TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA NANE Juzuu 8

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA NANE0%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA NANE Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: tafsiri ya Qurani

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA NANE

Mwandishi: Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 11503
Pakua: 1943


Maelezo zaidi:

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 17 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 11503 / Pakua: 1943
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA NANE

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA NANE Juzuu 8

Mwandishi:
Swahili

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA NANE

IMEANDIKWA NA: SHEIKH MUHAMMAD JAWAD MUGHNIYYA

IMETAFSIRIWA NA: SHEIKH HASAN MWALUPA

IMEHARIRIWA NA: USTADH ABDALLAH MOHAMED

IMEPANGWA KATIKA KOMPYUTA NA: UKHT PILI RAJABU

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu

UTANGULIZI WA MCHAPISHAJI

Kitabu hiki kilichoko mikononi mwako hivi sasa ni juhudi ya miaka mingi sana ya watu waliojitolea kuona kazi hii imefanikiwa bila ya kumsahau Marhum Abu Muhammad wa London.

Kama lilivyo jina la Tafsiri yenyewe ndivyo ilivyo Tafsiri yenyewe ambayo mwanachuoni huyu mahiri kabisa aliyeifafanua ni mtu aliyebobea katika fani zote ambazo mfasiri (Mfafanuzi) anatakiwa awe nazo. Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya ameonesha cheche zake katika vitabu vingi alivyoviandika katika maudhui mbali mbalimbali na hivyo kujipatia wasomaji wengi sana.

Msomi huyu, mwenye fikra huru na anayetetea kile anachokiamini, ni mtu mwenye mawazo mapana na kuyaangalia mambo kwa undani sana, kipaumbele chake ni katika maslahi ya umma huu na amejaribu sana kwenda na wakati.

Sifa kubwa pekee ya mwanachuoni huyu ni kuwa yeye hakujihusisha sana na kung'ang'ania madhehebu fulani tu, labda hii yatokana na wadhifa wake wa ukadhi aliokuwa nao katika nchi ya Lebanon ambayo ina madhehebu mengi, ambapo sula la madhehebu ni nyeti nchini humo, hata hivyo yeye aliweza kuamua matatizo ya watu kwenye ofisi yake kulingana na madhehebu yao pale walipomwendea, hiyo ilimsaidia sana hata kuweza kutoa kitabu kitwacho 'Al-Fiqh a'laa madhaahabil-khamsah' (Fikhi ya madhehebu matano) yaani ya Hanafi, Maaliki, Shafi, Hambali na Shia (ambacho twataraji kitatoka hivi karibuni Inshaallah).

Jambo lililotupa msukumo wa kukifasiri kitabu hiki kwa lugha ya Kiswahili ni zile faida nyingi atakazozipata msomaji na kujua mambo mengi na ya ajabu yaliyo mapya kwake ambayo si rahisi kuyapata kwa wafasiri wengine.

Msomaji atapata faida katika fani za Sayansi, Siasa, Historia, Mashairi, visa vizuri, na Saikolojia miongoni mwa mengine; ndiyo maana msomaji atashangaa kidogo anapoisoma Tafsiri hii atakapoona mwandishi amewataja na kuwanukuu watu kama kina Mfalme Edward, wanasyansi kama kina Enstein, Charlie Champlin (Mchekeshaji maarufu), na wengineo, hali inayoifanya tafsiri hii kuwa ni ya kipekee kabisa.

Mtindo alioutumia mwandishi ni sahali uliokusudiwa watu wa tabaka mbalimbali, wanavyuoni na watu wa kawaida.

Nia yetu ni kukigawanya kitabu hiki bure lakini tumelazimika kukiuza kwa bei nafuu ili kurudisha gharama za uchapishaji.

Mwisho : Shukrani kubwa iwaendee bila ya kuwataja watu waliojitolea usiku na mchana, jopo la wafasiri, wahariri, wachapaji, waliotupa moyo na kutoa maoni yao na walioisimamia ili kuhakikisha kwamba kitabu kimemfikia msomaji.

MAKOSA YA CHAPA

Sikumbuki kama nimewahi kusoma kitabu kilichotoka kupigwa chapa, cha zamani au cha sasa, bila ya kukuta makosa ya chapa, Nafikiri sitasoma kitabu kisichokuwa hivyo. Nimejaribu sana kuliepuka hilo katika tungo zangu, lakini sikufanikiwa.

Nilikuwa sifikirii kama ninaweza kuona makosa haya katika maandishi ya msahafu mtukufu, kama yale yaliyo katika baadhi ya chapa; kwa mfano neno yabswutu kwa swad, badala ya yabsutu kwa sin, na katika chapa ya Tafsir Arrazi ya Misr ya mwaka 1935, Sura ya (2:146). Imeandikwa La Ya'alamuun, (hawajui) badala ya Ya'alamuun (wanajua), Mfano wa makosa haya hausameheki.

Katika Tafsir Al-Manar, chapa ya Pili, sura (5:212), imeandikwa "Fawqahum ila yawmil qiyama” badala ya “Fawqahum yawamal qiyama",Hatuwezi kusema kosa hili ni kubwa zaidi kuliko lile.

Lakini mkosaji atatuletea udhuru kwa msemo mashuhuri huko kwetu jabal amail 'Makosa ya chapa.'

Katika Tafsiri Majmau chapa ya Urfan, Sura (46:15), imeandikwa: " Hatta idha balagha arbai' na sanah badala ya: Hattaidha balagha ashuddahu arbai ' na sanah"

Kusema hivi sio kama ninajitetea kutokana na makosa ya chapa atakayoyakuta msomaji katika kitabu hiki, ijapokuwa naomba msamaha kama litatokea hili, lakini makusudio yangu hasa ni kumwambia yule atakayefungua macho yake kwenye makosa ya matamko na kuufungia macho uzuri wa maana.

Vilevile ninamwambia yule ambaye siku moja aliniambia: "Vitabu vyako vimejaa makosa ya chapa, kama kwamba hakuna kitu chochote katika vitabu hivyo isipokuwa makosa ya chapa tu. Wote hao ninawaambia: Mungu awasamehe na aniongoze mimi na nyinyi.

Vyovyote iwavyo, mimi ninaomba msamaha kutokana na makosa ya kifikra na ya chapa. Anasema Amirul Muminiin(a.s) :"Watu wote ni wapungufu wenye kuchanganyikiwa, isipokuwa yule aliyehifadhiwa na Mwenyezi Mungu."

Na Mwenyezi Mungu (s.w.t) ndiye mwenye jukumu la kunikubali- ayale niliyoyapatia na kunisamehe niliyakosea, kwa jaha ya Mtume na kizazi chake, ziwashukie rehema na amani (Amin).

MUHAMMAD JAWAD MUGHNIYYAH

1

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA NANE

Muendelezo Wa Sura Ya Sita: Al-An'am

وَلَوْ أَنَّنَا نَزَّلْنَا إِلَيْهِمُ الْمَلَائِكَةَ وَكَلَّمَهُمُ الْمَوْتَىٰ وَحَشَرْنَا عَلَيْهِمْ كُلَّ شَيْءٍ قُبُلًا مَّا كَانُوا لِيُؤْمِنُوا إِلَّا أَن يَشَاءَ اللَّـهُ وَلَـٰكِنَّ أَكْثَرَهُمْ يَجْهَلُونَ ﴿١١١﴾

111.Na lau kama tungewateremshia Malaika, na wafu wakazungumza nao, na tukawakusanyia kila kitu ana kwa ana, wasingeliamini ila atake Mwenyezi Mungu, Lakini wengi wao wamo ujingani.

وَكَذَٰلِكَ جَعَلْنَا لِكُلِّ نَبِيٍّ عَدُوًّا شَيَاطِينَ الْإِنسِ وَالْجِنِّ يُوحِي بَعْضُهُمْ إِلَىٰ بَعْضٍ زُخْرُفَ الْقَوْلِ غُرُورًا وَلَوْ شَاءَ رَبُّكَ مَا فَعَلُوهُ فَذَرْهُمْ وَمَا يَفْتَرُونَ ﴿١١٢﴾

112.Na kama hivyo tukamfanyia kila Nabii adui, mashetani watu na majini. Baadhi yao wanawapa wenzao maneno ya kupambapamba kuwahadaa. Na kama Mola wako angelitaka wasingeliyafanya. Basi waache na wanayoyatunga.

وَلِتَصْغَىٰ إِلَيْهِ أَفْئِدَةُ الَّذِينَ لَا يُؤْمِنُونَ بِالْآخِرَةِ وَلِيَرْضَوْهُ وَلِيَقْتَرِفُوا مَا هُم مُّقْتَرِفُونَ ﴿١١٣﴾

113.Na ili zielekee hayo nyoyo za wale wasioamini akhera, nao wayaridhie na ili wayachume wanayoyachuma.

AINA YA WATU AYA

Aya 111 – 113

MAANA

Na lau kama tungewateremshia Malaika, na wafu wakazungumza nao, na tukawakusanyia kila kitu ana kwa ana, wasingeliamini ila atake Mwenyezi Mungu.

Tumesema katika Tafsir ya Aya iliyotangulia kuwa jamaa katika washirikina walimtaka Mtume(s.a.w.w) awaletee muujiza maalum; na kwamba waumini walitamani lau Mwenyezi Mungu angeliitikia maombi yao; na Mwenyezi Mungu akawajibu waumini kwa kauli yake: “Na ni kitu gani kitakachowatambulisha ya kuwa zitakapowafikia hawataamini?”

Baada ya kuishiria yote hayo, Mwenyezi Mungu Mtukufu amemfafanulia Mtume wake mtukufu, kwamba hawa washirikina ambao wamekutaka waliyoyataka katika miujiza, hawatakuamini kwa hali yoyote; hata kama tutawateremshia Malaika kutoka mbinguni, na tukawafufulia wafu wakashuhudia kwa lugha fasaha ya Kiarabu kuwa wewe ni Mtume, bali hata kama utakushuhudia ulimwengu ardhi yake na mbingu yake, wasingelikusadiki wala kukufuata ‘ila atake Mwenyezi Mungu;’ yaani Mwenyezi Mungu awalazimishe wakuamini wewe kwa nguvu.

Unaweza kuuliza : Je, kukadiria huku ni sawa?. Na je aina hii ya watu inaweza kupatikana, katika hali ya kawaida?. Itakuwaje kikundi kidogo kiukadhibishe ulimwengu na vilivyomo? Je, inawezekana mtu asiamini masikio yake na macho yake, kwa kuwaona wafu wanafufuka kutoka katika makaburi yaliyochakaa maelefu ya miaka na waseme. ‘Hapana mola isipokuwa Mwenyezi Mungu (na) Muhammad ni mjumbe wa Mwenyezi Mungu;’ wasikie wanyama na ndege na samaki na miti na nyota zote, zikinadi shahada mbili; inawezekana kweli aweko mtu atakayekadhibisha miujiza yote hii? Si ajabu hiyo?

Jibu : Kukadiria hivi si sawa, bali ni muhali kwa wale wanaoathirika na haki na dalili yake, na wanaokwenda pamoja na wahyi wa mantiki ya kiak- ili na umbile la Mwenyezi Mungu alilowaumbia watu. Kwa sababu miu- jiza hii ni dalili mkato isiyokuwa na shaka yoyote.

Ama kukadiria huku kwa watu ambao hisia zao zote zinatawaliwa na masilahi mahususi na kuyaona kuwa ndio akili, ndio umbile na ndiyo haki na uadilifu, basi ni sahihi. Kwa sababu aina hii ya watu ipo, nao ni wakoloni na walanguzi na wengineo mfano wao, ambao wanaishi kwa unyang’anyi na ufisadi.

Wale wanaoona ajabu kukadiria huku hawaitambui hali halisi ya kundi hili, na wamechanganya baina ya mantiki ya kiakili na ya yule mwenye kuongozwa na manufaa.

Akili kwa maana ya akili ni ile tu iliyo mwongozi, anayeamrisha na kukataza; wala haimsikilizi isipokua anayetafuta haki kwa njia ya haki. Ama chenye kuongoza na kuelekeza kwenye manufaa basi hicho ni manufaa ya kibinafsi.

Hicho peke yake ndicho kinachowaongoza katika mambo yao na silika zao. Ndiyo dini yao, ndiyo akili yao, bali ndiyo utu wao na uhai wao. Kwa sababu hiyo, hakuna mantiki yoyote yanayowafaa isipokuwa nguvu aliyoiashiria Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwa kauli yake: ‘Ila atake Mwenyezi Mungu.’

Lakini wengi wao wamo ujingani

Hawajui kuwa wao ni kikundi kiovu ambacho hakifaliwi na mantiki ya kiakili na maumbile wala na mantiki ya dini na utu; wala kitu chochote ila nguvu na kushindwa. Ni makosa na ni kupoteza wakati kuzungumza na watu hawa kwa lugha ya elimu na ubinadamu.

Na kama hivyo tukamfanyia kila Nabii adui, mashetani watu na majini.

Shetani mtu ni maarufu, ni kila anayehadaa watu kwa kuwaingiza kwenye batili na kuwavisha nguo ya haki. Ama jinni yeye ni katika mambo ya ghaibu ya Mwenyezi Mungu. Nasi tunaamini kijumla na kimsingi; wala hautuhusu ufafanuzi; kwani hatutaulizwa kuhusu yeye; sawa na ilivyo katika Malaika. Wala si ajabu kwa Manabii kuwa na maadui. Kwa sababu, ni kawaida kuwe na uadui kati ya kheri na shari, na baina ya haki na batili.

Unaweza kuuliza : Ikiwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) ndiye aliyewajaalia Manabii wawe na maadui, kama inavyoonyesha katika Aya, kwa nini basi awaadhibu kwa kuwafanyia uadui Mitume? Vilevile vipi ameamrisha kuwafuata Mitume kisha akawafanyia maadui watakaowapinga na kuwahadaa watu kuwapinga na kuupinga Utume wao?

Jibu : Hakika Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewatuma Mitume na akafanya kazi yao ni kulingania Tawhid na uadilifu na kuondoa dhuluma na ushirikina.

Kazi hii, kwa tabia yake, huleta mgongano na vita baina ya Manabii na wale waabudu masanamu na wanyonyaji. Hivyo basi, Mwenyezi Mungu (s.w.t) ni sababu ya kutumwa Manabii, na Manabii ni sababu ya uadui. Kwa kuzingatia haya umenasibishwa uadui kwake kimajazi, Anasema Mwenyezi Mungu akimsimulia Nuh(a.s) :

﴿قَالَ رَبِّ إِنِّي دَعَوْتُ قَوْمِي لَيْلًا وَنَهَارًا ﴿٥﴾ فَلَمْ يَزِدْهُمْ دُعَائِي إِلَّا فِرَارًا﴾

“Ewe Mola wangu! Kwa hakika nimewalingania watu wangu usiku na mchana, lakini mwito wangu haukuwazidishia ila kukimbia” (71: 5 – 6)

Kwa hiyo kukimbia kumenasibishiwa mwito wa Nuh(a.s) , na mwito wa Nuh(a.s) ni amri ya Mwenyezi Mungu. Kwa ufasaha zaidi tupige mfano huu: Mtu amemwachia mwanawe utajiri, na ule utajiri ukamsababishia uadui na husda. Basi kimajazi: “Mzazi wake ndiye aliyempa husda ile mwanawe!”

Baadhi yao wanawapa wenzao maneno ya kupambapamba kuwahadaa.

Maneno ya kupambapamba ni maneno yaliyochanganywa na uwongo. Dhahiri yake ni rehema na ndani yake ni adhabu. Maana ni kuwa waovu wanawatia wasiwasi wenzao kwa mambo ya batili yaliyochanganywa haki, kwa makusudio ya kuhadaa na kuipinga haki na watu wake.

Na kama Mola wako angelitaka wasingeliyafanya.

Dhamir ya wasingeliyafanya inarudia kwenye amali zao mbaya; yaani uadui kwa Mitume na kuambiana wao kwa wao maneno ya kupamba. Maana ni kuwa lau Mola wako angelitaka kuwazuia kwa nguvu kufanya ubaya wasingelikuwa na uadui huo wala kuambiana. Lakini hekima yake imepitisha kuwaacha kama walivyo, wawe na hiyari bila ya kuendeshwa, wapate kuhisabiwa waliyoyafanya na kuadhibiwa wanayostahiki.

Basi waache na wanayoyatunga katika uwongo.

Wajibu wako ni kufikisha na ni juu yetu kuhisabu na malipo.

Na ili zielekee hayo nyoyo za wale wasioamini akhera.

Yaani waovu wanaambiana kauli za kupambapamba ili wazisikilize makafiri na waridhie baada ya kuzisikiliza na wazitumie bila ya kufanya utafiti. Na ili wayachume wanayoyachuma katika maasi na madhambi; na apambanuke mumin na kafir na mwenye ikhlasi na mnafiki.

Kwa ufupi ni kuwa maiblis waovu wanapambapamba kauli ili wawahadae wenye nafsi dhaifu na wapondokee kwao na wachume dhambi.

Amesema Abu Hayani Al-andalusi: “Maneno haya yako katika upeo wa fasihi, kwani mwanzo inakuwa ni hadaa, inayofuatiwa na kupondokea, kisha kuridhia na kuchuma (dhambi); kama kwamba kila moja linasababishwa na lililo kabla yake.

فَغَيْرَ اللَّـهِ أَبْتَغِي حَكَمًا وَهُوَ الَّذِي أَنزَلَ إِلَيْكُمُ الْكِتَابَ مُفَصَّلًا وَالَّذِينَ آتَيْنَاهُمُ الْكِتَابَ يَعْلَمُونَ أَنَّهُ مُنَزَّلٌ مِّن رَّبِّكَ بِالْحَقِّ فَلَا تَكُونَنَّ مِنَ الْمُمْتَرِينَ ﴿١١٤﴾

114.Je, nimtafute hakimu asiyekuwa Mwenyezi Mungu na hali yeye ndiye aliyewateremshia Kitab kinachofafanua. Na wale tuliowapa Kitab wanajua kwamba imeteremshwa na Mola wako kwa haki, Basi usiwe miongoni mwa wanaotia shaka.

وَتَمَّتْ كَلِمَتُ رَبِّكَ صِدْقًا وَعَدْلًا ۚ لَّا مُبَدِّلَ لِكَلِمَاتِهِ ۚ وَهُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ ﴿١١٥﴾

115.Na limetimia neno la Mola wako kwa ukweli na uadilifu. Hakuna wa kubadilisha neno lake. Na Yeye ni msikizi, mjuzi.

وَإِن تُطِعْ أَكْثَرَ مَن فِي الْأَرْضِ يُضِلُّوكَ عَن سَبِيلِ اللَّـهِ ۚ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا الظَّنَّ وَإِنْ هُمْ إِلَّا يَخْرُصُونَ ﴿١١٦﴾

116.Na kama ukiwatii wengi katika waliomo ardhini watakupoteza na njia ya Mwenyezi Mungu. Hawafuati ila dhana na hawakuwa ila wenye kuzua tu.

إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعْلَمُ مَن يَضِلُّ عَن سَبِيلِهِ ۖ وَهُوَ أَعْلَمُ بِالْمُهْتَدِينَ ﴿١١٧﴾

117.Hakika Mola wako anawajua vyema wanaopotea njia yake na anawajua sana wanaoongoka.

NIMTAFUTE HAKIMU ASIYEKUWA MWENYEZI MUNGU

Aya 114 – 117

MAANA

Je, nimtafute hakimu asiyekuwa Mwenyezi Mungu na hali yeye ndiye aliyewateremshia Kitab kinachofafanua?

Aya hii inaambatana na ile Aya ya ugomvi na uadui baina ya Mtume na washirikina ambao walimtaka awaonyeshe muujiza. Maana ni kuwa Mtume(s.a.w.w) aliwaambia washirikina kwamba nyinyi mnatoa hukumu katika kutaka miujiza na mnanipangia mambo, na mimi siwezi kuikiuka hukumu ya Mwenyezi Mungu.

Qur’an imekwisha washukia, inatosha na kutekeleza mnayoyahitajia kujua haki, halali na haramu. Haina mfano wake katika misingi yake na mafunzo yake. Ni yenye kuthibitisha ukweli wake kwa kutumia ufasaha wake ushindao, ina sharia zenye kudumu milele na kutoa habari nyingi za ghaibu. Kwa hiyo, huku kutaka kwenu mambo mengi si lolote ispokuwa ni inadi tu.

Na wale tuliowapa Kitab wanajua kwamba imeteremshwa na Mola wako kwa haki.

Yaani wale wenye insafu katika maulama wa kiyahudi na kinaswara, wana- jua kwa yakini ukweli wa Qur’an na Utume wa Muhammad(s.a.w.w) . Tazama Aya yenye maneno kama haya katika Juz. 2 (2:146).

Basi usiwe miongoni mwa wanaotia shaka.

Wafasiri wengi wamesema kuwa msemo huu (usitie shaka) anaambiwa Mtume na makusudio ni asiyekuwa yeye kwa njia ya fumbo.

Ama sisi tunaona kuwa msemo unaelekezwa kwa Mtume, na yeye ndiye makusudio, pamoja na kujua kuwa Mtume hatii shaka Qur’an, bali ni muhali kwake kutia shaka. Imesihi kuelekezwa msemo kwake pamoja na isma yake, kwa vile unatoka kwa aliye juu (Mwenyezi Mungu) kwenda kwa aliye chini, Hayo tumeyaeleza mara nyingi.

Na limetimia neno la Mola wako kwa ukweli na uadilifu.

Makusudio ya neno la Mola wako hapa ni Qur’an au Uislam ambao umeshinda juu ya dini zote wajapochukia washirikina. Haya ndiyo makusudio kwa ukamilifu. Ama maana ya kwa ukweli na uadilifu ni kuwa Qur’an ni kweli katika kila inayoyasema, na ni uadilifu katika kila inay- ohukumu na kuwekea sharia.

Hakuna wa kubadilisha neno lake.

Kwa sababu ni ukweli na uadilifu na kila ambalo ni ukweli na uadilifu basi ni hali halisi, wala haiwezi kusemwa jambo ni ukweli na uadilifu ikiwa halina msingi halisi. Na msingi huu haubadiliki wala haugeuki; yaani hauepukani na athari na natija iliyopangiwa.

Na yeye msikizi wa wanayoyasemamjuzi wa wanayoyafanya na wanayoyadhamiria.

Na kama ukiwatii wengi katika waliomo ardhini watakupoteza na njia ya Mwenyezi Mungu. Hawafuati ila dhana na hawakuwa ila wenye kuzua tu.

Kila mwenye kushikamana na dini basi huamini kwa imani ya moja kwa moja, na hushikamana nayo kwa upofu, na kila rai anayoiona huona ni kweli, na kwamba mengineyo ni njozi na dhana tu. Kwa hiyo tukizikusanya rai zote na itikadi zote na tukazipima kwa vipimo vya Mwenyezi Mungu, natija ni kuwa watu wengi hufuata dhana za makosa na za uongo.

Kwa ajili hiyo ndipo Mwenyezi Mungu akamwamrisha Mtume wake asiwasikilize watu na kutowaheshimu na ada zao na itikadi zao; na kwamba ni juu yake kufuata yale aliyopewa Wahyi na Mwenyezi Mungu kwa sababu ndiyo njia ya haki na uwongofu.

Ikiwa watu wengi wako kwenye makosa katika rai na dini, basi hakuna kipimo cha kauli zao na hukumu zao kwa uwongofu wa hili na upotofu wa lile. Isipokuwa hukumu katika hilo ni ya Mwenyezi Mungu peke yake; yaani yale aliyoyabainisha katika misingi na uthabiti uliomo katika Kitabu chake chenye hekima.

Haya ndiyo makusudio ya kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

Hakika Mola wako anawajua vyema wanaopotea njia yake na anawajua sana wanaoongoka.

Katika msingi hiyo ya Mwenyezi Mungu inayowapambanua wenye haki na wenye batili ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿ وَمَنْ أَحْسَنُ قَوْلًا مِّمَّن دَعَا إِلَى اللَّـهِ وَعَمِلَ صَالِحًا وَقَالَ إِنَّنِي مِنَ الْمُسْلِمِينَ﴾

“Na ni nani mbora wa kusema kuliko alinganiaye kwa Mwenyezi Mungu, na akafanya amali njema na akasema: Mimi ni miongoni mwa waislamu.” (41:33).

2

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA NANE

فَكُلُوا مِمَّا ذُكِرَ اسْمُ اللَّـهِ عَلَيْهِ إِن كُنتُم بِآيَاتِهِ مُؤْمِنِينَ ﴿١١٨﴾

118.Basi kuleni katika wale waliosomewa jina la Mwenyezi Mungu ikiwa nyinyi mnaziamini ishara zake.

وَمَا لَكُمْ أَلَّا تَأْكُلُوا مِمَّا ذُكِرَ اسْمُ اللَّـهِ عَلَيْهِ وَقَدْ فَصَّلَ لَكُم مَّا حَرَّمَ عَلَيْكُمْ إِلَّا مَا اضْطُرِرْتُمْ إِلَيْهِ ۗ وَإِنَّ كَثِيرًا لَّيُضِلُّونَ بِأَهْوَائِهِم بِغَيْرِ عِلْمٍ ۗ إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعْلَمُ بِالْمُعْتَدِينَ ﴿١١٩﴾

119.Mna nini hamli katika wale waliosomewa jina la Mwenyezi Mungu? Na amewafafanulia aliyowaharamishia isipokuwa vile mnavyolazimika, Na hakika wengi wanapoteza kwa matamanio yao bila ya ilimu, Hakika Mola wako anawajua vyema wanaoru- ka mipaka.

وَذَرُوا ظَاهِرَ الْإِثْمِ وَبَاطِنَهُ ۚ إِنَّ الَّذِينَ يَكْسِبُونَ الْإِثْمَ سَيُجْزَوْنَ بِمَا كَانُوا يَقْتَرِفُونَ ﴿١٢٠﴾

120.Na acheni dhambi zilizo dhahiri na zilizofichikana. Hakika wale wanaochuma dhambi watalipwa yale waliyokuwa wakiyachuma.

وَلَا تَأْكُلُوا مِمَّا لَمْ يُذْكَرِ اسْمُ اللَّـهِ عَلَيْهِ وَإِنَّهُ لَفِسْقٌ ۗ وَإِنَّ الشَّيَاطِينَ لَيُوحُونَ إِلَىٰ أَوْلِيَائِهِمْ لِيُجَادِلُوكُمْ ۖ وَإِنْ أَطَعْتُمُوهُمْ إِنَّكُمْ لَمُشْرِكُونَ ﴿١٢١﴾

121.Wala msile wale wasiosomewa jina la Mwenyezi Mungu kwani huko ni ufasiki, Na hakika mashetani wanawafunza marafiki zao kubishana nanyi. Na kama mkiwatii, hakika mtakuwa washirikina.

BISMILLAH KWA KINACHOCHINJWA

Aya 118 – 121

MAANA

Basi kuleni katika wale waliosomewa jina la Mwenyezi Mungu ikiwa nyinyi mnaziamini ishara zake.

Waarabu wakati wa ujahiliya walikuwa wakila mfu, na wakitaja majina ya masanamu wanayoyaabudu wakati wa kuchinja. Mwenyezi Mungu akaharamisha hilo kwa Wailsamu; akahalalishia kula wanaochinjwa kwa sharti ya kutaja jina Lake na sio jina la mwengine.

Unaweza kuuliza : kuwa kujuzu kula aliyechinjwa, aliyesomewa jina la Mwenyezi Mungu, hakuambatani na kumwamini Mwenyezi Mungu na ishara zake. Ambapo inajuzu kwa kafiri kumla huyo; kama ambavyo kumwamini Mwenyezi Mungu hakuambatani na kula aliyesomewa Jina la Mwenyezi Mungu. Ambapo Mumin anakuwa Mumin hata kama hakumla. Lakini dhahiri ya Aya inafahamisha kuwa kuamini ni sharti la uhalali wa kula chinjo hilo. Kwa sababu maana yake ni, kuleni ikiwa nyinyi ni waumini.

Jibu : Kauli yake Mwenyezi Mungu, ‘Ikiwa nyinyi mnaziamini ishara zake,’ sio sharti la uhalali wa kula chinjo lililosomewa jina la Mwenyezi Mungu, isipokuwa hii ni kuonyesha kuwa anayemtaja asiyekuwa Mwenyezi Mungu kwa chinjo, basi amemfanyia Mwenyezi Mungu mshirika.

Kwa sababu, ameelekeza tendo lake hili kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu, kama walivyokuwa wakifanya washirikina wa Kiarabu; na kwamba mwenye kutaja jina la Mwenyezi Mungu kwa chinjo basi atakuwa amemwamini Mwenyezi Mungu na amemkanushia mshirika, Kwa vile atakuwa amemwelekea yeye tu peke yake.

Mna nini hamli katika wale waliosomewa jina la Mwenyezi Mungu?

Inaonyesha, kutokana na Aya hii, kwamba baadhi ya Waislamu walijizuilia kula chinjo ambalo limesomewa jina la Mwenyezi Mungu kwa kujitatiza; kwamba inakuwaje mtu achinje mnyama kwa mkono wake na ataje jina la Mwenyezi Mungu kisha ale na isijuzu kula mnyama aliyeuliwa na Mwenyezi Mungu ambaye amekufa mwenyewe!

Ndipo Mwenyezi Mungu akalipingia hilo kwa kusema: Mna nini hamli katika wale waliosomewa jina la Mwenyezi Mungu

Na amewafafanulia aliyowaharamishia isipokuwa vile mnavyolazimika.

Kuhusu aliyowafafanulia anakusudia wale aliowaishiria katika Aya 145, katika Sura hii, ambayo itakuja tafsir yake Inshaalah. Pia anaashiria wale waliotajwa katika Juz.2 (2:173).

Tumezungumzia kwa ufafanuzi kuhusu walioharamishwa na hukumu ya aliyelazimika katika Juz.2 (2:173).

Na hakika wengi wanapoteza kwa matamanio yao bila ya ilimu.

Yaani wanahalalisha na kuharamisha kulingana na matamanio yao bila ya dalili. Miongoni mwa hayo ni kuwa washirikina wa Kiarabu walihalalisha kula nyamafu na kuharamisha kula bahira, saiba, wasila na hami. Umetangulia ufafanuzi wa hayo katika Juz.6 (5:3).

Hakika Mola wako anawajua vyema wanaoruka mipaka.

Ambao wanahalalisha na kuharamisha kwa hawaa zao na matamanio yao, Na kwamba atawaadhibu inavyostahiki.

Na acheni dhambi zilizo dhahiri na zilizofichikana.

Makusudio ya dhambi ni kitendo cha haramu kinacholeta dhambi; na dhahiri yake ni kufanya maasi dhahiri; na kufichikana ni kuyafanya kisiri. Mwenyezi Mungu amekataza kufanya maasi yote ya dhahiri na ya batini.

Hakika wale wanaochuma dhambi watalipwa yale waliyokuwa wakiyachuma, katika kufuata matamanio bila ya elimu; wala hawataachwa bure bure bila ya hisabu na adhabu.

Wala msile wale wasiosemowa jina la Mwenyezi Mungu kwani huko ni ufasiki.

Dhamiri ya huko inarudia kula, Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kuhalalishia waliochinjwa kwa jina lake, anaharamisha ambao hawakutajiwa.

Kwa kutegemea hilo, ndipo mafakihi wote, isipokuwa Shafii, wamekonga- mana kuwa mchinjaji akiacha kutaja jina la Mwenyezi Mungu kwa makusudi, basi ni haramu; sawa na nyamafu. Inatosha jina la Mwenyezi Mungu tu, mfano: Allah, Allahu Akbar, Al-Hamdulillah, Bismillah, Lailaha illa Ilah na mfano wake.

Wametofautiana kuacha kusoma jina la Mwenyezi Mungu kwa kusahau. Hanafi, Jaafariya (Shia) na Hanbal wamesema si haramu nyama hiyo. Malik akasema ni haramu na Shafii amesema kuwa akiwacha kusoma jina la Mwenyezi Mungu kwa makusudi pia si haramu, sikwambii tena kusahau.

Na hakika mashetani wanawafunza marafiki zao kubishana nanyi.

Makusudio ya mashetani hapa ni maiblis–watu ambao wanauviringa ukweli na kutunga maneno wanayowahadalia wale wenye akili za juu juu. Kwa mafano, baadhi ya washirikana na maiblis wao walikuwa wakiwaambia wafuasi wao.

Waulizeni Masahaba wa Muhammad, vipi mnakula mnyama mliyemuua nyinyi wenyewe, kumchinja kwa mikono yenu; na wala hamli mnyama aliyeuawa na Mwenyezi Mungu, aliyekufa mwenyewe ambapo aliyeuawa na Mwenyezi Mungu ni bora kuliko mliyemuua nyinyi?

Huo ndio mjadala wao ambao mashetani waliwashauri marafiki zao kwa makusudio ya kuingiza shaka katika nyoyo dhaifu za baadhi ya Waislamu na kuwafitini na dini yao.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) akasema kuwaambia hawa wadhaifu:

Na kama mkiwatii, hakika mtakuwa washirikina.

Yaani mwenye kuwasikiliza washirikina na akahalalisha kula nyamafu, kama walivyohalalisha, basi yeye ni mshirikina kama wao, na hukumu hii haihusiki na kula nyamafu peke yake, bali kila anayepinga hukumu ya sharia akijua kuwa imethibiti, basi huyo ni kafiri.

أَوَمَن كَانَ مَيْتًا فَأَحْيَيْنَاهُ وَجَعَلْنَا لَهُ نُورًا يَمْشِي بِهِ فِي النَّاسِ كَمَن مَّثَلُهُ فِي الظُّلُمَاتِ لَيْسَ بِخَارِجٍ مِّنْهَا ۚ كَذَٰلِكَ زُيِّنَ لِلْكَافِرِينَ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿١٢٢﴾

122.Je, aliyekuwa maiti kisha tukamhuisha na tukamjaalia nuru, hutembea mbele za watu kwayo, mfano wake ni kama yule aliyegizani asiyeweza kutoka humo? Namna hiyo wamepambiwa makafiri waliyokuwa wakiyafanya.

وَكَذَٰلِكَ جَعَلْنَا فِي كُلِّ قَرْيَةٍ أَكَابِرَ مُجْرِمِيهَا لِيَمْكُرُوا فِيهَا ۖ وَمَا يَمْكُرُونَ إِلَّا بِأَنفُسِهِمْ وَمَا يَشْعُرُونَ ﴿١٢٣﴾

123.Na kama hivyo tumejaalia katika kila mji wakubwa wa wakosefu wake ili wafanye vitimbi humo; wala hawafanyii vitimbi isipokuwa wanajifanyia wenyewe, lakini hawatambui.

وَإِذَا جَاءَتْهُمْ آيَةٌ قَالُوا لَن نُّؤْمِنَ حَتَّىٰ نُؤْتَىٰ مِثْلَ مَا أُوتِيَ رُسُلُ اللَّـهِ ۘ اللَّـهُ أَعْلَمُ حَيْثُ يَجْعَلُ رِسَالَتَهُ ۗ سَيُصِيبُ الَّذِينَ أَجْرَمُوا صَغَارٌ عِندَ اللَّـهِ وَعَذَابٌ شَدِيدٌ بِمَا كَانُوا يَمْكُرُونَ ﴿١٢٤﴾

124.Na zinapowafikia ishara husema: Hatutaaamini mpaka tupewe sawa na yale waliyopewa Mitume wa Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu ndiye Mjuzi zaidi wa kujua mahali anapoweka ujumbe wake. Itawafika wale waliokosea dhila inayotoka kwa Mwenyezi Mungu na adhabu kali kwa sababu ya vitimbi walivyokuwa wakivifanya.

KUMHUISHA MAITI

Aya 122 – 124

MAANA

Je, aliyekuwa maiti kisha tukamhuisha na tukamjaalia nuru, hutem- bea mbele za watu kwayo, mfano wake ni kama yule gizani asiyeweza kutoka humo?

Huu ni mfano alioupiga Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa kulinganisha baina ya mumin na kafiri. Ufafanuzi wake ni kuwa, kuwalinganisha wawili hao ni sawa na kulinganisha mauti na uhai. Na mwanga na giza. Kafiri ni maiti akiamini hufufuliwa upya na kurudiwa na uhai na imani yake ni nuru anayokwenda nayo katika uhai wake.

Anayebakia kwenye ukafiri na shirki ni kama anajikokota gizani, anakwenda bila ya uongozi na haimfikii kheri yoyote katika maisha yake yote.

MWENYE KUULIZWA NA MUULIZAJI MKUU

Mtu anaweza kusema kuwa : Aya imefananisha imani na uhai; na ukafiri na mauti; ingawaje makafiri na walahidi, katika zama hizi, wanaishi maisha ya anasa na wenye utajiri zaidi kuliko waumini na wenye kuabudu?

Jibu : Makusudio ya uhai katika Aya hii sio kuishi mtu katika neema na anasa, akawa anakula vizuri, kuvaa nguo za thamani na kunywa vinywaji vitamu. Hakika anasa hazihusiani na ukafiri wala imani. Kama ni hivyo waumini wa Mashariki na Magharibi wangelikuwa sawa katika maendeleo na uchumi mzuri, vilevile walahidi na makafiri.

Hali nzuri ya maisha ina sababu na mambo yanayoambatana nayo ambayo hayafungamani na chochote katika imani au ukafiri. Isipokuwa makusudio ya uhai, katika Aya hii, ni imani na hisia za kidini zinazompa mtu msukumo wa kutekeleza wajibu, akiwa ni mtu atakayeulizwa kuhusu mwenendo wake, atahisabiwa na kulipwa thawabu kwa wema wake, na adhabu kwa uovu wake.

Lau mtu angelikuwa si mwenye kuulizwa chochote, ingelikuwa sharia na kanuni ni maneno tu, yasiyokuwa na maana yoyote. Na tukipitisha kuwa mtu ataulizwa wala hataachwa bure bure, basi itatulazimu tupitishe kwam- ba yeye ataulizwa mbele ya yule ambaye

﴿ لَا يُسْأَلُ عَمَّا يَفْعَلُ وَهُمْ يُسْأَلُونَ﴾

“Haulizwi anayoyafanya, na wao ndio wanaoulizwa” (21:23)

Lau muulizaji huyu anaulizwa, basi ingelipaswa kupatikana atakayemuuliza, na kuendelea hivyo hivyo bila mwisho.

Mwenye kukanusha kuweko muulizaji mkuu kabisa ambaye huuliza na haulizwi, basi atakuwa amekanusha maulizo; Kwa sababu hakuna maulizo bila ya muulizaji, Na mwenye kukanusha maulizo amekanusha maisha ya kijamii.

Unaweza kusema : Ndio mtu ataulizwa, lakini si lazima muulizaji awe Mwenyezi Mungu; watu wanaweza kuchagua kundi (kamati) ambalo litauliza watu.

Nasi tutauliza je kundi hilo likikosea, liulizwe na lihukumiwe na nani? Ikijibwa ni dhamir.

Tutasema :Kwanza , dhamir ni jambo la kimaana si la kidhati.

Pili , dhamiri anayo kila mtu, kwanini huyu aache dhamiri yake afuate ya mwingine?

Kwa hiyo, basi hakuna muulizaji asiyeulizwa ila Mwenyezi Mungu peke yake. Mwenye kumwamini Mwenyezi Mungu akailazimisha nafsi yake kufuata sharia za Mwenyezi Mungu na hukumu zake, basi atakuwa na busara ya mambo yake, itikadi yake na tabia zake. Vinginevyo atakuwa kama aliye gizani asiyeweza kutoka.

Namna hiyo wamepambiwa makafiri waliyokuwa wakiyafanya.

Yaani kama waliyvopambiwa waumini amali zao, vilevile washirikina wamepambiwa amali zao. Tofauti ni kuwa wao wamepambiwa kinyume na hali halisi, wamepambiwa, kimawazo na kinjozi tu.

Na kama hivyo tumeajaalia katika kila mji wakubwa wa wakosefu wake.

Makusudio ya mji ni kila jamii (mkusanyiko) wa watu, wachache au wengi. Maana ni kuwa: Ewe Muhammad kama ambavyo wanapatikana katika jamii yako viongozi wa waovu wanaofanya vitimbi na kuifanyia uadui dini ya Mwenyezi Mungu, vilevile katika jamii zilizotangulia walikuwapo; na hivi sasa pia wako viongozi wanaowafanyia vitimbi watu wao na kuwa katika msimamo wa kuifanyia uadui haki na wenye haki.

Unaweza kuuliza : Dhahiri ya Aya hii inafahamisha kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) ndiye aliyewafanya wakubwa kuwa waovu kwa watu wa haki, na tunajua kuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu hukataza vitimbi na uovu; je, kuna taawili gani hapa?

Jibu : Makusudio ya kunasibishwa kwake huku Mwenyezi Mungu Mtukufu, ni kuashiria kwamba matakwa ya Mwenyezi Mungu yamepitisha kuwa desturi ya jamii iwe kwenye misingi ya kupingana baina ya wenye haki na wenye batili, baina ya viongozi wenye kufanya uadui na wenye kufanyiwa uadui.

Hakuna kimbilio la kuepuka mgongano huu ila kumalizwa waovu; na hapana budi kutimia hilo na kutukuka neno la haki mikononi mwa wanaolingania uadilifu na utengenevu; hata kama batili itakuwa kubwa kiasi gani. Hilo amelisajili Mwenyezi Mungu (s.w.t) katika Kitabu chake, aliposema:

﴿اسْتِكْبَارًا فِي الْأَرْضِ وَمَكْرَ السَّيِّئِ وَلَا يَحِيقُ الْمَكْرُ السَّيِّئُ إِلَّا بِأَهْلِهِ فَهَلْ يَنظُرُونَ إِلَّا سُنَّتَ الْأَوَّلِينَ فَلَن تَجِدَ لِسُنَّتِ اللَّـهِ تَبْدِيلًا وَلَن تَجِدَ لِسُنَّتِ اللَّـهِ تَحْوِيلًا﴾

“Na vitimbi vibaya havimpati ila yule aliyevifanya, Basi hawangoji ila desturi iliyokuwa kwa watu wa zamani, wala hutakuta mabadiiko katika desturi ya Mwenyezi Mungu, wala hutakuta mageuko katika desturi ya Mwenyezi Mungu.” (35:43)

Kukaririka huku ni kutilia mkazo kwamba mwisho ni wa wanaomcha Mwenyezi Mungu; kadiri zitakavyorefuka zama. Hivi ndivyo tunapata tafsir ya kauli yake Mwenyezi Mungu:

Ili wafanye vitimbi humo; wala hawafanyii vitimbi isipokuwa wanajifanyia wenyewe, lakini hawatambui.

Na zinapowafikia ishara husema: Hatutaaamini mpaka tupewe sawa na yale waliyopewa Mitume wa Mwenyezi Mungu.

Wametofautiana wafasiri katika maana ya Aya hii kwa kauli mbili: Kwanza, kwamba wakubwa waovu katika Waarabu walimtaka Muhammad(s.a.w.w) awaletee muujiza kama aliopewa Musa, wa kupasua bahari; na wa Isa, wa kufufua wafu.

Kauli ya pili, ni kuwa wao walimwambia hatutakuamini mpaka utushushie wahyi kama ulivyowashukia Mitume. Razi akasema: “Hii ndio kauli mashuhuri baina ya wafasiri.”

Nasi tunaipa uzito kuliko ya kwanza; Kwa sababu mfumo wa Aya unafahamisha hivyo, ambapo Mwenyezi Mungu anawajibu wakubwa waovu kwa kauli yake:

Mwenyezi Mungu ndiye Mjuzi zaidi wa kujua mahali anapoweka ujumbe wake.

Kuongezea kuwa kutaka kwao Mwenyezi Mungu awateremshie Wahyi kunaafikiana na hasadi yao kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu amesema:

﴿ أَمْ يَحْسُدُونَ النَّاسَ عَلَىٰ مَا آتَاهُمُ اللَّـهُ مِن فَضْلِهِ﴾

“Au wanawahusudu watu kwa alichowapa Mwenyezi Mungu katika fadhila yake?.” Juz.5 (4:54)

Katika Majmaul-bayan na kwengine, imeelezwa kuwa Walid bin Mughira alimwambia Mtume(s.a.w.w) :“Lau Utume ungelikuwa ni kweli mimi ningelistahiki zaidi kuliko wewe, kwa sababu mimi ni mkubwa kuliko wewe, na nina mali nyingi kushinda wewe.”

Maana ya kauli yake Mwenyezi Mungu: ‘Mwenyezi Mungu ndiye Mjuzi zaidi wa kujua mahali anapoweka ujumbe wake’, ni kuwa yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu anauchagulia ujumbe wake mtu atakayefaa katika viumbe vyake, na Muhammad ni Mtukufu zaidi wa viumbe vya Mwenyezi Mungu na aheshimiwaye zaidi kwao.

Itawafika wale waliokosea dhila inayotoka kwa Mwenyezi Mungu.

Kwa sababu walijifanya wakubwa wakajiadhimisha, Ndipo wakastahiki malipo ya udhalilifu na fedheha. Kuna Hadith isemayo kuwa wenye kutakabari watafufuliwa katika Sura ya chembe (kama sisimizi) watakanyagwa na watu kwa nyayo zao, ikiwa ni malipo ya kujifanya kwao wakubwa katika dunia.

Na adhabu kali kwa sababu ya vitimbi walivyokuwa wakivifanya.

Udhalili ni malipo ya kiburi, na adhabu ni malipo ya vitimbi na hadaa. Kwa maneno mengine ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) anawafanyia wale wenye nia mbaya na malengo ya ufisadi kinyume cha wanavyokusudia na wanavyolenga.