TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MOJA Juzuu 11

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MOJA0%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MOJA Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MOJA

Mwandishi: Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 9786
Pakua: 1439

Maelezo zaidi:

Juzuu 11
Juzuu 1
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 15 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 9786 / Pakua: 1439
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MOJA

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MOJA Juzuu 11

Mwandishi:
Swahili

8

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MOJA

قُلْ مَن يَرْزُقُكُم مِّنَ السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ أَمَّن يَمْلِكُ السَّمْعَ وَالْأَبْصَارَ وَمَن يُخْرِجُ الْحَيَّ مِنَ الْمَيِّتِ وَيُخْرِجُ الْمَيِّتَ مِنَ الْحَيِّ وَمَن يُدَبِّرُ الْأَمْرَ فَسَيَقُولُونَ اللَّـهُ فَقُلْ أَفَلَا تَتَّقُونَ ﴿٣١﴾

31. Sema: Ninani anayewaruzuku kutoka mbinguni na ardhini? Au ni nani anayemiliki usikizi na uoni na ni nani amtoaye hai kutoka maiti na akamtoa maiti kutoka aliye hai na ni nani anayedabiri mambo yote? Watasema ni Mwenyezi Mungu. Waambie: Basi je hamchi?

فَذَٰلِكُمُ اللَّـهُ رَبُّكُمُ الْحَقُّ فَمَاذَا بَعْدَ الْحَقِّ إِلَّا الضَّلَالُ فَأَنَّىٰ تُصْرَفُونَ ﴿٣٢﴾

32. Basi huyo ndiye Mweyezi Mungu Mola wenu, tena ni nini baada ya haki isipokuwa upotevu? Basi mnageuzwa wapi.

كَذَٰلِكَ حَقَّتْ كَلِمَتُ رَبِّكَ عَلَى الَّذِينَ فَسَقُوا أَنَّهُمْ لَا يُؤْمِنُونَ ﴿٣٣﴾

33. Hivyo ndivyo lilivyothibiti neon la Mola wako juu ya wale waliofanya ufuska kwamba hataamini.

قُلْ هَلْ مِن شُرَكَائِكُم مَّن يَبْدَأُ الْخَلْقَ ثُمَّ يُعِيدُهُ قُلِ اللَّـهُ يَبْدَأُ الْخَلْقَ ثُمَّ يُعِيدُهُ فَأَنَّىٰ تُؤْفَكُونَ ﴿٣٤﴾

34. Sema: Je, katika Miungu yenu ya ushirikina yuko anayeanzisha kuumba viumbe kasha akakirejesha? Sema: Mwenyezi Mungu ndiye anayeanzisha kuumba kiumbe kasha akakirejesha, Basi mnadanganywa vipi?

NI NANI ANAYEWARUZUKU?

Aya 31 – 34

MAANA

Nguzo za imani ya haki kwa Mwenyezi Mungu ni tatu: Umoja, Utume na Ufufuo, Qur’ani imeonyesha aina mbali mbali za dalili ya nguzo hizi. Umetangulia ubainifu wake kwa ufanuzi pamoja na Aya hii tunayoifasiri sasa na iliyo baada yake.

Kwani Aya hizi zimekuja kubatilisha ushirikina na madai ya washirikina kuwa masanamu yao yanawakuribisha kwa Mwenyezi Mungu na kwamba hakuna ufufuo wala hisabu, na Qur’ani ni uzushi wa Muhammad kwa Mwenyezi Mungu. Yafuatayo ni kubadilisha madai hayo:

Sema: Ni nani anayewaruzuku kutoka mbinguni na ardhini?

Kila sababu miongoni mwa sababu za riziki, iwe yakaribu au mbali, haina budi kuwa ni ya mbinguni au ya kiardhi. Miongoni mwa sababu za mbingu ni mvua mwangaza na mengineyo ambayo wameyangudua wataalamu au watakuja kuyagundua. Na, katika sababu za ardhi ni mimea, wanyama na madini.

Sababu zote hizo zinarudia kwa Mwenyezi Mungu peke yake kupita desturi za kiulimwengu; kwa sababu yeye Mwenyezi Mungu mtukufu ndiye muumbaji; na washirikina wanajua hakika hii na kukiri kuwa Mwenyezi Mungu ndiye muumbaji mwenye kuruzuku.

Kwa hiyo hapa linakuja swali kuwa:

Enyi Washirikina! Maadamu mnaitakidi kuwa Mwenyezi Mungu ndiye muumbaji mwenye kuruzuku, vipi mnamfanyia washirika? Vipi kitu kinaweza kuwa mshirika, na inajulikana kuwa hakina athari naye kabisa? Je, inafaa wewe msomaji uwe mshirika wangu katika kutunga kitabu hiki, na mimi ndiye niliyefikiri, nikavumilia na kuandika?

Tumefafanua maudhui haya katika Juz. 5 (4: 48)

Au ni nani anayemiliki usikizi na uoni?

Mwenyezi Mungu amezihusisha hizi mbili, kwa sababu ndizo nyenzo za kwanza za kupata elimu; hata nadharia pia inatokana na hizo kwa sababu nadharia inakomea kwenye hisia na kuona, Razi anasema katika kufasiri Aya hii.

“Ali (r.a.) alikuwa akisema: “Utakatifu ni wa yule aliyeufanya uoni kwa shahamu na akaufanya usikizi kwa mifupa na akatamkisha kwa nyama”

Ni nani amtoaye hai kutoka maiti na akamtoa maiti kutoka aliyehai.

Yaani anayemiliki mauti na uhai. Miongoni mwa mifano ya kutoa hai kati- ka maiti ni vinavyoliwa na wanyama na kupitia matumboni kisha vinasagwa hatimae zinapatikana chembe mpya za uhai. Na mfano wa kutoa maiti katika hai ni kufa chembe ambazo zinatokana na mwili ulio hai kwa kupumua. Tumezugumza kwa ufafanuzi katika Juz.7 (4:95) kifungu cha ‘uhai umetoka wapi?’

Na ni nani anayeyadabiri mambo yote yaliyo katika ulimwengu?

Watasema ni Mwenyezi Mungu , Waambie basi je hamchi katika washirika mliowazusha?

Wao hawakatai kuwa Mwenyezi Mungu ni Mmoja aliyepeke yake, anayeruzuku, anayemiliki usikizi, uoni, mauti, uhai, na mambo yote. Lakini pamoja na hayo wanamfanyia Mwenyezi Mungu washirika.

Siri ya mgongano huu ni kwamba wao wanamtazama muumba kwa mtazamo wa kimaudhui. Wameamini kuwa yeye ndiye muumba na mwenye kupatisha vitu vyote; kisha wakatazama yale yatakayowakurubisha kwake kwa mtazamo wa kimapenzi yao, wakakosea. Badala ya kujikurubisha kwake kwa vitendo na ikhlasi, wamemzuishia washirika na wakajikurubisha kwa hao wanaowashirikisha

Basi huyo ndiye Mweyezi Mungu Mola wenu, tena ni nini baada ya haki isipokuwa upotevu?

Hakuna usaidizi baina yao; ama haki na uongofu au batili na upotevu. Na Mwenyezi Mungu (s.w.t) ndiye aliyeumba mbingu na ardhi ambazo ndani yake mna sababu za riziki. Na akaumba usikizi na uoni kwa haki ambazo ndio njia za elimu.

Na yeye anamiliki mauti na uhai kwa haki. Milki hiyo ni dalili ya uwezo na cheo. Naye ndiye mpangaji wa mambo kwa haki, ambako kunafahamisha elimu na hekima. Basi kuna nini tena baada haya yote isipokuwa upotevu, batili, ujinga na inadi.

Basi mnageuzwa wapi kuiacha haki na Tawhid na kufuata upotevu na kufuata shirk? Hivyo ndivyo lilivyothibiti neno la Mola wako juu ya wale waliofanya ufuska.

Hiyo ni ishara ya yale yaliyotangulia kwamba hakuna baada ya haki isipokuwa upotevu. Makusudio ya neno la Mola wako hapa ni adhabu; kama alivyosema Mwenyezi Mungu:

قَالُوا بَلَىٰ وَلَـٰكِنْ حَقَّتْ كَلِمَةُ الْعَذَابِ عَلَى الْكَافِرِينَ ﴿٧١﴾

“Lakini limekwishathibiti neon la haki kwa makafiri”(39:71).

Makusudio ya waliofanya ufuska ni washirikina. Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu atawaadhibu washirikina, adhabu ya mwenye kuifanyia inadi haki na akakataa imani kabisa. Hiyo ndiyo stahiki yao kwani walipewa mwito wa Tawhid, zikawasimamia hoja na ubainifu, lakini pamoja na hayo walig’ang’ania shirki na wakafa nayo.

Sema: Je, katika Miungu yenu ya ushirikina yuko anayeanzisha kuumba viumbe kisha akakirejesha? Sema: Mwenyezi Mungu ndiye anayeanzisha kuumba kiumbe kisha akakirejesha, Basi mnadanganywa vipi?

Yaani sema ewe Muhammad kuwaambia washirikina kuwa Mungu anaumba kitu bila ya kutumia kitu, anamrudishia uhai aliyekufa, Je hao mnaomshirikisha naye wanaweza hilo? Ikiwa hawawezi, basi inakuwaje mnaiacha Tawhid na kuifuata shirk?

Unaweza kuuliza kuwa : hoja ya kuumba iko wazi kwa washirikina, kwa vile wanakubali hilo, lakini hoja ya kurudisha uhai haiko wazi na hilo ndilo jambo wanalolipinga, kuwa hakuna ufufuo, Sasa kuna wajihi gani hapo?

Jibu : Qur’ani katika Aya kadhaa imeleta hoja za kutosha kuhusu kurudishwa uhai na ufufuo kwa ujumla na washirikina wakashindwa kuzijibu. Kushindwa kwao huko ndiyo hoja iliyowalazimu; kwamba Mwenyezi Mungu atavirudisha viumbe kama alivyovianzisha.Kwa maneno mengine ni kuwa hukumu inasimama kwa dalili sio kusalimu amri yule anayehukumiwa.

قُلْ هَلْ مِن شُرَكَائِكُم مَّن يَهْدِي إِلَى الْحَقِّ قُلِ اللَّـهُ يَهْدِي لِلْحَقِّ أَفَمَن يَهْدِي إِلَى الْحَقِّ أَحَقُّ أَن يُتَّبَعَ أَمَّن لَّا يَهِدِّي إِلَّا أَن يُهْدَىٰ فَمَا لَكُمْ كَيْفَ تَحْكُمُونَ ﴿٣٥﴾

35. Sema: Je, katika Miungu yenu ya ushirikina yuko aongozaye kwenye haki? Sema: Mwenyezi Mungu ndiye aongozaye kwenye haki Basi je anayestahiki kufuatwa ni yule aongozaye kwenye haki au ni Yule asiyeongoka isipokuwa aongozwe? Basi mni nini nyinyi? Mna hukumu vipi?

وَمَا يَتَّبِعُ أَكْثَرُهُمْ إِلَّا ظَنًّا إِنَّ الظَّنَّ لَا يُغْنِي مِنَ الْحَقِّ شَيْئًا إِنَّ اللَّـهَ عَلِيمٌ بِمَا يَفْعَلُونَ ﴿٣٦﴾

36. Na wengi wao hawafuati isipokuwa dhana tu. Hakika dhana haifai kitu mbele yake haki, Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa wanayoyatenda.

وَمَا كَانَ هَـٰذَا الْقُرْآنُ أَن يُفْتَرَىٰ مِن دُونِ اللَّـهِ وَلَـٰكِن تَصْدِيقَ الَّذِي بَيْنَ يَدَيْهِ وَتَفْصِيلَ الْكِتَابِ لَا رَيْبَ فِيهِ مِن رَّبِّ الْعَالَمِينَ ﴿٣٧﴾

37. Na haikuwa Qur’ani hii imezushwa, kuwa haitoki kwa Mungu. Lakini inasadikisha yaliyotangulia na ni ufafanuzi wa kitab. Haina shaka imetoka kwa Mola wa viumbe vyote.

أَمْ يَقُولُونَ افْتَرَاهُ قُلْ فَأْتُوا بِسُورَةٍ مِّثْلِهِ وَادْعُوا مَنِ اسْتَطَعْتُم مِّن دُونِ اللَّـهِ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ﴿٣٨﴾

38. Je, wanasema ameizuwa? Sema: Basi leteni Sura moja mfano wake na muwaite muwawezao asiyekuwa Mwenyezi Mungu, ikiwa nyinyi ni wakweli.

بَلْ كَذَّبُوا بِمَا لَمْ يُحِيطُوا بِعِلْمِهِ وَلَمَّا يَأْتِهِمْ تَأْوِيلُهُ كَذَٰلِكَ كَذَّبَ الَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ فَانظُرْ كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ الظَّالِمِينَ ﴿٣٩﴾

39. Bali wamekadhibisha wasiyoyajua elimu yake, Kabla haujawajia ufafanuzi wake, Kadhalika walikanusha waliokuwa kabla yao Basi angalia jinsi ulivyokuwa mwisho wa madhalimu.

MWENYE KUONGOZA KWENYE HAKI

Aya 35 – 39

MAANA

Sema: Je, katika Miungu yenu ya ushirikina yuko aongozaye kwenye haki?

Aya hii nikumfunga mdomo yule anayeabudu pamoja na Mwenyezi Mungu waungu wengine. Njia ya kufunga huko ni kwamba sifa ya kwanza anayotakikana kuwa nayo yule mwenye kuabudiwa ni kuwa yeye mwenyewe anaongoza kwenye haki bila ya kutegemea mwongozo wa mwingine, Ama yule asiyeongoza kwenye haki hastahiki uungu kabisa. Hakika hii ni wazi haina ubishi.

Kwa hiyo Mwenyezi Mungu amemwamrisha Mtume wake Muhammad(s.a.w.w.) kuwahoji washirikina na kuwatupia swali hili, kwamba je, katika masanamu yenu haya mnayoyaabudu anapatikana anayeweza kuongoza kwenye haki? Hakuna mwenye shaka kwamba wao hawakuthubutu kujibu hili.

Kwa sababu masanamu yao ni mawe tu, waliyoyatengeneza kwa mikono yao, kwa vile Mtume(s.a.w.w.) anayo hoja mkataa kwamba Mwenyezi Mungu ndiye anayeongoza kwenye haki, ndipo akalielekeza swali hili kwao.

Sema: Mwenyezi Mungu ndiye aongozaye kwenye haki sio mwingine.

Na mwongozo huo ni wake mwenyewe hautokani na mwingine. Dalili ya kuwa Mwenyezi Mungu anaongoza kwenye haki ni Mitume aliowatuma kwa waja wake wakitoa bishara na kuonya.

Vile vile vitabu alivyowateremshia ambavyo ndani yake mna Aya zinazobainisha ambazo zinawaon- goza watu kwenye shari yao na wema wao.

Huyu hapa Muhammad anawakabili washirikina ana kwa ana na aki- washinda kwa Qur’ani ambayo ndani yake mna ubainifu wa kila kitu.

Basi wako wapi wajumbe wa waungu wenu wa kishirikina? Viko wapi vitabu vyao, Lau Mwenyezi Mungu angelikuwa na mshirika, tungelimwona Mtume wake.

Ilivyo ni kwamba lengo sio kumlinganisha Mwenyezi Mungu, Mtume na masanamu, hapana! Ispokuwa lengo ni kuwaamsha washirikina na kuwazindua ujinga wao na upotevu wao, huenda wakazinduka.

Basi je anayestahiki kufuatwa ni yule aongozaye kwenye haki au ni yule asiyeongoka isipokuwa aongozwe?

Baada ya Mwenyezi Mungu kutaja utangulizi huu, hapa anabainisha natija yake, kwamba Mwenyezi Mungu peke yake ndiye anayestahiki kufuatwa, si mwingine.

Natija hii anaidokeza kwa swali lenye jawabu lake; nalo ni: Ni nani anayestahiki kufuatwa na kuongoza? Je, ni Mwenyezi Mungu anayeongoza yeye mwenyewe au ni waungu wenu wa ushirikina wanaongozwa?

Unaweza kuuliza kuwa : washirikina wa Makka wanaoambiwa maneno walikuwa wakiabudu masanamu na inajulikkana wazi kuwa masanamu hayo ni mawe ambayo hayawezi kuongozwa na walimu wala viongozi. Sasa kuna wajihi gani wa kauli ya Mwenyezi Mungu, ‘isipokuwa aongozwe?’

Wafasiri wamejibu kuwa hii ni haki ya kufaradhia na kukisia tu; yaani tufaradhie kuwa lau hayo masanamu yenu yangekuwa yanaongoza si ya takua hayo yenyewe yamefanywa kuongozwa? Na anayekuwa hivyo basi hafai kuwa Mwenyezi Mungu.

Jibu : zuri ni kuwa Aya haikuwashukia washirikina wa Makka peke yao, bali imewashukia wao, na wale wanaoabudu watu au Malaika n.k.

Kwa hiyo maana yanakuwa, kila asiyeweza kuongoza, basi hastahiki kuwa Mungu ni sawa awe hana uwezo wa kuongoza hata kwa kuongozwa; kama mawe, au anaweza kuongoza baada ya kuongozwa; kama binadamu na Malaika, Wote hao hawastahiki kuwa Mungu.

Basi mna nini nyinyi? Mnahukumu vipi?

Mnaamini upotevu na hali dalili ya ubatilifu na ufisadi wake iko wazi

Na wengi wao hawafuati isipokuwa dhana tu.

Wengi wao ni washirikina. Kwa sababu kulikuwa na baadhi ya washirikina waliokuwa na yakini na kukubali ukweli na utume wa Muhammad na wakijua fika kuwa masanamu yao si chochote, lakini wakafanya inadi na kiburi kwa kuchunga masilahi yao na vyeo vyao. Ama wengine ambao ndio wengi walikuwa wakiabudu masanamu kwa kufuata na kuwaiga wazazi wao.

Mwenyezi Mungu ameitolea ibara ya dhana, ibada yao hii, pamoja na kuwa wenyewe walikuwa na yakini kuwa masanamu yao yanadhuru na kunufaisha.

Kwa sababu yakini yao hii haina msingi wa usahihi, Na kila yakini inayotegemea kuiga inafaa kuitolea ibara ya dhana. Tumefafanua zaidi kuhusu kufuata na kuiga tulipofasiri Juz. Baqara (2:170).

Hakika dhana haifai kitu mbele yake haki.

Makusudioa ya dhana hapa sio kutokuwa na uhakika, kama inavyoonyesha katika ibara iliyopita, isipokuwa makusudio yake hapa ni kuamini msingi wowote katika misingi ya dini au tawi katika matawi yake bila ya dalili ya kiakili au ya wahyi; hata kama imani hiyo itaaminiwa kiuhakika; kama vile kuiga washirikina katika kuabudu masanamu na ulahidi kabla ya kufanya utafiti na kuchunguza sababu za kuweko ulimwengu na kupatikana kwake na nidhamu iliyoko ndani yake. Je ilikuwa kwa sadfa au kwa mpango wa mwenye ujuzi na hekima?

Aya hii ni dalili wazi ya kupinga kiyasi (kukisia) na kuwa haifai katika masuala ya dini. Kwa sababu kiyasi ni kutumia dhana ambayo haifai kitu mbele ya haki katika misingi ya kiitikadi na hukumu za sharia.

Ama maswala ya dunia yako nje ya maudhui ya Aya, Vipi Mungu atakataza dhana katika kilimo, biashara na mafungamano ya kijamii. Lau watu wangelingoja elimu na yakini katika kila kitu basi maisha yangedumaa Hata hivyo haifai kumtuhumu mtu na kosa au kuwa shahidi ila baada ya kujua na kupata yakini. Siri ya hilo ni kuyapeleka maisha kwenye njia iliyo sawa.

Kwa ufupi katika mambo ya kidunia kuna maswala ambayo inafaa kufuata dhana na ambayo haifai kufuata dhana na mengine kuna hiyari. Mwenye kutaka kujua ufafanuzi wa hayo na asome kitabu Faraidil-Usul kinachojulikana kama Arrasul cha Sheikh mkuu, Al-Answari. Yeye amezama sana kwenye utafiti wa suala hili na ameandika karibu kurasa

Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa wanayoyatenda

Hili ni kemeo kwa washirikina ambao wanafuata dhana katika kuabudu masanamu na kumkadhibisha Mtume(s.a.w.w) bila ya kuipima dhana yao hii kwa kipimo cha maumbile na akili. Vile vile ni kemeo kwa kila anayefuata dhana katika mambo ya dini.

Na haikuwa Qur’ani hii imezushwa kuwa haitoki kwa Mungu.

Kwa sababu ya mfumo wake wa ajabu na yale yaliyomo ndani yake; kama elimu, sharia ya watu, adabu za kijamii, kutolea habari mambo ya ghaib na mengineyo ambayo ni muhali kuwa hayakutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Lakini inasadikisha yaliyotangulia katika vitabu vya Mwenyezi Mungu, Na ni ufafanuzi wa kitab.

Makusudio ya kitab hapa ni kila sharia aliyoiweka Mwenyezi Mungu ambayo binadamu anaihitajia kwa ajili ya wema wake wa dunia na akhera.

Haina shaka imetoka kwa Mola wa viumbe vyote.

Yaani haitakikani kwa mwenye akili kutia shaka katika Kitab cha Mwenyezi Mungu, kikiwa kimekusanya miujiza na Aya zinazokubalika na kila mwenye umbile safi na akili iliyo salama.

Je, wanasema ameizuwa? Sema: Basi leteni Sura moja mfano wake na muwaite muwawezao asiyekuwa Mwenyezi Mungu, ikiwa nyinyi ni wa kweli.

Yametangulia maelezo yake kwa ufafanuzi zaidi katika Juz.1(2:23)

Bali wamekadhibisha wasiyoyajua elimu yake.

Ndivyo ilivyo kwa asiyejua, kufanya haraka kusadikisha na kukadhibisha, kabla ya kufanya uchunguzi.

Kusema kwake Mwenyezi Mungu: ‘Wasiyoyajua elimu yake,’ ni ishara ya kwamba akili haiwezi kuthibitisha kitu au kukanusha ila baada ya kukisoma kwa utulivu kwa darasa kamili inayokusanya pande zake zote.

Kabla haujawajia ufafanuzi wake,

Yaani washirikina waliikanusha Qur’ani kabla ya kujua uhakika wake na siri zake. Lau wao wangeyatilia maanani mafunzo yake na hukumu yake, basi wangeliisadiki, ikiwa wanatafuta uhakika.

Imeelezwa katika Tafsir Majmaul-bayan: “Inasemekana kuwa Amirul- mumini, Ali(a.s ) alichukua kutokana na Aya hii kauli yake:‘Watu ni maadui wa wasiyoyajua.’ Na kauli yake:‘Thamani ya mtu ni yale anayoyajua, ’ aliichukuwa katika Aya isemayo:

فَأَعْرِضْ عَن مَّن تَوَلَّىٰ عَن ذِكْرِنَا وَلَمْ يُرِدْ إِلَّا الْحَيَاةَ الدُّنْيَا ﴿٢٩﴾ ذَٰلِكَ مَبْلَغُهُم مِّنَ الْعِلْمِ ﴿٣٠﴾

“Basi mwachilie mbali yule aupaye kisogo ukumbusho wetu na wala asitake ila maisha ya dunia. Huo ndio mwisho wao wa ujuzi” (53:29–30)

Na kauli yake isemayo: ‘Zungumzeni mtajulikana’ aliitoa katika Aya:

وَلَتَعْرِفَنَّهُمْ فِي لَحْنِ الْقَوْلِ ﴿٣٠﴾

“Na hakika utawafahamu kwa namna ya usemi.” (47:30).

Kadhalika walikanusha waliokuwa kabla yao; kama vile watu wa Nuh, Adi, Thamud nk, waliokanusha Mitume yao kabla ya kujua uhakika wa heri na mwongozo waliokuja nao.

Basi angalia jinsi ulivyokuwa mwisho wa madhalimu katika maangamizi na mabalaa.

فَقُطِعَ دَابِرُ الْقَوْمِ الَّذِينَ ظَلَمُوا وَالْحَمْدُ لِلَّـهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿٤٥﴾

“Ikakatwa mizizi ya watu waliodhulumu; na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola wa viumbe vyote.” (6:45)

وَمِنْهُم مَّن يُؤْمِنُ بِهِ وَمِنْهُم مَّن لَّا يُؤْمِنُ بِهِ وَرَبُّكَ أَعْلَمُ بِالْمُفْسِدِينَ ﴿٤٠﴾

40. Na miongoni mwao wapo wanaoiamini, na miongoni mwao wapo wasioiamini. Na Mola wako anawajua sana wafisadi.

وَإِن كَذَّبُوكَ فَقُل لِّي عَمَلِي وَلَكُمْ عَمَلُكُمْ أَنتُم بَرِيئُونَ مِمَّا أَعْمَلُ وَأَنَا بَرِيءٌ مِّمَّا تَعْمَلُونَ ﴿٤١﴾

41. Na kama wakikudhabisha, basi sema: Mimi nina amali yangu na nyinyi mna amali yenu. Nyinyi hamna jukumu kwa ninayoyatenda, na mimi sina jukumu kwa mnayoyatenda.

وَمِنْهُم مَّن يَسْتَمِعُونَ إِلَيْكَ أَفَأَنتَ تُسْمِعُ الصُّمَّ وَلَوْ كَانُوا لَا يَعْقِلُونَ ﴿٤٢﴾

42. Na miongoni mwao wapo wanaokusikiliza, Je, wewe unaweza kuwasikilizisha viziwi ingawa hawafahamu?

وَمِنْهُم مَّن يَنظُرُ إِلَيْكَ أَفَأَنتَ تَهْدِي الْعُمْيَ وَلَوْ كَانُوا لَا يُبْصِرُونَ ﴿٤٣﴾

43. Na miongoni mwao wapo wanaokutazama, Je, wewe unaweza kuwaogoza vipofu ingawa hawaoni?

إِنَّ اللَّـهَ لَا يَظْلِمُ النَّاسَ شَيْئًا وَلَـٰكِنَّ النَّاسَ أَنفُسَهُمْ يَظْلِمُونَ ﴿٤٤﴾

44. Hakika Mwenyezi Mungu hadhulumu watu chochote, lakini watu wanajidhulumu wenyewe.

MIONGONI MWAO WAPO WANAOAMINI

Aya 40 – 44

MAANA

Na miongoni mwao wapo wanaoiamini na miongoni mwao wapo wasioamini.

Dhamir katika miongoni mwao inarudi kwa washirikina na inayoaminiwa ni Qur’ani. Maana ni kuwa washirikina kwa mtazamo wa Kiqur’ani wako mafungu mawili: Kuna walioacha ushirikina na kuamini Kitabu cha Mwenyezi Mungu kwa ikhlasi. Kimsingi ni kuwa kuamini Kitabu cha Mwenyezi Mungu ndio kumwamini Mohammad(s.a.w.w) .

Na wengine wameng’ang’ania ushirikina kwa inadi na kupupia manufaa. Hawa ndio wale aliowakemea Mwenyezi Mungu kwa kusema:

Na Mola wako anawajua sana wafisadi.

Hii inaonyesha kuwa neno mfisadi halimuhusu yule anayewafitini watu au kuwafanyia uovu bali linamuhusu kila aliyejua haki na asiitumie.

Na kama wakikudhabisha, basi sema: Mimi nina amali yangu na nyinyi mna amali yenu. Nyinyi hamna jukumu kwa ninayoyatenda, na mimi sina jukumu kwa mnayoyatenda.

Waumini wengi wameniuliza kuhusu jukumu lao kwa watoto wao waliopotea na wakaipuuza dini na hukumu yake.

Nikawajibu kuwa ni jukumu la mzazi kuwalea wanawe wadogo malezi ya kidini na awakuze kwenye misingi ya dharura ya dini, awaeleze misingi ya kiitikadi na kuwazowesha ibada za wajib; kama vile swala na saumu n.k. Vile vile kuwajulisha mambo ya haramu; kama uwongo, kusengenya, ulevi n.k.

Wakifikia makamo ya kujiongoza, basi awe kama muonyaji na mtoa bishara, Ikiwa hawataitikia mwito wake; basi yeye hana lawama mbele ya Mwenyezi Mungu.

Kisha nikawasome Aya hii na Aya nyingine iliyo na maana hii na Hadith; kama kauli yake Mwenyezi Mungu: “Na sema: Hii ni haki itokayo kwa Mola wenu, basi atakaye na amini na asiyetaka na akatae” (18:29) Mtume Mtukufu(s.a.w.w) anasema:

“Mtoto ni bwana wa miaka saba na mtumwa wa miaka saba na waziri wa miaka saba. Tosheka na tabia yake kwa miaka 21 vinginevyo achana naye, umeshatekeleza majukumu yako kwa Mwenyezi Mungu”

Yaani mtoto ataachwa katika miaka saba ya mwanzo kwa sbabu ya udogo wake na atatiwa adabu katika miaka saba ya pili; kama mtu asiyekuwa na hiyari na ataelekezwa katika miaka saba ya tatu; kama mtu huru. Kusema achana naye ni kukata tamaa, na kwamba mzazi hana majukumu juu ya uovu wa mwanawe.

Na miongoni mwao wapo wanaokusikiliza.

Yaani katika washirikina au wanaokadhibisha wapo wanaomsikiliza Mtume(s.a.w.w) kwa masikio tu. Ama nyoyo zao na akili zao ziko mbali naye, sawa na asiyesikia.

Je, wewe unaweza kuwasikilizisha viziwi, ingawa hawafahamu maneno ya Mwenyezi Mungu na maneno yako ewe Mtume? Yule anayesikia na asifahamu au anayefahamu na asisikie, Mwenyezi Mungu amemweka daraja ya asiyesikia.

Kwa sababu lengo la hisia za kusikia ni kufaidika na kunufaika nazo. Ikiwa lengo hilo halikutimia, basi ni sawa na kutokuwepo hizo hisia.

Na miongoni mwao wapo wanaokutazama kwa macho yao lakini hawajui cheo chako na daraja yako ewe Mtume; kama kwamba hawana macho.

Je, wewe unaweza kuwaongoza vipofu ingawa hawaoni?

Yaani kama ambavyo huwezi kumfanya kiziwi asikie na kipofu aone, basi vile vile huwezi kumwongoza na Qur’ani yule anayekusikiliza na kukuangalia kwa sababu ya malengo yake na tamaa yake. Walisema wahenga: “Tamaa inapofusha na kufanya uziwi.”

Hakika Mwenyezi Mungu hadhulumu watu chochote, lakini watu wanajidhulumu wenyewe.

Hilo halina shaka kwani Mwenyezi Mungu amewapa uwezo na utambuzi, akawabainishia njia ya kheri na ya shari, akawakataza hili akawaamrisha lile na akawapa hiyari. Basi atakayemtii Mwenyezi Mungu atakuwa amejichagulia yeye mwenyewe kuokoka na atakaye asi atakuwa amejichagulia kuangamia.

Ni ajabu kuwa hakika hii imefichika kwa Ashaira na ikadhihirika kwa Iblis mlanifu, pale atakapowaambia wafuasi wake siku ambayo haitakuwa na ubishi wala hadaa:

فَلَا تَلُومُونِي وَلُومُوا أَنفُسَكُم ﴿٢٢﴾

“Msinilaumu bali jilaumuni wenyewe” (14:22).