FADHILA ZA SAYYIDNA ALI (A.S)

FADHILA ZA SAYYIDNA ALI (A.S) 0%

FADHILA ZA SAYYIDNA ALI (A.S) Mwandishi:
Kundi: Imam Ali (A.S)

  • Anza
  • Iliyopita
  • 5 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 12943 / Pakua: 2170
Kiwango Kiwango Kiwango
FADHILA ZA SAYYIDNA ALI (A.S)

FADHILA ZA SAYYIDNA ALI (A.S)

Mwandishi:
Swahili

1

FADHILA ZA SAYYIDNA ALI (A.S) FADHILA ZA SAYYIDNA ALI (A.S)

DIBAJI

BISMILLAHIR RAHMANIR RAHIM

Hii ni tafsiri ya kitabu kiitwacho

kilichoandikwa na Najumuddeen Sharif Al-Askari, wa Najaf, Iraq. Katika kitabu hicho mno hadithi 77 za Mtukufu Mtume Muhammad (S.A.W.W.) ambazo zimepangwa katika mada 50 kuhusu fadhila, ustahili na sifa za Sayyidina Ali bin Abi Talib (A.S.). Mabwana Ahmad bin Hanbal, Ismail bin Ishaq Al-Kadhi, Ahmad bin ali bin Shuaib-An-Nasai, na Abu Ali An-Neshapuri wanatamka kuwa haukupokewa utukufu na ubora wa Sahaba yeyote kwa hadithi sahihi na sanadi madhubuti, kama ulivyopokelewa utukufu na ubora wa Ali bin Abi Talib (A.S.).

Hadithi zote zilizotajwa katika kitabu hiki zimepokewa na Masahaba mashuhuri kama Bw. Abu Bakr, Bw. Umar bin Khattab, bw. Uthman bin Affan, na Bw. Jabir bin Abdullah, Bibi Aisha, na Bw. Abdullah bin Umar (R.A.). Mtungaji ameyataja majina ya vitabu pamoja na Juzu na ukurasa zilimopatikana hadithi hizo. Wal-hamdu Lillahi Awwalan Wa Akhiran wa Swallal-llahu Ala Muhammadin wa Alihit-Taahireen. Al-Ahkar S. Muhammad Mahdi Al-Muusawy.

HADITHI YA KWANZA

"Hakuna atakayepita Sirati ila tu yule mwenye kuidhiniwa na Ali kupita." Ibn Hajar Al-Haitami Ash-Shafiiy katika kitabu chake cha As-Sawaaiqul-Muhriqa (uk. 78/97) ameeleza hadithi kutoka kwa Ibnu-Saman kuwa Abi Bakr amesema, "Nimemsikia Mtume (S.A.W.W.) akisema, 'Hakuna atakayepita Sirati (njia ya kuendea Peponi) ila tu yule aliyeidhiniwa na Ali kupita'".

Vile vile katika kitabu cha Sunan Addarqutni imeelezwa hadithi inayosema hivi: Ali aliwauziza wale watu sita waliowekwa na Umar kushauriana mambo ya Ukhalifa kama kuna anayeweza kuapa kwa jina la Mwenyezi Mungu kama kuna yeyote miongoni mwao aliyeambiwa na Mtume (S.A.W.W.) maneno haya, "Ewe Ali, wewe ndiye mgawaji wa Pepo na Moto siku ya Qiyama". Kama si mimi basi ni nani?' Wakasema, "Bila shaka ni wewe tu". Maneno hayo yanatokana na hadithi iliyoelezwa na Antara ambaye aliipokea kutoka kwa Ali al-Ridha ambaye amepokea kutoka kwa baba zake kwamba Mtume (S.A.W.W.) amesema, "Ewe Ali hakika wewe ni mgawaji wa Pepo na Moto. Siku ya Qiyama, utauambia moto: 'Huyu wangu na huyu wako'".

Na katika kitabu cha Manaqib cha Khowarazmi imetajwa hadithi ya Antara kuwa Mtume (S.A.W.W.) amesema, "Ewe Ali hakika wewe ni mgawaji wa Pepo na Moto na wewe ndiye utakayengoja mlango wa Pepo na kuingia ndani bila ya hisabu". 1 Katika kitabu cha Dhakhairul Uqba cha Tabari Assh-afii imeelezwa hadithi ya kumsifu Ali (A.S.) kuwa kwa hakika hapiti yeyote katika sirati ila yule aliyeidhiniwa na Ali kupita.2

Imepokewa hadithi kutoka kwa Qais bin Hatim ya kwamba walikutana mabwana Abu Bakr na Ali bin Abi Talib (A.S.). Abu Bakr akafurahi kumwona Ali (A.S.) na Ali akamwuliza amefurahia nini? Abu Bakr akamjibu, "Nimemsikia Mtume (S.A.W.W.) akisema: Hapiti yeyote katika sirati ila yule aliyedhiniwa na Ali kupita". Pia amesema kuwa amenakili hadithi Ibnu Saman katika kitabu Al-Muwafaqh na katika Manaqib cha Khowarazmi. 3 Na vile vile katika kitabu chake maarufu kiitwacho Maqtalul Husein 4 hadithi hiyo ilipokewa kutoka kwa Hasan Al-Basary ambaye alipokea kutoka kwa Abdallah, kuwa amesema Mtume (S.A.W.W.): "Siku ya Qiyama Ali bin Talib atakaa juu ya Firdausi (mlima ulio juu ya Pepo), na juu yake kuna Arshi ya Mola wa viumbe, na pembezoni mwa jabali yateremka mito ya Peponi na yatawanyika katika Pepo mbali mbali na yeye (Ali) amekaa katika kiti cha nuru, na mito yapita mbele yake iitwayo At-Tasneem, basi hapiti yeyote katika sirati ila awe nayo hati ya utii kwake na Ahli-Baiti zake. Ataangalia Ali, atamtia ampendaye Peponi, na amchukiaye Motoni."

Ibrahim Bin Muhammad Al-Hamwini Ash-Shafii katika Faraidus-Simtain 5 na Muhib At-Tabari katika Riyadhun-Nudhra 6 pia wameeleza hadithi hiyo. Kadhalika Hakim katika Al-Arbaeen pia amepokea hadithi hiyo. Ibn Abi Adsa katika historia amepokea hadithi hii hivi: Abu Bakr alimwambia Ali, "Nimemsikia Mtume (S.A.W.W.) akisema kuwa yeyote hapiti katika sirati ila tu yule aliyeruhusiwa na Ali kupita". Sulaiman Al-Hanifi katika kitabu chake cha Yana bee-ul-Mawad-dah 7, Ibnul Maghazili Shafii katika Manaa-qib na Ghaaya-tul Maraam na katika Tareekh cha Al-Katibul Baghdadiy 8, hadithi hiyo imesimuliwa kutokana na Ibnu Abbas. Vile vile Qadhi Ayadh ameeleza katika kitabu chake cha Shifaa, Allama Sayed Abu Bakr Shahabud-Deen Shafii katika kitabu chake cha Rash-fatus-Saa-di Min Buhuur, Fadhaail Bani Al-Hadi 9, Qarashi katika Shamsul Akbaar 10, Sheikh Abdallah Shabrawi Shafii katika Al-Ithnaaf Bihub-bil-Ashraaf 11 na katika Is-Afur-Raghibeen 12 Basi hadithi hiyo wamehadithia kikundi kikubwa cha Masahaba licha ya Abu Bakr, Ibn Abbas. Ibn Masood na Anas bin Malik.

HADITHI YA PILI

"Kuangalia Uso wa Ali ni Ibada"

Ibnu Hajar, katika kitabu chake kiitwacho Ass-Sawaiq, (uk. 108) ameeleza kwamba, "Abu Bakr (R.A.) alikuwa akimwangalia sana usoni Ali. Aisha akamwuliza sababu yake, naye akajibu, "Nimesikia Mtukufu Mtume (S.A.W.W.) akisema kuwa kuangalia uso wa Ali ni Ibada".

Hadithi hii imeelezwa na Muhib-buddeen Attabari Ash-Shafii katika kitabu chake Ar-Riyaadhun-Nadhra (J. 2, uk. 244), na Ibn Katheer katika "Al-Bidaya Wan-Nihaya (J. 7, uk. 357) kutokana na Mabwana Abu Bakr, Umari, Uthman bin Affani, Abdalla bin Masoodi, Maadhi bin Jabal, Imraan bin Haseen, Anas, Thubani, Aisha, Abidhar na Jabir. (Tena akaendelea kusema) na katika hadithi aliopokea Aisha inasema hivi: "Kumdhukuru Ali ni Ibada". Muhib-buddeen Attabari amesema katika kitabu chake Dhakhairul Uqba (Uk. 95) kuwa hadithi hii ameipata kutoka kwa kikundi cha Masahaba na kutoka kwa Ibnu Mas'udi, na Amru bin Asi, na Jabir, na Abu Hurayrah, na Aisha. Hadithi alioipokea Aisha imo katika kitabu cha Al-Muwaafaqa cha Ibnu Samran aliyoipokea Ibnu Mas'udi imeelezwa na Abul Hasan Al-Hirbi, aliyoipokea Amrul Asi imenakiliwa na Al-Ab-hari na aliyoipokea Jabir na Imran bin Haseeni, na Maadhi, na Abu-Hurayrah ameeleza Ibnu Abil-Furati.

Al-Kanji Ash-Shafii aliyefariki dunia mwaka 658 A.H., katika kitabu chake 'Kifaa-yatut-taalib (Uk. 67) amesema hivi, 'Abudhar anasimulia kwamba Mtume (S.A.W.W.) amesema, "Mfano wa Ali miongoni mwenu au amesema miongoni mwa Umma huu ni mithili ya Kaaba ilivyovikwa, kuiangalia ni Ibada na kuiendea kuhiji ni fardhi". Ameongezea kuwa Hadithi hii inayotokana na Abudhar na kupokewa kutoka kwa Abu Alman Al-Khitabi. Jalaa-lud-deen Assuyooti Ash-Shafii (aliyezaliwa katika mwaka 849 A.H., na kufariki dunia mwaka 911 (A.H.) katika kitabu chake "Taareekhul-Khulafaa (J.1, Uk. 9) pia ameitaja.

Vile vile hadithi hii ameitaja Ibnu Asaa-Kir kutokana na Abu Bakr, Uthmani bin Affani, Maadhi bin Jabali, Anas, Thobani, Jabir bin Abdillah na Aisha Al-Khowarazmi Al-Hanafi katika kitabu chake Al-Manaa-quib (Uk. 251) amesema aliipokea hadithi hii kutoka kwa Imraan bin Haseen nayo inaeleza hivi: "Kumwangalia Ali ni Ibada". Na Ibnu Asakir amepokea hadithi hiyo kwa njia ishirini na moja, baadhi yake zinahitilafiana maneno, baadhi ya maelezo yanasema hivi: Mtume (S.A.W.W.) amesema, "Kuangalia uso wa Ali ni Ibada". Na zingine zaeleza hivi: Mtume (S.A.W.W.) amesema, "Kumwangalia Ali ni Ibada", na zingine zaeleza hivi: Mtume (S.A.W.W.) amesema, "Kuangalia uso wa Ali ni Ibada". Na zingine zaeleza hivi: Mtume (S.A.W.W.) amesema, "Kumdhukuru Ali ni Ibada". Hii ya mwisho imepokewa na Bi Aisha kutoka kwa Mtukufu Mtume (S.A.W.W.).

Al-Muwaf-faq bin Ahmad Al-Hanafii, katika kitabu chake Al-Manaa-qulb (Uk. 251), ametaja hadithi kutokana na Imran bin Haseen kuwa "Nimemsikia Mtume (S.A.W.W.) akisema: "Kumuangalia Ali ni Ibada". Sheikh Kanduzi Al-Hanafii ametaja hadithi moja katika kitabu chake "Yanaa-bee-ul Mawad-dah (Uk. 254) kwa kunakili kutoka kitabu cha Mawad-datul Qurba cha Sayed Al Alo-Hamdani Ash-Shafii, kuwa Abdudhari amesema, Mtume (S.A.W.W.) alisema, "Ali ni mlango wa elimu yangu na mfafanuzi wa umma wangu baada yangu kwa yale niliyojia kutoka kwa Mwenyezi Mungu, basi kumpenda yeye (Ali) ni Imani, na kumbughudhi ni unafiki". Vile vile akaendelea kusema kuwa hadithi hii ameeleza Abu Naeem na ameinakili katika Uk. 235 kama ilivyopokelewa na Abi Dar-da ambaye amesema kuwa Mtume (S.A.W.W.) alitamka, "Ali ni mlango wa elimu yangu na mfafanuzi wa umma wagu baada yangu kwa yale niliyojia kutoka kwa Mola, basi kumpenda Ali ni Imani na kumbughudhi ni unafiki, na kumwangalia ni rehema na kumpenda ni Ibada."

Hadithi hii pia imo katika kitabu cha Firdausul-Akhbaar, cha Al-Daylami na al-Hamwini Ash-Shafii Ibrahim bin Muhammad aliyefariki dunia mwaka 772 (A.H.) ameinakili katika "Faraidu-Simtain", Al-Qanduzi Al-Hanafii katika Uk. 90 "Yanaabee-ul-Mawad-dah" amesema kwamba Ibnu Maghazili Ash-Shafii amenakili hadithi hiyo katika "Al-Manaa-quib" kutokana na Imrani bin Haseen na Waathila bin Al-Askari na Abu-Hurayrah. Maelezo ni kuwa "Mtume (S.A.W.W.) amesema, "Kumwangalia uso wa Ali ni Ibada", Hadithi hii Ibrahim bin Muhammad al Hamwini Ash-Shafii pia ameeleza katika kitabu chake Faraidus-Simtain, kutokana na sahaba Abu Saeed Al-Khudri na Al-Muwaffaq bin Ahmad Alhanafii katika "Manaaquib" Uk. 8 Al-Kanji As-Shafii katika Kifaayatut-Taalib Uk.

124 ameeleza hadithi ndefu ndani yake akieleza sifa nyingi za Ali. Miongoni mwao ni hadithi hiyo. Basi sasa tunataja maneno ya hadithi aliyonakili Al-Kanji kutoka kwa Jaffer bin Muhammad As-Saadiq (A.S.) ambaye amepokea kutoka kwa babu yake Ali bin Hussein naye ameipata kutoka kwa baba yake, Husain bin Ali, kutokana na baba yake Ameerul-Mumineen Ali (A.S.) kwamba Mtume (S.A.W.W.) amesema. "Hakika Mwenyezi Mungu amemjalia ndugu yangu Ali bin Abi Talib sifa nyingi ambazo hazidhibitiki kwa wingi wake. Atakayetaja sifa moja tu katika sifa zake anuwai na kuikiri Mwenyezi Mungu atamsamehe madhambi aliyoyatanguliza na yatakayokuja, na atakayeandika sifa yake moja katika sifa zake nyingi hawataacha malaika kumwombea maghfira muda wote maandishi hayo yatadumu na atakayesikiliza sifa moja katika sifa zake hizo Mwenyezi Mungu atamfutia dhambi zake kwa baraka ya kusikiliza, na atakayeangalia kitabu (kilichoandikwa) sifa zake Mwenyezi Mungu atamfutia madhambi yake kwa kuangalia hicho kitabu. Kisha Mtume akasema, "Kumwangalia ndugu yangu Ali ni ibada na kumtaja ni ibada. Mwenyezi Mungu haikubali imani ya mja, ila tu ya yule aliye chini ya uongozi wake (Ali) na ambaye ametengana na maadui zake."

Kwa vile katika vitabu vya hadithi inadhihirika kuwa waliosimulia na kupokea hadithi hiyo ni Masahaba wakubwa kumi na nane ambao wametajwa majina yao katika hadithi iliyotangulia, basi fikiri vema ili upate faida yake.

HADITHI YA TATU

"Ali kwangu mie kama vile ilivyo daraja yangu kwa Mola wangu". Ibn Abbas amehadithia kuwa siku ya sita baada ya kutawafu kwa Mtume Muhammad (S.A.W.W.), Ali na Abu Bakr walikwenda kuzuru kaburi la Mtume. Ali akamwambia Abu Bakr atangulie kuingia katika chumba alimozikwa Mtume (S.A.W.W.). Abu Bakr akasema kuwa asingeweza kumtangulia yule ambaye amesikia Mtume akimsifia kuwa ni mtu ambaye "Daraja ya Ali kwangu miye ni sawa a mimi nilivyo kwa Mola wangu". 13 Kadhalika kuna hadithi nyingi zilizopokewa na Abu Bakr zinazokariri utukufu wa Ali na kuonesha hadhi ya Ali. 14

HADITHI YA NNE

"Kwa hakika Ali ni mwingi wa huruma na upole"

Shaabi anaeleza kuwa safari moja Abu Bakr alimwona Ali akija mbele yake. Abu Bakr akatamka kuwa yeyote apendaye kufurahi kumwona mtu aliye karibu sana na Mtume (S.A.W.W.) aliye na daraja kubwa, aliyetaabika sana kwa ajili ya dini ya Mwenyezi Mungu na aliye bora mbele ya Mtume kuliko yeyote mwingine, basi anapaswa kumwangalia Ali ibn Abi Talib." Akaendelea kusema kuwa amemsikia Mtume (S.A.W.W.) akisema: "Kwa hakika Ali ni mwingi wa huruma na upole".

HADITHI YA TANO

"Ewe Abu Bakr! Gao langu na gao la Ali ni sawa".

Habashi Bin Junaadah anasimulia kuwa siku moja alikuwa amekaa mbele ya Abu Bakr. Basi akamsikia Abu Bakr akisema "yeyote yule aliyeahidiwa chochote na Mtume (S.A.W.W.) asimame." Mtu mmoja akasimama na kusema "Mtume (S.A.W.W.) aliniahidi kunipa magao matatu ya tende. Naomba nipimiwe." Abu Bakr akamwitisha Ali na kumweleza madai ya mtu yule. Ali akampimia tende na kisha akaamrisha tende zihisabiwe. Ikaonekana kuwa katika kila gao mlikuwa tende sitini bila kuzidi au kupungua. Hapo Abu Bakr akatamka "Mwenyezi Mungu na Mitume wake wamesema kweli. Usiku ule wa Hijra tulipokuwa tunatoka pangoni na kuelekea Madina Mtume akaniambia "Ewe Abu Bakr, gao langu na gao la Ali ni sawa katika hesabu".

HADITHI YA SITA

"Ewe Abu Huraira! Hujui kuwa mkono wangu na mkono wa Ali ni sawa katika Uadilifu?" Omar Ibn Al-Khattab amesema kuwa yeye alielezwa na Abu Bakr kwamba Abu Hureira alikwenda kwa Mtume (S.A.W.W.) na akakuta gao la tende mbele yake. Akamtolea salamu Mtume (S.A.W.W.) ambaye akamjibu na kumpa gao moja la tende. Alipohisabu akakuta tende 43. Baadaye akaenda kwa Ali Ibn Abi Talib ambaye pia akampa tende na alipozihisabu aliona kuwa idadi ilikuwa ile ile.

Jambo hilo likamshangaza sana. Akarejea kwa Mtume (S.A.W.W.) na kumweleza yale yaliyotokea. Mtume (S.A.W.W.) akatabasamu na kusema kuwa, "Ewe Abu Hureira hujui kuwa mkono wangu na mkono wa Ali ni sawa katika uadilifu?" 15

HADITHI YA SABA

"Mtume na Ahlul Kisaa"

Zaidi Ibn Yathee amekariri kuwa amemsikia Abu Bakr akisema kuwa alimwona Mtume (S.A.W.W.) amekaa katika hema akiegemea upinde wa Kiarabu. Pamoja naye walikuwa Seyyidna Ali (A.S.), Seyyidati Fatima (A.S.) Seyyidna Hassan na Seyyidna Hussein (A.S.). Mtume (S.A.W.W.) akatamka, "Enyi Waislamu, mimi nina amani na wale wanaokaa na amani na watu walio katika hema hili na ninapigana na wale wanaopigana nao. Pia ninawapenda wale wanaowapenda na nina uadui na wale wenye uadui nao. (Kadhalika) ni mtu yule tu aliye mwema na mwenye hadhi na aliyezaliwa kwa wema ndiye atakayewapenda hao na ni yule tu mwenye kizazi kibaya ndiye atakayewabughudhi hao."

Mtu mmoja akamwuliza Zaid, "Ewe Zaid, ulimsikia Abu Bakr akisema hivyo?" Akajibu kuwa "Naapa kwa jina la Mola wa Kaaba (kuwa nimesikia)". Hadithi hii ni mashuhuri kwa jina la HADITHUL-KISAA. Hadithi hiyo imepokewa kwa njia mbalimbali kutoka kwa wanazuoni wengi wa Kishaafy, Hanafy na wengineo.

HADITHI YA NANE

"Sifa pekee za Ali"

Imepokewa hadithi kutoka kwa Jabir bin Abdillah kuwa Umar amesema; "Masahaba wa Mtume wanazo sifa kumi na nane (18), ambazo kumi na tatu (13) katika hizo ni mahsusi kwa Ali, na tano tu ndizo tumeshirikiana naye kuwa nazo." 16

HADITHI YA TISA

Zimepokewa hadithi nyingi ambazo zinamhusu Ali kuwa daraja yake kwa Mtume (S.A.W.W.) ni kama daraja ya Haruni kwa Musa. Umar aliwahi kumsikia mtu mmoja akisema Ali. Basi Umar akamwambia mtu yule kuwa amekuwa miongoni mwa wanafiki kwa sababu alimsikia Mtume (S.A.W.W.) akimwambia Ali kuwa Ali kwake alikuwa mfano wa Harun kwa Musa ila tu utume ulimalizika baada yake.17

Mtungaji ameandika kuwa vitabu vingi vimetungwa juu ya hadithi hiyo (k.v.) Seyyid Meer Hamid Hussein Al-Hindy (R.A.) ametunga kitabu kikubwa cha hadithi zinazothibitisha wasia za Mtume kuhusu uongozi na ukhalifa baada yake.

HADITHI YA KUMI

Kumepokewa hadithi kutoka kwa Umar bin Khattab ambaye amesema "Nimemsikia Mtume (S.A.W.W.) akieleza sifa tatu za Ali ambazo miye ningetamani kuwa na walau moja kati ya hizo. Wakati wa kueleza hadithi hiyo tulikuwepo mimi, Abu Ubaida, Abu Bakari na kikundi cha Masahaba wa Mtume (S.A.W.W.). Mara Mtume (S.A.W.W.) akampiga Ali begani na akatamka: 'Ewe Ali, wewe ndiye wa kwanza katika walioamini na mwanzo katika waliosilimu na kwangu miye daraja yako mithili ya Harun kwa Musa."

Mtungaji amesema kwamba hadithi hiyo imetolewa na Kundi kubwa la wanazuoni wa Ki-Sunni, wa Ki-Hanafi na Shafii. Na katika 'Dhakaairul Uqba' cha Muhibudin Attabari Ashshafii (Uk. 58) chini ya maudhui ya "kuwa yeye (Ali A.S.) ndiye wa mwanzo miongoni mwa waliosilimu". Hadithi iliyopokewa kutoka kwa Umar (R.A.) imesema, "Mimi nilikuwa na Abu Ubaida na Abu Bakar, na watu wengi, alipopiga Mtume (S.A.W.W.) bega ya Ali bin Abi Talib na akasema, "Ewe Ali, wewe ndiye wa mwanzo wa kuamini kati ya walioamini. Na ni wa mwanzo wa kusilimu kati ya waliosilimu, na wewe daraja yako kwangu ni kama daraja ya Harun kwa Musa."

Pia Hadithi hiyo imeandikwa na Al-Khateeb Al-Muwaffak Ahmad Al-Hanafii, katika 'Manaqib' (Uk. 32), na Ibnu Kha'llikan katika 'Wafayatul Aayan' (J. 2, Uk. 104). Ali Al-Muttaqui Al-Hanafi katika 'Kanzul-Ummal' (J. 6, uk. 395) amenakili hadithi hiyo kutoka vitabu vingi kama vile Tareekh Baghad cha Ibnu Najjar, Al-Kuna' cha Hakim, na kitabu cha Hasan bin Badri, ambacho kimekusanya hadithi zilizopokewa na Makhalifa.

2

FADHILA ZA SAYYIDNA ALI (A.S)

HADITHI YA KUMI NA MOJA

"Imani ya Ali ni kubwa zaidi kuliko kitanga cha wakaazi wa mbingu na "Imenakiliwa katika Dhakhairul-Uqba (Uk. 100) hadithi kuwa Umar bin Khattab amesema: 'Nashuhudilia kwa Mtume (S.A.W.W.) kuwa bila shaka nimemsikia akisema: "Lau mbingu saba na ardhi saba zingewekwa katika kitanga kimoja (mizani) na ikawekwa imani ya Ali katika kitanga (mizani) cha pili, ingezidi (uzito) imani ya Ali". Hadithi hiyo imenakiliwa na Ibnu Saman katika Al-Muwafaka, Al-Hafidh As-Salafi katika Al-Mashikhatul baghadadiyah, na Al-Muhibbu Attabari As-Shafii katika kitabu chake "Ar-Riyaadhun Nadhra (J. 2, Uk. 226) na maneno ya hadithi hiyo katika vitabu hivyo viwili hayatafautiani.

Hadithi hii imenakiliwa na kundi la wanazuoni wa ki-Sunni, Shafii, Hanafi na wengine, kati yao ni Sheikh Suleman Al-Kunduzi katika "Yanabiul Mawadah" (Uk. 254) ambaye amesema, "Imepokewa hadithi kutoka kwa Ubaidullah Juwayshfa bin Murra Al-Iry kutoka kwa babu yake kuwa watu wawili walimwendea Umar bin Khattab na kumwuliza kuhusu Talaka ya mjakazi (ngapi?). Alikwenda nao katika mahala watu wamekaa duwara, katika duara hiyo alikuwa mtu mmoja kipara, Umar akasema, ewe mwenye upara unaonaje katika Talaka za mjakazi? Basi akaashiria (yule kipara) kwa kidole cha chanda na cha kati. Ibnul Khattabi akasema Talaka ni mbili. Kisha akawaambia: 'Huyu ni Ali bin Abi Talib".

Nimeshuhudia kuwa kwa hakika mimi nimemsikia Mtume (S.A.W.W.) akisema "Lau imani ya wakaazi wa mbingu saba na ardhi saba ikiwekwa katika kitanga kimoja cha mizani) na ikawekwa imani ya Ali katika kitanga (mizani) cha pili ingezidi (uzito) imani ya Ali Ibnu Abi Talib".

Hadithi hiyo imenakiliwa na Sayed Ali Hamadany Ash-Shafii katika Al-Mawaddah. Katika Mawaddah ya saba. Miongoni mwa walionakili hadithi hii pia ni Al-Khateeb Al-Muwaffak bin Ahmad Al-Khowarazmi Al-Hanafi katika "Al-Manaqib" (Uk. 78). Amesema kuwa hadithi hii imetoka kwa Sabrah kutoka kwa baba yake ambaye ameipata kutoka kwa babu yake nayo ni kuwa "watu wawili walimwendea Umar wakamuuliza nini hukumu ya Talaka ya mjakazi? Akaenda nao kwa kikundi cha watu waliokaa duara, ndani mwao, alikuwepo mtu mwenye kipara. Umar akamuuliza unasemaje katika hukumu ya Talaka ya mjakazi (ngapi?) Akajibu kwa ishara ya vidole vyake kuwa ni mbili. Hapo Umar akageuka na kuwaambia Talaka ni mbili. Mmoja ya wale wawili akasema, sisi tumekuja kwako na wewe ndio Khalifa tukauliza. Naapa kwa Mwenyezi Mungu kwamba (Ali) hakukusemeza (ila kwa ishara tu). Umar akamwambia, ole wako! Unamjua huyu ni nani? Huyu ni Ali bin Abi Talib. Mimi kwa hakika nimemsikia Mtume (S.A.W.W.) akisema, "Lau mbingu saba na ardhi saba zingaliwekwa katika kitanga cha mizani na ikapimwa imani ya Ali, uzito wa Imani ya Ali ungezidi uzito wa imani ya mbingu na ardhi."

Hadithi hii pia imeelezwa kutoka kwa Muskala Al-Abdi kutoka kwa baba yake ambaye ameipata kwa baba yake kuwa Umar bin Khattab amesema; "Ninathibitisha jina la Mtume (S.A.W.W.) kuwa nimemsikia akisema: "Lau zingewekwa mbingu sababu na ardhi saba katika kitanga (kimoja) cha mizani, na ikawekwa imani ya Ali bin Abi Talib katika kitanga cha (pili) cha mizani, ingezidi imani ya Ali." Kwa ufupi ninataja majina ya wapokezi wa hadithi hiyo na vitabu vyao: (a) Ali Al-Muttaki katika "Kanzul Ummali" (J. 6, Uk. 156) ambaye amenakili kutoka "Firdausul Akhbar" cha Daylami kutoka kwa Ibnu Umar si Umar. (b) Al-Kanji katika "Kifaytul Talib" (Uk. 129). (c) Al-Jawhari katika "Fadhailu Ali" (d) Muhaddithi wa Shaam katika Tareekh yake katika mlango kuhusu wasifu wa Ali (A.S.).

Tumeikuta hadithi hiyo katika kitabu cha Tareekh cha Ibnu Asakir (Uk. 88) katika juzu ambayo ni mahsusi kuhusu Ameerul Mumineen Ali bin Abi Talib (A.S.) na nakala yake ipo katika Maktaba ya Al-Imam Ameerul Muumineen katika mji wa An-Najaful Ash-raf, (e) As-Safuri Ash-Shafii aliyofariki mwaka 658 A.H. katika kitabu chake kiitwacho "Nuzhatul Majalis" (J.2, Uk. 240) kilipigwa chapa Misri mwaka 1320 A.H.

HADITHI YA KUMI NA MBILI

"Sifa pekee tatu za Ali"

Katika "Manaaqib" cha Al-Khateeb Al-Muwwafak bin Ahmed Al-Khowarazmi Al-Hanafii (Uk. 232) imenakiliwa hadithi kutokana na Umar bin Khattab kuwa amesema: "Hakika amepewa Ali bin Abi Talib mambo matatu ambayo kwayo natamani walau ningalikuwa nalo mojawapo ingekuwa bora kwangu kuliko kupewa ngamia wekundu. Akaulizwa ni yepi hayo? Akasema, "Kuozwa mtoto wa Mtume (S.A.W.W.) (Mwana Fatma); kukaa msikitini pamoja na Mtume (S.A.W.W.) kuwa na ruhusa kuwapo kwake msikitini kama ilivyo halalishiwa Mtume (S.A.W.W.), yaani, kuweko msikitini katika hali ya (janaba); na kupewa bendera siku ya (vita) ya Khaibar.

Hadithi hii imenakiliwa na kikundi kikubwa cha wanazuoni wa ki-Sunni, Hanafi, Shafii na wengine. Miongoni mwao ni Ubaidullah Amritsari Al-Hanafi katika kitabu chake Arjahu Mataalib. Jalalud-Deen Syooti, Ash-Shafii, katika kitabu chake Tareekhul Khulafaa (J. 1., Uk. 66) amesema hivi: 'Abu Huraira amesema kuwa Umar bin Khattabi ametamka ya kuwa; "Hakika amepewa Ali mambo matatu. Natamani ningalikuwa nalo moja tu katika hayo, ingekuwa bora kwangu kuliko kupewa ngamia wekundu." Aliulizwa ni yepi? Akasema: Kuozwa Fatma mtoto wa Mtume Muhammad (S.A.W.W.); kukaa msikitini pamoja na Mtume (S.A.W.W.) na kuhalalishiwa yeye (humo) alichohalalishiwa Mtume (S.A.W.W.); na kupewa kwake bendera siku ya Khaybar." Na miongoni mwao ni Al-Hakim Ash-Shafii katika Mustadrak-us-Sahiehain (J.3, Uk. 125) kutokana na Abu-Hurayra.

Maneno ya hadithi aliyopokea yeye na aliyoipokea Suyooti ni sawa, na ameongezea kusema kuwa "Hadithi hii ni yenye sanadi sahihi, lakini Bukhari na Muslim hawakuitaja." Vile vile hadithi hii imetajwa na Ibunu Hajar Al-Haytami Ash-Shafii katika As-Sawaiq (Uk. 78) na maneno yake na ya Suyooti ni sawa. Kadhalika, Ahmad bin Hambal kwa sanadi iliyo sahihi kutokana na Ibnu Umar na Ibnu Katheer Ad-Damashki katika kitabu chake Al-Bidaya-wannihaya (J. 6, Uk. 341) inayotokana na Umar wameinakili hiyo hadithi. Ali Al-Muttaki Al-Hanafi katika Kanzul-Ummal (J.6, Uk. 393) katika hadithi nambari 6013 iliyotokana na Musnad Ibnu Abi-Shaiba, ambayo maneno yake yanafanana na ya Khowarazmi. Na pia katika hadithi nambari 6014 na 6015. Mfano uliotolewa na Umar wa ngamia wekundu una maana ya kuwa zamani hizo ngamia kama hao walihisabika kuwa ni mali bora kabisa kwa Waarabu.

HADITHI YA KUMI NA TATU

"Kumpenda Ali ni kumpenda Mtume"

Imesimuliwa hadithi kutoka kwa Ibnu Abbas kuwa Umar bina Khattab alikuwa akisema, "Jizuieni na kumtaja (kwa ubaya) Ali bin Abi Talib; hakika mambo mengi nimeyaona kwake kutoka kwa Mtume natamani ningalikuwa nalo moja tu katika ukoo wa Al-Khattab ingekuwa bora kwangu kuliko kuvipata vitu vyote vinavyopata mwangaza wa jua. Nilikuwa mimi na Abu Bakr na Abu Ubaida pamoja na baadhi ya masahaba wa Mtume, tukaenda mpaka mlangoni kwa Ummu Salama, Ali alikuwa amesimama mlangoni, tukamwambia tunamtaka Mtume (S.A.W.W.). Akasema anakuja. Akatoka Mtume (S.A.W.W.) tukaenda kwake.

Mtume akamwegemea Ali bin Abi Talib, kisha akampiga begani (Ali) na kusema, "Wewe ni wa kwanza kuamini miongoni mwa walioamini, mwenye maarifa ya Neema za Mwenyezi Mungu, mwenye kutekeleza ahadi za Mungu, mwadilifu katika ugawaji, mpole mno kwa raia, mbora wao mno katika kuvumilia taabu, msaidizi wangu, utakayeniosha, utakayenizika, utakayetangulia katika mambo yote ya shida (magumu) na machungu, hutarudia ukafiri baada yangu, wewe utakuwa mbele yangu na umeshika mikononi 'Liwaul-Hamad', utawafukuza watu (wasiokupenda) kwenye hodhi (Kauthar) yangu". Kisha Ibnu Abbas akasema, "Hakika Ali amefuzu kwa kuwa ni mkwe wa Mtume (S.A.W.W.) na kuwa mbora katika jamaa (Ahli-Baiti) na mkarimu wa kusaidia katika jambo lolote la kheri, mjuzi wa Tanzeel (Qurani), mjuzi wa Taaweel (Mafafanuzi) ya Qurani, mwenye kuwapita na kuwashinda mashiyaa".

Zimepokewa hadithi nyingi zenye kueleza maudhui ya hadithi hii, zilizo pamoja na zilizo mbalimbali. Hadithi hiyo hiyo ameinakili Ali Al-Muttaqi Alhanafi katika kitabu cha "Kanzul-Ummal". 18 Yamo maongezeko katika maneno ambayo hayajanakiliwa mahala pengine isipokuwa hapa.

Katika Musnad ya Umar bin Khattab kutoka kwa Ibnu Abbas imeelezwa kuwa Umar bin Khattab amesema, "Jizuieni kumtaja Ali (kwa ubaya) kwani mimi nimemsikia Mtume (S.A.W.W.) akieleza sifa tatu za Ali; na mimi natamani zaidi kuwa na walau moja katika hayo kuliko kuvipata vitu vyote vinavyopata mwangaza wa jua. Mimi nalikuwa na Ab u bakr, Abu Ubaida na kundi la Masahaba wa Mtume (S.A.W.W.) na Mtume alimuegemea Ali bin Abi Talib, mpaka akampiga bega la Ali kwa mkono wake na kisha kusema: 'Ali wewe ni wa kwanza kuamini katika walioamini na ni wa kwanza katika kusilimu, wewe daraja yako kwangu kama daraja ya Harun kwa Musa. Mwenye kudai kuwa ananipenda miye na huku anakuchukia wewe ni mrongo."

HADITHI YA KUMI NA NNE

"Ubora wa Ali hauwezi kupimika"

Imepokewa hadithi kutoka kwa Umar Bin Khattab ambaye amesema kuwa Mtume (S.A.W.W.) amesema: "Lau bahari ingekuwa wino, miti kalamu, binadamu waandishi na majini wahasibu, wasingeweza kuuhesabu ubora wako, ewe Abal Hasan" 19 (yaani Ali).

HADITHI YA KUMI NA TANO

"Ali ni kiongozi wa kila aliyemkubali Mtume kuwa ni Kiongozi wake." Imepokewa hadithi hii kutoka kwa Umar bin Khatttab kwamba Mtume (S.A.W.W.) alimfanya Ali kuwa kiongozi na akasema; "Yeyote mimi nikiwa kiongozi wake basi Ali pia ni kiongozi wake. Ewe Mola! Mpende anayempenda Ali, umfanyie uadui anayemfanyia uadui Ali, mwache anayemwacha (kumsaidia) Ali, mnusuru anayemnusuru Ali. Ewe Mola! Wewe ndiye shahidi juu yao. Umar Bin Khattab akasema, "Ewe Mola! Wewe ndiye shahidi juu yao.

Umar Bin Khattab akasema, "Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu (wakati ule ulipokuwa ukituhutubia) kulikuwa mtu mmoja ubavuni kwangu kijana mwenye uso mzuri ananukia vizuri, akaniambia Ewe Umar hakika Mtume (S.A.W.W.) ametoa ahadi ambayo hatavunja ila aliye mnafiki, basi jihadhari na kuivunja hiyo ahadi. Hapo Mtume akaukamata mkono wangu na akaniambia; Ewe Umar kwa hakika kijana huyo si binadamu, bali alikuwa Jibril; ametaka kutilia mkazo kwenu maneno niliyoyasema kuhusu Ali" 20

Hadithi hii wameipokea wanazuoni wengi wa ki-Sunni katika Hanafy na Shafiy. Ni dhahiri kuwa tukio hili lilitokea siku ya Ghadiri. Sayyid Meer Hamid Husein Al-Hindi ametunga kitabu kikubwa juu ya hadithi ya Ghadeer ambacho ni juzuu moja katika Abaqaatul-Anvaar. Vile vile Al-Aminy ameeleza hivyo katika kitabu kiitwacho Al-Ghadeer.

HADITHI YA KUMI NA SITA

"Ali atakuwa na Mtume Peponi"

Amesimulia Umar bin Khattab kwamba alimsikia Mtume (S.A.W.W.) akimwambia Ali (A.S.), "Ewe Ali mkono wako uko katika mkono wangu, utaingia pamoja nami siku ya Kiyama popote nitakapoingia." Vile vile Anas bin Malik amesema kuwa Mtume (S.A.W.W.) amesema, "Siku ya Kiyama ataletwa ngamia wa peponi, Ewe Ali utampanda; goti langu na lako, paa lako na langu yatakuwa pamoja mpaka kuingia peponi."

Zimepokewa hadithi nyingi 21 kutoka kwa wanazuoni wa Kisunni kuwa hakika Ali (a.s.) atakuwa pamoja na Mtume (S.A.W.W.) Peponi. Miongoni mwao ni hadithi zilizopokewa na sahaba Zaidi Bin Arqam kuwa hakika Mtume (S.A.W.W.) alimwambia Ali: "Wewe utakuwa pamoja nami katika jumba langu Peponi pamoja na mtoto wangu Fatma. Kisha Mtume (S.A.W.W.) akasoma aya hii "Ikhwaanan alaa sururin mutqaabeleen (15:47), yaani "Ndugu wenye kupendana na waliokaa juu ya viti vya kifalme wameelekeana" (wanazungumza kwa furaha kubwa). (15:47).

Ameeleza Abdallah bin Mas'ud kwamba Mtume (S.A.W.W.) alimwambia Ali, "Huridhiki kuwa wewe utakuwa pamoja na mimi Peponi na Hasan, Husein na watoto wenu watakuwa nyuma yetu na wake zetu watakuwa nyuma ya watoto wetu, na Shia (wafuasi wetu watakuwepo kulia na kushoto kwetu?"

HADITHI YA KUMI NA SABA

"Udugu kati ya Mtume na Ali"

Imepokewa hadithi kuwa Umar bin Khattab amesema kuwa Mtume (S.A.W.W.) alipofunga udugu kati ya masahaba zake, akasema huyu Ali ni ndugu yangu katika dunia na akhera na Khalifa wangu kwa watoto wangu (Ahl) na Wasii wangu kwa umati wangu, na mrithi wa elimu yangu na ndiye mlipaji wa deni langu, mali yake ni yangu, na mali yangu ni yake, nafuu yake ni nafuu yangu, madhara yake ni madhara yangu; atakayempenda Ali hakika amenipenda mimi, na atakayembughudhi Ali hakika amenibughudhi mimi."

Kwa hakika Umar mwenyewe amekiri kwamba Ali ni wasii wa Mjumbe wa Mwenyezi Mungu (S.A.W.W.) katika umma wake, na mrithi wake kwa watu wa nyumba yake (Ahli). Kwa hakika zimepokewa Hadithi zaidi ya 200 kutoka kwa Mtume (S.A.W.W.) zenye madhumuni ya hadithi hii. Hadithi nyingi katika hizo tumezikusaya katika kitabu chetu kiitwacho 'Ali wal Wasiya' kilichopigwa chapa Najaf, Iraq.

3

FADHILA ZA SAYYIDNA ALI (A.S)

HADITHI A KUMI NA NANE

"Ali ni bora kuliko Masahaba wote"

Amehadithia Umar bin Khattab kwamba siku moja tulikuwa tumekaa katika duara na alipita Salman al-Farsi akienda kumwangalia mtu fulani. Kati yetu mmoja akasema, "Laiti mngependa nikujulisheni nani aliye bora wa umma huu baada ya Mtume wake, na aliye bora kuliko hawa watu wawili Abu Bakr na Umar?" Salman aliposimama kutaka kuondoka, akaulizwa: "Ewe Aba Abdallah unasemaje? Naye akasema, "Niliingia kwa Mtume (S.A.W.W.) wakati yumo katika sakaratil mauti na nikamwuliza, "Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Je, umeshausiya?" "Akasema, huwajui waliousiwa?" (ewe Salman). Nikasema "Mwenyezi Mungu na Mtume wake wanajua" Akasema, "Hakika Adam alimwusia (wasii wake) Shithi, hivyo alikuwa bora kuliko watoto wake wote baada yake. Nuhu alimuusia (wasii wake) Saam ambaye alikuwa bora baada yake. Musa akamusia Yusha, ambaye alikuwa bora baada yake. Suleiman akamwusia (wasii wake) Aasif Bin Barkhiya naye alikuwa bora baada yake. Isa akamwusiya Sha'muni As-Safaa ambaye alikuwa bora baada yake, na mimi nimemwusia (wasii wangu) Ali, ambaye ni mtu bora kuliko wote nitakayemwacha baada yangu".

Hadithi nyingi zenye maudhui haya zimepokewa katika vitabu vya ki-Sunni kutoka kwa Umar bin Khattab na Ibnu Umar. Katika Yanabi-ul-Mawddah (Uk. 253) hadithi iliyonakiliwa kutoka kitabu cha "Mawad-datulQurba" cha Sayyid Ali Hamdani as-Shafii, imeelezwa kuwa "Imepokewa adithi kutoka kwa mwana wa Umar (R.A.) kwamba alipita Salman Al-Farsi akienda kumuangalia mtu, na sisi tulikaa kikundi kwa duara. Kati yetu mmoja alisema: 'Laiti ningalikuambieni aliye bora katika umma huu baada ya Mtume wake, na bora kuliko hawa watu wawili Abu Bakr na Umar'. Akaulizwa Salman nani aliye bora? Akasema, "Bila shaka naapa kwa Mwenyezi Mungu, ningependa niwaambieni aliye bora katika umma huu baada ya Mtume wake, na bora kuliko hawa watu wawili, Abu Bakr na Umar." Kisha Salman akawa anaondoka, akaulizwa, "Ewe Aba Abdillahi umesema nini?" Akasema: "Niliingia nyumbani kwa Mtume (S.A.W.W.) wakati yuko katika sakaratil mauti; nikasema, "Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu je umeusiya? Akasema: "Ewe Salman unajua nani waliousiwa?" Nikasema, "Mungu na Mtume wake wanajua." Akasema, "Hakika Nabii Adam, alimwusia Shithi, ambaye alikuwa bora baada yake, Nuhu alimwusia Saam, ambaye alikuwa bora baada yake, Musa alimwusia Yusha, naye alikuwa bora baada yake, Isa alimwusia Sham-uni As-Safaa aliyekuwa bora baada yake. Na mimi nimemwusia Ali, ambaye ni bora kuliko wote baada yangu.

Hadithi hii inatueleza kwamba kila Mtume katika Mitume waliopita alikuwa na wasii wake, hakufa bila ya kumtaja wasii wake. Kadhalika, Mtume wetu (S.A.W.W.) alimjulisha Salman na watu wengi kuwa kwa hakika kuainisha na kumtaja Mwusiwa wa Mitume ni jambo la lazima; kwa hivyo, Mitume wameainisha wausiwa wao kwa amri ya Mwenyezi Mungu, sio amri yao binafsi. Basi kuchagua Mtume, wasii wa Mtume, Khalifa, na Imam iko mikononi mwa Mwenyezi Mungu, si kwa mtu mwingine. Mwenyezi Mungu amesema katika Kurani:

WA-RA-BUKA YAKH-LUKU MAA YA-SHAA-U WAYAKH-TAARU, MAA-KAANA LAHUMUL KHIYA-RATU, (28:68) (Na Mola wako huumba atakavyo na huchagua atakavyo; Hawana viumbe hiari).

HADITHI YA KUMI NA TISA

"Ubora wa pekee wa Imam Ali (A.S.)

Umar bin Khattab (A) amesema kwamba, Mtume Mtukufu (S.A.W.W.) alisema: "Hakupata kuchuma mtu yeyote chumo la ubora kama ubora wa Ali, unamwongoza mwenyewe utukufu huo katika uongozi, na humwepusha na ubaya na upotovu. Ilivyokuwa hakuchuma yeyote chumo alilochuma Ameerul-Mumineen Ali (A.S.) hajatokea Sahaba mwema yeyote mwenye utukufu kama wa Ali (A.S.). Wanazuoni wa ki-Sunni wamedhihirisha kuwa kati ya Masahaba watukufu hakuna mwenye utukufu kama wa Ameerul-Mumineen Ali bin Abi Talib (A.S.).

Jalalud-Dini Assuyuti Ash-Shafii ameeleza wazi maudhui haya katika kitabu chake "Tarikhul-Khulafaa" (J. 1, Uk. 65) ambamo amesema kuwa Ahmad bin Hambali amesema: "Haukupokewa wala haukuja ubora kwa yeyote katika Masahaba wa Mtume (S.A.W.W.) kama ule uliopokewa kuhusu Ali (R.A.)."

Ibun Abdil Bir amesema katika 'Al-Istiab (J.2, Uk. 479), kilichopigwa chapa Haydarabad (India) mwaka 1319 A.H., kuwa wamesema Ahmad bin Hambal na Ismail bin Ishak Al-Kadhi kuwa "Haikuwahi kupokewa utukufu na yoyote katika Masahaba kama utukufu wa Ali bin Talib (R.A.)" Ath-Thalabi ameitoa kauli hiyo katika tafsiri yake ya aya hii tukufu:

"INNAMA WALIYYUKU MULLAHU WA RASULUHU WALAD-HINA AMANULLADHINA YUQI-MUNASSALAATA WA YUTUNAZ-ZAKATA WA HUM RAKIUUN" (Hakika Bwana wetu hasa (mwenye mamlaka juu yenu) ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na walioamini ambao husimamisha swala na hutoa zaka katika hali ya rukuu. (Qur'an: 5:56)

HADITHI YA ISHIRINI

"Malaika mwenye sura ya Ali mbinguni"

Al-Muwaffaq bin Ahmad Al-Khowarazmi Al-Hanafi ameeleza hadithi katika kitabu chake Al-Manaaqib (Uk. 230) kutokana na Hamaad bin Thabit Al-Banani, ambaye ameipata kutoka Ubaid bin Umar Al-Laythi kutoka kwa Uthman bin Affani kutoka kwa Umar bin Khattabi kwamba Mwenyezi Mungu Subhanahu Wataala amewaumba Malaika kutokana na nuru ya uso wa Ali bin Abi Talib.

Wamepokea hadithi hii wanazuoni wa ki-Sunni katika vitabu vyao vingi vya hadithi. Miongoni mwao ni Al-Kanji As-Shafii katika kitabu chake "Kifaayatul-Taalib (Uk. 51) na hadithi yenyewe ni hii: "Anas amesema kuwa Mtume (S.A.W.W.) alisema, "Nilipokwenda Miraji usiku mbinguni nikamwona malaika mmoja amekaa juu ya mimbari ya nuru na malaika wengine wameizunguka ile mimbari. Nikamuuliza Jibreeli, huyu ni malaika gani? Akajibu, msogelee na mwamkie, nikamsogelea nipate kumwamkia, nikaona huyu ni ndugu yangu na Binamu wangu Ali Abi Talib!! Nikasema ewe Jibreeli, amenitangulia Ali kuja mbingu ya nne?"

Akanijibu "La sivyo, lakini malaika walimwomba Mwenyezi Mungu na kuonesha mapenzi yao kwa Ali; basi Mwenyezi Mungu akamwuumba malaika huyu kwa nuru yake katika sura ya Ali, basi malaika wanamzuru kila usiku wa kuamkia Ijumaa na siku ya Ijumaa kila mara malaika sabini elfu wanafika hapa na wanamtukuza na kumsifu Mwenyezi Mungu na thawabu ya tasbihi hizo, wanawatunzia wenye kumpenda Ali". Mtume akasema hadithi hii ni hasan na nzuri.

HADITHI YA ISHIRINI NA MOJA

"Ali ni mjuzi bora wa hukumu za Sharia"

Katika kitabu cha Ibnu Hajar Ash-Shafiiy 22 katika mlango ambamo ametaja sifa za Masahaba amemsifu Ali (A.S.) kwa kusema kuwa Ibnu Saadi ameeleza hadithi katika "Tabakati" aliyoipokea kutoka kwa Abi Hurairah akasema kuwa "Umar Bin Khattab amesema kuwa Ali ni mwenye kujua hukumu na maamrisho ya sheria kuliko sote. Mahala pengine Umar Bin Khattab (R.A.) amesema, "Ali Bin Abi Talib ndiye mwenye ujuzi zaidi wa hukumu na maamrisho ya Mwenyezi Mungu kuliko sote" 23

Jalalalud Deen As-Suyuti Shafii katika kitabu chake 24 katika mlango ambamo ametaja utukufu na sifa za Ali (A.S.) amesema Ibnu Saad amenakili hadithi kutoka kwa Ali. Hadithi hiyo ni kuwa aliulizwa Ali (A.S.) "Vipi wewe umepokea Hadithi nyingi sana za Mtukufu Mtume (S.A.W.W.) kuliko Masahaba wengine wa Mtume (S.A.W.W.)? Akasema, "Hakika mimi nilikuwa nikimwuliza naye akaniambia na nikinyamaza hunifunulia". Kadhalika Suyuti amenakili maneno haya kutoka kwa Abi Hurairah ambaye amesema kuwa Umar Bin Khattab amesema, "Ali ni mjuzi zaidi wa kila kitu katika hukumu za sheria kuliko sote". Hakim amenukulu maneno kutoka kwa Ibnu Masudi ambaye amesema: "Tulikuwa tunasema kuwa hakika mwenye maarifa ya hukumu zote za sheria kuliko watu wote wa Madina ni Ali". Suyuti ameendelea kusema, "Imepokewa kauli kutoka kwa Said Ibn Musayib kuwa amesema kuwa Umar bin Khattab alikuwa akiomba kwa Mwenyezi Mungu yasimfikie matatanishi yoyote wakati baba wa Hasan (Ali) hayupo."

Bila shaka kuomba kwa Umar (R.A.) asifikwe na matatizo wakati (Ali) baba wa Hasan asipokuwapo yametajwa na wanazuoni wengi wa Kisunni, Shafii na Hanafi; miongoni mwao ni Ibnu Abdil-Brr 25 ambaye alipokea maneno haya kutoka kwa Said Bin Musayyib kwamba "Umar alikuwa akiomba kwa Mwenyezi Mungu yasimpate matatizo mahali asipokuwapo Abul-Hasan." Vile vile Muhib-buddini Tabary Shafii katika kitabu chake 26 baada ya kueleza kisa cha mwanamke ambaye alizaa mtoto katika muda wa miezi sita na kupelekwa kwa Umar kutoa hukumu juu yake. Ameeleza maneno ya Said Bin Musayyib kwamba "Umar alikuwa akijilinda na matatizo wakati Abul-Hasan hayupo, (hadithi hii wamepokea Ahmad Bin Hambal na Abu Omar).

Aidha, Abul-Mudhaffar Yusuf Bin Kazaghli Hanafi katika kitabu chake 27 alisema kuwa, "Omar alisema kuwa katika hukumu yake kumbusu mwanamke aliyezaa katika (muda wa) miezi sita, aliamrisha apigwe mawe, lakini Ali Bin Abi Talib aliwazuia kufanya hivyo baada ya kuwabainishia sababu yake." Hapo Omar akasema, "Ewe Mola wangu usinibakishe katika matatizo wakati mtoto wa Abi Talib (A.S.) hayupo." Hayo yametolewa na Ali Al-Muttaqi Hanafiy katika kitabu chake kwa maneno yasemayo hivi: "Amesema Omar, "Ewe Mola wangu, usiniteremshie shida yoyote asipokuwepo Abul-Hasan (Ali) ubavuni mwangu." Muhib-buddin Tabary katika kitabu chake ameeleza maneno kutokana na Yahya Bin Aqeel kwamba Omar akimwambia Ali wakati anapomwuliza maswala yake: "Mwenyezi mungu asinibakishe duniani baada yako" (kwani hakuna awezaye kuondoa mashaka yangu). Mtungaji ameeleza hadithi hii kutokana na Abi Saidi Al-Khudriy kuwa yeye alimsikia Umar akimwambia Ali baada ya kumwuliza swali na kujibiwa, kuwa "Naomba kwa Mwenyezi Mungu nisiishi hata siku moja asipokuwepo huyo Abul Hasan."

Hakika Omar anayo maneno mengi na maelezo mbali mbali juu ya jambo hili aliyokuwa akiyasema wakati Ali (A.S.) alipokuwa akijibu swali lake. Baadhi ya maneno hayo tumeyakusanya katika kitabu chetu kiitwacho "Ali Wal-Khulafaa" 28 Angalia kitabu hicho ili upate kufahamu kuwa Ali (A.S.) alikuwa na daraja mbele ya watu wa zama zake, miongoni mwao wakiwa Makhalifa na wengine ijapokuwa alikuwa hukaa nyumbani tu. Ali ndiye aliyekuwa tegemeo la watu katika kuyatatua maswali na matatizo ya Waislamu. Na tumetaja katika hicho kitabu chetu "Ali Wal-Khulafaa" visa 140 vya matatizo na shida watu walizoleta kwa Ameerul Muumineen Ali (A.S.) na akawatatulia hata wakatosheka na kuridhika. Katika jumla ya wanazuoni wa Kishafii ambao waliotaja usemi huu wa Omar kuhusu Ali (A.S.) "Kuwa Ali ndio mjuzi wa sheria kuliko sote" ni Al-Kanjy Ash-Shafii katika kitabu chake 29 ambamo ameeleza hadithi aliyopokea Said Bin Jubayri kwa Ibnu Abbas kutoka kwa Omar (R.A.) kuwa yeye (Omar) alisema: "Ali ndiye mwenye ujuzi zaidi wa sheria kuliko sote." Tena akaendelea Umar kusema, "Nimeyachukua maneno haya juu ya Ali kwa Mtume (S.A.W.W.) wala sitaacha kamwe kuyasema."

Usemi huu wa Omar (R.A.) kuwa nimeyachukua hayo kwa Mtume (S.A.W.W.) ni dalili ya kwamba Mtume (S.A.W.W.) alisema: "Ali ndiye hakimu bora kuliko wote nyie." Kwa hivyo, Ali kuwa ndiye hakimu bora kuliko sisi sote inatokana na usemi wa Mtume (S.A.W.W.). Vile vile hadithi hiyo imeelezwa na Ibnu Sabbagh Al-Maliki katika kitabu chake 30 na Al-Kanji Ash-Shafii katika kitabu chake 31 baada ya kusema kuwa Ali alikuwa ndiye mjuzi zaidi kuliko Masahaba wote, na kuwa kuna njia na sababu nyingi zinazoonyesha kuwa Ali (A.S.) alikuwa mjuzi zaidi kuliko Masahaba wote. Neno lake Mtume (S.A.W.W.) lilikuwa "Ali ndiye hakimu kuliko nyote". Kwani hakimu (kadhi) anahitaji kujua kila namna ya elimu. Kwa vile akamchagua Ali juu ya wote kuwa hakimu (Kadhi), basi nidhahiri kuwa alizidi kuliko wote katika elimu zote.

Bila shaka miongoni mwa masahaba wengine kila mmoja wao alimshinda mwenziwe katika elimu fulani; kama alivyosema Mtume (S.A.W.W.) "Mjuzi kati yenu zaidi wa elimu ya mirathi ni Zaydi, na msomaji wenu zaidi ni Ubbay." Al-Kanjy akaendelea kusema kuwa Mtume (S.A.W.W.) alitaja daraja ya kila mmoja, na akataka azikusanye daraja hizo kwa binamu yake Ali Bin Abi Talib (A.S.) kwa tamko moja tu. Hivyo Mtume (S.A.W.W.) aliwaambia masahaba, "Hakimu (Kadhi) wenu (mwenye ujuzi kuliko wote) ni Ali". Na katika kitabu Riyaadhun nadhra 32 imepokewa hadithi ya Anas kutoka kwa Mtume (S.A.W.W.) kuwa amesema, "Hakimu (Kadhi) kuliko wote wa umati wangu ni Ali. Hadithi hii imeadikwa katika kitab cha El-Masaabeeh.

HADITHI YA ISHIRINI NA MBILI

"Ali ni Bwana wa kila mwenye kumsifu"

Akielezea cheo cha Ali (A.S.) kauli ya Omar (R.A.) ilikuwa "Ali ni bwana wangu na vile vile amenitatulia shida na kutoa hukumu ya haki mara nyingi sana." Yote haya utapata ukitazama kitabu cha Riyaa-Dhun-Nadhra, Juzu 2, Uk. 244.

Maelezo mafupi ya maneno ya Omar (R.A.) na kutaja kwake kuwa 'Ali ni bwana wangu' kumeelezwa na Muhib-Buddeen Attabary Ash-Shafiiyu katika kitabu chake Dha-Khaa-irul Uqba, Uk. 68, ambamo amenakili Omar (R.A.) kuwa: "Walikuja mabedui wawili wakigombana na kesi yao mbele yake. Omar akamwambia Ali (A.S.) "Hukumu kati yao ewe Abdul-Hassa!" Basi Ali (A.S.) akahukumu kati yao; Mmoja wao akasema, "Huyu ndiye ahukumu kati yetu!" Basi Omar (R.A.) aliruka na akamshika shingo ya (kanzu yake) na akasema: "Masikini wee! Unamjua huyu ni nai? Huyu ni bwana wangu na bwana wa kila mwenye kuamini, na yeyote asiyetaka kuwa Ali bwana wake basi si mwenye kuamini." Hadithi hii imeelezwa na Ibn as-Samani katika kitabu chake kiitwacho 'El-Muwaafaqah'. Muwaffaq Bin Ahmad El-Hanafiy pia ameitoa hadithi hii katika 'El-Munaaqib' na hadithi nyingine ya aina hiyo katika tukio jingine na Mwenyezi Mungu akipenda utaiona baadaye.

Omar (R.A.) katika kisa tulichokwishakieleza hapo awali maneno aliyomwambia yule mtu aliyetoa usafihi juu ya Ameerul-Mumeneen (Ali) (A.S.) kuhusu maneno ya Mtume (S.A.W.W.) juu ya cheo cha Ali, ni hadithi alioieleza El-Muhib Attabary katika kitabu chake tulichokitaja na kusema kuwa Mtume (S.A.W.W.) amesema, "Baada yangu Ali ni bwana wa kila mwenye kuamini." Hadithi aliyopokea Imran Bin Hussein ni kwamba Mtume (S.A.W.W.) amesema, "Hakika Ali ni katika mimi, na mimi ni katika yeye, na yeye baada yangu ni bwana wa kila mwenye kuamini." Hadithi hii imeelezwa na Tirmizi katika kitabu chake Saheeh Tirmizi; Juzuu 2, Uk. 46 (kimepigwa chapa Bara Hindi mwaka 1310 A.H.). Muhib-Buddeen Tabary Shafii amenukulu hadithi nyingine kwa jina la "Hadithi ya Omar (R.A.)" ambayo ni kama ifuatavyo:-

Buraydah Aslami alikuwa akimchukia na kumbughudhi Ali (A.S.). Basi Mtume (S.A.W.W.) akamwambia, "Ati unambughudhi Ali? Akasema ndiyo Mtume (S.A.W.W.) akamwambia usimchukie kabisa na ukiwa unampenda, basi mzidishie mapenzi (yako)." Baada ya hapo Buraydah akasema, "Hapana mtu yeyote aliye mpenzi zaidi kwangu baada ya Mjumbe wa Mwenyezi Mungu (S.A.W.W.) kuliko Ali, kwani yeye ni katika mimi na mimi ni katika yeye nay eye ndiye bwana wenu baada yangu." Hadithi mbili hizi zimenakiliwa na Ahmad bin Hambal na katika kitabu cha Ibnu Katheer kiitwacho "Al-Bidaaya Wan Nihaaya", Juzuu 7, Uk. 345. Vile vile katika Musnad Abi Daud Attayaalisi, Juzuu 11 Uk. 306 na kupigwa chapa Hayder Abad mwaka 1321 A.H. wawili hawa wamenakili hadithi nyingine zenye maana ya hadithi tuliyoitaja iliyomo ndani ya "Dhakhaa-irul-Uqba". Hadithi ya Imam Ahmad Bin Hambal imo katika kitabu cha Musnad Juzu 2, Uk. 460. Muwaffaq Bin Ahmad Al-Hanafii katika kitabu chake "Al-Manaaqib", Uk. 35 ameeleza hadithi nyingine iliyokuwa na sifa mbili kuhusu Ameerul-Muumeneen Ali Bin Abi Talib (A.S.) na hadithi hiyo imepokewa na Abi Hudhay-fa. Na siku ya kwanza ni Ali kuiteka Khaybar na ya pili ni kuwa "Hakika Mtume (S.A.W.W.) siku ya Ghadiri Khum alimsimamisha (Ali A.S.) na akawajulisha watu kuwa Ali ndiye bwana wa kila mwenye kuamini mwanamume na mwanamke". Hadithi yenyewe kama alivyoeleza Abi Hudhayfa kutokana na Abdurahman Bin Abii Laylaa ni kama hivi: Mtume (S.A.W.W.) siku ya (vita ya) Khaybar alitoa bendera kumpa Ali Bin Abi Talib, basi Mwenyezi Mungu akaifungua (akaiteka) Khaybar juu ya mkono wa Ali (A.S.) pia Mtume alimsimamisha Ali siku ya Ghadiir Khum na akawajulisha watu kuwa, "Hakika Ali ndiye Bwana wa kila mwenye kuamini mwanamume na mwanamke."

HADITHI YA ISHIRINI NA TATU

"Ali ni katika miye na mimi ni katika Ali".

Mtungaji wa kitabu cha "Riyadhun-Nadhra" Juzu 2 UK. 244, ameeleza hadithi inayotokana na Omar (R.A.) kuhusu Ali (A.S.) hadithi hiyo ni ya kupewa Bendera siku ya (vita ya) Khaybar, anahadithia ya kuwa Ali (A.S.) anazo sifa tatu, na ile hadithi ya mambo matatu aliyasema Mtume (S.A.W.W.) katika (habari) ya Ali (A.S.). (Na Omar) akatamani kuwa na mojawapo katika (mambo matatu) hayo, na hadithi aliyoisema Mtume (S.A.W.W.) kumwambia Ali (A.S.), "Wewe kwangu ni sawa na daraja ya Mtume Harun kwa Musa (A.S.)," na (ile) hadithi aliyosema Mtume (S.A.W.W.) Imani ya Ali ina uzito "Zaidi kuliko mbingu na ardhi saba; na hadithi ya kusema "Mtu yeyote ambaye mimi nimekuwa ndiye bwana wake basi na Ali ni bwana wake pia. Na neno lake (Omar) "Mimi sikupenda utawala ila siku Mtume (S.A.W.W.) alipomwambia Ali "(kuwa atampeleka kuiteka M.

Khaybar kadha." Na neno lake (Omar) kumwambia Ali, "Umekuwa bwana wa kila mwenye imani mwanamume na mwanamke" na neno lake, Ali ni bwana wa mtu ambaye Mtume (S.A.W.W.) ni bwana wake na neno lake Omar kwa Ali (A.S.) "Hakika Ali ni bwana wangu". Na kumtatulia matatizo yake. Na neno lake la kusema mjuzi na hakimu kuliko sote ni Ali; na mara nyingi kutaka msaada wake katika mambo mengi ya dini.

Tumezitaja baadhi ya hadithi nyingi alizozipokea Omar kuhusu ubora wa Amiril-Mumeneen Ali bin Abi Talib (A.S.) na baadhi yake zimesalia na tutazileta akipenda Mwenyezi Mungu, miongoni mwao ni uhakika wa kupewa kwake (Ali) bendera siku ya Khaybar na maelezo yake yametajwa katika vitabu vya hadithi na tarehe za wanavyuoni wa Kisunni na Shia.

Basi katika kitabu cha Kanzul-Ummal, Juzuu 6, Uk. 395 imeelezwa hadithi iliyopokewa kwa Ibnu Omar kuwa Omar Bin Khattab (R.A.) amesema kwamba Mtume (S.A.W.W.) amesema: "Bila shaka nitampa bendera mwanamume anayempenda (sana) Mwenyezi Mungu na Mtume wake, ni shujaa, si mwenye kukimbia (au kuogopa) na Mwenyezi Mungu atafungua (Khaybar) mikononi mwake, na huku Jibrili yu upande wake wa kulia, na Mikaili yu upande wake wa kushoto." Basi watu wakalala na shauku kubwa juu ya jambo hilo. Ilipofika asubuhi Mtume (S.A.W.W.) akasema, "Yuko wapi Ali?" Masahaba wakasema, Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu Ali anaumwa macho Mtume (S.A.W.W.) akasema mleteni (Ali). Alipoletwa Mtume akamwambia, "Sogea karibu kwangu." Alipokaribia Mtume (S.A.W.W.) akapaka mate yake kwa mkono wake machoni mwa Ali. Basi Ali akasimama mbele ya Mtume kana kwamba hakuumwa macho kabisa. Na Dara Qutni ameinakili hadithi hii katika Sunani yake, na El-Khatibu Baghdaadiy katika Tarekhe yake, Maliki katika riwaya ya Maliki na Ibnu Assakir katika tarekhe yake.

Uhakika wa kisa cha Ushindi wa Khaybar kwa mkono wa Ali (A.S.) ni jambo linalojulikana na mashuhuri na kupokewa na wanavyuoni wengi sana kwa njia mbalimbali. Hapa tunawataja baadhi ya wanavyuoni wa Kisunni. Miongoni mwao ni Imamu Bukhari katika Sahihi yake, Juzu 13, Uk. 301, iliyopigwa chapa bara Hindi mwaka 1282 A.H., na Imam Muslim katika Sahihi yake, Juzu 2 uk. 102, na El-Baghawiy katika Misbaahas-Sunna, Juzu 1, uk. 201, na Tirmizi katika Jaa-Mi, Juzu 2, uk. 461, na Ahmad Bin Hambal katika Musnad yake, mahali pengi, Juzu 1, uk. 99 na 133; na Juzu 3 uk. 16; na Juzu 4, uk. 128; na Juzu 5 uk. 358.

Vile hadithi hii imetajwa na El-Hakimu An-Nisha-puuriy katika Mustadrak, Juzu 3, uk. 108, Abu Naim katika kitabu chake Hil Yatul-Awliya, Juzu 1, uk. 62, na Ibnu Katheer katika kitabu Al-Bidaya Wan-Nihaaya, Juzu 7, uk. 4336, na Ali El-Muttaqi katika kitabu Kanzul-Ummal kilichoandikwa pembezoni mwa Musnad ya Ahmad, Juzu 4, uk. 130. Alisema Marhab (aliyoyasema) na Ali (a.s.) akajibu hivi "Mimi ndiye ambaye mama yangu ameniita Haydar kama simba wa porini aliyekuwa na sura ya kutisha, nitakuuweni kwa upanga na kukumalizeni kama vile ninafyeka majani bila ya hofu yoyote." Hapo Ali (a.s.) akaking'oa kichwa cha Marhab kwa upanga na ndipo ushindi wa (Khyabar) ukapatikana kwa mkono wake.

4

FADHILA ZA SAYYIDNA ALI (A.S)

HADITHI YA ISHIRINI NA NNE

"Hadithi ya Ghadeer-El-khum"

Katika Riyaadhan-Nazarah Juzu 2, uk. 244, imeelezwa hivi: Omar alimwambia Ali (a.s.) "As-Bahtal-Maw-Laa Kul-li Muminin wa Muminah" (Umekuwa bwana-mwenye mamlaka wa kila mwenye kuamini mwanamume na mwanamke). Maelezo kamili ya usemi wa Omar (r.a.) aliyomwambia Ali (a.s.) utapata kujua ukitazama katika vitabu walivyovitunga wanavyuoni wa Kisunni na wengineo juu ya kisa cha Ghadir. Na hapa tunataja alivyoandika Ibnu Kathir Al-Hanbaly katika kitabu chake Al-Bidaya Wan-Nihaya, Juzu 8, uk. 349. Anataja majina ya kikundi cha Masahaba kilichopokea hadithi ya Ghadir, na akasema kuwa: Omar Ibnu Khattab ni mmojawapo kati yao.

Hadithi yenyewe iliyotokana na El-Baraau imesema hivi: Tulitoka pamoja na Mtume (S.A.W.W.) mpaka tulipoteremka (mahali paitwapo) Ghadir Khum; akamtuma mpiga mbiu (mtangazaji) kuita watu, basi tulipokusanyika alisema Mtume (S.A.W.W.), "Je, mimi si bora zaidi na mwenye amri juu ya nafsi zenu?" Tukasema, "Ndiyo, vivyo hivyo unao mamlaka juu yetu." Mtume (S.A.W.W.) akasema (tena), Je, mimi si bora zaidi kuliko mama zenu? Tukasema, "Ndio bila shaka wewe ni broa zaidi, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu." Mtume akasema, "Je, mimi si bora mno kuliko baba zenu?" Tukasema, "Ndio bila shaka wewe ni bora zaidi, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu." Mtume (S.A.W.W.) akasisitiza kusema kuwa, "Je sikuwa mimi bora mno kwa jambo lolote kwenu?" Tukasema, "Ndiyo hivyo hivyo ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu." Mtume (S.A.W.W.) ndipo aliposema, "Mtu yeyote ambaye mimi ni bora mno kwake, basi na Ali Bin Abi Talib ni bora mno kwake katika kila jambo; Ewe Mola wangu mpende ampendaye Ali na mfanye adui amfanyiaye Ali uadui."

Basi Omar (r.a.) alisema, "Nakupongeza na kukupa mkono wa furaha ewe mtoto wa Abi Talib, leo umekuwa ndiyo bora mno wa kila mwenye kuamini." Na vile vile amepokea hadithi hii Ibnu Majah El-Qazwini katika 'Sunan' yake, kutokana na hadithi ya Hammadi bin Salma aliyoipokea kwa Ali bin Zaydi na Aba Haroon El-Abdi kutoka kwa Adi bin Thabit, naye amepokea kwa El-Barau na yeye ameipokea hadithi hii kwa Sa'ad El-Waq'qaas, na Talha bin Ubaydullah na Jabir bin Abdil-Laahi na kwa Abi Saeed El-Khudriyu na Habashi bin Junaadah na Jareer bin Abdil-Laah na vile vile Omar Bin Khattab na Abi Huray-rah.

Wapokeaji wa hadithi ya El-Ghadiir ni wengi sana, wala haiwezekani kuwaorodhesha wote katika kitabu kidogo kama hiki. Mtungaji mmoja maalum aliandika kitabu kuhusu wapokeaji wa hadithi ya El-Ghadiir; na mtungaji mwingine maalum aliadika kitabu kuhusu maelezo ya matamshi na maneno ya hadithi ya El-Ghadiir.

Na vitabu hivyo vimepigwa chapa India (bara hindi) na Iran (Uajemi). Na Ibnu Sabbaghu El-Maliki ameeleza katika kitabu chake 'Al-Fusuulul Muhimma' kauli ya Omar bin Khattab aliyemwambia Ali (a.s.) siku ya El-Ghadiir. Baada ya kumaliza Mtume (S.A.W.W.) hotuba yake, Omar bin El-Khattab alikutana na Ali Bin Abi Talib na akamwambia hivi: "Nakupa pongezi na mkono wa furaha ewe mtoto wa Abi Talib, wewe umekuwa ndiye bwana wa kila mwenye kuamini mwanamume na mwanamke." Na yeyote atakaye anaweza kuyapata na kuona yote hayo katika kitabu cha El-Ghadiir cha mwanachuoni mkubwa Al-Allama Sheikh Abdulhusein El-Aminii Mwenyezi Mungu amrehemu na kumridhia (Amin). Bila shaka atajua mambo ambayo yaliyopokewa katika hadithi ya El-Ghadiir kwa njia zote walizopokea.

HADITHI YA ISHIRINI NA TANO

"Haki iko na Ali na Ali yuko na haki"

Katika kitabu cha 'Riyaadhun Nadhra', Juzu 2, uk. 244 imesemwa kuwa katika jumla ya hadithi alizozipokea Omar (r.a.) kuhusu habari ya Ali (a.s.) ni ile hadithi aliyoisema Mtume (S.A.W.W.) kumwambia Ali: "Wewe kwangu ni katika daraja ya Harun kwa Mtume Musa."

Muhib-bud-Dini Tabary ameashiria katika maneno yake kuhusu hadithi ya Man-zilah: Hii ni hadithi maarufu sana na imepokelewa na kundi kubwa sana la Masahaba watukufu kutoka kwa Mtume (S.A.W.W.) kuhusu Ameerul Mumeneen Ali Bin Abi Talib (a.s.); na Omar Bin Al-Khattab ni miongoni mwao na ametiwa katika wapokeaji hadithi hii na kama inavyoonekana wazi wazi katika maneno ya Ibnu Kathiri katika kitabu chake Al-Bidaaya Wannihaya, Juzu 7, uk. 310 ambamo amesema: Katika Musnad ya Ibnu Hanbal imeelezwa hadithi iliyopokelewa na Aisha binti Saad kwa baba yake ni kuwa hakika Ali alitoka pamoja na Mtume (S.A.W.W.) hata walipofika mahali pa kuagana, Ali akawa analia huku akisema: Unanifanya kuwa ni Khalifa wako juu ya wanawake, watoto na wasioweza kwenda Mtume (S.A.W.W.) akasema: "Je, huridhii kuwa wewe kwangu ni katika daraja ya Harun kwa Musa ila tu utume unaishia kwangu?"

(Yaani, katika maneno ya hadithi hii ifahamike wazi wazi kuwa Ali (a.s.) hakupata utume isipokuwa yeye alipata daraja ya ukhalifa alioachiwa na Mtume (S.A.W.W.) hapo Madina wakati ambapo Mtume (S.A.W.W.) alipokuwa anakwenda katika vita vya Tabuuk, na daraja hii aliyopata Ali (a.s.) ya ukhalifa ni sawa na ile daraja aliyopata Nabii Harun (a.s.) kwa Nabii Musa (a.s.) isipokuwa Harun alikuwa Mtume ambapo Ali (a.s.) hakuwa Mtume kwani hapana tena utume baada ya Mtume Muhammad (S.A.W.W.) ambaye ni Mtume wa mwisho.

Na Ibnu Kathiri ameendelea kusema kuwa uhusiano wa Hadithi hii ni wa hakika na thabiti sana, na watu wengi walioipokea hadithi hii kwa Aisha binti Saad kutokana na baba yake. Na El-Hafidh bin Asaakar amesema: "Hadithi hii imepokelewa kutoka kwa Mtume (S.A.W.W.) na kundi kubwa la Masahaba na miongoni mwao akiwamo Omar bin Khattab, Ali, Ibnu Abbasi, Abdullah bin Jaffer, Muawiyah, Jaabir bin Sumra, Abu Said, El-Barau bin Aazib, Zayd bin Arqam, Zayd bin Abi Awfi, Thubayt bin Shareet, Habash bin Junaadah, Maalik bin El-Huwyrith, Anas bin Maalik, Abdul-Fadhl, Ummu Salmah, Asmaa binti Umaysi na Faatimah binti Hamza. (Na Ibn Kathir) amesema kuwa Al-Haafidh bin Asaakir amezipekua sana hadithi hizi kuhusu Ali (a.s.) katika kitabu chake cha Tarekh na hakika amefanya kazi nzuri na ya faida na amejitokeza na kujulikana kwa wenye kutazama na wenye shaka na kwa wapinzani.

Ibnu Kathiri ameinakili hadithi hii ya 'Manzilah' katika kitabu chake 'Al-Bidaaya Wannihaya' kutokana na Saad bin Abi Waq-qaas na amesema kuwa uhusiano na maelezo ya hadithi hii yote ni ya hakika na thabiti.

Idadi ya wale walioipokea hadithi hii ya 'Manzilah' inafikia (watu) ishirini, na mwanzo wao ni Omar bin Khattab (r.a.) na mwisho wao ni Saad bin Abi Waq-qaas, yaani ndiye baba wa yule Omar bin Saad ambaye aliyemwua Al-Imam Husein (a.s.) (mjukuu wa Mtume (S.A.W.W.)) El-Kunji Ash-Shafiy amesema katika kitabu chake Kifaa-yatu-taalib, uk. 151, kuwa wapokeaji wa hadithi ya 'Manzilah' ni kundi kubwa la Masahaba na miongoni mwao akiwemo Omar bin Khattab, Saad, Abu-Huray-rah, pamoja na kundi lile jingine ambalo lililokwishatajwa majina yao hapo mwanzo. Na wala haifichikani kabisa kwa yule mwenye kujua au kupekuwa kwa kutafuta hakika ya hadithi hii ya 'Manzilah' kuwa ni katika hadithi zilizo sahihi kwa wanavyuoni wa Kisunni na wa Kishi (Mwenyezi Mungu awarehemu).

Na Bukhari ameinakili hadithi hii ya 'Mazilah' katika kitabu chake Saheeh Bukhari, Juzu 14, uk. 385 kilichopigwa chapa India mwaka 1272 A.H. Juzu 17, uk. 475, na Muslim katika Saheeh Muslim J. 2, uk. 323 kilichopigwa chapa Misri mwaka 1322, na El-Haakim An-Nisaapuri Ash-Shafii katika Mustadrak, J. 3 Uk. 109 na 132, vile vile, Tirmidhiy katika kitabu chake Jami Tirmizee, Juzu 2, uk. 460, kilichopigwa chapa 1310 A.H., amepokea kwa njia nyingi hadithi hii. Na Ibnu Maajah El-Qazwini katika Sunani yake Juzu 1, uk. 28 kilichopigwa chapa mwaka 1313 A.H. ametaja hadithi hii ya 'Manzilah', Nasaaee katika kitabu chake El-Khasaais, uk. 7, uk. 8, uk. 23 na uk. 32, Adh-Dhahabi katika Tal-Khees Mustadrak As-Sahee-hain, Juzu 3, uk. 134, kilichopigwa chapa Haydarabad mwaka 1341 A.H., na El-Baghawi katika Masaa-Beeh As-Sunna, Juzu 2, uk. 201, chapa ya Misri 1318 A.H., na Abu Daudi Tayaalasi katika Musnad yake Juzu 1, uk. 29, kilichopigwa chapa Hydrabad, hadithi ya 209. Kadhalika, Ahmad bin Hambal ameitaja hadithi hii katika 'Musnad' yake kilichopigwa chapa Misri 1313 A.H., Juzu 1, uk. 170 na 173 na 175 na 177 na 182 na 184 na 331; na katika Juzu 3, uk. 32, na 338 na 369 na mahali mwingine zaidi katika hiyo hiyo Musnada.

Ibnu-Atheer El-Juzary Ash-Shafii ambaye alikufa mwaka 630 A.H. ameinakilia hadithi hii katika kitabu chake kiitwacho Taaree-khul-kaamil, Juzu 2, uk. 106 chapa ya Misri 1303 A.H., Ibu Asakir katika kitabu chake Mukhatasar Tareeh, Juzu 4, uk. 196, chapa ya Misri 1333 A.H., Ali El-Muttaqi Hanafii katika Kanzul-Ummal, J. 6, uk. 153 na mahali pengine, na Muhibbud-Deen Tabary katika kitabu chake Dhakhaa-Irul-Uqba, uk. 58 na 63, na katika kitabu chake kingine Riyaadhun-Nadhra J. 2, uk. 157, na Muwaffaq Bin Ahmad El-Khwarazmi Hanafi katika Munaaqib, uk. 32. Na Ibnu Hajar El-Haytami katika kitabu chake: As-Sawaa-iqul-Muhriqa, uk. 30 na 74. Aidha, Ibnu Khillikaan ameinakili katika kitabu chake Wafayaatul Aayaan J. 2, uk. 104, na Ibnu Hajar El-Asqalaani katika kitabu chake Al-Isabah, J.2, uk. 507. Shab-lanji Shafii katika Noorul-Ab-saar, uk. 68, Jalaalud-Deen Suyutee ameitoa hadithi hii ya Mazilah katika Taareekhul-Khulfaa, J. 1, uk. 65, Ibnu Abdi Rabbih katika Taareekhul-Khulafaa, J. 1 uk. 65, Ibnu Abdi Rabbih katika kitabu chake Al-Iqdul Fareed Juzu 2, uk. 194, kilichochapwa Boolaaq mwaka 1302 A.H. Abdul-Bir El-Qartaby katika kitabu chake 'Al-Isti-Aab' kilichopigwa chapa Haydarabad mwaka 1318 A.H. Al-Kanji Ash-Shafii ameeleza katika kitabu chake Kifaa-yatu-Taalib katika hadithi ndefu. Hapa tunaitaja kwa ufupi bila ya kuwataja wapokeaji wa hadithi hii; nayo ni kama hivi: Amehadithia Al-Harith bin Malika kwamba, "Nilikwenda Makka basi nikakutana na Saad bin Waqqaas, na nikamwambia, Je umepata kusikia daraja (sifa) ya Ali? (Saad bin Abii Waqqas) akasema: Bila shaka nimemshuhudia yeye (kuwa) anazo daraja nne! Na bila shaka ninapendelea sana kuwa na walau daraja mojawapo katika hizo nne na kwangu daraja hiyo ni bora mno kuliko ulimwengu na kuishi ndani yake wa umri wa Nuhu (A.S.).

"Hakika Mtume (S.A.W.W.) alimpendelea Abubakar kwenda Makka kuwasomea washirikina wa Kikureshi baadhi ya aya za mwanzo wa sura ya Baraa'a. Basi Abubakar akaenda nazo kwa muda wa mchana na usiku tu (siku moja). Baadaye Mtume (S.A.W.W.) akamwambia Ali: "Mfuate Abu-Bakar na uichukue hiyo Sura ya Baraa'a na uifikishe (wewe)," Basi Ali (A.S.) akamrudisha Abbakar (R.A.) na alirejea (Abu-Bakar) huku akilia na akasema, "Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Je, limeteremka juu yangu jambo lolote?" Mtume (S.A.W.W.) akasema: La, hakuna ila heri tu, bali kwa hakika hawezi kufikisha ujumbe wangu isipokuwa mimi mwenyewe au mwanaume aliye katika mimi; (au hapa badala ya kusema: mwanamume aliye katika mimi, Mtume (S.A.W.W.) alisema: Ahali Baytii).

Na Saad bin Abi Waq-qaasi ameendelea kusoma kuwa: "Tulikuwa msikitini siku moja pamoja na Mtume (S.A.W.W.) wakati alipotangaza wakati wa usiku kuwa watoke nje wote humo msikitini isipokuwa dhuria ya Mtume (S.A.W.W.) na dhuria ya Ali (A.S.). Basi tukatoka huku tukivivuta viatu vyetu. Ilipofika asubuhi, Abbas Ammi yake akamjia Mtume (S.A.W.W.) na akasema; Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Ammi zako na Masahaba wako umewatoa, na ukamweka mtoto huyu (Ali Bin Abi Talib), Mtume (S.A.W.W.) akasema: Mimi siye niliyeamrisha kuwatoeni wala kumweka mtoto huyu. Bila shaka Mwenyezi Mungu ndiye aliyeamrisha hayo. (Na daraja ya tatu), Saad amesema: Hakika Mtume wa Mwenyezi Mungu (S.A.W.W.) alimpeleka Omar (R.A.) pamoja na Saad kwenda kuiteka "Khaybar". Saad akajeruhiwa, na Omar (R.A.) akarejea bila ya kushinda. Hapo Mtume (S.A.W.W.) akasema "Nitampa kesho bendera mwanaume yule ambaye anayempenda Mwenyezi Mungu na Mtume wake, yeye anapendwa na Mwenyezi Mungu na Mtume wake na akataja sifa zake nyingi zingine. Kisha akamwita Ali (A.S.). Masahaba wakasema: "Yeye ni mgonjwa wa macho. Ali akaletwa huku akishikwa mkono na Mtume (S.A.W.W.) akamwambia, "Yafungue macho yako." Ali akajibu "Siwezi." (Saad) amesema: Mtume akamtia mate machoni mwake na akayasugua kwa kidole chake cha gumba na akampa bendera.

Saad bin Abi Waqqaas anaendelea kunena: "Daraja ya nne ni: Siku ya Ghadiri Khum, Mtume (S.A.W.W.) alisema: Enyi watu! Je, sikuwa mimi ndiye bora mno kwa wenye kuamini kuliko nafsi zao? Wakasema: hapana shaka wewe ni bora mno kwetu; na Mtume (S.A.W.W.) alisema hivyo mara tatu na wao wakaitika vivyo hivyo mara hizo pia; kasha akamwambia Ali "Nisogelee". Hapo basi Mtume (S.A.W.W.) akaunyanyua mkono wa Ali (A.S.) kwa mkono wake juu hadi kwapa lake nikaliona na Mtume (S.A.W.W.) akasema: Mtu yeyote ambaye mimi nimekuwa bora kwake na mwenye mamlaka juu yake, basi na Ali ni bora kwake na mwenye mamlaka juu yake. Na alisema mara tatu. Saad bin Abi Waqqaas amesema: (Daraja la tano) ni kuwa Mtume (S.A.W.W.) alikwishapanda ngamia wake mwekundu (kwenda katika vita ya Tabuuk) na alimwacha Ali kuwa ni Khalifa wake (hapo Madina).

Basi Makurayshi wakamwonea husuda na wakawa wanasema: Mtume amemwachia Ali kwa vile amemchukia (ndipo hakumchukua pamoja). Ali yakamfikia maneno hayo na hapohapo akamwendea Mtume (S.A.W.W.) akikamata kikuku cha kupandia ngamia wa Mtume huku akilia na kusema "Makurayishi wamedai kusema kwamba: umeniacha hapa kwa sababu umechukia kuwa pamoja na mimi. (Saad amesema). Hapo Mtume (S.A.W.W.) akawaita watu wote na walipokusanyika akasema, "Enyi watu, je miongoni mwenu yeyote (yule) huwa hakosi kuwa na husuda? Je, Huridhiki ewe mtoto wa Abi Talib kuwa kwangu miye wewe ni katika daraja ya Haruna kwa Musa, isipokuwa hapana Mtume yeyote baada yangu? Basi, Ali akasema: "Nimeridhika kwa Mwenyezi Mungu na Mtume wake." Kisha El-Ganji amesema, "Hadithi hii kweli na pande zake zote ndio sahihi na upande wake wa kwanza, ni ule aliopokea Imam wa watu wa hadithi - Ahmad Bin Hambali nao ni kule kupelekwa Abu Bakar na Sura ya Bara'-ah. Tabraani pia kuandika hayo.

Hadithi ya kuzuiliwa Abu Bakar katika kufikisha aya za Surat Bara'ah ni hadithi mashuhuri ambayo imepokelewa na wanazuoni wa Kisunni, Shafii na Hanafi, na mengineo katika vitabu vyao vinavyozingatiwa sana vya Tafsir na Tarekh. Na miongoni mwao ni Abul Fida Ismail bin Omar Ad-Dimishki aliyekufa mwaka 774 A.H. katika kitabu chake Al-Bidaaya Wan-Nihaya. Ibn Hajar El-Haytami Ash-Shafii katika kitabu chake "As-Swaaiqul", "Muhriqah", na Ibun Hajar Al-Asqlaani Ash-Shafii katika kitabu chake "Al-Isaaba." Vilevile imehadithiwa na El-Haakim An-Nisapuri Ash-Shafii katika kitabu chake Al-Mustadrak (ya) Saheehein, Tirmidhy Abu Isa Muhammad bin Isa katika Saheeh yake, Al-Mutaqy Hanafi katika Kanzul-Ummal. Imam Ahmad bin Hambal katika Musnad, Muhib-bud-Deen Tabary Ash-Shafii katika Saheehein yake, Al-Mutaqy Hanafi katika Kanzul-Ummal, Imam Ahmad bin Hambal katika Dhakhairul Uqba. Na wanazuoni wengi wengine wa Kishafii na Hanafii na wengineo ambao wameitaja na kueleza hadithi hii.

Na hadithi ya kufungwa milango aliyokuwa ikipitiwa kwenda katika Masjidin Nabawi (Msikiti wa Mtume) nayo ni milango ya vyumba walimokuwa wakiishi Muhaajirin (R.A.) wameipokea wanazuoni wa Kisunni, Shafii, na wegineo. Miongoni mwao ni Tirmidhi katika Saheeh yake, Ahmad bin Hambal katika Musnad yake, Al-Muhibbud-Deen Tabary katika Dhakhairul Uqba, Al-Mawaffaq bin Ahmad El-Khwarazmi katika Al-Manaaqib, El-Maghaaziliy Shafii katika kitabu chake kiitwacho El-Manaaqib, Sheikh Sulayman El-Kauduzi Hanafi katika kitabu chake Yanabii-ul-Mawaddah, Jalaaud-Deen Suyuti Shafii katika kitabu cha Adarurrul-Manthur kilichopigwa chapa Misri mwaka 1314 A.H. Al-Ganji Shafii amesema: "Ama ule upande wa tatu wa hadithi ya kutekwa kwa 'Khaybar' umeelezwa na Muslim katika saheeh yake."

Kwa hakika hadithi ya kutekwa kwa Khaybar kwa mikono ya Ameerul-Mumineen Ali (A.S.) imehadithiwa na kundi kubwa la wanazuoni wa Kisunni na Shia (Al-Imaaniyah). Mwenyezi Mungu awarehemu. Na miongoni mwao ni El-Haakim An-Nissapuri Ash-Shafiy katika 'Mustaadrak (ya) Saheehein. Al-Bukhaari katika Saheeh yake, Juzu 12, Juzu 14 na Juzu 15, Abul-Fida katika Al-Bidaaya Wan-Nihaya, Abu-Neem El-Isfahani katika Hilyatul Awliyaa, El-Baghawiy katika kitabu chake Massabeehus-Sunna Juzu 2, Tirmidhiy katika Saheeh yake, Juzu 2, Ibnu Maajah El-Qazwini katika Sunan yake ambacho ni kimojawapo katika Saheeh Sittah Ibnul Atheer Al-Jazari katika kitabu Usdul-Ghaba Juzu 4, katika maelezo ya maisha ya Ameerul Mumeneen Ali (A.S.)

Na upande wake wa nne umepokelewa na Ibnu Maajah na Tirmidhiy kutoka kwa Muhammad bin Bishaar, kutoka kwa Muhammad bin Jaffar. El-Ganji amesema:- Daraja na sifa ya tano ya Ali (A.S.) ni hadithi ya 'Manzilah! Hadithi hiyo imepokewa na kundi kubwa la wanazuoni wa Kisunni na wa Kishia (R.A.) na hadithi ya 'Manzilah' ni hadithi mashuhuri sana. Katika vitabu mahususi vya Kisunni na Shia na katika jumla ya vitabu hivyo ni Abakaatul An-Waari ndani ya Juzuu ambayo imehusika na habari za hadithi ya 'Manzilah' tu, nacho ni kitabu kikubwa sana kimepigwa chapa India. Basi katika kitabu kikubwa hicho mna uthibitisho wa kutosha kwa mwenye kutaka kujua ukweli na kumjua mwenye haki na kujua haki iko naye na yeye yu pamoja na haki.

HADITHI YA ISHIRINI NA SITA

"Laiti kama watu wote wangempenda Ali (A.S.) Mungu asingeumba Jahannamu.

Katika Yanaabee-ul-Mawaddah imeelezwa hadithi iliyopokewa na Sayyid Ali El-Hamdani kutoka kwa Omar Bin Khattaab kuwa amesema Mtume (S.A.W.W.) kwamba laiti kama watu wote wangekuwa wanampenda Ali, Mwenyezi Mungu asingeumba Moto." Wanazuoni wengi wa Kisunni, Shafii na Hanafy wamenakili hadithi hii kutoka kwa Omar Bin Khataab na kwa masahaba wengine watukufu. Na miongoni mwa (wanazuoni) hao ni Al-Muwaffaq Bin Ahmad El-Khwarazmi Hanafi katika Kitabu chake Taarekh Maqtalil Husein (A.S.) Juzu 1: ambaye ameinakili hadithi hii kutokana na Ibnu Abbas kuwa amesema kwamba Mtume (S.A.W.W.) amesema, "Laiti kama watu wote wangekuwa wanampenda Ali Bin Abi Talib Mungu asingeumba Moto".

Na miongoni mwa walioeleza hadithi hii ni: Allamah Sayyid Muhammad Saleh El-Hanafii, ambaye ameieleza hadithi hii katika kitabu chake Al-Kaw Kabud-Durry uk. 122, kilichopigwa chapa Pakistan, ikitokana na Omar Bin Khattab kuwa amesema kuwa Mtume (S.A.W.W.) amesema "Laiti kama watu wangekuwa wanampenda Ali Bin Abi Talib (A.S.) Mwenyezi Mungu asingeumba Moto."

HADITHI YA ISHIRINI NA SABA

"Kumpenda Ali ni kumpenda Mtume (S.A.W.W) na Mwenyezi Mungu (S.W.T.).

Katika "El-Kaw Kabud-Durri" kilichopigwa chapa Pakistan, na kilichotungwa na Sayyide Muhammad Salehe Al-Hanafi imesema kuwa Omar Bin Khattab amesema kwamba "Mtume (S.A.W.W) amesema, "Yeyote atakayekupenda ewe Ali, atakuwa pamoja na Mitume katika madaraka yao siku ya Kiyama; na yeyote atakayekufa hali anakuchukia basi hatajali (angalia) hali amekufa Myahudi au Mkristo."

Zimepokewa kutoka kwa Mtume (S.A.W.W) hadithi nyingi sana ambazo zaonesha faida za kumpenda Al-Imam Ali Bin Abi Talib (A.S.), na madhara ya kumchukia. Katika kitabu Arjahul-Mataalib uk. 319, kilichotungwa na Ubaydullah Al-Hanafy, imesemwa kuwa Ibnu Mas'ud amepokea hadithi kutoka kwa Mtume (S.A.W.W) akisema, "Kuwapenda dhuria ya Muhammad (yaani Mtume wetu (S.A.W.W) siku moja tu, ni bora kuliko ibada ya mwaka, na yeyote atakayekufa katika hali hiyo ataingia Peponi."

Katika Kanzul-Umaal, Juzuu ya 6, Al-Muttaqi Hanafi amedondoa hadithi kutoka Al-Muujamil Kabiir ya Tabaraani na katika Taareekh-ul-Kabiir ya Ibnu Asaaki ikitokana na Abi Ubaydah Bin Ammar bin Yaasir, ambaye ameipokea kutoka kwa baba yake na babu yake kuwa Mtume (S.A.W.W) amesema, "Ninamwusia kila aliyeamini kukubali kuwa Ali bin Abi Talib anayo mamlaka na amri juu yake; na yeyote anayekubali hayo kuhusiana na Ali (A.S.) basi amenikubali mimi, pia na mwenye kunikubali mimi amemkubali Mwenyezi Mungu kuwa anayo mamlaka na amri juu yake; na yeyote atakayempenda Ali (A.S.) ndiye mwenye kunipenda mimi; na yeyote mwenye kunipenda mimi basi hakika ndiye mwenye kumpenda Mwenyezi Mungu; na yeyote atakayemchukia Ali (A.S.) basi hakika ndiye mwenye kunichukia mimi; na yeyote atakayenichukia mimi, ndiye mwenye kumchukia Mwenyezi Mungu (Azza Wajallah).

HADITHI YA ISHIRINI NA NANE

"Ampendaye Ali (a.s.) anampenda Mungu na Mtume wake" Katika Taareekh ya Ibnu Asaakir imenakiliwa hadithi iliyotokana na Ibnu Abbas ambayo inasema, "Mimi nilikuwa pamoja na Omar bin Khattab katika baadhi ya njia za Madina huku tumeshikana mikono, mara Omar akasema: "Ewe Ibnu Abbas mimi sina shaka sahibu yako (yaani binamu yako Ameerul-Muuminiin Ali (a.s.) amedhulumiwa." Nikasema: Basi mrudishie (haki) yake aliyedhulumiwa, ewe Amiirul-Muuminiin! Akauvuta mkono wake na kuondoka kwa hasira. Kisha akasimama na kusema; Ewe Ibnu Abbas, watu hao walitaka kumdharau tu sahibu yako."

Nikasema, "Wallahi Mtume (S.A.W.W) hakumdharau wakati alipomtuma na kumwamrisha aichukue Suurat Baraa-ah kwa Abu Bakar na awasomee watu." Hakika tukio hili limeelezwa na kundi kubwa la wanazuoni wa Kisunni kwa maneno tofauti au kuongezwa maneno, na katika jumla ya wanazuoni walioieleza hadithi hii ni: Ali Al-Muttaqi katika 'Kanzul-Ummal', Juzu 6, kutoka kwa Ibnu Abbas ambaye amesema, "Nilikwenda na Omar bin Khattab katika vichochoro vya mji wa Madina. Omar bin Khattab akasema, "Ewe Ibnu Abbas (watu) wamemdharau rafiki yenu (Ali bin Abi Talib a.s.) kwa vile hawakumtawalisha katika mambo yenu. Nikasema "Wallahi hakika Mtume (S.A.W.W) hakumdharau wakati alipomchagua kuwasomea Surat Baraa-ah watu wa Makka." Omar akaniambia: "Unasema kweli, naapa kwa Mwenyezi Mungu kuwa bila shaka nimemsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu akamwambia Ali Bin Abi Talib, 'Yeyote atakayekupenda wewe ndiye amenipenda mimi; na yeyote atakayenipenda mimi amempenda Mwenyezi Mungu, na yeyote atakayempenda Mwenyezi Mungu ataingia Peponi."

Maudhui ya hadithi ya Omar (r.a.) inatoka kwa Mtume (S.A.W.W) na kundi la Masahaba walieleza kwa matamko mbali mbali. Katika Kanzul Ummal (juzu 6, 391) kutoka kwa Ibnu Abbas imeelezwa kuwa siku moja Mtume (S.A.W.W) alitoka hali ameukamata mkono wa Ali, na kusema, "Fahamuni! Yeyote atakayemchukia huyu (Ali), basi hakika amemchukia Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na yeyote atakayempenda huyu, basi hakika amempenda Mwenyezi Mungu na Mtume wake." Na katika Kanzul Ummal. Vile vile Juzu ya 6, yamenakiliwa maneno haya kutoka Mustadrak Sahiihain ya Hakim ambayo, kwa hakika ni hadithi kutoka kwa Salman ambaye amesema kuwa: Mtume (S.A.W.W) amesema "Yeyote ataayempenda Ali, basi hakika ndiyo amenipenda mimi, na yeyote atakayemchukia Ali, basi hakika amenichukia mimi."

HADITHI YA ISHIRINI NA TISA

"Omar Ibn Khattab akiri ubora wa Ali"

Omar bin Khattab (r.a.) amesema: "Najua kuwa Ali (a.s.) anayo mambo matatu, ambayo ningekuwa na mojawapo tu mimi, kati ya mambo hayo ningeona fakhari zaidi kuliko kupata ngamia wekundu. Jambo la kwanza ni kuwa Mtume (S.A.W.W) amemwoza Binti yake, na amemzalia mabwana wawili wa vijana wa watu wa Peponi: Hassan na Husain (A.S.) Na jambo la pili ni kufungwa milango yote isipokuwa mlango wake (yaani, Mtume (S.A.W.W) aliifunga milango yote iliyokuwa ikipitiwa na Masahaba kama vile Abu Bakar, Omar bin Khattab na wengineo kutoka majumbani mwao kuingia Masjidun-Nabawy. Na jambo la tatu ni kuwa Mtume (S.A.W.W) alimpa bendera siku ya vita ya Khaybar.

Hakika hili neno la Omar (R.A.) wamelitaja wanazuoni wengi wa Kisunni ima kwa ufupi au kwa maelezo marefu. Ambaye aliyelitoa kwa ufupi ni Muhibad-Deen Tabary katika Riyaadhun Nadhra Juzu 2, ambae amesema: "Na katika hadithi alizozipokea Omar (R.A.) kuhusu Ali ni ile hadithi ya mambo matatu, nayo ni kama hivi: Ali anayo mambo matatu; kuwa na mojawapo kwangu kati ya mambo hayo ni bora zaidi kuliko kupata ngamia wekundi. Na ambaye aliyeeleza kwa urefu ni Ali Al-Muttaqi Hanafi katika Kanzul Ummal, Juzu 6, ambaye amesema kuwa katika Musnad ya Abi Shayba hadithi iliyotokana na Abdalla bin Omar imesema kuwa: "Wallahi Ali anayo mambo matatu ambayo kwayo kuwa na mojawapo tu kati ya mambo hayo ni bora mno kwangu kuliko kupewa ngamia wekundu.

(1) (Mtume (s.a.w.w.) amemwoza binti wake ambaye alimzalia viongozi wa Peponi.

(2) Kufunga (kuziba) milango yote, isipokuwa mlango wake (wa Ali A.S.)

(3) Na Mtume (s.a.w.w.) alimpa Ali bendera siku ya Khaybar.

HADITHI YA THELATHINI

uAli kupewa Beramu siku ya Khybar"

Omar (R.A.) amesema kuwa Mtume (s.a.w.w.) amesema: Bila shaka, kesho nitampa bendera mwanaume anayempenda sana Mwenyezi Mungu na Mtume wake na Mwenyezi Mungu ataifungua (Khaybar) kwa kumshindisha mwanaume huyo." Omar (R.A.) amesema: ""Sikutamani Uamiri ila siku hiyo Basi ilipofika asubuhi mimi nikajitokeza kwa ajili ya Uamiri. Mtume (s.a.w.w.) akasema: uCEwe Ali! Nyanyuka uende (Khaybar) na ukapigane wala usigeuke (yaani, usiache mapigano mpaka Mwenyezi Mungu akupe ushindi katika mkono wako (hadi ushinde na kuuteka)".

Basi Ali akafuata amri hiyo na akaona karaha kugeuka kwa vile Mtume (s.a.w.w.) alimwamrisha asigeuke mpaka ashinde. Alipokuwa anakwenda alisema: Mpaka lini nipigane nao? Mtume (s.a.w.w.) akasema "Mpaka watakapokiri na kusema Laa-Ilaaha Ila Laah! Basi watakaposema hivyo itakuwa haramu kuwaua na kuzichukua mali zao ila kwa haki." Kwa hakika kisa cha kutekwa kwa Khaybar kwa mikono ya Amirul Mumineen Ali (A.S.) ni jambo lenye maana sana na wapokeaji wa hadithi hii ni kundi kubwa la Masahaba na Tabieen. Ama kauli hii ya Omar na mapokezi yake imeelezwa na kundi la wanazuoni wa Kisunni kwa ufupi na kwa urefu.

Na katika hao wanazuoni walioitaja hadithi hii kwa ufupi ni Muhibbud-Deen Tabary ambaye katika (hadithi) alizozipokea Omar (R.A.) kuhusu Ali (A.S.) ni kauli yake isemayo: "Sikupenda Uamiri ila siku hiyo (Mtume (s.a.w.w.) alipomwambia Ali: nitampeleka (mahali) fulani (Khaybar). Ama katika wanazuoni walioieleza hadithi hiyo kinaga ubaga ni Ahmad bin Hambari: hakika yeye ameieleza hadithi hii katika Musnad yake kutokana na Musnad ya Abi Hurayrah, kuwa amesema Mtume (s.a.w.w.)siku ya Khaybar kuwa: "Nitampa bendera mwanaume anayempenda sana Mwenyezi Mungu na Mtume wake;" Omar (R.A.) amesema, "Nikatamani uamiri siku hiyo, basi nikajitokeza na nikafanya bidii ya kutumaini kuwa atanipa mimi, basi ilipofika asubuhi (Mtume (s.a.w.w.) akamwita Ali, na akampa (hiyo bendera) na kumwambia: "Upigane wala usirejee mpaka (Mwenyezi Mungu) akujalie uiteke Khaybar kwa mkono wako Basi Ali akaenda kidogo kisha akasema "Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, nipigane hadi lini?" Mtume (s.a.w.w.) akasema: "Mpaka watoe shahada kuwa Mwenyezi Mungu ni mmoja tu na hakika Muhammad (s.a.w.w.) ni Mtume wake. Watakapofanya hivyo, hakika wamejikinga damu zao na mali zao (isipokuwa haki ya dini); na hesabu yao ni kwa Mwenyezi Mungu."

Hakika Bukhari na Muslim wamenakili hadithi na kisa hiki katika Saheeh zao mbili (Juzu 2, na katika Juzu 4 na katika Juzu 16). Na Muslim ameeleza katika Saheeh yake (Juzu 2) na kwa mapokezi mengihe katika J. 2, uk. 325. Na Ali El-Muttaqi Hanafi ameieleza katika kitabu chake Kanzul-Ummaal (Juzu 6) na vile vile wameieleza hadithi hii wanazuoni wengi wa Kisunni na Shia (Mwenyezi Mungu awarehemu).

HADITHI YA THELATHINI NA MOJA

"Ali ni katika Mtume (s.a.w.w.) na Mtume ni katika Ali"

Omar (R.A.) amesema kuwa Mtume (s.a.w.w.) alimwambia Ali: ""Wewe ni katika mimi, na mimi ni katika wewe."

Bukhari ameeleza hadithi hii ya Omar (R.A.) kuhusu Ameerul Mumineen Ali bin Abi Talib (A.S.) katika kitabu chake Saheeh, Juzu 14, katika mlango wa sifa za Ali (A.S.). Amesema kuwa Omar (R.A.) amesema: "Mtume (s.a.w.w.) amefariki dunia hali yeye yu radhi naye." (Yaani, Ali Bin Abi Talib) na amesema Mtume (s.a.w.w.) kumwambia Ali "Wewe ni katika mimi, na mimi ni katika wewe."

Na kwa hakika wameipokea hadithi hii kuhusu Ameerul Mumineen Ali bin Abi Tali (A.S.) kundi kubwa la wanazuoni wa Kisunni, Shafiiy na Hanafii kwa upokevu thabiti na sahihi ikitokana kwa masahaba na Tabieen watukufu wakubwa. Miongoni mwao ni Sibt Jawzi Hanafi katika kitabu chake Tadhkiratul Umma, kilichopigwa chapa Iran, Uk. 43. Yeye amesema: Mtume (s.a.w.w.) amesema, "Ali ni katika mimi na mimi ni katika yeye", siku ya vita ya Uhudi wakati kiongozi wa washirikina alipokusudia kumvamia Mtume (s.a.w.w.). Hapo Ali (A.S.) akajitolea kwa nafsi yake na akamhujumu yule kiongozi na akamwua. Papo hapo akateremka Jibreel (A.S.) na kusema: Ewe Muhammad, hakika huo ndio ukarimu na huku ndiko kusaidiana". Mtume (s.a.w.w.) akasema "Ali ni katika mimi na mimi ni katika yeye" Basi Jibreel akasema "Na mimi ni katika ninyi wawili." Na miongoni mwao ni Muhib bud-Deen Tabary Shafii katika kitabu chake Kifaa yatiit-Taalib, Uk. 142, AH El-Muttaqi Hanafi katika Kanzul Ummaal (Juzu 6, uk. 400). Angalia kitabu chetu All Wal Wasiy-Yah ambamo tumetaja wanazuoni wengine wengi wa Kisunni ambao wamenakili hadithi hiyo.

HADITHI YA THELATHINI NA MBILI

"Awapendaye Aali Muhammad ni mtu wa Peponi"

Omar bin Khattab (R.A.) amesema. "Fahamuni na mjuc kwamba utukufu hauwezi kukamilika ila kwa kumpenda Ali (A.S.) Kauli hii ya Omar (R.A.) Ibnu Hajar Ash-Shafii ameiandika katika kitabu chake, Assawaaiqul Muhriqa. Vile vile Ibnu Abdil Bir katika kitabu chake Istiab amenakili hadithi aliyopokea Ibnul-Musayyib ambaye amesema kuwa "Omar (R.A.) amesema "Wadhihirishieni mapenzi Masharifu na muwapende na mjilinde heshima na tabia zenu kutokana na watu wabaya na mfahamu kwamba haiwezi kukamilika heshima na sifa zenu zozote ila kwa kumpenda Ali.

Na Umar bin Khatab (r.a.) ameyachukua maneno haya kutoka kwenye hadithi ya Mtume (s.a.w.w.) iliyo mashuhuri sana iliyotolewa na wanavyuoni (Ulamaa) wengi wa Kisunni -Shafiiy na Hanafly, na wengineo. Na miongoni mwao ni Allama Ubaidullahi Ammrisari Al-Hanafiy, katika kitabu chake Ar-Jahul-Mataalib na kati yao ni al-Hamwini Shafiiy katika "Faraaidus Simtayin" Juzu ya pill. Na miongoni mwao ni Allama Zamakh-shari katika Tafsiri yake inayojulikana kwa jina la Al-Kash-shaf, jadala 2; na huyo Zamakh-shari ametoa hadithi hii kwa uthabiti na akasema Mtume (s.a.w.w.) amesema, "Yeyote atakayekufa katika (hali ya) kuwapenda (dhuria) wa Muhammad amekufa hali ya kuwa yu shahidi. Fahamuni si hivyo tu (bali) na yeyote atakayekufa katika (hali ya) kuwapenda Aali Muhammad, amekufa hali ya kuwa ni mwenye imani kamili.

Fahamuni (si hivyo tu (bali) yeyote atakayekufa katika (hali ya) kuwapenda Aali Muhammad amekufa hali ya kuwa ni mwenye imani kamili. Fahamuni (si hivyo tu; bali) ye yote atakayekufa katika (hali ya) kuwapenda Aali Muhammad (S.A.W.W) kwanza tu Malakul-Mawti atambashiria Pepo, kisha Munkar na Nakeer watambashiria Pepo. Fahamuni (si hivyo tu; bali) ye yote atakayekufa katika (hali ya) kuwapenda Aali Muhammad (A.S.) atafanyiwa shangwe kwenda peponi, kama vile anavyofanyiwa shangwe bibi arusi kwenda kwa mume wake, fahamuni (si hivyo tu; bali) na yeyote atakayekufa katika (hali ya) kuwapenda Aali Muhammad (A.S.) hufunguliwa yeye milango miwili ndani ya kaburi yake ya kwendea Peponi; fahamuni (si hivyo tu; bali) na yeyote atakayekufa katika (hali ya) kuwapenda Aali Muhammad (A.S.) Mwenyezi Mungu atafanya kaburi yake kuwa mahali pa kufanyia Ziara Malaika wa rehema kuja kuzuru."

Na hadithi hii ni ndefu sana; na tumetaja baadhi ya maneno yake tu. Je, unaweza kupatikana utukufu na usharifu wo wote utakaozidi sifa na utukufu wa mwenye kumpenda Muhammad na Aali Muhammad (s.a.w.w.) Je? Inaweza kukamilika heshima na utukufu wo wote bila ya (kupatikana )mapenzi ya Muhammad na Aali Muhammad (s.a.w.w.)?

Basi kauli ya Omar (R.A.) maafikiano na vile alivyotoa habari Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) katika alama za kuwapenda Aali Muhammad (s.a.w.w.) na Ali (A.S.) ndiye bora wao na ndiye mtukufu wao kwa maelezo ya hadithi nyingi za Mtume (s.a.w.w.).

5

FADHILA ZA SAYYIDNA ALI (A.S)

HADITHI YA THELATHINI NA TATU

uMalaika wameumbwa kwa nuru ya Ali"

Omar (R.A.) amesema kuwa: Mtume (s.a.w.w.) amesema, "Hakika Mwenyezi Mungu ameumba Malaika katika nuru ya uso wa Ali Bin Abi Talib, wanahimidi, kusifu na kumwadhamisha (Mwenyezi Mungu) na kuwaandikia thawabu za hiyo kazi yao wenye kumpenda (Ali) na wenye kupenda kizazi chake."

Hii ni hadithi nyingine aliyoipokea Omar (R.A.) kuhusu ubora wa Ameerul Mumeneen (Ali A.S.) mbali na ile iliyotangulia; na hadithi hii wameipokea Maulama wengi wa Kisunni, na miongoni mwao ni Al-Khateeb Ahmad Khwarizmi Hanafiy katika kitabu chake maarufu Taareekh Maqtalul Husein (A.S.) juzu ya kwanza kilichopigwa chapa Najaf (Iraq). Hakika yeye ameinakili hadithi hiyo kwa kuirejesha kwa Abi Bakar bin Abdillahi bin Abdir-Rahmaan ambaye amesema, "Nimemsikia Uthmani bin Affani akisema nimemsikia Omar bin Khattab, akisema nimesikia Abu Bakari Bin Abi Qahafa, akisema nimesikia Mtume (s.a.w.w.) akisema, "Kwa hakika Mwenyezi Mungu ameumba katika nuru ya uso wa Ali Bin Abi Taalib Malaika ambao wanamhimidi Mweneyzi Mungu na kumtukuza, nao huwaandikia thawabu za hiyo (kazi yao) wenye kumpenda Ali (A.S.) na wenye kuwapenda kizazi chake."

HADITHI YA THELATHINI NA NNE

"Hasan na Husein ni Mabwana wa watu wa Peponi na Ali ni bora kuliko wao"

Katika Kifaayatu-Taalib, imenakiliwa hadithi kutoka kwa Naafii ikitokana kwa Ibnu Omar kuwa Mtume (s.a.w.w.) amesema, "Hasani na Husein ndio mabwana wawili wa vijana wa watu wa peponi, na baba yao ndiye bora kuliko wao wawili. Kisha akasema hadithi hii ni kweli, thabiti; Mwenyezi Mung ametujaalia kuipata na tunamshukuru. Na ameendelea kusema, "Imaamu wa wanazuoni wa hadithi Abulqasim Tabrani katika kitabu chake kiitwacho Muujam Al-Kabeer katika sura kuhusu Hasan bin Ali (A.S.) anaeleza hadithi zinazotoka kwa masahaba na miongoni mwao ni Omari bin Khattab, na Ali Bin Abi Talib na Hudhayfah, nazo ni kama hivi: Imepokewa hadithi kutoka kwa Zari ikitoka kwa Hudhayfah ikisema kuwa, "Tuliona furaha kuu usoni mwa Mtume (s.a.w.w.) siku moja. Tukasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, tumeona katika uso wako bishara nyingi za furaha. Mtume (s.a.w.w.) akasema, "Namna gani nisifurahi! Na hali Jibrilu amenijia na amenibashiria kuwa hakika Hasan na Husein ndio mabwana wawili wa vijana wa watu wa Peponi, na Baba yao ndiye bora kuliko wao wawili." Kisha El-Ganji akasema, "Kukusanyika (kufungamana) hizi habari kwa pamoja ni thibitisho na dalili ya ukweli wake."

Mtungaji amesema: Kwa kauli ya Tabraani iliyo katika Al-Muujamil Kabir hadithi itakuwa miohgoni mwa hadithi alizozipokea Omar bin Khattabi kuhusu ubora wa Ameerul Mumineen, Ali Bin Abi Talib (A.S.); na hadithi hii wameitoa wanazuoni (Maulama) wengi wa Kisunni; miongoni mwao ni Al-Ganji Ash-Shafiiy, na Attabrani, na Muhibud-Deen Tabari Shafiiy katika kitabu chake 4Dhakhairul-Uqba' chini ya anwani kuwa (hao wawili Hasani na Husein ni mabwana wa vijana wa Peponi) amesema kuwa hadithi kutoka kwa Hudhayfah imesema. "Nilimwendea Mtume (s.a.w.w.) na nikasali pamoja nave. akaendelea kusali mpaka akasali sala ya Insha. Kisha akaondoka. nami nikamfuata aliposikia sauti yangu, alisema, "Nani huyu? Ni Hudahayfah?" Nikasema "ndiyo". Mtume (s.a.w.w.) akasema, "Hakika huyu ni Malaika. Hakupata kuteremka kabisa katika ardhi kabla ya leo, amemtaka idhini Mola wake ili anisalimie mimi, na anipe bishara kuwa, kwa hakika Fatimah ndiyo Bibi wa wanawake wa watu wa Peponi; na hakika Hasan na Husein ndiyo mabwana wawili wa vijana na watu wa Peponi."

Hadithi hiyo imenakiliwa na Ahmad bin Hanbal na Tirmidhi Abu Haatim amenakili hadithi yenyewe inayosema, "Tumeuona uso mtukufu wa Mtume (s.a.w.w.) unatoa bishara za furaha; Mtume akasema, "Kwa nini nisifurahi na hali imenijia Jibrilu na akanibahiria kuwa hakika Hasan na Husein ndio mabwana wawili wa vijana wa watu wa Peponi na Baba yao ndiye bora kuliko wao wawili." Na Abu-Ali Bin Shaadhani vile vile ameieleza hadithi hiyo kutoka kwa Ibni Omar na Ali Al-Mattaqi ameinakili hadithi hiyo katika Kanzul Ummal Jalada 6, uk. 222.

HADITHI YA THELATHINI NA TANO

"Ali ni bora kuliko wote baada ya Mtume (s.a.w.w.)"

Katika "Yanabiul-Mawaddah" imepokewa hadithi kwa Sayyid All Hamdaniy Shafiiy, kutoka kwa Ibnu Omar ambaye anaeleza kwamba Mtume (s.a.w.w.) amesema, "Bora wa wanaume wenu ni Ali Bin Abi Talib, na bora wa vijana wenu ni Hasan na Husein na bora wa wanawake wenu ni Fatimah binti Muhammad (s.a.w.w.)"

Wanazuoni wa Kisunni wamekariri hadithi hii au yenye maana kama hii katika vitabu vyao vingi kama vile Ali Al-Muttaqi Al-Hanafii katika Kanzul-Ummal (juzu ya 6), ya kutoka kwa Ibnu Abbas akisema kuwa, Mtume (s.a.w.w.) amesema "Ali ni bora miongoni mwa watu wote." Al-Ganji Shafiiy katika Kifaayatu-Taalib, alikariri hadithi kutokana na Jaabir Bin Abdillah, kuwa amesema, "Tulikuwa kwa Mtume (s.a.w.w.) akasema, basi mara Ali Bin Abi Talib akaja; Mtume (s.a.w.w.) akasema, "Hakika amekujieni ndugu yangu." Kisha akageuka kuelekea upande wa El-Kaaba akaipiga kwa mkono wake, na akasema, utNaapa kwa yule ambaye nafasi yangu ipo mikononi mwake, hakika huyu (Ali) na wafuasi wake, ndio wenye kufaulu siku ya Kiyama.

" Kisha akasema, "Hakika yeye ndiye wa mwanzo wenu kuamini, na ndiye mtekelezaji wenu zaidi wa ahadi ya Mwenyezi Mungu, na ndiye mwadilifu wenu zaidi kati ya raia, na ndiye mgawaji wenu zaidi wa usawa, na ndiye mkubwa wenu zaidi wa daraja mbele ya Mwenyezi Mungu." Na (Jaabir) amesema hapo ndipo ilipoteremka aya hii isemayo: "Hakika wale walioamini na wakatenda mambo mema basi hao ni wabora wa viumbe." (98:7) Na (Jaabir) amesema, "Sahaba wa Mtume Muhammad (s.a.w.w.) wakimwona Ali bin Abi Talib anakuja walikuwa wakisema, "Hakika amekuja aliye bora wa viumbe." El-Ganji amesema kuwa hivyo ndivyo alivyopokea mwanazuoni wa hadithi wa nchi ya Shamu aitwaye Ibnu Asaakir katika kitabu chake kinachojulikana sana kwa (jina) la Taarikh Ibn Asaakir, na mwanazuoni wa hadithi wa nchi ya Iraq amepata hadithi hiyo kutoka kwa Zar, ikitoka kwa Ali Bin Abi Talib (A.S.) kuwa amesema kwamba Mtume (s.a.w.w.) amesema.

"Mtu yeyote asiyesema kuwa (Ali) ndiye bora wa watu basi amekufuru," na katika hadithi nyingine iliyotokana na Hudhayfa amesema, "Nimemsikia Mtume (s.a.w.w.) akisema, "Ali ndiye bora wa watu', yeyote atakayekataa na kukanusha. basi amekufuru." Hivyo ndivyo alivyopokea El-Haafidh Ad-Dimishqi katika kitabu chake At-Taarikh kutoka kwa Al-Khatiib Al-Haafidh, na katika riwaya iliyotokana na Jaabir, amezidisha kusema: Mtume (s.a.w.w.) amesema "Ali ndiye bora wa watu, basi yeyote atakayekataa, hakika amekufuru."

Na katika riwayah ya mwanazuoni wa Shaami imeelezwa kuwa "Hawezi kumchukia (Ali) ila Kafir." Na katika riwaya ya Bibi Aisha ikitokana na Ata, amesema, "Nilimwuliza (Bibi) Aisha kuhusu Ali naye basi alisema, "Huyo ndiye bora wa watu, haoni shaka juu ya jambo hili ila Kafir." Kisha akasema, hivyo ndivyo alivyotaja Al-Haafidh Ibn Asaakir kuhusu Ali (A.S.) katika Tarehe yake, juzu ya hamsini. (Kitabu hiki kina majuzu mia tatu katika hayo ni za Ali (A.S.).

Na miongoni mwa hayo ni "Dhakhasirul Uqba", katika kitabu cha "Yanaabiul Mawadda" imenakiliwa hadithi ya (Bibi) Aisha iliyotangulia na hadithi ya Ali (A.S.) na hadithi ya Hudhayfa kuwa Mtume (s.a.w.w.) amesema: "Ali ndiye bora wa watu, na yeyote atakayekataa, basi hakika amekufuru. Vile vile zimeelezwa hadithi nyingi nyingine zenye maudhui ya hadithi hii zilizotokana na Jabir. Katika hadithi hizo ni zile ambazo zimo katika kitabu cha Kanzul Haqaaiq kilichopigwa chapa pembezoni mwa kitabu cha "Jamii Sagheer" Juzu 2, na zile zilizomo mwenye Musnad ya Ahmad Bin Hambal, Juzu ya tano, na katika Nuzhatul Majaalis ya (Sheikh) Assafuriyu Ash-Shaffly, Jalada 2, kilichopigwa chapa Misri mwaka 1320 A.H.

Katika Manaaqib ya (Sheikh) Al-Khwarazmi, imenakiliwa hadithi sahihi iliyotokana na Mtume (s.a.w.w.) kuwa kwa hakika amesema, "Bora wa waliopo juu ya ardhi baada yangu ni Ali Bin Abi Talib."

HADITHI YA THELATHINI NA SITA

Katika Yanabeul Mawaddah kutokana na kitabu "Mawad-datul-Qurba" cha Sayyid Ali El-Hamdaany Shafiiy imeelezwa hadithi kutoka kwa Abi Waail, iliyotokana na Ibn Omar ambaye amesema: Abu-Bakar, Omar, Othman basi mtu mmoja akasema:' "Ewe baba wa Abdir-Rahmani! Ali si katika masahaba wake'? Akasema: "Ali ni katika Ahli-Bayt, hakisiwi na yeyote; yeye yuko pamoja na Mtume (s.a.w.w.) katika daraja yake; hakika Mwenyezi Mungu anasema (katika Qur'ani tukufu), "Ambao waliamini na wakafuatwa na dhuria zao kwa kuamini, tutawakutanisha nao dhuria zao" (52:22) Basi Bibi Fatima (A.S.) yu pamoja na Mtume (s.a.w.w.) katika daraja yake na Ali (A.S.) yu pamoja nao.

Kwa hakika, kauli ya Ibnu Omar kuwa "Ali ni katika Ahli-Bayti, hakisiwi na yeyote," ni ushuhuda na uthibitisho wa kutosha. Kauli hiyo imekaririwa katika Dhakaairul-Uqba cha Muhib buddin Attabari Ash-Shafiiy; ambaye amesema chini ya maudhui kuwa (hakika wao hawakisiwi na yeyote) kutokana na Anas, ambaye amesema kuwa Mtume (s.a.w.w.) amesema, "Sisi ni Ahlul-Bayti, hakisiwi nasi yeyote". Na hakika hadithi hii imenakiliwa na Ubaydullah El-Haafiiy katika kitabu chake Ar-Jahul Mataalib kutokana na "Dhakaairul Uqba" isipokuwa amesema kuwa hadithi hiyo imeelezwa na Ibnu Marduwayhi katika El-Manaaqib, ambamo pia amesema kuwa Ali (a.s.) alisema juu ya mimbari kuwa, "Sisi ni katika watu wa nyumba ya Mtume (s.a.w.w.), hatukisiwi na yeyote". Hadithi hiyo imenakiliwa na Day-amiy katika Firdawsil Akhbar. Na katika Yanaabiiul-Mawaddah baada ya kueleza ile hadithi iliyonakiliwa kutoka kwa Ibnu Omar, amesema kuwa "Abdallah bin Ahmad bin Hambal alimwuliza baba yake kunako "Ubora" naye akasema, "Abu Bakar, Umar, Uthman." Tena akanyamaza. Abdallah bin Ahmad akasema, "Ewe baba yangu, yuko wapi Ali Bin Abi Talib?" Akasema: Yeye ni katika watu wa nyumba (ya Mtume S.A.W.W) hakisiwi na hawa." Na Ali Al-Muttaq El-Hanafiiy amenakili hadithi hii katika 'Kanzul Ummal' Juzu ya 6, kutokana na Firdawsul Akhbar ya Daylamiy, ambayo imesema, "Sisi ni katika Ahlul-Bayti, hakisiwi nasi yeyote."

HADITHI YA THALATHINI NA SABA

"Ali ni bwana wa mwumini baada yangu"

Katika Yanaabiiul-Mawaddatul Qurba imeelezwa hadithi ya Ibnu Omar kuwa amesema, "Tulikuwa tukiswali pamqja na Mtume (s.a.w.w.) basi akatupa jicho kwetu na akasema, "Enyi watu! Huyu ndiye mpenzi wenu baada yangu, duniani na akhera; basi muhifadhini (yaani, anamkusudia Ali a.s.)".

Hadithi hii au yenye maana kama hiyo imenakiliwa na kundi la wanazuoni wa Kishafiy, Hambali na Imaamiyah (Shia) katika vitabu vyao vinavyo zingatiwa sana; na katika jumla ya wanazuoni wa Kisunni waliopokea hadithi hii ni Ibnu Kathiri katika kitabu chake Al-Bidaya Wan-Nihaya, Juzu 7. Yeye ameinakili kwa Imraani bin Hasiini, ambaye amesema, w'Baadhi ya Masahaba walimshitaki Ali (a.s.) kwa Mtume (s.a.w.w.). Basi Mtume (s.a.w.w.) aliwaendea hali uso wake umebadilika kwa ghadhabu na akasema "Mwacheni Ali, mwacheni Ali, mwacheni Ali, hakika Ali ni katika mimi na mimi ni katika yeye, naye bwana wa kila mwenye kuamini baada yangu."

Kwa ufupi hadithi hiyo imemalizikia hapa. Na katika kitabu hicho hicho cha Al-Badaaya Wannihaya juzu ya saba, imekaririwa hadithi kwa mapokeo ikitoka kwa Wahab bin Hamza naye amesema kwa ufupi, "Nilisafiri pamoja na Ali basi niliporejea nikakutana na Mtume (s.a.w.w.) ambaye mara akamkumbuka Ali (a.s.). Mimi nilimsema Ali kwa maneno mabaya, basi Mtume (s.a.w.w.) akaniambia, "Usimseme Ali kabisa (maneno mabaya kama haya); kwani Ali ndiye bwana iwen baada yangu." Na Muhibbud Deen Tabari amenakili hadithi hiyo katika Dhakhaairul Uqba na Tirmidhi katika Saheeh yake, juzu ya pili, kwa mapokeo ya hadithi iliyotoka kwa Mtume (s.a.w.w.) ambaye kuhusu habari za Ali (a.s.) amesema kuwa, "Hakika yeye ndiye bwana wa kila mwenye kuamini baada yangu."

Na Ubaydullaah El-Hanafiy ameeleza hadithi hii katika kitabu chake Ar-Jahul Mataalib kwa mapokeo ikitokana na Imraan bin Hasiin ambaye amesema kuwa Mtume (s.a.w.w.) alipeleka jeshi, na Ali Bin Abi Talib alikuwa pamoja nao, basi akaenda na kikosi hicho, na (huko) akapata mjakazi wakamchukua masahaba wane (katika wao) wakafanya shauri yao na wakasema, "Tukimkuta Mtume (s.a.w.w.) tutamshitakia na (utamwambia namna alivyofanya (Ali)" Na Waislamu walipokuwa wanarejea safari zao, kwanza huenda kwa Mtume (s.a.w.w.) kumsalimu, kisha ndipo huenda zao makwao.

Basi kilipofika kile kikosi walimsalimu Mtume (s.a.w.w.); (kisha) mmoja wa wale watu wane akasimama na akasema "Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Je. hukumwona Ali amefanya hivi na hivi?" Basi Mtume (s.a.w.w.) akanyamaza kisha akasimama wa pili na akasema kama yule wa mwanzo na akasimama wa tatu na wane na wakasema kama vile walivyosema wenzao. Hapo Mtume (s.a.w.w.) akawakabili kwa uso wa ghadhabu na akasema, "Mnataka nini nyinyi kwa Ali?" Na alisema hivyo mara tatu, na akaendelea kusema kuwa: "Hakika Ali ni katima mimi na mimi ni katika yeye; na yeye ndiye Bwana wenu (mwenye mamlaka) baada yangu." Amenakili hadithi hiyo Abu-Daud At-Tayalisi katika kitabu chake "Sanaun" (J.H.). Vile vile Ahmad bin Hambal amenakili katika kitabu chake "Musnad" (J.H. uk 460) kwa kusema kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alimwambia Buraydah, "Ewe Buraydah! Usimseme Ali kwani yeye anatokana nami, na mimi natokana naye, na yeye ni bwana wenu na mwenye mamlaka juu yenu baada yangu."

HADITHI YA THELATHINI NA NANE

"Ali ni Nduguye Mtume (s.a.w.w.)"

Katika Dhakhairul Uqba imenakiliwa hadithi ya Ibnu Omar kuwa Mtume (s.a.w.w.) alifanya udugu kati ya masahaba wake; basi Ali alikuja na akasema, "Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, umefanya udugu kati ya masahaba wako, na wala hukufanya udugu kati yangu na kati ya mwingine yeyote?" Mtume (s.a.w.w.) akasema, "Wewe ndiye ndugu yangu katika dunia na akhera.

Hadithi hii imepokewa kutoka kwa Omari bin Khattab (r.a.) na kwa Abdalla bin Omar. Na hadithi aliyopokea Ibnu Omari imenakiliwa na mabingwa wa wanazuoni wa Kisunni; miongoni mwao Tirmidhiy katika Saheeh yake, juzu 2, uk. 461 na amesema (kuwa) hadithi hii ni hasa (kweli). Kadhalika El-Baghawi, katika Masaabiihus-Sunnah (juzu 2, uk. 202), Ibnu Kathiiri katika El-Bidaaya Wannihaya, juzu 7, uk. 335, Ali El-Muttaq El-Hanafiy katika KanzuI-Ummal, juzu 6. uk. 122, 152, 153. 159, 390, 394, 399, 400, 402 na 404. Na mahali pengine pengi kama vile Ibnu-Athiir El-Jazary katika Usdul Ghaba Juzu 4 uk. 16 na Al-Muwaffaq bin Ahmad El-Hanafiy katika El-Manaaqib, uk. 82,83,91 na95.

Vile vile Ahmad bin Hambal katika Musnad yake mahali chungu nzima ametaja, k.v. katika juzu 1, uk. 230, Ibrahim bin Muhammad Al-Hamwiniy Ash Shafiy katika Faraidus-Simtain, j. 1, babu 21, mahala aliponakili hadithi ya "Al-Muaa-khaat" (udugu) Al-Mannawi katika Kanzul Haqaaiq iliyoandikwa pembezoni mwa kitabu, Al-Jaamul Sagheer cha Suyuti Shafiiy (j. 2. uk. 70) na wanazuoni wengi wa Kisunni waliopokea hadithi hii minghairi ya hawa. Na vitabu mahsusi vimetungwa vya hadithi hii ya uMua-khaat". Angali kitabu cha Ghas-yatul Maraam cha Allama Al-Mujja As-Sayyid Hashim Al-Bahrani, kilichopigwa chapa Iran.

HADITHI YA THELATHINI NA TISA

"Anayefarakana na Ali anafarakana na Mtume"

Katika Manaaqib ya Al-Khateeb Al-Muwaffaq bin Ahmad Al-Khwarizmi Al-Hanafi uk. 62, imo hadithi iliyotokana na Ibnu Omar kuwa Mtume (s.a.w.w.) amesema. Mtu yeyote atakayefarakana (Kujitenga) na Ali ndiyo amefarakana na mimi na yeyote atakayefarakana na mimi ndiyo amefarakana na Mwenyezi Mungu.

Hadithi hii na hadithi yenye maudhuui kama haya imeelezwa na kikundi cha wanazuoni wa Kisunni katika vitabu vyao. Miongoni mwao ni Ali Al-Muttaqi Al-Hanafiy katika Kanzul Ummal (j. 9 uk. 156) kwa matamko mbalimbali kutokana na vitabu vingi, k.v. Al-Muu-jam Al-Kabeer ya Tabarani kutokana na Ibnu Omar kuwa Mtume amesema, wCMtu yeyote atakayefarakana na Ali ndiye amefarakana na Mwenyezi Mungu." Tena humo humo katika Al-Muu-jam Al-Kabeer, Ibnu Omar amesema kuwa Mtume (s.a.w.w.) amesema, "Yeyeote atakayefarakana nawe ewe Ali! Basi hakika ndiyo amefarakana na mimi, na yeyote atakayefarakana na mimi, basi hakika ndiye amefarakana na Mwenyezi Mungu." Na ameinakili tena katika "Al-Mus-tad-rak ya Saheehain (sahihi mbili) cha Al-Haakim Nisa-puri kutoka kwa Abu-Dhar; na tamko lake na tamko la Tabraani katika Al-Muu-jami ni sawa sawa.

HADITHI YA ARUBAINI

"Ali ni miongoni mwa wa mwanzo kuingia Peponi."

Katika Kanzul Ummal (j. 6, uk. 391) Ali Al-Muttaqi Al-Hanafiy amenakili hadithi hii kutokana na Ib un-Najjari katika tarehe yake, na kutoka kwa Ibnu Omar kuwa hakika Mtume (s.a.w.w.) alimwambia binamu yake Ali Bin Abi Talib (a.s.) kuwa. "Ewe Ali, wewe (utaingia) Peponi."

Zimepokewa hadithi nyingi katika vitabu vya wanazuoni wa Kisunni ambazo zinawaflkiana na hadithi hii katika maneno (yake) na kwa maana pia kwa matamshi mbali mbali zikitokana na Ibnu Omar na wengineo. Katika hadithi hizo ni ile ambayo iliyomo ndani ya Tarikh ya Ibnu Asaakir (J. 4, uk. 318) kuwa Ali (a.s.) amesema, "Nilimshitakia Mtume (s.a.w.w.) husuda za watu (wanazonifanyia mimi)" Mtume (s.a.w.w.) akasema, "Ewe Ali! Hakika watu wanne wa mwanzo watakaoingia Peponi ni mimi, na wewe, na Hassan, na Husain, na dhuria zetu watakuwa nyuma yetu, na wake zetu watakuwa nyuma ya dhuria zetu" Ali (a.s.) akauliza, "Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, watakuwa wapi wafuasi (Shia) wetu? Mtume (s.a.w.w.) akajibu, "Wafuasi (Shia) wenu watakuwa nyuma yenu."

Na katika hadithi hizo ni zile ambazo zimo ndani ya "AS-SAWA-IQUL MUHRIQA" uk. 98. Yeye amenakili hadithi ambayo ilinakiliwa na IBN ASKARI na amezidisha mwisho wa hadithi hiyo kuwa "Na wafuasi (Shia) wetu watakuwa upande wetu wa kulia na wa kushoto". Vilevile hadithi hii imo katika kitabu cha Tafsiri cha Nishaapuri ambacho kimepigwa chapa pembezoni mwa Tafsiri ya Tabari, (juzu 25, uk. 31).

Kadhalika, Ibrahim Bin Muhammad Al-Mamuuniy Ash-shafiiy katika kitabu chake, Faraidus-Simtayn, (]. 2, Mlango 9), Ali Al-Muttaqi katika Kanzul Ummal (J. 6 uk. 212), Sheikh Sulaymaan Al-Qanduuzi Al-Hanafy, katika Yanaabeeul-Mawaddah (Uk. 269), kwa hakika yeye ameikariri hadithi kutokana na Ali (a.s.) kutoka kwa Ibn Masud na kwa Abii Raafii (R.A.). Ama tamko la Ameerul-Momineen Ali Bin Abi Talib (a.s.) ni kuwa Ali (K.W.) amesema hivi, "Nilimshitakia Mtume (s.a.w.w.) husuda ya watu (wanayonifanyia) mimi; basi Mtume (s.a.w.w.) akasema kuniambia mimi; Je, huridhii kuwa wa nne katika (watu) wane? - Wa mwanzo atakayeingia peponi ni mimi, wewe, Hasan, na Husein; na wake zetu watakuwa upande wetu wa kulia, na wafuasi (Shia) wetu watakuwa upande wetu wa kushoto". Na dhuria zetu watakuwa nyuma ya wake zetu. Aidha ameitoa hivyo Ath-Thaalabiy, na Ahmad ameieleza katika Al-Manaaquib, na Sibtu Jawzi. ameelezea vivyo hivyo.

Na tamko la Ibnu Masud linasema hivi: Mtume (s.a.w.w.) alimwambia Ali (a.s.) "Je, huridhii kuwa hakika wewe utaingia peponi na mimi na Hassan na Hussein; na dhuria zetu, watakua nyuma ya migongo yetu na wake zetu watakuwa nyuma ya dhuria zetu; na wafuasi wetu watakuwa katika upande wetu wa kulia na wa kushoto. Hadithi hii imo katika Al-Manaqib. Ama tamko la Abbii Raafii ni kuwa Mtume (s.a.w.w.) amesema, "Ewe Ali! Hakika watu wane na mwanzo watakaoingia peponi ni mimi na wewe na Hassan na Husein, na dhuria zetu watakuwa nyuma ya migongo yetu, na wake zetu watakuwa nyuma ya dhuria zetu. na wafuasi wetu watakuwa upande wetu wa kulia, na wa kushoto". Tabarani katika "Al-Muujamul Kabeer"

HADITHI YA AROBAINI NA MOJA

"Imani ya Ali ni nzito kuliko ardhi na mbingu."

Katika Kanzul Ummal (J. 6 uk. 156) imo hadithi iliyopokewa na Ibnu Umar kuwa Mtume (s.a.w.w.) amesema, wwlwapo kama mbingu na ardhi zingewekwa katika kitanga kimoja (cha mizani) na Imani ya Ali Bin Abi Talib katika kitanga kingine, bila shaka Imani ya Ali ingalizidi." Angalia Daylami katika kitabu chake Firdawsul Akhbaar. Hadithi hii ilikwishatangulia iliyotokana na Umar Bin Khattab. kwa sababu ya hitilafu za mpokeaji na maneno tumekariri hadithi hii mara ya pili, kwa ajili ya kuthibitisha vile ilivyotakikana.

HADITHI YA AROBAINI NA MBILI

"Mambo matatu ni mahsusi kwa Ali (a.s.) tu"

Katika Manaaquib ya Al-Khateeh Al-Muwaffaq Bin Ahmad Al-Khwarazmi Al-Hanafi, (Uk. 187) imeelezwa hadithi kutoka kwa Abdalla Bin Umar kuwa Omar bin Khattab. Alisema Ali anayo mambo matatu na nilitamani kuwa na moja miongoni mwa (mambo) hayo, ingalikuwa bora zaidi kwangu kuliko kupewa ngamia wekundu: (1) kuozwa na Bibi Fatima (a.s.) (2) Kupewa bendera siku ya (vita ya) Khaybar (3) kutenda kama ilivyoamrishwa kwa mujibu wa aya ya NAJWA.

Imeshatangulia hadithi kuhusu mambo mawili; na lile jambo la tatu (yaani) lile la tokea la "Najwa" ni mashuhuri sana, tena ni katika mambo yanayomhusu Imam Ali (a.s.) peke yake. wala hashirikiani katika sifa hii na yeyote katika Masahaba. Na wanazuoni wa hadithi na Tafsiri zote wanawaflkiana katika jambo hilo. Basi katika "Kifaayatu-Taalib cha Al-Kanji Shafiiy, (uk. 52) mlango wa ishirini na tisa, imesemwa kuwa "Hakika aya ya "AN-NAJWA" ilifuata kitendo cha Ali (a.s.) tu wala si sahaba yeyote mwingine. Kisha aya hiyo ikanasikhishwa (kuondolewa na hakupata kuitenda mtu yeyote ila Ali a.s.)".

Kisha ameipokea hadithi kwa umadhubuti kwa Ali bin Alqama Al-Anmaary ikitokana na Ali bin Abi Talib (a.s.) kuwa amesema, "Iliposhuka aya (58:12) Enyi mlioamini: Mnapomsemeza Mtume kwa siri toeni sadaka kabla ya kumsemeza Mtume (s.a.w.w.) akaniita, na akaniambia: "Je, unaonaje dinari moja? Nikasema hawaiwezi. Mtume (s.a.w.w.) akasema ngapi basi? Nikasema, dhahabu yenye uzito wa kipimo cha punje au shayiri moja, Mtume akasema, "Hakika wewe ni mtawa! Basi ndipo ilipoteremka aya hii, "Oh! Mnaona taabu kutanguliza hiyo sadaka kabla ya kumsemeza kwenu? (58:13). Basi Ali (a.s.) akasema "Kwa sababu yangu Mwenyezi Mungu amefanya wepesi kwa umma huu, na wala haikupata kuteremka (yah hii) kwa yeyote kabla yangu, wala haikuteremka kwa yeyote baada yangu, wala hakuifuata aya hii mtu yeyote ila mimi tu".

Ibnu Umar amesema: "Ali bin Abi Talib alikuwa na mambo matatu. Laiti ningekuwa na moja tu miongoni mwa hayo, ingalikuwa inanipendeza mno kwangu kuliko (kitu kingine chochote) duniani. (1) Kuozwa Bibi Fatima (a.s.) (2) Kupewa bendera (3) kuteremka aya ya "AN NAJWA". Mujaahid amesema, "Masahaba walikatazwa kuonana faraghani na Mtume (s.a.w.w.) hadi watoe sadaka. "Basi ikawa hakuonana naye faraghani isipokuwa Ali bin Abi Talib (a.s.) (yeye) alikwenda na dinari moja, basi akaitoa sadaka, kisha ndipo ilipoteremka ruhusa. Kwa hiyo sadaka ilikuwa ni faradhi itokayo kwa Mwenyezi Mungu wakati wa maonano ya faragha. Basi aya hii iliyo katika kitabu cha Mwenyezi Mungu (Qurani) hakuifuata na kuitenda mtu mwingine isipokuwa Ali bin Abi Talib (a.s.). Kisha Al-Kanji amesema. "Katika jambo na tendo hilo kuna fadhila na utukufu usiokuwa na mfano, na wanafahamu na kujua wale wenye akili! Na kule kuenea kwake (kisa hiki) kwa mabingwa (waongozi) wa hadithi, kunatosheleza maneno na maelezo yake mwenye Ibn Jarir At-Tabary ambaye .amesema hivi: "Wamewafikiana mabingwa wa Tafsiri wote kuwa hakika hakufuata na kutenda juu ya aya hiyo yeyote isipokuwa Ali tu."

Tumekwishaeleza kwa ufupi tafisiri na maana ya aya AN NAJWA. Hapa tunakuelezea baadhi ya wale ambao wameandika kisa hiki katika vitabu vyao, katika wanazuoni wa Kihanafi na Shafiiy. Miongoni mwao ni Allaamah Jaral-Laah Mohmood bin Umar Al-Hanafy katika kitabu chake kiitwacho Al-Kash-Shaf (J. 2, Uk. 443) kilichopigwa chapa Misri mwaka 1308 A.H., Abu Jaffer At-Tabary mwenye Kitabu kiitwacho "Tafseer At-Tabary" (J. 28, Uk. 14) kilichopigwa chapa Misri mwaka 1321 A.II.. Muhammad bin Saib Al-Kalbi, katika tafsiri yake, (J. 4:105) iliyopigwa chapa Misri mwaka 1355 A.H., AsSuyooti Ash-Shalli, katika tafsiri yake maarufu AD-DURRUL MAN-THOOR (J. 6, Uk. 185), ALAA-UD-DEEN anayejulikana sana kwa jina la AL-KHAAZIM, katika tafsiri yake maarufu Tafsirul Khazin, au Lubabut-Taaweel wa Maani - Tanzeel (J. 4, Uk. 242), Ibrahim bin Maaqal An-Nasafi Al-Hanafi, katika kitabu chake kiitwacho Madaarikut Tanzeel wa Haqaaiqut-Taaweel kilichopigwa chapa pembezoni mwa kitabu cha tafsiri cha Al-Khazin (J. 4, Uk. 242). Na katika tafsiri hii hasa ametaja kwa urefu kisa cha aya ya "AN-NAJWA" na ameeleza kiasi alichotoa sadaka Ameerul-Mumineen Ali bin Abi Talib (a.s.) alipokwenda kuongea siri na Mtume (s.a.w.w.) baada ya kushuka aya yenyewe na ameeleza maswali kumi aliyouliza Ali kwa Mtume (s.a.w.w.) nayo ni mambo kumi muhimu na maelezo yake yameshatangulia.

Na mwisho wa maneno yake humo amesema hivi. "Alipokwishamaliza Ameerul Momineen Ali bin Abi Talib (a.s.) maswali yake (kwa Mtume (s.a.w.w.) ndipo iliteremshwa aya kufuta (Naskh) amri ya aya hiyo"

HADITHI YA AROBAINI NA TATU

"Kuwapenda Aali Muhammad (s.a.w.w.) ni bora kuliko Ibada"

Katika kitabu cha MANAA-QIB cha Al-Khateeb Al-Muwaffaq bin Ahmad Al-Khawarazmi Al-Hanafi, Uk. 43; imeelezwa hadithi kutoka kwa Naafii ikitokana na Ibn Umar kuwa Mtume (s.a.w.w.) amesema, "Yeyote atakayempenda Ali, Mwenyezi Mungu hukubali swala yake, na saumu yake, msimamo wake (ndani ya swala), humkubalia Dua lake, na yeyote atakayempenda Ali Mwenyezi Mungu atampa kwa kila mshipa ulio ndani ya mwili wake mji katika Pepo (Akhera). Fahamuni! Na yeyote atakayewapenda Aali Muhammad (Ahlul Bait a.s.) atasalimika katika Hesabu na Mizani na Sirati (huko Akhera): Fahamu! Na yeyote atakayekufa katika (hali) ya kuwapenda Aali Muhammad, basi mimi ninamdhaminia kuingia Peponi pamoja na Mitume; Fahamuni! Na yeyote atakayewachukia Aali Muhammad. atakuja siku ya Kiyama hali imeandikwa katika ya macho yake (kuwa) ni mwenye kukupuka) kukata tamaa katika rehema ya Mwenyezi Mungu."

"Hatuna haja ya kutaka kuthibitisha kupendwa kwa Ali (a.s.) au Aali Muhammad (s.a.w.w.) baada ya kuwa Mwenyezi Mungu kishawajibisha na kufaridhisha mapenzi yao juu ya watu wote katika Qurani tukufu, kama alivyosema Subhanahu Wataala, "Waambiye sikutakini malipo yoyote kwenu ila kuwapenda jamaa zangu. Basi jambo linalofaa kutajwa ni kubainisha dalili na thibitisho za kuwapenda na kuwabughudhi kwa hadithi zilizopokewa kutoka kwa Mtume mtukufu (s.a.w.w.)- Miongoni mwa hizo ni ile hadithi iliyotangulia aliyoinakili Al-Khwarazmi Al-Nanafy. Hakika zimepokelewa hadithi nyingi zenye madhumuni ya hadithi hii. Miongoni mwa hadithi hizo ni ile hadithi iliyotangulia tuliyonakili katika hadithi ya thelathini na mbili (32). Na hadithi hiyo na ile iliyonakiliwa mwanzo zatosha.

Hadithi iliyo nzuri mno ni ile hadithi fupi ya Mtume (s.a.w.w.) ambamo amebainisha faida ya kuwapenda jamaa za Mtume (Aali Muhammad s.a.w.w.) katika dunia na akhera. Nayo ni ile hadithi aliyoinakili mwanazuoni Al-Allama Ubaidullaah Al-Hanaty katika kitabu chake Ar-jahul-Mataalib (Uk. 319). Amesema, "Imepokewa hadithi kutoka kwa Ibnu Mas-udi kwamba Mtume (s.a.w.w.) amesema: "Kuwapenda Aali Mohammad (Jamaa za Mtume) siku moja ni bora kuliko kufanya Ibada kwa mwaka mmoja na atakayekufa na katika hali ya kutowapenda hawataingia Peponi."

HADITHI YA AROBAINI NA NNE

"Mtume Muhammad (s.a.w.w.) na Ali (a.s.) wameumbwa kwa Nuru moja"

Katika Manaaqibul Khateeb, Al-Muwaffaq bin Ahmad Al-Khwarazmi Al-Hanafiy (Uk. 47) na katika kitabu chake kingine kijulikanacho kwa jina la MAQ-TALUL Husein (a.s.) J. 1, Uk. 42) kilichopigwa chapa AN-NAJAAFUL ASHRAF amenakili hadithi kutoka kwa Abdullah Bin Umar kuwa amesema "Nimemsikia Mtume (s.a.w.w.) akiulizwa kwamba lugha (sauti) gani alisema naye Mola wako usiku wa Miraji? (Mtume s.a.w.w.) akasema, "Amenisemjga kwa lugha ya Ali Bin Abi Talib. Akanitia moyoni (mpaka) niKasema "Ewe Mola wangu! Wewe ndiye uliyenisemeza au Ali?" Mwenyezi Mungu akasema, "Pwe Ahmad! Mimi niko (lakini kuweko kwangu) si kama vitu vilivyopo, sifananishiwi na watu wala sisifiwi kwa vitu, nimekuumba kutokana na nuru yangu na nimemwuumba Ali kutokana na nuru yako. Basi nikatazama katika siri za roho yako nisimkute (mtu) umpendaye zaidi kuliko AJi Bin Abi Talib, basi nikakusemeza kwa lugha (sauti) ya Ali upate tulizo la roho yako."

Hilo (nililolitoa hapo juu) ndio tamko la Khwarazmi katika Manaqib. Ama tamko lake lililomo katika tarekh kinachojulikana kwa Maqtalul Husein (a.s.) linasema hivi, "Imetokana na AbduJlah Bin Umar kuwa amesema, "Nimemsikia Mtume (s.a.w.w.) wakati alimwuliza: kwa Lugha (sauti) gani aliyosema nawe Mola wako? Mtume (s.a.w.w.) akasema, "Amenisemeza kwa lugha (sauti) ya Ali Bin Abi Talib. Nikaingiwa na hamu (mpaka) nikasema, Ewe Mola (ni we we) uliyenisemeza au Ali? Mwenyezi Mungu akasema "Ewe Ahmad! Mimi niko (lakini kuweko kwangu) si kama viumbe; sifananishwi na watu, na sisifiwi na vyenye kufanana. nimekuumba kutokana na nuru yangu, nikamwumba Ali kutokana na nuru yako; basi nikaangalia katika siri za roho yako. basi sikukuta rohoni mwako mpenzi mno kuliko Ali, basi nikakusemeza kwa lugha (sauti) yake ili upate tulizo la roho yako."

Kwa kuangalia sana matamko hayo mawili, utajua tofauti zilizopo kati yao. Na kuhusu habari zilizopokewa kuwa hakika wao Mtume (s.a.w.w.) na Ali (a.s.) wameumbwa kwa nuru ya Mwenyezi Mungu na hakika nuru yao ni moja, zipo hadithi nyingi sana; wamezikariri wanazuoni wa ki-Sunni, Shafii, na Hanafi na wanazuoni wa Ki-Shia (radhi za Mwenyezi Mungu ziwaendee wote). Miongoni mwao ni mwaazuoni mkubwa Al-Allama Ubaidullah Al-Hanafi katika kitabu chake, "ARJAHUL-MATALIB" (Uk. 459) ambaye ametafsiri hadithi kutoka kwa Husin Bin Ali Bin Abi Talib (a.s.) kutoka kwa baba yake kuwa Mtume (s.a.w.w.) amesema, "Mimi na Ali tulikuwa kwa Mwenyezi Mungu kabla ya kuumbwa Adam (a.s.) kwa miaka elfu kumi na nne. Mwenyezi Mungu alipomwumba Adam (a.s.) akapitisha nuru ile katika mgongo wake. Ikawa Mwenyezi Mungu anaihamisha (ile nuru) kutoka mgongo mmoja hadi mgongo wa pili hadi ikafika mgongo wa Abdul Muttalib, baadaye akaigawa nuru mara mbili. Nusu moja (akaitia) katika mgongo wa Abdullah, na nusu ya pili (akaitia) katika mgongo wa Abi Talib.

Basi Ali ametokana nami na mimi natokana naye; nyama yake ni nyama yangu na damu yake ni damu yangu. Basi atakayempenda (Ali) ndio mpenzi wangu (na mimi) nitampenda. na atakaycmchukia (Ali) ndiye adui yangu (na mimi) nitamchukia." Hadithi hiyo imeelezwa na Ibnu Marduwaihi katika "manaaquib" na vilevile Khwarazmi, Shihabuddini Ahmad, Al-Matarrizi, na Aasimy. Pia katika kitabu hicho hicho UK. 459, amesema: tuKatika riwaya (hadithi) ya Abd-Fathi Muhammad bin Ali bin Ibrahim An-Naseeri (iliyomo) katika Khasaisul-Alawiya" kutoka kwa Salmani kuwa amesema: Nimemsikia Mtume (s.a.w.w.) akisema, "Mimi na Ali tumeumbwa kutokana na nuru iliyo upande wa kulia wa Arshi. Tunamtukuza Mwenyezi Mungu kabla hajamwumba Adam kwa miaka kumi na nne elfu. Mwenyezi Mungu alipomwumba Adam, akatuhamisha miongonrmwa wanaume na matumbo ya wanawakc watukufu hadi kufika katika mgongo wa Abdul-Muttalib. Akatugawa (katika mgongo huo) nusu mbili. Basi nusu moja akaitia katika mgongo wa Abdul-Laahi na ile nusu nyingine akaijalia katika mgongo wa Abi Talib.

Basi kwa nusu ile (iliyoingia kwa Abdallah) nikaumbwa mimi, na Ali akaumbwa kwa ile nusu ya pili (iliyoingia kwa Abi Talib). Akatupatia (Mwenyezi Mungu) majina kutoka majina yake matukufu, basi Mwenezi Mungu ni Mahmud na mimi ni Muhammad, Mwenyezi Mungu ni AL-AALAA na ndugu yangu ni Ali, Mwenyezi. Mungu ni Faatir na binti yangu ni Fatima, Mwenyezi Mungu ni Muhsin na wajukuu zangu ni Hasan na Husein. Basi jina langu likawa katika Utume, na jina lake (Ali) likawa katika ukhalifa na ushujaa. Basi mimi ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, na Ali ni upanga wa Mwenyezi Mungu.

Katika kitabu chetu cha ALI-WAL-WASIYYAH tumcnakili hadithi nyingi zinazohusu Nuru ambayo Mtume (s.a.w.w.) na Binamu Wake Ali (a.s.) wameumbwa nayo.

6

FADHILA ZA SAYYIDNA ALI (A.S)

HADITHI YA AROBAINI NA TANO

"Mtume asisitiza kumpenda Ali na Ahli Bayti"

Katika Kanzul Ummaal (J. 6, Uk. 155) imenakiliwa kutoka AL-MUUJAMUL KABEER cha Tabarani, hadithi nyingine zilizo sahihi kutoka kwa wanazuoni wa hadithi. Miongoni mwa hadithi hizo ni hadithi aliyoikariri kutoka kwa IBNU UMAR, kuwa Mtume (s.a.w.w.) amesema kumwambia Ali, "Ewe Ali, nikuridhishe na ufurahi? Wewe ni ndugu yangu na waziri wangu, utalipa deni langu, utatekeleza ahadi yangu, na utaniondolea jukumu langu. Basi atakayekupenda katika uhai wangu hakika ametekeleza wajibu wake, na atakayekupenda katika uhai wako baada yangu Mwenyezi Mungu atamfanya awe na mwisho (hatima) mwema, yenye Imani. Na atakayekupenda baada yangu bila kupata kukuona, Mwenyezi Mungu atamfanya awe na mwisho (hatima) mwema, na atamlinda siku ya kutisha (Qiyama). Ewe Ali! Na atakayekufa na hali anakubughudhi (basi) atakufa kifo cha ujinga (ukafiri). Mwenyezi Mungu atamchukulia hisabu kwa yale aliyoyafanya katika UISLAM.

Hadithi hii ni sahihi, maana imetangazwa na TABARANI na wengineo, katika AL-MUUJAMUL KABEER. Hadithi hii imechukuliwa katika vitabu vya wanazuoni wa Kisunni, Shafiiy na Hanafiiy. Miongoni mwao ni Abu Naeem Al-Isfahani katika HILYATUL-AW-LIYAA (J. 1, Uk. 86) Ali Al-Muttaqi Al-Hanafiy katika KANZUL-UMMAAL (J. 6, Uk. 155) ambaye ameyachukua kutoka katika AL-MUSTADRAK cha Saheehaini Bukhari na Muslim na kutoka kitabu cha Fadhailu-Sahaba cha Abi Naeem Al-Isfahani. Maneno yenyewe ya hadithi hiyo ni: "Kutoka kwa Zaidi bin Arqa ambaye amesema kuwa Mtume (s.a.w.w.) amesema, "Atakayependa kuishi (kama) maisha yangu na kufa kifo changu na kukaa katika Pepo ya milele, aliyoniahidi Mola wangu, hakika Mola wangu Mtukufu ameotesha miti (Peponi) kwa Qudra yake, basi AMPENDE Ali Bin Abi Talib, hakika yeye (Ali) hatawatoeni kutoka uongofu, na hatawatieni katika upotevu.

Ali Al-Muttaqi Al-Hanafiiy amekariri hadithi nyingine katika KanzuI-Ummaal (J. 6, Uk. 155) yenye maana ya hadithi iliyotajwa (pamoja na tofauti ndogo katika baadhi ya matamko yake) kutoka vitabu vingi kutokana na Mutayri, na Bawardi na Ibn Shaahin, na Ibnu Mundah, na Ziyaad bin Miitraf. Maelezo yake ni kuwa amesema Mtume (s.a.w.w.) "Atakayependa kuishi (kama) maisha yangu na kufa (kama) kifo changu na kuingia katika Pepo, ambayo ameniahidi Mola wangu, miti katika rq yake ameipanda kwa Qudra yake Mola, nayo ni ile Pepo ya milele, basi AMPENDE ALI na dhuria zake baada yake; hakika wao hawatawatoeni kutoka mlango wa uongofu, na hawatawatieni katika mlango wa upotevu".

Sayyid Muhammad Saleh Al-Hanafiy amenakili hadithi katika kitabu chake: "La-Kaw-Kabud-Dur-Riy" (Uk. Ill) kutoka katika "Khulaasatul Manaaquib" kutoka kwa Mtume (s.a.w.w.) kuwa amesema, "Atakayependa kuishi (kama) maisha yangu na kufa (kama) kifo changu na kuingia katika Pepo ambayo ameniahidi Mola wangu, basi amfanye Ali Bin Abi Talib na dhuria zake viongozi wake watakatifu (awakubali) Maimamu wa uongofu. na taa za kiza baada yake (Ali); hakika wao hawatakutoeni kutoka mlango wa uongofu (na hawatakutieni) katika mlango potevu.

Ali Al-Muttaqi Al-Hanafiy ameeleza hadithi katika Kanzul Ummaal (J. 6, Uk. 117) yenye maana ile ile, kutoka kwa Ibnu Abbasi, na humo mna ziada nyingi zilizo muhimu. Naye amenakili kutoka katika AL-MUUJAMUL KABEER cha Tabarani kuwa Mtume (s.a.w.w.) amesema, "Atakayefurahika kuishi maisha yangu, na kufa kifo changu, na kukaa mwenye Pepo ya milele ameipanda (miti) Mola wagu, basi ampende Ali baada yangu. na ampende anayempenda, na awafuate Ahli-Baiti zangu baada yangu. Hakika wao ni dhuria zangu, wameumbwa kutokana na udongo wangu, na wameruzukiwa fahamu zangu na elimu zangu. Basi adhabu iliyo (kali) kwa wanaokanusha utukufu wao katika umati wangu, wanaokata kwao udugu (sila) wangu: Mwenyezi Mungu hatawapa (watu hao) Shafaa."

Hakika Mtume (s.a.w.w.) katika hadithi hii tukufu, ameongeza (amezidisha) amri yake (kwa Umma) juu ya kuwapenda Ahlul-Bait zake na anawaamrisha Umati zake kuwafuata katika mambo ya ulimwengu wao na dini yao, na anataja sababu ya (man; yake kuhusu jambo hilo, (wameruzukiwa fahamu zangu na elimu yangu). Basi anathibitisha Mtume (s.a.w.w.) kuwa hakika wao (a.s.) ndiyo wanaofaa kuwafuata kwa vile wao wamebarikiwa na wanazo fahamu za Mtume (s.a.w.w.) na elimu ake si kwa sababu wao ni jamaa za Mtume (s.a.w.w.). Basi hadithi hii ni kama zile hadithi zinazojulikana kwa majina ya Hadithi ya Thaqalain na Hadithi ya Safina ambamo Mtume (s.a.w.w.) amesema wazi kwamba, hakika uongofu katika mambo yanayohilikisha hapa duniani na akhera unategemea na kushikamana nao, na kupanda jahazi (Safina) ya uongofu kwa kuwafuata wao.

Kwa sababu wao (a.s.) ndiyo hazina ya elimu yake, na ndiyo warithi wa upole wake na ndiyo waongozi wa (mambo) yanayo hitaji Ukhalifa na uongozi. Basi Mtume (s.a.w.w.) amewabainishia na kuwaeleza Masahaba zake, ili wawabainishie Waislamu katika njia ya uongofu na kufuzu mema. (Pia) amewabainishia yanayofaa (katika) mambo yao ya Kiislamu na yanayotia nguvu Uislamu wao kwa maelezo mbali mbali. Miongoni mwa maelezo hayo ni yale yaliyotangulia, nay^ale aliyoyatoa Ali Al-Muttaqui Al-Hanafiy, katika Kanzul Ummaal (J. 6 Uk. 218) kwa kunakili kutoka kitabu cha Tarehe cha (mwanazuoni wa hadithi ya mji wa Shaam) IBNU ASAAKIR. Sasa nakuletea^yaliyomo katika Kanzul Ummaal (J. 6, Uk. 218). Hakika yeye ameipata kwa "njia kutoka kwa Ali (a.s.) kuwa amesema, kuwa Mtume (s.a.w.w.) amesema: "Ewe Ali! Hakika Uislamu uko uchi, nguo yake kumcha Mungu (Taqwa) na nywele zake uongofu, na kipambo chake ni haya, na nguzo yake utawa, na nguvu zake ni amali njema na msingi wa Kiislam ni kunipenda mimi na kuwapenda Ahli Baiti zangu.

HADITHI YA AROBAINI NA SITA

"Ali ni Bwana wa Waarabu"

Katika "As-Sawaaiqul Muhriqa" cha Ibnu Hajar Al-Haytami Ash-Shafii (Uk. 75) na katika "Kanzul Ummaal" cha Ali Al-Muttaqui Al-Hanafi (J. 1, Uk. 157) na katika "Kifaayatut-Taalib" cha Al-Kanji Ash-Shafii (Uk. 91), na katika Yanaa-biul-Mawadah cha Sheikh Sulaiman Al-Kanduzi Al-Hanafii (Uk. 274) o kutokana na maneno ya Ali Muttaqi amepokea hadithi ilioelezwa na Bi. Aisha amesema kuwa Mtume (s.a.w.w.) amesema, "Ewe Aisha! Ukiwa wafurahishwa kumwangalia bwana wa Waarabu. basi mwangalie Ali Bin Abi Talib. (Aisha) akasema, nikasema, "Ewe Mtume (s.a.w.w.) wewe ni bwana wa Waarabu? Mtume (s.a.w.w.) akajibu, "Mimi ni Imamu wa Waislamu na ni bwana wa wacha Mungu.

Hakika hadithi hii wameipokea kundi la Masahaba kwa maneno mbali mbali. Miongoni mwa hadithi hizo ni ile aliyoipokea Al-Kanji Ash-Shafiiy katika Kifaayatut-Taalib (Uk. 91) kutoka kwa Hasan bin Ali, kuwa Mtume (s.a.w.w.) amesema, "Ewe Anas! Nenda ukaniitie bwana wa Waarabu. (Anakusudia Ali Bin Abi Talib) Aisha akasema: "Wewe si Bwana wa Waarabu?

(Mtume) akasema: "Mimi ni Bwana wa watoto wa Adam, na Ali ni Bwana wa Waarabu. (Anas) akasema, Ali alipokuja Mtume (s.a.w.w.) akampeleka (mtu) kwa Ansari (kuwaita); wakaja; Mtume (s.a.w.w.) akawaambia: "Enyi Ansari! Mwaonaje nikujulisheni jambo ambalo mkishikamana nalo hamtapotea baada yake? (Ansari) wakasema: Ndiyo ya Rasulal-Laahi (tujulishe); akasema: "Huyo Ali mpendeni kwa ajili ya kunipenda, na mhishimuni kwa ajili ya heshima yangu; hakika Jibrili ameniamrisha (kuyasema) hayo niliyokuambieni yametoka kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka. Kisha Al-Kanji akasema "Nasema hadithi hii imethibti na ni sahihi, alivyoithibitisha Imam wa hadithi Sulaiman bin Ahmad Tabarani katika kitabu chake Mujamul Kabeer kwa maelezo hayo hayo tulivyotoa.

Kisha akatoa hadithi nyingine yenye maana hiyo hiyo kutoka kwa Ibnu Abi Layla (kutoka kwa Husein Bin Ali (a.s.) kuwa amesema kuwa Mtume (s.a.w.w.) amesema, "Ewe Anas! Hakika Ali ni Bwana wa Waarabu"; wakasema, wewe siyo Bwana wa Waarabu? (Inaendelea kama ilivyotangulia hadithi iliyonakiliwa kutoka kwa Imam Hasan Bin Ali (a.s.). Kisha al-Kanji akascma: Hadithi hii ni mashuhuri. Na katika Kanzul Ummaal (j. 6, Uk. 400) amenakili hadithi Aitoka kwa Bi. Aisha kuwa amesema: Nilisema "Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, wewe ndiyo Bwana wa Waarabu? Akasema mimi ni Bwana wa watoto wa Adam (a.s.) na Ali ni Bwana wa Waarabu. Na katika kitabu hicho hicho amekariri hadithi iliyopita kutoka kwa Hasan bin Ali (a.s.) na katika kitabu cha Hilyatul Awliyaa cha Abi Nairn Isfahan!, maneno yake ni sawa na maneno ya Al-Kanji Ash-Shafliy ila yeye amesema Mtume (s.a.w.w.) amesema hivi: mwaonaje niwajulisheni jambo ambalo mkishikamana nalo hamtapotea baada yake abadan? Wakasema (Ansari); Ndiyo tujulishe. Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Mtume (s.a.w.w.) akasema, "Huyu Ali mpendeni kwa mapenzi yangu (mpaka mwisho wa hadithi).

HADITHI YA AROBAINI NA SABA

"Ali na Fatima walikuwa wakipendwa sana na Mtume"

Katika Kifaayatut-Taalib (Uk. 119) cha Al-Kanji Ash-Shafiy imenakiliwa hadithi kutoka kwa Ataa kuwa amesema kuwa: "Nilimuuliza Aisha kuhusu Ali Bin Abi Talib, akasema: "Yeye (huyo) ni mbora wa viumbe, hamtilii shaka ila kafiri". Hadithi hii pia ameitaja Hafidhi Bin Asaakir katika habari ya maisha ya Ali (a.s.) katika kitabu chake cha Taareekhul-Kabeer.

Hadithi hii imeikuta katika Tareekhul Kabeer cha Ibnu Asakir (kilichopo katika Maktaba ya Ameerul Monnineen (a.s.) katika Najaf-Iraq) na hadithi hii ya Aisha ameikariri Sheikh Sulaiman Al-Kanduzi Al-Hanafiiy katika Yanaabiul Mawaddah (Uk. 246). Al-Kanji Shafiy katika Kifaayatut-Taalib ameikariri hadithi hiyo kwa njia mbali mbali na kutoka Masahaba wengi mbali na Aisha. Katika Tiao ni Ameerul Momineen Ali Bin Abi Talib (a.s.) na Jaabir .na Hudhaifa na wengine. Maneno yao katika hadithi yatofautiana. Maneno ya Ameer (a.s.) ni hivi: "Asiyesema kuwa Ali ni Mbora wa viumbe, basi hakika amekufuru." Na kwa maelezo ya Hudhaifa ni hivi: "Nimemsikia Mtume (s.a.w.w.) anasema, "Ali ni Mbora wa viumbe, atakayekataa basi hakika amekufuru. Na riwaya ya Jabir ni sawa na ya Hudhaifa ila neno moja tu ni "Fe" iliyoko kabla ya Man). Maneno ya Jabir kutokana na upokezi wa Muhaddithu Shaami Ibnu Asakir, kutoka kwa Jabir kuwa: "Huyo (Ali) ni Mbora wa viumbe, hamchukii mtu yeyote ila Kafiri.

Sheikh Manawi ametoa hadithi hii katika kitabu chake Kanzul Haqaaiq, kilichopigwa chapa pembezoni mwa kitabu cha Al-Jaamius-Sagheer cha Suyuti (J. 2, Uk. 20, 21) kutoka kitabu cha Sunan Abi Yaal kutoka kwa Mtume (s.a.w.w.) kuwa hakika yeye (Mtume s.a.w.w.) amesema, "Ali ni Mbora wa viumbe, atakayetia shaka (katika jambo hilo) amekufuru." Hadithi hiyo hiyo imekaririwa katika Tareekh Al-Khateeb na Al-Baghdadi kuwa: "Ali ni mbora wa viumbe atakaye kataa basi hakika amekufuru." Ali Al-Muttaqi ameeleza hadithi hiyo katika Kanzul Ummaal (J. 6, Uk. 159) kutoka kwa Ali Bin Abi Talib na Ibnu Abbasi na Ibnu Mas-udi, na Jabir. Lakini maelezo ya hadithi kutoka kwa Jabir ni sawa na tuliyoyakuta katika Kanzul Haqaiqi cha Manawi. Na maneno na maelezo ya Ameerul Momineen (a.s.) na Ibn Masudi na Ibn Abbasi ni sawa na tuliyonakili kutoka Kifaayatut-Taalib. Kwa hakika baadhi ya (Ulamaa) wanazuoni wa Kishia.... Maneno ya hadithi hii katika kitabu maalum kiitwacho Nawaadirul Athar fee Aliyin Kharil Bashar kilichopigwa chapa Tehran (Iran) mwaka 1369 A.H.

HADITHI YA AROBAINI NA NANE

"Bi Aisha athibitisha mapenzi ya Mtume kwa Ali na Fatima"

Katika Kifaayatut-Taalib (Uk. 184) imeelezwa hadithi kutoka kwa Shuraih bin Hani, kutoka kwa baba yake kutoka kwa Aisha kuwa amesema, Mwenyezi Mungu hakuumba kiumbe aliyekuwa mpenzi mno kwa Mtume (s.a.w.w.) kuliko Ali Bin Abi Talib. Kisha akasema hadithi hii ni hasan (Sahihi) ambayo imepokewa na Ibnu Jareer katika kitabu chake cha Manaaqib na Ibnu Asakir ameinakili hadithi hiyo katika maelezo ya maisha ya Ali (a.s.).

Al-Hakim An-Nishapuri katika kitabu chake Mustadrak As-Sahee-hain (J. 3, Uk. 154) amekariri hadithi yenye maana ile ile lakini humo mna maneno zaidi, na hayo ndiyo aliyoyapata kutoka kwa Jamii bin Ibnu Umair ambaye amesema: Niliingia na mama yangu kwa Aisha, nikamsikia kwa nje ya pazia (nyuma) anaulizwa kuhusu Ali. Akasema, unaniuliza (habari za) mwanamume, Wallahi simjui mtu (mwanamume) yeyote aliyekuwa mpenzi mno kwa Mtume (s.a.w.w.) kuliko Ali na (simjui) katika ardhi mwaamke aliyekuwa mpenzi mno kwa Mtume (s.a.w.w.) kuliko mkewe Ali, Fatima (a.s.). Kisha akasema hadithi hii ni sahihi yenye uthibitisho kamili (lakini) kina Bukhari na Muslim hawakuinakili.

Muhibbuddeen At-Tabari ameikariri hadithi katika Dhakhairul Uqba (Uk. 35) na maelezo yake kutoka kwa Aisha kwamba yeye aliulizwa ni mtu gani aliye mpenzi mno wa Mtume (s.a.w.w.)? Akasema, "Fatima; akaulizwa tena, katika wanaume Je? Akasema, "Mumewe; nilivyojua ni mwingi wa kufunga na kuswali. Ameyaeleza Tirmidhi katika Saheeh yake (J. 2, Uk. 475). Ibnu Ubaid ameinakili hadithi hiyo hiyo na baada ya mwingi wa kuswali amezidisha maneno mwenye kauli ya kweli Buraydah amesema kuwa Fatima alikuwa kipenzi mno wa wanawake kwa Mtume (s.a.w.w.) na kwa waaume ni Ali. Hadithi hiyo ameikariri Abu Umar huo ndio mwisho wa maelezo ya Tabari katika (Dhakhair).

Al-Haakim ameeleza hadithi hii katika Mustadrak Saheehain (tazama J. 3, Uk. 157), Ibnu Atheer katika Ussdul Ghaba (J. 3 Uk. 522), Ibnu Abdil Bar katika Istlaab (J. 2, Uk. 772) Tirmidhi katika Saheeh yake (J. 2, Uk. 471), katika babu kuhusu sifa za Usama; na Khawarazmi Al-Hanafiiy katika Maqtal Al-Husein (a.s.) (J. 1, Uk. 57). Ali-Muttaqi Al-hanafi, katika Kanzul Ummaal (J. 6, Uk. 450). Hadithi hiyo imechukuliwa kutoka katika vitabu vya wanazuoni wa Kisunni.

HADITHI YA AROBAINI NA TISA

"Ali alikuwa mtu wa mwisho kuonana na Mtume (s.a.w.w.)"

Katika Kifaayatut Taalib (Uk. 133) imeelezwa hadithi kwa Aisha kuwa Mtume (s.a.w.w.) alisema (wakati) Mtume (s.a.w.w.) alipokuwepo nyumbani mwaka (Aisha) ilipomkaribia mauti): Niitieni mpenzi wangu. Nikamwita Aba Bakri, akamwangalia (kisha) akarudisha (akaweka) kichwa chake. Kisha akasema: Niitieni kipenzi changu, nikamwitia Umar, alipomwangalia tu akarudisha kichwa chake. Kisha alisema: Niitieni niitieni kipenzi changu. (Mimi nikasema: upotovu wenu, niitieni Ali, naapa kwa Mwenyezi Mungu hamkusudii (mtu) mwingine ila Ali. Basi (akaitwa) Ali, alipomwona Ali, Mtume akafunua nguo ambayo ilikuwa juu yake (aliyojifunika), kisha akamtia (Ali) katika ile nguo; akawa amemkumbatia mpaka ikachukuliwa roho yake, na mkono wake (Mtume) uko juu yake Ali."

Hadithi hii ameikariri Al-Kanji, ili kuthibitisha kwamba hakika Ali alikuwa karibu mno kuliko mtu yeyote kwa Mtume (s.a.w.w.) wakati alipofariki dunia. Kisha akasema Al-Kanju nina jambo linalo ni kuwa hakika Ali alikuwa karibu mno kuliko wote kwa Mtume (s.a.w.w.) wakati Mtume (s.a.w.w.) alipofariki. Hadithi hii imetajwa na Abu Yaala Al-Moosali katika Musnad yake, na Imam Ahmad bin Hanbal katika Musnad Mtume (s.a.w.w.) yake. (Kisha akaeleza) hadithi hii kutoka kwa Ummu-Salama ambaye amesema: 'Naapa kwa Mwenyezi Mungu (kuwa) Ali alikuwa mtu wa mwisho aliyeonana na Mtume (s.a.w.w.) katika uhai wake (Mtume s.a.w.w.). Akasema, Mtume (s.a.w.w.) alikuwa anasema, Ali amekuja? Ali amekuja? Mara kwa mara.

Fatima amesema: (Mtume s.a.w.w.) alikuwa amempeleka (Ali) akaulize mahitaji yake. Baada ya muda akaja Ali; nikadhani kwamba yeye (Mtume) anamhitaji Ali, basi tukatoka nje ya nyumba, na tukakaa mlangoni, nikawa karibu nao kutoka mlango, nikamwona Ali akamwangukia (Mtume) akawa anasema nayc kwa siri mpaka Mtume (s.a.w.w.) alipofariki siku hiyo. Basi akawa ndiye wa mwisho kuzungumza na Mtume (s.a.w.w.). Al-Kanji amesema: "Nasema, hadithi hii ameikariri Ahmad bin Hambal katika Musnda yake (J. 6, Uk. 300) Al-Moosali katika Musnad yake amesema kuwa Mtume (s.a.w.w.) alimwangukia Ali. Na Muhibbu Tabary amekariri katika Dhakhairul Uqba (Uk. 72) hadithi ya Ummu-Salama na Aisha na akasema kuwa hadithi hiyo amenakili Ahmad bin Hanbal katika Musnad yake, na maneno ya Muhib Attabari na Al-Kanji ni sawa ila katika baadhi ya sehemu.

HADITHI YA KHAMSINI

"Kuangalia Uso wa Ali ni Ibada"

Katika Kanzul-Ummaal (J. 6, Uk. 152) imekaririwa hadithi kutoka katika kitabu cha Firdausul-Akhabaar cha Daylami, kuwa Aisha amesema kuwa Mtume (s.a.w.w.) amesema: "Kuangalia uso wa Ali ni ibada".

Hadithi hii imekwishatangulia katika hadithi ya pili; nayo ni ile aliyoipokea ABU BAKR kuwa hakika Mtume (s.a.w.w.) amesema: "Kuangalia uso wa Ali ni ibada" Hadithi hii tumeichukua kutoka kitabu cha Al-Bidaya-Wan-Nihaya (J. 7, Uk. 357) na tumetaja kuwa hakika Ibnu Katheer amesema kuwa "Hadithi hii imepokewa na Masahaba wengi." Akawahisabu na kuwataja, kisha, akasema: Katika hao ni Aisha binti Abi Bakr, Jalaalud-Deen As-Suyooti Ashafiiy katika Tareekhul Khulafaa (J. 1, Uk. 96) amekariri hadithi hii inayosema: "Kuangalia uso wa Ali ni ibada." Ibnu Asaakir amekariri hadithi hii inayosema: "Kuangalia uso wa Ali ni ibada." Ibnu Asaakir amekariri hadithi hiyo hiyo iliyoelezwa na Abu Bakr na Uthmani bin Affan, na Maadhi bin Jabal, na Anasi na Thaubani, na Jabir bin Abdullahi, na Aisha.

Na katika Dhakaairul Uqba (Uk. 95) amenakili hadithi kutoka kwa Aisha, na Ibnu Mas-udi na Amri bin Asi, na Jabir na Abi Huraysah. Kisha akasema: Hadithi ya Aisha ameikariri Ibnus Samani katika kitabu chake Al-Muwaafiqa. Na katika Dhkhaairul-Uqba (Uk. 95) pia imo hadithi hii chini ya maelezo kuhusii ibada) kutoka kwa Aisha (R.A.) ambaye amesema: "Nimemwona ABA BAKRI anamwangalia sana usoni Ali, nikasema Ewe baba, nimekuona unaangalia sana uso wa Ali? Akasema, Ewe mwanangu nimemsikia Mtume (s.a.w.w.) anasema. "Kuangalia uso wa Ali ni ibada" Hadithi hiyo ameinakili Ibnu Sammani katika kitabu chake Al-Muwafiqa. Humo amesema kuwa Ibnu Mas'ud amesema: "Kuangalia uso wa Ali ni Ibada." Hadithi hiyo imekariri na Abdul Hasan Al-Harbi kutoka kwa Amr Bin Asi ambaye amepokea kama hivyo (hapo juu). Vile vile Al Abhari. Jabir amesema kuwa Mtume (s.a.w.w.) alimwambia Ali, nenda ukamtazame Imraan bin Haseen kwani yeye ni mgonjwa. (Ali) akaenda (huko) alikuwako Maadhi na Abu Haraira; basi. Imrani akawa anamwangalia sana Ali. Maadh akamwuliza kwa nini wamwangalia sana (Ali)? Akasema: Nimesikia Mtume (s.a.w.w.) anasema "Kumwangalia Ali ni ibada." Maadh akasema: Na mimi pia nimesikia (hadithi hiyo) kwa Mtume (s.a.w.w.) na Abu Huraira akasema na mimi pia nimeisikia kwa Mtume (s.a.w.w.).

Hadithi hiyo ameieleza Ibnu Abil-Furat. Na katika "Taarekhul kabeer cha Ibnu Asakir, kilichoko katika Maktaba ya Imaam Ameerul-Mumineen (a.s.) huko An-Najaf Al-Ashraf (Iraq) katika (Uk. 19) amekariri kutoka kwa Ibn Abbas kuwa Uthmani bin Affuni alikwenda kwa Ali na akamtaka Ali aende kwake na Ali akaenda, basi akawa Uthman anamwangalia sana. Ali akamwambia una nini waniangalia mno? (Uthman) akasema: Nimesikia Mtume (s.a.w.w.) akisema: "Kumwangalia Ali ni ibada"

Tunamaliza mukhtasari huu kwa hadithi ya "Kumwangalia Ali (a.s.)" iliyopokewa na Masahaba wengi watukufu, mwanzo wao ni Ameerul- Mumineen Ali bin Abi Talib, tena Ibnu Abbas, tena Abu Bakr na Umar, Uthman, na Thauban, na Imran bin Haseen, na Amr bin Asi, na Anasi bin Malik, na Jabir bin Abdillahi, na Abu Dhari, na Abu Huraira, na Abud-Dardai, na Abu Saeed al Khudri, na Wathila bin Al Asqa, na Maadh bin Jabal na Abdalla bin Masudi na Aisha.

Mwisho tunaomba rehema na amani zimwendee Mtume wake Muhammad Mtukufu, Al-Mustafa (s.a.w.w.) na Aali zake waongofu na sahaba zake watakatifu, ambao wametuhifadhia mambo waliyosikia kwa Mtume (s.a.w.w.) na wakayafikisha kwa waliofuata (Taabi-ina) na wakafuta maamrisho yake na wakaacha makatazo yake, na hao ndiyo wenye kufuzu.

13lllMuharram, 1391

11 Machi, 1971

MWISHO