JOHARI ZA HEKIMA KWA VIJANA

JOHARI ZA HEKIMA KWA VIJANA28%

JOHARI ZA HEKIMA KWA VIJANA Mwandishi:
: HEMEDI LUBUMBA SELEMANI
Kundi: Vitabu mbali mbali

JOHARI ZA HEKIMA KWA VIJANA
  • Anza
  • Iliyopita
  • 11 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 16133 / Pakua: 4464
Kiwango Kiwango Kiwango
JOHARI ZA HEKIMA KWA VIJANA

JOHARI ZA HEKIMA KWA VIJANA

Mwandishi:
Swahili

1

2

4

JOHARI ZA HEKIMA KWA VIJANA

3 - SEHEMU YA TATU

VIZUIZI VINAVYOZUWIA USTAWI WA VIJANA

KUTOJISHUGHULISHA

KUTOKUJISHUGHULISHA KWAKEMEWA

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Hakika Mwenyezi Mungu anamchukia mwenye siha asiyejishughulisha, hayupo katika kujishughulisha na dunia wala katika kujishughulisha na akhera ." [336] 335

Imam Ali(a.s) amesema: "Ikiwa kujishughulisha ni taabu basi kuendelea na kutojishughulisha ni uharibifu ."[337]

Imam Ali(a.s) amesema: "Moyo usiyojishughulisha hutafuta mabaya. Na mkono usiojishughulisha hupelekea kwenye ubaya ."[338]

Imam As-Sadiq(a.s) amesema: "Atakayefanya uvivu kwenye tohara yake na Swala yake basi hana kheri na jamabo la akhera yake. Na atakayefanya uvivu kwenye jambo litakalotengeneza maisha yake basi hana kheri na jambo la dunia yake ."[339]

Imam As-Sadiq(a.s) amesema: "Mwenyezi Mungu anachukia kuendekeza kulala na kuendekeza kukaa bila kujishughulisha ."[340]

Imepokewa kutoka kwa Umar bin Yazid amesema: "Nilimwambia Abu Abdillah(a.s) : Mtu anayesema: 'Nitakaa nyumbani kwangu, nitaswali, nitafunga na kumwabudu Mola wangu Mlezi. Ama riziki yangu itaniijia yenyewe.' Abu Abdillah(a.s) akasema:'Huyu ni mmoja kati ya watu watatu ambao dua zao hazijibiwi ."[341]

Asbatu bin Salim amesema: "Niliingia kwa Abu Abdillah(a.s) akatuuliza kuhusu Umar bin Muslim amefanya nini? Nikasema: Ni mwema lakini yeye ameacha biashara. Abu Abdillah(a.s) akasema: 'Kazi ya shetani.' Mara tatu. Kisha akasema:'Hivi hajui kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) alinunua bidhaa kutoka Shamu ndipo akajipatia riziki ambayo alilipia deni lake na kuwagawia karaba zake ."[342]

Zararah amesema: "Mtu mmoja alimjia Abu Abdillah(a.s) na kumwambia: 'Mimi siwezi kufanya kazi vizuri kwa mkono wangu, na wala siwezi kufanya vizuri biashara, nami ni muhitaji mwenye haja.' Akamwambia:'Fanya kazi, beba juu ya kichwa chako, na usiwahitajie watu ."[343]

Imepokewa kutoka kwa Al-Mufadhal bin Umar amesema: "Tafuteni msaada kupitia sehemu ya dunia kwa ajili ya akhera, kwani hakika mimi nimemsikia Abu Abdillah(a.s) akisema:'Tafuteni msaaada kupitia sehe- mu ya hii ili mpate hii. Na wala msiwe wategemezi kwa watu ."[344]

Imam Al-Kadhim(a.s) amesema: "Hakika Mwenyezi Mungu Mtukufu anamchukia mja mwenye kulalalala asiyejishughulisha ."[345]

MADHARA YA KUTOJISHUGHULISHA

Ibnu Abbas amesema: "Mtume wa Mwenyezi Mungu alikuwa amuonapo mtu na akavutiwa naye husema: 'Je ana kazi?' Wakimwambia hana, basi husema: 'Hana nafasi tena kwangu.' Huambiwa: Vipi hilo ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu? Husema:'Kwa sababu muumini akiwa hana kazi ataishi kwa dini yake ."[346]

Imam Ali(a.s) amesema: "Ujinga hutokana na kutojishughulisha ."[347]

Imam As-Sadiq(a.s) amesema: "Huko Madina kulikuwa na mtu asiyejishughulisha ambaye watu walikuwa wakimcheka. Akasema: 'Huyu mtu -Yaani Ali bin Husein - amenishinda kumchekesha. Basi akapita Ali(a.s) akiwa na vijana wake wawili, ndipo mtu yule akaja na kumnyang'anya joho lake toka shingoni, kisha akaondoka na wala Ali(a.s) hakumgeukia. Wakamwendea na kumnyanganya joho, wakalileta kwake na kumtupia. Umam(a.s) akawauliza ni nani huyu? Wakamwambia: Huyu ni mwanaume asiyejishughulisha huwa anawachekesha watu wa Madina. Basi akasema: 'Mwambieni:Hakika Mwenyezi Mungu ana siku ambayo wasiyojishughulisha watapa hasara humo ."[348]

Luqman(a.s) alisema: "Wenye hesabu kali siku ya Kiyama ni aliyetoshelezwa asiyejishughulisha, kwani ikiwa kujishughulisha ni taabu basi kutokujishughulisha ni uharibifu ."[349]

ULEVI

KILA KILEVI KIMEHARAMISHWA

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Fahamuni kila kilevi ni haramu, na kila kilegezacho ni haramu. Kila kileweshacho kwa wingi ni haramu hata kwa uchache. Na kila kichanganyacho akili ni haramu ." [350]

Ummnu Salamah amesema: "Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) alikataza kila kilevi na kila kilegezacho nguvu ."[351]

Imam Al-Kadhim(a.s) amesema: "Hakika Mwenyezi Mungu hajakataza pombe kwa ajili ya jina lake, lakini aliikataza kutokana na matokeo yake. Basi kila ambacho matokeo yake ni sawa na pombe nacho ni haramu ."[352]

TAHADHARI DHIDI YA MADAWA YA KULEVYA

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Umma wangu utafikiwa na zama watakuwa wanakula kitu jina lake ni Banji [353] .Mimi najitenga nao na wao wako mbali na mimi ."[354]

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Mtoleeni salamu Myahudi na Mnasara, lakini msimtolee salamu mlaji wa Banji ." [355]

(Nasema: Huenda kwa sasa ni aina moja ya madawa ya kuilevya ya kisasa. Na huenda ikawa ni jamii fulani ya milungi, japo maumbile yanatofautiana, kwani hata hii huliwa kama iliwavyo milungi.) - Mfasiri.

RAFIKI MBAYA

MADHARA YA RAFIKI MBAYA

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Mfano wa mwenza aliye mwema ni mfano wa muuza manukato, ikiwa hatakupa manukato yake basi harufu yake itakupata. Na mfano wa mwenza muovu ni mfano wa muhunzi, ikiwa hatakuunguza nguo yako basi harufu yake itakusibu ." [356]

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Ewe Mwenyezi Mungu! Hakika mimi najikinga kwako na sahiba mwenye mghafala na rafiki mbaya ." [357]

Imam Ali(a.s) amesema: "Kuandamana na watu waovu kunaleta uovu, ni kama upepo upitapo kwenye harufu mbaya huleta harufu mbaya ."[358]

Musa(a.s) amesema: "Atakayejiepusha na rafiki mbaya ni kana kwamba ameifanyia kazi Taurati ."[359]

Luqman(a.s) alimwambia mwanawe: "Anayefanya urafiki na mtu mbaya basi hatosalimika ."[360]

Ali bin Asbati amepokea kutoka kwa Maimamu(a.s) kuwa: "Miongoni mwa mawaidha ya Mwenyezi Mungu kwa Isa (a.s) ni: Ewe Isa! Jua kuwa rafiki mbaya ananifanyia uadui, na rafiki mbaya ananipinga. Na jua ni nani unayefanya naye urafiki. Na jichagulie ndugu miongoni mwa Waumini ."[361]

Imepokewa kutoka kwa Sufyan At-Thawriy amesema: "Nilikutana na mkweli mwana wa mkweli Jafar bin Muhammad(a.s) , nikamwambia: Ewe mwana wa Mtume wa Mwenyezi Mungu, naomba uniusie. Akaniambia: 'Ewe Sufyan! Mzazi wangu aliniamuru mambo matatu na akanikataza mambo matatu, na miongoni mwa hayo aliyoniambia ni:'Ewe mwanangu mpendwa! Atakayeandamana na rafiki mbaya hatosalimika ."[362]

Alama za rafiki mbaya: Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Anayemwamini Mwenyezi Mungu na Siku ya mwisho basi asifanye undugu na kafiri na wala asiandamane na muovu. Atakayefanya undugu na kafiri au akaan- damana na muovu atakuwa kafiri au muovu ." [363]

Imam Ali(a.s) amesema: "Atakayekusitiri aibu yako na akakuaibisha uwapo haupo basi ni adui, jihadhari naye ."[364]

Imam Ali(a.s) amesema: "Jiepusheni na wale ambao nyoyo zenu zinawachukia ."[365]

Imam Ali(a.s) amesema: "Ambaye mapenzi yake si kwa ajili ya Mwenyezi Mungu basi jihadhari naye. Kwani hakika mapenzi yake ni mabaya na usuhuba wake ni hatari ."[366]

Imam Ali(a.s) amesema: "Inafaa kwa anayetaka kuitengeneza nafsi yake na kuihifadhi dini yake ajiepushe kuandamana na watu wa dunia ."[367]

Imam As-Sadiq(a.s) amesema: "Tazama kila asiyekuwa na manufaa na wewe katika dini yako basi usiwe na mazoea naye, na wala usiwe na ragh- ba ya kusuhubiana naye, kwani hakika kila asiyekuwa katika njia ya Mwenyezi Mungu matokeo yake ni mabaya yenye kudhuru ."[368]

Adam(a.s) alimuusia mwanae Shi'ithi: "Nyoyo zenu zikikataa kitu basi jiepusheni nacho, kwani hakika mimi niliposogea kwenye mti ili nichume moyo wangu ulikataa, hivyo lau kama ningelijizuia kula basi yasingelinis- ibu yaliyonisibu ."[369]

Marafiki wabaya

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Msiandamane na waovu ." [370]

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Msifanye urafiki na mlevi wa pombe, kwani kufanya naye urafiki huleta majuto ." [371]

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Jizuieni kufanya urafiki na kila mwenye kheri ndogo, mwenye shari nyingi, khabithi wa nafsi. Anapokhofu hujikunyata na anapopata amani hufanya ujabari ." [372]

Imam Ali(a.s) amesema: "Aliye mbaya kati ya ndugu zako ni yule anayekuridhisha kwa batili ."[373]

Imam Ali(a.s) amesema: "Aliye mbaya kati ya ndugu zako ni anayekupaka mafuta ndani ya nafsi yako na kukuficha aibu zako ."[374]

Imam Ali(a.s) amesema: "Jiepushe kuwapenda maadui wa Mwenyezi Mungu, au kuonyesha mapenzi yako ya dhati kwa wasiokuwa mawalii wa Mwenyezi Mungu, kwani hakika atakayeipenda kaumu fulani atafufuliwa pamoja nao ."[375]

Imam Ali(a.s) amesema: "Mwenye kusuhubiana na watu wabaya ni sawa na alierakibu merkebu baharini ."[376]

Imam Jawad(a.s) amesema: "Jiepushe kusuhubiana na mtu muovu, kwani hakika yeye ni sawa na upanga wenye sumu, ukiutazama wavutia lakini athari zake ni mbaya ."[377]

ULEVI WA UJANA

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Ujana ni matawi ya uendawazimu ." [378]

Imam Ali(a.s) amesema: "Aina za ulevi ni nne: Ulevi wa ujana, ulevi wa mali, ulevu wa kulala na ulevi wa ufalme ."[379]

Imam Ali(a.s) amesema: "Inapasa kwa mwenye akili ajiepushe na ulevi wa mali, ulevi wa uwezo, ulevi wa elimu, ulevi wa sifa, na ulevi wa ujana,kwani hakika hayo yote yana riha mbaya inayoondoa akili na kupunguza unyenyekevu ."[380]

Imepokewa kuwa Imam Ali na Maimamu(a.s) walikuwa wakiomba ndani ya mwezi wa Shabani: "Ewe Mungu wangu nimemaliza umri wangu kwenye shari ya kukusahau Wewe. Na nimeumaliza ujana wangu katika ulevi wa kujitenga na Wewe. Ewe Mungu wangu ni siku nyingi sijaamka kwa ajili ya kukufanyia ujeuri, na kurakibu nikielekea njia ya ghadhabu Yako ."[381]

MATAMANIO YA KIJINSIA

MTEGO WA SHETANI

Mwenyezi Mungu amesema: "Waambie waumini wanaume wainamishe macho yao, na wazilinde tupu zao, hili ni takaso kwao, bila shaka Mwenyezi Mungu anazo khabari za yale wanayoyafanya. Na waambie waumini wanawake wainamishe macho yao na wazilinde tupu zao, wala wasionyeshe uzuri wao isipokuwa unaodhihirika. Na waangushe shungi zao juu ya vifua vyao, na wasionyeshe uzuri wao ila kwa waume zao, au baba zao, au baba za waume zao, au watoto wao, au watoto wa waume zao, au watoto wa kaka zao, au watoto wa dada zao, au wanawake wenzao, au wale waliomilikiwa na mikono yao au wafuasi wanaume wasio na matamanio (kwa wanawake), au watoto ambao hawajajua siri za wanawake. Wala wasipige chini miguu yao ili yajulikane mapambo waliyoyaficha. Na tubieni nyote kwa Mwenyezi Mungu enyi wenye kuamini ili mpate kufaulu ." (Surat Nuur: 30 -31).

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Mtazamo wa kwanza ni bahati mbaya, wa pili ni makusudi na wa tatu huangamiza ." [382]

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Ghadhabu ya Mwenyezi Mungu imeongezeka juu ya mwanamke mwenye mume aliejipodoa macho yake kwa ajili ya asiyekuwa mumewe au asiyekuwa maharimu wake. Kwani hakika yeye iwapo atafanya hivyo Mwenyezi Mungu humporomoshea kila amali aliyoitenda ." [383]

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Jiepusheni na mitazamo ya ziada, kwani yenyewe hupanda matamanio, na huzalisha mghafiliko ." [384]

Imepokewa kutoka kwa Abdullah bin Abbas amesema: "Mtume wa Mwenyezi Mungu alimuweka Fadhlu bin Abbas nyuma ya kipando chake

siku ya kuchinja (Siku ya Iddi kubwa), na Fadhlu alikuwa ni mwanaume mwenye mvuto, basi Mtume akasimama mbele ya watu akiwapa fatwa, ndipo akatokea mwanamke kutoka Khath'am naye akawa anamuuliza maswali Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) , basi Fadhlu akawa akimkodolea macho mwanamke yule na akapendezwa na uzuri wake. Mtume akageuka ilihali Fadhlu akiwa bado anamkodolea macho, ndipo(s.a.w.w) akakishika kidevu cha Fadhlu na kuuondoa uso wake kwa mwanamke yule." [385]

Imam Ali(a.s) amesema: "Macho ni mitego ya shetani ."[386]

Imam Ali(a.s) amesema: "Jicho lionapo tamanio basi moyo hufumbia ambacho ni matokeo ya baadaye ."[387]

Imam Ali(a.s) amesema: "Ni dhambi ngapi hupatikana kwa kufumba na kufumbua? "[388]

Imam Al-Baqir(a.s) amesema: "Mwanamke malaya alitoka kuwafuata vijana wa kibani Israil na akawafanyia fitina. Baadhi yao wakasema: Mfanya ibada fulani angemuona angemfitini. Basi akasikia kauli zao, akasema: 'Wallahi siendi nyumbani kwangu mpaka nimfitini. Ndipo akamwendea usiku akamgongea mlango, akasema: 'Nimekimbilia kwako.' Akamkatalia. Akasema: 'Baadhi ya vijana wa kibani Israil wamenitamani wao wenyewe hivyo niingize kwako la sivyo watanikuta hapa na kunifedhehesha.' Basi aliposikia kauli yake hiyo akamfungulia mlango. Alipoingia akavua nguo zake, basi alipoona uzuri wake na umbile lake akamtamani, na hatimaye akaweka mkono wake juu yake, kisha nafsi yake ikarejea, wakati huo alikuwa amewasha moto ambao ametenga chungu, basi akaweka mkono wake juu ya moto. Mwanamke akasema: 'Unafanya nini?' Akasema: "Nauunguza kwa sababu wenyewe umefanya kitendo." Basi mwanamke akatoka akaliendea kundi la kibani Israil, akawaambia: 'Muokoeni fulani ameweka mkono wake juu ya moto.' Basi wakamwen- dea wakamkuta mkono wake umeshaungua ."[389]

Imam As-Sadiq(a.s) amesema: "Mtazamo ni mshale miongoni mwa mishale ya Ibilisi wenye sumu, ni mitizamo mingapi ya muda mfupi imeleta hasara ya muda mrefu ."[390]

Imam As-Sadiq(a.s) amesema: "Mtume wa Mwenyezi Mungu alikuwa akiwasalimu wanawake na wanamjibu. Na jemedari wa waumini alikuwa akiwasalimu wanawake na alikuwa hapendi kuwasalimu mabinti miongoni mwao, na akisema: Nahofia sauti yake isinivutie nikaingiwa na mengi kuliko malipo niyatafutayo ."[391]

Masihi(a.s) amesema: "Usiwe na macho makali ya kukodolea kisicho cha kwako, kwani utupu wako hautazini madamu macho yako umeyahifadhi. Ukiweza kutoitazama nguo ya mwanamke ambaye si halali kwako fanya hivyo ."[392]

Masihi aliwaambia wanafunzi wake: "Jiepusheni kuwatazama wanawake ajnabiya (asiye maharim wako), kwani kwenyewe ni kupanda matamanio na ni miche ya ufuska ."[393]

Imam Ali(a.s) amesema: "Ashki huenda ikapatikana kwa sekunde chache ."[394]

Imam As-Sadiq(a.s) alipoulizwa kuhusu ashki alisema: "Nyoyo zilizojie- pusha na utajo wa Mwenyezi Mungu basi Mwenyezi Mungu akazionjesha mapenzi ya kumpenda asiyekuwa Yeye ."[395]

Maangamio ya wafuata matamanio:

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Ambaye hima yake kubwa ni kupata matamanio basi moyo wake hunyang'anywa utamu wa imani ." [396]

Imam Ali(a.s) amesema: "Ni mara ngapi starehe za muda mfupi hurithisha huzuni ya muda mrefu? "[397]

Imam Ali(a.s) amesema: "Jiepusheni matamanio yasizishinde nyoyo zenu, kwani hakika mwanzo wake ni nguvu na mwisho wake ni maangamizi ."[398]

Imam Ali(a.s) amesema: "Mwanzo wa matamanio ni burudani na mwisho wake ni karaha ."[399]

Madhara ya kujichanganya na wasiokuwa maharimu: Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Anayemwamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho halali sehemu ambayo mwanamke asiyekuwa maharimu wake anaisikia nafsi yake ." [400]

Imam Al-Baqir(a.s) amesema: "Nuh (a.s) alipomuomba Mola wake Mlezi kuwaombea kaumu yake, Ibilisi aliyelaaniwa na Mwenyezi Mungu alimjia na kumwambia: 'Ewe Nuh! Nikumbuke sehemu tatu, sehemu niwapo karibu mno na mja na awapo moja ya sehemu hizo: Nikumbuke unapoghadhibika. Nikumbuke uhukumupo kati ya watu wawili. Na nikumbuke uwapo pamoja na mwanamke faraghani mkiwa hamna yeyote pamoja nanyi ."[401]

Muhammad Tayar amesema: "Niliingia Madina na nikatafuta nyumba nikodishe, basi nikaingia nyumba ambayo ndani yake mna nyumba mbili, kati yake kuna mlango na humo mna mwanamke, akasema: 'Unakodi nyumba hii?' Nikasema: Kati yake kuna mlango nami ni kijana. Akasema: 'Mimi nitafunga mlango kati yangu na wewe.' Basi nikahamishia mizigo yangu humo na nikamwambia: Funga mlango. Akaniambia: 'Uache upepo unaingia kwangu kupitia hapo.' Nikamwambia: Hapana, mimi ni kijana na wewe ni binti, mimi naufunga. Akasema: 'Kaa wewe nyumbani kwako mimi sikuijii na wala sikukaribii.' Basi akakataa kufunga mlango, ndipo nikamwendea Abu Abdillah(a.s) nikamuuliza kuhusu hilo. Akasema:'Hama humo, kwani hakika mwanamke na mwanaume wanapokuwa faraghani ndani ya nyumba moja shetani huwa wa tatu wao ."[402]

MALIPO YA UTAWA WA JINSIA

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Atakayekuwa na uwezo juu ya kitendo cha haramu juu ya mwanamke au kijakazi lakini akamwacha kwa ajili ya kumuogopa Mwenyezi Mungu basi Mwenyezi Mungu ataharamisha moto juu yake na Mwenyezi Mungu Mtukufu atam- pa amani dhidi ya mshituko mkubwa (Kiyama) ." [403]

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Atakayetokewa na ufuska au matamanio kisha akajiepusha kwa ajili ya kumuogopa Mwenyezi Mungu basi Mwenyezi Mungu atamuharamishia moto na atampa amani dhidi ya mshituko mkubwa na atamtimizia alichomwahidi ndani ya Kitabu chake katika kauli yake: 'Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake atapata Bustani mbili ." [404]

Imam Zainul-Abidina(a.s) amesema: "Mwanaume mmoja alirakibu baharini akiwa na mkewe basi jahazi likawapasukia, hakuna aliyeokoka miongoni mwa waliokuwa ndani ya jahazi ila mke wa mwanaume yule. Yeye aliokoka kwa kutumia mbao za jahazi ambazo zilimpeleka hadi kwenye kisiwa miongoni mwa visiwa vya bahari. Ndani ya kisiwa hicho kulikuwa na mwanaume mmoja ambaye alikuwa akisafiri na hakuacha heshima yoyote kwa ajili ya Mwenyezi Mungu ila aliivunja. Basi hakujua lolote ila mwanamke aliyekuwa amesimama juu ya kichwa chake, akainua kichwa chake kumtazama, akasema: 'Ni binadamu au jini?' mwanamke akajibu: 'Mwanadamu.' Basi hakumzungumzisha neno lingine mpaka akawa amekaa kwake mkao wa mwanaume kwa mkewe. Alipoanza kumkusudia yule mwanamke akatetemeka, akamwambia: 'Kitu gani kinakutetemesha?' Akajibu: 'Namkimbia huyu.' Akaashiria mkono wake mbinguni. Akasema: 'Umemfanya huyu chochote?' Akasema: 'Hapana bali nguvu zake.'Akasema: 'Wewe unamkimbia huyu mbio zote hizi ilihali hujamfanya huyu chochote, basi mimi nakuchukia mno, wallahi mimi ndiye ninayefaa zaidi kukimbia huku na kukhofu kuliko wewe.' Basi mwanaume akasimama bila ya kufanya chochote, ndipo akarudi kwa mkewe akiwa hana hima yoyote ila kutubu na kurejea Kwake. Alipokuwa akitembea njiani ghafla akasadifiana na padri, basi jua likawa kali juu yao, ndipo padri akamwambia kijana: 'Muombe Mwenyezi Mungu atufunike kwa kivuli cha mawingu kwani hakika jua limekuwa kali juu yetu.' Kijana akasema: 'Mimi sijui kama nina jema mbele ya Mola wangu Mlezi hata nipate ujasiri wa kumuomba chochote.' Akamwambia: 'Mimi nitakuwa naomba nawe unaitikia.' Akasema: 'Ndio.' Basi padri akaanza kuomba na kijana akiitikia, basi haraka sana kivuli cha wingu kikawa kimewafunika. Wakatembea chini yake mchana kidogo, kisha wakaachana njiani. Kijana akachukua njia yake na padri njia yake, ndipo ghafla mawingu yakawa pamoja na kijana. Padri akasema: 'Wewe ni bora kuliko mimi, kwa ajili yako dua imejibiwa na wala haijajibiwa kwa ajili yangu. Nipe habari ni kipi kisa chako?' Ndipo akampa habari za yule mwanamke. Akasema: 'Umesamehewa yaliyopita kutokana na kuingiwa na khofu, na angalia mustakbali wako jinsi gani utakuwa."[405]

MALIPO YA MWENYE ASHKI ALIYE MTAWA

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Atakayekuwa na ashki akaficha na akajizuia na hatimaye akafariki basi yeye ni shahidi ." [406]

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Ashki pasipo na matamanio ni kafara ya dhambi ." [407]

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Atakayekuwa na ashki akaficha na akavuta subira, Mwenyezi Mungu atamghufiria na kumwingiza Peponi. " [408]

Imepokewa kutoka kwa Ibnu Abbas kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) kuwa amesema: "Watu bora katika umma wangu ni wale ambao hufanya utawa pindi Mwenyezi Mungu anapowapelekea balaa ya kitu." Wakamwambia: Ni balaa ipi? Akasema: 'Ashki ." [409]

MITEGO YA SHETANI

Imam Ridhaa(a.s) amepokea kutoka kwa baba zake kuwa: "Hakika Ibilisi alikuwa akiwajia Manabii(a.s) kuanzia kwa Adam(a.s) mpaka Mwenyezi Mungu alipomleta Masih(a.s) , alikuwa akiongea nao na kuwadadisi, na hakuna aliyekuwa akizungumza naye mara kwa mara kama Yahya bin Zakariya(a.s) . Yahya akamwambia: 'Ewe Abu Marah mimi nina haja kwako.' Akamwambia: 'Wewe una uwezo zaidi siwezi kukukatalia ombi basi niulize ulitakalo, hakika mimi si mwenye kukukhalifu katika jambo ulitakalo.' Yahya akasema: 'Ewe Abu Marah napenda unionyeshe mitego yako na mbinu zako ambazo kwazo huwanasa wanaadamu.' Ibilisi akasema: 'Kwa ukarimu wako na mapenzi yako, ninakuahidi hadi kesho.' Yahya alipoamka alikaa nyumbani kwake akisubiri ahadi na akamfungia mlango kabisa, ghafla akamhisi yuko usawa wake kutokana na mtego uliokuwa ndani ya nyumba yake, na hatimaye akaona sura ya uso wa kima na mwili wake ukiwa katika sura ya nguruwe, na macho yake yamepasuka kwa urefu. Kinywa chake kimepasuka kwa urefu na meno yake na kinywa chake ni mfupa mmoja bila kidevu wala ndevu, akiwa na mikono minne: Mikono miwili ikiwa kifuani mwake na miwili kwenye mabega yake. Mshipa wa kisigino ukiwa mbele na vidole vyake vikiwa nyuma na juu yake kukiwa na kuba na katikati yake kuna eneo lenye nyuzi zilizo kati ya rangi nyekundu, kijani njano na rangi zote, na mkononi mwake akiwa na kengele kubwa na juu ya kichwa chake kukiwa na yai na ndani ya yai kuna chuma kilichotungikwa kinashabihiana na koleo. Yahya alipotaamali akamwambia: 'Ni eneo gani hili ambalo liko katikati yako?' akajibu: 'Huu ni umajusi, mimi ndiye niliyeuanzisha na kuupamba kwa ajili yao.' Akamuuliza: 'Vipi hizi nyuzi zenye rangi?' akajibu: 'Hizi zote ni rangi za wanawake, mwanamke anaendelea kupaka rangi mpaka ananasa kwa rangi zake na kwazo nawatia watu kwenye fitina.' Akamuuliza: 'Vipi hii kengele iliyoko mikononi mwako?' Akasema: 'Huu ni mjumuiko wa ladha zote, kuanzia ngoma, zumali, gita, filimbi na ala. Na watu wanakaa kwenye vinywaji vyao wakiwa hawaburudiki kwa ladha basi hapo ndipo naitikisa kengele kati yao na hatimaye wanapoisikia basi mvuto wake huwavuta na hapo hupatikana anaecheza, mwenye kutikisa vidole vyake na hadi mwenye kuchana nguo yake.' Akamuuliza: 'Ni mambo gani ambayo yanakuridhisha sana?' Akasema: 'Wanawake, wao ndio mtego wangu, na kwa hakika wanapokusanyika walinganizi wema na watoa laana basi huenda kwa wanawake na wao huniridhisha.' Yahya akamwambia: 'Vipi hili yai lililopo juu ya kichwa chako?' Akasema: 'Kwalo najikinga na dua ya waumini.' Akamuuliza: 'Vipi hiki chuma nikionacho ndani yake?' Akajibu: 'Kwacho nazigeuza nyoyo za waumini.' Yahya akasema: 'Je kuna wakati wowote ulinishinda hata kido- go?' Akasema: 'Hapana, lakini kwako kuna sifa inivutiayo.' Yahya akamwambia: 'Ni ipi hiyo?' Akasema: 'Wewe ni mtu mlaji mno, unapofu- turu huendelea kula na kuvimbiwa na hilo hukukataza kutekeleza baadhi ya Swala na kisimamo chako cha usiku.' Yahya akamwambia: 'Hakika mimi nampa Mwenyezi Mungu ahadi kuwa sintoshiba chakula mpaka nitakapokutana naye.' Ibilisi akasema: 'Nami nampa Mwenyezi Mungu ahadi kuwa mimi sintomnasihi mwislamu mpaka nitakapokutana naye.' Kisha akatoka na hakurudi tena kwake baada ya hapo."[410]

3

JOHARI ZA HEKIMA KWA VIJANA

UDONDOZI KUTOKA KITABU: JAWAAHIRU AL-HIKMAH LI 'SH-SHABAAB

3 - HIJABU

Mwenyezi Mungu asema: "Ewe Nabii, waambie wake zako, na mabinti zako na wake wa wau- mini: Wateremshe juu yao shungi zao. Hivyo inaelekea zaidi waju- likane na wasiudhiwe, na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu ." (Surat Ahzab: 59).

Imam Al-Baqir(a.s) amesema: "Kijana mmoja wa kianswari alimgeukia mwanamke huko Madina na wanawake walikuwa wamevaa skafu zao nyuma ya masikio yao, basi akamtazama ilihali mwanamke yule akiwa mkabala naye, alipovuka mwanamke yule basi kijana akaingia mtaa uliokuwa ukiitwa Bani Fulani, akawa akimtazama kwa nyuma na hatimaye akaugonga uso wake kwenye ukuta na uso wake ukapasuka. Mwanamke alipotoweka akajitazama na kukuta damu zikishururuzika juu ya kifua chake na nguo yake, akasema: Wallahi ni lazima nimwendee Mtume wa Mwenyezi Mungu nikampe habari hii, basi akamwendea. Mtume wa Mwenyezi Mungu alipomuona akamwambia umefanya nini? Ndipo akampa habari ilivyokuwa, na ndipo Jibril akatelemka na Aya hii: "Waambie waumini wanaume wainamishe macho yao na wazilinde tupu zao, hili ni takaso kwao, bila shaka Mwenyezi Mungu anazo habari za yale wanayoyafanya ." (Surat Nur: 30)."[284]

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Mwenyezi Mungu amewalaani wanaume wenye kujishabihisha na wanawake. Na Mwenyezi Mungu amewalaani wanawake wenye kujishabihisha na wanaume ." [285]

Imam Ali(a.s) amesema: "Nilikuwa nimeketi pamoja na Mtume wa Mwenyezi Mungu huko Baqii siku yenye mvua na upepo, basi ghafla mwanamke akapita na punda na ghafla mkono wa punda ukaingia ndani ya shimo na hatimaye mwanamke akaanguka, basi Mtume akageuza uso. Wakamwambia: 'Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, hakika yeye amevaa suruwali.' Akasema: 'Ewe Mwenyezi Mungu wasamehe wanawake wenye kuvaa suruwali (Mara tatu). Enyi watu tengenezeni suruwali hakika zenyewe ni miongoni mwa nguo zenu zenye sitara mno, na wahifadhini wake zenu kwazo pindi watokapo ."[286]

Imam Ali(a.s) amesema: "Zama za mwisho, na karibu na Kiyama kutadhihiri wanawake wenye kujiacha wazi uchi, wenye kujitoa katika dini, wenye kuingia katika fitina, wenye kuelemea kwenye matamanio, wenye kuharakishia starehe, wenye kuhalalisha haramu basi hao watadumu motoni ."[287]

NDOA

A: MKAZO WA KUOA UJANANI

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Hakuna kijana anayeoa ujanani ila ni lazima shetani wake alie: 'Ole wangu, ole wangu! Amenizuilia theluthi ya dini yake.' Basi mja amche Mwenyezi Mungu kwenye theluthi mbili zilizobaki ." [288]

Imam Ali(a.s) amesema: "Enyi kundi la vijana! Ni juu yenu kuoa, na kama hamuwezi basi ni juu yenu kufunga, kwani kwenyewe ni kinga ."[289]

Imam Ali(a.s) amesema: "Ewe kijana oa na jiepushe na zinaa, kwani yenyewe huondoa imani moyoni mwako ."[290]

Imam As-Sadiq(a.s) amesema: "Kijana wa kianswari alimwendea Mtume wa Mwenyezi Mungu na kumlalamikia haja yake, basi akamshauri aowe. Kijana akasema: 'Mimi naona haya kurudi tena kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu.' Basi akakutana na mtu kati ya maasnwari, akamwambia: 'Mimi nina binti mzuri, na hatimaye akamuoza. Basi Mwenyezi Mungu akam- panulia riziki, na kijana akamwendea Mtukufu Mtume wa Mwenyezi Mungu na kumpa habari. Mtume wa Mwenyezi Mungu akasema: 'Enyi kundi la vijana! Ni juu yenu kuoa ."[291]

B: MUME MARIDHAWA

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Atakapowajieni mnayemridhia dini yake na tabia yake basi muozesheni na kama hamtofanya hivyo basi itakuwa ni uharibifu na ufisadi mkubwa aridhini ." [292]

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Nilimuoza Mikdad na Zayd ili iwe mbora wenu mbele ya Mwenyezi Mungu ni yule mwenye tabia njema kati yenu ." [293]

Alipoulizwa Imam Al-Baqir(a.s) kuhusu ndoa, alisema: "Atakayeleta posa kwenu na mkaridhia dini yake na uaminifu wake basi muozeni, na kama hamtofanya basi itakuwa ni uharibifu na ufisadi mkubwa aridhini ."[294]

Alikuja mtu mmoja kwa Husein(a.s) akimtaka ushauri juu ya kumuoza binti yake. Akasema: "Muoze kwa mwanamume mchamungu, kwani hakika yeye kama atampenda basi atamkirimu, na kama atamchukia basi hatomdhulumu. "[295]

C: MKE MARIDHAWA

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Oeni mabinti vijana kwani hakika wao ndio wenye tabia njema. " [296]

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Mwanamke huolewa kwa sifa nne: Kwa mali yake, dini yake, uzuri wake na kwa nasaba yake na familia yake, basi ni juu yako kwa mwenye dini ." [297]

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Atakayemuoa mwanamke kwa ajili ya uzuri wake basi hatopata kwake anachokipenda. Na atakaemuoa kwa ajili ya mali basi Mwenyezi Mungu atamtegemeza kwake. Basi ni juu yenu kwa mwenye dini ." [298]

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Atakayemuoa mwanamke kwa mali ya halali lakini akataka fahari na kujionyesha basi Mwenyzei Mungu hatomzidishia chochote ila udhalili na fedheha. " [299]

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Oeni kwenye matum- bo mema, kwani hakika damu hurithisha. " [300]

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Zichagulieni mbegu zenu sehemu yenye kheri, kwani hakika wanawake huzaa shabihi wa ndugu zao wa kiume na ndugu zao wa kike ." [301]

D: KUOA AKRABA

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Tafuteni wageni na wala msisababishe kuzaa wembamba ." [302]

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Msioe akraba (ndugu wa karibu), kwani hakika mtoto huumbwa mwembamba." [303]

HAYA

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Katika methali za Manabii haijabaki ila kauli ya watu: Ukiwa hauna haya basi fanya utakalo ." [304]

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Kuwa na haya ndio kheri yote ." [305]

Imam Ali(a.s) amesema: "Haya ni sababu ya kuelekea kwenye kila jamali. "[306]

Imam Ali(a.s) amesema: "Haya ni tabia njema. "[307]

Imam Ali(a.s) amesema: "Haya ni ufunguo wa kila kheri ."[308]

Imam Ali(a.s) amesema: "Haya huzuia kutenda tendo baya ."[309]

Imam As-Sadiq(a.s) amesema: "Haya ina sehemu kumi: Tisa kwa wanawake na moja kwa wanaume. "[310]

HAYA

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Haya ina namna mbili: Haya ya akili na haya ya ubaradhuli. Haya ya akili ni elimu na haya ya ubaradhuli ni ujinga ." [311]

Imam Ali(a.s) amesema: "Mambo matatu hayaonewi haya: Mtu kumhudumia mgeni wake. Kumsimamia baba yake na mwalimu wake toka alipokaa. Na kuitafuta haki hata kama ni ndogo ."[312]

Imam Ali(a.s) amesema: "Atakayeona haya kusema haki basi huyo ni baradhuli ."[313]

Imam As-Sadiq(a.s) amesema: "Haya zina wajihi mbili: Moja ni udhaifu na nyingine ni uimara nayo ndio Uislamu na imani ."[314]

Imam As-Sadiq(a.s) amesema: "Mwenye haya elimu yake ina manu- faa ."[315]

UNYENYEKEVU

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Aliye bora kati ya vijana wenu ni mwenye kujipamba kwa pambo la vikongwe wenu. Na aliye mbaya kati ya vikongwe wenu ni yule mwenye kujipamba kwa pambo la vijana wenu ." [316]

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Mwenyezi Mungu anampenda mtoto wa miaka ishirini anaposhabihiana na mtu wa miaka the- manini. Na anamchukia mtu wa miaka sitini anaposhabihiana na mtoto wa miaka ishirini ." [317]

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Mwenyezi Mungu huvutiwa na kijana asiyekuwa na kiburi . " [318]

Imam As-Sadiq(a.s) amesema: "Aliye bora kati ya vijana wenu ni mwenye kujishabihisha na vikongwe wenu. Na aliye mbaya kati ya vikongwe wenu ni yule mwenye kujishabihisha na vijana wenu ."[319]

MTAZAMO WA MBALI

Imam As-Sadiq(a.s) amesema: "Mtu mmoja alimjia Mtume(s.a.w.w) na kumwambia: 'Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu niusie.' Mtume wa Mwenyezi Mungu akamwambia:'Je utafuata usia iwapo mimi nitakuusia?' akamuuliza hivyo mara tatu naye akijibu ndio ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu. Basi Mtume wa Mwenyezi Mungu akamwambia:'Hakika mimi nakuusia utakapoazimia jambo chunguza matokeo yake, ikiwa kuna mafanikio basi litekeleze na kama kuna kufeli basi liache ." [320]

Imam Ali(a.s) amesema: "Kufikiri kabla ya kutenda kunakusalimisha na majuto ."[321]

Imam Ali(a.s) amesema: "Fikiri kabla ya kutenda ili usiaibike kwa uliyotenda ."[322]

Imam Ali(a.s) amesema: "Mwenye akili sana kati ya watu ni yule mwenye kuchunguza sana matokeo ya baadaye ."[323]

Imam Hasan(a.s) alipoulizwa kuwa ufanisi ni nini? Alisema: "Ni kusubiria fursa yako na kuharakisha yale uwezayo ."[324]

Imam As-Sadiq(a.s) amesema: "Simama kwenye kila jambo mpaka utakapojua mwanzo wake na mwisho wake, kabla hujaliingia ukaja kujuta ."[325]

Kuwataka ushauri wenye rai: Imam Al-Baqir(a.s) amesema: "Mtume wa Mwenyezi Mungu aliambiwa: Ufanisi ni nini? Akasema: 'Ni kuwataka ushauri wenye rai na kuwafuata ."[326]

Imam Ali(a.s) amesema: "Hakuna ushindi imara kama kuomba ushau- ri ."[327]

Imam Al-Kadhim(a.s) amesema: "Atakayeomba ushauri hatokosa kusifiwa iwapo atapatia, na hatokosa udhuru iwapo atakosea ."[328]

UHURU

Imam Ali(a.s) amesema: "Usiwe mtumwa wa mwenzako ilihali bila shaka Mwenyezi Mungu amekufanya huru ."[329]

Imam Ali(a.s) amesema: "Atakayejiepusha na matamanio basi atakuwa huru ."[330]

Imam Ali(a.s) amesema: "Hakika kuwa na haya na utawa ni miongoni mwa maumbile ya imani, nazo ni tabia za mtu huru na pambo la watu wema ."[331]

Imam As-Sadiq(a.s) amesema: "Sifa tano asiyekuwa nayo moja basi si mwenye kustarehe sana: Ya kwanza: ni utekelezaji wa ahadi. Pili: ni kupanga mipango. Tatu ni haya. Nne ni tabia njema. Tano ni uhuru, nayo ndiyo yenye kukusanya sifa zote hizi ."[332]

KUKUBALI UDHURU

Imam Ali(a.s) amesema: "Kubali msamaha wa ndugu yako, kama hana udhuru basi muombee udhuru ."[333]

Imam Ali(a.s) alipokuwa akimuusia mwanae Muhammad bin Al- Hanafiyah alisema: "Usimlazimishe ndugu yako kwa kufuata shaka, na wala usijitenge naye bila kumuomba akuelezee, kwani huenda ana udhuru nawe wamlaumu bure ."[334]

Imam Al-Kadhim(a.s) amesema: "Baba yangu alinishika mkono kisha akasema: 'Ewe mwanangu mpendwa! Hakika baba yangu Muhammad bin Ali alinishika mkono kama nilivyokushika na akaniambia: Hakika baba yangu mpendwa Ali bin Husain(a.s) alinishika mkono kama nilivyokushika na akaniambia:Ewe mwanangu mpendwa! Mfanyie kheri kila aliyeitafuta kutoka kwako, ikiwa ni anayestahiki basi utakuwa umepatia sehemu yake, na ikiwa si anayestahiki basi wewe utakuwa ni unayestahiki. Hata kama mtu atakushutumu kuliani mwako kisha akageuka kushotoni mwako na akakuomba msamaha basi kubali msamaha wake ."[335]


5

6

7