TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI Juzuu 10

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI20%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

Juzuu 10
Juzuu 1
  • Anza
  • Iliyopita
  • 13 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 11859 / Pakua: 2461
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI Juzuu 10

Mwandishi:
Swahili

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI

IMEANDIKWA NA: SHEIKH MUHAMMAD JAWAD MUGHNIYYA

IMETAFSIRIWA NA: SHEIKH HASAN MWALUPA

IMEHARIRIWA NA: USTADH ABDALLAH MOHAMED

IMEPANGWA KATIKA KOMPYUTA NA: UKHT PILI RAJABU

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu

UTANGULIZI WA MCHAPISHAJI

Kitabu hiki kilichoko mikononi mwako hivi sasa ni juhudi ya miaka mingi sana ya watu waliojitolea kuona kazi hii imefanikiwa bila ya kumsahau Marhum Abu Muhammad wa London.

Kama lilivyo jina la Tafsiri yenyewe ndivyo ilivyo Tafsiri yenyewe ambayo mwanachuoni huyu mahiri kabisa aliyeifafanua ni mtu aliyebobea katika fani zote ambazo mfasiri (Mfafanuzi) anatakiwa awe nazo. Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya ameonesha cheche zake katika vitabu vingi alivyoviandika katika maudhui mbali mbalimbali na hivyo kujipatia wasomaji wengi sana.

Msomi huyu, mwenye fikra huru na anayetetea kile anachokiamini, ni mtu mwenye mawazo mapana na kuyaangalia mambo kwa undani sana, kipaumbele chake ni katika maslahi ya umma huu na amejaribu sana kwenda na wakati.

Sifa kubwa pekee ya mwanachuoni huyu ni kuwa yeye hakujihusisha sana na kung'ang'ania madhehebu fulani tu, labda hii yatokana na wadhifa wake wa ukadhi aliokuwa nao katika nchi ya Lebanon ambayo ina madhehebu mengi, ambapo sula la madhehebu ni nyeti nchini humo, hata hivyo yeye aliweza kuamua matatizo ya watu kwenye ofisi yake kulingana na madhehebu yao pale walipomwendea, hiyo ilimsaidia sana hata kuweza kutoa kitabu kitwacho 'Al-Fiqh a'laa madhaahabil-khamsah' (Fikhi ya madhehebu matano) yaani ya Hanafi, Maaliki, Shafi, Hambali na Shia (ambacho twataraji kitatoka hivi karibuni Inshaallah).

Jambo lililotupa msukumo wa kukifasiri kitabu hiki kwa lugha ya Kiswahili ni zile faida nyingi atakazozipata msomaji na kujua mambo mengi na ya ajabu yaliyo mapya kwake ambayo si rahisi kuyapata kwa wafasiri wengine.

Msomaji atapata faida katika fani za Sayansi, Siasa, Historia, Mashairi, visa vizuri, na Saikolojia miongoni mwa mengine; ndiyo maana msomaji atashangaa kidogo anapoisoma Tafsiri hii atakapoona mwandishi amewataja na kuwanukuu watu kama kina Mfalme Edward, wanasyansi kama kina Enstein, Charlie Champlin (Mchekeshaji maarufu), na wengineo, hali inayoifanya tafsiri hii kuwa ni ya kipekee kabisa.

Mtindo alioutumia mwandishi ni sahali uliokusudiwa watu wa tabaka mbalimbali, wanavyuoni na watu wa kawaida.

Nia yetu ni kukigawanya kitabu hiki bure lakini tumelazimika kukiuza kwa bei nafuu ili kurudisha gharama za uchapishaji.

Mwisho: Shukrani kubwa iwaendee bila ya kuwataja watu waliojitolea usiku na mchana, jopo la wafasiri, wahariri, wachapaji, waliotupa moyo na kutoa maoni yao na walioisimamia ili kuhakikisha kwamba kitabu kimemfikia msomaji.

MAKOSA YA CHAPA

Sikumbuki kama nimewahi kusoma kitabu kilichotoka kupigwa chapa, cha zamani au cha sasa, bila ya kukuta makosa ya chapa, Nafikiri sitasoma kitabu kisichokuwa hivyo. Nimejaribu sana kuliepuka hilo katika tungo zangu, lakini sikufanikiwa.

Nilikuwa sifikirii kama ninaweza kuona makosa haya katika maandishi ya msahafu mtukufu, kama yale yaliyo katika baadhi ya chapa; kwa mfano neno yabswutu kwa swad, badala ya yabsutu kwa sin, na katika chapa ya Tafsir Arrazi ya Misr ya mwaka 1935, Sura ya (2:146). Imeandikwa La Ya'alamuun, (hawajui) badala ya Ya'alamuun (wanajua), Mfano wa makosa haya hausameheki.

Katika Tafsir Al-Manar, chapa ya Pili, sura (5:212), imeandikwa "Fawqahum ila yawmil qiyama” badala ya “Fawqahum yawamal qiyama", Hatuwezi kusema kosa hili ni kubwa zaidi kuliko lile.

Lakini mkosaji atatuletea udhuru kwa msemo mashuhuri huko kwetu jabal amail 'Makosa ya chapa.'

Katika Tafsiri Majmau chapa ya Urfan, Sura (46:15), imeandikwa: " Hatta idha balagha arbai' na sanah badala ya: Hattaidha balagha ashuddahu arbai ' na sanah"

Kusema hivi sio kama ninajitetea kutokana na makosa ya chapa atakayoyakuta msomaji katika kitabu hiki, ijapokuwa naomba msamaha kama litatokea hili, lakini makusudio yangu hasa ni kumwambia yule atakayefungua macho yake kwenye makosa ya matamko na kuufungia macho uzuri wa maana.

Vilevile ninamwambia yule ambaye siku moja aliniambia: "Vitabu vyako vimejaa makosa ya chapa, kama kwamba hakuna kitu chochote katika vitabu hivyo isipokuwa makosa ya chapa tu. Wote hao ninawaambia: Mungu awasamehe na aniongoze mimi na nyinyi.

Vyovyote iwavyo, mimi ninaomba msamaha kutokana na makosa ya kifikra na ya chapa. Anasema Amirul Muminiin(a.s) :"Watu wote ni wapungufu wenye kuchanganyikiwa, isipokuwa yule aliyehifadhiwa na Mwenyezi Mungu."

Na Mwenyezi Mungu (s.w.t) ndiye mwenye jukumu la kunikubali- ayale niliyoyapatia na kunisamehe niliyakosea, kwa jaha ya Mtume na kizazi chake, ziwashukie rehema na amani (Amin).

MUHAMMAD JAWAD MUGHNIYYAH

1

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI

Mwendelezo Wa Sura Ya Nane: Surat Al-Anfal

وَاعْلَمُوا أَنَّمَا غَنِمْتُم مِّن شَيْءٍ فَأَنَّ لِلَّـهِ خُمُسَهُ وَلِلرَّسُولِ وَلِذِي الْقُرْبَىٰ وَالْيَتَامَىٰ وَالْمَسَاكِينِ وَابْنِ السَّبِيلِ إِن كُنتُمْ آمَنتُم بِاللَّـهِ وَمَا أَنزَلْنَا عَلَىٰ عَبْدِنَا يَوْمَ الْفُرْقَانِ يَوْمَ الْتَقَى الْجَمْعَانِ وَاللَّـهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿٤١﴾

41. Na jueni kwamba chochote mlichopata ghanima, basi khumsi yake ni ya Mwenyezi Mungu na Mtume na jamaa na mayatima na masikini na msafiri. Ikiwa nyinyi mmemwamini Mwenyezi Mungu na tuliyoteremsha kwa mja wetu siku ya upambanuzi, siku yalipokutana majeshi mawili. Na Mwenyezi Mungu ni muweza juu ya kila kitu.

KHUMS

Aya 41

LUGHA

Neno; Ghanima kwa lugha ya kiarabu lina maana ya kupata kitu. Wametofautiana kuhusu maana ya Fay-u kwa kauli mbili: kauli ya Kwanza kuwa ni ghanima, na kauli ya pili kuwa ni mali inayochukuliwa bila ya vita.

Ama kuhusu Nafal yametangulia maelezo yake mwanzo wa Sura hii. Makusudio ya jamaa ni jamaa za Mtume. Yatima ni yule aliyefiwa na baba yake kabla ya kubaleghe. Na Khums ni humusi (sehemu moja ya tano).

MAANA

Na jueni kwamba chochote mlichopata ghanima, basi khumsi yake ni ya Mwenyezi Mungu na Mtume na jamaa na mayatima na masikini na msafiri.

Wafasiri wamefanya utafiti katika pande nyingi kuhusu Aya hii, Ama sisi tutatosheka na pande mbili tu:

Kwanza: dhahiri ya Aya inafahamisha pande hizo mbili.

Pili: kwamba upande mwingine hautumiki. Katika pande hizo mbili tutakazozitaja ni kueleza maana ya neno ghanima na kubainisha wale wanaostahiki Khumsi.

Wametofautiana Sunni na Shia kuhusu makusudio ya neno ghanima katika Aya. Sunni wamesema ni ngawira wanayoiteka waislamu kutoka kwa makafiri kwa vita.

Kulingana na kauli yao hii, suala la Khums linakuwa kwao halipo siku hizi; sawa na suala la utumwa. Kwa vile hakuna dola ya kiislamu inayopigana jihadi na makafiri na washirikina hivi sasa.

Shia wamesema kuwa ghanima ni zaidi ya ngawira ya vita inayochukuliwa na Waislamu kutoka kwa makafiri, na kwamba inakusanya madini; kama vile mafuta ya petroli, dhahabu nk. Vile vile dafina ikiwa haijulikani mwenyewe na wanavyovitoa watu kutoka baharini kwa kuzamia; kama vile lulu.

Nyingine ni mali inayozidi gharama za mtu yeye na watoto wake katika chumo la mwaka, mali ya halali iliyochanganyika na ya haramu na haijulikani kiwango cha haramu.

Pia ghanima ni ardhi aliyoinunua kafir dhimmi kutoka kwa Mwislamu. Ufafanuzi uko kwenye vitabu vya Fiqh, kikiwemo Fiqh Imam Jaffer As Sadiq Juz.2. Kulingana na kauli ya Shia suala ya khums linakuwa bado lipo.

Kama walivyotofautiana katika maana ya ghanima, vile vile wametofau- tiana katika idadi ya mafungu ya khums na wanaostahiki.

Shia wamesema: khums hugawanywa mafungu mawili: La kwanza litagawanywa mafungu matatu: Fungu la Mwenyezi Mungu, la Mtume wake na la jamaa. Lile la Mweneyzi Mungu ni la Mtume na la Mtume ni la jamaa zake.

Na msimamizi wa jamaa baada ya Mtume ni Imam anayesimamia kazi za Mtume. Akiweko atapewa yeye; kama hayuko basi ni wajibu kulitoa fungu hilo katika maslahi ya kidini, ambayo muhimu zake ni kuutangaza Uislamu na kazi ya kuusambaza na kuutukuza.

Ama fungu la pili, nalo lina sehemu ya mayatima wa ukoo wa Muhammad(s.a.w.w) , masikini wao na wasafiri wao. Wanaohusika katika fungu hilo ni ukoo wa Muhammad(s.a.w.w) tu peke yao, Kwa sababu Mwenyezi Mungu anawaharamishia sadaka akawawekea Khums.

Tabari katika tafsir yake na Abu Hayan Al-Andalus katika Bahrul-Muhit wanasema: “Amesema Ali bin Abu Talib(a.s) :Mayatima na maskini ni mayatima wetu. Anaongeza Tabari: “Ali bin Hussein (r.a) alimwambia mtu mmoja kutoka Sham: Je, hukusoma katika Sura Anfal:“Na jueni kwamba chochote mlichopata ghanima, basi hakika khums yake ni ya Mwenyezi Mungu na Mtume na jamaa na mayatima na masikini na msafiri.

Akasema yule mtu: “Naam! Kwani ndiyo nyinyi? Akasema: ndiyo” Ama wasemavyo Sunni, tuwaachie maulamaa wawili wakubwa, mmoja wao ni wa zamani, Razi, na mwingine ni wa hivi karibuni, Maraghi, mmoja wa Masheikh wa Az-har na rais wake wakati wake.

Razi anasema: “Kauli zilizo mashuhuri ni kwamba hiyo humusi ni sehemu tano:

1. Mtume wa Mwenyezi Mungu.

2. Jamaa zake katika Bani Hashim, na Bani Muttwalib, sio Bani Abdu Shams (Umayya) na Bani Naufal.

3. Mayatima.

4. Masikini.

5. Wasafiri.

“Hiyo ni katika uhai wa Mtume wa Mwenyezi Mungu. Ama baada ya kufa kwake(s.a.w.w) , kwa upande wa Shafii sehemu ni tano.

Ya Mtume wa Mwenyezi Mungu, inatolewa kwenye maslahi ya Waislamu, ya jamaa matajiri na makufara, ilyobaki ni ya mayatima, maskini na wasafiri.

Abu Hanifa anasema kuwa sehemu ya Mtume wa Mwenyezi Mungu inaondoka baada ya kufa kwake kwa saba Na hugawanywa Khums kwa mayatima, maskini na wasafiri. Malik naye anasema: “Mambo ya khums huachiwa rai ya Imam.”

Sheikh Maraghi anasema: “Amepokea Bukhari kutoka kwa Mut’im bin Jubair wa Bani Nawfal, kwamba yeye alikwenda na Uthman bin Affan wa Bani Abd Shams kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) akawaambia: “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Umewapa Bani Muttalib na ukatuacha na hali sisi na wao ni daraja moja. Akasema Mtume(s.a.w.w) : “Hakika Bani Muttalib na Bani Hashim ni kitu kimoja.”

Sheikh Maraghi anaongezea juu ya Hadith hii kwa kusema, na siri ya hilo ni kwamba Makuraish walipoandika maazimio yao ya kuwatoa Bani Hashim Makka na kuwazuia katika Shii’b waliingia humo pamoja na Bani Muttalib, na wala hawakuingia Bani Abu Shams wala Bani Nawfal kwa uadui waliokuwa nao na Bani Hashim wakati wa Jahaliyya na wakati wa Uislamu.

Akawa Abu Sufyan anapigana na Mtume(s.a.w.w) na kuungana na washirikina na watu wa Kitab dhidi yake, mpaka Mwenyezi Mungu alipompa ushindi Mtume wake na Waarabu wakaingia kwenye dini kwa ushindi wa Makka. Vile vile baada ya Uislamu Muawiya alimtokea Ali na akapigana naye.

Nasi tunaungia maneno ya Sheikh Maraghi kuwa vile vile Yazid mjukuu wa Abu Sufyan alimuuwa Hussein Bin Ali, mjukuu wa Mtume(s.a.w.w) . Mshairi anasema kuhusu uadui huu wa kurithiana baba na babu.

Bin Harb na Mustwafa, Aliy na mwana wa Hind, Husein hawakumfaa, alipambana na Yazid

Ikiwa nyinyi mmemwamini Mwenyezi Mungu na tuliyoteremsha kwa mja wetu siku ya upambanuzi, siku yalipokutana majeshi mawili. Na Mwenyezi Mungu ni muweza juu ya kila kitu.

Wafasiri wanasema kuwa makusudio ya siku ya upambanuzi na siku yalipokutana majeshi mawili ni siku ya Badr. Kwa sababu Mwenyezi Mungu alifarikisha baina ya ukafiri na imani kwa kuuweka Uislamu juu ya shirk. Vile vile ni siku yalipokutana majeshi mawili, la waumini na la washirikina ambapo jeshi la washirikina waliipata.

Maana ni kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t) hakubali kumwamini yeye, vitabu vyake na Mitume yake kama nadharia tu, bila ya vitendo, isipokuwa anakubali imani ya anayehukumu na kufanya amali kwa anavyohukumu Mwenyezi Mungu.

Razi anasema: “Kauli yake Mwenyezi Mungu: Mkiwa mmemwamini Mwenyezi Mungu, inafahamisha kuwa ikiwa haukupatikana ugavi huu, kama alivyohukumu Mwenyezi Mungu, basi imani nayo haipo.”

Nasi tunaongezea juu ya kauli ya Razi kuwa vile vile ikiwa hukumu haikupatikana katika usiokuwa ugavi huu, kama alivyohukumu Mwenyezi Mungu, basi imani nayo haitapatikana. Kwa vile, sababu inayowajibisha ukafiri ni moja nayo ni kuhalifu hukumu ya Mwenyezi Mungu makusudi. Kimisingi ni kwamba sababu hii haikubali kufungwa wala kuhusishwa na jambo moja tu.

Tumeeleza mara nyingi kwamba makusudio ya ukafiri katika mfano huu ni ukafiri wa kimatendo, yaani ufasiki sio ukafiri wa kiitikadi.

إِذْ أَنتُم بِالْعُدْوَةِ الدُّنْيَا وَهُم بِالْعُدْوَةِ الْقُصْوَىٰ وَالرَّكْبُ أَسْفَلَ مِنكُمْ وَلَوْ تَوَاعَدتُّمْ لَاخْتَلَفْتُمْ فِي الْمِيعَادِ وَلَـٰكِن لِّيَقْضِيَ اللَّـهُ أَمْرًا كَانَ مَفْعُولًا لِّيَهْلِكَ مَنْ هَلَكَ عَن بَيِّنَةٍ وَيَحْيَىٰ مَنْ حَيَّ عَن بَيِّنَةٍ وَإِنَّ اللَّـهَ لَسَمِيعٌ عَلِيمٌ ﴿٤٢﴾

42. Mlipokuwa kando ya bonde lililo karibu, nao wako kando ya bonde lililo mbali; na msafara upo chini yenu, Na lau mngeliagana mngelihitalifiana katika miadi. Lakini ili Mwenyezi Mungu alitimize jambo lililokuwa lifanyike Ili aangamie wa kuangamia kwa dalili dhahiri na awe hai wa kuwa hai kwa dalili dhahiri. Na hakika Mwenyezi Mungu ni mwenye kusikia mwenye kujua.

إِذْ يُرِيكَهُمُ اللَّـهُ فِي مَنَامِكَ قَلِيلًا وَلَوْ أَرَاكَهُمْ كَثِيرًا لَّفَشِلْتُمْ وَلَتَنَازَعْتُمْ فِي الْأَمْرِ وَلَـٰكِنَّ اللَّـهَ سَلَّمَ إِنَّهُ عَلِيمٌ بِذَاتِ الصُّدُورِ ﴿٤٣﴾

43. Alipokuonyesha katika usingizi wako kuwa ni wachache. Na lau angelikuonyesha kuwa ni wengi mngelivunjika moyo na mngelizozana katika jambo hilo, lakini Mwenyezi Mungu alilinda. Hakika yeye ni mjuzi wa yalimo vifuani.

وَإِذْ يُرِيكُمُوهُمْ إِذِ الْتَقَيْتُمْ فِي أَعْيُنِكُمْ قَلِيلًا وَيُقَلِّلُكُمْ فِي أَعْيُنِهِمْ لِيَقْضِيَ اللَّـهُ أَمْرًا كَانَ مَفْعُولًا وَإِلَى اللَّـهِ تُرْجَعُ الْأُمُورُ ﴿٤٤﴾

44. Na alipowaonyesha machoni mwenu mlipokutana kuwa ni wachache Na akawafanya nyinyi kuwa wachache machoni mwao ili Mwenyezi Mungu alitimize jambo lililokuwa lifanyike.

MLIPOKUWA KANDO YA BONDE LILILOKARIBU

Aya 42 – 44

MAANA

Aya hizi zinaonyesha baadhi ya sababu ambazo aliziandaa Mwenyezi Mungu kwa ajili ya ushindi wa waislamu kwa washirikina katika vita vya Badr. Miongoni mwa sababu hizo ni kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t) aliwapa ilhamu waislam kujiweka mwenye bonde lililo karibu na Madina. Ama washirikina wao walikuwa upande ulio mbali zaidi na hapa; na kati ya pande mbili kulikuwa na kilima kinachotenganisha.

Kulingana na mfumo wa maneno, inaonyesha kuwa upande wa waislamu ulikuwa ndio mahali pa vita walipomkusudia adui yao, Ni katika mipango yake Mwenyezi Mungu kuliweka kila jeshi mahali pake bila ya kujuana. Kwani lau waislamu wangeliwaona maadui zao kwa macho, wangeliogopa na kukata tamaa ya kuwashinda.

Vile vile ni katika mipango yake Mwenyezi Mungu, kwamba yeye – imetukuka hekima yake – aliwafanya wachache washirikina kwenye macho ya waislam walipokutana. Yote hayo ni kwa ajili kuidhirisha dini yake juu ya dini zote, hata kama watachukia washirikina.

Pia ni katika hekima yake kuwa Abu Sufyan aupeleka msafara wa ngamia kwenye mwambao wa bahari, ili majeshi mawili, ya batili na haki, yakutane na wala waislamu wasifuate msafara tu wakaacha jeshi.

Baada ya utangulizi huu, sasa tunaingilia kufasiri Aya:

Mlipokuwa kando ya bonde lililo karibu, nao wako kando ya bonde lililo mbali.

Msemo unatoka kwa Mwenyezi Mungu kuelekezwa kwa waislamu, akiwakumbusha mahali walipokuwa - kando ya bonde lililo karibu ya Madina, na mahali walipokuwa washirikina nao ni upande wa mbali: Vile vile anawakumbusha kugeuza njia kwa msafara wa ngamia kuelekea mwambao wa bahari, ambako Mwenyezi Mungu (s.w.t) amekuashiria kwa kauli yake:

Na msafara upo chini yenu.

Lengo la ukumbusho huu ni kwamba mambo yote yalikuwa kwa masilahi yao; kama ilivyobainika.

Na lau mngeliagana mngelihitalifiana katika miadi.

Waislamu walitoka pamoja na Mtume(s.a.w.w) kufuatia msafara wa ngamia na mizigo yake, bila ya kukusudia kupigana, lakini Mwenyezi Mungu akaigeuza safari hii ya kufuatia mali kuwa ya kupigania jihadi katika njia yake.

Hilo likawa ni heri kubwa kwao. Lau kama tangu mwanzo wangelijua kuwa wanakwenda kupigana na washirikina; kisha wakajua wingi wao, basi baadhi ya waislamu wangeligeuka kwa hofu, na kutofautiana na wale watakaotaka kupigana, Matokeo yake ushindi usingelipatikana.

Lakini ili Mwenyezi Mungu alitimize jambo lililokuwa lifanyike.

Yaani lakini Mwenyezi Mungu alipanga kukutana huku bila ya ahadi, ili litimie alilokukusudia la kutukuka dini na kudhalilika washirikina.

Ili aangamie wa kuangamia kwa dalili dhahiri na awe hai wa kuwa hai kwa dalili dhahiri.

Makusudio ya mwenye kuangamia ni kafiri, na mwenye kuwa hai ni yule mwenye kuamini. Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu aliwanusuru vipenzi vyake na kuwashinda nguvu maadui zake, siku ya Badr ili hilo liwe ni hoja mkataa kwa yule mwenye kupinga na hoja dhahiri kwa mwenye kuamini.

Utauliza : Dhahiri ya Aya inaonyesha kuwa mwenye kushindana na haki atashindwa, lakini tujuavyo, wabatilifu mara nying si wanaishinda haki?

Jibu : Mwenyezi Mungu (s.w.t) aliwaahidi ushindi waislamu kupitia kwa Mtume wake, kabla ya vita, ingawaje walikuwa wachache na wanyonge; kama alivyosema katika Aya ya 7 ya sura hii: “Na alipowaahidi moja ya makundi mawaili kuwa ni lenu.” Mwenyezi Mungu akatekeleza ahadi hiyo, ukathibiti muujiiza wa Muhammad(s.a.w.w) aliyewapa habari ya ushin- di wakati ambapo dalili zote zilionyesha ni kinyume na hivyo.

Zaidi ya hayo walisaidiwa na malaika, kama inavyofahamisha Aya ya 9 na fumba la mchanga au changarawe alilowatupia mtume(s.a.w.w) ; kama ilivyo katika Aya ya 17. Yote haya na mengineyo yalikuwa ni muujiza wa wazi uliodhihiri mikononi mwa Muhammad, siku ya Badr. Na ndiyo makusudio ya dalili dhahiri kwa anayekufuru na dalili dhahiri kwa anayeamini; na wala sio ushindi tu.

Kwa maneno mengine ni kutoa habari ya ushindi kabla ya kutokea kwake pamoja na miujiza; na wala sio makusudio ya ushindi wenyewe.

Na hakika Mwenyezi Mungu ni mwenye kusikia mwenye kujua.

Hakifichuki chochote katika kauli na vitendo na yanayopita nyoyoni.

Alipokuonyesha katika usingizi wako kuwa ni wachache. Na lau angelikuonyesha kuwa ni wengi mngelivunjika moyo na mngelizozana katika jambo (hilo), lakini Mwenyezi Mungu alilinda.

Huu nao ni muujiza mwingine wa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) . Nao ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) alimwonyesha usingizini kwamba washirikina ni wachache tena madhaifu; na kushujaika. Lau Mwenyezi Mungu angelimuonyesha kuwa maadui wana nguvu, basi azma ya waislamu ingelidhoofika, wakawa wanyonge wa kupigana na kutofautiana. Hilo lingelifuatiwa na kushindwa. Lakini Mwenyezi Mungu alilinda tatizo hili na akawahurumia waja wake waumini.

Hakika yeye ni mjuzi wa yalimo vifuani.

Yaani anajua kuwa nyoyo za waislamu zitahisi hofu ya kupigana zikijua wingi wa adui; ndipo akiziweka mbali, Mwenyezi Mungu, hisia hizi kwa alivyoona Mtume uchache wa maadui usingizini.

Na alipowaonyesha machoni mwenu mlipokutana kuwa ni wachache ili muwe imara enyi waislamu, na muwe na ukakamavu na uthabiti katika kupigana na adui yenu. Na akawafanya nyinyi kuwa wachache machoni mwao ili wasijiandae sana kupigana nanyi na kuchukua hadhari.

Hivyo ndiyo ilivyokuwa; hata Abu Jahl akasema: “Watu wa Muhammad ni mboga tu.” Mwisho wa dharau hii ulikuwa ni balaa na udhalili.

Matukio yamethibitisha kuwa silaha kubwa iliyo mkononi mwa adui ni kudharau na kutojiandaa vizuri.

Ili Mwenyezi Mungu alitimize jambo lililokuwa lifanyike.

Wafasiri wamesema: Jumla hii imekaririka kwa vile sababu yake katika Aya ya kwanza ni kukusanyika waislamu na washirikina katika vita bila ya miadi. Ama sababu katika Aya hii imekuja kwa kufanyisha uchache kila kundi machoni mwa mwenzake.

Nasi tumetangulia kusema kuwa kukaririka katika Qur’an ni aina ya utangazaji uliofaulu.

Na kwa Mwenyezi Mungu hurejeshwa mambo yote.

Hutokea kwake na huishia kwake. Yeye ndiye mwenye kuyapanga kwa uadilifu wake na hekima yake.

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا لَقِيتُمْ فِئَةً فَاثْبُتُوا وَاذْكُرُوا اللَّـهَ كَثِيرًا لَّعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ ﴿٤٥﴾

45. Enyi mlioamini! Mnapokutana na jeshi, basi kazaneni, na mumkumbuke Mwenyezi Mungu sana ili mpate kufaulu.

وَأَطِيعُوا اللَّـهَ وَرَسُولَهُ وَلَا تَنَازَعُوا فَتَفْشَلُوا وَتَذْهَبَ رِيحُكُمْ وَاصْبِرُوا إِنَّ اللَّـهَ مَعَ الصَّابِرِينَ ﴿٤٦﴾

46. Na mtiini Mwenyezi Mungu na Mtume wake wala msizozane, msije mkavunjika moyo na zikapotea nguvu zenu, na subirini. Hakika Mwenyezi Mungu yuko pamoja na wanaosubiri.

وَلَا تَكُونُوا كَالَّذِينَ خَرَجُوا مِن دِيَارِهِم بَطَرًا وَرِئَاءَ النَّاسِ وَيَصُدُّونَ عَن سَبِيلِ اللَّـهِ وَاللَّـهُ بِمَا يَعْمَلُونَ مُحِيطٌ ﴿٤٧﴾

47. Wala msiwe kama wale waliotoka majumbani mwao kwa fahari na kujionyesha kwa watu, na kuzuilia njia ya Mwenyezi Mungu: Na Mwenyezi Mungu ameyazunguka wanayoyafanya.

وَإِذْ زَيَّنَ لَهُمُ الشَّيْطَانُ أَعْمَالَهُمْ وَقَالَ لَا غَالِبَ لَكُمُ الْيَوْمَ مِنَ النَّاسِ وَإِنِّي جَارٌ لَّكُمْ فَلَمَّا تَرَاءَتِ الْفِئَتَانِ نَكَصَ عَلَىٰ عَقِبَيْهِ وَقَالَ إِنِّي بَرِيءٌ مِّنكُمْ إِنِّي أَرَىٰ مَا لَا تَرَوْنَ إِنِّي أَخَافُ اللَّـهَ وَاللَّـهُ شَدِيدُ الْعِقَابِ ﴿٤٨﴾

48. Na shetani alipowapambia vitendo vyao, na kusema: Leo hakuna wa kuwashinda na hali mimi ni mlinzi wenu. Yalipoonana majeshi mawili, alirudi nyuma na kusema: Mimi si pamoja nanyi, mimi naona msiyoyaona, mimi namwogopa, Mwenyezi Mungu; na Mwenyezi Mungu ni mkali wa kuadhibu.

إِذْ يَقُولُ الْمُنَافِقُونَ وَالَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٌ غَرَّ هَـٰؤُلَاءِ دِينُهُمْ وَمَن يَتَوَكَّلْ عَلَى اللَّـهِ فَإِنَّ اللَّـهَ عَزِيزٌ حَكِيمٌ ﴿٤٩﴾

49. Waliposema wanafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao: Hawa imewadanganya dini yao, Na mwenye kumtegemea Mwenyezi Mungu, basi hakika Mwenyezi Mungu ndiye mwenye nguvu mwenye hekima.

MNAPOKUTANA NA JESHI KAZANENI

Aya 45 – 49

MAANA

YANAYOLETA USHINDI

Enyi mlioamini! Mnapokutana na jeshi, basi kazaneni, na mumkumbuke Mwenyezi Mungu sana ili mpate kufaulu.

Makusudio ya jeshi ni lile linalofanya ufisadi katika nchi. Kauli yake Mwenyezi Mungu ili mpate kufaulu yaani mlishinde.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) ametaja mambo mawili yanayoleta ushindi katika Aya hii:

La kwanza: ni uthabiti na ushupavu, aliposema; “Kazaneni.”

La pili: ni ikhlas, aliposema “Mkumbukeni Mwenyezi Mungu sana.” Makusudio ya kumkumbuka Mungu vitani sio dhikri ya takbira na tahalili tu; isipokuwa ni kuwe kupigana na ukakamavu kwa ajili ya Mwenyezi Mungu tu; kwa maana ya kutoathirika vita na hali yoyote isipokuwa kwa ajili ya kuthibitika haki na kubatilika batili; kwa ajili ya kuhifadhi amani ya watu na usalama wao; na kuwapiga waovu wanaoeneza ufisadi katika nchi kwa kunyanganya na kupora huku wakileta vita na fitina ili watawale miji na riziki za waja.

Na mtiini Mwenyezi Mungu na Mtume wake wala msizozane, msije mkavunjika moyo na kupoteza nguvu zenu, na subirini. Hakika Mwenyezi Mungu yuko pamoja na wanaosubiri.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) ametaja katika Aya iliyotangulia mambo mawili ya kuleta ushindi; na katika Aya hii anataja matatu: Kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume, kujiepusha na mizozo na kusubiri (kuvumilia.) Lakini kuwa na subira ndiko kukazana. Kwa hiyo kauli yake Mwenyezi Mungu: Subirini ni ibara nyingine ya kazaneni; kama ambavyo kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake ndiyo ikhlasi. Ama kutofautiana kwingine ni kuzuri na kwengine ni kubaya, Ufafanuzi utafuatia.

Kwa ufupi mambo yanayoleta ushindi wa hakika yaliyoelezwa katika Aya mbili ni matatu:

1. Subira na kukazana, nako ni kujitolea mhanga kwa moyo wote ili kuinusuru haki ishinde batili; kama ambavyo haki inashinda kwa kuondoka batili, vile vile haki inashinda kwa kufichuka batili na kuidhihirisha kwa watu.

Subira ni lazima katika kufika lengo lolote. Hakuna mwanafunzi, mwalimu, mgunduzi, au mfanyi biashara yeyote anayeweza kupata kitu bila ya subira (uvuumilivu) na kukazana. Kiwango cha kuvumilia kwake mashaka na uchungu ndicho kiwango cha kufaulu kwake, Na hii ndiyo siri ya kauli yake Mwenyezi Mungu.

Hakika Mwenyezi Mungu yuko pamoja na wanaosubiri

وَبَشِّرِ الصَّابِرِينَ ﴿١٥٥﴾

“Wape habari njema wanaosubiri (2:155)

وَلَا يُلَقَّاهَا إِلَّا الصَّابِرُونَ ﴿٨٠﴾

Wala hawatapewa hayo isipokuwa wanaosubiri” (28:80)

وَلَئِن صَبَرْتُمْ لَهُوَ خَيْرٌ لِّلصَّابِرِينَ ﴿١٢٦﴾

“Na kama mkivumilia hiyo ni kheri kwa wanaosubiri” (16:126) na Aya nyinginezo.

Mimi nimejaribu kuwa na subira nilipokuwa mwanafunzi na mtunzi. Sikuona kitu chenye mwisho mtamu na manufaa kama hicho. Tumezungumzia kuhusu kuwa na subira na uvimilivu katika Juz.2 (Sura 2:155)

2. Ikhlasi: Kukusudia kitendo kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, kumtegemea yeye sio mwingine na kuamini kwa imani mkato kwamba yaliyoko mbele ya Mwenyezi Mungu ni bora na yatasalia kuliko jaha, mali na watoto, kisimwaathiri chochote katika hivi na kumtii Mwenyezi Mungu na radhi yake.

Mtu huweza kufikia malengo yake ya kishetani, lakini haya hayahisabiwi kuwa ni ushindi, ila kama tukizingatia batili ni fadhila, wizi ni ghanima na ufisadi ni takua na utengenevu.

3. Kujiepusha na aina yoyote ya kutofautiana. Inaweza kutokea kutofautiana katika maoni na mtazamo kwa ikhlasi. Kutofautiana huku hakupingani na kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume wala hakuzuii kuafikiana lengo; kama vile kupigana jihadi na wafisadi. Mara nyingi huko kunakuwa ni njia ya kufunguka uhakika.

Vile vile inaweza kuwa sababu ya kutofautiana ni hawaa, na ubinafsi na kupupia dunia. Hayo ndiyo makusudio ya kauli yake Mwenyezi Mungu mtukufu: “Wala msizozane msije mkaharibikiwa na kupoteza nguvu zetu.”

Mifano ya madhara ya kuzozana na kushindana haina idadi, na katika Historia ni mamia. Hatuna haja ya kutoa mfano wa historia ya mbali, Historia yetu tu ya sasa hivi inatutosha kwa mifano yote. Hivi karibuni nimesoma makala ya mwandishi wa Kimarekani, Salz Bridge aliyoiandika katika gazeti la Herald Tribune. Ninamnukuu:

“Washington inapima tofauti ya idadi ya waarabu na Israil; na inasisitiza kwamba, hata kama si kwa masilahi ya Israil, lakini daima kipimo kitakuwa ni kugawanyika kunakoendelea baina ya dola za kiarabu. Kwa sababu kugawanyika huku kunaifanya idadi ya waarabu iwe ni nambari tu, isiyokuwa na thamani yoyote.”

Kabla ya mwandishi huyu viongozi wa Israil wametangaza mara nyingi kuwa wao walifaulu katika vita vya tarehe 5 Juni kwa msaada wa Marekani na kutofautiana kwa waarabu. Na ni kitu gani kilichowapendeza waisrail kuliko kushikiana silaha waarabu wenyewe kwa wenyewe, badala ya kuwashikia Israil? Kwa ajili hiyo wakoloni wa kizayuni wamefanya kila wawezalo kuwagombanisha waarabu. Jambo la kusikitisha ni kuwa wamepatikana waliowaitikia, bali wanaozungumza kwa niaba yao, Hata hivyo, mapambano bado yanaendelea. Ni lazima wakoloni na vibaraka wao watashindwa, sasa au baadaye.

Wala msiwe kama wale waliotoka majumbani mwao kwa fahari na kujionyesha kwa watu, na kuzuilia njia ya Mwenyezi Mungu, Na Mwenyezi Mungu ameyazunguka wanayoyafanya.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kuwaamrisha waislamu mambo matatu wakiwa wanawaelekea vitani, sasa anawakataza mambo matatu: fahari, kujionyesha, na kuzuilia njia ya Mwenyezi Mungu.

Amenasibisha sifa hizi tatu kwa makafiri wa kiquraish kwa sababu wao waliotoka kuelekea Badr kumpiga vita Mtume(s.a.w.w) wakiwa wanajifaharisha, wanajionyesha na kuwazuilia waislamu na njia ya Mwenyezi Mungu.

Wafasiri wanasema: Abu Jahli alipokuwa akiwaongoza maquraish kumpiga vita Mtume huko Badr, njiani alijiwa na Ibn Al-Hiqaf Al-Kinaniy na zawadi kutoka kwa baba yake. Akamwambia Abu Jahli: “Baba yangu anakwambia, kama unataka atakuongozea watu, na kama unataka nitaungana nawe.” Abu Jahli akasema “Ikiwa tunapigana na Mwenyezi Mungu, kama anavyodai Muhammad, basi Wallahi hatumuwezi Mwenyezi Mungu na ikiwa tunapigana na watu, basi sisi ndio watu wenye nguvu zaidi, wala hatutarudi nyuma kupigana na Muhammad mpaka tufike Badr tunywe pombe na watuimbie watumwa na waarabu wasikie.”

Kujifaharisha kunadhihiri katika maana yake pana kwa kauli ya Abu Jahl: “Na sisi ni watu wenye nguvu zaidi.” Ama kujionyesha kuko katika kauli yake: “Na waarabu wasikie” Kwa ajili hii basi nasi tunaelemea kwenye kauli ya mwenye kusema kuwa Aya hii imemshukia Abu Jahli.

Ama mwisho wa fahari hiyo na ria ni kuuawa waliouawa, akiwemo Abu Jahli na kutekwa waliotekwa na kushindwa waliobakia.

Na shetani alipowapambia vitendo vyao, na kusema: Leo hakuna wa kuwashinda na hali mimi ni mlinzi wenu. Yalipoonana majeshi mawili, alirudi nyuma na kusema: Mimi si pamoja nanyi, mimi naona msiyoyaona, mimi namwogopa, Mwenyezi Mungu; na Mwenyezi Mungu ni mkali wa kuadhibu.

Aya hii inasema waziwazi kuwa kuna kitu kinachoitwa Shetani kiliwachochea maquraish kumpiga vita Mtume huko Badr na kuwapa dhamana ya ushindi, na kwamba yeye alipoyakinisha mwisho wao alijitoa.

Tumekwishaelezea mara nyingi kwamba sisi tunaamini kila linaoelezwa na wahyi na lisilokataliwa na akili; na kwamba tunaiachia ghaibu ufafanuzi. Hakuna kitu katika hukumu ya akili kinachozuia kupatikana kitu kinachoonekana au kisichoonekana kinachowatia mshawasha watu kwenye batili na kuwahadaa. Mwenyezi Mungu (s.w.t) alimwamrisha Mtume wake mtukufu ajilinde na shari ya mwenye kutia wasiwasi katika nyoyo za watu, awe jini au mtu.

Waliposema wanafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao: Hawa imewadanganya dini yao. Na mwenye kutegemea kwa Mwenyezi Mungu, basi hakika Mwenyezi Mungu ndiye mwenye nguvu mwenye hekima.

Wanafiki ni wale wanaodhihirisha Uislamu na kuficha ukafiri. Ama wale ambao nyoyoni mwao mna maradhi, ni wanafiki, makafiri na mafasiki.

Kwa hiyo kuunganisha wenye maradhi nyoyonni juu ya wanafiki ni kati- ka kuunganisha jumla juu ya mahsusi.

Mwenyezi Mungu amesimulia, katika Aya hii, kuhusu wenye maradhi ya moyo, kwamba wao walishangaa walipoona kujitokeza kwa waislamu wachache wa kupigana vita na makafiri; wala hawakufahamu tafsir ya kujitokeza huku isipokuwa kujiangamzia kwa waislamu na kuhadaliwa na matumaini ya kufuzu pepo. Kwao hayo ni maneno yasiyo na maana. Kwa sababu kila kitu kwao ni biashara tu; hata dini.

JE WAKOMBOZI NI WAHARIBIFU?

Wakati huu ambapo nguvu za shari zimeungana kuwafanyia njama waarabu na waislamu na kuwafukuza wazalendo wa Palestina katika ardhi zao na kuwatupa ufuoni wanawake, wazee na watoto; wakati huu ambapo wakombozi wanawanyima usingizi waisrail na kuwakosesha raha; na kutamka neno, uhuru juu ya ukombozi wa ardhi iliyovamiwa, ndipo anaposema Sheikh mwenye kilemba kwenye mpaka wa Israil katika kijiji kimoja cha kaskazini, akinadi kwa kupaza sauti kadamnasi na kusema: “Wakombozi ni waharibifu” sawa na anavyosema Moshe Dayan.

Ewe mheshimiwa! Wakombozi ni waharibifu! Je, wewe na Israil ndio watengenezaji? Kwa nini wakombozi wawe waharibifu? Je, ni kwa kuwa wanapigania haki zao, katika njia ya kuuawa na kuua; au ni kwa vile wao wamebadilisha jina la wakimbizi na kuwa wakombozi? Na, je, wewe katika kauli yako hii unamtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake na kupigana jihadi kutekeleza wajibu wa kidini na wa kiuzalendo?

Ni dini gani hiyo inayokataza kujitolea mhanga kwa ajili ya kulinda mtu nchi yake na kutaka kuishi huru na kuheshimiwa; hata kwa thamani ya namna gani?

Mimi nimeelewa mantiki yako ewe Sheikh, Wewe unasema kuwa Israil inajibu mashambulizi ya wakombozi kwa kuwatesa wanyonge, nasi twakuuliiza: Walikuwa wapi wakombozi mnamo tarehe 29 Juni 1897, wakati Uzayuni ulipofanya mkutano mkuu huko Uswisi, na kupitisha azimio la kuwafukuza waarabu Palestina na waikalie Mayahudi? Je, azimio hilo lilitokana na wakombozi wakati huo?

Kisha utasema nini kuhusu mauaji ya Diryasin na uchinjaji ulofanywa na Mayahudi kwa wakazi wasio na hatia, kabla ya jeshi kuingia Palestina?

Inakupasa ujue ewe mwenye kilemba cha usheikh na kila Mwarabu kwamba waisrail hawatosheki tu na Palestina, Jordan, Lebanon, Syria na Iraq; isipokuwa lengo lake ni kuwadhalilisha waarabu wote wanyenyekee Uzayuni na ukoloni kisiasa na kiuchumi. Israil inatamani mafuta ya Kuwait, Qatar, Abu Dhabi na Saudia.

Tamaa yao hii wameipanga na kuiwekea mkakati kwa kula njama pamoja na dola za kikoloni, Harakati za wakombozi ndizo zilizoharibu mikakati hii ya waisrail kiasi cha kufikiria kuwa Israil haitakuwako.

Ni bora mara elfu tuvumilie maumivu yanayosababishwa na vitendo vya wakombozi, kuliko kuwacha yatimie malengo ya Israil ambayo haiatoshe- ki na chochote; hata mto Nail na Furat.

Zaidi ya hayo, hivi sasa inatulazimu kumkabili adui kwa kupatikana wakombozi wa kujitolea mhanga; kama hatua ya kwanza na tuvumilie taabu zote zitakazosababishwa nao ili kukinga ambalo ni baya na kubwa zaidi.

Baada ya hayo, ewe Sheikh! Unasemaje kuhusu vikosi vilivyokuwa vikitumwa na Muhammad(s.a.w.w) kukata njia ya maadui zake washirikina na kuchukua mali zao, kuua na kuchukua mateka na kuwakosesha amani majumbani akiwa yeyey mwenye binafsiakiongoza baadhi ya mashmbulizi hayo; kama alivyowapiga Mayahudi wa Bani Quraidha baada ya kuvunja ahadi na kujiiunga na Abu Sufyan, adui wa Mwenyezi Mungu na Mtume wake katika vita vya Ahzab.

Mtume(s.a.w.w) aliliamrisha jeshi lake alilokuwa akiliongoza yeye mwenyewe lichome mimea ya mayahudi, na kukata miti yao na kuvunja majumba yao, Je, kitendo chake hicho Mtume kilikuwa cha utengezaji au uharibifu?

Imepokewa Hadith Mutawatir aliposema Mtume(s.a.w.w) : “Mwenye kufa akilinda mali yake amekufa Shahid” Je vipi kwa yule atakayokufa katika hali ya kumzuia Mwisrail adui wa Mwenyezi Mungu, wa nchi na wa binadamu wote?

Mwenyezi Mungu anasema:

إِنَّ اللَّـهَ اشْتَرَىٰ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ أَنفُسَهُمْ وَأَمْوَالَهُم بِأَنَّ لَهُمُ الْجَنَّةَ يُقَاتِلُونَ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ فَيَقْتُلُونَ وَيُقْتَلُونَ وَعْدًا عَلَيْهِ حَقًّا فِي التَّوْرَاةِ وَالْإِنجِيلِ وَالْقُرْآنِ وَمَنْ أَوْفَىٰ بِعَهْدِهِ مِنَ اللَّـهِ فَاسْتَبْشِرُوا بِبَيْعِكُمُ الَّذِي بَايَعْتُم بِهِ وَذَٰلِكَ هُوَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ ﴿١١١﴾

‘Hakika Mwenyezi Mungu amenunua kwa waumini nafsi zao na mali zao kuwa wao watapata pepo. Wanapigana katika njia ya Mwenyezi Mungu, wanaua na wanuawa. Hii ni ahadi aliyojilazimisha kwa haki katika Tawrat na Injili na Qur’an, Na ninani atimiziaye ahadi kuliko Mwenyezi Mungu? Basi furahini kwa biashara yenu mliyofanya naye, Na huko ndiko kufuzu kukubwa” (9:111)

Wala hakuna anayeitumia Aya hii katika umma wa Kiarabu isipokuwa wapiganaji ukombozi; na kujitolea kwao ndio jiwe la msingi la mapinduzi ya mataifa yote ya kiarabu.

2

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI

وَلَوْ تَرَىٰ إِذْ يَتَوَفَّى الَّذِينَ كَفَرُوا الْمَلَائِكَةُ يَضْرِبُونَ وُجُوهَهُمْ وَأَدْبَارَهُمْ وَذُوقُوا عَذَابَ الْحَرِيقِ ﴿٥٠﴾

50. Na lau ungeliwaona Malaika wanapowafisha wale waliokufuru wakipiga nyuso zao na migongo yao na (kuwaambia) ionjeni adhabu iunguzayo.

ذَٰلِكَ بِمَا قَدَّمَتْ أَيْدِيكُمْ وَأَنَّ اللَّـهَ لَيْسَ بِظَلَّامٍ لِّلْعَبِيدِ ﴿٥١﴾

51. Hayo ni kwa sababu ya yale yaliyokwishatangulizwa na mikono yenu, Na hakika Mwenyezi Mungu si mwenye kuwadhulumu waja.

كَدَأْبِ آلِ فِرْعَوْنَ وَالَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ كَفَرُوا بِآيَاتِ اللَّـهِ فَأَخَذَهُمُ اللَّـهُ بِذُنُوبِهِمْ إِنَّ اللَّـهَ قَوِيٌّ شَدِيدُ الْعِقَابِ ﴿٥٢﴾

52. Ni kama ada ya watu wa firaun na wale waliokuwa kabla yao; walizikufuru ishara za Mwenyezi Mungu, kwa hiyo Mwenyezi Mungu akawaadhibu kwa sababu ya makosa yao. Hakika Mwenyezi Mungu ni mwenye nguvu, mkali wa kuadhibu.

ذَٰلِكَ بِأَنَّ اللَّـهَ لَمْ يَكُ مُغَيِّرًا نِّعْمَةً أَنْعَمَهَا عَلَىٰ قَوْمٍ حَتَّىٰ يُغَيِّرُوا مَا بِأَنفُسِهِمْ وَأَنَّ اللَّـهَ سَمِيعٌ عَلِيمٌ ﴿٥٣﴾

53. Hiyo ni kwa sababu Mwenyezi Mungu habadilishi kabisa neema alizowaneemesha watu, mpaka wao wabadilishe yaliyomo nafsini mwao. Na hakika Mwenyezi Mungu ni mwenye kusikia mwenye kujua.

كَدَأْبِ آلِ فِرْعَوْنَ وَالَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ كَذَّبُوا بِآيَاتِ رَبِّهِمْ فَأَهْلَكْنَاهُم بِذُنُوبِهِمْ وَأَغْرَقْنَا آلَ فِرْعَوْنَ وَكُلٌّ كَانُوا ظَالِمِينَ ﴿٥٤﴾

54. Ni kama hali ya watu wa firaun na wale waliokuwa kabla yao; walizikadhibisha ishara za Mola wao, kwa hiyo tukawaangamiza kwa sababu ya dhambi zao, na tukawazamisha watu wa firaun, Na wote walikuwa madhalimu.

LAU UNGEONA

Aya 50 – 54

MAANA

Na lau ungeliwaona Malaika wanapowafisha wale waliokufuru wakipiga nyuso zao na migongo yao na (kuwaambia) ionjeni adhabu iunguzayo.

Maneno yanaelekezwa kwa kila mwenye kuona, kwa sababu makusudio ni mawaidha na mazingatio. Makusudio ya wale waliokufuru ni kila kafiri, kwa kuchukulia dhahiri ya tamko kama lilivyo. Imesemekana kwamba makusudio ni kuwahusu makafiri wa Kiquraish waliopigana na Mtume(s.a.w.w) katika vita vya Badr, kwa kuchukulia mfumo wa maneno. Kwa sababu bado maneno ni ya tukio la Badr.

Kupiga nyuso na migongo yao ni fumbo la adhabu wanayoipata makafiri wakati wa kufa. Inawezekana kuwa ni kupiga hasa kwa kiuhakika, hata kama hakuonekani. Vyovyoote iwavyo ni kwamba makafiri wanahizika wakati wa kufa na baada ya kufa; wala hatuna umuhimu wa kutaja aina ya hizaya yenyewe.

Hayo ni kwa sababu ya yale yaliyokwishatangulizwa na mikono yenu, Na hakika Mwenyezi Mungu si mwenye kuwadhulumu waja.

Vipi adhulumu naye anaikataza dhuluma na kuiwekea adhabu? Sunni wanasema kuwa akili inajuzisha kwa Mwenyezi Mungu mtukufu amwadhibu mtiifu na kumpa thawabu mwasi, Vile vile akili inajuzisha Mwenyezi Mungu ahalifu ahadi yake. Tazama Mawaqif 8 sehemu ya 5 na sita. Na Madhahibul-Islamiya cha Abu Zuhura uk. 104.

Shia wanasema: Akili haijuzishi kwa Mwenyezi Mungu amwaadhibu mtiifu na inajuzisha kumpa fadhila mwasi. Kwa sababu mwadilifu hamwadhibu mtiifu na mkarimu mpole humsamehe mwenye kumfayia uovu.

Ni kama ada ya watu wa firaun na wale waliokuwa kabla yao; walizikufuru ishara za Mwenyezi Mungu, kwa hiyo Mwenyezi Mungu akawaadhibu kwa sababu ya makosa yao. Hakika Mwenyezi Mungu ni mwenye nguvu, mkali wa kuadhibu.

Yaani yaliyowapata washirikina siku ya Badr, kuuliwa na kutekwa, ni kwa sababu wao walimkadhibisha Muhammad(s.a.w.w) . Yaliyowapata hawa yanafanana na yaliyowapata washirikina waliotangulia. Kwa sababu wali- wakadhibisha Mitume wao; kama watu wa Firaun na waliokuwa kabla yao.

Hiyo ni kwa sababu Mwenyezi Mungu habadilishi kabisa neema alizowaneemesha watu, mpaka wao wabadilishe yaliyomo nafsini mwao. Na hakika Mwenyezi Mungu ni mwenye kusikia mwenye kujua.

Dhahiri ya neema hapa ni riziki na kuibadilisha ni kuiondoa.

Hapa linajitokeza swali kuwa : dhahir ya Aya inafahamisha kwamba watu aliowaneemesha Mwenyezi Mungu kwa riziki hubakia kwao maadamu ni watiifu, Wakiasi hunyang’anywa. Lakini tunavyoona ni kuwa waasi wengi, kila wanavyozidi uasi ndivyo wanavyozidi utajiri wala hakibadili kitu kwao je ni vipi?

Jibu : Aya haikutaja tamko la maasi wala ukafiri. Lililofahamisha Aya ni kuwa Mwenyezi Mungu haondoi neema kwa watu wake ila wakibadilisha yaliyomo nyoyoni mwao, lakini Mwenyezi Mungu hakubainisha aina ya mabadiliko. Mfano wake ni Aya isemayo:

إِنَّ اللَّـهَ لَا يُغَيِّرُ مَا بِقَوْمٍ حَتَّىٰ يُغَيِّرُوا مَا بِأَنفُسِهِمْ ﴿١١﴾

“Hakika Mwenyezi Mungu habadilishi yaliyoko kwa watu mpaka wabadilishe yaliyomo nafsini mwao.. “ (13:11).

Watu wa Firaun, aliowatolea mfano Mwenyezi Mungu katika Aya iliyotangulia, walikuwa washirikina kabla na baada, Wao walizidisha kupetu- ka mipaka baada ya Musa kuwajia.

Kwa hiyo tutachukulia Aya tuliyonayo, kwenye maana ya kuwa Mwenyezi Mungu hawaangamizi watu duniani ila ni baada ya kuwapelekea Mtume na kuwalingania kwa Mwenyezi Mungu ana kwa ana; kisha waukatae mwito wake; kama vile watu wa Firaun na waliotangulia; wakiwemo watu wa Nuh, Lut na wengineo. Na kama hakuwapelekea Mtume, basi huchelewesha adhabu yao mpaka siku ya hisabu na malipo, Ama kuhusu Aya (13:11) tuna maoni katika tafsir yake tutayabainisha huko inshallah.

Ni kama hali ya watu wa firaun na wale waliokuwa kabla yao; wal- izikadhibisha ishara za Mola wao, kwa hiyo tukawaangamiza kwa sababu ya dhambi zao, na tukawazamisha watu wa firaun.

Umepita mfano wake katika Juz.3 (3:11)

Na wote walikuwa madhalimu.

Yaani kila mmoja katika watu wa Firaun ambao walimkadhibisha Musa(a.s) na makafiri wa Kiquraish ambao walimkadhibisha Muhammad(s.a.w.w) . Wamejidhullumu wao wenyewe na wakawadhlumu watu kwa kuwazuilia njia ya Mwenyezi Mungu.

إِنَّ شَرَّ الدَّوَابِّ عِندَ اللَّـهِ الَّذِينَ كَفَرُوا فَهُمْ لَا يُؤْمِنُونَ ﴿٥٥﴾

55. Hakika wanyama waovu kabisa mbele ya Mwenyezi Mungu ni wale wanaokufuru, basi hawataamini.

الَّذِينَ عَاهَدتَّ مِنْهُمْ ثُمَّ يَنقُضُونَ عَهْدَهُمْ فِي كُلِّ مَرَّةٍ وَهُمْ لَا يَتَّقُونَ ﴿٥٦﴾

56. Ambao umepeana nao ahadi kisha wanavunja ahadi yao kila mara; wala hawaogopi.

فَإِمَّا تَثْقَفَنَّهُمْ فِي الْحَرْبِ فَشَرِّدْ بِهِم مَّنْ خَلْفَهُمْ لَعَلَّهُمْ يَذَّكَّرُونَ ﴿٥٧﴾

57. Basi ukiwakuta vitani wakimbize kwa hao walio nyuma yao ili wapate kufahamu.

وَإِمَّا تَخَافَنَّ مِن قَوْمٍ خِيَانَةً فَانبِذْ إِلَيْهِمْ عَلَىٰ سَوَاءٍ إِنَّ اللَّـهَ لَا يُحِبُّ الْخَائِنِينَ ﴿٥٨﴾

58. Na kama ukihofia hiyana kwa watu, basi watupie kwa usawa, Hakika Mwenyezi Mungu hawapendi wafanyao hiana.

وَلَا يَحْسَبَنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا سَبَقُوا إِنَّهُمْ لَا يُعْجِزُونَ ﴿٥٩﴾

59. Wala wale waliokufuru wasifikirie kwamba wao wametangulia; kwa hakika wao hawatashinda

وَأَعِدُّوا لَهُم مَّا اسْتَطَعْتُم مِّن قُوَّةٍ وَمِن رِّبَاطِ الْخَيْلِ تُرْهِبُونَ بِهِ عَدُوَّ اللَّـهِ وَعَدُوَّكُمْ وَآخَرِينَ مِن دُونِهِمْ لَا تَعْلَمُونَهُمُ اللَّـهُ يَعْلَمُهُمْ وَمَا تُنفِقُوا مِن شَيْءٍ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ يُوَفَّ إِلَيْكُمْ وَأَنتُمْ لَا تُظْلَمُونَ ﴿٦٠﴾

60. Na waandalieni nguvu kama vile muwezavyo na kwa farasi waliofungwa ili mumtishe adui wa Mwenyezi Mungu na adui yenu, na wengineo msiowajua nyinyi, Mwenyezi Mungu anawajua, Na chochote mtakachotoa katika njia ya Mwenyezi Mungu, mtarudishiwa, wala nyinyi hamtadhulumiwa.

وَإِن جَنَحُوا لِلسَّلْمِ فَاجْنَحْ لَهَا وَتَوَكَّلْ عَلَى اللَّـهِ إِنَّهُ هُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ ﴿٦١﴾

61. Na kama wakielekea kwenye amani, nawe ielekee, na mtegemee Mwenyezi Mungu. Hakika yeye ni mwenye kusikia mwenye kujua.

وَإِن يُرِيدُوا أَن يَخْدَعُوكَ فَإِنَّ حَسْبَكَ اللَّـهُ هُوَ الَّذِي أَيَّدَكَ بِنَصْرِهِ وَبِالْمُؤْمِنِينَ ﴿٦٢﴾

62. Na kama wakitaka kukuhadaa, basi Mwenyezi Mungu atakutoshelezea. Yeye ndiye aliyekupa nguvu kwa msaada wake na kwa waumini.

وَأَلَّفَ بَيْنَ قُلُوبِهِمْ لَوْ أَنفَقْتَ مَا فِي الْأَرْضِ جَمِيعًا مَّا أَلَّفْتَ بَيْنَ قُلُوبِهِمْ وَلَـٰكِنَّ اللَّـهَ أَلَّفَ بَيْنَهُمْ إِنَّهُ عَزِيزٌ حَكِيمٌ ﴿٦٣﴾

63. Na akaziunganisha nyoyo zao; lau ungelitoa yote yaliyomo ardhini usingeliweza kuiunganisha mioyo yao, lakini Mwenyezi Mungu amewaunganisha, Hakika yeye ndiye mwenye nguvu mwenye hekima.

KANUNI NA HUKUMU KATIKA AMANI NA VITA

Aya 55 – 63

MAANA

Aya hizi zimekusanya kaida na hukumu katika hali ya usalama na ya vita. Tutazifafanua kulingana na mpango ufuatao:-

Hakika wanyama waovu kabisa mbele ya Mwenyezi Mungu ni wale wanaokufuru, basi hawataamini. Ambao umepeana nao ahadi kisha wanavunja ahadi yao kila mara; wala hawaogopi

Asili ya neno mnyama (Dabba) ni kila anayetembea ardhini. Kisha ikawa neno hilo linatumiwa sana na wenye miguu mine.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anasema kuwa jamaa waliokufuru, ambao imani yao haitarajiwi walielewana na Mtume(s.a.w.w) kuishi kwa amani na ujirani mwema. Lakini kumbe wamedhamiria uhaini na wakauvunja ahadi zaidi ya mara moja; hawakuogopa balaa wala adhabu itakayotokana na hayo. Mwenyezi Mungu amewataja hawa kuwa ni waovu zaidi kuliko mnyama.

Kuna kundi la wafasiri wamesema kuwa ni Mayahudi wa Bani Quraidha, waliahidiana na Mtume kisha wakavunja ahadi na kusaidiana na washirikina wa Makka siku ya Badr. Mtume(s.a.w.w) aliposhinda waliomba msamaha, akawakubalia na kuwasamehe.

Kisha wakawaahidiana mara ya pili, wakavunja ahadi siku ya Khandaq, Si ajabu kwa Mayahudi kufanya hiyana na kuvunja ahadi; isipokuwa ajabu ni kuwa na ukweli na uaminifu.

Basi ukiwakuta vitani wakimbize kwa hao walio nyuma yao ili wapate kufahamu.

Maneno haya anaambiwa Mtume(s.a.w.w) , Mwenyezi Mungu anabainisha hukumu ya hawa makafiri wasio na ahadi; kwamba akiwapata awatie adabu kali kabisa; hata wengine wanaotaka kufanya hiyana wapate funzo. Kwa hivyo basi inatubainikia kuwa makusudio ya walio nyuma yao ni wengine.

Na kama ukihofia hiyana kwa watu, basi watupie kwa usawa.

Makusudio ya kuhofia hapa ni kujua; na usawa ni kuwa sawa wewe na wao katika kujua kuvunja ahadi.

Maana ni ikiwa baina yako wewe Muhammad na watu kuna mapatano na ukajua kabisa kwamba wao watavunja ahadi, kwa kuonyesha alama wazi wazi kuwa wao wana dhamira mbaya au hiyana na kuyafanya mapatano ni pazia ya kupanga njama zao, basi yatupilie mbali mapatano yao na uwafahamishe kuwa umevunja mapatano yao; wala usianze kupigana kabla ya kuwafahamisha ili usinasibishiwe uhaini; kwani

hakika Mwenyezi Mungu hawapendi wafanyao hiana.

Kwa maneno mengine ni kwamba Uislamu unawajibisha kutekeleza ahadi kwa watekelezao ahadi. Ama wale wanaofanya ahadi ni nyenzo ya uhaini basi Uislamu unaamrisha kuivunja, kwavile hiyo si ahadi bali ni vitimbi.

وَأَنَّ اللَّـهَ لَا يَهْدِي كَيْدَ الْخَائِنِينَ ﴿٥٢﴾

Hakika Mwenyezi Mungu haongozi vitimbi vya wahaini” (12:52).

Imam Ali(a.s) anasema:Kuwatekelezea ahadi wavunja ahadi ni kuvunja ahadi na kuvunja ahadi kwa wavunja ahadi ni kutekeleza ahadi.”

Wala wale waliokufuru wasifikirie kwamba wao wametangulia; kwa hakika wao hawatashinda.

Maana ya wametangulia ni wameponyoka. Na hawatashinda, ni hawatanishinda mimi. Maana ya Aya kwa ujumla ni kuwa asifikirie yeyote kwamba Mwenyezi Mungu anapitwa na jambo.

Na waandalieni nguvu kama vile muwezavyo na kwa farasi waliofungwa.

Aya zilizotangulia zimeonyesha mfungamano wa mapatano na hukumu ya anayeyavunja. Katika Aya hii, Mwenyezi Mungu (s.w.t) anawaamrisha Waislamu kujianda kwa nguvu na kukamilisha maandalizi dhidi ya adui.

Makusudio ya nguvu ni chochote kile kinachotia nguvu. Katika kumkabili adui, iwe ni Mkuki, Roketi, au chochote. Mwenyezi Mungu amehusisha kutaja Farasi, kwa sababu wakati huo ndio ilikuwa silaha ya kutegemea.

Imepokewa hadith kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) kwamba yeye alisoma Aya hii na kusema:

“Tambueni kwamba nguvu ni kurusha” Alilikariri mara tatu, Makusudio ni kubainisha umuhimi wa kurusha na athari yake katika vita.

Historia imethibitisha umuhimu wa nadhari hiyo aliyoitamka Mtume(s.a.w.w) kiasi miaka elfu moja na mia tatu; ambapo hakukua na makombora wala mizinga. Wataalamu wameelekeza akili zao kila mara kukaza nguvu za kurusha kuanzia mishale hadi risasi; na kutoka kwenye mizinga hadi mabomu ya Atomic na Haidrogeni. Waislamu walitumia, pamoja na Mtume, teo katika vita ya Khaibar.

Ili mumtishe adui wa Mwenyezi Mungu na adui yenu, na wengineo msiowajua nyinyi, Mwenyezi Mungu anawajua.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewagawanya maadui aina mbili: Aina iliyo dhahir ambayo waislamu waliwajua na aina isiyodhahiri ambayo waislamu hawakuwajua uadui wao; nao ni kila anayetamani uislamu ushindwe, kwa kuhofia utawala wao; yakiwemo mataifa ya jirani; kama vile Fursi na Roma ambao baadae walishindwa na waislamu ulipopata nguvu.

NGUVU ZA KUJILINDA NA NGUVU ZA UCHOKOZI

Hebu tusimame kidogo kwenye kauli yake Mwenyezi Mungu mtukufu: “Ili mumtishe adui wa Mwenyezi Mungu na adui yenu.” Kwa sababu ina- fungamana na msingi wa kuilinda jamii ya binadamu kutoka na vurugu, na kuwazuia mataghuti kuchezea maisha ya binadamu na kuwakandamiza.

Msingi huu ni kupatikana nguvu, kwa watu wa haki na uadilifu, itakayoweza kuwazuia madhalimu na wavunjaji na kuwafanya wawe chini ya hukumu na sharia ya Mwenyezi Mungu inayowataka watu wote waishi kulingana na kanuni ya maisha na desturi yake, wala asikengeuke yeyote. Akitamani tu kupotoka basi nguvu hiyo imzime na kumrudisha kwenye desturi hiyo.

Lau mabingwa na wenye akili watafanya utafiti wa sababu ya matatizo ya maisha na maangamivu ni kudhoofisha nguvu ya kukinga maovu na kuipa ubabe nguvu ya uchokozi.

Mfano mzuri wa hilo ni ni nguvu wanazomiliki Marekani na kuzitumia katika uporaji na unyang’anyi bila ya pingamizi wala kizuizi, isipokuwa kutapatapa kwa wananchi wasiokuwa na silaha.

Anasema Nicholas Sparekman “Sisi Wamerekani tunaweza kutekeleza matakwa yetu na kuyalazimisha kwa wale wasiokuwa na nguvu kwa njia yoyote ile, ikiwemo kutumia nguvu; kama vile vita vya kubomoa”

Vile vile Leon Walsh anasema katika kitabu chake American strategic in world politics (Mbinu za Marekani katika siasa za ulimwengu)

“Wajibu wetu ni kutekeleza maongozi yetu ya sawa kwa nguvu duniani, kisiasa kiuchumi na kijamii. Na hilo sio jambo lenye muda maalum tu bali ni lazima kuendele haifai kuliacha.”

Hakuna siri ya kujifaharisha huku kwa maadui wa Mwenyezi Mungu na kudhihirisha uchokozi kwa waja wa Mwenyezi Mungu bila ya kujali, isipokuwa kutohofia nguvu yoyote ya kujikinga ambayo italiinua neno la Mwenyezi Mungu na kuiweka chini batili.

Viongozi wa Marekani wametekeleza yaliyoandikwa katika Kitab hicho na kukichikulia kama ni Injil yao takatifu badala ya Kitab cha Mwenyezi Mungu.

Wametekeleza njia zote za nguvu na za kuumiza, ikiwa ni pamoja na vita vyenye kuangamiza ili watekeleze matakwa yao kwa wale wasiokuwa na nguvu; wakatupa makombora ya kuunguza kwa watoto, vikongwe na waja wazito na wakatupa mabomu ya sumu kwenye nyenzo za riziki na uhai, wakiwemo wanyama na mimea ili waliobaki wafe kwa njaa.

Ni kwa lengo hilo ndipo Marekani ikaanzisha ngome za mauti katika ardhi yake, wakaanzisha humo uchunguzi wa kutafuta mikrobu kali zitakazoma- liza maisha ya binadamu, wanyama na mimea, na kwa ajili ya kutafuta gesi inayoondoa akili na kulemaza mishipa.

Kuna ajabu gani baada ya hayo yote kwa Marekani kuanzisha ngome ya mauti na kuweka silaha za kuharibu katika ardhi ya Palestina na kuipa jina la taifa la Israil? Hapana ajabu! Isipokuwa ajabu ni kwa madola, yakiwemo mataifa madogo yaliyo dhaifu, kuitambua ngome hii iliyosimamishwa kwa msingi ya uadui kwa binadamu wote, na kuwa na mwakilishi anyeitetea na kuangalia masihi yake katika Umoja wa Mataifa.

Pamoja na yote hayo, sisi hatukati tamaa kabisa kuwa iko siku haki itashin- da na batili itashindwa, Hicho kilio dhidi ya wachokozi kinasikika kila mahali ulimwenguni; hata katika Amerika. Huyu hapa mwananchi wa Vietnam ameiangamiza haiba ya Wamerekani, na kuua maelfu ya wanajeshi wao na kuwalazimisha kupoteza mabilioni ya dola zao[1] .

Na chochote mtakachotoa katika njia ya Mwenyezi Mungu; mtarudishiwa, wala nyinyi hamtadhulumiwa.

Hii ni kuhimiza kutoa mali ambayo hapana budi kuitoa ili kuandaa nguvu na kujikinga. Yametangulia malezo katika Juz.2 (2:196) na mwanzo wa Juz.4 (3:92)

Na kama wakielekea kwenye amani, nawe ielekee, na mtegemee Mwenyezi Mungu. Hakika yeye ni mwenye kujua.

Amani ni ya ujumla, ikiwa ni pamoja na kusimamisha vita na suluhu, kutoa kodi na kusilimu. Kauli yake Mwenyezi Mungu mtukufu kumwambia Mtume wake ‘nawe ielekee’ ni amri ya lazima ya kumpa amani mwenye kutaka amani, vyovyote atakavyokuwa, ila kukiwa na dalili mkato kuwa amani yake ni vitimbi na maandalizi ya uvamizi na kuvunja mkataba.

Ni lazima ifahamike kuwa makusudio ya amani katika Aya hii ni amani ya wote, mwenye kupigana na asiyepigana. Wala sio amani ya pande zinazozana tu; kama vile kuishi kwa amani baina ya Urusi na Marekani ambako nyuma yake kuna mipango ya njama na mapinduzi katika mataifa yasiyofungamana na upande wowote, na kupinga ukombozi katika Asia,

Afrika na Latin Amerika, ili wazidishe faida katika mashirika yao ya kilanguzi kupitia damu ya wazalendo, chakula chao na mustakbali wao.

Utauliza : Mwenyezi Mungu (s.w.t) katika Aya anasema: ‘Wakielekea kwenye amani nawe ielekee, na katika Aya nyingine anasema:

فَلَا تَهِنُوا وَتَدْعُوا إِلَى السَّلْمِ وَأَنتُمُ الْأَعْلَوْنَ وَاللَّـهُ مَعَكُمْ ﴿٣٥﴾

“Basi msilegee na kutaka amani na hali nyinyi mko juu, na Mwenyezi Mungu yu pamoja nanyi” (47:35)

Je, kuna wajihi gani wa kujumuisha Aya hizi mbili?

Jibu : Hakuna kupingana baina ya Aya hizi. Aya ya kwanza inawaamrisha waislamu kumpa amani mwenyewe kutoa amani na Aya ya pili inawataka wawe na moyo wa kupigana wakazane na wasilegee wakamkimbia adui. Hilo linatiliwa nguvu na kauli yake Mwenyezi Mungu: ‘Mwenyezi Mungu yu pamoja nanyi’.

Kwa hiyo Aya hii: “Basi msilegee” ni sawa na Aya isemayo:

وَلَا تَهِنُوا فِي ابْتِغَاءِ الْقَوْمِ إِن تَكُونُوا تَأْلَمُونَ فَإِنَّهُمْ يَأْلَمُونَ كَمَا تَأْلَمُونَ وَتَرْجُونَ مِنَ اللَّـهِ مَا لَا يَرْجُونَ ﴿١٠٤﴾

“Wala msilegee katika kuwafuatia hao watu, ikiwa mnaumia basi na wao wanaumia kama mnavyoumia nyinyi. Na nyinyi mwataraji kwa Mwenyezi Mungu ambayo wao hawayataraji”

Juz.5 (4:104)

Na kama wakitaka kukuhadaa, basi Mwenyezi Mungu atakutoshelezea. Yeye ndye aliyekupa nguvu kwa msaada wake na kwa waumini.

Mtume anaambiawa kuhusu hao walioelekea kwenye amani; kuwa kama wanakupangia njama za uhaini nyuma ya mwelekeo wao wa amani, basi usiogope njama zao. Wewe uko katika amani ya Mwenyezi Mungu na atakutosheleza na shari yao naye amekupa nguvu kwa msaada wake na kwa waumini.

Utauliza : Punde tu, yamepita maelezo ya kauli yake Mwenyezi Mungu akimwamrisha Mtume wake kuvunja mapatano ikiwa anahofia kwao hiyana na hadaa. Na katika Aya hii anamwamrisha kuwakubalia wakitaka amani bali hata kama wanataka kufanya hiyana, Je, kuna wajihi gani?

Jibu : Kule Mwenyezi Mungu, alimwamrisha kuvunja mapatano akiwa na yakini na kujua hiyana zao, kwa kumdhihirikia alama. Na, hapa ameamrishwa kuwapa amani hata kama wanakusudia hiyana, ikiwa hakuna dalili mkato za njama zao isipokuwa uwezekano tu wa hilo. Katika hali hii Mtume atachukulia dhahiri na kuamiliana nao kulingana na dhahiri. Kwani dhahiri ni ya watu na batini ni ya Mwenyezi Mungu.

Na akaziunganisha nyoyo zao; lau ungelitoa yote yaliyomo ardhini usingeliweza kuiunganisha mioyo yao, lakini Mwenyezi Mungu amewaunganisha, Hakika yeye ndiye mwenye nguvu mwenye hekima.

Hakuna mwenye shaka kwamba Mwenyezi Mungu ndiye aliyeunganisha nyoyo za masahaba baada ya kuwa na uhasama uliozoeleka; hasa baina ya Ausi na Khazraj ambao uliendelea kiasi cha miaka 120.

Vile vile hakuna mwenye shaka kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t) hupitisha mambo kulingana na desturi, kanuni, sababu na visababishi vyake. Sababu ya kuunganisha nyoyo za masahaba wa Mtume Muhammad ni Uislamu na imani yao kinadharia na kimatendo. Na, Uislamu unatoka kwa Mwenyezi Mungu, kwa hiyo imesihi kunasibishiwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Tumesema katika kufasiri Aya ya pili ya Sura hii kwamba dini haioteshi ngano isipokuwa inaotesha penzi na ikhlasi. Mfano wa Aya hii, tunayoifasiri, ni kama Juz.4 (3:103). Huko utakuta tafsiri yake kwa ufafanuzi.


3

4

5

6

7

8

9

10