AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU 25%

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU Mwandishi:
: Sheikh Haruna Pingili
Kundi: Imam Ali bin Husein (A.S)

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU
  • Anza
  • Iliyopita
  • 16 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 20747 / Pakua: 5086
Kiwango Kiwango Kiwango
AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

Mwandishi:
Swahili

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

KIMEANDIKWA NA: ALI IBN AL - HUSAYN IMAM ZAYNUL AL - ABIDIN (A.S)

KIMETAFSIRIWA NA: SHEIKH HAROON PINGILI

Kwa Jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu

Tunamshukuru Allah (s.w.t) na baraka za Mtukufu Mtume(s.a.w.w) na Ahlul Bayt(a.s) kwa kutujaalia kuweza kufanikia juhudi zetu hizi katika kuchapisha kitabu hiki "Sahifatul Kamillah Al-Sajadia".

Kitabu kilochopo mikononi mwako ni tafsiri ya kitabu cha Kiarabu, kiitwacho "As-Sahifatul Kamillah Al-Sajadia" kilichoandikwa na Imamu wa Nne Al-Imam Zainul Abdeen(a.s) . Ndani ya Kitabu hiki Imam(a.s) ameelezea Du'a mbali mbali.

Sababu iliyoifanya Mission yetu isimamie kazi hii ni kama zile za mwanzo, ambayo zinatokana na maombi ya Maulamaa wengi katika Afrika Mashariki kututaka tukifanyie tarjuma kitabu hiki kiingie kwenye lugha ya Kiswahili.

Tunamshukuru Shaikh Harun Pingili kwa kutukubalia ombi letu na kuifanya kazi hii kwa moyo mmoja, na vile vile Bilal Muslim Mission of Scandinavia kutukubalia kukichapisha kitabu hiki.

Tunamshukuru Mwenyezi Mungu tena kwani vitabu vyetu vya mwanzo vimependwa mno na wasomaji na hivyo kutupa ari ya kuchapisha hiki ulichonacho mkononi na kitakachofuatia Insha-Allah.

Mission inatoa shukurani zake za dhati kwa wale wote ambao kwa juhudi zao kitabu hiki kinawafikia wasomaji wetu mikononi na waliosaidia kwa njia moja au nyingine katika tarjuma na uchapishaji wa kitabu hiki. Tunamuomba Mwenyezi Mungu (s.w.t) awalipe malipo mema hapo Duniani na baadaye huko, Akhera.

Wa Ma Tawfeeq Illa Billah

Bilal Muslim Mission of Tanzania

UTANGULIZI

Kwa Jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu.

Utangulizi Na: Allamah Sayyid Muhammad Rizvi

Du'a, Sala, kwa maana ya mawasiliano na Allah (s.w.t), ni sehemu ya maumbile ya Mwanadamu. Mara nyingi, umuhimu wa Du'a upo dhahiri, na hata hivyo, katika nyakati zingine, dhiki na majanga humpelekea mwanadamu kujutia na kuomba msaada kutoka kwa Allah (s.w.t). Utafiti wa Kisayansi wa hivi karibuni uliofanyika mwaka 1999, katika Hospitali ya Maradhi ya Moyo Jijini Kansas U.S.A, umethibitisha kupona kwa njia ya Sala kwa Wagonjwa wenye kusali (bila ya wao wala daktari wao kufahamu) walionekana kupona maradhi yao kwa kupimwa na vyombo 35 vya vipimo vya afya ukilinganisha na Wagonjwa Wasiosali.. Allah (s.w.t) amesema wazi wazi kuwa wakati wote milango yake ipo wazi na kwamba (Allah) yupo karibu na (mja wake) mwanadamu wakati wote kuliko alivyo yeye Mwanadamu na mshipa wa shingo yake. Qur'an tukufu inasema: "Na Mwenyezi Mungu ana Majina mazuri mazuri, muombeni kwayo". (7:180) katika Aya nyingine Mwenyezi Mungu ansema: "Na Mola wenu anasema: "Niombeni nitakujibuni: Kwa hakika wale wajivunao kufanya ibada yangu, bila shaka wataingia Jahanamu, wadhalilike." (40:60) Ingawaje inaruhusiwa kuomba (du'a) kwa Allah (s.w.t) kwa njia yeyote tuipendayo, Mtume na Maimamu wa Ahlul Bayt(a.s) pia wametuongoza katika jambo hili. Miongoni mwa miongozo ya hekima ya Maimamu ni as-Sahifah as-Sajjadiyya ya Imamu 'Ali ibnul Husayn(a.s) . Imam 'Ali ibnul Husayn anafahamika na Waislamu wote kuwa ni Kiongozi Mkuu wa Imani ya Kiroho. Hii inaelezewa kwa majina yake maarufu: Zaynul 'Abidin kiongozi (mtukufu) wa Wachamungu na Sayyidus Sajidin, kiongozi wa wale wanaosujudu chini na kuabudu.

Kitabu chake cha as-Sahifah as-Sajjadiyya ni kitabu chenye mpangilio madhubuti wa Sala na Du'a. na kinajumuisha vipengele vyote anavyopambana navyo mwanadamu katika maisha yake, Matatizo ya Afya hadi Utajiri, furaha hadi upweke na unyonge; matukio ya mafanikio na mahitajio, siku za wiki hadi siku kuu maalum n.k. Mwanachuoni maarufu wa Ki-Sunni wa Misri (Egypt) Shaykh at-Tantawi al-Jawhari ameandika yafuatayo kuhusiana na Kitabu cha Sahifah. "Nimekisoma kitabu hiki kwa makini, NimezisomaDu'a zake na Munajjat kwa jicho la utafiti, nimeshangazwa na mantiki na falsafa lliyomo ndani yake. Nimevutiwa mno kwa ubora na mtiririko wa maandishi (tungo) haya. Ninashangaa ni vipi Waislamu kwa muda mrefu wamekuwa hawajui (jahili) kuhusu hazina hii tukufu. Wamekuwa katika usingizi mzito kwa karne nyingi. Hawakuweza hata kuzinduka na kutambua kuwa Allah (s.w.t) amewapatia Hazina hii kubwa ya Elimu. Tungo za Kitabu hiki zaweza kuwekwa katika mitazamo miwili mikubwa; kwanza ni kutafuta Elimu na mwongozo ili kujitenga mbali na madhambi na vitendo viovu wakati ambapo mtazamo mwingine ni kufuata na kuyatenda matendo mema ya kiroho ambayo tunaweza kusema matendo haya yaliyojaa maarifa na mwongozo mwema ni Hazina ya ajabu na ni siri iliyojaa Hekima. Mikakati yote hii inapatikana katika sehemu ya mwanzo ya Kitabu na sehemu ya pili imejaa sifa za Allah (s.w.t), Uumbaji wa viumbe na miujiza ya Allah (s.w.t). "Je hii haishangazi? Je hii sio siri ambayo hawa Watukufu wanaweka dhahiri siri nyingi kwa kusoma na kuiweka wazi Elimu ya Waislamu ambao wanaonekana hawajui kitu? Na huu ni ukweli kwamba mambo ya Wanadamu yamegawika katika sehemu mbili kubwa. Kwanza ni yale yanayohusiana na kujitenga (kuwa mbali) na vitendo viovu na pili ni yale matendo mema pamoja na kutambua kuwepo kwa Allah ambayo ni muhimu kwa utakaso binafsi na ukamilifu wa roho" (At-Tantawi Ad'iyyatu 'Ali Zayni 'l-'Abidin katika jarida la Huda 'l-Islam la Misri (Egypt)). Nina uhakika kwa kukisoma hiki kitabu kikubwa kutoka kwa Ahlul Bayt, sio tu utapata njia sahihi ya kuwasiliana na Allah, lakini pia kitakuweka karibu na Itikadi sahihi kuhusu uwezo na rehema ya Allah (s.w.t). Hatimaye utatambua kuwa maarifa (Elimu) sahihi ya Allah inapatikana tu kwa kupitia mafundisho sahihi ya Maimamu wa Ahlul Bayt wa Mtume. Allah, subhanah wa Taala, wakati wote yupo tayari kutusikiliza na Imam Zaynul Abidin(a.s) ametuwekea njia sahihi ya kuwasiliana na Allah. Hivyo huhitajii kwenda kwa mshauri yeyote au mganga wa kienyeji ambao kwao utatoa pesa ili kusikiliza matatizo yako; Allah (s.w.t) wakati wote yupo tayari kukusikiliza, bila muda maalum wala malipo yoyote!

Sayyid Muhammad Rizvi

NENO LA WACHAPAJI

Kwa Jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu.

Allah (s.w.t) ameumba uhai na umauti kwa makusudio maalum Amelielezea hilo kwa njia ya vitabu vinavyobainisha wazi wazi kati ya matendo mema na maovu. Maelezo fasaha na yenye mtiririko mzuri yanatuthibitishia kuwa kila mmoja wetu na wa kila rika na jamii tofauti anaweza kukielewa kitabu hiki kwa urahisi. Imani ya Dini imemuweka mwanadamu katika upeo wa juu ambao haulinganishwi na zama za Kijahiliyya. Kwa kuujua uwezo wa Allah (s.w.t) huwapelekea watu kuwa na matumaini na furaha katika maisha ya hapa Ulimwenguni na Akhera. Katika mada hii Quran tukufu inasema: "Ambao ni wale walioamini na zikatulia nyoyo zao kwa kumkumbuka Mwenyezi Mungu. Sikilizeni! Kwa kumkumbuka Mwenyezi Mungu nyoyo hutulia" Al-Raad:28. Hapana yeyote mwenye kuujua udhaifu wa mwanadamu na mapenzi ya Allah (s.w.t); atashindwa kubadilika kwa mafunzo yaliyomo katika Sahifa. Ndani yake tunapata mafunzo ya kiroho ya Kiislam au mafundisho ya kina na mapana ya Dini ya Kiislamu yanayohusu matendo na ukweli katika maisha na mahusiano kati ya mwanadamu na Allah (s.w.t) ambayo yameandikwa katika lugha za Kimataifa kwa kuweka misingi imara ya kiroho kwa ukamilifu. Kwa Niaba yetu sote tunatoa shukurani zetu za dhati kwa Mtukufu Allah (s.w.t) na kwa mwandishi wa kitabu hiki kitukufu kilichotuwezesha kuandika tafsiri ya pili na tunaungana na kufurahia kazi ngumu ya tafsiri yake ya Kiswahili pamoja na Mzee wetu Ayatullah Allamah Sayyid Saeed Akhtar Rizvi wa Bilal Mission of Tanzania. Tunamuomba Allah (s.w.t) ambariki na amlipe kwa kazi yake kubwa aliyoifanya katika nyanja hii; pamoja na wale waliotoa mchango wao wa hali na mali Mission na Mwandishi pia wanatoa shukurani zao za dhati kwa wale wote waliotoa mchango wao katika kazi hii. Tunaweka kalamu yetu chini kwa kumalizia na methali ya Kiswahili isemayo, "Fuata nyuki ule asali."

DIBAJI KUHUSIANA NA USHUHUDA - THABITI WA SAHIFA

Kwa Jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema - Mwenye Kurehemu

Mtukufu Sayyed Najmu Deen Bahausharafu Abul-Hasan Muhammad bin Ahmad bin Ali bin Muhammad bin Umar bin Yahya Al-Alawi Al-Husayn - Mungu amrehemu - alituhadithia Alisema: Alitupa khabari Shaikh heri zimfikiye Abu Abdilahi Muhammad bin Ahmad bin Shahriyar muweka hazina wa hazina ya Amiyrul Muuminen Maulana Aliy bin Abiy Taalib alayhis-salaam katika mwezi wa Rabi-u-Awal (mwezi wa tatu A.H.) mwaka wa 516 mwezi May - June wakati Sahifa ilikuwa inasomwa mbele yake nami nasikia.

Alisema nimeisikia kutoka kwa Shaikh ikisomwa mbele yake Shaikh Swaduqu Abiy Mansoor Muhammad bin Muhammad ibun Ahmad bin Abdil-Aziz Al-Ukbari mwadilifu Mungu amreheu kutoka kwa Abil-Mufazzali Muhammad bin Abdilahi ibnil-Mutalib Ashaybaanee. Alisema: Sharifu Abu Abdilahi Jaafar bin Muhammad ibun Jaafar ibunil Hasani ibin Jaafar ibunil Hasan Ibunil Hasan ibun Ameril-muumineena Aliy ibn Abiy Taalib amani juu yake ametuhadithia. Amesema: Ametuhadithia Abdulahi ibin Umar ibin Khataab Azaya mwaka wa mia mbili sitini na tano 265 (878-9) Amesema: Ametuhadithia mjomba wangu Ali bin Anuumani Al-Aalamu. Amesema: Ametuhadithia Umairi bin Mutawakili Athaqafiyu Al-Balakhiyu naye... kutoka kwa baba yake Mutawakili bin Haroon. Alisema nimekutana na Yahya bin zaid bin Aliy Alayhi-salaam naye akiwa yu aelekea khurasani baada ya kuuliwa baba yake nilimsalimia. Aliniuliza umetoka wapi? Nikasema kutoka Hajji. Aliniuliza kuhusu Ahli wake na watoto wa ami yake huko Madina na alisisitiza swali kuhusu Jaafar bin Muhammad amani iwe juu yake.Nilimuelezea khabari zake na khabari zao na huzuni walionayo kuhusu baba yao Zaid bin Aliy amani iwe juu yake. Aliniambia: Ami yangu Muhammad bin Aliy amani iwe juu yake alimshauri baba yangu asitoke na alimjulisha kuwa endapo atatoka na kuiacha Madina mambo yatavyomuwia. Je ulipata kukutana na mtoto wa ami yangu Jaafar bin Muhammad amani iwe juu yake? Nikamwambia ndio. Akasema je ulipata kumsikia anasema chochote kunihusu? Nikasema ndio.

Akasema: Alisema nini kunihusu? Nikasema nimejitoa muhanga kwako sipendi nikukabili kwa yale niliyoyasikia kutoka kwake. Akasema wanitishia umauti? Lete ulichosikia. Nikasema nimemsikia akisema kwa hakika kabisa kuwa utauliwa na utasulubiwa kama alivyouliwa baba yako na alisulubiwa. Basi uso wake ulibadilika na akasema: (Mungu huyafuta apendayo na huyathibitisha na kwake ipo asli ya kitabu). Ewe! Mutawakilu hakika Mwenyezi Mungu mwenye enzi na ametukuka ameliunga mkono jambo hili kupitia kwetu na ametupa sisi elimu na upanga. Haya mawili yameunganishwa na sisi na wamepewa wana wa ami yetu khususan elimu tu peke yake. Nikasema nimejitoa kwako muhanga mimi naona watu wanaelemea sana kwa mwana wa ami yako Jaafar amani iwe juu yake kuliko kwako na kwa baba yake. Akasema: kwa hakika ami yangu Muhammad na mwanawe Jaafar amani iwe juu yao wamewaita watu kwenye uhai na sisi tumewaita kwenye umauti. Nikasema ewe mwana wa mjumbe wa Mungu je wao wanaelimu zaidi au ninyi? Aliinama punde kisha akainuwa kichwa chake na akasema: Sote tunaelimu isipokuwa wao wanayajua yoote tuyajuwayo nasi hatujuwi yote wayajuwayo. Kisha aliniambia: Je umeandika chochote kutoka kwa mwana wa ami yangu? Nikasema naam. Akasema nionyeshe, nikamtolea aina kadhaa za elimu na nikamtolea duwa nilizoandika kutoka kwake Abiy Abdilahi amani iwe juu yake. Na alinihadithia kuwa baba yake Muhammad bin Aliy amani iwafikie alimwandikia kwa imla na akampa khabari kuwa ni miongoni mwa DU'A za baba yake Aliy bin Husain amani ziwe juu yao ni miongoni mwa DU'A za Sahifa al-Kamila. Yahya aliiangalia mpaka mwisho wake na aliniambia: Je waniruhusu niinakili? Nikasema Ewe mwana wa mjumbe wa Mungu waomba ruhusa kile ambacho ni kutoka kwenu? Akasema hakika nitakutolea Sahifa ya DU'A kamili zile alizozihifadhi baba yangu kutoka kwa baba yake na kwa hakika baba yangu ameniusia kuilinda na kutompa asiyestahiki. Umairu alisema: Alisema baba yangu: Basi nilisimama na kumwendea nikabusu kichwa chake. Na nikamwambia naapa ewe mwana wa mjumbe wa Mungu hakika mimi nitafanya dini ya Mungu kupitia upendo wenu na kuwatii ninyi, nami nataraji anipe Mungu maisha ya faraja na umauti mwema kwa wilaya yenu (kuwa penda). Basi alitupa zile kurasa zangu nilizompa kwa mtoto alikuwa pamoja naye na akasema andika DU'A hii kwa hati bayana nzuri kisha nipe huenda nikaihifadhi kwani nilikuwa naiomba kutoka kwa Jafari Mungu amhifadhi naye alikuwa akiniziwiya nayo. Mutawakilu alisema: Nilijutia nililofanya sikujuwa la kufanya na Abu Abdilahi amani imfikiye hakuniambia kuwa nisimpe yeyote! Baadaye aliagiza kisanduku ambacho humo alitowa sahifa iliyofungwa na kupigwa muhuri akauangalia ule muhuri na akaubusu akalia akavunja na kufunguwa kufuli. Kisha aliikunjuwa ile sahifa na akaiweka kwenye macho yake na kuipitisha usoni kwake na akasema walahi ewe! Mutawakilu lau kama kwa ajili ya yale uliyoyasema miongoni mwa usemi wa mwana wa Amiy yangu yakuwa mimi nitauwawa na kusulubiwa nisingekupa hii sahifa ningeifanyia ubakhili. Lakini natambua kuwa usemi wake ni wa haki ameuchukua kutoka kwa baba zake na itatimia hivyo basi nimeogopa elimu kama hii iwafikie baniy Umayya wataificha katika kabati zao kwa ajili yao tu. Ichukue ihifadhi kwa niaba yangu na ungoje ukiwa nayo Mungu atapopitisha jambo langu na jambo la hawa watu na atapitisha.

Basi hiyo ni amana yangu kwako mpaka uifikishe kwa wana wawili wa Amiy yangu Muhammad na Ibrahim wana wawili wa Abdilahi bin Hassan bin Hassan amani iwafikie. Kwa sababu wao ndio watakaoshika jambo hili baada yangu.Mutawakilu akasema: Niliipokea sahifa. Na alipouliwa Yahya bin Zaid nilikwenda Madina nikakutana na Aba Abdilah, amani imfikie. Nilimsimulia zile khabari kumuhusu Yahya alilia sana na huzuni kumuhusu ilikithiri na akasema: Mungu mrehemu mwana wa Amiy yangu na amkutanishe na baba zake na babu zake. Wallahi ewe Mutawakilu halikunizuwia kumpa ile DU'A yeye isipokuwa lile alilolihofia kuhusu sahifa ya baba yake, basi iwapi sahifa? Nikasema: Ni hii.Aliifungua na akasema: Wallahi hizi ni hati za Amiy yangu Zaid na ni DU'A ya babu yangu Aliy bin Hussain amani iwafikie. Kisha alimwambia mwanawe: Simama ewe Ismael niletee ile DU'A ambayo nilikuamuru uihifadhi kwa moyo na kuilinda Ismael alisimama na aliitowa ile sahifa kama ile aliyo mkabidhi Yahya bin Zaid Abu Abdilahi aliibusu na aliiweka machoni kwake na akasema huu ni mwandiko wa baba yangu na aliiandika kwa imla aliyoifanya babu yangu amani iwe juu yao mimi nikiwa naona. Nikasema ewee mwana wa Mtume wa Mungu waonaje nikiilinganisha na sahifa ya Zaidi na Yahya? Aliniruhusu kufanya hivyo na alisema: Nakuona wafaa kwa hilo.Nikazichunguza naona kuwa zi kitu kimoja sikuipata hata herufi moja inatofautiana na zilizo kwenye sahifa nyingine. Kisha nilimwomba ruhusa Aba Abdilah amani iwe juu yake ili niwape sahifa watoto wawili wa Abdilahi bin Husain. Akasema (hakika Mungu anakuamrisheni kuzifikisha amana kwa wenyewe) ndio wape hao wawili.Nilipoinuka ili kukutana nao aliniambia: bakia mahali pako. Kisha alituma waitwe Mohammad na Ibraheem, na akasema huu ni urithi wa mwana wa Amiy yenu Yahya kutoka kwa baba yake amempeni ninyi khususan na kuwaacha ndugu zake. Nasi tunakuwekeeni sharti. Wakasema sema kwani kauli yako yakubalika. Akasema musitoke nayo sahifa hii nje ya Madina.Wakasema: Kwanini iwe hivyo? Akasema: Kwa hakika mwana wa Amiy yenu aliihofia jambo nami nalihofia kwenu. Wakasema kwa hakika aliihofia alipojua kuwa atauwawa. Akasema Abu Abdilah amani imwendee; na ninyi musijiaminishe, kwa kweli najua kuwa ninyi mutapinga kama alivyopinga na mutauwawa kama alivyouwawa. Walisimama huku wakisema hapana hila wala nguvu ila kwa kuwezeshwa na Mungu aliye na enzi ya juu mno mtukufu.Walipokwisha toka akaniambia Abuu Abdilahi amani imfikiye: Ewe Mutawilu: vipi Yahya alikwambia kuwa hakika Amiy yangu Mohammad bin Aliy na mwanawe Jaafar wanawaita watu kwenye uhai nasi tunawaita kwenye umauti? Nikasema ndio Mungu akuweke katika islahi aliniambia hivyo mwana wa ami yako Yahya. Akasema Mungu amrehemu Yahya, hakika baba yangu alinihadithia naye alihadithiwa na baba yake naye toka kwa babu yake toka kwa Aliy amani juu yake kuwa mjumbe wa Mungu(s.a.w.w) alisinzia kidogo akiwa juu ya membari yake akaona akiwa katika usingizi wake kuwa watu wanaruka ruka juu ya membari yake kama ngedere na kuwafanya watu warudi kinyume nyume.Mtume wa Mungu alikaa sawasawa(s.a.w.w) hali ikiwa huzuni imetanda usoni kwake. Jibrilu (a.s) alimjia na aya hii: (Hatukuifanya njozi tuliyokuonyesha isipokuwa ni mtihani kwa watu na mti ulio laaniwa katika Qur'an na tunawahofisha lakini haiwazidishii ila kuvuka mipaka kukubwa) Awakusudia Baniy Umayya kwa tamko la mti uliolaaniwa katika Qur'an.

Akasema ewe Jibril watakuwa katika muda wangu na katika wakati wangu? Akasema la hapana lakini kinu cha Uislamu kitazunguka toka kuhama kwako na kubaki miaka kumi baada ya hapo kinu cha Uislam kitazunguka mpaka miaka thelathini na tano toka kuhama kwako. Baada ya hapo kitabaki miaka mitano kisha hapana budi kutakuwa na maongozi potovu ya kuwa katika muhimili wake kisha kutakuwa na ufalme wa mafirauni. Akasema na Mungu mtukufu aliteresha aya ya Qur'an kuhusiana na hayo: (Kwa hakika tumeiteremsha usiku wa maazimio kitu gani kitakujulisha usiku wa maazimio nini usiku wa maazimio ni bora kuliko miezi elfu). Watamiliki Baniy Umayya wakati ambao hautakuwa na usiku wa maazimio. Akas.ema Mwenyezi Mungu mtukufu alimjulisha Nabiy wake(s.a.w.w) utawala wa umaa huu na mamlaka yao muda wote huu. Hata lau milima ingerefuka kupita kiasi wangejirefusha na wao hata kushinda mirima mpaka Mungu mtukufu aidhinishe kutoweka ufalme wao na wao katika wakati huo wote wamepandisha bendera ya chuki na bughudha dhidi yetu sisi Ahla Bayt. Mungu alimpasha khabari Nabiy wake yale watakayopambana nayo Ahli Bayt wa Muhammad na wapenzi wao na Shia wao toka kwao (Baniy Umayya) katika siku za ufalme wao. Akasema: Mungu ameteremsha kuhusu hawa watu: (huwaoni ambao wameibadilisha neema ya Mungu kwa kukufuru na kuwafanya watu wao kubaki katika maangamizi wataunguwa katika jahannam na ni makazi mabaya mno.) Na neema ya Mungu ni Muhammad na Ahli Bayt wake kuwapenda wao ni iymani yaingiza peponi na kuwachukia ni ukafiri na unafiki uingizao motoni.Mtume wa Mungu aliiweka siri hiyo kwa Aliy na kwa Ahli Bayt wake. Akasema: Kisha Abu Abdilahi amani iwe juu yake alisema: Hajatokea wala hatotokea kati yetu Ahli Bayt yeyote mpaka siku ya kusimama na kujitokeza kwa qaim wetu Imamu Mehdi ili aziwiye dhulma au kuifanya haki itekelezeke ila atagongana na balaa na itakuwa kujitokeza kwake ndio sababu ya kuzidisha uadui na msiba juu yetu na Shia wetu. Mutawakilu bin Haroon alisema: kisha Abu Abdilahi aliniandikia DU'A kwa njia ya imla nazo zikiwa katika milango 75 imenipotea kutokana nazo milango kumi na moja na nimehifadhi miongoni mwa DU'A hizo milango sitini na kitu. Ametuhadithia Abul-Fazzal amesema: Na amenihadithia Muhammad bin Al-Hassan Ibun Ruzbih Abu Bakr Al-madaini mwandishi ni mkazi wa Arrah'ba alitusimulia akiwa nyumbani mwake. Amesema: Amenihadithia Mohammad bin Ahmad bin Muslim Al-Mutaharyu, amesema: amenihadithia baba yangu kuutoka kwa Umairi bin Mutawakili Al-Balkhiyi toka kwa baba yake Al-Mutawakilu bin Haroon. Alisema: Nilikutana na Yahya bin Zain bin Aliy amani iwe juu yao na aliitaja hadithi kikamilifu mpaka ile njozi ya Nabiy(s.a.w.w) ambayo Jaafar bin Muhammad aliitaja toka kwa baba zake amani iwafikie. Na katika riwaya ya Almutahari imetajwa milango nayo ni:

1. Kumuhimidi Mungu mwenye enzi na ametukuka.

2. Sala kwa Muhammad na Ali wake.

3. Sala kwa wabeba arshi (kitanda.)

4. Sala kwa wanomsadiki Mtume.

5. DU'A kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya watu wamuhusuo.

6. DU'A ya kila asubuhi na jioni.

7. DU'A yake kwa ajili ya mambo yanayotisha na muhimu.

8. DU'A yake kwa ajili ya kujikinga.

9. DU'A yake kwa ajili ya ayapendayo.

10. DU'A yake kwa kutaka Mungu awe ndio kimbilio lake.

11. DU'A yake kwa ajili ya mwisho mwema.

12. DU'A yake kwa ajili ya kukiri.

13. DU'A yake kwa ajili ya mahitaji.

14. DU'A yake kwa ajili ya matendo ya dhuluma.

15. DU'A yake wakati wa ugonjwa.

16. DU'A yake kutaka ufumbuzi.

17. DU'A yake dhidi ya shetani.

18. DU'A kwa kujihadhari na hatari.

19. DU'A yake kuomba maji.

20. DU'A yake kwa ajili ya kuwa na tabia njema.

21. DU'A yake akihuzunishwa na jambo.

22. DU'A yake wakati wa shida.

23. DU'A yake kwa ajili ya afya njema.

24. DU'A yake kwa ajili ya wazazi wake wawili.

25. DU'A zake kwa ajili ya watoto wake.

26. DU'A yake kwa ajili ya majirani zake na rafiki zake.

27. DU'A yake kwa ajili ya walinda mipaka.

28. DU'A yake katika mfadhaiko.

29. DU'A yake inapokuwa haba riziki.

30. DU'A zake ili kupata msaada wa kulipa deni.

31. DU'A yake kwa ajili ya toba.

32. DU'A yake katika sala za usiku.

33. DU'A yake katika kumwomba Mungu amchagulie lililobora (istikhara)

34. DU'A yake apatwapo na balaa au aona balaa ya nyemelea

kumfedhehesha kwa dhambi.

35. DU'A yake kuonyesha ridha kwenye maamuzi ya Mola.

36. DU'A yake asikiapo radu.

37. DU'A yake katika kuonyesha shukurani.

38. DU'A yake kuomba udhuru.

39. DU'A yake kuomba msamaha.

40. DU'A yake akumbukapo umauti.

41. DU'A yake kuomba kusitiriwa na hifadhi.

42. DU'A yake wakati wa kuhitimisha Qur'an.

43. DU'A yake anapouona mwezi mwandamo.

44. DU'A yake uingiapo mwezi wa Ramadhani.

45. DU'A yake kuuaga mwezi wa Ramadhani.

46. DU'A yake kwa ajili ya Iddi ya Fitri na Ijumaa.

47. DU'A yake siku ya Arafat.

48. DU'A yake siku ya uzhiya (kuchinja) na siku ya Ijumaa.

49. DU'A yake kujikinga na vitimbi vya maadui.

50. DU'A yake wakati wa hofu.

51. DU'A yake katika kumwomba Mungu sana na unyenyekevu.

52. DU'A yake katika kuomba kwa bidii.

53. DU'A yake katika kujidhalilisha (mbele ya Mungu).

54. DU'A yake ili kuondoa maudhi.

Ama milango iliobaki ni kwa matamko ya Abiy Abdilahi Al-Hasaniy rehma za Mungu zimfikie.

Ametuhadithia Abu Abdilah Jaafar bin Mohammad Al-Hasaniy, amesema: Ametuhadithia Abdulahi bin Umairi bin Khataab Azzayatu. Amesema: Amenihadithia mjomba wangu Aliy bin Annuumani Al-Halam.

Amesema: Amenihadithia umairu bin Mutawakilu Athaqafiyu Al-Balakhiyu kutoka kwa baba yake Mutawakilu bin Haroon. amesema amenifanyia imlaa bwana wangu Aswadiqu Abu Abdilahi Jaafar bin Muhammad.

Amesema: Babu yangu Aliy bin Husain alimfanyia imla mbele ya macho yangu baba yangu Muhammad bin Aliy, juu ya wote amani ya Mungu iwafikie.

1

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

DUA YA KWANZA

Na Alikuwa(a.s) Akianza Kuomba Du'a Huanza Kumhimidi Mungu Mtukufu Na Kumsifu Husema Hivi:

Sifa Njema Zote Ni Zake Mwenyezi Mungu. Ambaye ni wa mwanzo bila ya chanzo kilikuwa kabla yake, na wa mwisho bila ya cha mwisho kitakuwa baada yake: Ambaye yameshindwa kumwona macho ya watazamaji, yameshindwa kumuainisha mawazo ya wasifiaji. Kwa uwezo wake alianza kuumba viumbe. Aliwabuni (viumbe) kwa utashi wake wa kubuni, Kisha aliwapitisha njia ya utashi wake. Na aliwatuma katika njia ya upendo wake. Hawana uwezo wa kuchelewesha alichowatangulizia. Wala hawawezi kutanguliza alichowacheleweshea. Na ameifanyia kila roho miongoni mwao lishe ijulikanayo iliyogawanywa kutoka kwenye ruzuku yake. Mpunguzaji hawezi kumpunguzia aliye mzidishia. Wala mzidishaji hawezi kumzidishia aliempunguzia.

Kisha akaipigia kila nafsi muda wenye kikomo. Na akaisimamishia kila nafsi muda wenye mpaka. Yanatembea kuuelekea, kupitia siku za umri wake. Anaufikia kupitia miaka ya muda wake. Mpaka afikapo hatua ya mwisho, na kutimiliza hesabu za umri wake. Mungu humshika na kumpeleka kwenye thawabu zake nyingi au kwenye adhabu yake aliyo muhadharisha nayo. Ili awalipe ambao wamefanya vibaya waliyotenda, na awalipe wema ambao wamefanya mema. Ikiwa ni uadilifu kutokana naye. Yametakasika majina yake. Neema zake zimejitokeza!

"LA YUS'ALU AMMA YAF'ALLU' (Haulizwi atendayo) "WA HUM YUS' ALUNA" (Wao ndio wataulizwao). Sifa njema zote ni za Mungu ambaye lau angewaficha waja wake utambuzi wa Himidi yake, juu ya aliyowafanyia majaribu kwa neema zake zenye kufuatana, na amewakithirishia neema zake za wazi, wangezitumia neema zake, bila ya kumhimidi! Na wangejitanua katika riziki yake bila ya kumshukuru.

Na wangekuwa hivyo wangetoka nje ya mipaka ya ubinadamu na kuingia kwenye mipaka ya unyama na wangekuwa kama alivyo waelezea katika kitabu chake thabiti:

"IN HUM ILA KAL AN AAMI BAL HUM ADWAllU SABIILA" (Hakika wao ni kama wanyama, bali wao ni wapotovu mno wa njaa). Sifa njema ni za Mungu juu ya ujuzi aliotupa kumtambua yeye binafsi, na ametupa ilhamu ya kumshukuru. Ametufungulia milango ya elimu ya kutambua kuwa yeye ndiye Bwana. Na ametuelekeza tuwe wanyofu kwake katika kumpwekesha. Ametuepusha na upotovu na kuwa na mashaka katika amri yake. Sifa njema ambazo kwazo tutapata maisha marefu miongoni mwa viumbe wake walio muhimidi, na kwazo tumpite aliye tangulia kwenye ridhaa yake na msamaha' wake. Sifa njema ambazo zitatuangazia giza la BARZAKH na iturahisishie njia ya kufufuliwa. Ienzi mafikio yetu kwenye kisimamo cha mashahidi

'YAUMA TUJ'ZA KULU NAFSIN BIMA KASABAT WA HUM LAA YUDH'LAMUUN"

(Siku ambayo kila nafsi italipwa ilichotenda nao hawato dhulumiwa). "YAUMA LA YUGHNIIMAULA AN MAUL.4 SHA-I-AN WALA HUM YUN SWARUN"

(Siku ambayo Bwana hatomfaa chochote mtetezi wake nao hawatopata usaidizi) Sifa njema itatunyanyuwa juu mpaka juu zaidi ya walio juu) "FIKITABINMARQUMI. YASH'A HADU HUL-MUQARABUN"

(Katika kitabu kilicho andikwa. Wakishuhudia walio sogezwa karibu.) Sifa njema ambayo macho yetu yatapata utulivu pindi macho yatafanywa kiwi na kwayo sura zetu zitafanywa ziwe nyeupe pindi ngozi zitafanywa nyeusi. Sifa njema ambazo kwazo tutaachwa huru, kutoka moto mkali wa Mungu natuingiye kwenye karama ya ujirani wa Mungu. Sifa njema ambazo kwazo tutasongamana na Malaika wake walio kurubishwa, na tuungwe kwayo na Manabii wake waliotumwa.

Katika nyumba ya kudumu haitoweki, na mahali pa ukarimu wake ambao haubadiliki. Sifa njema ni za Mungu ambaye ametuchagulia maumbile mazuri.Na ametutunukia riziki muwafaka.Ametupa ubora kuvitawalia viumbe vyote. Viumbe wake wote wako chini ya utii wetu kwa Qudra yake waja kwenye kututii kwa enzi yake. Sifa njema ni zake Mungu ambaye amefunga kwa ajili yetu mlango wa mahitaji isipokuwa kwake. Kwa hiyo vipi tutaweza kumsifu? Au lini tutaweza kutekeleza shukrani zake Lahasha! Lini? Na sifa njema ni za Mungu ambaye ameunganisha katika sisi viungo vya mwili vyenye kupanuka, na ametujaalia viungo vya kushika. Ametustarehesha kwa roho ya maisha. Ametuunganishia kuwa imara viungo vya kazi. Na ametupa lishe maridhawa. Ametutosheleza kwa fadhila zake ili tusiwe na haja.

Ametumilikisha kwa wema wake. Kisha ametupa amri ili kututihani utiii wetu. Na ametukataza ili ajuwe shukrani zetu. Tumehalifu njia ya amri yake. Tumeparamia migongo ya makaripio yake! Hata hivyo hakutuharakishia adhabu yake, wala hakutuharakishia kisasi chake. Bali alikwenda nasi pole pole kwa huruma yake ikiwa ni takrima. Alitungoja turejee kwa huruma yake, ni upole (wake). Sifa njema ni za Mungu ambaye ametuonyesha jinsi ya kufana toba ambayo hatungefaulu isipokuwa kwa fadhila zake. Lau hatungeweza kuhesabu fadhila zake isipokuwa haya majaribu yake kwetu yamekuwa mema kwetu. Hisani zake kwetu ni kubwa mno. Fadhila zake kwetu ni za kutosha. Si kama hivi ulikuwa mwendo wake katika toba kwa waliokuwa kabla yetu. Ametuondolea lisilokuwa katika uwezo wetu. Hajatukalifisha isipokuwa lililo kwenye uwezo wetu hajatulazimisha jambo ila ni jepesi. Hajamwachia yeyote kati yetu udhuru wala hoja. Basi mwenye kuangamia kati yetu ni yule mwenye kuhiliki japo hataki.

Na mwenye heri kati yetu ni yule mwenye kumronga yeye. Na sifa njema ni za Mungu kwa kila aliye mhimidi malaika wake wa karibu naye. Na viumbe wake walio na heshima sana kwake, na wenye kumridhisha mno miongoni mwa wanao muhimidi. Sifa njema zilizo bora kuliko zote kama ubora wa Mola wetu juu ya viumbe wake wote. Kisha zake ni sifa njema mahali pa kila neema yake juu yetu na juu ya waja wake wote waliopita na waliobaki kwa idadi ya yaliyo zungukwa na elimu yake, toka vitu vyote. Na mahali pa kila moja miongoni mwazo idadi yake ni zaidi na zaidi milele mpaka siku ya Qiyama. Sifa njema isiokuwa na mwisho. Idadi yake haihesabiki. Mwisho wake haufikiwi. Muda wake hauna mwisho. Sifa njema itakuwa kiungo cha utii wake na msamaha wake, na ni sababu ya maridhawa yake. Na njia ya kwenye msamaha wake. Na njia ya kwenye pepo yake. Na mlinzi wa malipizi yake. Na ni usalama kwa ghadhabu yake. Usaidizi wa utii wake. Kizuizi cha maasi yake. Ni msaada wa kutekeleza haki yake na wajibu wake. Sifa njema ambazo zitatupa furaha miongoni mwa wenye furaha katika mawalii wake. Na kwayo tutakuwa katika daraja ya waliouliwa kwa upanga wa maadui wake. Hakika yeye ni mpendwa msifika.

DUA YA 2

NA ILIKUWA KATIKA DU'A YAKE(A.S) BAADA YA KUMUHIMIDI MUNGU KAMA HIVI: HUANZA KUMTAKIA REHMA MJUMBE WA MUNGU(S.A.W.W)

Sifa njema ni zake Mungu ambaye amekuwa na huruma kwetu kupitia Nabiy wake Muhammad(s.a.w.w) mbali na umma zilizopita na vizazi vilivyopita. Kwa uwezo wake ambao haushindwi kitu japo kiwe kikubwa mno. Wala haupitwi na kitu japo kiwe chepesi, au chenye hila nyingi, janja. Na alihitimisha kwetu kwa wote waumba na kutufanya tuwe mashahidi kwa wanaopinga. Kwa wema wake ametufanya tuwe wengi kwa walio wadogo. Ewe Mola mrehemu Muhammad mwaminifu wako juu ya wahyi wako (ufunuo) mteule wako kati ya viumbe wako mwenye kujitoa wakfu katika waja wako. Imamu wa rehema. Kiongozi wa mema. Funguo wa baraka. Aliye jitaabisha nafsi yake kwa ajili ya mambo yako. Amejitoa mwili wake kuyakabili yachukizayo kwa ajili yako. Alijionyesha kwenye uadui wa wazi toka kwa ndugu zake kwa kuwaita kwako. Amepigana na famili yake kwa ajili ya ridhaa yako. Amejikata na kujiweka mbali na watu wa ukoo wake ili kuihuisha dini yako. Aliwaweka mbali na ndugu wa karibu kwa upinzani wao. Aliwasogelea walio mbali kwa kuitikia kwao wito wako. Aliwafanya marafiki watu wa mbali kwa ajili yako. Na aliwafanya maadui kwa ajili yako watu wa karibu. Alijibidisha nafsi yake kuifikisha risala yako.

Aliichosha nafsi yake kuwalingania watu kwenye dini yako. Alijishughulisha kwa kutoa nasaha kwa watu waliostahiki wito wako. Alihamia ugenini mahali mbali na maeneo ya vipandwa vyake na maweko ya miguu yake mbali na alipozaliwa mbali na maeneo yafurahishayo nafsi yake. Akitaka kuienzi dini yako na kuomba msaada dhidi ya makafiri wasiokuamini wewe. Mpaka yalitimia aliyojaribu kuyafanya dhidi ya maadui wako. Na yalifanikiwa aliyoyapanga kwa ajili ya wapenzi wako. Aliibuka na ushindi kwa msaada wako akiwa na nguvu kwa nusura yako pamoja na udhaifu wake. Aliwapiga wakiwa ndani ya miji yao.

Aliwahujumu ndani ya makazi yao mpa amri yako ilishinda neno lako likawa juu kabisa ingawaje washirikiina walichukia. Ewe Mwenye enzi Mungu mwinuwe kwa kuwa ametaabika kwa ajili yako, afikie daraja la juu kabisa katika jannah zako ili asilingane kwa daraja. Ili asiwe rika katika daraja wala malaika waliokaribu wasimkurubie hata Nabiy mursalu. Umtambulishe katika Ali wake waliotakaswa na umma wake walio waumini kuwa watakuwa na uombezi mwema zaidi ya vile ulivyo muahidi. Ewee mtekelezaji wa ahadi mtimizaji wa qauli. Ewee! mwenye uwezo wa kubadilisha maovu kwa mema mengi hakika wewe ndio mwenye fadhila tukufu mno.

DUA YA 3

NA MIONGONI MWA DU'A ZAKE KWA MALAIKA WABEBAO ARSHI NA KWA KILA MALAIKA

Ewe Mola na kwa wabeba arshi yako ambao hawalegei kukusabihi wala hawachoki kukutakasa, wala hawafifii kukuabudu wewe hawazembei kufanya bidii katika amri yako. Na wala hawaghafiliki kuwa na nguvu ya mapenzi yako. Na Israafil malaika wa baragumu amesimama tayari angoja idhini yako tu na amri yako ili awazinduwe kwa pulizo waliotupwa chini makaburini. Na Mikail mwenye hadhi kwako na nafasi ya daraja la juu katika kukutii wewe. Na Jibril atambulikaye kwa uaminifu kufikisha wahyi (ufunuo) wako, mwenye kutiiwa na wakazi wa mbingu yako mwenye kuheshimiwa mbele yako na mwenye kusogezwa karibu na wewe. Na roho ambaye yuna ngazi ya juu miongoni mwa malaika wa hijabu, na roho ambaye ni amri yako, Ewe Mola warehemu na wale malaika walio chini yao miongoni mwa wakazi wa mbingu zako ambao ni miongoni mwa waamini wao kwa risala yako (jumbe) ambao hawachoshwi na hali ya kudumu wala hawaishiwi nguvu kwa kazi ngumu wala hawalegei. Wala hawasumbuliwi na matamanio ili waache kuku takasa wewe. Hawakatishwi na wakati wa usahaulifu katika kukutukuza. Wanyenyekevu wa macho hawathubutu kuinua macho yao kukuangalia videvu vyao viko chini ambao utashi wao umekuwa mrefu kwa yaliyo kwako. Wamerukwa na akili kwa upendo wa kuzitaja neema zako. Wanyenyekevu mbele ya utukufu wako na utukufu wa ukubwa wako. Wasemao waangaliapo jehanam ikiunguruma kwa ajili ya wanaokuasi, utakasifu ni wako hatujakuabudu ipasavyo kukuabudu wewe. Hivyo basi uwarehemu na rawhaniyyeena miongoni mwa malaika wako na wale wenye ukaribu kwako.Na wale wapelekao mambo yaliyo ghaibu kwa mitume wako na walioaminiwa kwa wahyi wako.Na kabila za malaika uliowafanya mahsusi kwa ajili yako na uliowaepusha na haja ya chakula na kinywaji kwa kukutakasa wewe uliowafanya waishi ndani ya tabaka za mbingu zako. Na ambao watasimama kwenye mipaka ya mbingu iteremkapo amri kwa kutimia ahadi yako.

Wahifadhi wa mvua na watawanyaji wa mawingu ambaye kwa sauti ya karipio lake husikika muungurumo wa radu. Na mrindimo wa mawingu unapoelea kuelekea kwenye umeme sauti ya muwako itajitokeza. Na mpelekaji wa theluji na baridi na wateremkao na matone ya mvua yateremkapo na walinzi wa hazina za upendo. Mawakala wa ulinzi wa mirima isije poromoka. Na wale uliowajulisha uzito wa maji na vipimo vilivyomo katika mvuwa kubwa na wingi wake. Na malaika ambao ni wajumbe wako kwa wana ardhi kwa mambo yachukizayo na yashukayo miongoni mwa balaa na raha ipendwayo. Na malaika watukufu waandishi na malaika wa mauti na wasaidizi wake. Na Munkari na Nakiiri. Na Ruman mtahini wa kaburini na wazunguka Baitul-maamur na Maliki malaika mlinzi wa moto na Rizwan malaika walinzi wa jannah. Na ambao (hawamuasi Mungu aliyowaamrisha na wafanya wanayo amriwa). Na ambao husema (salamu iwe juu yenu kwa vile mulivumilia neema ni nyumba ya mwisho). Na Mazabaniya ambao wakiambiwa: (Mchukuweni mtupeni kisha mchomeni katika jehannam) watamharakia upesi sana hawatompa muda.Na yule ambaye tumeshindwa kumtaja na hatukujua mahali pake kwako na kwa jambo gani umemuwakilisha.Na malaika wakazi wa hewani na ardhini na majini, na wale uliowawakilisha kwa viumbe.Warehemu siku ambayo kila nafsi itakuja ikiwa na msukumaji na shahid. Uwarehemu kwa rehema zitakazo wazidishia heshima juu ya heshima zako na kuwazidishia usafi juu ya usafi wao. O Mola ukiwarehemu malaika wako na wajumbe wako na kuwafikishia (maombi yetu ya) rehma kwao (twakuomba) uwarehemu kwa kauli njema uliotufungulia kwa ajili yao. Wewe ni mpaji mkarimu.

Dua ya 4

NA MIONGONI MWA DU'A ZAKE AMANI IMFIKIE KATIKA KUWA TAKIA REHMA WAFUWASI WA MITUME NA WALIO WASADIKI MITUME

Ewe Mola na kwa ajili ya wafuasi wa mitume na waliowasadiki bila kuonekana miongoni mwa wana wa ardhini wanapokabiliwa na upinzani wa wale wanaowapinga kwa kuwafanya waongo. Na kuwaonea shauku mitume kwa njia ya iymani ya hakika. Ulituma katika kila muda na zama uliwatuma mitume wakiwa na dalili kwa ajili ya watu. Tokea Nabiy Adam mpaka zama za Muhammad (s.a.w.) miongoni mwa maimamu waongofu na viongozi wa wachamungu wote amani iwafikie. wakumbuke kwa msamaha na ridhaa. Ewe Mola khususan kwa swahaba wake Muhammad waliokuwa wema katika usuhuba. Waliokuwa na majaribu mema katika kumsaidia na kumhami. Walimwitikia kwa haraka alipowasikilizishia hoja za ujumbe wake. Walitengana na wake, na watoto ili kulidhihirisha neno lake. Waliwapiga vita mababa na watoto ili kuuthibitisha unabiy wake kupitia kwake walishinda. Waliozingirwa na upendo wake watarajia biashara ambayo haitokuwa na hasara katika upendo wake. Na wale waliotengwa na jamaa zao pale tu waliposhikamana naye, na ukiraba kwao ulikwisha ili tu wakitulia chini ya kivuli cha ukaribu wake. Hivyo basi ewe Mola usiwasahau kwa yale waliyoyaacha kwa ajili yako na katika wewe waridhishe kwa ridhaa zako. Kwa ajili ya faida ya viumbe wamejitoa kwako. Walipokuwa na mjumbe wako walikuwa walinganiaji wako kwa ajili yako, waonyeshe ridhaa yako kwa kuhama nyumba za watu wao kwa ajili yake na kutoka kwao nje ya maisha ya wasaa na kwenda kwenye maisha ya dhiki. Wale ambao kwa kudhulumiwa kwao umewazidishia ili kuienzi dini yako. Ewe Mola wape taabeena waliotenda mema kwa kufuata nyayo za masahaba.Wanasema: (Ee! Mola wetu tusamehe sisi na ndugu zetu waliotutangulia kwa iymani) malipo yako yaliyomema kwa waliokwenda njia yao waliochagua mwendo wao na walikwenda kwa utaratibu wao hawakugeuzwa upande na shaka katika utambuzi wao. Na wala hawakuingiwa na shaka katika kufuata nyayo zao na kuongoka na mwongozi wa nuru yao.Waendesha dini yao hali ya kuwahami na kuwasaidia.Wanaongoka kwa mwongozo wao, wanawafikiana nao. Wala hawawatuhumu kwa yale waliowapa. Ewe Mola wape rehma taabeena toka siku yetu hii mpaka siku ya malipo na rehma iwafikie wake zao na kizazi chao na wale waliokutii miongoni mwao. Rehma ambayo itawalinda wasikuasi na itawapatia nafasi katika maeneo ya janna yako.

Na itawakinga na makidi ya shetani. Na itawasaidia kwa yale waliokuomba msaada kwa ajili yake miongoni mwa wema. Na itawalinda na matukio ya ghafla ya usiku na mchana isipokuwa tukio lijalo kwa wema. Kwazo utawaimarisha kuwa na iymani ya matarajio mema kwako na kutumai yale uliyonayo. Na watokane na tuhuma kwa ajili ya yale yaliyomo mikononi mwa waja. Ili uwarejeshe kwenye upendo wako na kukuogopa wewe. Washawishhi waache kupigania wingi wa mapato ya haraka. Na uwapendezeshe kufanya mema kwa ajili ya baadaye na kujiandaa kwa yatakayojitokeza baada ya umauti. Na uwafanyie wepesi kila tatizo litakalo wafika siku nyoyo zitokapo nje ya viwili wili vyake. Na uwaepushe na yaletayo fitna miongoni mwa yaliyo hadharishwa, kutupwa motoni na kubaki milele humo.Uwafanye wawe katika amani miongoni mwa makazi ya wachamungu.

2

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

DUA YA 5

NA ILIKUWA MIONGONI MWA DU'A ZAKE KWA AJILI YAKE MWENYEWE (A.S) NA KWA WALIO CHINI YA WILAYA YAKE

Ewee! ambaye maajabu ya utukufu wake hayatokwisha. Mrehemu Muhamadi na Ali zake tuzuwiye kupotoka katika utukufu wako. O we ambaye muda wa ufalme wake hautakoma. Mrehemu Muhammad na Aali zake zikomboe shingo zetu na lipizi zako. Oh! wee ambaye hazishi hazina za rehma zake mrehemu Muhammad na Aali zake. Na utupe sehemu katika rehema zako, Oh wee ambaye macho yanashindwa kumwona. Mrehemu Muhammad na Aali zake, tusogeze karibu yako. Oh! wee ambaye unakuwa mdogo ukubwa wa kila kikubwa mbele yake. Mrehemu Muhammad na Aali zake utupe heshima. Oh, wee ambaye mbele yake hujitokeza kila kilichojificha. Mrehemu Muhammad na Aali zake. Usitufedheheshe mbele yako. Ewe Mola! tuonndolee haja ya hiba ya watowao hiba kupitia hiba zako. Tutosheleze tusisumbuliwe na kitwea cha wajitengao nasi kwa mawasiliano yako ili tusimsihi yeyote pamoja na kuwa wewe watupa bure. Wala tusione kitwe kutokana na yeyote ikiwa fadhila zako twazipata. Ewee Mola! Mrehemu Muhammad na Aali wake. Na utupangie wala usipanguwe dhidi yetu. Tupe ushauri kwa faida yetu wala si kinyume chake. Mzunguko wa neema udumishe kwetu wala usiuelekeze kwingine. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aali zake na utulinde sisi kuwa dhidi yako. Na utulinde kupitia wewe mwenyewe.

Utuongoze kuelekea kwako wala usituweke mbali na wewe. Kwa hakika umlindaye huwa salama. Na umwongozaye hujuwa. Umwekaye karibu nawe hupata ngawira. Ewee Mola mrehemu Muhammad na Aali zake. Na tukinge na makali ya mabadiliko ya wakati, na shari ya windo la shetani. Na ukali wa udhalimu wa kisultani Ewe Mola kwa hakika wajitoshao wajitosha kwa fadhila za uwezo wako. Msalie Muhammad na Aali zake kwa hakika hutowa watowao kupitia wingi wa utajiri wako. Mrehemu Muhammad na Aali zake na utupe, huongoka waongokao kwa nuru ya uso wako, msalie Muhammad na Aali wake na tuongoze. Ewe Mola hakika uliyemfanya rafiki hakumdhuru kutelekezwa na watelekezaji. Na uliyempa hapungukiwi kwa kunyimwa na wanyimaji. Na uliyemwongoza haumpotezi upotovu wa wapotovu. Mrehemu Muhammad na Aali zake. Na utuzuiye (tusidhuriwe na waja wako) kwa nguvu zako. Tutosheleze tusimhitaji mwingine mbali na wewe kwa kuungwa mkono na wewe. Tupitishe njia za haki kwa mwongozo wako. Ewe Mola msalie Muhammad na Aali zake. Na jaalia usalama wa nyoyo zetu kwa kukumbuka utukufu wako. Na nafasi ya wazi ya miili yetu iwe twakushukuru neema zako. Na ujaaliye mtiririko wa ndimi zetu uwe katika kusifu ihisani zako. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aali zake. Tujaalie tuwe miongoni mwa wahitaji wako wanaowaita watu kuja kwako na viongozi wako waongozao kuelekea kwako. Na tuwe miongoni mwa watu makhsusi uliowafanya wawe makhsusi kwako. Ewe mwenye kurehemu mno kuliko wenye kurehemu wote.

DUA YA 6

NA ILIKUWA MIONGONI MWA DU'A ZAKE A.S. NYAKATI ZA ASUBUHI NA JIONI

Sifa njema ni za Mungu ambaye ameumba usiku na mchana kwa nguvu zake. Na amezipambanuwa kwa uwezo wake. Na amekifanyia kila kimoja kati ya hivi viwili mpaka wenye kikomo na muda ulio na mwisho. Hukiingiza kila kimoja ndani ya mwenzake. Na humwingiza mwenzake ndani.yake. Kwa mpango kutokana na yeye, kwa ajili ya waja kwa vile awalishavyo na kwa hivyo ndivyo awakuzavyo. Amewaumbia usiku ili wapumzike humo kutokana na harakati za taabu na juhudi zenye kuchosha. Na ameufanya (usiku) kuwa vazi ili wajisitiri kwa mapumziko humo kwa kulala, iwe kwao kiburudisho na nguvu mpya na waifanyie kwa huo usiku furaha na matamanio. Na amewaumbia mchana uwezeshao kuona ili wazifikie fadhila zake. Na iwe sababu ya kuipata rizki yake. Na wazunguke kwa uhuru katika ardhi yake wakitafuta kipato cha mwenye haraka ya dunia yake na kufanikiwa ya baadaye katika maisha ya akhera. Kwa yote hayo awawekea sawa hali yao na kuuzifanyia mtihani khabari zao, ili awaangalie wakoje wakati wa utii wake na mahali mwa wajibu zake. Na sehemu za hukumu zake.(Ili awalipe waliotenda maovu kulingana na waliyotenda. Na awalipe waliotenda mema wema.) Ewe Mola! sifa zote njema ni zako. Kwa kutukunjulia asubuhi, na kutufanya tufurahie mwanga wa mchana. Na umetufanya tuone jinsi ya kuitafuta chakula na umetulinda na maafa. Tumekuwa asubuhi na vimekuwa vitu vyote pamoja ni vyako. Mbingu, ardhi na ulicho kitawanya kwa kila mmoja wao chenye kutulia na chenye kufanya harakati kikazi na chenye kusafiri na kirukacho juu kabisa angani na kijifichacho chini ya ardhi twapambazukiwa na asubuhi katika ushiko wako. Twazingirwa na ufalme wako na mamlaka yako. Tumo ndani ya utashi wako. Tunakwenda hapo na pale kwa amri yako. Tunageuka geuka ndani ya mpango wako.Hatumiliki letu jambo ila ulilolipitisha, wala hatulimiliki jambo la kheri isipokuwa ulilotoa. Na hii siku mpya imekuja, itakuwa shahidi madhubuti kwetu, tukifanya mema itatuaga iondokapo kwa sifa njema. Na tufanyapo maovu itatuacha kwa lawama. Ewe! Mola msalie Muhammad na Aali wake. Na utupe uzuri wa kusuhubiana naye na utulinde na kutengana naye vibaya, kwa kutenda yasiyofaa au kutenda dhambi yeyote ile ndogo au kubwa. Tufanye tuwe na matendo mema mengi humo na tuepushe na matendo maovu humo. Na jaza kwa ajili yetu kati ya ncha zake mbili sifa njema na shukrani, ujira na akiba, fadhila na ihsani. Ewe Mola wepesisha mizigo yetu kwa waandishi watukufu, na lijaze mema yetu katika sahifa zetu (karatasi za hesabu) usitudharaulishe kwako kwa matendo yetu maovu. Ewe Mola tujaaliye hadhi toka kwa waja wako katika kila sehemu ya shukurani zako. Na ushahidi wa kweli miongoni mwa malaika wako.

Ewe Mola msalie Muhammad na Aali zake. Utuhifadhi mbele yetu na nyuma yetu kuliani kwetu na kushotoni kwetu na pande zetu zoote, hifadhi inayotulinda na kukuasi wewe, yenye kutuongoza kwenye utii wako, yenye kutekeleza upendo wako. Ewe Mola! msalie Muhammad na Aali zake. Na utukubalie katika siku yetu hii na usiku wetu huu na katika siku zetu zoote kuitenda kheri na kuihama shari na kuishukuru neema na kuzifuata sunnah na kujiepusha na bidaa, na tuwe wenye kuamrisha mema na kukemea maovu. Kuulinda Uislamu na kuutweza ubatili na kuudhalilisha ili kuinusuru haki na kuipa nguvu kumwongoza aliyepotoka kumsaidia mnyonge kumkomboa aliyekatika taabu. Ewe Mola msalie Muhammad na Aali zake. Na ifanye (siku) kuwa ya baraka mno kuliko siku ya baraka tuijuayo na mwenzi bora kuliko mwenzi yeyote tumepata kuwa naye na wakati uwe ni wakati bora kuliko wakati wowote tumepata kuwa chini ya kivuli chake. Na utufanye tuwe wenye kuridhiwa mno miongoni mwa waliopitiwa na usiku na mchana katika jumla ya viumbe wako. Wenye kushukuru sana kati yao kwa mema uliowapa miongoni mwa neema zako. Watekelezaji kwa uthabiti mno wa sheria uliowawekea miongoni mwa sheria zako. Na wenye kujizuia sana na uliyo yahadharisha miongoni mwa makatazo yako. Ewe Mola mimi nakufanya shahidi nawe nishahidi tosha. Na ninazifanya mbingu zako na ardhi zako na uliowafanya kuwa wakazi wa mbingu na ardhi kuwa mashahidi miongoni mwa malaika wako na viumbe wako wengine. Katika siku yangu hii saa yangu hii usiku wangu huu na kikazi changu hiki. Hakika mimi nashuhudia kuwa hakika wewe ni Mungu ambaye hapana Mungu mwingine isipokuwa ni wewe! mwenye kuidhibiti adala uko mwadilifu katika hukumu mwenye huruma kwa waja-u-Mfalme wa Wafalme mwenye huruma kwa viumbe. Yakuwa Muhammad ni mja wako na ni mjumbe wako mteule wako miongoni mwa viumbe wako. Umembebesha risala yako na ameitekeleza. Ulimuamuru kuitowa nasaha kwa umma wake na aliunasihi. Ewe Mola msalie Muhammad na Aali zake. Zaidi ya vile ulivyomsalia yeyote katika viumbe wako. Umpe kwa niaba yetu kilicho bora ulichompa yeyote katika waja wako. Na umlipe kwa niaba yetu kilicho bora na hheshima zaidi kuliko ulichomlipa yeyote miongoni mwa Manabiy wako kwa niaba ya umma wake. Hakika wewe ndiye mtowaji kwa wingi na msamehevu wa makubwa nawe u mwenye huruma zaidi kuliko mwenye huruma yeyote. Msalie Muhammad na Aali zake wema waliotahirika wateule waheshimiwa.

DUA YA 7

NA ILIKUWA MIONGONI MWA DU'A ZAKE (A.S) ANAPOTOKEWA NA JAMBO SUMBUFU AU KUSHUKIWA NA TAABU NA WAKATI WA KUKERWA

Oh! we ambaye kwake hufunguka mafundo ya mambo yachukizayo. Ee! wee ambaye kwake makali ya shida huwa butu. Ee we! ambaye huombwa njia ya kutoka kuelekea kwenye burudisho la faraja. Magumu yamekuwa dhalili mbele ya nguvu zako. Kwa huruma zako sababu zimepatikana. Kwa nguvu zako hukumu zimepita. Kwa utashi wako vitu vimekwenda kama ilivyotakiwa. Kwa utashi wako bila ya kauli yako vimewajibika. Kwa utashi wako vimejiziwiya bila ya kutumia katazo lako, wewe ndiye wa kuombwa wakati wa jambo litishalo. Na ndio kimbilio la wakati wa shida haiondoki isipokuwa ile shida ulioiondowa. Haitoki isipokuwa uliyoitowa, yameniteremkia ewe Mola wangu ambayo uzito wake umenielemea.Juu yangu kumeshuka jambo ambalo uzito wake umenishinda. Kwa nguvu zako umeshusha juu yangu kwa mamlaka yako umeelekeza kwangu.

Hakuna wa kuondowa ulichokileta, wala kuziwiya ulichokielekeza, wala wakufunguwa ulicho funga, wala wakufunga ulichokifunguwa, wala wa kufanya kiwe chepesi ulichokifanya kigumu, wala wakumsaidia uliyemwacha. Msalie Muhammad na Aali zake, na nifungulie ewe Mola wangu mlango wa faraja kwa rehma zako, niondolee mamlaka yatishayo kwa nguvu zako. Unipe mtazamo mzuri kwa malalamiko yangu. Unionjeshe utamu wa matendo kwa niliyoomba. Na unipe kutoka kwako rehmah na faraja njema. Na nijaalie mwanya wa kupenya kutoka kwako. Usinifanye nijishughulishe na mengine na kuacha wajibu wako. Na kuifanya sunnah yako. Nimezikika na yaliyo nishukia Ee Mola wangu nimejawa na huzuni kwa kuyabeba yaliyo niteremkia.Wewe ndiye mwenye uwezo wa kuondoa yaliyo nifika na kuyaweka mbali niliyoangukia, nifanyie hivyo ingawaje sistahiki kwako hivyo Ewee! bwana wa arshi tukufu.

DUA YA 8

DU'A ZAKE KATIKA KUJILINDA NA MAMBO YACHUKIZAYO NA TABIA MBAYA NA MATENDO YALAUMIWAYO

Ewe Mola najilinda na wewe dhidi ya uchochezi wa pupa na ukali wa ghadhabu na kuhemewa na husda na kudhofika kwa subira na uchache wa kutosheka na ukali wa tabia.Na uchochezi wa harara. Na kumilikiwa na msukumo wa tabia au jadhba. Na mgeuzo wa nia na kwenda kinyume na uongofu na sinzio la kughafilisha na kujikalifisha (yaani kujitwisha mambo zaidi ya uwezo) kuchaguwa batili na kuiacha haki. Na kujibakisha na kuendelea na madhambi na kuyadogesha maasi na kuukuza utii. Na kujifaharisha kwa matajiri na kuwadharau masikini na uangalizi mbaya kwa walio chini yetu. Na kutokuwa na shukrani kwa waliotutendea mema au tumsaidiye dhwalimu au kumtelekeza mwenye taabu au kujitakia yasiyo haki. Kwetu au tuongee kuhusu elimu bila ya elimu au kujihusisha na kumghushi yeyote na kujionea fahari matendo yetu. Na kuwa na matumaini marefu. Na tunajilinda na wewe kuwa na undani na kukidharau kidogo. Na kudhibitiwa na shetani. Au kuhujumiwa na wakati, au kudhulumiwa na mtawala. Na tunajilinda na wewe kufanya israfu na kuwa na kisichotosha. Na tunajilinda na wewe na masimango ya maadui. Na kukosa wenzi, na kuishi katika shida na kufa bila ya maandalizi. Na twajilinda na hasara kubwa mno na msiba mkubwa na twajilinda na mwisho mbaya, na kunyimwa thawabu na kufikwa na adhabu. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aali zake na unilinde na yote hayo kwa huruma yako na waumini wote wanaume na wanawake. Ewe! mwingi wa rehma kuliko wenye kurehemu wote.

DUA YA9

NA MIONGONI MWA DU'A ZAKE AKIWA NA SHAUKU SANA YA KUOMBA MSAMAHA KWA MWENYE ENZI MUNGU MTUKUFU

Ewe Mola msalie Muhammad na Aali zake, tufanye tuelekee kwenye toba uipendayo. Na ututoe tusiendelee kutenda uchukialo. Oh! Mola tusimamapo kati ya hali mbili ya upungufu iwe siku ya dini au dunia uiondoe hali ile ya upungufu haraka iishe. Na ujaalie kwangu toba iwe ya kubaki sana miongoni mwa mawili hayo. Na tuyakusudiapo mambo mawili moja la kuridhisha kutoka kwetu na la pili lakuchukiza toka kwetu. Tufanye tuelemee kwenye lile likuridhishalo toka kwetu. Dhoofisha nguvu zetu kwenye linalokuudhi na kutuchukia kwa ajili yake. Usiziache nafsi zetu kuchaguwa kwa sababu zenyewe huchaguwa batili isipokuwa ulizozipa taufiki. Na zenye kuamrisha mabaya isipokuwa ukirehemu. Ewe Mola kutokana na unyonge umetuumba, na umetujenga juu ya hali duni umetuanza (kutuumba) kutokana na maji hafifu. Hatuna uwezo isipokuwa kwa nguvu zako, wala nguvu hatuna isipokuwa kwa msaada wako. Tuwezeshe kwa kutufanikisha. Tuongoze kwenye njia ya sawa kwa mwongozo wako.

Ipofushe nguvu ya kuona ya nyoyo zetu dhidi ya yaendayo kinyume na mahaba yako. Usikijaalie chochote katika viungo vyetu vya mwili upenyo wa kwenye maasi yako. Ewe Mola! mrehemu Muhammad na Aali zake. Na jaalia nong'ono za nyoyo zetu na harakati za viuongo vyetu na mitupo ya macho yetu na semi za ndimi zetu viwe kwa ajili ya mambo yawajibishayo thawabu zako. Ili tusije pitwa na jema twastahiki kwalo malipo yako. Na usitubakishie tendo baya ambalo tutastahiki kwa ajili yake adhabu yako.

DUA YA 10

MIONGONI MWA DU'A ZAKE AKIOMBA KIMBILIO KWA MUNGU

Ewe Mola! Ukipenda tusamehe kwa fadhila zako na ukipenda utatuadhibu na hiyo itakuwa kwa uadilifu wako. Hivyo basi tufanyie wepesi msamaha wako kwa huruma yako. Tuepushe na adhabu yako kwa subira zako. Kwa kuwa hatuna uwezo kuukabili uadilifu wako. Wala hakuna atayeokoka bila ya msamaha wako. Ewe mwenye kujitosheleza kuliko matajiri wote. Tu hapa waja wako mbele yako. Nami ni fakiri kuliko mafakiri wote kwako. Urekebishe ufakiri wetu kwa wasaa wako. Usikate matumaini yetu kwa zuio lako, utakuwa umemdhalilisha mwenye kukuomba heri. Na umemnyima aliyekuomba fadhila zako. Kwa hiyo tugeukie kwa nani mbali na wewe, twende! Wapi kama si mlangoni kwako! Utakatifu ni wako, sisi ni wenye kudhikika ambao umewajibisha kuwakubalia. Ni wenye uovu uliowaahidi kuwaondolea uovu wao. Ni kitu chafanana sana na utashi wako. Na ni bora kulingana na utukufu wako, kumuhurumia aliye kuomba umuhurumie. Kumsaidia aliekuomba msaada uhurumie ungamo letu kwako. Tutosheleze tujitupapo mbele yako. Oh! Mola wetu hakika shetani ametusimanga, kwa kuwa tumemfuata katika kukuasi wewe. Mrehemu Muhammad na Aali zake usimwache atusimange baada ya kuwa tumemwacha kwa ajili yako. Tumemtelekeza na kuelekea kwako.

3

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

DUA YA 11

DU'A ZAKE KWA AJILI YA MWISHO MWEMA

Ewe! mwenye utajo wake ni heshima kwa wamtajao. Ewe! mwenye shukrani yake ni ufanisi kwa wenye kumshukuru. Owe! Mwenye utii wake ni uokovu kwa wenye kumtii. Mswaliye Muhammad na Aali zake. Zihangaishe nyoyo zetu katika kukutaja wewe na kuziweka mbali na utajo mwingine wote. Na zihangaishe ndimi zetu katika kukushukuru na ziwe mbali na shukuru zingine zote. Na viungo vyetu vya miili vihangaike kukutii wewe na kuwa mbali na utii mwingine wowote. Ukitupangia wakati wa faragh (usio na kazi) basi jaalia faragha iliyo salama. Tusifuatwe na lipizi baya, wala usituambatanishie humo na kuchoshwa, ili watuondokee waandishi wa maovu na nyaraka tupu zisizotaja chochote katika maovu yetu. Na warudi waandishi wa mema kutoka kwetu wakiwa na furaha na waliyoyaandika miongoni mwa mema yetu. Na ziishapo siku za maisha yetu na kumalizika kwa muda wa umri wetu. Na kutufikia wito wako ambao hapana budi utufikie na pia hapana budi kuujibu. Msalie Muhammad na Aali zake. Na jaalia mwisho wa matokeo ya hesabu ya waandishi wa mabaya yetu kuwa toba yenye kukubaliwa. Usitusimamishe na dhambi tuliyotenda baada yake, wala maasi tuliyoyafanya, wala usifichue sitara uliyotusitiri mbele ya mashahidi siku zitakapojaribiwa khabari za waja wako. Hakika wewe ni mpole kwa akuombaye na u mwenye kuitika kwa akuitaye.

DUA YA 12

DU'A ZAKE KATIKA KUKIRI NA KUOMBA TOBA KWA MUNGU MTUKUFU

Ewe Mola! tabia tatu zaniziwiya kukuomba na moja yanihimiza nikuombe, iniziwiayo jambo umeamrisha na nikazembea kulifanya. Na katazo umenikataza nikaharakia kulitenda. Na neema ulinineemesha nayo nikashindwa kuishukuru. Na linihimizalo kukuomba ni fadhila zako kwa mwenye kuelekeza uso wake kwako. Na akaja kwa dhana nzuri kwako kwa kuwa ihsani zako zote ni fadhila. Na kwa sababu neema zako zote ni mwanzo mpya. Basi mimi huyu hapa Ewee! Mola wangu mwenye kusimama kwenye mlango wa enzi yako msimamo wa aliyesalim amri dhalili.Nikikuomba nikiwa na haya ombi la fakiri hohe hahe mnyonge. Mwenye kukiri kwako, sikusalimu amri wakati wa ihsani yako isipokuwa kwa kujiweka mbali na maasi yako. Sijapata kuwa katika hali zangu zote bila ya huruma zako. Je kutanifaa ewe Mola wangu kukiri kwangu kwako kwa maovu niliyotenda? Je kutaniokoa kutambua kwangu kwako kwa mabaya niliyotenda? Au utawajibisha makasiriko yako kwangu katika kikao changu hiki? Au chukio lako litaniambata wakati wa DU'A yangu? Utakatifu ni wako, sikati tamaa nawe hali umenifungulia mlango wa toba kwako. Bali nasema usemi wa mja mnyonge mwenyekujidhulumu nafsi yake, mwenye kuifanya haramu ya Mola wake kuwa kitu chepesi. Ambaye dhambi zake zimekuwa kubwa mno. Ambaye siku zake zimemtumbia mgongo na kutokomea. Mpaka aonapo muda wa kazi ya ibada umeisha. Na upeo wa umri umekwisha. Na akawa na yakini kuwa hana njia ya kujiepusha nawe, na hana kimbilio litalomweka mbali nawe.

Akugeukia kwa marejeo ya mara kwa mara, na kufanya toba kwako kwa ikhlaswi. Atasimama mbele yako kwa moyo safi kabisa. Na kukuomba kwa sauti dhalili ya chini, ameinama mbele yako na kujipinda hali ameinamisha kichwa chake chini, woga wake watetemesha miguu yake machozi yamtiririka mashavuni mwake. Akuomba akisema Ewe mwingi wa kurehemu kuliko wote! Ewe mwingi wa kurehemu wa wanaorejea kwake wakimwomba huruma. Ewee mwenye huruma mno kwa wenye kumzunguka waombao msamaha. Ewe ambaye msamaha wake ni mwingi kuliko malipizi yake. Ewe ambaye ridhaa yake ni nyingi sana kuliko makasiriko yake. Ewe yule ambaye amesifika kwa waja wake na njema saburi njema. Ewe ambaye amewazowesha waja wake kwa kukubali marejeo yao ya mara kwa mara. Oh! yule ambaye amewarekebisha waharibifu wao kwa njia ya tobah. Oh! yule ambaye ameridhika na madogo katika matendo yao. Oh! yule ambaye huwalipa mengi kwa machache yao. Oh! yule ambaye amechukuwa dhamana kwa ajili yao kuzikubali DU'A. Oh! yule ambaye amewaahidi mwenyewe binafsi kwa fadhila zake malipo mema. Mimi sio muasi zaidi kuliko waliokuasi na umewasamehe, wala mimi si mlaumiwa mno miongoni mwa walioomba udhuru kwako na umewakubalia, wala mimi si mdhalimu mno miongoni mwa waliotubu kwako na umepokea toba yao. Natubu kwako katika kikao changu hiki toba ya mwenye kujutia waliyompita. Mwenye kutambua yaliyomzunguka, mwenye haya sana kwa yaliyo mfika, ajua kuwa kuisamehe dhambi kubwa mno haliwi jambo kubwa kwako.

Na kuyafumbia macho madhambi makubwa kabbisa haiwi ngumu kwako. kuyavumilia makosa mabaya sana ya jinai hayakupi tabu. Na yakuwa mja wako mpendwa sana kwako ni mwenye kuacha kibri mbele yako. Na akajiepusha na kung'ang'ania, kashikamana na kuomba msamaha. Nami najitakasa kwako nisiwe na kibri na ninajilinda kwako nisiwe mwenye kung'ang'ania nakuomba msamaha kwa nililozembea. Naomba msaada kwa nililohemewa ewe Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake. Nipe yaliyowajibu wangu kwako, niondolee ninayostahiki kwako. Nitakase na wayaogopayo waovu. Wewe ni mwingi wa msamaha, mwenye kutumainiwa msamaha, wajulikana kuwa umvumilivu. Haja yangu haina pakuitafutia isipokuwa kwako. Wala dhambi zangu hazina wakuzisamehe asiyekuwa wewe. Je! lawezekana hilo? Sijihofu binafsi ila kwako, hakika wewe ni mstahiki wa taqwa na mstahiki wa msamaha.Mrehemu Muhammad na Aliy zake nikidhie haja yangu. Fanikisha ombi langu. Nisamehe dhambi zangu. Nipe dhamana ya woga wa nafsi yangu hayo ni mepesi kwako, aameen ewe bwana wa maumbile yote.

DUA YA 13

DU'A ZAKE KUMWOMBA HAJA MUNGU MTUKUFU

Oh Allah. Ewe! mwisho wa maombi ya haja zote. Ewe! ambaye kupitia kwake mahitaji hupatikana. Ewe! ambaye hauzi neema zake kwa thamani. Oh! yule ambaye hakipaki tope akitowacho kwa masimbulizi. Ewe! yule ambaye hutosheka kwa kupitia kwake hatosheki mtoshekaji bila ya yeye. Ewe yule ambaye hutakiwa na hauwi utashi kando na yeye. Ewe yule ambaye hazina zake hazimalizwi na maombi. Ewe yule ambaye sababu hazibadilishi hikima yake. Oh! yule ambaye hazishi kwake haja za wahitaji. Oh! yule ambaye hayampi dhiki maombi ya waombao, umesifika kwake kutokuwa muhitaji toka kwa viumbe wako. Wewe wastahiki kuwa uwahitajii wao, umewahusisha na ufakiri wao ndio wahitaji kwako. Hivyo basi mwenye kujaribu kuziba pengo lake kupitia kwako. Na akusudia kujiondolea ufakiri kwa njia yako. Atakuwa ametafuta mahitaji yake mahali pafaapo. Na atakuwa ameyaleta mahitaji yake katika njia zake. Na mwenye kuelekeza mahitaji yake kwa yeyote miongoni mwa viumbe wako au kuifanya sababu ya kufanikiwa kwake kando na wewe atakuwa amejiweka kwenye hatari ya kunyimwa. Na atakuwa amestahiki kwako kukosa ihsani. Oh! Allah ninahaja kwako. Juhudi yangu imeshindwa, mbinu zangu zimeshindwa kuifikia nafsi yangu imenishawishi kuifikisha haja yangu kwa awezaye kuifikisha kwako. Wala hajitoshi katika mahitaji yako kando na wewe, na huku ni kuteleza miongoni mwa mtelezo wa watenda makosa na ni kujikwaa wanako jikwaa watenda madhambi. Kisha nilizinduka kwa kumbusho lako kwangu kutokana na mghafala wangu. Nimeinuka kwa taufiki yako kutoka kwenye mtelezo wangu.

Nimeimarika kwa imarisho lako na kujitoa kwenye telezo langu. Nasema subhana Rabiy (utakatifu ni wa Mola wangu), vipi muhitaji amwomba muhitaji mwingine? Ni vipi asiyekuwa na kitu amwomba asiyekuwa na kitu mwingine! Hivyo nimekuja kwako ewe Mola wangu kwa upendo, nimeyaelekeza matumaini yangu juu yako kwa kukuamini. Na nimejua kuwa mengi nikuombayo ni kitu kidogo mbele ya utajiri wako. Mazito nikuombayo ni kidogo kulinganisha na wasaa wako. Na ukarimu wako hautakuwa mdogo kwa sababu ya ombi la yeyote. Na kwa hakika mkono wako kwa utowaji uko juu kuliko kila mkono. Ewee Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake, nichukuwe kwa ukarimu wako kwa kunifadhili. Na usinichukuwe kulingana na uadilifu wako si kwa ninavyostahiki. Mimi si wa kwanza kukusihi miongoni mwa aliokusihi umempa hali ilikuwa astahiki kunyimwa. Na wala si kuwa mwombaji wa kwanza katika aliyekuomba na ukamfadhili hali ya kuwa alikuwa apaswa kunyimwa. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake. Na nikubalie ombi langu kwa wito wangu kuwa karibu. Uhurumie unyenyekevu wangu, isikilize sauti yangu, usiyakate matumaini yangu, usikate kiungo changu na wewe. Usinielekeze kwa haja yangu hii au nyingine kwa mtu mwingine. Nitilie manani ili kufanikisha ombi langu, na kidhi haja yangu ili kukipata nilichokiomba kabla sijatoka hapa niliposimama, kwa kunirahisishia kwako mimi magumu. Na uzuri wa kunikadiria kwako katika mambo yote. Mrehemu Muhammad na Jamiy yake, rehema ya kudumu na yenye kukuwa, kuendelea kusiko katika. Muda wake uwe hauna mwisho. Fanya hivyo iwe ni msaada kwangu, na iwe ndio sababu ya kufanikiwa ombi langu.Wewe ni mwenye wasaa mkarimu na miongoni mwa haja zangu ewe bwana wangu ni fulani na fulani (hapo utafanya sijda na kuisema haja yaneyewe badala fulani fulani). (Useme haya ukiwa ndani ya sijda):- Fadhila zake zimenipa raha. Ihsani yako imenionyesha njia. Nakuomba kwako na kwa Muhammad na Aliy wake ziwafikie rehma zako usinirudishe kinyume na matumaini yangu.

DUA YA 14

MIONGONI MWA DU'A ZAKE AKIFANYIWA UCHOKOZI NA AONAPO ASIYOYAPENDA TOKA KWA WADHALIMU

Ewe! ambaye hazifichiki kwake habari za waliolemewa. Oh! wee ambaye kuhusu visa vyao ahitajii ushahidi. Oh! wee ambaye msaada wake upo karibu na wadhulumiwa. Ewe! ambaye msaada wake uko mbali na wadhalimu. Unajua ewe Mola wangu alivyoniumbua (fulani bin fulani) uliyomhadharisha na amekiuka kwangu uliyomkataza. Akionyesha hali ya kutokuwa na shukrani kwa neema zako kwake. Akidanganyika na uliyomkataza. Ewe Mola! mrehemu Muhammad na Aliy zake. Mchukue aliyenidhulumu adui yangu kwa nguvu zako. Dugisha makali yake dhidi yangu kwa uwezo wako. Mshughulishe na aliyonayo, na ashindwe kumfikia amfanyiaye uadui ewe Mola! msalie Muhammad na Aliy zake, usimwachie anidhulumu. Nipe msaada mwema dhidi yake, nilinde na mfano wa vitendo vyake, usiniweke katika hali kama yake, ewe Mola! wangu mswalie Muhammad na Aliy zake. Na unisaidie dhidi yake msaada wa papo kwa papo, uwe kitulizo cha ghadhabu yangu kwake na kumaliza makasiriko yangu kumwelekea 'yeye. Ee Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake.Nifidie msamaha wako kwa dhulma yake kwangu. Nibadilishie uovu wa matendo yake kwangu iwe rehma zako kwangu. Kila chukizo kubwa liko chini kuliko ghadhabu zako. Na kila afa si sawa kulinganisha na ghadhabu zako. Ewe! Mola wangu kama ulivyonifanya nichukie kudhulumiwa, basi nilinde nisidhulumu. Ewe Mola sitolalamika kwa yeyote mbali na wewe. Na sitoomba msaada kwa hakimu ambaye si wewe. Vipi nithubutu hivyo! msalie Muhammad na Aliy zake. Iunganishe DU'A yangu na jibu, yakutanishe malalamiko yangu na mabadiliko. Ewe Mola wangu, usinifanyie majaribu ya kukata tamaa na insaafu yako. Wala usimfanyie yeye majaribu ya kujiona yuko salama na makatazo yako, asijeendelea kunidhulumu. Na kunizuia nisipate haki yangu. Mtambulishe haraka ulivyomuahidi mtenda dhulma. Na nijulishe mimi ahadi yako kuwajibu wenye kuzidiwa.

Ewe Mola msalie Muhammad na Aliy zake, unipe taufiki ya kukubali uliyoniamulia kwa faida yangu na kinyume chake, nifanye niridhie uliyochukua kwa ajili yangu na uliyoyacbukuwa kutoka kwangu.Niongoze kwenye lililo sawa, na nitumikishe kwa lililo salama. Ewe Mola ikiwa ni bora kwangu uonavyo ni kuahirisha kuchukua kwa ajili yangu na kuacha kulipiza kisasi kwa aliyenidhulumu mpaka siku ya maamuzi na mkusanyiko wa magonvi! basi msalie Muhammad na Aliy zake.Nipe nguvu kutoka kwako kwa nia ya kweli na subira ya kudumu, nilinde na utashi mbaya na pupa ya wachoyo. Nifanyie picha ya mfano moyoni mwangu wa ulicho nihifadhia miongoni mwa thawabu zako na ulilomwandalia mgomvi wangu miongoni mwa malipo yako na adhabu yako. Fanya hilo iwe ndiyo sababu ya kukinai kwangu uliyohukumu na ithbati kwangu kwa uliyoyachagua. Ameen Oh! bwana wa malimwengu hakika wewe u mwenye fadhila kubwa na wewe u muweza wa kila kitu.

DUA YA 15

NA MIONGONI MWA DU'A ZAKE (A.S.) AKIWA MGONJWA AU AKISUMBULIWA NA JAMBO AU KUPATWA NA BALAA

Oh! Mola wangu sifa njema ni zako kwa vile nipo katika hali ya salama ya kiwiliwili changu. Sifa njema ni zako kwa kuwa ndio sababu ya uele kiwili wili changu. Sijui ewe Mola wangu ni ipi katika hali mbili hizi unastahiki kushukuriwa zaidi? Na upi katika nyakati mbili hizi uliobora kukuhimidi? Je ni wakati wa siha njema ambao umenipendezesha humo riziki zako nzuri, na umenipa uzima humo nitake radhi zako na fadhila zako. Kwayo umenipa nguvu kwa yale uliyonipa taufiki katika utii wako? Au wakati wa uele ambao humo umenichuja. Na neema ambazo umenitunukia? Ili kufanya wepesi yaliyonitopea juu ya mgongo wangu miongoni mwa makosa na kunitakasa maovu niliyozama ndani yake. Na kuniongoza kwenye toba na ukumbusho wa kuondoa matendo yasiyofaa kwa njia ya neema za hapo nyuma. Na kwa yote hayo yale waliyoniandikia malaika wawili waandishi wa matendo yangu mema ambayo moyo haukuweza kuyafikiria wala ulimi haukuweza kutamka wala kiungo cha mwili hakijatenda bali ni ufadhili mtupu toka kwako kwa ajili yangu.

Na hisani miongoni mwa matendo yako ya hisani kwangu. Ewe Mola msalie Muhammad na Aliy zake. Nipendezeshe uliyoyaridhia kwangu. Nifanyie wepesi uliyoniteremshia, nitakase uchafu nilioutanguliza. Nifutie shari niliyoitanguliza. Nionyeshe utamu wa afya njema, nionjeshe hali poa ya usalama. Na jaalia kutoka kwangu kwenye uele iwe kuelekea kwangu kwenye msamaha wako. Na mgeuko wangu toka kwenye kulemewa kwangu uwe ndio mwelekeo wangu kwenye kufumbiwa macho kwako. Epuko langu toka kwenye dhiki yangu liwe kuelekea kwenye burudisho lako. Usalama wangu toka kwenye shida hii uwe kuelekea faraja yako. Hakika wewe ni msifika kwa ihsani mwingi wa ihsani na huruma. Mpaji mkarimu mwenye utukufu na wema.

DUA YA 16

DU'A ZAKE AOMBAPO KUJITOA KWENYE DHAMBI ZAKE AU AKINYENYEKEA KUOMBA MSAMAHA WA DOSARI ZAKE

Oh! wee ambaye kwa rehma zake wanaomba msaada watenda dhambi. Oh! wee ambaye kwa kukumbuka ihsani yake hukimbilia wenye dhiki. Oh! wee ambaye kwa kumwogopa hulia wakosaji. Oh! wee faraja ya kila mpweka mgeni, Oh! we mfariji wa kila mwenye huzuni. Oh! wee msaada wa kila aliyetelekezwa mpweka. Oh! we msaidizi wa kila muhitaji aliyefukuzwa. Wewe ndiye ambaye umeeneza kwa kila kitu rehma na elimu. Na wewe ndiye ambaye umemfanyia kila kiumbe awe na hisa katika neema zako. Nawe ndiye ambaye msamaha wake uko juu zaidi kuliko adhabu zake. Wewe ndiye ambaye zatiririka rehma zake mbele ya ghadhabu zake. Na wewe ndiye ambaye upaji wake zaidi kuliko nyimo lake. Na wewe ndiye ambaye viumbe wote wamefunikwa na rehema zake, wewe ndiye ambaye hapendi malipo toka kwa aliyempa. Wewe ndiye ambaye hazidishi adhabu ya aliyemuasi. Mimi ewe! Mola wangu ni mja wako ambaye uliyemuamuru kukuomba. Akasema: Labeika na niko chini ya utumishi wako. Ni hapa ewe! bwana wangu nimejitupa mbele yako. Mimi ndiye yule ambaye makosa yameuzidi uwezo wa mgongo wake. Mimi ni yule ambaye madhambi yamemaliza umri wake. Na mimi ni yule ambaye kwa ujinga wake amekuasi, hali ukiwa haukustahiki hivyo toka kwake. Je! ewe Mola wangu utamrehemu akuombaye ili nikithirishe DU'A? Au utamsamehe mwenye kukulilia ili nifanye haraka kulia. Au wewe ni mwenye kumfumbia macho mwenye kutia mchanga uso wake kwa ajili yako akijidhalilisha? Au wewe ni mwenye kumtosheleza mwenye kushitakia kwako ufakiri wake akiwa na matumaini! Ewe Mola wangu usimvunje moyo ambaye asiye mpata mpaji mwingine mbali nawewe.

Usimtelekeze asiyeweza kujitosheleza kando yako na mwingine yeyote. Ewe Mola wangu mrehemu Muhammad na Aliy zake. Usinitumpie hali nimekuelekea. Usininyime hali nimekuomba, usinipige kofi la uso kwa kunikatalia hali nimesimama mbele yako. Wewe ndiye uliyejisifu nafsi yako kwa rehema. Basi mswalie Muhammad na Aliy zake nirehemu. Wewe ndiye uliyejiita mwenyewe kuwa umsamehevu, basi nisamehe. Waona ewe Mola wangu mbubujiko wa machozi kwa kukuogopa, yote hayo ni haya nionayo kwa ubaya wa matendo yangu. Kwa ajili hiyo imezima sauti yangu kukulilia. Umebutuka ulimi wangu sinong'oni nisalipo. Ewe Mola wangu yako ni sifa njema aibu ngapi umenisitiri hukunifedhehi dhambi ngapi umezifunika kwa ajili yangu hukunifanya niwe mashuhuri kwazo. Makosa mangapi nimeyatenda wala hukunichania pazia la sitara, wala haukunibandika utepe wa chuki ya fedheha yake, wala haukudhihirisha aibu yake kwa atafutaye aibu zangu miongoni mwa majirani wangu na wenye husda ya neema zako kwangu. Hata hivyo hayakuniziwiya yote hayo nimepita kwenye maovu uliyoyajuwa kwangu. Hivyo basi ni nani mjinga zaidi wa mwongozo wake ewe Mola wangu kuliko mimi?

Nani mwenye kughafilika mno na hadhi yake kuliko mimi? Nani yu mbali sana na kuirekibisha nafsi yake kuliko mimi? Kwa kuwa naitumia riziki yako uliyoniruzuku katika mambo uliyonikataza miongoni mwa maasi yako. Nani aliyezama mbali sana katika mambo ya batili na mwenye kuyaendea maovu kuliko mimi? Nisimamapo kati ya wito wako na wito wa shetani huufuata wito wake bila kuwa niko kipofu katika kumjua wala sifanyi hivyo kwa kuwa kuna usahaulifu katika kumtambua. Hali yakuwa ninayakini kuwa mwisho wa wito wako ni peponi. Na mwisho wa wito wake ni motoni, utakatifu ni wako. Ajabu iliyoje juu ya ushahidi ni ubebao dhidi yangu mwenyewe. Na hesabu toka yaliyojificha katika mambo yangu? Ajabu kubwa kuliko hiyo ni ule upole wako kwangu na kwenda kwa utaratibu bila kuniharakishia. Hiyo si kwamba ninayo heshima kwako; bali ni uvumilivu wako kwangu, na ni fadhila zako juu yangu.Ili nijiepushe na maasi yako ya kukasirishayo, nipate mwanya wa kujing'oa toka maovu yangu yaniaibishayo. Kwa sababu kunisamehe wapendezwa sana kuliko kuniadhibu. Bali mimi ewe! Mola wangu ninadhambi nyingi sana na nyayo mbaya sana na matendo ya ovyo mno. Najitumbukiza vibaya sana katika batili. Niko dhaifu mno kuwa macho katika utii wako.

Ni mchache mno wakuzindukana na makamio yako na kuyachunga. Kwa kiasi cha kuweza kuzidhibiti aibu zangu. Au kuweza kuzikumbuka dhambi zangu kwa hayo nailaumu nafsi yangu tu nikiwa na tamaa ya huruma yako ambayo kwayo ndiyo kurekebika kwa mambo ya wenye dhambi. Na kutaraji rehma zako ambazo kwazo ndiyo ukombozi wa shingo za wakosaji. Oh! Mola hii ni shingo yangu imeshikwa utumwa na dhambi, msalie Muhammad na Aliy zake. Ikomboe kwa msamaha wako. Huu mgongo wangu umetopewa na makosa. Msalie Muhammad na Ali zake, uupunguzie uzito wake kwa huruma yako. Ewe Mola wangu lau ningekulilia mpaka zidondoke mbone za macho yangu na niliye mpaka ikatike sauti yangu. Na nisimame kwa ajili yako mpaka zifure nyayo zangu, na nirukuu kwa ajili yako mpaka ung'oke mgongo wangu, na nisujudu kwa ajili yako mpaka macho yangu yang'oke, na nile mchanga wa ardhini umri wangu wote, na ninywe maji yenye jivu mpaka mwisho wa umri wangu, na niwe na kutaja muda wote huo mpaka ulimi wangu uwe butu nisiinuwe uso wangu vyote hivyo nikikuonea haya isingewajibika kufutiwa ovu moja miongoni mwa maovu yangu. Ingawaje ulikuwa wanisamehe inapobidi nipate msamaha wako, na wanisamehe ninapostahiki msamaha wako. Kwani hilo haliwi wajibu kwa ajili yangu kwa kustahiqi wala silipati hilo kwa kuwa ni wajibu. Kwa kuwa malipo yangu toka kwako toka nilipokuasi kwa mara ya kwanza ilikuwa ni moto. Hivyo basi endapo utaniadhibu wewe sidhwalimu kwangu. Oh! Mola wangu kwa vile ulisitiri aibu yangu wala haukunifedhehi, ulinivumilia kwa ukarimu wako wala haukuniharakia. Ulinifanyia huruma kwa fadhila zako hukuibadilisha neema zako kwangu wala hukuyaboronga matendo yako mema kwangu. Hurumia unyenyekevu wangu wa muda mrefu. Na ukali wa umasikini wangu. Hali yangu mbaya. Ewe Mola msalie Muhammad na Aliy zake. Nilinde na maasi, nifanye niwe mtii, niruzuku kurejea kwako mara kwa mara, nisafishe kwa toba, nipe nguvu kwa kunilinda, nirekebishe kwa afya, nionjeshe utamu wa msamaha, nijaalie niwe niliye kombolewa kwa msamaha wako na niliyekombolewa utumwa kwa rehma zako, niandikie dhamana ya kutokasirikiwa nawe, nipe bishara ya haraka si ya baadaye bishara niitambuayo, itambulishe kwa alama nitaibainisha nayo. Hilo halikupi dhiki katika wasaa wako, wala halikusumbui katika nguvu zako, wala haliuzidi upole wako, wala haikuchokeshi katika hiba zako tukufu ambazo zimeonyeshwa na aya zako. Hakika wewe wafanya ulitakalo na wahukumu upendalo. Hakika wewe nimuweza wa kila kitu.

DUA YA 17

DU'A ZAKE(A.S) AMTAJAPO SHETANI HUJILINDA NAYE NA HUJILINDA NA UADUI WAKE NA VITIMBI VYAKE

Ewe Mola kwa hakika twajilinda kwako na mvuto wa shetani maluuni na vitimbi vyake na mitego yake. Na kuwa na matumaini ya ahadi zake.Udanganyifu wake na mawindo yake na asijipe tamaa nafsini mwake ya kutupoteza mbali na utii wako. Na kutotweza kwa sababu ya kukuasi tusije yaona kuwa ni mazuri aliyotufanya tuyaone mazuri. Na yasije onekana mazito kwetu aliyoyachukiza kwetu. Ewe Mola mtupe mbali nasi kwa njia ya ibada yako. Mtupe chini kwa upendo wetu wa kudumu kwako. Weka kati yetu na yeye kiziwizi asichoweza kukiondoa. Na kinga madhubuti hawezi ikiuka. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake. Mshughulishe awe mbali na sisi kwa baadhi ya maadui wako. Utulinde naye kwa uzuri wa uangalizi wako. Tufanye atusumbuliwi na khiyana yake, tugeuzie mgongo wake. Ukate kabisa ufuatilio wake kwetu. Ewe Mola msalie Muhammad na Ali zake. Tufurahishe kwa kutupa uongofu mfano wa upotovu wake. Tuzidishie uchamungu dhidi ya ushawishi wake. Tupitishe katika uchaji mungu kinyume na njia yake ya maangamio.

Ewe Mola usimjalie upenyo mioyoni mwetu. Usimfanyie makazi kwa yale tuliyonayo. Ewe Mola tutambulishe njia potovu atufanyiazo. Na tuitambuapo tulinde nayo tuonyeshe cha kumrubuni nacho. Tupe ilhamu ili kujiweka tayari naye tuamshe ili tutokane na sinzio la mghafala wa kumtegemea yeye. Ufanye uzuri msaada wako kwetu dhidi yake. Ewe Mola zinyweshe nyoyo zetu kuyakanusha matendo yake. Tufanyie upole kwa kutangua hila zake. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake.Yageuze mamlaka yake mbali nasi, kata matumaini yake kwetu, mziwie uchu wake kwetu, Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake.Wajaalie baba zetu, mama zetu, watoto wetu, ahli zetu, ndugu zetu wa karibu na majirani zetu miongoni mwa waumini wanaume na waumini wanawake katika ulinzi madhubuti dhidi yake. Na ngome yenye hifadhi na pango lenye kizuizi. Wavishe dhidi yake kinga iwalindayo, wape silaha dhidi yake silaha kali kali Ewe Mola waeneze hayo wenye kushuhudia kuwa wewe ndiyo Rabbu. Na akakutengea wewe umoja. Na amfanyiaye uadui (shetani) kwa ajili yako kwa hakika ya uja. Na akuomba msaada dhidi yake kwa maarifa ya elimu za kiungu.

Ewe Mola! fungua aliyoyafunga na rarua aliyoyashona. Haribu aliyoyapanga, mvunje moyo anapoazimia, yaharibu aliyoyafanya. Ewe Mola lishindishe jeshi lake, batilisha vitimbi vyake, bomoa pango lake, isuguwe pua yake chini ya ardhi. Ewe Mola! tuweke sisi katika ngazi ya maadui zake tutoe tusiwe katika idadi ya marafiki zake ili tusimtii anapotushawishi. Tusimwitikie atuitapo, tumpe amri mwenye kutii amri yetu amfanyie uadui, na tumuwaidhi ili asimfuate mwenye kufuata karipio letu. Ewe Mola! mrehemu Muhammad mwisho wa manabiy na bwana wa mitume na warehemu ahli bayt wake wema na wasafi. Na utulinde sisi na ahali zetu, ndugu zetu na jumla ya waumini wanaume na waumini wanawake, yale tuliyojilinda nayo. Na ututakase kwa yale tuliyokuomba ututakase nayo kwa hofu yake. Tusikilize tuliyokuomba na utupe tuliyoghafilika kuyaomba, ulinde na tuliyoyasahau. Kwa yote hayo tufanye tuwe katika daraja za watu wema na ngazi za waumini - Aameen ewe Mola wa ulimwengu wote.

DUA YA 18

LINDWA NA JAMBO ANALOLIHOFIA AU KUHARAKISHIWA AYATAKAYO

Oh! Mola sifa njema ni zako kwa uzuri wa utekelezaji wako. Kwa kuniondolea mitihani yako, usiijaalie hadhi yangu katika rehma zako ile ulioniharakishia katika afya yako nisije kuwa duni kwa niliyo nikiyapenda. Na mwingine awe na maisha mema kwa yale niliyoyachukia. Ikiwa hali njema niliyo nayo mchana wote au usiku wote kwa afya hii itafuatiwa na balaa isiyokoma na mzigo wa dhambi ambao usiotoweka.! Bora nitangulizie ambacho ungekichelewesha na nicheleweshee ambacho ungenitangulizia. Kwa kuwa ambacho mwisho wake ni kuteketea hakina wingi. Na ambacho matokeo yake ni kubakia hakina udogo. Msalie Muhammad na Aliy zake.

DUA YA 19

DU'A ZAKE(A.S) KUOMBA MAJI WAKATI WA UKAME

Oh! Mola tupe maji kwa kutuletea mvua. Tukunjulie rehma zako kwa mvua yako nyingi kutoka mawingu yasukumwayo kwenye mimea ya ardhi yako muwafaka kwa kuotesha katika zoni zote. Wahurumie waja wako kwa kuivisha matunda. Irudishie uhai nchi yako kwa kutungika maua. Wafanye malaika wako waheshimiwa waandishi kuwa mashahidi kwa mvua yenye manufaa toka kwako. Wingi wake uwe wa daima, mbubujiko wake uwe wa wasaa, mvua nyingi ya haraka, kwayo uirudishie uhai iliyonyauka, ukilete kwayo kinachokuja, kwayo ulete chakula nyingi, mawingu yenye kurundikana yenye kutosheleza, katika tabaka za mawingu yatoayo sauti mvua inyeshayo sio ile isiyo simama kuwe na umulikaji wenye matunda. Oh! Mola tupe mvua, yenye kusaidia, iletayo mazao yenye rutuba, yenye kuenea, nyingi, yakutosha inayotengeneza upya kilichovunjika. Oh! Mola tupe mvua, itakayofanya mawe ya mlimani yaporomoke itakayojaza visima, itakayoifanya mito itiririke, itakayootesha miti, itakayofanya bei za vitu irudi chini katika nchi zote, itakayo tia uzima wanyama na viumbe vingine, itakayotukamilishia chakula yakufaa, itakayotuoteshea mimea, itakayoongeza mtiririko wa maziwa katika chuchu za wanyama, itakayo tuongezea nguvu kwenye nguvu zetu. Ewe Mola usijaalie kivuli chake juu yetu kuwa upepo uunguzao, wala usiifanye baridi yake kwetu ya kukata, usiufanye mbubujiko wake kwetu kuwa ni pigo la mawe, wala usiyafanye maji yake kwetu kuwa ya chumvi. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake. Turuzuku miongoni mwa baraka za mbingu na ardhi. Hakika wewe u muweza wa kila kitu.


3

4

5

6

7

8