TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA NANE Juzuu 8

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA NANE22%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA NANE Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: tafsiri ya Qurani

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
  • Anza
  • Iliyopita
  • 17 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 13120 / Pakua: 3694
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA NANE

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA NANE Juzuu 8

Mwandishi:
Swahili

5

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA NANE

قُل لَّا أَجِدُ فِي مَا أُوحِيَ إِلَيَّ مُحَرَّمًا عَلَىٰ طَاعِمٍ يَطْعَمُهُ إِلَّا أَن يَكُونَ مَيْتَةً أَوْ دَمًا مَّسْفُوحًا أَوْ لَحْمَ خِنزِيرٍ فَإِنَّهُ رِجْسٌ أَوْ فِسْقًا أُهِلَّ لِغَيْرِ اللَّـهِ بِهِ ۚ فَمَنِ اضْطُرَّ غَيْرَ بَاغٍ وَلَا عَادٍ فَإِنَّ رَبَّكَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿١٤٥﴾

145.Sema: Sioni katika niliyopewa wahyi kilichoharamishiwa mlaji kukila isipokuwa kiwe ni mzoga au damu inayomwagika au nyama ya nguruwe, kwani hivyo ni uchafu; au kwa uharamu, kimetajiwa jina la asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Lakini aliyefikwa na dharura bila ya kutamani wala kupita kiasi, basi Mwenyezi Mungu ni mwingi wa maghufira, mweye kurehemu.

وَعَلَى الَّذِينَ هَادُوا حَرَّمْنَا كُلَّ ذِي ظُفُرٍ ۖ وَمِنَ الْبَقَرِ وَالْغَنَمِ حَرَّمْنَا عَلَيْهِمْ شُحُومَهُمَا إِلَّا مَا حَمَلَتْ ظُهُورُهُمَا أَوِ الْحَوَايَا أَوْ مَا اخْتَلَطَ بِعَظْمٍ ۚ ذَٰلِكَ جَزَيْنَاهُم بِبَغْيِهِمْ ۖ وَإِنَّا لَصَادِقُونَ ﴿١٤٦﴾

146.Na kwa wale walio mayahudi tuliharamisha kila mwenye kucha. Na katika ng’ombe na mbuzi na kondoo tukawaharamishia mafuta yao; isipokuwa yale iliyobeba migongo yao, au matumbo, au iliyochanganyika na mifupa. Tuliwalipa hivyo kwa sababu ya uasi wao, Na hakika sisi ndio wakweli.

فَإِن كَذَّبُوكَ فَقُل رَّبُّكُمْ ذُو رَحْمَةٍ وَاسِعَةٍ وَلَا يُرَدُّ بَأْسُهُ عَنِ الْقَوْمِ الْمُجْرِمِينَ ﴿١٤٧﴾

147.Wakikukadhibisha, basi sema: Mola wenu ana rehema nyingi; wala adhabu yake haizuiliwi kwa watu waovu.

SIONI KATIKA NILIYOPEWA WAHYI

Aya 145 – 147

MAANA

Sema: Sioni katika niliyopewa wahyi kilichoharamishiwa mlaji kukila isipokuwa kiwe ni mzoga au damu inayomwagika au nyama ya nguruwe, kwani hivyo ni uchafu; au kwa uharamu, kimetajiwa jina la asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Lakini aliyefikwa na dharura bila ya kutamani wala kupita kiasi, basi Mwenyezi Mungu ni mwingi wa maghufira, mwenye kurehemu.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kubainisha uzushi wa washirikina kwa Mwenyezi Mungu, katika vyakula walivyoharamisha na kuhalalisha, kati- ka Aya hii anabainisha vilivyoharamishwa na Mwenyezi Mungu kuliwa.

Navyo ni vinne: Mfu, damu yenye kutirizika, nyama ya nguruwe na kilichotajiwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu; yaani aliyechinjwa kwa jina la asiyekuwa Mwenyezi Mungu.

Haifai kwa yeyote kula chochote katika hivyo ila akiwa amelazimika; katika hali hiyo anaruhusiwa kula kiasi kile kitakachoweza kuzuia madhara ya nafsi yake tu. Umetangulia ufafanuzi wa hayo katika kufasiri Juz.2 (2:173) Huko tumejibu swali la mwenye kuuliza, kuwa inaonyesha vilivyo haramu ni hivi vinne tu, lakini tunaelezewa vingi, Vilevile umetangulia ufafanuzi zaidi katika Juz.6 (5:3).

Na kwa wale walio Mayahudi tuliharamisha kila mwenye kucha.

Katika Aya iliyotangulia, Mwenyezi Mungu ameharamisha aina zilizotajwa kwa watu wote, Mayahudi na wasiokuwa Mayahudi. Ama vilivyoharamishwa, katika Aya hii, vinawahusu Mayahudi tu, kwa dalili ya kauli yake Mwenyezi Mungu: “Na kwa wale walio Mayahudi tuliharamisha:

Kwanza : ni, kila mwenye kucha; yaani wote wenye kucha bila ya kuacha wengine. Tabari katika Tafsir yake anasema: “Mwenye kucha katika wanyama na ndege ni ambaye vidole vyake havikuachana; kama vile ngamia, mbuni na bata.”

Pili :Na katika ng’ombe na mbuzi na kondoo tukawaharmishia mafuta yao.

Mwenyezi Mungu hakuwaharamishia sehemu yote ya nyama ya ng’ombe na mbuzi na kondoo,ispokuwa nyama nyeupe tu sio nyekundu. Na pia katika hiyo amevua kwa kusema:

Isipokuwa yale iliyobeba migongo yao.

Yaani mafuta yaliyogandana na mgongo.

Au matumbo yaani mafuta yanayogandamana na utumbo.

Au iliyochanganyika na mifupa nayo ni mafuta ya mkia kulingana na wafasiri wote waliokuwako wakati wa Razi. Na mfupa uliochanganyika na na mafuta ya mkia ni kifandugu.

Tuliwalipa hivyo kwa sababu ya uasi wao, Na hakika sisi ndio wakweli.

Hii ni kubainisha sababu ya kuharamishiwa mayahudi vitu hivi vizuri, na kwamba hivyo ni malipo ya makosa yao yasiyo na idadi, yakiwemo kuua mitume, kula mali za watu kwa batili, kusema kwao mikono ya Mwenyezi Mungu imefumba na mengineyo. Tazama Juz.4 (3:93).

Wakikukadhibisha, basi sema: Mola wenu ana rehema nyingi; na adhabu yake haizuiliwi (kuwafikia) watu waovu.

Yaani wakikukadhibisha Ewe Muhammad, basi usiwakatishe tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu na uwaambie kuwa mkitubia, basi Mwenyezi Mungu atawakubali na atawasamehe; kama ambavyo atawaadhibu mkiendelea na mliyo nayo.

Katika Aya hii kuna ahadi na kiaga kikali. vilevile radhi ya Mwenyezi Mungu na ghadhabu yake: Radhi yake ni kwa atakayekimbilia kwake akitaka msamaha na ghadhabu yake ni kwa atakayeendelea na uasi. Mwenyezi Mungu anasema:

﴿لَئِنْ شَكَرْتُمْ لَأَزِيدَنَّكُمْ وَلَئِنْ كَفَرْتُمْ إِنَّ عَذَابِي لَشَدِيدٌ﴾

“Mkishukuru, nitawazidishia; na mkikufuru (jueni) kuwa adhabu yangu ni kali” (14:7)

سَيَقُولُ الَّذِينَ أَشْرَكُوا لَوْ شَاءَ اللَّـهُ مَا أَشْرَكْنَا وَلَا آبَاؤُنَا وَلَا حَرَّمْنَا مِن شَيْءٍ ۚ كَذَٰلِكَ كَذَّبَ الَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ حَتَّىٰ ذَاقُوا بَأْسَنَا ۗ قُلْ هَلْ عِندَكُم مِّنْ عِلْمٍ فَتُخْرِجُوهُ لَنَا ۖ إِن تَتَّبِعُونَ إِلَّا الظَّنَّ وَإِنْ أَنتُمْ إِلَّا تَخْرُصُونَ ﴿١٤٨﴾

148.Watasema walioshirikisha: Lau angelitaka Mwenyezi Mungu tusingelimshirikisha sisi wala baba zetu; wala tusingeliharamisha chochote. Kama hivi walikadhibisha waliokuwa kabla yao mpaka wakaonja adhabu yetu, Je, mnayo elimu mtutolee? Nyinyi hamfuati ila dhana tu, na hamsemi ila uwongo tu.

قُلْ فَلِلَّـهِ الْحُجَّةُ الْبَالِغَةُ ۖ فَلَوْ شَاءَ لَهَدَاكُمْ أَجْمَعِينَ ﴿١٤٩﴾

149.Sema: Basi Mwenyezi Mungu ndiye mwenye hoja ikomeshayo, Na kama angelitaka angeliwaongoza nyote.

قُلْ هَلُمَّ شُهَدَاءَكُمُ الَّذِينَ يَشْهَدُونَ أَنَّ اللَّـهَ حَرَّمَ هَـٰذَا ۖ فَإِن شَهِدُوا فَلَا تَشْهَدْ مَعَهُمْ ۚ وَلَا تَتَّبِعْ أَهْوَاءَ الَّذِينَ كَذَّبُوا بِآيَاتِنَا وَالَّذِينَ لَا يُؤْمِنُونَ بِالْآخِرَةِ وَهُم بِرَبِّهِمْ يَعْدِلُونَ ﴿١٥٠﴾

150.Sema: Leteni mashahidi wenu wanaoweza kushuhudia kuwa Mwenyezi Mungu ameharamisha haya, Basi wakitoa ushahidi, wewe usishuhudie pamoja nao. Wala usifuate matamanio ya wale waliozikadhibisha ishara zetu na wale wasioamini Akhera, na ambao humlinganisha Mola wao.

ANGELITAKA MWENYEZI MUNGU TUSINGELISHIRIKISHA

Aya 148 – 150

MAANA

Watasema walioshirikisha: Lau angelitaka Mwenyezi Mungu tusingelimshirikisha sisi wala baba zetu; wala tusingeliharamisha chochote.

Wanaokubali nasaha na kufuata kauli nzuri ni wachache sana; na wanaokubali makosa yao ni wachache zaidi. Kwani wengi wanaona makosa yao ndiyo mambo bora na maovu yao kuwa ni mema.

﴿كَذَٰلِكَ زُيِّنَ لِلْمُسْرِفِينَ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ﴾

“… Namna hii wamepambiwa wale wapitao mipaka yale waliyokuwa wakiyatenda,” (10:12).

Wanaposhindwa kuboresha uovu wao wanajivua na kusema kuwa ni matakwa ya Mwenyezi Mungu au sababu yoyote nyingine.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) ametakata na hayo wanayomsifu nayo. Yeye anawaamrisha na kuwakataza, na kuwafanya wawe na hiyari katika wanayoyafanya na kuyaacha. Ili aangamie mwenye kuangamia kwa dalili zilizo dhahiri na apone yule atakayepona kwa dalili zilizo dhahiri. Wala hakuna yeyote mwenye mamlaka kwa mwingine; hata shetani atasema siku itakapokatwa hukumu:

﴿إِنَّ اللَّـهَ وَعَدَكُمْ وَعْدَ الْحَقِّ وَوَعَدتُّكُمْ فَأَخْلَفْتُكُمْ وَمَا كَانَ لِيَ عَلَيْكُم مِّن سُلْطَانٍ إِلَّا أَن دَعَوْتُكُمْ فَاسْتَجَبْتُمْ لِي فَلَا تَلُومُونِي وَلُومُوا أَنفُسَكُم﴾

“Hakika Mwenyezi Mungu aliwaahidi ahadi ya kweli, nami nikawaahidi, lakini sikuwatimizia, Wala sikuwa na mamlaka juu yenu isipokuwa niliwaita tu, nanyi mkaniitikia. Basi msinilaumu, bali jilaumuni wenyewe … (14:22).

Katika Aya hii tuliyonayo, Mwenyezi Mungu anasimulia madai ya washirikina kuwa shirki yao na shirk ya mababa zao na kuharamisha kwao mimea na wanyama, ilitokana na matakwa ya Mwenyezi Mungu na amri yake. Lau angelitaka wasishirikishe angeliwazuia na shirk.

Kama hivi walikadhibisha waliokuwa kabla yao mpaka wakaonja adhabu yetu.

Yaani washirikina wa Kiarabu walimkadhibisha Muhammad(s.a.w.w) , aliyewakataza ushirikina na kumzulia Mwenyezi Mungu uwongo; sawa na walivyokadhabisha Mitume wale waliokuwa kabla yao; na hawakuwasadiki mpaka baada ya kuteremshiwa adhabu ya malipo ya kukadhibisha kwao.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kusimulia madai ya washirikina, na mababu zao, alimwamrisha Mtume wake kuwajibu kwa swali litakalowazima na kubatilisha madai yao nalo ni:

Je, mnayo elimu mtutolee?

Makusudio ya elimu hapa ni dalili. Hiyo ni katika kutumia chenye kus- ababisha kuwa ndio sababu; Kwa sababu dalili ndiyo sababu ya kupatikana elimu.

Makusudio ya swali hili ni kudhihirisha uwongo wao na kushindwa kwao.

Kwa sababu maana yake ni kuwa nyinyi washirikina! Mmedai shirk ilikuwa ni kwa kuridhia kwake Mwenyezi Mungu; sasa ni nani basi aliyewaambia haya?

Kutoka wapi mmejua matakwa yake Mwenyezi Mungu Mtukufu? Hiyo ni katika siri zake Mwenyezi Mungu wala hamdihirishii siri yake ila Mtume wake aliyemridhia, Na Mtume hakuwaambia haya nyinyi wala wengineo, Kwa hiyo vipi mnafanyia hila Mwenyezi Mungu?

Nyinyi hamfuati ila dhana tu, na hamsemi ila uwongo tu.

Sisi hatuna shaka kwamba wakubwa wa waasi wanajua kuwa wao ni waongo katika wanayoyasema; isipokuwa wanaysema kwa kuifanyia inadi haki ambayo inaipomosha batili yao na kumaliza malengo yao na matendo yao ya uadui.

Sema: Basi Mwenyezi Mungu ndiye mwenye hoja ikomeshayo.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amebainisha katika Aya iliyotangulia kuwa washirikina hawana hoja ya madai yao isipokuwa dhana na uwongo. Katika Aya hii amebainisha kuwa hoja inayokomesha ni ya Mwenyezi Mungu pekee yake, juu yao na juu ya wengine. Maana ya kuwa inakomesha ni kwamba ina nguvu ya kukomesha nyudhuru zote.

Na kama angelitaka angeliwaongoza nyote.

Katika kufasiri Juz.1 (2: 26), tumetaja kuwa Mwenyezi Mungu ana matakwa mawili: Matakwa ya kuumba ambayo yanakuwa katika ibara yake “Kuwa na ikawa” (kun fayakun) na Matakwa ya kuweka sharia, ambayo ni amri zake na makatazo yake.

Na Yeye Mwenyezi Mungu (s.w.t) anaumba ulimwengu kwa matakwa yake ya kuumba na hajiingizikama sikosei - katika matakwa haya kwenye mambo ya watu ya kijamii; bali huweka sharia na mwongozo.

Maelezo haya ndiyo yanatufafanulia maana ya kauli yake:‘Na kama angelitaka angeliwaongoza nyote; Yaani lau angelitaka kujiingiza katika mambo yenu ya kijamii kwa matakwa ya neno “Kuwa ikawa” (ya kuumba), basi mngeliamini nyote, Lakini yeye hafanyi hivyo. Kwa sababu lau angelifanya hivyo ingelibatilika taklifu na kusingekuwapo thawabu na adhabu.

Tunarudia kusema tena kuwa washirikina walidai kuwa shirki yao ilikuwa kwa matakwa ya Mwenyezi Mungu, ndipo Mwenyezi Mungu (s.w.t) aka- batilisha madai yao haya kuwa ni madai yasiyo na dalili. Kwa sababu Mwenyezi Mungu hajiingizi katika mambo ya watu kwa matakwa ya kuumba.

Lau tukichukulia kuwa Mwenyezi Mungu anajiingiza katika mambo hayo, basi kwa hali ilivyo angeliwaelekeza kwenye imani ya umoja wake na sio kwenye uasi, ukafiri na ushirikina.

Sema: Leteni mashahidi wenu wanaoweza kushuhudia kuwa Mwenyezi Mungu ameharamisha haya.

Washirikina walimzulia Mwenyezi Mungu uwongo katika kuharamisha waliyoyaharamisha katika mimea na wanyama; vilevile walimzulia katika kunasibisha shirki yao kwake. Ndipo Mwenyezi Mungu akamwamrisha Mtume wake Muhammad, katika Aya ya kwanza, kuwambia kuwa kama wanayo dalili waitoe.

Katika Aya ya pili akamwamrisha kuuwaambia kuwa dalili mkataa ni ya Mwenyezi Mungu tu, si yenu. Kisha katika Aya hii amemwamrisha kuwaambia nionyesheni anayeshuhudia kuwa Mwenyezi Mungu amewapa wahyi moja kwa moja au kupitia kwa Mtume miongoni mwa Mitume yake kuwa yeye ameharamisha mliyoyaharamisha. Kwa sababu kushuhudia haki kuna sharti la kuweko elimu yenye kuondoa shaka na dhana. Wala hakuna nyenzo ya kujua yaliyoharamishwa na yaliyohalalishwa ila Wahyi tu; basi mleteni atakeyelishuhudia hilo.

Basi wakitoa ushahidi, wewe ushishuhudie pamoja nao.

Katazo hili ni fumbo la uwongo wao katika ushahidi wao. Kwa sababu ni muhali mtume kushuhudia pamoja na washirikina. Na fumbo ni fasaha zaidi kuliko ufafanuzi.

Wala usifuate matamanio ya wale waliozikadhibisha ishara zetu na wale wasioamini Akhera, na ambao humlinganisha Mola wao.

Baada ya Mwenyezi Mungu kuwahukumia uwongo na uzushi, anabainisha sababu ya hukumu yake hiyo kwa mambo matatu:

Kwanza : kuwa wao wanafuata hawaa na matamanio. Hilo ameliletea ibara ya:

Wala usifuate matamanio ya wale waliokadhibisha ishara zetu, kwa sababu ni muhali kwa Mtume kumfuata anayekadhibisha utume wake.

Pili : kwamba wao ni wale wasioamini Akhera; na asiyeamini Akhera hao- gopi mwisho wa uwongo.

Tatu : kwamba wao Humlinganisha Mola wao. Yaani wanamfanya kuwa ana wa kulingana naye katika kuumba. Na yeyote anayemshirikisha Mwenyezi Mungu haukubaliwi ushahidi wake, sababu yeye amefanya madhambi mabaya zaidi.

6

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA NANE

قُلْ تَعَالَوْا أَتْلُ مَا حَرَّمَ رَبُّكُمْ عَلَيْكُمْ ۖ أَلَّا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا ۖ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا ۖ وَلَا تَقْتُلُوا أَوْلَادَكُم مِّنْ إِمْلَاقٍ ۖ نَّحْنُ نَرْزُقُكُمْ وَإِيَّاهُمْ ۖ وَلَا تَقْرَبُوا الْفَوَاحِشَ مَا ظَهَرَ مِنْهَا وَمَا بَطَنَ ۖ وَلَا تَقْتُلُوا النَّفْسَ الَّتِي حَرَّمَ اللَّـهُ إِلَّا بِالْحَقِّ ۚ ذَٰلِكُمْ وَصَّاكُم بِهِ لَعَلَّكُمْ تَعْقِلُونَ ﴿١٥١﴾

151.Sema: Njooni niwasomee aliyowaharamishia Mola wenu: Kwamba msimshirikishe na chohote, Na kuwafanyia wema wazazi wawili. Wala msiwaue watoto wenu kwa kuogopa kuishiwa sisi tutawaruzuku nyinyi na wao. Wala msikurubie mambo machafu, yaliyodhihirika na yaliyofichika; wala msiiue nafsi ambayo Mwenyezi Mungu ameharamisha (kuiua), ila kwa haki. Hayo amewausia Mwenyezi Mungu ili mpate kutia akili.

وَلَا تَقْرَبُوا مَالَ الْيَتِيمِ إِلَّا بِالَّتِي هِيَ أَحْسَنُ حَتَّىٰ يَبْلُغَ أَشُدَّهُ ۖ وَأَوْفُوا الْكَيْلَ وَالْمِيزَانَ بِالْقِسْطِ ۖ لَا نُكَلِّفُ نَفْسًا إِلَّا وُسْعَهَا ۖ وَإِذَا قُلْتُمْ فَاعْدِلُوا وَلَوْ كَانَ ذَا قُرْبَىٰ ۖ وَبِعَهْدِ اللَّـهِ أَوْفُوا ۚ ذَٰلِكُمْ وَصَّاكُم بِهِ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ ﴿١٥٢﴾

152.Wala msiikurubie mali ya yatima isipokuwa kwa njia bora zaidi, Mpaka afikie kukomaa kwake. Na kamilisheni vipimo vya ujazo na uzani kwa uadilifu. Hatuikalifishi nafsi ila kwa uweza wake Na msemapo semeni kwa uadilifu hata kama ni jamaa, Na tekelezenim ahadi ya Mwenyezi Mungu. Haya ameusiwa ili mpate kukumbuka.

وَأَنَّ هَـٰذَا صِرَاطِي مُسْتَقِيمًا فَاتَّبِعُوهُ ۖ وَلَا تَتَّبِعُوا السُّبُلَ فَتَفَرَّقَ بِكُمْ عَن سَبِيلِهِ ۚ ذَٰلِكُمْ وَصَّاكُم بِهِ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ ﴿١٥٣﴾

153.Na kwa hakika hii ndiyo njia yangu iliyonyooka, basi ifuateni wala msifuate njia nyingine zikawatenga mbali na njia yake (Mwenyezi Mungu). Hayo amewausia ili muwe na takua.

ALIYOWAHARAMISHA MOLA WENU

Aya 151 – 153

MAANA

Katika Aya zilizoatangulia, Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameonyesha kuwa washirikina walihalalisha na wakaharamisha kwa dhana na matamanio; na kwamba wao walimnasibishia Mwenyezi Mungu shirki kwa uzushi na bila ya ujuzi wowote. Akawajibu kwa mantiki ya kiakili na kimaumbile, na akataja katika vilivyo haramu: Mfu, damu ya kutirizika, nyama ya nguruwe na kilichochinjwa bila ya kutajwa jina la Mwenyezi Mungu.

Katika Aya hizi tatu (tulizo nazo) ametaja baadhi ya yaliyo haramu, Kwa upande mwingine ametaja baadhi ya mambo yaliyowajibu; kama vile kutopunja katika vipimo, kutekeleza ahadi na kufuata usawa.

Kimsingi ni kuwa kila ambalo ni wajib kulifanya, basi ni haramu kuliacha na kila lililoharamu kulifanya basi ni wajib kuliacha.

Baadhi ya wafasiri wameuita mkusanyiko wa Aya hizi tatu kuwa nasaha kumi.

NASAHA KUMI

Sema: Njooni niwasomee aliyowaharamishia Mola wenu: Kwamba msimshirikishe na chohote.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameanzia na msingi wa kwanza wa itikadi, ambao ni kukana shirki ambako mkabala wake ni kuthibitisha Tawhid. Haki zote na wajibu wote unategemea kwenye msingi huu, na kwa msingi huu hukubaliwa twaa na amali za kkheri. Maana ya Tawhid yanafupika katika kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿لَيْسَ كَمِثْلِهِ شَيْءٌ﴾

“Hakuna chochote kama mfano wake” (42:11)

Si katika dhati wala sifa au vitendo.

Na kuwafanyia wema wazazi wawili.

Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amekutanisha nasaha kwa wazazi wawili pamoja na uungu wake, kutambulisha kuwa kuwafanyiwa wema wazazi wawili kunapasa kuwe kwa aina yake. Ni kama kwamba amesema: Msimshirikishe Mwenyezi Mungu na kitu wala msishirikishe kuwafanyia wema wazazi wawili na wema wowote. Tumeyafafanua hayo katika kufasiri Juz.1 (2:83)

Wala msiwaue watoto wenu kwa kuogopa kuishiwa, sisi tutawaruzuku nyinyi na wao pia.

Baada ya kuwausia watoto kwa mababa, sasa anawausia mababa kwa watoto, Yametangulia maelezo yake katika kufasiri Aya 137 ya Sura hii.

Wala msikurubie mambo machafu, yaliyodhihirika na yaliyofichika.

Kila linalopetuka mpaka katika ubaya ni ovu; kama vile zina, ulawiti, dhuluma na kuvunja heshima. Vilevile uwongo, kusengenya, fitina, na husuda. Uovu mkubwa zaidi ni ulahidi, kumshirikisha Mwenyezi Mungu, kuwaudhi wazazi wawili, kuua nafsi isiyo na hatia na kula mali ya yatima.

Mwenyezi Mungu amehusisha kuyataja haya pamoja na kuwa yanaingia katika uwovu, kwa kufahamisha kuwa yamefikilia ukomo wa ubaya na uovu; ni sawa yawe yamefanywa kisiri au kidhahiri.

Imepokewa kutoka kwa Ibn Abbas kwamba watu wa wakati wa ujahiliya walikuwa wakichukia zinaa kufanywa dhahiri na walikuwa wakiifanya kisiri, ndipo akawakataza Mwenyezi Mungu katika hali zote mbili. Na imepokewa kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.w.t), amesema: “Je, niwafahamishe yule aliye mbali na mimi?” Wakajibu: “Ndio Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu!” Akasema: “Ni mwovu mno, mwenye kuchukiza, bahili, mwenye kiburi, hasidi, aliyesusuwaa moyo, aliye mbali na kila kheri inayotarajiwa na asiyeaminiwa na kila shari inayoogopwa.”

Wala msiiue nafsi ambayo Mwenyezi Mungu ameharamisha (kuiua), ila kwa haki.

Kimsingi, kuua nafsi ni haramu, wala hakuwi halali ila kwa sababu moja kati ya nne ambazo tatu katika hizo zimeelezwa na Hadith ya Mtume(s.a.w.w) : “Haiwi halali damu ya Mwislamu (kuuawa) ila kwa moja ya mambo matatu: Kukufuru baada ya kuamini, kuzini baada ya kuoa na kuua nafsi bila ya haki.” Qur’an nayo imeelezea sababu ya nne iliposema:

﴿ إِنَّمَا جَزَاءُ الَّذِينَ يُحَارِبُونَ اللَّهَ وَرَسُولَهُ وَيَسْعَوْنَ فِي الْأَرْضِ فَسَادًا أَنْ يُقَتَّلُوا أَوْ يُصَلَّبُوا﴾

“Hakika malipo ya wale wanaopigana na Mwenyezi Mungu na Mtume wake na kufanya ufisadi katika ardhi, ni kuuawa au kusulubiwa” (5:33).

Hayo amewausia Mwenyezi Mungu ili mpate kufahamu.

Yaani mjue ubaya wa ushirikina, kuua nafsi, kufanya uovu na mjue uzuri wa kuwafanyia wema wazazi wawili.

Wala msiikurubie mali ya yatima isipokuwa kwa njia bora zaidi.

Kuzuia kukurubia ndio ufasaha zaidi wa kukataza kuliko kukataza tendo lenyewe, na kunahusu njia zote za matumizi; kama ambavyo bora zaidi ni nzuri kuliko bora tu.

Maana yaliyokusudiwa ni kutilia mkazo katika kutunza mali ya kila asiyeweza kutumia mali yake; awe yatima, mwendawazimu, safihi, aliyepotea au mtoto mdogo anayesimamiwa mali zake na baba yake. Kwa hiyo ni juu ya wasimamizi kuzichunga mali za wanaowasimamia na kuangalia vizuri mambo yao.

Kuanzia hapa ndio wamesema kundi la mafakihi wakubwa, kwamba haiwezekani kwa msimamzi kutumia mali ya anayemsimamia ila kwa masilahi ya mwenye mali. Na sisi tuko pamoja na rai hii; hata kama msimamizi ni baba au babu. Dalili yetu ni neno ‘njia bora zaidi’ Ama Hadith isemayo: “Wewe na mali yako ni (milki) ya baba yako”, ni hukumu ya kimaadili tu, si ya kisharia; kwa dalili ya neno ‘Wewe’, kwa sababu, mtoto si bidhaa anayomiliki baba.

Utauliza kuwa : neno yatima linahusika na yule aliyefiwa na baba yake akiwa mdogo, sasa imekuaje kulihusisha na kila asiyeweza kutumia?

Sisi tunajua kabisa kwamba sababu ya kutumia kwa njia iliyo bora zaidi ni kule kushindwa kutumia yule mwenye mali na wala sio uyatima; na kushindwa kutumia kumethibitika kwa wote waliotajwa bila ya tofauti.

Mpaka afikie kukomaa kwake . Utaipata tafsiri yake katika Juz.5 (4:6)

Na kamilisheni vipimo vya ujazo na uzani kwa uadilifu mkiuza au mkininua.

Hatuikalifishi nafsi ila kwa uweza wake. Jumla hii imeingia katikati ikiwa na makusudio ya kufahamisha kuwa ukamilishaji wa vipimo uliotajwa ni ule uliozoelekea kwa watu; husamehewa kiasi kichache kilichozidi au kupungua. Kwa sababu kutekeleza kipimo cha sawaswa kabisa ni aina ya uzito:

﴿ وَمَا جَعَلَ عَلَيْكُمْ فِي الدِّينِ مِنْ حَرَجٍ﴾

“Wala hakuwawekea mambo mazito katika dini” (22:78)

Kwa hali yoyote ni kuwa msingi katika aina zote za biashara ni kuridhia pande zote mbili, iwe ni bidhaa inayopimwa kwa kilo, kwa kuhesabiwa kwa mita, kukadiriwa kwa kifikra, kama kuandika, au kwa kuangalia tu, kama sanaa iliyoundwa kwa mkono.

Na msemapo semeni kwa uadilifu hata kama ni jamaa.

Huu ndio ushupavu wa yule anayemwogopa Mwenyezi Mungu na kumfanyia ikhalsi na kutambua kuwa mbele yake kuna majukumu, sio kuwa mbele yake kuna mke, baba, mama, mtoto au mkwe. Hakuna chochote isipokuwa haki na uadilifu tu. Ama mwenye kutumia jina la dini, kisha afuate matamanio yake kwa ndugu au rafiki, basi huyo hana dini kitu.

Na tekelezeni ahadi ya Mwenyezi Mungu.

Kila aliloharamisha Mwenyezi Mungu na alilolikataza ni ahadi yake. Utekelezaji wake ni kufuata amri na kutii. Hayo amewausia ili mpate kukumbuka, Msimsahau kumtii yule asiyewasahau.

Na kwa hakika hii ndiyo njia yangu iliyonyooka.

Hii ni ishara ya yote yaliyotajwa; ndiyo njia ya Mwenyezi Mungu iliyonyooka, vinginevyo ni upotevu.

Basi ifuateni wala msifuate njia nyingine ; kama vile shirki, ulahidi, vikundi na dini za ubatilifu.Zikawatenga mbali na njia yake (Mwenyezi Mungu).

Njia yoyote isiyokuwa Qur’an na Uislam basi hiyo ni njia ya matamanio tu, Na matamanio hayana udhibiti wala mpaka wowote. Watu wakiyafuata ndipo hugawanyika vikundi na vyama mbalimbali. Lakini kama wote wakifuata dini ya Mwenyezi Mungu basi itikadi ya kweli na imani ya sawa itawaweka pamoja.

Kuna Hadith isemayo kuwa Mtume(s.a.w.w) alipiga msitari kwa mkono wake kisha akasema: “Hii ndiyo njia ya Mwenyezi Mungu iliyonyooka:” Kisha akapiga msitari kuumeni na kushotoni mwa msitari ule, akasema: “Hii siyo njia ispokuwa shetani ndiyo anayoilingania; kisha akasoma: “Na kwa hakika hii ndiyo njia yangu iliyonyooka, basi ifuatie wala msifuate njia nyingine zikawatenga mbali na njia yake (Mwenyezi Mungu).”

ثُمَّ آتَيْنَا مُوسَى الْكِتَابَ تَمَامًا عَلَى الَّذِي أَحْسَنَ وَتَفْصِيلًا لِّكُلِّ شَيْءٍ وَهُدًى وَرَحْمَةً لَّعَلَّهُم بِلِقَاءِ رَبِّهِمْ يُؤْمِنُونَ ﴿١٥٤﴾

154.Kisha tulimpa Musa Kitab, kwa kumtimizia yule aliyefanya wema. Na kuwa ni ufafanuzi wa kila kitu na mwongozo na rehema ili wapate kuamini kukutana na Mola wao.

وَهَـٰذَا كِتَابٌ أَنزَلْنَاهُ مُبَارَكٌ فَاتَّبِعُوهُ وَاتَّقُوا لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ ﴿١٥٥﴾

155.Na hii ni Kitab tulichokiteremsha kilicho barikiwa. Basi kifuateni na muwe na takua ili mrehemiwe.

أَن تَقُولُوا إِنَّمَا أُنزِلَ الْكِتَابُ عَلَىٰ طَائِفَتَيْنِ مِن قَبْلِنَا وَإِن كُنَّا عَن دِرَاسَتِهِمْ لَغَافِلِينَ ﴿١٥٦﴾

156.Msije mkasema kuwa vitabu viliteremshiwa makundi mawili tu, yaliyokuwa kabla yetu nasi tulikuwa hatuna habari ya yale waliyoyasoma.

أَوْ تَقُولُوا لَوْ أَنَّا أُنزِلَ عَلَيْنَا الْكِتَابُ لَكُنَّا أَهْدَىٰ مِنْهُمْ ۚ فَقَدْ جَاءَكُم بَيِّنَةٌ مِّن رَّبِّكُمْ وَهُدًى وَرَحْمَةٌ ۚ فَمَنْ أَظْلَمُ مِمَّن كَذَّبَ بِآيَاتِ اللَّـهِ وَصَدَفَ عَنْهَا ۗ سَنَجْزِي الَّذِينَ يَصْدِفُونَ عَنْ آيَاتِنَا سُوءَ الْعَذَابِ بِمَا كَانُوا يَصْدِفُونَ ﴿١٥٧﴾

157.Au mkasema: Lau tungeliteremshiwa Kitab bila shaka tungelikuwa waongofu zaidi kuliko wao. Basi imewafikia hoja kutoka kwa Mola wenu, uwongofu na rehema. Basi ni nani dhalimu mkubwa kuliko yule anayezikadhibisha ishara za Mwenyezi Mungu na akajitenga nazo? Tutawalipa wale wanaojitenga na ishara zetu, adhabu mbaya kwa sababu ya kule kujitenga kwao.

KISHA TULIMPA MUSA KITAB

Aya 154 – 157

MAANA

Kisha tulimpa Musa Kitab.

Wameduwaa wafasiri kuhusu neno ‘Kisha’ Kwa sababu mazungumzo ni ya Qur’an katika Aya zilizotangulia. Na Aya hii inazungumzia Tawrat iliyoshuka kabla ya Qur’an; na ‘Kisha’ inafahamisha kuja nyuma ya kilicho kabla yake kwa wakati. Sasa imekuwaje itajwe Qur’an kisha Tawrat na iliyoanza ni Tawrat?

Razi ametaja njia tatu, na Tabrasi akazidisha ya nne, Sisi hatuoni jambo lolote la kurefusha maneno hapo. Kwa sababu mpangilio hapa ni wa maneno sio wa wakati, na uunganisho ni wa habari kuungana na habari nyingine sio maana kuungana na maana nyingine.

Kumtimizia yule aliyefanya wema.

Yaani tumempa Musa Kitab nacho kinatimiza upungufu wa aliyefanya wema, kunafaika nacho; kama kusema kwake Mwenyezi Mungu:

﴿الْيَوْمَ أَكْمَلْتُ لَكُمْ دِينَكُمْ وَأَتْمَمْتُ عَلَيْكُمْ نِعْمَتِي وَرَضِيتُ لَكُمُ الْإِسْلَامَ دِينًا﴾

“Leo nimewakamilishia dini yenu na kuwatimizia neema yangu na nimewapendelea Uislamu kuwa dini” (5:3)

Na kuwa ni ufafanuzi wa kila kitu.

Hii ni sifa ya pili ya Kitab cha Musa(a.s) kwamba kimekusanya hukumu zote walizozitaja watu wa wakati ule. Mwenyezi Mungu mtukufu anasema:

﴿وَكَتَبْنَا لَهُ فِي الْأَلْوَاحِ مِن كُلِّ شَيْءٍ مَّوْعِظَةً وَتَفْصِيلًا لِّكُلِّ شَيْءٍ﴾

“Na tukamwandikia katika mbao mawaidha ya kila kitu na ufafanuzi wa kila kitu” (7:144).

Na mwongozo na rehema.

Sifa mbili nyingine za Kitab cha Musa, Kwa mwongozo, watu watajua haki na kheri, na kwa rehema, watu wataishi maisha ya utulivu.

Ili wapate kuamini kukutana na Mola wao.

Dhamiri inawarudia waisrael, kwa maana tumempa Musa Kitab kilichokusanya sifa zilizotajwa, ili watu wake wamwamini Mwenyezi Mungu na thawabu zake na adhabu yake. Lakini wao waling’ang’ania inadi yao, na wakasema miongoni mwa waliloyasema:

﴿ يَا مُوسَىٰ لَنْ نُؤْمِنَ لَكَ حَتَّىٰ نَرَى اللَّهَ جَهْرَةً﴾

“Ewe Musa! Hatutakuamini mpaka tumwone Mungu waziwazi” Juz.1 (2:55)

Tukadrie kama wangemwona Mwenyezi Mungu waziwazi - na kukadiria muhali si muhali - basi wao wangesema kuwa huyu si Mola, kwa vile yeye si pauni wala dola.

Na hii ni Kitab tulichokiteremsha kilichobarikiwa na baraka.

Hii ni Qur’an tukufu, nayo ni yenye baraka kwa sababu ina kheri na manufaa mengi.

Basi kifuateni na muwe na takua ili mrehemiwe.

Fuateni aliyowaamrisha na muache aliyowakataza ili iwaenee rehma yake duniani na akhera.

Msije mkasema kuwa vitabu viliteremshiwa makundi mawili tu, yaliyokuwa kabla yetu nasi tulikuwa hatuna habari ya yale waliyoyasoma.

Wanaambiwa washirikina wa Kiarabu. Makusudio ya vitabu ni Tawrat na Injil; na makundi mawili ni watu wa Kitab: Mayahudi na Manaswara (Wakristo).

Maana ni kuwa enyi Waarabu, tumewateremshia Qur’an kwa lugha yenu na kwa mtu wenu anayetokana nanyi ili msiwe na udhuru wa shirki yenu, kwamba hakikuteremshwa Kitab kwa lugha yenu na kuwa hamkujua kuk- isoma na kujifundisha mafunzo yake.

Au mkasema: Lau tungeliteremshiwa Kitab bila shaka tungelikuwa woaongofu zaidi kuliko wao.

Katika Aya iliyotangulia Mwenyezi Mungu anawaondolea udhuru wa lugha, na katika Aya hii anawaondolea udhuru wa kufikiwa na Kitabu chenyewe. Kwa ufupi ni kuwa Aya hii na iliyo kabla yake inafanana na kauli ya asemaye: “Fulani ni tajiri na mimi sina chochote, lau ningekuwa na kitu basi ningelifanya mengi.” Ndipo Mwenyezi Mungu akawajibu kwa jawabu mkataa:

Basi imewafikia hoja kutoka kwa Mola wenu, na uwongofu na rehema.

Makusudio ya hoja ni Qur’an, ndani yake mna dalili na ubainifu wa kumsadikisha Muhammad(s.a.w.w) . Vilevile mna hukumu na mafunzo yenye kuwatoa watu kwenye giza kwenda kwenye mwanga.

Basi ni nani dhalimu mkubwa kuliko yule anayezikadhibisha ishara za Mwenyezi Mungu na akajitenga nazo?

Hakuna kabisa dhalimu mkubwa wa nafsi yake na watu kuliko yule anayekana haki na kheri, akahangaika katika dunia kufanya ufisadi na kupinga njia ya Mwenyezi Mungu.

Tutawalipa wale wanaojitenga na ishara zetu adhabu mbaya kwa sababu ya kule kujitenga kwao.

Ishara za Mwenyezi Mungu ni hoja zake na dalili zake. Maana ni kuwa yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu amesimamisha dalili na hoja mkataa juu ya umoja wake na juu ya utume wa Muhammad na ukweli wa aliyokuja nayo kutoka kwa Mola wake, lakini washirikina walipinga wakakataa kuzingatia vizuri hoja hizo kwa kuifanyia inadi haki na watu wa haki. Kwa hiyo wakastahiki hizaya na adhabu kali.

3

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اذْكُرُوا اللَّـهَ ذِكْرًا كَثِيرًا ﴿٤١﴾

41. Enyi ambao mmeamini! Mkumbukeni Mwenyezi Mungu kwa wingi.

وَسَبِّحُوهُ بُكْرَةً وَأَصِيلًا ﴿٤٢﴾

42. Na mumtakase asubuhi na jioni.

هُوَ الَّذِي يُصَلِّي عَلَيْكُمْ وَمَلَائِكَتُهُ لِيُخْرِجَكُم مِّنَ الظُّلُمَاتِ إِلَى النُّورِ وَكَانَ بِالْمُؤْمِنِينَ رَحِيمًا ﴿٤٣﴾

43. Yeye ndiye anayewaswalia na malaika wake, ili awatoe vizani na kuwatia kwenye nuru. Naye ni mwenye kuwarehemu waumini.

تَحِيَّتُهُمْ يَوْمَ يَلْقَوْنَهُ سَلَامٌ وَأَعَدَّ لَهُمْ أَجْرًا كَرِيمًا ﴿٤٤﴾

44. Maamkuzi yao siku ya kukutana naye yatakuwa ni Salaam na amewaandalia malipo yenye heshima.

يَا أَيُّهَا النَّبِيُّ إِنَّا أَرْسَلْنَاكَ شَاهِدًا وَمُبَشِّرًا وَنَذِيرًا ﴿٤٥﴾

45. Ewe Nabii! Hakika sisi tumekutuma uwe shahidi na mbashiri na muonyaji.

وَدَاعِيًا إِلَى اللَّـهِ بِإِذْنِهِ وَسِرَاجًا مُّنِيرًا ﴿٤٦﴾

46. Na mlinganiaji kwa Mwenyezi Mungu kwa idhini yake, na taa iangazayo.

وَبَشِّرِ الْمُؤْمِنِينَ بِأَنَّ لَهُم مِّنَ اللَّـهِ فَضْلًا كَبِيرًا ﴿٤٧﴾

47. Wape bishara waumini ya kwamba wanafadhila kubwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

وَلَا تُطِعِ الْكَافِرِينَ وَالْمُنَافِقِينَ وَدَعْ أَذَاهُمْ وَتَوَكَّلْ عَلَى اللَّـهِ وَكَفَىٰ بِاللَّـهِ وَكِيلًا ﴿٤٨﴾

48. Wala usiwatii makafiri na wanafiki na acha udhia wao na mtegemee Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu anatosha kuwa mlinzi.

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا نَكَحْتُمُ الْمُؤْمِنَاتِ ثُمَّ طَلَّقْتُمُوهُنَّ مِن قَبْلِ أَن تَمَسُّوهُنَّ فَمَا لَكُمْ عَلَيْهِنَّ مِنْ عِدَّةٍ تَعْتَدُّونَهَا فَمَتِّعُوهُنَّ وَسَرِّحُوهُنَّ سَرَاحًا جَمِيلًا ﴿٤٩﴾

49. Enyi ambao mmeamini! Mkiwaoa wanawake waumini kisha mkawaacha kabla ya kuwagusa, basi hamna eda juu yao mtakayoihisabu. Hivyo wapeni cha kuwaliwaza na waacheni muachano mzuri.

NDIYE ANAYEWAREHEMU

Aya 41 – 49

MAANA

Enyi ambao mmeamini! Mkumbukeni Mwenyezi Mungu kwa wingi na mumtakase asubuhi na jioni.

Hii ni amri ya kudumu kwenye Swala tano na kumkumbuka, Mwenyezi Mungu wakati wote, kwa kumbukumbu nzuri.

Yeye ndiye anayewaswalia na malaika wake.

Kuswalia kukitoka kwa Mwenyezi Mungu, maana yake ni maghufira na rehema na kukitoka kwa mwenginewe ni kuombea maghufira na rehema. Kwa hiyo inampasa kila mtu kumswalia na kumwombea amani kila mwenye kuamini na katenda mema.

Ni vizuri kudokeza kwamba Sunni, aghlabu wakimtaja sahaba mtukufu au imam mkuu husema: Radhiallah anh (Mwenyezi Mungu awe radhi naye). Shia wao husema: Alayhissalam (amani ishuke juu yake). Chimbuko la kauli zote mbili ni moja – Qur’an. Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema: “Awe radhi nao Mwenyezi Mungu na wao wawe radhi naye.” Juz. 7 (5:119) na akasema:“Amani kwa Ilyasin” (37:130) na amesema kwenye Aya hii tuliyo nayo: “Yeye ndiye anayewaswalia na malaika wake.”

Katika Tafsir Ruhul-bayan imeelezwa: “Bani Israil walimuuliza Musa: “Mola wetu naye anaswali? Basi hili likawa zito kwa Musa.” Hilo si ajabu kwa Waisrail.

Ili awatoe vizani na kuwatia kwenye nuru.

Makusudio ya viza hapa ni viza vya moto; na nuru ni nuru ya neema; yaani Mwenyezi Mungu na malaika wake wanawaswalia waumini ili wawe mbali na adhabu ya moto na waingie kwenye raha. Imesekana kuwa makusudio ya viza ni ukafiri na nuru ni nuru ya imani, lakini hii haiafikiani na kauli yake Mwenyezi Mungu inayofuatia:

Naye ni mwenye kuwarehemu waumini.

Vile vile haiafikiani na kuwa Mwenyezi Mungu na malaika wake hawarehemu makafiri ili awatoe kwenye imani.

Maamkuzi yao siku ya kukutana naye yatakuwa ni Salaam na amewaandalia malipo yenye heshima.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 11 (10:10) Juz. 13 (14:23).

Ewe Nabii! Hakika sisi tumekutuma uwe shahidi na mbashiri na muonyaji na mlinganiaji kwa Mwenyezi Mungu kwa idhini yake.

Mwenyezi Mungu alimtuma Muhammad(s.a.w. w ) kulingania haki na akamsheheneza hoja za kutosha, kumpa habari njema ya pepo yule mtiifu na kumwonya na adhabu chungu yule mwenye kuasi. Kesho atakuwa shahidi wa huyu kwamba alipinga na akatupilia mbali na atakuwa shahidi wa yule kwamba alisikia na akatii.

Kwenye Nahjul-balagha kuna maelezo haya: “Alimtuma kuwa ni mlingania kwenye haki na shahidi kwa viumbe. Akafikisha ujumbe wa Mola wake bila ya kubweteka wala kuzembea, na akapigana jihadi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na maadui zake bila ya kudhoofika wala kutafuta visababu. Ni imamu wa mwenye takua na busara ya mwenye kutaka kuongoka.

Na taa iangazayo inayowaongoza wanaohangaika kwenye ufukwe wa salama.

Wape bishara waumini ya kwamba wanafadhila kubwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Umepita mfano wake katika Juz.11 (9-112)

Wala usiwatii makafiri na wanafiki.

Imetangulia neno kwa neno katika Juzuu iliyopita mwanzo wa sura hii tuliyo nayo.

Na acha udhia wao.

Mtume hakuwaudhi, ispokuwa washirikina ndio waliomuudhi, kiasi cha kufikia kusema: “Hakuudhiwa Nabii mfano wa nilivyoudhiwa mimi.” Kwa hiyo maana ni, achana nao, usikushughulishe ujinga na upumbavu wao.

Na mtegemee Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu anatosha kuwa mlinzi.

Kwenye Nahjul-balagha imesemwa: “ Mwenye kumtegemea Mwenyezi Mungu anamtoshea na mwenye kumwomba atampa na mwenye kumkopesha atamlipa, na mwenye kumshukuru atampa jaza yake.

Enyi ambao mmeamini! Mkiwaoa wanawake waumini kisha mkawaacha kabla ya kuwagusa, basi hamna eda juu yao mtakyoihisabu. Hivyo wapeni cha kuwaliwaza na waacheni muachano mzuri.

Kabla ya kuwagusa ni kabla ya kuwaingilia. Cha kuwaliwaza kisharia ni kitu anachokitoa mtaliki akiwa hajamwingilia na hakutaja mahari yake. Ikiwa ametaja itakuwa ni wajibu kutoa nusu ya mahari. Tazama Juz. 2 (2:236 – 237).

يَا أَيُّهَا النَّبِيُّ إِنَّا أَحْلَلْنَا لَكَ أَزْوَاجَكَ اللَّاتِي آتَيْتَ أُجُورَهُنَّ وَمَا مَلَكَتْ يَمِينُكَ مِمَّا أَفَاءَ اللَّـهُ عَلَيْكَ وَبَنَاتِ عَمِّكَ وَبَنَاتِ عَمَّاتِكَ وَبَنَاتِ خَالِكَ وَبَنَاتِ خَالَاتِكَ اللَّاتِي هَاجَرْنَ مَعَكَ وَامْرَأَةً مُّؤْمِنَةً إِن وَهَبَتْ نَفْسَهَا لِلنَّبِيِّ إِنْ أَرَادَ النَّبِيُّ أَن يَسْتَنكِحَهَا خَالِصَةً لَّكَ مِن دُونِ الْمُؤْمِنِينَ قَدْ عَلِمْنَا مَا فَرَضْنَا عَلَيْهِمْ فِي أَزْوَاجِهِمْ وَمَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُمْ لِكَيْلَا يَكُونَ عَلَيْكَ حَرَجٌ وَكَانَ اللَّـهُ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴿٥٠﴾

50. Ewe Nabii! Hakika sisi tumekuhalalishia wake zako ambao umewapa ujira wao, na uliowamiliki kwa mkono wako wa kuume katika aliokupa Mwenyezi Mungu, na mabinti wa ami zako, na mabinti wa shangazi zako, na mabinti wa wajomba zako na mabinti wa khalat zako waliohama pamoja nawe, na mwanamke mumin akijitoa mwenyewe kwa Nabii ikiwa Nabii anataka kumuoa. Ni halali kwako wewe tu, si kwa waumini wengine. Tunajua tuliyowafaradhishia wao kuhusu wake zao na wale waliomilikiwa na mikono yao ya kuume. Ili isiwe dhiki juu yako. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

تُرْجِي مَن تَشَاءُ مِنْهُنَّ وَتُؤْوِي إِلَيْكَ مَن تَشَاءُ وَمَنِ ابْتَغَيْتَ مِمَّنْ عَزَلْتَ فَلَا جُنَاحَ عَلَيْكَ ذَٰلِكَ أَدْنَىٰ أَن تَقَرَّ أَعْيُنُهُنَّ وَلَا يَحْزَنَّ وَيَرْضَيْنَ بِمَا آتَيْتَهُنَّ كُلُّهُنَّ وَاللَّـهُ يَعْلَمُ مَا فِي قُلُوبِكُمْ وَكَانَ اللَّـهُ عَلِيمًا حَلِيمًا ﴿٥١﴾

51. Unamwakhirisha umtakaye katika wao na na unamsogeza kwako umtakaye. Na unayemtaka katika uliyemtenga si vibaya kwako. Hivyo itakuwa ni karibu zaidi kuburudika macho yao wala wasihuzunike na wawe radhi juu ya kile unachowapa wao wote. Na Mwenyezi Mungu anajua yaliyomo nyoyoni mwenu. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, Mpole.

لَّا يَحِلُّ لَكَ النِّسَاءُ مِن بَعْدُ وَلَا أَن تَبَدَّلَ بِهِنَّ مِنْ أَزْوَاجٍ وَلَوْ أَعْجَبَكَ حُسْنُهُنَّ إِلَّا مَا مَلَكَتْ يَمِينُكَ وَكَانَ اللَّـهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ رَّقِيبًا ﴿٥٢﴾

52. Hawakuhalalikii wanawake baadaye wala kuwabadilisha kwa wake wengine, ijapo uzuri wao utakupendeza; isipokuwa uliyemmiliki kwa mkono wako wa kuume. Na Mwenyezi Mungu ni Mchungaji wa kila kitu.

TUMEKUHALALISHIA WAKE ZAKO

Aya 50 – 52

MAANA

Mwenyezi Mungu (s.w.t) katika Aya hii ametaja aina ya wanawake walio halali kwa Mtume(s.a.w. w ) na kumwachia hiyari ya kumlalia na kutomlalia anayemtaka. Kisha akamharamishia kuzidisha wale aliokuwa nao au kubadilisha mwingine. Wakati huo alikuwa na wake tisa. Ufuatao ni ufafanuzi:

Ewe Nabii! Hakika sisi tumekuhalalishia wake zako ambao umewapa ujira wao.

Makusudio ya ujira hapa ni mahari. Na kuwapa hayo mahari kunakuwa ni lazima. Aya inaashiria kuwa Mtume anaweza kuoa idadi yoyote anayoitaka. Haya ni katika mambo yanayomuhusu yeye tu.

Unaweza kuuliza : kufunga ndoa kunaswihi hata kama mahari hayakuta- jwa, kwa nini basi Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameufunga uhalali kwa mahari?

Jibu : Ulazima hapa ni wa kuyatoa hayo mahari sio kuyataja kwenye ndoa. Ikiwa mahari hayakutajwa kwenye ndoa, basi ni lazima kutoa mahari kifani; yaani yanayofana na mwingine wa aina yake. Mahari ya mtume, wakati huo, yalikuwa ni Dirhamu 500. wamekadiria Dirhamu moja kuwa ni sawa na Lira 25 za dhahabu.

Na uliowamiliki kwa mkono wako wa kuume katika aliokupa Mwenyezi Mungu katika mateka waliowatekwa nyara na waislamu kati- ka vita na washirikina, ambao wanaitwa masuria. Mwenyezi Mungu amemuhalishia Mtume wake na umma wake, wanawake hawa.

Na mabinti wa ami zako, na mabinti wa shangazi zako, na mabinti wa wajomba zako na mabinti wa khalat zako waliohama pamoja nawe.

Unaweza kuuliza : Mabinti wa ami, wa shangazi, wajomba na wa khalat (dada wa mama) si wanaingia katika aina ya kwanza ya wanawake, sasa kuna haja gani ya kuhusishwa kutajwa?

Jibu : Inawezekana kuwa makusudio ya kutajwa ni kuwa inavyopendeza ni kuwa hadhi ya Mtume ni kuoa makuraishi aliohama nao kutoka mji wa ukafiri hadi mji wa Uislamu. Ama waumimi wengine ni bora kutowaoa.

Swali la pili : Watu wa sira wamesema kuwa Mtume alikuwa na ami tisa: Abbas, Hamza, Abu Twalib, Zabeir, Harith, Hijla, Muqawwam, Dhirar na Abu Lahab. Na shangazi sita: Swafiya, Ummu Hakim al-baydhau, Atika, Umayma, Arwa na Barra (Assiratu nnabaawiya cha Ibn Hisham).

Na wakasema: “Mtume hakuwa na wajomba wala khalat (mama wadogo au wakubwa), kwa sababu mama yake Amina bint Wahb(a.s) hakuwa na kaka wala dada.” (Tafsir Ruuhul-bayan).

Sasa kuna wajihi gani wa Mwenyezi Mungu kusema: ‘Na mabinti wa ami zako, na mabinti wa shangazi zako, na mabinti wa wajomba zako na mabinti wa khalat zako?’

Jibu : Makusudio ya wajomba na khalat wa Mtume ni ukoo wa mama yake unaoitwa Bani Zuhra, ambao walikuwa wakisema: “Sisi ni wajomba zake Mtume.”

Na mwanamke mumin akijitoa mwenyewe kwa Nabii ikiwa Nabii anataka kumuoa. Ni halali kwako wewe tu, si kwa waumini wengine.

Katika mambo yanayomuhusu Mtume tu ni kumuoa mwanamke, akitaka, ikiwa atajitoa mwenye kwa Mtume bila ya mahari, kwa masharti ya kuwa mumini. Ndio! Inajuzu kwa mwinginewe kuoa kwa mahari, kisha mke asamehe mahari, kama anavyosamehe mtu yoyote mali yake kwa mwingine.

Tunajua tuliyowafaradhishia wao kuhusu wake zao na wale waliomi- likiwa na mikono yao ya kuume. Ili isiwe dhiki juu yako. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

Mwenyezi Mungu, ameweka idadi ya wake waungwana na akaharamisha mwanamke kujitoa mwenyewe bila mahari. Lakini akaliruhusu hilo kwa Mtume ili isiwe dhiki juu yake.

Vile vile kufahamisha utukufu wa cheo chake na juhudi zake. Mwenyezi Mungu (s.w.t) ndiye anayejua zaidi li lilo na masilahi zaidi kwa watu, akiwa anawahurumia na kuwaghufuria.

Unamwakhirisha umtakaye katika wao na na unamsogeza kwako umtakaye.

Katika Aya iliyotangulia Mwenyezi Mungu (s.w.t) amempa uhuru Mtume wake mtukufu katika idadi ya wanawake na katika Aya hii amempa hiyari ya kuongeza au kupunguza zamu ya yeyote anayemtaka.

Na unayemtaka katika uliyemtenga si vibaya kwako.

Yaani anaweza kumrudia aliyemaliza zamu naye na kumwacha aliyekuwa kwenye zamu yake. Kwa ibara ya wanaoimudu lugha ni, anaweza kumtanguliza wa mwisho na kumweka mwisho wa kwanza.

Hivyo itakuwa ni karibu zaidi kuburudika macho yao wala wasihuzunike na wawe radhi juu ya kile unachowapa wao wote.

‘Hivyo’ ni huko kuachiwa hiyari Mtume(s.a.w.w) . Maana ni kuwa wao wakijua kuwa hiyari ni yako sio yao ya zamu sawa, basi kila mmoja ataridhia na vile utakavyokuwa kwake kwa siku kidogo au nyingi kwa kujua kuwa ziada hiyo imetokana na wewe wala si wajibu kwako. Pamoja na hayo, lakini Mtume alikuwa akikaa siku sawa baina ya wake zake.

Na Mwenyezi Mungu anajua yaliyomo nyoyoni mwenu ya kupondokea zaidi kwa baadhi ya wake zenu kuliko wengine. Mwenyezi Mungu hayachukulii mapenzi yaliyo moyoni au chuki; isipokuwa anachukulia matendo. Hii ndio maana ya kauli yake Mwenyezi Mungu:

Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, Mpole.

Hawakuhalalikii wanawake baadaye wala kuwabadilisha kwa wake wengine, ijapo uzuri wao utakupendeza.

Wafasiri wametaja maana tatu za Aya hii; iliyo karibu zaidi na maana ya dhahiri ni ile isemayo kuwa Mwenyezi Mungu baada ya kumhalalishia Mtume wanawake aliowaishiria katika Aya iliyotangulia, amewajibisha katika Aya hii kutosheka na alio nao ambao walikuwa tisa na akaharamishiwa kumwacha yeyote katika wao na kuweka mwingine mahali pake, hata kama atakuwa amempendeza.

Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: ‘Ijapo uzuri wao utakupendeza’ inafahamisha kuwa mwanamume anaruhusiwa kumwangalia mwanamke anayetaka kumuoa.

Na ndio mafakihi wakalitolea fatwa hilio kwa kutegemea Aya hii na Hadith za Mtume mtukufu(s.a.w. w ) .

Isipokuwa uliyemmiliki kwa mkono wako wa kuume, aliokupa Mwenyezi Mungu katika mateka.

Na Mwenyezi Mungu ni Mchungaji wa kila kitu, hata kilicho siri na kwenye dhamiri:

وَهُوَ مَعَكُمْ أَيْنَ مَا كُنتُمْ ﴿٤﴾

“Naye yu pamoja nanyi popote mlipo.” (57:4).

4

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَدْخُلُوا بُيُوتَ النَّبِيِّ إِلَّا أَن يُؤْذَنَ لَكُمْ إِلَىٰ طَعَامٍ غَيْرَ نَاظِرِينَ إِنَاهُ وَلَـٰكِنْ إِذَا دُعِيتُمْ فَادْخُلُوا فَإِذَا طَعِمْتُمْ فَانتَشِرُوا وَلَا مُسْتَأْنِسِينَ لِحَدِيثٍ إِنَّ ذَٰلِكُمْ كَانَ يُؤْذِي النَّبِيَّ فَيَسْتَحْيِي مِنكُمْ وَاللَّـهُ لَا يَسْتَحْيِي مِنَ الْحَقِّ وَإِذَا سَأَلْتُمُوهُنَّ مَتَاعًا فَاسْأَلُوهُنَّ مِن وَرَاءِ حِجَابٍ ذَٰلِكُمْ أَطْهَرُ لِقُلُوبِكُمْ وَقُلُوبِهِنَّ وَمَا كَانَ لَكُمْ أَن تُؤْذُوا رَسُولَ اللَّـهِ وَلَا أَن تَنكِحُوا أَزْوَاجَهُ مِن بَعْدِهِ أَبَدًا إِنَّ ذَٰلِكُمْ كَانَ عِندَ اللَّـهِ عَظِيمًا ﴿٥٣﴾

53. Enyi ambao mmeamini! Msiingie majumba ya Mtume ila mkipewa ruhusa ya kwenda kula, sio kungojea kiive. Lakini mtakapoitwa, basi ingieni. Na mkisha kula, tawanyikeni wala msiweke mazungumzo. Hakika hayo yanamuudhi Nabii, naye anawastahi nyinyi. Lakini Mwenyezi Mungu hastahi kwa haki. Na mnapowaomba chombo cha nyumbani, basi waulize nyuma ya mapazia. Hilo linasafisha zaidi nyoyo zenu na nyoyo zao. Haiwafalii nyinyi kumuudhi Nabii wala kuwaoa wake zake kabisa. Hakika hilo ni kubwa mbele ya Mwenyezi Mungu.

إِن تُبْدُوا شَيْئًا أَوْ تُخْفُوهُ فَإِنَّ اللَّـهَ كَانَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمًا ﴿٥٤﴾

54. Mkidhihirisha chochote au mkikificha, basi hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.

لَّا جُنَاحَ عَلَيْهِنَّ فِي آبَائِهِنَّ وَلَا أَبْنَائِهِنَّ وَلَا إِخْوَانِهِنَّ وَلَا أَبْنَاءِ إِخْوَانِهِنَّ وَلَا أَبْنَاءِ أَخَوَاتِهِنَّ وَلَا نِسَائِهِنَّ وَلَا مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُنَّ وَاتَّقِينَ اللَّـهَ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ شَهِيدًا ﴿٥٥﴾

55. Hapana ubaya kwao kwa baba zao, wala watoto wao, wala kaka zao, wala watoto wa kaka zao, wala watoto wa dada zao, wala wanawake wao, wala wale waliomilikiwa na mikono yao ya kuume. Hakika Mwenyezi Mungu ni mwenye kushuhudia kila kitu.

MKISHAKULA TAWANYIKENI

Aya 53 – 55

MAANA

Enyi ambao mmeamini! Msiingie majumba ya Mtume ila mkipewa ruhusa ya kwenda kula, sio kungojea kiive. Lakini mtakapoitwa, basi ingieni. Na mkisha kula, tawanyikeni wala msiweke mazungumzo.

Yaani msikae kabisa si kwa mazungumzo wala kwa jambo jingine. Yametajwa mazungumzo kwa vile mara nyingi mtu anakaa kwa kupiga gumzo.

Dhahiri ya Aya inaonyesha kuwa baadhi ya maswahaba walikuwa wakiingia nyumba ya Mtume(s.a.w. w ) bila ya idhini kama ilivyo ada ya kijahiliya; na kwamba wakiona chakula kinapikwa basi wanakingoja na baada ya kula walikuwa wakipiga gumzo.

Hakuna mwenye shaka kwamba aina hii ya upuzi na kukosa adabu inamuudhi binadamu yeyote, awe Mtume au si Mtume. Ni kwa ajili hii Mtume(s.a.w. w ) aliwafundisha adabu mswahaba na wengineo kuwa wasiingie nyumba yoyote bila ya idhini ya wenyewe - hayo yamedokezwa kwenye Juz. 18 (24:28) – na kwamba wasiende kula ila wakiitwa, tena chakula kiwe kimeandaliwa na wakishamaliza kula wasingoje tena.

Haya hayahusiki na nyumba ya Mtume peke yake; isipokuwa Mwenyezi Mungu amemtaja yeye kwa vile ndio sababu ya kushuka Aya. Mara nyingi tumesema kuwa sababu ya kushuka Aya haiifungi na hilo lililoishukia.

Hakika hayo yanamuudhi Nabii, naye anawastahi nyinyi. Lakini Mwenyezi Mungu hastahi kwa haki.

Makusudio ya haki aliyokuwa akiistahi Mtume ni haki yake ya kiutu – kuwatoa wapuuzi nyumbani kwake. Mtume aliwanyamazia kwa kuwaonea haya; ndipo Mwenyezi Mungu (s.w.t) akatanabahisha kwamba kubaki kwao baada ya chakula kunamuudhi Mtume, vile vile kuingia kwao nyumbani kwake bila ya idhini yake.

Kuna Hadith isemayo: “Haya ni tawi la imani na asiyekuwa na haya hana dini.” Kuna Hadith nyingine isemayo:“Hakukubakia katika mifano ya mitume isipokuwa kauli ya watu: Kama huna haya basi fanya utakavyo.”

Katika maelezo ya wasifu wa Mtume(s.a.w. w ) ni kuwa yeye alikuwa na haya kuliko mwanamwali kwenye ushungi wake. Katika Nahjul-balagha imesemwa:“Hakuna imani kama haya na subira.” Farazdaq katika kumsifu Imam Zaynul-abdin anasema:

Hufumba macho kwa haya kwa haiba yake. Hazungumzi ila kuonekana tabasamu yake Maajabu ni yale yaliyoandikwa kwenye kitabu Muhadharatul-udabai cha Asfahaniy:

“Doezi mmoja alilaumiwa kwa kudoea kwake, akasema akijitetea: “Ala! Ikiwa bani Israil walimdoea Mungu, je sisi tusidoee watu?”

Na mnapowaomba chombo cha nyumbani, basi waulize ni nyuma ya mapazia. Hilo linasafisha zaidi nyoyo zenu na nyoyo zao.

Yaani mnapowaomba haja wakeze Mtume. Kutaja chombo cha chumbani ni kutolea mfano tu, sio kuhusisha na kuondoa hukumu kwa vingine. Hilo linafahamishwa na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Hilo linasafisha zaidi nyoyo zenu na nyoyo zao.” Inayotambulisha kuwa kuchanganyika na kuondoa pazia baina ya wanawake na wanaume kunaleta ufisadi na fitna.

Maana yake ni kuwa kuchanganyika ni haramu, au angalau ni bora kuacha. Hapa inatubainikia kuwa kuchanganyika ni sababu ya kuleta matamanio ya kijinsiya, na wala sio kumtia adabu mwanamke na kumkandamiza; kama wanavyodai wale wasemao: “Mungu amesema hivyo na mimi nasema hivi” Ni nani aliye mkweli zaidi kwa mazungumzo kuliko Mwenyezi Mungu?

Haiwafalii nyinyi kumuudhi Nabii wala kuwaoa wake zake kabisa. Hakika hilo ni kubwa mbele ya Mwenyezi Mungu.

Hukumu hii inamuhusu Mtume tu peke yake. Kwa sababu wakeze wako katika daraja ya mama wa waumini. Imeelezwa katika Tafsir Arrazi na Ruhul-bayan ya Ismail Haqiy: “Hakika Aya hii ilishuka pale aliposema Twalha bin Abdallah Attaymiy:“Akifa Muhammad(s.a.w. w ) nitamuoa Aisha.”

Hilo linataliwa nguvu na kauli yake Mwenyezi Mungu:

Mkidhihirisha chochote au mkikificha, basi hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.

Hilo ni karipio kwa yule aliyedhamiria kuoa wake za Mtume baada yake.

Hapana ubaya kwao kwa baba zao, wala watoto wao, wala kaka zao, wala watoto wa kaka zao, wala watoto wa dada zao, wala wanawake wao, wala wale waliomilikiwa na mikono yao ya kuume. Hakika Mwenyezi Mungu ni mwenye kushuhudia kila kitu.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kuamrisha kuzungumza na wanawake nyuma ya pazia (hijabu) hapa anavua wale ambao hawawezi kuoana nao, ambao ni: baba, mtoto, kaka, mtoto wa kaka na mtoto wa dada, mtumwa na wanawake. Lakini Mwenyezi Mungu amesema wanawake wao, yaani wanawake wenzao walio waumini, kwa sababu wasiokuwa waumini watawasifia wanaume zao.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 18 (24:31).

إِنَّ اللَّـهَ وَمَلَائِكَتَهُ يُصَلُّونَ عَلَى النَّبِيِّ يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا صَلُّوا عَلَيْهِ وَسَلِّمُوا تَسْلِيمًا ﴿٥٦﴾

56. Hakika Mwenyezi Mungu na malaika wake wanamswalia Nabii. Enyi ambao mmeami- ni! Mswalieni na mumsalimu kwa salamu.

إِنَّ الَّذِينَ يُؤْذُونَ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ لَعَنَهُمُ اللَّـهُ فِي الدُّنْيَا وَالْآخِرَةِ وَأَعَدَّ لَهُمْ عَذَابًا مُّهِينًا ﴿٥٧﴾

57. Hakika wale ambao wanamuudhi Mwenyezi Mungu na Mtume wake, Mwenyezi Mungu amewalaani duniani na Akhera, na amewaandalia adhabu ya kufedhehesha.

وَالَّذِينَ يُؤْذُونَ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ بِغَيْرِ مَا اكْتَسَبُوا فَقَدِ احْتَمَلُوا بُهْتَانًا وَإِثْمًا مُّبِينًا ﴿٥٨﴾

58. Na wale ambao wanawaudhi waumini wanaume na waumini wanawake pasi na wao kufanya, hakika wamebeba dhulma kubwa na dhambi kubwa.

MSWALIENI MTUME

Aya 56 – 58

MAANA

Hakika Mwenyezi Mungu na malaika wake wanamswalia Nabii. Enyi ambao mmeamini! Mswalieni na mumsalimu kwa salamu.

Makusudio ya Mwenyezi Mungu kumsalia Mtume ni kumridhia kumrehe- mu na kumsifu kwa kila kheri, swala ya malaika ni kumsifu, na kutoka kwa waumini ni kumwombea dua ya kuwa na daraja ya juu. Imam Ar-Ridha(a.s) aliulizwa kuhusu maana ya kauli ya Mwenyezi Mungu: malaika na waumini humswalia Mtume, akasema:“Swala kutoka kwa Mwenyezi Mungu ni rehema, kutoka kwa malaika ni kumsifu na kutoka kwa waumni ni kumwombea.”

Kuswaliwa huku hakuhusiki na risala ya Muhammad(s.a.w. w ) peke yake. Kila mtu anayetumia desturi ya risala ya Muhammad(s.a.w. w ) , kuifundisha au kuijulisha au kutaja fadhila yoyote katika fadhila zake basi atakuwa amemswalia, awe mumin au sio mumin, akitaka hilo au asitake.

Imam Ja’far As-Sadiq(a.s) anasema: “Mtu kumswalia Muhammad(s.a.w. w ) ni kama kusema:“Subhanallah walhamdulillah walailaha illaha wallahu akbar” (Kutakasika ni kwa Mwenyezi Mungu na sifa njema ni za Mwenyezi Mungu na hapana Mola isipokuwa Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu ni mkubwa).

Imam hapa anakusudia kuwa thawabu za kumswalia Mtume ni sawa na thawabu za tasbih, tahmid, tahlil na takbir. Imepokewa Hadith kutoka kwa Mtume mtukufu(s.a.w. w ) , amesema:“Bakhili wa kweli ni yule ambaye nikitajwa mbele yake haniswalii” .

VIPI TUTAMSWALIA MTUME?

Katika Sahih Al-Bukhariy Juz. 8, mlango wa kumswalia mtume, Tafsir At- Tabariy, Tafsir Ar-Raziy, Tafsir Al-Maraghi na wafasiri wengineo, pia katika vitabu vya Hadith, kuna maelezo haya: “Mtume aliulizwa: Vipi tutakuswalia ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?Akasema: semeni:

Allahumma swalli a’la muhammdi wa a’la aali Muhammad, kama swal-layta a’la Ibrahima wa a’laa aali Ibrahim, Innaka hamidum majiid Allahumma barik ala muhammdi wa a’la ali Muhammad, kama barakta a’la Ibrahima wa a’la ali Ibrahim, Innaka hamidum majid.

(Ewe Mwenyezi Mungu mswalie Muhammad na kizazi cha Muhammad, kama ulivyomswalia Ibrahim na kizazi cha Ibrahim, hakika wewe ni mwenye kusifiwa mwenye kutukuzwa. Ewe Mwenyezi Mungu mbariki Muhammad na kizazi cha Muhammad, kama ulivyombariki Ibrahim na kizazi cha Ibrahim. Hakika wewe ni Mwenye kusifiwa Mwenye kutukuzwa. )

Katika tafsir Ruhul-bayan ya Ismail Haqiy, amesema: “Inatakikana mwenye kuswali aseme: Allhumma swali a’la Muhammad wa a’la AliMuhammad” kwa kulirudia neno ‘a’la’; kwani Sunni wanaweka neno hilo kabla ya aali, kuwapinga Shia ambao hawaliweki neno hilo.

Sisi hatuoni tofauti yoyote baina ya anayesema: neno hilo na asiyelisema. Ama kuhusu ile Hadith isemayo:“Mwenye kutenganisha baina yangu na kizazi changu, hatapata shafaa yangu,” Mwenyezi Mungu ndiye anayejua zaidi usahihi wake.

Imam Shafii naye amesema katika shairi lenye maana hii: Enyi watu wa nyumba ya Mtume pendo lenu ni faradhi kutoka kwa Mwenyezi Mungu amelieleza katika Qur’an. Inawatosha kuwa ni cheo kikuu kwamba nyinyi asiyewaswalia hana Swala

Hakika wale ambao wanamuudhi Mwenyezi Mungu na Mtume wake Mwenyezi Mungu amewalaani duniani na Akhera, na amewaandalia adhabu ya kufedhehesha.

Makusudio ya kumuudhi Mwenyezi Mungu Mtukufu ni kumghadhabisha, na sababu yenye kuwajibisha hilo ni kumpinga, kumnasibishia mshirika au mtoto, au kuasi hukumu miongoni mwa hukumu zake. Na kuumuudhi Mtume(s.a.w. w ) ni kupinga utume wake au kupuuza mwenendo wake.

Laana kutoka kwa Mungu ni kwa kuwekwa mbali na rehema yake na kutoka kwa watu ni shutuma na kuombewa mabaya. Katika Nahjul-balagha imeelezwa:“Mwenyezi Mungu amewalaani wanaoamrisha mema na kuacha kuyatenda na wanaokataza maovu na wanayoyatenda.”

Na wale ambao wanawaudhi waumini wanaume na waumini wanawake pasi na wao kufanya, hakika wamebeba dhulma kubwa na dhambi kubwa.

Pasi na wao kufanya, yaani kufanya kosa linalostahili udhia. Kuudhi kunakuwa ni kwa kusengenya, vitimbi, uzushi n.k. Kuna Hadith zisemazo:

“Mwislamu ni yule ambaye watu wamesalimika na mkono wake na ulimi wake.”

“Utukufu wa mumin ni kwa kujizuia na kuwaudhi watu.”

“Aliye dhalili zaidi katika watu ni yule anayewadharau watu.”

Imam Ali(a.s) anasema: Mwenye hali mbaya zaidi katika watu ni yule asiyemwaamini yeyote kwa dhana zake mbaya, na asiyeaminiwa na yeyote kwa vitendo vyake vibaya.”

5

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

يَا أَيُّهَا النَّبِيُّ قُل لِّأَزْوَاجِكَ وَبَنَاتِكَ وَنِسَاءِ الْمُؤْمِنِينَ يُدْنِينَ عَلَيْهِنَّ مِن جَلَابِيبِهِنَّ ذَٰلِكَ أَدْنَىٰ أَن يُعْرَفْنَ فَلَا يُؤْذَيْنَ وَكَانَ اللَّـهُ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴿٥٩﴾

59. Ewe Nabii! Waambie wake zako na wake za waumini, wajiteremshie jalbab zao. Hilo ni karibu zaidi kuweza kujulikana wasiudhiwe. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

لَّئِن لَّمْ يَنتَهِ الْمُنَافِقُونَ وَالَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٌ وَالْمُرْجِفُونَ فِي الْمَدِينَةِ لَنُغْرِيَنَّكَ بِهِمْ ثُمَّ لَا يُجَاوِرُونَكَ فِيهَا إِلَّا قَلِيلًا ﴿٦٠﴾

60. Kama wanafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao, na wale wanaoeneza fitna Madina, hawataacha, basi kwa yakini tutakusalitisha juu yao, kisha hawatakaa humo karibu yako ila muda mchache tu.

مَّلْعُونِينَ أَيْنَمَا ثُقِفُوا أُخِذُوا وَقُتِّلُوا تَقْتِيلًا ﴿٦١﴾

61. Wamelaaniwa! Popote waonekanapo, na wakamatwe na wauliwe kabisa.

سُنَّةَ اللَّـهِ فِي الَّذِينَ خَلَوْا مِن قَبْلُ وَلَن تَجِدَ لِسُنَّةِ اللَّـهِ تَبْدِيلًا ﴿٦٢﴾

62. Ni desturi ya Mwenyezi Mungu iliyokuwa kwa wale waliopita zamani. Wala hutapata mabadiliko katika desturi ya Mwenyezi Mungu.

WAJIBU WA HIJABU

Aya 59 – 62

LUGHA

Kuna kauli nyingi kuhusu neno Jalbab: kuna wanaosema kuwa ni nguo inayomfunika mwanamke kutoka kichwani hadi nyayoni. Wengine wakasema ni ushungi unaofunika kichwa cha mwanamke na uso wake. Kauli hii ndio aliyo nayo mwenye Majmaul-Bayan.

MAANA

Zimekwishatangulia Aya mbili zinazofahamisha wajibu wa hijabu kwa wanawake:

Ya kwanza ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Wala wasidhihirishe uzuri wao ila kwa waume zao.” Juz. 18 (24: 31). Ya pili ni ile Aya ya 53, katika Sura hii tuliyo nayo: “Na mnapowaomba chombo cha nyum- bani, basi waulizeni nyuma ya mapazia.”

Aya iliyo wazi zaidi ya hizi mbili ni hii tuliyo nayo, isemayo:

Ewe Nabii! Waambie wake zako na wake za waumini, wajiteremshie nguo zao.

Kusema kwake Mwenyezi Mungu Mtukufu: ‘wajiteremshie nguo zao’ inaenea kusitiri na kufunika sehemu zote za mwili, kikiwemo kichwa na uso. Hilo linatiliwa nguvu na kauli yake Mwenyezi Mungu:

Hilo ni karibu zaidi kuweza kujulikana wasiudhiwe.

Waislamu, mwanzoni walikuwa wakitoka bila ya kujitanda, kama ilivyokuwa desturi ya kijahiliya, ndio Mwenyezi Mungu (s.w.t) akamtaka Mtume wake mtukufu, katika Aya hii, awaamrishe wake zake kujisitiri na kuvaa hijabu. Na amri inafahamisha wajibu. Kwa hiyo hijabu ni wajibu.

Hata hivyo uso na viganja viwili havimo kwenye wajibu huu, kutokana na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

وَلَا يُبْدِينَ زِينَتَهُنَّ إِلَّا مَا ظَهَرَ مِنْهَا ﴿٣١﴾

“Wala wasionyeshe uzuri wao, isipokuwa unaodhihirika.” Juz. 18 (24:31).

Hilo ni karibu zaidi kuweza kujulikana kutokana na kujistahi na kujichunga. Kwani hijabu ni kinga baina ya mwanamke na tamaa ya watu wenye shakashaka na mafasiki,wasiudhiwe kwa kuangaliwa na mafasiki.

Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

Anasamehe yaliyopita na anamuhurumia mwenye kutubia na kurejea nyuma.

Kama wanafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao, na wale wanaoeneza fitna Madina, hawataacha, basi kwa yakini tutakusalitisha juu yao, kisha hawatakaa humo karibu yako ila muda mchache tu.

Wanafiki walificha ukafiri na wakadhihirisha imani. Wanaoeneza fitna ni watu katika wananfiki waliokuwa wakieneza propaganda dhidi ya Mtume(s.a.w. w ) na maswahaba na wakawatia shaka wale wadhaifu wa imani ambao Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewaletea ibara ya wenye mardhi nyoyoni mwao. Aya inatoa onyo la kuuawa na kufukuzwa wanafiki, waeneza fitna na wale watakaowasikiliza, ikiwa hawatajizuia na upotevu na ufisadi wao.

VITA VYA NAFSI

Siku hizi kueneza fitna kunaitwa ‘vita vya nafsi.’ Nguvu ya shari imetafuta njia nyingi sana za kueneza uongo na mambo ya ubatilifu kwa kila nyenzo. Kuanzia magazeti, radio, runinga, sinema, hotuba, vipeperushi, shule, vyuo, vitabu n.k.

Vyombo hivi vimekaririka masikioni mwa watu kila siku, kiasi ambacho uhakika haupati nafasi kwa watu na wenye ikhlasi, isipokuwa kwa mwamko mkamilifu na elimu itakayotangulia propaganda za wakoloni na wazayuni.

Nimesoma kwenye gazeti linaloitwa Akhabar Al-yawm la Misr, la 13/12/69, kwamba Israil ina magazeti ya propaganda yanayofikia 890 ulimwenguni kwa ajili ya kueneza habari za uongo. Zaidi ya hayo wametawala vyombo vingi vya habari ulimwenguni, kwa njia isiyokuwa ya moja kwa moja; kama vile runinga, radio n.k.

Kwenye mahisabu haya hayaingii magazeti ya Beiruti yenye uhusiano mkubwa na wakoloni na wazayuni.

Kwa vyovyote iwavyo, Alhamdu lillah, Israil imehisi mapigo kutoka kwa waarabu na kwamba propaganda zao zilizotengenezwa na Marekani, na kutangazwa na vibaraka, zimeanza kujulikana.

Wamelaaniwa! Popote waonekanapo na wakamatwe na wauliwe kabisa.

Wamelaaaniwa na kila ulimi, kwa sababu dini yao ni pesa na matendo yao ni udanganyifu, uwongo na hadaa. Hawana dawa isipokuwa kuuawa popote walipo; kama kiungo kilichoharibika, kisipokatwa kitaharibu mwili wote.

Ni desturi ya Mwenyezi Mungu iliyokuwa kwa wale waliopita zamani. Wala hutapata mabadiliko katika desturi ya Mwenyezi Mungu.

Makusudio ya desturi ya Mwenyezi Mungu hapa ni hukumu ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwa mpotevu anayepoteza, ambayo ni kuuliwa ambako amekuwekea sharia, ambaye imetukuka hekima yake, tangu zamani. Hukumu hii itabakia milele bila ya mabadiliko wala mageuzi.

يَسْأَلُكَ النَّاسُ عَنِ السَّاعَةِ قُلْ إِنَّمَا عِلْمُهَا عِندَ اللَّـهِ وَمَا يُدْرِيكَ لَعَلَّ السَّاعَةَ تَكُونُ قَرِيبًا ﴿٦٣﴾

63. Watu wanakuuliza kuhusu Saa. Sema: Ujuzi wake uko kwa Mwenyezi Mungu tu. Na nini kitakachokujulisha? Pengine hiyo saa iko karibu.

إِنَّ اللَّـهَ لَعَنَ الْكَافِرِينَ وَأَعَدَّ لَهُمْ سَعِيرًا ﴿٦٤﴾

64. Hakika Mwenyezi Mungu amewaandalia makafiri moto unaowaka.

خَالِدِينَ فِيهَا أَبَدًا لَّا يَجِدُونَ وَلِيًّا وَلَا نَصِيرًا ﴿٦٥﴾

65. Watadumu humo milele. Hawatapata mlinzi wala wa kuwanusuru.

يَوْمَ تُقَلَّبُ وُجُوهُهُمْ فِي النَّارِ يَقُولُونَ يَا لَيْتَنَا أَطَعْنَا اللَّـهَ وَأَطَعْنَا الرَّسُولَا ﴿٦٦﴾

66. Siku ambayo nyuso zao zitapinduliwa pinduliwa katika Moto. Watasema: Laiti tungelimtii Mwenyezi Mungu na tungelimtii Mtume!

وَقَالُوا رَبَّنَا إِنَّا أَطَعْنَا سَادَتَنَا وَكُبَرَاءَنَا فَأَضَلُّونَا السَّبِيلَا ﴿٦٧﴾

67. Na watasema: Mola wetu! Hakika sisi tuliwatii mabwana zetu na wakubwa wetu, wakatupoteza njia.

رَبَّنَا آتِهِمْ ضِعْفَيْنِ مِنَ الْعَذَابِ وَالْعَنْهُمْ لَعْنًا كَبِيرًا ﴿٦٨﴾

68. Mola wetu wape adhabu mara mbili, na walaani laana kubwa.

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَكُونُوا كَالَّذِينَ آذَوْا مُوسَىٰ فَبَرَّأَهُ اللَّـهُ مِمَّا قَالُوا وَكَانَ عِندَ اللَّـهِ وَجِيهًا ﴿٦٩﴾

69. Enyi ambao mmeamini! Msiwe kama wale ambao walimuudhi Musa, lakini Mwenyezi Mungu akamtaksa na waliyoyasema; naye alikuwa ni mwenye heshima mbele ya Mwenyezi Mungu.

WANAKUULIZA KUHUSU SAA

Aya 63 – 69

MAANA

Watu wanakuuliza kuhusu Saa. Sema: Ujuzi wake uko kwa Mwenyezi Mungu tu. Na nini kitakachokujulisha? Pengine hiyo saa iko karibu.

Makusudio ya saa ni Kiyama Umetangulia mfano wake katika Juz. 9 (7:187).

Hakika Mwenyezi Mungu amewaandalia makafiri moto unaowaka. Watadumu humo milele. Hawatapata mlinzi wala wa kuwanusuru. Siku ambayo nyuso zao zitapinduliwa pinduliwa katika Moto. Watasema: Laiti tungelimtii Mwenyezi Mungu na tungelimtii Mtume!

Makafiri na waasi kesho watasukumwa kwenye adhabu ya moto, hawatakuwa na msaidizi wala udhuru. Watauma vidole vyao kwa kujutia walivyomuasi Mwenyezi Mungu na Mtume, lakini ‘majuto ni mjukuu.’

Umetangulia mfano wake katika Juz. 19 (25:27).

Na watasema: Mola wetu! Hakika sisi tuliwatii mabwana zetu na wakubwa wetu, wakatupoteza njia. Mola wetu wape adhabu mara mbili, na walaani laana kubwa.

Makusudio ya mabwana na wakubwa ni viongozi wa dini na dunia. Laana ni kufedheheka. Wadhaifu watawageuzia adhabu na watamtaka Mwenyezi Mungu awaongezee adhabu.

Mwenye kuichunguza historia ataona kwamba aghlabu umma wa kijinga unaongozwa na mataghuti na waovu. Lakini watu wenye mwamko na maarifa hawaamini kuweka masilahi yao isipokuwa kwa waaminifu wenye ikhlasi.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 8 (7:38).

Enyi ambao mmeamini! Msiwe kama wale ambao walimuudhi Musa, lakini Mwenyezi Mungu akamtaksa na waliyoyasema; naye alikuwa ni mwenye heshima mbele ya Mwenyezi Mungu.

Waliomuudhi Musa(a.s) ni Wana wa Israil, hilo halina shaka; ambapo walimsifu sifa zisizokuwa za mitume.

Aya hii inaashiria kwamba badhi ya swahaba walimuudhi Mtume mtukufu(s.a.w.w) na wakambandika mambo asiyokuwa nayo, ndipo Mwenyezi Mungu (s.w.t) akawakataza waislamu hilo.

Kuna riwaya inayosema kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) siku moja aliapa, basi mtu mmoja katika Answar akasema: “Kiapo hiki hakikusudiwa radhi ya Mwenyezi Mungu.” Hapo uso wa Mtume ukaiva wekundu na akasema:“Amrehemu Musa, hakika aliudhiwa zaidi ya hivi na akasubiri.”

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّـهَ وَقُولُوا قَوْلًا سَدِيدًا ﴿٧٠﴾

70. Enyi ambao mmeamini! Mcheni Mwenyezi Mungu na semeni kauli ya sawa.

يُصْلِحْ لَكُمْ أَعْمَالَكُمْ وَيَغْفِرْ لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ وَمَن يُطِعِ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ فَقَدْ فَازَ فَوْزًا عَظِيمًا ﴿٧١﴾

71. Atawatengenezea matendo yenu na atawaghufiria dhambi zenu. Na mwenye kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hakika amefuzu kufuzu kukubwa.

إِنَّا عَرَضْنَا الْأَمَانَةَ عَلَى السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَالْجِبَالِ فَأَبَيْنَ أَن يَحْمِلْنَهَا وَأَشْفَقْنَ مِنْهَا وَحَمَلَهَا الْإِنسَانُ إِنَّهُ كَانَ ظَلُومًا جَهُولًا ﴿٧٢﴾

72. Kwa hakika tulizitolea amana mbingu na ardhi na milima na vikakataa kuichukua na vikaiogopa, lakini mwanadamu akaichukua. Hakika yeye ni dhalimu mkubwa, mjinga sana,

لِّيُعَذِّبَ اللَّـهُ الْمُنَافِقِينَ وَالْمُنَافِقَاتِ وَالْمُشْرِكِينَ وَالْمُشْرِكَاتِ وَيَتُوبَ اللَّـهُ عَلَى الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ وَكَانَ اللَّـهُ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴿٧٣﴾

73. Ili Mwenyezi Mungu awaadhibu wanafiki wanaume na wanafiki wanawake na washirikina wanaume na washirikina wanawake; na awapokelee toba waumini wanaume na waumini wanawake. Na Mwenyezi Mungu ni mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

TULIZITOLEA AMANA

Aya 70 – 73

MAANA

Enyi ambao mmeamini! Mcheni Mwenyezi Mungu na semeni kauli ya sawa. Atawatengenezea matendo yenu na atawaghufiria dhambi zenu.

Kauli ya sawa ni kusema haki na ukweli, bila ya kuficha kitu; hata kama inamuhusu mwenyewe. Makusudio yake hapa ni ile inayowanufaisha watu kwa kulinganisha na kauli yake Mwenyezi Mungu ‘Atawatengenezea amali zenu;’ ambapo Mwenyezi Mungu (s.w.t) amejaalia kauli ya haki ni sababu ya matendo mema; kwa mfano kumwongoza aliyepotea kwenye njia ya heri na amani, kumsaidia aliyedhulumiwa kwa neno la usawa au kauli ambayo italeta suluhu baina ya watu wawili na mengineyo yanay- owanufaisha watu kwa namna moja au nyingine.

Na mwenye kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hakika amefuzu kufuzu kukubwa.

Atafuzu duniani kwa kufaulu na kuwa na sera nzuri na katika Akhera atafuzu kwa kupata radhi za Mwenyezi Mungu na thawabu zake.

Kwa hakika tulizitolea amana mbingu na ardhi na milima na vikakataa kuichukua na vikaiogopa, lakini mwanaadamu akaichukua.

Wafasiri wametofautiana kuhusu maana ya amana. Kuna waliosema kuwa ni taklifa na twaa. Wengine wakasema ni tamko la Lailaha illahha (Hapana Mola isipokuwa Mwenyezi Mungu). Kuna waliosema ni viungo vya mwanadamu; kama masikio yake, macho yake, mikono yake na miguu yake. Kwamba ni juu yake kuvitumia kwa ajili ya lengo lilioumbiwa. Pia kuna wale waliosema kuwa ni amana katika mali.

Tuonavyo sisi maana yake ni kujitolea muhanga kwa ajili ya manufaa ya jamii, si kwa lololote isipokuwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu na ya ubinadamu.

Kwa sababu kujitolea huku ni kuzito na kukubwa kiasi ambacho maumbile yenye nguvu zaidi, kama mbingu, ardhi na majabali yangelikataa kubeba, kama yangelikuwa na hisia.

Kwa hiyo lengo la kutaja mbingu na ardhi ni kuashiria ukubwa wa kuji- tolea huku, na kwamba binadamu ni kiumbe pekee anayeweza kupingana na nafsi yake na matamanio yake.

Ama kauli yake Mwenyezi Mungu:Hakika yeye ni dhalimu mkubwa, mjinga sana, maana yake ni kuwa binadamu atajidhulumu yeye mwenyewe na mwingine ikiwa ataifanyia hiyana amana hii na kutojua mwisho muovu utakotokana na hiyana yake hiyo.

Ili Mwenyezi Mungu awaadhibu wanafiki wanaume na wanafiki wanawake ambao wanajionyesha kuwa wanatekeleza amana, lakini kumbe ni wahaini.

Na washirikina wanaume na washirikina wanawake. Mwenyezi Mungu atawaadhibu kwa vile kosa la ushirikina haliwezi kufutwa hata na kujitolea muhanga.

Na awapokelee toba waumini wanaume na waumini wanawake. Na Mwenyezi Mungu ni mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

Yaani anawaghufiria wenye kutubia na kuwahurumia wanyonge. Ewe Mwenyezi Mungu mrehemu Muhammad na kizazi chake, rehema ambayo atatuombea nayo siku tutakapohitajia.

MWISHO WA SURA YA THELATHINI NA TATU: SURAT AL-AHZAB


3

4

5

6

7

8

9