنفُسَكُمْ لَا يَضُرُّكُم مَّن ضَلَّ إِذَا اهْتَدَيْتُمْ إِلَى اللَّـهِ مَرْجِعُكُمْ جَمِيعًا فَيُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ﴾

105.Enyi mlioamini! Jiangalie nafsi zenu. Hawawadhuru waliopotea ikiwa mmeongoka. Marejeo yenu nyote ni kwa Mwenyezi Mungu. Atawaambia yale mliyokuwa mkiyatenda.

HAKUNA BAHIRAWALA SAIBA

Aya 103-105

MAANA

Mwenyezi Mungu hakujaalia Bahira wala Saiba wala Waswila wala Hami.

Bahira, ni ngamia aliyetobolewa masikio, watu wa wakati wa Jahilia walikuwa wakifanya hivyo, ikiwa ngamia atazaa mimba kumi ; na inasemekana ni mimba tano. Wanamwacha bila ya kutumiwa na mtu yoyote. Saiba ni ngamia waliyemwekea nadhiri kwa waungu, na wana mwacha akijilisha mwenyewe popote bila ya kufungwa wala kuwa na mchungaji sawa na Bahira.

Wasila ni mbuzi anayezaa mtoto wa kiume na wa kike pamoja. Desturi yao ilikuwa kama akizaa mume wanamfanya ni wa waungu na akizaa mke ni wao. Iwapo atazaa mume na mke pamoja, hawamchinji mume wakisema kuwa ameunganishwa na dada yake. Hami ni dume aliyezalisha mimba kumi, wanamwacha hazuiliwi na maji wala malisho, wakisema ameuhami mgongo wake.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anabainisha kwamba yote hayo hayamo katika dini, na kwamba dume, jike na mbuzi, vyovyote wanavyofanyiwa, wanabakia na uhalali wake kama walivyokuwa mwanzo na wala hawaharamishwi na porojo hizo.

Lakini waliokufuru wanamzulia Mwenyezi Mungu uwongo na wengi wao hawafahamu.

Watu wa kijahilia walikuwa wakikubali kuweko kwa muumba kwa dalili kwamba wao wamenasibishia uharamu wa Hami, Saiba, Bahira na Waswila, lakini pamoja na hayo Mwenyezi Mungu amewanasibishia ukafiri.

Kwa sababu wao wamemnasibishia uharamu kwa uwongo na uzushi. Kwa hiyo, basi kila anayemnasibishia Mwenyezi Mungu na yasiyokuwa na dalili ya Kitab wala Hadith ya Mtume wake basi huyo ni kafir kwa sharti ya kutegemea kumnasibishia Mungu, huku akijua kutokuwepo dalili.

Hii, kwa lugha ya watu wa sharia, huitwa Bid'a (uzushi). Kuna Hadithi isemayo: "Kila bid'a ni upotevu na kila upotevu ni motoni".

Ilivyo ni kuwa kufaradhia huko kuko mbali na hali halisi ilivyo, Ni nani anayemnasibishia hukumu Mwenyezi Mungu huku akijua kuwa hakuna dalili. Pengine anaweza akadhani ni dalili, lakini kumbe sio dalili.

Wakiambiwa njooni katika yale aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu na kwa Mtume, husema: "Yanatutosha yale tuliyowakuta nayo babu zetu. Je hata kama babu zao walikuwa hawajui kitu wala hawakuongoka?

Razi anasema: "Maana yanajulikana, nayo ni jibu la kuwapinga watu wa Taqlid (kufuata)". Tumezungumzia kuhusu Taqlid katika Juz.2 (2:170)

Enyi mlioamini! Jiangalieni nafsi zenu, Hawawadhuru waliopotea ikiwa mmeongoka, Marejeo yenu nyote ni kwa Mwenyezi Mungu.

Razi ametaja njia nane za kufasiri Aya hii. Mmoja wa wafasiri wapya ameandika kurasa 33. Lililowafanya wawili hawa na wengineo kurefusha mambo hivi ni kuwa kuamrisha mema ni wajibu na dhahiri ya Aya inafahamisha kutokuwa wajib na kwamba ni juu ya mtu kujishughulikia mwenyewe. Ama wengine wana majukumu yao juu ya nafsi zao wala si wajibu kwa yoyote kuiongoza au kuikanya nafsi ya mwingine.

Ilivyo tafsir ya Aya hii ni kwamba, ni juu ya mtu kuamrisha mema. Kuamrisha kwake kukinufaisha basi hayo ndiyo yanayotakikana. Vinginevyo basi atakuwa ametekeleza lile aliloamrishwa wala hautamdhuru upotevu wa aliyepotea.

Mwenye jukumu baada ya kuamrisha ni yule aliyepotea na wala sio mwamrishaji. Tafsir hii imetilia mkazo wajibu wa kuamrisha mema na sio kupinga.

3

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA SABA

﴿جَعَلَ اللَّـهُ الْكَعْبَةَ الْبَيْتَ الْحَرَامَ قِيَامًا لِّلنَّاسِ وَالشَّهْرَ الْحَرَامَ وَالْهَدْيَ وَالْقَلَائِدَ ذَٰلِكَ لِتَعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ يَعْلَمُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ وَأَنَّ اللَّـهَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ﴾

97.Mwenyezi Mungu amefanya Al-Kaaba nyumba tukufu, kuwa ni kisimamo cha watu na miezi mitukufu na wanyama wa kuchinja na vigwe; hayo ni kwa sababu mjue kuwa Mwenyezi Mungu anayajua yaliyomo mbinguni na yaliyomo ardhini na kwamba Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.

﴿اعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ شَدِيدُ الْعِقَابِ وَأَنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ﴾

98. Jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni mkali wa kuadhibu na kwamba Mwenyezi Mungu ni mwingi wa maghufira, Mwingi wa kurehemu.

﴿مَّا عَلَى الرَّسُولِ إِلَّا الْبَلَاغُ وَاللَّـهُ يَعْلَمُ مَا تُبْدُونَ وَمَا تَكْتُمُونَ﴾

99.Haimlazimu Mtume ila kufikisha tu, na Mwenyezi Mungu anajua mnayo yadhihirisha na mnayoyaficha.

NYUMBA TAKATIFU

Aya 97-99

MAANA

Mwenyezi Mungu ameifanya Al-Kaaba, nyumba takatifu, kuwa ni kisimamo cha watu na miezi mitakatifu na wanyama wa kuchinja na vigwe.

Kisimamo cha watu; yaani mahali pa ibada na ibada za Hijja. Miezi mitakatifu ni ile minne Rajab, Dhul-qa'da, Dhul-Hijja na Muharram[5] Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameharamisha kupigana huko na katika miezi hiyo; ispokuwa kutetea nafsi au mali. Anasema:

﴿وَلَا تُقَاتِلُوهُمْ عِندَ الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ حَتَّىٰ يُقَاتِلُوكُمْ فِيهِ﴾

"Wala msipigane nao karibu na Msikiti Mtakatifu mpaka wakupigeni huko" (2:191) Na akasema tena:

﴿الشَّهْرُ الْحَرَامُ بِالشَّهْرِ الْحَرَامِ وَالْحُرُمَاتُ قِصَاصٌ فَمَنِ اعْتَدَىٰ عَلَيْكُمْ فَاعْتَدُوا عَلَيْهِ بِمِثْلِ مَا اعْتَدَىٰ عَلَيْكُمْ ﴾

"Mwezi mtakatifu kwa mwezi mtakatifu; na vitu vitakatifu vina kisasi. Basi wanaowachokoza, pia nanyi wachokozeni kwa kadiri walivyowachokoza" (2:194)

Mnyama wa kuchinja, ni wale wanaochinjwa Makka. Na kigwe ni ukambaa anaofungwa nao mnyama wa kuchinja kuwa ni alama ya kufahamisha kuwa ni wa Al-Kaaba ili asitaradhiwe na yeyote. Kwa hiyo kuunganisha vigwe kwa wanyama ni kuunganisha maalum katika ujumla.

Makusudio ya kutaja chinjo pamoja na Nyumba takatifu na miezi mitakatifu ni kwamba mnyama wa kuchinja inapasa awe salama yeye na anayemchunga, kwa sababu yeye anakusudia Haram tukufu.

Bali ni kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewapa amani ndege na wanyama walio katika haramu yake; isipokuwa mwewe, kipanga, kunguru, panya, nge, mbwa anayeuma watu na kila tunayemuona anaudhi.

Hayo ni kwa sababu mjue kuwa Mwenyezi Mungu anayajua yaliomo mbinguni na yaliyomo ardhini na kwamba Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa kila kitu.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kubainisha miko ya Al-Kaaba, miezi mitukufu na wanyama wa kuchinja, anaashiria kwamba hekima ya sharia hii ni kuwa watu wajue kwamba Mwenyezi Mungu anajua ufafanuzi wa mambo katika ardhi na katika mbingu; na ambayo yana masilahi kwa watu katika dini yao na dunia yao.

Kuna masilahi gani makubwa zaidi ya usalama wa maisha ya mtu na mali yake ijapokuwa ni kwa kipindi fulani. Tumeyaona mataifa makubwa yanayotwangana, wakati huu, yakiafikiana kuwa baadhi ya miji iwe ni maeneo maalumu ya amani, haijuzu kwa taifa linalopigana kuishirikisha katika vita wala kuweka vituo vya kijeshi katika ardhi hiyo au kupita wanajeshi wake.

Jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni mkali wa kuadhibu na kwamba Mwenyezi Mungu ni mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amekutanisha adhabu na rehema na maghufira ili mja awe anahofia adhabu yake na kutaraji rehema yake. Kwa sababu mja, akiwa na hofu atajiepusha na maasi na akiwa na matarajio atajitahidi katika twaa.

Razi anasema: "Mwenyezi Mungu (s.w.t) ametaja kuwa yeye ni mkali wa kuadhibu, kisha akafuatishia kwa wasifu wa rehema na maghufira. Na huu ni uzinduzi juu ya undani kuwa kupatikana kiumbe ni kwa ajili ya rehema. Na kwa dhahiri ni kuwa mwisho hauwi ila kwa rehema" Hiyo ni kweli kabisa.

Haimlazimu Mtume ila kufikisha tu.

Hatakiwi jingine zaidi ya hilo, ambapo hapana udhuru baada ya kufikisha kwa anayepuuza na kupetuka mpaka. Ama hisabu na adhabu hiyo ni juu ya Mwenyezi Mungu pekee Yake. Mwenyezi Mungu anasema:

"Hakika ni juu yako kufikisha tu, na ni juu yetu hisabu." (13:40)

Mwenyezi Mungu anayajua mnayoyadhihirisha katika kauli na vitendo na mnayoyaficha. Haya ni makemeo kwa anayeinyamazia haki, na hasa yule anayeifanyia biashara kwa kujipanua na jina la dini na la nchi.

﴿قُل لَّا يَسْتَوِي الْخَبِيثُ وَالطَّيِّبُ وَلَوْ أَعْجَبَكَ كَثْرَةُ الْخَبِيثِ فَاتَّقُوا اللَّـهَ يَا أُولِي الْأَلْبَابِ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ﴾

100.Sema: Hawi sawa habithi na mwema, hata ukikupendeza wingi wa habith, Basi mcheni Mwenyezi Mungu enyi wenye akili ili mpate kufaulu.

WINGI WA MWOVU

Aya 100

MAANA

Aya hii inarudufu Aya ile isemayo:

﴿لَا يَسْتَوِي أَصْحَابُ النَّارِ وَأَصْحَابُ الْجَنَّةِ أَصْحَابُ الْجَنَّةِ هُمُ الْفَائِزُونَ﴾

"Hawawi sawa watu wa Motoni na watu wa Peponi, watu wa Peponi ndio wenye kufuzu" (59:20)

Wingi wa habithi ni anayoyamiliki miongoni mwa jaha na mali. Mwenye akili hawezi kumweka sawa habithi, na mwema hata kama ana mali nyingi na jaha kubwa. Kwa sababu jaha na mali hazimfanyi mwovu kuwa mwema; wala ufakiri na udhaifu haumfanyi mwema kuwa mwovu.

Mtu habith katika kipimo cha dini ni yule anayeasi hukumu za Mwenyezi Mungu katika kitabu chake na Sunna za Mtume wake. Na katika desturi ya watu ni yule wanayemhofia kwa shari yake na wasiyemwamini kwa jambo lolote na kutomsadiki katika kauli au vitendo vyake. Kimsingi ni kwamba mwenye sifa hizi, ni mbaya pia mbele ya Mwenyezi Mungu. Mtume wa Mwenyezi Mungu anasema:"Utukufu zaidi wa imani ni kuaminiwa na watu." Ama mtu mwema ni yule aliye kinyume cha mtu habithi katika sifa zake zote.

JE RIZIKI NI BAHATI AU MAJAALIWA?

Unaweza kuuliza : Ikiwa habithi anachukiwa na Mwenyezi Mungu na mwema anaridhiwa na Mwenyezi Mungu, kwa nini basi habithi anafaulu katika maisha haya na kuneemeshwa kwa jaha na utajiri, na mwema anaanguka na wala hapati matakwa yake?

Jibu : Maisha yana desturi na kanuni zinazokwenda nayo, na hazigeuki kwa hali yoyote ile. Kwa sababu hisia na uoni unakataa mkorogano katika ulimwengu. Desturi na kanuni hizi ni katika matengenezo ya Mwenyezi Mungu Mtukufu: Kwa sababu yeye ni muumbaji wa asili na vilivyomo katika asili.

Kimsingi ni kuwa desturi ya kawaida ya tabia inakataa kuwa mali, afya na ilimu, vishuke tu kutoka mbinguni. Isipokuwa vitu hivi na mfano wake vinakuja kwa njia zake na sababu zake za kimaumbile. Elimu inatokana na kujifundisha, afya inatokana na lishe na kinga, na mali inatokana na kazi. Kwa hiyo mwenye kujifunza hujua, mwenye kujiepusha na visababishi vya maradhi husalimika, mwenye kujinyonga atakufa tu; awe mwema au mwovu, mumin au kafiri.

Kwa hiyo wema au imani hauoteshi ngano wala hauponeshi ugonjwa wala haumfanyi asiyejua kuwa mjuzi, Yote haya na mfano wake yanakwenda kwa desturi ya tabia na desturi ya tabia inakwenda kwa matakwa ya Mwenyezi Mungu, hilo halina shaka.

Kwa sababu yeye ndiye aliyejaalia kujifundisha ndio sababu ya elimu na kujikinga ndio sababu ya afya na kupanda kuwa ndio sababu ya kuvuna. Yeye ni Muumba wa kila kitu na kwake yeye ni mwishilio wa kila jambo.

Ndiyo! kuchuma mali kuna njia nyingi, na milango mingi, nyingine Mwenyezi Mungu amezihalalisha na nyingine akaziharamisha. Mwenyezi Mungu (s.w.t) amehalalisha biashara, kilimo na viwanda; na akaharamisha riba, utapeli, rushwa, kupora na ulanguzi.

Mwenye kuchuma mali kwa njia ya halali hunasibishwa chumo lake kwake, kwa sababu yeye amejitahidi na kufanya bidii kuitafuta, na vilevile hunasabishwa kwa Mwenyezi Mungu. Kwa sababu yeye ndiye aliyepitisha sababu hizi na kuzihalalisha kwa kila azitakaye, awe mwema au mwovu.

Ama mwenye kuchuma mali kwa njia za haramu; kama vile riba na unyang'anyi; chumo lake litanasibishwa kwake na kwa hali aliyoitumia, wala halinasibishwi kwa Mwenyezi Mungu, kwa sababu yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu ameharamisha njia hizi kwa mwema na mwovu.

Utasema : Haya yote ni kweli, lakini hayajibu swali wala hayatatui mushkeli. Tumewahi kumuona mwema na mwovu wote wakifuata njia za sharia za riziki, na kuzitafuta riziki kwa njia zile alizozihalalisha Mwenyezi Mungu na kuziharamisha, lakini pamoja na hayo, riziki inakuwa zaidi kwa mwovu aliye habith na kuwa dhiki kwa mwema, pengine huyu mwema ametoa juhudi maradufu ya yule mwovu, bali mara nyingine riziki humjia mwovu bila ya kutazamia wala maandalizi au juhudi, na inazuilika kumwendea mwema anapoitazamia na kuifanyia maandalizi na juhudi?

Jibu : Baadhi ya watu wanakimbilia kulifasiri hilo kwa kusema ni sadfa au bahati. Hakuna kinachofahamika kutokana na maelezo hayo zaidi ya kushindwa kwao kutoa tafsiri sahihi. Vinginevyo wasingelikimbilia kwenye maelezo ya kubahatisha tu.

Kwa hiyo sisi tunapinga Sadfa na bahati na tunaamini kwa imani ya mkato kwamba kuna chaguo la juu linajiingiza kwa sababu tusizozijua. kwa vile elimu katika masuala hayo na mfano wake, bado ni changa. Na kushindwa kwa elimu hakumaanishi kuwa kitu hakiko. Imani yetu hii inatiliwa mkazo na kauli zake Mwenyezi Mungu zifuatazo:

﴿وَاللَّـهُ فَضَّلَ بَعْضَكُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ فِي الرِّزْقِ﴾

"Na Mwenyezi Mungu amewafadhilisha baadhi yenu kuliko wengine katika riziki" (16:71)

﴿اللَّـهُ يَبْسُطُ الرِّزْقَ لِمَن يَشَاءُ وَيَقْدِرُ﴾

"Mwenyezi Mungu hukunjua riziki kwa amtakaye na huidhikisha (13:26) Ay a hii imekuja kwa herufi zake katika 17:30, 28:82, 29:62, 30:37, 34: 36, 34: 39, 39:52, 42:12.

Kwa hiyo basi aliyesema au anayesema: Mwenyezi Mungu amemtajirisha fulani kwa kuwa yeye ni mwema basi atakuwa anazungumza mantiki ya Firaun na kupima kwa kipimo cha Shetani. Hekima yake Mwenyezi Mungu Mtukufu imetaka kumlipa mwema malipo mazuri na kumwadhibu mwovu katika akhera inayobakia sio katika hii dunia inayokwisha. Hii ni Nyumba ya matendo na ile ni Nyumba ya Hisabu. Zaidi ya haya ni kuwa wingi wa mali wa mwovu huenda ukawa ni balaa kwake na sababu ya kuadhibiwa kwake. Mwenyezi Mungu anasema:

﴿ذَرْهُمْ يَأْكُلُوا وَيَتَمَتَّعُوا وَيُلْهِهِمُ الْأَمَلُ فَسَوْفَ يَعْلَمُونَ﴾

"Waache wale na wafurahi na iwazuge tamaa, watakuja jua." (15:3)

﴿يَتَمَتَّعُونَ وَيَأْكُلُونَ كَمَا تَأْكُلُ الْأَنْعَامُ وَالنَّارُ مَثْوًى لَّهُمْ﴾

"Hujistarehesha na hula kama walivyo wanyama, na moto ndio makazi yao." (47:12)

Kwa ufupi ni kwamba riziki inategemea mambo mawili. Kuhangaika na matakwa ya Mwenyezi Mungu. Asiyehangaika ataishi omba omba; na mwenye kuhangaika Mwenyezi Mungu humruzuku kutokana na bidii yake, akitaka humpa nyingi na akitaka humpa chache.

Uhakika huu umo katika maumbile ya binadamu na anaufanya bila ya kujitambua. Mfanya biashara humwomba Mwenyezi Mungu (s.w.t) amruzuku kupata soko zuri la bidhaa zake na watu wazikubali. Mkulima anamwomba Mungu aiteremshie mimea yake mvua; wala hamuombi kumwoteshea mimea bila ya mvua.

Mimi hapa namwomba Mwenyezi Mungu ampe tawfiq mwanangu katika masomo yake na kufaulu mtihani; wala si mwombi akipe mawazo chuo kikuu kimpatie shahada bila ya kusoma na kufanya mtihani. Iko methali isemayo: Mgaagaa na upwa hali wali mkavu.

Pengine inawezekana mahangaiko yasiambulie kitu, lakini pamoja na hayo inatakikana kupanga mipango na kuongeza juhudi. Kwa sababu kuongeza juhudi, kutumia mipango, na kuvumilia tabu ni sababu ya matakwa ya kufaulu kutoka kwake Mwenyezi Mungu Mtukufu.

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَسْأَلُوا عَنْ أَشْيَاءَ إِن تُبْدَ لَكُمْ تَسُؤْكُمْ وَإِن تَسْأَلُوا عَنْهَا حِينَ يُنَزَّلُ الْقُرْآنُ تُبْدَ لَكُمْ عَفَا اللَّـهُ عَنْهَا وَاللَّـهُ غَفُورٌ حَلِيمٌ﴾

101.Enyi Mlioamini! Msiulize mambo ambayo mkidhihirishiwa yatawachukiza. Na mnapoyauliza inapoteremshwa Qur'an mtabainishiwa. Mwenyezi Mungu ameyasamehe hayo. Na Mwenyezi Mungu ni mwingi wa maghufira Mpole.

﴿قَدْ سَأَلَهَا قَوْمٌ مِّن قَبْلِكُمْ ثُمَّ أَصْبَحُوا بِهَا كَافِرِينَ﴾

102.Waliyauliza watu waliokuwa kabla yenu kisha wakawa makafiri kwayo.

MSIULIZEULIZE MAMBO

Aya 101-102

MAANA

Enyi Mlioamini! Msiulize mambo ambayo mkidhihirishiwa yatawachukiza.

Kauli yake Mwenyezi Mungu 'Msiulize' inaishiria kuwa baadhi ya Masahaba walikuwa waking'ang'ania kuuliza mambo yasiyokuwa na dharura yoyote kuyajua na huenda jibu lake likawaudhi waulizaji. Kuna riwaya isemayo kuwa mtu mmoja alimuuliza Mtume(s.a.w.w) : "Ni nani baba yangu?" Mtume akamwambia, "baba yako ni Fulani" Mwingine akauliza "Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Baba yangu yuko wapi? Mtume akajibu: "Yuko motoni," ndipo ikashuka Aya hiyo.

Riwaya nyingine inasema kuwa Mtume alisema: "Mwenyezi Mungu amewafaradhishia kuhiji, basi hijini." Wakauliza: "Kila mwaka ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?" Mtume akanyamaza. Wakarudia kuuliza, akasema La; lau ningelisema naam, ingelikuwa wajib." Ndipo ikashuku Aya hii. Riwaya hii ndiyo yenye nguvu kuliko ile ya kwanza.

Na mnapoyauliza inapoteremshwa Qur'an mtabainishiwa.

Yaani msijikalifishe kuuliza mambo ila baada ya kuteremshwa Qur'an. Mtakapoanza kuuliza Mtume(s.a.w.w) atawadhirishia mliyokuwa mkiyauliza.

Kwa hali hii, inatubainikia kuwa riwaya ya Hija ndiyo yenye nguvu katika sababu ya kushuka Aya, kuliko riwaya ya kuuliza mababa na wahenga wa Masahaba. Kwa sababu Qur'an inaanza kuleta itikadi na sharia na wala sio kuanzia kwa mababa na mababu wa Masahaba. Katika Hadith imeelezwa:"Hakika Mwenyezi Mungu ameweka mipaka msiikiuke; amewafaradhishia faradhi msizipoteze; ameharamishia vitu msivifanye; na ameacha vitu vingine si kwa kusahau, lakini ni kwa kuwahurumia, basi vikubalini wala msivifanyie utafiti".

Mwenyezi Mungu amesamehe hayo

Yaani maswali yenu yaliyotangulia, kwa hiyo msiyarudie. Imesemekana kuwa maana yake ni amezuia kutaja vitu mlivyoviulizia, basi nanyi jizuieni wala msijikalifu kuviulizia. Tafsir zote mbili zina uwezekano hazikataliwi na dhahiri ya tamko.

Na Mwenyezi Mungu ni mwingi wa maghufira, Mpole.

Humsamehe mkosaji akikosea tena.

Waliyauliza watu waliokuwa kabla yenu kisha wakawa makafiri kwayo.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kuwakataza kuuliza mambo wasiyokuwa na haja nayo, anawapigia mfano wa watu waliokuwa kabla yao, waliuliza wakang'ang'ania kuuliza. Walipobainishiwa na Mwenyezi Mungu walichukia wakaasi na wakastahiki adhabu. Lau wangeliacha kuuliza ingelikuwa bora kwao.

Wafasiri wamerefusha maneno katika kubainisha makusudio ya watu waliouliza, kisha wakawa makafiri kwa sababu ya kuuliza, lakini Aya haikubainisha. Pamoja na hivyo, tunaweza kusema kuwa watu waliouliza wakawa makafiri kwa sababu ya kuuliza ni wana wa Israil, kwa sababu ya kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu akiwasimulia:

﴿فَقَدْ سَأَلُوا مُوسَىٰ أَكْبَرَ مِن ذَٰلِكَ فَقَالُوا أَرِنَا اللَّـهَ جَهْرَةً ﴾

"Hakika walimtaka Musa makubwa kuliko hayo, Walisema: Tuonyeshe Mwenyezi Mungu waziwazi" (4:153)

﴿مَا جَعَلَ اللَّـهُ مِن بَحِيرَةٍ وَلَا سَائِبَةٍ وَلَا وَصِيلَةٍ وَلَا حَامٍ وَلَـٰكِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا يَفْتَرُونَ عَلَى اللَّـهِ الْكَذِبَ وَأَكْثَرُهُمْ لَا يَعْقِلُونَ﴾

103.Mwenyezi Mungu hakujaalia Bahira wala Saiba wala Waswila wala Hami; Lakini waliokufuru wanamzulia Mwenyezi Mungu uwongo na wengi wao hawafahamu.

﴿وَإِذَا قِيلَ لَهُمْ تَعَالَوْا إِلَىٰ مَا أَنزَلَ اللَّـهُ وَإِلَى الرَّسُولِ قَالُوا حَسْبُنَا مَا وَجَدْنَا عَلَيْهِ آبَاءَنَا أَوَلَوْ كَانَ آبَاؤُهُمْ لَا يَعْلَمُونَ شَيْئًا وَلَا يَهْتَدُونَ﴾

104.Wakiambiwa njooni katika yale aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu na kwa Mtume, husema: Yanatutosha yale tuliyowakuta nayo babu zetu. Je hata kama baba zao walikuwa hawajui kitu wala hawakuongoka?

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا عَلَيْكُمْ أَنفُسَكُمْ لَا يَضُرُّكُم مَّن ضَلَّ إِذَا اهْتَدَيْتُمْ إِلَى اللَّـهِ مَرْجِعُكُمْ جَمِيعًا فَيُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ﴾

105.Enyi mlioamini! Jiangalie nafsi zenu. Hawawadhuru waliopotea ikiwa mmeongoka. Marejeo yenu nyote ni kwa Mwenyezi Mungu. Atawaambia yale mliyokuwa mkiyatenda.

HAKUNA BAHIRAWALA SAIBA

Aya 103-105

MAANA

Mwenyezi Mungu hakujaalia Bahira wala Saiba wala Waswila wala Hami.

Bahira, ni ngamia aliyetobolewa masikio, watu wa wakati wa Jahilia walikuwa wakifanya hivyo, ikiwa ngamia atazaa mimba kumi ; na inasemekana ni mimba tano. Wanamwacha bila ya kutumiwa na mtu yoyote. Saiba ni ngamia waliyemwekea nadhiri kwa waungu, na wana mwacha akijilisha mwenyewe popote bila ya kufungwa wala kuwa na mchungaji sawa na Bahira.

Wasila ni mbuzi anayezaa mtoto wa kiume na wa kike pamoja. Desturi yao ilikuwa kama akizaa mume wanamfanya ni wa waungu na akizaa mke ni wao. Iwapo atazaa mume na mke pamoja, hawamchinji mume wakisema kuwa ameunganishwa na dada yake. Hami ni dume aliyezalisha mimba kumi, wanamwacha hazuiliwi na maji wala malisho, wakisema ameuhami mgongo wake.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anabainisha kwamba yote hayo hayamo katika dini, na kwamba dume, jike na mbuzi, vyovyote wanavyofanyiwa, wanabakia na uhalali wake kama walivyokuwa mwanzo na wala hawaharamishwi na porojo hizo.

Lakini waliokufuru wanamzulia Mwenyezi Mungu uwongo na wengi wao hawafahamu.

Watu wa kijahilia walikuwa wakikubali kuweko kwa muumba kwa dalili kwamba wao wamenasibishia uharamu wa Hami, Saiba, Bahira na Waswila, lakini pamoja na hayo Mwenyezi Mungu amewanasibishia ukafiri.

Kwa sababu wao wamemnasibishia uharamu kwa uwongo na uzushi. Kwa hiyo, basi kila anayemnasibishia Mwenyezi Mungu na yasiyokuwa na dalili ya Kitab wala Hadith ya Mtume wake basi huyo ni kafir kwa sharti ya kutegemea kumnasibishia Mungu, huku akijua kutokuwepo dalili.

Hii, kwa lugha ya watu wa sharia, huitwa Bid'a (uzushi). Kuna Hadithi isemayo: "Kila bid'a ni upotevu na kila upotevu ni motoni".

Ilivyo ni kuwa kufaradhia huko kuko mbali na hali halisi ilivyo, Ni nani anayemnasibishia hukumu Mwenyezi Mungu huku akijua kuwa hakuna dalili. Pengine anaweza akadhani ni dalili, lakini kumbe sio dalili.

Wakiambiwa njooni katika yale aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu na kwa Mtume, husema: "Yanatutosha yale tuliyowakuta nayo babu zetu. Je hata kama babu zao walikuwa hawajui kitu wala hawakuongoka?

Razi anasema: "Maana yanajulikana, nayo ni jibu la kuwapinga watu wa Taqlid (kufuata)". Tumezungumzia kuhusu Taqlid katika Juz.2 (2:170)

Enyi mlioamini! Jiangalieni nafsi zenu, Hawawadhuru waliopotea ikiwa mmeongoka, Marejeo yenu nyote ni kwa Mwenyezi Mungu.

Razi ametaja njia nane za kufasiri Aya hii. Mmoja wa wafasiri wapya ameandika kurasa 33. Lililowafanya wawili hawa na wengineo kurefusha mambo hivi ni kuwa kuamrisha mema ni wajibu na dhahiri ya Aya inafahamisha kutokuwa wajib na kwamba ni juu ya mtu kujishughulikia mwenyewe. Ama wengine wana majukumu yao juu ya nafsi zao wala si wajibu kwa yoyote kuiongoza au kuikanya nafsi ya mwingine.

Ilivyo tafsir ya Aya hii ni kwamba, ni juu ya mtu kuamrisha mema. Kuamrisha kwake kukinufaisha basi hayo ndiyo yanayotakikana. Vinginevyo basi atakuwa ametekeleza lile aliloamrishwa wala hautamdhuru upotevu wa aliyepotea.

Mwenye jukumu baada ya kuamrisha ni yule aliyepotea na wala sio mwamrishaji. Tafsir hii imetilia mkazo wajibu wa kuamrisha mema na sio kupinga.


4

5

6

7

8

9

10

11

12

13

14

15