TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI Juzuu 10

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI0%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI

Mwandishi: Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 9828
Pakua: 1214

Maelezo zaidi:

Juzuu 10
Juzuu 1
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 13 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 9828 / Pakua: 1214
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI Juzuu 10

Mwandishi:
Swahili

5

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI

أَمْ حَسِبْتُمْ أَن تُتْرَكُوا وَلَمَّا يَعْلَمِ اللَّـهُ الَّذِينَ جَاهَدُوا مِنكُمْ وَلَمْ يَتَّخِذُوا مِن دُونِ اللَّـهِ وَلَا رَسُولِهِ وَلَا الْمُؤْمِنِينَ وَلِيجَةً وَاللَّـهُ خَبِيرٌ بِمَا تَعْمَلُونَ ﴿١٦﴾

16. Je, mnadhani kuwa mtaachwa na hali Mwenyezi Mungu hajawabainisha wale wanaopigana jihadi miongoni mwenu, na hawakumfanya mwandani asiyekuwa Mwenyezi Mungu na Mtume wake na waumin? Na Mwenyezi Mungu ana habari za mnayoyafanya.

مَا كَانَ لِلْمُشْرِكِينَ أَن يَعْمُرُوا مَسَاجِدَ اللَّـهِ شَاهِدِينَ عَلَىٰ أَنفُسِهِم بِالْكُفْرِ أُولَـٰئِكَ حَبِطَتْ أَعْمَالُهُمْ وَفِي النَّارِ هُمْ خَالِدُونَ ﴿١٧﴾

17. Haiwi kwa washirikina kuamirisha Misikiti ya Mwenyezi Mungu, hali wanajishuhudia wenyewe ukafiri, Hao vitendo vyao vimeporomoka, Nawatadumu katika moto.

إِنَّمَا يَعْمُرُ مَسَاجِدَ اللَّـهِ مَنْ آمَنَ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ وَأَقَامَ الصَّلَاةَ وَآتَى الزَّكَاةَ وَلَمْ يَخْشَ إِلَّا اللَّـهَ فَعَسَىٰ أُولَـٰئِكَ أَن يَكُونُوا مِنَ الْمُهْتَدِينَ ﴿١٨﴾

18. Wanaoamirisha misikiti ya Mwenyezi Mungu ni wale tu wanaomwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho na wakasimamisha swala na wakatoa zaka na wasiogope ila Mwenyezi Mungu, Basi hao huenda wakawa miongoni mwa waliongoka.

MNADHANI MTAACHWA

Aya 16-18

MAANA

Je, mnadhani kuwa mtaachwa na hali Mwenyezi Mungu hajawabain- isha wale wanaopigana jihadi miongoni mwenu.

Imetangulia tafsir yake katika Juz.4 (3:142)

Na hawakumfanya mwandani asiyekuwa Mwenyezi Mungu na Mtume wake na waumin?

Utiifu bora zaidi kwa Mwenyezi Mungu ni kuwapiga vita wabatilifu- maadui wa haki na ubinadamu. Ndipo akadokeza Mwenyezi Mungu: ‘Na hali hajawabainisha wale wanaopigana jihadi miongoni mwenu.”

Na maasi makubwa zaidi ni kuwapondokea, hapo akaeleza Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwa kusema: “Na hawakumfanya mwandani”

Kila mwenye kuwategemea watu wa dhulma na uadui na kuyaunganisha maslahi yake na yao, basi yeye ni adui wa Mwenyezi Mungu na Mtume wake na waumin. Ni juu ya kila mwenye ikhlas kumtangaza na kufichua njama zake ili watu wamtofautishe yeye na mwaminifu na kumweka kila moja anapostahiki.

Na Mwenyezi Mungu ana habari za mnayoyafanya

Ndio yeye ni mjuzi mwenye habari, lakini hamwadhibu yeyote kwa anay- oyajua kwake, bali hata kwa yanayofichuka katika vitendo vyake na tabia zake.

Haiwi kwa washirikina kuamirisha misikiti ya Mwenyezi Mungu.

Katika vitabu vya lugha husemwa, Nyumba imaamirika kwa wakazi wake, yaani wamekuwa wakazi humo au fulani amemuamirisha Mola wake, yaani amemwabudu. Ikaenea midomoni mwa watu Misikiti inaamirishwa kwa kutajwa Mwenyezi Mungu. Kuna Hadith isemayo: “Mwenyezi Mungu anasema: Majumba yangu katika ardhi ni misikiti, na wanaonizuru humo ndio wanaoiiamirisha.”

Hayo ndiyo maana yanayochukuliwa katika kauli yake Mwenyezi Mungu kuamirisha misikiti, Yaani washirikina wasiingie na kufanya ibada zao za mizimu, kama walivyokuwa wakifanya siku za jahiliya. Ni bora pia wasiwe na usimamizi. Maana hiyo yanatiwa nguvu zaidi na kauli yake Mwenyezi Mungu:

Hali wanajishuhudia wenyewe ukafiri.

Kwa sababu kuabudu kwao masanamu na kuwaomba Lata na Uzza ni ushahidi wao juu yao wenyewe kwamba wao wanamkufuru Mwenyezi Mungu, Na mwenye kumkufuru hastahiki kuingia majumba ya Mwenyezi Mungu.

Hao vitendo vyao vimeporomoka.

Kwa sababu Mwenyezi Mungu haikubali amali pamoja na shirk.

Na katika moto watadumu.

Kwa sababu shirk imeangusha vitendo vyao vyote, hata vilivyokuwa vizuri.

Wanaoamirisha misikiti ya Mwenyezi Mungu ni wale tu wanaomwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho na wakasimamisha swala na wakatoa zaka na wasiogope ila Mwenyezi Mungu.

Yaani haijuzu kwa yeyote kuingia msikitini na kufanya ibada humo au kusimamia jambo lake lolote ila zikikusanyika humo sifa hizo. Kumwamini Mungu na Siku ya mwisho, na kuwa na nembo za dini ambazo muhimu zaidi ni kuswali na kutoa zaka na kumhofia Mwenyezi Mungu, yaani kumfanyia ikhlas katika kauli na vitendo.

Basi hao huenda wakawa miongoni mwa waliongoka kwenye haki na kuitumia.

Neno huenda kutoka kwa Mwenyezi Mungu, linamaanisha yakini kwa sababu shaka ni mahali kwake.

أَجَعَلْتُمْ سِقَايَةَ الْحَاجِّ وَعِمَارَةَ الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ كَمَنْ آمَنَ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ وَجَاهَدَ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ لَا يَسْتَوُونَ عِندَ اللَّـهِ وَاللَّـهُ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الظَّالِمِينَ ﴿١٩﴾

19. Je, mnafanya kuwanywesha mahujaji na kuamirisha msikiti mtukufu ni sawa na yule aliyemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho na akapigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu? Hawawi sawa mbele ya Mwenyezi Mungu Na Mwenyezi Mungu hawaongozi watu madhalimu.

الَّذِينَ آمَنُوا وَهَاجَرُوا وَجَاهَدُوا فِي سَبِيلِ اللَّـهِ بِأَمْوَالِهِمْ وَأَنفُسِهِمْ أَعْظَمُ دَرَجَةً عِندَ اللَّـهِ وَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْفَائِزُونَ ﴿٢٠﴾

20. Wale walioamini na wakahama na wakapigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu, kwa mali zao na nafsi zao, wana cheo kikukbwa mbele ya Mwenyezi Mungu, na hao ndio wenye kufuzu.

يُبَشِّرُهُمْ رَبُّهُم بِرَحْمَةٍ مِّنْهُ وَرِضْوَانٍ وَجَنَّاتٍ لَّهُمْ فِيهَا نَعِيمٌ مُّقِيمٌ ﴿٢١﴾

21. Mola wao anawabashiria rehema kutoka kwake na radhi na pepo ambazo watapata humo neema zitakazodumu.

خَالِدِينَ فِيهَا أَبَدًا إِنَّ اللَّـهَ عِندَهُ أَجْرٌ عَظِيمٌ ﴿٢٢﴾

22. Watadumu humo milele, Hakika kwa Mwenyezi Mungu kuna malipo makubwa.

KUWANYWESHA MAHUJAJI

Aya 19-22

MAANA

Je, mnafanya kuwanywesha mahujaji na kuamirisha msikiti mtukufu ni sawa na yule aliyemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho na akapigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu?

Makusudio ya kunywesha mahujaji ni kuwapa watu maji ya kunywa katika Hijja na kuamirisha msikiti hapa ni kuuhudumia.

Tafsir nyingi, ikiwemo tafsir ya Tabari, Razi, Naisaburi na Suyuti, imeelezwa kuwa Abbas bin Abdul Muttalib alikuwa akiwanywesha maji watu katika Hijja, na Twalha bin Shayba kutoka ukoo wa Abduddar alikuwa na funguo za Al-Kaaba. Twalha akasema mimi ndio mwenye Al-Kaaba, nina funguo zake. Abbas naye akasema mimi ndio mwenye kunywesha, Ali Bin Abutalib akasema.

Sijui mnasema nini? Mimi nimeswali kibla miezi sita kabla ya watu wengine na mimi ni mwenye jihadi ndipo, Mwenyezi Mungu akateremsha Aya hiyo.

Kwa hiyo Ali ndio makusudio ya ‘yule aliyemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho na akafanya jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu’

Hiki ndicho kipimo cha ubora mbele ya Mwenyezi Mungu - imani na kupigana jihadi katika njia yake. Ama wadhifa na vyeo mara nyingi humwongoza mtu kwenye ufisadi na maangamizi.

Hawawi sawa mbele ya Mwenyezi Mungu katika malipo na thawabu, Na Mwenyezi Mungu hawaongozi watu madhalimu.

Baada ya kuwalingania kwenye uongofu na kukataa kwa chaguo lao ovu.

Wale walioamini na wakahama na wakapigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu, kwa mali zao na nafsi zao, wana cheo kikukbwa mbele ya Mwenyezi Mungu, na hao ndio wenye kufuzu.

Wapi na wapi kunywesheleza mahujaji na kutumikia miskiti kulinganisha na imani, Hijra na Jihadi?

Umekwishapita mfano wa Aya hii katika Juzuu hii Sura (8:72). Neno cheo kikubwa hapa halina maana ya kuzidiana, isipokuwa ni kuthibitisha ubora wa waumini tu, kwani makafiri hawana cheo hata kile kidogo mbele ya Mwenyezi Mungu.

Mola wao anawabashiria rehema kutoka kwake na radhi na pepo ambazo watapata humo neema zitakazodumu, Watadumu humo milele. Hakika kwa Mwenyezi Mungu kuna malipo makubwa.

Anasema mwenye Bahrul-Muhit: “Waumin wamesifika na sifa tatu: Imani, Hijra na Jihad. Kwa hiyo Mwenyezi Mungu akawakabili na matatu Rehema, Radhi na Pepo”

Razi amerefusha maneno katika kubainisha tofauti ya sifa hizi, Ama sisi tunaona kuwa sifa hizo pamoja na kufuzu na malipo ni kwa maana moja kwamba waumin wenye kufanya amali wako katika hifadhi ya Mwenyezi Mungu. Na neno ‘Radhi ya Mwenyezi Mungu’ lingetoshelezea yote, kwa sababu Mwenyezi Mungu anasema:

وَرِضْوَانٌ مِّنَ اللَّـهِ أَكْبَرُ ﴿٧٢﴾

“Na radhi za Mwenyezi Mungu ndizo kubwa zaidi” (9:72)

Lakini Mwenyezi Mungu na Mtume wake(s.a.w.w) alitaka kuwatukuza na kuwahimiza waja wake kwenye Imani na Matendo mema.

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَتَّخِذُوا آبَاءَكُمْ وَإِخْوَانَكُمْ أَوْلِيَاءَ إِنِ اسْتَحَبُّوا الْكُفْرَ عَلَى الْإِيمَانِ وَمَن يَتَوَلَّهُم مِّنكُمْ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ ﴿٢٣﴾

23. Enyi mlioamini! Msiwafanye baba zenu na ndugu zenu kuwa mawalii ikiwa wamestahabu kufuru kuliko imani, Na atakayewafanya mawalii katika nyinyi basi hao ndio madhalimu.

قُلْ إِن كَانَ آبَاؤُكُمْ وَأَبْنَاؤُكُمْ وَإِخْوَانُكُمْ وَأَزْوَاجُكُمْ وَعَشِيرَتُكُمْ وَأَمْوَالٌ اقْتَرَفْتُمُوهَا وَتِجَارَةٌ تَخْشَوْنَ كَسَادَهَا وَمَسَاكِنُ تَرْضَوْنَهَا أَحَبَّ إِلَيْكُم مِّنَ اللَّـهِ وَرَسُولِهِ وَجِهَادٍ فِي سَبِيلِهِ فَتَرَبَّصُوا حَتَّىٰ يَأْتِيَ اللَّـهُ بِأَمْرِهِ وَاللَّـهُ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الْفَاسِقِينَ ﴿٢٤﴾

24. Sema ikiwa baba zenu na wana wenu na ndugu zenu na wake zenu na jamaa zenu na mali mlizozichuma na biashara mnazohofia kuharibikiwa, na majumba mnayopenda, ni vipenzi zaidi kwenu kuliko Mwenyezi Mungu na Mtume wake na jihadi katika njia yake, basi ngojeni mpaka Mwenyezi Mungu alete amri yake, na Mwenyezi Mungu hawaongozi watu mafasiki.

MSIWAFANYE BABA ZENU NA NDUGU ZENU MAWALII

Aya 23-24

MAANA

Enyi mlioamini! Msiwafanye baba zenu na ndugu zenu kuwa mawalii ikiwa wamestahabu kufuru kuliko imani.

Makusudio ya uwalii hapa ni kusaidia. Uislamu unaamrisha kutokata udugu, ukazingatia kuwa kuwaudhi wazazi ni katika madhambi makubwa, ukausia ujirani, kutekeleza haki ya urafiki na mikataba na ahadi zote.

Vilevile waislamu wamehalalishiwa kuwafanyia wema na uadilifu washirikina na yote hayo yanajuzu, lakini kwa sharti la kutoharamisha halali au kuhalalisha haramu.

Kwa mfano baba akiwa upande wa batili, haijuzu kwa mtoto kumsaidia, bali ni juu ya mtoto kumzuia na kumkataza akiweza.

Kwa hiyo kauli yake Mwenyezi Mungu ‘ikiwa wamestahabu kufuru kuliko imani,’ inakusanya maasia yote, Ikiwa baba yako au ndugu yako ni Mwislamu na akamdhulumu mwingine, basi ni juu yako kumsaidia aliyedhulumiwa dhidi ya huyo baba yako au ndugu yako.

Na atakayewafanya mawili katika nyinyi basi hao ndio madhalimu.

Kuna Hadith isemayo “Mwenye kufanya dhuluma na mwenye kuisaidia na mwenye kuiridhia ni mshiriki” Kwa maneno mengine ni kuwa haki iko juu ya ndugu na urafiki.

Sema: ikiwa baba zenu na wana wenu na ndugu zenu na wake zenu na jamaa zenu na mali mlizozichuma na biashara mnazohofia kuharibikiwa, na majumba mnayopenda, ni vipenzi zaidi kwenu kuliko Mwenyezi Mungu na Mtume wake na jihadi katika njia yake, basi ngojeni mpaka Mwenyezi Mungu alete amri yake, na Mwenyezi Mungu hawaongozi watu mafasiki.

Inasemekana kuwa Aya hii ilishuka kwa ajili ya tukio maalum. Inawezekana kuwa ni kweli, lakini tamko lake ni la ujumla, pia hukumu yake.

Aya hii inawaelezea mumin kwa maelezo wazi na ya uhakika. Mwenye kuathirika na haki kuliko maslahi yake binafsi wakati yana-pogongana na haki basi huyo ni mumin mwema, vinginevyo basi ni mnafiki mwovu.

Hiyo ndiyo njia inayomtofautisha mumin na asiyekuwa mumin, kama ilivyoelezewa na Aya. Kutajwa ndugu mali na majumba ni mfano tu wa kuweka mbele manufaa kuliko haki ambayo Mwenyezi Mungu ameitolea ibara ya kumpenda Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Zaidi ya hayo yako manufaa mengine; kama vile kupupia maisha, kupenda jaha, utawala n.k.

Mtu kwa maumbile yake hujipenda na kupenda watu wake na mali yake, na dini haikatai hilo, wala haimzuii yeyote kustarehe atakavyo na kumpenda amtakaye, mradi tu amwogope Mwenyezi Mungu katika starehe hiyo, na yote hayo yamekutana na juhudi yake sio juhudi za wengine.

Imepokewa kutoka kwa Bukhari kwamba Umar Bin Al-Khattab alimwambia Mtume(s.a.w.w) . Kwa hakika wewe unapendeza kwangu kuliko chochote isipokuwa nafsi yangu iliyo mbavuni mwangu”

Mtume(s.a.w.w) akamwambia: Hapana! Naapa kwa yule ambaye nafsi yangu iko mikononi mwake, ni mpaka niwe napendeza kwako kuliko nafsi yako iliyo mbavuni mwako”

Wala hakuna maana ya kumpenda Mtume(s.a.w.w) isipokuwa kumtii na kufanya mambo kulingana na sharia yake. Tumeyazungumzia haya katika Juz.5 (4:135)

لَقَدْ نَصَرَكُمُ اللَّـهُ فِي مَوَاطِنَ كَثِيرَةٍ وَيَوْمَ حُنَيْنٍ إِذْ أَعْجَبَتْكُمْ كَثْرَتُكُمْ فَلَمْ تُغْنِ عَنكُمْ شَيْئًا وَضَاقَتْ عَلَيْكُمُ الْأَرْضُ بِمَا رَحُبَتْ ثُمَّ وَلَّيْتُم مُّدْبِرِينَ ﴿٢٥﴾

25. Hakika Mwenyezi Mungu amewasaidia katika mwahala mwingi, kama vile na siku ya Hunain ulipowafuraisha wingi wenu. Lakini haukuwafaa chochote, na ardhi ikawa finyu juu yenu ingawa ilikuwa pana, kisha mkageuka mkirudi nyuma.

ثُمَّ أَنزَلَ اللَّـهُ سَكِينَتَهُ عَلَىٰ رَسُولِهِ وَعَلَى الْمُؤْمِنِينَ وَأَنزَلَ جُنُودًا لَّمْ تَرَوْهَا وَعَذَّبَ الَّذِينَ كَفَرُوا وَذَٰلِكَ جَزَاءُ الْكَافِرِينَ ﴿٢٦﴾

26. Kisha Mwenyezi Mungu akateremsha utulivu wake juu ya Mtume wake na juu ya waumin, Na akawateremshia majeshi ambayo hamkuyaona. Na akawaadhibu wale waliokufuru, Na hayo ndiyo malipo ya makafiri

ثُمَّ يَتُوبُ اللَّـهُ مِن بَعْدِ ذَٰلِكَ عَلَىٰ مَن يَشَاءُ وَاللَّـهُ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿٢٧﴾

27. Kisha baada ya haya Mwenyezi Mungu atamkubalia toba amtakaye, Na Mwenyezi Mungu ni mwingi wa maghufira mwenye kurehemu.

MWENYEZI MUNGU AMEWANUSURU

Aya 25-27

KISA CHA HUNAIN

Hunain ni bonde lilioko baina ya Makka na Taif, Vita vilvyopiganwa hapo vinaitwa vita vya Hunain, vita vya Autas au vita vya Hawazin. Vita hivyo vilikuwa mwezi wa Shawwal (mfunguo mosi) mwaka wa nane Hijra.

Mtume(s.a.w.w) alipoiteka Makka walimlia njama Hawazin na Thaqif wakakusanya maelfu kumpiga vita Mtume. Ilipomfikia Mtume(s.a.w.w) habari hiyo, alijiandaa na kukusanya jeshi la watu elfu 12, Elfu kumi kati yao ni Maswahaba wake aliotoka nao Makka na elfu mbili walikuwa ni Tulaqau[5] akiwemo Abu Safyan na mwanawe Muawiya.

Mtume(s.a.w.w) akaelekea kwa Hawazin njia yake ilipitia bonde la Hunain na ilikuwa nyembamba yenye maporomoko. Jeshi la adui lilikuwa limewatangulia kufika kwenye uchochoro wake wakajificha.

Mara tu jeshi la Waislamu lilipofika katikati ya bonde, maadui waliwamiminia mishale, watu wakaanza kusambaratika na Abu Sufyan ndiye wa mwanzo wao.

Sheikh Ghazali katika kitabu Fiqh Sera, Anasema: “Wengine walirudia ukafiri wao. Abu Sufyan akasema: ‘Kushindwa kwao hakutakoma mpaka baharini.’ Hilo si ajabu kwani mburuga alizokuwa akiagulia wakati wa Jahilia bado ziko mkobani mwake”.

Ali akabaki na Mtume wa Mwenyezi Mungu akiwa ameuchomoa upanga wake, huku Abbas ameshika lijamu ya farasi wake, Al-fadhl bin Abbas akiwa kuumeni kwa Mtume pamoja na Mughira Bin Harith Bin Abdul Muttalib, Zaid Bin Usama na Aiman Bin Ummu Aiman. Wakapigana mbele ya mtume wa Mwenyezi Mungu.

Washirikina walipoona waislam wanasamabaratika, walitoka kwenye ngome za bonde wakimfuatia Mtume wa Mwenyezi Mungu. Mtume(s.a.w.w) akamwambia Ami yake Abbas aliyekuwa na sauti kubwa. Waite watu na uwakumbushe ahadi.

Akanadi kwa sauti kubwa: “Enyi watu wa Baia ya mti! (Mliombai mtume chini ya mti) Enyi watu wa Sura ya Baqara! Mnakwenda wapi? Kumbukeni ahadi mliyomwahidi Mtume wa Mwenyezi Mungu. Ansar waliposikia mwito wa Abbas walirudi na wakavunja ala za panga zao wakiwa wanasema: Labeka! Labeka! Wakamkabili adui na makundi mawili yakapambana vikali

Mshika bendera na shujaa wa washirikina alikuwa ni Abu Jarwal. Huyu alikuwa akiwashambulia waislamu na kuwaua. Ali Bin Abu Talib akapambana naye na kumuua. kwa kuliwa kwake jeshi la washirikina lilitawanyika na ushindi wa Mtume(s.a.w.w) na wa waumin ukapatikana.

Tulaqau walipojua kuwa waislamu wameshinda na kuna ngawira nyingi, walirudi kwa Mtume(s.a.w.w) , Katika Tafsir Bahrul-Muhit imeelezwa kuwa Tulaqau walikimbia wakikusudia waumin washindwe”.

Sharqawi naye anasema katika kitabu Muhammad Rasulul-Huriyya (Muhammad Mtume wa uhuru): “Maquraish elfu mbili wakiongozwa na Abu Suffin walisilimu kwa hofu au tamaa. Walikuja hiyo siku si kwa ajili ya kuusaidia Uislamu bali ni kwa ajili ya kuudhalilisha na kueneza ulegevu kwa wapiganaji jihadi waliowatangulia”.

Hivi ndivyo walivyo wanafiki na watu walio huku na kule. Wanajifanya ni wenye ikhlas, wanajiingiza katika safu za wapigania ukombozi na kupanga mambo. Wakichunguza mbinu zao, kisha wanapanga njama, zikifaulu njama zao, inakuwa wamepata waliyoyataka, au wakifaulu wakombozi, basi husema sisi na nyinyi tuko pamoja, Yametangulia maelezo ya hawa katika kufasiri Juz. 5 (4:141)

Hakika Mwenyezi Mungu amewasaidia katika mwahala mwingi.

Kama vile vita vya Badr, Quraidha, Nadhr, Hudaibiya, Khaibar na kuiteka Makka.

Na siku ya Hunain ulipowafurisha wingi wenu.

Razi anasema, “Mtu moja katika waislam alisema, Hatutashindwa kwa uchache leo. Akaona vibaya Mtume wa Mwenyezi Mungu. Inasemekana kuwa aliyesema hayo ni Mtume(s.a.w.w) na ilisemakana ni Abu Bakr. Kutegemeza neno hili kwa Mtume ni mbali”

Lakini haukuwafaa chochote, na ardhi ikawa finyu juu yenu ingawa ilikuwa pana, kisha mkageuka mkirudi nyuma.

Kuanzia kufura kichwa hadi kulemewa kabisa kiasi cha kutopata hata upenyo wa kujiokoa na adui yao. Huu ndio mwisho wa kila mwenye kujigamba na kumdharau adui yake.

Kisha Mwenyezi Mungu akateremsha utulivu wake juu ya Mtume wake na juu ya waumin.

Utulivu ni kuwa na mategemeo na umakini. Maana ya kuuteremsha kwa Mtume(s.a.w.w) ni kubakia kwake mwenye kuthibiti katikati ya vita akiwa makini na mwenye ushupavu akipangilia mambo, ingawaje wanajeshi wake, waliokuwa kiasi cha watu elfu kumi na mbili, wamekimbia wote, isipokuwa watu wasiozidi kumi, na huku jeshi la maadui likiwa na idadi ya maelfu.

Wapokezi wanasema Mtume(s.a.w.w) alikuwa akimchochea nyumbu wake kuwaelekea maadui huku akiwalingania wale waliokimbia. Njooni enyi waja wa Mwenyezi Mungu! Mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, mimi ni Mtume sisemi uwongo mimi ni mwana wa Abdul-Muttalib.

Waumin ambao Mwenyezi Mungu aliwateremshia utulivu ndio wale waliothibiti bila ya kumkimbia, na wale waliorudi baada ya kushindwa na kuitikia mwito wa Mtume(s.a.w.w) wakiwa wenye ikhlas. Maana ya kuteremshiwa utulivu ni kuwa na utulivu katika nyoyo zao na kuwaondokea hofu.

Na akawateremshia majeshi ambayo hamkuyaona.

Razi anasema: “Hakuna tofauti kwamba makusudio ni kuteremshwa Malaika”. Ama sisi tunaitakidi kwamba Mwenyezi Mungu ana jeshi la Malaika na lisilokuwa Malaika kwa aina isiyokuwa na idadi. Miongoni mwa aina hizo ni nguvu ya nafsi na silika yake na nguvu za nje, Aya haikubainisha aina hii ya jeshi aliloteremsha Mwenyezi Mungu siku ya Hunain. Kwa hiyo ujuzi wake tunamwachia Mwenyezi Mungu aliyesema:

وَمَا يَعْلَمُ جُنُودَ رَبِّكَ إِلَّا هُوَ ﴿٣١﴾

“Na hakuna ajuaye majeshi ya Mola wako ila yeye tu” (74:31)

Na akawaadhibu wale waliokufuru.

Aliwaadhibu duniani kwa kuuliwa kutekwa, kushindwa na kuchukuliwa mali na atawaadhibu Akhera kwa moto wa Jahannam na ni marejeo mabaya.

Kisha baada ya haya Mwenyezi Mungu atamkubalia toba amtakaye, Na Mwenyezi Mungu ni mwingi wa maghufira mwenye kurehemu.

Mwenyezi Mungu ni mkarimu, hashindwi kusamehe dhambi kubwa, na mlango wake uko wazi kwa kila mwenye kubisha. Aliyekimbia Mtume wa Mwenyezi Mungu katika waislamu, kisha akatubia basi Mwenyezi Mungu anawapenda wanaotubia. Na mwenye kukufuru na akampiga vita Mwenyezi Mungu na Mtume wake(s.a.w.w) kisha akatubia na akaamini na akafanya amali njema basi yeye ni katika waliofaulu.

Wanahistoria wanasema baada ya kwisha vita na ngawira kugawanywa ulikuja ujumbe kutoka Hawazin hali ya kuwa ni waislamu. Wakasema Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu wewe ni bora wa watu na mwema wao, wake zetu na watoto wetu wametawaliwa na mali zetu zimechukuliwa. Basi Mtume(s.a.w.w) akawakubalia Uislamu wao na wakarudishiwa wake na watoto wao.