TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI Juzuu 10

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI0%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI

Mwandishi: Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 9977
Pakua: 1265

Maelezo zaidi:

Juzuu 10
Juzuu 1
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 13 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 9977 / Pakua: 1265
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI Juzuu 10

Mwandishi:
Swahili

7

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI

إِنَّ عِدَّةَ الشُّهُورِ عِندَ اللَّـهِ اثْنَا عَشَرَ شَهْرًا فِي كِتَابِ اللَّـهِ يَوْمَ خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ مِنْهَا أَرْبَعَةٌ حُرُمٌ ذَٰلِكَ الدِّينُ الْقَيِّمُ فَلَا تَظْلِمُوا فِيهِنَّ أَنفُسَكُمْ وَقَاتِلُوا الْمُشْرِكِينَ كَافَّةً كَمَا يُقَاتِلُونَكُمْ كَافَّةً وَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ مَعَ الْمُتَّقِينَ ﴿٣٦﴾

36. Hakika idadi ya miezi kwa Mwenyezi Mungu ni miezi kumi na mbili katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu (tangu) siku alipoumba mbingu na ardhi. Katika hiyo iko mine mitakatifu, Hiyo ndiyo dini iliyo sawa, Basi msidhulumu nafsi zenu humo. Na piganeni na washirikina nyote, kama wanavyopigana nanyi wote, na jueni kuwa Mwenyezi Mungu yuko pamoja na wenye takua.

إِنَّمَا النَّسِيءُ زِيَادَةٌ فِي الْكُفْرِ يُضَلُّ بِهِ الَّذِينَ كَفَرُوا يُحِلُّونَهُ عَامًا وَيُحَرِّمُونَهُ عَامًا لِّيُوَاطِئُوا عِدَّةَ مَا حَرَّمَ اللَّـهُ فَيُحِلُّوا مَا حَرَّمَ اللَّـهُ زُيِّنَ لَهُمْ سُوءُ أَعْمَالِهِمْ وَاللَّـهُ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الْكَافِرِينَ ﴿٣٧﴾

37. Hakika kuahirisha ni kuzidi katika kufru, kwa hayo hupotezwa wale walio kufuru. Wanauhalalisha mwaka mmoja na kuuharamisha mwaka Ili wafanye sawa idadi ya ile aliyoiharamisha Mwenyezi Mungu, hivyo huhalalisha aliyoharamisha Mwenyezi Mungu. Wamepambiwa ubaya wa vitendo vyao, Na Mwenyezi Mungu hawaongozi watu makafiri.

IDADI YA MIEZI

Aya 36 – 37

MIEZI MIANDAMO NDIYO MIEZI YA KIMAUMBILE

MAANA

Hakika idadi ya miezi kwa Mwenyezi Mungu ni miezi kumi na mbili katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu (tangu) siku alipoumba mbingu na ardhi.

Makusudio ya kwa Mwenyezi Mungu na katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu ni kwamba miezi kumi na mbili iko kihakika katika ulimwengu wa kimaumbile, sawa na mbingu na ardhi si katika ulimwengu wa mazingatio na sharia, kama vile halali na haramu.

Makusudio ya siku alipoumba mbingu na ardhi ni kwamba yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu aliumba ulimwengu kwenye hali ambayo idadi ya miezi ni kumi na mbili, tangu siku ya kwanza ya kupatikana mbingu na ardhi; yaani idadi ya miezi hii, sio kwamba imewekwa na binadamu na ugunduzi wake; isipokuwa ni desturi na nidhamu ya maumbile.

Haya ndiyo maana ya Aya, Kimsingi ni kwamba binadamu hupima wakati na kuupanga kwa anavyoona na kuhisi. Tukiangalia maumbile ambayo yatatuongoza katika kujua wakati, hatupati zaidi ya jua na mwezi. Jua kila siku linakwenda kwa mfumo mmoja kutoka mashariki na kutua magharibi, bila ya kuweko tofauti.

Kupitia hilo jua twajua wakati wa asubuhi mchana na jioni, na wala halihusiki na kujua mwezi si kwa karibu wala mbali. Lakini mwezi ni kinyume na hivyo. nHuwa unajitokeza kwa picha maalum kuanzia siku ya kwanza, ya kila mwezi, ambao ndiyo siku ya kwanza ya mwezi, Tunapojua mwezi ndio tunajua mwaka.

Na kwa ajili hii ndipo ikawa miezi miandamano, ndiyo miezi inayo kwenda na maumbile, kinyume cha miezi mingine, na kwa ajili hii ndio Mwenyezi Mungu ameiwekea wakati wa Hijja, Swaumu eda ya watalikiwa na kunyonyesha, kama ambavyo wakati wa swala amuweka kwa jua, kwa vile ndio njia ya kujua mafungu ya siku. Kwa maneno mengine, jua ni la kujua saa na mwezi mwandomo ni wa kujua miezi. Binadamu alikuwa akihisabu muda wake kwa misingi hii.

Anasema Razi: “Desturi ya Waarabu tangu zamani ni kuwa na mwaka wa mwezi na sio wa jua Hukumu hii walirithi kutoka kwa Ibrahim na Ismail”

Katika baadhi ya tafsir imeelezwa kuwa hekima ya kujaaliwa Hijja na Swaumu katika miezi miandamo ni kuwa izunguke katika vipindi vyote vya mwaka; mara inakuwa nzito na mara nyingine inakuwa sahali[8] , Lakini jitihadi hii haitegemei asili yoyote, hata hivyo haina kizuizi kwani haikukusudiwa kuthibitisha hukumu ya sharia, isipokuwa kubainisha masilahi ya hukumu yenye kuthibiti kisharia.

Katika hiyo iko mine mitakatifu.

Mitatu katika miezi mine hii, inafuatana: Dhul-qaada, Dhul-hajj na Muharram[9] , Na mwezi mmoja, Rajab, uko peke. Imeitwa mitakatifu kwa kukatazwa kupigana katika miezi hiyo wakati wa jahiliya na wa Uislamu, Hayo tumeyaeleza zaidi ya mara moja.

Hiyo ndiyo dini iliyo sawa.

Yaani kugawa miezi kwa idadi ya kumi na mbili kwa hisabu ya mwezi mwandamo ndio magawanyo sahihi wala haijuzu kufanya upotofu kwa hawa na matakwa mengine katika miezi hiyo wala katika miezi mitakatifu.

Basi msidhulumu nafsi zenu humo.

Kwa kuhalalisha kupigana katika miezi mitakatifu, au kufanyiana uadui katika wakati wowote, Kila anayemwasi Mwenyezi Mungu katika dhambi kubwa na ndogo, basi ameidhulumu nafsi yake kwa kujiingiza kwenye adhabu ya Mwenyezi Mungu na ghadhabu yake.

Na piganeni na washirikina nyote, kama wanavyopigana nanyi wote.

Hii ndiyo dawa; watu wote jihadi, ni desturi ya Mwenyezi Mungu na huwezi kupata mabadiliko katika desturi ya Mwenyezi Mungu. Ama vikao vya kutatua ugomvi ni kumyenyekea adui na kusalimu amri kwake. Wazayuni wote na wakoloni wamejitokeza kuwapiga waarabu na waislamu wote; wakaweka kambi ya kiadui katika ardhi ya waarabu, na kuipa jina ‘Taifa la Israil’, ili wapitishie mashambulizi yao kutokea hapo!

Hivi tuko katika mwezi Novemba 1968, katika umoja wa mataifa, inaendelea mipango ya kutafuta suluhisho la kudumu kutatua tatizo la mashariki ya kati kwa njia ya mazungumzo ambapo adui anatoa masharti, kila anapopata fursa, ambayo yanamzidisha mori wa uadui na kupata yote ayatakayo, kisha arudie tena mazungumzo. Mambo yatakuwa hivyo hivyo mpaka atawale sehemu zote.

Dawa pekee ya kuondoa mzizi wa fitina ni ile aliyoipanga Mwenyezi Mungu kwa kauli yake:

Na piganeni na washirikina nyote, kama wanavyopigana nanyi wote, na jueni kuwa Mwenyezi Mungu yu pamoja na wenye takua.

Ambao wamejikomboa na chuki na tamaa na kuungana pamoja wote kwa ajili ya kupigana na adui wao na adui wa Mwenyezi Mungu na wa utu.

Hakika kuahirisha ni kuzidi katika kufru, kwa hayo hupotezwa wale walio kufuru. Wanauhalalisha mwaka mmoja na kuuharamisha mwaka mwingine.

Washirikina walikuwa wakiahirisha utukufu wa mwezi, kama vile Muharram, mpaka mwezi mwingine, kama vile Safar.

Ikiwa ni masilahi yao kupigana katika mwezi mtukufu basi hupigana bila ya kujali, lakini wanautukuza mwezi mwingine badala yake, katika miezi ya halali, ili ipatikane miezi mitukufu minne ya mwaka.

Ili wafanye sawa idadi ya ile aliyoiharamisha Mwenyezi Mungu, hivyo huhalalisha aliyoharamisha Mwenyezi Mungu.

Tafsiri wazi zaidi kuhusu hii ni yale yaliyonukuliwa kutoka kwa Ibn Abbas aliposema: “Hakika wao hawakuhalalisha mwezi katika miezi mitakatifu ila huharamisha mahali pake mwezi wa halali. Na hawakuharamisha mwezi katika miezi ya halalali ila huhalalisha mahali pake mwezi mtakatifu. Wanafanya hivyo ili idadi ya miezi mitukufu iwe minne kwa kufuata aliyoyataja Mwenyezi Mungu” Haya ndiyo makusudio ya kufanya sawa.

Wamepambiwa ubaya wa vitendo vyao.

Matamanio na malengo mengine ndiyo yanayompofusha mtu na ubaya wa amali yake. Anaiona shari kuwa ni heri na uzuri kuwa mbaya.

Na Mwenyezi Mungu hawaongozi watu makafiri.

Yaani anawaacha kama walivyo baada ya kukata tamaa na kuongoka kwako. Angalia Juz. 5 (4:88).

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا مَا لَكُمْ إِذَا قِيلَ لَكُمُ انفِرُوا فِي سَبِيلِ اللَّـهِ اثَّاقَلْتُمْ إِلَى الْأَرْضِ أَرَضِيتُم بِالْحَيَاةِ الدُّنْيَا مِنَ الْآخِرَةِ فَمَا مَتَاعُ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا فِي الْآخِرَةِ إِلَّا قَلِيلٌ ﴿٣٨﴾

38. Enyi mlioamnini! Mna nini mnapoambiwa nendeni katika njia ya Mwenyezi Mungu mnajitia uzito katika ardhi?. Je, mmeridhia maisha ya dunia kuliko ya Akhera?. Lakini starehe za maisha ya dunia kulinganisha na Akhera ni kidogo tu.

إِلَّا تَنفِرُوا يُعَذِّبْكُمْ عَذَابًا أَلِيمًا وَيَسْتَبْدِلْ قَوْمًا غَيْرَكُمْ وَلَا تَضُرُّوهُ شَيْئًا وَاللَّـهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿٣٩﴾

39. Kama hamwendi atawaadhibu kwa adhabu iumizayo na atawaleta watu wengine badala yenu, wala hamtamdhuru chochote Na Mwenyezi Mungu ni muweza wa kila kitu.

إِلَّا تَنصُرُوهُ فَقَدْ نَصَرَهُ اللَّـهُ إِذْ أَخْرَجَهُ الَّذِينَ كَفَرُوا ثَانِيَ اثْنَيْنِ إِذْ هُمَا فِي الْغَارِ إِذْ يَقُولُ لِصَاحِبِهِ لَا تَحْزَنْ إِنَّ اللَّـهَ مَعَنَا فَأَنزَلَ اللَّـهُ سَكِينَتَهُ عَلَيْهِ وَأَيَّدَهُ بِجُنُودٍ لَّمْ تَرَوْهَا وَجَعَلَ كَلِمَةَ الَّذِينَ كَفَرُوا السُّفْلَىٰ وَكَلِمَةُ اللَّـهِ هِيَ الْعُلْيَا وَاللَّـهُ عَزِيزٌ حَكِيمٌ ﴿٤٠﴾

40. Kama hamtamsaidia, basi Mwenyezi Mungu alimsaidia walipomtoa wale waliokufuru Alipokuwa wa pili katika wawili alipomwambia sahibu yake: Usihuzunike hakika Mwenyezi Mungu yuko pamoja nasi. Mwenyezi Mungu akamteremshia utulivu wake, na akamsaidia kwa majeshi msiyoyaona. Na akalifanya neno la wale waliokufuru kuwa chini, na neno la Mwenyezi Mungu ndilo la juu. Na Mwenyezi Mungu ni mwenye nguvu mwenye hekima.

MNANINI MNAPOAMBIWA

Aya 38 – 40

VITA VYA TABUK

Aya hizi ziko karibu na mwisho wa sura iliyoshuka katika vita vya Tabuk. Kwa ufupi ni kuwa Roma ilikuwa ikimiliki Sham iliyopakana na Bara Arabu. Walisikia nguvu ya Uislamu na kukua kwake. Hercules, mfalme wa Roma, aliwahofia waislamu akasema: “Nikiwaacha mpaka wanikabili basi dola yangu haitakuweko mashariki” Akaazimia kuanza vita.

Mtume(s.a.w.w) naye kwa upande wake akaona asingoje mpaka ajiwe na Hercules na jeshi lake Madina. Akawataka watu watoke wakapigane na Waroma. Wakati huo joto lilikuwa kali sana.

Wanafiki wakapata fursa na kuwahofisha waislamu kwa umbali wa safari, joto kali na wingi wa adui. Wakaitikia mwito wao wale wadhaifu wa imani; wakatoa udhuru na kutafuta sababu, lakini Mtume akatangaza jihadi na kwamba watu wote. Hakutoa ruhusa kwa yoyote isipokuwa mgonjwa na asiye na cha kutoa Pamoja na njama za wanafiki, lakini walijotokeza wapiganaji kiasi elfu thelathini.

Kabla ya Mtume(s.a.w.w) kutoka na jeshi lake alimweka Ali bin Abu Talib kuwa kaimu wake kwa watu wake na familia yake. Muslim katika sahih yake, Sahih Muslim J2 uk 108 chapa ya mwaka 1348 A.H, anasema: “Ali akamwambia mtume: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu unaniacha nyuma na wanawake na watoto? Mtume(s.a.w.w) akasema: Je, huridhiii kuwa wewe kwangu mimi ni daraja ya Harun na Musa; isipokuwa hakuna Mtume baada yangu?”

Jeshi la Waislamu likaosonga; wote wakawa wako jangwani kwenye mvuke unachoma nyuso na mili. Njiani walimkuta sahaba mtukufu Abu Dhar akitembea kwa miguu kwa vile hakuwa na cha kupanda; wakati ambapo kiongozi wa wanafiki Abdallah bin Ubayya alijitoa na sehemu ya jeshi wakarudi Madina. Wanawake wakawapokea kwa kuwazoma na kuwarushia michanga nyusoni.

Baada ya mwendo wa siku saba, jeshi la waislamu likafika mpakani mwa dola ya Roma. Mkuu wa mji akataka suluhu na Mtume(s.a.w.w) kuwa atoe jiziya, Mtume akakubali. Akaendelea mbele na jeshi lake mpaka akafika katika mji wa Tabuk ulioko kati kati ya njia baina ya Damascus na Madina. Wakati huo ilikuwa ni mwezi wa Rajab mwaka wa 9 A.H.

Ikatokea kuwa kiongozi wa Tabuk ametoka nje kwenda kuwinda. Waislamu wakamteka na kuuchukua mji. Mtume akawa anatoka mahali fulani hadi mahali pengine mpaka akawashinda nguvu walinzi wa mpakani, akakomboa makabila ya kiarabu kutoka katika serikali ya Roma, Haya yote yalifanyika ndani ya siku ishirini.

Waislamu wakarudi Madina wakiwa na ngawira; na Mtume(s.a.w.w) akatoa agizo la kuwasusia waliorudi nyuma, akazuia wasizungumze na kuamiliana na watu hata wake na watoto. Ufafanuzi zaidi utakuja katika Aya zitakazofuatia; hasa Aya 117 na 118 katika sura hii.

MAANA

Enyi mlioamnini! Mna nini mnapoambiwa nendeni katika njia ya Mwenyezi Mungu mnajitia uzito katika ardhi.?

Mtume(s.a.w.w) alipowataka waislamu watoke kwa ajili ya vita vya Tabuk, liliwatia uzito hilo baadhi yao wakaathirika kubaki ardhini mwao na majumbani mwao.

Ilikuwa ni desturi ya Mtume(s.a.w.w) , anapotoka kwa ajil ya vita, kuwapa dhana watu kuwa anatokea jambo jingine kwa masilahi ya siri katika vita, lakini katika vita hivi alisema wazi wazi, ili watu wajue taabu zinazowangojea.

Baadhi ya wafasiri wamewatolea udhuru wale waliojitia uzito kutoka, kwamba wakati ulikuwa wa joto kali, watu wanadhiki ya chakula na mazao yamekwisha komaa tayari kwa kuvunwa.

Vyovyote iwavyo maneno kwa hali ilivyo – yanaelekezwa kwa waliojitia uzito na jihadi. Na Mwenyezi Mungu akawalaumu kwa kuwaambia:

Je, mmeridhia maisha ya dunia kuliko ya Akhera.? Lakini starehe za maisha ya dunia kulinganisha na Akhera ni kidogo tu.

Je, ni sawa imani yenu na akili zenu kuathirika na neema ya dunia inayokiwisha kuliko neema ya Akhera iliyo adhimu na yenye kudumu?

Kama hamwendi atawaadhibu kwa adhabu iumizayo na atawaleta watu wengine badala yenu, wala hamtamdhuru chochote.

Yaani kama hamtaitikia mwito wa Mtume wa kutoka naye kupigana na Waroma, basi Mwenyezi Mungu atawateremshia adhabu iumizayo, enyi wanafiki mnaojitia uzito; na atamsaidia Mtume wake kwa mikono ya wengine, wala kurudi nyuma kwenu hakuwezi kumdhuru Mwenyezi Mungu na Mtume wake.

Na Mwenyezi Mungu ni muweza wa kila kitu.

Hashindwi kuwaadhibu wala kuinusuru dini yake na Mtume wake kwa watu bora zaidi yenu.

Kama hamtamsaidia, basi Mwenyezi Mungu alimsaidia walipomtoa wale waliokufuru;

Inadokeza tukio la vitimbi na njama walizopanga makafiri wa Kiquraish, kumua Mtume(s.a.w.w) akiwa amelala kitandani kwake, jinsi alivyomwokoa nao kwa kulala Ali mahali pake na alivyo hama kutoka Makka kwenda Madina baada ya Mwenyezi Mungu kumfichulia njama zao, Hayo tumeyaeleza katika kufasiri (8:30).

Alipokuwa wa pili katika wawili alipomwambia sahibu yake: Usihuzunike hakika Mwenyezi Mungu yuko pamoja nasi.

Makusudio ya wa pili katika wawili na sahibu ni Abu Bakr, kwa vile yeye alikuwa pamoja na Mtume katika kuhama kwake na walijificha pamoja katika pango Thawr. Razi anasema: “Washirikina walipofuata nyayo na kukurubia pango, Abu Bakr alilia akimhofia Mtume(s.a.w.w) , Mtume(s.a.w.w) akamwambia usihuzunike, hakika Mwenyezi Mungu yuko pamoja nasi. Abu Bakr akasema: Hakika Mwenyezi Mungu yuko pamoja nasi, Mtume(s.a.w.w) akasema ndio.

Mwenyezi Mungu akamteremshia utulivu wake, na akamsaidia kwa majeshi msiyoyaona.

Amesema Abu Hayan Al-Andalusi katika tafsir yake: “Amesema Ibnu Abbas: Utulivu ni rehma, na dhamir katika akateremshia inamrudia Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) , kwa vile yeye ndiye anayezungumziwa.”

Hayo yanafikiana na kauli ya Sheikh wa Al az-har, Al Maraghi, aliposema katika tafsir yake, ninamnakuu: “Yaani akateremsha utulivu wake, unao tuliza moyo, kwa Mtume wake(s.a.w.w) , akampa nguvu kwa majeshi kutoka kwake ambao ni Malaika.” Vile vile yanaafikiana na mfumo wa Aya Kwa sababu dhamir katika kumsaidia na kumtoa inamrudia Mtume(s.a.w.w) .

Na akalifanya neno la wale waliokufuru kuwa chini, na neno la Mwenyezi Mungu ndilo la juu. Neno la Mwenyezi Mungu ni Tawhid na neno la waliokufuru ni shirk na ukafiri.

Na Mwenyezi Mungu ni mwenye nguvu mwenye hekima.

Hekima yake ilipitisha kumnusuru Mtume wake(s.a.w.w) kwa nguvu yake na kuidhihirisha dini yake juu ya dini zote.

انفِرُوا خِفَافًا وَثِقَالًا وَجَاهِدُوا بِأَمْوَالِكُمْ وَأَنفُسِكُمْ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ ذَٰلِكُمْ خَيْرٌ لَّكُمْ إِن كُنتُمْ تَعْلَمُونَ ﴿٤١﴾

41. Nendeni mkiwa wepesi na wazito, na mpiganie jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu kwa mali zenu na nafsi zenu. Hilo ni kheri kwenu mkiwa mnamjua.

لَوْ كَانَ عَرَضًا قَرِيبًا وَسَفَرًا قَاصِدًا لَّاتَّبَعُوكَ وَلَـٰكِن بَعُدَتْ عَلَيْهِمُ الشُّقَّةُ وَسَيَحْلِفُونَ بِاللَّـهِ لَوِ اسْتَطَعْنَا لَخَرَجْنَا مَعَكُمْ يُهْلِكُونَ أَنفُسَهُمْ وَاللَّـهُ يَعْلَمُ إِنَّهُمْ لَكَاذِبُونَ ﴿٤٢﴾

42. Lau ingekuwa ni faida iliyo karibu na safari nyepesi wangelikufuata. Lakini imekuwa ndefu kwao yenye mashaka, Na wataapa kwa Mwenyezi Mungu lau tungeliweza bila shaka tungelitoka pamoja nanyi. Wanaziangamiza nafsi zao, Na Mwenyezi Mungu anajua kuwa hakika hao ni waongo.

عَفَا اللَّـهُ عَنكَ لِمَ أَذِنتَ لَهُمْ حَتَّىٰ يَتَبَيَّنَ لَكَ الَّذِينَ صَدَقُوا وَتَعْلَمَ الْكَاذِبِينَ ﴿٤٣﴾

43. Mwenyezi Mungu amekusamehe! Kwa nini umewapa ruhusa kabla ya kubainika kwako wanaosema kweli na ukawajua waongo.

NENDENI MKIWA WAZITO NA MKIWA WEPESI

Aya 41-43

KWENDA WOTE

MAANA

Nendeni mkiwa wepesi na wazito, na mpiganie jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu kwa mali zenu na nafsi zenu.

Makusudio ya wepesi nikwenda kupigana jihadi kwa wepesi, na uzito ni kupigana kwa mashaka. Aya inafahamisha wajibu wa kutoka wote. Ufuatao ni ubainifu:

Adui akijaribu kuichokoza dini ya Kiislam kwa kukipotoa kitabu cha Mwenyezi Mungu na yaliyothibiti katika sunna ya Mtume wake, au kuwazuiya waislamu kutekeleza wajibu wao na nembo za kidini; akijaribu kutawala mji katika miji yao, basi hapo itakuwa ni wajibu kwa waislam kumpiga jihadi adui huyu na kuzuia upotevu wake.

Ikiwa baadhi wanaweza kumzuia, basi wajibu utakuwa ni kutosheana (kifaya) kwa maana kuwa wakitekeleza baadhi, basi jukumu litawaondokea wote, na wakipuza wote, basi jukumu ni lao wote na watastahiki adhabu wote.

Na kama haiwezekani ila kwa watu wote, basi itakuwa ni lazima kwa vijana, wazee, wanawake, vilema, vipofu na hata wagonjwa, kadiri mtu atakavyoweza.

Mwenye Jawahir anasema!” Adui akishambulia waislamu na kuhofiwa kuutia doa Uislamu au kafiri akitaka kutawala miji ya waislamu na kuwateka na kuchukua mali zao, basi ni wajibu kupigana kwa mungwana, mtumwa, mwana mume, mwanamke, mzima, mgonjwa, kipofu, mlemavu na wengineo; iwapo kuna haja ya kufanya hivyo.

Wala lilo halitahitajia kuweko Imam wala idhini yake; na wala halitahusika na wale waliochokozwa tu, bali ni wajibu kwa kila atakayelijua hilo, hata kama hakuchokozwa, Kama hakujua kuwa waliochokozwa wanaweza kumkabili adui.”

Hii ni ahadi aliyoichukua Mwenyezi Mungu kwa kila mwislamu kwa maafikiano ya madhehebu yote; sawa na walivyoafikiana juu ya wajibu wa Swaum, Swala, Hijja na Zaka.

Waislamu na waarabu hivi sasa wamejaribiwa kwa uchokozi wa Uzayuni wa kikoloni juu ya dini yao na miji yao. Wameuliwa wamefukuzwa na wakafungwa kwa maelefu. Kwa hiyo ni juu ya kila Mwarabu na Mwislamu popote alipo, Mashariki au Magharibi apigane kwa nguvu zake zote dhidi ya genge hili linalojiita dola ya Israil.

Hilo ni kheri kwenu.

Yaani hilo la kutoka ni kheri kwa waislamu katika dini yao na dunia yao.

Mkiwa mnamjua.

Ndio sisi tunajua kwamba kutoka kuwapiga jihadi waisrail ni wajibu kwa kila Mwislamu, lakini linalotuzuia kuwapiga jihadi waisrail ni viongozi wahaini. Kwa hiyo basi ni wajibu kuwapiga jihadi hawa kabla ya chochote. Kwa sababu wao ndio sababu ya sababu; lau si hiyana yao kwa dini yao, uma wao na kuwatii kwao wazayuni na ukoloni, basi Israil isigekuwako kabisa.

Lau ingekuwa ni faida iliyo karibu na safari nyepesi wangelikufuata.

Dhamiri ya wangekufuata inawarudia walio rudi nyuma katika vita vya Tabuk, Faida ya karibu ni ngawira baridi. Maana ni kuwa Ewe Muhammad! lau ungeliwaita kwenye manufaa ya haraka wangelikuitikia haraka haraka.

Lakini imekuwa ndefu kwao yenye mashaka.

Safari ya Sham kupitia jangwani kwenye vumbi la upepo na joto kali na adui Mrumi ndiye mwenye nguvu wakati huo, vipi watakuitikia?

Sifa hizi hazihusiki na wale waliorudi nyuma katika vita vya Tabuk tu, bali nafsi hupendelea raha na manufaa. Lakini watu wa imani wanaojiridhia kwa takua, wanaona chepesi kila kitu anachokiridhia Mwenyezi Mungu na Mtume wake.

Imam Ali(a.s) anasema:“Amali bora ni ile inayokirihisha nafsi yako.”

Yametangulia maelezo yanayoambatana na hayo katika Juz.5 (4:37).

Na wataapa kwa Mwenyezi Mungu lau tungeliweza bila shaka tungelitoka pamoja nanyi.

Hii ni habari kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa Mtume wake kwamba wanafiki waliorudi nyuma ya vita vya Tabuk, wamemwandalia viapo na nyudhuru za uwongo atakaporudi. Kimsingi ni kwamba sifa ya uongo haiepukani na mnafiki; kama si hivyo basi asingelikuwa mnafiki.

Wanaziangamiza nafsi zao.

Kwa vile wao wameiangamiza dini yao kwa uwongo na unafiki.

Na Mwenyezi Mungu anajua kuwa hakika hao ni waongo katika nyudhuru zao na viapo vyao.

Inasemekana kuwa hasemi uwongo isipokuwa mwoga, nasi tunaogozea kuwa anayeangamizwa na tamaa pia ni mwoga.

Mwenyezi Mungu amekusamehe! Kwa nini umewapa ruhusa kabla ya kubainika kwako wanaosema kweli na ukawajua waongo.

Mtume(s.a.w.w) alipotoa mwito wa kwenda kwenye Jihadi, baadhi walimwomba ruhusa ya kutokwenda, wakatoa sababu kadhaa. Mtume akawakubalia kabla ya kujua ukweli wao na uwongo wao katika nyudhuru.

Ndipo Mwenyezi Mungu (s.w.t) akamlaumu kwa hilo, akamwambia, ingekuwa vizuri kungoja kuwapa ruhusa mpaka ikufunukie hakika yao.

Hayo ndiyo yanayofahamika kutokana na dhahiri ya Aya.

Utaweza kuuliza kuwa : Mtume(s.a.w.w) ni Maasumu, na kauli yake Mwenyezi Mungu ‘Amekusamehe’ inaonyesha kuweko kosa (dhambi), pia kauli yake Mwenyezi Mungu ‘kwa nini umewapa ruhusa.’

Jibu : Msamaha kutoka kwa Mwenyezi Mungu haulazimishi kuweko dhambi. Mara nyingi inakuwa ni ibara ya thawabu yake na rehema yake, Mitume wote walikuwa wakiomba msamaha kwake Mwenyezi Mungu. Ama kusema “Kwa nini”, hilo ni jambo jepesi ambapo inasihi katika mambo ya halali na mengineyo. Unaweza kumwambia sahibu yako; kwa nini umefanya hivi?, Bila ya kuona kuwa amefanya jambo baya, isipokuwa unakusudia angefanya jingine.

Lengo la lawama hapa inayotoka kwa Mwenyezi Mungu kwa Mtume wake, ni kubainisha uwongo wa wanafiki katika nyudhuru zao, na kwamba hilo lilikuwa ni kukimbia jihadi tu. Mfumo huu ni fasaha zaidi katika kukanusha udhuru kuliko mifumo yote. Zaidi ya hayo Mwenyezi Mungu amesema katika Aya 117 ya Sura hii: “Mwenyezi Mungu amekubalia toba wahajir na answar waliomfuata katika saa ya dhiki Ikiwa toba haifahamishi kuweko dhambi, basi msamaha na kuuliza kwa nini, ndiko kusikofahamisha zaidi dhambi.

لَا يَسْتَأْذِنُكَ الَّذِينَ يُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ أَن يُجَاهِدُوا بِأَمْوَالِهِمْ وَأَنفُسِهِمْ وَاللَّـهُ عَلِيمٌ بِالْمُتَّقِينَ ﴿٤٤﴾

44. Hawakuombi ruhusa ambao wanamwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho ya kuacha kupigana jihadi kwa mali zao na nafsi zao. Na Mwenyezi Mungu ni mwenye kuwajua wenye takua.

إِنَّمَا يَسْتَأْذِنُكَ الَّذِينَ لَا يُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ وَارْتَابَتْ قُلُوبُهُمْ فَهُمْ فِي رَيْبِهِمْ يَتَرَدَّدُونَ ﴿٤٥﴾

45. Hakika wanaokuomba ruhusa ni wale tu wasiomwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho. Na nyoyo zao zikatia shaka, kwa hiyo wanasitasita katika shaka yao.

وَلَوْ أَرَادُوا الْخُرُوجَ لَأَعَدُّوا لَهُ عُدَّةً وَلَـٰكِن كَرِهَ اللَّـهُ انبِعَاثَهُمْ فَثَبَّطَهُمْ وَقِيلَ اقْعُدُوا مَعَ الْقَاعِدِينَ ﴿٤٦﴾

46. Lau wangelitaka kutoka bila shaka wangeliandalia maandilio, Lakini Mwenyezi Mungu alichukia kutoka kwao, kwa hiyo akawazuia Na ikasemwa: Kaeni pamoja na wakaao.

لَوْ خَرَجُوا فِيكُم مَّا زَادُوكُمْ إِلَّا خَبَالًا وَلَأَوْضَعُوا خِلَالَكُمْ يَبْغُونَكُمُ الْفِتْنَةَ وَفِيكُمْ سَمَّاعُونَ لَهُمْ وَاللَّـهُ عَلِيمٌ بِالظَّالِمِينَ ﴿٤٧﴾

47. Lau wangelitoka pamoja nanyi wasingeliwazidisha ila mchafuko na wangelikwenda huku na huko kati yenu kuwatakia fitina, Na miongoni mwenu wako wanawaosikiliza, Na Mwenyezi Mungu anawajua madhalimu.

لَقَدِ ابْتَغَوُا الْفِتْنَةَ مِن قَبْلُ وَقَلَّبُوا لَكَ الْأُمُورَ حَتَّىٰ جَاءَ الْحَقُّ وَظَهَرَ أَمْرُ اللَّـهِ وَهُمْ كَارِهُونَ ﴿٤٨﴾

48. Walikwishataka fitina tangu zamani na wakakupindulia mambo. Mpaka ikaja haki na ikadhihiri amri ya Mwenyezi Mungu na wao wamechukia.

HAWAKUOMBI RUHUSA AMBAO WANAWAMWAMINI MWENYEZI MUNGU

Aya 44 – 48

MAANA

Hawakuombi ruhusa ambao wanamwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho ya kuacha kupigana jihadi kwa mali zao na nafsi zao.

Kutakuwa na sababu gani ya kuomba ruhusa ikiwa jihadi ni wajibu. Je, mumin wa kweli anaweza kuomba ruhusa ya kuacha kuswali na kufunga na kusema lailaha illa llah, Muhammad Rasullah?

Hakika wanaokuomba ruhusa ni wale tu wasiomwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho.

Kila moja katika Aya mbili hizi inafahamisha juu ya mwenzake, Kwa sababu maana ya kuwa Mumin hakuombi ruhusa nikuwa asiyekuwa mumin hukuomba, Na maana ya asiyekuwa mumin anakuomba ruhusa ni kuwa mumin hakuombi. Mwenyezi Mungu amechanganya Aya mbili hizi kwa kusisitiza maana.

Na nyoyo zao zikatia shaka, kwa hiyo wanasitasita katika shaka yao.

Yaani kwamba wao wanajionyesha kuwa ni waislamu, lakini kumbe walivyo ni kuwa wanashaka shaka, hawasemi kuwa ni kweli au ni uwongo. Huu ndio unafiki, Kwa sababu mkweli mwenye ikhlasi hufanya vile inavyoonelea akili yake na kudhihirisha kwa watu, iwe ni shaka au yakini.

Lau wangelitaka kutoka pamoja na mtume kwenye vita vya Tabuk,bila shaka wangeliandalia maandilio ya vipando na masurufu ya njiani; nao walikuwa wakiliweza hilo.

Lakini Mwenyezi Mungu alichukia kutoka kwao, kwa sababu hawana wanalolitokea isipokuwa ufisadi na fitina; kama walivyofanya katika vita vya Hunain, wakati Abu Sufyan na walio mfano wake walipotoka na Mtume vita vilipochacha waligeuka wakakimbia na likalegea jeshi la waislamu.

Kwa hiyo akawazuia.

Mwenyezi Mungu aliwaamrisha kutoka kwa ajili ya Jihadi, lakini wao waliazimia ufisadi kwa kuleta migongano katika jeshi la wislamu; kama alivyosema katika Aya inayofuatia:

Lau wangelitoka pamoja nanyi wasingeliwazidisha ila mchafuko.

Kwa hiyo aliwazuia Mwenyezi Mungu na hili la fitina sio na jihadi, ambayo amewaaamrisha.

Na ikasemwa: Kaeni pamoja na wakaao.

Yaani kaeni pamoja na wanawake, watoto na vikongwe.

Mwenyezi Mungu hakubainisha aliyewaambia hivyo, Je, ni nafsi zao, au hali yenyewe ilivyokuwa au waliambiana wenyewe? Mwenyezi Mungu ndiye ajuae.

Unaweza kuuliza : Katika Aya 43, Mwenyezi Mungu amesema: Kwa nini umewapa ruhusa na katika Aya hii anasema: Mwenyezi Mungu hakupenda kutoka kwao, Sasa tutazichanganya vipi Aya hizi?

Jibu : litaeleleweka kulingana na tuliyoyasema katika kufasiri kauli yake Mwenyezi Mungu: ‘Kwa nini umewaruhusu’ kwamba hiyo sio lawama na swali la kiuhakika; isipokuwa lengo ni kubainisha uwongo wa wanafiki katika nyudhuru zao.

Lau wangelitoka pamoja nanyi wasingeliwazidisha ila mchafuko na wangelikwenda huku na huko kati yenu kuwatakia fitina.

Huu ni ubainifu wa hekima ya Mwenyezi Mungu wa kutopenda kwake Mwenyezi Mungu na Mtume kutoka wanafiki pamoja na jeshi la waislam. kwamba wao wangefanya mbinu za kuwatenganisha na kuleta vurugu ndani ya jeshi. Watu wa aina hii wapo kila mahali na kila wakati. Siku hizi wanajulikana kwa jina la kikosi cha tano (Fifth Column).

Na miongoni mwenu wako wanawaosikiliza.

Nao ni wale wenye akili za juu juu ambao wanachukua maneno ya waongo ni bendera wanaofuata upepeo.

Walikwishataka fitina tangu zamani na wakakupindulia mambo.

Mwenyezi Mungu anadokeza vitimbi vyao na hadaa zao kwa Mtume kabla ya vita vya Tabuk, ikiwa ni pamoja na kukimbia Abu Sufyan katika vita vya Hunain, na kujitoa bin Ubayya pamoja na theluthi ya jeshi katika vita vya Uhud.

Mpaka ikaja haki na ikadhihiri amri ya Mwenyezi Mungu na wao wamechukia.

Kila aliyopenda Mwenyezi Mungu ni haki na kila aliyoyachukia ni batili. Mwenyezi Mungu alipenda Uislam pamoja na Mtume wake ushinde. Kwa hiyo yakatimia aliyoyataka Mwenyezi Mungu na akamwandalia sababu kwa ushindi wa kuiteka Makka, ushindi katika vita vya Hunain na Tabuk na kusafika bara Arabu kutokana na uchafu wa Mayahudi waovu.

Makusudio ya kauli yake Mwenyezi Mungu: ‘Na ikadhihiri amri ya Mwenyezi Mungu’ ni kwamba ushindi huu waliushuhudia watu wote, na mpaka leo hivi hadi siku ya mwisho jina la Muhammad bin Abdullah linatajwa pamoja na la Mwenyezi Mungu kote - Mashariki mwa Ardhi na Magharibi.