TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN12%

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: tafsiri ya Qurani

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN
  • Anza
  • Iliyopita
  • 29 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 42573 / Pakua: 4763
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

Mwandishi:
Swahili

1

2

3

4

5

6

7

22

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

SURA QADR (QADR) (NA. 97)

INA AYA 5

Kwa jina la Allah Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu.

إِنَّا أَنزَلْنَاهُ فِي لَيْلَةِ الْقَدْرِ ﴿١﴾

1. Hakika sisi tumeiteremsha Qur'an katika Laylatul Qadri.

وَمَا أَدْرَاكَ مَا لَيْلَةُ الْقَدْرِ ﴿٢﴾

2. Na ni lipi la kukujulisha wewe ni nini Laylatul Qadri?

لَيْلَةُ الْقَدْرِ خَيْرٌ مِّنْ أَلْفِ شَهْرٍ ﴿٣﴾

3. Laylatul Qadri ni bora kuliko miezi elfu.

تَنَزَّلُ الْمَلَائِكَةُ وَالرُّوحُ فِيهَا بِإِذْنِ رَبِّهِم مِّن كُلِّ أَمْرٍ ﴿٤﴾

4. HushukaMalaika na Roho katika (usiku) huo kwa amri ya Mola wao kwa ajili ya kila jambo.

سَلَامٌ هِيَ حَتَّىٰ مَطْلَعِ الْفَجْرِ ﴿٥﴾

5. (Ni) amani mpaka alfajiri.

Ubainifu Sura hii inaelezea kushuka Qur'an katika usiku wa "Laylatul -qadr" na kuutukuza usiku huo kwa kuufanya bora kuliko miezi elfu. Sura hii inawezekana kuwa imeshuka Makka au Madina, lakini yale yaliyopokewa kwa Maimamu katika Ahlul Bait wa Mtume(s.a.w.w) kuhusu sababu za kushuka kwake, yanatilia nguvu kuwa Sura hii imeshuka Madina.

Aya Na 1

Dhamira katika neno "tumeiteremsha" ni ya Qur'an. Kwa dhahiri inaonyesha kushuka Qur'an yote na wala sio baadhi ya aya zake. Hilo linatiliwa nguvu na ibara ya neno "Anzalnahu" ambalo kwa dhahir lina maana ya kushuka kwa mkupuo mmoja; kinyume cha neno "Tanziyl" ambalo kwa dhahiri lina maana ya kushuku kwa awamu nyingi. Katika maana ya aya hiyo Mwenyezi Mungu anasema: "Naapa kwa kitabu kinachobainisha. Hakika sisi tumeiteremsha (Qur'an) katika usiku uliobarikiwa ". (44:2-3).

Kwa dhahiri hapo Mwenyezi Mungu anaapa kwa jumla ya kitabu chote kisha anatolea habari ya kila kilichoapiwa. Kwa hiyo ufahamisho wa aya ni kuwa Qur'an imeshuka jumla kwa Mtume.

Hakuna katika manen ya Mwenyezi Mungu yanayobainisha kuwa usiku huo ni usiku wowote na kwamba sio usiku ulio katika neno lake Mwenyezi Mungu: "Ni Mwezi wa Ramadhan ambao imeteremshwa ndani yake Qur'an " (2:185) kwa sababu aya hii ikichanganywa na Aya Na Sura ya Al-Qadr (tunayoizungumza) inafahamisha kuwa usiku huo ni katika nyusiku za Ramadhan. Mwenyezi Mungu ameuita usiku huo Laylatul Qadri. Kwa dhahiri inaonyesha kwamba makusudio ya neno Qadri ni kukadiria. Kwa hiyo ni usiku wa kukadiria ambao anakadiria Mwenyezi Mungu matukio ya mwaka mzima kama vile uhai, mauti na riziki. Vile vile wema, uovu nk, kama alivyosema Mwenyezi Mungu: "Katika usiku huo hubainishwa kila jambo la hekima. Ndio hukumu inayotoka kwetu; kwa hakika sisi ni waletao mitume. Ni rehema itokayo kwa Mola wako " (44:4-6).

Kwa hivyo hakukuwa kubainisha jambo la hekima ila ni hekima za matukio yenye kutuka katika sehemu zake zinazohusika kwa kukadiria. Hilo linafahamisha kwamba usiku huo unakaririka kwa kukaririka miaka. Kwa hiyo katika mwezi wa Ramadhan wa kila mwaka kuna usiku unaokadiriwa mambo ya mwaka. Kwa sababu hakuna maana ya kuukadiria usiku mmoja (ulioshuka Qur'an) kwamba umekadiriwa ndani yake matukio ya kabla yake na baada yake. Na neno 'hubainisha' ambalo kwa dhahiri linaonyesha kuendelea vile vile neno 'hushuka' Malaika yanatilia nguvu hilo.

Basi hakuna njia inayoonyesha yale yaliyosemwa kuwa usiku huo ni ule usiku mmoja tu ulioteremshwa Qur'an. Au kwamba ulikuwa ukikaririka katika miaka ya zama za Mtume(s.a.w.w) kisha Mwenyezi Mungu akauondoa. Vile vile hakuna njia inayoonyesha kuwa usiku huo upo katika miaka yote, lakini unabadilika kwa kukaririrka miaka; kwamba mwaka mwengine uwe katika mwezi wa Ramadhan, mwengine uwe katika mwezi wa Shaaban, nk. Imesemwa neno Qadr limekuja kwa maana ya hadhi na heshima na kwamba umeitwa usiku wa hadhi kutokana na umuhimu wa hadhi yake, au kwa hadhi ya wale wenye kuabudu katika usiku huo. Imesemwa tena Qadr ni kwa maana ya ufinyu, na kwamba umeitwa usiku finyu kwa sababu ardhi inakuwa finyu kutkana na kushuka Malaika.

Maana ya aya ni kwamba huo ni usiku ulio katika mwezi wa Ramadhan katika kila mwaka ambao ndani yake mnahukumiwa mambo kwa kiasi cha makadiro. Hilo halikanushi kutokea mabadiliko katika muda wa mwaka kwa sababu kuhakikika kile chenye kukadiriwa ni jambo jengine na mbadiliko katika kukadiria ni jambo jengine; kama vile kutokea mabadiliko ya matukio ya kilimwengu kwa kiasi cha matakwa ya Mungu, hakukanushi kuainiwa kwake katika "Lauhil Mahfudh"! Amesema Mwenyezi Mungu: "Na asili ya hukumu zote iko kwake " (13:39).

Uwezekano wa kutokea mambo kwa kuhakikika kwake kuna mipangilio kwa kutimia na kupungua. Inawezekana kutokea baadhi ya mipangilio katika Laylatul-Qadr na kuchelewa kutimia kupitishwa mpaka wakati mwengine, lakini hadithi zitakazokuja haziwafiki hilo.

Aya Na 2

Ni fumbo la utukufu wa cheo cha usiku na daraja yake kubwa. Hilo linatiliwa nguvu na kudhihiri kwa jina la huo usiku mara kwa mara, pale iliposemwa: "Nini Laylatul-Qadr, Laylatul-Qadr ni bora ". Na wala isisemwe nini huo, huo ni bora.

Aya Na 3

Ni ubainifu wa kijumla kwa lile limaloishiriwa na aya tatu katika ukubwa wa jambo la huo usiku. Makusudio ya kuwa ni bora kuliko miezi elfu ni ubora wa ibada kama walivyofasiri wafasiri. Hilo ni lenye kunasibiana na makusudio ya Qur'an na kuwatia hima watu kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu. Kwa hiyo kuufanyia ibada ni bora kuliko ibada ya miezi elfu na baraka iliyotajwa katika Sura ya (44:3) inafahamisha hilo. Na kuna maana mengine yatakayokuja katika utafiti wa hadith (Inshallah).

Aya Na 4

Kwa dhahiri roho hapa ni roho iliyotajwa katika Aya Na (85:17) "Sema roho ni jambo linalohusika na Mola wangu ". Herufi Min katika neno Min Kulli imesemwa kuwa imekuja kwa maana ya herufi Ba yaani kwa kila jambo. Na imsemwa ni ya kuanzia makusudio na kufahamisha sababu yaani kwa sababu ya kila jambo la Mungu. Pia imesemwa ina maana ya sababu ya lengo, yaani kwa ajili ya kuzingatia kila jambo katika mambo. Kwa kweli hasa ikiwa makusudio ya neno Amr ikiwa ni amri ya Mungu inayofasiriwa na neno lake Mwenyezi Mungu katika Sura (36:82): "Hakika amri yake anapotaka chochote ni kukiambia kuwa kikawa". Basi Min ni ya kuanza na kufahamisha sababu kwa maana ya "Hushuka Malaika na Roho katika Laylatul-Qadr kwa idhini ya Mola wao hali ya kuanza kushuka kwao kutokana na kila amri ya Mungu ".

Ikiwa Amr ina maana ya kilimwengu, basi itakuwa kwa maana ya Lam ya kwa ajili, yaani kwa idhini ya Mola wao kwa ajili ya kuzingatia kila jambo katika mambo ya kilimwengu.

Aya Na 5

Amesema katika Mufradat neno Salaam lina maana ya kuepukana na maafa ya nje na ndani. Kwa hivyo neno hilo katika aya linaonyesha hifadhi ya Mungu kwa kueneza rehema kwa waja wake wenye kuelekea kwake na kuziba mlango wa mateso. Aya mbili hizi za mwisho ni tafsiri ya Aya Na tatu.

Utafiti Wa Hadith Katika Tafsiri ya Bur'han kutoka kwa Sheikh Tusi naye kutoka kwa Abu Dharri amesema: Nilimuuliza Mtume(s.a.w.w) : "Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu Laylatul-Qadr ni jambo linalokuwa katika zama za Mitume, wakiondoka nalo linaondoka?" Akasema "La! bali Laylatul-Qadr inaendelea mpaka siku ya Kiyama". Na imekuja hadithi hiyo katika maana mbali mbali katika njia ya Ahli Sunnah. Katika Majmau kutoka kwa Hammad bin Uthman, naye kutoka kwa Hassan bin Abu Ali amesema, "nilimuuliza Abu Abdillahi(a.s) kuhusu Laylatul-Qadr akasema: 'Utafute katika usiku wa 19, 21 na 23". Katika baadhi ya habari zilizopokewa ni kuwa kati ya usiku wa 21 na 23 kama inavyoeleza riwAya Na Iyashi kutoka kwa Abdul-Wahid naye kutoka kwa Baqir(a.s) .

Imefahamika kutoka katika riwaya kwamba haukuainiwa (haukutajwa) kwa ajili ya kuutukuza ili usidharauliwe kwa kufanyiwa maasi. Katika hiyo hiyo Majmau katika riwAya Na Abdillahi bin Bakir kutoka kwa Zurara kutokana na mmoja wa Maimamu wawili (Abu Abdillahi na Baqir) amesema: "Hakika usiku wa Laylatul-Qadr ni usiku wa "Jahaniy". Hadith ya Jahaniy ni kwamba yeye alisema kumwambia Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) . Hakika nyumba yangu nimeijenga nje ya mji niamrishe usiku wa kuingia kwenye nyumba hiyo, akamwamrisha usiku wa 23. Hadith ya Jahaniy imepokewa kwa njia ya Ahli Sunnah vile vile katika Durril Manthur kutoka kwa Malik na Bayhaqi. Katika Kafi kwa isnadi ya Zurarah amesema; "Amesema Abu Abdillahi(a.s) kukadiria ni mwezi 19, kukata hukumu ni mwezi 21, na kutia saini ni mwezi 23." Na kuna riwaya nyengine zenye maana hiyo.

Zimeafikiana habari za Ahlul Bait kwamba usiku huo ni wenye kubakia ukikaririka kila mwaka na kwamba huo ni usiku katika usiku wa mwezi wa Ramadhan na kwamba uko katika moja ya nyusiku tatu. Ama kwa upande wa Ahli sunnah riwaya zimehitalifiana kiajabu kiasi kisicho dhibitika na lililo maarufu ni kwamba huo ni usku wa mwezi 27 ambao imeshuka Qur'an. Katika Durril Manthur ametoa Hatib kutoka kwa Ibn El-Musabbib amesema: "Amesema Mtume(s.a.w.w) niliona katika ndoto Bani Umayya wakipanda mimbari yangu likanitia dhiki hilo, ndio akateremsha Mwenyezi Mungu Sura ya Qadr.

Imepokewa mfano wa hadith hiyo kutoka kwa Hatib katika Tarekh yake naye kutoka kwa Ibn Abbas, vile vile imepokewa katika maana hayo kutoka kwa Tirmidhi, ibn Jariyr, Tabrani Ibn Murdawahyh na Bayhaqi katoka kwa Hassan bin Ali. Na ziko riwaya nyingi katika maana haya kwa upande wa Shia kutoka kwa Maimam wa Ahlul Bait(a.s) . Katika riwaya hizo ni kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu alimfariji Mtume wake(s.a.w.w) kwa kumpa Laylatul Qadr na kuifanya bora kuliko miezi elfu ambao ni muda wa ufalme wa Bani Umayya. Katika Kafi kwa isnadi yake kutoka kwa Ibn Abu Umayya naye kutoka kwa watu zaidi ya mmoja nao kutoka kwa Abu Abdillah(a.s) kwamba walimuuliza baadhi ya sahaba zetu wala simjuwi ila Said Assiman: "Vipi itakua Laylatul Qadr ni bora kuliko miezi elfu?' "Akasema amali katika usiku huo ni bora kuliko amali ya miezi elfu bila Laylatul Qadr".

Katika hiyo hiyo Kafi kwa isnadi yake kutoka kwa Fadhili, Zurara na Muhammad bin Muslim, kutoka kwa Humran kwamba yeye alimuuliza Abu Jaffar(a.s) kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: "Hakika sisi tumeiteremsha (Qur'an) katika usiku uliobarikiwa". Akasema: "Ndio Laylatul Qadr nao uko katika kila mwaka katika mwezi wa Ramadhan katika kumi la mwisho, haikushuka Qur'an illa katika Laylatul Qadr, amesema Mwenyezi Mungu: "Katika (usiku) huo hubainishwa kila jambo la hekima ." (44:4).

Akaendelea kusema: "Hukadiriwa katika Laylatul Qadr kila kitu kinachokuwa mwaka huo kwa mkabala wake; heri na shari, utii na uasi na kuzaliwa na ajali au riziki. Kinachokadiriwa katika usiku huo na kupitishwa basi kimekwishapitishwa. Na Mwenyezi Mungu ana matakwa yake katika hilo. Akasema tena: "Na amali njema katika usiku huo kama vile swala, zaka na namna ya mambo ya heri, ni bora kuliko amali katika miezi elfu isiyokuwa na Laylatul Qadr."

Kuhusu jumla ya "Mwenyezi Mungu ana matakwa yake katika hilo" anakusudia uhuru wa kudura yake. Anaweza kufanya analotaka hata kama amelipitisha. Kwani kuwajibisha jambo hakuwezi kuufunga uweza, kwa hiyo anaweza kuichangua hukumu aliyoipitisha. Katika Majmau amepokea Ibn Abbas kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) kwamba yeye Mtume amesema: "Unapokuwa Laylatul Qadr hushuka Malaika ambao ni wakazi wa Sidratul Muntaha miongoni mwao akiwa ni Jibril. Anashuka pamoja na bendera, bendera moja anaisimamisha kwenye kaburi yangu, nyengine kwnye Baytul-Muqadas, nyengine Masjidul-Haram, na nyengine anaisimamisha Mlima Sinai. Wala hamwachi yeyote mwanamume au mwanamke ila humpa salam isipokuwa, mnywaji tembo, mwenye kula nyama ya nguruwe na mwenye kujipaka zafarani".

Katika Tafsiri ya Bur'han kutoka kwa Said bin Abdillahi naye kutoka kwa Abu Baswiyr amesema. "Nilikuwa pamoja na Abu Abdillahi(a.s) akataja kitu kuhusu kuzaliwa Imam, akasema inawajibisha kuzidi Roho katika Laylatul Qadr , nikamwambia: niwe mkombozi wako kwani Roho si Jibril? Akasema Jibril ni katika Malaika na Roho ni mkubwa kuliko Jibril huoni Mwenyezi Mungu anasema: "Hushuka Malaika na Roho". Riwaya ni nyingi sana zinazoeleza ubora wa Laylatul Qadr na baadhi yake zimetaja alama ambazo tumezifungia jicho; kama kutokeza mwanga wa jua na kulingana sana hewa, nk.

SURA BAYYINA ( HOJA) (NA. 98)

INA AYA 8

Kwa jina la Allah. Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu.

لَمْ يَكُنِ الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْ أَهْلِ الْكِتَابِ وَالْمُشْرِكِينَ مُنفَكِّينَ حَتَّىٰ تَأْتِيَهُمُ الْبَيِّنَةُ ﴿١﴾

1. Hawakuwa wale ambao wamekufuru katika watu wa kitabu na washirikina, ni wenye kuachana na waliyonayo mpaka iwajie hoja.

رَسُولٌ مِّنَ اللَّـهِ يَتْلُو صُحُفًا مُّطَهَّرَةً ﴿٢﴾

2. (Nayo) ni Mtume atokaye kwa Allah awasomee kurasa zilizotakaswa.

فِيهَا كُتُبٌ قَيِّمَةٌ ﴿٣﴾

3. (Ambazo) ndani yake mna maandishi yaliyosawasawa

وَمَا تَفَرَّقَ الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ إِلَّا مِن بَعْدِ مَا جَاءَتْهُمُ الْبَيِّنَةُ ﴿٤﴾

4. Wala hawakutengana wale waliopewa kitabu ila baada ya kuwajia hiyo hoja.

وَمَا أُمِرُوا إِلَّا لِيَعْبُدُوا اللَّـهَ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ حُنَفَاءَ وَيُقِيمُوا الصَّلَاةَ وَيُؤْتُوا الزَّكَاةَ وَذَٰلِكَ دِينُ الْقَيِّمَةِ ﴿٥﴾

5. Na hawakuamrishwa ila wamuabudu Allah kwa kumtakasia yeye dini, hali wameshikamana na haki na wasimamishe swala na watoe zaka na hiyo ndiyo dini iliyo sawasawa

إِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْ أَهْلِ الْكِتَابِ وَالْمُشْرِكِينَ فِي نَارِ جَهَنَّمَ خَالِدِينَ فِيهَا أُولَـٰئِكَ هُمْ شَرُّ الْبَرِيَّةِ ﴿٦﴾

6. Hakika wale ambao wamekufuru katika watu wa kitabu na wenye kushirikisha (wataingia) katika moto wa Jahannam watakaa humo milele na hao ndio waovu wa viumbe.

إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ أُولَـٰئِكَ هُمْ خَيْرُ الْبَرِيَّةِ ﴿٧﴾

7. Hakika wale amabo wameamini wakatenda (amali) njema hao ndio bora wa viumbe.

جَزَاؤُهُمْ عِندَ رَبِّهِمْ جَنَّاتُ عَدْنٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا أَبَدًا رَّضِيَ اللَّـهُ عَنْهُمْ وَرَضُوا عَنْهُ ذَٰلِكَ لِمَنْ خَشِيَ رَبَّهُ ﴿٨﴾

8. Malipo yao kwa Mola wao ni mabustani ya milele yanayopita mito chini yake watakaa humu milele. Allah yuradhi nao na wao waradhi naye. Na hayo ni kwa mwenye kumcha Mola wake.

UBAINIFU

Sura hii inasajili ujumbe wa Muhammad kwa wote wale waliopewa kitabu na washirikina. Kwa maneno mengine, kwa wote wale wenye mila na wasiokuwa na mila. Ujumbe huo ni katika utaratibu wa Mwenyezi Mungu - desturi za uongofu - ambazo zimeelezwa katika Qur'an; kwa mfano kamanalivyosema Mwenyezi Mungu (s.w.t): "Hakika sisi tumemuongoa (tumembainishia) njia, basi ama atakua mwenye kushukuru au mwenye kukufuru ." (76:3).

Na amesema tena Mwenyezi Mungu : "Na hakuna umma wowote ila alipitia humo muonyaji ." (35:24).

Ujumbe wa Muhammad(s.a.w.w) unatoa hoja kuwa ni kwa ajili ya watu wote, kwa vile unakusanya maslahi ya jamii ya binadamu ikiwa ni pamoja na itikadi na matendo; kama utakavyokuja ufafanizi (Inshallah). Sura hii inauwezekano wa kuwa imeshuka Makka au Madina, ingawaje mpangilio wake unaonyesha kuwa imeshuka Madina.

Aya Na 1

Ayah hii ambayo ndiyo kichwa cha maneno ya Sura, inaonyesha kusimama hoja juu ya wale ambao wamekufuru na wale waliopewa kitabu wakati walipoanza kuhitalifiana. Makusudio hasa ni kuwa Mtume(s.a.w.w) ni mmojawapo wa waliyothibitisha hoja ya Mwenyezi Mungu ana wajibu wa kuleta mwokozi kwa watu. Hii ni kutokana na (uadilifu) wa mwenendo wake. Makusudio ya 'waliokufuru' hapa ni waliokanusha mwito wa utume wa kiislamu. Herufi: min ni ya kuelezea baadhi, yaani baadhi ya waliopewa kitabu. Washirikina ni wale wanaoabudu masanamu na wengineo.

Kwa ujumla ni kuwa; wale walioukanusha ujumbe wa Mtume(s.a.w.w) walikuwa ni wenye kuhitajia kusimamishiwa hoja wakati wote, mpaka alipokuja Mtume(s.a.w.w) wajibu huo wa kupatiwa hoja ulikwisha. Wamehitalifiana kiajabu katika tafsiri ya ayah ii na maana yake, mpaka baadhi yao wakasema kwamba aya hiyo ndiyo ngumu zaidi katika Qur'an kimpangilio na kitafsiri. Maana haya tuliyoyaleta ndiyo yanayolingana sawa na mpangilio wote wa Sura bila ya kupingana na aya. Mwenye kutaka maelezo zaidi na ayatafute haya katika vitabu vilivyorefushwa maelezo.

Aya Na 2

Neno Suhuf lina maana ya kitu kinacho andikiwa juu yake. Makusudio yake hasa ni mafungu ya Qur'an yanayoshuka kwa ujumla. Neno hili limekaririka katika maneno yake Mwenyezi Mungu kwa maana ya mafungu ya vitabu vya mbinguni; kama alivyosema Mwenyezi Mungu (s.w.t): "Huo waadhi umo katika kurasa tukufu. Zenye kutukuzwa (na) zenye kutakaswa. Zimo katika mikono ya waandishi. Watukufu watenda mema ." (8:13-16).

Makusudio ya kuwa kurasa. Zimetakaswa, ni kuwa imetakaswa na uchafu wa ubatilishi kwa kuguswa na shetani. Na imekaririwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwamba hayo ni maandishi ya haki yenye kuhifadhiwa na muingilio wa kishetani. Mwenyezi Mungu kasema: "Hapana aigusaye ila waliotakaswa na mabaya" (56:79).

Aya Na 3

Neno kutubu lina maana ya kila chenye kuandikwa, iwe ni ubao au karatasi nk. Vile vile lina maana ya hukumu: Kama alivyosema Mwenyezi Mungu (s.w.t); "Mmehukumiwa (mmelazimishwa) kufunga ".(2:183).

"Na mmehukumiwa (mmelazimishwa) kupigana vita " (2:216).

Kwa dhahiri ni kuwa makusudio yake ni maandishi yaliyomo katika kurasa zenye hukumu za Mungu zenye kufungamana na itikadi na matendo. Dalili yake ni kuyasifu kwa neno Qayyima linalotokana kusimamia kitu kwa maana ya kukihifadhi, kuchunga maslahi yake na kudhamini wema wake. Inajulikana kuwa vitabu vya mbinguni vinasimamia mambo ya jamii ya watu, na kuchunga maslahi yake kutokana na hukumu zake zenye kufungamana na itikadi na amali. Kwa hiyo maana ya aya hizi mbili ni kuwa: hoja iliyowazi ambayo amewaletea Mtume(s.a.w.w) kutoka kwa Mwenyezi Mungu kuwasomea vitabu vya mbiguni vyenye kutakaswa na batili, ni hukumu zenye kusimamia mambo ya jamii ya watu, zenye kuchunga maslahi yake.

Aya Na 4

Aya Na kwanza ilikuwa inaonyesha kumkanusha kwao Mtume na kitabu chake chenye kudhamini mlingano (mwito) wa haki. Aya hii inaonyesha kukhitalifiana kwao juu ya mlingano wa Kiislamu. Hayo yameonyweshwa kwenye sehemu nyengine katika Qur'an kama: "Na hawakukhitalifiana waliopewa kitabu ila baada kuwajia elimu ". (3:19).

Kuwajia hoja ni ubainifu wa utume ambao umewabainikia katika vitabu vyao au ule waliofafanuliwa na mitume yao, kama alivyosema Mwenyezi Mungu (s.w.t): "Na alipofika Isa kwa dalili zilizo wazi, alisema "Nimekujieni na elimu (yenye nafuu na nyie), na ili nikuelezeni baadhi ya yule mliyohitalifiana; basi mcheni Allah na nittini. Kwa hakika Allah ndiye Mola wenu; basi muabuduni, hii ndiyo njia iliyonyooka, lakini yalihitalifiana makundi wao kwa wao ". (43:63-65).

Kama ukiuliza, kwa nini imeelezwa kutengana kwa watu wa kitabu na haikuelezewa kutengana kwa washirikina.

Jibu ni kuwa, sio mbali kuwa neno: wale ambao wamepewa kitabu, lililoko katika ayah ii linawachanganya watu wa kitabu na washirikina. Limebadilishwa neno 'watu wa kitabu' ambao katika Qur'an wanajulikana kuwa ni Mayahudi, Wakristo na Majusi, kuwa wale ambao 'wamepewa kitabu'. Bila shaka ibara hizi mbili zinatofautiana. Mwenyezi Mungu amefafanua kuwa Yeye ameteremsha kitabu ambacho ni sharia iliyofaradhaiwa juu yao yenye kuhukumu katika hitilafu za mambo yao ya kimaisha - tangu mwanzo zilipodhihiri hitilafu zao za kimaisha wao wakahitalifiana katika dini baada ya kuwabainikia wao haki na kuwasimamia wao hoja. Kwa hiyo watu wote wameletewa kitabu; kisha wakahitalifiana, kuna katika wao waliosahau kile walichopewa, kuna waliochukulia kimakosa na kuna wale waliohifadhi kile walichopewa wakakiamini. Mwenyezi Mungu (s.w.t) anasema: "Watu wote walikuwa wa dini moja (kisha wakahitalifiana). Basi Allah akawaleta manabii watoao habari njema na waonyao na pamoja nao akawateremshia vitabu vilivyoshikamana na haki ili vihukumu baina ya watu katika yale waliyokhitalifiana na hawakuhitalifiana katika hayo ila wale waliopewa vitabu hivyo; baada ya kuwafikia hoja zilizo wazi kwa sababu ya uhasidi (uliokuwa) baina yao ." (2:213).

Katika maana hayo Mwenyezi Mungu anasema: - mpaka aliposema- Na kama Mwenyezi Mungu angelitaka wasingelipigana wale waliokuwa baada yao (baada ya mitume) baada ya kuwafikia hoja zilizowazi. Lakini walihitalifiana, kwa hiyo wako katika wao walioamini na wako katika wao waliokufuru.. (2:253).

Kwa ujumla neno wale ambao wamepewa vitabu linaenea kwa wote, watu wa kitabu na washirikina.

Aya Na 5

Dhamira katika neno hawakuamrishwa inawarudia wale waliokanusha katika waliopewa kitabu na washirikina. Makusudio yake ni kuwa, ujumbe wa Mtume(s.a.w.w) na maandishi yaliyomo katika kurasa na wahyi, hayakudhamini kitu isipokuwa ibada ya Mwenyezi Mungu kwa kuifunga pamoja na Ikhlas katika dini na kutomshirikisha Mwenyezi Mungu na kitu chochote. Neno Hunafaa lina maana ya kuondoka kwenye upande wa kupetuka mipaka na kuelekea kwenye kulingana sawa (kuwa ndani ya mipaka ya Mwenyezi Mungu). Na Mwenyezi Mungu ameiita Dini ya Kiislamu Hanifa kwa vile Uislamu unaamrisha 'uwastani' katika mambo yote na kujiepusha na kukiuka vipimo. "Kisha wasimamshe swala na watoe zaka". Baada ya kuelezea dini kwa ujumla anaelezea mafungu ya dini yenye kuhusikana. Swala na kutoa zaka ni miongoni mwa nguzo za Uislamu ambazo ni mwelekeo wa kiibada unaomhusu Mwenyezi Mungu na kutoa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu.

Makusudio ya dini iliyo sawasawa ni dini ya maandishi yenye msimamo ulio sawasawa kama walivyofasiri. Ikiwa makusudio ya maandishi ni maandishi yote ya mbiguni kama maandishi ya Nuh na wengineo katika mitume, maana yake yatakuwa hAya Na liyoamriwa na kulinganiwa katika mlingano (mwito) wa Muhammad, ndio yale yale waliyoamriwa katika vitabu vyao vyenye msimamo na wala sio jambo la kuzusha, kwani dini ya Mwenyezi Mungu ni moja na ni juu yao kuifuata dini hiyo, kwa sababu ndiyo yenye msimamo. Na ikiwa makusudio ya maandishi yenye msimamo ni yale wanayosemewa na Mtume(s.a.w.w) kutoka katika maandishi yaliyomo katika kurasa zenya kutoharishwa, basi itakuwa maana yake ni kuwa wao hawakuamrishwa ila kufuata hukumu zenye msimamo na zenye maslah ya jamii ya kiutu.

Kwa vyovyote iwavyo aya inaishiria dini ya Tawhid (kumpwekesha Mwenyezi Mungu) ambayo inadhaminiwa na Qur'an inayosadikisha vitabu vilivyo kabla yake na kuhukumia yale yanayoamrisha jamii ya watu, hali ya kusimamia mambo yao na kuchunga maslahi ya maisha yao; kama alivyo lifafanua hilo Mwenyezi Mungu kwa uwazi katika neno lake: "Basi uelekeze uso wako katika dini iliyosawasawa, ndilo umbile ambalo Allah amewaumbia watu (dini iliyosawa). Hakuna mabadiliko katika maumbile ya viumbe vya Allah. Hiyo ndiyo dini ya sawa (30:30).

Kwa aya hii basi, yanakamilika ubainifu wa kuenea ujumbe wa Mtume(s.a.w.w) na kuenea mwito wa Kiislamu kwa watu wote. Kwa hiyo neno lake Mwenyezi Mungu: "Hawakuwa wale ambao wamekufuru katika watu wa kitabu" mpaka mwisho, linaonyesha kuwa kuna ulazimu kutokana na desturi ya uongozi wa Mungu, kutimiza hoja kwa yule mwenye kuukanusha mwito miongoni mwa watu wa kitabu na washirikina. Kuhusu neno lake Mwenyezi Mungu "Mtume atokae kwa Allah" inaonyesha kuwa hiyo hoja ni Mtume Muhammad(s.a.w.w) . Kufarikiana kwao na kukanusha kwao haki kwa zamani, pia kuliendelea baada ya kuja Mtume Mhuhammad(s.a.w.w) kama anavyosema Mwenyezi Mungu katika Sura hii: "Wala hawakutengana".

Aya Na 6-7

Baada ya kuelezea ukanushaji wao wa hoja na mambo wanayolinganiwa, sasa anaingilia kutoa onyo kwa wale wakanushaji na kuwapa biashara waumini. Maana ya Aya Na ko wazi hakuna haja ya ufafanuzi.

Aya Na 8

Maana halisi ya neno Adn ni kutulia na kuthibiti, kwa hiyo makusudio yake ni pepo ya kudumu. Mwenyezi Mungu analisisitiza hilo kwa kusema: "Watakaa humo milele".

Mwenyezi Mungu kuwa radhi nao ni uhakika wa thawabu alizowapa, ikiwa ni malipo ya imani zao na matendo yao. "Hayo ni ya mwenye kumuogopa Mola wake" hiyo ndio chapa ya wema wa akhera na Mwenyezi Mungu amesema: "Kwa hakika wale wanaomuogopa Allah miongoni mwa waja wake ni wale wataalamu (wanavyuoni) ". (35:28).

Kwa hiyo kumjua Mwenyezi Mungu kunafuatia kumuogopa na kumuogopa kunafuatia kumuamini kwa maana ya kuamini kimoyo uungu wake kisha kutenda amali njema. Kuna hitilafu kubwa sana katika kufasiri aya hizi. Hitilafu hizi hazina umuhimu wa kuzielezea. Mwenye kutaka kuzijua na aangalie vitabu vyenye maelezo marefu.

Utafiti Wa Hadith Katika Tafsiri ya Qumii katika riwAya Na Abu-Jarud kutoka kwa Abu Jaffar(a.s) anasema: Hoja ni Muhammad(s.a.w.w) . Katika Durril Manthur ametoa Ibn Murdawy kutoka kwa Aisha amesema: "Nilimuuliza ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu" Ni nani Mtukufu zaidi wa viumbe kwa Mwenyezi Mungu? Akasema: "Ewe Aisha kwani hukusoma aya inayosema: Hakika wale ambao wameamini na wakatenda matendo mema hao ndio bora wa watu?" Katika hiyo hiyo Durril-Manthur ametoa Ibn Asaki, kutoka kwa Jabir bin Abdillahi amesema: "Tulikuwa mbele ya Mtume akaja Ali akasema Mtume(s.a.w.w) . "Naapa kwa yule ambaye nafsi yangu iko mikononi mwake hakika huyu na wafuasi wake ndio wenye kufuzu siku ya Kiyama." Kisha ikashuka aya hiyo, ikiwa masahaba wa Mtume(s.a.w.w) wakijiwa na Ali husema: "Amekuja bora wa watu."

Imepokewa hadith kwa maana hiyo kutoka kwa Addi kutoka kwa Ibn Abbas, vile vile kutoka kwa Ibn Murdawayh, naye kutoka kwa Ali(a.s) . Na imepokewa vile vile katika Bur'han kutoka kwa Muwaffaq bin Ahmad katika kitabu Manaqib kutoka kwa Yazid bin Sharahiyl El-Ansari, vile vile katika Majmau kutoka katika kitabu cha Shawahiduttanzil cha Hakim naye kutoka kwa Yazid bin Sharahiyl kutoka kwa Ali amesema: Wakati Mtume(s.a.w.w) akikaribia kufa, na mimi nimemwigamiza katika kifua changu, aliniambia: "Ewe Ali hivi hukusikia neno la Mwenyezi Mungu. "Hakika wale ambao wameamini na wakatenda (amali) njema hao ndio bora wa viumbe". Wao ni wafuasi wako na kukutana kwangu na nyinyi ni kwenye birika wakati utakapokusanyika umati kwa ajili ya hisabu. Wafuasi wako watakuwa wana mapako yenye kung'aa (katika viungo vya udhu).

Katika Majmau kutoka kwa Muqatil bin Salman, naye kutoka kwa Adh-dhah-hak naye kutoka kwa Ibn Abbas kuhusu neno lake Mwenyezi Mungu: "Hao ndio bora wa viumbe" amesema ilishuka kwa Ali na Ahlul Bait wake.

23

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

SURA SILZAAL ( TETEMEKO)(NA. 99)

INA AYA 8

Kwa jina la Allah, Mwingi wa Rehema , Mwenye kurehemu

إِذَا زُلْزِلَتِ الْأَرْضُ زِلْزَالَهَا ﴿١﴾

1. Itakapotetemeshwa ardhi huo mtetemeko wake.

وَأَخْرَجَتِ الْأَرْضُ أَثْقَالَهَا ﴿٢﴾

2. Na ikatoa ardhi mizigo yake.

وَقَالَ الْإِنسَانُ مَا لَهَا ﴿٣﴾

3. Na akasema mwanadamu ina nini?

يَوْمَئِذٍ تُحَدِّثُ أَخْبَارَهَا ﴿٤﴾

4. Siku hiyo itatoa habari zake.

بِأَنَّ رَبَّكَ أَوْحَىٰ لَهَا ﴿٥﴾

5. Kwa kuwa Mola wako ameiamrisha.

يَوْمَئِذٍ يَصْدُرُ النَّاسُ أَشْتَاتًا لِّيُرَوْا أَعْمَالَهُمْ ﴿٦﴾

6. Siku hiyo wataondoka watu wametawanyika tawanyika ili kuonyeshwa amali zao.

فَمَن يَعْمَلْ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ خَيْرًا يَرَهُ ﴿٧﴾

7. Basi atakayefanya wema (hata) uzani wa sisimizi atauona.

وَمَن يَعْمَلْ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ شَرًّا يَرَهُ ﴿٨﴾

8. Na atakayefanya uovu (hata) uzani wa sisimizi atauona.

UBAINIFU

Sura hii inaelezea Kiyama, kutolewa watu kwa ajili ya malipo ya sharti za kiyama ambazo ni tetemeko la ardhi na kuzungumza habari zake. Sura hii inawezekana kuwa imeshuka Makka au Madina.

Aya Na 1

Mwenyezi Mungu anasema "Itakapotetemeshwa ardhi huo mtetemeko wake" kwa maana ya kuwa tetemeko hilo ni la aina yake, kutokana na ukubwa wake.

Aya Na 2

Neno athqal lina manna ya mizigo. Kwa vyovyote vile iwavyo makusudio ya aya ni kuwa ardhi itatoa mizigo yake iliyoichukua ambayo ni wafu kama ilivyosemwa au hazina za madini au vyote hivyo. Kauli ya kwanza (wafu) ndyo iliyokaribu zaidi na maana.

Aya Na 3

Yaani mtu atapigwa na mshangao wa ajabu kutokana na tetememko hilo kiasi cha kujiuliza: Ina nini ardhi? Mbona inatetemeka hivi? Imesemwa kuwa makusudio ya mtu hapa ni kafiri asiyeamini ufufuo, na yamesemwa zaidi ya hayo kama yatakavyokuja maelezo (Inshallah).

Aya Na 4 -5

Ardhi itakuwa shahidi wa vitendo vya mwanadamu, kama vile vitavyokuwa shahidi viungo vya binadamu na maandishi ya Malaika. Hiyo ni kutokana na amri ya Mwenyezi Mungu. Na hii inafahamisha kuwa vitu vina uhsai na hisia, ijapokuwa sisi hatujui hilo, kama alivyosema Mwenyezi Mungu: "Na hakuna chochote ila kinamsabihi (Mwenyezi Mungu) kwa sifa zake njema lakini nyinyi hamfahamu kusabihi (kutukuza) kwake.." (17:44).

Akasema tena: "Hata watakapoujia (huo moto), hapo ndipo masikio yao, na macho yao na ngozi zao zitakapotoa ushahidi juu yao kwa yale waliyokuwa wakiyatenda.. Na wao waziambie ngozi zao; "Mbona mnatushuhudilia? "Nazo ziwaambie: "Allah aliyekitamkisha kila kitu ndiye aliyetutamkisha, naye ndiye aliyekuumbeni mara ya kwanza. Na kwake hivi sasa) mnarudishwa (41:20-21).

Kumekuwa na hiitilafu kubwa juu ya maana ya kuzungumza ardhi; kuwa itapewa uhai na hisia au itaumbwa sauti tu! Lakini hatuna haja na hitilafu hizo, kwa sababu vyovyote iwavyo ni kwamba ardhi itatoa ushahidi.

Aya Na 6

Makusudio ya kuondoka kutawanyika tawanyika, ni kuenda zao kwenye makazi yao katika pepo na katika moto. Na kuona matendo yao ni kuona malipo ya matendo ya au kuona umbo halisi la hayo matendo. Imesemwa kuwa makusudio yake ni kutoka makaburini mwao kuelekea kwenye mkusanyiko wakitofautina kwa nyuso nyeusi na nyeupe,na kwa fazaa na amani, ili yafahamike malipo yao kwa kuangalia tu!, kama alivyosema Mwenyezi Mungu; "Siku ambayo kila nafsi itakuta mema iliyoyafanya yamehudhurishwa, na pia ubaya iliofanya .(3:30).

Kauli ya kwanza ndiyo iliyo karibu zaidi na maana.

Aya Na 7-8

Dharra ni chembe ndogo za vumbi zinaonekana katika mwanga wa jua au sisimizi wadogo. Aya hiyo inatilia mkazo yaliyotangulia kuwa amali yoyote hata iwe ndogo kiasi gani, itaonekana. Lakini aya hizo hazikanushi kuharibika kwa amali, au kugura amali kwenda kwenye nafsi nyingine; kama kugura mema ya mwuuaji kwenda kwa mwenye kuuwa, au kubadilika maovu kuwa mema kwa baadhi ya wenye kutubia, nk; kama ilivyoelezwa katika Sura zilizotangulia kama aya inayosema: "Ili Allah apate kuwapambanua walio wabaya na walio wazuri ." (8:37).

Kwa hiyo aya hizo zinahukumia aya hizi mbili, kwani mwenye kuharibikiwa na amali yake ya heri, ni kuwa hana amali ya heri atakayoiona. Na juu ya mfano huu unaweza kukisia na kufahamu..

Utafiti Wa Hadith Katika Durril Manthur, ametoa Ibn Murdawayh na Bayhaqi kutoka jwa Anas bin Malik, kwamba Mtume(s.a.w.w) amesema: "Hakika Ardhi itatoa habari siku ya Kiyama kila lililofanywa juu ya mgongo wake, na akasoma Mtume(s.a.w.w) : "Itakapotetemeshwa ardhi huo mtetemeko wake" mapaka alipofikia: "Siku hiyo itatoa habari zake" akasema " Je, mnajua habari yake? Jibril amenijia akaniambia kuwa; kitakapokuwa Kiyama ardhi itatoa habari ya kila yaliyofanywa juu ya mgongo wake". Na imepokewa hadith ya mfano huo kwa Abu Huraira.

Ametoa Hussein bin Sufiani na Abu Naim kutoka kwa Shaddad bin Aus; amesema: Nimemsikia Mtume(s.a.w.w) akisema: "Enyi watu, hakika dunia ni maonyesho ya sasa hivi anakula mwema na muovo. Na hakika Akhera ni kiaga cha kweli, atahukumu huko Mfalme muweza, itathibiti haki na itabatilika batili, Enyi watu kuweni watoto wa akhera wala msiwe watoto wa dunia, kwani kila mtoto humfuata mama yake. Fanyeni amali kwa tahadhari. Jueni kwamba mtaonyeshwa amali zenu na mtakutana na Mwenyezi Mungu. Basi mwenye kufanya wema (hata) uzani wa sisimizi atauona na mwenye kufanya uovu (hata) uzani wa sisimizi atauona! Katika Tafsiri ya Qummi, kuhusu Aya Na 2, amesema: Mizigo ni watu. Na kuhusu aya 4-6 amesema: Yatakuja makundi ya waumin, makafiri na ya wanafiki ili waone matendo yao. Katika riwAya Na Abu Jarudi kutoka kwa Ab Jaffar(a.s) kuhusu Aya Na 7-8 anasema: Ikiwa mtu ni katika watu wa motoni na amefanya amali ya heri ya uzani wa sisimizi itakuwa ni majuto ikiwa ameifanya siyo kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. Na akiwa ni mtu wa peponi na amefanya amali ya shari ya uzani wa sisimizi, ataonyeshwa shari hiyo, kisha atasamehewa.

SURA ADIYAAT (FARASI) (NA. 100)

INA AYA 11

Kwa jina la Allah, Mwingi wa Rehema , Mwenye kurehemu.

وَالْعَادِيَاتِ ضَبْحًا ﴿١﴾

1. Naapa kwa farasi wanaokwenda mbio wakihema.

فَالْمُورِيَاتِ قَدْحًا ﴿٢﴾

2. Wanaotoa moto, kwa kupiga kwata.

فَالْمُغِيرَاتِ صُبْحًا ﴿٣﴾

3. Wanaowashambulia maadui ghafla wakati wa asubuhi.

فَأَثَرْنَ بِهِ نَقْعًا ﴿٤﴾

4. Wakatifua vumbi wakati huo.

فَوَسَطْنَ بِهِ جَمْعًا ﴿٥﴾

5. Wakaliingilia kati wakati huo kundi (la maadui).

إِنَّ الْإِنسَانَ لِرَبِّهِ لَكَنُودٌ ﴿٦﴾

6. Hakika mwanadamu ni mwenye utovu wa shukrani sana kwa Mola wake.

وَإِنَّهُ عَلَىٰ ذَٰلِكَ لَشَهِيدٌ ﴿٧﴾

7. Na yeye ni shahidi wa hilo.

وَإِنَّهُ لِحُبِّ الْخَيْرِ لَشَدِيدٌ ﴿٨﴾

8. Na hakika yeye kwa sababu ya kupenda mali ni bakhili.

أَفَلَا يَعْلَمُ إِذَا بُعْثِرَ مَا فِي الْقُبُورِ ﴿٩﴾

9. Je, hajuwi watakapofufuliwa waliomo makaburini.

وَحُصِّلَ مَا فِي الصُّدُورِ ﴿١٠﴾

10. Yakadhihirishwa yalipo nyoyoni.

إِنَّ رَبَّهُم بِهِمْ يَوْمَئِذٍ لَّخَبِيرٌ ﴿١١﴾

11.Hakika Mola wao siku hiyo ni mjuzi mno wa hali zao.

UBAINIFU

Sura inataja ukanushaji wa mtu kwa neema ya Mola wake na kupenda kwake sana heri. Na yeye atahisabiwa juu ya hayo. Sura hii imeshuka Madina kwa ushahidi wa habari ya vita inayoelezwa katika Sura hiyo kwa mfano: "Naapa kwa farasi wa wapigania Jihadi"; kama yatakavyokuja maelezo yake. Na vita vya jihadi vilianza baada ya Hijra. (kuhama wa Mtume(s.a.w.w) . Hayo yanatiliwa nguvu na hadith zilizopokewa na Shia kutoka Maimamu wa Ahlul Bait kuwa, Sura hiyo ilishuka kwa ajili ya Ali(a.s) katika vita vya Salasil (Minyororo). Yatakuja maelezo yake katika utafiti wa hadith (Inshallah) kwa kufuatana na mapokezi ya Ahli Sunnah.

Aya Na 1

Mwenyezi Mungu anaapa kwa farasi wanaokwenda mbio wakihema; yaani wakitoa sauti ya pumzi mbele ya maadui na hali hiyo ni maarufu kwa farasi, ingawaje inadaiwa kuwa wanyama wengine wanayo. Maana yake ni kuwa Mwenyezi Mungu anaapa kwa jeshi lililo na farasi wa namna hiyo. Imesemwa kuwa makusudio yake ni ngamia wa mahujaji wanapokuwa Mina siku wa Nahr (ya kuchinja). Na pia imesemwa kuwa ni ngamia wa vita. Lakini aya zinazofuata hazionyeshi kuwa makusudio yake ni ngamia !

Aya Na 2

Yaani farasi wanaotoa moto kwa kupiga kwato katika mawe au ardhi ngumu. Imesemwa kuwa makusudio ya kuwasha moto hapa ni hila za wanaume katika vita. Na imesemwa kuwa ni kuwasha moto tu! Na pia imesemwa kuwa makusudio ni ndimi za wanaume zinazowasha moto kutokana na uzito wa yale wanayoyasema. Lakini njia zote hizo ni dhaifu kwa dhahiri kabisa.

Aya Na 3

Wanatajwa farasi kuwa ndiyo wenye kushambulia maadui kwa njia ya fumbo kwa maana ya wenye farasi hao.

Aya Na 4

Watawatimulia vumbi maadui kutokana na mashambulizi.

Aya Na 5

Yaani kuliingilia kati kundi la maadui. Imesemwa kuwa maana yake ni kuingia kati ngamia katika Mina siku ya Hijja. Lakini kuzifikiria aya zote tano kuwa na maana ya ngamia wa mahujaji wanaomiminika kwenda Mina, ni kinyume kabisa. Ilivyo hasa makusudio yake ni farasi wa vitani. Na mpangilio wa aya inayosema: (Wanaoshambulia maadui ghafla wakati wa asubuhi:) na (wakaingia katikati ya kundi), unafahamishwa kuwa Mwenyezi Mungu anaapa kwa farasi wa vita. Ne herufi fa katika aya nne, inafahamisha mpangilio wa kufuatana kila moja baada ya nyingine.

Aya Na 6

Ni jawabu ya Qasam (kiapo) inayotolea habari yale yaliyo katika tabia ya mtu, kama kufuata matamanio, kuyavamia na mambo ya dunia yanayokwisha na kuacha kumshukuru Mola wake juu ya alivyomneemesha. Inaonyesha aina ya watu wanaoshambuliwa. Inaonyesha kuwa makusudio ya kukanusha kwao, ni kukanusha neema ya uislamu aliyowaneemesha Mwenyezi Mungu juu yao. Nayo ni neema kubwa waliyopewa na kutengeneza vizuri maisha yao ya dunia na wema wa maisha yao mengine ya milele.

Aya Na 7

Dhamira katika neno "na yeye" inamrudia mtu, kwa hiyo makusudio yanakuwa: mtu yeye mwenyewe anashuhudia juu ya kukanusha na kukufuru kwake. Kwa hiyo aya iko katika maana ya aya nyengine inayosema: "Bali mtu juu ya nafsi yake ni mwenye kushuhudia ". (75:14).

Na imesemwa kuwa dhamira inamrudia Mwenyezi Mungu, kwa maana kuwa yeye Mwenyezi Mungu ni shahidi. Lakini mpangilio wa dhamira hauliwafiki hilo.

Aya Na 8

Neno Khayr hapa limekuja kwa maana ya mali, yaani mtu kwa ajili ya kupenda sana mali anakuwa bakhili. Imesemwa kuwa makusudio yake ni hakika mtu ni mwingi wa kupenda mali na hilo linampelekea kujuzuwiya na kutoa haki ya Mwenyezi Mungu na kutoa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. Namna hii wamefasiri. Lakini hayo hayaweki mbali kuwa makusudio ya Khayr ni kheri ya aina yoyote. Na kwamba kupenda kheri ni maumbile ya kiutu, ndipo mtu anaona anasa za dunia ndio kheri, kwa hiyo zinamuingia na zinamsahauliza kumshukuru Mola wake.

Aya Na 9 – 10

Yaliyo katika nyoyo ni sifa ya imani au ukafiri, kama alivyosema Mwenyezi Mungu "Siku itakayofuniliwa siri ". (87:9).

Na maana kwa ujumla - na Mwenyezi Mungu ndiye mjuzi zaidi - ni kuwa; hivi hajui mtu kuwa kwa sababu ya kukanusha kwake na kumkufuru kwake Mola wake atalipwa? Wakati watakapotolewa waliomo makaburini na kudhihirishwa siri za nafsi, miongoni mwa imani na kufuru na utii na uasi. Hakika Mola wao, siku hiyo ni mjuzi mno wa hali zao, kwa hiyo atawalipa.

Utafiti Wa Hadith Katika Majmau imesemwa kuwa; Mtume(s.a.w.w) alipeleka kikosi katika makao ya ukoo wa Kinana kikiongozwa na El-Mundir bin Amri El-Ansari mmoja wa Makamanda. Walipochelewa kurudi, Mwenyezi Mungu akampa khabari Mtume(s.a.w.w) kwa kusema: "Naapa kwa farasi wenye kwenda mbio wenye kuhema." Imesemwa kuwa Sura hii ilishuka wakati Mtume(s.a.w.w) alipompeleka Ali(a.s) kwa Dhatus-Salasil (Wenye Minyororo) na akawashinda. Na hilo ni baada ya kuwapeleka masahaba wengine mara nyingi. Wote wakarudi kwa Mtume bila ya kufaulu. Hadith hii imepokewa kutoka kwa Abu Abdillah(a.s) katika hadith ndefu. Na vita hivyo viliitwa vya minyororo kwa sababu baadhi yao walitekwa, wakauawa na wakafungwa mateka kwa kamba za mikoni kama vile wamefungwa na nyororo.

Utafiti Wa Hadith Iliposhuka Sura hii Mtume(s.a.w.w) alitoka akawaswalisha watu swala ya asubuhi na akasoma katika swala Sura hiyo. Alipomaliza kuswali masahaba zake wakasema: "Sura hii haituijui", Mtume(s.a.w.w) akasema: "Ndio hakika Ali amewashinda maadui wa Mwenyezi Mungu na Jibrail amenifahamisha hilo usiku huu. Baada ya siku kidogo Ali akafika pamoja na ngawira na mateka kadhaa ."

14

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

SURA AL-FAJR (ALFAJIRI) (NA. 89)

INA AYA 30

Kwa jina la Allah, Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu

وَالْفَجْرِ ﴿١﴾

1. Naapa kwa Alfajiri.

وَلَيَالٍ عَشْرٍ ﴿٢﴾

2. Na (kwa) masiku kumi.

وَالشَّفْعِ وَالْوَتْرِ ﴿٣﴾

3. Na (kwa) shufwa na witiri.

وَاللَّيْلِ إِذَا يَسْرِ ﴿٤﴾

4. Na (kwa) usiku unapopita.

هَلْ فِي ذَٰلِكَ قَسَمٌ لِّذِي حِجْرٍ ﴿٥﴾

5. Katika hayo mna kiapo kwa mwenye akili.

أَلَمْ تَرَ كَيْفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍ ﴿٦﴾

6. Je, hujui jinsi Mola alivyoifanya (kabila) ya Aad.

إِرَمَ ذَاتِ الْعِمَادِ ﴿٧﴾

7. Iram wenye nguzo ndefu?

الَّتِي لَمْ يُخْلَقْ مِثْلُهَا فِي الْبِلَادِ ﴿٨﴾

8. Ambayo haikuumbwa mfano wake katika miji.

وَثَمُودَ الَّذِينَ جَابُوا الصَّخْرَ بِالْوَادِ ﴿٩﴾

9. Na (kabila) ya Thamud ambao walikua wakipasua majabali katika (mji wa) waad.

وَفِرْعَوْنَ ذِي الْأَوْتَادِ ﴿١٠﴾

10. Na Firaun mwenye vigingi.

الَّذِينَ طَغَوْا فِي الْبِلَادِ ﴿١١﴾

11. Ambao walipetuka mipaka katika miji.

فَأَكْثَرُوا فِيهَا الْفَسَادَ ﴿١٢﴾

12. Wakazidisha humo mambo maovu.

فَصَبَّ عَلَيْهِمْ رَبُّكَ سَوْطَ عَذَابٍ ﴿١٣﴾

13. Akawateremshia Mola wako namna za adhabu.

إِنَّ رَبَّكَ لَبِالْمِرْصَادِ ﴿١٤﴾

14. Hakika Mola wako ni Mwenye kuotea.

فَأَمَّا الْإِنسَانُ إِذَا مَا ابْتَلَاهُ رَبُّهُ فَأَكْرَمَهُ وَنَعَّمَهُ فَيَقُولُ رَبِّي أَكْرَمَنِ ﴿١٥﴾

15. Ama mwanadamu - Mola wake anapomjaribu, akamtukuza, akamneemesha, husema: Mola wangu amenitukuza.

وَأَمَّا إِذَا مَا ابْتَلَاهُ فَقَدَرَ عَلَيْهِ رِزْقَهُ فَيَقُولُ رَبِّي أَهَانَنِ ﴿١٦﴾

16. Ama anapomjaribu akampunguzia riziki yake husema Mola wangu amenitweza.

كَلَّا بَل لَّا تُكْرِمُونَ الْيَتِيمَ ﴿١٧﴾

17. La, si hayo tu! Bali nyinyi humumtukuzi yatima.

وَلَا تَحَاضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ الْمِسْكِينِ ﴿١٨﴾

18. Wala hamhimizani katika kumlisha maskini.

وَتَأْكُلُونَ التُّرَاثَ أَكْلًا لَّمًّا ﴿١٩﴾

19.Na mnakula mirathi kula kwa pupa.

وَتُحِبُّونَ الْمَالَ حُبًّا جَمًّا ﴿٢٠﴾

20. Na mnapenda mali mapenzi makubwa.

كَلَّا إِذَا دُكَّتِ الْأَرْضُ دَكًّا دَكًّا ﴿٢١﴾

21. Si hivyo! Ardhi itakapo pondwa pondwa!

وَجَاءَ رَبُّكَ وَالْمَلَكُ صَفًّا صَفًّا ﴿٢٢﴾

22. Akaja Mola wako na Malaika (wamejipanga) safu kwa safu.

وَجِيءَ يَوْمَئِذٍ بِجَهَنَّمَ ۚ يَوْمَئِذٍ يَتَذَكَّرُ الْإِنسَانُ وَأَنَّىٰ لَهُ الذِّكْرَىٰ ﴿٢٣﴾

23. Ikaletwa siku hiyo Jahannam! Siku hiyo ndipo mwanadamu atakapokumbuka, lakini kutamfaa nini kukumbuka (kwake)?!

يَقُولُ يَا لَيْتَنِي قَدَّمْتُ لِحَيَاتِي ﴿٢٤﴾

24. Atasema laiti niliyatangulizia (wema) maisha yangu.

فَيَوْمَئِذٍ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُ أَحَدٌ ﴿٢٥﴾

25. Basi siku hiyo hapana yoyote atakayeadhibu kama adhabu yake (Mwenyezi Mungu).

وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُ أَحَدٌ ﴿٢٦﴾

26. Wala hapana yoyote atakayefunga kama kufunga kwake.

يَا أَيَّتُهَا النَّفْسُ الْمُطْمَئِنَّةُ ﴿٢٧﴾

27. Ewe nafsi iliyotua!

ارْجِعِي إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةً مَّرْضِيَّةً ﴿٢٨﴾

28. Rejea kwa Mola wako hali yakuwa uradhi (na) mwenye kuridhiwa.

فَادْخُلِي فِي عِبَادِي ﴿٢٩﴾

29. Kisha ingia katika waja wangu (wema).

وَادْخُلِي جَنَّتِي ﴿٣٠﴾

30. Na uingie katika pepo yangu.

UBAINIFU

Katika Sura hii kuna makemeo juu ya kufungamana na dunia kwenye kufuatiwa na kupetuka mpaka na ukafiri, na kuwaogopesha watu wenye mambo hayo na ukali wa adhabu ya Mwenyezi Mungu katika dunia na akhera. Kwa hiyo Sura inabainisha kuwa mtu kwa ufupi wa mtazamo wake na ubaya wa fikra yake anaona kuwa anayoletewa na Mwenyezi Mungu miongoni mwa neema yake ni katika ukarimu wake Mwenyezi Mungu, na yale anayovaana nayo miongoni mwa ufakiri ni utwezo. Kwa hiyo anapetuka mpaka na kuwa mfisadi katika ardhi anapopata na anakufuru anapokosa. Basi yanayompata katika cheo na utajiri na katika ufakiri na dhiki ya maisha, ni mitihani na balaa za Mungu ili adhihirishe kwayo yale atakayoyatanguliza akhera yake kutoka katika dunia yake.

Basi mambo hayako kama vile anavyofikiri mtu na anavyosema, bali mambo yalivyo kama atakavyoyakumbuka itakapotuka hisabu na kuletwa adhabu, kwamba yaliyompata miongoni mwa ufakiri au utajiri na nguvu au unyonge yalikuwa ni mitihani ya Mungu. Ilikuwa inamuwezekania yeye kutangulizia kesho yake kutokana na leo yake, lakini hakufanya na akaathirika na mateso kuliko thawabu. Basi haitapata maisha mema katika akhera isipokuwa nafsi iliyotua kwa Mola wke, isiyoyumba kwa vimbunga vya balaa wala kupetuka mpaka kwa kipato au kukufuru kwa kukosa. Sura hii imeshuka Makka kwa ushahidi wa mpangilio wa aya zake.

Aya Na 1-4

Aya hizo zote ni kiapo. Huenda dhahiri ya neno Alfajiri, Alfajiri yoyote, lakini sio mbali kuwa makusudio yake ni Alfajiri ya usiku wa Ijumaa. Imesemwa ni swala ya Alfajiri na imesemwa ni mchana wote na imesemwa ni kupasuka chemchem katika miamba na mengineyo. Njia zote hizi ziko mbali. Kuhusu masiku kumi huenda makusudio ni masiku kumi ya mwanzo katika mwezi wa Dhulhijja. Imesemwa makusudio ni siku za mwisho za mwezi wa Ramadhan, na ikasemwa ni za mwanzo wake. Pia imesemwa ni siku kumi za mwanzo za mwezi wa Muharram na ikasemwa kuwa ni ibada ya masiku kumi kuchukulia kuwa makusudio ya Alfajiri ni swala ya Alfajiri. Kuhusu Shufwa wa Witiri maana yanakubali kufungamana na kuwa ni siku wa Tarwiya (tarehe 8 Dhul-hijja) na siku ya Arafa (tarehe 9 Dhul-hijja). Imesemwa kuwa makusudio yake ni swala mbili ( rakaa mbilimbili na rakaa moja) katika mwisho wa usiku. Na imesemwa ni swala yoyote, ziko mbili mbili na moja.

Pia imesemwa kuwa Shufwa ni siku ya Idd ya Dhul-hijja wa Witiri ni siku ya Arafa, na imesemwa Shufwa ni viumbe vyote, kwa sababu Mwenyezi Mungu anasema: "Na tukawaumba wanawake na wanaume " (78:8).

Na Witiri ni Mwenyezi Mungu (s.w.t) Kuna riwaya nyingi zitakazokuja juu ya kauli hizi katika utafiti wa hadith 8 Vile Vile imesemwa makusudio yake ni hisabu ya viwiliviwili na kimojakimoja na kwamba kuapa kwa hisabu, ni kuwa kudhibiti idadi katika kiasi ni katika nema kubwa itokayo kwa Mwenyezi Mungu. Imesemwa kuwa ni viumbe vyote, kwa sababu vitu vyote ama vitakuwa ni jozi au kimoja. Imesemwa kuwa makusudio ya Witiri ni Adam na Shufwa ni kuwa pamoja na mkewe Hawa.

Na imesemwa Shufwa ni mchana, na usiku, na Witiri ni mchana ambao, hauna usiku nao ni siku ya Kiyama. Imesemwa Shufwa ni Safa na Marwa na Witiri ni Al-Ka'aba, na imesemwa ni siku za kabila la Ad na Witiri ni nyusiku zake. Na imesemwa Shufwa ni milango ya motoni saba. Na zaidi ya hayo mengi yaliyosemwa zaidi ya kauli thelethini na sita (36). Kuhusu kauli yake; Na (kwa) usiku unapopita ni kama Aya Na 33, Sura ya 74 inayosoma: "Na (kwa) usiku unapokucha".

Kwa dhahiri herufi Lam ni ya jinsi yaani usiku wowote, lakini wengine wamesema ni usiku wa Muzdalifa (usiku wa kuamkia Idd) ambao mahujaji wanapita kutoka Arafa mpaka Muzdalifa wanakusanyika Mahujaji kwa kumtii Mwenyezi Mungu kisha wanaamkia kwenda Mina kwa hiyo kama unavyoona itakuwa makusudio ya usiku kumi ni usiku kumi za mwanzo katika mwezi wa Hijja (Dhul-Hijja).

Aya Na 5

Ni ishara ya yaliyotangulia katika kiapo na ni swali la kuthibitisha, maana yake kwa ujumla, ni kwamba, katika hayo tuliyoyatanguliza kuyaapia yanatosha kwa mwenye akili ya utambuzi wa maneno inayopambanua haki na batili. Na Mwenyezi Mungu akiapa naye haapi isipokuwa lile lenye utukufu na daraja linakuwa ni neno la haki lenye kutiliwa mkazo ambalo halina shaka katika ukweli wake. Jawabu la kiapo limeondolewa linafahamika kutokana na yatakayotajwa katika adhabu ya watu waliopetuka mipaka na ukafiri katika dunia na akhera na thawabu ya nafsi yenye kutulia na kwamba kuneemesha kwake Mwenyezi Mungu (s.w.t) juu ya aliyomneemesha na kumzuilia, hakika hayo ni majaribio na mitihani. Kuondoa jawabu la kiapo na kulileta kwa njia ya fumbo, ni kutilia mkazo zaidi katika hali ya kuonya na kutoa biashara.

Aya Na 6

Ni kabila la Aad wa kwanza nao ni kaumu ya Mtume Hud(a.s) . Vimekaririka visa vyao katika Qur'an tukufu na imeonyesha kwa wao walikuwa watu wa nchi yenye machunguu ya michanga. Yameelezwa yale yanayopatikana katika visa vyao katika Sur ya Hud (11).

Aya Na 7-8

Neno Imad ni nguzo za nyumba. Kwa dhahiri ya aya mbili hizi, ni kuwa Iram ulikua ni mji uliokuwa wa aina yake wenye majumba marefu na maguzo marefu. Hakika habari zao zimekatika na athari zao zimefutika, kwa hiyo hakuna njia ya ufafanuzi itakayoeleza hali zao kiasi cha kuituliza nafsi isipokuwa yale tu, yaliyohadithiwa na Qur'an tukufu kwa ujumla juu ya kisa chao; kwamba wao walikuwa baada ya kaumu ya Nuh, wakazi wa nchi yenye machuguu ya mchanga, na walikuwa ni wenye umbo kubwa na nguvu kubwa zaidi na walikuwa na maendeleo, miji yenye majengo mengi ardhi za rutuba zenye mabustani ya mitende na mimea na mahali pazuri. Kimeelezewa zaidi kisa chao katika Sura ya Nuh.

Imesemwa kuwa makusudi ya neno Iram ni hao kaumu ya Aad - na sili na neno hilo ni jina la baba yao kwa hiyo wakaitwa kwa jina la baba yao, kama inavyosemwa Quraish kwa kukusudia wanawe au Israil kwa kukusudia wana Israil. Makusudio ya kusema wenye maguzo marefu ni kuwa wao ni watu wenye nguvu, na maana yake ni Je, hujui jinsi Mola wako alivyoifanya (kabila) ya Aad Iram wenye nguvu ambao haukumbwa mfano wao katika miji, au katika dunia nzima, lakini hayo hayaepukani na kuwa mbali na dhahiri ya tamko. Ya umbali zaidi ya yaliyosemwa kwamba makusudio ya kuwa wao ni wenye maguzo marefu, ni vile kuwa wao walikuwa ni watu wa kuazimia kusafiri katika wakati wa maleleji na mimea inaponyauka basi hurudi majumbani mwao. Kisa cha bustani ya Iram kilichopokewa kutoka kwa Wahb bin Manbih na Kaabulahbar, ni katika ngano za watu wakale tu!

Aya Na 9

Yaani walipasua miamba ya milima kwa kuichonga kuwa nyumba. Aya hii iko katika maana ya aya inayosema: "Na mnachonga milimani majumba mkastarehe tu! " (26:149)

Aya Na 11

Huyo ni Firaun wa Musa, ameitwa mwenye vigingi- kutokana na yaliyo katika baadhi ya riwaya - kwamba yeye alikuwa akitaka kumuadhibu mtu humnyoosha juu ya ardhi na kuipingilia mikono yake na miguu yake kwa vigingi vine katika ardhi, au humnyoosha juu ya ubao na kumfanyia hivyo. Hayo yanatiliwa nguvu na yale aliyoyasimulia Mwenyezi Mungu kuhusu kauli yake Firaun akiwatisha wachawi walipomwamini Musa kwa kusema: "Nitawasulubu katika mashina ya mitende ." (20:71).

Hakika wao walikuwa wakiwamba mikono ya msulubiwa na miguu yake juu ya ubao wa kusulubu.

Aya Na 12

Ni sifa wa waliotajwa, Ad, Thamud na Firaun, maana yako wazi.

Aya Na 13

Ametaja kumimina kwa njia ya fumbo kwa maana ya kufuatana, maana yake ni kuwa Mwenyezi Mungu aliteremsha kwa mataghut wote hawa wenye kukithirisha uharibifu mara tu, baada ya kupetuka kwao mipaka na ufisadi wao, adhabu kali ya aina yake yenye kufuatana mfululizo.

Aya Na 14

Kuwa Mwenyezi Mungu yuko katika kuotea, ni istiara ya kufananisha Mwenyezi Mungu anavyochunga matendo ya waja wake na mtu anayeotea mtu apite amchukue, bila ya kutambua. Basi Mwenyezi Mungu anachunga matendo ya waja wake, wakipetuka mipaka na kukithirisha ufisadi tu, huwaadhibu kwa adhabu kali. Aya hiyo ni sababu ya yaliyotangulia katika mazungumzo ya kuadhibu wanaopetuka mipaka wenye kukithirisha ufisadi. Kuongeza dhamira katika neno Mola na kuwa "mola wako", ni kuonyesha kuwa desturi hiyo ya adhabu ilikuwa ni yenye kupita katika umma wake Mtume(s.a.w.w) kama ilivyopita katika umati zilizotangulia.

Aya Na 15

Ni mtiririko wa yaliyotangulia, ndani yake mna ufafanuzi kuhusu hali ya mtu anapopewa neema ya dunia au anapozuiliwa, ni kama vile imesemwa: Hakika mtu yuko chini ya ulinzi wa Mungu, anaotewa na Mola wake kuwa je, atatengenea au ataharibika?. Kwa hiyo anamjaribu na kumtahini katika yale atakayompa katika neema yake au kunyima kwake. Ama mtu yeye akineemeshwa huhisabu kwamba huo ni utukuzo wa Mungu kwa hiyo anaweza kufanya vile anavyotaka. Hivyo anapetuka mipaka na kukithirisha ufisadi. Na akimzuilia na kuifanya chache riziki yake, huhisabu kuwa ametwezwa na Mungu, basi hukufuru na kulalamika Makusudio ya mtu ni jinsi ya mtu. Kusema kwake: akamtukuza akamneemesha ni tafsiri ya majarabio yaani Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemtukuza na akampa nema iliamshukuru na amuabudu, lakini yeye mtu mwenyewe anajaalia ni mateso juu ya nafsi yake yanayofuatiwa na adhabu. Kuhusu neno "husema Mola wangu amenitukuza" yaani amenijaalia juu ya ukarimu unaotokana naye kwa neema ambazo amenipa, kwa hiyo ninaweza kufanya lile ninalo taka.

Kusema "Mola wangu amenitukuza" kuko katika mnasaba wa kumzingatia Mungu - hayo hayasemwi na waabudu masanamu na wanaomkanusha Mungu - na ni kwenye kujengwa juu ya kumkubali Mungu kwa kiasi cha maumbile yalivyo ijapokuwa ulimi unajizuia na hilo, vile vile aya inayofuatia.

Aya Na 16

Yaani akifanya mtihani ikawa dhiki riziki yake, basi husema Mola wangu amenidhalilisha. Kutokana na aya hizi (15 na 16) yanadhihirika mambo yafuatayo:

Kwanza : Kukaririka majaribio na kuthibitika katika sura mbili za neema na kuzuiliwa, ni kwamba kupewa neema na kuzuiliwa vyote ni katika majaribio na mitihani ya Mungu kama alivyosema: "Tutawajaribu kwa (mambo) ya shari na heri " (21:35).

Pili : Kupewa neema kwa kuwa ni fadhila na rehema, ni utukufu iwapo wanadamu hawakukubadilisha kuwa adhabu. Tatu: Mtu anaona wema wake katika maisha ya dunia ni kuneemeshwa katika dunia ka neema za Mwenyezi Mungu, hivyo anaona ndio utukufu na kunyima kunakotokana na Mwenyezi Mungu anakuona kuwa ni uovu. Ilivyo nikuwa, utukufu uko katika kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu kwa imani na amali njema, ni mamoja iwe ni utajiri au ufakiri, kupata au kukosa, yote hayo ni mitihani. Wanayo maana nyengine kuhusu aya hizi mbili lakini tumeacha kuyaonyesha kwa kutokuwa na umuhimu wowote.

Aya Na 17

Na makemeo kwa yale wanayoyasema kwamba utukufu uko katika utajiri na kwamba ufakiri na kukosa ni madhila. Basi si hivyo isipokuwa kutoa kwake Mwenyezi Mungu (s.w.t) neema, na kuizuia yote hayo ni mitihani anayojaribiwa mtu. Kusema kwake Mwenyezi Mungu: Bali nyinyi hamumtukuzi yatima, ni kutilia mkazo makemeo kwa kutaja baadhi ya neema ambayo haikusanyi utukufu kabisa, kama kukosa kumtukuza yatima kwa kula urathi wake na kumzuilia nao na kukosa kuhimizana juu ya kumlisha maskini kwa ajili ya kupenda mali. Kuacha kumtukuza yatima ni kumzuilia na urathi wa mzazi wake kama walivyokuwa wakiwazuilia watoto wadogo na kurithi, kama inavyotia nguvu aya inayofuatia.

Aya Na 18

Yaani hamuhimizani kutoa sadaka. Hayo yanatokana na kupenda mali sana kama ilivyo katika aya inayofuatia.

Aya Na 19

Maana ya neno Lamma ni mtu kula fungu lake na la mwengine, na kula chochote anachokipata kiwe kibaya au kizuri. Aya hii ni tafsiri ya kukosa kumtukuza yatima kama iliyotangulia.

Aya Na 20

Aya hiyo nayo inafasiri kukosa kuhimizana katika kumlisha maskini kama ilivyotangulia.

Aya Na 21

Makusudio yake ni kufika siku ya Kiyama. Hilo ni kemeo la pili kutokana na yale anayoyasema mtu katika hali mbili za utajiri na ufakiri. Aya hii inasimamia sababu za makemeo kwa maana ya kuwa, sio kama anavyosema mtu, kwani yeye atakumbuka kitakaposimama Kiyama kwamba maisha ya dunia na vilivyomo ndani yake miongoni mwa utajiri na ufakiri sio makusudio kwa dhati, bali yamekuwa ni majaribio na mitihani kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) Anapambanua kutokana na mitihani hiyo mwema na mwovu na inamuandalia mtu yale atakayoishi kwayo katika akhera. Hakika mtu ametatizika akadhania kuwa utukufu ndio makusudio kwa dhati akajishughulisha nao na wala asitangulize chochote kwa maisha yake ya Akhera. Kwa hiyo wakati huo atatamani huku akisema: Laiti mimi niliyatanguliza (wema) maisha yangu, lakini matamani hayatatoshelezea lolote na adhabu.

Aya Na 22

Kunasibisha kuja Mungu ni katika mikanganyo ambayo inahukumuliwa na kauli yake Mwenyezi Mungu (s.w.t) "Hakuna chochote mfano wake " (42:11). Na yaliyokuja katika alama za Kiyama, ni katika upambanuzi wa kuondoa sababu na mapazia yaliyowaziba na kushihiri kwamba Mwenyezi Mungu ni haki iliyo wazi. Kwa hiyo yale yaliyopokewa katika hadith yanalirudia hilo kwamba makusudio ya kuja kwake Mwenyezi Mungu (s.w.t) ni kuja amri yake kama alivyosema Mwenyezi Mungu: "Na amri siku hiyo ni ya Allah " (82:19).

Kunatilia nguvu njia hii kusema kwake Mwenyezi Mungu: "Je, kuna jengine wanalongojea ila kuwafikia Allah katika vivuli vya mawingu na kuwafikia malaika na imekwishapitishwa amri ". (2:210).

Kama tukikikutanisha na kusema kwake. "Je, wanangoja jengine (hawa makafiri) ila wawafikie Malaika? Au iwafikie amri ya Mola wako? " (16:33). Kwa hiyo basi kuna neno lililondolewa, kukadiria kwake ni: ikaja amri ya Mola wako. Au kunasibisha kuja Mungu ni kwa majazi (fumbo) ya kiakili.

Aya Na 23

Sio mbali kuwa makusudio ya kuletwa Jahannam ni kudhihirishwa, kama ilivyo katika kauli yake. "Basi tumekuondolea pazia yako kuona kwako leo kumekuwa kukali " (50:22).

Kusema kwake "Siku hiyo atakumbuka mtu" yaani atakumbuka kwa uwazi zaidi kwamba yale yaliyokuwa yakimjia katika maisha ya dunia miongoni mwa heri au shari yalikuwa ni majaribio ya Mwenyezi Mungu na mitihani yake na yeye akapuuza. Hivyo ndivyo unavyofahamisha mpangilio wa maneno. Kusema kwake "wapi kutamfaa kukumbuka" ni fumbo la kukosa kunufaika na kukumbuka isipokuwa kukumbuka kungefaa kama angekuunganisha na kutubia na kutenda amali njema kwa yale aliyoyapuuza, na leo ni siku ya malipo sio siku ya kutubia na kufanya amali.

Aya Na 24

Maisha hapa ni ya akhera au ni maisha ya kihakika ambayo ndiyo hayo maisha ya akhera, kama kulivyozindua kusema kwake: "Na hayakuwa haya maisha ya dunia ila ni upuzi na mchezo; na nyumba ya akhera ndio maisha hasa: Laiti wangalijua ". (29:64) Makusudio ya kuyatanguliza maisha ni kuyatangulizia amali njema.

Aya Na 25-26

Dhamir katika neno adhabu na kufunga inamrudia Mwenyezi Mungu. Yaani siku hiyo hakika adhabu yake na kufunga kwake kutakuwa zaidi ya adhabu ya kiumbe chochote. Wengine wamesoma kwa Fat'ha ya Dhali na Thau. Dhamir kwa kisomo hiki itakuwa inamrudia mtu, yaani hataadhibishwa yoyote siku hiyo mfano wa adhabu ya mtu wala hatafungwa yoyote siku hiyo mfano wa kufunga kwa mtu.

Aya Na 27

Mpangilio wa maneno uonaokubaliana na 'nafsi' hii kutokana na yale yaliyotajwa kabla yake katika sifa zinazofungamana na dunia, upitukaji mipaka, ufisadi na ukafiri na yale yaliyoahidiwa katika mwisho mbaya, unaonyesha kuwa nafsi yenye kutulia ni ile inayotulizana kwa Mola wake na kurudhia kile kinachoridhiwa na Mola wake, inajiona kuwa ni mtumwa asiyejimiliki na chochote katika kheri na inaiona dunia ni nyumba ya kupita, na inayoyakabili katika hiyo dunia miongoni mwa utajiri au ufakiri, manufaa au madhara, ni majaribio na mitihani ya Mungu. Kwa hiyo mtiririko wa neema haumpelekei kupetuka mipaka, kufanya ufisadi mwingi au kujifanya mkubwa wala ufakiri na kukosa kitu hakumuingizi katika ukafiri na kuwacha kushukuru, bali yeye ni mwenye kutulizana, hakosei njia yake yenye kunyooka kwa kupetuka mipaka au kuwapitusha mipaka wengine.

Aya Na 28

Kuisifu nafsi kwa hali yakuwa radhi ni kwamba kutulizana kwale kwa Mola wake kunalazimisha kuridhia kwake yale yaliyokadiriwa na kuhukumiliwa na wala hayamchukizi. Mtu akimridhia Mola wake naye humridhia, kwani Mwenyezi Mungu S.W.T. huchukia sana kutoka mja katika kipambo chake. Basi akilazimiana na njia ya kuwa mja wa Mwenyezi Mungu, litawajibisha hilo radhi ya Mola wake, kwa hiyo ndio maana hali ya kuridhia imefuatishwa na kuridhiwa.

Aya Na 29

Inaungana na aua iliyotangulia inafahamisha kuwa mwenye nafsi yenye kutulia yuko katika kundi la waja wa Mwenyezi Mungu. Hilo ni kwamba alipotulia kwa Mola wake alijiondoa kujiona huru, na akaridhia ile iliyohaki kwa Mola wake, akaona dhati yake, sifa zake na vitendo vyake ni miliki ya Mola wake. Hakupita katika yaliyokadiriwa kuhukumiliwa wala katika yaliyo amrishwa na kukatazwa isipokuwa yale anayoyataka Mola wake. Huko ndiko kudhihiri uja wenye kutimia. Kwa hiyo kusema kwake "ingia katika waja wangu" ni ikrari ya mahali pa uja wake hiyo nafsi. Neno lake "na ingia katika pepo yangu" ni kubainisha kituo chake. Kuitegemeza pepo kwa dhamiri ya mwenye kusema (pepo yangu) ni utukuzo mahsusi wala halipatikani hilo katika maneno yake Mwenyezi Mungu (s.w.t) isipokuwa katika aya hii tu!.

Utafiti Wa Hadithi Katika Majmau kuhusu kusema kwake "na (kwa) Shufwa na Witiri, imesemwa kuwa Shufwa ni kuumba kwa sababu Mwenyezi Mungu amesema: "Na tukawaumba nyinyi wanaume na wanawake (jozi) " (78:8). na Witiri ni Mwenyezi Mungu Mtukufu. Hadithi hiyo imeyoka kwa Atiyal-Aufiy, Abu Saleh, Ibn Abbs na Mujahid, hiyo ni riwAya Na Abu Saad El-Khudriy naye amepokea kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) .

Imesemekana kuwa Shufwa na Witiri ni swala: kuna katika hiyo swala ya Shufwa na ya Witiri. Hiyo ni riwAya Na Ibn Haswin naye amepokea kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) .

Imesemwa kuwa Shufwa ni siku ya kuchinja na Witiri ni siku ya Arafa, kutoka kwa Ibn Abbas Akrama na Adh-Dhah-hak nayo ni riwAya Na Jabir kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) .

Imesemwa kuwa Shufwa ni siku ya Tarwiya (siku ya nane ya mwezi Dhul-Hijja) na Witiri ni siku ya Arafa (siku ya tisa ya Dhul-Hijja), hayo yamepokewa kutoka kwa Abu Jaffar na Abu Abdillah.

Riwaya hizo tatu zimepokewa kwa njia ya Ahli Sunnah. Inawezekana kukusanya kati ya hizo riwaya kwamba makusudio ni Shufwa na Witiri yoyote. Katika Tafsiri ya Qummi kuhusu "Masiku kumi" amesema ni ya mwezi wa Dhul-Hijja na "Shufwa na Witiri" amesema ni rakaa mbili na moja. Katika hadith Shufwa ni Hassan na Hussein na Witiri ni Amiirul Muuminiin(a.s) . Katika riwAya Na Abu Jarud, kutoka kwa Abu Jaffar kuhusu Aya Na tano anasema ni "Mwenye akili". Katika ulal kwa isnadi yake kwa Abana Al-Ahmar amesema: "Nilimuuliza Abu Abdillahi kuhusu kusema kwake Mwenyezi Mungu. Na Firaun mwenye vigingi, kwanini ameitwa hivyo?" Akasema : "Kwa sababu alikuwa anapomwadhibu mtu humtandaza juu ya ardhi na kumnyoosha mikono yake na miguu yake kisha humwamba kwa vigingi vinne. Mara nyengine humtandaza juu ya ubao na kumwamba miguu yake na mikono yake kwa vigingi vine, kisha humwacha mpaka afe, ndio Mwenyezi Mungu akamwita mwenye vigingi."

Katika Majmau kuhusu "Hakika Mola wako ni mwenye kuotea" imepokewa kutoka kwa Ali(a.s) kwamba yeye amesema: Hakika maana yake ni kwamba Mola wako ni muweza wa kuwalipa waasi malipo yao. Katika hiyo hiyo Majmau imepokewa kwa Swadiq amesema maana ya neno Mirswad ni korongo kwenye Swirat halipiti korongo hilo mja ambaye hakujiweka kimja. Kutoka kwa Ghawali naye kutoka kwa Aswadiq(a.s) katika hadithi ya kutafsiri kauli ya Mwenyezi Mungu (s.w.t): "Na dhun-nun (Yunusi) alipoondoka hali amechukiwa na akadhani ya kwamba hatutamdhikisha." (21:87) Amesema: Husikii kauli yake Mwenyezi Mungu. "Ama amjaribupo, akamdhikisha riziki yake, husema: Mola wangu amenitweza"? Katika Tafsiri ya Qummi katika riwAya Na Abu Jarud, kutoka kwa Abu Jaffar(a.s) kuhusu kauli yake "si hivyo ardhi itakapopondwa pondwa' Amesema hilo ni tetemeko.

Katika Durril-Manthur ametoa Ibn Murduwayh kutoka kwa Ali bin Abu Twalib amesema: "Amesema Mtume(s.a.w.w) he, mnajua nini tafsiri ya aya hii! "Si hivyo ardhi Takapondwa pondwa ikaleta siku hiyo Jahannam" akasema: Kitakapokuwa Kiyama Jahannam itaongozwa kwa hatamu elfu sabini kwa mikono ya Malaika elfu sabini itachomoza mchomozo mmoja, lau Mwenyezi Mungu sikuifunga ingeliunguza mbingu na ardhi. Hadith hii pia ni yenye kupokewa kutoka cha Amali Sheikh kwa isnadi yake kutoka kwa Arridha naye kutoka kwa baba yake naye kutoka kwa Ali(a.s) naye kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) .

Katika Uyun katika mlango wa yaliyokuja kutoka kwa Arridha katika Akhbaru Tawhid kwa isnadi yake kutoka kwa Ali bin Fadh-dhal naye kutoka kwa baba yake amesema: Nilimuuliza Arridha(a.s) kuhusu kusema kwake Mwenyezi Mungu "Na akaja Mola wako na Malaika (wamejipanga) safu kwa safu" Akasema: "Hakika Mwenyezi Mungu Mtukufu hasifiwi na kuja na kwenda isipokuwa maana ni, na ikaja amri ya Mola wako."

Katika Kafi kwa isnadi yake kutoka kwa Sadiyr Asswayrafiy amesema: "Nilimwambia Abu Abdillah(a.s) niwe mkombozi wako ewe mtoto wa Mtume wa Mwenyezi Mungu, Je, muumin anachukia anapotolewa roho yake akasema: Hapana, hakika yeye anapojiwa na Malaika wa Mauti kuchukua roho yake hufadhaika, Malaika wa Mauti huwambia: Ewe walii wa Mwenyezi Mungu usifadhaike, ninaapa kwa ambaye amempa utume Muhammad, hakika mimi nitakufanyia wema na upole kuliko mzazi, fungua macho uone.

Hapo atafanishiwa Mtume(s.a.w.w) , Amirul Muminiin, Fatima, Hassan and Hussein na Maimamu katika kizazi chao(a.s) ataambiwa hawa ni marafiki zako. Atafungua macho yake na atanadi mnadi kutoka mbele ya Mwenyezi Mungu atasema; Ewe nafsi iliyotua! Kwa Muhammad na Ahlul Bait wake rudi kwa Mola wako hali ya kuridhia wilaya na hali ya kuridhiwa thawabu, ingia katika waja wangu yaani Muhammad na Ahlul Bait wake na ingia katika pepo yangu. Litakua ni jambo la kupendeza kwake kutolewa roho yake na kumsikia mnadi. Amepokea Qummi riwaya kwa maana haya katika Tafsiri yake na Al-Barqi katika Mahasin.

15

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

SURA BALAD (MJI) (NA. 90)

INA AYA 20

Kwa jina la Allah, Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu

لَا أُقْسِمُ بِهَـٰذَا الْبَلَدِ ﴿١﴾

1. Naapa ka mji huu.

وَأَنتَ حِلٌّ بِهَـٰذَا الْبَلَدِ ﴿٢﴾

2. Na hali yakuwa wewe ni mkazi wa mji huu.

وَوَالِدٍ وَمَا وَلَدَ ﴿٣﴾

3. Na (kwa) mzazi na alichokizaa.

لَقَدْ خَلَقْنَا الْإِنسَانَ فِي كَبَدٍ ﴿٤﴾

4. Hakika tumemuumba mwanadamu, katika mateso.

أَيَحْسَبُ أَن لَّن يَقْدِرَ عَلَيْهِ أَحَدٌ ﴿٥﴾

5.Je anadhani kwamba hatawezekana na yeyote?

يَقُولُ أَهْلَكْتُ مَالًا لُّبَدًا ﴿٦﴾

6. Anasema: Nimepoteza mali mengi!

أَيَحْسَبُ أَن لَّمْ يَرَهُ أَحَدٌ ﴿٧﴾

7. Anadhani kwamba hakuonekana na yeyote?

أَلَمْ نَجْعَل لَّهُ عَيْنَيْنِ ﴿٨﴾

8. Ja hatukumpa macho mawili?

وَلِسَانًا وَشَفَتَيْنِ ﴿٩﴾

9. Na ulimi na midomo miwili?

وَهَدَيْنَاهُ النَّجْدَيْنِ ﴿١٠﴾

10. Tukamuonyesha njia mbili?

فَلَا اقْتَحَمَ الْعَقَبَةَ ﴿١١﴾

11. Basi mbona hakupita njia nzito?

وَمَا أَدْرَاكَ مَا الْعَقَبَةُ ﴿١٢﴾

12. Na umejuaje, ni ipi njia nzito?

فَكُّ رَقَبَةٍ ﴿١٣﴾

13. Ni kumwacha huru mtumwa.

أَوْ إِطْعَامٌ فِي يَوْمٍ ذِي مَسْغَبَةٍ ﴿١٤﴾

14. Au kumlisha siku ya njaa.

يَتِيمًا ذَا مَقْرَبَةٍ ﴿١٥﴾

15. Yatima aliye jamaa.

أَوْ مِسْكِينًا ذَا مَتْرَبَةٍ ﴿١٦﴾

16. Au maskini mwenye haja.

ثُمَّ كَانَ مِنَ الَّذِينَ آمَنُوا وَتَوَاصَوْا بِالصَّبْرِ وَتَوَاصَوْا بِالْمَرْحَمَةِ ﴿١٧﴾

17. Kisha akawa ni katika ambao wameamini, wakausiana kusubiri na wakausiana kuoneana huruma.

أُولَـٰئِكَ أَصْحَابُ الْمَيْمَنَةِ ﴿١٨﴾

18. Hao ndio watu wa heri.

وَالَّذِينَ كَفَرُوا بِآيَاتِنَا هُمْ أَصْحَابُ الْمَشْأَمَةِ ﴿١٩﴾

19. Na ambao wamezikanusha alama zetu, hao ndio wa shari.

عَلَيْهِمْ نَارٌ مُّؤْصَدَةٌ ﴿٢٠﴾

20. Juu yao ni moto uliokomewa.

UBAINIFU

Sura inataja kwamba umbo la mtu ni lenye kujengwa juu ya tabu na mashaka. Huwezi kukuta jambo lolote katika mambo ya maisha isipokuwa litakuwa limekutanishwa na matatizo na tabu, tangu roho inapoingia katika kiwiliwili chake mpaka anapokufa. Hana raha inayoepukana na tabu na mashaka, wala furaha isiyoandamana na misukusuko au huzuni isipokuwa katika nyumba ya akhera tu, mbele ya Mwenyezi Mungu. Basi mtu na avumulie uzito wa taklifa za Mwenyezi Mungu kwa kusubiri juu ya kufanya twaa na kuepukana na maasia. Na ajitahidi kueneza huruma juu ya wale waliopatwa na majaribio na balaa za dunia kama uyatima, ufakiri na maradhi ili awe ni katika watu wa heri. Kama si hivyo, basi akhera yake itakuwa kama dunia yake na atakuwa katika watu waovu juu yao ni moto uliofungiwa.

Mpangilio wa Aya Na Sura nii unafanana na wa Makka, kwa hiyo unatilia nguvu kuwa Sura imeshuka Makka. Baadhi wamedai kuwa hilo (la kushuka Makka) ni kwa Ijmai (mkusanyiko wa makubaliano ya wanazuoni). Imesemekana kwamba Sura hii imeshuka Madina na kwamba mpangilio wa aya za mwanzo hausaidii kusema kuwa imeshula Makka. Na pia imesemwa imeshuka Madina isipokuwa aya nne za mwanzo. Utakuja ufafanuzi katika utafiti wa hadith (Inshallah).

Aya Na 1

Wametaja kuwa makusudio ya mji huu ni Makka na hilo linatilia nguvu kuwa Sura imeshuka Makka.

Aya Na 2

Kuliweka jina dhahiri mahali pa dhamir ni kwa ajili ya kuadhimisha (mji huo) na kushughulika nao ambao ni mji mtukufu. Neno Hillun ni masdar kiarifa chenye kutumika kama jina kwa maana ya kukaa na kuthibiti mahali. Masdar hapa imekuja kwa maana ya (fail) Mtendaji maana yake kwa ujumal: ninaapa kwa mji huu na hali ya kuwa wewe ni mkazi wake. Na hilo uzindushi juu ya utukufu wa Makka kwa sababu ya kukaa kwake Mtume(s.a.w.w) na kuwa ni mahali pake pa kuzaliwa.

Inasemekana jumla hiyo imeingia kati tu; kati ya kiapo na chenye kuapiwa na makusudio yake ni kuhalalishwa. Anasema katika Kash-shaf "Na ameingilia kati ya kiapo na chenye kuapiwa kwa Kusema: "Na hali yakuwa wewe ni mwenye kuhalalishwa katika mji huu" yaani ni katika mateso kwamba mfano wako wewe juu ya ukubwa na utukufu wako unahalalishwa katika mji huu mtukufu, kama linavyohalalishwa windo nje ya haram. Wanaharamishwa kuua windo na kupukusa majani, lakini wanahalalisha kukutoa wewe na kukuua. Hadith hiyo imepokewa katuka kwa Sharhabil. Katika hilo ni uthabiti kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu na uwezekano na mateso aliyokuwa akiyapata kutoka kwa watu kustajaabu kutokana na hali yao ya uadui. Kisha akasema: "au alimfariji Mtume kwa kuapa kwa mji wake kwamba mtu haepukani na shida kisha akaingilia kati kwa kusema kuwa kiaga chake cha ushindi wa Makka kitatimu ili kumpa faraja, kwa hiyo akasema: na hali ya kuwa wewe ni mwenye kuhalalishiwa (yaliyoharamu) katika mji huu yaani na hali wewe utahalilishiwa hapo mbeleni utafanya ndani ya mji huu yale utakayoyataka maka kuua na kuteka".

Kwa hiyo inakuwa tafsiri ya neno Hillum ni kwa maana ya mwenye kuhalilishiwa kinyume chake ni mwenye kuharamishiwa; yaani tutakuhalalishia siku ya ushindi wa kuichukua Makka kwa muda utapigana na utamuua unayemtaka.

Aya Na 3

Ni kulazimisha namna ya kunasibika na kufungamana kati ya kiapo na chenye kuapiwa, kunapelekea kuwa makusudio ya mzazi na alichokizaa, kwamba kuna mnasaba iliowazi kati yake na mji wenye kuapiwa. Hilo linakubaliana na Ibrahim na mtoto wake Ismail(a.s) . Wao ndio chanzo cha kujengwa mji wa Makka na ndio wajenzi wa Al-Ka'aba tukufu: Mwenyezi Mungu anasema; "Na (kumbukeni) alipoinua Ibrahim kuta za nyumba (Al-Ka'aba) na Ismail (pia); (wakaomba wakasema) Ewe Mola wetu tutakabalie (amali yetu). Hakika wewe ndio mwenye kusikia, na mwenye kujua ." (2:127).

Kuleta herufi "Maa" yenye maana ya ambacho badala ya kuleta Man yenye maana ya ambaye, ni kwa ajili ya kulikuza jambo na kulistaajabia jambo lenyewe; kama alivyosema; "na Allah anajua zaidi alichokizaa ." (3:36).

Maana kwa ujumla ni naapa kwa mzazi mwenye jambo kubwa ambaye ni Ibrahim na alichokizaa ambacho ni mtoto wa ajabu wa jambo lake mwenye kubarikiwa; naye ni Ismail. Na wao wawili ndio waliojenga Al-Ka'aba. Ufahamisho wa aya tatu ni kuapa kwa mji mtukufu Makka kwa Mtume ambae amekaa katika mji huo na kwa Ibrahim na Ismail ambao wameujenga. Inasemekana kuwa makusudio ya mzazi ni Ibrahim na alichokizaa ni watoto wake wote Waarabu. Lakini ni umbali kwa Mwenyezi Mungu kuwa Mtume (SAWW) na Nabii Ibrahim(a.s) awakutanishe na watu kama akina Abu Lahab, Abu Jahal na wengineo katika viongozi wa ukafiri na awaapie wote. Na Ibrahim(a.s) alijiepusha na kila asiyemfuata katika watoto wake juu ya Tawhid wakati aliposema: "Na uniepushe mimi na wanangu na kuabudu masanamu. Mola wangu! Hakika (masanamu) hawa wamepoteza watu wengi. Basi aliyenifuata ni wangu mimi na aliyeniasi (unaweza kumsamehe) kwani wewe ni mwingi wa msamaha na Mwingi wa rehema ". (14:35-36).

Basi mwenye kufasiri alichokizaa kuwa ni watoto wa Ibrahim, ni juu yake kuwahusisha waislamu tu, katika kizazi chake, kama ilivyo katika dua ya Ibrahim. "Ewe Mola wetu! Utufanye tuwe wenyenyekevu kwako. Na miongoni mwa kizazi chetu (pia ufanye) umma mnyenyekevu kwako na utuonyeshe njia ya ibada yetu na utusameha ." (2:128).

Inasemekana kuwa makusudio ya mzazi na alichokizaa na Adma(a.s) na kizazi chake chote kwa kuzingatia kuwa kilichoapiwa viapo hivi ni kule kuumbwa mwanadamu katika mateso. Na Mwenyezi Mungu ameweka utaratibu wa kuzaliana ili kuhifadhi jinsi hii. Kwa hiyo ameapia katika aya hizi kwa kupitia utaratibu huu na matokeo yake - nayo ni mzazi na alichokizaa - kuwa mtu yuko katika tabu na mateso kulingana na namna ya kuumbwa kwake kuanzia anapopata uhai mpaka kufa.

Maelezo haya hayana ubaya, lakini kunabakia kubainisha mnasaba uliopo kati ya mji wa Makka na mzazi na kila mwenye kuzaliwa katika kuwakusanya kwenye viapo. Pia imesemwa kuwa makusudio ni Adam na watu wema katika kizazi chake. Maelezo haya ni kama yanamtakasa Mwenyezi Mungu kuapia kwa maadui wake wenye kupetuka mipaka na wafisadi katika makafiri.

Imesemwa kuwa makusudio ni kila mzazi na kila mwenye kuzaliwa na pia imesemwa kuwa ni mwenye kuzaa na asiyezaa kwa kuchukulia herufi Maa kuwa ni ya kukanusha. Vile vile imesemwa makusudio ya mzazi ni Mtume na alichokizaa ni umati wake kwa sababu yeye yuko katika daraja ya baba kwa umati wake; lakini hayo yote ni maelezo yaliyo mbali.

Aya Na 4

Jumla hiyo ni jawabu ya kiapo. Mateso katika umbile la binadamu na tabu katika mambo yake yote ya uhai ni jambo lisilofichika kwa kila mwenye roho. Mwanadamu hakusudii neema yoyote katika neema ya dunia ila huwa na matatizo katika dunia uzuri wako. Wala hawezi kupata kitu chochote katika dunia ila kitakuwa kimechanganyika na usumbufu pamoja na matatizo na mateso kuongozea misiba ya balaa za dunia na matukio ya ghafla.

Aya Na 5

Katika natija ya hoja iliyotangulia, uthibitisho wake ni kuwa; kwa kuwa mtu umbile lake limejengewa tabu, hapati kitu chochote katika anavyovitaka ila hupata asivyotaka, basi yeye ni mwenye kuzungukwa katika umbile lake, mwenye kushindwa katika matakwa yake na ni mwenye kushindwa nguvu katika analoliweza. Anayemshinda katika matakwa yake na kumshinda nguvu kufanya mambo anayoyaweza ni Mwenyezi Mungu (s.w.t) naye ni muweza katika kila upande, yeye anaweza kumfanyia mtu lolote analolitaka na kumchukua wakati anapomtaka.

Kwa hiyo mtu asifikirie kuwa hawezwi na yeyote, kwani fikra hiyo itampelekea kujifanya mkubwa mbele ya Mwenyezi Mungu na kutakabari katika kumwabudu. Au akitoa katika baadhi ya aliyoamrishwa, na kutoa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, basi anajiona ni mwingi wa mali, na husimbulia baada ya kufanya ria, kwa kusema: "Nimepoteza mali mengi!'.

Aya Na 6

Mpangilio wa aya na nyengine zinazofuatia mpaka mwisho wa Sura unaonyesha kuwa kulikuwa na baadhi ya wenye kudhihirisha Uislamu; akitoa baadhi ya mali yake anajifaharisha kuwa ametoa sana kwa kusema: nimepoteza mali mengi! Ndio ikashuka aya kumjibu, kwamba kufuzu kwa kheri za uhai hakutimu ila kwa kupita njia nzito ya kutoa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na kuingia katika kundi la wale ambao wameamini wakausiana kusubiri na kuoneana huruma. Yatatilia nguvu hilo yale yatakayokuja katika utafiti wa hadith (Inshallah).

Aya Na 7

Ni kukanusha hilo neno la mtu kwa njia ya fumbo. Maana yanayopatikana ni kwamba vile mtu anavyolazimika kusema kuwa amepoteza mali mengi, akafikiria kuwa mimi nimeghafilika na sijui, yale aliyotoa? Basi amekosea katika hilo na Mwenyezi Mungu ni mwenye kuona aliyoyatoa, lakini kiasi hicho hakitoshi kumfanya awe ni mwenye kufuzu kwa maisha ya kheri bali hana budi kuvumilia zaidi ya hayo katika mashaka ya kimja, apite njia nzito na awe pamoja na waumini katika yote waliyonayo.

Aya Na 8-10

Yaani tumemtayarisha katika mwili wake kwa yale anayoonea ili apate elimu ya vinavyoonwa kwa kadri ya upana wa elimu hiyo Na je, hatukumpa ulimi na midomo miwili vitakavyomsaidia kutamka yaliyo katika dhamir yake miongoni mwa elimu na aongoke kwa hilo mwenzake kwa kujua mambo yaliyofichika na macho? Na tumemfahamisha njia ya heri na ya shari kwa ilhamu itokayo kwetu, hivyo yeye anujua heri na anapambanua shari. Na aya hii ya tisa iko katika maana ya Aya Na nane ya Sura Shams Na. (91).

Aya hizo tatu ni hoja juu ya kauli yake Mwenyezi Mungu "Anadhani kwamba hakuonekana na yeyote" Yaani Yeye Mwenyezi Mungu anaona matendo ya waja wake na anajua yaliyo katika dhamiri yao kwa njia ya matendo na anapambanua kheri na shari na mema na mabaya. Kwa ujumla ni kuwa hakika Mwenyezi Mungu S.W.T. ndiye ambaye anamfahamisha yenye kuonekana kupitia macho yake mawili na namna anavyoweza kupiga picha kumfahamisha jambo asilolijua, na ni Yeye ambaye anamfahamisha yaliyo katika dhamiri kupitia kusema Je, inaingilika akilini kuwa Mwenyezi Mungu amfunulie mtu mambo ambayo Yeye mwenyewe hayajui?

Na yeye ndiye ambaye anampambanulia mtu heri na shari kwa ilhamu, Je, inawezekana kuwa Yeye hawezi kujua wala kupambanua? Yeye Mwenyezi Mungu anaona aliyoyafanya mtu na najua anayonuia kuyafanya na kuyapambanua kuwa ni kheri au shari.

Aya Na 11

Maana ya neno Iqtahama ni kuingia kwa haraka na kwa shida kujigagamiza na neno Aqaba ni njia nzito yenye vikwazo vya kupanda majabali. Kujigagamiza kuparamia njia nzito ni ishara ya kutoa (mali) ambako kunakuwa vigumu kwa mtoaji, kama itakavyoelezwa. Inasemekana kuwa jumla yote ni dua dhidi ya mtu anayesema nimepoteza mali mengi lakini si hivyo.

Aya Na 12

Ni kulikuza jambo lenyewe, kama ilivyopita katika mtazamo wake.

Aya Na 13

Yaani njia nzito ni kumwachia hutu mtumwa. Makusudio ya njia nzito ndiyo huko kuacha huru ambako ni kitendo chenyewe, na kujigagamiza kunaamanisha kukitenda. Kwa hiyo basi inaharabika kauli ya baadhi ya wanaosema kwa kumwachia huru mtumwa ndiko kupita njia nzito lakini sio njia nzito yenyewe, kwamba kuna mudhafu (neno lenye kutegemezwa) uliondolewa kukisia kwake ni: Na umejuaje ni nini kupita njia nzito, kupita njia nzito ni kumwacha huru mtumwa. Hayo yaliyotajwa katika kubainisha njia nzito ambayo ni kumwacha huru mtumwa au kulisha siku ya njaa, katika kueneza huruma yamehusishwa kutajwa kutokana na umuhimu wake. Na kumetangulizwa kuacha huru mtumwa kwa sababu dini imeshughulikia sana suala hilo.

Aya Na 14-16

Neno Matraba linatoka katika neno Turab (mchanga) na maana yake ni kushikwa na mchanga (vumbi) kutokana na shida ya ufakiri. Maana yake kwa ujumla ni, au kumlisha siku ya njaa. Yatima mwenye udugu au maskini mwenye ufakiri sana.

Aya Na 17

Kuusiana kusubiri ni kuusiana kusubiri juu ya kumtii Mwenyezi Mungu na kuusiana kuoneana huruma ni kuusiana kuwaonea huruma wenye ufakiri na umaskini. Jumla nzima inaungana na jumla ya kupita njia nzito.

Aya Na 18

Neno Maymana limekuja kwa maana ya heri kinyume chake na Mash'ama uovu. Kuleta ishara ya neno (hao) kwa unavyofahamisha mpangilio wa maneno uliotangulia, ni kuwa: Wale ambao wamepita njia nzito na wakawa katika wale ambao wameamini, na wakausiana kusubiri na wakausiana kuoneana huruma ni watu wa heri. Walilolifanya katika imani na amali yao ni njema wataliona ni jambo lenye kubarikiwa, zuri na lenye kurudhiwa. Imesemekana kuwa makusudio ya Maymana ni Yamin upande wa kuume na watu wa upande ya kuume ndio ambao watapewa vitabu vyao kwa upande wao wa kuume, lakini hilo halifuatani na neno Mash'ama (uovu).

Aya Na 19

Alama zetu ni alama za mbinguni na za kinafsi nazo zinafahamisha juu ya umoja katika uungu na kuzikanusha ndio kumkanusha Mwenyezi Mungu, vile vile ni kukanusha Qur'an tukufu na aya zake na yote yaliyoshuka na kufikishwa kwa njia ya ujumbe.

Utafiti Wa Hadith Katika Majmau Aya Na 2 imesemwa kuwa maana yake ni na hali ya kuwa ni halali kwako kumuua unayemwona anastahiki kuuliwa katika makafiri. Hilo ni wakati alipoamrishwa kupigana siku wa kuichukua Makka; Mwenyezi Mungu akamhalalishia hata akaweza kupigana na kuua. AmesemaMtume(s.a.w.w) haikuhalalishiwa kwa yoyote kabla yangu wala haitakuwa halali baada yangu kwa yoyote, na mimi sikuhalalishiwa isipokuwa saa moja katika mchana. Hadith hiyo imepokewa kutoka kwa Ibn Abbas, Mujahid na Ata.

Imepokewa kutoka kwa Abu Abdillah amesema: "Maquraish walikuwa wakiuadhimisha mji na kumuhalalisha Muhammad(s.a.w.w) katika mji huo, akasema: Naapa kwa mji na halo ya kuwa wewe ni mwenye kuhalalishwa katika mji huu anakusudia kusema kuwa wao wamehalalisha kukuudhi kukuadhibisha na kukutukana. Na wao walikuwa hawamwadhibu hata mtu aliyeua baba wa mmoja wao. Na walikuwa wakivaa majani wa mti kumpa amani, lakini wakahalalisha kwa Mtume(s.a.w.w) yale ambayo hawakumuhalalishia mwengine. Katika hiyo Majmau kuhusu Aya Na tatu imesemwa kuwa ni Adam an alichokizaa katika Mitume, mawalii na wafuasi wao. Hadith hiyo imepokewa kutoka kwa Abu Abdillahi.

Maana yaliyotangulia pia yamepokewa katika njia ya Ahli Sunna. Pia amepokea Qummi katika Tafsiri yake. Katika Tafsiri ya Qummi kuhusu Aya Na sita amesema maana ya neno Lubada ni mkusanyiko. Na katika Majmau kuhusu aya hiyo hiyo imesemwa huyo aliyesema hivyo ni Harith bin Naufal bin Abdul Manaf, wakati alipofanya dhambi fulani, akataka fatuwa kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) akamwamrisha kutoa kafara, akasema: Tangu nilipoingia dini ya Muhammad mali yangu imeisha katika makafara na kulisha. Hadith hiyo imepokewa na Muqatil. Katika hiyo hiyo Majmau, imesemwa kuwa, aliulizwa Amirul-Miminin Ali(a.s) kwamba watu wanasema kuhusu neno ya Mwenyezi Mungu "Na tukamuongoza njia mbili" kwamba hizo njia mbili ni matiti? Akasema hapana njia mbili hizo ni heri na shari.

Katika Kafi kwa isnadi yake kutoka kwa Hamza bin Muhammad naye kutoka kwa Abu Abdillahi(a.s) amesema nilimuuliza kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu tukamwongoza njia mbili akasema ni njia ya heri na shari. Imepokewa riwaya hii katika Durril Manthur kwa njia ya Ali(a.s) Anas, Abu Amama na wengineo kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) .

Katika Kafi kutoka kwa Jaffar bin Khilad amesema: Alikuwa Abul-Hassan Ridha(a.s) anapokula, huletewa chano karibu na chakula chake, anaangalia chakula kizuri katika vyakula alivyoletewa na kukiweka katika chano, kisha anaamrisha kipewe masikini kisha anasoma ayah ii: 'Haya naapite hiyo njia nzito 'kisha anasema: "Mungu anajua kuwa sio kila mtu anaweza kuacha huru mtumwa kwa hiyo amewafanyia njia nyengine ya kwenda peponi".

Katika Majmau imepokewa hadith Marfuu kutoka kwa Baraa bin Azib amesema: "Alikuja bedui kwa Mtume(s.a.w.w) akasema: "Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu nijulishe amali itakayonitia peponi" Mtume akasema: "Ukiwa umefupisha hotuba basi umerefusha masuala; muache huru mtu, na uifungulie shingo." Akasema yule bedui "kwani yote hayo sio kitu kimoja?" Akasema Mtume: La! Kuacha huruni kumuacha aende zake na kuifungulia shingo ni kumsaidia katika thamani yake. Kama si hivyo, basi mlishe mwenye njaa, na mnyweshe mwenye kiu na uamrishe mema na ukataze maovu na uzuiye ulimi isipokuwa katika jambo la kheri tu. Katika Tafsiri ya Qummi kuhusu kauli yale Mwenyezi Mungu : "Au maskini mwenye shida" ni yule asiyeweza kujikinga na mchanga (vumbi).


10

11

12

13

14

15

16