TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MOJA Juzuu 11

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MOJA0%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MOJA Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MOJA

Mwandishi: Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 9756
Pakua: 1428

Maelezo zaidi:

Juzuu 11
Juzuu 1
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 15 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 9756 / Pakua: 1428
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MOJA

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MOJA Juzuu 11

Mwandishi:
Swahili

6

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MOJA

وَلَوْ يُعَجِّلُ اللَّـهُ لِلنَّاسِ الشَّرَّ اسْتِعْجَالَهُم بِالْخَيْرِ لَقُضِيَ إِلَيْهِمْ أَجَلُهُمْ فَنَذَرُ الَّذِينَ لَا يَرْجُونَ لِقَاءَنَا فِي طُغْيَانِهِمْ يَعْمَهُونَ ﴿١١﴾

11. Lau Mwenyezi Mungu angeli waharakishia watu shari, kama wanavyoharakishia kheri, hakika wangelikwisha timiziwa muda wao. Basi tunawaacha wale wasio taraji kukutana nasi wakihangaika katika upotevu wao.

وَإِذَا مَسَّ الْإِنسَانَ الضُّرُّ دَعَانَا لِجَنبِهِ أَوْ قَاعِدًا أَوْ قَائِمًا فَلَمَّا كَشَفْنَا عَنْهُ ضُرَّهُ مَرَّ كَأَن لَّمْ يَدْعُنَا إِلَىٰ ضُرٍّ مَّسَّهُ كَذَٰلِكَ زُيِّنَ لِلْمُسْرِفِينَ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿١٢﴾

12. Na dhara inapomgusa mtu hutuomba naye ameegesha ubavu wake, au katika hali ya kukaa, au katika hali ya kusi mama; lakini tunapomwon dolea dhara yake huendelea kama kwamba hakupata kutuomba tumwondolee dhara iliyomgusa, Namna hii wamepambiwa wapetukao mipaka yake waliyokuwa wakiyatenda.

وَلَقَدْ أَهْلَكْنَا الْقُرُونَ مِن قَبْلِكُمْ لَمَّا ظَلَمُوا وَجَاءَتْهُمْ رُسُلُهُم بِالْبَيِّنَاتِ وَمَا كَانُوا لِيُؤْمِنُوا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْقَوْمَ الْمُجْرِمِينَ ﴿١٣﴾

13. Hakika tumekwishaziangamiza kaumu za kabla yenu walipodhulumu; na waliwajia Mitume wao kwa hoja zilizo wazi, lakini hawakuwa wenye kuamini, Namna hii tunawalipa watu wakosefu.

ثُمَّ جَعَلْنَاكُمْ خَلَائِفَ فِي الْأَرْضِ مِن بَعْدِهِمْ لِنَنظُرَ كَيْفَ تَعْمَلُونَ ﴿١٤﴾

14. Kisha tukawafanya nyinyi ndio mnaowafuatia baada yao katika ardhi ili tuone jinsi mtakavyotenda.

LAU MWENEYEZI MUNGU ANGELIWAHARAKISHIA SHARI

Aya 11 – 14

MAANA

Lau Mwenyezi Mungu angeliwaharakishia watu shari, kama wanavyoharakishia heri, hakika wangelikwishatimiziwa muda wao.

Makusudio ya heri hapa ni yale yanayowanufaisha watu katika maisha haya, Kwa ajili hii ndio wanaiharakia wala hawana subira nayo. Makusudio ya shari ni yale wanavyodhurika nayo; huyakataa na kuyaachukia kwa maumbile yao; ila kukiwa na sababu; kama vile kuondoa ambayo ni shari zaidi. Mshairi anasema: Navumilia shari kuhofia shari Shari nyingine ni shari kuliko shari.

Au pengine mtu akiwa katika hali isiyo ya kawaida; kama vile mtu anayetaka kujinyonga. Au kuwa katika hali ya inadi ya kumkabili hasimu aliyemshinda kwa hoja; kama vile walivyoshindwa washirikina kumjibu Muhammad(s.a.w.w) wakati Mwenyezi Mungu alipodhihirisha miujiza mikononi mwake wakasema:

“Ewe Mungu! Ikiwa (anayoyasema Muhammad) ni haki, basi tuteremshie mvua ya mawe au tuletee adhabu iumizayo.” Juz. 8 (8:32)

Mwenyezi Mungu (s.w.t) alimjibu kila anayeharakisha adhabu na shari kwamba hekima ina inapitisha kutomkubalia matakwa yake mpaka wakati mwingine. Pengine linaweza kutokea jambo jengine la heri baada yake; kama ilivyotokea kwa wengi waliosema: Tuteremshie mvua ya mawe. Kuna kundi katika wao walisilimu na wengine wakazaa waumini wengi, Kama Mwenyezi Mungu angehiharakisha muda wao kusingelitokea kitu.

Kwa ufupi ni kwamba wao waliharakisha shari, sawa na wanavyoharak- isha heri, lakini Mungu (s.w.t) aliwachelewesha mpaka alipowatakia heri.

Basi tunawaacha wale wasiotaraji kukutana nasi wakihangaika katika upotevu wao.

Yaani Mwenyezi Mungu Mtukufu haharikishi adhabu kwa yule asiyeamini kufufuliwa katika wale waliomkufuru Muhammad, bali anaachana nao; hata kama wameasi amri yake na kuendelea katika uasi.

Na dhara inapomgusa mtu hutuomba naye ameegesha ubavu wake au katika hali ya kukaa, au katika hali ya kusimama.

Kuegesha ubavu, kukaa na kusimama ni fumbo la unyenyekevu wake kati- ka hali zake zote harakati zake na kutulia kwake.

Maana ni kuwa lau inamshukia chembe ya shari aliyoiharakisha, atakosa subira na atahangaika na kutukimbilia kwa unyenyekevu kwa kujidhalilisha katika hali zake zote ili tumuondolee.

Lakini tunapomwondolea dhara yake huendelea kama kwamba hakupata kutuomba tumwondolee dhara iliyomgusa.

Hali mbaya inaweza kumlazimisha mtu kusema uwongo, ria na kujipendekeza kwa mtu aliye na haja naye. Lakini ni jambo gani linalomlazimisha mtu kuasi, kukana jambo zuri na kumkana ambaye jana alikuwa akimyenyekea amtekelezee haja yake? Na alipompatia tu haja yake akamsahau kwamba hakumwomba kitu?

Hakuna tafsiri nyingine ya hilo zaidi ya kutojali, kuikana haki na misimamo na kupetuka mipaka katika hayo.

Namna hii wamepambiwa wapetukao mipaka yake waliyokuwa wakiyatenda.

Waliopambiwa vitendo vibaya ni wale wasiojali chochote ila manufaa yao na tamaa zao.

Hakika tumekwishaziangamiza kaumu za kabla yenu walipodhulumu; na waliwajia Mitume wao kwa hoja zilizo wazi, lakini hawakuwa wenye kuamini, Namna hii tunawalipa watu wakosefu.

Hili ni onyo kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa wale waliomkadhibisha Muhammad(s.a.w.w) kwamba nao itawafika adhabu kama iliyowafikia waliokua kabla yao walipowakadhibisha Mitume yao. Umepita mfano wa Aya hii katika Juz.7 (6:6).

Kisha tukawafanya nyinyi ndio mnaowafuatia baada yao katika ardhi ili tuone jinsi mtakavyotenda.

Umma unaondoka na kufuatiwa na mwingine. Ama lengo la kuweko mtu katika ardhi hii ni elimu na amali ya kunufaisha.

Utauliza kuwa : Mwenyezi Mungu (s.w.t) anasema:

وَمَا خَلَقْتُ الْجِنَّ وَالْإِنسَ إِلَّا لِيَعْبُدُونِ ﴿٥٦﴾

“Sikuumba majini na watu ila waniabudu” (51:56).

Na wewe unasema kuwa Mwenyezi Mungu amemuumba mtu kwa elimu ya manufaa.

Jibu : Makusudio ya ibada iliyotajwa ni amali njema kwa dalili ya kauli yake Mwenyezi Mungu:

وَالْعَمَلُ الصَّالِحُ يَرْفَعُهُ ﴿١٠﴾

“Na amali njema huiinua…” (35:10)

Bali Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameumba ulimwengu pamoja na ardhi yake na mbingu yake kwa ajili ya amali njema. Mwenyezi Mungu (s.w.t) anasema:

وَهُوَ الَّذِي خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ فِي سِتَّةِ أَيَّامٍ وَكَانَ عَرْشُهُ عَلَى الْمَاءِ لِيَبْلُوَكُمْ أَيُّكُمْ أَحْسَنُ عَمَلًا ﴿٧﴾

“ Yeye ndiye aliyeziumba mbingu na ardhi katika siku sita na Arshi yake ilikuwa juu ya maji, ili awajaribu ajulikane ninani miongoni mwenu ni mzuri zaidi wa vitendo” (11:7).

Tumebanisha maana ya kujaribiwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu katika Juz.7 (5:94)

وَإِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِمْ آيَاتُنَا بَيِّنَاتٍ قَالَ الَّذِينَ لَا يَرْجُونَ لِقَاءَنَا ائْتِ بِقُرْآنٍ غَيْرِ هَـٰذَا أَوْ بَدِّلْهُ قُلْ مَا يَكُونُ لِي أَنْ أُبَدِّلَهُ مِن تِلْقَاءِ نَفْسِي إِنْ أَتَّبِعُ إِلَّا مَا يُوحَىٰ إِلَيَّ إِنِّي أَخَافُ إِنْ عَصَيْتُ رَبِّي عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ ﴿١٥﴾

15. Na wanaposomewa Aya zetu zilizo wazi, wale wasiotaraji kukutana nasi husema: “Lete Qur’ani isiyokuwa hii, au ibadilishe. Sema: Haifai mimi kubadilisha kwa hiyari ya nafsi yangu; sifuati ila niliyopewa wahyi. Hakika mimi naogopa, nikimwasi Mola wangu, adhabu ya siku iliyo kuu.

قُل لَّوْ شَاءَ اللَّـهُ مَا تَلَوْتُهُ عَلَيْكُمْ وَلَا أَدْرَاكُم بِهِ فَقَدْ لَبِثْتُ فِيكُمْ عُمُرًا مِّن قَبْلِهِ أَفَلَا تَعْقِلُونَ ﴿١٦﴾

16. Sema: lau Mwenyezi Mungu angelitaka nisingeliwasomea hiyo wala nisingeliwajuza, Nimekaa kwenu umri kabla yake, basi hamtii akili.

فَمَنْ أَظْلَمُ مِمَّنِ افْتَرَىٰ عَلَى اللَّـهِ كَذِبًا أَوْ كَذَّبَ بِآيَاتِهِ إِنَّهُ لَا يُفْلِحُ الْمُجْرِمُونَ ﴿١٧﴾

17. Basi ninani aliye dhalimu zaidi kuliko yule amzuliaye Mwenyezi Mungu uwongo au akadhibishaye Aya zake? Hakika hawafaulu wakosefu.

LETE QUR’AN ISIYOKUWA HII

Aya 15 – 17

MAANA

Na wanaposomewa Aya zetu zilizo wazi, wale wasiotaraji kukutana nasi husema: “Lete Qur’ani isiyokuwa hii, au ibadilishe.

Makusudio ya wale wasiotaraji kukutana na Mwenyezi Mungu ni washirikina. Mtume(s.a.w.w) alikuwa akiwapa hoja wao, mayahudi na wakristo kwa Qur’ani; na alikuwa akijadaliana nao kwa mjadala mzuri. Mjadala wake na washirikina na mayahudi ulikuwa mkali, kwa sababu wao ndio waliokuwa maadui na wapinzani sana; kama ilivyoelezwa katika Aya kadhaa zilizotangulia.

Ama wakristo kuna waliomtembelea na wakakubali kutoa kodi; kama vile wakristo wa Najran. Na wengine walikusudia kumpiga vita Madina, Mtume akawakatia njia na kupigana nao katika ardhi ya Sham.

Washirikina walikuwa wakimpa Mtume maoni ya kila aina ya ujinga wao na mchezo wao; kama vile ilivyodokezwa katika Juz,1(2:118), walipomtaka Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) awazungumzishe Mwenyezi Mungu kwa mdomo.

Aya hii tuliyonayo inasimulia maoni yao kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) kuwa awaletee Qur’ani nyingine au aibadilishe kwa vile Qur’ani hii imewaletea dini mpya. Inawalingania kwenye Tawhid na kuamini ufufuo na malipo.

Pia inathibitisha misingi ya uadilifu na usawa, kutupilia mbali utabaka na kuharamisha riba na dhuluma; wakati ambapo wao wana dini ya waungu wengi, wanapinga ufufuo na kuharakisha wanayoyatamani. Ndipo wakamtaka Muhammad(s.a.w.w) awaletee Qur’ani itakayothibitisha dini yao na kuiga kwao au angalau, waondoe ile sehemu wasiyoiridhia.

Kuna tofauti gani kati ya maombi haya ya washirikina wa Kijahiliya na vijana wengi wa karne ya ishirini, wasemao kuwa kuna haja gani ya dini na kwa nini kuwe na halali na haramu? Na, maendeleo ya makompyuta hayahitaji msingi na dini.

Sema: Haifai mimi kubadilisha kwa hiyari ya nafsi yangu; sifuati ila niliyopewa wahyi. Hakika mimi naogopa, nikimwasi Mola wangu, adhabu ya siku iliyo kuu.

Mtume ni mwenye kunakili tu kutoka kwa Mwenyezi Mungu sio mwenye kuweka sharia; sawa na mpokezi wa Hadith kutoka kwa Mtume. Kuna Hadith iliyopokewa kutoka kwake isemayo “Mwenye kunikadhibisha basi na ajichagulie makazi yake motoni,” sasa itakuwaje yeye amkadhibishe Mwenyezi Mungu. Haiwezekani kwa mwenye isma kukosea au kuteleza.

Aya hii inampinga yule mwenye kutoa fatwa na kuhukumu bila ya dalili ya kisharia. Vile vile ni dalili mkataa kuwa Mtume kamwe hakutoa hukumu kwa ijtihadi yake, na kwamba hukumu zake zote zilikuwa ni wahyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu, na mwenye kusema kuwa alifanya ijtihad basi, atakuwa hakumtofautisha na mafakihi wengine, Shia wanapinga kuwa Mtume alifanya ijitihadi ambapo Sunni wanatofautiana. Wengine wanaafikiana na Shia na wengi wamesema kuwa alifanya ijitihadi.

Sema: lau Mwenyezi Mungu angelitaka nisingliwasomea hiyo wala nisingeliwajuza.

Dhamir ya hiyo ni ya Qur’ani. Maana ni kuwa lau Mwenyezi Mungu asingeliileta nisingelifanya hayo, lakini nimefanya niliyoyafanya kwa kutekeleza matakwa ya Mwenyezi Mungu.

Nimekaa kwenu umri kabla yake, basi hamfahamu.

Mtu ambaye ameishi kwa watu miaka arubaini kabla ya kupewa wahyi akiwa hakusoma kitabu chochote au kufundishwa na mwalimu, wala hakuwahi kufanya jambo la kulaumiwa; bali maisha yake yote yalikuwa ni mema, mwenye ukweli na uaminifu mpaka akaitwa Amin (mwaminifu). Pamoja na yote haya hamfahamu kuwa mtu aliye hivi yuko mbali na uwongo na uzushi?

Basi ni nani aliye dhalimu zaidi kuliko yule amzuliaye Mwenyezi Mungu uwongo au akadhibishaye Aya zake?

Maana ya kumzulia Mwenyezi Mungu uwongo ni kuweka kwenye dini jambo lililo mbali na dini. Maana ya kukadhibisha Aya zake ni kukanusha yale ambayo kwa asili yanatoka kwake. Hii ndiyo bid’a ambayo Mtume ameielezea kwa kusema: “Kila bid’a ni upotevu na kila upotevu ni katika moto.”

Hakika hawafaulu wakosefu.

Kwa sababu njia ya kufaulu na kuokoka ni ukweli na ikhlasi. Ama uwongo na uzushi ni njia ya maangamivu na utwevu, na haifati njia hiyo isipokuwa mwovu mkosefu.

وَيَعْبُدُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ مَا لَا يَضُرُّهُمْ وَلَا يَنفَعُهُمْ وَيَقُولُونَ هَـٰؤُلَاءِ شُفَعَاؤُنَا عِندَ اللَّـهِ قُلْ أَتُنَبِّئُونَ اللَّـهَ بِمَا لَا يَعْلَمُ فِي السَّمَاوَاتِ وَلَا فِي الْأَرْضِ سُبْحَانَهُ وَتَعَالَىٰ عَمَّا يُشْرِكُونَ ﴿١٨﴾

18. Na wanaabudu wasiowadhuru wala kuwanufaisha badala ya Mwenyezi Mungu, Na wanasema: “Hawa ndio waombezi wetu kwa Mwenyezi Mungu.” Sema: Je, mnamwambia Mwenyezi Mungu asiyoyajua katika mbingu wala katika ardhi? Ametakasika na ametukuka na hao wanaomshirikisha naye.

وَمَا كَانَ النَّاسُ إِلَّا أُمَّةً وَاحِدَةً فَاخْتَلَفُوا وَلَوْلَا كَلِمَةٌ سَبَقَتْ مِن رَّبِّكَ لَقُضِيَ بَيْنَهُمْ فِيمَا فِيهِ يَخْتَلِفُونَ ﴿١٩﴾

19. Na hawakuwa watu ila ni umma mmoja tu kisha wakahitalifiana. Na lau si neno lililotangulia kutokana na Mola wako, bila shaka hukumu ingelikwishakatwa baina yao katika hayo wanayokhitalifiana.

وَيَقُولُونَ لَوْلَا أُنزِلَ عَلَيْهِ آيَةٌ مِّن رَّبِّهِ فَقُلْ إِنَّمَا الْغَيْبُ لِلَّـهِ فَانتَظِرُوا إِنِّي مَعَكُم مِّنَ الْمُنتَظِرِينَ ﴿٢٠﴾

20. Na wanasema: “Kwanini hakuteemshiwa ishara kutoka kwa Mola wake?” Sema: hakika ghaibu ni ya Mwenyezi Mungu tu, basi ngojeni na mimi niko pamoja nanyi katika kungoja.

WANASEMA HAWA NI WAOMBEZI WETU

Aya 18-20

MAANA

Na wanaabudu wasiowadhuru wala kuwanufaisha badala ya Mwenyezi Mungu.

Hawa ni wale waliomwambia Mtume alete Qur’ani nyingine au aibadilishe. Wao walikuwa wakiabudu masanamu; wakiamini kuwa yanawanu- faisha na kuwadhuru; kama anavyosema Mwenyezi Mungu:

Na wanasema: “Hawa ndio waombezi wetu kwa Mwenyezi Mungu.

Lakini imani yao hii haina msingi wowote isipokuwa ni njozi na mawazo tu. Mwenyezi Mungu alimwamrisha Mtume wake Muhammad(s.a.w. w ) akanushe madai yao kwa kuwaambia:

Je, mnamwambia Mwenyezi Mungu asiyoyajua katika mbingu wala katika ardhi? Ametakasika na ametukuka na hao wanaomshirikisha naye.

Washirikina walidai kuwa masanamu yao yatawaombea kwa Mwenyezi Mungu. Ikiwa haya ni kweli, basi Mwenyezi Mungu angeliujua uombezi huu na kwa kuwa haujui basi ina maana kuwa washirikina ni waongo na wazushi.

Na hawakuwa watu ila ni umma mmoja tu kulingana na maumbile aliyowaumbia Mwenyezi Mungu; kisha hawa zao zikawatenganisha kutoka asili yao na ufuasi ukawagawa vikundi katika dini yao baada ya kushindana kupata raha za maisha.

Na lau si neno lililotangulia kutokana na Mola wako, bila shaka hukumu ingelikwishakatwa baina yao katika hayo wanayokhitalifiana.

Makusudio ya neno hapa ni kutoharakisha Mwenyezi Mungu adhabu ya waasi na thawabu za watiifu; bali anangojea mpaka siku ya ufufuo; ili kila mtu, kwa hiyari na radhi ya nafsi yake, afikie heri au shari na ubora au uduni.

Lau Mwenyezi Mungu angeliharakisha adhabu ya muovu katika watu basi wangelikuwa sawa, lakini kwa kuhofia tu si kwa utiifu.

Hakuna mwenye shaka kwamba hili ni kinyume na kuondoa maana ya thawabu na adhabu. Vile vile litapingana na hekima yake Mwenyezi Mungu Mtukufu ya kudhihirisha hakika ya mtu kulingana na matendo yake na uchaguzi wake. Umetanglia mfano wake katika Juz. 2 (213) na Juz. 6 (6:48).

Na wanasema: “Kwa nini hakuteremshiwa ishara kutoka kwa Mola wake?”

Mwenyezi Mungu alimteremshia Muhammad ishara nyingi na miujiza kadhaa, lakini washirikina waliosema hivi walitaka ishara kulingana na hawa zao na miujiza wanayoitaka wao; kama walivyosema:

“Mbona Mwenyezi Mungu hasemi nasi” Juz; 1 (2:218).

لَوْلَا أُنزِلَ إِلَيْهِ مَلَكٌ فَيَكُونَ مَعَهُ نَذِيرًا ﴿٧﴾

“Mbona hakuteremshiwa Malaika akawa muonyaji pamoja naye” (25:7).

Sema : hakika ghaibu ni ya Mwenyezi Mungu tu, basi ngojeni na mimi niko pamoja nanyi katika kungoja.

Yaani, ewe Muhammad waambie hawa wenye inadi kuwa ishara mnazozitaka ziko mikononi mwa Mwenyezi Mungu mimi sina langu jambo wala sijui kuwa Mwenyezi Mungu ataiteremsha kutoka mbinguni au Mimi na nyinyi katika hili ni sawa katika hilo. Basi tuone ni kundi gani litasalimika na hasira za Mwenyezi Mungu.

7

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MOJA

وَإِذَا أَذَقْنَا النَّاسَ رَحْمَةً مِّن بَعْدِ ضَرَّاءَ مَسَّتْهُمْ إِذَا لَهُم مَّكْرٌ فِي آيَاتِنَا قُلِ اللَّـهُ أَسْرَعُ مَكْرًا إِنَّ رُسُلَنَا يَكْتُبُونَ مَا تَمْكُرُونَ ﴿٢١﴾

21. Na tunapowaonjesha watu rehema baada ya dhara kuwagusa, huanza kuzipangia njama Aya zetu, Sema: Mwenyezi Mungu ni mwepesi zaidi wa kupanga njama, Hakika wajumbe wetu wanayaandika mnayoyapanga.

هُوَ الَّذِي يُسَيِّرُكُمْ فِي الْبَرِّ وَالْبَحْرِ حَتَّىٰ إِذَا كُنتُمْ فِي الْفُلْكِ وَجَرَيْنَ بِهِم بِرِيحٍ طَيِّبَةٍ وَفَرِحُوا بِهَا جَاءَتْهَا رِيحٌ عَاصِفٌ وَجَاءَهُمُ الْمَوْجُ مِن كُلِّ مَكَانٍ وَظَنُّوا أَنَّهُمْ أُحِيطَ بِهِمْ دَعَوُا اللَّـهَ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ لَئِنْ أَنجَيْتَنَا مِنْ هَـٰذِهِ لَنَكُونَنَّ مِنَ الشَّاكِرِينَ ﴿٢٢﴾

22. Yeye ndiye anayewaendesha bara na baharini. Hata mnapokuwa majahazini na yakaenda nao upepo mzuri na wakaufurahia, mara upepo mkali ukawazukia yakawajia mawimbi kutoka kila upande na wakaona wamekwishazongwa, basi hapo humwomba Mwenyezi Mungu kwa kumfanyia ikhlasi: ukituokoa na haya bila shaka tutatakuwa miongoni mwa wanaoshukuru.

فَلَمَّا أَنجَاهُمْ إِذَا هُمْ يَبْغُونَ فِي الْأَرْضِ بِغَيْرِ الْحَقِّ يَا أَيُّهَا النَّاسُ إِنَّمَا بَغْيُكُمْ عَلَىٰ أَنفُسِكُم مَّتَاعَ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا ثُمَّ إِلَيْنَا مَرْجِعُكُمْ فَنُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ ﴿٢٣﴾

23. Lakini alipowaokoa, mara wanafanya jeuri katika ardhi pasipo haki. Enyi watu! Hakika jeuri yenu itawarudia nyinyi wenyewe tu. Ni starehe ya maisha ya dunia kisha marejeo yenu ni kwetu ndipo tuwaambie mliyokuwa mkiyatenda.

SEMA: MWENYEZI MUNGU NI MWEPESI ZAIDI WA KUPANGA NJAMA

Aya 21-23

MAANA

Na tunapowaonjesha watu rehema baada ya dhara kuwagusa, huanza kuzipangia njama Aya zetu.

Imesemekana kuwa makusudio ya watu ni washirikina. Kauli hii haiko mbali na mfumo wa maneno, kwa sababu Aya inawazungumzia washirikina lakini haizuwii kuwa makemeo yanamhusu kila mwenye kukana neema za Mwenyezi Mungu, ni sawa upinzani utokane na mu’min au kafiri, kabla ya madhara au baada.

Madhumuni ya Aya hii yanalingana na Aya ya 12 ya Sura hii: “Na dhara inapomgusa mtu hutuomba naye ameegesha ubavu wake au katika hali ya kukaa au katika hali ya kusimama Lakini tunapomwondolea dhara yake huendelea kama kwamba hakupata kutuomba tumwondolee dhara iliyomgusa.” Hiyo inasema kuwa mtu anamkumbuka Mwenyezi Mungu katika saa ya dhiki na hii tunayoifasiri sasa inasema kuwa anapomjaalia wepesi huzipangia njama Aya zake.

Mkusudio ya njama hizo ni kupinga Aya za Mwenyezi Mungu na kukataa kuwa Mwenyezi Mungu ndiye msababishaji katika kumwondolea madhara na balaa na kufasiri sababu nyingine zizisizo na msingi wala asili; kama masanamu, nyota, sadfa na tafsiri nyinginezo mbovu zinazotofautiana kulingana na watu, mawazo yao na uigaji wao.

Sema: Mwenyezi Mungu ni mwepesi zaidi wa kupanga njama, Hakika wajumbe wetu wanayaandika mnayoyapanga.

Makusudio ya njama za Mwenyezi Mungu ni kwamba yeye anawalipa wapanga njama kwa njama zao na kuwaandalia adhabu kali bila ya wao kutambua. Pia tumelizungumzia hilo katika Juz.3 (3:54).

Makusudio ya wajumbe waandishi ni Malaika. Maana ni kuwa Yeye Mwenyezi Mungu mtukufu anavidhibiti vitendo vya wenye njama na kuwalipa wanayostahiki.

Yeye ndiye anayewaendesha bara na baharini.

Yaani Yeye Mwenyezi Mungu mtukufu amempa mja wake uwezo wa kutembea humo. Makusudio ya ishara hii ni kukumbusha fadhila zake na nema zake ili awe katika wenye shukrani, “Utukufu ni wako ewe Mola wangu! Ni ubainifu ulioje wa ukarimu wako kwa anayekuridhisha na anayekuchukiza”

La kushangaza ni kauli ya Abu Bakr Al-mughafiri katika Kitabu Ahkamul- Qur’an, kwamba Aya hii inafahamisha kuwa usafiri wa baharini ni halali sio haramu; tena akarefusha maneno katika kutoa dalili ya uhalali wa kusafiri bahrini. Amesahau kuwa kawaida ya sharia, ambayo anaijua asiye- jua na Mjuzi, ni uharamu ndio unaohitajia dalili na sio uhalali.

Hata mnapokuwa majahazini na yakaenda nao upepo mzuri na wakaufurahia, mara upepo mkali ukawazukia yakawajia mawimbi kutoka kila upande na wakona wamekwishazongwa, basi hapo humwomba Mwenyezi Mungu kwa kumfanyia ikhlasi: ukituokoa na haya bila shaka tutatakuwa miongoni mwa wanaoshukuru.

Aya hii inafahamisha kuwa binadamu ana maumbile ya kumwamini Mungu kwa sababu ya kurejea kwake katika shida. Angalia kifungu: ‘Mwenyezi Mungu na maumbile’ katika Juz.7 (6:41).

Mwenye Al-manar amesema katika kufasiri Aya hii, ninamnukuu: “Washirikina walikuwa hawamuombi yeyote wakati wa shida, isipokuwa Mwenyezi Mungu muumba Mola wao. Ama waislamu wengi, zama hizi, hawamuombi Mwenyezi Mungu, kama wanavyodai hilo hao wenyewe, isipokuwa wanawaomba wafu; kama vile Badawiy, Rifai, Dasuqi, Jaylani, Almatbuli, Abu sarii na wengineo wasiokuwa na hisabu.

Na utawakuta wenye vilemba wa Azhar na wengineo hasa waangalizi wa makaburi yanayoabudiwa wakitumia wakfu na nadhiri zake kutoka kwa wale wanaowahadaa kwa shirki yao wakieguza jina katika Lugha ya kiarabu kwa kuiita tawassul n.k.” Mfano wa maneo haya yamo katika Tafsir ya Maraghi.

Nimesoma katika gazeti la Misri kuwa wamisri wanaandika karatasi wakizitupa kwenye kaburi la waliy, Humo wanaandika mashtaka ya wahasimu wao wakitaraji maiti awalipizie kisasi kutokana na dhulma na uovu walio- fanyiwa. Nimenukuu mashtaka haya katika kitabu Minhuna wa hunaka (Huku na huko).

Ama kuhusu mkusanyiko wa hafla ya mazazi ya walii, tuuchie gazeti la Aljumhuriya la tarehe 1-11-1968, likisema: “Msongamano ulikuwa kama siku ya kufufulia watu; ni kama mawimbi au shamba lililopandwa miti”

Lakini alipowaokoa, mara wanafanya jeuri katika ardhi pasipo haki.

Walimwahidi Mwenyezi Mungu kumcha na kumshukuru akiwaondolea, lakini alipowafanyia walivunja ahadi.

Hii inakariri aya iliyotangulia kwa ibara nyingine. Ile inasema wanazipangia njama Aya zetu na hii inasema wanafanya uovu katika ardhi. Maana ni moja au yanaoana. Lengo ni kuonyesha inadi yao na jeuriyao kwa picha mbaya.

Enyi watu! Hakika jeuri yenu itawarudia nyinyi wenyewe tu.

Kwani mwenye kuchomoa upanga wa jeuri atauliwa kwa huo.

Ni starehe ya maisha ya dunia kisha marejeo yenu ni kwetu ndipo tuwaambie mliyokuwa mkiyatenda.

Mjeuri anaweza kufurahi na kuburudika na ushindi, lakini ni wa muda; kisha inakuja balaa na hasara. Mtume(s.a.w.w) anasema: “Mambo matatu yanawarudia watu wake: Njama, njama za uovu hazimpati ila mwenyewe[4] .

Kuvunja ahadi, basi mwenye kuvunja ahadi anjivunjia ahadi mwenyewe[5] , Ujeuri, enyi watu! Hakika jeuri yenu itawarudia nyinyi wenyewe tu[6] .

إِنَّمَا مَثَلُ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا كَمَاءٍ أَنزَلْنَاهُ مِنَ السَّمَاءِ فَاخْتَلَطَ بِهِ نَبَاتُ الْأَرْضِ مِمَّا يَأْكُلُ النَّاسُ وَالْأَنْعَامُ حَتَّىٰ إِذَا أَخَذَتِ الْأَرْضُ زُخْرُفَهَا وَازَّيَّنَتْ وَظَنَّ أَهْلُهَا أَنَّهُمْ قَادِرُونَ عَلَيْهَا أَتَاهَا أَمْرُنَا لَيْلًا أَوْ نَهَارًا فَجَعَلْنَاهَا حَصِيدًا كَأَن لَّمْ تَغْنَ بِالْأَمْسِ كَذَٰلِكَ نُفَصِّلُ الْآيَاتِ لِقَوْمٍ يَتَفَكَّرُونَ ﴿٢٤﴾

24. Hakika mfano wa maisha ya dunia ni kama mfano wa maji tuliyoyateremsha kutoka mbinguni, kasha ikachanganyika na mimea ya ardhi wanayokula watu na wanyama. Mpaka ardhi ilipokamilisha uzuri wake na ikapambika. Na wenyeji wake wakadhani kuwa wana nguvu juu yake, amri yetu iliifkia usiku au mchana na tukaifanya imefyekwa, kama kwamba jana haikuweko. Namna hiyo tunazieleza Aya kwa watu wenye kufikiri.

وَاللَّـهُ يَدْعُو إِلَىٰ دَارِ السَّلَامِ وَيَهْدِي مَن يَشَاءُ إِلَىٰ صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍ ﴿٢٥﴾

25. Na Mwenyezi Mungu anaita kwenye nyumba ya amani, Na humwongoza amtakaye kwenye njia iliyonyooka.

MFANO WA MAISHA YA DUNIA

Aya 24-25

MAANA

Hakika mfano wa maisha ya dunia ni kama mfano wa maji tuliyoyateremsha kutoka mbinguni, kisha ikachanganyika na mimea ya ardhi.

Yaani dunia hii mnayoshindana nayo na kujifaharisha inafanana na mvua iliyotermka ardhini, ikapata rutuba na kuotesha aina za mimea zikachanganyika kutokana na wingi wake na kukua kwake.

Wanayokula watu na wanyama

Kila kiumbe hai kinalishwa na ardhi, inajaza matumbo yaliyo na njaa. Watu wanakula nafaka na mtunda na wanyama wanakula nyasi na vinginevyo.

Mpaka ardhi ilipokamilisha uzuri wake na ikapambika, kama harusi aliyejitengeza ili amfuruhishe harusi mwenzake,

Na wenyeji wake wakadhani kuwa wana nguvu juu yake na kuweza kutumia utajiri wake wakijaza mifuko yao na hazina zao. Baada ya mategemeo haya na kutuliaamri yetu iliifkia ya maafa na maangamizi,usiku au mchana na tukaifanya imefyekwa, kama kwamba jana haikuweko, kutokana na kuondoka kila kitu, haikubaki hata alama ya vilivyokuwepo, matumaini yote na ndoto zote zimeyayuka.

Namna hiyo tunazieleza Aya kwa watu wenye kufikiri kuwa starehe za dunia zinaisha na kwamba mwenye kuzitegemea basi atakuwa ametege- mea kwenye mawingu na kwamba hakuna haja ya kumwagiana damu, kuanzisha vita na kuzidhalilisha akili za wajuzi.

Na Mwenyezi Mungu anaita kwenye nyumba ya amani.

Wafasiri wamesema kuwa makusudio ya nyumba ya amni ni pepo. Hakuna mwenye shaka kuwa pepo ni nyumba ya wema na amani, lakini mwito wa Mwenyezi Mungu unaenea kwenye kila jambo litaklohakikisha raha kwa watu wake; bali Mwenyezi Mungu ameiharamisha pepo isipokuwa kwa watakaotumikia njia hii.

Na humwongoza amtakaye kwenye njia iliyonyooka.

Mwito wa Mwenyezi Mungu wa kutenda heri, unamwenea kila aliye baleghe na mwenye akili timamu bila ya kumtoa yeyote. Basi atakayeasi na akaipuuza atakuwa amepotea na mwenye kutii akaitenda, atakuwa amaeongoka. Inafaa kutegemezwa uongofu wake kwa Mwenyezi Mungu, kwa sababu njia ya kuufuata ilikuwa ni kwa amri ya Mwenyezi Mungu.

Ama upotevu wa aliyepotea, haifai kuutegemeza kwa Mwenyezi Mungu, kwa sababu ameukataza na Mwenyezi Mungu hawezi kukataza jambo kisha alielekeze lifuatwe.

لِّلَّذِينَ أَحْسَنُوا الْحُسْنَىٰ وَزِيَادَةٌ وَلَا يَرْهَقُ وُجُوهَهُمْ قَتَرٌ وَلَا ذِلَّةٌ أُولَـٰئِكَ أَصْحَابُ الْجَنَّةِ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ ﴿٢٦﴾

26. Kwa wafanyao wema ni wema na ziyada, Na vumbi halitafunika nyuso zao wala udhalili. Hao ndio watu wa Peponi; hao humo watadumu.

وَالَّذِينَ كَسَبُوا السَّيِّئَاتِ جَزَاءُ سَيِّئَةٍ بِمِثْلِهَا وَتَرْهَقُهُمْ ذِلَّةٌ مَّا لَهُم مِّنَ اللَّـهِ مِنْ عَاصِمٍ كَأَنَّمَا أُغْشِيَتْ وُجُوهُهُمْ قِطَعًا مِّنَ اللَّيْلِ مُظْلِمًا أُولَـٰئِكَ أَصْحَابُ النَّارِ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ ﴿٢٧﴾

27. Na wale waliochuma maovu, malipo ya uovu ni mfano wake. Na utawafunika udhalili, Hawatakuwa na wa kuwalinda na Mwenyezi Mungu. Kama kwamba nyuso zao zimefunikwa na kipande cha usiku wenye giza. Hao ndio watu wa motoni hao humo watadumu.

وَيَوْمَ نَحْشُرُهُمْ جَمِيعًا ثُمَّ نَقُولُ لِلَّذِينَ أَشْرَكُوا مَكَانَكُمْ أَنتُمْ وَشُرَكَاؤُكُمْ فَزَيَّلْنَا بَيْنَهُمْ وَقَالَ شُرَكَاؤُهُم مَّا كُنتُمْ إِيَّانَا تَعْبُدُونَ ﴿٢٨﴾

28. Na siku tutakayowakusanya wote, kisha tuwaambie wale walioshirikisha: Simameni mahali penu nyinyi na washirika wenu. Kisha tutawatenga baina yao. Na wao walioshirikisha watasema: Nyinyi hamkuwa mkituabudu sisi.

فَكَفَىٰ بِاللَّـهِ شَهِيدًا بَيْنَنَا وَبَيْنَكُمْ إِن كُنَّا عَنْ عِبَادَتِكُمْ لَغَافِلِينَ ﴿٢٩﴾

29. Mwenyezi Mungu anatosha kuwa shahidi baina yetu na nyinyi. Hakika sisi tulikuwa hatuna habari na ibada yenu.

هُنَالِكَ تَبْلُو كُلُّ نَفْسٍ مَّا أَسْلَفَتْ وَرُدُّوا إِلَى اللَّـهِ مَوْلَاهُمُ الْحَقِّ وَضَلَّ عَنْهُم مَّا كَانُوا يَفْتَرُونَ ﴿٣٠﴾

30. Huko kila nafsi itajua iliyoyatanguliza na watarudishwa kwa Mwenyezi Mungu, Mola wao wa haki, na yote waliyokuwa wakiyazua yatawapotea.

KWA WAFANYAO WEMA

Aya 26 – 30

MAANA

Kwa wafanyao wema ni wema na ziyada.

Razi anasema kuwa mfano wa Aya hii ni kauli yake Mwenyezi Mungu mtukufu:

هَلْ جَزَاءُ الْإِحْسَانِ إِلَّا الْإِحْسَانُ ﴿٦٠﴾

“Je, malipo ya hisani si ni hisani tu” (55:60).

Lakini ilivyo ni kwamba hisani inahusika na kumfanyia mtu mwingine, na wema ni ule unaopendeza kimaumbile, ni sawa uwe ni kumfanyia mwingine au la. Huo ni pamoja na itikadi njema, kauli njema vitendo vyema na nia njema; na hata kuhisi dhambi.

Yote hayo yanapendeza kwa Mwenyezi Mungu na kwa maumbile, naye Mwenyezi Mungu (s.w.t) ataulipa wema. Kwa hiyo basi Aya iko katika mfano wa kauli yake Mwenyezi Mungu mtukufu.

وَمَن يَقْتَرِفْ حَسَنَةً نَّزِدْ لَهُ فِيهَا حُسْنًا ﴿٢٣﴾

“Na anayefanya wema tutamzidishia wema…” (42:23).

Wametofautiana wafasiri katika maana ya ziada, Kwa sababu ikiwa ni katika aina ya wema basi si ziada na kama siyo basi neno litakuwa halijulikani. Lile tunalolifahamu ni kuwa makusudio ya ziada hapa ni kuwa yeye Mwenyezi Mungu mtukufu atawalipa wale waliofanya wema zaidi ya wanavyostahiki. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema:

فَأَمَّا الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ فَيُوَفِّيهِمْ أُجُورَهُمْ وَيَزِيدُهُم مِّن فَضْلِهِ ﴿١٧٣﴾

“Ama wale ambao wameamini na wakatenda mema,atawalipa ujira wao sawa, na atawazidishia kwa fadhila yake” Juz.6 (4:173)

Na vumbi halitafunika nyuso zao wala udhalili, Hao ndio watu wa Peponi; hao humo watadumu.

Kila kilichomo moyoni kiwe ni huzuni au furaha, amani au hofu, athari yake hudhihiri usoni wazi wazi, lakini athari ya hofu na kiherehere inadhi- hiri zaidi kuliko nyingineyo; hasa nyuso za watu wa motoni watakapouona. Zitasawajika kwa hofu; kama kwamba zimegubikwa na moshi au vumbi jeusi.

Ama watu wa Peponi nyuso zao zitacheka na kufurahi:

وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ مُّسْفِرَةٌ ﴿٣٨﴾ ضَاحِكَةٌ مُّسْتَبْشِرَةٌ ﴿٣٩﴾ وَوُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ عَلَيْهَا غَبَرَةٌ ﴿٤٠﴾ تَرْهَقُهَا قَتَرَةٌ ﴿٤١﴾

“Nyuso siku hiyo zitanawiri. Zitacheka na kufurahika. Na nyuso nyingin siku hiyo zitakuwa na vumbi. Zimefunikwa na weusi” (80:38–41).

Na wale waliochuma maovu, malipo ya uovu ni mfano wake.

Hakika Mwenyezi Mungu ni mwadilifu atamlipa anayefanya uovu anayostahiki; wala hatamdhulumu hata uzani wa sisimizi, bali atasamehe mengi. Kwa sababu yeye ni mkarimu; Na kwa ukarimu humwongezea mwenye kufanya wema ziada nyingi.

Na utawafunika udhalili.

Yaani fedheha itawafunika waovu, Hakuna mwenye kudhalilika na kufedheheka zaidi kuliko yule anayefed- heheka mbele ya watu.

Hawatakuwa na wa kuwalinda na Mwenyezi Mungu.

Kuwalinda na machukivu ya Mwenyezi Mungu na adhabu yake.

Kama kwamba nyuso zao zimefunikwa na kipande cha usiku wenye giza. Hao ndio watu wa motoni hao humo watadumu.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kusema kuwa watu wema hazitafu- nikwa nyuso zao na vumbi wala udhalili, anasema kuwa wale waovu nyuso zao zitasawajika, kama kwamba ni kipande cha usiku.

Imam Ali(a.s ) amesema:“Heri siyo heri ikiwa baada yake ni moto; na shari si shari ikiwa baada yake ni Pepo , Na kila neema isiyokuwa Pepo ni kazi bure na kila balaa isiyokuwa moto ni nafuu”.

Na siku tutakayowakusanya wote, wale walioefanya wema na, wale waliofanya uovu;kisha tuwaambie wale walioshirikisha: Simameni mahali penu nyinyi na washirika wenu.

Kesho watasimama kwa hisabu, washirikina na wale waliokuwa wakidai kuwa ni washirika wa Mwenyezi Mungu; watakabiliana uso kwa uso ili kila kikundi kitoe dalili kwa hoja yake. Hapo yatayeyuka matumaini waliyokuwa wakiyatamani washirikina na kutaraji manufaa na itawabainikia kuwa wao walikuwa kwenye upotevu katika kushirikisha kwao na inadi yao kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu na vitabu vyake.

Kisha tutawatenga baina yao

Yaani Mwenyezi Mungu (s.w.t), siku ya Hisabu, atapambanua viumbe vyake vyote kwa sifa zao walizo nazo, na kudhihirisha hakika ya kila mmoja. Hapo itawabainikia washirikina kwamba hakuna yeyote anayeza kujidhuru yeye au mwingine au kujinufaisha na kwamba amri ni ya Mwenyezi Mungu peke yake hana mshirika wala mpinzani.

Na wao walioshirikisha watasema: Nyinyi hamkuwa mkituabudu sisi.

Wakati Mwenyezi Mungu atakapowasimamisha, mahali pamoja, washirik- ina na wale waliokuwa wakiwaabudu, na kukabiliana uso kwa uso, wataambiana: Nyinyi hamkuwa mkituabudu sisi; isipokuwa ni mawazo yenu kuwa Mwenyezi Mungu ana washirika na kwamba sisi ndio hao washirika walio katika mawazo yenu tu. Kwa hakika nyinyi hamwabudu chochote, na sisi ni chochote; kwa hiyo hamtuabudu sisi.

Mwenyezi Mungu anatosha kuwa shahidi baina yetu na nyinyi

Yeye anajua kuwa hao washirika mliowazua kwenye mawazo yenu hawako, Vile vile anajua kuwa sisi tuko mbali na huo ushirikina wenu.

Hakika sisi tulikuwa hatuna habari na ibada yenu.

Hatujui chochote. Hiyo ni kuashiria kukana kuabudiwa na kwamba wao ni waabudu sio waabudiwa.

Huko kila nafsi itajua iliyoyatanguliza na watarudishwa kwa Mwenyezi Mungu, Mola wao wa haki, na yote waliyokuwa wakiyazua yatawapotea.

Yaani Mwenyezi Mungu Mtukufu atawakusanya watu kuwahesabu na kumlipa kila mtu aliyoyachuma, wala hatakuta kile alichokuwa akikiitakidi na kukiwazia kuwa kinafaa na kumkinga; isipokuwa mtendo ya ikhlasi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu peke yake. Maana haya yamekaririka kwa mifumo mbali mbali katika Aya kadhaa.