• Anza
  • Iliyopita
  • 8 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 7146 / Pakua: 3308
Kiwango Kiwango Kiwango
HIDAYA YA RAMADHANI

HIDAYA YA RAMADHANI

Mwandishi:
Swahili

HIDAYA YA RAMADHANI

Kitabu hiki kinazungumzia kufunga na kufungua katika mwezi mtukufu wa Ramadhani na vile Muislamu anatakiwa awe katika mwezi huu.

Kimeandaliwa na: Ahlulbayt Organization

KHUTBATU SHAABAANIYYA

Khutba hii ilitolewa na Mtume Muhammad(s.a.w.w) katika Ijumaa ya mwisho ya mwezi wa Shaabaan.

Imepokewa na Imam Ali(a.s) amesema; "Mtume(s.a.w.w) alituhutubia siku hiyo na alisema:

'Enyi watu! kwa hakika umewakaribieni mwezi wa Mwenyezi Mungu, kwa baraka na rehma na maghfira, (huo ni) mwezi ambao mbele ya Mwenyezi Mungu ni bora ya miezi yote, na masiku yake ni bora ya masiku yote, na usiku zote, na masaa yake ni bora ya masaa yote. Huo ni mwezi ambao mmealikwa ndani yake katika dhifa ya Mwenyezi Mungu, na mmefanywa kuwa ni watu wenye karama ya Mwenyezi Mungu.

“Pumzi zenu katika mwezi huo ni tasbihi, na usingizi wenu katika mwezi huo ni ibada, na amali zenu katika mwezi huo ni zenye kukubaliwa, na du'a zenu ni zenye kujibiwa, basi muombeni Mwenyezi Mungu, Mola wenu kwa niyya zenye ukweli, na mioyo misafi ili awawezeshe kuufunga mwezi huo na kukisoma kitabu chake, kwani yule aliyepata hasara ni yule aliyekosa maghfira ya Mwenyezi Mungu katika mwezi huu mtukufu. Na kumbukeni kwa njaa yenu na kiu yenu katika mwezi huo, njaa na kiu ya siku ya kiyama.

“Wapeni sadaka mafakiri wenu na masikini wenu, na waheshimuni wakubwa wenu, na wahurumieni wadogo wenu, na dumisheni undugu wenu, na chungeni ndimi zenu, na kifungieni macho kile ambacho hakifai kutizamwa na macho yenu, na kile ambacho hakifai kusikizwa na masikio yenu, wafanyieni upole mayatima wa watu wengine ili nao wawafanyie upole mayatima wenu. Na tubieni kwa Mwenyezi Mungu madhambi yenu, na mnyanyulieni mikono yenu mnapo omba du'a katika nyakati za sala zenu, kwani hizo ni nyakati bora zaidi, Mwenyezi Mungu huwatizama waja wake katika nyakati hizo kwa upole, huwajibu pindi wanapomuomba, huwapa wanapomuuliza.

“Enyi watu, hakika nafsi zenu zimewekwa rehani kwa amali zenu, basi zifungueni kwa kuomba kwenu msamaha, migongo yenu ni mizito kwa mizigo yenu ya madhambi, ipunguzieni uzito huo kwa kurefusha sajda zenu, na jueni ya kwamba Mwenyezi Mungu ameapa kwa utukufu wake kuwa hatawaadhibu wenye kusali na kusujudu, na kwamba hatawaadhibu kwa moto siku watakapo simama watu kwa Mola wa walimwengu.

“Enyi watu, mwenye kumfuturisha mtu mu'umin aliyefunga miongoni mwenu katika mwezi huu, jambo hilo mbele ya Mwenyezi Mungu ni sawa na kumuachilia mtumwa huru, na husamehewa madhambi yake yaliyopita.

Ikasemwa:-

'Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, sio wote kati yetu wanaoweza jambo hilo.'

Mtume(s.a.w.w.) akasema:-

'Ogopeni moto japo (mfuturishe) kwa tende moja, ogopeni moto japo kwa kunywesha maji'.

“Enyi watu! mwenye kuifanya tabia yake iwe nzuri miongoni mwenu katika mwezi huu, malipo yake ni kuweza kupita katika Swiraat kwa usalama siku ambayo miguu ya watu wengine itakapokuwa ikiteleza. Na mwenye kumpunguzia katika mwezi huu kazi, mjakazi ambaye amemumiliki kwa mkono wake wa kulia, Mwenyezi Mungu atampunguzia hesabu (madhambi) zake.

“Na atakayezuia shari yake katika mwezi huu, Mwenyezi Mungu atazuia ghadhabu zake siku atakayo kutana naye. Na atakayemkirimu yatima katika mwezi huu, Mwenyezi Mungu atamkirimu mtu huyo siku ya Kiyama. Na atakaye dumisha undugu katika mwezi huu, Mwenyezi Mungu atamdumishia rehma zake siku atakayokutana naye. Na atakayevunja undugu ndani yake, Mwenyezi Mungu atamvunjia rehma zake siku atakayokutana naye.

“Na atakaye sali sunna ndani yake, Mwenyezi Mungu atamwandikia awe mbali na moto. Na atakayetimiza faradhi moja ndani yake, atakuwa na thawabu amabazo atakuwa sawa na atakayetimiza faradhi sabini zenye kuwa sawa katika miezi mingine. Na mwenye kukithirisha kuniswalia mimi ndani ya mwezi huu, Mwenyezi Mungu atamfanyia uwepesi mizani yake siku itakayokuwa ni mzito mizani nyengine (kwa madhambi). Na atakayesoma ndani yake aya moja ya Qur'ani malipo yake yatakuwa ni sawa na yule aliyehitimisha Qur'ani katika miezi mingine isiyokuwa Ramadhani.

Enyi watu! hakika milango ya pepo katika mwezi huu iko wazi, basi muombeni Mola wenu asiifunge kwenu nyinyi. Na milango ya moto imefungwa, muombeni Mwenyezi Mungu asiifungue kwenu. Na Mashetani wamefungwa, basi muombeni Mola wenu wasije wakawatawala juu yenu..."

Imam Ali Ibn Abi Talib(a.s) alimuuliza Mtume(s.a.w.w) :

"Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, ni tendo gani lililo bora kabisa katika mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani?"

Mtume Mtukufu(s.a.w.w) alijibu:

"Ewe Abu'l Hasan, bora ya matendo yote katika mwezi huu Mtukufu ni kujiweka mbali kabisa na yale yaliyoharamishwa na Allah s.w.t.

“Enyi mlioamini! Mmelazimishwa kufunga (saumu) kama walivyolazimishwa waliokuwa kabla yenu ili mpate kumcha Mungu, Siku chache tu (kufunga huko). Na atakaye kuwa mgonjwa katika nyinyi au katika safari (akafungua baadhi ya siku), basi (atimize) hisabu katika siku nyingine.

Na wale wasioweza, watoe fidia kumlisha masikini. Na atakayefanya wema kwa radhi ya nafsi yake, basi ni bora kwake. Na (huku) kufunga ni bora kwenu. Ikiwa mnajua (haya sasa basi fuateni).

Al Baqarah 2: 183 – 184.

HIDAYA YA RAMADHANI

SAUMU NI AMRI YA MUNGU

Sisi kama Waislamu, hatufuati amri yeyote ile ila sharti iwe imenasiwa katika Qur'ani ama katika Hadithi tukufu za Mtume wetu(s.a.w.w)

Saumu katika Qur'ani imetajwa kutoka Aya ya 183 ya Sura ya pili 'Albaqarah' hadi Aya ya 187 ya Sura hiyo hiyo.

Mwenyezi Mungu ametufunza kama ifuatavyo:

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُتِبَ عَلَيْكُمُ الصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ ﴿١٨٣﴾

"Enyi mlioamini, mmelazimishwa kufunga Saumu kama walivyolazimishwa wa kabla yenu ili mpate kumcha Mwenyezi Mungu."

أَيَّامًا مَّعْدُودَاتٍ فَمَن كَانَ مِنكُم مَّرِيضًا أَوْ عَلَىٰ سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ وَعَلَى الَّذِينَ يُطِيقُونَهُ فِدْيَةٌ طَعَامُ مِسْكِينٍ فَمَن تَطَوَّعَ خَيْرًا فَهُوَ خَيْرٌ لَّهُ وَأَن تَصُومُوا خَيْرٌ لَّكُمْ إِن كُنتُمْ تَعْلَمُونَ ﴿١٨٤﴾

183. Ni siku chache tu (zinazohesabiwa) lakini miongoni mwenu awaye mgonjwa au katika safari, basi atimize hesabu katika siku zingine. Na wale wanaoweza, watoe fidia kwa kumlisha masikini. Na atakayefanya wema kwa radhi ya nafsi yake basi ni bora kwake, na mkifunga ni bora kwenu mkiwa mnajua.

شَهْرُ رَمَضَانَ الَّذِي أُنزِلَ فِيهِ الْقُرْآنُ هُدًى لِّلنَّاسِ وَبَيِّنَاتٍ مِّنَ الْهُدَىٰ وَالْفُرْقَانِ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ وَمَن كَانَ مَرِيضًا أَوْ عَلَىٰ سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ يُرِيدُ اللَّـهُ بِكُمُ الْيُسْرَ وَلَا يُرِيدُ بِكُمُ الْعُسْرَ وَلِتُكْمِلُوا الْعِدَّةَ وَلِتُكَبِّرُوا اللَّـهَ عَلَىٰ مَا هَدَاكُمْ وَلَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ ﴿١٨٥﴾

185. (Mwezi mnaoambiwa kufunga) ni mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur'ani kuwa mwongozo kwa watu na ishara zilizo wazi za mwongozo na kipambanuzi. Basi miongoni mwenu atakayeuona mwezi (au atakayekuwa mkazi asiwe msafiri pindi mwezi ufikapo) afunge Saumu na mwenye kuwa mgonjwa au safarini basi atimize hesabu katika siku zingine. Mwenyezi Mungu Huwatakieni mepesi wala Hawatakieni yaliyo mazito, na kamilisheni hesabu na kumtukuza Mwenyezi Mungu kwa kuwaongozeni na ili mpate kumshukuru.

وَإِذَا سَأَلَكَ عِبَادِي عَنِّي فَإِنِّي قَرِيبٌ أُجِيبُ دَعْوَةَ الدَّاعِ إِذَا دَعَانِ فَلْيَسْتَجِيبُوا لِي وَلْيُؤْمِنُوا بِي لَعَلَّهُمْ يَرْشُدُونَ ﴿١٨٦﴾

186. Na waja wangu watakapokuuliza juu yangu basi hakika Mimi nipo karibu, Nayaitika maombi ya mwombaji anaponiomba, basi waniitikie na waniamini ili wapate kuongoka.

أُحِلَّ لَكُمْ لَيْلَةَ الصِّيَامِ الرَّفَثُ إِلَىٰ نِسَائِكُمْ هُنَّ لِبَاسٌ لَّكُمْ وَأَنتُمْ لِبَاسٌ لَّهُنَّ عَلِمَ اللَّـهُ أَنَّكُمْ كُنتُمْ تَخْتَانُونَ أَنفُسَكُمْ فَتَابَ عَلَيْكُمْ وَعَفَا عَنكُمْ فَالْآنَ بَاشِرُوهُنَّ وَابْتَغُوا مَا كَتَبَ اللَّـهُ لَكُمْ وَكُلُوا وَاشْرَبُوا حَتَّىٰ يَتَبَيَّنَ لَكُمُ الْخَيْطُ الْأَبْيَضُ مِنَ الْخَيْطِ الْأَسْوَدِ مِنَ الْفَجْرِ ثُمَّ أَتِمُّوا الصِّيَامَ إِلَى اللَّيْلِ وَلَا تُبَاشِرُوهُنَّ وَأَنتُمْ عَاكِفُونَ فِي الْمَسَاجِدِ تِلْكَ حُدُودُ اللَّـهِ فَلَا تَقْرَبُوهَا كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللَّـهُ آيَاتِهِ لِلنَّاسِ لَعَلَّهُمْ يَتَّقُونَ ﴿١٨٧﴾

187. Mmehalalishiwa usiku wa Saumu kuwaingilia wake zenu (yaani kutangamana nao) wao ni nguo kwenu na nyinyi ni (kama) nguo kwao, Mwenyezi Mungu amejuwa kuwa mlikuwa mkizihini nafsi zenu, kwa hivyo amewakubalieni toba zenu na amewasameheni, basi sasa changanyikeni nao (yaani laleni nao) na takeni aliyowaandikieni Mwenyezi Mungu. Na kuleni, mnyweni mpaka ubainike kwenu uzi mweupe katika uzi mweusi wa Alfajiri, kisha timizeni Saumu mpaka usiku, wala msitangamane nao na hali mnakaa itikafu misikitini. Hiyo ni mipaka ya Mwenyezi Mungu basi msiikaribie. Hivi ndivyo Mwenyezi Mungu anavyobainisha hoja zake kwa watu ili wapate kumcha.

Maneno hayo ufasaha usioweza kukabiliwa na mfasaha yeyote, ndiyo asili na misingi ya Saumu. Yeyote abishanaye au kukaidi Amri tunamjibu na kumlainisha kwa nasaha hiyo.

FUNGA UKIUONA

Fungeni Mkiuona Na Fungueni Mkiuona (Mtume(s.a.w.w).

Ndugu Mwislamu, yakupasa kujua kwamba kufunga mwezi wa Ramadhani hakutegemei kuwa sikia watu wakizungumza kwamba "Kesho ni Saumu, kesho ni Saumu...." Na hujui sababu ya hao watu na usemi wao huo, bali na wewe mwenyewe wahitajika kujua matukio ya dini yako:

a. Utakapouona mwezi umeandama, ni lazima juu yako kuamkia kufunga na sawa watu wengine wamefunga au hawakufunga, kwako si halali kula hata kidogo na ukila ni juu yako kuilipa siku hiyo na kafara.

b. Habari zikienea mitaani, mijini au barabarani kwamba mwezi umeandama na ukaonekana, na kukawa hakuna uwezekano wa wao kusema uongo, basi ni lazima kuanza Saumu mara moja asubuhi yake.

c. Habari zikitoka mji mwengine ambao si wa mbali sana (kama hapa Kenya na Tanzania na mfano wake) kwa njia ya Radio au simu kwa ushahidi unaoaminika au kutegemewa, Saumu italazimu.

d. Watu wawili unaowaamini watakapokupa habari za kuonekana Hilal (mwezi mwandamo) utalazimika kuwaamini na kuamkia Saumu ingawa wewe mwenyewe hukuona.

e. Pengine kunaweza kuwa na mawingu ambayo yanaweza kuzuia kuonekana kwa mwezi, hapa basi lililo lazima kwako ni kutimiza 30 za Sha’bani na baadaye kuzingatia kuonekana kwa mwezi kutakuwa hakuhitajiki.

ANGALIZO

Kauli ya mnajimu (yaani mtu mwenye utaalamu wa kinyota) akitoa hukumu yake ya kinyota kuhusu kuonekana kwa mwezi hazingatiwi.

SOMA DUA HIZI UKIUONA MWEZI

Ukiuona mwezi umeandama, simama wima huku umeelekea Kibla, na usome:

"Ee Mwenyezi Mungu! Tunakuomba Utuukaribishie mwezi huu kwa amani, imani, na kwa Uislamu kamili (na tunakuomba katika mwezi huu) afya bora, riziki pana, na utuondolee maradhi. Ee Mola wetu! Tujaalie tuufunge wote, tusimame kwa Ibadati, tusome Qur'ani kwa wingi, tujaalie tuupokee, (nao mwezi) Utupokee, na tunakuomba Utuvushe salama.

Pia ni vizuri kusoma Dua hii ya Amiril Muuminina Aly Bin Abi Talib (a.s) baada ya kuuona mwezi.

“Ee Mola wetu! Ninakuomba heri za mwezi huu na heri za mwanzo wake na ninakuomba mwangaza wake, pia nusura yake, baraka zake, utufuku wake na riziki zake. Pia ninakuomba heri zilizomo katika mwezi huu na heri zijazo, na ninajilinda kwako na shari zitakazokuwemo katika mwezi huu na shari zitakazokuja baada yake.

“Ee Mwenyezi Mungu! Ulete kwetu kwa amani, imani, usalama, na kwa Uislamu, pia tunakuomba baraka, na Utujaalie tukuogope zaidi katika mwezi huu, na mambo yetu yawe ni yenye kuwafikiana na Uyapendayo na Ukayaridhia.”

Dua hizi ni bora zaidi kwa Mwislamu kuzisoma punde tuu baada ya kuonekana mwezi. Na wakati wa kuzisoma ni bora zaidi uwe umeelekea Kibla - yaani huko Makkah.

FAIDA ZA SAUMU

Limekuwa jambo jema kueleza faida za Saumu ili kila afungaye ajuwe hasa masumbuko yake ni kwa sababu gani? Kwani si vyema mtu kutaabika na hali hajui matokeo ya shughuli zake, na pengine huenda akaingia katika kundi la wale waliotajwa na mshairi mmoja kwamba:

Mfisada mkubwa ni mjuzi mwenye kupotosha (bila kujua) na aliye muovu zaidi ni mjinga mwenye (kupenda) ibada. Hao watu wa aina mbili hizi ni fitina kubwa kwa watu na hasa kwa mtu aliyeshikamana na dini kwa kuwafuata. Jee, vipi utamfuata mtu ambaye hajui?

Mshairi mwengine amenena:

Ewe mtu (mjinga) unayemfundisha mwenzako, jee wewe nafsi yako unajua unachofundisha? Wampa dawa mtu aliyokonda na mwenye maradhi ili apone (kwa hizo dawa) na hali wewe ni mgonjwa?"

Faida za kufunga ni nyingi mno, miongoni mwazo ni: kutekeleza mojawapo ya amri za Mwenyezi Mungu Alizotufaradhia kwetu sisi na faida ya utekelezaji huu ni kuingia peponi.

Faida ya pili ya Saumu ni kujizoeza subira, yaani katika mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani, mtu anajifunza jinsi ya kuweza kuvumilia na kustahamilia njaa, kiu, na kila matamanio ya kimwili. Mtume(s.a.w.w) amenena:

"Huo mwezi wa Ramadhani ni mwezi wa kusubiri, na hakika subira malipo yake ni pepo tu".

Faida ya tatu ni kuwa na uadilifu na kujifundisha usawa baina ya tajiri na maskini.

Imam Ja'far As-sadiq(a.s ) alisema:

"Hakika si jingine, Mwenyezi Mungu amefaradhisha kufunga ili wapate kulingana tajiri na maskini (katika shida ya njaa na kiu) basi akapenda viumbe vyake wawe sawa, na Amwonjeshe tajiri maumivu ya kushikwa na njaa ili apate kumhurumia mnyonge, na apate kumsikitikia mwene njaa".

Faida ya nne na ambayo ni muhimu zaidi ni kughufiriwa katika mwezi huu na kusamehewa madhambi yote ya mwaka ikiwa mwenye kufunga ameyafuata masharti yote na kufunga kwa ajili ya Mwenyezi Mungu kama alivyosema Mtume(s.a.w .w ) katika mojawapo ya hotuba alizozitoa kwa minajili ya mwezi huu akasema:

"Enyi watu! Hakika umewaelekeni nyinyi, mwezi wa Mwenyezi Mungu (mwezi wa Ramadhani) kwa baraka, rehema na msamaha. Mwezi ambao ni bora mbele ya Mwenyezi mungu kuliko miezi yote, na siku zake ni bora kuliko siku zote, na masiku yake ni bora kuliko masiku mengine yote na masaa yake ni bora na muhimu kuliko masaa yote."

AFYA

Faida ya tano ya Saumu inahusu upande wa afya. Kwa kawaida chochote kifanyacho kazi sharti kipumzike kwa muda. Hata mitambo, kwa mfano, ambayo imeundwa kwa vyuma imara tena vyenye nguvu, hufika wakati ambao huwa lazima kusimama kwa marekebisho ili ipate nguvu zingine za kuendelea upya. Jee vipi kwetu sisi ambao tumeumbwa wadhaifu tusivipumzishe baadhi ya viungo vyetu na hasa tumbo ambalo huendelea na kazi mfululizo kva miezi kumi na moja? Hapo utauona ulazima wa kuyapumzisha matumbo yetu ili kuhifadhi siha zetu.

MADAKTARI

Madaktari wote wakuu ulimwenguni, wamekariri na kuthibitisha faida hii, na wote wa nyuma ya Daktari wetu mkuu(s.a.w.w) Aliposema:

"Fungeni ili mpate siha nzuri." Naye lmam Ja'far As-sadiq(a.s.) anasema:"Kila kitu kina utakaso, na kitakaso cha mwili ni kufunga (Saumu).”

"Ni wajibu juu ya kila mtu mgonjwa ajizuie kula ijapokuwa kwa muda wa siku moja tu katika kila mwaka". Haya yalisemwa na daktari wa Kimarekani aitwaye Dr. CAR. Pia akaongeza "Vijidudu viambukizavyo maradhi huendelea na kunawiri maadam mwenye mwili anaendelea na kula na kuvilisha na hivyo basi vitaendelea kukua. Ama lau utajizuia kula vitadhoofika.”

Madaktari wote Waislamu na wasio Waislamu wameliwafiki shauri hili. Miongoni mwao ni Dr. Abdul Aziz bin Ismail aliyesema kwamba kufunga siku moja ni kinga ya maradhi ya mwaka. Isitoshe kwa siku hizi kumetokea hospitali mbali mbali ambazo zimehimiza na kusisitiza umuhimu huu, kadhalika mara nyingi tunashuhudia wagonjwa wengi sana ambao huzuiwa kula kwa manufaa ya afya zao.

Mwalimu wa Cairo University aitwaye Dr Muhammad Dhawahir asema: "Ugonjwa wa kuzidi maji mwilini, unene, moyo, ini, pafu, n.k. huzuiwa na kufunga (Saumu)."

HIDAYA YA RAMADHANI

MAANA YA 'SAUMU'

Neno 'Saumu' ki lugha ya Kiarabu lina maana ya kujizuia. Pia ni neno ambalo lilitumika kabla ya zama za Uislamu. Baadaye Uislamu ulipokuja ukalijaalia neno hili kuwa ni moja kati ya maneno yatumikayo kiibada.

Ama maana ya neno hili Kisheria, ni kujizuia kutokana na mambo yanayobatilisha Saumu yaitwayo 'al-Muftiraat'.

Kinyume cha watu wengi wanavyodhani kwamba Saumu hasa ni kujizuia kula na kunywa tu. La Hasha! Bali Saumu ni kukihifadhi kila kiungo chako kutokana na mambo yasiyotakikana.

Amesema lmam Ja'far As-sadiq(a.s.) :"Kufunga siko kujilinda na kula na kunywa tu, bali utakapofunga hifadhi (chunga) macho yako, ulimi wako, tumbo lako, masikio yako na uchi wako. Vile vile ilinde mikono yako, pendelea sana kunyamaza ila katika heri tu (kama kusoma Qur'ani n.k.) na umhurumie mtumishi wako."

Naye Mtume(s.a.w.w) amesema:"Mambo matano hutengua Saumu ya mtu: Uongo, kuseng'enya, kufitinisha, kula viapo vya uongo na (mwanamke) kumkazia macho mwanamume asiye maharimu wake au (mwanamume) kumkazia macho mwanamke asiye maharimu wake kimatamanio.”

Kuseng'enya kumekatazwa katika kauli hii ya Mtume(s.a.w.w) na badala yake tunahimizwa na hadithi nyingi tujiepushe na lolote la kutuharibia Saumu zetu.

Mtume(s.a.w.w) anasema:"Mwenye kufunga huwa ibadani wakati wowote hata kama analala madamu hajaitengua Saumu yake kwa kusengenya".

Kwa hapa utaona kwamba, kule kutokula na mfano wake kama tulivyo yabaini hapo mbeleni siko kufunga hasa kunakotakikana, bali kufunga ni kujizuia na makatazo yote na mabaya.

NYAMA MDOMONI

Siku moja Mtume(s.a.w. w ) alimsikia mwanamke mmoja akisengenya na hali amefunga. Mtume(s.a.w. w ) akamwitishia chakula ili ale. Yule mwanamke akasema: "Mimi nimefunga". Mtume akaendelea kuhimiza chakula iletwe mara moja ili yule bibi ale naye, yule bibi azidi kukariri kuwa angali anafunga.

Hapo Mtume akamwambia:

"Unafungaje na hali menoni mwako mna kipande cha nyama? Yule mwanamke akazidi kubishana na huku Mtume amwambia"Hebu tia mkono wako kinywani mwako" na kweli alipouingiza mkono wake menoni, alitoa kipande cha nyama. Hapo Mtume(s.a.w. w ) akamwambia"Waona? Wataka kula nyama ya nduguyo aliyekufa?” Yaani kusengenya ni sawa na kula nyama ya mfu tena nduguyo.

Hapo waona ndugu? Kwa hakika kile kipande cha nyama mdomoni mwa yule bibi kilipatikana kwa kule kusengenya, na yeyote asengenyaye huwa Saumu yake si sawa na huwa amekula nyama ya mfu tena nduguye.

PIA KUTUKANANA

Siku moja Mtume(s.a.w. w ) alimsikia mwanamke mmoja akimtusi msichana wake - mfanya kazi - na yule bibi alikuwa amefunga. Mtume(s.a.w. w ) akaitisha maji ampe yule bibi afuturu (na ilikuwa ungali mchana).

Yule bibi akasema "Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, hakika mimi nimefunga". Mtume(s.a.w. w ) akajibu,"Unawezaje kumtusi mtu au kumteta na hali umefunga? Wewe tayari Saumu yako ni batili, yaani si makbuli.”

Viungo vyako ni hadiya ya Mwenyezi Mungu kwako, kwa hivyo haifai kuvifanyia hiana.

Katika masiku haya ya Saumu, na mengine pia ambayo ni heshima kuu na utukufu kwa Waislamu, ni lazima kujilinda.

Miguu : Isielekee kulikokatazwa ambako kunajulikana kama Makadara, kwenda disco, kwenda sinema na kadhalika, na badali yake ni muhimu lau tutakwenda misikitini, kutembeleana kwa heri kama alivyotuhimiza Mola wetu kwa kutuambia: "Saidianeni katika mema na kwa kumcha Mwenyezi Mungu, lakini msisaidiane katika kumwasi Mola na kufanyiana uadui.” Na kujilinda huku kuendelee hata baada ya Ramadhani.

Mikono : Izuie kuwadhuru watu kwa kuwaibia, kuua, kupiga na kadhalika, na badala yake ishikishe Qur'ani, iamkize jamaa na kadhalika.

Macho : Usiyatizamishe ulichokatazwa. Kuwaangalia watu wasio wa maharimu yako, kutamani kisicho chako na kadhalika bali fungua Msahafu usome.

Masikio : Usisikilize upuzi uliokatazwa kama nyimbo, kusengenya, udaku na kadhalika na badala yake nenda ukasikilize mawaidha na kama hayo ambayo ndani yake mna radhi ya Allah (s.w.t).

MASHARTI YA SAUMU

Saumu Ni Wajibu Kwa Masharti Manane

Mwenyezi Mungu amesema:

"Basi atakayekuwa katika mji (asiwe msafiri) katika mwezi huu afunge". Qur'ani 2:185.

Wakati tunapojiandaa kwa kuianza Ramadhani, tunapaswa kujua kwamba, amri ya kufunga ni yake Mwenyezi Mungu. Na wala amri hii haikuwa ya yeyote yule kati ya viumbe. Muda huu wa Saumu mtu hutakiwa kufanya ibada kwa wingi. Kuomba, kusoma dua mbali mbali na kuomba maghfira.

Na masharti yafuatayo ukiwa umeyakamilisha utalazimika kuanza Saumu, na wala hutokuwa na udhuru wowote ukuzuiao kufunga.

1. Al-Islam: Uislamu ni shuruti moja katika shuruti za kukubaliwa Saumu na ibada zote. Ijapokuwa juu ya kafiri pia ni wajibu kufunga na kufanya ibada zote, lakini kwa vile yeye si Mwislamu basi haitasihi na kukubaliwa ibada zake.

Mwenyezi Mungu anaamrisha wasali lakini shuruti (watawadhe au watayammamu). Basi kafiri pia inampasa afunge, lakini shururti za kusihi hiyo saumu yake ni kukubali Islamu, na Kafiri anaweza kusilimu.

2. Baleghe: Ukiwa umebaleghe (mwanamume) kwa kutimiza miaka kumi na mitano na mwanamke kwa kutimiza miaka tisa; au ukiwa wewe ni mwanamke aliyewahi kutokwa na damu ya mwezi, au ukiwa umewahi kuota ndoto kama unatangamana na mke (ukiwa mume) au na mume (ukiwa mke) na kutokwa na manii kwa ndoto hiyo, utalazimika kuanza kufunga.

3. Nia: Ni makusudio ya kutenda, nayo ni fardhi kwa kila ibada na ni sharti katika ibada zote. Lazima kunuia kujizuia na kila kinachobatilisha Saumu, na si lazima wakati wa nia kuzikumbuka zote kwa jina, inatosha kuweka nia ya kujitenga na kila kinacho haribu na kubatilisha Saumu.

Kuweka nia ni wajib. Ikiwa kwa mfano, siku moja kabla ya kuingia Ramadhani mtu bila ya nia ya kufunga akalala na asizindukane ila baada ya magharibi ya usiku wa pili wa mwezi wa Ramadhani, basi kukosa kula na kunywa siku hiyo moja ya Ramadhani bila ya nia haitasihi, na lazima baadaye ailipe.

Mtu anaweza kila usiku wa Ramadhani kuweka nia ya kufunga kesho yake, na ni vizuri usiku wa kwanza wa mwezi wa Ramadhani aweke nia ya mwezi mzima.

WAKATI WA KUWEKA NIA

Wakati wa kuweka nia ya Saumu ni kutoka mwanzo wa usiku hadi adhana ya asubuhi (Alfajiri) kwa saumu za fardhi, ama saumu za sunna huanzia mwanzo wa usiku, hadi kiasi cha kunuia kumebaki kufikia magharibi, ikiwa mpaka wakati ule hakutenda kitu cha kuvunja saumu, basi hapo aweke nia ya saumu, na saumu itasihi.

Ikiwa mtu bila ya kuweka nia kabla ya Alfajiri akalala, na akaamka kabla ya adhuhuri na hapo akiweka nia, saumu yake itasihi, ikiwa saumu ya fardhi au ya sunna; lakini akizindukana baada ya adhuhuri, basi hapo hawezi kuweka nia ya saumu ya fardhi. Ikiwa kabla ya alfajiri kanuia na akalala na asiamke ila baada ya magharibi, saumu hiyo itasihi haidhuru neno.

AL-KHULUUS

Lil-Laahi Ta'ala, maana yake, kufunga kwake iwe Lil-Laahi, Ta'ala tu, lau akiongeza Riya (kwa kujipendekeza) tu hapa saumu yake haitasihi.

4. Ukiwa (wewe mke) unayo damu ya mwezi au ya uzazi, unashauriwa kusubiri hadi itakapokoma ndipo uanze kufunga, hata hivyo utalazimika kuzilipia siku ambazo zimekupita.

5. Kwa aliye na kichaa na wazimu huyo anasamehewa Saumu zitakazompita muda wa udhuru wake huo.

6. Ukiwa umgonjwa hulazimiki kufunga hadi utakapopata nafuu, hata hivyo ni ugonjwa usiokuwezesha kufunga tu ndio unaokusudiwa kwa hapa, kama mtu mwenyewe anajihisi udhaifu, na kutovumilia Saumu atafuturu.

7. Ujue vile vile kwamba, msafiri (safari yenye umbali maalumu) si halali kwake kufunga hadi arudipo uwenyejini.

8. Pia kwa aliye na ugonjwa wa kifafa halazimiki kufunga na badala yake anaruhusiwa kula.

MZEE NA NAHODHA

Mzee mkubwa, na kadhalika vikongwe wasio na uwezo wa kustahamilia Saumu, wanaruhusiwa na sheria wasifunge na watoe sadaka ya kibaba (sawa na kilo kasorobo) kwa kila siku. Kibaba hiki kiwe ni cha chakula kitumiwacho sana na watu wa sehemu hiyo, na pia hukumu hii humhusu mwanamke anayenyonyesha na aliye na mimba wakijichelea au kuchelea wana wao, wanaruhusiwa na sheria kufuturu.

Isipokuwa hawa wawili wa mwisho watalazimika kulipa nyudhuru zao zikiisha kabla ya Ramadhani nyengine kufika.

Msafiri asafiriye umbali wa Km. 48 halazimiki kufunga, bali atafuturu ingawa haambiwi ale bali atajizuia vivyo hivyo na kulipa baada ya Ramadhani kumalizika. Na safari, sharti iwe ya halali; pia isiwe kazi yake kama kondakta, dereva nahodha n.k. asiwe atakaa huko zaidi ya siku 10 akiwa atakaa zaidi ya siku 10 atafunga hata huko huko safarini.

Kafiri wa kuzaliwa akisilimu halazimiki kulipa Saumu zilizompita alipokuwa ukafirini. Kadhalika mtoto akibaleghe, na aliyekuwa na kicha (wazimu). Ama aliyepitiwa na Saumu kwa kuwa na hedhi, nifasi, ugonjwa,n.k. hulipa.

PIA SALA

Ili kuthibitisha utiifu wetu kwa Mwenyezi Mungu na ili Saumu zetu zikubaliwe, ni sharti tutekeleze amri zake zote pasina kuziacha zingine. Sala ni mojawapo wa mahimizo makubwa kwa Mwislamu na lau atajisumbua kwa kuumwa na njaa bure pasina kusali, ajuwe kuwa hana fungu lolote katika Saumu yake. Kwa hivyo tukiwa tunataka thawabu zaidi na zaidi ni lazima sala hata tusiziache.

Sala ni nguzo ya pili katika nguzo za Islamu, na tukumbuke kwamba, tukiwa na sala pungufu, hata mali zetu zi katika mafungu yasiyotakikana, na zikiwa kamili, hata ibada zinginezo zitakuwa makbuli Inshaallah.

'NAFSI' NI ADUI

Mwenyezi Mungu Anasema,"Na kiwe katika nyinyi (Waislamu) kipote ambacho kitawalingania watu katika mambo ya kheri, kiwe kinaamrisha mema na kinakataza maovu.”

Kuamrishana mema na kukatazana maovu ni jambo la lazima kwa kila mwislamu awaye mume au mke, na hasa wakati wa Ramadhani.

Ingawa mwezi huu mashetani hufungwa kama ilivyopokewa katika hadithi, pana adui mwengine kwa mwanadamu ambaye husononeka sana anapomwona mwanadamu katika mwangaza wa utiifu, na ye si mwengine bali ni "Nafsi".

Mwenyezi Mungu Anasema:"Nafsi ni yenye kuamrisha (sana) maovu."

Mmoja wa wanavyuoni anasema: "Nafsi ni kitu kiovu zaidi ya mashetani elfu."

Nafsi hii hii ndiyo ambayo huwaghafilisha baadhi ya watu wasifunge mwezi huu, wala wasikumbuke kabisa adhabu ziwasubirizo wasiofunga.

Mtume(s.a.w. w ) alisema"Watu wasiofunga hufungwa miguu yao kwa pingu kisha wakaninginizwa vichwa vyao chini na miguu yao juu na huku wapigwa na kucharazwa mijeledi kemkem, pia huwa nyuma yao wale wanaokula kabla ya wakati maalum wa kufuturu haujafika."

Jee ndugu waona!!! Lakini lao kubwa ni kama alivyosema Mwenyezi Mungu katika Qur'ani: "Hakika wao wanaoiona (siku ya kiama) iko mbali nasi Tunaiona iko karibu sana."

Pia wanaofunga na huku hawasali, wao ni mfano mbaya sana kwa umma wa Kiislamu. Allah Anasema,"Adhabu kali sana itawathibitikia wale wanaosali na ambao wao katika sala zao hughafilika."

Waliokusudia hapa ni watu ambao wao husali leo kesho hawasali, husali asubuhi jioni hawasali na kadhalika. Ikiwa Mwenyezi Mungu Amekasirika hivyo hadi kufikia hatua ya kuapa kuwatia adabu wasiosali sawasawa, waonaje kwa yule asiyesali kabisa? Ama wasiosali wamewekeana mkataba na Mwenyezi Mungu wa kusameheana?

HIDAYA YA RAMADHANI

YANAYOHARIBU SAUMU

Kwa kuwa Mwislamu huwa na hamu kubwa ya kuukaribisha mwezi wa Ramadhani, kadhalika anatakiwa kuwa na hamu ya kujichunga na mambo ambayo huenda yakamharibia saumu yake. Na mambo yenyewe ni haya:

1. Kula japo kitu kidogo sana;

2. Kunywa hata kama ni tone moja;

3. Kumwingilia mwanamke mchana hata kama manii hayakutoka;

4. Kujitoa manii kwa kujichezesha, au kwa kumchezesha mwanamke hata kama ni mkeo pia kunatengua;

5. Kutooga Janaba, Hedhi, au Nifasi hadi alfajiri pasina sababu ya udhuru maalumu pia kunabatilisha Saumu;

6. Kujifikisha vumbi - zito - kooni makusudi na kadhalika moshi wa sigara pia hubatilisha;

7. Enema-Kupigwa bomba yenye kitu cha majimaji (dawa) kwenye tundu ya nyuma pia kutaharibu;

8. Kujitapisha makusudi;

9. Kumkadhibisha Mwenyezi Mungu au Mtume wake Mohammad(s.a.w.w) au Maimamu watakatifu kuwa katika jambo fulani walisema hivi hali ni uongo kunabatilisha Saumu;

10. Kujitosa majini makusudi kwa kupiga mbizi, au kukitumbukiza tu kichwa pekee majini pia kunaharibu Saumu.

MASWALA TOFAUTI

Ingawa kula kunabatilisha Saumu lakini kunasamehewa kwa mtu yeyote aliyekula kwa kusahau, vile vile kunywa. Ama kuyameza mate yaliyojaa kinywani, hakuna makosa.

Kuyameza mabaki yaliyaliyosalia menoni wakati wa kula ama kunywa, kunabatilisha.

Kukiangalia chakula kwa hali ya kukitamani na hali umefunga hakubatilishi Saumu. Lakini ni vizuri zaidi kutokiangalia ukiwa wakitamani.

Kudungwa sindano si makosa kwa mtu aliyefunga. Naam, ni vizuri kutumia Ihtiyat (yaani kujitoa mashakani) kwa kutodungwa sindano iliyo na chakula.

Kumbuka kwamba nia ni muhimu sana na Saumu haisihi pasina kutia nia. Kunuia huku ni kusema moyoni. "Nia yangu ni kufunga kesho kwa ajili ya Mwenyezi Mungu". Kadhalika amali zote za ibada hazisihi pasina nia maalum kama alivyosema Mtume(s.a.w .w ) :"Matendo yote hufanywa kwa nia" . Na hivyo basi nia ni muhimu sana.

Mwenye Saumu akiazimia usiku kwamba mimi kesho sito funga basi Saumu ya siku hiyo haitasihi hata kama atabadili dhamira na kufunga tena hivyo basi atalazimika kuilipa siku hiyo. Na tukumbuke tena kwamba, mtu yeyote aliyeitengua Saumu haimfalii kula au kuendelea na vitendo vilivyokatazwa, bali analazimika kujizuia.

Kusukutua wakati wa kutawadha hakukatazwi lakini ni bora kukuepuka maana huenda maji yakakutangulia pasina kutegemea. Ama kule kupiga mswaki nako ni hivyo hivyo.

Mtume(s.a.w. w ) alisema "Harufu ya mdomoni wa mwenye kufunga ni bora na yenye manukato zaidi kwa Mwenyezi Mungu kuliko marashi yoyote yale".

Ukimlazimisha mkeo kumwingilia na hali yeye mwenyewe hayuko radhi utalazimika kulipa na kutoa kafara, na pia kuaziriwa kwa kupigwa viboko 50. Na lau nyote mtaridhiana mtalazimika kulipa, kutoa kafara na kuaziriwa kwa kupigwa viboko 25 kila mmoja.

Ingawa tulieleza kwamba kutoka manii kwa kujimai (kuingiliana mke na mume) kunabatilisha Saumu na wanaohusika na kitendo hivyo huwa na janaba, hukumu hii haimhusu aliyetoka manii mchana wa Ramadhani kwa kuota usingizini, bali ataoga tu na Saumu yake haina dosari.

Udhuru wa kutokwa damu ya hedhi ukitokea japo bado kidogo tu magharibi kuingia Saumu yako itakuwa batili, na hivyo basi utalazimika kuirudia.

Kuteta katika mchana wa Saumu na hatimaye kupigana ni jambo baya sana na hasa kwa kuwa mwezi huu ni wa kusameheana, kuhurumiana n.k. Pindi ufungapo unapomuona mtu yeyote akikukabili na upuzi wowote ule, sema: "Innii Saaim", yaani:

“Hakika yangu mimi nimefunga” na ukifanya hivyo utakuwa umeukimbia uovu wote ambao huletwa na shetani.

Kutengua Saumu kwa jambo lolote la haramu kama kuzini, kulewa, na kadhalika, adhabu yake ni:

a. Kulipa siku 60 kwa siku mmoja iliyotenguliwa;

b. Kuwalisha maskini 60;

c. Kumwacha huru mtumwa.

HESHIMA YA RAMADHANI

"Mwezi wa Ramadhani ni ambao imeteremshwa humo Qur'ani kuwa mwongozo kwa watu..." (Qur'ani: 2:185)

Waislamu kote ulimwenguni hufunga mwezi ambao ni mwema kuliko miezi yote, ulio na masiku bora kuliko masiku yote, wenye masaa ya baraka kuliko masaa yote na amali zifanyikazo katika mwezi huo ni makbuli kuliko baki ya maombi. Nao ni mwezi wa Ramadhani.

Mwezi huu wa Ramadhani ambao ni mwezi wa tisa wa miezi wa Kiislamu, ni mwezi wa pekee wa aina yake kwa utukufu. Ni mwezi wa kusameheana, kuombeana heri na hata kufanya ibada kwa wingi na kwa usahali kabisa.

Mwezi huu una matukio mbali mbali ya kihistoria ambayo hayatasahaulika, na ambayo vile vile hupambanua wazi utukufu wake.

Imam Ja'far As-sadiq(a.s.) alisema kutoka kwa Babuye, Mtume(s.a.w. w ) "Taurati ilishuka na kumfikia Nabii Musa(a.s.) tarehe 6 Ramadhani, nayo Injili iIiteremshiwa Nabii Isa(a.s.) tarehe 12 za Ramadhani, kadhalika Zaburi ya Nabii Daud(a.s.) iliteremshwa mnamo tarehe 18 za Ramadhani, vile vile Qur'ani Takatifu iliteremka katika usiku wa Laylatul Qadri ambao kwa kawaida huwa katika mwezi huu wa Ramadhani."

Bila shaka hiyo ni heshima kuu kabisa. Na umejionea mwenyewe, hakuna kitabu kati ya vitabu vitukufu vinne kutoka kwa Mungu kilichoshuka ila kilishuka mwezi huu wa Ramadhani, na hayo yote ni kuonyesha utukufu wa mwezi huu. Kwa hivyo lazima vitendo vyetu katika mwezi huu viwe vitukufu kama mwezi wenyewe ulivyo.

Na katika Historia, tunasimuliwa baadhi ya matukio ya mwezi huu huu wa Ramadhani, kwa mfano:

1. Imam Hasan bin Ali bin Abi Talib(a.s.) mwanawe Sayyidna Ali(a.s.) wa kwanza, na Mjukuu wa Mtume(s.a.w. w ) alizaliwa mwezi huu wa Ramadhani tarehe 15 mwaka wa 3 wa tangu Mtume kugura toka Makkah kuja Madina. Mtume mwenyewe ndiyo aliyemfanyia Akiki kwa kumchinjia mbuzi alipotimiza siku 7. Sayyidna Hasan(a.s.) , kama ilivyokuja katika Historia, alimfanana sana Babuye, Mtume(s.a.w. w ) sehemu ya juu. Naye Mtume(s.a.w. w ) alimnbashiria kuwa"Bwana wa vijana wa peponi".

2. Vita vya Badr vinavyojulikana zaidi (vita vikuu vya Badr, au Ghazwatul Badr) vilitukia siku ya Ijumaa mwezi wa Ramadhani tarehe 17 mwaka wa 624 A.D. Vita hivi ndivyo vilivyopambanua baina ya wakweli na waongo. Mushirikina (waabudu masanamu) waliharibikiwa sana na Waislamu ndio walioibuka na ushindi.

3. Katika mwezi huu huu, Mtume(s.a.w. w ) aliirudisha Makkah chini ya himaya ya Kiislamu tarehe 10 mwaka wa 630 A.D. Baada ya kuiteka Makkah, dini ya Islamu ilizidi mno nguvu na makafiri kuharibikiwa.

4. Imam, Sayyidna Ali bin Abi Talib(a.s.) , bin Ami yake Mtume(s.a.w. w ) aliyezaliwa katika Kaaba, alipigwa upanga na adui wa Uislamu, Abdu Rahmani bin Muljim tarehe 19 ya mwezi huu wa Ramadhani mwaka wa 40 Hijria.

Alipigwa upanga msikitini huko Kufa, Iraq alipokuwa amekwenda kusali sala ya Alfajiri, na alifariki siku ya tatu yake, yaani tarehe 21 Ramadhani.

Sayyidna Ali(a.s.) , Simba wa Mungu alishirikiana sana na Mtume(s.a.w. w ) na kuhudhuria vita vyote pasina kukimbia na ndiye aliyebaki kitandani cha Mtume(s.a.w. w ) alipokuwa akihamia Madina.

NASAHA KWA VIJANA

Vijana wa Kiislamu! Mwezi wa Ramadhani umetuwadia, hatuna wakati mwengine tuutarajiao tena na kuutumaini katika kufuzu kwetu usio huu. Balaa zote za kutuletea maafa hapo kesho (Akhera) tuziepuke na tuwe mbali kabisa nazo.

Katika mwezi huu hakuna masingizio yoyote, ambayo tunaweza kujisingizia nayo kama vile kudai kwamba 'O'..... Shetani ametushika sana! Kwani Mtume(s.a.w. w ) ametudokezea kwamba, "Mwezi wa Ramadhani unapoingia, milango yote ya rehema huwa wazi (kuwapokea wanaotaka kuingia), milango yote ya Jahannam hufungwa na Mashetani wote hutiwa minyororo ili wasiwahangaishe."

Ajabu kubwa zaidi ni kijana wa Kiislamu kuvaa ushanga, mikufu na bangili namna wafanyavyo wanawake. Ni hadi lini watajisitahi na kuwa na haya juu ya haya wayafanyayo?

Ni aibu kubwa kwa vijana wa Kiislamu kuhalifu sheria za dini yao hasa katika mwezi huu. Kwa kila aliye na uchunguzi, atastaajabu sana kumwona mtu aliyekuwa mnyenyekevu mchana kutwa, msalihina, kubadili hali hiyo na kuufanya usiku kuwa sitara ili kumdumishia maasi yake.

Ikiwa hawatajinasihi katika muda huu wa rehma na maghfira wakumbuke kuwa wamo hatarini ya kupoteza imani.

Badala ya kuketi mabarazani kusengenyana na kufitiniana, tunahimizwa kuingia misikitini na kuendesha ibada mbali mbali na tukisome kitabu cha Mwenyezi Mungu kwa wingi yaani Qur'ani. Kwani pasi na kufanya hivyo, tutakuwa tunaupoteza wakati wetu ambao ni wa thamani sana kama ilivyopokelewa katika kauli za wahenga wa kiarabu kwamba: 'Wakati ni kama upanga, usipouvunja, (mwishowe) utakukata.'

KWA AKINA DADA

Dada wapendwa wa Kiislamu, mwezi mtukufu wa Ramadhani hutujia mara moja tu kwa mwaka. Tunapokaribia kuumaliza mwezi wa Sha’bani, huwa na furaha tele nyoyoni mwetu ya kuukaribisha mwezi wa Ramadhani. Na kwa wakati huu hatunalo ila kumshukuru Mumba wetu aliyetuongoza kwenye njia yake nyofu (ya Kusilimu), maana lau si Yeye, kamwe hatungeongoka.

Dada wapendwa, tunapaswa kukumbuka kwamba, kufunga siyo kutozingatia kula na kunywa tu na hatimaye kutayarisha futari, bali kufunga kunakotakikana ni kuzingatia maamrisho yake Sub'haanuhu Wata’ala na Mtumewe(s.a.w. w ).

Miongoni mwa maamrisho yake kwetu ni kuwatii waume zetu kwani Mwenyezi Mungu hako tayari kuzipokea Saumu zetu tukiwa na ufidhuli kwa waume zetu kwani Mola wetu Anatuambia katika Qur'ani:"Waume ndio wasimamizi wa wanawake."

Naye Mtume(s.a.w. w ) anasema kutufunza namna ya kutunza nyumba zetu kwamba"Mwanamke akifunga Saumu yake ya wajibu, asali sala zake fardhi na amtii mumewe, bila shaka ataingia peponi."

Huo ndio wajibu wetu. Ama mtindo wa kuwasengenya wenzetu, majirani zetu, waume zetu, au waume wa wenzetu ni kinyume cha dini ya Islam, na wakati wowote ule haitakikani kuendesha mikutano ya namna hii, na hasa katika Ramadhani, maana yanaweza kukuharibia Saumu yako.

Pia kujifahiri kubughudhiana, kukaripiana, kunyimana vifaa vya nyumbani kama shoka, chumvi, mwiko n.k. na kujiunga katika makundi ya karata hasa na waume ni dhambi isiyosameheka ila kwa kutubia hasa wakati kama huu wa Ramadhani.

JICHAGULIE MWENYEWE

Sote tukiwa Waislamu halisi na walio na gheri juu ya dini yetu tunapaswa kujihifadhi na kuutambua umuhimu wa uwajibu wetu. Katika Saumu hii ambayo huendelea nayo kila mwaka, tunapaswa kutambua kwamba wafungao wako makundi tofauti kadha wa kadha.

1. Wako watu ambao wao ni vijana wa Kiislamu, lakini kwa bahati mbaya wao hawajali na wala hawafungi kamwe wakidai eti kufunga kulianzishwa na Masheikh waliokuwa hawana chakula, na kwamba mtu aliye na chakula kufunga ni kama upumbavu.

2. Wapo watu wafungao lakini wao hufungana kujizuia chakula tu na kutotangamana na wake michana ya Ramadhani, ama katika mambo mengine wao huwa hawajali; kama kusengenya, kusema uongo, na kadhalika, huku wakiwa wamejisahaulisha kuwa hayo ni miongoni mwa yafuturishayo.

3. Kundi jengine hufunga na kufanya baadhi ya yatakikanayo, lakini huwa wao ni wenye kukereka na Saumu, na huwa wao ni wenye kuomba na kutaka Saumu imalizike haraka.

4. Kundi hili hufunga tena kwa unyenyekevu na hushinda misikitini, lakini ufikapo usiku ama Ramadhani imalizikapo, huanza vioja na kuanza upya kuyarejelea yaliyokuwa marufuku nyakati za Ramadhani, basi watu wa namna hii, ni sawa na mtu aliyeweka akiba ya Sh. 5000/- asubuhi, ili zimfae baadaye atakapopatwa na dhiki ya ghafla, na ufikapo usiku huzitumia zote katika starehe zisizo za lazima na kutobakisha kitu.

5. Wa mwisho, ni wale wafungao kwa Imani kamili na baada ya Ramadhani kumalizika wanaendelea na majonzi ya kusikitika kwani hawajui kama watajaaliwa tena kuifikia Ramadhani nyengine. Kundi hili ndilo la wafungao kikweli wajulikanao kama "Mo’ominoon" - yaani waumini halisi.

Ndugu mpendwa, unatakiwa kujikagua ili ujuwe kundi ulimo hivi sasa, la sivyo, kiri kutojitambua wewe mwenyewe.

Tunawatakieni nyinyi na sisi mwisho mwema ili tufungapo, tuimalize Saumu kwa baraka na amani ili iishapo tuwe kuendelea na utu wetu.

'SAUMU' KATIKA BIBLIA

Saumu kama ilivyopokewa katika Qur'ani kadhalika imepokewa katika vitabu vya dini mbali mbali.

Kulingana na ushahidi wa Aya tuliyoitaja huko nyuma inayosema "Enyi mlioamini, mmefaradhiwa kufunga kama walivyofaradhiwa wa kabla yenu ili mpate kumcha Mwenyezi Mungu! Ulazima wa Saumu kwa watu wote wa leo na wa kale umethibiti”

Ingawa katika Aya hiyo Mwenyezi Mungu atujulisha kama, jee Saumu tuliyofaradhiwa sisi ndiyo ile ile na kwa namna ile ile na kwa idadi zile zile walizofaradhiwa wa kabla yetu ama kwa namna iliyo tofauti? Hata hivyo si lazima juu yetu kujua.

Na Mwenyezi Mungu alitujulisha hili ili tusiwe na malalamiko (kama ilivyo ada ya mwanadamu) kuwa, kwa nini sisi tulazimishwe Saumu na hali wa kabla yetu hawakufunga na hali wao ni waja kama sisi? Ndiyo maana Akatujulisha mapema kabla ya nyudhuru zetu kutolewa. Ingawa ndugu zetu Wakristo wanatambua wazi Fardhi hii, kwa bahati mbaya wao hawakuijali bali wameyashughulikia mengine.

Hebu na tuangalie katika kitabu chao (Biblia - Agano jipya).

Katika Mathayo 6, kifungu cha 16 hadi 18 kumeandikwa hivi: "Tena mfungapo msiwe kama wanafiki wenye uso wa kukunjamana, maana hujiumbua nyuso zao ili waonekane na watu kuwa wanafunga. Amin nawaambia, wamekwisha kupata thawabu yao. Bali wewe ufungapo jipake mafuta kichwani, unawe uso, ili usionekane na watu kuwa unafunga, ila na Baba yako aliye sirini na Baba yako aonaye sirini atakujazi."

Pia katika Mathayo 4, kifungu cha 1-2 imeandikwa hivi: "Kisha Yesu alipandishwa na Roho nyikani, ili ajaribiwe na Iblisi. Akafunga siku Arobaini mchana na usiku, mwisho akaona njaa."

Ndugu mpendwa, jee pana udhuru wowote tena wa kutofunga kwa Wakristo baada ya ushahidi huu? Jee inafaa kutumia mbinu zozote zile za ulaghai ili kuupuza maamrisho ya Allah? Jee inasihi mtu kutangatanga mabarabarani akinadi kwa kila namna ya vishindo eti "Mimi nimeokoka.....Mimi nimeokoka..." Na hali anaihepa Saumu? Hasha Wakalla.......hilo haliwi.

2

TADWIN AL HADITH

UANDISHI WA HADITH

9. MAONI YA BAADHI YA SAHABA KUHUSIANA NA UANDIKAJI WA HADITH

Mbali na imani ya baadhi ya Sahaba kuwa Hadith zisiandikwe, kikundi miongoni mwao kiliendelea kufanya hivyo. Ukweli huu ni dalili yenyewe inayoelezea kuwa kuharamishwa kwa uandishi wa Hadith ulitokana na Makhalifa na wala si Mtumes.a.w.w. kama inavyodaiwa. Miongoni mwa Sahaba waliokuwa wakiamini ruhusa ya uandishi wa Hadith walikuwa Amir al-Muminiin Ali ibn Abi Taliba.s. na mwana wake al-Hasana.s. ambao si tu kwamba waliziandika Hadith, bali walitilia mkazo juu ya uandikaji wake pia.

Abdallah ibn al-Abbass, imeripotiwa kuwa alizoea kusema, "Ikamateni (kuitia mahabusi) 'ilim kwa njia ya kuiandika." Harun ibn Antarah anaripoti kutokea baba yake kuwa abd Allah ibn al-Abbass baada ya kuitamka hiyo Hadith aliyomwomba aiandike. Salami anaripoti kuwa yeye aliona vipande vya maandishi kwa Ibn abbass ambamo alikuwa ameandika matendo ya Mtumes.a.w.w. kama vile ilivyokuwa imesimuliwa na Abu Rafi. Imeripoti kuwa Anas ibn Malik alizoea kumwambia mwanae:"Ikamateni ilim kwa kuiandika." Al-Kattani anaripoti kuwa Ayadh alizoea kusimulia ruhusa ya kuziandika Hadith kutokea Sahaba na Tabi'un. Hata hivyo, wengi wa Sahaba, inavyoonekana, ama walikuwa hawana uhakika katika yale waliyoyaandika kuhusu kuruhusiwa kwa kuziandika Hadith au hawakuwa na ari ya kuyazingatia na kuyasisitiza hayo kimatendo; uthibitisho huo ni kule kujiepusha kwao katika ukusanyaji wa Hadith.

Zaazan anaripoti: "Mimi nilichukua baadhi ya maandishi (tasabih) kutoka Umm Ya'fur na kumwendea Imam Ali ibn Abi Taliba.s. Naye alinifundisha hayo na baadaye aliniambia nikayarudishe kwa Umm Ya'fur."

Imenakiliwa pia kwamba Ibn Abbass alizoea kuziandika Sunan za Mtumes.a.w.w. juu ya vibao vya kuandikia, ambazo alizichukua mwenyewe hadi pale palipokuwapo na mkusanyiko wa Wanazuoni. Pia imeanakiliwa kwa wingi (mutawatir) kuwa alipofariki aliacha vitabu vingi mno vinavyoweza kupakiwa juu ya ngamia mmoja. Kwa mujibu wa ripoti kuwa Abu Bakr aliandika baadhi ya Hadith baada ya Mtumes.a.w.w. na baadaye alizichoma moto, nayo pia inadalilisha kuwa uandishi wa Hadith ulikuwa ni desturi iliyokuwa inakubaliwa miongoni mwa Sahaba.

Riwaya iliyonakiliwa kutoka Imam Ali ibn Abi Taliba.s ambamo alisema kuwa yeyote aandikaye Hadith basi aandike pamoja na sanad yake navyo pia inaungana na mawazo hayo. Vianzio vyote vyote ni dhahiri kuwa idadi ya Sahaba walikubaliana kuwa uandishi wa Hadith ulikuwa umeruhusiwa. Ripoti kuhusu Sahifah ya Ja'abir ibn Abd Allah ambayo ilikuwanayo Hadith za Mtumes.a.w.w. pia inaunga mkono juu ya tabia na mazoea ya Sahaba katika uandishi wa Hadith zilikuwapo miongoni mwa Sahaba. Katika misingi hiyo, tunaweza kumalizia kuwa uandishi wa Hadith ulikuwa umekubaliwa na vikundi vya Sahaba na upinzani wa Mahalifa juu ya uandishi wa Hadith haukutokana na kukatazwa na Mtumes.a.w.w. kama inavyodaiwa, bali ulitokana na uamuzi wao wenyewe.

9. AL-QURAN NA UANDISHI

Al-Khatib al-Baghdadi, ili kuunga mkono maelezo yake juu ya ruhusa ya uandikaji wa Hadith, anaelezea uthibitisho kutokea aya za Qurani.Katika misingi ya Quran inayotuamrisha kuandika vyote vile ambavyo vina hatari ya kuweza kusahaulika, yeye anaelezea kuwa Hadith, ambayo pia ipo hatarini kupotea, basi ni lazima ziandikwe. Katika uhusiano huu yeye anaelezea aya zifuatazo za Quran 2:282, 6:91 na 31:157 Al-Tahawi, pia anaelezea akitoa Aya: "Wala msipuuze kuandika, mapatano yawe ni madogo au makubwa mpaka muda wake" (2:282) kuhusu uandishi wa madeni, anasema kuwa pale Mwenyezi Mungu anapotuamrisha kuandika madeni ili kuepukana na kutokezea mashaka na mizogo, na uhakika wa elimu ambavyo pia kuuchunga kwake ni vigumu kabisa na muhimu mno kuliko kurikodi madeni basi inasimama pamoja na umuhimu mno katika kuandikwa ili kuepukana na mashaka yaliyoelezwa hapo juu. Abu Hanifa, Abu Yusuf na Muhammad ibn al-Hassan al-Shaybani pia ni watu waliokuwa na msimamo kama huo.

10. MTUME S.A.W.W. KUHARAMISHA UANDISHI WA HADITH NA SABABU ZA KWELI

Uchambuzi wetu wa hapo mwanzoni unatuonyesha kuwa lawama zozote katika ucheleweshwaji wa uandishi wa Hadith hauwezi kamwe kutupiwa Mtumes.a.w.w. kwani riwaya zote zilizozuliwa juu yake haziwezi kamwe kukubaliwa kwa sababu mbali mbali. Katika jaribio hili, sisi tutakuwa tukitegemea mno juu ya riwaya zitegemewazo na Ahl al-Sunnah na penginepo tutatumia riwaya za Mashia. Ni mategemeo yetu kuwa msomaji ataweza kukadiria usahihi na ukweli wa uchambuzi huu kwa makini.

Aisha anaripotiwa kusema: "Baba yangu alikuwa amezikusanya Hadith mia tano za Mtumes.a.w.w. Asubuhi moja, alinijia na kusema,''Lete Hadith zote zilizopo kwako.' Nami nilizileta mbele yake. Yeye aliziunguza zote kwa moto na kusema: 'Nisije mimi nikafa huku nimekuachia vyote hivi.''

Imeripotiwa kwa mamlaka ya al-Zuhri kuwa: Umar alikuwa akitaka kuandika Sunan ya Mtumes.a.w.w. Yeye alikuwa akilifikiria kwa muda wa mwezi mmoja, alitarajia mwongozo kutokea kwa Allah swt katika swala hili. Siku moja asubuhi, alichukua uamuzi na kubainisha: "Mimi niliwakumbuka watu wote wale waliokwisha nitangulia, ambao waliandika na wakawa wamevutiwa mno katika yale waliyokuwa wameyaandika na ambao hatimaye walikiacha kitabu cha allah (yaani Quran)."

Abd al-'Ala ansema: "Qasim ibn Muhammad ibn Bakr alizoea kutamka Hadith mbele yangu. alisema kuwa kulikuwapo na ongezeko katika Hadith katika zama za Umar. Naye Umar aliamrisha Ahadith zote zikusanywe, na zilipokusanywa, alizichoma moto zote kwa pamoja, akibainisha: Kama muthnat ya Ahl al-Kitab 'Mathnat' kama inavyoonekana kilikuwa ni kitabu ambacho Mayahudi walikiandika wao wenyewe na ambacho kilikuwa ni tofauti na Taurati. Hapa Umar alikilinganisha kitabu hicho pamoja na Hadith za Mtumes.a.w.w. , ambavyo alikuwa hataki ziwepo pamoja na Kitabu cha Allah (yaani Quran). Yahya ibn Ju'dah naye pia ameripoti kuwa 'Umar alidhamiriwa kuandika hadith na Sunan. Lakini alibadilisha dhamira yake na kutuma ujumbe wake katika miji yote, ikibainisha:"Yeyote yule aliyenacho chochote kutokana na hayo, ayateketeze yote."

Imeripotiwa kutoka 'Urwah ibn al-Zubayr kuwa, "Umar ibn al-Khattaab alikuwa akitaka kuandika Sunan ya Mtumes.a.w.w. Kuhusiana na swala hili, alishauriana na Sahaba wengineo. Sahaba wote waliafikiana kuwa Hadith zote ziandikwe.Lakini Umar alikuwa akizingatia swala hilo hadi ikafika asubuhi moja alipochukua uamuzi wake wa kughairi hivyo, na akasema, 'mimi nilitaka kuandika sunan. Lakini baadaye nilijikumbusha watu walionitangulia ambao waliandika vitabu na kukiacha kitabu cha Allah (yaani Quran). Kwa kiapo cha Allah swt mimi sitakifunika Kitabu cha Allah kwa kitu chochote kile." Riwaya hii inatuonyesha kuwa Sahaba wote au angalau wale waliokuwa wameshauriwa walikubali juu ya uandishi wa Hadith. Lakini Khalifa, baada ya kufikiri kwa muda wa mwezi mmoja hivi, aliharamisha uandikaji wa Hadith katika misingi aliyoelezea yeye mwenyewe, jambo ambalo, bila shaka, halikuwepo pamoja na Sunnah za Mtumes.a.w.w. .

10. UPINZANI WA BAADHI YA SAHABA NA TABIUN KATIKA UANDISHI WAHADITH

Baada ya Khalifa kukataza uandishi wa Hadith, kwani mienendo yao ilichukuliwa na watu kama ni Sunnah, basi kikundi cha Sahaba na Tabiun pia walijiepusha na uandishi wa Hadith na walikuwa wakitegemea mno juu ya kile kimehifadhiwa akilini mwao.Wao walieneza Hadith kwa midomo tu na walichukia wazo la kuziandika. Kwao ilikuwa sivyo sahihi katika kuziandika Hadith za Mtumes.a.w.w . ambapo Quran na Mtumes.a.w.w . vyote vimeweka msisitizo mkubwa juu ya uandishi kwa ujumla. Abu Burdah anaripotiwa akisema kuwa baba yake alimwambia Abu Musa al-Ash'ari amletee chochote kile alichokuwa amekiandika kutokana na riwaya za baba yake.Na yote yalipoletwa, aliyaangamiza yote na alisema, "Wewe nae pia, kama sisi, lazima ukariri tu bila ya kuandika chochote." Abd al-Rahman ibn Salamah al-Jamhi anaripoti: "Mimi nilisikia Hadith ya Mtumes.a.w.w. kutoka kwa Abd Allah ibn Amr na niliiandika. Na baada ya kuhifadhi (kuikariri) akilini mwangu, nilikiteketeza kile nilichokiandika."

Asim alisema: "Mimi nilitaka kumwachia Ibn Sirin kitabu, lakini yeye alikataa kukiweka, akisema kuwa yeye hakutaka kuwa na kitabu chochote karibu yake." Abu Nadhrah asema: "Mimi nilimwambia Abu Sa'id awe akituandikia sisi, yeye alijibu, 'mimi sitawaandikieni na mimi siwezi kuwafanyieni chochote kama Quran kwa ajili yenu. Wewe uichukue (Hadith) kutoka sisi vile tulivyopokea kutoka Mtumes.a.w.w. ' Abu Sa'id alizoea kusema, Simulieni Hadith miongoni mwenu, kwani mmoja wenu anamkumbusha mwingine vile kujali." Imeripotiwa kuwa mamlaka ya Ibn Abi Tamin kuwa Ibn Sirin na wenzake wasingeliziandika Hadith.

Al-Harawi anaandika kuwa Sahaba na Tabiun walikuwa hawaziandiki Hadith na walikuwa wakizihifadhi akilini mwao, isipokuwa kitabu cha Sadaqa. Al-Nuwawi anaandika: "Mwelekeo wote wa Sahabah ulikuwa juu ya jihad, harakati dhidi ya matamanio ya mwili, na vile vile juu ya ibadah. Kwa hivyo wao hawakuwa na muda wa kunakili na kuandika (!).

Kwa sababu kama hizo, Tabiun pia hawakuweza kuleta chochote kile kilichoandikwa (tasnif)." Abu Kathir al-Ghubri anamnakili Abu Hurayrah akiwa amesema:"Ahadith zisifichwe wala zisiandikwe." Abd Allah ibn Muslim anaripoti kuwa Sa'id ibn Jubayr alikuwa anachukizwa na uandishi. Vivyo hivyo, Ibrahim al-Nakhai alibainisha kuwa yeye kamwe alikuwa hajawahi kuandika chochote. Wakati alipoulizwa sababu ya kutoandika, yeye alijibu, "Wakati mtu anapoandika kitu chochote, basi huja kutegemea juu ya yale aliyoyaandika."

Habib ibn Abi Thabit anaripotiwa kusema: "Mimi sina kitabu chochote ulimwenguni kote, isipokuwa kwa ajili ya Hadith ambayo ni kwa ajili ya sanda yangu."

Al-Hassan ibn Abi al-Hassan wakati wa kifo chake alimwamrisha mfanyakazi wake aliwashe tanuru na kuvitupa vitabu vyote alivyokuwa navyo isipokuwa kimoja tu. Ibn Sirin alikuwa akisema: "Iwapo mimi nitahitaji kuandika kitabu basi nitaandika kitabu juu ya barua za Mtumes.a.w.w. "

Yahya ibn Sa'id anasema: "Mimi niliwaona Wanzuonini katika hali ambayo wanapingana juu ya kunakili na kuandika." Suleyman ibn Harb anaripoti: "Yahya ibn Sa'id alitujia na alikuwa akisema Hadith. Mwanzoni mwenzi wetu walikuwa hawaziandiki Hadith alizokuwa akizisimulia, lakini baada ya muda kupita, wao walianza kuziandika."

Qasim ibn Muhammad ibn Abi Bakr alikuwa akimwambia Abd Allah ibn 'Ala asiwe akiandika Hadith. Sufyan ameripoti kuwa, pale alipoambiwa Amr ibn Dinar kuwa yeye alikuwa akiziandika Hadith za Amr, 'Amr alisimama na kusema, "Yeyote yule anayeziandika Hadith basi atoke hapa kwangu." Sufyan anasema kuwa kuanzia hapo hakuandika chochote kile alichokisikia kutoka Amr isipokuwa alikuwa akihifadhi tu.

Imeripotiwa kutoka Ibn Tawus kuwa baba yake alisema: "mtu mmoja alimwuliza Abd Allah ibn Abbass, swali ambalo lilimfurahisha mno. Huyo mtu alimwomba Ibn Abbass amwandikie jibu lake.Lakini Ibn Abbass alisema kuwa wao kamwe hawaandiki chochote kile kilicho cha 'ilim' Riwaya hii ipo katika mzozano pamoja na riwaya zinginezo zilizotangulia za Ibn Abbass.

Malik ibn Anas anaripoti kuwa Ibn Musayyab alipofariki, hakuacha hata kitabu kimoja. Vivyo hivyo ndivyo ulivyokuwa ukweli wa Qasim ibn Muhammad, Urwah ibn al-Zubayr na Ibn Shihab al-Zuhri. Mansur ibn Mu'tamir ameripotiwa akiwa amesema: "Mimi sijaandika chochote hadi leo." Na taarifa kama hiyo hiyo ipo imeripotiwa kutokaYunus ibn Ubayd. Imeripotiwa kuhusu Ibn Abi Dhu'ayb kuwa yeye alikuwa akikariri tu Hadith. Yeye alitokana na tabaka la tano na aliishi katikati ya karne ya 2 A.H./8 A.D. Imesemwa kuhusu Sa'id ibn Abd al-Aziz alikuwa haandiki chochote. Ismail ibn Ayyash, aliyetokana na tabaka la sita alikuwa amehifadhi akilini mwake kiasi cha Hadith elfu kumi lakini hakuandika hata moja. Abu Hatim anaripoti kuwa yeye kamwe hakuona chochote kilichoandikwa mikononi mwa Abd al-Walid al-Tayalisi. Wote hao walikuwamo katika tabaka la saba na walichukia mno uandishi wa Hadith. Pia imesemwa kuwa al-Nufayli kamwe hakuonekana pamoja na kitabu chochote. Vile vile Sahib al-Basri inasemekana alichukia mno uandikaji.

12. KITABU KINGINECHO MBALI NA QURAN

Kama itakavyoonekana kutokana na riwayah zinazotokana na wale wote waliokuwa wakizingatia kuharamishwa kwa Hadith kuandikwa, kwamba madai yao yote ya hasa kuficha ukweli yalikuwa ni khofu ya kutokezea kwa 'kitabu kinginecho mbali na Quran', na kwamba matokeo yake yatakuwa ni kutumika vitabu vingine na kuachwa kwa Quran. Hapa sisi tutajaribu kuchambua uhakika wa khofu kama hiyo na itaonekana wazi kuwa hayo yalikuwa ni hoja za kutaka kuuficha ukweli na wala hapakuwapo na makusudio mengineyo. Al-Quran na Sunnah vinakamilishana, na kama vile Waislamu wote wanavyoelewa kuwa kimoja hakikamiliki bila ya kingine - isipokuwa tu labda wale wenye kusema kuwa:"Kitabu cha Allah kinatutosha."

Jambo ambalo linahitaji kuzingatiwa hapa ni kuwa wale mabingwa wote wa kuharamisha uandishi wa Hadith iwapo wao walikuwa ni Makhalifa au wale waliofuata katika swala hili na waliweza kutumia hivyo kwa kuhalalisha tendo lao- walikuwa wakijua kauli ya Mtumes.a.w.w . kuhusu "Kitabu ubavuni mwa Kitabu cha Allah swt." Hata hivyo kimakosa au kimakusudi wao waliitumia visivyo hivyo kauli ya Mtume wa Mwenyezi Mungu. Ni kweli kuwa katika zama za uhai wa Mtumes.a.w.w. baadhi ya Sahaba waliweza kujipatia vitabu vya Taurati na vitabu vinginevyo vya Mayahudi. Na Mtumes.a.w.w. alipokuja kupata habari kuhusu hayo, aliwaambia wasivilinganishe sambamba na Kitabu cha Al-lah, al-Quran. Katika uhusiano huu itatubidi kuzingatia riwaya ifuatayo iliyonakiliwa na Jaabir. Jaabir anaripoti kuwa Umar al-Khattab alileta nakala moja ya Tawrati mbele ya Mtumes.a.w.w. na kusema: "Hii ni nakala ya Tawrati ambayo mimi huwa ninaisoma." Mtumes.a.w.w.

alikaa kimya lakini rangi ya uso wake ulibadilika. Abu Bakr aliiona hali hiyo, na alimwambia Umar, "Mama yako alie katika kilio chako, je, hauoni uso wa Mtumes.a.w.w .! Umar alipouona uso wa Mtumes.a.w.w. akasema, "Mimi najikinga na Mungu kwa ghadhabu za Mtumes.a.w.w. Mimi namkubalia Allah kama mmiliki wa vyote, Islam kama Dini na Muhammad kama Mtume." Juu ya hayo Mtumes.a.w.w. alisema:"Kwa kiapo cha Mungu, iwapo Musa angalitokea hapa na wewe umfuate yeye kwa kuniacha mimi, basi ungalikuwa umepotoka njia ya haki. Iwapo Musa angalikuwa hai na kuniona mimi, angalikuwa akinifuata mimi."

Mapokezi haya yanatuonyesha Mtumes.a.w.w. alivyokuwa amekasirishwa kwa sababu Umar alikuwa amekichukulia kitabu kingine sambamba na Quran. Katika mapokezi mengine kama haya, mtu kutoka Ansaar anachukua nafasi ya Abu Bakr. Inawezekana kuwa mapokezi hayo mawili yanatuelezea matukio mawili tofauti na kwamba tunaweza kuelewa kuwa matukio hayo mawili yametokea katika nyakati mbalimbali. Imepokelewa kutoka Abu Qalabah kuwa mara moja Umar ibn al-Khattab alipita karibu na mtu aliyekuwa akisoma kitabu. Baada ya kumsikiliza kwa muda mfupi, Umar alipendezewa na kile alichokisikia. Basi alimwomba mtu yule amwandikie kutoka kitabu hicho. Mtu huyo alikubali kumwandikia hivyo. Hapo Umar alilinunua jani na kumletea huyo mtu, ambamo mtu yule aliandika kwa kujaza sehemu zote mbili.

Baadaye Umar alifika mbele ya Mtumes.a.w.w. na kumsomea yaliyokuwa yameandikwa. Papo hapo rangi ya Mtumes.a.w.w. ilibadilika kwa ghadhabu. Basi hapo mtu aliyetokana na Ansaar alimwambia Umar: "Mama yako alilie kilio chako! Je, hauoni uso wa Mtumes.a.w.w. ? "Kwa hayo Mtumes.a.w.w. alisema: "Mimi nimetokezea kama Mtume, kama mfunguzi (fatih) na kama mfungaji (khatim), na mimi nimeleta kila kitu ambacho ilinibidi kujanacho (hivyo hakuna kilichobakia hadi nyinyi) kwenda kuvitafuta kutoka kwa watu wengineo."

Imeripotiwa kwa mamlaka ya al-Zuhri kuwa Hafsah binti yake Umar, alikileta kitabu chenye Hadith (masimulizi za Mtume Yusufa.s mbele ya Mtumes.a.w.w . Yeye alianza kukisoma huku Mtumes.a.w.w . akiwa akisikiliza na uso wake kubadilika rangi kuwa mwekundu. Hapo ndipo Mtumes.a.w.w . aliposema, "kwa haki ya Mungu, iwapo Yusuf mwenyewe angalikuja hapa na iwapo wewe ungalimfuata yeye na kuniacha mimi basi wewe ungalikuwa umepotoka." Riwaya hizi zote zinatuonyesha kile alichokuwa akikichukia Mtumes.a.w.w. kilikuwa ni maandishi mapotofu ambayo athari zake zilikuwa ni kueneza imani potofu za Mayahudi ambazo zilikuwa zikiitwa Israilayyat - miongoni mwa Waislamu. Mtumes.a.w.w. alikuwa hataki vile vitabu vya Mayahudi viwe sambamba na Quran Tukufu, maneno yote ambayo yalikuwa ni maneno ya Allah swt; katika vitabu vya Mayahudi kulikuwamo na visa na Hadithi za uwongo na zenye imani za ushirikina na kuamini uchawi, vinaweza kumfanya mtu apotoke na njia iliyo na mafundisho halisi ya Quran ambayo yameelezwa mbele yao.

Riwaya zilizoelezwa hapo juu pia zinaonyesha kuwa Khalifa na binti yake walikuwa wakipendezewa mno na usomaji wa vitabu kama hivyo na mara nyingine ilitokea kuchunguzwa na Mtumes.a.w.w. Hata hivyo, kwa bahati mbaya, tunaona kuwa baadaye ambapo Ka'aba al-Ahbar, Myahudi aliyesilimu kidhahiri tu, alipomwijia Umar na kumwomba ruhusa ya kuisoma Tawrati, Umar alimwambia: "Iwapo wewe unajua kuwa hiyo ndiyo Tawrati aliyokuwa ameteremshiwa Musaa.s . huko katika Milima ya Sinai, basi uisome usiku na mchana." Na haya ndiyo yaliyokuwa majibu ya Umar baada ya Mtumes.a.w.w. kumkataza yeye mwenyewe kutoisoma Tawrati wala mambo yoyote kama hayo.

Zipo riwaya zingine ambazo zinathibitisha fikara zetu kuwa Mtumes.a.w.w . alichokuwa akiharamisha kuwapo kwa kitabu sambamba na Quran yalikuwa ni maandiko ya Mayahudi yaliyokuwa yakitumiwa na Waislamu. Ipo imeripotiwa kuwa Abdallah ibn Mas'ud aliposikia kuwa watu walikuwanacho kitabu ambacho walistaajabishwa na yale yaliyokuwemo,basi alikichukua na kuki teketeza, akisema:"Watu wa vitabu (Ahl al-Kitaab) waliangamia kwa sababu wao walikuwa wakitegemea mno maandiko ya Wanazuoni wao (ulamaa) na walikuwa wamepuuzia Kitabu cha Allah (yaani Tawrati)" Neno ulamaa katika Waarabu wa zama hizo ilikuwa ikimaanisha Wanazuoni wa Kiyahudi na Kikiristo na vitabu vinavyozungumzwa katika riwaya hizi ni maandishi ya Kiyahudi.

Riwaya ifuatayo inaelezea vizuri zaidi swala hili. Murrah al-Hamdani anasema: Abu Murrah al-Kindi alikileta kitabu kutoka Syria (al-Shaam) na alimpatia Ibn Mas'ud alikipitia kitabu hicho, akaleta maji na kuyaosha yale maandishi yaliyokuwa yameandikwa katika kitabu hicho. Na hapo alisema, 'Watu walioishi kabla yenu waliangamia kwa sababu ya kuvifuata vitabu kama hivi na kukiacha cha Allah (yaani Quran)" Al-Husayn anasema, "Kwa hakika asingeteketeza maandishi hayo kama yangalikuwa ni Quran na Sunnah (yaani Hadith za Mtumes.a.w.w. Bali kilikuwa ni kitabu cha Ahl al-Kitaab."

Imam Ali ibn Abi Taliba.s . ameripotiwa akisema:"Yeyote yule miongoni mwenu aliyenacho kitabu (mbali na Quran na Sunnah) akiteketeze.Watu waliowatangulia nyinyi waliangamizwa kwa sababu ya kufuata masimulizi ya Wanazuoni wao huku wakikiacha Kitabu cha Allah (yaani Quran)."

Al-Imam al-Sadiqa.s . ameripotiwa akisema: "Baadhi ya Wanazuoni wapo wanafuatilia riwaya za Mayahudi na Wakristo, huku wakitegemea kuongeza elimu yao. Watu kama hao, nafasi yao ipo chini mno ndani mwa Jahannam. Imeripotiwa kwa mamlaka ya amr ibn Yahya ibn Ju'dah kuwa kilipokuwa kimeletwa kitabu mbele ya Mtumes.a.w.w. alisema: "Inatosheleza kwa upumbavu na upotofu wa Ummah kwa kuyaacha yale yaliyokuwa yameletwa na Mtume wake na kuanza kuangalia yaliyokuwa yameletwa na Mitume mingine." Riwaya hii pia inatuonyesha aina ya kila kitabu kilichokuwa kimeletwa mbele ya Mtumes.a.w.w. na pia kutupia nuru juu ya maana ya: 'Kitabu sambamba na Kitabu cha Allah (yaani Quran).'

Vile vile Ibn Abbass anasema: "Je utawaulizaje swali Ahl al-Kitaab kuhusu matatizo wakati ambapo Al-Qur'an ipo miongoni mwetu ?" Riwaya na masimulizi na mapokezi yote haya yanaonyesha kuwa Mtumes.a.w.w. aliharamisha kutayarishwa kwa kitabu sambamba na Quran huku akitahadharisha hatari ya uingiliaji wa Israiliyyat na kamwe, vyovyote vile, hakumaanisha Sunnah yake, ambayo ipo imeshikamana (wajib al-'ita'ah), kama vile wanavyokubalia Waislamu wote. Mabishano yetu yanazidi kupata nguvu kwa uhakika kuwa Wanazuoni wa Hadith wa Islam walikuja baadaye wakaziandika na kuzikusanya Hadith. Ama kwa mfano wa wale kama 'Urwah walichoma moto Hadith walizokuwa wameziandika kwa kudai kuwa "sisi hatutaki kuwanacho kitabu sambamba na Kitabu cha allah (al-Quran),' basi ni lazima tuseme kuwa wao walitenda kwa sababu ya kutoelewa vyema mafhumu ya kauli ya Mtumes.a.w.w.

Kama itakavyokuwa imeonekana hapo awali kuwa sisi hatuwezi kusema kuwa Mtumes.a.w.w. ndiye aliyehusika na uharamishwaji huo wa kuziandika Hadith; na msimamo kama huo unaweza kuchomoza maswali ambayo hayana majibu. Ilieleweka hapo awali kuwa baadhi ya Makhalifa walihusika moja kwa moja katika swala hili la kutoziandika Hadith na wao ndio walioharamisha uandishi wa Hadith. Hapa, baada ya kutaja sababu zilizotolewa nao kwa kuchukuwa hatua kama hiyo, sisi tutajaribu kutafuta maelezo yake. Baada ya kuthamini sababu chache zilizotolewa nao katika swala hili, sisi tutajaribu kuelezea kile tunachokiona kuwa ndiyo sababu maalum kuhusiana na uharamishwaji huo, pamoja na uthibitisho wa kutosheleza katika kuugana na maelezo yetu.

13. SABABU ZILIZOTOLEWA KWA KUHARAMISHA UANDISHI WA HADITH ZA MTUME S.A.W.W.

1. Sababu ya kwanza iliyotolewa ni khofu ya watu kushindwa kutofautisha baina ya Quran na Hadith za Mtumes.a.w.w. ambazo zingalisababisha uharibifu (tahrif) wa maandiko ya Quran, madhambi yasiyo samehewa. Mazungumzo haya, ambayo hayawezi kukubalika, yamekanushwa na Ustadh Abu Riyyah katika maneno yafuatayo: "Mtu kama huyo anaweza kuwashawishi watu wa kawaida, lakini haiwezi kukubalika kiutafiti. Kwa sababu itakuwa ikimaanisha kuwa ufasaha wa Quran unasimama sawasawa na ufasaha wa Hadith za Mtumes.a.w.w. Kile anachokimaanisha hapa ni muujiza wa ufasaha wa Quran unavyo tambulikana miongoni mwa watu, hatuwezi kudai kuwa wao wangalikuwa chini ya upotofu kwa kuzichanganya aya za Quran kwa Hadith za Mtumes.a.w.w, ambazo zipo chini kwa kulinganishwa na ufasaha wa Quran. Msimamo kama huu, kwa hakika unamfanya mtu akipingana na muujiza wa Quran.

Zaidi ya hayo, kuamini katika uwezekano wa kuchanganyika kwa Aya za Quran na Hadith ni sawa na kuamini katika uwezekano wa kuja kupotea kwa maandiko ya Quran. Imani kama hiyo inakanushwa kwa sababu uhalisi wa Quran upo unathibitishwa na Allah swt katika Quran: Sura Hijr, 15:9. Tunaweza kusema zaidi ya hayo kuwa kikundi cha Sahaba walikuwa wamehifadhi moyoni mwao Quran nzima, na kwa uangalifu mkubwa na upendo wao mkubwa juu ya Quran. Hatuwezi kamwe kuwafikiria kuwa wao walikuwa na hatari ya kuchanganyikiwa baina ya Quran na Hadith. Sisi twaweza kusema kuwa labda kulikuwapo na hatari ya uwezekano tu, na uwezekano huo hauwezi kupewa uzito sawa na madhara na hatari za kutoziandika Hadith. Madhara yaliyokuwa yameshajulikana kuanzia awali kabisa Shabaha hawakukubaliana miongoni mwao katika siku za awali kuhusu baadhi ya Shariah za Kiislamu na ilikuwa ni dhahiri kuwa athari za ufarakano huo ungelikuwa na hatari kubwa iwapo Hadith za Mtumes.a.w.w. zingalikuwa hazikuandikwa. Lakini hatari hiyo ilitokea tu. Baina ya tishio la zamani na hatari fulani, iliwabidi wao walitilie mkazo swala la uandishi wa Hadith, ingawaje, kimsingi swala la kutoruhusu uandishi wa Hadith halikuwa na uzito wowote.

2. Maelezo ya pili yatolewayo na Abu Riyyah yanasema baada ya kukubalia uharamisho wa kuandika Hadith ulitokana na Mtumes.a.w.w. kwamba Mtumes.a.w.w. alitaka maamrisho ya Shariah yawe katika mipaka iliyodhibitiwa na alipinga kueneza zaidi kwa maamrisho ya Shariah (adillah). Haya, kwa mujibu wake, ni sababu ambayo pia inatokana na nyakati zinginezo ambapo Mtumes.a.w.w. alichukia kuulizwa maswali. Sababu hiyo hiyo ipo inatumika katika hali ambapo Hadith ambazo zilikuwa sahihi katika kipindi fulani na ambapo haikuruhusiwa kufuata hapo baadaye.

Sisi tunachukulia maelezo hayo kuwa ni dhaifu mno, kwani haiwezekani kamwe kudai kuwa Mtumes.a.w.w. alipinga kwa kuenea Hadith halali kisheria zikitumika kama misingi ya kanuni halali za shariah. Je, itawezekanaje kwetu sisi kukubaliana nayo wakati Quran na Hadith kwa pamoja zinawajibika kujibu mahitaji katika sura mbalimbali ya Shariah kwa ajili ya siku ya Kiyama na siku zote kutoa maongozi kwa mwanadamu? Pamoja na hayo, sisi tutaelezea tena kwa mara ya pili kuwa sisi hatuamini ya kwamba Mtumes.a.w.w. alitoa amri ya kuharamisha uandishi wa Hadith.

3. Al-Awzai anatoa maelezo mengineyo, anaandika: "Sayansi ya Hadith ni tukufu pale inapoenezwa kwa mdomo tu, inawafanya watu wakumbushana daima Hadith. Lakini, pale inapoandikwa, nuru yake inafifia na pia huweza kufikia mikono ya watu wasiostahili kupatiwa." Sisi tunaweza kuonyesha kuwa ingawaje kuenezwa kwa Hadith kwa mdomo kuna faida ya kukumbusha watu yaliyomo ndani mwa Hadith, utumiaji wake kama halisi, na pekee, njia za kuzirekodi hizo zipo mashakani. Kwa hakika, faida kama hizo ziliambatana na madhara makubwa mno. Hata hivyo, hii ndiyo sababu mojawapo ambayo al-Awzai ameibuni, na ipo inashukiwa iwapo ikizingatiwa na wale waliokuwa wameharamisha uandishi wa Hadith.

4. Ibn Abd al-Birr, anaandika wakati wa kutoa maelezo kama hayo: Uandishi wa Hadith uliharamishwa ili watu wasitegemee mno yale yaliyoandikwa na wao, wakiepukana na huzihifadhi. Katika hali kama hiyo, desturi ya kuhifadhi moyoni Hadith ingalikuwa imepotea. Wazo kama hilo pia haliwezi kukubalika, kwa sababu madhara yaliyotokana na kushindwa kuziandika Hadith yalikuwa ni makubwa mno kwa kulinganishwa na faida iliyotokana na kupigwa marufuku kwa uandishi wa Hadith. Ustaarabu na utamaduni wa mwanadamu umekuwa ukilindwa kwa kupitia maandishi na wala si kwa kusema tu, ingawaje kuhifadhi Hadith kwenyewe ni tabia nzuri na yenye maana.

5. Sababu nyingine imetolewa pamoja na haya ni kwamba iwapo Hadith zingalikuwa zimeandikwa basi watu wangalikuwa wameiacha Quran huku wakizipatia Hadith umuhimu wote. Mazungumzo hayo pia hayawezi kuchukuliwa kuwa ni kinga, kwani jambo kama hilo linaweza kusemwa iwapo Hadith itakayomaanishwa itakuwa ni zile zisemwazo kwa mdomo tu, na Quran kwa upande wa pili. Ni kweli kabisa kuwa kupitia umuhimu wote Hadith ni upotofu ambao wale wafanyao hivyo waonywe na wachukue umuhimu kama huo katika Quran. Lakini uharamisho wa uandishi wa Hadith, umeleta uharibifu usioweza kutegemewa katika utamaduni wa Islam, kwa njia hiyo si ya kupatikana kwa matokeo sahihi.

6. Abjad al-'ulum anaandika: "Sahaba na Tabi'un, kwa sababu ya uhalisi wa imani yao na kuwapo kwao karibu na kipindi cha Mtumes.a.w.w ., na kutokuwapo kwa mabishano na uwezekano wa kuwaelekea watu waliotegemewa, hawakuwa na hitajio la kuziandika Hadith na shariah.Lakini vile Islam ilipoanza kuenea penginepo, wao walianza kuzikusanya na kuziandika Hadith, Fiqh na tafsiri ya Quran.' Kile anachokitaka kukisema huyu mwandishi siyo sababu ya kupinga kwa baadhi ya Sahaba kwa ajili ya uandishi wa Hadith, bali ni maelezo tu- nayo pia siyo sahihi- ni kwa nini Hadith hazikuandikwa; sababu yake halisi ilikuwa ni kupingwa kwa uandishi wa Hadith, na wala si kutohitajika kama vile anavyodai mwandishi huyo. Zaidi ya hayo, ueneaji wa Islam ulitokea katika miaka ya ishirini au zaidi ya miaka hamsini baada ya kifo cha Mtumes.a.w.w. Uandishi na ukusanyaji wa Hadith ulicheleweshwa hadi kufikia nusu ya karne ya 2 A.H./8 A.D. mbali na nukta hizo mbili inaeleweka kuwa sifa hii ya kumzulia Mtumes.a.w.w. ilianza katika maisha yake, na hatimaye iliweza kuongezeka kwa sababu ya kutokuwepo kwa Hadith zilizoandikwa. Pia ilikuwa ni wajibu wa Sahaba, ambao walitofautiana miongoni mwao katika mambo ya Shariah, kuzuia kukua kwa upotoshi na tofauti kwa kuanza kuziandika Hadith.

8. Sababu hasa ambayo ipo nyuma ya kuharamishwa kwa uandishi wa Hadith, ambayo mimi ninaamini, imeelezwa na mwanachuo mashuhuri aitwaye Sayyid Jaafar Murtadha na imethibitishwa kwa ushahidi uliopo:- Kulikuwapo na madhehebu mawili miongoni mwa Mayahudi. Dhehebu moja waliamini katika uandishi wa Hadith, ambapo dhehebu la pili halikuafiki hivyo, waliamini katika kutoandika chochote kile isipokuwa Taurati peke yake. Kundi hili la pili liliitwa Qurra (wasomaji). Haya yapo yamedokezwa na Dhadha katika kitabu chake cha fikara za Dini ya Kiyahudi. Ka'aba al-Ahbar Myahudi aliyesilimu (katika zama za Umar) alitokana na kundi hilo la pili. Mara moja Umar alimwuliza swali kuhusu mashairi ya vitu avisemavyo kuhusu Waarabu, kuwa kikundi cha kizazi cha Ismail, walikuwa wamehimili Biblia katika nyoyo zao na walizungumza kwa busara.....Labda inawezekana kuwa Khalifa alilichukua wazo hilo (la kutoandika chochote kile isipokuwa Quran tu) kutoka kwa Ka'b al-Khalifa na vile vile alikuwa akiheshimiwa kwa ushauri wake.

Zaidi ya hayo, uharamisho juu ya uandishi wa Hadith ulikuwa ukienda vyema pamoja na Siasa za tawala, kwani waliweza kuyazima malalamiko dhidi yao na kuendelea kuimarisha utawala wao. Kwa hakika hatua kama hiyo inawezekana kuwa na matokeo ya upotezi wa sehemu ya Hadith izungumziayo juu ya haki za wapinzani na ustahiki na ambayo ilifaa kuletea nguvu sehemu walizokuwa wamezidhibiti. Mtunzi huyo, kama vile taarifa yake ionyeshavyo, anadhani zipo sababu mbalimbali zilizosababisha kuharamishwa kwa Hadith, moja na muhimu kabisa ni kushawishiwa kwa mawazo ya Ahl al-Kitab juu ya Khalifa wa pili, ambaye, inavyoonekana, alipenda kusoma vitabu vyao kuanzia wakati aliposilimu. Uthibisho unaothibitisha ushawishi huu ni riwaya ya Urwah ibn al-Zubayr, isemayo kuwa Khalifa alikuwa amenuia kukusanya 'sunan' na hata pia aliwasiliana na Sahaba wengineo juu ya mpango wake huo. Wao walikubaliana nalo, lakini alibadilisha mpango wake huo kwa kusema kuwa watu wa Ahl al- Kitaab waliviacha vitabu vitukufu na kuanza kuvifuata vile walivyokuwa wameviandika na hivyo yeye hakutaka kufuata kitakachotokea juu ya Quran kama hivyo ilivyokuwa imetokea.

Ni jambo la kuweza kutokea kuwa maelezo hayo ya Khalifa yaliletwa na Ka'b al-ahbar, aliyetokana na kikundi cha Qurra, ambaye alijiepusha na kuandika chochote kile mbali na Tawrati. Ka'b alikuwa na njama mbaya dhidi ya Islam; ingawaje Khalifa alikuwa hana nia kama hizo, naye, kwa bahati mbaya, alishindwa kuona kwa kupitia ulaghai wa Ka'b. Mabishano ya Umar dhidi ya uandishi wa Hadith yalirudiwa na wengineo. Abu Burdah anaripoti kutokea baba yake aliyesema: "Banu Israil waliandika vitabu na kukiacha Kitabu cha Allah." Hakam ibn Atiyyah anaripoti kutokea Muhammad (bila shaka, Muhammad ibn Sirin) kuwa alizoea kusema: "Imenukuliwa kuwa Banu Israil walipotoshwa kwa sababu ya vitabu walivyovirithi kutokea mababu zao."

Mwanachuoni mwingine anaandika: "Moja ya ushawishi mkubwa wa Mayahudi juu ya Waislamu ulikuwa ni kuepukana na desturi ya kuandika Hadith. Imeandikwa katika Talmud, "Nyinyi hamna haki ya kuandika mambo ambayo munayazungumzia tu. "Huwezi kupinga kuwa Waislamu hawaku shawishiwa na Ka'b al-ahbar katika swala hili, ingawaje wao waliileta mbele katika sura ya Hadith ya Mtumes.a.w.w. Ushahid wake ni amri iliyotolewa na Khalifa baada ya kuzichoma Hadith alizokuwa amezikusanya: "Mathnat (au Mishnah) kama Mathnat ya Ahl al-Kitab." Maneno haya pia yanatuonyesha vile alivyokuwa ameshikamana pamoja na desturi za Mayahudi. Abu Ubayd katika Gharib al-Hadith, anaandika: "Mimi nilimwuliza mwanachuo wa Taurati na Injili kuhusu neno 'Mathnat.' Yeye alinijibu: "Mapadre wa Kiyahudi na waalimu wa Kiyahudi waliviandika baadhi ya vitabu baada ya Musa, mbali na vitabu vitukufu, na ambavyo wao waliviita kwa jina la 'Mathnat.'

Ni dhahiri kuwa Khalifa alikuwa akiufuata mfano wa Mayahudi ambao wao walikuwa katika kambi mbali na iliyoelezwa hapa. Abu Ubayd anaendelea kusema: Baada ya kupata maelezo hayo, mimi nimeelewa maana ya riwaya hii. Na hii ndiyo iliyokuwa sababu Abd Allah ibn Amr ibn al-As alikuwa akichukia kukichukua chochote kile kutokea kwa Ahl al-Kitaab, ingawaje yeye alikuwa na baadhi ya vitabu alivyovipata wakati wa kampeni ya Yarmuk (kutokea Makanisa ya Kiyahudi).

Abu 'Ubayd anaongezea: "Ni lazima, uharamisho (wa uandishi na usambazaji) haukuhusiana na Hadith na Sunnah za Mtumes.a.w.w. , kwa sababu itawezekanaje kuharamisha uandishi wa Hadith wakati ambapo wengi wa Sahaba wenyewe walikuwa wakinakili Ahadith. Hii inatuonyesha waziwazi kuwa Umar aliharamisha uandishi wa Hadith za Mtumes.a.w.w. na Sunnah zake kwa sababu yeye alichukulia msimamo kama ule wa maandishi yaliyokuwa yametolewa na waalimu wa Kiyahudi. Kwa hivyo, badala ya kuangalia na kuchunga kuenea kwa imani za Isra'iliyyat, yeye alikuwa ameshawishiwa nayo, ushawishi ambao ulisababisha katika kuangamizwa kwa Sunnah za Mtumes.a.w.w. Vile vile ni lazima iongezwe kuwa Abd Allah ibn Amr mwenyewe alikuwa mmoja wa waenezaji wa 'Isra'iliyyatambaye kamwe alikuwa si mtu aliyechukiwa mbele yao. Ilikuwa ni kwa sababu ya elimu yake ya Tawrati kwamba watu walimwambia awaeleze tabia ya Mtume mmoja.

Kile kilichotokea, katika mtizamo wetu, ni hivi: "Hadith za Mtume s.a.w.w. kwa ujumla hazikuandikwa hadi kufikia mwishoni mwa karne ya 1 A.H./7 A.D., ingawaje baadhi ya Sahaba walipendelea uandikaji wake na vile vile wengineo walikuwa na vibao vilivyokuwa vimeandikwa Hadith. Uandikaji wa hapa na pale ulianza kutokea katika karne ya 2 A.H. /8. A.D. , lakini ukusanyaji na uandikaji wa Hadith ulianza kwa nguvu mwishoni mwa karne ya 2 A.H./8 A.D., na hasa katika karne ya 3A.H./8 9 A.D. Ingawaje inawezekana kuwa wakusanyaji walikuwa na mkusanyiko usio na utaratibu (kwani walikuwa wakikusanya chochote kile walichokipata bila ya kufanyia utafiti juu ya usahihi wake au ni nani aliyeileza), ni dhahiri kuwa wingi wa Hadith walizozikusanya zilikuwa zimetokana na kutamkwa tu. Ushahidi uliopo ni kwamba uandishi mdogo kabisa-ambao hauwezi kulinganishwa na kazi kubwa ya ukusanyaji wa Hadith-zipo dalili kidogo kabisa zenye kuonyesha kuwa kulikuwepo na uandishi wa Hadith katika karne ya 2 A.H./88 A.D. Hivyo inaweza kusemwa kuwa Hadith hazikuwa zikiandikwa kwa kipindi kirefu na zilikuwa zikisemwa kwa midomo tu bila ya kuandikwa katika kipindi hicho.