UCHUNGUZI JUU YA UWAHABI

UCHUNGUZI JUU YA UWAHABI13%

UCHUNGUZI JUU YA UWAHABI Mwandishi:
: SHEIKH MUSABBAH SHA'ABANI
Kundi: Vitabu mbali mbali

UCHUNGUZI JUU YA UWAHABI
  • Anza
  • Iliyopita
  • 24 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 53076 / Pakua: 6142
Kiwango Kiwango Kiwango
UCHUNGUZI JUU YA UWAHABI

UCHUNGUZI JUU YA UWAHABI

Mwandishi:
Swahili

1

2

3

4

5

6

7

UCHUNGUZI JUU YA UWAHABI

MATOKEO MAZURI YANAYOPATIKANA KUTOKANA NA KUWAZURU WATU MUHIMU WA KIDINI

Makaburi yanayopata hadhi ya kutunzwa na kuheshimiwa na watu wanaomuamini Mwenyezi Mungu katika ulimwengu - hasa Waislamu ni yale ambayo mara nyingi yanakuwa ni makaburi ya watu ambao wamebeba ujumbe wa amani na kuufikisha kama ilivyotakiwa ufike. Watu hawa wamegawanyika sehemu tatu:

1. Manabii: Ambao ndiyo viongozi wa dini, walibeba mabegani mwao ujumbe kutoka mbinguni, walizitoa nafsi zao na mali zao pamoja na wanavyovipenda kwa ajili ya kufikisha ujumbe huo, na wakavumilia aina mbali mbali za taabu na matatizo ili wapate kuwaongoa watu.

2. Wanachuoni na wanafikra: Ambao ni kama mshumaa unaowangazia wengine wakati wenyewe unateketea.

Watu hawa waliishi maisha ya kichamungu na kujinyima na wakaupatia ulimwengu maelezo yenye thamani na uchambuzi mzuri, katika nyanja za elimu, fikra, tabia na elimu za maumbile na ufunuo kutoka mbinguni na elimu za ulimwengu, viumbe na mengineyo.

3. Mujahidina (wapiganaji Jihadi): Hawa ni wale wenye kupigania mabadiliko ambao walihuzunishwa na hali ya maisha ya jamii kutokana na dhulma na ubaguzi wa rangi na kabila na hawakuivumilia hali hiyo, wakapigana dhidi ya dhulma na ukandamizaji na wakadai heshima na haki za binadamu zilindwe, na wakajenga ngome ya uadilifu kwa kutoa damu zao zenye thamani kubwa. Mapinduzi yoyote au mabadiliko ya jamii hayalinganishwi na kitu chochote isipokuwa kwa kutoa kitu cha thamani ili mafaniko yapatikane. Na thamani ya mapinduzi inayoweza kubomoa tawala za madhalimu na kuwasonga koo, ni kutoa damu tukufu ambayo wapiganaji mashujaa hujitolea muhanga kwa damu hiyo ili kurejesha haki na uhuru kwenye nchi za Kiislamu.

Kwa hiyo watu huwa wanazuru makaburi ya watu wa aina hizi, na hutokwa machozi wawapo makaburini na huwa wanakumbuka ushujaa wao na kujitoa kwao muhanga, pia huziliwaza roho za mashujaa hao kwa kusoma Qur'an kisha kuwazawadia thawabu za visomo hivyo. Kadhalika huimba Qasida ambazo hutaja sifa zao na utukufu wao na kiwango cha daraja zao tukufu. Hakika kuzuru makaburi ya watu hawa muhimu ni moja katika aina ya kuwashukuru na kuwatukuza kwa kujitolea kwao na pia kujulisha kizazi kilichopo kuwa, hayo ndiyo malipo ya wale ambao hupita njia ya haki na uongofu na ubora, na ndiyo malipo ya wale wanaopigana na kulinda misingi ya itikadi (Uislamu).

Malipo yao ni kudumu kwa utajo wao, utajo ambao ni mwema na sifa nzuri hata kama ni muda mrefu umepita toka kufariki kwao. Mpaka hapa tumefahamu umuhimu wa kuhuyisha utajo wa watu hawa muhimu wa dini, na kwa msingi huu inapasa kufanya juhudi ili kuendelea kuzifanya kumbukumbu zao kuwa hai na kuzihifadhi na kusimamisha sherehe kubwa za kukumbuka siku za kuzaliwa kwao na kuvaa mavazi ya kuonyesha msiba na kufanya hafla za kuomboleza na kukumbuka kufa kwao, pia kufanya vikao na mikusanyiko mikubwa na kutoa hotuba za kuwatambulisha watu hao watukufu na itikadi zao zilizopelekea wao wajitoe muhanga. Kadhalika kuyaheshimu malazi yao (makaburi) na kujiepusha na kila linalotia dosari heshima yao, kwani kuyaheshimu makaburi yao ndiko kuheshimu ujumbe wao na itikadi zao.

Kinyume cha hivyo ni kuyadharau na kuyapuuza makaburi yao, na itakuwa ndiyo kuudharau ujumbe wao na ni kuwadharau wao wenyewe. Katika siku zetu hizi, mtu anapoingia katika makaburi ya Baqii ili akazuru makaburi ya watu wa kizazi cha Mtume[s.a.w.w] na makaburi ya viongozi wa Kiislamu na watetezi wa dini na Masahaba, atayaona makaburi hayo yako katika hali inayohuzunisha kutokana na dharau yaliyofanyiwa, jambo ambalo linatetemesha nafsi na kuifanya ishangazwe na uovu wa kikundi cha Mawahabi ambao wanadai kuwa wao ndiyo watetezi wa Uislamu. Ajabu ni kwamba, kwa upande mmoja Mawahabi huwataja masahaba kwa wema na kuwasifu katika majukwaa ya hotuba zao, lakini kwa upande wa pili wanayaacha makaburi ya Masahaba bila ya heshima yoyote, na katika hali ya kusikitisha katika kuyadharau na kuyapuuza makaburi hayo, Mawahabi hawayajali kabisa hata kama wanyama wataingia na kuharibu sehemu ya makaburi ya Masahaba. Zawadi ya pekee ambayo Mawahabi huwapatia mahujaji na wanaozuru (makaburi ya Baqii) ni kuwaita kuwa ni washirikina na tendo lao la kuyazuru makaburi hayo ni tendo la shirki.

Mawahabi wanawaambia Waislamu maneno (haya machafu) kwa sababu tu Waislamu hao wanawaheshimu viongozi wa dini, na wanawatukuza Mawalii wa Mwenyezi Mungu. Hali hii inaonyesha kwamba, Mawahabi wanaficha mioyoni mwao chuki na kero waliyonayo dhidi ya Mawalii wa Mwenyezi Mungu na viongozi wa dini yake. Na sasa umefika wakati wa kuzungumzia ziyara ya kaburi la Mtume[s.a.w.w] kwa mujibu wa mtazamo wa dalili za Kiislamu.

KUZURU KABURI LA MTUKUFU MTUME

Katika maelezo yafuatayo tutatoa baadhi ya aya za Qur'an na hadithi tukufu za Mtume[s.a.w.w] ambazo zinahimiza kulizuru kaburi lake. Na tunataraji kuwa msomaji atapata maelekezo zaidi na kufahamu.

USHAHIDI WA QUR'AN

Qur'an tukufu inawaamrisha wenye madhambi wafike mbele ya mjumbe wa Mwenyezi Mungu na wamuombe awaombee msamaha kwa Mwenyezi Mungu, kwani dua au maombi ya Mtume yatakubaliwa kwa ajili yao. Mwenyezi Mungu anasema:

وَلَوْ أَنَّهُمْ إِذ ظَّلَمُوا أَنفُسَهُمْ جَاءُوكَ فَاسْتَغْفَرُوا اللَّـهَ وَاسْتَغْفَرَ لَهُمُ الرَّسُولُ لَوَجَدُوا اللَّـهَ تَوَّابًا رَّحِيمًا ﴿٦٤﴾

"Na lau wangelikuja kwako walipojidhulumu nafsi zao wakaomba msamaha kwa Mwenyezi Mungu, na Mtume pia akawaombea msamaha, bila shaka wangelinikuta Mwenyezi Mungu ni mwenye kupokea toba tena mwenye kurehemu. (Qur'an, 4:64).

Lau aya hii ingekuwa ndiyo pekee katika mada hii, basi tungelisema kuwa inahusika tu katika zama za uhai wa Mtume[s.a.w.w] na ni kwa kipindi kile tu cha yeye kuwepo miongoni mwa watu. Lakini sisi tunachukua hukmu ya jumla inayoenea, ambayo haimuwekei Mtume mpaka wa mwisho kwa maisha yake ya dunia. Hukmu hiyo iko katika maelezo yafuatayo:

Kwanza : Qur'an inabainisha kuwa, Manabii, Mawalii na baadhi ya watu wengine wako hai katika Bar-zakh (uhai baada ya kufa) na inawazingatia kuwa wanaona na wanasikia katika huo ulimwengu wa Barzakh.

Tutazionyesha hizo aya zinazobainisha jambo hili katika sehemu ya kuzungumzia kutawasal kwa roho tukufu.

Pili : Hadithi tukufu zinabainisha kwamba, Malaika humfikishia Mtume[s.a.w.w] salamu za yeyote anayemsalimia. Imekuja hadithi katika Sihah: "Hakika Mtume wa Mwenyezi Mungu amesema: "Hapana yeyote atakayenisalimia, isipokuwa Mwenyezi Mungu hunirudishia roho yangu mpaka nami nimrudishie salamu ". [89] Na amesema Mtume[s.a.w.w] : "Niswaliyeni, kwani swala zenu zinanifikia (kutoka) popote mlipo ." [90]

Tatu : Waislamu wamefahamu tangu siku hizo kwamba maana ya aya tuliyotangulia kuitaja inaendelea kutumika na wala haikomi kwa kufariki Mtume[s.a.w.w] , kiasi kwamba kuna baadhi ya mabedui (kwa mujibu wa fikra zao nzuri) walikuwa wakilikusudia kaburi Ia Mtume na wanalizuru na wanaisoma aya hii kaburini kwa Mtume na kumuomba awatakie msamaha.

Ametaja Taqiyyud-din As-Subaki katika kitabu kiitwacho "Shifaus-siqami" na pia As-Samhudi katika kitabu kiitwacho "Wafa-ul Wafa" mifano mbali mbali ya Waislamu kuzuru kaburi la Mtume[s.a.w.w] na kusoma kwao aya hii mbele ya kaburi lake tukufu. Tunataja baadhi ya mifano kama ifuatavyo: Amepokea Sufyan bin Anbar kutoka kwa Al-Utbi, na wawili hawa ni Masheikh wa Imamu Shafii na ni wallimu wake, kwamba yeye amesema, "Nilikuwa nimekaa kwenye kaburi la mjumbe wa Mwenyezi Mungu[s.a.w.w] , mara akaja bedui mmoja akasema: "As-Salaamu Alaika ya Rasulallah, nimemsikia Mwenyezi Mungu akisema: "Na lau wangelikuja kwako walipojidhulumu nafsi zao wakaomba msamaha kwa Mwenyezi Mungu na Mtume pia akawaombea msamaha, bila shaka wangelimkuta Mwenyezi Mungu ni mwenye kupokea toba tena mwenye kurehemu". Nami nimekujia mwenye kutaka msamaha kutokana na dhambi zangu mwenye kutaka Shafaa kwako (uniombee) kwa Mola wangu". Kisha bedui yule akalia, na akawa anasema:

"Ewe mbora wa waliozikwa ardhini, kwa uzuri wako ardhi na mimea (iliyopo hapa) vimependeza, nafsi yangu iwe fidia ya kaburi ulilomo, ndani yake kuna utakatifa na kuna kila ukarimu na ubora". Kisha bedui yule akaomba msamaha na akaenda zake.[91] Naye Abu Said As-Sam-ani anapokea kutoka kwa Imam Ali bin Abi Talib[a.s] kwamba, bedui mmoja alikuja Madina baada ya siku tatu tangu Mtume[s.a.w.w] azikwe, akajitupa kwenye kaburi tukufu la Mtume akajipaka udongo wa kaburi kichwani mwake na akasema: "Ewe mjumbe wa Mwenyezi Mungu, ulisema nasi tukaisikia kauli yako, umepokea kwa Mwenyezi Mungu mambo ambayo tumeyapokea kwako na katika aliyokuteremshia Mwenyezi Mungu ni "Na lau wangelikuja kwako walipojidhulumu nafsi zao.... nami nimedhulumu nafsi yangu na nimekuja ili unitakie msamaha kwa Mola wangu"[92] Yote haya yanajulisha cheo kikubwa alichokitoa Mwenyezi Mungu kwa Mtume[s.a.w.w] kama ilivyobainisha aya hii kwamba cheo hicho siyo makhsusi katika uhai wake tu, bali inatia mkazo kuwa kinathibiti hata baada ya kufa vile vile.

Kwa ujumla Waislamu wanazizingatia aya zote zilizoshuka kwa ajili ya kumtukuza Mtume[s.a.w.w] kwamba, zinakusanya kipindi cha uhai wake na baada ya kufa, na hapana yeyote anayezihusisha katika wakati wa uhai wake tu. Na katika historia imekuja kwamba: Alipouawa Imam Hasan bin Ali[a.s] na mwili wake Mtukufu ukaletwa ndani ya msikiti wa Mtume[s.a.w.w] , Banu Ummayya walidhani kwamba Banu Hashim wanataka kumzika karibu na kaburi la Babu yake, wakaeneza fitna na makelele ili asizikwe karibu na Babu yake. Imam Husein[a.s] akasoma kauli ya Mwenyezi Mungu isemayo: "Enyi mulioamini, musipaze sauti zenu kuliko sauti ya Mtume . Qur'an, 49:2.

Hakuna mtu yeyote aliyempinga Imam Husein[a.s] eti kuwa aya hii inahusu zama za uhai wa Mtume[s.a.w.w] , hata hao Banu Ummayya hawakuthubutu. Na leo hii utawaona Mawahabi wameiandika aya hii na kuiweka kwenye ukuta unaokabiliana na kaburi la Mtume[s.a.w.w] hali ya kuwa wanakusudia kuzuwiya watu wasipaze sauti zao mahala hapo. Na kwa mtiririko huu tunaweza kutoa maana pana zaidi ya aya hii, nayo ni kwamba, ni juu ya Waislamu wa leo kusimama mbele ya kaburi la Mtume[s.a.w.w] na wamuombe Mtume awatakie msamaha kwa Mwenyezi Mungu. Kwa hiyo kumzuru Mtume[s.a.w.w] hakuna maana isipokuwa kufanya yale ambayo yamo katika aya hii na zinginezo. Aya hii inajulisha maudhui mbili nazo ni:

1. Mtu anawajibika kusimama kwenye kaburi la Mtume[s.a.w.w] baada ya kufa kwake na kumuomba Mtume amtakie msamaha kwa Mwenyezi Mungu.

Tutafafauna maudhui haya wakati wa uchambuzi kuhusu kutawassal kwa Mawalii wa Mwenyezi Mungu, Insha-Allahau Taala.

2. Aya hii inashuhudia kuweko ruhusa ya kuzuru kaburi la Mtume[s.a.w.w] kwani ukweli wa ziyara huwa hauna maana isipokuwa mwenye kuzuru afike pale alipo anayemzuru. Basi ikiwa kusimama mbele ya kaburi la Mtume[s.a.w.w] na kumuomba atutakie msamaha kwa Mwenyezi Mungu ni jambo linalojuzu, bila shaka yatathibiti mambo mawili:

1. Tutakuwa tumemuomba atuombee msamaha kwa Mwenyezi Mungu.

2. Tumefika mbele yake na tumemsemesha.

Na maana ya ziyara hakuna isipokuwa mambo haya mawili.

DALILI NYINGINE

lj-mai ya Waislamu juu ya hukmu fulani miongoni mwa hukmu za kisheria katika zama mbali mbali, huwa inazingatiwa kuwa ni dalili iliyo wazi kabisa ya kusihi kwa hukmu hiyo na kuthibiti kwake. Na ziyara kwenye kaburi la Mtume[s.a.w.w] ni miongoni mwa mambo haya na unadhihiri ukweli wa mambo iwapo tutarejea vitabu vya hadithi, Fiqhi, Akhlaq na Historia na hasa sehemu zinazohusu ibada ya Hija katika vitabu hivyo. Ameutaja ubora wa kuzuru kaburi la Mtume[s.a.w.w] Al-Marhum Al-Allama AI-Amini kutoka katika rejea arobaini na mbili zikiwa ni miongoni mwa rejea muhimu za elimu za Kiislamu. Ndani ya kitabu chake kiitwacho Al-Ghadir kwenye juzuu ya tano ukurasa wa 106 mpaka ukurasa wa 129, amezitaja nassi na ibara zinazohusu maudhi hii kwa undani sana. Miongoni mwa vitabu ambavyo tumevitegemea kutolea ushahidi kuhusu mada hii ni kama ifuatavyo:

1. Shifaus-siqami fi Ziyarati Khairil-Anami, kilichoandikwa na Taqiyyud-din As-Subaki as-Shafii, aliyefariki mwaka 706 A.H. Ndani ya Kitabu chake hiki ametaja mkusanyiko wa maneno ya wanachuoni walioboresha ziyara ya kuzuru makaburi na kuisisitiza sana.

2. Wafa-ul Wafa, kilichoandikwa na As-Samhudi aliyefariki mwaka 911 A.H., naye ametaja katika kitabu chake maneno ya wanachuoni katika kuboresha na kupendekeza ziyara.

3. Al-Fiqhu Alal-madhahibil-ar-baa, kilichotungwa na wanachuoni wanne wa Madhehebu manne, na wamekusanya ndani ya kitabu hicho Fatwa za Maimamu wa Madhehebu manne mashuhuri kwa Masunni. Wanachuoni hawa wanasema: "Kulizuru kaburi la Mtume[s.a.w.w] ni sunna iliyo bora kuliko Sunna zote kwani hadithi nyingi zimekuja juu ya jambo hili".[93] Sasa umefika wakati wa kutaja baadhi ya hadithi zilizopokelewa na wanahadithi kuhusu kuzuru kaburi Ia Mtume[s.a.w.w]

HADITHI TUKUFU JUU YA KUZURU KABURI LA MTUME [s.a.w.w]

Hadithi tukufu ambazo wanachuoni wa hadithi wamezipokea kuhusu kumzuru Mtume[s.a.w.w] ni nyingi mno kiasi kufikia daraja ya Mutawatir, kwa hiyo hatuoni sababu ya kuzihakiki katika Sanadi zake wala wapokezi wake. Mahafidh kutoka Madh-hebu zote za Kiislamu wameziandika katika vitabu vyao na Sihahi zao, na hadithi zote kwa ujumla zinajulisha kwamba, kulizuru kaburi la Mtume ilikuwa ni sunna iliyothibiti kwa wanachuoni hao wa hadithi. Na lau tungetaka kuzitaja zote ingechukuwa nafasi kubwa, kwa hiyo tunatosheka kutaja baadhi yake kama ifuatavyo:

1. Imepokewa toka kwa Abdallah bin Omar kwamba: Mtume[s.a.w.w] amesema: "Ye yote mwenye kuzuru kaburi langu, yamemuwajibikia maombezi yangu ". Hadithi hii imekuja katika kitabu cha Al-fiqhi Alal-madhahibil-ar-baa, Juz. 1 uk. 590.

Wanachuoni wa madhehebu manne wametoa fatwa kwa mujibu wa hadithi hii. Ili kufahamu rejea zilizotumika, rejea kitabu kiitwacho Wafa-ul Wafa, Juz. 4 uk. 1336. Katika mambo yasiyo na shaka ni kwamba, hadithi wanayoipokea mahafidh na maulamaa tangu nusu ya karne ya pili Hijiriya mpaka leo haiwezekani kuwa ni uzushi na eti haina msingi. Sheikh Taqiyyud-din As-Subaki, ameandika uchunguzi wa hadithi hii na Sanadi zake na wapokezi wake katika kitabu chake Shifaus-siqami na akathibitisha kuwa ni hadithi sahihi. (Na kitabu hiki ni kitabu bora mno kilichoandikwa na masunni dhidi ya Ibn Taymiyyah kuhusu kuharamisha kwake Safari ya kwenda kuzuru kaburi la Mtume[s.a.w.w] .

2. Amesema Mtume[s.a.w.w] : "Ye yote atakayenijia kwa lengo la kunizuru na ikawa hakuna kingine kilichomfikisha kwangu ila kunizuru mimi tu, basi nitakuwa na wajibu wa kuwa muombezi wake siku ya Qiyama ". Hadithi hii imetajwa na mahafidh na wanachuoni wahadithi kumi na sita ndani ya vitabu vyao. Naye Taqiyyud-din As-Subaki ameizungumzia hadithi hii katika kitabu chake tulichokwisha kitaja juu ya sanadi zake na wapokezi wake, na vile vile As-Samhudi ameitaja katika kitabu chake Wafa-ul Wafa Juz. 4, uk. 1340.

3. Amesema Mtume[s.a.w.w] "Mwenye kuhiji nyumba tukufu (Al-Kaaba) na asinizuru, basi mtu huyo amenidhulumu ". Hadithi hii wameipokea Masheikh na Mahafidh wa hadithi tisa, na As-Samhudi amewataja kwa ufafanuzi katika kitabu chake Juz. 4, uk. 1342.

4. Mtume[s.a.w.w] amesema "Mwenye kuhiji kisha akalizuru kaburi langu baada ya kufa kwangu, atakuwa kama amenizuru katika zama za uhai wangu ". Wameipokea hadithi hii watu kumi na tano miongoni mwa wanahadithi na mahafidhi mashuhuri. Sheikh Taqiyyud-din As-Subaki katika kitabu chake amezungumzia Sanadi za hadithi hii, kama ambavyo As-Samhudi ameitaja katika kitabu chake Juz. 4, uk. 1340.

5. Mtume[s.a.w.w] amesema: "Mwenye kuzuru kaburi langu au mwenye kunizuru, nitakuwa muombezi wake". Hadithi hii imepokewa na wana hadithi na mahafidhi kumi na watatu, As-Samhudi amewataja ndani ya kitabu chake Juz. 4, uk. 1347. 6. Amesema Mtume[s.a.w.w] : "Mwenye kunizuru baada ya kufa kwangu ni kama amemzuru wakati wa uhai wangu ". Hii ilikuwa ni mifano ya hadithi nyingi ambazo zimepokelewa kutoka kwa Mtume[s.a.w.w] zinazowataka watu na kuwahimiza kulizuru kaburi tukufu la Mtume(s.a.w.w) . Mar-hum Sheikh Al-Amini katika kitabu chake kiitwacho "Al-Ghadir" amekusanya hadithi ishirini na mbili juu ya maudhui hii. As-Samhudi katika kitabu chake, yeye ametaja hadithi kumi na saba na amezungumzia sanadi zake na wapokezi wake kiasi kwamba hakuna Ia kuongeza. [94] Ikiwa Mtume[s.a.w.w] amewataka watu walizuru kaburi lake tukufu, basi bila shaka ni kutokana na matokeo na athari na faida za kimaada na kimaana zinazoambatana na kumzuru yeye na kuwazuru watu wengine mashuhuri wa kidini. Kwa hakika, kutokana na kuzuru kaburi la Mtume[s.a.w.w] Waislamu hupata fursa ya kukifahamu kituo cha Uislamu na pia kuyafahamu matukio yaliyopata kutokea na yanayotokea kwa kipindi hicho na kutoka huko huwa wanajipatia elimu na maarifa ya Kiislamu ambayo huyachukua na kuyasambaza kila pembe ya dunia.

DALILI ZA MAWAHABI KATIKA KUHARAMISHA SAFARI ZA KUZURU MAKABURI

Kinachojitokeza kwa Mawahabi ni kwamba, asili ya kufanya ziyara wanaruhusu, lakini wanaharamisha kufanya safari kwa nia ya ziyara. Muhammad Abdul-Wahabi anasema katika risala yake ya pili miongoni mwa risala za "Hadiyatus-saniyyah" kama ifuatavyo: "Inasuniwa kumzuru Mtume[s.a.w.w] , isipokuwa haiwezi kufungwa safari ila kwa (nia ya) kuzuru msikiti na kuswali ndani yake". Na dalili wanayoshikilia katika kuharamisha ziyara ni ile hadithi iliyotajwa katika Sihahi zao kutoka kwa Abu Huraira!! Kwamba Mtume[s.a.w.w] amesema, "Haifungwi safari isipokuwa kwa Misikiti mitatu: Msikiti wangu huu na Masjidil-haram (Makka) na Masjidil-Aqsaa (Baitul-Muqadas). Na imepokewa tena hadithi hii kwa namna nyingine kama ifuatavyo: "Hakika hufanywa safari kwenda kwenye Misikiti mitatu: Msikiti wa Al-Kaaba, na msikiti wangu na msikiti wa Il-Yaa. Vile vile imepokewa kwa namna ya tatu nayo ni hii: "Hufungwa safari kwenda kwenye Misikiti mitatu..."

Hadithi zote hizi tatu amezileta Muslim ndani ya Sahih yake.[95] Hapana shaka yoyote kwamba hadithi hii imo katika Sihahi lakini sasa hivi sisi hatuko katika uwanja wa kuijadili hadithi hii, hasa kwa kuwa katika sanadi hii yako Bwana Abu Huraira (ambaye hali yake inaeleweka kwa wanachuoni) bali makusudio yetu ni kutazama hadithi hii inamaanisha nini. Basi hebu na tukadirie kwamba Nassi ya hadithi hii iko kama ifuatavyo: "Haifungwi safari ila ya kwenda kwenye Misikiti mitatu...." Ukweli unaothibiti ni kwamba harfu ya "Il-la" ni "Adatustith-Nai" kwa hiyo hapana budi awepo "Mustathna minhu" na ni wajibu afahamike. Na kwa kuwa hapa katika Nassi hayupo, basi hapana budi kumkadiria kuwa yupo katika maneno haya.

Na kabla ya kuonyesha dalili zinazopatikana inawezekana kumkadiria Mustath-na Min-hu kwa namna mbili:

1. Haifungwi safari kwenda kwenye Msikiti miongoni mwa Misikiti isipokuwa Misikiti Mitatu...

2. Haifungwi safari kwenda sehemu miongoni mwa sehemu yoyote isipokuwa kwenye misikiti mitatu... Kuifahamu hadithi hii na kuichunguza maana yake kutategemea moja ya makadirio haya mawili. Basi iwapo tutachagua makadirio ya kwanza, maana ya hadithi itakuwa kutokufungwa safari kwenda msikiti wowote isipokuwa misikiti ile mitatu, wala haitakusudia kutoruhusu kufungwa safari kwenda sehemu yoyote hata kama sehemu hiyo siyo msikiti. Kwa hiyo katazo lililopo hapa halimhusu yule anayefunga safari kwa ajili ya kuwazuru Manabii, Maimamu Watukufu na wachamungu, kwani mahala panapofanyiwa uchambuzi ni ufungwaji wa safari za kuzuru misikiti kwa kuwa misikiti iliyovuliwa ni mitatu. Ama anayefunga safari kuyazuru maziyara matukufu hatahusika na katazo hili wala haingii katika maudhui hii. Maelezo haya ni kwa mujibu wa makadirio ya kwanza.

Tukija kwenye makadirio ya pili ni lazima zihusike safari za aina zote za kidini isipokuwa safari za kwenda sehemu hizo tatu zilizotajwa, sawa sawa kama safari hizo zitakuwa ni kwa ajili ya kuzuru msikiti au kuzuru sehemu nyinginezo. Lakini qarina na dalili zinaelekeza kwamba makadirio ya mwanzo ndiyo sahihi kama tutakubali kwamba sanadi ya hadithi hii ni sahihi. Ama qarina zinazoonyesha kusihi kwa makadirio ya kwanza ni kama ifuatavyo: Kwanza: Misikiti iliyovuliwa ni mitatu na hiyo Istith-nai ni Mut-tasil kama inavyoonekana wazi, basi hapana budi mustathnaminhu awe ni misikiti na wala siyo mahala. Kama mtu atasema: "Majaa Il-la Zaidun" yaani "hakuja isipokuwa Zaidi" basi "Mustath-na Min-hu" katika sentensi hii atakuwa ni mtu au watu na wala haliwezi kuwa ni tamko la ujumla kwa mfano kitu. Pili: Lau kama lengo lingekuwa ni kuzuwiya safari zote basi Istith-nai ya misikiti mitatu tu haitosihi kwani mtu hukusudia safari katika msimu wa hija na akafanya safari kwenda "Arafa" na "Mash-ari na Mina".

Kwa hiyo kama safari za dini zisizokuwa za misikiti mitatu zingekuwa haramu, basi ni kwa nini zinafanywa katika sehemu hizi tulizozitaja? Tatu: Qur'an Tukufu na hadithi tukufu vinaashiria kuwepo kwa safari zingine za kidini na kumekuja msukumo wa kuhimiza na kusisitiza kuhusu safari hizo, kama vile safari kwa ajili ya kupigana Jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu, kutafuta elimu na kuunganisha udugu, kuwazuru wazazi na mfano wa hayo. Na miongoni mwa hayo yapo ambayo Mwenyezi Mungu ameyazungumzia aliposema:

وَمَا كَانَ الْمُؤْمِنُونَ لِيَنفِرُوا كَافَّةً فَلَوْلَا نَفَرَ مِن كُلِّ فِرْقَةٍ مِّنْهُمْ طَائِفَةٌ لِّيَتَفَقَّهُوا فِي الدِّينِ وَلِيُنذِرُوا قَوْمَهُمْ إِذَا رَجَعُوا إِلَيْهِمْ لَعَلَّهُمْ يَحْذَرُونَ ﴿١٢٢﴾

"Kwa nini halitoki kundi katika kila Taifa miongoni mwao liende likajifundishe vyema dini na kisha wakaja kuowaonya wenzao (waliosalia) ili wapate kujihadharisha". Qur'an, 9:122.

Na kwa sababu ya aya hii wafasiri wakubwa na wahakiki wa hadithi wameifasiri hadithi hii kama tulivyoonyesha sisi.

Kwa mfano: Ghazali anasema katika kitabu chake Ih-yaau Ulumid-din: Sehemu ya Pili: Nayo ni kuwa, asafiri kwa ajili ya ibada ima ya Hija au Jihadi na inaingia katika jumla ya hayo, kuzuru makaburi ya Manabii[a.s] , na kuzuru makaburi ya Masahaba na Tabiina na wanachuoni na Mawalii na kila ambaye (watu) hutabaruku kwake zama za uhai wake, basi watatabaruku kwa kumzuru baada ya kufa kwake." "Na inajuzu kufunga safari kwa lengo hili na wala halizuwiliki hili kutokana na kauli ya Mtume[s.a.w.w] aliposema: "Haifungwi safari isipokuwa kwenda kwenye misikiti mitatu, musikiti wangu huu na masjidil-haram na masjidil-Aqsa: Kwa sababu hadithi hii inahusu misikiti tu kwani misikiti yote ni sawa sawa katika ubora isipokuwa misikiti mitatu na hakuna tofauti baina ya kuzuru makaburi ya Mitume, Mawalii na wanachuoni katika asili ya ubora japo katika daraja kuna tofauti kubwa kutegemea vyeo vyao mbele ya Mwenyezi Mungu.[96] Kwa hiyo kilichokatazwa katika hadithi ni kufungwa safari kwenda kwenye Misikiti yoyote isiyokuwa hiyo mitatu, na haihusiki safari ya kuzuru au kwa malengo mengine ya dini.

Na kwa kumalizia, hapana budi tuonyeshe kwamba Mtume[s.a.w.w] wakati aliposema "Haifungwi safari isipokuwa kwenda kwenye Misikiti mitatu", alikuwa hana maana kwamba kufunga safari kwenda kwenye Misikiti mingine ni haramu, bali maana yake ilikuwani kwamba haistahiki mtu kufunga safari na kupambana na mashaka ya safari kwa ajili ya kuzuru Misikiti hiyo kwani Misikiti hiyo haitofautiani katika ubora kwa tofauti kubwa, sawa sawa kama Msikiti uko mjini an kijijini au schemu fulani hapana tofauti kubwa, na kwa ajili hiyo hapana kinachomlazimisha mtu kuifungia safari Misikiti hiyo. Ama akifunga safari kwa ajili ya Misikiti yoyote basi tendo la mtu huyo haliwi ni haramu wala lenye kwenda kinyume cha sunna tukufu, hilo linajulishwa na kile walichokipokea As-habus-sihah Wassunan: "Mtume[s.a.w.w] alikuwa akienda kwenye msikiti wa Qubaa hali akiwa kwenye kipando au kwa miguu, basi (akifika) huswali rakaa mbili msikitini. [97] Sisi tunawajibika kujiuliza ni vipi itawezekana kuwa haramu kufunga safari na kukata masafa marefa kwa ajili ya kusimamisha sala katika moja ya nyumba miongoni mwa nyumba za Mwenyezi Mungu kwa ajili ya Mwenyezi Mungu? Ikiwa kuswali msikitini ni Mustahabu basi kilichodhahiri ni kuwa kitangulizi cha Mustahabu ni Mustahabu vile vile.

9

HADITHI ZA MTUME (S.A.W.W) PAMOJA NA MAIMAMU (A.S)

AL IMAM 'ALI IBN ABI TALIB (A.S)

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) ametaja madhara ya kimwili ya kijicho:

"Naustaajabia mghafala wa mahasidi juu ya uzima wa miili yao."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 494.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Kijicho huuangamiza mwili."

Ghuraru 'l-Hikam, uk.32.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Jihadharini na uhasidi, kwani huitia ila nafsi."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 141.

AL IMAM ZAYNUL ABIDIN (A.S)

Al Imam Zaynul Abidin(a.s) alimwomba Allah swt hivi:

"Ewe Allah swt ! Teremsha rehema na baraka kwa Muhammad na Aali za Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ; na nipe kifua kilichohifadhika na uhasidi, ili kwamba nisimwonee wivu yoyote kati ya viumbe Vyako juu ya fadhila Zako; wala nisione kijicho juu ya neema Zako ulizompa yeyote kati ya viumbe Vyako - ziwe ni neema za dini au dunia, afya au takwa, nyingi au nyepesi, ila kwamba nitamani bora zaidi kwa ajili yangu lakini kutoka Kwako peke Yako, (Ewe) usiye na mshirika."

Sahifah Kamilah, dua ya 22.

AL IMAM 'ALI IBN ABI TALIB (A.S)

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Shindaneni katika maadili yanayovutia, matumaini makubwa na mawazo matukufu ili mpate jazaa kubwa."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 355.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Lau Allah swt angeruhusu kiburi kwa waja wake, basi angewaruhusu Manabii na Mawalii Wake. Lakini Allah swt amewakataza kuwa na kiburi na amewaridhia kuwa na unyenyekevu. Hivyo, huweka videvu vyao juu ya ardhi (kumnyenyekea Allah swt), huzisugua nyuso zao kwenye ardhi, na huwanyenyekea waumini."

MTUME MUHAMMAD MUSTAFA (S.A.W.W)

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

"Jiepusheni na kiburi, kwani mja anapotakabari, Allah swt husema: 'Mwandikeni mja huyu miongoni mwa waasi.'"

Nahju 'l-Fusahah, uk. 12.

AL IMAM JA'AFER AS-SADIQ (A.S)

Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) ametaja kwa ufupi asili ya kinafsi ya ndweo na majivuno:

"Hakuna mtu anayeugua kiburi ila kwamba amehisi uduni (dhila) nafsini mwake."

Al-Kafi, jz. 3, uk. 461.

Al Imam Musa bin Jaafar(a.s) amesema:

"Maringo na majivuno yana vidato; kimojawapo ni kumpambia mja amali yake mbaya akaiona nzuri na akaipenda na kufikiria kwamba amefanya vizuri."

Wasa'ilu 'sh-Shi'ah, jz.1, uk. 74.

AL IMAM 'ALI IBN ABI TALIB (A.S)

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Jihadhari na kujipenda (kujiona) mwenyewe, kwani utazidiwa na wenye kukuchukia."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 147.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Kiburi huharibu akili."

Ghuraru 'l-Hikam, uk 26.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Mwenye kudhoofisha fikra zake huimarisha ghururi yake."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 651.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Unyenyekevu ni kiini cha akili, na majivuno ni kiini cha ujinga."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 102.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Kibur ni maradhi ya ndani."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 478.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Mwenye kuona bora mwendo wake, hushindwa kurekebisha nafsi yake."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 677.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Mwenye kujipenda nafsi yake haoni aibu zake, na lau angejua mema ya wengine angetengeneza dosari na hasara zake."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 95.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Jikingeni kwa Allah swt kutokana na ulevi wa utajiri, kwani una nishai (ulevi) inayochelewa kutoka."

Ghuraru 'l-Hikam, uk.138.

MTUME MUHAMMAD MUSTAFA (S.A.W.W)

Siku moja tajiri mmoja alikwenda katika baraza la Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) Baadaye akaja maskini mmoja na akakaa karibu na tajiri huyo. Tajiri akakusanya nguo zake alipomwona maskini amekaa ubavuni mwake. Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) akamwambia tajiri:"Unaogopa umaskini wake ukuguse?" Tajiri akajibu: "Hapana!" Akamwuliza:"Unaogopa sehemu ya mali yako aipate yeye?" Akajibu:"Hapana!" Akamwuliza:"Unaogopa nguo zako ziingie uchafu?" Akajibu: "Hapana!"

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) akamwuliza: "Basi kwa nini umezikusanya nguo zako na umekikunja kipaji chako ?" Tajiri akasema:"Ewe mtume wa Allah swt! Utajiri wangu na mali zangu zimenifumba macho yangu nisitambue uhakika, na zimenifanya niyaone mazuri yale mabaya yangu. Kwa kufuta kosa hilo lisilofaa, natoa nusu ya mali zangu kumpa maskini huyu." Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) akamwuliza maskini:"Je, unaikubali tuzo hiyo?"

Maskini akakataa, na alipoulizwa sababu yake, akasema:"Naogopa nami pia nisiwe na sifa mbaya kama yake baada ya kuwa na utajiri mwingi."

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

"Wafanyieni uadilifu watoto wenu katika kutoa zawadi kama vile mtakavyopenda wakufanyieni uadilifu kwa mema na mapenzi."

Nahju 'l-Fasahah, uk. 66.

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

"Mcheni Allah swt na adiliana na watoto wenu kama vile mpendavyo wakutendeeni wema."

Nahju 'l-Fasahah, uk. 8.

AL IMAM 'ALI IBN ABI TALIB (A.S)

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Wafanyie (Wamisri) uadilifu, endeana nao kwa upole, changamka nao, na fanya insafu katika kuwatazama pia ili kwamba watukufu wasitazamie dhuluma kutoka kwako wala wanyonge wasikate tamaa ya kuona uadilifu kutoka kwako." Mabalozi wa Allah swt ni waasisi wa uadilifu na waratibu wa sera ya ukamilifu wa mwanadamu. Katika zama za ukhalifa wa Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) , siku moja Aqil alikwenda kwa ndugu yake mtawala (yaani Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) ). Baada ya kumwelezea matatizo yake na umaskini wake, akamshika nduguye (Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) .) ampe karibu mani moja (ratili mbili) ya ngano zaidi kuliko sehemu yake kutoka Baitul Maal (Hazina). Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) badala ya kumkubalia akamsogezea kipande cha chuma kilichopashwa moto ili kumwonya. Aqil akapiga kelele. Hapo Imam(a.s) akamwambia:

"Ewe Aqil! Mamako akulilie! Unapiga kelele hivyo kwa kuogopa kipande cha chuma tu kilichopashwa moto na mtu, lakini mimi nitavumilia vipi moto utakaowashwa kwa ghadhabu za Allah swt ? Je, inafaa wewe upige kelele kwa sababu ya kuungua mwili, nami nivumilie adhabu ya roho?"

Baada ya ya kusema hayo, akaongeza: "Wallahi! Hata kama nitapewa dunia nzima pamoja na utajiri wake wote ili kwamba nimnyang'anye siafu ganda la shayiri alilonalo mdomoni mwake, sitafanya hivyo kamwe! Mimi ni duni na haina thamani kuliko ganda hilo hata kutaka kumuudhi siafu."

Nahaj 'l-Balaghah, uk. 877.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Kutosamehe ni aibu mbaya kuliko zote, na kulipiza kisasi ni dhambi kubwa kuliko zote."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 537.

Vile vile Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amewasifu waungwana wanasamehe makosa ya wengine, kwa kusema:

"Ni murua wa watukufu kusamehe makosa kwa haraka."

Ghuraru 'l-Hikam, uk.768.

Mambo mazuri na mabaya hayawi kamwe sawasawa katika dunia hii. Hivyo, ni afadhali kulipa ubaya kwa amali njema kabisa ili kwamba yule aliyekufanyia ubaya na uadui awe ni rafiki yako wa karibu.

Msamaha huwa na thamani kubwa sana wakati mtu anapokuwa na uwezo na nguvu za kulipiza.

AL IMAM JA'AFER AS-SADIQ (A.S)

Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) ameihesabu sifa hii tukufu kuwa ni miongoni mwa sifa njema za Mitume na wachaji:

"Msamaha wakati wa (kuwepo) uwezo (wa kulipiza ubaya) ni miongoni mwa mienendo ya Mitume na wacha-Mungu."

Safinatu 'l-Bihar, jz. 2, uk. 702.

AL IMAM 'ALI IBN ABI TALIB (A.S)

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) ameutaja msamaha kama ni silaha bora kabisa ya kuwapigia wapinzani:

"Mlaumu nduguyo kwa (kumfanyia) mema, na jiepushe na shari yake kwa kumfadhili."

Nahju 'l-Fasahah, uk. 1150.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amefichua uhakika wa ndani wa maana ya kinyongo na chuki kwa kutoa usemi mfupi:

"Moyo wa mwenye kinyongo ni mgumu kuliko nyoyo zote."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 178.

Wakati wa adhabu ya roho daima humtesa mwenye chuki.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Kinyongo huadhibu nafsi na huzidisha adhabu yake."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 85.

. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Dhamiri zinapotibiwa ndipo siri zinapojitokeza na kuonekana."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 490.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Chuki ni moto wa ndani ndani usiozimika ila kwa ushindi."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 106.

Chuki hukoka moto wa hamaki.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Chuki huwasha hasira."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 21.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Mwenye kuondoa chuki hutuliza moyo na akili yake."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 666.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Mja mwenye furaha ni yule ambaye moyo wake hauna chuki wala wivu."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 399.

AL IMAM JA'AFER AS-SADIQ (A.S)

Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema:

"Hamaki huziba (nuru ya) moyo wa mwenye hekima. Asiyeweza kuidhibiti hamaki yake hawezi kuitawala akili yake."

Usulu 'l-Kafi, jz. 2, uk. 305.

AL IMAM 'ALI IBN ABI TALIB (A.S)

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Mwenye kuiacha hamaki yake ipande, huharakisha mauti yake."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 625.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Jihadhari na hamaki, kwani mwanzo wake ni wendawazimu na mwisho wake ni majuto."

Vile vile Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Hamaki ni moto uliokokwa, mwenye kuipoza hamaki huuzima (moto wake), na mwenye kuiachilia huwa ni wa kwanza kuungua humo."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 71.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) ametuusia tuwe na subira na uvumilivu ili tuweze kukabiliana na hasira na hamaki, kwa sababu tunavihitajia hivyo kuepukana na maumivu yake.

"Jilindeni kutokana na ukali wa hamaki na jiandaeni kupambana nao kwa kuvunja hamaki na kwa kuvumilia."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 133.

Vile vile Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Kujidhibiti wakati wa kushikwa na hasira humsalimisha mtu wakati wa maangamizo."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 463.

AL IMAM MUHAMMAD AL-BAQIR (A.S)

Al Imam Muhammad al-Baqir(a.s) amesema:

"Kitu gani kilicho kiovu zaidi kuliko hamaki wakati mtu aliyepandwa na hamaki hutoa roho iliyoharamishwa na Mungu.?"

Al-Wafi, jz. 3, uk. 148.

MTUME MUHAMMAD MUSTAFA (S.A.W.W)

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ametoa mwongozo mzuri wa kufanya wakati mtu anapopandwa na hamaki:

"Ikiwa mmoja wenu atapandwa na hamaki, kama amesimama akae chini, na kama amekaa alale. Na kama hamaki haikupoa baada ya kufanya hivyo, basi atawadhe kwa maji baridi au aoge-kwani moto hauzimiki ila kwa maji."

Ahyau 'l-Ulumu 'd-Din, jz. 3, uk. 151.

AL IMAM MUHAMMAD AL-BAQIR (A.S)

Al Imam Muhammad al-Baqir(a.s) amesema:

"Allah swt hakumruhusu mtu yeyote kwenda kinyume katika mambo matatu: " Kuweka amana ya mwema au mwovu; " kutimiza ahadi ya mwema au mwovu; na " kuwatendea mema wazazi wema au waovu."

Al-Kafi, jz. 2, Uk. 162.

MTUME MUHAMMAD MUSTAFA (S.A.W.W)

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ametaja kuvunja ahadi kama ni alama mojawapo ya unafiki:

"Mwenye kuwa na sifa nne (zifuatazo) ni mnafiki; na hata akiwa nayo mojawapo kati ya hizo pia atasifika kwa unafiki isipokuwa aiache: " Mwenye kusema uwongo anapozungumza; " mwenye kuvunja ahadi anapoahidi; " mwenye kufanya hiana anapoaminiwa; na " mwenye kufisidi anapogombana."

Biharu 'l-Anwar, jz. 15, uk. 234.

AL IMAM 'ALI IBN ABI TALIB (A.S)

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) ameandika:

"Jihadhari usiwasimange raia zako kwa hisani ulizowafanyia, wala usijione bora kwa ajili ya kazi unazowafanyia, na unapowaahidi usiende kinyume na ahadi zako. Hakika masimango huharibu hisani, na kujiona huondoa nuru ya haki, na kuvunja ahadi husababisha kuchukiwa na Allah swt na watu. Allah swt anasema: katika Qur'an Tukufu, Surah Ass'af, 61, Ayah 3 'Ni chukizo kubwa mbele ya Allah swt kusema msiyoyatenda."

Mustadriku 'l-Wasa'il, jz. 2, uk. 85.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Kutimiza ahadi hufuatana na uaminifu, nami sikijui kinga kinachokinga vizuri zaidi kuliko kutimiza ahadi."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 228.

MTUME MUHAMMAD MUSTAFA (S.A.W.W)

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

"Mtu asimwahidi mwanae asipoweza kutimiza."

Nahju 'l Fasahah, uk. 201.

AL IMAM 'ALI IBN ABI TALIB (A.S

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) ameonyesha namna ya mtu kusuhubiana na mwenzake:

"Ukimchagua mtu kuwa rafiki yako, basi kuwa mtumishi wake na mwonyeshe uaminifu wako wa kweli na moyo safi."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 323.

MTUME MUHAMMAD MUSTAFA (S.A.W.W)

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

"Mwenye furaha kayaya kuliko watu wote ni yule mwenye kuingiliana na watu watukufu na ambaye huendeana na watu bila ya kuwadhulumu, huzungumza nao bila ya kuwadanganya, na huahidiana nao bila ya kuvunja. Hakika mtu kama huyu amekamilisha murua wake, amedhihirisha uadilifu wake, na anastahiki udugu na urafiki wake."

QUR'AN TUKUFU

Allah swt amezitaja sheria alizowatungia waja wake kama ni amana, na amekataza kabisa kufanya khiana ya aina yoyote: katika Qur'an Tukufu, Surah Al-Anfaal, 8, Ayah 27:

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَخُونُوا اللَّـهَ وَالرَّسُولَ وَتَخُونُوا أَمَانَاتِكُمْ وَأَنتُمْ تَعْلَمُونَ﴾

Enyi mlioamini! Msimfanyie khiana Allah swt na Mtume Muhammad Mustafa (s.a.w.w) na mkakhini amana zenu na hali mnajua.

Vile vile Allah swt amesema: katika Qur'an Tukufu, Surah An-Nisaa, 4., Ayah 58:

﴿إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُكُمْ أَن تُؤَدُّوا الْأَمَانَاتِ إِلَىٰ أَهْلِهَا﴾

Hakika Allah swt anakuamrisheni kuzirudisha amana kwa wenyewe.

AL IMAM 'ALI IBN ABI TALIB (A.S)

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema: Ghuraru 'l-Hikam, uk. 505. "Ukomo cha khiana ni kumfanyia khiana rafiki mpendwa na kuvunja ahadi." Vile vile Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema: Ghuraru 'l-Hikam, uk. 446. "Mtu mwovu kuliko wote ni yule asiyeamini kuweka amana wala hajizuii kufanya khiana."

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Jihadharini na khiana kwani ni dhambi mbaya kabisa; na kwamba mwenye kukhini ataadhibiwa katika Moto kwa khiana yake."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 150.

AL IMAM JA'AFER AS-SADIQ (A.S)

Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema:

"Halahala na kusema ukweli na kurejesha amana kwa mwema au mwovu, kwani sifa mbili hizi ni ufunguo wa riziki."

Safinatu 'l-Bihar, jz. 1, Uk. 41.

AL IMAM ZAYNUL ABIDIN (A.S)

Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Halahala na kuweka amana. Naapa kwa yule aliyembaathi Muhammad kwa haki kuwa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) , kwamba lau mwuaji wa babangu Husayn bin Ali angenipa upanga ule aliomwulia bababngu, kumwekea amana, nisingemfanyia khiana."

Amali as-Sadaq, uk. 149.

MTUME MUHAMMAD MUSTAFA (S.A.W.W)

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

"Mwenye kutenda kitendo kiovu atalipwa (hapahapa) duniani."

Nahju 'l-Fasahah, Uk. 592.

AL IMAM 'ALI IBN ABI TALIB (A.S)

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Uaminifu katika (kuweka) amana ni alama ya usafi wa mwenye imani."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 453.

Vile vile Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Khiana ni dalili ya upungufu wa uchaji na utovu wa dini."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 53.

AL IMAM SAJJAD (A.S)

Al Imam Sajjad(a.s) amesema:

"Una wajibu wa kumlea (Mwanao) kwa adabu nzuri, kumwongoza kwa Mola wake Mtukufu, na kumsaidia katika kumtii."

Al-Wafi, uk. 127.

AL IMAM 'ALI IBN ABI TALIB (A.S)

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Wenye akili huhitajia adabu kama vile shamba linavyohitajia mvua."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 224.

MTUME MUHAMMAD MUSTAFA (S.A.W.W)

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

"Hakuna jambo linalochukiwa mno katika Uislamu kama uchoyo."

Nahju 'l-Fasahah, uk. 549.

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

"Mwenye kuwa na raha kidogo kabisa kati ya watu wote ni bakhili."

Nahju 'l-Fasahah, uk. 81.

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

"Allah swt amrehemu mtu anayebana mengi (ziada) ya maneno yake, na anayetoa ziada ya mali yake."

Nahju 'l-Fasahah, uk. 81.

Vile vile Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

"Jihadhari na uchoyo, kwani uchoyo umewaangamiza waliokutangulia, umewafanya wamwage damu zao, na wahalalishe yaliyoharamishwa."

Nahju 'l-Fasahah, uk. 8.

AL IMAM 'ALI IBN ABI TALIB (A.S)

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Nashangaa juu ya bakhili mwovu; huuharakisha umaskini anaokimbia na huupoteza utajiri anaotafuta. Huishi katika dunia maisha ya maskini na atahukumiwa katika Akhera kwa hesabu ya matajiri."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 497.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Ukarimu wa mtu huwafanya maadui zake wampende, na ubakhili wake humfanya achukiwe na watoto wake."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 368.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Uroho na uchoyo umesimama juu ya msingi wa shaka na kutoaminiwa."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 488.

AL IMAM MUSA AL-KADHIM (A.S)

Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) ameelezea juu ya thamani ya ukarimu:

"Karimu mwenye murua yuko katika ulinzi wa Allah swt; na Allah swt hamwachi mpaka amtie Peponi. Allah swt hamtumi Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) wala Wasii yeyote ila kwamba huwa ni karimu; wala hakutokea mwema yeyote ila kwamba alikuwa karimu. Babangu hajafariki mpaka aliponiusia ukarimu."

Furu' al-Kafi, jz. 4, uk. 38.

AL IMAM MUHAMMAD AL-BAQIR (A.S)

Al Imam Muhammad al-Baqir(a.s) ameshabihisha maisha ya mroho na taswira hii:

"Mfano wa mwenye tamaa ya dunia ni kama kiwavi cha nondo, kila akizidi kujizungushia nyuzi (za hariri) ndivyo hujifungia mpaka kufa kwa kujisonga roho."

Usulu 'l-Kafi, Babu ya Huba ya Dunia.

MTUME MUHAMMAD MUSTAFA (S.A.W.W)

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

"Jihadharini na uchu wa mali, kwani uliwaangamiza waliokutangulieni. Uchu uliwashawishi mabakhili na wakafanya ubakhili; uliwaamrisha kukata ujamaa na wakakata; na uliwaamrisha ufisadi na wakafanya ufisadi."

Nahju 'l-Fasahah, uk. 199.

AL IMAM 'ALI IBN ABI TALIB (A.S)

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Epukaneni na mwenye tamaa, kwani kuingiliana naye huleta udhalili na mashaka."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 135.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Mwenye tamaa ni mfungwa wa udhalili na kifungo chake hakifungiki."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 50.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) ameashiria jambo hili kwa usemi murua:

"Mtukufu kuliko wote ni yula ambaye hukata tamaa (juu ya watu), hushika ukinaifu na uchaji, na huacha uroho na tamaa, kwani tamaa na uroho ni sawa na umaskini, na kukata tamaa (juu ya watu) na ukinaifu ni utajiri wa dhahiri."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 255.

Anayejifanya mtumwa wa tama na uchu, huutia maradhi mwili na roho yake.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) anasema:

"Kila mwenye tamaa ni mgonjwa."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 544.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema;

"Tamaa huchafua nafsi, huharibu dini (imani) na huondoa uungwana."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 77.

MTUME MUHAMMAD MUSTAFA (S.A.W.W)

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ametaja matatizo yanayotokana na tamaa:

"Mwenye tamaa husumbuliwa na matatizo saba mabaya:

1. Fikra inayomdhuru mwili wake na isiyomnufaisha;

2. hamu (hima) isiyokwisha;

3. tamaa isiyompa raha ila baada ya kufa na wakati wa kupumzika huona taabu zaidi;

4. hofu isiyoacha kumhangaisha;

5. huzuni inayofanya maisha yake machungu bila ya kuwa na faida;

6. hesabu isiyomsalimisha na adhabu ya Allah swt ila asemehewe na Allah swt; na

7. adhabu asiyoweza kuikimbia wala kuiepuka."

Mustadriku 'l-Wasa'il, jz. 2, uk. 435.

AL IMAM 'ALI IBN ABI TALIB (A.S)

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Tamaa humsukuma mtu kwenye mabaya."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 16.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) vile vile amesema:

"Matokeo ya tamaa ni kumtia mtu katika aibu."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 360.

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

"Miongoni mwa (alama za) uungwana ni mtu kunyamaza kimya na kumsikiliza ndugu yake anaposema."

Nahju 'l-Fasahah, uk. 633.

AL IMAM MUHAMMAD AL-BAQIR (A.S)

Al Imam Muhammad al-Baqir(a.s) amesema:

"Na jifunze kusikiliza vizuri kama vile unavyojifunza kusema vizuri, wala usimkatize mtu yeyote anaposema."

AL IMAM JA'AFER AS-SADIQ (A.S)

Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema:

"Mja hataipata imani halisi mpaka atakapoacha ubishi hata kama ni haki."

Safinatu 'l-Bahar, jz. 2, uk. 522.

AL IMAM HAD (A.S)

Al Imam Had(a.s) amesema:

"Ubishi huharibu urafiki wa muda mrefu, huvunja uhusiano ulio madhubuti, na sehemu ndogo ya kitu kinachopatikana ni mashindano - na mashindano yenyewe ni chanzo hasa cha kutosikilizana."

AL IMAM JA'AFER AS-SADIQ (A.S)

Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema:

"Epukaneni na mabishano, kwani huunguza moyo, huleta unafiki na husababisha chuki."

Usulu 'l-Kafi, jz. 1, uk. 452.

MTUME MUHAMMAD MUSTAFA (S.A.W.W)

Mtume Mtukufu(s.a.w.w) amesema:

"Hakika,miongoni mwa dalili za saa, ni kuwa

1. watu watapuuza sala

2. watafuata matamanio yao wenyewe

3. wataelekeza kujipendelea wao wenyewe, watawaheshimu matajiri,

4. na watauza Dini yao kwa manufaa ya kidunia

5. wakati huo roho na moyo wa Muumin itayayuka (kwa huzuni) kama chumvi inavyoyayuka katika maji, kwa sababu ataona mambo yaliyoharamishwa na hataweza kuyabadili."

Salman akasema: "Haya yatatokea, ewe Mtume wa Allah swt?" Mtume Mtukufu(s.a.w.w) akasema:"Ndiyo, naapa kwa Aliyonayo roho yangu mkononi mwake." "Ewe Salman ,

6. wakati huo watawala watakuwa wadhalimu

7. Mawaziri watakuwa waasi,

8. na wadhamini (wale waliopewa amana kwa kuaminiwa) watafanya hiana,

9. hakika wakati huo maovu yatakuwa mema na mema yatakuwa maovu,

10. wale wafanyao hiana wataaminiwa na waaminifu watafikiriwa kuwa si waaminifu;na mwongo atasadikiwa,na msema kweli atahesabiwa mwongo.

11. Wakati huo kutakuwapo na utawala wa wanawake,

12. Masuria watashauriwa,

13. na watoto watakaa juu ya mimbar,

14. udanganyifu utahesabiwa kuwa ni uerevu

15. na Zaka itakuwa ni kama kutozwa faini;na mateka ya vita (yaani mali ya ummah) yatakuwa kama ni mali ya mtu binafsi;na mtu atakuwa mjeuri kwa wazazi wake na atakuwa mwema kwa marafiki zake,

16. na wakati huo kutatokea na nyota zenye mikia (comets)."

Salman akasema: "Haya yatatokea,ewe Mtume wa Allah swt?" Mtume Mtukufu(s.a.w.w) akasema:"Ndiyo,naapa kwa Aliyonayo roho yangu mkononi mwake." "Ewe Salman!

17. wakati huo mwanamke atakuwa mshiriki wa mumewe katika biashara,

18. na mvua itakuwa moto sana

19. na watu wema watabaki katika huzuni;na masikini hawata heshimiwa;na wakati huo masoko yatakaribiana,

20. Tena huyu atasema,"Mimi sikuuza chochote,na yule atasema, "Mimi sikupata faida yoyote." Kwa hivyo hutamkuta mtu yeyote asiyemlalamikia Allah swt.

"Ewe Salman!

21. tena itatokea iwapo watu watawazungumzia watawala wao, watawaua, na ikiwa watanyamaza kimya, watanyang'anywa mali yao, watanyimwa heshima zao,watamwaga damu yao na mioyo ya watu itajaa woga;kisha hutamwona mtu yeyote ila atakuwa mwoga,mwenye khofu,ametishika na ameshstushwa" "Ewe Salman!

22. Bila shaka wakati huo mambo fulani yataletwa kutoka Mashariki

23. na mambo fulani yataletwa kutoka Magharibi,

24. Basi ole kwa watu walio dhaifu (wa imani) katika Ummah wangu kutokana na hayo; Ole ya Allah swt iwe kwa hayo. Wao hawatakuwa na huruma juu ya wadogo

wao,wala hawatamsamehe yeyote aliyefanya kosa.Miili yao itakuwa ya wanadamu,lakini mioyo yao itakuwa ya mashetani."

"Ewe Salman!

25. Wakati huo wanaume watawaashiki wanaume,

26. na wanawake watawaashiki wanawake;

27. na watoto wa kiume watapambwa kama wanawake;

28. na wanaume watajifanya kama wanawake

29. na wanawake wataonekana kama wanaume;

30. na wanawake watapanda mipando

31. Hapo tena patakuwepo laana ya Allah swt juu ya wanawake wa Ummah wangu."

"Ewe Salman!

32. Bila shaka wakati huo Misikiti itapambwa (kwa dhahabu n.k.) kama inavyofanywa katika masinagogi na makanIssa,

33. na Qur'an zitapambwa (kwa nakshi na rangi za kupendeza n.k.)

34. na minara (ya misikiti) itakuwa mirefu;na safu za watu wanaosimama katika sala zitazidi,lakini nyoyo zao zitachukiana na maneno yao yatatofautiana."

"Ewe Salman!

35. Wakati huo wanaume watatumia mapambo ya dhahabu;kisha watavaa hariri,na watatumia ngozi za chui."

"Ewe Salman!

36. Wakati huo riba itakuwako,

37. na watu wata- fanyia biashara kwa kusemana na rushwa

38. na dini itawekwa chini,na dunia itanyanyuliwa juu."

"Ewe Salman!

39. Wakati huo talaqa zitazidi

40. na mipaka ya Allah swt hayatasimamishwa

41. Lakini hayo hayatamdhuru Allah swt."

"Ewe Salman!

42. Wakati huo watatokea wanawake waimbaji,

43. na ala za muziki

44. na wabaya kabisa watawatawala Ummah wangu."

"Ewe Salman!

45. Wakati huo matajiri katika Ummah wangu watakwenda Kuhiji kwa matembezi,na walio wastani kwa biashara,na masikini kwa kujionyesha.

46. Hivyo basi wakati huo watakuwapo watu ambao watajifundisha Qur'an si kwa ajili ya Allah swt na wataifanya Qur'an kama ala ya muziki.

47. Na watakuwapo watu ambao watasoma dini si kwa ajili ya Allah swt

48. na idadi ya wanaharamu itazidi

49. watu wataiimba Qur'an,

50. na watu watavamiana kwa uroho wa kidunia."

"Ewe Salman!

51. Haya yatatokea wakati heshima zitakapo- ondoka,na madhambi yatatendwa

52. na watu waovu watakuwa na uwezo juu ya watu wema,

53. na uongo utaenea na mabishano (matusi) yatatokea

54. na umasikini utaenea,

55. na watu watajiona kwa mavazi yao

56. na itakuwepo mvua wakati si wake

57. na watu watacheza dama, kamari na Ala za muziki,

58. na hawatapenda kuhimizana mema wala kukatazana maovu

59. na kwa ajili hali itakavyokuwa hata itafikia wakati huo kuwa Muumin atakuwa na heshima ndogo kuliko hata mjakazi

60. na wanaosoma na wanaotumia wakati wao katika kumwabudu Allah swt watalaumiana.

61. Hao ndio watu watakaoitwa wachafu na wanajisi katika Ufalme wa mbinguni."

"Ewe Salman!

62. Wakati huo matajiri hawataogopa chochote isipokuwa mtu masikini; hadi kwamba masikini wataendelea kuomba kati ya ijumaa mbili,na hawatamwona mtu yeyote wa kutia chochote mikononi mwao."

"Ewe Salman!

63. Wakati huo itazungumzwa Ruwaibidhah."

Salman akauliza:"Ni nini Ruwaibidhah ? Ewe Mtume wa Allah swt, baba na mama yangu wawe fidia kwako."

Mtukufu Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) akajibu:

64. "Watu fulani watazungumza kuhusu mambo ya watu ambayo hayakuwahi kuzungumzwa namna hii zamani.

65. Tena baada ya muda mchache machafuko yatatokea duniani,na kila nchi itafikiri kuwa machafuko yapo katika nchi yao tu."

66. "Watabaki katika hali hiyo kwa muda ambao Allah swt atapenda wabaki;

67. kisha ardhi itatapika vipande vya moyo wake dhahabu, fedha na madini mengineyo; (Hapo Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w.) alinyosha kidole chake penye nguzo, na akasema:"Kama hizi (kwa ukubwa), lakini siku hiyo dhahabu wala fedha hazitamsaidia mtu yeyote. Na hii ndiyo maana ya maneno ya Allah swt 'Hakika dalili Zake zimekuja. '

UBASHIRI WA IMAM JAAFER AS-SADIQ (A.S)

Mazungumzo yafuatayo yamefanywa na Imam Jaafer as-Sadiq(a.s) ambamo ameripoti ubashiri wa siku za mwisho wa dunia hii. Yametolewa kutoka Darul Islam,Bihar-ul-Anwar na Raudhat-ul-Kafi. Wanaoripoti habari hizo ni Allamah Naraqi na Sheikh Kulaini r.a. kutokea kwa Himran.

Imam(a.s) alisema:

1 "Haki itakuwa imetokomezwa na watu walio katika haki hawatapatikana.

4. Dhulma na uonevu utaenea katika miji yote.

5. Kufuata Qur'an kimatendo itajulikana kama tabia ya kizamani.

6. Zitatolewa maana ya Aya za Qur'an kwa mujibu wa matakwa ya watu,hivyo mafhum ya Qur'an itakuwa imebadilishwa na kupotoshwa.

7. Wadhalimu watakuwa wakiwa kandamiza wale walio katika haki.

8. Uchokozi na uchochezi utatokea kutoka kila pande na pembe.

9. Matendo maovu na kukosa aibu vitaenea na kuzagaa kila mahala.

10. Ulawiti utakuwa ni jambo la kawaida.

11. Muumin atakuwa akionekana kama mtu dhalili ilhali waovu watakuwa wakiheshimiwa

12. Vijana hawatakuwa wakiwaheshimu wakubwa wao.

13. Huruma itakuwa imepotea kabisa.

14. Waovu watakuwa wakitukuzwa kwa udhalimu wao na hakutakuwapo na mtu yeyote wa kuwapinga.

15. Wanaume watafurahishwa mno kwa kuingiliana na wanaume wenzao.

16. Wanawake watawaoa wanawake wenzao.

17. Mapesa yatatumika kwa ajili ya matumizi yale yaliyo haramishwa na Allah swt.

18. Starehe, anasa na zinaa zitashamiri.

19. Zinaa itajulikana kama maadili yaliyopitwa na muda.

20. Muumin atatengwa kwa sababu ya kufanya ibada za Allah swt.

21. Jirani mmoja atafurahi mno kwa kumuudhi na kumbughudhi jirani mwenzake.

22. Wazushi (kama Salman Rushdie wa Uingereza) watatukuzwa na kusifiwa katika kueneza fitina na yale wanayozusha.

23. Ushauri mzuri utakanwa.

24. Milango ya wema yatafungwa wakati milango ya maovu yatafunguliwa.

25. Al-Kaaba haitatumika au haitafikika kwa sababu ya vikwazo na ugumu utakaowekewa mahujaji.

26. Watu watalazimishwa kuacha kwenda Makkah kuhiji.

27. Watu hawatakuwa wakitimiza ahadi zao watakazokuwa wakizitoa.

28. Wanaume watakuwa wakitumia dawa za kuamsha tamaa za kiume kwa ajili kulawiti na wanawake watakuwa wakitumia vyakula vya mafuta ili kujitayarisha kwayo.

29. Baadhi ya wanaume watakuwa wakiishi kwa kujipatia mapesa kwa kuuza mikundu yao.

30. Na wanawake watakuwa wakijipatia mapesa kwa kufanyisha biashara kuma zao.

31. Wanawake wataunda vilabu vyao,mashirika na umoja wao.

32. Wanaume atajigeuza kama wanawake na watavutia na wanawake.

33. Wanaume watajirembesha kama wanawake.

34. Ulawiti utachukuliwa kama ndiyo ustaarabu na starehe ya kweli.

Na Banu Abbas watalipia ulawiti.

35. Wanawake wataona fakhari kwa kuwa na waume nje ya mume mmoja wa ndoa na vivyo hivyo wanaume watakuwa hivyo hivyo.

36. Heshima itakuwa ikitolewa kwa utajiri wa mtu na wala si ucha Mungu.

37. Riba ndiyo itakayokuwa biashara ya kila siku.

38. Ushahidi wa uongo utakuwa ukIssadikiwa mno.

39. Kile alichokiharamisha Allah swt kitachukuliwa ni halali na chochote kile alichokihalalisha Allah swt kitachukuliwa ni haramu.

40. Maamrisho ya Dini yatageuzwa kwa mujibu wa matakwa yao.

41. Wachokozi na waovu watatenda maovu kwa udhahiri bila ya khofu yoyote ile na Muumin hawataweza kuwazuia vyovyote vile.

42. Watawala watawapenda mno Makafiri kuliko Muumiin.

43. Rushwa ndiyo itakuwa njia ya kujitimizia kazi kutoka maofIssa wanaohusika.

44. Wanaume wata walawiti wake zao.

45. Watu watakuwa wakiuawa kwa visingizio vidogo vidogo na magomvi madogo madogo.

46. Wanawake watawafanyia wanaume dhihaka, nao watashawishiwa kufanya uhusiano na wanawake.

47. Wanaume wataishi kwa mapato ya wake zao zitakazopatikana kwa zinaa.

48. Wanawake watakuwa wakiendesha hukumu majumbani huku wanaume wakiwatii wake zao kwa sababu wanawake hao ndio watakuwa wenye mapato.

49. Wanawake watatumiwa katika kupatikana huduma mbalimbali.

50. Kula kiapo kwa jina la Allah swt litakuwa ni jambo lililowekwa ulimini.

51. Pombe na kamari vitapatikana kila mahala na vitakuwa vimezagaa.

52. Wanawake wa Kiislamu wataingiliana na Makafiri,ambapo Waislamu hawataweza kuwazuia na wala hawatakuwa na uwezo kama huo.

53. Maadui wetu watasaidiwa na watawala na marafiki zetu watadhalilishwa kiasi kwamba hata kiapo chao hakitakubaliwa.

54. Udanganyifu na hila ndizo zitakuwa desturi miongoni mwa watu.

55. Usomaji na usikilizaji wa Qur'an utakuwa ni bughudha kwa watu.

56. Kusikiliza mambo fidhuli ndiyo itakuwa ikipendelewa na watu.

57. Jirani hatamstahi jirani mwenzake illa kwa khofu ya ulimi mkali na mchafu.

58. Sheria na kanuni za Allah swt hazitatambuliwa na waovu hawataadhibiwa kwa maamrisho hayo.

59. Ghiba na kulaghaiana ndivyo vitakuwa vitu vya kawaida.

60. Madhumuni ya Hajj na Jihad yatakuwa mbali na yale ya Kiislamu.

61. Misikiti itarembeshwa kwa dhahabu.

62. Watawala watawataka ushauri kwa nia ya Makafiri.

63. Litakuwa ni jambo la kawaida kuibia katika uzani na vipimo vya biashara.

64. Kumwaga damu ya watu wegine litakuwa ni jambo la kawaida.

65. Watu watajigamba kwa ndimi zao chafu zenye matusi mabaya ili kuwatishia watu wengine.

Imam a.s. aliendelea kusema:

66. "Watu watakuwa wakipuuzia sala na kutojali.

67. Watu hawatakuwa wakilipa zaka ingawaje watakuwa na utajiri mkubwa.

68. Sanda za maiti zitakuwa zikiibiwa na kuuzwa tena.

69. Mauaji yatakithiri mno kiasi kwamba hata wanyama pia wataanza kuuana wenyewe kwa wenyewe.

70. Watu watakuwa wakIssali katika mavazi ya kiajabu.

71. Macho na mioyo itapoteza nuru zao za heshima na huruma.

72. Watu watakuwa wamejishughulisha na maswala ya kutafuta mali na mapesa tu.

73. Watu watasali kwa kuonyesha tu.

74. Watu watatafuta ilimu ya Dini kwa ajili ya kujipatia mali ya dunia.

75. Ushirika katika makundi yatakuwa ndiyo mambo ya maisha.

76. Wale watakaojipatia riziki kwa njia ya halali,watasifiwa kwa midomo tu.

77. Matendo maovu na machafu yataenea hata Makkah na Madina.

78. Watu waliokufa watafanyiwa mizaha na vichekesho.

79. Mwaka hadi mwaka hali itakuwa ikiendelea kuharibika kuwa mbaya zaidi.

80. Matajiri wataigwa.

81. Masikini, mafukara watafanyiwa dhihaka na kufedheheshwa.

82. Matukio ya kudura kama yale ya mitetemeko,maporomoko n.k. yatakuwapo lakini watu watakuwa hawaviogopi.

83. Matendo maovu yatakuwa yakitendwa kiwaziwazi.

84. Wazazi watatupa watoto wao na watoto watawatusi wazazi wao na daima watakuwa wakitaka mali na utajiri wa wazazi wao.

85. Wanawake hawatawatii na kuwafuata waume wao.

86. Siku itakayopita bila ya mtu kutenda madhambi,basi itachukuliwa ni siku yenye nuksi.

87. Watu wenye uwezo wataficha mali muhimu na kuviuza kwa bei ya ulanguzi.

88. Waombaji na walaghai watajumuika katika kucheza kamari na kulewa.

89. Pombe itatumika kama ni kitu chenye kuponya i.e.dawa.

90. Makafiri watatukuzwa juu ya watu wengine na Muumin watadhalilishwa na kupuuzwa.

91. Kutafanywa malipo kwa ajili ya kutoa Adhan na sala.

92. Misikiti itajaa kwa watu wasiokuwa na khofu ya Allah swt.

93. Watu wenye fahamu na akili kasoro ndio watakaokuwa wakiongoza sala za jamaa' na watu kama hao kamwe hawatashutumiwa au kusutwa na badili yake wataheshimiwa."

9

HADITHI ZA MTUME (S.A.W.W) PAMOJA NA MAIMAMU (A.S)

AL IMAM 'ALI IBN ABI TALIB (A.S)

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) ametaja madhara ya kimwili ya kijicho:

"Naustaajabia mghafala wa mahasidi juu ya uzima wa miili yao."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 494.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Kijicho huuangamiza mwili."

Ghuraru 'l-Hikam, uk.32.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Jihadharini na uhasidi, kwani huitia ila nafsi."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 141.

AL IMAM ZAYNUL ABIDIN (A.S)

Al Imam Zaynul Abidin(a.s) alimwomba Allah swt hivi:

"Ewe Allah swt ! Teremsha rehema na baraka kwa Muhammad na Aali za Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ; na nipe kifua kilichohifadhika na uhasidi, ili kwamba nisimwonee wivu yoyote kati ya viumbe Vyako juu ya fadhila Zako; wala nisione kijicho juu ya neema Zako ulizompa yeyote kati ya viumbe Vyako - ziwe ni neema za dini au dunia, afya au takwa, nyingi au nyepesi, ila kwamba nitamani bora zaidi kwa ajili yangu lakini kutoka Kwako peke Yako, (Ewe) usiye na mshirika."

Sahifah Kamilah, dua ya 22.

AL IMAM 'ALI IBN ABI TALIB (A.S)

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Shindaneni katika maadili yanayovutia, matumaini makubwa na mawazo matukufu ili mpate jazaa kubwa."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 355.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Lau Allah swt angeruhusu kiburi kwa waja wake, basi angewaruhusu Manabii na Mawalii Wake. Lakini Allah swt amewakataza kuwa na kiburi na amewaridhia kuwa na unyenyekevu. Hivyo, huweka videvu vyao juu ya ardhi (kumnyenyekea Allah swt), huzisugua nyuso zao kwenye ardhi, na huwanyenyekea waumini."

MTUME MUHAMMAD MUSTAFA (S.A.W.W)

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

"Jiepusheni na kiburi, kwani mja anapotakabari, Allah swt husema: 'Mwandikeni mja huyu miongoni mwa waasi.'"

Nahju 'l-Fusahah, uk. 12.

AL IMAM JA'AFER AS-SADIQ (A.S)

Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) ametaja kwa ufupi asili ya kinafsi ya ndweo na majivuno:

"Hakuna mtu anayeugua kiburi ila kwamba amehisi uduni (dhila) nafsini mwake."

Al-Kafi, jz. 3, uk. 461.

Al Imam Musa bin Jaafar(a.s) amesema:

"Maringo na majivuno yana vidato; kimojawapo ni kumpambia mja amali yake mbaya akaiona nzuri na akaipenda na kufikiria kwamba amefanya vizuri."

Wasa'ilu 'sh-Shi'ah, jz.1, uk. 74.

AL IMAM 'ALI IBN ABI TALIB (A.S)

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Jihadhari na kujipenda (kujiona) mwenyewe, kwani utazidiwa na wenye kukuchukia."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 147.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Kiburi huharibu akili."

Ghuraru 'l-Hikam, uk 26.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Mwenye kudhoofisha fikra zake huimarisha ghururi yake."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 651.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Unyenyekevu ni kiini cha akili, na majivuno ni kiini cha ujinga."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 102.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Kibur ni maradhi ya ndani."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 478.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Mwenye kuona bora mwendo wake, hushindwa kurekebisha nafsi yake."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 677.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Mwenye kujipenda nafsi yake haoni aibu zake, na lau angejua mema ya wengine angetengeneza dosari na hasara zake."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 95.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Jikingeni kwa Allah swt kutokana na ulevi wa utajiri, kwani una nishai (ulevi) inayochelewa kutoka."

Ghuraru 'l-Hikam, uk.138.

MTUME MUHAMMAD MUSTAFA (S.A.W.W)

Siku moja tajiri mmoja alikwenda katika baraza la Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) Baadaye akaja maskini mmoja na akakaa karibu na tajiri huyo. Tajiri akakusanya nguo zake alipomwona maskini amekaa ubavuni mwake. Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) akamwambia tajiri:"Unaogopa umaskini wake ukuguse?" Tajiri akajibu: "Hapana!" Akamwuliza:"Unaogopa sehemu ya mali yako aipate yeye?" Akajibu:"Hapana!" Akamwuliza:"Unaogopa nguo zako ziingie uchafu?" Akajibu: "Hapana!"

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) akamwuliza: "Basi kwa nini umezikusanya nguo zako na umekikunja kipaji chako ?" Tajiri akasema:"Ewe mtume wa Allah swt! Utajiri wangu na mali zangu zimenifumba macho yangu nisitambue uhakika, na zimenifanya niyaone mazuri yale mabaya yangu. Kwa kufuta kosa hilo lisilofaa, natoa nusu ya mali zangu kumpa maskini huyu." Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) akamwuliza maskini:"Je, unaikubali tuzo hiyo?"

Maskini akakataa, na alipoulizwa sababu yake, akasema:"Naogopa nami pia nisiwe na sifa mbaya kama yake baada ya kuwa na utajiri mwingi."

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

"Wafanyieni uadilifu watoto wenu katika kutoa zawadi kama vile mtakavyopenda wakufanyieni uadilifu kwa mema na mapenzi."

Nahju 'l-Fasahah, uk. 66.

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

"Mcheni Allah swt na adiliana na watoto wenu kama vile mpendavyo wakutendeeni wema."

Nahju 'l-Fasahah, uk. 8.

AL IMAM 'ALI IBN ABI TALIB (A.S)

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Wafanyie (Wamisri) uadilifu, endeana nao kwa upole, changamka nao, na fanya insafu katika kuwatazama pia ili kwamba watukufu wasitazamie dhuluma kutoka kwako wala wanyonge wasikate tamaa ya kuona uadilifu kutoka kwako." Mabalozi wa Allah swt ni waasisi wa uadilifu na waratibu wa sera ya ukamilifu wa mwanadamu. Katika zama za ukhalifa wa Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) , siku moja Aqil alikwenda kwa ndugu yake mtawala (yaani Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) ). Baada ya kumwelezea matatizo yake na umaskini wake, akamshika nduguye (Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) .) ampe karibu mani moja (ratili mbili) ya ngano zaidi kuliko sehemu yake kutoka Baitul Maal (Hazina). Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) badala ya kumkubalia akamsogezea kipande cha chuma kilichopashwa moto ili kumwonya. Aqil akapiga kelele. Hapo Imam(a.s) akamwambia:

"Ewe Aqil! Mamako akulilie! Unapiga kelele hivyo kwa kuogopa kipande cha chuma tu kilichopashwa moto na mtu, lakini mimi nitavumilia vipi moto utakaowashwa kwa ghadhabu za Allah swt ? Je, inafaa wewe upige kelele kwa sababu ya kuungua mwili, nami nivumilie adhabu ya roho?"

Baada ya ya kusema hayo, akaongeza: "Wallahi! Hata kama nitapewa dunia nzima pamoja na utajiri wake wote ili kwamba nimnyang'anye siafu ganda la shayiri alilonalo mdomoni mwake, sitafanya hivyo kamwe! Mimi ni duni na haina thamani kuliko ganda hilo hata kutaka kumuudhi siafu."

Nahaj 'l-Balaghah, uk. 877.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Kutosamehe ni aibu mbaya kuliko zote, na kulipiza kisasi ni dhambi kubwa kuliko zote."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 537.

Vile vile Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amewasifu waungwana wanasamehe makosa ya wengine, kwa kusema:

"Ni murua wa watukufu kusamehe makosa kwa haraka."

Ghuraru 'l-Hikam, uk.768.

Mambo mazuri na mabaya hayawi kamwe sawasawa katika dunia hii. Hivyo, ni afadhali kulipa ubaya kwa amali njema kabisa ili kwamba yule aliyekufanyia ubaya na uadui awe ni rafiki yako wa karibu.

Msamaha huwa na thamani kubwa sana wakati mtu anapokuwa na uwezo na nguvu za kulipiza.

AL IMAM JA'AFER AS-SADIQ (A.S)

Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) ameihesabu sifa hii tukufu kuwa ni miongoni mwa sifa njema za Mitume na wachaji:

"Msamaha wakati wa (kuwepo) uwezo (wa kulipiza ubaya) ni miongoni mwa mienendo ya Mitume na wacha-Mungu."

Safinatu 'l-Bihar, jz. 2, uk. 702.

AL IMAM 'ALI IBN ABI TALIB (A.S)

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) ameutaja msamaha kama ni silaha bora kabisa ya kuwapigia wapinzani:

"Mlaumu nduguyo kwa (kumfanyia) mema, na jiepushe na shari yake kwa kumfadhili."

Nahju 'l-Fasahah, uk. 1150.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amefichua uhakika wa ndani wa maana ya kinyongo na chuki kwa kutoa usemi mfupi:

"Moyo wa mwenye kinyongo ni mgumu kuliko nyoyo zote."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 178.

Wakati wa adhabu ya roho daima humtesa mwenye chuki.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Kinyongo huadhibu nafsi na huzidisha adhabu yake."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 85.

. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Dhamiri zinapotibiwa ndipo siri zinapojitokeza na kuonekana."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 490.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Chuki ni moto wa ndani ndani usiozimika ila kwa ushindi."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 106.

Chuki hukoka moto wa hamaki.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Chuki huwasha hasira."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 21.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Mwenye kuondoa chuki hutuliza moyo na akili yake."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 666.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Mja mwenye furaha ni yule ambaye moyo wake hauna chuki wala wivu."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 399.

AL IMAM JA'AFER AS-SADIQ (A.S)

Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema:

"Hamaki huziba (nuru ya) moyo wa mwenye hekima. Asiyeweza kuidhibiti hamaki yake hawezi kuitawala akili yake."

Usulu 'l-Kafi, jz. 2, uk. 305.

AL IMAM 'ALI IBN ABI TALIB (A.S)

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Mwenye kuiacha hamaki yake ipande, huharakisha mauti yake."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 625.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Jihadhari na hamaki, kwani mwanzo wake ni wendawazimu na mwisho wake ni majuto."

Vile vile Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Hamaki ni moto uliokokwa, mwenye kuipoza hamaki huuzima (moto wake), na mwenye kuiachilia huwa ni wa kwanza kuungua humo."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 71.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) ametuusia tuwe na subira na uvumilivu ili tuweze kukabiliana na hasira na hamaki, kwa sababu tunavihitajia hivyo kuepukana na maumivu yake.

"Jilindeni kutokana na ukali wa hamaki na jiandaeni kupambana nao kwa kuvunja hamaki na kwa kuvumilia."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 133.

Vile vile Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Kujidhibiti wakati wa kushikwa na hasira humsalimisha mtu wakati wa maangamizo."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 463.

AL IMAM MUHAMMAD AL-BAQIR (A.S)

Al Imam Muhammad al-Baqir(a.s) amesema:

"Kitu gani kilicho kiovu zaidi kuliko hamaki wakati mtu aliyepandwa na hamaki hutoa roho iliyoharamishwa na Mungu.?"

Al-Wafi, jz. 3, uk. 148.

MTUME MUHAMMAD MUSTAFA (S.A.W.W)

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ametoa mwongozo mzuri wa kufanya wakati mtu anapopandwa na hamaki:

"Ikiwa mmoja wenu atapandwa na hamaki, kama amesimama akae chini, na kama amekaa alale. Na kama hamaki haikupoa baada ya kufanya hivyo, basi atawadhe kwa maji baridi au aoge-kwani moto hauzimiki ila kwa maji."

Ahyau 'l-Ulumu 'd-Din, jz. 3, uk. 151.

AL IMAM MUHAMMAD AL-BAQIR (A.S)

Al Imam Muhammad al-Baqir(a.s) amesema:

"Allah swt hakumruhusu mtu yeyote kwenda kinyume katika mambo matatu: " Kuweka amana ya mwema au mwovu; " kutimiza ahadi ya mwema au mwovu; na " kuwatendea mema wazazi wema au waovu."

Al-Kafi, jz. 2, Uk. 162.

MTUME MUHAMMAD MUSTAFA (S.A.W.W)

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ametaja kuvunja ahadi kama ni alama mojawapo ya unafiki:

"Mwenye kuwa na sifa nne (zifuatazo) ni mnafiki; na hata akiwa nayo mojawapo kati ya hizo pia atasifika kwa unafiki isipokuwa aiache: " Mwenye kusema uwongo anapozungumza; " mwenye kuvunja ahadi anapoahidi; " mwenye kufanya hiana anapoaminiwa; na " mwenye kufisidi anapogombana."

Biharu 'l-Anwar, jz. 15, uk. 234.

AL IMAM 'ALI IBN ABI TALIB (A.S)

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) ameandika:

"Jihadhari usiwasimange raia zako kwa hisani ulizowafanyia, wala usijione bora kwa ajili ya kazi unazowafanyia, na unapowaahidi usiende kinyume na ahadi zako. Hakika masimango huharibu hisani, na kujiona huondoa nuru ya haki, na kuvunja ahadi husababisha kuchukiwa na Allah swt na watu. Allah swt anasema: katika Qur'an Tukufu, Surah Ass'af, 61, Ayah 3 'Ni chukizo kubwa mbele ya Allah swt kusema msiyoyatenda."

Mustadriku 'l-Wasa'il, jz. 2, uk. 85.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Kutimiza ahadi hufuatana na uaminifu, nami sikijui kinga kinachokinga vizuri zaidi kuliko kutimiza ahadi."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 228.

MTUME MUHAMMAD MUSTAFA (S.A.W.W)

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

"Mtu asimwahidi mwanae asipoweza kutimiza."

Nahju 'l Fasahah, uk. 201.

AL IMAM 'ALI IBN ABI TALIB (A.S

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) ameonyesha namna ya mtu kusuhubiana na mwenzake:

"Ukimchagua mtu kuwa rafiki yako, basi kuwa mtumishi wake na mwonyeshe uaminifu wako wa kweli na moyo safi."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 323.

MTUME MUHAMMAD MUSTAFA (S.A.W.W)

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

"Mwenye furaha kayaya kuliko watu wote ni yule mwenye kuingiliana na watu watukufu na ambaye huendeana na watu bila ya kuwadhulumu, huzungumza nao bila ya kuwadanganya, na huahidiana nao bila ya kuvunja. Hakika mtu kama huyu amekamilisha murua wake, amedhihirisha uadilifu wake, na anastahiki udugu na urafiki wake."

QUR'AN TUKUFU

Allah swt amezitaja sheria alizowatungia waja wake kama ni amana, na amekataza kabisa kufanya khiana ya aina yoyote: katika Qur'an Tukufu, Surah Al-Anfaal, 8, Ayah 27:

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَخُونُوا اللَّـهَ وَالرَّسُولَ وَتَخُونُوا أَمَانَاتِكُمْ وَأَنتُمْ تَعْلَمُونَ﴾

Enyi mlioamini! Msimfanyie khiana Allah swt na Mtume Muhammad Mustafa (s.a.w.w) na mkakhini amana zenu na hali mnajua.

Vile vile Allah swt amesema: katika Qur'an Tukufu, Surah An-Nisaa, 4., Ayah 58:

﴿إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُكُمْ أَن تُؤَدُّوا الْأَمَانَاتِ إِلَىٰ أَهْلِهَا﴾

Hakika Allah swt anakuamrisheni kuzirudisha amana kwa wenyewe.

AL IMAM 'ALI IBN ABI TALIB (A.S)

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema: Ghuraru 'l-Hikam, uk. 505. "Ukomo cha khiana ni kumfanyia khiana rafiki mpendwa na kuvunja ahadi." Vile vile Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema: Ghuraru 'l-Hikam, uk. 446. "Mtu mwovu kuliko wote ni yule asiyeamini kuweka amana wala hajizuii kufanya khiana."

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Jihadharini na khiana kwani ni dhambi mbaya kabisa; na kwamba mwenye kukhini ataadhibiwa katika Moto kwa khiana yake."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 150.

AL IMAM JA'AFER AS-SADIQ (A.S)

Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema:

"Halahala na kusema ukweli na kurejesha amana kwa mwema au mwovu, kwani sifa mbili hizi ni ufunguo wa riziki."

Safinatu 'l-Bihar, jz. 1, Uk. 41.

AL IMAM ZAYNUL ABIDIN (A.S)

Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Halahala na kuweka amana. Naapa kwa yule aliyembaathi Muhammad kwa haki kuwa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) , kwamba lau mwuaji wa babangu Husayn bin Ali angenipa upanga ule aliomwulia bababngu, kumwekea amana, nisingemfanyia khiana."

Amali as-Sadaq, uk. 149.

MTUME MUHAMMAD MUSTAFA (S.A.W.W)

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

"Mwenye kutenda kitendo kiovu atalipwa (hapahapa) duniani."

Nahju 'l-Fasahah, Uk. 592.

AL IMAM 'ALI IBN ABI TALIB (A.S)

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Uaminifu katika (kuweka) amana ni alama ya usafi wa mwenye imani."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 453.

Vile vile Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Khiana ni dalili ya upungufu wa uchaji na utovu wa dini."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 53.

AL IMAM SAJJAD (A.S)

Al Imam Sajjad(a.s) amesema:

"Una wajibu wa kumlea (Mwanao) kwa adabu nzuri, kumwongoza kwa Mola wake Mtukufu, na kumsaidia katika kumtii."

Al-Wafi, uk. 127.

AL IMAM 'ALI IBN ABI TALIB (A.S)

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Wenye akili huhitajia adabu kama vile shamba linavyohitajia mvua."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 224.

MTUME MUHAMMAD MUSTAFA (S.A.W.W)

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

"Hakuna jambo linalochukiwa mno katika Uislamu kama uchoyo."

Nahju 'l-Fasahah, uk. 549.

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

"Mwenye kuwa na raha kidogo kabisa kati ya watu wote ni bakhili."

Nahju 'l-Fasahah, uk. 81.

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

"Allah swt amrehemu mtu anayebana mengi (ziada) ya maneno yake, na anayetoa ziada ya mali yake."

Nahju 'l-Fasahah, uk. 81.

Vile vile Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

"Jihadhari na uchoyo, kwani uchoyo umewaangamiza waliokutangulia, umewafanya wamwage damu zao, na wahalalishe yaliyoharamishwa."

Nahju 'l-Fasahah, uk. 8.

AL IMAM 'ALI IBN ABI TALIB (A.S)

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Nashangaa juu ya bakhili mwovu; huuharakisha umaskini anaokimbia na huupoteza utajiri anaotafuta. Huishi katika dunia maisha ya maskini na atahukumiwa katika Akhera kwa hesabu ya matajiri."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 497.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Ukarimu wa mtu huwafanya maadui zake wampende, na ubakhili wake humfanya achukiwe na watoto wake."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 368.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Uroho na uchoyo umesimama juu ya msingi wa shaka na kutoaminiwa."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 488.

AL IMAM MUSA AL-KADHIM (A.S)

Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) ameelezea juu ya thamani ya ukarimu:

"Karimu mwenye murua yuko katika ulinzi wa Allah swt; na Allah swt hamwachi mpaka amtie Peponi. Allah swt hamtumi Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) wala Wasii yeyote ila kwamba huwa ni karimu; wala hakutokea mwema yeyote ila kwamba alikuwa karimu. Babangu hajafariki mpaka aliponiusia ukarimu."

Furu' al-Kafi, jz. 4, uk. 38.

AL IMAM MUHAMMAD AL-BAQIR (A.S)

Al Imam Muhammad al-Baqir(a.s) ameshabihisha maisha ya mroho na taswira hii:

"Mfano wa mwenye tamaa ya dunia ni kama kiwavi cha nondo, kila akizidi kujizungushia nyuzi (za hariri) ndivyo hujifungia mpaka kufa kwa kujisonga roho."

Usulu 'l-Kafi, Babu ya Huba ya Dunia.

MTUME MUHAMMAD MUSTAFA (S.A.W.W)

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

"Jihadharini na uchu wa mali, kwani uliwaangamiza waliokutangulieni. Uchu uliwashawishi mabakhili na wakafanya ubakhili; uliwaamrisha kukata ujamaa na wakakata; na uliwaamrisha ufisadi na wakafanya ufisadi."

Nahju 'l-Fasahah, uk. 199.

AL IMAM 'ALI IBN ABI TALIB (A.S)

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Epukaneni na mwenye tamaa, kwani kuingiliana naye huleta udhalili na mashaka."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 135.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Mwenye tamaa ni mfungwa wa udhalili na kifungo chake hakifungiki."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 50.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) ameashiria jambo hili kwa usemi murua:

"Mtukufu kuliko wote ni yula ambaye hukata tamaa (juu ya watu), hushika ukinaifu na uchaji, na huacha uroho na tamaa, kwani tamaa na uroho ni sawa na umaskini, na kukata tamaa (juu ya watu) na ukinaifu ni utajiri wa dhahiri."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 255.

Anayejifanya mtumwa wa tama na uchu, huutia maradhi mwili na roho yake.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) anasema:

"Kila mwenye tamaa ni mgonjwa."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 544.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema;

"Tamaa huchafua nafsi, huharibu dini (imani) na huondoa uungwana."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 77.

MTUME MUHAMMAD MUSTAFA (S.A.W.W)

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ametaja matatizo yanayotokana na tamaa:

"Mwenye tamaa husumbuliwa na matatizo saba mabaya:

1. Fikra inayomdhuru mwili wake na isiyomnufaisha;

2. hamu (hima) isiyokwisha;

3. tamaa isiyompa raha ila baada ya kufa na wakati wa kupumzika huona taabu zaidi;

4. hofu isiyoacha kumhangaisha;

5. huzuni inayofanya maisha yake machungu bila ya kuwa na faida;

6. hesabu isiyomsalimisha na adhabu ya Allah swt ila asemehewe na Allah swt; na

7. adhabu asiyoweza kuikimbia wala kuiepuka."

Mustadriku 'l-Wasa'il, jz. 2, uk. 435.

AL IMAM 'ALI IBN ABI TALIB (A.S)

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

"Tamaa humsukuma mtu kwenye mabaya."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 16.

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) vile vile amesema:

"Matokeo ya tamaa ni kumtia mtu katika aibu."

Ghuraru 'l-Hikam, uk. 360.

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

"Miongoni mwa (alama za) uungwana ni mtu kunyamaza kimya na kumsikiliza ndugu yake anaposema."

Nahju 'l-Fasahah, uk. 633.

AL IMAM MUHAMMAD AL-BAQIR (A.S)

Al Imam Muhammad al-Baqir(a.s) amesema:

"Na jifunze kusikiliza vizuri kama vile unavyojifunza kusema vizuri, wala usimkatize mtu yeyote anaposema."

AL IMAM JA'AFER AS-SADIQ (A.S)

Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema:

"Mja hataipata imani halisi mpaka atakapoacha ubishi hata kama ni haki."

Safinatu 'l-Bahar, jz. 2, uk. 522.

AL IMAM HAD (A.S)

Al Imam Had(a.s) amesema:

"Ubishi huharibu urafiki wa muda mrefu, huvunja uhusiano ulio madhubuti, na sehemu ndogo ya kitu kinachopatikana ni mashindano - na mashindano yenyewe ni chanzo hasa cha kutosikilizana."

AL IMAM JA'AFER AS-SADIQ (A.S)

Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema:

"Epukaneni na mabishano, kwani huunguza moyo, huleta unafiki na husababisha chuki."

Usulu 'l-Kafi, jz. 1, uk. 452.

MTUME MUHAMMAD MUSTAFA (S.A.W.W)

Mtume Mtukufu(s.a.w.w) amesema:

"Hakika,miongoni mwa dalili za saa, ni kuwa

1. watu watapuuza sala

2. watafuata matamanio yao wenyewe

3. wataelekeza kujipendelea wao wenyewe, watawaheshimu matajiri,

4. na watauza Dini yao kwa manufaa ya kidunia

5. wakati huo roho na moyo wa Muumin itayayuka (kwa huzuni) kama chumvi inavyoyayuka katika maji, kwa sababu ataona mambo yaliyoharamishwa na hataweza kuyabadili."

Salman akasema: "Haya yatatokea, ewe Mtume wa Allah swt?" Mtume Mtukufu(s.a.w.w) akasema:"Ndiyo, naapa kwa Aliyonayo roho yangu mkononi mwake." "Ewe Salman ,

6. wakati huo watawala watakuwa wadhalimu

7. Mawaziri watakuwa waasi,

8. na wadhamini (wale waliopewa amana kwa kuaminiwa) watafanya hiana,

9. hakika wakati huo maovu yatakuwa mema na mema yatakuwa maovu,

10. wale wafanyao hiana wataaminiwa na waaminifu watafikiriwa kuwa si waaminifu;na mwongo atasadikiwa,na msema kweli atahesabiwa mwongo.

11. Wakati huo kutakuwapo na utawala wa wanawake,

12. Masuria watashauriwa,

13. na watoto watakaa juu ya mimbar,

14. udanganyifu utahesabiwa kuwa ni uerevu

15. na Zaka itakuwa ni kama kutozwa faini;na mateka ya vita (yaani mali ya ummah) yatakuwa kama ni mali ya mtu binafsi;na mtu atakuwa mjeuri kwa wazazi wake na atakuwa mwema kwa marafiki zake,

16. na wakati huo kutatokea na nyota zenye mikia (comets)."

Salman akasema: "Haya yatatokea,ewe Mtume wa Allah swt?" Mtume Mtukufu(s.a.w.w) akasema:"Ndiyo,naapa kwa Aliyonayo roho yangu mkononi mwake." "Ewe Salman!

17. wakati huo mwanamke atakuwa mshiriki wa mumewe katika biashara,

18. na mvua itakuwa moto sana

19. na watu wema watabaki katika huzuni;na masikini hawata heshimiwa;na wakati huo masoko yatakaribiana,

20. Tena huyu atasema,"Mimi sikuuza chochote,na yule atasema, "Mimi sikupata faida yoyote." Kwa hivyo hutamkuta mtu yeyote asiyemlalamikia Allah swt.

"Ewe Salman!

21. tena itatokea iwapo watu watawazungumzia watawala wao, watawaua, na ikiwa watanyamaza kimya, watanyang'anywa mali yao, watanyimwa heshima zao,watamwaga damu yao na mioyo ya watu itajaa woga;kisha hutamwona mtu yeyote ila atakuwa mwoga,mwenye khofu,ametishika na ameshstushwa" "Ewe Salman!

22. Bila shaka wakati huo mambo fulani yataletwa kutoka Mashariki

23. na mambo fulani yataletwa kutoka Magharibi,

24. Basi ole kwa watu walio dhaifu (wa imani) katika Ummah wangu kutokana na hayo; Ole ya Allah swt iwe kwa hayo. Wao hawatakuwa na huruma juu ya wadogo

wao,wala hawatamsamehe yeyote aliyefanya kosa.Miili yao itakuwa ya wanadamu,lakini mioyo yao itakuwa ya mashetani."

"Ewe Salman!

25. Wakati huo wanaume watawaashiki wanaume,

26. na wanawake watawaashiki wanawake;

27. na watoto wa kiume watapambwa kama wanawake;

28. na wanaume watajifanya kama wanawake

29. na wanawake wataonekana kama wanaume;

30. na wanawake watapanda mipando

31. Hapo tena patakuwepo laana ya Allah swt juu ya wanawake wa Ummah wangu."

"Ewe Salman!

32. Bila shaka wakati huo Misikiti itapambwa (kwa dhahabu n.k.) kama inavyofanywa katika masinagogi na makanIssa,

33. na Qur'an zitapambwa (kwa nakshi na rangi za kupendeza n.k.)

34. na minara (ya misikiti) itakuwa mirefu;na safu za watu wanaosimama katika sala zitazidi,lakini nyoyo zao zitachukiana na maneno yao yatatofautiana."

"Ewe Salman!

35. Wakati huo wanaume watatumia mapambo ya dhahabu;kisha watavaa hariri,na watatumia ngozi za chui."

"Ewe Salman!

36. Wakati huo riba itakuwako,

37. na watu wata- fanyia biashara kwa kusemana na rushwa

38. na dini itawekwa chini,na dunia itanyanyuliwa juu."

"Ewe Salman!

39. Wakati huo talaqa zitazidi

40. na mipaka ya Allah swt hayatasimamishwa

41. Lakini hayo hayatamdhuru Allah swt."

"Ewe Salman!

42. Wakati huo watatokea wanawake waimbaji,

43. na ala za muziki

44. na wabaya kabisa watawatawala Ummah wangu."

"Ewe Salman!

45. Wakati huo matajiri katika Ummah wangu watakwenda Kuhiji kwa matembezi,na walio wastani kwa biashara,na masikini kwa kujionyesha.

46. Hivyo basi wakati huo watakuwapo watu ambao watajifundisha Qur'an si kwa ajili ya Allah swt na wataifanya Qur'an kama ala ya muziki.

47. Na watakuwapo watu ambao watasoma dini si kwa ajili ya Allah swt

48. na idadi ya wanaharamu itazidi

49. watu wataiimba Qur'an,

50. na watu watavamiana kwa uroho wa kidunia."

"Ewe Salman!

51. Haya yatatokea wakati heshima zitakapo- ondoka,na madhambi yatatendwa

52. na watu waovu watakuwa na uwezo juu ya watu wema,

53. na uongo utaenea na mabishano (matusi) yatatokea

54. na umasikini utaenea,

55. na watu watajiona kwa mavazi yao

56. na itakuwepo mvua wakati si wake

57. na watu watacheza dama, kamari na Ala za muziki,

58. na hawatapenda kuhimizana mema wala kukatazana maovu

59. na kwa ajili hali itakavyokuwa hata itafikia wakati huo kuwa Muumin atakuwa na heshima ndogo kuliko hata mjakazi

60. na wanaosoma na wanaotumia wakati wao katika kumwabudu Allah swt watalaumiana.

61. Hao ndio watu watakaoitwa wachafu na wanajisi katika Ufalme wa mbinguni."

"Ewe Salman!

62. Wakati huo matajiri hawataogopa chochote isipokuwa mtu masikini; hadi kwamba masikini wataendelea kuomba kati ya ijumaa mbili,na hawatamwona mtu yeyote wa kutia chochote mikononi mwao."

"Ewe Salman!

63. Wakati huo itazungumzwa Ruwaibidhah."

Salman akauliza:"Ni nini Ruwaibidhah ? Ewe Mtume wa Allah swt, baba na mama yangu wawe fidia kwako."

Mtukufu Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) akajibu:

64. "Watu fulani watazungumza kuhusu mambo ya watu ambayo hayakuwahi kuzungumzwa namna hii zamani.

65. Tena baada ya muda mchache machafuko yatatokea duniani,na kila nchi itafikiri kuwa machafuko yapo katika nchi yao tu."

66. "Watabaki katika hali hiyo kwa muda ambao Allah swt atapenda wabaki;

67. kisha ardhi itatapika vipande vya moyo wake dhahabu, fedha na madini mengineyo; (Hapo Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w.) alinyosha kidole chake penye nguzo, na akasema:"Kama hizi (kwa ukubwa), lakini siku hiyo dhahabu wala fedha hazitamsaidia mtu yeyote. Na hii ndiyo maana ya maneno ya Allah swt 'Hakika dalili Zake zimekuja. '

UBASHIRI WA IMAM JAAFER AS-SADIQ (A.S)

Mazungumzo yafuatayo yamefanywa na Imam Jaafer as-Sadiq(a.s) ambamo ameripoti ubashiri wa siku za mwisho wa dunia hii. Yametolewa kutoka Darul Islam,Bihar-ul-Anwar na Raudhat-ul-Kafi. Wanaoripoti habari hizo ni Allamah Naraqi na Sheikh Kulaini r.a. kutokea kwa Himran.

Imam(a.s) alisema:

1 "Haki itakuwa imetokomezwa na watu walio katika haki hawatapatikana.

4. Dhulma na uonevu utaenea katika miji yote.

5. Kufuata Qur'an kimatendo itajulikana kama tabia ya kizamani.

6. Zitatolewa maana ya Aya za Qur'an kwa mujibu wa matakwa ya watu,hivyo mafhum ya Qur'an itakuwa imebadilishwa na kupotoshwa.

7. Wadhalimu watakuwa wakiwa kandamiza wale walio katika haki.

8. Uchokozi na uchochezi utatokea kutoka kila pande na pembe.

9. Matendo maovu na kukosa aibu vitaenea na kuzagaa kila mahala.

10. Ulawiti utakuwa ni jambo la kawaida.

11. Muumin atakuwa akionekana kama mtu dhalili ilhali waovu watakuwa wakiheshimiwa

12. Vijana hawatakuwa wakiwaheshimu wakubwa wao.

13. Huruma itakuwa imepotea kabisa.

14. Waovu watakuwa wakitukuzwa kwa udhalimu wao na hakutakuwapo na mtu yeyote wa kuwapinga.

15. Wanaume watafurahishwa mno kwa kuingiliana na wanaume wenzao.

16. Wanawake watawaoa wanawake wenzao.

17. Mapesa yatatumika kwa ajili ya matumizi yale yaliyo haramishwa na Allah swt.

18. Starehe, anasa na zinaa zitashamiri.

19. Zinaa itajulikana kama maadili yaliyopitwa na muda.

20. Muumin atatengwa kwa sababu ya kufanya ibada za Allah swt.

21. Jirani mmoja atafurahi mno kwa kumuudhi na kumbughudhi jirani mwenzake.

22. Wazushi (kama Salman Rushdie wa Uingereza) watatukuzwa na kusifiwa katika kueneza fitina na yale wanayozusha.

23. Ushauri mzuri utakanwa.

24. Milango ya wema yatafungwa wakati milango ya maovu yatafunguliwa.

25. Al-Kaaba haitatumika au haitafikika kwa sababu ya vikwazo na ugumu utakaowekewa mahujaji.

26. Watu watalazimishwa kuacha kwenda Makkah kuhiji.

27. Watu hawatakuwa wakitimiza ahadi zao watakazokuwa wakizitoa.

28. Wanaume watakuwa wakitumia dawa za kuamsha tamaa za kiume kwa ajili kulawiti na wanawake watakuwa wakitumia vyakula vya mafuta ili kujitayarisha kwayo.

29. Baadhi ya wanaume watakuwa wakiishi kwa kujipatia mapesa kwa kuuza mikundu yao.

30. Na wanawake watakuwa wakijipatia mapesa kwa kufanyisha biashara kuma zao.

31. Wanawake wataunda vilabu vyao,mashirika na umoja wao.

32. Wanaume atajigeuza kama wanawake na watavutia na wanawake.

33. Wanaume watajirembesha kama wanawake.

34. Ulawiti utachukuliwa kama ndiyo ustaarabu na starehe ya kweli.

Na Banu Abbas watalipia ulawiti.

35. Wanawake wataona fakhari kwa kuwa na waume nje ya mume mmoja wa ndoa na vivyo hivyo wanaume watakuwa hivyo hivyo.

36. Heshima itakuwa ikitolewa kwa utajiri wa mtu na wala si ucha Mungu.

37. Riba ndiyo itakayokuwa biashara ya kila siku.

38. Ushahidi wa uongo utakuwa ukIssadikiwa mno.

39. Kile alichokiharamisha Allah swt kitachukuliwa ni halali na chochote kile alichokihalalisha Allah swt kitachukuliwa ni haramu.

40. Maamrisho ya Dini yatageuzwa kwa mujibu wa matakwa yao.

41. Wachokozi na waovu watatenda maovu kwa udhahiri bila ya khofu yoyote ile na Muumin hawataweza kuwazuia vyovyote vile.

42. Watawala watawapenda mno Makafiri kuliko Muumiin.

43. Rushwa ndiyo itakuwa njia ya kujitimizia kazi kutoka maofIssa wanaohusika.

44. Wanaume wata walawiti wake zao.

45. Watu watakuwa wakiuawa kwa visingizio vidogo vidogo na magomvi madogo madogo.

46. Wanawake watawafanyia wanaume dhihaka, nao watashawishiwa kufanya uhusiano na wanawake.

47. Wanaume wataishi kwa mapato ya wake zao zitakazopatikana kwa zinaa.

48. Wanawake watakuwa wakiendesha hukumu majumbani huku wanaume wakiwatii wake zao kwa sababu wanawake hao ndio watakuwa wenye mapato.

49. Wanawake watatumiwa katika kupatikana huduma mbalimbali.

50. Kula kiapo kwa jina la Allah swt litakuwa ni jambo lililowekwa ulimini.

51. Pombe na kamari vitapatikana kila mahala na vitakuwa vimezagaa.

52. Wanawake wa Kiislamu wataingiliana na Makafiri,ambapo Waislamu hawataweza kuwazuia na wala hawatakuwa na uwezo kama huo.

53. Maadui wetu watasaidiwa na watawala na marafiki zetu watadhalilishwa kiasi kwamba hata kiapo chao hakitakubaliwa.

54. Udanganyifu na hila ndizo zitakuwa desturi miongoni mwa watu.

55. Usomaji na usikilizaji wa Qur'an utakuwa ni bughudha kwa watu.

56. Kusikiliza mambo fidhuli ndiyo itakuwa ikipendelewa na watu.

57. Jirani hatamstahi jirani mwenzake illa kwa khofu ya ulimi mkali na mchafu.

58. Sheria na kanuni za Allah swt hazitatambuliwa na waovu hawataadhibiwa kwa maamrisho hayo.

59. Ghiba na kulaghaiana ndivyo vitakuwa vitu vya kawaida.

60. Madhumuni ya Hajj na Jihad yatakuwa mbali na yale ya Kiislamu.

61. Misikiti itarembeshwa kwa dhahabu.

62. Watawala watawataka ushauri kwa nia ya Makafiri.

63. Litakuwa ni jambo la kawaida kuibia katika uzani na vipimo vya biashara.

64. Kumwaga damu ya watu wegine litakuwa ni jambo la kawaida.

65. Watu watajigamba kwa ndimi zao chafu zenye matusi mabaya ili kuwatishia watu wengine.

Imam a.s. aliendelea kusema:

66. "Watu watakuwa wakipuuzia sala na kutojali.

67. Watu hawatakuwa wakilipa zaka ingawaje watakuwa na utajiri mkubwa.

68. Sanda za maiti zitakuwa zikiibiwa na kuuzwa tena.

69. Mauaji yatakithiri mno kiasi kwamba hata wanyama pia wataanza kuuana wenyewe kwa wenyewe.

70. Watu watakuwa wakIssali katika mavazi ya kiajabu.

71. Macho na mioyo itapoteza nuru zao za heshima na huruma.

72. Watu watakuwa wamejishughulisha na maswala ya kutafuta mali na mapesa tu.

73. Watu watasali kwa kuonyesha tu.

74. Watu watatafuta ilimu ya Dini kwa ajili ya kujipatia mali ya dunia.

75. Ushirika katika makundi yatakuwa ndiyo mambo ya maisha.

76. Wale watakaojipatia riziki kwa njia ya halali,watasifiwa kwa midomo tu.

77. Matendo maovu na machafu yataenea hata Makkah na Madina.

78. Watu waliokufa watafanyiwa mizaha na vichekesho.

79. Mwaka hadi mwaka hali itakuwa ikiendelea kuharibika kuwa mbaya zaidi.

80. Matajiri wataigwa.

81. Masikini, mafukara watafanyiwa dhihaka na kufedheheshwa.

82. Matukio ya kudura kama yale ya mitetemeko,maporomoko n.k. yatakuwapo lakini watu watakuwa hawaviogopi.

83. Matendo maovu yatakuwa yakitendwa kiwaziwazi.

84. Wazazi watatupa watoto wao na watoto watawatusi wazazi wao na daima watakuwa wakitaka mali na utajiri wa wazazi wao.

85. Wanawake hawatawatii na kuwafuata waume wao.

86. Siku itakayopita bila ya mtu kutenda madhambi,basi itachukuliwa ni siku yenye nuksi.

87. Watu wenye uwezo wataficha mali muhimu na kuviuza kwa bei ya ulanguzi.

88. Waombaji na walaghai watajumuika katika kucheza kamari na kulewa.

89. Pombe itatumika kama ni kitu chenye kuponya i.e.dawa.

90. Makafiri watatukuzwa juu ya watu wengine na Muumin watadhalilishwa na kupuuzwa.

91. Kutafanywa malipo kwa ajili ya kutoa Adhan na sala.

92. Misikiti itajaa kwa watu wasiokuwa na khofu ya Allah swt.

93. Watu wenye fahamu na akili kasoro ndio watakaokuwa wakiongoza sala za jamaa' na watu kama hao kamwe hawatashutumiwa au kusutwa na badili yake wataheshimiwa."


10

11

12

13

14

15

16

17

18

19

20

21

22

23