TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA TISA Juzuu 9

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA TISA0%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA TISA Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA TISA

Mwandishi: Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 10629
Pakua: 1291

Maelezo zaidi:

Juzuu 9
Juzuu 1
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 15 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 10629 / Pakua: 1291
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA TISA

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA TISA Juzuu 9

Mwandishi:
Swahili

6

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA TISA

قُلْ يَا أَيُّهَا النَّاسُ إِنِّي رَسُولُ اللَّـهِ إِلَيْكُمْ جَمِيعًا الَّذِي لَهُ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ يُحْيِي وَيُمِيتُ فَآمِنُوا بِاللَّـهِ وَرَسُولِهِ النَّبِيِّ الْأُمِّيِّ الَّذِي يُؤْمِنُ بِاللَّـهِ وَكَلِمَاتِهِ وَاتَّبِعُوهُ لَعَلَّكُمْ تَهْتَدُونَ ﴿١٥٨﴾

158. Sema: Enyi watu! Hakika mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu nyinyi nyote, ambaye ni wake ufalme wa mbingu na ardhi, hapana Mola ila yeye, ndiye ahuyishaye na ndiye afishaye, basi mwamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake asiyesoma wala kuandika ambaye humuamini Mwenyezi Mungu na maneno yake. Na mfuateni ili mpate kuongoka.

وَمِن قَوْمِ مُوسَىٰ أُمَّةٌ يَهْدُونَ بِالْحَقِّ وَبِهِ يَعْدِلُونَ ﴿١٥٩﴾

159. Na katika kaumu ya Musa kuna umma unaoongoza kwa haki, na kwayo hufanya uadilifu.

MTUME WA MWENYEZI MUNGU KWENU NYOTE

Aya 158 – 159

MAANA

Sema: Enyi watu! Hakika mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu nyinyi nyote.

Aya hii imeshuka Makka katika Sura ya Makka, Inakadhibisha wale waliosema kuwa Nabii Muhammad(s.a.w.w) alipokuwa dhaifu, alisema mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa ajili ya watu wa Makka na walio viungani mwake, na baada ya kuwa na nguvu, eti ndio akasema mimi ni Mtume wa watu wote. Tumewajibu hao kwa jibu mkataa katika kufasiri Juz.7 (6:92).

Amabaye ni wake ufalme wa mbingu na ardhi, hapana Mola ila yeye, ndiye ahuyishaye na ndiye afishaye.

Aya hii na nyingine nyingi inatilia makazo na kusisitiza kuwa hakuna wa katikati baina ya Mwenyezi Mungu na waja wake, na kwamba milki na amri ni ya Mwenyezi Mungu peke yake.

Kwa hiyo Nabii Muhammad(s.a.w.w) , ingawaje ni Mtume wa watu wote, wakati wote na mahali popote na ni mtukufu wa viumbe na mwisho wa Mitume na bwana wao, lakini yeye mwenyewe hajimiliki chochote, sikwambii mwingine tena.

Mwenyezi Mungu anasema:

قُل لَّا أَمْلِكُ لِنَفْسِي ضَرًّا وَلَا نَفْعًا إِلَّا مَا شَاءَ اللَّـهُ ﴿٤٩﴾

“Sema sijimilikii nafsi yangu madhara wala kwa manufaa ila apendavyo Mwenyezi Mungu” (10: 49)

Maana haya yamekaririka katika Aya kadhaa, na makusudio yake ni kuwafahamisha waislamu hakika ya Nabii Muhammad(s.a.w.w) na kwamba yeye ni mtu kama wao, ili wasijingize sana kwake waislamu kama walivyojingiza Wakristo kwa Bwana Masih(a.s) .

Tamko Lailaha illallah nabii Muhammadu-rasulullah (Hapana Mola isipokuwa Mwenyezi Mungu, Nabii Muhammad ni Mtume wa mwenyezi Mungu) wanalolikariri Waislamu usiku na mchana, linatosha kuwa ni dalili ya kuepukana Waislamu na kujingiza sana, na vilevile kuamini kwao kuwa Nabii Muhammad(s.a.w.w) hamiliki jambo lolote zaidi ya Utume na kufikisha (tabligh).

Basi mwaminini Mwenyezi Mungu na Mtume wake asiyesoma wala kuandika ambaye anamwamini Mwenyezi Mungu na maneno yake. Na mfuateni ili mpate kuongoka.

Kusema kwake mfuateni baada ya kusema kwake basi mwaminini, ni dalili kwamba imani tu haitoshi kitu bila ya kuwa na vitendo vinavyofuata Kitab cha Mwenyezi Mungu na Sunna ya Mtume wake, Rudia Juz.2 (2:212) kifungu ‘hakuna imani bila ya takuwa.’

UZAYUNI NA UYAHUDI

Na katika kaumu ya Musa kuna umma unaoongoza kwa haki, na kwayo hufanya uadilifu.

Razi anasema: “Wametofautiana kuhusu umma huo, ulipatikana lini, na wapi? Ikasememkana kuwa ni Mayahudi waliomwamini Nabii Muhammad(s.a.w.w) , kama vile Abdallah bin Salam na bin Suria. Na imesemekana kuwa ni watu waliothibiti kwenye dini ya Nabii Musa bila ya kugeuza, kama walivyofanya wengineo waliozusha mambo.”

Sisi tuko katika upande wa hao wasemao kuwa ni waliokuwa katika wakati wa Nabii Musa, kisha wakaisha, kama linavyodokeza neno lake Mwenyezi Mungu: Na katika kaumu ya Nabii Musa. Ama bin Salam na bin Suria hao wawili wala kumi mfano wao hawawezi kuitwa umma au kundi.

Kwa vyovyote iwavyo, Qur’an katika Aya kadhaa imewapa Mayahudi kila sifa mbaya, na kuiambatanisha historia yao kuwa ya aibu. Kwa hiyo linalofahamika kutokana na kauli, katika kaumu ya Nabii Musa ni kuwa katika desturi yoyote kunapatikana nadra; na nadra haibadilishi kawaida, baliinatilia nguvu.

Hata kama tutaifungia macho Qur’an Tukufu yenye hekima, kwani ufisadi na upotevu uko mbali na tabia na sera ya Mayahudi? Je, Mayahudi wametakata na upotevu na kujifanya? Bali historia ya Mayahudi ina kitu hata kimoja kinachotambulisha kheri? Pengine mtu anaweza kusema kuwa ufisadi ni sifa inayolazimiana na uzayuni kwa vile ni harakati za siasa za ubaguzi na ufashisti zenye lengo la kuhudumia na kueneza ukoloni. Lakini Uyahudi ni dini tu, kama dini nyingine.

Jibu :Kwanza , kwani hatujui kuwa chimbuko la tofauti hii ni Mayahudi wenyewe ili wajikinge na historia yao ya zamani na sasa, ya aibu, inayoambatana nao. Rudia Juz.6 (5:64).

Pili , kukadiria kuweko na tofauti baina ya Uyahudi na Uzayuni, ni jambo ambalo haliwezekani. Je, Mayahudi kwa ujumla wanauridhia au wanachuikia Uzayuni ambao umejisheheneza silaha, kwa jina la Israel, wenye lengo la kuuhami ukoloni na kupinga ukombozi?

Kwa nini basi Mayahudi wameusaidia Uzayuni kwa hali na mali na kujitolea wake kwa waume, baada ya kujifundisha silaha kali, katika vita vya tarehe 5 Juni 1967?

Tena je, si Mayahudi wanaoamini kidini na kiitikadi kwamba wao ni taifa teule la Mwenyezi Mungu na kwamba Mwenyezi Mungu yuko upande wao dhidi ya watu wote, na kwamba Mwenyezi Mungu ameharamisha damu zao na kuwahalalalishia wao damu za watu wengine wote, na kwamba wao wameweka kanuni zao na nidhamu zao juu ya misingi hii na watekelezaji ni Israel?

Baada ya hayo, Uyahudi ni dini kama dini nyingine, iliyoteremshwa kwa Nabii Musa(a.s) , lakini imekwisha na wamekwisha watu wake, hakuna aliyebakia; kama zilivyokwisha dini nyingine. Uyahudi wa leo ni Uzayuni isipokuwa nadra sana, na kama tulivyotangulia kusema kuwa nadra sio kipimo.

وَقَطَّعْنَاهُمُ اثْنَتَيْ عَشْرَةَ أَسْبَاطًا أُمَمًا وَأَوْحَيْنَا إِلَىٰ مُوسَىٰ إِذِ اسْتَسْقَاهُ قَوْمُهُ أَنِ اضْرِب بِّعَصَاكَ الْحَجَرَ فَانبَجَسَتْ مِنْهُ اثْنَتَا عَشْرَةَ عَيْنًا قَدْ عَلِمَ كُلُّ أُنَاسٍ مَّشْرَبَهُمْ وَظَلَّلْنَا عَلَيْهِمُ الْغَمَامَ وَأَنزَلْنَا عَلَيْهِمُ الْمَنَّ وَالسَّلْوَىٰ كُلُوا مِن طَيِّبَاتِ مَا رَزَقْنَاكُمْ وَمَا ظَلَمُونَا وَلَـٰكِن كَانُوا أَنفُسَهُمْ يَظْلِمُونَ ﴿١٦٠﴾

160. Na tukawagawanya katika koo kumi na mbili, mataifa mbalimbali. Na tukampa wahyi Musa walipomuomba maji watu wake kuwa lipige jiwe kwa fimbo yako. Mara zikabubujika chem-chemi kumi na mbili, na kila watu wakajua mahali pao pa kunywea. Na tukawatilia kivuli kwa mawingu na tukawateremshia manna na salwa, Kuleni katika vizuri tulivyowaruzuku. Wala hawakutudhulumu bali, wamejidhulumu wenyewe.

وَإِذْ قِيلَ لَهُمُ اسْكُنُوا هَـٰذِهِ الْقَرْيَةَ وَكُلُوا مِنْهَا حَيْثُ شِئْتُمْ وَقُولُوا حِطَّةٌ وَادْخُلُوا الْبَابَ سُجَّدًا نَّغْفِرْ لَكُمْ خَطِيئَاتِكُمْ سَنَزِيدُ الْمُحْسِنِينَ ﴿١٦١﴾

161. Na walipoambiwa kaeni katika mji huu na kuleni humo maridhawa popote mpendapo na ingieni katika mlango (wake) kwa kunyenyekea na semeni: Tusamehe. Tutawasamehe makosa yenu na tutawazidishia wale wafanyao mazuri.

فَبَدَّلَ الَّذِينَ ظَلَمُوا مِنْهُمْ قَوْلًا غَيْرَ الَّذِي قِيلَ لَهُمْ فَأَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ رِجْزًا مِّنَ السَّمَاءِ بِمَا كَانُوا يَظْلِمُونَ ﴿١٦٢﴾

162. Wakabadilisha wale walio dhulumu kauli isiyokuwa ile waliyoambiwa. Na ndipo tukaiteremsha juu ya wale waliodhulumu adhabu kubwa kutoka mbinguni kwa vile walivyokuwa.

TULIWAGAWANYA KOO KUMI NA MBILI

Aya 160 – 162

MAANA

Na tukawagawanya katika koo kumi na mbili, mataifa mbalimbali.

Yaani tuliwagawanya waisrael makundi kumi na mawili, kila kundi likiishia kwa wajukuu kumi na wawili wa Yaqub bin Is-Haq bin Ibrahim. Alikuwa na watoto kumi na wawili na kila mtoto alikuwa na kizazi chake.

Na tukampa wahyi Musa walipomuomba maji watu wake kuwa lipige jiwe kwa fimbo yako. Mara zikabubujika chemchem kumi na mbili, na kila watu wakajua mahali pao pa kunywea.

Umetangulia mfano wake katika Juz.1 (2:60).

Na tukawatilia kivuli kwa mawingu na tukawateremshia manna na salwa. Kuleni katika vitu vizuri tulivyowaruzuku, Wala hawakutudhulumu bali, wamejidhulumu wenyewe.

Umetangulia mfano wake katika Juz.1 (2:57), Pia zinazofuatia mfano wake uko katika Juz,1 (2: 58 - 59).

وَاسْأَلْهُمْ عَنِ الْقَرْيَةِ الَّتِي كَانَتْ حَاضِرَةَ الْبَحْرِ إِذْ يَعْدُونَ فِي السَّبْتِ إِذْ تَأْتِيهِمْ حِيتَانُهُمْ يَوْمَ سَبْتِهِمْ شُرَّعًا وَيَوْمَ لَا يَسْبِتُونَ لَا تَأْتِيهِمْ كَذَٰلِكَ نَبْلُوهُم بِمَا كَانُوا يَفْسُقُونَ ﴿١٦٣﴾

163. Na waulize habari za mji uliokuwa kando ya bahari walipokuwa wakivunja Sabato, samaki wao walipowajia juu juu siku ya Sabato na siku wasiyofanya Sabato hawakuwajia. Kama hivyo tuliwajaribu kwa sababu walikuwa wakifanya ufuska.

وَإِذْ قَالَتْ أُمَّةٌ مِّنْهُمْ لِمَ تَعِظُونَ قَوْمًا اللَّـهُ مُهْلِكُهُمْ أَوْ مُعَذِّبُهُمْ عَذَابًا شَدِيدًا قَالُوا مَعْذِرَةً إِلَىٰ رَبِّكُمْ وَلَعَلَّهُمْ يَتَّقُونَ ﴿١٦٤﴾

164. Na kikundi katika wao waliposema: Kwa nini mnawaonya watu ambao Mwenyezi Mungu atawaangamiza au atawaadhibu kwa adhabu kali? Wakasema: Ili uwe ni udhuru mbele ya Mola wenu na huenda wakawa na takua.

فَلَمَّا نَسُوا مَا ذُكِّرُوا بِهِ أَنجَيْنَا الَّذِينَ يَنْهَوْنَ عَنِ السُّوءِ وَأَخَذْنَا الَّذِينَ ظَلَمُوا بِعَذَابٍ بَئِيسٍ بِمَا كَانُوا يَفْسُقُونَ ﴿١٦٥﴾

165. Basi walipoyasahau waliyokumbushwa tuliwaokoa waliokuwa wakikataza maovu na tukawapatiliza walio dhulumu kwa adhabu kali kwa sababu walikuwa wakifanya ufuska.

فَلَمَّا عَتَوْا عَن مَّا نُهُوا عَنْهُ قُلْنَا لَهُمْ كُونُوا قِرَدَةً خَاسِئِينَ ﴿١٦٦﴾

166. Walipoasi waliyokatazwa tuliwaambia kuweni manyani wadhalilifu.

WAULIZE HABARI ZA MJI

Aya 163 – 166

MAANA

Na waulize habari za mji uliokuwa kando ya bahari.

Maneno anaambiwa Nabii Muhammad(s.a.w.w) , na mji maana yake ni watu wa mji. Dhamir ya waulize ni ya mayahudi wa Madina ambao waliishi na Mtume Nabii Muhammad(s.a.w.w) . Kwa sababu Aya hii ilishuka Madina kutokana na inavyowakabili mayahudi wa huko, imeingizwa katika Sura ya Makka kwa kukamilisha mazungumzo kuhusu mayahudi. Mwenyezi Mungu hakutaja jina la mji, Inasemekana ulikuwa kando kando ya bahari ya Sham.

Kwa vyovote iwavyo mji wenyewe unajulikana kwa Mayahudi walioulizwa na Mtume Nabii Muhammad(s.a.w.w) .

Kuna mambo mawili yaliyoyopelekea swali hili: Kwanza, ni kuwasuta mayahudi wa Madina kwamba wao wamepinga utume wake wakiwa na yakini katika nafsi zao.

Kwa vile yeye amewapa masimulizi mengi katika historia ya wakale wao, ikiwa ni pamoja na kisa hiki cha watu wa mji uiliokuwa kando ya bahari, ingawaje yeye hakusoma katika Kitab wala kusikia kwa yoyote. Ila ni wahyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Jambo la pili, ni kuwazindua kuwa wao wana kiburi na ni wapinzani wa haki na kwamba inadi yao hii si jambo la kushangaza, kwani ndio mazoweya yao tangu zamani.

Dalili ni kisa cha watu wa mji huo ambacho kimedokezwa na kauli yake Mwenyezi Mungu.

Walipokuwa wakivunja Sabato, samaki wao walipowajia juu juu siku ya Sabato yao na siku wasiyofanya Sabato hawakuwajia. Namna hiyo tuliwajaribu kwa sababu walikuwa wakifanya ufuska.

Ufupi wa kisa hiki ni kwamba: Mwenyezi Mungu aliwaharamishia Mayahudi kufanya kazi siku ya Sabato (Jumamosi) ikiwa ni pamoja na kuvua samaki, kwa ajili ya kuwajaribu hali yao na kuwadhihirishia watu hakika yao.

Mwenyezi Mungu alikuwa akiwapelekea samaki kwa wingi wakionekana juu juu ya maji siku ya Jumamosi na kuwazuia siku nyingine, wakafanya hila ya kuhalalisha aliyowaharamishia Mwenyezi Mungu, wakachimba mfuo unaoungana na maji na kuwavuta samaki mpaka kwenye mfuo kisha hawawezi kutoka. Wakawa wanawachukua siku ya Jumapili huku wakisema: “Tunavua siku ya Jumapili.

Wenzao wakawakataza na kuwakemea kutokana na hila hii na kuchezea dini, na wakawahadharisha na adhabu ya Mwenyezi Mungu, lakini hawakusikia.

Na kikundi katika wao waliposema: Kwa nini mnawaonya watu ambao Mwenyezi Mungu atawaangamiza au atawaadhibu kwa adhabu kali?

Yaani, kikundi katika waisrael kiliwaambia wenzao waliowakataza mambo mabaya: Kuna faida gani kuwakataza waasi na kuwahadharisha maadam hawataacha wala kuwa na hadhari? Waacheni, kwani Mwenyezi Mungu atawango’a hadi wa mwisho wao kutoka katika ardhi hii, au awabakishe na kuwaadhibu adhabu kali.

Wakasema wale wa kundi la kuamrisha mema:

Ili uwe ni udhuru mbele ya Mola wenu na huenda wakawa na takuwa.

Yaani tumewakataza maovu ili Mwenyezi Mungu ajue kuwa hatuko pamoja nao na kwamba tunachukia matendo yao; wakati huohuo tukitaraji kuwa huenda wakunufaika na makatazo na mawaidha yetu.

Basi walipoyasahau waliyokumbushwa tuliwaokoa waliokuwa wakikataza maovu na tukawapatiliza waliodhulumu kwa adhabu kali kwa vile walivokuwa wakifanya ufuska.

Mwenyezi Mungu amewasifu na ufuska, kwa vile waliasi amri yake, na waliodhulumu, kwa sababu kila anayeasi amri ya Mola wake basi huyo ameidhulumu nafsi yake. Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu aliwaadhibu wakosaji kwa sababu ya madhambi yao na aliwaokoa watiifu kwa sababu ya utiifu yao.

Walipoasi waliyokatazwa, tuliwaambia: Kuweni manyani wadhalilifu.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) aliwaadhibu waasi hao kwa kuwageuza manyani. Kuna Hadith inayosema kuwa wao walibakia siku tatu, kisha wakaangamia kwa sababu mwenye kugeuzwa haishi zaidi ya muda huu wala hazai chochote jinsi yake.

Utauliza : Desturi ya Mwenyezi Mungu imepita kutomwadhibu mwenye dhambi kwa dhambi zake katika dunia, kwa ushahidi ulivyoonekana, kuongezea kauli yake Mwenyezi Mungu mtukufu:

وَلَوْ يُؤَاخِذُ اللَّـهُ النَّاسَ بِمَا كَسَبُوا مَا تَرَكَ عَلَىٰ ظَهْرِهَا مِن دَابَّةٍ وَلَـٰكِن يُؤَخِّرُهُمْ إِلَىٰ أَجَلٍ مُّسَمًّى ﴿٤٥﴾

“Lau Mwenyezi Mungu angeliwachukulia watu kwa waliyoyachuma, asingeliacha juu ya ardhi hata mnyama mmoja” (35:45).

Kwa nini aliwaadhibu hao waliotoka kwenye twaa yake katika kuvua samaki, na kuwaacha wale waliomwaga damu za watu wasiokuwa na hatia katika Palestina na Vietnam, na kabla yake Congo, Japan na wengineo wengi wasiokuwa na idadi?

Jibu : ndio imepita desturi yake Mwenyezi Mungu mtukufu kutomuadhibu mwenye dhambi kwa dhambi zake katika maisha haya kadiri itakavyokuwa kubwa.

Na kama angefanya hivyo basi asingelipambanuka mwovu na mwema, na mwenye kuacha uovu asingelikuwa na fadhila yoyote.

Kwa sababu kuacha kutakuwa ni kwa msukumo wa hofu. Sio kupenda kheri na kuchukia shari, lakini hekima yake Mwenyezi Mungu (s.w.t) imepitisha kuivua desturi hii kwa miujiza ya Mitume na kuitikia dua zao kwa waasi na wafisadi kwa vyeo vyao mbele ya Mwenyezi Mungu na kuthibitisha utume wao. Wafasiri wanasema katika kufasiri:

لُعِنَ الَّذِينَ كَفَرُوا مِن بَنِي إِسْرَائِيلَ عَلَىٰ لِسَانِ دَاوُودَ وَعِيسَى ابْنِ مَرْيَمَ ذَٰلِكَ بِمَا عَصَوا وَّكَانُوا يَعْتَدُونَ ﴿٧٨﴾

“Walilaaniwa wale waliokufuru miongoni mwa wana wa Israil kwa ulimi wa Daud na wa Isa mwana wa Maryam, Hayo ni kwa sababu waliasi, nao walikuwa wakiruka mipaka.” (5:78)

Kwamba Daud(a.s) aliwalaani watu wa Ayla katika waisrael walipoasi kwa kuvua siku ya Sabato na kusema: “Ewe Mwenyezi Mungu wavishe laana mfano wa nguo” Mwenyezi Mungu akawageuza manyani.

Kwa hiyo sababu ya kugeuzwa wavuvi kuwa manyani ni dua ya Mtume Daud wala hakuna Mtume wakati huu atakayewaombea wamwagaji damu na waporaji wa mali za wananchi.

Vyovyote iwavyo, sisi tunaamini uadilifu wa Mwenyezi Mungu na kuwa haki haiendi bure, na mtu atalipwa kwa matendo yake.

وَإِذْ تَأَذَّنَ رَبُّكَ لَيَبْعَثَنَّ عَلَيْهِمْ إِلَىٰ يَوْمِ الْقِيَامَةِ مَن يَسُومُهُمْ سُوءَ الْعَذَابِ إِنَّ رَبَّكَ لَسَرِيعُ الْعِقَابِ وَإِنَّهُ لَغَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿١٦٧﴾

167. Na alipotangaza Mola wako (kwamba) hakika atawaleta watu ambao watawaadhibu kwa adhabu mbaya mpaka siku ya Kiyama. Hakika Mola wako ni mwepesi wa kuadhibu na hakika yeye ni mwingi wa maghufira mwenye kurehemu.

MAYAHUDI NA ADHABU MBAYA

Aya 167

MAANA

Qur’an imezungumzia kwa urefu kuhusu waisrael, imezungumzia kufuru yao, na ufisadi wao katika ardhi, kuasi kwao haki. Nasi, kwa kufuatilia Aya tukufu, tumewazungumzia sana, tukataja mifano kadhaa ya sera yao, ikiwa ni ufafanuzi wa Qur’an kuwahusu. Lakini hapa kuna swali ambalo linapelekea shaka na kudangana kuhusu Aya hii na ile isemayo:

ضُرِبَتْ عَلَيْهِمُ الذِّلَّةُ أَيْنَ مَا ثُقِفُوا ﴿١١٢﴾

“Wamepigwa na udhalili popote wanapokutikana” Juz, 4 (3:112).

Tumelijibu swali hili katika Juz,7 (5:112). Vilevile tumelijibu kwa mfumo mwingine hivi karibuni katika kufasiri Aya 153 ya Sura hii. Hata hivyo hapa tutadokeza kwa ufupi.

Mwenyezi Mungu aliwasalitia waisrael, Mafirauni, kisha wababilon, wafursi, makhalifa wa Alexander kisha manaswara (wakristo).

Imeelezwa katika Tafsir Bahrul-Muhit kuwa kundi la manaswara walifukarika wakawauza wayahudi walio katika mji wao kwa mji ulio jirani yao.

Mwisho mayahudi wakakimbia udhalili na mateso kutaka hifadhi katika miji ya Kiarabu. Wakaishi huko kwa amani. Lakini wao wakavunja ahadi waliyopewa na Mtume(s.a.w.w) .

Baadhi wakauawa, na Umar bin Al-Khattab akawafukuza waliobaki, wakatawanyika duniani, Mashariki na Magharibi wakiwa ni wenye kufuata tu, bila ya kuwa huru, wakisikiliza amri na kuzitii wakiwa dhalili.

Hatimaye mayahudi wakaona kuwa hawatakuwa na jina isipokuwa wajitoe kwa wakoloni. Kwa ajili hii wakajiuza kwa kila mkoloni mwenye nguvu wamtekelezee njama zake.

Hivi sasa, tukiwa katika majira ya Kusi ya mwaka 1968, imegunduliwa kuwa dola moja ya kikoloni imewashauri mayahudi wa Ulaya Mashariki wafanye mageuzi ya kuendesha miji hiyo chini ya wakoloni, Mayahudi wakaanza kutekeleza njama, lakini njama zao zikafichuka kabla ya kutimia, walikaribia kuuingiza ulimwengu kwenye vita vya tatu.

Kwa ajili ya njama hizo, ndio wakoloni wakatengeneza kikosi cha silaha cha mayahudi katika ardhi ya wapalestine na kukipa jina ya dola la Israel.

Kila mwenye akili anajiuliza, Je, inafaa Israel kuitwa dola kwa maana yake sahihi, ambapo inajuliakana wazi kuwa lau wakoloni watajiepusha nayo siku moja tu, basi haitakuwako.

Je, duniani kuna dola yoyote ambayo haitambuliwi na hata dola moja inayopakana nayo? Ikiwa kweli Israel ni dola kwa nini inaishi kiuadui na kujipanua kwenye nchi jirani?

Dola hasa sio uhaini na silaha; isipokuwa kabla ya chochote, ni kuwa na tabia inayosimamia misingi ya amani, nidhamu inayotilia mkazo haki na msimamo ulio mbali na ubaguzi.

Na tabia ya Israel ni tabia ya kiaskari inayosimama kwa misingi ya vita, nidhamu yake ni kuendeleza uchokozi na msimamo wake ni uzayuni, ubaguzi, chuki, vitimbi na uhaini.

Mwandishi mmoja Mwingereza, Christopher Marlo, anasema katika tamthilia ya Kiyahudi. “Hakika mawazo ya uwezekano wa kuishi pamoja na mayahudi ni aina ya wazimu, wala hawana dawa isipokuwa upanga wenye kukata.”

Je, baada ya yote hayo waarabu wataambiwa ishini kwa amani na mayahudi au mayahudi wataambiwa ni watukufu kwa vile ni kikosi cha silaha kinachoitwa Taifa la Israel kinachoua na kuwafukuza maelfu kwa kusaidiwa na wakoloni? Ikiwa uovu ni ukarimu, basi mayahudi wako katika kilele cha utukufu na ukarimu.

Hatimaye ni Mwenyezi Mungu peke yake ndiye anayejua hatua itakayofuatia, na mwenye akili hahadaiki na mambo ya dhahiri wala hatapitwa na matukio.

Hakika Mola wako ni mwepesi wa kuadhibu wale waliothibitikiwa na adhabu.

Na hakika yeye ni mwingi wa maghufira mwenye kurehemu.

Yule atakayejing’oa na dhambi zake na akatubia.