Site ya Al-Imaamaini Al-Hassanaini (A.S) ya usambazaji wa utamaduni wa Kiislamu na mafunzo ya Kidini

MI’RAJ UN-NABII

0 Voti 00.0 / 5

MI’RAJ UN-NABII
Qur’an Tukufu, Surah Bani – Israil, 17, Ayah:1
Kwa jina la Allah swt Mwingi wa Rehema na Ne’ema.
“Utukufu ni wake Yeye ambaye alimpeleka Mja wake usiku (mmoja tu ) kutoka Msikiti Mtukufu (wa Makka) mpaka Msikiti wa mbali (wa Baytul Mugaddas-Falastini) ambao (tumeubariki na ) tumevibariki vilivyoko pembezoni mwake. (Tulimpeleka hivyo) ili tumwonyeshe baadhi ya Alama zetu.
Hakika yeye Allah swt ni mwenye kusikia (na ) Mwenye kuona.
Umri wa Mtume Muhammad Mustafa bin ‘Abdullah s.a.w.w. ulikuwa ni miaka 52 ambao ni mwaka wa pili kabla ya Hijrah au ni mwaka 621 A.D.
Huko Makka, tarehe 27 ya mwezi Rajab katika mwaka kumi na mbili wa Utume wake, wakati Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. baada ya sala zake za usiku katika nyumba ya binamu wake, binti wa Abu Talib a.s. aitwae ‘Umma Hani na ambapo wote waliokuwa nyumbani walikuwa wamelala, mara Malaika Jibraili a.s. alitokezea na kuja kwake na kumchukua hadi Al-Ka’aba Tukufu huku akiwa amemwendesha Farasi mzuri, mwenye uso kama wa Kibinadamu mwenye mabawa meupe, aliyeitwa Buraq na limwelekeza hadi huko Jerusalemu ambako wao waliutembelea Msikiti. Baada ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuongoza sala ya Mitume iliyokuwa imemtangulia, yeye tena alipanda Farasi wake na alichukuliwa hadi Jannat ( Peponi ) na vile vile kuyaona yale matisho ya Jahannam ( Motoni ).
Miongoni mwa zile Nuru za Hidaya za kudumu alizopata kutoka kwa Allah swt, alipewa mafundisho na maamrisho mapya na ile amri ya kusali sala tano za kila siku kwa ajili ya ‘Ummah wake, yeye aliliona jina lake pamoja na jina la Al Imam ‘Ali ibn Abi Talib a.s. likiwa limeandikwa katika Kalimah:
‘Hakuna mungu mwingine illa Allah swt na Muhammad ni Mtume Wake na ‘Ali ibn Abi Talib ni Khalifa baada yake.’
Baada ya kuonyeshwa hayo yote yaliyo kuwemo Jannat ( Peponi ), na Jahannam (Motoni) basi Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alirudishwa hapo nyumbani mwake, alitambua kuwa kuweko kwake nje kulikuwa ni kitambo tu. Huu usiku wa safari unatambuliwa kama Lailat-al-Mi’raj au Usiku wa Mi’raj ambavyo vile vile imelezwavyo katika Qur’an Tukufu, Surah Bani – Israil, 17, Ayah:1
Kwa jina la Allah swt Mwingi wa Rehema na Ne’ema.
“Utukufu ni wake Yeye ambaye alimpeleka Mja wake usiku (mmoja tu ) kutoka Msikiti Mtukufu (wa Makka) mpaka Msikiti wa mbali (wa Baytul Mugaddas-Falastini) ambao (tumeubariki na ) tumevibariki vilivyoko pembezoni mwake. (Tulimpeleka hivyo) ili tumwonyeshe baadhi ya Alama zetu.
Hakika yeye Allah swt ni mwenye kusikia (na ) Mwenye kuona.
Haistahiliki kwa Mwislamu yeyote yule kuwa na shaka kuhusu tukio hili. Kuna alama ya miguu ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. yuu ya jiwe la Msikiti wa Jeruslem, ndipo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alipopandia yule Buraq kuelekea mbinguni. Msikiti ulijengwa na jiwe ambalo bado lipo papo hapo.
JE ‘AYESHA NA MU’AWIYAH WALIKUWAPO WAKATI WA MI’RAJ?
Hata hivyo kuna shakhsiya zingine ambao wao walikuwa hawakukubali yale yaliyokuwa yamesimuliwa na Allah swt kuhusu hii safari yake ya kwenda mbinguni mbali na kuthibitishwa na Qur’ani Tukufu. Nao ni Ayesha binti Abu Bakr, mkewe Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. na mwingine ni Mo’awiya, mwana mashuhuri wa Abu Sufiyan.
Natumaini kuwa kwa kueleza mambo hapa hakutanifanya mimi kujisahau yale niyazungumzayo. Wakati wa Mi’raj ulipokuwa, Ayesha alikuwa na umri wa miaka saba (7) tu na ambavyo alikuwa bado chini ya malezi ya wazazi wake na wala siyo kuwa alikuwa na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.; lakini yeye alikabidhiwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. baada ya miaka miwili aliyofuatia baada ya hayo kutokea huko Medina. Mzazi wake Ayesha, Abu Bakar, ingawaje nafsi yake mwenyewe alikuwa anaamini na kuwa na uadilifu juu ya Mi’raj .
Mu’awiya alikuwa bado hakuzaliwa wakati wa Mi’raj. Alizaliwa mwaka mmoja baadaye (katika mwaka ule ambao Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alijisitiri katika mapango) walipokuwa wameamua wazazi wake ambao walikuwa maadaui halisi wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika nyakati hizo. Yeye alikuwa Mwisalmu kiasi cha miaka kumi baadaye.
Yafuatayo ni meelezo zaidi yaliyo kuwa mengineyo yamekusanywa kuhusu safari hii ya usiku ya Mtukufu Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w., aliyoandikwa na W. Irving katika kitabu chake cha ‘Life of (Mtume) Muhammad Mustafa s.a.w.w.’ hasa kufuatana na maelezo ya Al-Bukhari, Abul Fida ambavyo ni kwa ajili ya manufaa kwa wasomaji ili kupata kujua zaidi.
KISA CHA MI’RAJ
Wakati wa masaa za katikati za saa za usiku, Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. aliamshwa na sauti iliyokuwa ikisema, “Amka, wewe uliyelala!” Mkuu wa Malaika wote, Farasi mweupe mwenye umbo la ajabu kabisa na sifa za ajabu zake ambavyo yeye Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alikuwa hajawahi kumwona hata (kabla) wakati mmoja katika maisha yake yote hayo hapo awali; na kusema ukweli, huyu farasi anatofautiana kabisa na farasi wengineo kwani hakuwanazo dosari zozote zile kulinganishwa na farasi wengineo wa kawaida. Farasi alikuwa na uso wa kibinadamu lakini mashavu yake yalikuwa ya ki-farasi; macho yake yalikuwa kama mekundu-manjano (kama jiwe lenye thamani sana) na macho yakiwa yakimetameta kama nyota. Alikuwa na mabawa ya furukombe zote zilikuwa zikitoa miale ya nuru; mwili wake ulikuwa umejaa johari na majiwe mazuri na vyenye thamani. Kutokana na ule mwendo wake wa kasi kabisa basi aliitwa Buraq au Radi (mwale wa nuru).
MTUME KUSALI MLIMA SINAI
Mnyama alimjongelea na kujituliza ili akaliwe, na alirudi kupaa akiwa amekaliwa na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. mgongoni mwake, basi alipaa hadi kufikia juu kabisa, juu ya milima ya Makkah. Hawa walivyopita ni kama radi baina ya mbingu na ardhi, basi Malaika alitoa sauti kwa nguvu; ‘Simama; Ewe Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.: rudi ardhini na usalishe sala.” Wao waliteremka juu ya ardhi na baadaye kumaliza sala ….” Oh rafiki na mpendwa sana wa roho yangu; alinena Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w., “Kwanini umenitaka nisali hapa?”. “Kwa sababu ni Mlima Sinai, ambako Allah swt alikuwa akiongea na Mtume Musa a.s.”
MTUME ASALISHA BAITUL MUQADDAS
Wakiendelea na safari yao hiyo walifika katika lango la msikiti wa Jerusalem, ambako kutokana na Nuru ya Buraq, yeye alipitiliza hadi kule kuingia msikitini yeye aliwaona Mitume Ibrahimu, Musa na Isa a.s. na wengineo wengi. Baaada ya yeye kusalisha sala pamoja nao, mara Nuru iliteremka toka mbinguni ikiwa katika hali ya ngazi ambayo ncha yake ya mwisho uligusa na kuegemea juu ya Shakra au jiwe la Msingi la nyumba tukufu, ilikuwa ni jiwe la Yakub. Akisaidiwa na Malaika Jibraili a.s. basi Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. aliipanda ile ngazi ya nuru kuendelea na safari yake.
KUWASILI MBINGU YA KWANZA
Baada ya kufikia mbinguni ya kwanza, Malaika Jibraili a.s. aligonga kilango.
Je yuko nani? Sauti iliuliza kutoka ndani. ‘Malaika Jibraili a.s. “Je uko na nani pamoja?”. “Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w..” “ Je yeye ameshaupokea Utume wake?” “Ndiyo ameshaupokea.” “Basi anakaribishwa!” Na ule mlango ulifunguliwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alipojongea ndani tu, mtu wa Kale sana alimkaribisha, na Jibraili a.s. alisema, “Huyu ni baba yako Adamu a.s., mtolee heshima.” Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alifanya hivyo na Mtume Adam a.s. alimkumbatia, huku akiwa akinena kuwa mkuu wa wana wake wote na mkwanza wa Mitume yote. Katika mbingu hii ya kwanza, kulikuwa na wanyama waliokuwa na kila aina ambao walikuwa ni Malaika ambao waliomba kuwa kama wale wanyama waliomo ardhini. Miongoni mwao alikuwa ndege mwenye urefu wa mshangao ambaye kishungi chake kilikuwa kikigusa mbingu ya pili, ingawaje ni safari ya miaka mia tano kutokea ile ya kwanza. Huyu ndege wa ajabu alikuwa anaimba kila siku kwa sauti yake tamu kila asubuhi. Wanyama wote juu ya ardhi, humsaidia binadamu; na wanaamshwa na sauti yake na wale ndege wote wa namna au kundi lake pia wanafuatisha sauti zake.
Ndege wa namna huyo huyo ameelezwa, anavyosema Dr. Prideaux, katika Bava-Bartha cha kitabu cha mafundisho cha Babyloi cha aliyeitwa ‘Zig’, ambaye alisimama juu na miguu yake juu ya ardhi na kulifunika jua lote na hivyo kulisababisha kupatwa kwa jua kikamilifu. Huyu ndege Chaldee kulingana na ufafanuzi juu ya kazi inatuelezea kuwa huwa anawika kila asubuhi, na Mola huwa anampa busara kutokana na kazi hiyo.
KUWASILI MBINGU YA PILI
Sasa wao walifika katika mbingu ya pili. Jibraili a.s. kama hapo awali alibisha hodi, maswali na majibu yalimiminika kama hapo awali, mlango ulifunguliwa nao waliingia humo. Huko wao walikutana na Mtume Nuh a.s., ambaye, alimkumbatia Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. na alimchukua na kumsifu kuwa alikuwa Mkuu kuliko Mitume yote iliyomtangulia.
KUWASILI MBINGU YA TATU
Walipofikia mbingu ya tatu, waliingia kwa shangwe hizo hizo. Hapa alikuwa malaika ambaye hapimiki kwa ukubwa, ambaye macho yake yalikuwa mbali na nyingine kiasi cha safari ya siku elfu sabini. Yeye alikuwa na vikosi mamia ya maelfu ya watu ambao waliokuwa wakisubiri amri yake. Mbele yake kulikuwa na kijitabu kikubwa kweli kweli ambamo yeye kila mara alikuwa ameshughulika na kuandika na kupekua pekua na kufutia mbali mengineyo. Malaika Jibrail a.s. alimweleza kuwa: “Huyu, Ewe Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w.” aliendelea Jibraili a.s.“Ndiye Izraeli, Malaika wa vifo, ambaye yuko katika amri ya Allah swt. Katika kitabu chake hicho yeye alikuwa anaandika tu kila wakati majina ya wale waliokuwa wameshamaliza maisha yao, yaani wale waliokwisha kuhitimu maisha yao au kufikia wakati wao na ambao wanafariki papo hapo.
KUWASILI MBINGU YA NNE
Na hapo baadaye, wao walifikia sasa mbingu ya nne. Miongoni mwa wale Malaika waliokuwamo huko. Kulifikia sasa mbingu ya nne. Miongoni mwa wale Malaika waliokuwamo huko, kulikuwako na malaika mmoja ambaye akianziwa kuanzia Mbinguni hadi kichwani kunachukua muda wa miaka mia tano. Uso wake ulikunjika na ya kusumbulika na mito ya machozi yaliyokuwa yakitiririka tokea machoni mwake. “huyu,” alisema Malaika Jibraili a.s., “ni malaika wa machozi, ameteuliwa kuwachunguza wana wa Adamu wanavyotenda madhambi na kuwabashiria maovu yanayowasubiri.”
KUWASILI MBINGU YA TANO
Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alipokelewa na Mtume Harun a.s. na huku akipongezwa na wale Malaika wa kuadhibu ambao wanaishi huko na ambao huwa wanautawala moto. Kulingana na Malaika wote ambao walionwa na Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ni Malaika mmoja tu ambaye alikuwa anatisha sana kuliko wote wenzake. Uso wake ulikuwa wa shaba, alikuwa amevikwa au kufunikwa na mauvimbe na visugu. Macho yake yalikuwa yaking’ara kama radi na alikuwa ameudaka moto. Yeye alikuwa amekalia kiti kilichokuwa kimezungukwa na moto, na mbele yake kulikuwako na minyororo miekundu kwa sababu ya moto. Kama yeye akifika ardhini basi milima yote itayeyuka, maziwa na bahari yatakauka na viumbe vyote vitakufa kwa vishindo vyake. Kwake yeye na Malaika, mawaziri wake, ndiko walikopewa amri ili kuteremsha ile adhabu ya Mola kwa ajili ya wale makafiri na watenda madhambi.
WAKIACHA YALE YA KUTISHA HAPO, WALIWASILI MBINGU YA SITA
Walipofika mbingu ya sita, hapo palikuwa na Malaika mkubwa kabisa na ambaye nusu upande alikuwa ni theluji ya nusu upande mwingie alikuwa ni moto; na katika hivyo hiyo theluji na nusu upande mwingine alikuwa ni moto; na hata hivyo hiyo theluji haikuyeyuka hata moto pia haukuzimika Wakimzunguka huyo malaika wengi sana walikuwa wakisema: “Ewe Allah swt ! Ambaye ameviunganisha moto na theluji; waunganishe wale watawa wako wote katika utekelezaji wa amri zao.” ‘ Huyu’ alisema Malaika Jibraili, “ni mlinzi na mlezi wa Malaika wa mbinguni na ardhini.” Hapa palikuwa na Mtume Musa a.s., ambaye badala ya kumkaribisha kwa furaha Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kama walivyokuwa wamefanya Mitume mingine iliyomtangulia, yeye, alilia sana
Na hapo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alipomwona aliuliza
“Je nini kinachokuliza?”
Mtume Musa a.s. alijibu:
“Kwa sababu tu kuwa mimi niko na mrithi wenu, ambaye ametumwa ilikuwarekebisha watu wa taifa lake kuingizwa huko Jannat (Peponi ) kuliko hata mimi nilishindwa kutimiza na kufikia kwa ajili ya hao wapotofu wana wa Israili.”
KUWASILI MBINGU YA SABA
Alilakiwa na furaha nyingi na Mzee Mkuu mwenye heshima, Mtume Ibrahim a.s. Hapa pamejaa mwanga wa Nuru na kudura ya Allah swt, usifa wake ambao kwa kweli ulimi wala mdomo wa mtu hauwezi kuuelezea. Mmoja wao tu atosha kutupa mwangaza juu ya wengineo tutakavyowafikiria. Yeye amegawa dunia katika mistari mirefu sambamba, na alikuwa na vichwa elfu sabini, na kila kichwa kilikuwa na midomo elfu sabini, na kila mdomo ulikuwa na ndimi elfu sabaini; na kila ulimi ulisema lugha elfu sabini mbalimbali; na yote haya yaliyokuwa yakisemwa yalishughulika na kumsifu Allah swt!”
Wakati Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alikaa huku akishika tama kuhusu huyu kiumbe, basi Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. mara kwa ghafla alivutiwa na mmea uliokuwa Myungiyungi ambao uliitwa Sedrat, ambao unanawiri vyema kwa upande wa kulia wa kiti cha Enzi cha Allah swt. Matawi yake yalisambaa zaidi ya umbali wa kati ya jua na ardhi. Malaika zaidi ya hata mchanga wa pwani au kingo za mito, wanafurahi chini ya kivuli cha mti huo. Majani yake ni sawa na masikio ya tembo kwa ukubwa ambako hujazana ndege mbalimbali na wote wakiwa wanasoma zile aya za Qur’an Tukufu. Matunda yake yalikuwa ni meupe kuliko maziwa na matamu, moja tu lingelitosha wote kwa chakula chao. Kila mbegu ilikuwamo na Mwanamwali mzuri au Hur al-‘ain mwenye kuwaongoza wenye Imani huko Jannat ( Peponi ).
AL-MA’MOUR
Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. na mwongozi wake waliongozana hadi kufikia Al-Ma’mour au Nyumba ya kusujudia, lililokuwa na sifa sita kupendeza sana; ambalo lilijengwa kwa majiwe manjano-mekundu au mawe ya vitu vyekundu vya thamani; ikiwa imezungukwa na taa chungu mzima zilizokuwa zikiwaka. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. aliingia ndani, alikaribishwa kwa vyungu vitatu, kimoja kikiwa kimejaa pombe, ya pili maziwa na ya tatu asali. Yeye alilichukua chungu la maziwa na kuyanywa. “Vyema kabisa ulivyofanya ndilo chaguo jema sana,” alinena Malaika Jibraili a.s.. “Kama ungalikunywa pombe basi watu wa ‘ummah yako wangali potea. “Nyumba hiyo tukufu inalingana kabisa na ile Ka’aba ambayo iko Makkah, na ipo juu ya mbingu ya saba moja kwa moja juu yake.
Walikuwapo wakati huo wakifanya Tawaf yaani kulizunguka jumba hilo mara saba ambapo ndipo naye Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alijiunga nao.
Sasa umefika wakati ambako Malaika Jibraili a.s. hawezi tena kusonga mbele kwani hapo ndipo palipokuwa kikomo chake. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. sasa aliendelea peke yake, mwepesi hata kuliko mawazo, uwanja mkubwa, akipitia eneo mbili zenye kuwaka taa na moja giza tupu. Kutokezea hapa gizani yeye alijiwa na wimbi la ukimya na uoga wakati alipojiona yuko amesimama mbele ya Allah swt . Lakini alishukuriwa mara mbili kutoka kiti cha Enzi. Alihisi kuwa alijawa na wimbi la furaha ambayo ndiyo kulivyofuata, wakati mzuri na manukato yalinusika pote mzungukoni ambavyo hakuna mwingine ambaye anaweza kuelewa ila yule tu ambaye yuko mbele yake – Allah swt .
Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kwa sasa alipata kutoka Allah swt zile Imani ambazo zimeelezwa na kuambatanishwa katika Qur’ani Tukufu; na sala tano za siku zilielezwa kuwa ni fardhi ya waumini kuzisali.
Kwa kuishikilia ile ile ngazi ya Nuru ambayo iliyokuwa imemleta hadi mbinguni ndiyo aliyoshukia nayo hadi katika Msikiti wa Jeruslem, ambako alimkuta Buraq akiwa amefungwa kama vile alivyokuwa amemwacha; na mara alimpanda na kurudishwa nyumbani mwake wakati ule ule na pale pale ambako alikuwa amechukuliwa na Malaika Jibraili a.s..
Maelezo yote haya yanayoelezwa hapo juu kuhusu hii safari ya usiku ni kufuatana na maneno yaliyonenwa au kuelezwa na wana historia mashuhuri kama vile Abul Fida, Al-Bokhari na vile vile yameelezwa kwa mapana zaidi sana na Irwing katika chacke cha ‘Life of Muhammad’ kilichoandikwa katika lugha ya Kiingereza.
Safari hii yenyewe imefungua mlango wa mabishano na maoni mbalimbali na chuki miongoni mwa wasomi. Baadhi yao wamethibitisha kuwa hakuna chochote zaidi ya ndoto za usiku au ni mawazo tupu; na hujikinga na kujiunga mkono kwa kunakili zile habari za mapokeo ya Ayesha kuwa kiwiliwili chake Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kilikuwa vile vile bila ya kutingishika na kwamba ni ki-roho tu ambavyo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alifanya hiyo safari ya usiku – Mi’raj.
Kwa kuelezea haya maelezo ya mapokeo, nasikitika sana kwani wao (hao wanaosema) hawakufikiria wala kuwaza na vile vile hawakuchunguza, ni kwamba wakati hiyo safari ilipotokea, ‘Ayesha alikuwa bado yu mtoto na ingawaje alikuwa ameposwa, lakini bado hakuwa mkewe Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. na hivyo alikuwa bado nyumbani kwa babake mzazi – Abu Bakar.
Wengine husema kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alifanya safari kimwili. Kulingana na Ahmad bin Joseph, safari ya usiku huko Msikitini (Jeruslem) imehakikishwa na mtu Mzee mwenye heshima, mkazi wa Jeruslem. “Wakati huo,” amesema yeye, “ ambapo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alipotuma ujumbe kwa Mfalme Heraclius, huko Costantinopole, akimwalika kuukubali Uislamu, basi huyu mzee alikuwako hapo pamoja na Mfalme. Huo ujumbe ulipoelezea kuhusu ile safari ya Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ya usiku, basi yule mzee alishikwa na maajabu makuu, na yeye huyo mzee alimwelezea Mfalme vivyo hivyo yule mfalme kama vile walivyoelezea wale wajumbe. “Hiyo ni tabia yangu ,” alinena Mzee “ilikuwa ni mwiko kwangu mimi kulala kabla ya kufunga milango yote ya Msikitini. Katika usiku ambao unaelezwa, mimi nilifunga milango yote isipokuwa mlango mmoja tu ambao uligoma kufungika. Kutokana na hayo, mimi niliwaita mafundi seremala ambao baada ya kuufugua vyema ule mlango, walinihakikishia kuwa kizingiti chake juu ya mlango na jumba lenyewe yamepishana katika nyuzi upimo mkubwa ambavyo ilikuwa ni zaidi ya nguvu za kuweka kuufunga mlango huo. Na hivyo mimi nililazimika kuuacha wazi. Alfajri na mapema, palipokucha, mimi nilipatembelea hapo na kuwepo hapo, na pale pale palipo kuwa pamewekwa jiwe lilikuwa limetobolewa na kulikuwa na dalili za alama ya kufungwa kwa Buraq zilithibitika. Hapo ndipo mimi nilisema, kuwa huu mlango usingelikuwa umebandikwa kama kusingelikuweko na kuzuru kwa Mitume kwa ajili ya Sala.”
Habari zingine zanakili kuwa wakati Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alipokuwa akielezea ‘Ummah juu ya safari yake hiyo ya usiku huko Makka, basi wengi walikuwa wakionekana wakiamini na wengineo walikuwa na kigeugeu ambapo wana wa Qureisha walivunjika mbavu kwa vicheko na huku wakimdharau. “Amesema kuwa ati yeye alikuwa katika Msikiti wa Jerusalem!?” Alibweka Abu Jahal; “Athibitishe maneno yake kwa kutoa ushahidi hai na maelezo yake. “Kwa muda huo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alighafilika kwa sababu yeye alikuwako huko Msikitini usiku ule ambamo vilikuwa havionekani, na mara kwa ghafla alitokea Jibraili a.s. ubavuni mwake na kuyaweka yale yote yaliyotokea ule usiku mbele yake na hivyo ndivyo alivyokuwa ameweza kuyajibu maswali hata madogo kabisa.

MWISHO

Toa maoni yako

Maoni ya watumiaji

Hakuna maoni
*
*

Site ya Al-Imaamaini Al-Hassanaini (A.S) ya usambazaji wa utamaduni wa Kiislamu na mafunzo ya Kidini