AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU 25%

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU Mwandishi:
: Sheikh Haruna Pingili
Kundi: Imam Ali bin Husein (A.S)

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU
  • Anza
  • Iliyopita
  • 16 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 20815 / Pakua: 5111
Kiwango Kiwango Kiwango
AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

Mwandishi:
Swahili

6

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

DUA YA 31

DU'A ZAKE (A.S) KATIKA KUIELEZEA TOBA NA KUIOMBA

Oh Allah! Oh yule ambaye hazi sifa za wenye kumsifu kumsifia. Oh we ambaye hayamvuki matarajio ya watarajiao. Oh we ambaye kwake hayapotei malipo ya watenda mema. Oh we ambaye yeye ndiye mwisho wa hofu ya wachapa ibada. Oh we ambaye ni upeo wa woga wa wachamungu. Hiki ni kituo cha aliyepitiwa na madhambi mkono kwa mkono. Hatamu za makosa zimemwongoza na shetani amemtawala. Amezembea kutekeleza uliyomwamrisha kwa kupuuza. Na akajipa uliyomkataza ajiepushe nayo katika hali ya kudanganyika akiwa kama asiyejua uwezo wako juu yake, au akiwa kama mfano wa akanushaye ubora wa ihisani yako kwake! Mpaka jicho la uongofu litakapo mfungukia. Viwingu vya upofu vitakapomtanduka atahesabu vile ambavyo ameidhulumu nafsi yake. Na atatafakari katika yale amemkhalifu bwana wake. Hivyo ataona ukubwa wa maasi yake kuwa ni mkubwa na uzito wa kumkhalifu kwake kuwa ni mzito. Kwa hiyo ataelekea upande wako akikutumainia, akikuonea haya. ataelekeza maombi yake kwa kukuamini atakuwa amejitengeneza upya kwako kwa tamaa zake akiwa na yakini. Amekukusudia moja kwa moja kwa hofu na unyofu, tamaa zake zimeepukana na yote ya kufanyiwa tamaa bali ni wewe tu.

Kwa hiyo amesimama mbele yako akijitetea ameyaelekeza macho yake chini mnyenyekevu, ameinamisha kichwa chake kwa ajili ya utukufu wako mwenye kujidhalilisha. Akudhihirishia siri zake ambazo wewe wazijua vizuri mno kuliko yeye hali ya unyenyekevu. Atakuwa amezihesabu dhambi zake kwa unyenyekevu hali wewe wazijua vizuri mno idadi yake. Atakuomba sana msaada kwa lakutisha ambalo ameangukia humo katika elimu yako Na kwa ajili ya baya lililomfedhehesha katika hukumu yako miongoni mwa dhambi ambazo starehe zake zimetumba mgongo na kutokomea ambazo matokeo ya ubaya wake yamethibiti na kulazimu. Hato kanusha Oh! Mola wangu uadilifu wako endapo utamwadhibu wala hatouzingatia msamaha wako kuwa ni jambo kubwa endapo utamsamehe na kumuhurumia kwa sababu wewe ni bwana mkarimu ambaye hadogeshwi na msamaha wa dhambi kubwa. Oh Allah ! mimi ni huyoo! Nimekujia hali nikiwa mtii wa amri yako kwa kuwa umeamuru kuomba DU'A kwa hiyo nakuomba kutekeleza ahadi yako kwa uliyoahidi kujibu kwa vile wasema: (niombeni nitakujibuni). Oh Allah! mrehemu Muhammad na Aliy zake, kutana na mimi kwa msamaha wako kama nilivyokutana na wewe kwa kukiri kwangu. Niinuwe kutokana na mweleka wa dhambi kama nilivyojitupa chini kwako, nisitiri kwa sitara yako kama vile ulivyoacha kunifanyia haraka malipizi. Oh Allah! Iimarishe nia yangu katika utii wako upe nguvu ufahamu wangu katika ibada yako, nipe tawfiki katika matendo mema ambayo yataniosha uchafu wa makosa. Nifishe nikiwa katika mila yako na mila ya Nabiy wako Muhammad amani imfikie Oh Allah!, Hakika mimi natubu kwako katika kikao changu hiki kuwa nitaacha madhambi yangu makubwa na madogo.

Maovu yangu ya ndani na nje kupotoka kwangu kulikotangulia na kwa hivi sasa toba ya mtu asiyeweza fanya maasi wala hana dhamira ya kurejea kwenye makosa. Na kwa hakika umekwisha sema ewee Mola wangu katika kitabu chako thabiti kuwa hakika wewe waikubali toba ya waja wako na wasamehe maovu. Na unawapenda wanaotubu basi ikubali toba yangu kama ulivyoahidi na nisamehe maovu yangu kama ulivyochukua dhamana. Na niwajibishie mapenzi yako kama ulivyoweka sharti, sharti yangu kwako Oh bwana wangu sitorudi kwenye machukio yako na dhamana yangu nitoayo ni kuwa sitorudi kwenye yalaumiwayo na wewe. Na ahadi yangu ni kwamba nitayahama maasi yako yote. Oh Allah! hakika wewe wajua zaidi niliyoyatenda. Basi nighofirie uliyoyajua niepushe kwa uwezo wako na nielekeze kwenye ambayo wayapenda. Oh Allah ! na dhidi yangu kuna haki daiwa nimezihifadhi, na haki daiwa nimezisahau zote hizo zi jichoni mwako ambalo halilali. Na elimu yako ambayo haisahau wafidie wenye haki na nipunguzie mzigo wake, nifanyie wepesi uzito wake, nilinde nisiikurubie iliyo mfano wake. Oh Allah! kwa hakika sina uwezo wa kutekeleza toba yangu isipokuwa kwa kulindwa na wewe wala kujiziwiya na makosa isipokuwa kwa uwezo wako nipe uwezo wa kutosha. Nipe ulinzi wako wenye kuzuiya. Oh Allah! mja yeyote ametubu kwako naye katika elimu yako ya ghaibu ataitanguwa toba yake, na atarejea katika dhambi zake na makosa yake. Kwa hakika mimi najilinda kwako nisiwe kama vile, ifanye toba yangu hii toba sihitajii baada yake toba yeyote. Iwe toba iwajibishayo kufuta yaliyotangulia, na ya salama kwa yaliyobaki. Ewe Mola! Hakika mimi nakuomba msamaha kwa sababu ya ujinga wangu. Nakuomba usitilie manani vitendo vyangu viovu, niunganishe kwenye kivuli cha rehma yako kwa ihsani, nisitiri kwa sitara ya afya yako kwa fadhila zako. Oh Allahl kwa hakika mimi ninatubu kwako kutokana na kila kilichokwenda.

Kinyume na utashi wako au kimekuwa mbali na mapenzi yako kutoka mawazo ya moyoni mwangu, mtizamo wa macho yangu na hekaya za ulimi wangu.Toba ambayo kila kiungo cha mwili wangu kitabaki salama bila malipizi yako na kitakuwa na amani bila ya woga wa yale wayaogopayo wakiukaji miongoni mwa machungu ya adhabu zako. Oh Allah! Uhurumie upweke wangu mbele yako, na kupondekana kwa moyo wangu kutokana na kukuogopa wewe. Nakutetemea kwa viungo vya mwili wangu kwa ajili ya haiba yako. Ewe Bwana wangu! Dhambi zangu zimeniweka weko la kudharauliwa uwanjani pako. Nikinyamaza hakuna atakayenisemea na nikiomba Shafaa sikuwa miongoni mwa wenye haki ya kupata Shafaa. Oh Allah! Mrehemu Muhammad na Aali Zake Ufanye ukarimu wako kwa mwombezi wa makosa yangu. Yarejelee maouvu yangu kwa msamaha wako. Usinilipe malipo ninayostahiki katika adhabu zako. Ni kunjuliye juu yangu ihisani zako ni viringishe sitara yako. Nitendee kitendo cha mtu mwenye enzi wakati mtumwa dhalili amnyenyekeapo na akamuhurumia. Au tendo la mtu tajiri fakiri anapomnyenyekea naye akamtajirisha. Oh Allah! Sina wakunilinda dhidi yako hivyo basi naomba Enzi yako inilinde. Sina mwombezi kwako hivyo basi fadhila zako ziwe ndiyo mwombezi wangu. Makosa yangu yamenitia hofu wacha msamaha wako unipe amani. Siyo yote niliyotamka kwa ujinga wangu kwa sababu ya ufuatiliaji wangu mbaya wala sikusahau yaliyopita miongoni mwa matendo yangu yastahiliyo kulaumiwa.

Lakini ili mbingu zako zisikie na waliomo humo na ardhi yako na waliomo juu yake niliyokudhihirishia miongoni mwa majuto. Na nimekimbilia kwako kutubu. Huwenda baadhi yao kwa Rehema Zako watanirehemu kwa sababu ya ubaya wa kikao changu. Au mtu ashikwe na huruma juu yangu kwa sababu ya ubaya wa hali yangu. Huenda nikapata kutoka kwake DU'A ambayo sikilizwa mno kwako kuliko Duwa yangu. Au ombezi lenye nguvu mno kwako kuliko ombezi langu. Humo utakuwa uwokovu wangu epukana na ghadhabu zako. Na kufuzu kwangu kwa ridhaa zako

Oh Allah! Ikiwa kujuta ni toba ya kukubaliwa kwako, basi mimi ni mjutaji mno wa wajutaji wote. Na ikiwa kuacha kukuasi ndio kurejea kwako, basi mimi ni mrejea wa kwanza kwako kuliko warejeao wote. Na ikiwa kuomba ghofira ni sababu ya kupunguziwa dhambi, basi mimi ni miongoni mwa wakuombao ghofira. Oh Allah! Kama ulivyoamrisha toba na ukachukuwa dhamana msalie Muhammad na Aali zake ikubali toba yangu. Wala usinirudishe Rudisho la kutofanikiwa Rehma zako. Hakika wewe ni mwingi wa kupokea toba ya watenda dhambi. Na mwenye Rehma sana kwa wakosaji wanaorejea kwako. Oh Allah! Mrehemu Muhammad na Aali Zake. Na kama vile umetuongoza kwa sababu yake mrehemu Muhammad na Aali zake. Kama ulivyotuokowa kwa sababu yake mrehemu Muhammad na Aali Zake Rehema itakayotuombea siku ya Kiyama na siku ya kukuhitajia. Hakika wewe ni muweza wa kila kutu na ni rahisi kwako.

DUA YA 32

DU'A ZAKE BAADA YA KUMALIZA SALA ZA USIKU

Oh Allah! mmiliki wa ufalme wa kudumu wa melele. Utawala usioshindika bila ya askari wala wasaidizi. Na enzi ya kubaki miaka nenda miaka rudi zama nenda zama rudi siku nenda siku rudi. Yana Enzi mamlaka yako Enzi isiyo na mpaka wa mwanzo wala mwisho. Ufalme wako umekuwa wa juu zaidi vimeporomoka vitu bila ya kuufikia muhula wake. Sifa zenye uwezo wambali za wenye kusifu hazitoweza kukufikia kile kidogo mno ulichojitengea kwa ajili yako. Kwako sifa zimepotoka. Zimeshindwa kukufikia sifa. Mawazo yame DU'A mbele ya utukufu wako. Kwa ajili hiyo wewe ni wa Daima hutoweki. Nami ni Mja dhaifu wa matendo mwenye matumaini makubwa kabisa. Sababu za kuwasiliana zimeponyoka toka mikononi mwangu isipokuwa zilizo wasilishwa na Rehma zako. Hamana za matumaini zimenikatika isipokuwa ni ishikiliayo katika msamaha wako. Kimekuwa kidogo mno niwezacho kukihesabu katika utii wangu kwako. Yamekithiri dhidi yangu maasi yangu kwako haitokuwia dhiki kumsamehe mja wako japo afanye maovu basi nisamehe Oh Allah!

Elimu yako ya chunga kazi zilizojificha kila kilicho sitirika kimefichuka mbele ya utambuzi wako. Hayafichiki kwako mambo madogo sana na viroja vya siri kabisa havifichiki kwako. Adui yako amenishinda nguvu adui ambaye alikuomba umbakishe ili anipotoshe na ulimbakisha. Alikuomba umpe muhla wa kubakia mpaka siku ya hukumu ili anipoteze ulimpa muhula. Hivyo basi amenitupa chini ingawaje nimekimbilia kwako kutokana na madhambi madogo madogo angamizi na amali kubwa ziuwazo mpaka nilipotenda maasi yako na kwa ubaya wa juhudi yangu nimewajibika chuki yako. Amegeuza toka kwangu ugwe ya udanganyifu wake. Akakutana na mimi kwa neno lake la kufuru. Akajitenga na mimi. Akatumba mgongo anikimbia. Kwa hiyo akanitupa kwenye jangwa la ghadhabu zako peke yangu. Amenitoa nje na kuniweka kwenye uwanja wa malipizi ya kisasi chako nikiwa mwenye kufukuzwa. Hakuna mwombezi atakayeniombea kwako wala mlinzi atakayenifanya niwe na amani kwako. Wala hakuna ngome itakayonificha wewe usinione. Wala hapana kimbilio niwezalo kukimbilia kukukimbia wewe. Hivyo hiki ni kikao cha ajilindae na wewe nani mahali pa mtu akutambuaye. Basi fadhila zako zisinijie finyu, wala usikose kunifika msamaha wako wala nisiwe miongoni mwa waja wako wasio fanikiwa mno katika waja wako waliotubu. Wala nisiwe miongoni mwa wakata tamaa miongoni mwa wajao kwako wakiwa na matumaini. Nisamehe hakika wewe mghofiri bora miongoni mwa wenye kughofiri. Oh Allah! Hakika umeniamrisha nikaacha. Umenikataza nikafanya. Mawazo mabaya yamenifanyia majaribu kufanya mabaya nikazembea. Wala siwezi kutolea ushahidi funga yangu mchana. Wala siwezi kuomba kimbilio kwa ajili ya sala yangu ya Tahajudi usiku wala Sunnah hainipi sifa kwa kuihuisha.

Isipokuwa faradhi zako ambazo atakayezembea atahiliki siwezi kutaka wasila kwako kwa fadhila za sala za naafila hali yakuwa mengi nimeghafilika kuyatenda miongoni mwa nyadhifa za faradhi zako na nimevuka mipaka yako. Na kukiuka sehemu takatifu. Madhambi makubwa nimeyatenda ingawa afya yako ilikuwa kwangu ndio sitara kwa kuepukana na fedheha yake. Haya ni makazi ya mwenye kujionea haya binafsi mbele yako, na ameikasirikia nafsi yake, na ameridhika na wewe. Kwa hiyo akutana na wewe kwa moyo mnyenyekevu. Shingo iliyoinama chini. Mgongo mzito kwa makosa. Amesimama akibabaika kati ya kukupenda na kukuogopa. Na wewe ni bora wa aliowatumainia. Na umwenye haki mno kati ya alio waogopa na kuwa hofu. Basi nipe ewe Bwana wangu niliokutumainia. Nipe Nipe amani kwa niliyojihadhari nayo nihurumie kwa huruma za Rehema yako hakika wewe u mkarimu mno miongoni mwa wenye kuombwa. Oh Allah! kwa vile umenisitiri kwa afya yako. Na umenikinga kwa fadhila zako katika makazi yenye mwisho mbele ya marika nipe kimbilio la kujiepusha na fedheha za makazi ya kubaki milele waliko simama mashahidi. Miongoni mwa malaika walioletwa karibu na mitume waheshimiwa na watu waliokufa mashahidi na watu wema. Miongoni mwa jirani nilikuwa na mficha maovu yangu. Na ndugu watumbo moja nilikuwa namwonea haya siri zangu. Sikuwa na waamini kunisitiri Oh Rabi! Nimekuamini wewe Oh! Mola wangu, katika kunighofiria. Na wewe ni bora mno wa kuaminiwa. Na u mtowaji mno kuliko wote waombwao u mwema mno kuliko wote wanaoombwa Rehema, hivyo ni Rehemu. Ewe Mola wewe ndiwe uliye nifanya nitoke kwenye asili ya maji duni. Kutoka kiuno chenye mifupa miembamba na mapito ya shida.

Mpaka kwenye tumbo jembamba uliloli sitiri kwa mifuniko. Wani hamisha toka hali moja kwenda hali nyingine. Mpaka ulinimalizia kwenye umbo lililo kamilika. Ukaniweka viungo vya mwili, kama ulivyoaridhia katika kitabu chako (tone la Manii) kisha pande la Damu, kisha nyama, kisha mifupa, kisha uliivisha mifupa na nyama, kisha ulinifanya umbo jingine) kama ulivyopenda mpaka nilipohitaji riziki yako siku jitosha bila ya msaada wa fadhila zako. Ulinifanyia chakula chenye lishe kutoka fadhila ya chakula na kinywaji ulichomtunukia kijakazi wako ambaye tumbo lake ulifanya kuwa makazi yangu. Uliniweka chini ya tumbo lake la uzazi. Ewe Mola wangu! Lau ungeniwakilisha katika hali zile kwenye uwezo wangu au ungenifanya ni lazimike kutumia nguvu zangu. Uwezo ungekuwa haupo kwangu. Na nguvu zingekuwa mbali na mimi. Ulinipa lishe kwa fadhila zako lishe ya mtu mwema mwenye huruma. Wanitendea hayo kwa wema tu juu yangu mpaka kwenye mwisho wangu huu. Siyakosi mema yako. Mema yako haya niachi ningojee, pamoja na yote hayo 'ithibati' yangu haijaimarika. Kiasi cha kuwa niwe nina nafasi kwa ajili ya lile ambalo lina hadhi sana kwangu mbele yako.

Shetani ameshika barabara hatamu yangu kupitia dhana yangu mbaya. Na udhaifu wa yakini. Kwa hiyo mimi na nung'unika ubaya wa ujirani wake na mimi, na nafsi yangu kumtii yeye! Nakuomba hifadhi niepukane na utawala wake. Ninanyenyekea kwako ili niondolewe vitimbi vyake dhidi yangu. Sifa njema ni zako kwa sababu ya kuanza kwako Neema kubwa na kwa sababu ya Il-Hamu yako iwezeshayo kutambuwa ihsani na neema. Msaliye Muhammad na Aali Zake na unirahisishiye riziki yangu na unifanye niwe natosheka na makadirio yako kwangu. Unifanye ni ridhike na hisa yangu katika ulichonigawiya. Na ujaaliye kilicho toweka toka mwili wangu na umri wangu kiwe ni kwa ajili ya njia ya utii wako. Hakika wewe ni mbora wa watowao riziki.

Oh Allah! Hakika mimi najilinda nawe ili kuepukana na moto ulioutia makali dhidi ya watakaokuasi. Moto ambao umemuonya mwenye kugeuka mbali na ridhaa zako na moto ambao mwanga wake ni giza. Ambao nafuu yake ni machungu na umbali wake ni karibu. Kutokana na moto ambao baadhi yake yaila baadhi nyingine. Moto ambao waiacha mifupa imekwisha teketeza. Unawanywesha watu wake maji yachemkayo. Moto ambao haumwachii mwenye kukiri kwake. Hautomhurumia mwenye kuomba Rehema. Hauwezi kujipunguza makali kwa mwenye kuunyenyekea na kusalimu amri kwake. wapambana na wakazi wake kwa joto ililo nalo kwa mateso yaumizayo na ghadhabu kali mno. Najilinda kwako na nge wake walio midomo wazi. Na nyoka wake wenye meno yagege DU'A yo. Na kinywaji chake kinacho kata utumbo na nyoyo za wakazi wake na kuutowa ubongo wao. Nakuomba mwongozo kutoka kwako wa kile ambacho kitaweka mbali na huwo moto na kuufanya urudi nyuma. Oh Allah!

Mrehemu Muhammad na Aali Zake nipe kimbilio ili niepukane nao kwa fadhila za Rehema Zako. Nisamehe kujikwaa kwangu kwa uzuri wa msamaha wako. Wala usinitupe Ewe Mbora wa kutowa kimbilio. Oh Allah! Hakika wewe wahifadhi lichukizalo, Na watowa lililo zuri. Watenda upendalo, na U-muweza juu ya kila kitu. Oh Allah! mrehemu Muhammad na Aali Zake watajwapo watu wema. Na mrehemu Mhammad na Aali Zake kwa kadiri ya usiku na mchana unavyopishana kwa heri. Rehema ambazo ongezo lake halikatiki idadi yake haihesabiki. Rehema itakayojaza anga, na itajaaza ardhi na mbingu. O Allah! Mrehemu yeye mpaka aridhike O Allah! Mrehemu yeye na Aali Zake baada ya kuridhika. Rehema zisizo na mpaka wala mwisho OWEE Mwingi wa Kurehemu miongoni mwa wanaorehemu.

Dua ya 33

MIONGONI MWA DUWA ZAKE KATIKA ISTIKHARA

Oh Allah! Hakika mimi nakuomba ambalo ni zuri zaidi katika ujuzi wako. Msaliye Muhammad na Aali Zake na tuamuliye lililo zuri zaidi. Na tupe Il-Hamu ya maarifa ya kuchagua. Na ifanye iwe ni sababu ya kuridhiya uliyo yapitisha kwa ajili yetu na kusalimu amri kwa uliyotuhukumia tuondolee mashaka ya kusita sita tu imarishe kwa yakini ya watu wanyofu. Usitupatilize kwa kushindwa kutambua uliyo yachagua tusije tukadharau kadirio lako. Na tusije chukia mahali pa ridhaa zako na kuelemea kwenye ambalo li mbali na mwisho mwema na li karibu sana na kinyume cha afya njema.Tupendezeshe tukichukiacho katika Agizo lako. Na tusahilishiye tuonacho kuwa kigumu katika hukumu yako. Tufunulie kuwa wasikivu kwa uliletalo kwetu katika utashi wako mpaka iwe hatupendi kuchelewesha uliloliharakisha wala kuharakisha uliyolichelewesha. Wala tusichukie ulichopenda wala kuchaguwa ulichokichukia na tuhitimishiye kile chenye mwisho wenye sifa njema mno na matokeo yenye heshima zaidi hakika wewe unafisha chenye heshima na watowa kingi, watenda utakalo nawe u muweza wa kila kitu.

Dua ya 34

DU'A ZAKE AKIPATWA NA BALAA AU AMWONAPO MWENYE KUPATWA NA FEDHEHA, KWA AJILI YA DHAMBI

Oh Allah! Himidi ni yako kwa sababu ya kusitiri kwako baada ya kujuwa kwako. Na msamaha wako baada ya kuelewa kwako. Kila mmoja kati yetu amefanya aibu lakini hukumtangaza na amefanya tendo la utovu wa adabu na wala haukumfedhehesha. Na Alijisitiri kwa maovu wala haukumuonesha. Ni makatazo yako mangapi tumeyatenda! Amri yako umetuagiza na tumeikiuka; matendo maovu tumeyatenda. Makosa tumeyatenda. Ulikuwa ukiyaona na watazamaji wengine hawaoni.

Na muweza wa kuyatangaza kuliko wawezao wote. Uislama uliotupa ni pazia mbali na macho yao. Na kiziwizi dhidi ya masikio yao. Ifanye aibu uliyotufichiya na mambo ya ndani uliyoyaficha yawe onyo kwetu. Na kemeo dhidi ya matendo mabaya na kutenda makosa. Na viwe kichocheo cha juhudi ya kufanya toba ifuatayo na njia yenye kuhimidiwa na usogeze wakati wa toba. Usitupatilize kwa kukusahau kwa hakika sisi twakuomba. Na twatubu kwa kuacha dhambii. Oh Allah! Na mrehemu mteule wako katika viumbe wako Muhammad na kizazi chake, wateule miongoni mwa viumbe wako wa Taharifu. Na tujaaliye sisi kuwa wasikivu na watii kwao kama ulivyoamrisha.

DUA YA 35

MIONGONI MWA DU'A ZAKE(A.S) KATIKA RIDHAA AWAANGALIAPO WANA WA DUNIA HII

Sifa njema ni za Allah kwa kuridhika na hukumu ya Allah Nimeshuhudia kuwa Mungu amegawa maisha ya waja wake kwa uadilifu. Amechukuwa jukumu la fadhili viumbe wake wote. Ewe Allah! Mrehem Muhammad na Aali zake. Usinifanyie kishawishi kwa uliyowapa viumbe wako. Wala usiwafanyiye kishawishi kwa uliyoninyima, ili nisije mwonea husuda kiumbe wako na kuyadharau maamuzi yako. Oh Allah! Mrehemu Muhammad na Aali Zake. Ipendezeshe nafsi yangu maamuzi yako. Kipanuwe kifuwa changu katika maeneo ya maamuzi yako. Nipe imani ili nikirikwa imani hiyo ya kuwa maamuzi yako hayafanyiki ila kwa kheri. Na ifanye shukurani yangu kwako juu ya ulichokiondoa kwangu iwe kubwa zaidi kuliko shukrani yangu kwako juu ya ulichonipa.

Unilinde nisije dhaniya kuwa kutokuwa na kitu kwa mtu ni kudunishwa au ni mdhaniye mwenye utajiri kuwa mwenye ubora (kwa Mungu). Kwa kuwa mbora ni yule aliye boreshwa na utii wako. Na mwenye enzi ni yule aliye enziwa na Ibada zako. Mswalie Muhammad na Aliy zake tupe starehe kwa mali isiyokwisha. Tupe nguvu kwa Enzi isiyotoweka. Tupe nafasi katika ufalme wa milele. Hakika wewe ni Mmoja peke yako kimbilio la milele. Haukuzaa wala haukuzaliwa, wala hakuna anayelingana na wewe.

DUA YA 36

DU'A ZAKE AANGALIAPO MAWINGU NA UMULIKAJI NA ASIKIAPO SAUTI YA RADI

Oh Allah! hakika hizi ni alama zako mbili na hawa ni wasaidizi wako wawili wa harakiao utii wako imma kwa Rehema yenye manufaa au kisasi kiumizacho. Usituteremshie kutoka kwa wawili hao mvua mbaya. Usituvishe toka kwa wawili hao vazi la balaa. Oh Allah! Mrehemu Muhammad na Aali zake. Na ututeremshie manufaa ya mawingu haya na baraka zake. Na utuondolee adha yake na madhara yake. Usitufikishie maafa kutokana nao usitutumie uharibifu wowote katika maisha yetu. Oh Allah! Ikiwa umewapeleka hao kwa kisasi na umewatuma kwa makasiriko basi twakuomba kimbilio ili kuepukana na ghadhabu zako.

Tunakusihi utupe msamaha wako elemea kwa washirikina kwa ghadhabu. Tupa jiwe la ghadhabu zako kwa makafiri. Oh Allah! Ondoa ukame wa nchi yetu kwa maji yako. Ondoa ukorofi wa vifua vyetu kwa riziki yako. Usituzuie kwako kwa kutushughulisha na kingine mbali na wewe. Usitukatie sote sisi vitu vya wema wako, kwa kuwa tajiri ni yule uliyemtajirisha aliyesalimika ni yule uliyemlinda. Hakuna yeyote mwenye ulinzi bila ya wewe. Hapana yeyote awezaye kuzuia adhabu yako. Waamua utakalo kwa umtakaye. Wapitisha utakalo kwa umtakaye. Sifa njema ni zako kutulinda na balaa. shukrani ni zako kwa kutupa neema. Sifa njema zitakazo ziwacha nyuma sifa njema za wenye kusifu kwa sifa njema. Sifa njema zitakazojaa ardhi yake na mbingu yake. Hakika wewe mwenye huruma nyingi mpaji wa neema nyingi. Mpokeaji wa sifa kidogo mwenye kushukuru ihisani ndogo matenda mema mtenda mzuri mfadhili. Hapana muabudiwa ila wewe. Na kwako ndio Marejeo.

7

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

DUA YA 37

DU'A ZAKE(A.S) ANAPOTAMBUWA KUSHINDWA KUTEKELEZA SHUKRANI IPASAVYO

Oh Allah! Hakika hakuna awezaye kufikia upeo wa kukushukuru isipokuwa atakuwa amepata hisani yako ambayo pia itamlazimu akushukuru. Wala hafikii kiwango cha kutosha katika kukutii japo afanye juhudi atakuwa chini ya haki yako kwa sababu ya uwingi wa fadhila zako. Kwa hiyo, mwenye shukrani zaidi miongoni mwa waja wako ashindwa kukushukuru ipasavyo. Na mcha mungu mno miongoni mwao yuko chini ya kiwango cha kukutii. Si wajibu kwa yeyote umsamehe kwa kuwa yu astahiki kusamehewa. Wala hana haki ya kuwa umridhiye kwa kustahiki umghofiriyae ni kwa sababu ya huruma zako. Na umridhiaye ni kwa sababu ya ukarimu wako. Waridhika na shukrani ndogo ulioshukuriwa. Walipa kiasi kikubwa kwa kadiri ndogo uliyotiiwa. Hata yaonekana kana kwamba. Shukurani ya waja wako ambayo umewajibisha malipo yao kwa ajili yake. Na umekithirisha malipo yao kwa sababu yake ni jambo wanamiliki uwezo wa kujizuia bila ya wewe na utawalipa na wala haikuwa sababu yake mkononi mwako ndio ukawalipa! Ukweli ni kuwa umemiliki Ewe Mola wangu! Mambo yao kabla ya waja wako hawajamiliki ibada yako. Uliandaa malipo mema kwa ajili yao kabla hawajaanza kukutii wewe. Hiyo ni kwa sababu sunnah yako ni kufadhili. Na tabia yako ni kufanya ihsani na njia yako ni kusamehe. Kwani kila kiumbe cha tambuwa kuwa wewe si dhalimu kwa uliyemwadhibu. Na chashuhudia kuwa unafanya ukarimu kwa uliyemsamehe, kila mmoja anakiri nafsini mwake kuwa hafanyi uliyowajibisha juu yake ipasavyo.

Lau si kama shetani kuwahadaa na kuwaweka mbali na utii wako asingekuasi mwenye kukuasi lau asingewaonesha batili katika mfano wa haki asingepotea njia yako mpoteaji. Hivyo basi utukufu ni wako ubainifu ulioje wa ukarimu wako katika kumtendea anayekutii au anayekuasi. Wamridhia mtii hali yakuwa wewe ndiye uliyesimama kwa ajili yake. Ulimpa muda mfanya maasi hali yakuwa ulikuwa na uwezo wa kumuharakishia adhabu yake. Kila mmoja wao umempa asilopaswa kupewa. Umempa fadhila kila mmoja wao isio lingana na kazi yake. Lau ungemlipa mtii kulingana na kiwango cha utii wake. Angekaribia kukosa malipo yao mema. Na imtoke neema yako. Lakini kwa ukarimu wako umemlipa muda mfupi uishao kwa muda mrefu wakudumu. Na badali ya upeo wa karibu wakutoweka. Kwa upeo mrefu wakubaki milele kisha hukumfanyia kisasi kwa ajili ya aliyokula miongoni mwa riziki yako inayompa nguvu ya kukutii. Wala haukumdadisi kuhusu viungo vya mwili ambavyo matumizi yake imekuwa ndio sababu ya kuufikia msamaha wako. Ungemfanyia hivyo yangekwenda yote aliyotaabikia na yote aliyoyafanyia juhuudi. Ikiwa ni malipo ya kidogo mno miongoni mwa nufaisho lako na huruma yako. Na angebakia rehani mkononi mwako kuhusiana na neema zako zingine. Basi vipi atakuwa anastahiki kupata chochote katika thawabu zako hakika ni vipi? Hii ewe Mola wangu ndio hali ya aliyekutii na aliyefanya ibada kwa ajili yako. Vipi hali ya mwenye kuasi amri yako na kutenda katazo lako!

Wala haukumuharakishia adhabu yako ili aibadilishe hali yake katika kukuasi wewe na hali ya kurejea kwenye utii wako. Alikuwa anastahiki O Mola wangu! Pale mwanzo alipokuasi kila ulilowaandalia viumbe wako wote miongoni mwa adhabu zako. Kwa hiyo yote uliyoyachelewesha miongoni mwa adhabu na umemcheleweshea kumtia adabu. Ni kuiacha haki yako na kuridhia bila ya wajibu wako. Basi E Mola wangu! Ni nani mkarimu zaidi kuliko wewe? Nani mwenye hali mbaya zaidi kuliko aliyeangamia kwa kutokukujali wewe! Hapana ni Nani? U mwenye baraka mno haiwezekani usifike isipokuwa kwa ihsani, umkarimu mno haiwezekani uogopwe isipokuwa uadilifu. Huogopwi kuwa utamdhulumu aliye kuasi. Wala haiogopwi kuwa utaghafilika kumpa malipo aliyekuridhisha msaliye Muhammad na Aali Zake na unipe matumaini yangu. Nizidishiye mwongozo wako utakaonifikisha kufanikisha amali yangu. Hakika wewe mwenye huruma mkarimu.

DUA YA 38

DUWA ZAKE(A.S) KATIKA KUOMBA RADHI KWA KUWATENDEA VIBAYA WAJA WA MWENYEZI MUNGU KWA KUTOWAJIBIKA IPASAVYO KUHUSU HAKI ZAO NA KUIKOMBOA SHINGO YAKE IEPUKANE NA MOTO

Oh Allah! Mimi nakuomba msamaha kutokana na mdhulumiwa alidhulumiwa mahali mimi nipo na sikumsaidia. Na kutokana na wema nimetendewa sikuwa mwenye shukurani. Na mtenda maovu aliniomba msamaha sikumsamehe. Mwenye shida aliniomba sikumpa kipaombele kuliko nafsi yangu. Na haki ya mwenye haki iliyo nilazimu ya muumini sikuitekeleza. Na aibu ya muumini ilinidhihirikia na sikumsitiri. Na kila aina ya dhambi ilijitokeza mbele yangusikuihama. Nakuomba msamaha Ewe Mola wangu kwa yote haya na kwa yafananayo na haya. Msamaha wa kujuta ambao utakuwa onyo kwa yaliyo mfano wake hapo baadaye. Msaliye Muhammad na Aali zake na jaaliya kujuta kwangu juu ya yale niliyojiingiza katika mitelezo iwe azma ya kujiepusha na yanayojitokeza mbele yangu miongoni mwa maovu. Iwe toba itakayo niwajibishia mapenzi yako. Ewe mpenzi wa wafanyao toba.

DUA YA 39

DUWA ZAKE(A.S) KATIKA KUOMBA MSAMAHA NA REHEMA

Oh Allah! msaliye Muhammad na Aali zake.Yavunje matamanio yangu ya kila haramu. Uondowe uchu wangu wa kila tendo la dhambi. Niziwiye kumuudhi muumini yeyote Muislamu mwanaume na mwanamke. Oh Allah! mja yeyote amenitendea baya ulilo hadharisha kwake na amekiuka kwa kunitendea ulilo mgombeza na amekufa na aliyo nidhulurnu au nimemlalamikia akiwa hai. Msamehe aliyonitendea na umuwiye radhi kwa yale aliyenitumbiya mgongo. Msimsimamishe kumtaka aliyonitendea. Usimuumbue kwa aliyoyachuma kwangu. Na jaaliya niliyosamehe kwa kuwawia radhi na niliyojitolea miongoni mwa sadaka kwao iwe sadaka safi mno miongoni mwa sadaka za watoao sadaka. Na zawadi ya hali ya juu mno miongoni mwa zawadi za watafutao ukaribu na wewe. Nifidiye msamaha wangu kwao kwa msamaha wako. Na DU'A yangu kwao nipate rehema zako ili kila mmoja wetu apate hali njema kwa fadhila zako. Na ili aokoke kila mmoja wetu kwa huruma zako. Oh Allah!

mja yeyote katika waja wako amepata kutoka kwangu ovu au aliguswa na madhara kutoka kwangu au lisilofaa limemfika kupitia kwangu au kwa sababu yangu amedhulumiwa. Nimeshindwa kuwa mwangalifu wa haki yake au nimekwenda (kufa) na haki yake iliyo dhulumiwa. Mswalie Muhammad na Aali zake mridhishe kwa ajili yangu kutaka utajiri wako. Mpe haki yake kamili kutoka kwako kisha nilinde na liwajibishalo hukumu yako kwa ajilii yake. Na niepushe na lihukumiwalo na uadilifu wako. Kwa sababu nguvu zangu haziwezi kuhimili adhabu yako. Na kwa sababu uwezo wangu hauwezi kusimama mbele ya makasiriko yako. Kwa hakika ikiwa utanilipa kulingana na haki utanihilikisha. Na kama hautonikinga na rehema zako utaniangamiza. Oh Allah ! hakika mimi nakuomba Ewe Mola wangu ambacho kukitowa kwake hakukupunguzii (chochote).

Nakuomba kubeba ambalo uzito wake haukutopei. Nakuomba uipe nafsi yangu Ewe Mola wangu! Ambayo haukuiumba ili ujikinge na uovu au iwe ndio njia ya manufaa, bali umeiumba ili kuthibitisha uwezo wako kwa nyingine iliyo mfano wake na kwa sababu iwe ni hoja dhidi ya iliyo mfano wake. Nakuomba ubebe mizigo yangu ya dhambi ambayo uzito wake umenishinda nguvu kubeba. Naomba msaada kwako kwa ajili ya ambalo uzito wake umenielemea. Msaliye Muhammad na Aali zake uipe nafsi yangu ingawa imetenda maovu. Iwakilishe Rehma yako kubeba mzigo wangu (dhambi). Wangapi miongoni mwa watenda mabaya imewafika Rehma zako! Wadhalimu wangapi msamaha wako umewajumuisha. Mswaliye Muhammad na Aali Zake. Na nifanye mimi mfano wa ulio wainuwa kwa kuwastahmilia kutoka kwenye mweleka wa wakosefu. Na umemwokowa kwa tawfeeki yako kutoka kwenye hali mbaya ya waovu. Na akawa aliyeachwa huru na msamaha wako kutoka pingu za makasiriko yako.

Na aliyeachwa huru na wema wako toka kamba za uadilifu wako. Hakika wewe ufanyapo hayo Ewe Mola wangu! wamfanyia ambaye hakanushi kustahiki kwake adhabu yako wala haji takasi nafsi yake kutoka wajibikiwa na malipizi yako. Wamfanyia hivyo Ewe Mola Wangu! Ambaye hofu yake kwako ni nyingi kuliko tamaa yake kwako. Na yule ambaye kukata tamaa kuwa hatofanikiwa ni saana kuliko matumaini yake ya kuokoka. Sio kutokuwa na matumaini kwake ni kukata tamaa au matumaini yake yawe ni kughurika (kudanganyika). Bali ni kwa sababu ya uchache wa mema yake kati ya maovu yake na udhaifu wa hoja zake katika matendo yake yote. Na wewe Ewe Mola wangu, ni mstahiki wa kuwa asi danganyike mbele yako mkweli. Wala asikatishwe tamaa na wewe muovu kwa sababu wewe ni bwana mtukufu ambaye fadhila zake hamziwii yeyote. Wala hamfuatilii yeyote haki yake. Jina lako litukuzwe zaidi ya watukuzwao, yametakasika majina yako zaidi kuliko wote watajwao. Neema zako kwa viumbe wote zimewaenea; zako ni sifa njema kwa yote hayo Ewe Bwana wa Ulimwengu wote.

DUA YA 40

MIONGONI MWA DU'A ZAKE(A.S) AKITANGAZIWA KIFO CHA MTU AU AKUMBUKAPO UMAUTI

Oh Allah! Msaliye Muhammad na Aali Zake. Tutosheleze na matumaini marefu tupunguzie nayo kwa kazi ya ukweli ili tusitumainiye kuikamilisha saa baada ya saa. Wala kuikamilisha siku baada ya siku wala kukutana pumzi na pumzi nyingine. Wala kukutana hatuwa na hatua nyingine, Tusalimishe na udanganyifu wake tupe amani na shari yake. Uweke umauti mbele yetu dhahiri usijaaliye kumbukumbu yake kwetu kuwa ni ya mara moja na kupotea utujaaliye kuwa miongoni mwa watenda mema. Ili tuone kwa ajili yake kuja kwako kuna chelewa mpaka ifikiye tuuone umauti ni jambo tunalopendezwa nalo. Na tuone umauti ni mahali tulipopazowea tuna shauku napo na mlinzi wetu tumpendaye kuwa karibu naye. Ukiuleta kwetu na kututeremshia tufanye tuwe na furaha nao kama mgeni aliyekuja kututembelea. Tuweke katika raha naye ajapo usitufanye tuwe katika mashaka ya kumpokea kwake. Usitudhalilishe katika kumpokea kwake. Wala usitutweze kwa ziara yake. Mfanye kuwa mlango miongoni mwa milango ya ghofirani zako awe ufunguo miongoni mwa funguo za Rehma zako. Tufishe katika hali ya uongofu si katika hali ya upotovu tuwe watii si wenye kukirihishwa. Wenye kutubu si katika hali ya uasi wala wenye kung'ang'ania maasi. Ewe mwenye kudhamini malipo ya watendao mema. Na mrekebishaji wa matendo ya waharibifu.

DUA YA 41

DU'A ZAKE(A.S) KATIKA KUOMBA SITARA NA ULINZI

Oh Allah! Msaliye Muhammad na Aali Zake. Nitandikiye kitanda cha heshima yako nipeleke kwenye manyweo ya maji ya rehema zako. Nikalishe kati kati ya bustani yako usinipe mtihani wa kukataliwa na wewe. Usininyime kwa kutokukutumainia. Usinifuatilie niliyoyatenda. Wala usinifuatilie nilioyafanya. Usiyadhihirishe yaliyofichika na kwangu wala usiyafichuwe yaliyositirika kwangu. Usiyaweke matendo yangu katika mizani ya uadilifu. Usizitangaze habari zangu mbele ya macho ya kundi la watu. Wafiche lile ambalo kulitangaza ni aibu kwangu. Likunje mbali nao litakaloniaibisha mbele yako. Ipe heshima daraja yangu kwa ridhaa zako. Nikamilishiye heshima yangu kwa ghofirani zako. Nipange katika watu wa mkono wa kulia, niongoze katika mapito ya walio katika amani. Nifanye niwe katika kundi la waliofaulu. Visitawishe vikao vya watu wema kwa kunitumikisha. Aameen. Ewe Bwana wa ulimwengu.

Dua ya 42

DU'A YAKE(A.S) WAKATI WA KUHITIMISHA QUR'AN

Oh Allah! Hakika wewe umenisaidia kuihitimisha Qur'ani kitabu chako ambacho umekiteremsha kikiwa nuru na umekifanya mlinzi wa kila kitabu ulichokiteremsha. Na umekiboresha juu ya kila hadithi uliyoisimulia. Na ni kitenganishi kwacho umetenganisha kati ya halali yako na haramu yako. Qur'an ambayo kwayo umeiweka wazi sheria ya hukumu yako. Kitabu umekipambanuwa kwa waja wako upambanuzi wa wazi. Ni Wahyi ulio uteremsha uteremsho kwa Nabii wako Muhammad Rehma Zako zimfikie na ziwafikiye Aali zake. Umeifanya kuwa nuru ituongoze katika giza ya upotevu na ujinga kwa kuifuata. Kiponyesho kwa mwenye kuisikiliza kwa kuifahamu na kuisadiki. Ni mizani ya kiadilifu isiyopotoka ulimi wake na kuwa mbali na haki. Nuru ya uongofu ambayo Burhani yake haiwazimikii watizamaji wake. Na alama ya uokovu ambayo hapotei mwenye kufuata mafunzo yake. Wala haitomfikia mikono ya maangamizi mwenye kujiambatanisha na kishiko chake cha ulinzi. Oh Allah! Kwa vile umetusaidia kuisoma. Na umeturahisishia ugumu wa ndimi zetu kwa uzuri wa ibara yake hivyo basi tufanye tuwe miongoni mwa wanaoichunga haki ya kuichunga na wakutumikia kwa itikadi ya kusalimu amri ya aya zake zilizothabiti waombao kimbilio kwa kuzikubali zile aya mutashabih na zile ufafanuzi wake uko bayana. Oh Allah! Hakika wewe umeiteremsha kwa Nabii wako Muhammad Rehema za mungu zimfikiye yeye na Aali zake kwa ujumla.

Na umeturithisha sisi Elimu yake tukiwa wafasiri. Na umetuboresha juu ya wasioijuwa elimu yake. Umetupa nguvu juu yake ili utunyanyuwe juu ya wasio weza Ibada. Oh Allah! kama vile umezifanya nyoyo zetu kuwa zenye kuibeba. Na kwa rehema zako umetutambulisha utukufu na ubora wake. Basi msaliye Muhammad, muhubiri wake na Aali zake wahifadhi wa Qur'ani. Utujaalie kuwa miongoni mwa wanaotambuwa kuwa yatoka kwako. Ili isituzukiye shaka katika kuisadiki. Wala upotovu usitutikise na kututowa nje ya njia yake nyofu. Ewe Allah, mswaliye Muhammad na Aali Zake. Na tujaaliye sisi kuwa miongoni mwa wanaoshikamana na kamba yako, na wakimbiliao kutoka kwenye aya mutashabihati kwenda kwenye ngome yake madhubuti na kuketi kwenye kivuli cha bawa lake, na aongokaye na mwanga wake wa asubuhi. Aongokaye na kuchomoza kwa mng'aro wake. Anamulika kwa taa yake. Wala hatafuti uongofu katika kitu kingine.

Ewe Mola! Kwa hiyo Qur'an umemweka Muhammad kuwa alama ya kukujuwa wewe. Na kupitia Ahlul-Bayt wake umeweka wazi njia za ridhaa zako. Msaliye Muhammad na Aali Zake na ifanye Qur'ani kwetu kuwa njia za kwenye daraja la utukufu. Na iwe ngazi tuipandayo kwenda mahali pa salama. Na iwe sababu tutakayolipwa uokovu kwenye uwanja wa kiyama. Na njia ambayo kwayo tutazifikia neema za nyumba ya kudumu. Ewe Allah! Msaliye Muhammad na Aali Zake. Kwa Qur'ani tupunguziye uzito wa dhana utupe sifa njema za watu wema na tufanye tufate athari za waliosimama kwa ajili yako nyakati za usiku na mwisho wa mchana. Ili ututakase na kila uchafu kwa utakaso wake. Utufanye tufate athari ya walioangaza kwa nuru yake. Wala matumaini hayakuwa zuiya kutenda kazi iliyowatenge mbali kwa vitimbi vya udanganyifu wake. Ewe Allah! Mrehemu Muhammad na Ali Zake. Rekebisha kwa Qur'an upungufu wetu tusiwe mafakiri. Kwa Qur'ani tusukumiye maisha ya raha na wasaa wa riziki. Tuepushe kwayo na tabia mbaya na mwenendo duni. Tuhifadhi kwa Qur'ani tusiingiye ndani ya shimo la maangamizi kufuru na mwendo wa kinafiki.

Ili iwe mwongozo uelekezao kwenye maridhawa yako na bustani zako siku ya kiyama. Na iwe kwetu mlinzi hapa duniani dhidi ya makasiriko yako na kukiuka mipaka yako. Na iwe kwa yale uliyonayo kwa kuhalalisha halali yake na kuharamisha haramu yake shahidi. Ewe Allah! Mrehemu Muhammad na Aali Zake na kwa Qur'ani urahisishe umauti nafsini mwetu wakati wa kufa. Na usumbufu wa kukokotwa (Roho) Uuguaji. Na taabu ya mauguzi, na mfuatano wa kutatarika. (Ifikapo roho kooni na itasemwa: Mganga ni nani?) Atajitokeza Malaika wa umauti ili aichukue toka nyuma ya pazia ya mambo yasiyojulikana. Na kuitupa toka upinde wa umauti kwa mshale wa kuachwa peka na kuwa changanyiya sumu iuwayo kwenye kikombe chenye mwonjo wa sumu wakati msafara wa kuelekea akhera ukitusogelea. Kazi zitakuwa ukosi wa shingo makaburi yatakuwa ndio kimbilio mpaka wakati wa siku ya kukutana. Ewe Allah! Mrehemu Muhammad na Aali zake. Na utubariki wakati wa kuingia nyumba ya kuoza na makazi ya muda mrefu kati ya tabaka za udongo. Yajaaliye makaburi baada ya kuiaga dunia yawe mafikio yetu mema tupanulie mbano wa mwana ndani zetu kwa rehema zako Usitufedheheshe mbele ya walio hudhudhiria siku ya Kiyama kwa sababu ya madhambi yetu ya angamizayo. Kwa Qur'ani irehemu hali yetu duni katika kikao cha kuletwa mbele yako Kwa Qur'ani zithibitishe nyayo zetu zisiteleze wakati daraja la Jehannam litakapoyumba yumba.

Kwayo ing'arishe giza ya makaburi yetu kabla ya kufufuka. Utuokowe kwa Qur'ani na kila taabu ya siku ya Kiyama na shida za kutisha siku ya maafa. Zing'arishe nyuso zetu siku ambayo nyuso za wadhalimu zitakuwa nyeusi siku ya kuhasirika na majuto. Utujaaliye upendo ndani ya nyoyo za waumini. Usiyafanye maisha kwetu kuwa ya shida. Ewe Allah! mrehemu Muhammad mja wako na mjumbe wako kwa vile ameifikisha risala yako na alitekeleza amri yako. Aliwanasihi waja wako Ewe Allah! Mjaaliye Nabii wetu Rehema Zako ziwe juu yake, na juu ya Aali zake - Awe karibu mno na wewe siku ya kiyama miongoni mwa Manabii watakaokuwa karibu ya kikao. Na mwenye uwezo mkubwa sana kwako wakuombea. Mwenye Enzi kubwa miongoni mwao kwako. Mwenye cheo kikubwa mno mbele yako. Oh Allah! Mrehemu Muhammad na Aali wa Muhammad. Itukuze nyumba yake, Bur'hani yake itukuze, Mizani yake ipe uzito, ya kubali maombezi yake usogeze karibu wasila wake, ufanye uwe mweupe uso wake, ikamilishe nuru yake iinue daraja yake. Tufanye sisi tuishi na sunna yake, tufishe tukiwa katika mila yake, tupeleke tufikishe kwenye njia yake. Tupitishe njia yake. Tujaaliye tuwe miongoni mwa watu watii wake.

Tufufuwe katika kikundi chake tuelekeze kwenye dimbwi lake, tunyweshe kwa bilauri yake. Rehemu Muhammad na Aali zake. Rehema ambayo utamfikisha nayo kwenye ubora asio uwazia miongoni mwa kheri na fadhila zako, na heshima zako. Hakika wewe ni mwenye Rehma kubwa na fadhila tukufu. Oh! Allah mlipe kwa aliyoyafikisha katika jumbe zako. Na amefikisha aya zako, amepigana jihadi katika njia yako malipo yaliyo bora umepata kumlipa yeyote miongoni mwa Malaika wako wa karibu na Manabii wako walio Mursali wateule. Amani imfikie yeye na iwafikiye watoto wake watakatifu wema, na rehema za Mungu na baraka zake.

DUA YA 43

MIONGONI MWA DU'A ZAKE AUONAPO MWEZI MWANDAMO

Ewe Kiumbe mtii. Mwenye mwendo wa haraka usiochoka. Wenye kurudia rudia katika mafikio yalio kadiriwa. Wenye kupita katika mviringo uliopangwa. Na mwamini ambaye kwa kukutumia wewe ameangaza nuru kwenye giza na ameangaza kupitia wewe weusi na amekufanya alama katika alama za ufalme wake. Na alama miongoni mwa alama za mamlaka yake. Na amekufanya mnyenyekevu kwa kuzidi na kupunguwa. Kuchomoza na kuzama, kung'ara na kupatwa uko mtii kwake kwa yote hayo. Na kwenye utashi wake uko haraka ajabu ilioje mpango wake katika mambo yako. Werevu ulioje aliofanya katika kazi yako. Amekufanya kuwa ndio mwanzo wa mwezi mpya na hali mpya. Na mwomba Mungu Bwana wangu na Bwana wako, Muumba wangu na Muumba wako. Muweka vikomo wangu na muweka vikomo wako. Mfanya taswira wangu na mfanya tasweira wako. Amrehemu Muhammad na watoto wake. Na akufanye wewe uwe mwezi mwandamo wenye baraka isiyo futwa na kupitiwa na usiku. Na usafi usiochafuliwa na dhambi. Mwandamo wenye amani bila ya maafa na salama bila maovu. Mwandamo wenye heri bila ya ndege mbaya na ufanisi bila ya shida. Mwandamo wenye urahisi usiochanganyika na ugumu.

Na wenye heri isio changanyika na shari. Mwanadamo wa amani na imani neema na hisani. Salama na Uislamu. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aali zake. Na tujaalie sisi kuwa wenye kuridhika mno miongoni mwa waliochomozea nao. Na wasafi mno miongoni mwa waliouangalia. Na waliobahatika mno katika wale waliokuabudu katika huwo. Utukubalie humo toba utulinde utulinde humo na matendo yasiyofaa utuhifadhi humo tuwe hatujihusishi na kukuasi wewe. Utugawiye humo kushukuru neema zako. Na utuvalishe humo kwa sitara ya afya njema. Tukamilishiye neema zako kwa ukamilifu wa utii wako. Kwa hakika wewe mwenye huruma msifika wa sifa njema. Na Rehema za Allah zimfikiye Muhammad na Aali zake wema waliotahirika.

DUA YA 44

MIONGONI MWA DU'A ZAKE UINGIAPO MWEZI WA RAMADHANI

Utukubalie humo toba utulinde litulinde humo na matendo yasiyofaa utuhifadhi humo tuwe hatujihusishi na kukuasi wewe. Utugawiye humo kushukuru Neema zako. Na utuvalishe humo kwa sitara ya afya njema. Tukamilishiye Neemza zako kwa ukamilifu wa utii wako. Kwa hakika wewe mwenye huruma msifika wa sifa njema. Na Rehema za Allah zimfikie Muhammad na Aali zake wema waliotahirika. Sifa njema ni za Allah ambaye ametuongoza kwenye sifa zake na kutujaalia sisi kuwa wastahiki wake. Ili tuwe wenye kushukuru ihsani zake. Ili atulipe kwa hilo malipo ya watu wema. Sifa njema ni za Allah ambaye ametupendelea kwa dini yake. Na ametuhusisha na mila yake na ametuelekeza katika njia za hissani zake. Ili tuzipate kwa upaji wake tuzifikie radhi zake. Himidi ambayo ataikubali kutoka kwetu, na ataridhika nayo. Sifa njema ni za Mungu ambaye amejaalia miongoni mwa njia hizo mwezi wake.

Mwezi wa Ramadhani mwezi waswiyam mwezi wa Uislamu. Mwezi wa usafi na ni mwezi wa mchekecho. Mwezi wa kusimama kwa ajili ya Sala. Mwezi ambao Qur'ani iliteremshwa humo ili iwe mwongozo kwa watu na ni ubainifu katika mwongozo na kitenganishi. Amebainisha ubora wake kwa kulinganisha na miezi mingine. Kwa kuwa ameujaalia matakatifu mengi na mengi yaliyo bora na mashuhuri. Hivyo basi ameharamisha humo ambayo aliyoyahalalisha katika miezi mingine ili kuuadhimisha. Ameziwia humo malaji na vinywaji ili kuupa heshima. Ameujaalia wakati bainifu, haruhusu Mtukufu Mwenye Enzi utangulizwe kabla ya wakati wake. Wala hakubali ucheleweshwe. Kisha ameuboresha usiku mmoja miongoni mwa usiku wake kwa daraja ya sawa na miezi elfu moja. Na ameuita Laylatul-qadri (Malaika na Arruhu huteremka usiku huo kwa idhini ya bwana wao na kila amri). Amani yenye baraka ya kudumu mpaka kuchomoza kwa alfajiri kwa amtakaye katika waja wake kwa aliyohukumu kulingana na maamuzi yake. Ewe Allah mrehemu Muhammad na Aali zake. Tupe Ilhamu ya kutambuwa ubora wao, na kutukuza heshima yake. Na kuchunga uliyoyazuiya. Tusaidie kutekeleza funga yake kwa kuvizuia viungo vya mwili visikuasi na kuvitumia humo (mwezini) kwa yakuridhishayo.

Kwa kiasi kwamba hatusikilizi kwa masikio yetu maongezi ya ovyo. Na tusiharakie kwa macho yetu kwenye upuuzi; na kwa kiasi kwamba hatunyoshi mikono yetu kwenye ambayo yamehadharishwa. Wala tusipige hatua kwa miguu yetu kuyaelekea yaliyokatazwa. Hata tusishibishe tumbo zetu isipokuwa iliyohalalishia, ndimi zetu zisitamke isipokuwa yale yaliyo mfano. Wala tusijibebeshe isipokuwa yanayosogeza karibu na thawabu zako wala tusijishughulishe isipokuwa na yale tu yanayozuia adhabu yako. Kisha yote hayo yaepushe na riya ya wapendao kusifiwa na yaepushe na kusikika kwa wapendao umashuhuri. Tusimshirikishe (kwenye matendo hayo yote) yeyote asiyekuwa wewe. Tusitaraji kwayo mradi usiokuwa wewe. Ewe Allah! mrehemu Muhammad na Aali zake na tujaalie humo kuhudhuria nyakati za Sala tano. Kwa mipaka yake uliyoiweka na wajibu uliowajibishia na nyadhifa zake ulizoziweka na nyakati zake ulizoweka. Na katika sala tuweke weko la waliofanya sawa mahali mwake, wenye kuhifadhi nguzo zake, watekelezao kwa wakati wake. Kama alivyofanya mja wako na mjumbe wako. Rehma zako zimfikie yeye na Aali zake.

Katika rukuu na katika Sijida na fadhaili zake zote kwa ukamilifu wa Twahara na wa sawa kabisa. Na unyenyekevu uliobayana na wa uhakika. Na tupe taufiki ndani yake ili tuunganishe udugu kwa mema na kujitolea. Na kuwa pamoja na majirani wetu kwa kuwafadhili. Tuziepushe mali zetu na madai na zitakase kwa kutoa zaka. Tumwendeee aliye tuwekea upasi na tumtendee uadilifu aliye tudhulumu. Tumsalimishe mwenye kutufanyia uadui isipokuwa yule afanyiwaye uadui kwa ajili yako kwa kuwa yeye ndiye adui ambaye hatutamfanya rafiki na ni kundi ambalo hatutalitakasa na tujikurubishe kwako humo kwa amali safi ambayo kwayo utatutakasa nayo na kutuweka mbali na dhambi. Utuhifadhi humo na kuzirudia aibu ili asikuletee malaika yeyote isipokuwa machache tuyaletayo katika milango ya utii wako na aina za ukaribu kwako. Ewe Allah hakika mimi nakuomba kwa haki ya mwezi huu. Na kwa haki ya walio abudu kwa ajili yako humo toka mwanzo wake mpaka wakati wa kwisha kwake, miongoni mwa Malaika uliyemsogeza karibu au Nabii uliyemtuma au mja mwema umemchagua makhsusi. Umrehemu Muhammad na Aali zake na utuandamishiye kwa yale uliyo waahidi wapenzi wako miongoni mwa karama zako. Twajibishiye humo uliowa wajibishia watu waliokwenda mbali sana katika kukutii.

Tuweke katika daraja la walio stahiki ngazi ya juu kwa rehema zako. Ewe Allah mrehemu Muhammad na Aali zake tuepushe na kupotoka katika kukupwekesha. Na kutofanya ipasavyo katika kukutukuza. Na kuwa na shaka katika Dini yako na kutoiona njia yako na mghafala wa heshima yako. Tuepushe na kudanganywa na adui yako shetani aliyewekwa kando na rehema zako.

Ewe Allah, mrehemu Muhammad na aali zake, tuelemeapo upande katika huu mwezi tuweke sawa. Tukienda kombo humo tuweke sawa. endapo adui wako shetani atatudhibiti tuokoe. Ewe Mola ujaze kwa Ibada zetu kwako zipambe nyakati zake kwa utii wetu kwako. Tusaidie katika nyakati zake za mchana kuufunga na usiku wake. Utusaidie kutekeleza sala na kukuomba wewe na kukunyenyekea kujidhalilisha mbele yako. Ili mchana wake usiwe shahidi dhidi yetu kwa mghafala wala usiku wake kwa kuzembea. Ewe Allah tujaaliye katika miezi mingine na mchana hivyo hivyo kwa kadiri utupavyo uzima. Tufanye tuwe miongoni mwa waja wako wema (ambao watarithi Janna ya Firdausi humo watabaki milele). ( Na wale ambao wanatoa wakitoacho hali ya kuwa nyoyo zao zaogopa kuwa watarejea kwa Mola wao) na miongoni mwa ambao (wanaharakia katika mambo ya kheri nao kwayo ni wenye kushinda). Ewe Allah! Mrehemu Muhammad na Aali Zake katika kila wakati na muda wote na hali zote kwa idadi uliomrehemu. Na zaidi ya yote hayo kwa ziyada ambayo hawezi kuihesabu asiyekuwa wewe! Hakika wawe ni mtendaji wa utakalo.

2

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

DUA YA 5

NA ILIKUWA MIONGONI MWA DU'A ZAKE KWA AJILI YAKE MWENYEWE (A.S) NA KWA WALIO CHINI YA WILAYA YAKE

Ewee! ambaye maajabu ya utukufu wake hayatokwisha. Mrehemu Muhamadi na Ali zake tuzuwiye kupotoka katika utukufu wako. O we ambaye muda wa ufalme wake hautakoma. Mrehemu Muhammad na Aali zake zikomboe shingo zetu na lipizi zako. Oh! wee ambaye hazishi hazina za rehma zake mrehemu Muhammad na Aali zake. Na utupe sehemu katika rehema zako, Oh wee ambaye macho yanashindwa kumwona. Mrehemu Muhammad na Aali zake, tusogeze karibu yako. Oh! wee ambaye unakuwa mdogo ukubwa wa kila kikubwa mbele yake. Mrehemu Muhammad na Aali zake utupe heshima. Oh, wee ambaye mbele yake hujitokeza kila kilichojificha. Mrehemu Muhammad na Aali zake. Usitufedheheshe mbele yako. Ewe Mola! tuonndolee haja ya hiba ya watowao hiba kupitia hiba zako. Tutosheleze tusisumbuliwe na kitwea cha wajitengao nasi kwa mawasiliano yako ili tusimsihi yeyote pamoja na kuwa wewe watupa bure. Wala tusione kitwe kutokana na yeyote ikiwa fadhila zako twazipata. Ewee Mola! Mrehemu Muhammad na Aali wake. Na utupangie wala usipanguwe dhidi yetu. Tupe ushauri kwa faida yetu wala si kinyume chake. Mzunguko wa neema udumishe kwetu wala usiuelekeze kwingine. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aali zake na utulinde sisi kuwa dhidi yako. Na utulinde kupitia wewe mwenyewe.

Utuongoze kuelekea kwako wala usituweke mbali na wewe. Kwa hakika umlindaye huwa salama. Na umwongozaye hujuwa. Umwekaye karibu nawe hupata ngawira. Ewee Mola mrehemu Muhammad na Aali zake. Na tukinge na makali ya mabadiliko ya wakati, na shari ya windo la shetani. Na ukali wa udhalimu wa kisultani Ewe Mola kwa hakika wajitoshao wajitosha kwa fadhila za uwezo wako. Msalie Muhammad na Aali zake kwa hakika hutowa watowao kupitia wingi wa utajiri wako. Mrehemu Muhammad na Aali zake na utupe, huongoka waongokao kwa nuru ya uso wako, msalie Muhammad na Aali wake na tuongoze. Ewe Mola hakika uliyemfanya rafiki hakumdhuru kutelekezwa na watelekezaji. Na uliyempa hapungukiwi kwa kunyimwa na wanyimaji. Na uliyemwongoza haumpotezi upotovu wa wapotovu. Mrehemu Muhammad na Aali zake. Na utuzuiye (tusidhuriwe na waja wako) kwa nguvu zako. Tutosheleze tusimhitaji mwingine mbali na wewe kwa kuungwa mkono na wewe. Tupitishe njia za haki kwa mwongozo wako. Ewe Mola msalie Muhammad na Aali zake. Na jaalia usalama wa nyoyo zetu kwa kukumbuka utukufu wako. Na nafasi ya wazi ya miili yetu iwe twakushukuru neema zako. Na ujaaliye mtiririko wa ndimi zetu uwe katika kusifu ihisani zako. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aali zake. Tujaalie tuwe miongoni mwa wahitaji wako wanaowaita watu kuja kwako na viongozi wako waongozao kuelekea kwako. Na tuwe miongoni mwa watu makhsusi uliowafanya wawe makhsusi kwako. Ewe mwenye kurehemu mno kuliko wenye kurehemu wote.

DUA YA 6

NA ILIKUWA MIONGONI MWA DU'A ZAKE A.S. NYAKATI ZA ASUBUHI NA JIONI

Sifa njema ni za Mungu ambaye ameumba usiku na mchana kwa nguvu zake. Na amezipambanuwa kwa uwezo wake. Na amekifanyia kila kimoja kati ya hivi viwili mpaka wenye kikomo na muda ulio na mwisho. Hukiingiza kila kimoja ndani ya mwenzake. Na humwingiza mwenzake ndani.yake. Kwa mpango kutokana na yeye, kwa ajili ya waja kwa vile awalishavyo na kwa hivyo ndivyo awakuzavyo. Amewaumbia usiku ili wapumzike humo kutokana na harakati za taabu na juhudi zenye kuchosha. Na ameufanya (usiku) kuwa vazi ili wajisitiri kwa mapumziko humo kwa kulala, iwe kwao kiburudisho na nguvu mpya na waifanyie kwa huo usiku furaha na matamanio. Na amewaumbia mchana uwezeshao kuona ili wazifikie fadhila zake. Na iwe sababu ya kuipata rizki yake. Na wazunguke kwa uhuru katika ardhi yake wakitafuta kipato cha mwenye haraka ya dunia yake na kufanikiwa ya baadaye katika maisha ya akhera. Kwa yote hayo awawekea sawa hali yao na kuuzifanyia mtihani khabari zao, ili awaangalie wakoje wakati wa utii wake na mahali mwa wajibu zake. Na sehemu za hukumu zake.(Ili awalipe waliotenda maovu kulingana na waliyotenda. Na awalipe waliotenda mema wema.) Ewe Mola! sifa zote njema ni zako. Kwa kutukunjulia asubuhi, na kutufanya tufurahie mwanga wa mchana. Na umetufanya tuone jinsi ya kuitafuta chakula na umetulinda na maafa. Tumekuwa asubuhi na vimekuwa vitu vyote pamoja ni vyako. Mbingu, ardhi na ulicho kitawanya kwa kila mmoja wao chenye kutulia na chenye kufanya harakati kikazi na chenye kusafiri na kirukacho juu kabisa angani na kijifichacho chini ya ardhi twapambazukiwa na asubuhi katika ushiko wako. Twazingirwa na ufalme wako na mamlaka yako. Tumo ndani ya utashi wako. Tunakwenda hapo na pale kwa amri yako. Tunageuka geuka ndani ya mpango wako.Hatumiliki letu jambo ila ulilolipitisha, wala hatulimiliki jambo la kheri isipokuwa ulilotoa. Na hii siku mpya imekuja, itakuwa shahidi madhubuti kwetu, tukifanya mema itatuaga iondokapo kwa sifa njema. Na tufanyapo maovu itatuacha kwa lawama. Ewe! Mola msalie Muhammad na Aali wake. Na utupe uzuri wa kusuhubiana naye na utulinde na kutengana naye vibaya, kwa kutenda yasiyofaa au kutenda dhambi yeyote ile ndogo au kubwa. Tufanye tuwe na matendo mema mengi humo na tuepushe na matendo maovu humo. Na jaza kwa ajili yetu kati ya ncha zake mbili sifa njema na shukrani, ujira na akiba, fadhila na ihsani. Ewe Mola wepesisha mizigo yetu kwa waandishi watukufu, na lijaze mema yetu katika sahifa zetu (karatasi za hesabu) usitudharaulishe kwako kwa matendo yetu maovu. Ewe Mola tujaaliye hadhi toka kwa waja wako katika kila sehemu ya shukurani zako. Na ushahidi wa kweli miongoni mwa malaika wako.

Ewe Mola msalie Muhammad na Aali zake. Utuhifadhi mbele yetu na nyuma yetu kuliani kwetu na kushotoni kwetu na pande zetu zoote, hifadhi inayotulinda na kukuasi wewe, yenye kutuongoza kwenye utii wako, yenye kutekeleza upendo wako. Ewe Mola! msalie Muhammad na Aali zake. Na utukubalie katika siku yetu hii na usiku wetu huu na katika siku zetu zoote kuitenda kheri na kuihama shari na kuishukuru neema na kuzifuata sunnah na kujiepusha na bidaa, na tuwe wenye kuamrisha mema na kukemea maovu. Kuulinda Uislamu na kuutweza ubatili na kuudhalilisha ili kuinusuru haki na kuipa nguvu kumwongoza aliyepotoka kumsaidia mnyonge kumkomboa aliyekatika taabu. Ewe Mola msalie Muhammad na Aali zake. Na ifanye (siku) kuwa ya baraka mno kuliko siku ya baraka tuijuayo na mwenzi bora kuliko mwenzi yeyote tumepata kuwa naye na wakati uwe ni wakati bora kuliko wakati wowote tumepata kuwa chini ya kivuli chake. Na utufanye tuwe wenye kuridhiwa mno miongoni mwa waliopitiwa na usiku na mchana katika jumla ya viumbe wako. Wenye kushukuru sana kati yao kwa mema uliowapa miongoni mwa neema zako. Watekelezaji kwa uthabiti mno wa sheria uliowawekea miongoni mwa sheria zako. Na wenye kujizuia sana na uliyo yahadharisha miongoni mwa makatazo yako. Ewe Mola mimi nakufanya shahidi nawe nishahidi tosha. Na ninazifanya mbingu zako na ardhi zako na uliowafanya kuwa wakazi wa mbingu na ardhi kuwa mashahidi miongoni mwa malaika wako na viumbe wako wengine. Katika siku yangu hii saa yangu hii usiku wangu huu na kikazi changu hiki. Hakika mimi nashuhudia kuwa hakika wewe ni Mungu ambaye hapana Mungu mwingine isipokuwa ni wewe! mwenye kuidhibiti adala uko mwadilifu katika hukumu mwenye huruma kwa waja-u-Mfalme wa Wafalme mwenye huruma kwa viumbe. Yakuwa Muhammad ni mja wako na ni mjumbe wako mteule wako miongoni mwa viumbe wako. Umembebesha risala yako na ameitekeleza. Ulimuamuru kuitowa nasaha kwa umma wake na aliunasihi. Ewe Mola msalie Muhammad na Aali zake. Zaidi ya vile ulivyomsalia yeyote katika viumbe wako. Umpe kwa niaba yetu kilicho bora ulichompa yeyote katika waja wako. Na umlipe kwa niaba yetu kilicho bora na hheshima zaidi kuliko ulichomlipa yeyote miongoni mwa Manabiy wako kwa niaba ya umma wake. Hakika wewe ndiye mtowaji kwa wingi na msamehevu wa makubwa nawe u mwenye huruma zaidi kuliko mwenye huruma yeyote. Msalie Muhammad na Aali zake wema waliotahirika wateule waheshimiwa.

DUA YA 7

NA ILIKUWA MIONGONI MWA DU'A ZAKE (A.S) ANAPOTOKEWA NA JAMBO SUMBUFU AU KUSHUKIWA NA TAABU NA WAKATI WA KUKERWA

Oh! we ambaye kwake hufunguka mafundo ya mambo yachukizayo. Ee! wee ambaye kwake makali ya shida huwa butu. Ee we! ambaye huombwa njia ya kutoka kuelekea kwenye burudisho la faraja. Magumu yamekuwa dhalili mbele ya nguvu zako. Kwa huruma zako sababu zimepatikana. Kwa nguvu zako hukumu zimepita. Kwa utashi wako vitu vimekwenda kama ilivyotakiwa. Kwa utashi wako bila ya kauli yako vimewajibika. Kwa utashi wako vimejiziwiya bila ya kutumia katazo lako, wewe ndiye wa kuombwa wakati wa jambo litishalo. Na ndio kimbilio la wakati wa shida haiondoki isipokuwa ile shida ulioiondowa. Haitoki isipokuwa uliyoitowa, yameniteremkia ewe Mola wangu ambayo uzito wake umenielemea.Juu yangu kumeshuka jambo ambalo uzito wake umenishinda. Kwa nguvu zako umeshusha juu yangu kwa mamlaka yako umeelekeza kwangu.

Hakuna wa kuondowa ulichokileta, wala kuziwiya ulichokielekeza, wala wakufunguwa ulicho funga, wala wakufunga ulichokifunguwa, wala wa kufanya kiwe chepesi ulichokifanya kigumu, wala wakumsaidia uliyemwacha. Msalie Muhammad na Aali zake, na nifungulie ewe Mola wangu mlango wa faraja kwa rehma zako, niondolee mamlaka yatishayo kwa nguvu zako. Unipe mtazamo mzuri kwa malalamiko yangu. Unionjeshe utamu wa matendo kwa niliyoomba. Na unipe kutoka kwako rehmah na faraja njema. Na nijaalie mwanya wa kupenya kutoka kwako. Usinifanye nijishughulishe na mengine na kuacha wajibu wako. Na kuifanya sunnah yako. Nimezikika na yaliyo nishukia Ee Mola wangu nimejawa na huzuni kwa kuyabeba yaliyo niteremkia.Wewe ndiye mwenye uwezo wa kuondoa yaliyo nifika na kuyaweka mbali niliyoangukia, nifanyie hivyo ingawaje sistahiki kwako hivyo Ewee! bwana wa arshi tukufu.

DUA YA 8

DU'A ZAKE KATIKA KUJILINDA NA MAMBO YACHUKIZAYO NA TABIA MBAYA NA MATENDO YALAUMIWAYO

Ewe Mola najilinda na wewe dhidi ya uchochezi wa pupa na ukali wa ghadhabu na kuhemewa na husda na kudhofika kwa subira na uchache wa kutosheka na ukali wa tabia.Na uchochezi wa harara. Na kumilikiwa na msukumo wa tabia au jadhba. Na mgeuzo wa nia na kwenda kinyume na uongofu na sinzio la kughafilisha na kujikalifisha (yaani kujitwisha mambo zaidi ya uwezo) kuchaguwa batili na kuiacha haki. Na kujibakisha na kuendelea na madhambi na kuyadogesha maasi na kuukuza utii. Na kujifaharisha kwa matajiri na kuwadharau masikini na uangalizi mbaya kwa walio chini yetu. Na kutokuwa na shukrani kwa waliotutendea mema au tumsaidiye dhwalimu au kumtelekeza mwenye taabu au kujitakia yasiyo haki. Kwetu au tuongee kuhusu elimu bila ya elimu au kujihusisha na kumghushi yeyote na kujionea fahari matendo yetu. Na kuwa na matumaini marefu. Na tunajilinda na wewe kuwa na undani na kukidharau kidogo. Na kudhibitiwa na shetani. Au kuhujumiwa na wakati, au kudhulumiwa na mtawala. Na tunajilinda na wewe kufanya israfu na kuwa na kisichotosha. Na tunajilinda na wewe na masimango ya maadui. Na kukosa wenzi, na kuishi katika shida na kufa bila ya maandalizi. Na twajilinda na hasara kubwa mno na msiba mkubwa na twajilinda na mwisho mbaya, na kunyimwa thawabu na kufikwa na adhabu. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aali zake na unilinde na yote hayo kwa huruma yako na waumini wote wanaume na wanawake. Ewe! mwingi wa rehma kuliko wenye kurehemu wote.

DUA YA9

NA MIONGONI MWA DU'A ZAKE AKIWA NA SHAUKU SANA YA KUOMBA MSAMAHA KWA MWENYE ENZI MUNGU MTUKUFU

Ewe Mola msalie Muhammad na Aali zake, tufanye tuelekee kwenye toba uipendayo. Na ututoe tusiendelee kutenda uchukialo. Oh! Mola tusimamapo kati ya hali mbili ya upungufu iwe siku ya dini au dunia uiondoe hali ile ya upungufu haraka iishe. Na ujaalie kwangu toba iwe ya kubaki sana miongoni mwa mawili hayo. Na tuyakusudiapo mambo mawili moja la kuridhisha kutoka kwetu na la pili lakuchukiza toka kwetu. Tufanye tuelemee kwenye lile likuridhishalo toka kwetu. Dhoofisha nguvu zetu kwenye linalokuudhi na kutuchukia kwa ajili yake. Usiziache nafsi zetu kuchaguwa kwa sababu zenyewe huchaguwa batili isipokuwa ulizozipa taufiki. Na zenye kuamrisha mabaya isipokuwa ukirehemu. Ewe Mola kutokana na unyonge umetuumba, na umetujenga juu ya hali duni umetuanza (kutuumba) kutokana na maji hafifu. Hatuna uwezo isipokuwa kwa nguvu zako, wala nguvu hatuna isipokuwa kwa msaada wako. Tuwezeshe kwa kutufanikisha. Tuongoze kwenye njia ya sawa kwa mwongozo wako.

Ipofushe nguvu ya kuona ya nyoyo zetu dhidi ya yaendayo kinyume na mahaba yako. Usikijaalie chochote katika viungo vyetu vya mwili upenyo wa kwenye maasi yako. Ewe Mola! mrehemu Muhammad na Aali zake. Na jaalia nong'ono za nyoyo zetu na harakati za viuongo vyetu na mitupo ya macho yetu na semi za ndimi zetu viwe kwa ajili ya mambo yawajibishayo thawabu zako. Ili tusije pitwa na jema twastahiki kwalo malipo yako. Na usitubakishie tendo baya ambalo tutastahiki kwa ajili yake adhabu yako.

DUA YA 10

MIONGONI MWA DU'A ZAKE AKIOMBA KIMBILIO KWA MUNGU

Ewe Mola! Ukipenda tusamehe kwa fadhila zako na ukipenda utatuadhibu na hiyo itakuwa kwa uadilifu wako. Hivyo basi tufanyie wepesi msamaha wako kwa huruma yako. Tuepushe na adhabu yako kwa subira zako. Kwa kuwa hatuna uwezo kuukabili uadilifu wako. Wala hakuna atayeokoka bila ya msamaha wako. Ewe mwenye kujitosheleza kuliko matajiri wote. Tu hapa waja wako mbele yako. Nami ni fakiri kuliko mafakiri wote kwako. Urekebishe ufakiri wetu kwa wasaa wako. Usikate matumaini yetu kwa zuio lako, utakuwa umemdhalilisha mwenye kukuomba heri. Na umemnyima aliyekuomba fadhila zako. Kwa hiyo tugeukie kwa nani mbali na wewe, twende! Wapi kama si mlangoni kwako! Utakatifu ni wako, sisi ni wenye kudhikika ambao umewajibisha kuwakubalia. Ni wenye uovu uliowaahidi kuwaondolea uovu wao. Ni kitu chafanana sana na utashi wako. Na ni bora kulingana na utukufu wako, kumuhurumia aliye kuomba umuhurumie. Kumsaidia aliekuomba msaada uhurumie ungamo letu kwako. Tutosheleze tujitupapo mbele yako. Oh! Mola wetu hakika shetani ametusimanga, kwa kuwa tumemfuata katika kukuasi wewe. Mrehemu Muhammad na Aali zake usimwache atusimange baada ya kuwa tumemwacha kwa ajili yako. Tumemtelekeza na kuelekea kwako.

3

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

DUA YA 11

DU'A ZAKE KWA AJILI YA MWISHO MWEMA

Ewe! mwenye utajo wake ni heshima kwa wamtajao. Ewe! mwenye shukrani yake ni ufanisi kwa wenye kumshukuru. Owe! Mwenye utii wake ni uokovu kwa wenye kumtii. Mswaliye Muhammad na Aali zake. Zihangaishe nyoyo zetu katika kukutaja wewe na kuziweka mbali na utajo mwingine wote. Na zihangaishe ndimi zetu katika kukushukuru na ziwe mbali na shukuru zingine zote. Na viungo vyetu vya miili vihangaike kukutii wewe na kuwa mbali na utii mwingine wowote. Ukitupangia wakati wa faragh (usio na kazi) basi jaalia faragha iliyo salama. Tusifuatwe na lipizi baya, wala usituambatanishie humo na kuchoshwa, ili watuondokee waandishi wa maovu na nyaraka tupu zisizotaja chochote katika maovu yetu. Na warudi waandishi wa mema kutoka kwetu wakiwa na furaha na waliyoyaandika miongoni mwa mema yetu. Na ziishapo siku za maisha yetu na kumalizika kwa muda wa umri wetu. Na kutufikia wito wako ambao hapana budi utufikie na pia hapana budi kuujibu. Msalie Muhammad na Aali zake. Na jaalia mwisho wa matokeo ya hesabu ya waandishi wa mabaya yetu kuwa toba yenye kukubaliwa. Usitusimamishe na dhambi tuliyotenda baada yake, wala maasi tuliyoyafanya, wala usifichue sitara uliyotusitiri mbele ya mashahidi siku zitakapojaribiwa khabari za waja wako. Hakika wewe ni mpole kwa akuombaye na u mwenye kuitika kwa akuitaye.

DUA YA 12

DU'A ZAKE KATIKA KUKIRI NA KUOMBA TOBA KWA MUNGU MTUKUFU

Ewe Mola! tabia tatu zaniziwiya kukuomba na moja yanihimiza nikuombe, iniziwiayo jambo umeamrisha na nikazembea kulifanya. Na katazo umenikataza nikaharakia kulitenda. Na neema ulinineemesha nayo nikashindwa kuishukuru. Na linihimizalo kukuomba ni fadhila zako kwa mwenye kuelekeza uso wake kwako. Na akaja kwa dhana nzuri kwako kwa kuwa ihsani zako zote ni fadhila. Na kwa sababu neema zako zote ni mwanzo mpya. Basi mimi huyu hapa Ewee! Mola wangu mwenye kusimama kwenye mlango wa enzi yako msimamo wa aliyesalim amri dhalili.Nikikuomba nikiwa na haya ombi la fakiri hohe hahe mnyonge. Mwenye kukiri kwako, sikusalimu amri wakati wa ihsani yako isipokuwa kwa kujiweka mbali na maasi yako. Sijapata kuwa katika hali zangu zote bila ya huruma zako. Je kutanifaa ewe Mola wangu kukiri kwangu kwako kwa maovu niliyotenda? Je kutaniokoa kutambua kwangu kwako kwa mabaya niliyotenda? Au utawajibisha makasiriko yako kwangu katika kikao changu hiki? Au chukio lako litaniambata wakati wa DU'A yangu? Utakatifu ni wako, sikati tamaa nawe hali umenifungulia mlango wa toba kwako. Bali nasema usemi wa mja mnyonge mwenyekujidhulumu nafsi yake, mwenye kuifanya haramu ya Mola wake kuwa kitu chepesi. Ambaye dhambi zake zimekuwa kubwa mno. Ambaye siku zake zimemtumbia mgongo na kutokomea. Mpaka aonapo muda wa kazi ya ibada umeisha. Na upeo wa umri umekwisha. Na akawa na yakini kuwa hana njia ya kujiepusha nawe, na hana kimbilio litalomweka mbali nawe.

Akugeukia kwa marejeo ya mara kwa mara, na kufanya toba kwako kwa ikhlaswi. Atasimama mbele yako kwa moyo safi kabisa. Na kukuomba kwa sauti dhalili ya chini, ameinama mbele yako na kujipinda hali ameinamisha kichwa chake chini, woga wake watetemesha miguu yake machozi yamtiririka mashavuni mwake. Akuomba akisema Ewe mwingi wa kurehemu kuliko wote! Ewe mwingi wa kurehemu wa wanaorejea kwake wakimwomba huruma. Ewee mwenye huruma mno kwa wenye kumzunguka waombao msamaha. Ewe ambaye msamaha wake ni mwingi kuliko malipizi yake. Ewe ambaye ridhaa yake ni nyingi sana kuliko makasiriko yake. Ewe yule ambaye amesifika kwa waja wake na njema saburi njema. Ewe ambaye amewazowesha waja wake kwa kukubali marejeo yao ya mara kwa mara. Oh! yule ambaye amewarekebisha waharibifu wao kwa njia ya tobah. Oh! yule ambaye ameridhika na madogo katika matendo yao. Oh! yule ambaye huwalipa mengi kwa machache yao. Oh! yule ambaye amechukuwa dhamana kwa ajili yao kuzikubali DU'A. Oh! yule ambaye amewaahidi mwenyewe binafsi kwa fadhila zake malipo mema. Mimi sio muasi zaidi kuliko waliokuasi na umewasamehe, wala mimi si mlaumiwa mno miongoni mwa walioomba udhuru kwako na umewakubalia, wala mimi si mdhalimu mno miongoni mwa waliotubu kwako na umepokea toba yao. Natubu kwako katika kikao changu hiki toba ya mwenye kujutia waliyompita. Mwenye kutambua yaliyomzunguka, mwenye haya sana kwa yaliyo mfika, ajua kuwa kuisamehe dhambi kubwa mno haliwi jambo kubwa kwako.

Na kuyafumbia macho madhambi makubwa kabbisa haiwi ngumu kwako. kuyavumilia makosa mabaya sana ya jinai hayakupi tabu. Na yakuwa mja wako mpendwa sana kwako ni mwenye kuacha kibri mbele yako. Na akajiepusha na kung'ang'ania, kashikamana na kuomba msamaha. Nami najitakasa kwako nisiwe na kibri na ninajilinda kwako nisiwe mwenye kung'ang'ania nakuomba msamaha kwa nililozembea. Naomba msaada kwa nililohemewa ewe Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake. Nipe yaliyowajibu wangu kwako, niondolee ninayostahiki kwako. Nitakase na wayaogopayo waovu. Wewe ni mwingi wa msamaha, mwenye kutumainiwa msamaha, wajulikana kuwa umvumilivu. Haja yangu haina pakuitafutia isipokuwa kwako. Wala dhambi zangu hazina wakuzisamehe asiyekuwa wewe. Je! lawezekana hilo? Sijihofu binafsi ila kwako, hakika wewe ni mstahiki wa taqwa na mstahiki wa msamaha.Mrehemu Muhammad na Aliy zake nikidhie haja yangu. Fanikisha ombi langu. Nisamehe dhambi zangu. Nipe dhamana ya woga wa nafsi yangu hayo ni mepesi kwako, aameen ewe bwana wa maumbile yote.

DUA YA 13

DU'A ZAKE KUMWOMBA HAJA MUNGU MTUKUFU

Oh Allah. Ewe! mwisho wa maombi ya haja zote. Ewe! ambaye kupitia kwake mahitaji hupatikana. Ewe! ambaye hauzi neema zake kwa thamani. Oh! yule ambaye hakipaki tope akitowacho kwa masimbulizi. Ewe! yule ambaye hutosheka kwa kupitia kwake hatosheki mtoshekaji bila ya yeye. Ewe yule ambaye hutakiwa na hauwi utashi kando na yeye. Ewe yule ambaye hazina zake hazimalizwi na maombi. Ewe yule ambaye sababu hazibadilishi hikima yake. Oh! yule ambaye hazishi kwake haja za wahitaji. Oh! yule ambaye hayampi dhiki maombi ya waombao, umesifika kwake kutokuwa muhitaji toka kwa viumbe wako. Wewe wastahiki kuwa uwahitajii wao, umewahusisha na ufakiri wao ndio wahitaji kwako. Hivyo basi mwenye kujaribu kuziba pengo lake kupitia kwako. Na akusudia kujiondolea ufakiri kwa njia yako. Atakuwa ametafuta mahitaji yake mahali pafaapo. Na atakuwa ameyaleta mahitaji yake katika njia zake. Na mwenye kuelekeza mahitaji yake kwa yeyote miongoni mwa viumbe wako au kuifanya sababu ya kufanikiwa kwake kando na wewe atakuwa amejiweka kwenye hatari ya kunyimwa. Na atakuwa amestahiki kwako kukosa ihsani. Oh! Allah ninahaja kwako. Juhudi yangu imeshindwa, mbinu zangu zimeshindwa kuifikia nafsi yangu imenishawishi kuifikisha haja yangu kwa awezaye kuifikisha kwako. Wala hajitoshi katika mahitaji yako kando na wewe, na huku ni kuteleza miongoni mwa mtelezo wa watenda makosa na ni kujikwaa wanako jikwaa watenda madhambi. Kisha nilizinduka kwa kumbusho lako kwangu kutokana na mghafala wangu. Nimeinuka kwa taufiki yako kutoka kwenye mtelezo wangu.

Nimeimarika kwa imarisho lako na kujitoa kwenye telezo langu. Nasema subhana Rabiy (utakatifu ni wa Mola wangu), vipi muhitaji amwomba muhitaji mwingine? Ni vipi asiyekuwa na kitu amwomba asiyekuwa na kitu mwingine! Hivyo nimekuja kwako ewe Mola wangu kwa upendo, nimeyaelekeza matumaini yangu juu yako kwa kukuamini. Na nimejua kuwa mengi nikuombayo ni kitu kidogo mbele ya utajiri wako. Mazito nikuombayo ni kidogo kulinganisha na wasaa wako. Na ukarimu wako hautakuwa mdogo kwa sababu ya ombi la yeyote. Na kwa hakika mkono wako kwa utowaji uko juu kuliko kila mkono. Ewee Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake, nichukuwe kwa ukarimu wako kwa kunifadhili. Na usinichukuwe kulingana na uadilifu wako si kwa ninavyostahiki. Mimi si wa kwanza kukusihi miongoni mwa aliokusihi umempa hali ilikuwa astahiki kunyimwa. Na wala si kuwa mwombaji wa kwanza katika aliyekuomba na ukamfadhili hali ya kuwa alikuwa apaswa kunyimwa. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake. Na nikubalie ombi langu kwa wito wangu kuwa karibu. Uhurumie unyenyekevu wangu, isikilize sauti yangu, usiyakate matumaini yangu, usikate kiungo changu na wewe. Usinielekeze kwa haja yangu hii au nyingine kwa mtu mwingine. Nitilie manani ili kufanikisha ombi langu, na kidhi haja yangu ili kukipata nilichokiomba kabla sijatoka hapa niliposimama, kwa kunirahisishia kwako mimi magumu. Na uzuri wa kunikadiria kwako katika mambo yote. Mrehemu Muhammad na Jamiy yake, rehema ya kudumu na yenye kukuwa, kuendelea kusiko katika. Muda wake uwe hauna mwisho. Fanya hivyo iwe ni msaada kwangu, na iwe ndio sababu ya kufanikiwa ombi langu.Wewe ni mwenye wasaa mkarimu na miongoni mwa haja zangu ewe bwana wangu ni fulani na fulani (hapo utafanya sijda na kuisema haja yaneyewe badala fulani fulani). (Useme haya ukiwa ndani ya sijda):- Fadhila zake zimenipa raha. Ihsani yako imenionyesha njia. Nakuomba kwako na kwa Muhammad na Aliy wake ziwafikie rehma zako usinirudishe kinyume na matumaini yangu.

DUA YA 14

MIONGONI MWA DU'A ZAKE AKIFANYIWA UCHOKOZI NA AONAPO ASIYOYAPENDA TOKA KWA WADHALIMU

Ewe! ambaye hazifichiki kwake habari za waliolemewa. Oh! wee ambaye kuhusu visa vyao ahitajii ushahidi. Oh! wee ambaye msaada wake upo karibu na wadhulumiwa. Ewe! ambaye msaada wake uko mbali na wadhalimu. Unajua ewe Mola wangu alivyoniumbua (fulani bin fulani) uliyomhadharisha na amekiuka kwangu uliyomkataza. Akionyesha hali ya kutokuwa na shukrani kwa neema zako kwake. Akidanganyika na uliyomkataza. Ewe Mola! mrehemu Muhammad na Aliy zake. Mchukue aliyenidhulumu adui yangu kwa nguvu zako. Dugisha makali yake dhidi yangu kwa uwezo wako. Mshughulishe na aliyonayo, na ashindwe kumfikia amfanyiaye uadui ewe Mola! msalie Muhammad na Aliy zake, usimwachie anidhulumu. Nipe msaada mwema dhidi yake, nilinde na mfano wa vitendo vyake, usiniweke katika hali kama yake, ewe Mola! wangu mswalie Muhammad na Aliy zake. Na unisaidie dhidi yake msaada wa papo kwa papo, uwe kitulizo cha ghadhabu yangu kwake na kumaliza makasiriko yangu kumwelekea 'yeye. Ee Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake.Nifidie msamaha wako kwa dhulma yake kwangu. Nibadilishie uovu wa matendo yake kwangu iwe rehma zako kwangu. Kila chukizo kubwa liko chini kuliko ghadhabu zako. Na kila afa si sawa kulinganisha na ghadhabu zako. Ewe! Mola wangu kama ulivyonifanya nichukie kudhulumiwa, basi nilinde nisidhulumu. Ewe Mola sitolalamika kwa yeyote mbali na wewe. Na sitoomba msaada kwa hakimu ambaye si wewe. Vipi nithubutu hivyo! msalie Muhammad na Aliy zake. Iunganishe DU'A yangu na jibu, yakutanishe malalamiko yangu na mabadiliko. Ewe Mola wangu, usinifanyie majaribu ya kukata tamaa na insaafu yako. Wala usimfanyie yeye majaribu ya kujiona yuko salama na makatazo yako, asijeendelea kunidhulumu. Na kunizuia nisipate haki yangu. Mtambulishe haraka ulivyomuahidi mtenda dhulma. Na nijulishe mimi ahadi yako kuwajibu wenye kuzidiwa.

Ewe Mola msalie Muhammad na Aliy zake, unipe taufiki ya kukubali uliyoniamulia kwa faida yangu na kinyume chake, nifanye niridhie uliyochukua kwa ajili yangu na uliyoyacbukuwa kutoka kwangu.Niongoze kwenye lililo sawa, na nitumikishe kwa lililo salama. Ewe Mola ikiwa ni bora kwangu uonavyo ni kuahirisha kuchukua kwa ajili yangu na kuacha kulipiza kisasi kwa aliyenidhulumu mpaka siku ya maamuzi na mkusanyiko wa magonvi! basi msalie Muhammad na Aliy zake.Nipe nguvu kutoka kwako kwa nia ya kweli na subira ya kudumu, nilinde na utashi mbaya na pupa ya wachoyo. Nifanyie picha ya mfano moyoni mwangu wa ulicho nihifadhia miongoni mwa thawabu zako na ulilomwandalia mgomvi wangu miongoni mwa malipo yako na adhabu yako. Fanya hilo iwe ndiyo sababu ya kukinai kwangu uliyohukumu na ithbati kwangu kwa uliyoyachagua. Ameen Oh! bwana wa malimwengu hakika wewe u mwenye fadhila kubwa na wewe u muweza wa kila kitu.

DUA YA 15

NA MIONGONI MWA DU'A ZAKE (A.S.) AKIWA MGONJWA AU AKISUMBULIWA NA JAMBO AU KUPATWA NA BALAA

Oh! Mola wangu sifa njema ni zako kwa vile nipo katika hali ya salama ya kiwiliwili changu. Sifa njema ni zako kwa kuwa ndio sababu ya uele kiwili wili changu. Sijui ewe Mola wangu ni ipi katika hali mbili hizi unastahiki kushukuriwa zaidi? Na upi katika nyakati mbili hizi uliobora kukuhimidi? Je ni wakati wa siha njema ambao umenipendezesha humo riziki zako nzuri, na umenipa uzima humo nitake radhi zako na fadhila zako. Kwayo umenipa nguvu kwa yale uliyonipa taufiki katika utii wako? Au wakati wa uele ambao humo umenichuja. Na neema ambazo umenitunukia? Ili kufanya wepesi yaliyonitopea juu ya mgongo wangu miongoni mwa makosa na kunitakasa maovu niliyozama ndani yake. Na kuniongoza kwenye toba na ukumbusho wa kuondoa matendo yasiyofaa kwa njia ya neema za hapo nyuma. Na kwa yote hayo yale waliyoniandikia malaika wawili waandishi wa matendo yangu mema ambayo moyo haukuweza kuyafikiria wala ulimi haukuweza kutamka wala kiungo cha mwili hakijatenda bali ni ufadhili mtupu toka kwako kwa ajili yangu.

Na hisani miongoni mwa matendo yako ya hisani kwangu. Ewe Mola msalie Muhammad na Aliy zake. Nipendezeshe uliyoyaridhia kwangu. Nifanyie wepesi uliyoniteremshia, nitakase uchafu nilioutanguliza. Nifutie shari niliyoitanguliza. Nionyeshe utamu wa afya njema, nionjeshe hali poa ya usalama. Na jaalia kutoka kwangu kwenye uele iwe kuelekea kwangu kwenye msamaha wako. Na mgeuko wangu toka kwenye kulemewa kwangu uwe ndio mwelekeo wangu kwenye kufumbiwa macho kwako. Epuko langu toka kwenye dhiki yangu liwe kuelekea kwenye burudisho lako. Usalama wangu toka kwenye shida hii uwe kuelekea faraja yako. Hakika wewe ni msifika kwa ihsani mwingi wa ihsani na huruma. Mpaji mkarimu mwenye utukufu na wema.

DUA YA 16

DU'A ZAKE AOMBAPO KUJITOA KWENYE DHAMBI ZAKE AU AKINYENYEKEA KUOMBA MSAMAHA WA DOSARI ZAKE

Oh! wee ambaye kwa rehma zake wanaomba msaada watenda dhambi. Oh! wee ambaye kwa kukumbuka ihsani yake hukimbilia wenye dhiki. Oh! wee ambaye kwa kumwogopa hulia wakosaji. Oh! wee faraja ya kila mpweka mgeni, Oh! we mfariji wa kila mwenye huzuni. Oh! wee msaada wa kila aliyetelekezwa mpweka. Oh! we msaidizi wa kila muhitaji aliyefukuzwa. Wewe ndiye ambaye umeeneza kwa kila kitu rehma na elimu. Na wewe ndiye ambaye umemfanyia kila kiumbe awe na hisa katika neema zako. Nawe ndiye ambaye msamaha wake uko juu zaidi kuliko adhabu zake. Wewe ndiye ambaye zatiririka rehma zake mbele ya ghadhabu zake. Na wewe ndiye ambaye upaji wake zaidi kuliko nyimo lake. Na wewe ndiye ambaye viumbe wote wamefunikwa na rehema zake, wewe ndiye ambaye hapendi malipo toka kwa aliyempa. Wewe ndiye ambaye hazidishi adhabu ya aliyemuasi. Mimi ewe! Mola wangu ni mja wako ambaye uliyemuamuru kukuomba. Akasema: Labeika na niko chini ya utumishi wako. Ni hapa ewe! bwana wangu nimejitupa mbele yako. Mimi ndiye yule ambaye makosa yameuzidi uwezo wa mgongo wake. Mimi ni yule ambaye madhambi yamemaliza umri wake. Na mimi ni yule ambaye kwa ujinga wake amekuasi, hali ukiwa haukustahiki hivyo toka kwake. Je! ewe Mola wangu utamrehemu akuombaye ili nikithirishe DU'A? Au utamsamehe mwenye kukulilia ili nifanye haraka kulia. Au wewe ni mwenye kumfumbia macho mwenye kutia mchanga uso wake kwa ajili yako akijidhalilisha? Au wewe ni mwenye kumtosheleza mwenye kushitakia kwako ufakiri wake akiwa na matumaini! Ewe Mola wangu usimvunje moyo ambaye asiye mpata mpaji mwingine mbali nawewe.

Usimtelekeze asiyeweza kujitosheleza kando yako na mwingine yeyote. Ewe Mola wangu mrehemu Muhammad na Aliy zake. Usinitumpie hali nimekuelekea. Usininyime hali nimekuomba, usinipige kofi la uso kwa kunikatalia hali nimesimama mbele yako. Wewe ndiye uliyejisifu nafsi yako kwa rehema. Basi mswalie Muhammad na Aliy zake nirehemu. Wewe ndiye uliyejiita mwenyewe kuwa umsamehevu, basi nisamehe. Waona ewe Mola wangu mbubujiko wa machozi kwa kukuogopa, yote hayo ni haya nionayo kwa ubaya wa matendo yangu. Kwa ajili hiyo imezima sauti yangu kukulilia. Umebutuka ulimi wangu sinong'oni nisalipo. Ewe Mola wangu yako ni sifa njema aibu ngapi umenisitiri hukunifedhehi dhambi ngapi umezifunika kwa ajili yangu hukunifanya niwe mashuhuri kwazo. Makosa mangapi nimeyatenda wala hukunichania pazia la sitara, wala haukunibandika utepe wa chuki ya fedheha yake, wala haukudhihirisha aibu yake kwa atafutaye aibu zangu miongoni mwa majirani wangu na wenye husda ya neema zako kwangu. Hata hivyo hayakuniziwiya yote hayo nimepita kwenye maovu uliyoyajuwa kwangu. Hivyo basi ni nani mjinga zaidi wa mwongozo wake ewe Mola wangu kuliko mimi?

Nani mwenye kughafilika mno na hadhi yake kuliko mimi? Nani yu mbali sana na kuirekibisha nafsi yake kuliko mimi? Kwa kuwa naitumia riziki yako uliyoniruzuku katika mambo uliyonikataza miongoni mwa maasi yako. Nani aliyezama mbali sana katika mambo ya batili na mwenye kuyaendea maovu kuliko mimi? Nisimamapo kati ya wito wako na wito wa shetani huufuata wito wake bila kuwa niko kipofu katika kumjua wala sifanyi hivyo kwa kuwa kuna usahaulifu katika kumtambua. Hali yakuwa ninayakini kuwa mwisho wa wito wako ni peponi. Na mwisho wa wito wake ni motoni, utakatifu ni wako. Ajabu iliyoje juu ya ushahidi ni ubebao dhidi yangu mwenyewe. Na hesabu toka yaliyojificha katika mambo yangu? Ajabu kubwa kuliko hiyo ni ule upole wako kwangu na kwenda kwa utaratibu bila kuniharakishia. Hiyo si kwamba ninayo heshima kwako; bali ni uvumilivu wako kwangu, na ni fadhila zako juu yangu.Ili nijiepushe na maasi yako ya kukasirishayo, nipate mwanya wa kujing'oa toka maovu yangu yaniaibishayo. Kwa sababu kunisamehe wapendezwa sana kuliko kuniadhibu. Bali mimi ewe! Mola wangu ninadhambi nyingi sana na nyayo mbaya sana na matendo ya ovyo mno. Najitumbukiza vibaya sana katika batili. Niko dhaifu mno kuwa macho katika utii wako.

Ni mchache mno wakuzindukana na makamio yako na kuyachunga. Kwa kiasi cha kuweza kuzidhibiti aibu zangu. Au kuweza kuzikumbuka dhambi zangu kwa hayo nailaumu nafsi yangu tu nikiwa na tamaa ya huruma yako ambayo kwayo ndiyo kurekebika kwa mambo ya wenye dhambi. Na kutaraji rehma zako ambazo kwazo ndiyo ukombozi wa shingo za wakosaji. Oh! Mola hii ni shingo yangu imeshikwa utumwa na dhambi, msalie Muhammad na Aliy zake. Ikomboe kwa msamaha wako. Huu mgongo wangu umetopewa na makosa. Msalie Muhammad na Ali zake, uupunguzie uzito wake kwa huruma yako. Ewe Mola wangu lau ningekulilia mpaka zidondoke mbone za macho yangu na niliye mpaka ikatike sauti yangu. Na nisimame kwa ajili yako mpaka zifure nyayo zangu, na nirukuu kwa ajili yako mpaka ung'oke mgongo wangu, na nisujudu kwa ajili yako mpaka macho yangu yang'oke, na nile mchanga wa ardhini umri wangu wote, na ninywe maji yenye jivu mpaka mwisho wa umri wangu, na niwe na kutaja muda wote huo mpaka ulimi wangu uwe butu nisiinuwe uso wangu vyote hivyo nikikuonea haya isingewajibika kufutiwa ovu moja miongoni mwa maovu yangu. Ingawaje ulikuwa wanisamehe inapobidi nipate msamaha wako, na wanisamehe ninapostahiki msamaha wako. Kwani hilo haliwi wajibu kwa ajili yangu kwa kustahiqi wala silipati hilo kwa kuwa ni wajibu. Kwa kuwa malipo yangu toka kwako toka nilipokuasi kwa mara ya kwanza ilikuwa ni moto. Hivyo basi endapo utaniadhibu wewe sidhwalimu kwangu. Oh! Mola wangu kwa vile ulisitiri aibu yangu wala haukunifedhehi, ulinivumilia kwa ukarimu wako wala haukuniharakia. Ulinifanyia huruma kwa fadhila zako hukuibadilisha neema zako kwangu wala hukuyaboronga matendo yako mema kwangu. Hurumia unyenyekevu wangu wa muda mrefu. Na ukali wa umasikini wangu. Hali yangu mbaya. Ewe Mola msalie Muhammad na Aliy zake. Nilinde na maasi, nifanye niwe mtii, niruzuku kurejea kwako mara kwa mara, nisafishe kwa toba, nipe nguvu kwa kunilinda, nirekebishe kwa afya, nionjeshe utamu wa msamaha, nijaalie niwe niliye kombolewa kwa msamaha wako na niliyekombolewa utumwa kwa rehma zako, niandikie dhamana ya kutokasirikiwa nawe, nipe bishara ya haraka si ya baadaye bishara niitambuayo, itambulishe kwa alama nitaibainisha nayo. Hilo halikupi dhiki katika wasaa wako, wala halikusumbui katika nguvu zako, wala haliuzidi upole wako, wala haikuchokeshi katika hiba zako tukufu ambazo zimeonyeshwa na aya zako. Hakika wewe wafanya ulitakalo na wahukumu upendalo. Hakika wewe nimuweza wa kila kitu.

DUA YA 17

DU'A ZAKE(A.S) AMTAJAPO SHETANI HUJILINDA NAYE NA HUJILINDA NA UADUI WAKE NA VITIMBI VYAKE

Ewe Mola kwa hakika twajilinda kwako na mvuto wa shetani maluuni na vitimbi vyake na mitego yake. Na kuwa na matumaini ya ahadi zake.Udanganyifu wake na mawindo yake na asijipe tamaa nafsini mwake ya kutupoteza mbali na utii wako. Na kutotweza kwa sababu ya kukuasi tusije yaona kuwa ni mazuri aliyotufanya tuyaone mazuri. Na yasije onekana mazito kwetu aliyoyachukiza kwetu. Ewe Mola mtupe mbali nasi kwa njia ya ibada yako. Mtupe chini kwa upendo wetu wa kudumu kwako. Weka kati yetu na yeye kiziwizi asichoweza kukiondoa. Na kinga madhubuti hawezi ikiuka. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake. Mshughulishe awe mbali na sisi kwa baadhi ya maadui wako. Utulinde naye kwa uzuri wa uangalizi wako. Tufanye atusumbuliwi na khiyana yake, tugeuzie mgongo wake. Ukate kabisa ufuatilio wake kwetu. Ewe Mola msalie Muhammad na Ali zake. Tufurahishe kwa kutupa uongofu mfano wa upotovu wake. Tuzidishie uchamungu dhidi ya ushawishi wake. Tupitishe katika uchaji mungu kinyume na njia yake ya maangamio.

Ewe Mola usimjalie upenyo mioyoni mwetu. Usimfanyie makazi kwa yale tuliyonayo. Ewe Mola tutambulishe njia potovu atufanyiazo. Na tuitambuapo tulinde nayo tuonyeshe cha kumrubuni nacho. Tupe ilhamu ili kujiweka tayari naye tuamshe ili tutokane na sinzio la mghafala wa kumtegemea yeye. Ufanye uzuri msaada wako kwetu dhidi yake. Ewe Mola zinyweshe nyoyo zetu kuyakanusha matendo yake. Tufanyie upole kwa kutangua hila zake. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake.Yageuze mamlaka yake mbali nasi, kata matumaini yake kwetu, mziwie uchu wake kwetu, Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake.Wajaalie baba zetu, mama zetu, watoto wetu, ahli zetu, ndugu zetu wa karibu na majirani zetu miongoni mwa waumini wanaume na waumini wanawake katika ulinzi madhubuti dhidi yake. Na ngome yenye hifadhi na pango lenye kizuizi. Wavishe dhidi yake kinga iwalindayo, wape silaha dhidi yake silaha kali kali Ewe Mola waeneze hayo wenye kushuhudia kuwa wewe ndiyo Rabbu. Na akakutengea wewe umoja. Na amfanyiaye uadui (shetani) kwa ajili yako kwa hakika ya uja. Na akuomba msaada dhidi yake kwa maarifa ya elimu za kiungu.

Ewe Mola! fungua aliyoyafunga na rarua aliyoyashona. Haribu aliyoyapanga, mvunje moyo anapoazimia, yaharibu aliyoyafanya. Ewe Mola lishindishe jeshi lake, batilisha vitimbi vyake, bomoa pango lake, isuguwe pua yake chini ya ardhi. Ewe Mola! tuweke sisi katika ngazi ya maadui zake tutoe tusiwe katika idadi ya marafiki zake ili tusimtii anapotushawishi. Tusimwitikie atuitapo, tumpe amri mwenye kutii amri yetu amfanyie uadui, na tumuwaidhi ili asimfuate mwenye kufuata karipio letu. Ewe Mola! mrehemu Muhammad mwisho wa manabiy na bwana wa mitume na warehemu ahli bayt wake wema na wasafi. Na utulinde sisi na ahali zetu, ndugu zetu na jumla ya waumini wanaume na waumini wanawake, yale tuliyojilinda nayo. Na ututakase kwa yale tuliyokuomba ututakase nayo kwa hofu yake. Tusikilize tuliyokuomba na utupe tuliyoghafilika kuyaomba, ulinde na tuliyoyasahau. Kwa yote hayo tufanye tuwe katika daraja za watu wema na ngazi za waumini - Aameen ewe Mola wa ulimwengu wote.

DUA YA 18

LINDWA NA JAMBO ANALOLIHOFIA AU KUHARAKISHIWA AYATAKAYO

Oh! Mola sifa njema ni zako kwa uzuri wa utekelezaji wako. Kwa kuniondolea mitihani yako, usiijaalie hadhi yangu katika rehma zako ile ulioniharakishia katika afya yako nisije kuwa duni kwa niliyo nikiyapenda. Na mwingine awe na maisha mema kwa yale niliyoyachukia. Ikiwa hali njema niliyo nayo mchana wote au usiku wote kwa afya hii itafuatiwa na balaa isiyokoma na mzigo wa dhambi ambao usiotoweka.! Bora nitangulizie ambacho ungekichelewesha na nicheleweshee ambacho ungenitangulizia. Kwa kuwa ambacho mwisho wake ni kuteketea hakina wingi. Na ambacho matokeo yake ni kubakia hakina udogo. Msalie Muhammad na Aliy zake.

DUA YA 19

DU'A ZAKE(A.S) KUOMBA MAJI WAKATI WA UKAME

Oh! Mola tupe maji kwa kutuletea mvua. Tukunjulie rehma zako kwa mvua yako nyingi kutoka mawingu yasukumwayo kwenye mimea ya ardhi yako muwafaka kwa kuotesha katika zoni zote. Wahurumie waja wako kwa kuivisha matunda. Irudishie uhai nchi yako kwa kutungika maua. Wafanye malaika wako waheshimiwa waandishi kuwa mashahidi kwa mvua yenye manufaa toka kwako. Wingi wake uwe wa daima, mbubujiko wake uwe wa wasaa, mvua nyingi ya haraka, kwayo uirudishie uhai iliyonyauka, ukilete kwayo kinachokuja, kwayo ulete chakula nyingi, mawingu yenye kurundikana yenye kutosheleza, katika tabaka za mawingu yatoayo sauti mvua inyeshayo sio ile isiyo simama kuwe na umulikaji wenye matunda. Oh! Mola tupe mvua, yenye kusaidia, iletayo mazao yenye rutuba, yenye kuenea, nyingi, yakutosha inayotengeneza upya kilichovunjika. Oh! Mola tupe mvua, itakayofanya mawe ya mlimani yaporomoke itakayojaza visima, itakayoifanya mito itiririke, itakayootesha miti, itakayofanya bei za vitu irudi chini katika nchi zote, itakayo tia uzima wanyama na viumbe vingine, itakayotukamilishia chakula yakufaa, itakayotuoteshea mimea, itakayoongeza mtiririko wa maziwa katika chuchu za wanyama, itakayo tuongezea nguvu kwenye nguvu zetu. Ewe Mola usijaalie kivuli chake juu yetu kuwa upepo uunguzao, wala usiifanye baridi yake kwetu ya kukata, usiufanye mbubujiko wake kwetu kuwa ni pigo la mawe, wala usiyafanye maji yake kwetu kuwa ya chumvi. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake. Turuzuku miongoni mwa baraka za mbingu na ardhi. Hakika wewe u muweza wa kila kitu.


3

4

5

6

7

8