WAULIZE WANAOFAHAMU

WAULIZE WANAOFAHAMU10%

WAULIZE WANAOFAHAMU Mwandishi:
: SHEIKH MUSABBAH SHA'ABANI
Kundi: Misingi mikuu ya Dini

WAULIZE WANAOFAHAMU
  • Anza
  • Iliyopita
  • 26 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 53004 / Pakua: 6383
Kiwango Kiwango Kiwango
WAULIZE WANAOFAHAMU

WAULIZE WANAOFAHAMU

Mwandishi:
Swahili

1

2

3

4

5

6

7

13

WAULIZE WANAOFAHAMU

ABUBAKR BAADA YA UHAI WA MTUME (s.a.w.w)

NAMNA ALIVYOMPINGA BIBI FATMAH, KWA KUMNYANG'ANYA HAKI YAKE

Bukhari amethibitisha ndani ya sahih yake juzuu ya tano ukurasa 82 Kitabul-Maghazi Babu Ghaz-watukhaibar amesema: "Imepokewa kutoka kwa Ur-wah naye kutoka kwa Aisha kwamba Fatmah(a.s) binti ya Mtume(s.a.w.w) alituma ujumbe kwa Abubakr akimuomba ampe mirathi yake kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) miongoni mwa mali ambazo Mwenyezi Mungu alimpa Mtume hapo Madina na Fadak na sehemu iliyobaki katika khumsi ya Khaibar.Abubakar akasema: Bila shaka Mtume wa Mwenyezi Mungu amesema: Sisi (Mitume) haturithiwi tunachokiacha ni sadaka, hakika watakula kizazi cha Muhammad katika mali hii, na kwa hakika Wallahi sibadilishi chochote katika sadaka ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) kutoka katika hali iliyokuwa nayo katika zama za Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) na nitaitumia kama alivyoitumia Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) . Basi Abubakar akakataa kumpa chochote bibi Fatmah (a.s) na ndipo bibi Fatimah alipomkasirikia Abubakar kuhusu jambo hilo na hakumsemesha mpaka alipofariki, na aliishi miezi sita tu baada ya kufariki Mtume(s.a.w.w) ."

Bibi Fatmah alipofariki, mumewe (ambaye ni Sayyidna Ali ibn Abi Talib) alimsalia na akamzika usiku wala hakumruhusu Abubakr kuhudhuria maziko hayo. Katika uhai wa bibi Fatmah(a.s) Imam Ali(a.s) alikuwa akithaminiwa mno na watu, lakini alipofariki watu wakampuuza Imam Ali, ndipo alipotaka mapatano na Abubakar na akambai, na kabla ya miezi hiyo sita alikuwa hakumbai.

Naye Muslim ameandika ndani ya sahihi yake, juzuu ya pili Kitabul-jihad mlango unaohusu kauli ya Mtume, "La Nuurathu Mataraknahu Sadaqah" Imepokewa toka kwa Ummul-Muuminina Aisha (r.a) kwamba, baada ya kufa Mtume bibi Fatmah(a.s) binti ya Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) alimuomba Abubakr, mirathi yake katika alivyoviacha Mtume(s.a.w.w) na mali aliyompa Mwenyezi Mungu, basi Abubakar akasema: "Hakika Mtume wa Mwenyezi Mungu amesema, Haturithiwi tulichokiacha ni Sadaka ." Basi Fatmah binti ya Mtume wa Mwenyezi Mungu akakasirika na akakata mawasiliano na Abubakar na alibakia hivyo mpaka akafariki. Na aliishi miezi sita tu baada ya Mtume(s.a.w.w) , Aisha amesema: "Fatmah alikuwa akimuomba Abubakr ampe sehemu yake iliyoachwa na Mtume wa Mwenyezi Mungu katika Khaibar na Fadak na sadaka yake iliyoko Madina, basi Abubakar alimkatalia Fatmah na kusema, Siwezi kuacha chochote ambacho Mtume alikifanya ila nami nitakifanya, kwani mimi nachelea ikiwa nitaacha kitu katika mambo yake nitapotea ."

Ama sadaka ya Mtume(s.a.w.w) ya pale Madina, Umar aliitoa kwa Ali na Abbas, na ile ya Khaibar na Fadak, Umar alizizuwiya na akasema: "Hizo ni sadaka za Mtume wa Mwenyezi Mungu, zilikuwa ni haki yake ambayo inamuhusu yeye na mambo yake, usimamizi wake uko chini ya yeyote atakayetawala, basi zimebakia hivyo hadi leo ."

Pamoja na kuwa Masheikh hao wawili (Bukhari na Muslim) kuikata riwaya hii na kuifupisha ili ukweli usije ukaonekana kwa wale wanaotafiti, lengo lao wamekusudia kulinda heshima ya Makhalifa hawa watatu, na tabia hii (ya kuficha mambo) ni fani yao inayofahamika. Kuhusu (tabia hii ya) Bukhari na Muslim ndani ya maudhui hii, hivi punde Mwenyezi Mungu apendapo tutaifanyia uchambuzi na tutakutosheleza.

Jambo la kuzingatia ni kwamba, riwaya hizi ambazo wao wamezifanyia marekebisho, zinatosha sana kueleza mazingira halisi ya Abubakr ambaye alikanusha madai ya bibi Fatmah, jambo ambalo lilimfanya bibi Fatmah amkasirikie na kumsusa mpaka alipofariki, na mumewe akamzika usiku tena kwa siri kutokana na usia wa bibi Fatmah mwenyewe bila kumruhusu Abubakar (kuhudhuria mazishi hayo). Kama ambavyo tunafaidika kutokana na riwaya hizi kwamba Ali hakumpa baia Abubakar muda wote wa miezi sita ya uhai wa bibi Fatmah baada ya kufariki baba yake, na kwamba Ali(a.s) alilazimika kumbai Abubakar pale alipoona watu wamempuuza, basi akataka mapatano na Abubakar.

Na kitu walichokibadilisha Bukhari na Muslim miongoni mwa ukweli ni kuwa madai ya bibi Fatimah(a.s) kwamba baba yake ambaye ndiye Mtume wa Mwenyezi Mungu alimpa Fadak katika zama za uhai wake na hiyo siyo katika mirathi, na tujaalie kwamba Mitume hawarithiwi kama alivyoyaeleza hayo Abubakr kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) , na bibi Fatmah akayapinga maelezo hayo na akayalinganisha maelezo ya Abubakr kwenye Qur'ani ambayo inasema kuwa "Na Sulaiman akamrithi Daud ." Basi Fadak haingii katika hadithi hii inayodaiwa, kwani Fadak ni zawadi siyo miongoni mwa mirathi kwa namna yoyote ile. Kwa ajili hiyo basi utawakuta wanahistoria wote, wafasiri na watu wa hadithi wanaeleza kwamba bibi Fatmah alidai kwamba Fadak ni mali yake, na Abubakr akamkanusha na kumtaka alete ushahidi juu ya madai yake, basi akamleta Ali ibn Abi Talib na Ummu Aiman, Abubakr hakuukubali ushahidi wa hawa na akauona kuwa hautoshelezi.

Maelezo kama haya ameyakubali Ibn Hajar ndani ya As-Sawaiqul-Muhriqa pale alipoeleza kwamba bibi Fatimah alidai kwamba, Mtume(s.a.w.w) alimzawadia Fadak, na hakuleta shahidi juu ya hilo isipokuwa Ali ibn Abi Talib na Ummu Aiman kwa hiyo kiwango cha ushahidi wake hakikukamilika.

Na kama alivyosema Al-Imam Fakhrur-razi ndani ya tafsiri yake kuwa, Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) alipofariki bibi Fatmah(a.s) alidai kwamba Mtume alimzawadia Fadak, basi Abubakr akamwambia Fatmah, "Wewe ni mtu muhimu mno kwangu na ni mwenye kupendelewa mno kwangu mimi kuliko wengine, lakini mimi sielewi usahihi wa kauli yako kwa hiyo siwezi kukupa." Anasema. (Bibi Fatmah) akamshuhudisha Ummu Aiman huru wa Mtume wa Mwenyezi Mungu, lakini Abubakar akamtaka bibi Fatmah alete shahidi ambaye ushahidi wake utakubalika katika sheria, ikawa hakupatikana. Madai ya Fatimah(a.s) kwamba Fadak ni zawadi aliyopewa na Mtume(s.a.w.w) na kwamba Abubakar aliyapinga madai hayo na hakuukubali ushahidi wa Ali na Ummu Aiman, ni jambo linalofahamika kwa wanahistoria na Ibn Taimiyyah amelieleza, na mwandishi wa Siiratul-halabiyyah, na Ibnul-Qayyim Al-jauziyyah na wengineo.

Lakini Bukhari na Muslim wamelifupisha tukio hili na hawakutaja isipokuwa ombi la bibi Fatimah juu ya mirathi peke yake, ili tu wamfikirishe msomaji kwamba bibi Fatmah alimkasirikia Abubakr mahala ambapo hapakustahiki kwani Abubakr hakufanya ila kile alichokisikia kwa Mtume(s.a.w.w) , kwa hiyo bibi Fatimah alifanya dhuluma na Abubakr alidhulumiwa. Bukhari na Muslim waliyafanya vote haya ili kulinda heshima ya Abubakr bila kutilia maanani uaminifu katika kunakili wala ukweli wa hadithi ambazo zilikuwa zinaumbua aibu za Makhalifa na kuondoa uzushi na vizuwizi vilivyowekwa na Banu Ummayyah na wasaidizi wa Makhalifa, hilo hawakujali japokuwa litakuwa linaharibu heshima ya Mtume mwenyewe(s.a.w.w) au binti yake Fatmah (a.s) (bora tu Makhalifa wao wasalimike).

Ni kwa ajili hiyo tu ndiyo maana Bukhari na Muslim wamemiliki uongozi wa wanachuoni wa hadithi kwa Masunni na hao Masunni wakavizingatia vitabu vyao (Bukhari na Muslim) kuwa ndiyo vitabu sahih mno baada ya kitabu cha Mwenyezi Mungu. Huu ni uzushi usiokuwa na dalili ya kielimu na tutauchambua katika mlango maalum mpaka tuudhihirishe ukweli kwa mwenye kuutaka apendapo Mwenyezi Mungu. Pamoja na hayo sisi tunawahoji Bukhari na Muslim ambao wamezithibitisha fadhila nyingi za Fatmah(a.s) kwa mukhtasari, lakini unatosheleza kumkosoa Abubakar ambaye alimfahamu bibi Fatimah na daraja yake mbele ya Mtume(s.a.w.w) zaidi kuliko walivyomfahamu kina Bukhari na Muslim. Pamoja na hayo Abubakr alimkanusha bibi Fatmah na wala hakukubali ushahidi wake wala ushahidi wa mumewe ambaye Mtume amesema kumuhusu kwamba "Ali yu pamoja na haki, na haki iko pamoja na Ali, haki inazunguka popote azungukiapo. Na hebu tutosheke na ushahidi wa Bukhari na ushahidi wa Muslim kuhusu yale aliyoyathibitisha mwenyewe Mtume(s.a.w.w) juu ya ubora wa binti yake bibi Fatimah.

Fatmah ni Maa'sum kwa mujibu wa maandiko ya Qur'an Muslim amethibitisha ndani ya sahihi yake juzuu ya saba, mlango wa Fadhail za Ahlul-Bait. Aisha (r.a) amesema: "Mtume(s.a.w.w) alitoka asubuhi mapema akiwa amejitanda guo la sufi nyeusi, basi akaja Hasan ibn Ali akamuingiza humo, kisha akaja Husein ibn Ali naye akamuingiza pamoja naye, kisha alikuja Fatmah akamuingiza na hatimaye akaja Ali naye akamuingiza kisha akasema: "Hakika Mwenyezi Mungu anataka kukuondoleeni uchafu enyi watu wa nyumba (ya Mtume) na kukutakaseni mno." Sasa basi, ikiwa Fatmah(a.s) ni mwanamke pekee ambaye Mwenyezi Mungu amemuondolea uchafu na kumtakasa kwa kumuepusha na kila aina ya dhambi na maasi katika umma huu basi inakuwaje Abubakar anamkanusha na kumtaka ushahidi, ewe bwana unayaona hayo? Fatmah ndiye mwanamke bora miongoni mwa wanawake waumini, na ndiye mwanamke bora katika umma huu.

Bukhari amethibitisha ndani ya sahih yake juzuu ya saba katika Kitabul-isti-idhan ndani ya mlango wa Man Najaa Baina yadain-nas walam Yukhbir Bisirri Sahibih Faidha Maata Akhbara Bih, na Muslim katika Kitabul-Fadhail, Imepokewa kutoka kwa Ummul-Muuminina Aisha amesema: "Sisi wakeze Mtume(s.a.w.w) wote tulikuwa mbele ya Mtume(s.a.w.w) hapana aliyekosekana miongoni mwetu, basi Fatmah (a.s) akaja akitembea, Wallahi hapakufichikana chochote katika mwendo wake kutokana na mwendo wa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) , basi Mtume alipomuona Fatmah akasema, karibu binti yangu, kisha akamkalisha kuliani kwake au kushotoni kwake, halafu akamnong'oneza, Fatmah akalia sana. Mtume alipoiona huzuni yake akamnong'oneza kwa mara ya pili, mara Fatmah akacheka, mimi nikamwambia, Mimi ni miongoni mwa wakeze (Mtume) lakini Mtume wa Mwenyezi Mungu amekuhusisha wewe kwa jambo la siri kati yetu kisha wewe unalia.

Mtume wa Mwenyezi Mungu aliposimama nikamuuliza Fatmah, Ni jambo gani alikunong'oneza? Akasema: Siwezi kutoa siri ya Mtume wa Mwenyezi Mungu. Mtume alipofariki nikamwambia Fatmah, Nimekukusudia wewe kwa jambo ambalo nina haki nalo juu yako hujanieleza bado. Bibi Fatmah akasema, Amma sasa ni sawa kukueleza. Akanieleza akasema, Wakati aliponinong'oneza katika jambo la kwanza alinieleza kuwa, Jibril alikuwa akija kumuaridhia Qur'an kila mwaka mara moja na kwamba mwaka huu ameniaridhia mara mbili, na wala sioni isipokuwa muda umekaribia, basi mche Mungu na uwe mvumilivu, kwani mimi ndiye mtangulizi bora kwako wewe, ndipo nilipolia kilio changu ulichokiona, na alipoiona huzuni yangu akaninong'oneza mara ya pili akasema: Ewe Fatmah huridhii kuwa wewe ndiwe mwanamke bora miongoni mwa waumini au mwanamke bora wa umma huu?"

Ikiwa Fatmah(a.s) ndiye mwanamke bora kuliko wanawake wa waumini kama yalivyothibiti hayo kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu, na Abubakar anamkatalia Fatmah madai yake ya Fadak na wala hakukubali ushahidi wake, je ni ushahidi gani mwingine utakaokubalika baada yake unaoudhania ewe bwana? Fatmah ndiye mbora wa wanawake wa peponi. Bukhari amethibitisha ndani ya sahihi yake katika juzuu ya nne ndani ya Kitabu bad-il-khalq; Babu Manaqib Qarabatu Rasulillahi, Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) "Fatmah ni mbora wa wanawake wa peponi." Basi kama Fatmah ni mwanamke bora kuliko wanawake wote wa peponi, na maana yake ni kwamba yeye ni mwanamke bora ulimwenguni kwani watu wa peponi siyo ummati wa Muhammad peke yao kama inavyofahamika, sasa vipi Abubakr anamkanusha? Je, hawakudai kwamba laqab ya As-sidiq (ya Abubakr) aliipata kwa kuwa yeye alikuwa akisadikisha kila alilokuwa akilisema sahibu yake ambaye ni Mtume Muhammad, sasa ilikuwaje hakumsadiki Mtume(s.a.w.w) juu ya mambo aliyoyasema kuhusu bibi Fatmah?

Fatmah ni sehemuya mwili wa Mtume(s.a.w.w) , na Mtume hukasirika iwapo Fatmah atakasirika. Bukhari amethibitisha ndani ya sahih yake, juzuu ya nne Kitabu Bad-ilkhalq Babu Manaqib Fatmah(a.s) Bintun-nabiyyi(s.a.w.w) amesema: "Ametusimulia Abul-walid, ametusimulia Ibn Uyanah kutoka kwa Amr ibn Dinar kutoka kwa Abi Mulaikha, kutoka kwa Al-Musawar ibn Mukhrimah, kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: Fatmah ni sehemu itokanayo nami, yeyote mwenye kumkasirisha basi kanikasirisha mimi." "Fatmah ni sehemu itokanayo nami kinanikera kinachomkera na kinaniudhi kinachomuudhi."

Ikiwa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) anakasirika kwa kukasirika Fatmah na anaudhika kwa kuudhika kwake, basi maana ya maneno hayo ni kuwa yeye Fatmah ni ma'asum hatendi makosa, vinginevyo isingefaa kwa Mtume kusema namna hiyo, kwani mtu atendaye maasi uwezekano wa kumbughudhi na kumkera upo hata kama ana cheo kikubwa namna gani. kwani sheria ya Kiislamu haiangalii aliyekaribu au yule wa mbali, awe ni mwenye heshima (kubwa namna gani) au mnyonge, tajiri au masikini. Na iwapo mambo yatakuwa namna hiyo, iweje basi Abubakr asijali kukasirika kwa Fatmah mpaka akafa hali ya kuwa kamkasirikia, bali alimsusia kabisa na hakumsemesha mpaka alipofariki huku akimuombea dua (ya maangamizo) katika kila sala yake (aliyosali), kama yalivyo maelezo hayo ndani ya kitabu cha historia cha Ibn Qutaibah na wengineo mioneoni mwa wanahistoria.

Naam, hakika mambo haya ni ukweli wenye uchungu na ni ukweli unaouma ambao unatikisa nguzo na kutikisa imani, kwani mchunguzi muadilifu mwenye kujitenga kwa ajili ya kutafuta haki na ukweli hana njia isipokuwa kukubali kwamba, Abubakar alimdhulumu bibi Fatmah na akampokonya haki yake. Jambo hili lilikuwa ndani ya uwezo wake (Abubakr) akiwa ni Khalifa wa Waislamu angemridhia bibi Fatmah na ampe kile alichokidai, kwa kuwa alikuwa mkweli na Mwenyezi Mungu anashuhudia ukweli wake, na Mtume pia ashuhudia ukweli wake, na Waislamu wote akiwemo Abubakr wanashuhudia ukweli wake, ni siasa tu ndio inayogeuza kila kitu kwa hiyo mkweli huwa muongo na muongo huwa mkweli.

Naam, hakika hii ni aina mojawapo ya njama zilizofumwa ili kuwaweka kando Ahlilbait mbali na cheo na daraja ambayo Mwenyezi Mungu Mtukufu aliwapa na zilianza kwa kumuweka Ali ibn AbiTaalib kando mbali na Ukhalifa, na kupokonya zawadi ya bibi Fatmah na mirathi yake, kumfanya muongo na kumnyanyasa ili pasibakie heshima yoyote katika mioyo ya Waislamu. Njama ziliendelea mpaka Ali, Hassan na Hussein, wakauawa. Ama kwa upande wa Hussein aliuliwa yeye pamoja na watoto wake bila huruma, na akina mama waliobakia walichukuliwa mateka. Njama hizo hazikuishia hapo tu, bali Mashia wa Ahlilbait, wapenzi wao na wafuasi wao waliuliwa, na hapana shaka zingali zinaendelea hadi leo na zinafanya kazi yake na zinatoa matunda ya kazi yake. Naam Muislamu yeyote aliyehuru na muadilifu atatambua asomapo vitabu vya historia na kutafiti ukweli na kuiweka kando batili, ataona kuwa Abubakr ni wa kwanza kabisa kuwafanyia dhulma Ahlilbait, na atatosheka na kuisoma sahihi Bukhari tu vile itakapomwekea wazi ukweli endapo atakuwa mtafiti wa kweli.

Bukhari ni huyo (umjuaye) pia Muslimu, wote wanakiri kuwa Abubakar Sidiq alimkubalia sahaba yeyote yule wa kawaida tu kwa dai lake, na akamkatalia Fatuma Zahra na kuudai kuwa ni muongo hali ya kuwa Fatumah Zahra ni mwanamke bora katika wanawake wa peponi na ni yule ambaye Mwenyezi Mungu ameshuhudia kwa kumuondolea madhambi na kumfanya mtakatifu pia Abubakr alimfanya Ali kuwa ni muongo pia Umu Aiman naye akamfanya kuwa ni muongo. Hebu soma sasa uone wayasemayo Bukhari na Muslim. Bukhari ameandika katika sahihi yake juzuu ya tatu kitabu cha Shahadaati mlango wa Man amara bi injazil-waadi. Na Muslim katika sahihi yake ndani ya kitabu cha Al-fadha-il mlango wa Maasuila Rasulullahi shai-an qat, faqala -la, wakathurat a'taihi. Imepokewa kutoka kwa Jabir ibn Abdillah (r.a) amesema: Alipokufa Mtume(s.a.w.w) , kuna mali ilimfikia Abubakar kutoka kwa Al-a'laa ibn Al-Hadhrami, Abubakr akasema: Yeyote ambaye alikuwa na deni kwa Mtume(s.a.w.w) au alikuwa na ahadi kwa Mtume basi na aje kwetu, Jabir akasema, Mimi, nikasema, Mtume wa Mwenyezi Mungu aliniahidi kuwa atanipa hivi na hivi na hivi, akakunjua mikono yake mara tatu, basi zikahesabiwa mikononi mwangu mia tano, kisha mia tano, kisha mia tano."

Je, hivi kuna mtu atakayemuuliza Abubakr, "Ni kwa nini alimuamini Jabir ibn Abdallah katika madai yake kwamba Mtume(s.a.w.w) alimuahidi kumpa hivi na hivi na hivi, kisha Abubakr akaijaza mikono yake mara tatu kwa kiwango cha elfu moja mia tano bila ya kumtaka alete shahidi japo mmoja tu ili kuthibitisha madai yake? Na je Jabir ibn Abdillahi alikuwa mcha Mungu na mtakatifu mno kuliko Fatmah ambaye ni mwanamke bora ulimwenguni? Cha kushangaza kuliko yote ni kwa yeye kuukataa ushahidi wa mumewe Fatmah; Ali ibn Abi Talib ambaye Mwenyezi Mungu amemtakasa mno na akajaalia kuwa ni faradhi kwa Waislamu wote kumtakia rehma (Ali) kama wamtakiavyo rehma Mtume(s.a.w.w) . Na ni huyo huyo Ali ibn Abi Talib ambaye Mtume wa Mwenyezi Mungu amesema kuwa, "Kumpenda Ali ni (alama ya) imani na kumchukia ni (alama ya) unafiki.

Zaidi ya hayo ni kwamba, Bukhari mwenyewe amethibitisha katika tukio jingine linalotupatia picha halisi ya dhulma aliyofanyiwa bibi Fatmah na watu wa nyumba ya Mtume(s.a.w.w) . Bukhari amethibitisha ndani ya sahihi yake Baku maala yahillu liahadin an yar-jia' fi hibatih wasadaqatih, Kitabul-hibat wafadhliha wat-tahridh a'laiha: Amesema kwamba, "Watoto wawili wa Suhaib rum wa Judh'an walidai nyumba mbili na chumba kimoja na kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu alimpa vitu hivyo Suhaib, basi Mar-wan akasema: Nani atakushuhudieni juu ya madai yenu? Wakasema, Ibn Umar, Akamwita akashuhudia kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) alimpa Suhaib nyumba mbili na chumba kimoja, basi Mar-wan akaukubali ushahidi wake kwa jamaa hao" Tazama ewe Muislamu matendo haya na maamuzi haya ambayo yanatekelezwa kwa wengine na wengine yanakataliwa, je, hii siyo miongoni mwa dhulma na hila? Na ikiwa Khalifa wa Waislamu anaamua kwa faida ya wanaodai kwa kiasi tu cha ushahidi wa Ibn Umar, basi je, Muislamu anaweza kujiuliza ni kwa nini basi ushahidi wa Ali ibn Abi Talib ulipingwa pia ushahidi wa Ummu Aiman (nao ulikataliwa yeye) pamoja na Imam Ali? (Lakini ni lazima pia ufahamu kwamba) ushahidi wa mwanamume na mwanamke una nguvu kuliko ushahidi wa mwanamume mmoja peke yake ikiwa hatutataka kukifikia kile kiwango ambacho Qur'ani inakitaka.

Au tuseme watoto wa Suhaib ni wakweli mno katika madai yao kuliko Binti wa Mtume(s.a.w.w) , na kwamba Abdallah ibn Umar ni mkweli mno mbele ya watawala hao wakati ambapo Ali siyo mkweli kwa watawala hao? Ama madai yasemayo kwamba Mtume(s.a.w.w) harithiwi, nayo ni ile hadithi aliyokuja nayo Abubakar, na bibi Fatmah akaipinga kwa Kitabu cha Mwenyezi Mungu ambacho ni hoja isiyopingika kamwe, kwani imesihi hadithi kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) aliposema: "Itakapokujieni hadithi kutoka kwangu basi ipimeni kwenye Kitabu cha Mwenyezi Mungu, ikikubaliana na Kitabu cha Mwenyezi Mungu itumieni na ikienda kinyume ipigeni ukutani."

Basi hapana shaka hadithi hii inapingwa na aya nyingi katika Quran, je yuko mtu atakayemuuliza Abubakr ni kwa nini ushahidi wa Abubakr peke yake unakubalika katika riwaya ambayo inapinga aya na akili, isitoshe kitabu cha Mwenyezi Mungu kinaipinga hadithi hiyo? (Lakini jambo la kushangaza ni kwamba), ushahidi wa bibi Fatmah haukukubalika hali ya kuwa unaafikiana na nukuu na akili, na haupingani na Qur'an!! Zaidi ya hapo ni kwamba, pamoja na kuwa Abubakr daraja yake ilipanda na wanaomuunga mkono na wanaomtetea wakamtengenezea chungu nzima ya ubora, bila shaka hawezi kufikia daraja ya bibi Fatmah ambaye ni mwanamke bora ulimwenguni, wala (Abubakr) hawezi kufikia daraja ya Ali ibn Abi Talib ambaye Mtume(s.a.w.w) amemtukuza juu ya Masahaba wote katika kila nyanja, nazitaja baadhi yake kama mfano:

Siku aliyompa bendera na Mtume akamthibitisha kwamba yeye Ali anampenda Mwenyezi Mungu na Mtume wake na Mwenyezi Mungu na Mtume wake nao wanampehda Ali. Na siku hiyo Masahaba waliingojea kwa hamu kila mmoja akitaraji kupewa yeye, basi Mtume hakumpa isipokuwa Ali. Pia Mtume wa Mwenyezi Mungu alisema kuhusu Ali kwamba, "Bila shaka Ali anatokana nami, na mimi natokana naye, na yeye ni msimamizi wa kila Muumini baada yangu. Na kama watafanya shaka wang'ang'anizi na wenye chuki juu ya usahihi wa hadithi hizi, basi kamwe hawatakuwa na shaka kwamba kumtakia rehma Ali na Fatmah ni sehemu ya sala ya Mtume(s.a.w.w) , na haikubaliki sala ya Abubakr, Umar wala Uthman na wale waliobashiriwa pepo na Masahaba wote pamoja na Waislamu wote ikiwa ndani ya sala zao hakusaliwa Mtume Muhammad na kizazi cha Mtume Muhammad ambao Mwenyezi Mungu amewaondolea uchafu na akawatakasa mno, kama yalivyokuja maelezo hayo ndani ya Sihahi za Masunni zikiwemo Sahih Muslim na Bukhari na Sihah nyinginezo mpaka Imam Shafii amefikia kusema kuhusu haki yao kwamba: "Yeyote asiyekusalieni (enyi watu wa nyumba ya Mtume) mtu huyo hana sala."

Basi ikiwa watu hawa wa nyumta ya Mtume inafaa kusema uongo na kudai madai yasiyo ya kweli basi Uislamu umeingia katika mtihani Ama ukiuliza ni kwa nini ushahidi wa Abubakr unakubalika na ushahidi wa watu wa nyumba ya Mtume unapingwa? .Tawabu ni kuwa, yeye ndiye mtawala na mtawala ana uwezo wa kuamua akitakacho na kwa hali yoyote ile yeye ndiye mwenye haki, kwani madai ya mwenye nguvu ni kama madai ya mnyama mkali kwa meno na makucha aliyo nayo-kwani hiyo ndiyo-hoja yake.

Na ili ukubainikie vema ukweli wa mambo ewe msomaji mtukufu, hebu tuwe pamoja ili uyasome aliyoyathibitisha Bukhari ndani ya sahih yake kuhusu kugongana kwa suala la mirathi ya Mtume ambalo yeye Bukhari alilisema kama alivyolieleza Abubakr kwamba (Mtume kasema) "Sisi Mitume haturithiwi tunachokiacha ni sadaka." Haya ni mapokezi ambayo Masunni wote wanayakubali na kuyatolea dalili ya Abubakr kutokubali maombi ya bibi Fatmah (juu ya mirathi yake kwa Mtume). Jambo litakachokujulisha juu ya kutosihi kwa hadithi hii na kwamba haifahamiki (kwa Waislamu) ni bibi Fatmah(a.s) kudai mirathi yake, na isitoshe wakeze Mtume ambao ni mama wa waumini nao walimtumia ujumbe Abubakr wakitaka mirathi yao. Hayo ndiyo aliyoyaandika Bukhari na ndiyo yanayotolewa dalili juu ya kutokurithiwa kwa Mitume, lakini Bukhari anajipinga mwenyewe pale alipothibitisha kwamba Umar ibn Khatab aligawa mirathi ya Mtume kwa wake zake.

Amethibitisha Bukhari ndani ya sahih yake, Kitabul-Wakala, Babul-Muzara'ah Bis-shatri. Imepokewa kutoka kwa Nafi'i kwamba, Abdallah ibn Umar (r.a) alimwambia kuwa, Mtume alimuwakilisha Khaibar kwenye sehemu ambayo kunatoka matunda au mimea, basi alikuwa akiwapa wakeze Mtume mafungu mia moja na mafungu themanini yakiwa ni ya tende na ishirini ya shairi, basi Umar akaigawa Khaibar akawakhiyarisha wakeze Mtume(s.a.w.w) awakatie sehemu ya maji na ardhi au yeye awaamulie, basi miongoni mwao kuna waliochagua ardhi na kuna waliochagua shehena za tende na shairi, na Aisha alikuwa miongoni mwa waliochaguwa ardhi."

Riwaya hii inajulisha wazi kwamba Khaibar ambayo ndiyo aliyoitaka bibi Fatmah apewe sehemu yake kama mirathi yake kwa baba yake na Abubakar akamkatalia maombi yake kwa kuwa eti Mtume wa Mwenyezi Mungu harithiwi, na riwaya hii inajulisha wazi pia kwamba Umar ibn Khatab aliigawa Khaibar katika zama za Ukhalifa wake kuwagawia wakeze Mtume(s.a.w.w) na akawakhiyarisha baina ya kumiliki ardhi au shehena, na Aisha alikuwa miongoni mwa waliochagua ardhi. Basi ikiwa Mtume(s.a.w.w) harithiwi ni vipi Aisha ambaye ni mke anarithi na Fatmah ambaye ni binti asiweze kurithi? Tuelimisheni juu ya mambo kama hayo enyi wenye kufahamu nanyi mtapata ujira (mwema) na thawabu.

Zaidi ya hayo ni kwamba bibi Aisha binti Abubakr aliikalia nyumba nzima ya Mtume(s.a.w.w) na hakuna mke yeyote wa Mtume(s.a.w.w) aliyepata hadhi kama aliyopata Aisha, naye Aisha ndiye aliyemzika baba yake ndani ya nyumba hiyo ya Mtume(s.a.w.w) , na akamzika Umar karibu ya baba yake, na ni Aisha huyo huyo aliyemzuwia Husein (a.s) asimzike nduguye Hasan pembeni mwa babu yake. Jambo hili lilimfanya Ibn Abbas aseme kama ifuatavyo juu ya bibi Aisha; "Ulipanda ngamia ukapanda na nyumbu, lau utaishi zaidi utapanda tembo, yako ni sehemu moja kati ya tisa katika thumni (moja ya nane) lakini wewe yote umeitumia."

Iwe iwavyo, mimi sikusudii kurefusha maudhui hii, bali hapana budi kwa wanaotafiti kuirejea historia, lakini si vibaya nikataja sehemu ya khutuba ambayo aliitoa bibi Fatimah(a.s) mbele ya Abubakr na Masahaba wengine, ili aangamie mwenye kuangamia miongoni mwao kutokana na ukweli (kama atakataa kuutambua) na aokoke mwenye kuokoka miongoni mwao kutokana na ukweli (iwapo ataukubali).

Bibi Fatmah alisema: "Je, hivi ni kwa makusudi mumekiacha Kitabu cha Mwenyezi Mungu mkakitupa nyuma ya migongo yenu? Kwani Mwenyezi Mungu anasema: Na Sulaiman alimrithi Daudi. Na akasema akisimulia kisa kuhusu habari ya Zakariya: Basi nipe mrithi kutoka kwako atakayenirithi mimi na kuwarithi kizazi cha Ya'aqub na umfanye (mrithi huyo) ewe Mola wangu awe mwenye kukuridhisha. Na amesema Mwenyezi Mungu: Basi nipe mrithi kutoka kwako, atakayenirithi na kuwarithi kizazi cha Ya'aqub na umfanye ewe Mola wangu awe mwenye kukuridhisha. Na amesema tena: Mwenyezi Mungu anakuusiyeni juu ya watoto wenu, mwanamume apate sawa na sehemu ya wanawake wawili.

Na amesema pia kwamba: Na ndugu wa nasaba wanastahikiana wenyewe kwa wenyewe (katika kurithiana hivyo ndivyo ilivyo) katika kitabu cha Mwenyezi Mungu. Na amesema tena: Mmefaradhishiwa, mmoja wenu anapofikwa na mauti, kama akiacha mali, Aiusie kwa wazazi (wake) na jamaa zake kwa namna njema, haya ni wajibu kwa wamchao Mwenyezi Mungu." (Bibi Fatmah anaendelea kusema baada ya aya hizo za Qur'an) Je, hivi Mwenyezi Mungu amekuhusisheni ninyi kwa aya fulani na akamtoa baba yangu katika aya hizo? Au ninyi mnaijua mno Qur'an inapohusisha (kitu maalum) na inapozungumza kwa kuenea kuliko ajuavyo baba yangu na ibn ammi yangu (Ali)? Au mnasema kuwa watu wa mila mbili hawarithiani.

10

WAULIZE WANAOFAHAMU

UTENDAJI WA MASAHABA KUHUSU MAAMRISHO YA MTUME (s.a.w.w) BAADA YA KUFARIKI KWAKE

NAMNA WALIVYOIPOTOSHA SUNNA YA MTUME (s.a.w.w)

Bukhari ameandika katika Sahihi yake, juzuu ya kwanza Babu tadh-yius-salah. Imepokewa toka kwa Ghailan, Anas ibn Malik amesema: "Sikioni chochote miongoni mwa mambo ambayo yalikuwepo zama za Mtume (s.a.w.w)." Akaambiwa, "Sala (ipo)" akasema: "Je, hivi hamjaipoteza kwa kuyaacha yaliyomo ndani ya Sala ?" Na amesema: nilimsikia Az-zuhri anasema: "Niliingia kwa Anas ibn Malik alipokuwa Damascus nikamkuta analia, nikamwambia kitu gani kinakuliza? Akasema: sikioni chochote vitu nilivyovifahamu isipokuwa hii sala, na hii sala imekwisha puuzwa ." [12]

Kama ambavyo Bukhari ameandika katika juzuu ya kwanza mlango wa fadhila za sala ya alfajiri kwa jamaa, amesema: "Ametusimulia A'amash, amesema: Nilimsikia Salim, kasema:Nilimsikia Ummud-dar-dai akisema, alikuja kwangu Dar-dai hali yakuwa amekasirika, nikamwambia, Kitu gani kimekukasirisha? Akasema, Wallahi sikioni chochote katika umma wa Muhammad ila ni kwamba wote wanasali tu ."[13] .

Na ameandika Bukhari ndani ya juzuu ya pili Babul-khuruji Ilal-musalla bighair minbar kutoka kwa Abu Said Al-khudri amesema: "Mtume(s.a.w.w) alikuwa akitoka kwenda kusali siku ya Idil-fitri au Al-az'ha, basi kitu cha kwanza alichokuwa akianza ni sala kisha baada ya hapo huwapa mawaidha watu, hivyo basi watu waliendelea kufanya hivyo mpaka siku moja nilitoka na Mar-wan akiwa ndiyo amiri wa Madina, katika sala ya Idul-az-ha au Idid-fitr, basi (Mar-wan) akataka kupanda juu ya Minbar kabla ya kusali, nikaivuta nguo yake naye akaivuta kisha akapanda na akahutubu kabla ya sala, baadaye nikamwambia "Wallahi mmebadilisha.

"Akasema: "Ewe Abu Said yamekwisha toweka uyajuwayo wewe." Nikamwambia "Wallahi niyajuwayo mimi ni bora kuliko yale nisiyoyajua." Akasema: "Hakika watu walikuwa hawakai kwa ajili yetu baada ya sala, ndiyo maana mimi nikaifanya hotuba kabla ya Sala."[14] Ni vipi Masahaba katika zama za Anas ibn Malik na zama za Abud-dardai pia katika zama za Mar-wan zama ambazo ziko karibu mno na zama za uhai wa Mtume(s.a.w.w) , wanabadilisha Sunna za Mtume na kupuuza kila kitu mpaka sala kama ulivyosikia? Si hivyo tu bali wamezigeuza Sunna za Mtume(s.a.w.w) kwa maslahi yao yasiyo na maana na hasa kwa kuwa, Banu Umayyah walijitengenezea Sunna ya kumtukana na kumlaani Ali na watu wa nyumba ya Mtume. Waliwatukana juu ya mimbari kila baada ya khutba, kwa ajili hiyo watu wengi wakawa hutawanyika siku ya Idul-az-ha au Idul-fitr kila inapomalizika sala kwa kuwa walikuwa hawapendi kumsikia Imam wao anamlaani Ali ibn Abi Talib na watu wa nyumba ya Mtume. Kwa sababu hiyo basi, Banu Umayyah wakafanya makusudi hasa kubadilisha Sunna ya Mtume na wakatanguliza hotuba kabla ya Sala katika sikukuu hizo mbili ili wapate fursa ya kumtukana na kumlaani Ali mbele ya Waislamu wote na yote hayo ni kuonesha chuki yao. Kiongozi wa hawa wote ni Muawiyah ibn Abi Sufiyani, yeye ndiye aliyewawekea mwenendo huo ambao waliufanya kuwa ni miongoni mwa sunna tukufu ambayo kwayo wakijikurubishia kwa Mwenyezi Mungu.

Kuna baadhi ya wanahistoria wamesimulia kwamba, mmoja wa Maimamu wao alikamilisha hotuba yake siku ya Ijumaa na akasahau kumlaani Ali akawa anateremka kutoka kwenye mimbari ili aje kusalisha, basi ghafla watu wakawa wanapiga kelele kutoka kila upande, "Umeacha Sunna, umesahau Sunna." Sunna gani hiyo? Naam kwa masikitiko makubwa basi, hii ndiyo Bid'a iliyozushwa na Muawiyyah ibn Abi Sufiyan na ilidumu kwa miaka themanini ikizunguka kwenye mimbari za Waislamu na makovu yake yamebakia hadi leo. Pamoja na yote hayo Ahlus-Sunna Wal-Jamaa wanamuombea radhi Muawiyyah na wafuasi wake, na wala hawawezi kumkosoa wala kumtia kombo kwa madai ya kuwaheshimu Masahaba. Kila sifa njema zinamstahiki Mwenyezi Mungu, watafiti wenye moyo safi miongoni mwa Umma wa Kiislamu sasa wameanza kufahamu haki kutokana na isiyo kuwa haki, na wengi kati yao wameanza kujinasua kwenye kifungo cha masahaba ambacho hakuna aliyekitebgeneza isipokuwa Muawuya na wafuasi wake na wale wampendao. Sasa hivi Masunni wameanza kuzinduka kutokana na tatizo hili, ingawaje wakati huo wanawatetea Masahaba wote kiasi cha kumlaani mwenye kumkosoa mmoja miongoni mwa Masahaba. Iwapo Masunni utawaambia kwamba "Bila shaka laana yenu hii mnayolaani pia inamkumba Muawiya ibn Abi Sufyaan kwani yeye Muawiya kwa kufanya hivyo alikusudia moja kwa moja kumtukana Mtume wa Mwenyezi Mungu ambaye amesema: Yeyote atakaye mtukana Ali, basi hakika amenitukana mimi basi atakuwa amemtukana Mwenyezi Mungu." Basi hapo utawaona wanachanganyikiwa na kushindwa kujibu na hatimaye husema vitu ambavyo ikiwa vina maana Fulani basi maana hiyo itakuwa ni mawazo duni na ung'anga'nizi wa kipofu ambao unakera.

Kwa mfano baadhi yao husema: Huu ni uongo uliofanywa na Shia, na baadhi yao husema, Ee Bwana hao ni Masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) wanao uhuru wa kuwasema Masahaba wenzao namna watakavyo, amma sisi hatuna daraja hata ya kuwakosoa. Umetakasika ewe Mwenyezi Mungu na sifa njema ni zako, kwa hakika maneno yako yamenifahamisha katika Qur'an Tukufu juu ya ukweli ambao ilikuwa vigumu mimi kuufahamu na kuuamini, na kila nilipokuwa nikisoma maneno yako yasemayo kwamba:

وَلَقَدْ ذَرَأْنَا لِجَهَنَّمَ كَثِيرًا مِّنَ الْجِنِّ وَالْإِنسِ لَهُمْ قُلُوبٌ لَّا يَفْقَهُونَ بِهَا وَلَهُمْ أَعْيُنٌ لَّا يُبْصِرُونَ بِهَا وَلَهُمْ آذَانٌ لَّا يَسْمَعُونَ بِهَا أُولَـٰئِكَ كَالْأَنْعَامِ بَلْ هُمْ أَضَلُّ أُولَـٰئِكَ هُمُ الْغَافِلُونَ ﴿١٧٩﴾

Na bila shaka tumewaumbia moto wa Jahannam wengi katika majini na wanadamu (kwani) wanazo nyoyo lakini kwa nyoyo hizo hakuna wanachokifahamu, na wanayo macho, lakini hawaoni kwa macho hayo, na wanayo masikio lakini hawasikii kwa masikio hayo. Basi hao ni kama wanyama, bali wao ni wapotofu zaidi, hao ndio walioghafilika" (Qur'ani, 7:179).

Nisomapo maneno hayo nashangaa moyoni mwangu na ninasema ni vipi itakuwa hivyo? Je, inawezekana mnyama asiyesema akawa ameongoka kuliko mtu? Inawezekana mtu akachonga jiwe kisha akaliabudia na kuliomba riziki na msaada? Lakini namshukuru Mwenyezi Mungu, kushangaa kwangu kumetoweka baada ya kupanuka mawasiliano yangu na watu, na niliposafiri kwenda India nimeona maajabu makubwa, nimewaona madaktari katika elimu ya viumbe wanaofahamu umbile la mtu na viungo vyake. lakini bado wanaabudu ng'ombe, lakini lau jambo hili baya lingefanywa na watu wajinga miongoni mwa Wahindu udhuru wao ungekubalika, lakini utamuona mwana taaluma mzuri miongoni mwao anaabudia ng'ombe, jiwe, bahari, jua na mwezi!! Kwa hali hii huna la kufanya baada ya (kuona haya) isipokuwa ukubali na ufahamu maana inayojulishwa na Qur'ani kuhusu watu ambao wao ni wapotevu mno kuliko mnyama.

Ushahidi wa Abud-dharri kuhusu baadhi ya Masahaba Bukhari ameandika ndani ya juzuu ya pili mlango wa Man ud-diyat Zakatuhu falaisa Bikanzin, Imepokewa kutoka kwa Al-Ahnaf ibn Qais amesema: "Nilikaa na watu miongoni mwa Maquraishi, basi alikuja mtu mwenye nywele na nguo zilizochakaa pia na hali yake mpaka akasimama mbele yao akasalimia kisha akasema, Wabashirie kuwa (watachomwa) kwa mawe yaliyochemshwa katika moto wa jahannam, kisha yatawekwa juu ya chuchu ya maziwa ya mmoja wenu na kutokea kwenye sehemu inayoanzia shingo katika bega na kuwekwa (tena) kwenye sehemu inayoanzia shingo katika bega na kutokea kwenye chuchu, kisha (mtu huyo) akageuka na akakaa kwenye nguzo, nami nikamfuata nikakaa naye na hali yakuwa simfahamu kuwa ni nani, basi nikamwambia mimi sioni isipokuwa jamaa wamechukizwa kwa maneno uliyoyasema. Akasema: Bila shaka hao hawafahamu chochote, kipenzi changu aliniambia ndiye aliyeniambia... Mimi nikamwambia ni nani huyo kipenzi chako?

Akasema Mtume(s.a.w.w) aliniambia: Ewe Abudharri wauona (mlima wa) Uhd? Nikaliangalia jua na muda wa mchana uliobakia na hali ya kuwa nahisi kwamba Mtume anataka kunituma kwa shida aliyonayo, nikamwambia, Naam, Akasema: Mimi sipendi kuwa na dhahabu mfano wa Uhud (bali nikiwa nayo) nitaitoa yote isipokuwa dinari tatu. Watu hawa hawana akili, bali wanaikusanya (mali ya) dunia, hapana Wallahi siwaombi dunia yao wala sitaki wanilipie deni mpaka nitakapokutana na Mwenyezi Mungu Mtukufu[15] .

Bukhari pia ameandika katika juzuu ya saba, Babul-haudh Waqaulullahi Taala In-naa A'atainakal-kawthar. Imepokewa toka kwa At'a ibn Yasar kutoka kwa Abu Hurairah kwamba, Mtume(s.a.w.w) amesema: "Kuna wakati mimi nitakuwa nimesimama (siku ya Qiyama), ghafla watafika jamaa, nami nitakapowatambua atatokea mtu kati yangu na wao, atasema Njooni, Mimi nitasema, Waende wapi? Atasema Wallahi motoni, Nitasema Yalikuwaje mambo yao? Atasema, Hakika wao waligeuka baada yako kinyumenyume.

Kisha jamaa wengine watafika mpaka nitapowafahamu, atatoka mtu kati yangu na wao atasema, Njooni, Nitasema waende wapi? Atasema Wallahi motoni, Nitasema Yalikuwaje mambo yao? Atasema: Hakika wao waligeuka baada yako kinyumenyume, Sitamuona miongoni mwao anayesalimika isipokuwa wachache tu." Na imepokewa kutoka kwa Abu Said Al-khudri kwamba: Siku hiyo patasemwa: "Bila shaka wewe hufahamu waliyoyazusha baada yako, basi mimi nitasema na aangamie, aangamie aliyebadilisha baada yangu."[16]

Kama alivyoandika Bukhari katika juzuu ya tano mlango wa Ghaz-watul-Hudaibiyyah na kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu isemayo, "Kwa hakika Mwenyezi Mungu amewapa radhi Waumini waliofungamana nawe chini ya mti." Imepokewa kutoka kwa Al-alaa ibn Al-musayyab naye kapokea kwa baba yake amesema: "Nilikutana na Al-barra ibn A'zib (r.a) nikamwambia, pongezi wewe ulisuhubiana na Mtume(s.a.w.w) na ukampa baia chini ya mti, akasema, Ewe mtoto wa ndugu yangu hakika wewe hujuwi tuliyoyazua baada yake."[17]

Na huo ni ushahidi mkubwa utokao kwa Sahaba mkubwa ambaye kwa uchache alikuwa mkweli kwa nafsi yake na watu, na ushahidi wake unakuja kutia nguvu maneno aliyoyasema Mwenyezi Mungu kuwahusu Masahaba alipowaambia, "(Muhammad) akifa au akiuawa mtageuka nyuma kwa visigino vyenu." Na unatia nguvu maneno aliyoyasema Mtume(s.a.w.w) , "Nitaambiwa, hakika wao walirudi baada yako kinyume nyume." Huyu Al-barraa ibn Azib ni Sahaba Mtukufu miongoni mwa wale wa mwanzo ambao walimpa baia Mtume(s.a.w.w) chini ya mti, yeye anaishuhudia nafsi yake na za wengine miongoni mwa Masahaba kwamba, wao walizusha baada ya kufa Mtume(s.a.w.w) ili watu wasije danganyika kutokana na Masahaba, na alibainisha wazi kwamba kuwa sahaba wa Mtume(s.a.w.w) na kumpa baia chini ya mti ambako kumeitwa kuwa ni Baia'tur-ridh-wan vitu hivi havizuwii Sahaba kupotoka na kuritadi baada ya Mtume(s.a.w.w) .

Bukhari ameandika katika juzuu ya nane mlango wa kauli ya Mtume(s.a.w.w) isemayo. Mtafuata mwenendo wa watu waliopita kabla yenu. Imepokewa kutoka kwa Ataa ibn Yasar, kutoka kwa Abu Said Al-Khudri naye kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) amesema: "Mtafuata mwenendo wa waliopita kabla yenu hatua baada ya hatua na dhiraa baada ya dhiraa, mpaka hata wakiingia kwenye shimo la kenge nanyi mtawafuata." Tukamwambia Mtume, "Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu hao ni Mayahudi na Wakristo?" Mtume akasema, "Ni kina nani basi (kama si hao)?" [18] Ushahidi wa historia kuhusu Masahaba Baada ya Qur'ani na Sunna tunao ushahidi mwingine ambao huenda ukawa bayana na wazi zaidi, kwani unatambulikana kwa watu walioishi katika kipindi hicho na wakaushuhudia na kuwa nao sambamba, na hatimaye ukawa ni historia na ni matukio yaliyohifadhiwa. Tutaposoma vitabu vya historia vya Ah-lusunna Wal-Jamaa kama vile Tabari, Ibnul-Athir, Ibn Sa'ad, Abul-Fidai, Ibnu Qutaibah na wengineo tutaona maajabu makubwa na tutafahamu kwamba, wayasemayo Masunni juu ya uadilifu wa Masahaba na kwamba haifai kumkosoa yeyote miongoni mwao ni maneno yasiyoweza kusimamisha dalili,wala akili iliyosalimika haiwezi kukubali isipokuwa (kwa watu) wang'ang'anizi ambao kiza limewazibia mwangaza kiasi ambacho hawawezi kutofautisha baina ya Mtume Muhammad ambaye ni Ma'asum, hatamki kwa matamanio na wala hafanyi kitu isipokuwa ni cha haki tu. Wanashindwa kutofautisha kati yake na Masahaba wake ambao Qur'ani imeshuhudia juu ya unafiki na uovu wao na uchache wa uchamungu walionao, ndiyo maana utawaona Masunni wanawatetea Masahaba zaidi ya vile wanavyomtetea Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) .

Nakupigia mfano kuhusu hilo. Wakati unapomwambia mmoja wao kwamba (maonyo yaliyomo katika) Sura ya Abasa Watawalla hayakukusudiwa kwa Mtume(s.a.w.w) , bali aliyekusudiwa ni mmoja wa Masahaba wakubwa ambaye Mwenyezi Mungu alimlaumu kwa kiburi chake na kuchukizwa kwake alipomuona yule kipofu masikini. Hapo utamuona (Sunni) hakubaliani na tafsiri hii na atasema, "Muhammad hakuwa ila ni mtu tu, kwani ni mara nyingi alikosea na Mola wake akamlaumu mahala pengi tu, yeye hakuhifadhika isipokuwa katika kufikisha Qur'ani. Basi huu ndiyo mtazamo wa Masunni kumhusu Mtume wa Mwenyezi Mungu. Lakini iwapo wewe utasema kwamba, "Umar ibn Khatab alikosea alipozusha sala ya tarewehe ambayo Mtume wa Mwenyezi Mungu alikataza isisaliwe Msikitini na akawaamuru watu wasali majumbani mwao mmoja mmoja sala ya sunna (yaani isiyo ya faradhi), hapo utamuona Sunni anamtetea Umar ibn Khatab kwa nguvu na hakubali majadiliano bali atasema: "Hiyo ni Bid'a nzuri", na atajaribu kwa juhudi zake zote kumtafutia sababu (ya kumuepushia kosa) pamoja na kuwepo kwa tamko la Mtume(s.a.w.w) inalokataza.

Na ukimwambia kwamba, "Umar alizuwia haki ya Muallafatul-Qulubi haki ambayo Mwenyezi Mungu aliipitisha ndani ya Kitabu chake kitukufu." Pia utamuona anasema, "Bila shaka Bwana wetu Umar alifahamu kwamba Uislamu umekwishapata nguvu, ndiyo maana aliwaambia hao wanaoimarishwa nyoyo zao katika dini kwamba: Hatuna haja nanyi, naye (Umar) alikuwa akifahamu maana za Qur'ani zinavyoeleza kuliko watu wote! Loh! (ewe bwana) halikushangazi jibu kama hili? Kuna mtu mmoja miongoni mwa Masunni kwa hakika yeye amevuka mpaka pale nilipomwambia; "Hebu tuachane na Bid'a nzuri na hao wanaoimarishwa nyoyo zao katika dini, Je, utamteteaje Umar pale alipoanza kutoa onyo kwamba angeliichoma moto nyumba ya Bibi Fatmah pamoja na waliomo, isipokuwa (watasalimika tu) iwapo watatoka kwenda kula kiapo cha utii (kwa Abubakr)?" Huyu bwana alinijibu wazi wazi (bila woga akasema): "Anayo haki (ya kufanya hivyo) kwani lau asingefanya hivyo watu wengi miongoni mwa Masahaba wangejizuwia (kutoa baia) wakabaki kwa Ali ibn Abi Talib na fitina ingetokea." Watu kama hawa kuzungumza nao haisaidii wala kunufaisha kitu, na kwa masikitiko makubwa nasema kwamba, "Wengi wa Masunni wana mawazo ya aina hii, kwani wao hawaitambui haki isipokuwa kupitia kwa Umar ibn Khatab na matendo yake, kwa hiyo wameigeuza kanuni na wakawa huitambua haki kupitia kwa watu, wakati kinachotakiwa ni kuwatambua watu kupitia kwenye haki. Itambue haki utawatambua watu wa haki kama alivyosema Imam Ali(a.s) .

Kisha kanuni hii imeenea kwa Masunni na ikamvuka Umar ibn Khatab mpaka ikawafikia Masahaba wote, na wote ni waadilifu haiwezekani kwa mtu yeyote kuwakosoa au kuwapinga, kwa maana hiyo basi Masunni wameweka pazia zito na kizuwizi kigumu kwa mchunguzi anayetaka kufahamu haki, utamuona hawezi kukwepa wimbi moja mpaka yanapomkumba mawimbi mengi na hawawezi kukwepa hatari yeyote mpaka hatari nyingi zinapozuia njia yake, na masikini hawezi kufikia ukingoni kwa amani isipokuwa atapokuwa miongoni mwa wenye azma, subira na ushujaa. Tukirudi kwenye maudhui ya historia ni kwamba, baadhi ya Masahaba wamevuliwa nguo zao, siri zao za moyoni kukashifika na ulidhihiri ukweli wao ambao walijaribu kwa juhudi zao zote kuuficha mbele za watu, au watetezi wao na wafuasi wao walijaribu kuuficha au unaweza kusema kuwa watawala waovu na mashabiki wao ndiyo waliojaribu kila namna kuficha ukweli huo. Kitu cha kwanza kukitupia macho ni msimamo wa Masahaba hawa juu ya Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) waliouonyesha mapema baada ya kufariki kwake, na ni vipi walimuacha na hawakushughulika kumuandaa, kumkosha na wala kumvika sanda na hatimaye kumzika, bali walikimbilia kwenye mashauriano yao katika Klabu ya Bani Saidah, wakagombana na kushindana ni nani aupate Ukhalifa ambao walikuwa wakimfahamu fika muhusika wake kisheria ambaye walikula kiapo cha utii kwake katika zama za uhai wa Mtume(s.a.w.w) .

Kinachotuthibitishia kwamba watu hawa waliitumia fursa ya kutokuwepo kwa Ali na Bani Hashim ambao utu wao haukuwapa nafasi ya kuuacha mwili wa Mtume(s.a.w.w) ukiwa umefunikwa eti tu wakagombee Ukhalifa katika Saqifah, kwa ajili hiyo jamaa hawa wakapitisha haraka haraka maamuzi kuhusu Ukhalifa kabla Bani Hashim hawajamaliza kazi yao tukufu ya kumuandaa Mtume kwa ajili ya mazishi ili hatimaye wawalazimishe kukubali matokeo hayo, na wasiweze kusema chochote wala kutoa hoja hasa kwa kuwa jamaa hao waliokuwa Saqifa walikwisha kukubaliana kumuua yeyote atakayejaribu kutengua kile walichokipitisha, eti kwa madai ya kuwadhibiti wapinzani na kutuliza machafuko. Wanahistoria wanaeleza mambo ya ajabu yaliyotokea katika siku hizo yaliyofanywa na hao Masahaba ambao baadaye walikuwa ndiyo Makhalifa wa Mtume(s.a.w.w) na pia wakawa ndiyo maamiri wa Waumini. Miongoni mwa mambo hayo ni kama vile kuwalazimisha watu kutoa Baia (kiapo cha utii) kwa kuwapiga na kuwatisha kwa nguvu na kuihujumu nyumba ya Bibi Fatmah kisha kuikashifu nyumba hiyo na pia kumbana tumbo lake (Bibi Fatimah) kwenye mlango ambao alikuwa yuko nyuma yake mpaka mimba yake ikaporomoka.

Si hivyo tu bali walimtoa nje Ali hali ya kuwa kafungwa na kumuonya kuwa watamuua iwapo atakataa kutoa Baia, na walimpokonya Bibi Fatmah haki zake ikiwa ni pamoja na zawadi (ya Fadak) na mirathi yake na sehemu ya Qaraba wa Mtume kiasi kwamba, Bibi Fatimah amekufa hali ya kuwa amewakasirikia waliomfanyai hayo na akiwaombea katika kila Sala (waangamizwe), na (Mwana Fatmah) alizikwa usiku tena kwa siri na hao jamaa hawakuhudhuria jeneza lake!! Vile vile jamaa hao wa Saqifah, waliwaua Masahaba waliokataa kutoa zaka kwa Abubakr kutokana na kusita kwao ili tu wafahamu sababu za Ali kutokuwa Khalifa, kwani wakijuwacho wao ni kuwa yeye ndiye waliyempa Baia (ya kuwa Khalifa wao) zama za uhai wa Mtume(s.a.w.w) huko kwenye Bonde la Khum. Pia miongoni mwa mambo waliyoyafanya ni kama vile kuhalalisha mambo ya haramu, kuivuka mipaka ya Mwenyezi Mungu na kuwaua watu wema miongoni mwa Waislamu kisha wakawaingilia wake zao bila kuheshimu kipindi cha Eda. Walibadilisha hukumu za Mwenyezi Mungu na Mtume wake zilizojengeka kwa msingi wa Kitabu Qur'an na Sunnah wakaweka badali yake hukumu za ijitihadi zitakazotumikia maslahi yao binafsi.

Na kama vile kunywa kwao pombe na kudumu kwenye zinaa hali yakuwa ni viongozi wa Waislamu na ni watawala ndani ya Waislamu, vile vile kumuondosha Abudharri Al-Ghifari na kumfukuza kutoka Madina mji wa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) mpaka akafa akiwa peke yake (na alifanyiwa hivyo) bila ya kosa lolote alilolitenda, walimpiga Ammar mpaka wakampasua, walimpiga Abdallah ibn Mas-udi mpaka wakamvunja mbavu zake, na pia wakawauzulu Masahaba wema kwenye madaraka na kuwatawalisha waovu miongoni mwa Banu Umayyah ambao ni maadui wa Uislamu. Na (miongoni mwa mambo yao) ni kama vile kuwatukana na kuwalaani watu wa nyumba ya Mtume ambao Mwenyezi Mungu amewaondolea uchafu na amewatakasa mno, na pia kuwaua wale wanaowafuata watu wa nyumba ya Mtume miongoni mwa Masahaba wema. Na kama vile kukalia kwao Ukhalifa kwa shinikizo la nguvu, mauaji, vitisho na kumdhibiti yeyote anayewapinga kwa njia mbali mbali kama vile kumuua kwa kumvamia au kumtilia sumu na mengineyo. Na miongoni mwa hayo ni kuushambulia mji wa Mtume kwa jeshi la Yazid. likafanya lilivyotaka bila kujali kauli ya Mtume aliyosema: "Bila shaka mji wangu huu wa Madina ni mji mtukufu, basi yeyote atakayezua ndani yake tukio la uovu laana ya Mwenyezi Mungu na Malaika na watu wote iwe juu yake." Na kama vile kuipiga kwao nyumba ya Mwenyezi Mungu kwa Manjaniq na kuichoma moto nyumba hiyo tukufu ya Mwenyezi Mungu, na ndani yake waliwaua baadhi ya Masahaba.

Na kama vile kumpiga kwao vita Amirul-Muumina Ali ambaye ni Bwana wa Mawasii na ndiye kiongozi wa kizazi kitukufu ambaye mbele ya Mtume wa Mwenyezi Mungu alikuwa na cheo cha Harun kwa Musa, (walimpiga vita) katika vita vya Jamal, vita ya Siffin, na vita ya Nah-rawan (yote hayo) kwa sababu ya tamaa duni na dunia yenye kutoweka. Na kama vile kuwaua mabwana wawili wa vijana wa peponi, Imam Hasan kwa kumtilia sumu na Imam Husein kwa kumchinja, haikuwatosha hali hiyo bali walikiandama na kukiuwa kizazi cha Mtume(s.a.w.w) chote, na hakusalimika isipokuwa Ali ibn Husein, na matendo yao mengine yanayomfanya mtu atoe machozi, nami naiepusha kalamu yangu isiyaandike. Masunni wanayajua mengi miongoni mwa hayo na ndiyo maana huwa wanajaribu kwa juhudi zao zote kuwazuiwia Waislamu kusoma vitabu vya historia na kuchunguza maisha ya Masahaba. Niliyoyataja sasa hivi kutoka katika vitabu vya historia miongoni mwa maovu na machafu hapana shaka ni matendo ya Masahaba, basi haiwezekani kwa mtu mwenye akili baada ya kuyasoma haya akaendelea kuwatakasa masahaba na kuhukumu kuwa wao ni waadilifu ila kama atakuwa hana akili. Pamoja na yote tuliyoyayaeleza sisi tunangalia kwa makini mno na, tunauthamini uadilifu wa baadhi ya Masahaba na usafi wao, uchamungu wao na kumpenda" kwao Mwenyezi Mungu na Mtume wake(s.a.w.w) , na msimamo wao zama za Mtume(s.a.w.w) mpaka walipokufa na hawakubadilisha kamwe, basi Mwenyezi Mungu awaridhie na awape makazi karibu na mpenzi wao na Mtume wao Muhammad(s.a.w.w) .

Masahaba hawa ni watukufu na ni bora, hawezi kuifedhehesha heshima yao mfedheheshaji, au akawazulia mwenye kuzua, na kwa hakika Mwenyezi Mungu Mtukufu amewasifu mahala pengi ndani ya Kitabu chake kitukufu, kama ambavyo Mtume ameutukuza usuhuba wao na ikhlasi yao si mara moja. Na kama ambavyo historia haikusajili kwao isipokuwa msimamo Mtukufu uliojaa utu, wema, ushujaa, uchamungu na kujinyima (mambo ya dunia) kwa ajili ya dhati ya Mwenyezi Mungu. Basi pongezi ni zao na marejeo yao ni kwenye mabustani ambayo milango yake iko wazi kwa ajili yao na radhi ya Mwenyezi Mungu kwao ni kubwa na hayo ndiyo malipo ya wenye kushukuru, na wenye kushukuru kama kilivyosema Kitabu cha Mwenyezi Mungu. usisahau kuwa ni wachache mno. Ama wale waliojisalimisha na imani haikuingia mioyoni mwao na wakasuhubiana na Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) kwa tamaa (ya mambo fulani) na kwa khofu au kwa haja ya nafsi zao, Qur'ani imewalaumu na kuwaonya, naye Mtume(s.a.w.w) amewahadharisha na amewalaani mahala pengi, na historia nayo imeyasajili matendo yao na misimamo yao mibaya. Watu hawa basi, hawastahiki heshima ya aina yoyote wala cheo chochote, achilia mbali kuwatakia radhi (kitu ambacho kinafanya) tuwaweke daraja ya Mtume na Mashahidi na watu wema. Kwa hiyo basi, huu ndiyo msimamo wa haki ambao unapima mizani kwa uadilifu wala hauchupi mipaka aliyoiweka Mwenyezi Mungu kwa waja wake kwamba, wawatawalishe (viongozi) waaminifu na wawapinge (viongozi) waovu na wajitenge nao mbali. Mwenyezi Mungu anasema:"

أَلَمْ تَرَ إِلَى الَّذِينَ تَوَلَّوْا قَوْمًا غَضِبَ اللَّـهُ عَلَيْهِم مَّا هُم مِّنكُمْ وَلَا مِنْهُمْ وَيَحْلِفُونَ عَلَى الْكَذِبِ وَهُمْ يَعْلَمُونَ ﴿١٤﴾ أَعَدَّ اللَّـهُ لَهُمْ عَذَابًا شَدِيدًا إِنَّهُمْ سَاءَ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿١٥﴾ اتَّخَذُوا أَيْمَانَهُمْ جُنَّةً فَصَدُّوا عَن سَبِيلِ اللَّـهِ فَلَهُمْ عَذَابٌ مُّهِينٌ ﴿١٦﴾ لَّن تُغْنِيَ عَنْهُمْ أَمْوَالُهُمْ وَلَا أَوْلَادُهُم مِّنَ اللَّـهِ شَيْئًا أُولَـٰئِكَ أَصْحَابُ النَّارِ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ ﴿١٧﴾ يَوْمَ يَبْعَثُهُمُ اللَّـهُ جَمِيعًا فَيَحْلِفُونَ لَهُ كَمَا يَحْلِفُونَ لَكُمْ وَيَحْسَبُونَ أَنَّهُمْ عَلَىٰ شَيْءٍ أَلَا إِنَّهُمْ هُمُ الْكَاذِبُونَ ﴿١٨﴾ اسْتَحْوَذَ عَلَيْهِمُ الشَّيْطَانُ فَأَنسَاهُمْ ذِكْرَ اللَّـهِ أُولَـٰئِكَ حِزْبُ الشَّيْطَانِ أَلَا إِنَّ حِزْبَ الشَّيْطَانِ هُمُ الْخَاسِرُونَ ﴿١٩﴾ إِنَّ الَّذِينَ يُحَادُّونَ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ أُولَـٰئِكَ فِي الْأَذَلِّينَ ﴿٢٠﴾ كَتَبَ اللَّـهُ لَأَغْلِبَنَّ أَنَا وَرُسُلِي إِنَّ اللَّـهَ قَوِيٌّ عَزِيزٌ ﴿٢١﴾لَّا تَجِدُ قَوْمًا يُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ يُوَادُّونَ مَنْ حَادَّ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ وَلَوْ كَانُوا آبَاءَهُمْ أَوْ أَبْنَاءَهُمْ أَوْ إِخْوَانَهُمْ أَوْ عَشِيرَتَهُمْ أُولَـٰئِكَ كَتَبَ فِي قُلُوبِهِمُ الْإِيمَانَ وَأَيَّدَهُم بِرُوحٍ مِّنْهُ وَيُدْخِلُهُمْ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا رَضِيَ اللَّـهُ عَنْهُمْ وَرَضُوا عَنْهُ أُولَـٰئِكَ حِزْبُ اللَّـهِ أَلَا إِنَّ حِزْبَ اللَّـهِ هُمُ الْمُفْلِحُونَ ﴿٢٢﴾

Je, huwaoni wale ambao wamewatawalisha watu aliowakasirikia Mwenyezi Mungu? Hao si miongoni mwenu wala si miongoni mwao, na huapa viapo vya uongo na hali wanajua kuwa ni uongo. Mwenyezi Mungu amewaandalia adhabu kali, kwa hakika waliyokuwa wakiyatenda ni mabaya kabisa. Wamefanya viapo vyao kuwa ngao (yao) wakawazuwia (watu) njia ya Mwenyezi Mungu, basi watapata adhabu ifedheheshayo, mali zao na watoto wao hawatawafaa kitu mbele ya Mwenyezi Mungu, hao ndiyo watu wa motoni watakaa humo milele. (Wakumbushe) siku atakayowafufua Mwenyezi Mungu wote wamuapie (viapo vya uongo) kama wanavyoapa kwenu na wanadhani ya kwamba wamepata kitu! Kwa hakika wao ndio waongo kabisa. Shetani amewatawala akawasahaulisha kumkumbuka Mwenyezi Mungu, hao ndiyo kundi la shetani, fahamuni kwamba bila shaka kundi la shetani ndilo lenye kupata hasara. Hakika wale wanaompinga Mwenyezi Mungu na Mtume wake hao ndiyo miongoni mwa watakaodhalilika. Mwenyezi Mungu amekwishaandika yakuwa bila shaka nitashinda Mimi na Mitume wangu, hakika Mwenyezi Mungu ni mwenye nguvu, mwenye kushinda. Huwezi kuwakuta watu wanaomuamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho kuwa wanawapenda wale wanaompinga Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hata kama watakuwa ni baba zao au watoto wao au ndugu zao au jamaa zao, hao ndiyo ambao Mwenyezi Mungu ameithibitisha imani nyoyoni mwao na akawatia nguvu kwa roho itokayo kwake, na atawaingiza katika mabustani yapitayo mito ndani yake, humo watakaa daima, Mwenyezi Mungu amewawia radhi na wao wanamridhia, hao ndiyo kundi la Mwenyezi Mungu, Fahamuni! bila shaka kundi la Mwenyezi Mungu ndilo lenye kufaulu, (58:14-22).

Arnesema kweli Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Nami siachi fursa kuandika katika makusudio haya kwamba, Mashia ndiyo wako kwenye ukweli, kwani wao hawampendi yeyote isipokuwa ni kwa ajili ya Mtume Muhammad na watu wa nyumba yake na Masahaba waliopita kwenye njia ya Mtume na watu wa nyumba yake, na ( hawa Mashia wanawapenda) waumini ambao waliwafuata hao kwa wema mpaka siku ya mwisho. Amma wasiokuwa Mashia miongoni mwa Waislamu wanawapenda Masahaba wote bila kujali wanaompinga Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na mara nyingi hutolea ushahidi kauli ya Mwenyezi Mungu isemayo:

وَالَّذِينَ جَاءُوا مِن بَعْدِهِمْ يَقُولُونَ رَبَّنَا اغْفِرْ لَنَا وَلِإِخْوَانِنَا الَّذِينَ سَبَقُونَا بِالْإِيمَانِ وَلَا تَجْعَلْ فِي قُلُوبِنَا غِلًّا لِّلَّذِينَ آمَنُوا رَبَّنَا إِنَّكَ رَءُوفٌ رَّحِيمٌ ﴿١٠﴾

"Ewe Mola wetu! tusamehe sisi na ndugu zetu waliotutangulia katika imani, wala usijaalie ndani ya nyoyo zetu undani kuwafanyia wale walioamini, Ewe Mola wetu! hakika wewe ni mpole mwenye huruma." (Qur'ani, 59:10).

Na kwa ajili hiyo basi utawaona Masunni wanawaombea radhi Ali(a.s) na Muawiyyah bila kujali aliyoyatenda Muawiyah miongoni mwa matendo ambayo yaweza kusemwa ni kufru na upotofu na ni kumpiga vita Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na nimetaja katika maelezo yaliyopita habari hizo si vibaya kuzirejea kama ifuatavyo: Mtu mmoja miongoni mwa wacha Mungu alizuru kaburi la Sahaba Mtukufu Hujri ibn Adiyyi Al-kindi, akamkuta kaburini hapo mtu fulani analia sana, akamdhania kuwa huyo ni miongoni mwa Mashia akamuuliza; "Kwa nini unalia?" Yule mtu akajibu, "Namlilia Sayyidna Hujri Radhi yallahu anhu. " akasema: "Ni yepi yaliyompata?" Akasema: "Aliuawa na Sayydna Muawiyah Radhiyallahu anhu. " Akamwambia: "Kwa nini alimuuwa?" Akajibu:"Kwa sababu alikataa kumlaani Sayidina Ali Radhiyallahu anhu.

Yule mtu mwema akamwambia yule aliyekuwa akilia: "Nami nakulilia wewe radhi ya Mungu ikufikie." Basi faida gani ya kupokezana huku kwa kuwapenda Masahaba wote mpaka tunawaona Masunni hawamswalii Mtume Muhammad na kizazi chake isipokuwa wataongeza juu yake Masahaba wake wote. Si Qur'an iliyowaamuru kufanya hivyo wala Mtume wa Mwenyezi Mungu hakuwataka kufanya hivyo wala yeyote miongoni mwa Masahaba hakulisema jambo hilo (ilivyo sawa ni kwamba), sala ya Mtume ilikuwa ni kwa Muhammad na kizazi cha Muhammad kama ilivyoshuka Qur'ani na kama alivyoifundisha Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) . Kama nitakuwa nashaka juu ya kitu fulani, basi sina na sitakuwa nashaka kwamba, Mwenyezi Mungu amewataka waumini kuwapenda Al-Qurba ambao ni watu wa nyumba ya Mtume na akafanya upendo huo kwao kuwa ni faradhi kama ndiyo malipo ya ujumbe wa Mtume Muhammad, akasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

قُل لَّا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ أَجْرًا إِلَّا الْمَوَدَّةَ فِي الْقُرْبَىٰ ﴿٢٣﴾

"Waambie sikuombeni malipo (yoyote kwa kazi hii ya Utume) isipokuwa muwapende Qaraba (zangu), (Qur'an, 42:23).

Hapana shaka Waislamu wote wameafikiana bila tofauti kati yao juu ya kuwapenda watu wa nyumba ya Mtume(a.s) , lakini Waislamu wametofautiana juu ya kuwapenda wasiokuwa hao, na Mtume(s.a.w.w) amesema: "Wacha lenye kukutia shaka ufanye lisilokutia shaka. " Kauli ya Mashia juu ya kuwapenda watu wa nyumba ya Mtume na wanaowafuata haina shaka, na (amma) kauli ya Masunni juu ya kuwapenda masahaba wote, ina mashaka ndani yake, basi itakuwaje kwa Muislamu awapende maadui wa watu wa nyumba ya Mtume ambao waliwauwa na eti awatakie radhi maadui hao? Je, huu si utata unaochukiza?

Hebu wachana na kauli za watu waliochanganyikiwa na baadhi ya Masufi ambao wanadai kwamba, mtu hawezi kuutakasa moyo wake wala hawezi kuijuwa imani ya kweli mpaka pale itakapokuwa haikubakia moyoni mwake chembe ndogo ya kuwabughudhi waja wa Mwenyezi Mungu wote miongoni mwao wakiwa ni Mayahudi, Wakristo na Walahidi na Washirikina, na (hawa jamaa) wanazo kauli za ajabu zinazoshangaza kuhusiana na jambo hili ambazo zinaambatana na zile za wabashiri miongoni mwa watu wa Kanisa la Kikiristo ambao wanawadanganya watu kuwa "Mwenyezi Mungu ni upendo na dini ni upendo, basi yeyote mwenye kuwapenda viumbe wa Mungu hana haja ya kusali na kufunga na kuhiji na mengineyo." Mambo hayo kwa hakika naapa ni uzushi ambao Qur'ani na Sunna havikubaliani nao wala akili haikubali. Qur'ani inasema: "Huwezi kuwakuta watu wamuaminio Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho wanawapenda watu wanaompinga Mwenyezi Mungu na Mtume wake." Na amesema tena:

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَتَّخِذُوا الْيَهُودَ وَالنَّصَارَىٰ أَوْلِيَاءَ بَعْضُهُمْ أَوْلِيَاءُ بَعْضٍ وَمَن يَتَوَلَّهُم مِّنكُمْ فَإِنَّهُ مِنْهُمْ إِنَّ اللَّـهَ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الظَّالِمِينَ ﴿٥١﴾

"Enyi mlioamini msiwafanye Mayahudi na Wakristo kuwa walinzi wa maslahi (yenu), wao kwa wao ni marafiki, basi yeyote atakayewatawalisha miongoni mwenu yeye atakuwa miongoni mwao, bila shaka Mwenyezi Mungu hawaongozi watu madhalimu." (Qur'an, 5:51).

Na amesema tena Mwenyezi Mungu:

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَتَّخِذُوا آبَاءَكُمْ وَإِخْوَانَكُمْ أَوْلِيَاءَ إِنِ اسْتَحَبُّوا الْكُفْرَ عَلَى الْإِيمَانِ وَمَن يَتَوَلَّهُم مِّنكُمْ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ ﴿٢٣﴾

"Enyi mlioamini, msiwafanye baba zenu na ndugu zenu kuwa walinzi wa maslahi yenu ikiwa watauboresha ukafiri kuliko imani, na yeyote miongoni mwenu atakayewafanya kuwa walinzi wa maslahi yake (yote) hao ndio madhalimu." (Qur'an, 9:23).

Na pia amesema:

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَتَّخِذُوا عَدُوِّي وَعَدُوَّكُمْ أَوْلِيَاءَ تُلْقُونَ إِلَيْهِم بِالْمَوَدَّةِ وَقَدْ كَفَرُوا بِمَا جَاءَكُم مِّنَ الْحَقِّ... ﴿١﴾

"Enyi mlioamini msiwafanye adui zangu na adui zenu kuwa walinzi wa maslahi yenu na mukawapenda hali yakuwa wameikanusha haki iliyokujieni." (Qur'an, 60:1).

Naye Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: "Haikamiliki imani ya Muumini mpaka yawe mapenzi yake ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, na chuki yake iwe kwa ajili ya Mwenyezi Mungu ." Pia amesema: "Hayakutani ndani ya moyo wa Muumini, mapenzi ya kumpenda Mwenyezi Mungu na mapenzi ya kumpenda adui wa Mwenyezi Mungu ." Hadithi zinazohusu jambo hili ni nyingi mno, na akili yatosha peke yake kuwa ni dalili, kwani Mwenyezi Mungu ameijaza imani (katika nyoyo za) waumini na akaipamba ndani ya nyoyo zao, na akachukia kwao kufru na uovu na uasi, hivyo basi mtu anaweza kumchukia mwanawe au baba yake au nduguye kwa sababu ya kupinga haki na kudumu katika njia ya shetani, na anaweza kumpenda na kumfanya rafiki mtu baki asiye na uhusiano naye isipokuwa udugu wa Kiislamu.

Kutokana na yote haya basi ni wajibu mapenzi yetu na urafiki wetu uwe kwa wale ambao Mwenyezi Mungu ameamrisha tuwapende, kama ambavyo ni wajibu ghadhabu zetu na chuki yetu na kujitenga kwetu kuwe juu ya wale ambao Mwenyezi Mungu ameamrisha tujitenge nao. Na kwa ajili hiyo basi, ndiyo maana tumemtawalisha Ali na Maimamu ambao ni miongoni mwa wanawe bila ya kuwa sisi tunauhusiano nao hapo kabla ya kuwapenda, na kuwapenda wao ni kwa sababu Qur'ani na Sunna na historia na akili hazikuachia nafasi yoyote ya kuwatilia mashaka ya aina yoyote.

Na kwa ajili hiyo pia kujitenga kwetu na Masahaba ambao walipora haki ya Ali katika Ukhalifa, kumekuja bila ya kuwepo uhusiano fulani uliotangulia wa kuwachukia, na hayo ni kwa sababu Qur'ani na Sunna na historia na akili vimetuachia sisi mashaka makubwa kuhusu wao. Na kwa kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) ametuamrisha kwa kusema: "Acha linalokutia shaka ufanye lisilokutia shaka ." Basi haifai kwa Muislamu kufuata jambo lolote lenye mashaka, akaacha Qur'ani ambayo haina shaka ndani yake. Kama ambayo ni wajibu juu ya kila Muislamu kujikomboa kutoka katika kifungo alichofungwa na kufuata kwake bila kujua bali aipe akili yake maamuzi bila kujali mawazo ya hapo kabla na chuki iliyojificha ndani, kwani nafsi na shetani ni maadui wa hatari wanaompambia mwanaadamu matendo yake mabaya akayaona kuwa mazuri.

Uzuri ulioje wa maneno aliyoyasema Imam Busairi ndani ya Burdah: "Ipinge nafsi na shetani uviasi (viwili hivi), bila shaka nasaha (yao) wanakudanganya, basi wachukie." Ni wajibu juu ya Waislamu kumuogopa Mwenyezi Mungu kuhusu waja wake wema miongoni mwao, ama wale ambao hawakuwa miongoni mwa wachamungu basi hawana heshima yoyote (wanayostahiki) kwani Mtume wa Mwenyezi Mungu amesema: "Si uteti kuzungumza habari za mtu muovu " ili Waislamu wapate kuyafahamu mambo yake wasije wakadanganyika kwake na wasijempa utawala. Pia Waislamu wanawajibika leo hii wawe wakweli kwa nafsi zao na waangalie hali yao inavyotia uchungu na huzuni na udhalili walio nao, wasitosheke na kujifaharisha kwa sifa za wakubwa zao waliopita, lau kama viongozi wetu waliopita wangekuwa kwenye haki kama tunavyodhania leo hii, basi sisi tusingefikia kwenye matokeo haya ambayo moja kwa moja yamekuja kutokana na kugeuka ambako kulitokea katika Ummah baada ya kufariki kwa Mtume wake. Roho yangu na roho za Walimwengu ziwefidia kwake.

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُونُوا قَوَّامِينَ بِالْقِسْطِ شُهَدَاءَ لِلَّـهِ وَلَوْ عَلَىٰ أَنفُسِكُمْ أَوِ الْوَالِدَيْنِ وَالْأَقْرَبِينَ إِن يَكُنْ غَنِيًّا أَوْ فَقِيرًا فَاللَّـهُ أَوْلَىٰ بِهِمَا فَلَا تَتَّبِعُوا الْهَوَىٰ أَن تَعْدِلُوا وَإِن تَلْوُوا أَوْ تُعْرِضُوا فَإِنَّ اللَّـهَ كَانَ بِمَا تَعْمَلُونَ خَبِيرًا ﴿١٣٥﴾

"Enyi mlioamini kuweni wenye kusimamisha uadilifu, wenye kushuhudia kwa ajili ya Mwenyezi Mungu japokuwa (ushahidi huo) ni dhidi ya nafsi zenu au wazazi wenu na jamaa zenu, akiwa tajiri au masikini, Mwenyezi Mungu anawastahikia zaidi, basi msifuate matamanio mkaacha kufanya uadilifu, na kama mkipotosha (ushahidi) au mkajitenga, basi Mwenyezi Mungu anajua yale mnayoyatenda." (Qur 'an, 4:135).


10

11

12

13

14

15

16

17

18

19