TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA TISA Juzuu 9

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA TISA22%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA TISA Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

Juzuu 9
Juzuu 1
  • Anza
  • Iliyopita
  • 15 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 12114 / Pakua: 2208
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA TISA

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA TISA Juzuu 9

Mwandishi:
Swahili

2

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA TISA

تِلْكَ الْقُرَىٰ نَقُصُّ عَلَيْكَ مِنْ أَنبَائِهَا وَلَقَدْ جَاءَتْهُمْ رُسُلُهُم بِالْبَيِّنَاتِ فَمَا كَانُوا لِيُؤْمِنُوا بِمَا كَذَّبُوا مِن قَبْلُ كَذَٰلِكَ يَطْبَعُ اللَّـهُ عَلَىٰ قُلُوبِ الْكَافِرِينَ ﴿١٠١﴾

101. Miji Hiyo tunakusimulia baadhi ya habari zake, Hakika waliwajia Mitume wao kwa ishara zilizo wazi-wazi, lakini hawakuwa wenye kuamini waliyoyakadhibisha zamani, Namna hii Mwenyezi Mungu anazipiga muhuri nyoyo za makafiri.

وَمَا وَجَدْنَا لِأَكْثَرِهِم مِّنْ عَهْدٍ وَإِن وَجَدْنَا أَكْثَرَهُمْ لَفَاسِقِينَ ﴿١٠٢﴾

102. Na hatukuona kwa wengi wao ahadi yoyote. Na hakika tuliwakuta wengi wao ni mafasiki.

MIJI HIYO TUNAKUSIMULIA

Aya 101 – 102

MAANA

Miji hiyo tunakusimulia baadhi ya habari zake.

Miji hiyo ni ishara ya watu wa miji hiyo ambao ni aina tano: Watu wa Nuh, wa Hud, wa Swaleh, wa Lut na wa Shuaib.

Maneno yanaelekezwa kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu, Nabii Muhammad(s.a.w.w) wakikusudiwa waislamu kupewa habari ya hali za waliopita, ili wazingatie na watahadhari.

Hakika waliwajia Mitume wao kwa ishara zilizo waziwazi, lakini hawakuwa wenye kuamini waliyoyakadhibisha zamani.

Ametaja Razi njia tatu za kutafsiri kipande hiki cha Aya, na Tabrasi naye akazidisha ya nne. Hakuna hata moja waliyoitilia nguvu, na wakamwacha msomaji wa kawaida kwenye mataa; ambapo maana yako wazi yasiyokuwa na undani wowote.

Kwa ufupi ni kuwa watu wa miji hiyo kabla ya kupelekewa Mitume wa Mwenyezi Mungu, walikuwa kwenye shirki na upotevu; na kwamba wao waliendelea katika shirki yao na upotevu baada ya kuwafikia Mitume kwa dalili na miujiza. Na hawakuathirika na chochote, wakawa kama ambao hawakupelekewa mjumbe anayetoa bishara na maonyo. Haya yanafahamishwa na kauli yake Mwenyezi Mungu:

Namna hii Mwenyezi Mungu anazipiga muhuri nyoyo za makafiri.

Muhuri hapa ni fumbo la kususuwaa kwa nyoyo zao na kwamba hazijali kupotea kwake wala haitarajiwi kheri yake.

Na hatukuona kwa wengi wao ahadi yoyote.

Hawaamini dini ya Mwenyezi Mungu wala hawalazimiani na chochote kinachohusiana na ubinadamu. Hata hivyo wanayo ahadi moja tu wanayolazimiana nayo wala hawapingani nayo, nayo ni kufuata masilahi na hawaa.

Na hakika tuliwakuta wengi wao ni mafasiki.

Yaani wamepotea kufuata njia.

ثُمَّ بَعَثْنَا مِن بَعْدِهِم مُّوسَىٰ بِآيَاتِنَا إِلَىٰ فِرْعَوْنَ وَمَلَئِهِ فَظَلَمُوا بِهَا فَانظُرْ كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ الْمُفْسِدِينَ ﴿١٠٣﴾

103. Kisha baada yao tukamtuma Musa na ishara zetu kwa Firauni na wakuu wake lakini wakazikanusha. Basi tazama jinsi ulivyokuwa mwisho wa wafisadi.

وَقَالَ مُوسَىٰ يَا فِرْعَوْنُ إِنِّي رَسُولٌ مِّن رَّبِّ الْعَالَمِينَ ﴿١٠٤﴾

104. Akasema Musa: Ewe Firauni! Hakika mimi ni Mtume nitokaye kwa Mola wa walimwengu.

حَقِيقٌ عَلَىٰ أَن لَّا أَقُولَ عَلَى اللَّـهِ إِلَّا الْحَقَّ قَدْ جِئْتُكُم بِبَيِّنَةٍ مِّن رَّبِّكُمْ فَأَرْسِلْ مَعِيَ بَنِي إِسْرَائِيلَ ﴿١٠٥﴾

105. Yanipasa nisiseme juu ya Mwenyezi Mungu isipokuwa haki. Nimewajia na dalili wazi itokayo kwa Mola wenu. Basi waache wana wa Israel waende nami.

قَالَ إِن كُنتَ جِئْتَ بِآيَةٍ فَأْتِ بِهَا إِن كُنتَ مِنَ الصَّادِقِينَ ﴿١٠٦﴾

106. Akasema: Ikiwa umekuja na ishara, basi ilete ukiwa ni miongoni mwa wasemao kweli.

فَأَلْقَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ ثُعْبَانٌ مُّبِينٌ ﴿١٠٧﴾

107. Akaitupa fimbo mara ikawa nyoka dhahiri.

وَنَزَعَ يَدَهُ فَإِذَا هِيَ بَيْضَاءُ لِلنَّاظِرِينَ ﴿١٠٨﴾

108. Na akautoa mkono wake. Mara ukawa mweupe kwa watazamao.

قَالَ الْمَلَأُ مِن قَوْمِ فِرْعَوْنَ إِنَّ هَـٰذَا لَسَاحِرٌ عَلِيمٌ ﴿١٠٩﴾

109. Wakasema wakuu wa watu wa Firauni: Hakika huyu ni mchawi mjuzi.

يُرِيدُ أَن يُخْرِجَكُم مِّنْ أَرْضِكُمْ فَمَاذَا تَأْمُرُونَ ﴿١١٠﴾

110. Anataka kuwatoa katika ardhi yenu. Basi mnatoa shauri gani?

قَالُوا أَرْجِهْ وَأَخَاهُ وَأَرْسِلْ فِي الْمَدَائِنِ حَاشِرِينَ ﴿١١١﴾

111. Wakasema: Mwache kidogo yeye na ndugu yake, na uwatume wakusanyao watu mijini.

يَأْتُوكَ بِكُلِّ سَاحِرٍ عَلِيمٍ ﴿١١٢﴾

112. Wakuletee kila mchawi, mjuzi.

MUSA NA FIRAUNI

Aya 103 – 112

MUHTASARI WA KISA

Tumepitia Aya kadhaa zinazoeleza kisa cha Nabii Musa(a.s) na wa Israel. Sasa tunaeleza kisa cha Nabii Musa(a.s) na Firauni katika Aya hizi tunazofasiri.

Neno ‘Firauni’ ni msimbo wa wafalme wa Misri wa zamani; kama vile msimbo wa Kaizari kwa wafalme wa Roma, Kisra kwa wafalme wa Fursi (Iran ya sasa) na Najashi kwa wafalme wa Uhabeshi (Ethiopia ya sasa).

Imenukuliwa kutoka kwa wale wanaojishughulisha sana na Historia ya Misri ya zamani, kwamba jina la Firauni aliyekuwa wakati wa Nabii Musa ni Munfitah.

JINA LA MAMAKE MUSA NA VIGANO

Ama Nabii Musa(a.s) ni mtoto wa Imran ambaye watu wa Kitab wanamwita Imram. Katika Juz.1 (2:51), tumeeleza kwamba jina la Nabii Musa ni maneno mawili yaliyochanganywa: neno ‘Mu’ lenye maana ya maji na ‘Sa ‘ lenye maana ya mti. Kwa sababu mama yake alimweka katika sanduku, akalifunga kufuli na akalitupa katika mto Nile kwa kumhofia Fir’aun.

La kushangaza ni uzushi wa mgunduzi wa kufuli hii, aliyotumia mama yake Nabii Musa kumfungia mwanawe, kuzusha kigano kilichoenea na kutangaa karne kwa karne na ambacho wamekiamini wapuzi wengi.

Nacho ni kuwa hakuna kufuli yoyote ila hufunguka ikisomewa jina la mama yake Nabii Musa. Kwa ajili hii hawalijui jina hilo isipokuwa watu maalum wenye siri.

Siku moja nilikwenda kwa mtu mmoja katika watu wa dini mwenye jina kubwa kati ya watu wake. Nikamkuta anapekua kwa hima sana mijalada ya kitabu Biharul-Anwar cha Allama Majlisi. Nikamwuliza: “Kwani una nini?” Akajibu: “Ninataka kujua jina la mama yake Nabii Musa.”

Miaka miwili iliyopita, bwana mmoja alinifuata akidhani mimi ni katika watu wa siri na kuniuliza jina la mama yake Nabii Musa. Nikamwambia: “Wewe wajua zaidi kuliko mimi,” lakini hakukubali. Nikamwambia: “Lakini huu ni upuuzi.” Akaona kuwa mimi namuhepa tu, sitaki kumfichulia siri hii. Nilipokata tamaa kabisa ya kumtuliza nikamwambia: “Haifai nikufichulie, kwa sababu sikuamini, utaiba mali za watu.” Basi akaapa kwa kiapo kizito kwamba yeye hataiba lakini mimi nikajifanya simwamini.

Siku zikapita nikaingilia kufasiri Qur’an Tukufu, nilipofika Aya hii nikawa narudia rejea mbalimbali, miongoni mwazo ni kitabu Qasasul–Quran kili- choandikwa na waandishi wane wa Kimisri: Muhammad Ahmad Jadul-Maula, Ali Muhammad Al-Bajawi, Muhamad Abul-Fadhl na Sayyid Shahatih, mara nikaona jina la mama yake Nabii Musa Yukabid (Jochebed) lakini watungaji hawakulinasibisha kwenye chimbuko lake.

Baada ya kutoka nje kidogo, turudie kisa cha Musa na Firauni; kama kilivyokuja katika Aya tulizo nazo. Kwa ufupi maana yake ni kwamba Firauni alikuwa akidai uungu badala ya Mwenyezi Mungu na alikuwa akiwakandamiza WaIsrael.

Mwenyezi Mungu akamtuma Nabii Musa na Harun kwa Firauni. Wakaenda na kujitosa kwenye kikao chake bila ya kuhofia usultani na utaghuti wake. Nabii Musa akamkabili na kumwambia: “Ewe Firauni! Mimi ni Mtume kutoka kwa Mola wa viumbe vyote nimetumwa kwako na kwa kila mpizani; na ninayo yanayothibitisha ujumbe wangu, Sasa waache waisrael na uwape uhuru waende watakapo”

Firauni akadharau akasema: “Lete hayo yanayothibitisha utume wako.” Nabii Musa akaitupa fimbo yake mara ikawa nyoka. Akaweka mkono wake kwenye mfuko wa kanzu yake alipoutoa ukawa unameremeta kwa weupe, na Nabii Musa hakuwa mweupe bali maji ya kunde.

Watu wa Firauni na halmashauri yake wakasema huyu ni mchawi bingwa, Basi Firauni akawakusanya wachawi. Kabla ya kuanza mazingaombwe yao walimwambia Firauni, “Je, tutapata malipo tukimshinda Musa?” Akasema: “Mtakuwa na malipo na kuwa karibu yangu.”

Wachawi wakaanza kutupa kamba na fimbo zao; mara watazamaji wakaona ni kama nyoka wanaotembea, Nabii Musa akatupa fimbo yake, ikameza yote waliyoyabuni. Wale wachawi wakasilimu na kuamini utume wa Nabii Musa. Firauni akawatishia kuwaadhibu na kuwatesa, lakini hawakurudi nyuma na wakathibiti kwenye imani yao, Riwaya nyingi zimeeleza kuwa Firauni alitekeleza vitisho vyake. Na hali ilivyo inalitilia nguvu hilo.

Firauni akawa anampa Nabii Musa na waliokuwa pamoja naye aina kwa aina za adhabu, lakini Nabii Musa aliendelea na mwito wake kwa Mwenyezi Mungu. waisrael wakampigia kelele Nabii Musa: “Tumeudhiwa kabla ya wewe kutujia na baada ya kutujia pia.” Nabii Musa akawaamuru kuvumilia na kuwapa tamaa ya kufaulu.

Mwenyezi Mungu akawaadhibu watu wa Firauni kwa kahati na dhiki. Akawapelekea mvua ya kuharibu mimea na mazao yao, nzinge waliokula vilivyobakishwa na athari ya mafuriko, chawa waliouma miili yao na vyura walioharibu maisha yao. Zaidi ya haya yote, maji yao yaligeuka na kuwa damu.

Hapo walifazaika kwa Nabii Musa. Wakamwambia: “Mola wako akituondolea adhabu tutakuwa miongoni mwa walioamini.” Mwenyezi Mungu akawaondoloea adhabu ili nao warejee, lakini wakavunja ahadi na wakaendelea na ukafiri. Mwenyezi Mungu akawaangamiza kwenye bahari na ikakatwa mizizi ya makafiri. Huu ndio muhtasari wa haraka haraka unaoelezwa na Aya tulizo nazo kuanzia Aya (103) mpaka mwisho wa Aya (137).

Sasa tufafanue yanayofahamishwa na Aya hizo.

MAANA

Kisha baada yao tukamtuma Musa na ishara zetu kwa Fir’aun na wakuu wake lakini wakazikanusha.

Dhamir ya baada yao inawarudia Mitume watano. Nuh, Hud, Swaleh, Lut na Shuaib. Ishara alizotumwa nazo Nabii Musa ni miujiza inayofahamisha utume wake. Wakuu wa Fir’aun, ni wale watukufu wa watu wake ambao mambo yote yako mikononi mwao, wengine ni kufuata na kunyenyekea tu.

Basi tazama jinsi ulivyokuwa mwisho wa wafisadi.

Ambao ni Fir’aun na wasaidizi wake waliozikalia shingo za watu. Mwisho huu utaelezwa katika mfumo mzima wa maelezo.

Akasema Musa: Ewe Firauni! Hakika mimi ni Mtume nitokaye kwa

Mola wa walimwengu.

Hivi ndivyo alivyomwita, “Ewe Firauni” bila ya kumtukuza na kumwadhimisha. Kwa sababu Nabii Musa alikuwa akizungumza lugha ya Mwenyezi Mungu na akafiksha ujumbe wa Mwenyezi Mungu ambao unamfanya mdogo mkubwa yeyote.

Kutokana na hivi ndio tunajua siri ya sera ya watu wema, wakijitukuza kwa mafasiki na kuwanyenyekea kwa udhalili na huruma waumin.

Yanipasa nisiseme juu ya Mwenyezi Mungu isipokuwa haki.

Hivi ndivyo ilivyo kwa kila Mtume aliyeaminiwa na Mwenyezi Mungu juu ya wahyi na kumchaguwa kuwa ni mjumbe wake.

Nimewajia na dalili wazi itokayo kwa Mola wenu.

Inayofahamisha kuwa mimi ni Mtume kutoka kwa Mola wa walimwengu.

Basi waache wana wa Israel waende nami.

Firauni alikuwa amewafanya waisraili watumwa na kuwatumia katika kazi ngumu, Ndipo Nabii Musa akataka waachiwe huru waende popote watakapo.

Akasema: Ikiwa umekuja na ishara, basi ilete ukiwa ni miongoni mwa wasemao kweli.

Inaonyesha kuwa Firauni alikuwa akidhani kuwa Nabii Musa ni mwongo katika madai yake, akataka kumfedhesha mbele ya wakuu, akamwambia: “Ilete hiyo hoja kama ni mkweli.” Nabii Musa akamziba mdomo wake kwa hoja mkataa.

Akatupa fimbo yake, mara ikawa nyoka dhahir . yaani nyoka halisi. Hapo Firauni akafazaika, lakini akajikaza kwa vile alikuwa akidai kuwa yeye ni Mungu Mkuu.

Nabii Musa tena akamshutukizia na muujiza wa pili.Na akautoa mkono wake. Mara ukawa mweupe kwa watazamao na mkono wa Nabii Musa ulikuwa rangi ya kahawia, sasa umekuwaje mweupe bila ya ugonjwa wowote?

Fir’aun akahisi unyonge na udhalili, akajiona yuko chini kabisa. Wale waliokaa naye wakatambua hilo kwamba Nabii Musa amewangusha kutoka juu.

Wakasema wakuu wa watu wa Firauni: Hakika huyu ni mchawi mjuzi.

Hiyo ndiyo hoja ya mwenye kushindwa nayo ni kutuhumu watu wema. Kisha wakuu wakaendelea kusema:

Anataka kuwatoa katika ardhi yenu .

Yaani Nabii Musa anataka kuwaondoa kwenye ufalme. Fir’aun aliposikia hivi akasema:

Basi mnatoa shauri gani? Wakasema: Mwache kidogo yeye na ndugu yake kwa sababu ukiwaua, watu watakasirika na utawala wako utakuwa hatarini.

Na uwatume mijini wakusanyao Yaani askariWakuletee kila mchawi mjuzi.

Watu wa Historia wanasema kuwa nchi ya Misri wakati wa Mafir’aun ilikuwa ikichemka na uchawi. Makuhani na waangalizi wa miungu ndio waliokuwa wakiendeleza kazi ya Uchawi. Anasema Aqqad katika Kitabu Iblisi kwenye kifungu cha Maendeleo ya Kimisr:

“Mafirauni wenyewe walikuwa wakikimbilia wachawi kwa kushindana na roho zilizojifiicha. Na tunayo mabaki ya visa vya uchawi ambayo hawakuyachagua wanaokusanya athari, lakini waliafikiana kuwa ni kazi za kichawi.

Walikuwa wakiugawanya uchawi kwenye mafungu: Kuna ule unaosaidiwa na uwezo wa mungu wa kheri dhidi ya mungu wa shari na ule unaosaidiwa na uwezo wa shetani mkubwa dhidi ya shetani mdogo.”

Kuenea uchawi wakati wa Firauni kunatufasiria sisi fimbo ya Nabii Musa na unatilia nguvu msingi unasema kuwa kila mwujiza wa Mtume ulikuja kulingana na aina iliiyoenea wakati wake, ili ushindi uwe mkubwa katika hoja na kukata kila udhuru – hoja mkataa.

Kwa hiyo Nabii Musa alivunja uchawi kwa vile ulienea zama zake.

Nabii Isa akafufua wafu, na Nabii Muhammad akawanyamazisha wanafasihi, kwa lengo hilo hilo.

وَجَاءَ السَّحَرَةُ فِرْعَوْنَ قَالُوا إِنَّ لَنَا لَأَجْرًا إِن كُنَّا نَحْنُ الْغَالِبِينَ ﴿١١٣﴾

113. Wakaja wachawi wa Firauni, wakasema: Tutapata ujira ikiwa tutashinda?

قَالَ نَعَمْ وَإِنَّكُمْ لَمِنَ الْمُقَرَّبِينَ ﴿١١٤﴾

114. Akasema: Ndio, nanyi hakika mtakuwa miongoni mwa wanaokurubishwa.

قَالُوا يَا مُوسَىٰ إِمَّا أَن تُلْقِيَ وَإِمَّا أَن نَّكُونَ نَحْنُ الْمُلْقِينَ ﴿١١٥﴾

115. Wakasema: Ewe Musa utatupa wewe au tutupe sisi?

قَالَ أَلْقُوا فَلَمَّا أَلْقَوْا سَحَرُوا أَعْيُنَ النَّاسِ وَاسْتَرْهَبُوهُمْ وَجَاءُوا بِسِحْرٍ عَظِيمٍ ﴿١١٦﴾

116. Akasema: Tupeni. Walipotupa waliyazuga macho ya watu na wakawaogopesha, wakaleta uchawi mkubwa.

وَأَوْحَيْنَا إِلَىٰ مُوسَىٰ أَنْ أَلْقِ عَصَاكَ فَإِذَا هِيَ تَلْقَفُ مَا يَأْفِكُونَ ﴿١١٧﴾

117. Tukampelekea wahyi Musa kwamba tupa fimbo yako, mara ikavimeza walivyovibuni.

فَوَقَعَ الْحَقُّ وَبَطَلَ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿١١٨﴾

118. Ukweli ukasimama na yakabatilika waliyokuwa wakiyatenda.

فَغُلِبُوا هُنَالِكَ وَانقَلَبُوا صَاغِرِينَ ﴿١١٩﴾

119. Kwa hiyo hapo walishindwa wakageuka wakawa wadogo.

وَأُلْقِيَ السَّحَرَةُ سَاجِدِينَ ﴿١٢٠﴾

120. Wachawi wakapomoka kusujudu.

قَالُوا آمَنَّا بِرَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿١٢١﴾

121. Wakasema: Tumemwamini Mola wa Walimwengu.

رَبِّ مُوسَىٰ وَهَارُونَ ﴿١٢٢﴾

122. Mola wa Musa na Harun.

قَالَ فِرْعَوْنُ آمَنتُم بِهِ قَبْلَ أَنْ آذَنَ لَكُمْ إِنَّ هَـٰذَا لَمَكْرٌ مَّكَرْتُمُوهُ فِي الْمَدِينَةِ لِتُخْرِجُوا مِنْهَا أَهْلَهَا فَسَوْفَ تَعْلَمُونَ ﴿١٢٣﴾

123. Akasema Firauni: Je, mmemwamini kabla sijawaruhusu. Hakika hizi ni njama mlizozipanga mjini ili muwatoe wenyewe lakini punde mtajua.

لَأُقَطِّعَنَّ أَيْدِيَكُمْ وَأَرْجُلَكُم مِّنْ خِلَافٍ ثُمَّ لَأُصَلِّبَنَّكُمْ أَجْمَعِينَ ﴿١٢٤﴾

124. Nitawakata mikono yenu na miguu yenu kwa kubadilisha, kisha nitawasulubu nyote.

قَالُوا إِنَّا إِلَىٰ رَبِّنَا مُنقَلِبُونَ ﴿١٢٥﴾

125. Wakasema: Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu.

وَمَا تَنقِمُ مِنَّا إِلَّا أَنْ آمَنَّا بِآيَاتِ رَبِّنَا لَمَّا جَاءَتْنَا رَبَّنَا أَفْرِغْ عَلَيْنَا صَبْرًا وَتَوَفَّنَا مُسْلِمِينَ ﴿١٢٦﴾

126. Na wewe hutufanyii kisasi ila kwa sababu tumeziamini ishara za Mola wetu zilipotujia. Ewe Mola, tumiminie subira na utufishe hali ya kuwa waislamu.

WAKAJA WACHAWI

Aya 113 – 126

MAANA

Wakaja wachawi kwa Firauni, wakasema: Tutapata ujira ikiwa tutashinda? Akasema, ndiyo, nanyi hakika mtakuwa miongoni mwa wanaokurubishwa.

Wachawi hawa waliojiuza kwa Firauni dhidi ya Nabii Musa walikuwa wanawakilisha dini katika zama zao, Nao wana mifano kila wakati. Wanauza dini yao na dhamiri kwa kila mwenye kutoa pesa. Siku hizi Wazayuni na Wakoloni wamewanunua wengi wenye kofia na vilemba wakawalipa na kuwashika sawasawa wasaidie ukoloni na unyonyaji kwa kuwavunga watu na kuwapoteza. Wakaanzisha jumuia mbalimbali na vitengo kwa jina la dini kwa lengo hilo. Lakini ni haraka mno kufedheka na kuwa kwenye midomo ya dharau ya kila mwenye mwamko mwenye ikhlasi.

Wakasema: Ewe Musa! Utatupa wewe au tutatupa sisi?

Walimuhiyarisha kuanza au waanze wao kwa kutegemea uchawi wao kuwa watashinda na kutomjali Nabii Musa(a.s) . La kushangaza ni kauli ya Razi, kwamba wachawi walimuhiyarisha Nabii Musa kwa kumheshimu.

Akasema: Tupeni ! Akiwadharau wao na uchawi wao.

Walipotupa waliyazuga macho ya watu na wakawaogopesha, na wakaleta uchawi mkubwa.

Kunasibisha kuzuga kwenye macho ya watu ni dalili kwamba uchawi wao si tukio la kweli, isipokuwa ni kuwavunga watu tu.

Kuwaogopesha, ni kwamba wachawi waliwatisha watazamaji na wakaleta uchawi mkubwa katika kuzuga na kupoteza si katika uhakika au hali halisi.

Tukampelekea wahyi Musa kwamba tupa fimbo yako, Mara ikavimeza walivyovibuni, Ukweli ukasimama na yakabatilika waliyokuwa wakiyabuni.

Nabii Musa alihofia wajinga wasihadaike na mizungu ya wachawi na upotevu wao. Mwenyezi Mungu akamfunga mkanda na kumpa wahyi kwamba yuko pamoja naye; na kwamba waliyoyaleta si chochote ni mizungu tu.

Akamwamrisha atupe fimbo, Alipoitupa ikameza yale waliyoyabuni kukabatilika kujifanya kwao ikadhihiri haki machoni kwa wote.

Firauni akaduwaa kwa mshtuko uliompata mbele ya umma wa watu. Amewaleta wachawi kutoka kila pembe ili wakilinde kiti chake na awathibitishie watu uwongo wa Nabii Musa na uzushi wake, Leo mambo yamebadilika kichwa chini miguu juu. Wote wakiwemo wachawi wameamini ukweli wa Nabii Musa na uaminifu wake na kukadhibisha uwongo wa Firauni na hiyana yake.

Kwa hiyo hapo walishindwa wakageuka wakawa wadogo baada ya kiburi kile.

Lau mambo yangeishia hivyo hivyo, kidogo Firauni angelipumua, lakini alishtukiziwa kwa jambo zito na chungu.

Na wachawi wakapomoka wakasujudu, Wakasema: Tumemwamini Mola wa waliimwengu (wote), Mola wa Musa na Harun si Firauni aliyewaleta kubatilisha mwito wa Mwenyezi Mungu na wa haki.

Utauliza : kuna makusudio gani ya kauli ya Wachawi ‘Mola wa Musa na Harun’ ambapo ingelitosha tu kusema ‘Mola wa walimwengu’?

Jibu : Firauni alikuwa akiwaambia watu:

فَقَالَ أَنَا رَبُّكُمُ الْأَعْلَىٰ ﴿٢٤﴾

“Mimi ndiye Mola wenu mkubwa (79: 24)

مَا عَلِمْتُ لَكُم مِّنْ إِلَـٰهٍ غَيْرِي ﴿٣٨﴾

“Simjui kwa ajili yenu Mungu asiyekuwa mimi” (28: 38).

Lau wachawi wangelitosheka na kusema Mola wa walimwengu, basi Firauni angeligeuza na kujisifu yeye na kusema wananikusudia mimi Mola wa walimwengu. Ndipo wakaikata njia ya majisifu yake na kubadilisha kwake mambo.

UCHAWI

Katika Juz.1 (2:103) Tulizungumzia kuhusu uchawi kwa anuani ya ‘Uchawi na hukumu yake’, Tukasema katika tuliyoyasema, kwamba sisi tuko pamoja na wale waonao kuwa uchawi hauna chochote na tukatoa dalili ya hilo. Kuunganisha yaliyopita hapa tunaongezea haya yafuatayo:

Kauli yake Mwenyezi Mungu Wakayazuga macho ya watu ni dalili wazi kwamba uchawi hauna kitu chochote, na kwamba ni ujanja na kiini macho.

Ama kauli yake Mwenyezi Mungu: wakaleta uchawi mkubwa maana yake ni kwamba walifika kikomo cha ujanja na kubadilisha mambo. Maana haya yafafanuliwa na kusisitizwa na kauli yake Mwenyezi Mungu.

فَإِذَا حِبَالُهُمْ وَعِصِيُّهُمْ يُخَيَّلُ إِلَيْهِ مِن سِحْرِهِمْ أَنَّهَا تَسْعَىٰ ﴿٦٦﴾

“Mara kamba zao na fimbo zao zikadhaniwa mbele yake, kwa uchawi wao, kuwa zinapiga mbio”(20:66).

Hazikuwa zikienda hasa, bali ni dhana na mawazo tu. Mtume mtukufu(s.a.w.w) amesema: “Mwenye kumwendea mchawi au kuhani na mwongo akamsadiki, basi amekufuru aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu.”

Wafasiri wengi wamesema kuwa wachawi wa Firauni walifanya hila ya kutingisha kamba na fimbo kwa kuziwekea Zebaki ili zitingishike na joto la jua.

Vyovyote iwavyo tunaamini kwa imani isiyo na shaka kwamba mchawi ni mwongo hakuna anayemsadiki ila mpuzi; na kwamba waliyoyafanya wachawi wa Firauni na wanayofanya wahindi na wengineo ambayo yanashangaza, yana sababu bila ya shaka yoyote.

Na sisi ijapokuwa hatujui sababu yenyewe, tunaamini kwa yakini kabisa kwamba uchawi hauwezi kubadilisha kitu, vinginevyo basi mchawi angeliweza kujizuia yeye na madhara na kujinufaisha na kutawala ulimwengu wote kwa kutaka kwake na matabano yake; na angelikuwa mshirika wa Mwenyezi Mungu katika milki yake Mwenyezi Mungu. Ametukuka kabisa na hayo Mwenyezi Mungu.

Akasema Firauni: Je, mmemwamini kabla sijawaruhusu?

Unaona mantiki hii? Anawataka wamwombe ruhusa katika mambo ya nyonyo zao imani, mapenzi na chuki. Hata mtu ulimwenguni asiutawale moyo wake mwenyewe! Lakini hiyo ni mantiki ya kitaghuti.

Hakika hizi ni njama mlizozipanga mjini ili muwatoe wenyewe, lakini punde mtajua.

Firauni anawaelekezea wachawi tuhuma hizi kuwa kumwamini kwao Nabii Musa hakukuwa kwa hoja na kukinaika, isipokuwa ni hila na hadaa tu walizozipanga pamoja kabla na kwamba lengo la njama hizi ni kuwatoa watawala na kuwavua utawala wao katika Misri.

Firauni alisema maneno haya akiwa anajua kwamba yeye ni mwongo katika kauli yake, lakini alitaka kuwababaisha watu akihofia wasimwache yeye wakamwamini Nabii Musa, lakini watu wanajua kwamba wachawi hawakuamini isipokuwa kwa kuona na kukinai. Vilevile watu wanajua kwamba Nabii Musa hakuwa pamoja na wachawi. Kwa sababu Firauni aliwakusanya huku na huko.

Nitawakata mikono yenu na miguu yenu kwa kubadilisha, kisha nitawasulubu nyote.

Kukata kwa kubadilisha ni kukata mkono wa kuume na mguu wa kushoto, na kinyume.

Hiyo ndiyo silaha ya mataghuti katika kuikabili haki, Anasema Masud katika kitabu Muruju-dhahab: “Katika mwaka 59 (A.H.) Muawiya ali- wakusanya watu ili wambai mwanawe Yazid. Akasimama kuhutubu mtu mmoja kutoka Azdi akasema:

“Akifa huyu akimwonyesha Muawiya basi ni huyu,akimwonyesha Yazid. Na atakayekataa basi ni huu, akautingisha upanga. Muawiya akamwambia: “Kaa, wewe ni hatibu bora kuliko watu wote.”

Wakasema: Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu.

Fanya utakavyo hatukujali wewe wala kuua kwako, Sisi tuna yakini ya kukutana na Mola wetu na uadilifu wake.

Kila mwenye kuamini kukutana na Mwenyezi Mungu anakuwa na msimamo huu bali anaona kufa shahidi ni kheri na nyenzo ya kupata radhi ya Mwenyezi Mungu na thawabu zake, Ama wale ambao wanaoogopa mauti katika njia ya Mwenyezi Mungu, wanaamini kinadharia tu; ama kimatendo wao wanakanusha.

Na wewe hutufanyii kisasi ila kwa sababu tumeziamini ishara za Mola wetu zilipotujia.

Kauli yao hii ina madhumuni ya kumtisha Firauni. Kwa sababu maana yake ni kwamba wewe hutuchukulii kisasi isipokuwa unamchukulia kisasi Mwenyezi Mungu na Mtume Muhammad(s.a.w.w) wake hasa. Kwa sababu hatuna kosa sisi ila kumwamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake Nabii Musa:

أَلَمْ يَعْلَمُوا أَنَّهُ مَن يُحَادِدِ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ فَأَنَّ لَهُ نَارَ جَهَنَّمَ ﴿٦٣﴾

“Je hawajui kwamba anayeshindana na Mwenyezi Mungu na Mtume wake, basi yeye atapata moto wa Jahanam.” (9:63).

Ewe Mola wetu tumiminie subira . Katika msimamo huu.

Unasifiwa uvumilivu (subira) kwa kuuliwa na kuadhibiwa katika njia ya Mwenyezi Mungu (s.w.t). Walimuomba Mungu awaruzuku fadhila hii kwa kuhofia wasilegeze mkanda na kurudi nyuma watakapohisi upanga ukipenya milini mwao.

Na utufishe hali ya kuwa ni waislamu, wanyenyekevu kwako na kwa Mtume wako tukiwa radhi na adhabu na mateso katika njia yako.

3

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA TISA

وَقَالَ الْمَلَأُ مِن قَوْمِ فِرْعَوْنَ أَتَذَرُ مُوسَىٰ وَقَوْمَهُ لِيُفْسِدُوا فِي الْأَرْضِ وَيَذَرَكَ وَآلِهَتَكَ قَالَ سَنُقَتِّلُ أَبْنَاءَهُمْ وَنَسْتَحْيِي نِسَاءَهُمْ وَإِنَّا فَوْقَهُمْ قَاهِرُونَ ﴿١٢٧﴾

127. Na wakasema wakuu wa kaumu ya Firauni: Je, utamwacha Musa na watu wake walete uharibifu katika nchi na kukuacha wewe na waungu wako. Akasema: Tutawauwa watoto wao wa kiume na tutawaacha hai wanawake wao. Na hakika sisi ni wenye nguvu juu yao.

قَالَ مُوسَىٰ لِقَوْمِهِ اسْتَعِينُوا بِاللَّـهِ وَاصْبِرُوا إِنَّ الْأَرْضَ لِلَّـهِ يُورِثُهَا مَن يَشَاءُ مِنْ عِبَادِهِ وَالْعَاقِبَةُ لِلْمُتَّقِينَ ﴿١٢٨﴾

128. Musa akawaambia watu wake: Ombeni msaada kwa Mwenyezi Mungu na subirini. Ardhi ni ya Mwenyezi Mungu atamrithisha amtakaye katika waja wake na mwisho ni wa wenye takuwa.

قَالُوا أُوذِينَا مِن قَبْلِ أَن تَأْتِيَنَا وَمِن بَعْدِ مَا جِئْتَنَا قَالَ عَسَىٰ رَبُّكُمْ أَن يُهْلِكَ عَدُوَّكُمْ وَيَسْتَخْلِفَكُمْ فِي الْأَرْضِ فَيَنظُرَ كَيْفَ تَعْمَلُونَ ﴿١٢٩﴾

129. Wakasema: Tumeudhiwa kabla hujatufikia na baada ya kutujia. Akasema: Huenda Mola wenu atamwangamiza adui yenu na kuwafanya makhalifa katika ardhi aone jinsi mtakavyokuja fanya.

UTAMWACHA MUSA?

Aya 127 – 129

MAANA

Na wakasema wakuu wa kaumu ya Fir’aun: Je, utamwacha Musa na watu wake walete uharibifu katika nchi.”

Baada ya kwisha tukio hilo la kutisha ambalo Nabii Musa alipata ushindi na kufedheheka Firauni. Nabii Musa aliendelea kuwalingania kwenye ibada ya Mwenyezi Mungu peke yake, na dalili yake ni yaliyotukia jana tu kati yake na wachawi, Watu wengi wakamkusanyikia.

Wakuu wa Firauni wakahofia hali isibadilike na mambo yakawageukia wao na bwana wao, hapo wakamchochea Firauni na kumwambia: “Mpaka lini utamnyamazia Musa na kumwacha akiharibu nchi?” Kuharibu nchi, wanamaanisha watu kumwabudu Mwenyezi Mungu peke yake.

Na wakuache wewe na waungu wako.

Kauli hii ya wakuu wa Firauni inafahamisha kuwa alikuwa nao waungu anaowaabudu; nayo inapingana, kwa dhahiri yake, na kauli ya Firauni kuwa Mimi ndiye mola wenu mkubwa na simjui kwa ajili yenu Mungu asiyekuwa mimi.

Wafasiri wamelijibu hilo kwa majibu kadhaa. Lenye nguvu zaidi ni kuwa Firauni alikuwa na miungu akidai kuwa yeye ni mwana kipenzi wa hiyo miungu na kwamba yeye anaitegemeza hukumu yake na utawala wake kwenye hiyo miungu. Kwa hiyo kauli yake simjui kwa ajili yenu Mungu na Mola isipokuwa yeye peke yake inamaanisha kuwa hakuna yeyote mwenye kuhukumu kwa jina la mungu isipokuwa yeye. Maana haya yanatiliwa nguvu na kauli yake:

أَلَيْسَ لِي مُلْكُ مِصْرَ وَهَـٰذِهِ الْأَنْهَارُ تَجْرِي مِن تَحْتِي ﴿٥١﴾

“Kwani ufalme wa Misri si wangu na hii mito inapita chini yangu?” (43:51).

Akasema: Tutawaua watoto wao wakiume na tutawaacha hai wanawake wao.

Kabla ya kuzaliwa Nabii Musa, Fir’aun alikua akwaiua watoto wa kiume wa Bani Israel waliposisitizia wakuu katika watu wake apambane na Nabii Musa, aliwajibu atarudisha mpango huo wa mwanzo.

Na hakika sisi ni wenye nguvu juu yao.

Yaani tuna nguvu juu yao kama ilivyokuwa kabla ya Musa.

Musa akawaambia watu wake: Ombeni msaada kwa Mwenyezi Mungu na subirini. Ardhi ni ya Mwenyezi Mungu atamrithisha amtakaye katika waja wake na mwisho ni wa wenye takuwa.”

Waisrael waliposikia vitisho vya Firauni na kiaga chake waliogopa. Nabii Musa(a.s) akawatuliza na kuwaamrisha kuwa na subira (uvumilivu) na kumtegemea Mwenyezi Mungu; na akawapa tumaini la ushindi ikiwa wao watasubiri na kumwogopa Mwenyezi Mungu. Kwa sababu ardhi ni ya Mwenyezi Mungu si ya Firauni, na Mwenyezi Mungu yuko pamoja na wenye kumcha.

Wakasema: Tumeudhiwa kabla hujatufikia na baada ya kutujia!

Firauni alikuwa akiwakandamiza waisrael kabla ya kuja Nabii Musa na akawashtua kuwakandamiza zaidi baada ya kuja kwake. Walipomwambia Nabii Musa hivyo akasema:

Huenda Mola wenu akamwangamiza adui yenu na kuwafanya makhalifa katika nchi aone jinsi mtakavyokujafanya.

Nabii Musa(a.s) alikuwa anajua wazi kuwa Firauni ataangamia na kwamba Mungu atawaokoa wana wa Israil na kuwamakinisha katika ardhi, lakini alitoa ibara ya huenda ili wasibweteke na ahadi yake.

Kisha akaishiria Nabii Musa kwamba, si muhimu kuwa adui ataangamia na wao kuwa makhalifa katika ardhi, lakini muhimu zaidi ni kumcha Mungu na kuutumia vizuri huo ukhalifa katika ardhi yake; na kwamba Mungu atawaangalia je, watatengeza au wataharibu?

Na wamefanya mengi sana katika ardhi; hapo mwanzo waliwaua mitume na viongozi wema, baadae wakaunda dola isiyokuwa na sharia isipokuwa matamanio ya kuua na kufukuza watu makwao.

Mwaka huu wa 1968, kimetoka kitabu huko Israil kinaitwa Siyakh lokhamim yaani simulizi za wanajeshi. Gazeti la Al-ahram la Misr toleo la tarehe 23-8-1968, limefasiri baadhi ya yaliyomo katika kitabu hicho:

“Ambaye hawezi kuvunja nyumba na kuwafurusha waliomo katika nyumba hiyo, basi bora akae nyumbani kwake tu. Sisi tulipokuja kwenye nchi ya Palestina kulikuwa na watu wengine wanaoishi humo; hatukuwa na matumaini kuwa wataweza kukubali kutuachia mashamba yao na majumba yao. Kwa hiyo ikawa hakuna budi tuwaue au kuwatishia kuwaua ili wakimbie watuachie majumba na mashamba”

Hii ndiyo sharia na lengo la Israil: kuua na kufukuza. Hii sio dola kama dola nyinginezo; isipokuwa ni kikosi cha kizayuni cha mauaji chenye lengo la kuwafukuza wenyeji na kukalia nchi zao kuanzia mto Nail hadi Furat.

Je Waarabu wamejiandaa na nini? Hakuna njia wala mbinu yoyote isipokuwa misimamo ya kivietnam inayosema: ‘Kufa na kupona’ ama kusiweko na Israil au kusiweko na Mwarabu.

وَلَقَدْ أَخَذْنَا آلَ فِرْعَوْنَ بِالسِّنِينَ وَنَقْصٍ مِّنَ الثَّمَرَاتِ لَعَلَّهُمْ يَذَّكَّرُونَ ﴿١٣٠﴾

130. Na hakika tuliwaadhibu watu wa Firauni kwa ukame na kwa kupungukiwa na mazao, ili wapate kukumbuka.

فَإِذَا جَاءَتْهُمُ الْحَسَنَةُ قَالُوا لَنَا هَـٰذِهِ وَإِن تُصِبْهُمْ سَيِّئَةٌ يَطَّيَّرُوا بِمُوسَىٰ وَمَن مَّعَهُ أَلَا إِنَّمَا طَائِرُهُمْ عِندَ اللَّـهِ وَلَـٰكِنَّ أَكْثَرَهُمْ لَا يَعْلَمُونَ ﴿١٣١﴾

131. Ulipowafikia wema, walisema: Huu ni kwa ajili yetu na ulipowafikia ubaya walimnasibishia mkosi Musa na walio pamoja naye. Sikilizeni! Hakika mkosi wao unatoka kwa Mwenyezi Mungu lakini wengi wao hawajui.

وَقَالُوا مَهْمَا تَأْتِنَا بِهِ مِنْ آيَةٍ لِّتَسْحَرَنَا بِهَا فَمَا نَحْنُ لَكَ بِمُؤْمِنِينَ ﴿١٣٢﴾

132. Na wakasema: Hata ukituletea ishara yoyote kutur- oga hatutakuamini.

فَأَرْسَلْنَا عَلَيْهِمُ الطُّوفَانَ وَالْجَرَادَ وَالْقُمَّلَ وَالضَّفَادِعَ وَالدَّمَ آيَاتٍ مُّفَصَّلَاتٍ فَاسْتَكْبَرُوا وَكَانُوا قَوْمًا مُّجْرِمِينَ ﴿١٣٣﴾

133. Basi tukawapelekea tufani na nzige na chawa na vyura na damu kuwa ishara mbalimbali, lakini wakatakabari na wakawa watu wakosefu.

TULIWAADHIBU WATU WA FIRAUNI

Aya 130-133

MAANA

Na hakika tuliwaadhibu watu wa Firauni kwa ukame na kwa kupungukiwa na mazao, ili wapate kukumbuka.

Misri ilikuwa ikibubujika rutuba na mazao. Firauni akajifaharusha kwa rutuba hii na kusema:

وَهَـٰذِهِ الْأَنْهَارُ تَجْرِي مِن تَحْتِي ﴿٥١﴾

"Na pia mito hii ipitayo chini yangu" (43:51)

Mwenyezi Mungu alitia balaa ya kahati na dhiki ya maisha wakati wa Firauni wa Musa ili ajutie upotevu wake na aitikie mwito wa haki. Kuna Hadith isemayo: "Wakiwa waovu watawala hufungwa mvua."

Ni sawa iwe kulikuwako na uhusiano baina ya dhuluma ya mtawala na kahati kwa njia ya ujumla au isiweko, lakini Mwenyezi Mungu aliwaadhibu watu wa Firauni kwa dhulma yao ili wao wakumbuke kabla ya kuwaingiza ndani kwenye uchungu.

Ulipowafikia wema, walisema: Huu ni kwa ajili yetu na ulipowafikia ubaya walimnasibishia mkosi Musa na walio pamoja naye.

Wanafasiri matukio kwa mantiki haya, Kila heri inayowapata basi wanaistahiki wao. Kwa sababu wao wanatawala watu, na kila ubaya unaowapa- ta, basi sababu yake ni yule anayewalingania kwenye haki. Ama rutuba na ukame wanautenga na Mwenyezi Mungu na maumbile aliyo yaumba.

Ndipo Mwenyezi Mungu akawajibu kwa kusema: Sikilizeni! Hakika mkosi wao unatoka kwa Mwenyezi Mungu lakini wengi wao hawajui. Mkosi wao ni fumbo la ukame uliowapata na huo ni kwa matakwa ya Mwenyezi Mungu ambayo sababu zote huishia kwake, na kumnasibishia Musa na ujinga na upumbavu tu.

Utauliza : Kwa nini Mwenyezi Mungu ametumia neno wema kwa ibara yenye al (Al-Hasana) ambayo katika sarufi ya Kiarabu inaitwa ma'rifa, na neno ubaya aktumia bila ya al ambyo ni nakira?

Jibu : Sio mbali kuwa ni ishara ya kwamba maumbile ya heri, kama vile rutuba n.k, ni mengi, na kwamba ubaya, kama vile matetemeko na tufani na ukame ni machache.

Na wakasema: Hata ukituletea ishara yoyote kuturoga hatutakuamini

Huku ni kukiri wazi, kwamba wao wanaikataa haki, wakati huo huo wanakiri kushindwa kwao kwa hoja na dalili. Yakawa malipo ya inadi yao hii ni kuwapata balaa ya aina tano za adhabu:

1.Tukawapelekea tufani ya mvua ikaharibu mimea na mifugo.

2.Na nzige waliokuja baada ya tufani,kama kawaida, wakala mimea yao iliyobakia.

3.Na chawa.

4.Na vyura waliowaghasi maisha yao.

5.Na damu. Inasemekana maji yao yaligeuka kuwa damu na wasi weze kupata maji matamu. Na inasemekana walipatwa na maradhi ya kutokwa na damu za pua.

وَلَمَّا وَقَعَ عَلَيْهِمُ الرِّجْزُ قَالُوا يَا مُوسَى ادْعُ لَنَا رَبَّكَ بِمَا عَهِدَ عِندَكَ لَئِن كَشَفْتَ عَنَّا الرِّجْزَ لَنُؤْمِنَنَّ لَكَ وَلَنُرْسِلَنَّ مَعَكَ بَنِي إِسْرَائِيلَ ﴿١٣٤﴾

134. Na ilipowaangukia adhabu wakasema: Ewe Musa Tuombee kwa Mola wako kwa yale aliyokuahidi. Kama ukituondolea adhabu bilashaka tutakuamini na hakika tutawaacha wana wa Israil waende nawe.

فَلَمَّا كَشَفْنَا عَنْهُمُ الرِّجْزَ إِلَىٰ أَجَلٍ هُم بَالِغُوهُ إِذَا هُمْ يَنكُثُونَ ﴿١٣٥﴾

135. Lakini tulipowaondolea adhabu kwa muda watakaoufikia, mara wakavunja ahadi.

فَانتَقَمْنَا مِنْهُمْ فَأَغْرَقْنَاهُمْ فِي الْيَمِّ بِأَنَّهُمْ كَذَّبُوا بِآيَاتِنَا وَكَانُوا عَنْهَا غَافِلِينَ ﴿١٣٦﴾

136. Basi tuliwapatiliza na tukawazamisha baharini kwa sababu walizikadhibisha ishara zetu na wakaghafilika nazo

وَأَوْرَثْنَا الْقَوْمَ الَّذِينَ كَانُوا يُسْتَضْعَفُونَ مَشَارِقَ الْأَرْضِ وَمَغَارِبَهَا الَّتِي بَارَكْنَا فِيهَا وَتَمَّتْ كَلِمَتُ رَبِّكَ الْحُسْنَىٰ عَلَىٰ بَنِي إِسْرَائِيلَ بِمَا صَبَرُوا وَدَمَّرْنَا مَا كَانَ يَصْنَعُ فِرْعَوْنُ وَقَوْمُهُ وَمَا كَانُوا يَعْرِشُونَ ﴿١٣٧﴾

137. Tukawarithisha watu walionekana wadhaifu mashariki na magharibi ya ardhi tuliyoibariki. Na likatimia neno jema la Mola wako kwa wana wa Israil, kwa sababu walikuwa na subira; na tukayaangamiza yale aliyokuwa akiyafanya Firauni na kaumu yake na yale waliyokuwa wakiyajenga.

ILIPOWAANGUKIA ADHABU

Aya 134-137

MAANA

Katika Aya iliyotangulia Mwenyezi Mungu (s.w.t) ametaja aina tano za adhabu alizowaadhibu watu wa Firauni. Na walikuwa kila inapowapata adhabu hutawasali kwa Musa kutaka kuondolewa adhabu hiyo kwa karamu yake mbele ya Mwenyezi Mungu.

Walikuwa wakijiwekea ahadi wao wenyewe kwa Musa kuwa akifanya, basi wataitikia mwito wa haki. Mwenyezi Mungu naye alikuwa akiwaondolea adhabu kwa muda fulani ili wajiandae na toba na kuwasimamishia hoja, Lakini walikuwa wakivunja ahadi, hawakutekeleza wanayoyasema.

Hapo Mwenyezi Mungu huwateremshia mara ya pili, Tena wanarudia kunyenyekea na kutawasali, na Mwenyezi Mungu huwaondolea. Ikawa namna hii mpaka adhabu ya tano, au jaribio la tano, ndipo akawatesa na kuwatupa ndani ya bahari.

Baada ya muda mrefu kupita tangu kufamaji Firauni na kufariki Musa na Harun, alitokea katika waisrail, Daudi na Suleiman wakafanya dola yenye mipaka mashariki na magharibi.

Lakini haraka sana dola iliyeyuka na Waisrail wakatawaliwa na Ebuchadnezer, wafursi na makhalifa wa Alexandria kisha wa Roma.

وَجَاوَزْنَا بِبَنِي إِسْرَائِيلَ الْبَحْرَ فَأَتَوْا عَلَىٰ قَوْمٍ يَعْكُفُونَ عَلَىٰ أَصْنَامٍ لَّهُمْ قَالُوا يَا مُوسَى اجْعَل لَّنَا إِلَـٰهًا كَمَا لَهُمْ آلِهَةٌ قَالَ إِنَّكُمْ قَوْمٌ تَجْهَلُونَ ﴿١٣٨﴾

138. Na tukawavusha bahari wana wa Israil na wakawafikia waliokuwa wakiyaabudu masanamu yao; wakaema: Ewe Musa! Hebu nasi tufanyie waungu kama hawa walivyo na waungu. Akasema Hakika nyinyi ni watu wafanyao ujinga.

إِنَّ هَـٰؤُلَاءِ مُتَبَّرٌ مَّا هُمْ فِيهِ وَبَاطِلٌ مَّا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿١٣٩﴾

139. Hakika waliyona hawa yatawangamiza na ni bure waliyokuwa wakiyafanya.

قَالَ أَغَيْرَ اللَّـهِ أَبْغِيكُمْ إِلَـٰهًا وَهُوَ فَضَّلَكُمْ عَلَى الْعَالَمِينَ ﴿١٤٠﴾

140. Akasema je, niwatafutie mungu badala ya Mwenyezi Mungu, hali yeye ameweafadhilisha juu ya walimwengu?

وَإِذْ أَنجَيْنَاكُم مِّنْ آلِ فِرْعَوْنَ يَسُومُونَكُمْ سُوءَ الْعَذَابِ يُقَتِّلُونَ أَبْنَاءَكُمْ وَيَسْتَحْيُونَ نِسَاءَكُمْ وَفِي ذَٰلِكُم بَلَاءٌ مِّن رَّبِّكُمْ عَظِيمٌ ﴿١٤١﴾

141. Na Tulipowaokoa kwa kaumu ya Firaun waliowapa adhabu mbaya wakiwaua watoto wenu wa kiume na kuwaacha hai wanawake wenu. Na katika hayo ulikuwa mtihani mkubwa uliotokea kwa Mola wenu.

TULIWAVUSHA WANA WA ISRAIL

Aya 138-141

MAANA

Na tukawavusha bahari wana wa Israil na wakawafikia waliokuwa wakiyaabudu masanamu yao; wakaema: Ewe Musa! Hebu nasi tufanyie waungu kama hawa walivyo na waungu. Akasema: Hakika nyinyi ni watu wafanyao ujinga.

Baadhi ya riwaya zinaeleza kuwa Musa aliendelea miaka ishirini na tatu akipigana jihadi na Firauni kwa ajili ya Tawhid na kuwakomboa wana wa Israil kutokana ukandamizaji, Wakashuhudia miujiza ya kushangaza iliyodhihiri mikononi mwa Musa.

Mwisho wakaona kupasuka bahari kwa fimbo ya Musa, na jinsi zilivyotokea njia kavu kumi na mbili. Kila ukoo ukawa na njia yake. Vile vile waliona jinsi bahari ilivyofungika kwa Firauni na askari wake.

Yote hayo waliyashuhudia, lakini kabla ya kupita muda walisahau miujiza waliyoiona na macho yao yakawa kwa watu wanaoabudu masanamu, wakamtaka Musa awafanyie sanamu la kuabudu. Walitaka haya wakiwa wanajua kwamba Musa ni mtu wa Mwenyezi Mungu na kwamba umuhimu wake wa kwanza ni mwito wa Tawhid na kupiga vita ushirikina. Vile vile walikuwa wakijua kuwa Mwenyezi Mungu alimwangamiza Firauni na jeshi lake, kwa sababu ya ushirikina wake. Baadhi ya wafisri wanasema; "Lau wao wenyewe wangejifanyia mungu, mshangao ungelikuwa mdogo kuliko kumtaka Mtume wa Mola wa walimwengu wote kuwafanyia mungu. Lakini hao ndio Waisrail!

Hakika yaliyo na hawa yatawangamiza na ni bure waliyokuwa wakiyafanya.

Musa(a.s) alianza kuwajibu watu wake kuwa wao ni wajinga na wapumbavu; kisha akawapa habari kwamba mwisho wa washirikina na waabudu masanamu ni hasara na maangamizi.

Akasema je, niwatafutie mungu badala ya Mwenyezi Mungu, hali yeye ameweafadhilisha juu ya walimwengu?

Imepita tafsiri yake katika Juz.1 (2:47)

Kwa vyovyote kufadhilishwa kwao juu ya Firauni na watu wake hakuhisabiwi kuwa ni fadhila kubwa.

Na Tulipowaokoa kwa kaumu ya Firaun waliowapa adhabu mbaya wakiwaua watoto wenu wa kiume na kuwaacha hai wanawake wenu. Na kati- ka hayo ulikuwa mtihani mkubwa uliotokea kwa Mola wenu.

Umepita mfano wake katika Juz.1(2:49)

6

ILI NIWE PAMOJA NA WAKWELI

UCHAMBUZI WA MADA

Madda muhimu katika uchambuzi: Imebakia madda moja muhimu ndani ya uchambuzi wote huu, madda ambayo inataka kuangaliwa kwa makini na kusomwa, na huenda hiyo pekee ndiyo kikwazo ambacho huwachemua wapinzani pale wanaposhinikizwa kwa hoja nzito. Utawaona wanashangaa na kutokuamini ya kuwa Masahaba wapatao laki moja walihudhuria kutawazwa kwa Imam Ali (kuwa Khalifa wa Mtume) na hatimaye hao hao Masahaba wakaafikiana wote kumkhalifu Imam Ali na kumpuuza na miongoni mwao wamo Masahaba wakubwa.

Hali hii (ya kushangazwa kwa wapinzani) imepata kunitokea mimi mwenyewe wakati nilipoingia kikamilifu ndani ya utafiti, sikuamini na haiwezekani kwa mtu yeyote kuamini pindi tukio hili linapoaridhiwa kama lilivyo, lakini wakati tunapolisoma tukio hili kwa pande zote basi kule kushangaa kunaondoka kwani hali halisi haiko kama tunavyoitazamia sisi au kama wanavyoiaridhi Masunni (ya kuwa) haiwezekani Masahaba laki moja wakaenda kinyume na amri ya Mtume, hivyo basi ilikuwaje mambo yakatokea kama yalivyotokea?

Kwanza Siyo kila aliyehuduria Baia ya Ghadir alikuwa akiishi Madina, bali ilikuwa kama ambavyo hali halisi ilivyokuwa kwamba kwa kiasi kikubwa itakuwa ni watu elfu tatu au Nne tu miongoni mwa Masahaba hao ndiyo waliokuwa wakiishi Madina.Na tutakapofahamu ya kwamba wengi wa hawa walikuwa ni watumwa na walioachwa huru na wanyonge ambao walimfikia Mtume (s.a.w.) kutoka sehemu mbali mbali na hapo Madina hawakuwa na uwenyeji wala jamaa (kwa mfano watu wa As-Safah) basi haitabakia isipokuwa nusu yao yaani watu elfu mbili tu, na hata hawa nao ni watiifu kwa viongozi wa makabila na muongozo wa kidugu ambao ndiyo wanaohusika nao na Mtume aliwakubalia (kuwa watiifu kwa viongozi wao) kwani ulipokuwa ukimfikia ujumbe wa kabila fulani, Mtume (s.a.w.) humtawalisha juu yao kiongozi wao, na kwa ajili hiyo ndiyo tumekuta katika Uislamu Istilahi ya kuitwa kwao kuwa ni Ahlul-Hilli wal-Iqdi, watu wanaotumainiwa kutowa maamuzi katika jamii au nchi.

Kadhalika tunapoutazama mkutano wa Saqifah ambao ulikutana mara tu baada ya kufariki Mtume (s.a.w.), tunawakuta waliohudhuria ambao waliuthibitisha uchaguzi wa Abubakar kuwa ni khalifa, idadi yao haizidi watu mia moja kwa makadirio ya juu, kwani katika Ansari ambao ndiyo wenyeji wa Madina hawakuhudhuria isipokuwa viongozi wao kama ambavyo Muhajirina ambao ni wenyeji wa Maka waliohama pamoja na Mtume (s.a.w.) hawakuhudhuria isipokuwa watu watatu au wanne wakiwakilisha Maquraishi. Hali hii itoshe basi kuwa ni dalili ya kupima ukubwa wa hiyo Saqifah ikoje, Saqifah ambayo ilikuwa haina nafasi ya kutosha, kwani haikuwa inakosa kuwa karibu katika kila nyurnba.

Kwa hiyo haikuwa uwanja wa maadhimisho wala siyo jumba la mikutano, na tunaposema kuwa watu mia moja walihudhuria hapo Saqifah bani Saida basi idadi hiyo sisi ndiyo tunaoizidisha ili tu, mwenye kutafiti aweze kufahamu kwamba wale Masahaba laki moja hawakuwepo wala hata hawakusikia mazungumzo yalivyofanyika ndani ya Saqifah isipokuwa baada ya muda mrefu kupita, .kwani hapo zamani hapakuwa na mawasiliano ya anga wala simu au Satellite.

Na baada ya mabwana wakubwa hawa kuafikiana juu ya Abubakar pamoja na upinzani wa bwana wa Kiansari Saad bin Ubbadah ambaye ni kiongozi wa kabila la Khazraj na mwanawe Qais, lakini wengi mno miongoni mwao (kama isemwavyo hii leo) walipitisha makubaliano hayo na kumpa Abubakar mkono wa Baia, wakati ambapo Waislamu wengi hawakuwepo hapo Saqifah, na baadhi yao walikuwa wameshughulika kumuandaa Mtume (s.a.w.) kwa mazishi au walihamanika kutokana na khabari za kifo chake, ambapo Umar bin Al-Khatab naye alikuwa amewatisha na kuwatia khofu iwapo watasema kuwa Mtume amefariki. Taz: Sahih BukhariJuz. 4 -195.

Zaidi ya hayo wengi wa Masahaba wa Mtume walikuwa amewateua wawemo ndani ya Jeshi la Usamaha na wengi wao walikuwa wameweka kambi mahala paitwapo Jorfi wakiwa tayari kwenda vitani na jeshi la Usamah hawakuwepo Mtume alipofariki wala hawakuhudhuria mkutano wa Saqifah. Basi je, inaingia akilini baada ya haya yaliyotokea kwamba mtu fulani katika kabila au ukoo kumpinga kiongozi wake kwa lile alilolipitisha na hasa inapokuwa hilo alilolipitisha lina ubora na utukufu mkubwa ambao kila kabila linaukimbilia? Ni nani ajuwaye ya kwamba huenda siku moja naye atawatawalia Waislamu wote, maadamu mwenye haki hiyo kisheria amekwisha tupwa mbali na mambo sasa yanakwenda kwa kushauriana wanabadilishana kwa kuachiana, basi ni kwa nini wasilifurahie hilo, na ni kwa nini wasiliunge mkono?

Pili Ikiwa wenye uwezo wa kuamua ni wakaazi wa Madina na wamepitisha jambo fulani, basi watu walio mbali katika sehemu mbali mbali za bara Arabu hawawezi kupinga na hali ya kuwa hawajui yanayopita wakati hawapo kwani vifaa vya mawasiliano kwa zama hizo vilikuwa ni vile vya kizamani kisha wao walikuwa wakifahamu kwamba wakazi wa Madina ndiyo waliokuwa wakiishi na Mtume wa Mwenyezi Mungu hivyo basi hao ndiyo wajuao mno mambo mapya miongoni mwa hukmu, kwani huenda ukashuka Wahyi wakati wowote au siku yoyote. Kisha kama kuna kiongozi wa kabila lolote lililo mbali na makao makuu basi jambo la Ukhalifa kwake si muhimu sana sana iwapo Abubakr atakuwa Khalifa au Ali au mtu mwingine yeyote, kwani watu wa Maka ndiyo wajuao zaidi utaifa wao, na cha muhimu kwao ni kubakia kwenye uongozi wa ukoo wake ambapo hakuna anayemkera katika uongozi huo.

Basi ni nani ajuwaye kwamba huenda baadhi ya watu waliulizia juu ya jambo hilo (la Ukhalifa) na walitaka kufahamu mambo yalivyokwenda lakini vyombo vya mtawala viliwanyamazisha sawa iwe kwa njia ya kuwapa tamaa ya mali au vyeo au vitisho, na huenda kisa cha Malik bin Nuwairah ambaye alikataa kutoa zaka kwa Abubakr ni utokea jambo hilo. Na yeyote mwenye kufuatilia matukio hayo yaliyotokea katika vita ya wanaokataa kutoa zaka katika zama za Abubakr atakuta kuna kupingana (kwa maelezo), wala hawezi kutosheka kwa maelezo yaliyoelezwa na baadhi .ya wanahistoria kwa lengo la kulinda heshima ya Masahaba na hasa wale watawala.

Tatu Kiini cha tatizo hili ni kule kushitukizwa ghafla kupatikana kwa Khalifa, hili ni jambo lililochangia mno kukubalika kwa kile ambacho leo kinaitwa kuwa "Hali halisi iliyopo". Kwani mkutano wa Saqifah ulifanyika ghafla kwa kuwashitukiza baadhi ya Mashaba ambao walikuwa wakimshughulikia Mtume (s.a.w.), na miongoni mwao alikuwa Imam Ali na Abbas na wengine miongoni mwa Bani Hashim, Miq-dad, Salman, Abu Dharri, Ammar, Zubair na wengineo wengi. Ama wale waliokuwa Saqifah walipotoka huko hali ya kuwa wakimshangilia Abubakr walielekea msikitini huku wakitoa mwito kwa watu wafanye baia ya jumla na watu wakaipokea baia hiyo kwa wingi watake wasitake kipindi hicho Imam Ali na wafuasi wake walikuwa hawajamaliza wajibu wao Mtukufu ambao tabia zao (mwenendo wao) mwema uliwalazimisha (wautimize) basi haikuwezekana kwao kumuacha Mtume (s.a.w.) bila ya kumkosha, kumvisha sanda, kumtayarisha na kumzika eti badala yake wakimbilie Saqifah kugombea Ukhalifa.

Walipomaliza wajibu wao huo, mambo yalikuwa yamekwisha kamilika kwa Abubakr na yeyote mwenye kwenda kinyume na baia hiyo akawa anahesabiwa kuwa ni miongoni mwa watu wenye fitna ambaye anabomoa umoja wa Waislamu, hivyo ni wajibu kwa Waislamu kumpinga au hata kumuuwa ikiwa itabidi, na ndiyo maana tunamuona Umar alimuonya Saad bin Ubbadah kuwa atauawa pale alipokataa kumbai Abubakr, Umar akasema, "Muuweni hakika yeye ni mtu wa fitna"[52] na baada ya hapo Umar aliwatishia wote waliobaki ndani ya nyumba ya Ali ya kuwa atachoma moto nyumba hiyo na wote waliomo humo. Tukishakufahamu vyema maoni ya Umar bin Al-Khatab kuhusu baia tutatambua mengi baada ya hapo miongoni mwa mambo yanayotatanisha.

Kwa hakika Umar anaona kuwa baia inatosha kusihi pale mmoja miongoni mwa Waislamu anapowahi, basi hapo inakuwa ni lazima kwa wengine kumfuata na yeyote atakayeasi miongoni mwao huyo atakuwa ametoka nje ya mshikamano ya Waislamu na ni wajibu kumuuwa. Basi hebu na tumsikilize yeye mwenyewe hasa kuhusu baia, kama alivyoeleza Bukhar ndani ya Sahih yake juzuu ya nane ukurasa wa ishirini na nane, Babu Rajmi Al-Hubla Minaz-Zinaa Idha-Ah-Sanat amesema: akisimulia yale yaliyotokea ndani ya Saqifah. "Basi fujo ikazidi na sauti zikapaa mpaka nikatishika kuwa kutatokea kuhitilafiana, nikasema, Ewe Abubakr kunjua mkono wako, Abubakar akakunjua mkono wake nikambai nao muhajirina wakambai[53] Ansari (nao wakambai) na tukamruka Saad bin Ubbadah, akasema msemaji miongoni mwao, "Mmemuuwa Saad bin Ubbadah" Mimi nikasema:

"Mwenyezi Mungu amuuwe Saad bin Ubbadah" Umar akasema: "Wallahi sisi hatujakutana na jambo gumu katika yote tuliyohudhuria kuliko kumbai Abubakar, tulichelea kuwa hawa jamaa tukiwaacha bila kupitisha baia, basi watambai mtu miongoni mwao baada yetu, hivyo imma tuwape madaraka, jambo ambalo hatulikubali, au tuwapinge itokee uharibifu, (naonya) yeyote atakayetoa baia bila ya kushauriana na Waislamu asifuatwe yeye wala yule aliyembai ili asiuawe. Basi jambo lililovyo kwa Umar siyo uchaguzi wala hiyari wala mashauriano, bali inatosha pale Mwislamu mmoja anapoiwahi baia hiyo iwe ni hoja kwa wengine na ndiyo maana alimwambia Abubakr, "Kunjua mkono wako Ewe Abubakar," na Abubakr naye akakunjua mkono wake akambai bila ya mashauriano tena haraka haraka kwa kuchelea kutanguliwa na mwingine na kwa hakika Umar amekwisha ieleza rai hii pale aliposema:

"Tulichelea lau tutawaacha watu hawa bila ya kuipitisha baia, watambai mtu miongoni mwao baia yetu (Umar aliwachelea Maansar wasimtangulie wakambai mtu miongoni mwao), na kinachomuongezea ufafanuzi zaidi ni pale anaposema: "Basi imma tuwape Baia jambo ambalo hatulikubali na au tuwapinge patokee uharibifu."[54]

Na ili tuwe waadilifu katika maamuzi na wenye kuchunguza kwa undani, inatupasa tukiri kwamba Umar bin Al-Khatab alibadilisha mtazamo wake kuhusu baia mwishoni mwa uhai wake na hilo ni pale mtu mmoja alipomjia Umar mbele ya Abdur-Rahman bin 'Auf katika Hijja yake ya mwisho aliyohiji, yule mtu akamwambia: "Ewe Amirul-Muuminina unayo habari kuwa fulani anasema, bila shaka Umar akifa hakika nitambai fulani kwani wallahi baia ya Abubakar haikuwa isipokuwa kwa kushitukiza tu na ilitimia". Umar alikasirika na kwa ajili hii alisimama akawahutubia watu alipokuwa akirudi Madina, miongoni mwa aliyoyasema katika khutba yake ni haya yafuatayo:

"Kwa hakika nimepata habari kwamba kuna asemaye miongoni mwenu kuwa, Wallahi lau Umar atakufa nitambai fulani, basi na asijidanganye mmoja wenu kusema kuwa baia ya Abubakar ilikuwa hivyo lakini Mwenyezi Mungu aliikinga shari yake.."[55] Kisha Anasema: "Yeyote mwenye kumbai mtu bila mashauriano kutoka kwa Waislamu, basi huyo asipewe baia yeye wala huyo aliyembai kuhofia asije uwawa.[56]

Basi laiti Umar angekuwa na mtazamo huu siku ya Saqifah na asiwalazimishe Waislamu kumbai Abubakr ambako kulikuwa kwa kushitukiza, na Mwenyezi Mungu aliikinga shari yake kama alivyoshuhudia yeye mwenyewe, lakini imekuwaje Umari awe na rai hii mpya katika mtazamo huu mpya, hakika atakuwa amejihukumia kifo yeye mwenyewe na rafiki yake (Abubakr) kwa kuwa kwenye mtazamo wake mpya anasema: "Yeyote mwenye kumbai mtu bila ya mashauriano toka kwa Waislamu basi asipewe Baia yeye wala huyo aliyembai ili asije uwawa."

Imebakia juu yetu kufahamu ni kwa nini Umar alibadilisha maoni yake mwishoni mwa uhai wake pamoja na kwamba yeye anafahamu mno kuliko mwingine ya kuwa mtazamo wake mpya unatengua baia ya Abubakar iliyotimia bila ya mashauriano toka kwa Waislamu na ilikuwa ni baia ya kushitukiza? Pia mtazamo wake huu mpya unatengua baia yake yeye aliyopewa, kwani aliupata ukhalifa kwa tamko la Abubakar wakati wa kufa bila ya makubaliano kutoka kwa Waislamu, kiasi baadhi ya masahaba walikwenda kwa Abubakar wakamkemea kwa kuwatawalishia mtu msusuavu tena mgumu wa tabia.[57] Na Umar alipotoka ili awasomee watu maandiko ya Abubakr kuna mtu alimuuliza: "Ewe Baba Hafs kuna nini ndani ya waraka huo?" Umar akasema, Sijuwi, lakini mimi nitakuwa wa kwanza kusikiliza na kutii." yule mtu akasema: "Lakini Wallahi mimi najua kilichomo, wewe ulimtawalisha (Abubakar) kipindi cha mwanzo naye amekutawalisha kipindi hiki".

Taz: Al-Imam Was-Siyasah cha Ibnu Qutaibah Juz. 1 uk. 25Mlango unaohusu maradhi ya Abubakri na kumtawalisha kwake Umar. Kauli hii inafanana na kauli ya Imam Ali kumwambia Umar pale alipomuona anawalazimisha watu kwa nguvu wambai Abubakr akasema "Nifanye jambo ambalo wewe utakuwa na hisa (wanitaka) leo nilikazanie jambo lake ili kesho akurudishie"? Taz: Al-Imamah Was-Siyasah cha ibnu Qutaiba Juz. 1 uk. 18. Cha muhimu ni kufahamu ni kwa nini Umar alibadilisha mtazamo wake kuhusu Baia?

Mimi ninakurubia kuamini kwamba, wakati alipowasikia baadhi ya Masahaba wanataka kumbai Ali bin Abi Talib baada ya kufa Umar jambo ambalo yeye Umar kamwe hakubaliani nalo, kwa kuwa yeye ndiye aliyezipinga maagizo ya Mtume yaliyobayana, na akapinga Mtume (s.a.w.) asiwaandikie yale maandiko[58] kwa kuwa yeye alilifahamu lengo lake kiasi kwamba akamtuhumu Mtume kuwa anaweweseka na akawatisha watu wasiseme kuwa Mtume amekufa[59] yote hayo ni kwa sababu wasije wakawahi kumbai Ali. Umar alitilia mkazo baia ya Abubakr na akawalazimisha watu kwa nguvu waikubali baia hiyo na kisha kumuonya kila atayepinga kuwa atamuua[60] ili tu kumtenga mbali Ali na ukhalifa.

Hivi itawezekana Umar aridhie aseme msemaji kwamba fulani atapewa baia lau Umar atakufa? Hasa pale msemaji huyu ambaye jina lake limebakia kuwa halijulikani na hapana shaka kuwa alikuwa miongoni mwa Masahaba wakubwa? Msemaji huyu alitumia hoja ya kitendo alichokitenda Umar mwenyewe alipombai Abubakar pale anaposema: "Wallahi Baia ya Abubakr haikuwa isipokuwa ya kushitukiza na ikatimia", yaani pamoja na kuwa ilitokea kwa kuwashitukiza Waislamu na bila kupata ushauri wao lakini ilitimia na likawa jambo lililothibitika, kwa hiyo ilifaa kwa Umar kulifanya kwa Abubakr kwa nini isifae kwake kulifanya yeye mwenyewe kwa njia ile ile kwa mwingine? Na hapa tunaona kwamba ibn Abbas na Abdur-Rahman bin Auf na Umar bin Khatab wanakwepa kulitaja jina la huyu msemaji kama ambavyo wanakwepa kulitaja jina la mtu anayetaka kupewa baia msemaji huyu. Na ilipokuwa wawili hawa wanao umuhimu mkubwa kwa Waislamu, tunamuona Umar alikasirika kwa usemi huu na haraka katika Ijumaa ya kwanza aliwahutubia watu na akaieleza maudhui ya Ukhalifa itakavyokuwa baada yake na akawaonesha maoni yake mapya kuhusiana na Ukhalifa, ili azuwie njia ya huyu anayetaka kurudisha ile ghafla iliyokwisha tokea kwani njia hiyo itamnufaisha mgomvi wake, kwani kwa kupitia uchunguzi tumefahamu kuwa usemi huo haukuwa ni maoni ya fulani tu peke yake, bali ulikuwa ndiyo mtazamo wa Masahaba wengi, na ndiyo maana Bukhari anasema: "Umar alichukia na kisha akasema bila shaka apendapo Mwenyezi Mungu mimi nitasimama usiku huu miongoni mwa watu niwaonye hawa ambao wanataka kuwapora mambo yao..." [61]

Basi kubadilisha kwa Umar mtazamo wake kuhusu Baia ilikuwa ni kuwapinga hawa ambao wanataka kuwapokonya watu mambo yao na wambai Ali, na hili ni jambo ambalo Umar hakubaliani nalo kwani yeye anaitakidi kuwa Ukhalifa ni miongoni mwa mambo ya watu na siyo haki ya Ali bin abi Talib, na itikadi hii itapokuwa ni sahihi, basi ni kwa nini yeye Umar aliruhusu kuwapokonya watu mambo yao baada ya kufariki Mtume (s.a.w.) na haraka haraka akambai Abubakar bila ya makubaliano na Waislamu. Na msimamo wa Abu Hafs (Umar) dhidi ya Abul-Hasan (Ali) unaeleweka na ni mashuhuri mno, nao ni kumtenga Ali kwenye utawala kwa kutumia njia yoyote inayowezekana.

Na matokeo haya hatukuyafahamu kutokana na hotuba yake (Umar) iliyotangulia hapo kabla peke yake, lakini yeyote mwenye kufuatilia historia atafahamu kuwa Umar bin Al-Khatab alikuwa ndiye mtawala mtendaji hata katika Ukhalifa wa Abubakr na ndiyo maana tunamuona Abubakr anamuomba Usamah bin Zaid amuachie Umar bin Al-Khatab ili amsaidie kuhusu suala la Ukhalifa kama alivyoeleza hilo Ibn Saad ndani ya Tabaqat yake na pia wanahistoria wengi walioelezea jeshi la Usamah - pamoja na hayo tunamuona Ali bin Abi Talib anabakia mbali na majukumu, hawakumpa cheo chochote wala utawala wowote wala kumpa uamiri wa jeshi lolote lile na wala hawakumuamini kuwa mweka hazina na yote haya ni kwa kipindi cha Ukhalifa wa Abubakr, Umar na Uthman, nasi sote twamjua Ali bin Abi Talib ni nani.

Cha kushangaza kuliko yote haya ni kuwa, sisi tunasoma ndani ya vitabu vya historia kwamba kifo kilipomfikia Umar alisikitika kwamba lau Abu Ubaidah bin Al-Jarrah au Salim Huru wa Abu Hudhaifah wangekuwa hai angewatawalisha baada yake. Lakini hapana shaka Umar alikumbuka kuwa hapo kabla alikwisha badilisha mtazamo wake juu ya baia kama hii na akaiona kuwa ni ya kushitukiza na ni kupokonya mambo ya Waislamu, basi hapana budi kwake aweke njia mpya kuhusu baia ili kati kwa kati asije yeyote akafaulu kumbai amuonaye kuwa anafaa na kuwalazimisha watu kumfuata kama alivyofanya yeye kwa Abubakr na kama alivyofanya Abubakar kwake Umar au kama atakavyofanya fulani ambaye anangoja kufa kwa Umar ili ambai jamaa yake.Basi hili haliwezekani baada ya Umar kuwa ameuhukumia Ukhalifa kuwa ni jambo lililofanyika ghafla na kuwa linataka kuwa ni jambo la kupora, na haiwezekani pia kwake kuliacha jambo hili liwe la makubaliano baina ya Waislamu. Na ule mkutano wa Saqifah uliofuatia kufariki kwa Mtume (s.a.w.) yeye Umar alihudhuria na akajionea mwenyewe hitilafu iliyotokea ambayo karibu zitoke roho za watu na damu imwagike.

Basi baadaye alitoa fikra ya watu wa mashauriano au (tuseme) watu sita ambao peke yao ndiyo wenye haki ya kumchagua Khalifa na Muislamu mwingine yeyote hana haki ya kushirikiana nao katika jambo hilo, na Umar alikuwa akitambua kwamba tofauti baina ya watu hawa sita haiwezi kuepukwa, ndiyo maana aliusia ikiwa watatofautiana basi wawe kwenye upande alioko Abdur-Rahman bin Auf hata kama itapelekea kuwauwa watu watatu ambao watamkhalifu Abdur-Rahman bin Auf wakati watakapogawika watu hawa sita makundi mawili, na hilo ni muhali kwani Umar anafahamu kwamba Saad bin Abi Waqas ambaye ni ibn Ammi ya Abdur-Rahman bin Auf na wawili hawa ni ukoo wa Bani Zuhrah, na alifahamu pia kwamba Saad hampendi Ali na moyoni mwake kulikuwa na chuki kwani Ali ndiye aliyewauwa wajomba zake wa ukoo wa Abdis-Shams, kama ambavyo Umar alikuwa akifahamu kwamba Abdur-Rahman bin Auf ni shemeji wa Uthman kwani mkewe aliyekuwa akiitwa Ummu Kul-thum ni dada wa Uthman. Si hivyo tu kadhalika alifahamu kuwa Tal-hah akimpenda Uthman kutokana na mahusiano yaliyokuwepo baina yao kufuatana na maelezo ya baadhi ya wapokezi wa khabari, na hakika ilitosha kwa Tal-hah kumpenda Uthman kutokana na kumpinga kwake Ali kwani yeye Tal-hah ni katika ukoo wa Bani Taym, na kulikuwa na chuki fulani baina ya Bani Hashim na Bani Taym kutokana na Ukhalifa wa Abubakar.

Taz: Shark Najul-Balaghah ya Muhammad Abdoh, Juz. 1 uk. 88.

Umar alikuwa akiyajuwa yote hayo na kwa ajili hii ndiyo maana akawachagua hawa peke yao. Umar aliwachagua hawa watu sita na wote wakiwa ni Maquraish na wote ni kutoka katika Muhajirina na hakuna yeyote kati yao ambaye ni kutoka miongoni mwa Ansar na wote hawa kila mmoja wao akiwakilisha na kuongoza kabila lenye umuhimu wake na athari yake.

1. Ali bin Abi Talib, kiongozi wa Bani Hashim.

2. Uthman bin Affan kiongozi wa Bani Umayyah

3. Abdur-Rahman bin Auf, kiongozi wa Bani Zuhrah

4. Saad bin Abi Waqqas, yeye ni kutoka katika Bani Zuhrah na wajomba zake ni Bani Umayyah.

5. Tal-ha bin Ubaidullah, Bwana wa Bani Taym.

6. Zubair bin Al-Awwan, yeye ni mtoto wa Safiyyah ambaye ni shangazi yake Mtume na ni mume wa As-maa binti Abubakr.

Basi hawa ndiyo wenye kutoa maamuzi, na hukmu yao ikubaliwe na Waislam wote, sawa sawa wakiwa ni wakaazi wa Madina (Makao Makuu ya Ukhalifa) au wengineo katika ulimwengu wote wa Kiislamu na ni wajibu wa Waislamu yeyote atakayetoka miongoni mwao akawa kinyume cha maamuzi yao basi damu yake imwagwe (auawe). Na hili ndilo jambo pekee tulilokuwa tunataka kulisogeza katika akili ya msomaji kuhusiana na kunyamaziwa kwa tamko la Ghadir katika maelezo yaliyotangulia.

Na ikiwa Umar anaufahamu undani, mapenzi na mtazamo wa watu hawa sita, basi bila shaka yeye alikuwa kisha mpendekeza Uthman bin Affan kuwa Khalifah au alikuwa anajua kuwa wengi miongoni mwa hawa sita hawamkubali Ali, vinginevyo ni kwa nini na ni kwa haki gani Umar anatilia nguvu upande wa Abdur-Rahman bin Auf dhidi ya Ali bin Abi Talib wakati ambapo Waislamu tangu hapo zamani na mpaka leo wamekuwa wakishindana juu ya ubora wa Ali na Abubakar na hatujamsikia yeyote akimlinganisha Ali na Abdur-Rahman bin Auf.

Na hapa hapana budi nisimame kidogo ili niwaulize Masunni ambao wanatetea msingi wa mashauriano na pia (niwaulize) watu wenye fikra iliyohuru wote kwa ujumla, nawauliza wote hawa, ni vipi mnaafiki baina ya mashauriano kwa maana yake ya Kiislamu na baina ya fikra hii ambayo kama itajulisha kitu fulani basi haitajulisha isipokuwa ni maoni ya ki-dikteta, kwani yeye Umar ndiye aliyewachagua watu hawa sita na siyo Waislamu, na iwapo kuufikia kwake Ukhalifa lilikuwa ni jambo la ghafla, basi ni kwa haki ipi anawalazimisha Waislamu wakubali mmoja wa hawa sita?

Kinachojitokeza kwetu ni kwamba Umar anauona Ukhalifa kuwa ni haki ya Muhajirina peke yao na mwingine yeyote hana haki ya kuwakorofisha kwenye jambo hili, bali zaidi ya hivi ni kuwa Umar anaitakidi kama anavyoitakidi Abubakar kwamba Ukhalifa ni milki ya Maquraish, bali wamo pia wasiokuwa Waarabu, hivyo basi haistahiki kwa Sal-man Al-Farisi wala Ammar bin Yasir wala Bilal wa Uhabeshi wala Suhayb Mrumi, wala Abu Dharri Al-Ghifari wala maelfu ya Masahaba ambao siyo Maquraish (haistahiki kwao) kujitokeza kwa ajili ya Ukhalifa. Na haya siyo madai ya hivi hivi tu sivyo kabisa, bali hiyo ndiyo itikadi yao ambayo historia na wataalamu wa hadithi wameisajili kutoka vinywani mwao (kina Abubakar na Umar) na hebu tuirudie khutba yenyewe ambayo Bukhari na Muslim wameieleza ndani ya Sahih zao:

Umar bin Al-Khatab anasema:

"Nilitaka kusema, na nilikuwa nimetunga vizuri usemi ambao ulinifurahisha nikitaka niutamke mbele ya Abubakr na nilikuwa nikimzunguka karibu. Basi nilipotaka kusema Abubakr akasema, tulia (ewe Umar), na sikupenda kumkasirisha. Abubakar akazungumza, na alikuwa mpole mno kuliko mimi na mtulivu mno, Wallahi hakuacha neno lolote katika maneno nilioyaandaa isipokuwa aliyasema vizuri zaidi mpaka aliponyamaza kisha akasema, nilichokieleza kwenu katika wema ninyi ndiyo mnaostahiki (akiwaambia Maansari) na wala jambo hili halitatambulika isipokuwa kwa upande huu wa Maquraish. Taz: Sahih Bukhar Babul-Wasiyyah.

Kwa hiyo inatubainikia wazi- kwamba Abubakr na Umar hawaamini mashauriano na hiyari, na baadhi ya wanahistoria wanasema kwamba Abubakar alitoa hoja dhidi ya Maansar kwa hadithi ya Mtume (s.a.w.) isemayo kuwa "Ukhalifa uko kwa Maquraish" Na hadithi hiyo hapana shaka ni sahihi (kama walivyoitaja Bukhar na Muslim na Sahih zote kwa Masunni na Mashia) Mtume (s.a.w.) amesema: "Makhalifa baada yangu ni kumi na wawili na wote ni kutoka kwa Maquraishi" na hadithi iliyo wazi zaidi kuliko hii ni ile kauli ya Mtume (s.a.w.) aliposema:

"Jambo hili (la Ukhalifa) halitakoma kwa Maquraish muda wote hata wakibakia watu wawili"[62] pia kauli yake isemayo "Watu ni wafuasi wa Maquraishi katika kheri na shari[63].

Basi ikiwa Waislamu wote wanaziamini hadithi hizi, ni vipi mtu aseme kuwa Mtume aliliwacha suala la Ukhalifa liwe la mashauriano baina ya Waislamu wamchague wamtakaye? Na haiwezekani kwetu sisi kukwepa kupingana huku, isipokuwa tutakapoyachukua maneno ya Maimamu wa nyumba ya Mtume na wafuasi wao na baadhi ya wanachuoni wa Kisunni ambao wanasisitiza kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu aliwataja Makhalifa na akawabainisha kwa idadi yao na majina yao, na hapo ndipo utakapoweza pia kuufahamu msimamo wa Umar na kuuthibiti Ukhalifa kwa Maquraish na huyu Umar ni mtu aliyefahamika kwa Ijtihadi yake dhidi ya maagizo ya Mtume hata katika uhai wake mwenyewe Mtume (s.a.w.), kwani matukio ya Sul-hu ya Hudaybiyah[64] kuwasalia wanafiki,[65] msiba wa siku ya Al-Khamis,[66] na kuzuwiya kwake kubashiria watu pepo[67] ni ushahidi mkubwa wa haya tuyasemayo.

Basi haishangazi kwa Umar kufanya Ij-tihad baada ya kufariki Mtume dhidi ya hadithi inayohusu Ukhalifa, haoni ulazima wa kukubali agizo linalomuhusu Ali bin Abi Talib ambaye ni Quraish, mdogo kwa umri. Ni yeye aliyeidhibiti haki ya kumchagua Khalifa kwa Maquraish peke yao, na ni yeye ambaye alilazimisha peke yake kuchagua watu sita miongoni mwa watukufu wa Kiquraishi kabla hajafa ili ikubaliane kati ya hadithi ya Mtume (s.a.w.) na vile aonavyo yeye juu ya haki ya Maquraishi peke yao kuhusika na Ukhalifa. Huenda kumuingiza Ali katika kundi hilo hali yakuwa akifahamu kwamba wao hawatamchagua, ni udhibiti wake kwa Umma ili amlazimishe Ali kuingia pamoja nao ndani ya mchezo wa Kisiasa kama wanavyouita leo hii na ili pasibakie kwa Ali na wafuasi wake na wapenzi wake ambao walikuwa wakidai kuwa yeye ndiye wa mwanzo (pasibakie kwao) hoja yeyote. Lakini Imam Ali aliyazungumza yote hayo katika hotuba yake mbele ya watu wote akasema kuhusu jambo hilo:

"Nilivumilia muda wote wa taabu na majaribu mpaka alivyoondoka akauweka (Ukhalifa) chini ya maamuzi ya kikundi cha watu sita akidhania kuwa mimi nafanana nao oh! hayawi sawa ya Mungu na mashauriano! Toka lini nikatiliwa mashaka na wa kwanza miongoni mwao mpaka imebidi nilinganishwe na watu kama hawa! lakini nilitua walipotua na niliruka waliporuka (yaani, niliishi nao kwa hekima).

Nne: Hakika Imam Ali (a.s.) alitoa hoja dhidi yao kwa kila namna lakini bila mafanikio, na je, Imam Ali aombe baia ya watu ambao walimgeuzia nyuso zao na nyoyo zao zikawaelekea wengine imma kwa husuda dhidi yake kutokana na yale aliyompa Mwenyezi Mungu miongoni mwa fadhila zake, na imma kwa chuki dhidi yake kwani yeye ndiye aliyewaua mabwana zao, akawabomoa mashujaa wao, akawakatisha tamaa, akawadhalilisha na kuvunja ujeuri wao kwa upanga wake na ushujaa wake mpaka wakasilimu na kujisalimisha hali ya kuwa Imam Ali akiwa ni Mtukufu akimtetea mwana wa ammi yake (Mtume s.a.w.) na alipokuwa akifanya hayo haikumzuwia kuyatenda kwa ajili ya Mwenyezi Mungu lawama ya mwenye kulaumu na wala hakurudi nyuma kwenye azma yake kutokana na tamaa ya dunia. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) naye alikuwa akiyajua vema hayo na kila tukio alikuwa akitilia mkazo fadhaila za nduguye na mwana wa ammi yake ili kuwafanya wampende. Mtume alikuwa akisema "Kumpenda Ali ni (dalili ya) imani na kumchukia (ni dalili ya) unafiki"[68] Na pia husema "Ali anatokana nami, nami natokana na Ali."[69] Na alikuwa akisema: "Ali ni mtawala wa kila muumini baada yangu"[70] na husema kuwa, "Ali ni mlango wa mji wa elimu yangu na ni baba wa wanangu."[71] Pia Mtume alikuwa akisema, "Ali ni Bwana wa Waislamu na ni Imamu wa wachamungu na ni kiongozi wa waumini wenye kutowa mwanga na nuru."[72]

Lakini inasikitisha kwamba yote hayo hayakuwazidishia isipokuwa chuki na husuda na kwa ajili hiyo Mtume alimuita Ali kabla ya kufariki akamkumbatia kisha akalia na akamwambia: "Ewe Ali bila shaka mimi nafahamu kwamba ndani ya nyoyo za jamaa hawa kuna shinikizo la chuki dhidi yako, na hapo baadaye watakudhihirishia baada yangu mimi, iwapo watakupa baia kubali vinginevyo basi subiri mpaka hapo utapokutana nami hali ya kuwa mwenye kudhulumiwa". Taz: Ar-Riyadun-Naz-Rah Fi Manaqibil-Asharah cha Tabari Babu Fadail Ali ibn Abi Talib. Basi ikiwa Abul-Hasan (a.s.) ilimlazimu kuvumilia baada ya baia ya Abubakr, hilo ni kutokana na usia wa Mtume kwake yeye na ndani ya hilo muna hekima ambayo iko wazi.

Tano: Zaidi ya yote hayo yaliyotangulia ni kwamba, Muislamu ataposoma Qur'an Tukufu na kuzizingatia aya zake, atafahamu kwa kupitia masimulizi yake kuhusu mambo ambayo yaliwafika watu na mataifa yaliyopita kwamba, kwao yalitokea mengi kuliko yale yaliyotokea kwetu sisi. Basi mwangalie huyu Qabil anamuuwa nduguye Habil kwa dhulma na uadui tu, na huyu hapa Nuh ambaye ni babu wa Manabii, baada ya miaka elfu moja ya jihadi hakuna aliyemfuata katika watu wake isipokuwa wachache tu, isitoshe mkewe na mwanawe walikuwa miongoni mwa makafiri.

Mtazame Nabii Lut haikupatikana katika kitongoji chake isipokuwa nyumba moja tu ya Waumini. Nao Mafirauni ambao walikuwa wenye kiburi katika nchi wakawafanya watu kuwa watumwa, hapakuwepo miongoni mwao isipokuwa Muumini mmoja anayeficha imani yake. Hawa hapa nduguze Yusuf watoto wa Yaaqub nao ni kikundi, wanakula njama kumuuwa ndugu yao mdogo asiye na kosa lolote lakini (wanafanya hivyo) kwa kumhusudu kwa kuwa yeye ni kipenzi kwa baba yao. Watazame wana wa Israel ambao Mwenyezi Mungu aliwaokoa kupitia kwa Musa na akawapasulia bahari na kumuangamiza adui yao Firauni na askari wake bila ya kuwakalifisha taabu yoyote ya vita, basi mara walipotoka baharini na nyayo zao hata hazijakauka, wakawafikia watu wanaoabudia sanamu (wana wa Israel) wakasema:

"Ewe Musa tutengenezee Mungu kama wao walivyo na Miungu, Musa akawaambia hakika ninyi ni watu msiojua." Na alipokwenda kwenye ahadi ya Mola wake na kumuacha nduguye Harun, walifanya njama dhidi yake karibu wamuuwe, wakamkufuru Mwenyezi Mungu, na wakamuabudia ndama kisha baadaye waliwauwa Manabii wa Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu anasema: "Kila walipokufikieni Mitume kwa yale ambayo nafsi zenu haziyapendi mlijivuna, kundi moja mlilipinga na kundi jingine mkaliua".(Qur'an, 2:87)

Huyu hapa naye Bwana wetu Yahya bin Zakariya naye ni Nabii na Mtawa miongoni mwa watu wema anauwawa na kichwa chake anazawadiwa mtu muovu miongoni mwa waovu wa Kibani Israel. Mayahudi na Wakristo nao walikula njama kumuua na kumsulubu bwana wetu Isa. Nao ummati wa Muhammad wanaandaa jeshi la kiasi ya watu elfu thelathini ili kumuuwa kipenzi cha Mtume wa Mwenyezi Mungu na Bwana wa vijana wa peponi ambaye hawakuwa pamoja naye isipokuwa watu Sabini miongoni mwa wafuasi wake, wakawauwa wote ikiwa ni pamoja na mwanawe mchanga. La ajabu ni lipi baada ya yote haya? Lipi litashangaza baada ya kauli ya Mtume kuwaambia Masahaba wake yakuwa: "Mutafuata nyendo za wale waliokuwa kabla yenu shubiri baada ya shubiri na dhiraa baada ya dhiraa mpaka hata wakiingia kwenye shimo la kenge nanyi mutaingia". wakasema, "Wadhani kuwa hao ni Mayahudi na Wakristo"? Mtume akasema, "Ni kina nani basi (kama si hao)"?

Taz: Sahih BukharJuz. 4 uk. 144 na Juz. 8 uk. 151. Ni kipi cha ajabu basi, nasi twasoma ndani ya Bukhar na Muslim kauli ya Mtume (s.a.w.) isemayo: "Siku ya Kiyama Masahaba wangu watapelekwa upande wa kushoto nami nitasema wanapelekwa wapi? Patasemwa Wallahi Motoni, nitasema, Ewe Mola wangu Masahaba wangu hao, patasemwa, Hakika wewe hujuwi waliyoyazusha baada yako, nitasema atengwe mbali aliyebadilisha baada yangu, na sitamuona anaokoka miongoni mwao isipokuwa kikundi kidogo kama cha ngamia waliotelekezwa".

Tax: Sahih Bukhar Juz. 7 uk. 209 na Sahih Muslim Babul-Haudh. Basi lipi la ajabu baada ya kauli yake Mtume (s.a.w.) aliposema: "Umati wangu utagawanyika makundi sabini na tatu na yote yataingia motoni isipokuwa kundi moja". Taz: Sunan Ibn Majah Kitabul-Fitan Juz. 2 hadith Na. 3993, Ahmad Juz. 3 uk. 120, Sunan Tirmidhi Kitabul-Iman. Amesema kweli Mwenyezi Mungu Mtukufu Mola mwenye nguvu na Utukufu, mjuzi wa undani wa nyoyo pale aliposema: "Na watu wengi hawataamini japo utapupia" (Qur'an, 12:103)

"Bali amewajia na ukweli na wengi wao wanaichukia kweli" (Qur'an,23:70)

"Bila shaka tumekujieni na ukweli lakini wengi wenu hawaupendi ukweli" (Qur'an 43:78)

"Fahamuni ya kwamba ahadi ya Mwenyezi Mungu ni ya kweli lakini wengi wao hawafahamu" (Qur'an, 10:55)

"Wanakuridhisheni kwa vinywa vyao na nyoyo zao zinakataa, na wengi wao ni mafasiki (Qur'an, 9:8)

"Bila shaka Mwenyezi Mungu ni mwenye fadhila juu ya watu, lakini watu wengi hawashukuru" (Qur'an, 10:60)

"Wanaitambua Neema ya Mwenyezi Mungu kisha wanaipinga na wengi wanakataa ila kukufuru tu" (Qur'an, 25:50)

"Na wengi wao hawawezi kumuamini Mwenyezi Mungu ila hali ya kuwa wanamshirikisha" (Qur'an, 12:106)

"Bali wengi wao hawaijuwi haki basi wao wanapinga" (Qur'an, 21:24)

"Hivi mwashangazwa na mazungumzo haya na mnacheka wala hamlii hali ya kuwa ninyi mmeghafilika (mmejisahau)" (Qur'an, 53:61


3

4

5

6

7

8

9