TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN12%

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: tafsiri ya Qurani

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN
  • Anza
  • Iliyopita
  • 29 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 42564 / Pakua: 4763
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

Mwandishi:
Swahili

1

2

3

4

5

6

7

8

26

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

SURA MAUN ( MANUFAA) (NA. 107)

INA AYA 7

Kwa jina la Allah, Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu.

أَرَأَيْتَ الَّذِي يُكَذِّبُ بِالدِّينِ ﴿١﴾

1. Je, umemwona (unamjua) yule ambaye anakadhibisha dini.

فَذَٰلِكَ الَّذِي يَدُعُّ الْيَتِيمَ ﴿٢﴾

2. Huyo ni ambaye humsukuma yatima.

وَلَا يَحُضُّ عَلَىٰ طَعَامِ الْمِسْكِينِ ﴿٣﴾

3. Wala hahimizi kulisha maskini.

فَوَيْلٌ لِّلْمُصَلِّينَ ﴿٤﴾

4. Basi ole wao wenye kuswali.

الَّذِينَ هُمْ عَن صَلَاتِهِمْ سَاهُونَ ﴿٥﴾

5. Ambao wanapuuza swala zao.

الَّذِينَ هُمْ يُرَاءُونَ ﴿٦﴾

6. Ambao wao hujionyesha.

وَيَمْنَعُونَ الْمَاعُونَ ﴿٧﴾

7. Na wakazuilia (watu) manufaa.

UBAINIFU

Sura hii inaelezea kiaga anachopewa yule mwenye kusifika na sifa za kiunafiki kama vile kuipuuza swala kufanya ria na kuzuwiya misaada. Sura hii inawezekana kuwa imeshuka Makka au Madina. Na inasemekana nusu yake imeshuka Makka na nusu yake imeshuka Madina.

Aya Na 1

Neno Araayta lina maana ya kuona kwa macho au kwa kiakili. Makusudio ya dini hapa ni malipo siku ya malipo na kukadhibisha malipo maana yake ni kukadhibisha kufufuliwa. Imesemwa kuwa makusudio ya dini ni kwa maana ya mila.

Aya Na 2

Neno yaduu lina maana ya kusukuma na kufukuza kwa nguvu na jeuri. Hapa ina maana ya yule anayemsukuma na kumfukuza yatima kwa nguvu na jeuri bila ya kujali matokeo ya mabaya hayo ayafanyao. Lau hakukataa siku ya malipo angeliogopa siku hiyo. Na lau aliigopa siku hiyo angelimhurumia yatima.

Aya Na 3

Yaani ni yule ambaye hapendelei watu wawalishe maskini. Imekuja ibara ya kuhimiza, kwa vile kuhimiza kunaenea zaidi kuliko kufanya tu! Inasemekana kuna neno Twaam lina maana ya chakula kama lilivyo, kwa kufahamisha kwamba yule mwenye kupewa ni kama vile anamiliki kile anachopewa, kama alivyosema Mwenyezi Mungu: "Na katika mali zao ilikuwako haki ya kupewa maskini aombae na ajizuiae kuomba ." (51:19).

Na inasemwa Twaam katika aya ina maana ya kulisha.

Aya Na 4-5

Wanaopuuza swala ni wale wasiopatiliza swala wala hawajali kukosa swala zote au baadhi, au kuchelewa na wakati wake bora (wa mwanzo). Aya hii inawaunganisha wale wanaopuuza swala na wale wanaokadhibisha malipo, kufahamisha kuwa wao hawaachani na unafiki wao kwa vitendo huku wakijidhihirisha kwa imani.

Aya Na 6

Wanaojionyesha ni wale wanaofanya ibada kwa kujionyesha kwa watu, kwa hiyo wanafanya ibada kwa ajili ya watu na sio kwa ajili ya Mwenyezi Mungu (s.w.t).

Aya Na 7

Neno Maun lina maana ya msaada wa aina yoyote inayoondoa dhiki au tatizo la aina yoyote kama vile kumkopesha mtu pesa, au kumfanyis wema au kumuazima chombo cha nyumbani.

Utafiti Wa Hadithi. Katika Tafsiri ya Qummi kuhusu Aya Na 1 anasema ilishuka kwa Abu Jahl na makafiri wa Kiquraish, na kuhusu Aya Na 5 wanakusudiwa wale wanaocha swala na wala sio kusahau, kwa sababu kila mtu anaweza kusahau katika swala. Amesema Abu Abdiallah(a.s) : "Ni kuichelewesha swala na wakati wake bila ya udhuru ". Katika Khiswal katika hadith ya mia nne imepokewa kutoka kwa Ali(a.s) amesema: "Hakuna amali inayopendeza zaidi kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) kuliko swala, kwa hivyo kisiwashughulishe chochote na swala kwani Mwenyezi Mungu amewashutumu watu kwa kusema: "Wale ambao swala zao wanazipuuza" yaani wanaopuuza wakati wake.

Katika Kafi kwa isnadi ya Muhammad bin Alfadhil, anasema: "Nilimuuliza mja mwema(a.s) kuhusu Aya Na 5 akasema ni kupuuza, na ziko riwaya nyingi katika madhumuni haya haya. Katika Durril Manthur ametoa Ibn Jariyr, Ibn Hatim na Bayhaqai kutoka ka Ali bin Abu Twalib kuhusu neno, wale amabo wanafanya ria ni kufanya ria katika swala. Katika hiyo hiyo Durril Manthur ametoa Abu Naim, Dilami na Ibn Asakir kutoka kwa Abu Hurayra naye kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) kuhusu Aya Na 7 ni vitu wanavyosaidiana watu kama shoka, ndoo, sufuria nk.

Katika Kafi kwa Abu Baswir naye kutoka kwa Abu Abdiallah(a.s) amesema: "Na neno lake Mwenyezi Mungu (s.w.t): Na wakazuilia (watu) na manufaa" ni kuzuilia kukopeshana na kufanyiana mema na kuazimana vyombo vya nyumbani na pia kuzuilia zaka. Kilifasiri neno Maun kwa maana ya zaka pia imepokewa kwa njia ya Ahli Sunnah, kutoka kwa Ali(a.s) kama ilivyo katika Durril Manthur kuwa tamko Maun ni zaka ya wajibu. Yaani wanajionyesha katika swala zao na huku wanazuia zaka zao.

Katika hiyo Durril Manthur ametoa Ibn Qani kutoka kwa Ali Ibn Abu Twalib(a.s) amesema: "Nimemsikia Mtume(s.a.w.w) akisema: "Muislamu ni ndugu ya muislamu mwengine anapokutana naye humuamkia kwa salam na humpatia kila chenye heri na hamzuilii Maun nikasema, "Ewe Mtume wa Mungu nini maun" akasema Mtume "ni jiwe, chuma, maji nk." Amefafanua Mtume(s.a.w.w) katika hadith nyengine kuwa chuma ni sufuria za shaba na shoka ya chuma. Na mawe ni nyungu za mawe.

SURA KAWTHAR (HERI NYINGI) (NA. 108)

INA AYA 3

Kwa jina la Allah, Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu.

إِنَّا أَعْطَيْنَاكَ الْكَوْثَرَ ﴿١﴾

1. Hakika sisi tumekupa kheri nyingi.

فَصَلِّ لِرَبِّكَ وَانْحَرْ ﴿٢﴾

2. Basi mswalie Mola wako na uchinje mnyama.

إِنَّ شَانِئَكَ هُوَ الْأَبْتَرُ ﴿٣﴾

3. Hakika mwenye kukubughudhi wewe yeye ndiye mwenye kuishiwa.

UBAINIFU

Sura hii inaeleza kuneemeshwa kwa Mtume kwa kupewa neema nyingi. Na Sura hii ndiyo Sura fupi katika Qur'an. Mapokezi yamekithalifiana kuwa Sura imeshuka Makka au Madina, lakini inaonyesha kwamba imeshuka Makka. Wengine wamesema imeshuka mara mbili.

Aya Na 1

Imesemwa katika Majmau kwamba neno Kawthar liko katika kipimo cha Faw-al yenye maana ya wingi, kwa hiyo Kawthar ni heri nyingi. Wamehitilafiana kiajabu sana katika tafsiri ya neno Kawthar. Imesemwa kuwa ni heri nyingi, wengine wamesema ni mto peponi, wengine wamesema ni birika ya Mtume katika pepo au katika siku ya kukusanywa watu. Pia imesemwa ni watoto wake, masahaba wake, wafuasi wake mpaka siku ya Kiyama, au wanavyuoni wa umma wake.

Na imesemwa ni Uislamu, Tawhid, elimu na hekima, ubora wake, maqamu yenye kusifiwa, nuru ya moyo wake na zaidi ya hayo yamesemwa mpaka kufikia kauli ishirini na saita (26). Baadhi ya riwaya zimetegemea kwenye kauli mbili za mwanzo (heri nyingi na to katika pepo). Lakini kauli nyingine pia haziwezi kuachwa. Kwa hali yoyote iwayo. Neno abtar kwa dhahiri lina maana ya mwenye kukatikiwa na kizazi. Kwa hiyo makusudio hapa ya kawthar ni kizazi kingi, au heri nyingi kwa maana ya kuwa hicho kizazi ni heri nyingi lau kama si hivyo, basi ingelikuwa jumla ya aya ya haina faida yoyote.

Hadith zimeeleza kwamba Sura hii ilishuka, kutokana na mtu mmoja aliyemtusi Mtume(s.a.w.w) , kwa kuwa eti amekatikiwa na kizazi chake kutokana na kufa kwa watoto wake wa kiume (Kassim na Abdulla). Kwa hivyo Mwenyezi Mungu akamrudishia majibu kwa kusema huyo mwenye kukubughudhi wewe ndiye abtar aliyekatikiwa na heri zote: Neno "hakika sisi tumekupa wewe", limekuja kwa wingi kwa kuadhimisha tu. Jumla yote hiyo ya maneno inafahamisha kuwa kizazi cha Fatima(a.s) ni kizazi cha Mtume(s.a.w.w) . Mwenyezi Mungu amekifanya kingi sana kizazi hicho kuliko kizazi kingine chochote pamoja na misiba iliyowashukia na kuuliwa kwa makundi katika mauaji ya kuchukiza na ya kinyama.

Aya Na 2

Kushukuru neema ni jambo linalotakikana. Hapa Mwenyezi Mungu anamwamrisha Mtume wake kuwa tumekupa heri nyingi, basi wewe shukuru neema hiyo kwa kusali na kuchinja mnyama. Imesemekana maana ya ayah ii ni kuswali swala ya Idd na kuchinja mnyama. Pia imesemwa maana ya neno wanhar ni kunyanyua mikono miwili katika swala wakati wa kusoma takbira.

Aya Na 3

Imesemwa maana ya neno abtar hapo ni kuepukana na heri au kuepukana na watu wake. Yatakuja maelezo katika utafiti wa hadith. Neon shani ni yule mwenye kubughudhi naye ni Asi bin Wail.

Utafiti Wa Hadith Katika Durril Manthur ametoa Bukhari, Ibn Jariyr na Hakim kwa njia ya Abu Bashar kutoka kwa Said bin Jubayr naye amepokea kutoka kwa Ibn Abbas kwamba yeye amesema: "Kawthar ni heri alizopewa Mtume". Abu Bashar akasema kumwambia Said bin Jubayr: "Hakika watu wanadai kuwa kawthar ni mto katika pepo". Akajibu "mto katika pepo ni katika heri ya Mwenyezi Mungu aliyompa Mtume wake." Katika hiyo hiyo Durril Manthur ametoa Ibn Abu Hatim, Hakim, Ibn Murdawayh na Bayhaqi katika hadith zake kutoka kwa Ali bin Abu Twalib(a.s) amesema:

"Iliposhuka Sura ya Kawthar, Mtume(s.a.w.w) alisema kumwambia Jibril: Ni uchinjo gani huu alioniamrisha Mungu? Jibril akasema: "Sio uchinjo isipokuwa anakuamrisha kunyanyua mikono yako katika swala wakati wa kuhirimia, kurukui na wakati wa kunyanyua kichwa baada ya rukui, kwani hiyo ndiyo swala yetu na swala ya Malaika walioko katika mbigu saba, na kwamba kila kitu kina kipambo chake na kipambo cha swala ni kunyanyua mikono miwili kila unaposoma takbira. Katika Majmau imepokewa kutoka kwa Muqatil naye kutoka kwa Asbagh bin Nabata, kisha akasema wamepokea Thaalabi na Wahidi katika tafsiri zao, kwamba imepokewa kutoka kwa kizazi chote kitakatifu cha Mtume kitabu hicho hicho ametoa Ibn Jariyr kutoka kwa Abu Jaffar kwamba maana ya msalie Mola wako, ni swala na maana ya wanhar ni unyanyue mikono miwili unapotoa takbira mwanzo wa swala.

Tena katika hiyo hiyo Majmau ametoa Ibn Murdawayh kutoka kwa Ibn Abbas kuhusu Aya Na 2 amesema: Hakika Mwenyezi Mungu alimpelekea Wahyi Mtume wake kwa kusema : "Nyanyua mikono yako muelekeo wa sehemu ya juu ya kifua hiyo ndiyo nahr". Katika hiyo hiyo Majmau imepokewa kutoka kwa Umar bin Yazid amesema: "Nimesikia Abu Abdillahi akisema? Maana ya wanhar ni kunyanyua mikono yako pambizoni mwa uso wako. Na pia imepokewa kutoka kwa Abdulla bin Sinan mfano wa hadith iliyo karibu na maana hayo kutoka kwa Jamil. Katika Durril Manthur ametoa Ibn Saad na Ibn Asakir katika njia ya Kalabi kutoka kwa Abu Saleh naye kutoka kwa Ibn Abbas amesema: "Alikuwa mtoto mkubwa wa Mtume(s.a.w.w) ni Kassim kisha Zaynab, Abdulla, Ummu Kulthum, Fatima na Ruqayya. Akafa Kassim, naye ndiye maiti wa kwanza katika kizazi chake, kisha akafa Abdullah. Ndipo akasema Asi bin Wail Assahmi :"Kizazi chake kimekwisha katika, kwa hiyo yeye ni abtar. Basi akateremsha Mwenyezi Mungu; Hakika mwenye kukubughudhi wewe yeye ndiye abtar (mwenye kuepukana na heri zote)".

Katika hiyo hiyo Durril Manthur ametoa Ibn Abu Hatim kutoka kwa Assadi amesema. "Walikuwa Maquraish wakisema: mtu anapofiwa na mtoto wa kiume, ni abtar basi alipokufa mtoto wa Mtume(s.a.w.w) , Asi bin Wail akasema Mtume ni abtar. Tena katika hiyo hiyo Durril Manthur ametoa Zubeir bin Bakar na Ibn Muhhamd kutoka kwa baba yake amesema: "Alikufa Kassim mtoto wa Mtume wa Mwenyezi Mungu huko Makka, Mtume alipokuwa akitoka kuzika akapita kwa Asi Bin Wail akiwa na mtoto wake Amru, akasema alipomwona Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) . "Mimi ninamchukia sana." Akasema Asi: "Achana naye kwani yeye ameshakua Abtar". Mwenyezi Mungu ndio akateremsha Sura hiyo.

Ibn Abi Hatim amepokea kutoka kwa Assadi amesema: "Mtu anapofiliwa na mtoto wa kiume, Quraish walikuwa wakisema: "Fulani ameshakuwa abtar." Basi alipokufa mtoto wa Mtume(s.a.w.w) Asi bin Wail alisema : "Amekuwa abtar". Wamehitalifiana juu ya aliyembughudhi Mtume(s.a.w.w) ; wengine wanasema ni Walid bin Al-Mughira, wengine wanasema ni Abu Jahl, wengine ni Uqbah bin Abu Muiit na wengine wanasema ni Ka'ab bin Ahsraf. Lakini kauli yenye tutegemewa ni ile inayomtaja Asi nin Wail.

Hayo yanatiliwa nguvu na yale yaliyo katika Ihtijaj ya Tabrasiy kutoka kwa Hasan bin ali(a.s) katika hadith anayomwambia Amru bin Al-Asi: "Hakika wewe umezaliwa kutokana na kitanda kilichoshirikianwa, wakabishana juu yako wanaume wa Kiquraish ambao ni Abu Sufyan bin Harb, Walid bin Al-Mughira, Uthman bin Al-Harith, Annadhri bin Al-Harith bin Kaldah na Asi bin Wail. Kila mmoja anadai kuwa wewe ni mtoto wake, ndipo akashinda yule mchafu wao zaidi.

Katik Tafsiri ya Qummi amesema Kawthar ni mto katika pepo aliopewa Mtume badala ya mtoto wake Ibrahim (aliyekufa). Kwa vyovyote iwavyo kutafsiri Kawthar kuwa ni mto katika pepo hakupingani na tafsiri ya heri nyingi, kama yalivyokwisha tangulia maelezo ya Ibnu Jubeir.

SURA KAFIRUN (MAKAFIRI)(NA. 109)

INA AYA 6

Kwa jina la Allah, Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu.

قُلْ يَا أَيُّهَا الْكَافِرُونَ ﴿١﴾

1. Sema: Enyi makafiri

لَا أَعْبُدُ مَا تَعْبُدُونَ ﴿٢﴾

2. Mimi siabudu mnachokiabudu.

وَلَا أَنتُمْ عَابِدُونَ مَا أَعْبُدُ ﴿٣﴾

3. Wala nyinyi hamkiabudu ninachokiabudu mimi.

وَلَا أَنَا عَابِدٌ مَّا عَبَدتُّمْ ﴿٤﴾

4. Wala mimi sitaabudu mnachokiabudu nyinyi.

وَلَا أَنتُمْ عَابِدُونَ مَا أَعْبُدُ ﴿٥﴾

5. Wala nyinyi hamtakiabudu ninachokiabudu mimi.

لَكُمْ دِينُكُمْ وَلِيَ دِينِ ﴿٦﴾

6. Nyinyi mna dini yenu, na mimi nina dini yangu.

UBAINIFU

Katika Sura hii Mwenyezi Mungu anamwamrisha Mtume kudhihirisha kujitenga kwake na dini yao. Dini yake haingilii dini yao wala dini yao haingilii dini yake. Yeye katu haabudu lile wanaloliabudu wala wao katu hawaabudu anachokiabudu. Kwa hivyo wakate tamaa na namna yoyote ile ya kudanganya. Wamekhitalifiana wafasiri kuwa Sura imeshuka Makka au Madina, lakini mpangilio wa maneno unaonyesha kuwa imeshuka Makka.

Aya Na 1

Kwa dhahiri ni watu maalum sio makafiri wote. Hilo linafahamisha kuamrishwa kwake Mtume(s.a.w.w) kuwambia makafiri kutakasika kwake na dini yao na kujizuilia kwao na dini yake.

Aya Na 2

Makusudio ya kile mnachokiabudu, ni masanamu waliyokuwa wakiyaabudu. Herufi laa hapa ni ya kukanusha kwa muda ujao (mustaqbal) na herufi maa ni ya muda wa sasa hivi. Yaani siabudu milele kile mnacho kiabudu hivi sasa katika msanamu.

Aya Na 3

Pia ni ya kukanusha kwa muda ujao yaani kumpa habari Mtume(s.a.w.w) kwamba makafiri hawataabudu kile anachokiabudu Mtume(s.a.w.w) kama walivyokuwa wakidai. Kwa kuunganisha amri iliyo katika mwanzo wa maneno, aya hizi mbili zinaonyesha ya kwamba Mwenyezi Mungu ameniamrisha kudumu kumuabudu Yeye. Halikadhalika ameniamrisha kuwaeleza kama nyingi hamtamuabudu katu. Kwa hivyo hapana ushirikiano wa dini kati yangu na nyinyi. Ayah ii ina maana sawa na ile aya isemayo: "Bila shaka kauli (ya adhabu) imehakikika juu ya wengi katika wao, kwa hivyo hawaamini ." 36:7.

Halikadhalika inakubaliana na aya isemayo: "Hakika wale waliokufuru (Kwa ukaidi na inadi) ni sawa kwao ukiwaonya au usiwaonye, hawataamini ". (2:6). Ilikuwa sawa ni kusema: "Wala nyinyi siwenye kuabudu ninayemuabudu". Lakini imesemwa "Ninachokiabudu". Kwa jili ya kufuata mpangilio ulioanzia: "Siabudu mnachokiabudu".

Aya Na 4-5

Ni kutilia mkazo yale yaliyotangulia, kama ilivyo katika Sura ya (102: 3-4); aliposema: "Komeni punde kidogo tu! Mtajua kisha komeni punde kidogo tu! Mtajua ". Na katika Sura (74: 19-29):

"Amelaaniwa, namna gani alivyokadiria (kutia ila Qur'an) kasha amelaaniwa, namna gani aliyokadiria (kutia ila Qur'an) ."

Imesemekana kuwa ma katika neno Abadtum sio mausul yenye maana kurejea kwenye jina, bali ni ya masdariya ya kufanya jina la kitendo yenye maana wa Wala mimi siabudu ibada yenu wala nyinyi siwenye kuabudu ibada yangu. Kwa maana kuwa siwashirikishi wala hamnishirikishi si katika mwenye kuabudiwa wala ibada. Ninayemuabudu mimi ni Mungu na mnayeabudu nyinyi ni sanamu. Na ibada yangu ni ile aliyoiweka Mwenyezi Mungu, lakini ibada yenu ni ile mliyoizusha wenyewe kwa ujinga na uzushi. Yatakuja maelezo katika utafiti wa hadith (Inshallah).

Aya Na 6

Nikuzidi kutilia mkazo kukanusha kushirikiana. Na herufi lam ni ya kuhusisha, yaani dini yenu ya kuabudu masanamu inahusika na nyinyi na hii dini yangu inahusikana na mimi tu! Inasemekana kwamba dini hapa ina maana ya malipo yaani; Mna malipo yenu na nina malipo yangu. Na inasemekana pia kuna kitu kilichoondoshwa yaani, mna malipo ya dini yenu nami nina malipo ya dini yangu. Lakini njia mbili zote hizo, ziko mbali na ufahamu.

Utafiti Wa Hadithi Katika Durril Manthur ametoa Ibn Jariyr, na Ibn Abu Hatim na Ibn Anbari, kutoka kwa Said Ibn maynai Huru (aliyekuwa mtumwa) wa Abul Bakhtari amesema: "Walid bin El-Mughira, Asi bin Wail, sa-wad bin El-Mutwalib na Umayya bin Khalaf, walikutana na Mtume wakamwambia "Ewe Muhammad ! njoo tuabudu kile unachokiabudu na wewe uabudu kile tunachokiabudu na tushirikiane sisi na wewe katika mambo yetu yote, ikiwa haya yetu ni sahihi zaidi kuliko yako, basi utakuwa umepata cha kupata, na kama ikiwa yale unayoyaabudu wewe ni sahihi zaidi kuliko yetu, basi tutakuwa tumechukua la kuchukua". Mwenyezi Mungu ndio akateremsha Sura hiyo yote.

Katika Tafsiri ya Qummi amepokea kutoka kwa baba yake naye amepokea kutoka kwa Ibn Abu Umeir amesema: "Abu Shakir alimuuliza Abu Jaffar El-Ahwal kuhusu Sura ya Kafirun "Jee Mwenye hekima anasema maneno kama haya na kuyarudia mumo kwa mumo? "Abu Jaffar El-Ahwal hakuwa na jibu. Basi akaenda Madina kumuuliza Abu Abdillahi(a.s) akasema: :Sababu ya kushuka Sura hiyo na kukariri maneno hayo, ni kwamba Maquraish walimwambia Mtume(s.a.w.w) : 'abudu miungu wetu mwaka mmoja na tuabudu Mungu wako mwaka mmoja na tena abudu miungu wetu mwaka moja na tuabudu Mungu wako mwaka mmoja".

Mwenyezi Mungu akawajibu kama vile walivyo sema. Akasema juu ya yale waliyoyasema kuwa aabudu miungu yao mwaka alisema: Sema enyi makafiri. Mimi siabudu mwachokiabudu. Na katika yale waliyoyasema kuwa watamwabudu Mungu wake mwaka alisema: Wala nyinyi hamkiabudu ninachokiabudu mimi. Na juu ya yale waliyosema aabudu miungu yao mwaka mmoja alisema: Wala mimi siabudu mnachokiabudu nyinyi.

Na katika yale waliyoyasema wataabudu Mungu wake mwaka mmoja alisema: Wala nyinyi hamtakiabudu ninachokiabudu mimi. Nyinyi mna dini yenu na mimi nina dini yangu. Akarudi Abu Jaffar El-Ahwal kwa Abu Shakir akampa habari juu ya hayo!

27

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

SURA NASR (MSAADA)NA 110

INA AYA 3

Kwa jina la allah, Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu.

إِذَا جَاءَ نَصْرُ اللَّـهِ وَالْفَتْحُ ﴿١﴾

1. Utakapokuja msaada wa Allah na ushindi.

وَرَأَيْتَ النَّاسَ يَدْخُلُونَ فِي دِينِ اللَّـهِ أَفْوَاجًا ﴿٢﴾

2. Ukawaona watu wanaingia katika dini ya Allah makundi makundi.

فَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ وَاسْتَغْفِرْهُ إِنَّهُ كَانَ تَوَّابًا ﴿٣﴾

3. Basi hapo mtakase Mola wako pamoja na kumsifu na umwombe maghufira. Hakika yeye ni mwingi kukubali toba.

UBAINIFU

Mwenyezi Mungu alimwahidi Mtume(s.a.w.w) ushindi na kwamba yeye atawaona watu wakiinga katika Uislamu makundi kwa makundi, akamwamrisha kufanya tasbih, tahlil na istighfar. Sura hii imeshuka Madina baada ya Sul-hul Hudaibiya (mapatano ya Hudaibiya) na kabla ya ushindi wa Makka, kama vile itakavyobainika.

Aya Na 1

Idha ni neno linaloonyesha muda ujao, kwa hiyo madhumuni ya aya hii ni kulitolea habari jambo litakalo hakikika baadaye. Ikiwa jambo linalotolewa habari ni msaada na ushindi na hilo ni katika mambo yanayomtuliza moyo Mtume, basi ni ahadi nzuri na biashara kwake. Msaada na ushindi uliokusudiwa hapa sio ule ambao amempatia Mwenyezi Mungu katika msimamo wake wote kama vile ushindi juu ya maadui zake katika vita na iman ya Ansar na watu wa Yemen, wala pia sio makusudio ya Sulhul Hudaibiya (mapatano ya amani ya Hudaibiya) ambayo Mwenyezi Mungu ameyaita ushindi wakati aliposema: "Hakika sisi tumekupa ushindi ulio wazi ". (48: 1).

Kwa vile Aya Na pili haioani na madhumuni yake. Kwa hiyo makusudio hapa ni ushindi wa kuiteka Makka ushindi ambao ulikuwa ndio mama wa ushindi wake Mtume(s.a.w.w) katika zama za ushindi wake na ulikuwa msaada wa ushindi ambao ulivunja vizingiti vya ushirikina katika Bara-arabu.

Hayo yanatiliwa nguvu na kiaga cha msaada uliotajwa katika aya zilizoshuka katika Sul-hul Hudaybiya: "Hakika sisi tumekupa ushindi ulio wazi, ili Allah akusamehe makosa yako yaliyotangulia na yanayokuja, na kukutimizia neema zake na kukuongoa katika njia iliyonyooka. Na akunusuru Allah nusura (msaada) yenye nguvu habisa " (48:1-3).

Lililo karibu zaidi kufahamika kutokana na yaliyomo katika aya hizo ni msaada wa Mwenyezi Mungu kwa Mtume(s.a.w.w) wake juu ya Maquraish kwa kuichukua Makka ijapokuwa ni baada ya kupita miaka miwili baada ya ushindi wa Alhudaibiya. Pia hayo ni jawabu la madai kuwa ni kuitikia watu wa Yemen kuiingia kwao katika Usilamu, bila ya vita. Yenye kukubalika ni kuwa kusudio la ushindi hapa ni ushindi wa Mtume(s.a.w.w) juu ya Maquraish na kuiteka Makka. HAya Na nadhihirisha kuwa Sura hii iliteremka baada ya Sulhul Hudaibiya kuteremka Suratul Fath (ushindi) na kabla ya kutekwa Makka.

Aya Na 2

Raghib amesema: Fawj ina maana ya makundi yanayopita kwa haraka. Wingi wa Fawj ni Afwaja. Maana ya kuingia watu makundi ni kuingia kundi baada ya kundi jengine. Makusudio ya dini, ni dini ya Kiislamu, kama alivtyosema Mwenyezi Mungu: "Hakika dini mbele ya Allah ni Uislamu ." (3:19)

Aya Na 3

Msaada huu na ushindi huu, ni namna mojawapo ya kuidhalilisha shirki na kuipa nguvu Tawhid. Au kwa maneno mengine, kuibatilisha batili na kuihakikisha haki. Basi hayo yananasabiana na kumtakasa Mwenyezi Mungu, na kumsabihi kwa upande wa kwanza na kumsifu (Sifa) Menyezi Mungu na kumshukuru kwa upande wa pili. Ndio akaamrishwa Mtume(s.a.w.w) ikasemwa (Mtakase mola wako pamoja na kumsifu na umtake msamaha.) Mwelekeo mwengine wa amri ya kumtakasa Mungu, kumsifu na kumtaka msamaha, ni kwamba ni juu ya mja kumkumbuka mola wake kwa sifa za ukamilifu wake, na kujikumbusha (mja) upungufu wake na haja yake. Ilivyokuwa kwamba ushindi huu umemaliza lile alilokuwa akilihangaikia Mtume(s.a.w.w) katika kuondoa batili na kukata shina la ufisadi, basi ameamrishwa Mtume(s.a.w.w) kumkumbuka Mola wake kwa utukufu na mwisho kujikumbusha upungufu wake wa kumhitajia kwake Mwenyezi Mungu ambako nikutaka maghufira. Maana ya kutaka maghufira, (msamaha) hapa ni kudumu hayo maghufira, kwani Mtume(s.a.w.w) amekwisha ghufiriwa.

Utafiti Wa Hadithi Katika Majmau imepokewa kutoka kwa Muqatil. Iliposhuka Sura hii, Mtume(s.a.w.w) aliwasomea Masahaba zake, wakafurahi. Alipoisikia Abbas alilia. Mtume(s.a.w.w) akamwambia: "Ni lipi linalokuliza ewe ami?" Akasema Abbas: "Ninadhani umejitolea habari za kifo chako ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu." Akasema Mtume(s.a.w.w) : "Ndio kama unvyosema". Basi akaishi baadae miaka miwili, hakuonekana akicheka kwa furaha. Simepokewa hadith nyingi kwa maana haya. Katika hiyo Majmau, imepokewa kutoka kwa Ummu Salama, amesema: "Alikuwa Mtume(s.a.w.w) siku za mwisho hasimami wala hakai, wala hendi au kuja mahali illa husema: "Subhanallahi wabihamdihi, astaghfirullah waatubu ilaihi." Kutakakata na maovu ni kwa Mwenyezi Mungu na pamoja na kumsifu. Namtaka maghufira Mwenyezi Mungu na ninarejea (tubia) kwake." Tukamuuliza juu ya hilo, akasema: "Hakika mimi nimeamrishwa hilo" kisha akasoma "Sura ya Idhaa- jaa (Nasr).

Pia ziko hadith zaidi zilizokuja kwa maana haya, lakini kwa kuhitalifiana yale aliyoyasema Mtume(s.a.w.w) . Katika kitabu cha Uyun kwa isnadi yake kwa Hussein bin Khalid, amesema: "Amesema Ridha(a.s) : "Nimemsikia baba yangu anazungumza kutokana na baba yake(a.s) kwamba Sura ya kwanza ni Iqraa (Alaq) na Sura ya mwisho kushuka ni Idha-jaa (Nasr)". Huenda ikawa makusudio ni Sura ya mwisho kushuka ikiwa kamilifu.

Katika Majmau, katika kisa cha ushindi wa Makka imesemwa: Alipotiliana mkataba wa amani Mtume(s.a.w.w) pamoja na Maquraish, katika mapatano ya Hudaibiya (Sulhul-Hudaibiya), ilikuwa moja ya masharti ni kwamba atakayetaka kujiunga na Mtume(s.a.w.w) aruhusiwe. Basi kabila la Khuzaa likajiunga na Mtume(s.a.w.w) , na Bani Bakr wakajiunga na Maquraish, makabila haya mawili yalikuwa na ugomvi mkubwa sana tangu zamani. Baadaye vikazuka vita kati ya Bani Bakr na Khuzaa. Maquraish wakawa wanawapa silaha Bani Bakr, na pia wakawa wanawasidia kupigana wakati wa usiku hali ya kujificha. Miongoni mwa waliokuwa wakiwasaidia ni Akrama bin Abu Jahal na Suhail bin Amru.

Mtu mmoja katika Khuzaa anayeitwa Amru bin Salim, akasafiri hadi Madina kwa Mtume(s.a.w.w) . Na hilo lilikuwa ni miongoni mwa mambo yaliyoleta harakati za ushindi wa kuiteka Makka. Basi Salim akasimama mbele ya Mtume alipokuwa msikitini katikati ya watu na akasema: "Leo mimi meazimu mumwona Muhammadi Rafiki mwema rahimu Ja mzaziwe wa jadi Quraishi madhalimu wamepangua ahadi Miadi yako muhimu wameivunja kusudi wakatuua kaumu Rukuuni na Sujudi". Mtume akasema kumwambia Amru: :Inatosha ewe Amr". Kisha akasimama akaingia nyumba ya mkewe Maymuna Akamwambia: "Nimiminie maji" Akawa anajiosha huku akisema "Kama sikulisaidia kundi la Amr basi itakuwa sikusaidia kitu." Baadaye akaja tena kwa Mtume(s.a.w.w) Badil bin War'qai na kikundi cha Bani Khuzaa wakampasha habari Mtume(s.a.w.w) yale wanayofanyiwa na Maquraish na jinsi walivyojitokeza kuwasaidia bani Bakr.

Kisha wakaenda zao kurejea Makka. Mtume(s.a.w.w) alikuwa ameshawaambia watu: Naona kana kwamba Abu Sufiani atakuja kuitilia nguvu mkataba na kuongeza muda wake. Walipofika sehemu inayoitwa Asfa na wakakutana na Abu Sufiani akiwa ametumwa na Maquraish ili aongeze muda wa Mkataba. Basi Abu Sufiani alipokutana na hao jamaa alimuuliza Badil, "umetoka wapi?" Badil akamwambia "nimekwenda katika mwambao huu ndani ya wangwa huu". Akauliza tena Abu Sufiani, "hukumwendea Muhammad ?" Akajibu, "La!" Basi alipoondoka Badil kuelekea Makka Abu Sufiani akajisemea, "Ikiwa ametoka Madina atakuwa amemlisha ngamia wake kokwa za tende," kwa hivyo akaenda pale alipokuwa ametulia ngamia wa Badil akachukua kinyesi chake na kukichangua, akaona kokwa za tende, akasema,: "Ninaapa kuwa Badil ametoka Madina kwa Muhammad".

Kisha katoka Abu Sufiani mpaka kwa Mtume(s.a.w.w) akamwambia "Ewe Muhammad ilinde damu ya watu, upatane na Maquraish na uongeze muda wa Mkataba wetu." Mtume(s.a.w.w) akasema: "Ewe Abu Sufiani mnajifanya wajanja !" Akasema "La! Sisi bado tunashikilia mkataba wetu na amani" Akatoka Abu Sufiani akakutana na Abu Bakr akasema "Fanya mapatano na Maquraish." Aby Bakr akajibu "Ole wako! Kuna mtu anayeweza kufanya mapatano zaidi ya Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) ". Kisha akakutana na Umar akamwambia hivyo hivyo. Kisha akatoka akaingia nyumbani kwa Ummu Habiba, (mke wa Mtume) akawa anataka kukaa kwenye tandiko. Ummu Habiba akanyanyua tandiko na kulikunja, akasema: "Ewe binti yangu kwa nini unanikataza kukalia hili tandiko?" Akasema: "Ndio hili ni tandiko la Mtume wa Mwenyezi Mungu haiwezekani ulikalie wewe najisi unayemshirikisha Mwenyezi Mungu."

Basi akatoka akaingia nyumba ya Fatima(a.s) akamwambia: "Ewe binti wa bwana wa waarabu, hufanyi mapatano na Maquraishi na kuongeza muda wa mkataba ili uwe bibi mkarimu zaidi katika watu?" Akasema" "Mapatano yangu ni mapatano ya Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) . Kisha akasema: "Basi waamrishe watoto wako (Hassan na Hussein) wafanye mapatano" Akasema: "Hawajafikia watoto wangu kufanya mapatano, na hakuna yeyote anayeweza kufanya mapatano zaidi ya Mtume(s.a.w.w) .

Akasema: Abu Sufiani "Ewe Abul-Hassan(a.s) naona mambo yamekuwa magumu, nishauri". Akasema Ali(a.s) "Wewe ndiwe mzee wa Maquraish, basi simama msikitini uwapatanishe Maquraish. Halafu wende zako kwenu". Abu Sufiani akasema: "Unaona kua hilo litatosha?" Akasema: "Hapana wallah sioni hivyo, lakini sina jengine zaidi ya hilo". Basi akasimamam Abu Sufiani msikitini akasema: "Enyi watu! Hakika mimi ninataka mapatano kati ya Maquraish". Akapanda ngamia wake akaenda zake, alipofika kwa Maquraish akaulizwa, akawapa kisa, wakasema: "Wallah Ali Bin Abu Twalib hakukufanyia lolote ila kukuchezea tu". Tumefaidika nini kwa hayo uliyasema? Akasema : "Lakini sikupata jengine zaidi ya hilo.

Mtume(s.a.w.w) akaamrisha maandalizi ya vita vya kuipiga Makka. Akawaamrisha watu wajitayarishe. Akaomba dua kwa kusema: "Ewe Mwenyezi Mungu yapoteze macho na ziepushe habari zetu hizi na Maquraish mpaka tuwaiingilie mjini mwao ghafla". Hatib bin Abu Bal-Taah akawaandikia Maquraish kuwafahamisha habari hizi za vita, lakini Mtume wa Mwenyezi Mungu akapata habari kutoka mbinguni, akamtuma Ali(a.s) na Zubeir kuchukua barua ka mwanamke aliyetumwa na Hatib. Kisa cha barua hii kimeelezwa zaidi katika Sura ya 60.

Kisha mtume(s.a.w.w) akatoka na jeshi la Waislamu elfu kumi wakiwemo wapanda farasi mia nne. Hakubakia yeyote katika Muhajirina na Ansar. Akamwacha Abudharr El- Ghifari kuwa khalifa wake hapo Madina. Ikatokea Abu Sufiani bin Harith bin Abdul Muttwalib na Abdalla bin Ummay kukutana na Mtume(s.a.w.w) kati ya Makka na Madina wakaomba kukutana na Mtume lakini hakuwapa idhini. Ummu Salama akamwambia Mtume: "Ewe Mtume na Mwenyezi Mungu binamu yako ni mkoi wako aliye mkweo (hao hapo)." Mtume akasema: "Sina haja nao; huyo binamu yangu ndiye aliyevunja heshima yangu na huyo mkoi aliye mkwe wangu ndie aliyesema aliyoyasema juu yangu huko Makka." Basi walipopopata habari hiyo, Abu Sufiani ambaye alikua pamoja na mtoto wake akasema: "Wallah! kama hataniruhusu kusema naye nitakwenda mbali pamoja na mtoto wangu huyu mpaka tufe kwa kiu na njaa." Mtume alipopata habari hiyo akawaonea huruma, hivi akawaruhusu kuzungumza naye na wakasilimu."

Mtume(s.a.w.w) alipopita Dhahran, huku Maquraish wakiwa hawana habari yoyote, alitoka usiku huo Abu Sufiani bin Harb, Hakim bin Huzam na Badil bin Warqai wakipeleleza Abbas alikuwa amekwishasema usiku huo: "Ee kupambaukiwa kubaya kwa Maquraish; kama Mtume akifanikiwa kuwavamia kuingia Makka, basi ndio itakuwa kuangamia kwa Maquraish milele." Akaendelea kusema: " Wacha nitoke huenda nitakamwona, kidomo domo au muuza maziwa au yeyote yule anayeingia Makka ambaye anaweza kwenda kuwapa habari Maquraish wakaweza kumjia Mtume(s.a.w.w) .

Abbas anaendelea kusema: "Wallah nilipokua nazunguuka kwenye miti ya miswaki, mara nikasikia sauti ya Abu Sufiani, Hakim bin Hizam na Badil bin Warqai, nikamsikia Abu Sufiani akisema: "Wallahi sijaona moto kama huu wa leo", akasema Badil: "hii ni mioto ya Bani Khuzaa." Akasema Abu Sufiani "Khuzaa niwachache kuliko hao". Basi nikajua sauti yake nikamwambia: "Ewe Abu Handalah (Abu Sufiani)!" Akasema "Ewe Abul Fadhli" nikasema "Naam!" Akasema" "Labeka! Baba yangu na mama yangu wawe wakombozi wako! Niambie kuna nini nyuma yako? Nikamwambia " Huyo hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu amekuja na kundi la Waislamu wasiopungua Elfu Kumi (10,000).

Akasema : "Sasa unasemaje?" Nikamwambia "Panda juu ya mgongo wa ngamia huyu na nitakutakie amani kwa Mtume: "Kwani naapa kwa Mwenyezi Mungu wakikupata wataikatilia mbali shingo yako." Basi nitatoka naye, kila nilipokuwa nikipita kwenye kikundi fulani walikuwa wakisema huyo ni Ami wa Mtume na yuko juu ya ngamia wa Mtume mpaka tulipofika katika kundi la Umar bin Al-Khattab akasema Umar: "Sifa njema ni za Mwenyezi Mungu ambaye ametuwezesha kukupata wewe bila ya taabu wala mapatano yoyote."

Kisha tukafanya haraka tukaelekea kwa Mtume(s.a.w.w) , akatangulia Umar kwa Mtume, akasema : "Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu huyu Abu Sufiani adui wa Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu amekuletea bila matatizo yoyote, kwa hiyo wacha nimkate shingo yake!" Nikasema: "Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu mwacheni kwanza." Lakini Umar alikuwa bado anashikilia tu! Basi nikwambia" "Ngoja ewe Umar". Huyu mtu ni katika watu wa Bani Abdu Manaf, lau angelikuwa ni katika Bani Adi nisingesema, hivyo Akasema Mtume(s.a.w.w) : "Nenda naye mpaka kesho."

Basi kulipopambazuka, nikaenda naye kwa Mtume(s.a.w.w) , alipomwona akasema: "Ole wako ewe Abu Sufiani! Bado hujafikiwa kujua kuwa hapana Mola illa Mwenyezi Mungu? Akasema: "Mkombozi wako ni baba yangu na mama yangu ni huruma zako zilioje na upole wako!, Wallah nimedhani kwamba, lau angelikuwako Mungu mwingine, basi angelitosheleza siku ya vita vya Badr na Uhud". Akasema tena Mtume(s.a.w.w) : "Je, bado hujafikiwa kujua kwamba mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu? Akasema: "Ama hili moyoni mwangu mna kitu". Basi nikamwambia: "Ole wako! Toa shahada ya kweli kabla hawajakiondoa kichwa chako", basi akashahadia."

Mtume(s.a.w.w) akamwambia Abbas: "Nenda naye na umfunge kwenye njia ya jangwani mpaka jeshi la Mwenyezi Mungu lipite." Anaendelea kusema Abbas: "Nikamfunga kwenye jabali, yakawa yanapita makabila mbali mbali na yeye anasema : "Ni nani hawa" nikamjibu: "Aslam, Juhayna na Fulani na ?.." mpaka akapita Mtume(s.a.w.w) katika kikosi cha kijani wakiwemo Muhajirina na Ansar akiwa amezungukwa huko na huko. Akasema Abu Suffiani "Ni kina nani hawa? Nikamwambia: "Huyu ni Mtume, wa Mwenyezi Mungu akiwa pamoja na ndugu yako amekuwa mfalme mkubwa" Nikamwambia: "Ole wako! Huo si ufalme, bali ni utume" akasema "Ndio hivyo, sasa!"

Akaja Hakim bin Hizam na Badil bin Warqai kwa Mtume(s.a.w.w) , wakasilimu na wakambai. Basi Mtume(s.a.w.w) akawatuma kwa Maquraish kuwalingania katika uislamu. Akasema Mtume(s.a.w.w) "Mwenye kuiingia nyumba ya Abu Sufiani iliyoko sehemu ya juu ya Makka, amesalimika na mwenye kuinigia nyumba ya Hakim iliyoko chini ya Makka, amesalimika, na mwenye kufunga mikono yake amesalimika. Alipotoka Abu Sufiani na Hakim kuelekea Makka, Mtume alimpeleka Zubeir bin Awam, akamwamrisha kukita bendera yake sehemu ya juu ya Makka na akamwambia " Usiondoke mpaka nije huko." Kisha Mtume(s.a.w.w) akaingia Makka na akapiga kambi. Akaanza kumpeleka Saad bin Ubadah na kikosi cha Ansar na akampeleka Khalid bin El-Walid pamoja na wale waliosilimu katika Kudhaa na Bani Salim, akamwamrisha kuingia sehemu ya chini ya Makka na kukita bendera yake kando ya majumba.

Mtume(s.a.w.w) akaamrisha wote kuizuwiya mikono yao, wasipigane na mtu yoyote isipokuwa yule anayetaka kupigana nao Na akamrisha kuuliwa watu wane, (1) Abdalla bin Saad bin Abu Sarh (2) Huwayrith bin Nufayl (3) Ibn Khatal (4) Muqbis bin Dhubaba. Pia akamrisha kuuwawa wajakaza wawili waliokuwa wakiimba nyimbo za kumkebehi Mtume. Akasema Mtume(s.a.w.w) : "Wauweni hao hata kama mkiwakuta wamejifunika pazia ya Al-Kaaba." Ali(a.s) akamuuwa Huwayrith bin Nufayl, na mmoja wa wajakazi wawili na mjakazi mwingine akatoroka, akamuuwa Muqbis katika soko na akamkuta Ibn Khatwal amejifunika na pazia ya Al-kaaba, wakatangulia Said bin Hureith na Ammar bin Yassir , Said akatangulia yeye akamuuwa. Abu Sufiani akamuendea Mtume akachukua kikuku chake cha kupandia farasi akakibusu, kisha akasema: "Makombozi wako ni baba yangu na mama yangu hivi hukusikia yale anayosema Saad: "Leo ni siku ya vitakuu, leo wanawake watatekwa."

Mtume(s.a.w.w) akamwambia Ali mfuate, uchukue bendera kwake, na uwe wewe ndiye utakayeingia nayo na uingie nayo kwa upole. Basi ali akaichukua akaingia nayo kama alivyoamrishwa. Mtume(s.a.w.w) alipoingia Makka, alikwenda kusimama kwenye mlango wa Al-Kaaba akasema: "Hapana Mola isipokua Allah hali ya kuwa yupekee yake, ametekeleza ahadi yake. Na amemnusuru mja wake, amevishinda vikundi vya madui hali yakuwa yupeke yake. Jueni kwamba mambo yote na damu inayodaiwa, vyote hivo viko chini ya miguu yangu hii, isipokuwa utumishi wa Al-Kaaba na kunywesha mahujaji. Hivyo viwili vitarudishiwa wenyewe. Jueni kwamba Makka ni yenye kuharamishwa kwa uharamisho wa Mwenyezi Mungu, haikua halali kwa yeyote aliyekuwa kabla yangu na haikua halali kwangu isipokuwa saa moja katika mchana, nayo ni yenye kuharimishwa mpaka Kiyama; Haukatwi mti wake wala hawindwi mnyama wake, wala sihalali kuokota kitu ila kwa atakayekitangaza kisha akasema: "Eee! Majirani wabaya wa Mtume(s.a.w.w) mlikuwa mkifanya mrongo, mkamfukuza na mkamuudhi; kisha hamkutosheka na hayo mpaka mkanifuata katika mji wangu kunipiga vita, basi nendeni nimewasamehe. Wakatoka watu kama walifufuliwa kutoka makaburini na wakaingia katika Uislamu. Mwenyezi Mungu alikuwa amemwezesha Mtume kuwachukua mateka, lakini akaacha, kwa hiyo wakaitwa watu wa Makka 'walioachiwa'. Kisha akaja Ibn Zabary akasilimu.

Imepokewa kutoka kwa Ibn Masud amesema: aliingia Mtume(s.a.w.w) siku ya kuichukua Makaa akakuta katika Al-Kaaba sanamu mia tatu na sitini, akawa anazichoma kwa mti aliokuwa mkononi mwake huku akisema: "Imekuja haki na batil haina msingi wala haitarudi tena, imekuja haki na imeondoka batil, hakika batil ni yenye kuondoka."

Imepokewa kwa Ibn Abbas, amesema: "alipofika Mtume Makka alikataa kuingia Al- Kaaba ikiwa na masanamu akamrisha yatolewe miongoni mwayo yalikuwepo masanamu ya Ibrahim na Ismail(a.s) yakiwa na miti ya kupigia mburuga mikononi mwake. Mtume(s.a.w.w) akasema: " Mungu awatokemeze. Kwa hakika walijua kuwa hawakuwa wakipiga mburuga kabisa." Hadith katika kisa hiki cha ushindi wa Makka ni nyingi na yaliyotangulia ni kama muhtasar tu!

16

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

SURA SHAMS (JUA) (NA. 91)

INA AYA 15

Kwa jina la Allah, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu

وَالشَّمْسِ وَضُحَاهَا ﴿١﴾

1. Naapa kwa jua na mwanga wake.

وَالْقَمَرِ إِذَا تَلَاهَا ﴿٢﴾

2. Na (kwa) mwezi unapoliandamana.

وَالنَّهَارِ إِذَا جَلَّاهَا ﴿٣﴾

3. Na (kwa) mchana unapoifunia.

وَاللَّيْلِ إِذَا يَغْشَاهَا ﴿٤﴾

4. Na (kwa) usiku unapoifunika.

وَالسَّمَاءِ وَمَا بَنَاهَا ﴿٥﴾

5. Na (kwa) mbingu na aliyeziweka.

وَالْأَرْضِ وَمَا طَحَاهَا ﴿٦﴾

6. Na (kwa) ardhi na aliyeitandika.

وَنَفْسٍ وَمَا سَوَّاهَا ﴿٧﴾

7. Na (kwa) nafsi na aliyelingamanisha.

فَأَلْهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقْوَاهَا ﴿٨﴾

8. Akaifahamisha maasia yake na twaa yake.

قَدْ أَفْلَحَ مَن زَكَّاهَا ﴿٩﴾

9. Hakika amefaulu mwenye kuitakasa.

وَقَدْ خَابَ مَن دَسَّاهَا ﴿١٠﴾

10. Na hakika amepata hasara mwenye kuitweza.

كَذَّبَتْ ثَمُودُ بِطَغْوَاهَا ﴿١١﴾

11. Ilikadhibisha (kabila ya) thamud kwa kupetuka mipaka.

إِذِ انبَعَثَ أَشْقَاهَا ﴿١٢﴾

12. Wakati walipomshakiza mwovu wao (kumuua ngamia).

فَقَالَ لَهُمْ رَسُولُ اللَّـهِ نَاقَةَ اللَّـهِ وَسُقْيَاهَا ﴿١٣﴾

13. Akawaambia Mtume wa Allah, (tahadharini na) ngamia wa Allah na maji yake.

فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمْدَمَ عَلَيْهِمْ رَبُّهُم بِذَنبِهِمْ فَسَوَّاهَا ﴿١٤﴾

14. Wakamkadhibisha (na) wakamchinja. Mola wao akaeneza (adhabu) kwa sababu ya madhambi yao, na akaifanya sawa.

وَلَا يَخَافُ عُقْبَاهَا ﴿١٥﴾

15. Wala haogopi matokeo yake.

UBAINIFU

Sura inataja kwamba kufaulu kwa mtu ni kuitakasa nafsi yake na kuikuza makuzi mema kwa kuipamba na takua na kuitakasa na uovu. Na kupata hasara na kuzuiliwa wema ni kwa mwenye kuitweza. Yanatolea ushahidi hilo yale yaliyowapitia kabila la Thamud walipong'olewa na adhabu pale walipomkadhibisha Mtume was Saleh na kumchinja ngamia. Hilo ni kuwaonyesha watu wa Makka. Sura imeshuka Makka kwa ushahidi wa mpangilio wake wa maneno.

Aya Na 1

Maana ya neno Dhuhaa ni kukunjuka jua na kuenea mchana na neno hilo limetumiwa kwa wakati. Katika aya hii kuna kiapo kwa jua na kuangaza kwake juu ya Ardhi.

Aya Na 2

Inaungana na Aya Na kwanza na nikuapa kwa mwezi hali yakuwa unaandamia jua. Makusudio ya kuandamia ikiwa inamaanisha kule kupata mwezi nuru yake kutoka kwa jua, basi itakuwa ni kuapa kwa wakati wote wa mwezi. Na ikiwa ni kuchimbuka kwa mwezi baada ya kutua jua, basi itakuwa kuapa ni tangu kuwa mwezi mchanga mpaka kuwa mpevu.

Aya Na 3

Maana ya neno Jallaha ni kudhihirisha na dhamir ni ya Ardhi kwa maana ya kuwa: ninaapa kwa mchana unapoidhirisha ardhi kwa macho. Inasemekana kuwa dhamir ya (mtendaji) ni ya mchana na dhamir ya (mtendwa) ni ya jua, kwa maana ya kuwa, ninaapa kwa mchana wakati Mwenyezi Mungu anapolidhihirisha jua, na hiyo ni njia iliyo mbali.

Aya Na 4: Yaani unapoifunika ardhi, dhamir ni ya ardhi kama katika aya iliyotangulia. Na inasemekana kuwa ni ya jua na hiyo pia ni njia iliyo mbali, kwa sababu usiku haufuniki jua isipokuwa unafunika ardhi na vilivyo juu yake. Ibara ya kufunika ardhi imekuja kwa (kitendo cha sasa) kinyume cha aya zilizotangulia ambapo ibara zake zimekuja kwa kitendo cha muda uliopita. Hiyo ni kufahamisha kufunika uovu wa ardhi kwa wakati uliopo ambao ndio mwanzo wa kudhihiri mlingano (mwito) wa Kiislamu, kutokana na yaliyotangulia kuwa kuna muungano kati ya kuapa na mwenye kuapiwa.

Aya Na 5-6

Herufi Maa katika neno Maabanaaha na Maatwahaaha ni kiwakilishi yaani na ambaye ameziweka na kuitandika ni Mwenyezi Mungu. Kuleta ibara bila ya kumtaja Mwenyezi Mungu ni athari ya kuficha kunakofahamisha ukubwa na ajabu, kwa maana ya kuwa; Ninaapa kwa mbingu na kitu chenye nguvu cha ajabu kilichoziweka. Na ninaapa kwa ardhi na kitu chenye nguvu cha ajabu kilichoitandika. Imesemwa kuwa Maa ni kiarifa chenye kutumika kama jina kwa maana ninaapa kwa mbingu na kuziweka kwake. Na ardhi na kuitandika kwake, lakini mpangilio wa maneno katika Sura kama vile aya inayofuatia haulisaidii hilo.

Aya Na 7

Yaani ninaapa kwa nafsi na kitu chenye uwezo, ujuzi na hekima ambacho kimeilingamanisha, kuipanga umbo lake na viungo vyake na kuilingamanisha sawa nguvu yake. Makusudio na nafsi ni nafsi ya mtu yoyote. Imesemwa kuwa makusudio ni nafsi na Nabii Adam(a.s) , lakini mpangilio wa maneno hauafikiani na hilo hasa Aya Na tisa na kumi.

Aya Na 8

Neno Fujuur kama alivyotaja Raghib ni kupasua sitara ya dini. Makatazo ya Mungu ya kufanya au kuacha, ni sitara iliyowekwa kati ya binadamu na Mwenyezi Mungu na kufanya yaliyokatazwa ni kupasua sitara hiyo. Neno Taqwa kama alivyotaja Raghib ni kuifanya nafsi katika kinga ya yanayohifiwa. Makusudio ya Taqwa kwa kuilinganisha na aya inayofuatia ni kujiepusha na maovu na kujilinda na yaliyo katazwa. Imefasiriwa katika hadith kwamba ni kujichunga ya yaliyoharamishwa.

Kuifunga silika (Ilham) juu ya anuani mbili za uovu wa nafsi na takua yake, ni kwa ajili ya kufahamisha kwamba makusudio ni kwamba Mwenyezi Mungu anamfahamisha mtu sifa ya kitendo chake kuwa ni kizuri au kibaya, baada ya kumfahamisha kitendo chenyewe hasa, kwa kuangalia asili yake ya mwenzo, ambapo kitendo kinaweza kuwa ni kizuri na kibaya wakati mmoja. Kwa mfano kula mali ya yatima ambako ni kuovu na kula mali yake mwenyewe ambako ni kitendo kizuri au kuvaana na mwanamke ambako kunashirikiana kati ya zina ambayo ni uovu na ndoa ambayo ni takua. Kwa ujumla makusudio na kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemfahamisha mtu kuwa kitendo anachokifanya ama kitakuwa cha uovu au cha takua na akampambanulia takua na uovu.

Kuifuatisha silika juu ya usawa katika kauli yake: "na mwenye kuilingamanisha. Akaifahamisha." ni kuashiria kuwa (mtu) kufahamu uovu na heri - ambapo ndiyo akili ya kimatendo - ndiyo kusawazisha nafsi. Na hiyo ni miongoni mwa sifa za umbile la hiyo nafsi; kama alvyosema Mwenyezi Mungu (s.w.t): "Basi uelekeze uso wako katika dini iliyo sawasawa ndiyo umbile Allah alilowaumbia watu; hakuna mabadiliko katika maumbile ya viumbe vya Allah. Hiyo ndiyo dini iliyo haki " (30:30).

Kutegemeza uovu na takua kwenye dhamir na nafsi ni kuonyesha kwamba makusudio ya uovu na takua zinafahamishwa hapa ni uovu na wema kuhusika na hii nafsi iliyoelezewa ya mtu na zile za majini kama ilivyodhihiri katika Qur'an tukufu kuwa wao ni wenye kukalifiwa na imani na kutenda amali njema.

Aya Na 9 -10

Kufaulu ni kushinda matakwa na kupata matakwa, kinyume chake ni kupata hasara. Kutakata ni kukua kwa makuzi mema yenye baraka. Na kutweza ni kuingiza kitu katika kitu chengine, makusudio yake kwa kukutanisha na aya, inayokabiliana na kutakasa, ni kuikuza nafsi katika misingi inayohitalifiana na tabia yake na kuipandanisha nayo. Aya hizo mbili ni jawabu la kiapo na Aya Na pili inaungana na ya kwanza. Kuleta ibara ya kutengenea nafsi na kuharibika kwake kwa neno kutakasa na kutweza ni udhihirisho wa inavyofahamisha kauli yake Mwenyezi Mungu. Akaifahamisha maasi yake na twaa yake, kwamba ni katika ukamilifu wa nafsi ya kiutu kwamba hiyo nafsi kimaumbile inapambanua uovu kutokana na twaa, yaani dini ya Kiislamu ni dini ambayo Mwenyezi Mungu anaikusudia kwa maumbile ya mtu, kwa hiyo kuipamba nafsi kwa twaa ni kuitakasa.

Aya Na 11

Aya hii na zinazofuatia mpaka mwisho wa Sura ni ushuhuda na uthibitisho wa yaliyotangulia katika kauli yake Mwenyezi Mungu: "Hakika amefaulu mwenye kuitakasa ".

Aya Na 12

Makusudio ya mwovu wa Thamud ni yule aliyemchinja ngamia. Jina lake kutokana na yaliyo katika riwaya ni Qidar bin Salif. Na kushakiza kulikuwa na kushakiza kwa watu kama zinavyofahamisha aya zinazofuatia kutokana na dhamir zake za wingi.

Aya Na 13

Makusudio ya Mtume wa Mwenyezi Mungu hapa ni Saleh(a.s) Mtume wa Thamud. Maana yake: akawaambia Mtume Saleh kwa ujumbe utokao kwa Mwenyezi Mungu: "Tahadharini na ngamia wa Allah na maji yake wala msimtaaradhi kuwa kutaka kumuua au kumzuwia na zamu yake ya kunywa maji ." Mwenyezi Mungu amekifafanua kisa hiki katika Sura ya II (Hud) na nyenginezo.

Aya Na 14

Kusema kwake akaifanya sawa, kwa dhahiri dhamir ni ya Thamud kwa kuzingatia kuwa ni kabila yaani akalifanya sawa na ardhi hilo kabila au ni kufanya sawa kwa maana ya kuitandaza hiyo ardhi. Inasemekana kuwa dhamir ni ya neno kueneza kwa maana ya kuwa akawaeneza adhabu na akaifanya sawa kwa wote hila ya kuangalia mwenye nguvu, wala myonge au mkubwa wala mdogo.

Aya Na 15

Dhamir ni ya kueneza au kufanya sawa yaani Mola wao haogopi mwisho wa kueneza adhabu na kuifanya sawa, kama wanavyoogopa wafalme na wenye nguvu mwisho wa mateso kwa maadui zao; kwa sababu mwisho wa mambo ni vile anavyotaka yeye Mwenyezi Mungu na kuafikiana na anavyoidhinisha. Aya hii iko karibu katika maana na aya inayosema: "Haulizwi anayoyafanya, lakini wao wataulizwa " (21:23).

Inasemekana kuwa dhamir ya neno haogopi ni ya mwovu kwa maana ya kuwa haogopi mchinjaji ngamia mwisho wa aliofanya. Na pia imesemekana kuwa dhamir ya haogopi ni ya Saleh na dhamir ya mwisho wake ni ya kueneza adhabu kwa kutegemea kuokoka. Udhaifu wa njia zote hizo mbili uko wazi.

Utafiti Wa Hadith Katka Tafsiri ya Qummi kuhusu Aya Na saba amesema: Akaiumba na kuitia Sura. Katika Majmau amepokea Zurarah na Hamran, na Muhammad bin Muslim kutoka kwa Abu Jaffar na Abu Abdillah(a.s) katika kauli yake Mwenyezi Mungu: Akaifahamisha maasis yake na twaa yake, ni kuwa ameibanisha yale ya kufanya na ya kuwacha. Na katika kauli yake Mwenyezi Mungu: "Hakika amefaulu mwenye kuitakasa". Amesema: "Hakika amefaulu mwenye kutwii" Na kuhusu na hakika amepata hasara mwenye kuitweza. Amesema: "Hakika amepata hasara mwenye kuasi".

Katika Durril Manthur ametoa Ahmad, Muslim, Ibn Jariyr, Ibn Mundhir, Ibn Murdawayh kutoka kwa Amran bin Haswiyn kwamba mtu mmoja alisema: "Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu unaona wanayoyafanya watu leo wanajitahidi katika jambo ambalo limekwisha hukumuliwa na kupitishwa katika kadar iliyotangulia? Au katika ambayo wanamkubalia Mtume wao"? Akasema: "Bali ni jambo lililokwisha pitishwa.' Akasema huyo mtu kwa nini wanafanya basi? Akasema Mtume: "Ambaye Mwenyezi Mungu amemuumbia kwa moja ya daraja mbili humuandalia kuifanya. Na ukweli wa hayo ni katika kitabu cha Mwenyezi Mungu: "Na (kwa) nafsi na aliyelingamanisha akaifahamisha maasia yake na twaa yake ."

Ufafanuzi Wa Hadith Hiyo Aliposema au katika wanayomkubalia Mtume wao, inaungana na sehemu ya kwanza kama swali yaani, Je, katika kumtii Mtume wao kumepitishwa na kukadiriwa tayari? Aliposema: "Kwa nini wanafanya basi, yaani nini maana ya amali yao na kutugemezwa kitendo kwao"? Na aliposema; "Ambaye Mwenyezi Mungu amemuandalia " Maana yake ni kuwa: Matokeo ya kutenda wema au uovu yanatokana na wao pamoja na kuangalia kuwa yamekwishapitishwa na kukadiriwa; huko hakukanushi kutokea kwake kwa kumwangalia mtu na hiyari yake. Na hayo yamefafanuliwa mara nyingi. Katika utafiti uliotangulia katika kitabu hiki.

Katika hiyo Durril Manthur, ametoa Ibn Abu Hatim,Abu Shakh, Ibn Murdawayah na Addilami kutoka kwa Juwaybir naye kutoka Adh-dhahak naye kutoka kwa Ibn Abbas amesema: Nimemsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) akisema: "Hakika amefaulu mwenye kuitakasa". Imefaulu nafsi aliyoitakasa Mwenyezi Mungu na imepata hasara nafsi aliyoihasirisha Mwenyezi Mungu na kila heri".

Kunasibisha utakaso na hasara kwa Mwenyezi Mungu S.W.T. ni kwa njia ambayo haikanushi kunasababishwa twaa na maasi kwa mtu. Na hakika hunasababishwa upotevu kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwa njia ya fumbo; kaa S.W.T. kwa njia ya fumbo; kama alivyosema Mwenyezi Mungu "Na hamwachii yoyote kupotea kwa mfano huo isipokuwa wale wavunjao amri zake (mafasiki) " (2:26).

Katika Majmau anasema: " Imesihi riwaya kwa kutegemeza Uthman bin Suhaib naye kutoka kwa baba yake amesema" "Mtume(s.a.w.w) alisema kuumuliza Ali bin Abu Twalib: ni nani mwovu zaidi wa watu wa mwanzo?" Akasema: " aliyemchinja ngamia". Mtume akasema, "umepata". "Na nani mwovu wa watu wa mwisho?" Akasema "sijuwi ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu." Akasema Mtume: "Ambaye atakupiga kwenye huu (akaonyesha utosi wake)". Na imepokewa hadith nyengine kwa maana haya haya kutoka kwa Ammar bin Yassir. Katika Tafsiri ya Burhan amepokea Thalaabi ne Wahidi kwa kutegemezwa kwao, kutoka kwa Ammar na kutoka kwa Athman Bin Suhaib na kutoka kwa Adh-dhahhak.

Na amepokea Ibn Murdawayh kutoka kwa Jabir bin Samra; na kutoka kwa Ammar kutoka kwa Ibn Adi na amepokea Attabari na Muswili. Amepokea Ahmad kutoka kwa Adh- dhahhak naye kutoka kwa Ammar kwamba yeye amesema: Amesema Mtume(s.a.w.w) : "Ewe Ali mwovu zaidi wa kwanza ni mchinja ngamia na mwovu zaidi wa mwisho ni muuaji wako ".

17

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

SURA LAYL (USIKU) (NA. 92)

INA AYA 21

Kwa jina la Allah, Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu

وَاللَّيْلِ إِذَا يَغْشَىٰ ﴿١﴾

1. Naapa kwa usiku unapofunika

وَالنَّهَارِ إِذَا تَجَلَّىٰ ﴿٢﴾

2. Na (kwa) mchana unapofunuka.

وَمَا خَلَقَ الذَّكَرَ وَالْأُنثَىٰ ﴿٣﴾

3. Na (kwa) mwenye kuumba kiume na kike.

إِنَّ سَعْيَكُمْ لَشَتَّىٰ ﴿٤﴾

4. Hakika matendo yenu ni mbali mbali.

فَأَمَّا مَنْ أَعْطَىٰ وَاتَّقَىٰ ﴿٥﴾

5. Ama mwenye kutoa akamcha (Mwenyezi Mungu).

وَصَدَّقَ بِالْحُسْنَىٰ ﴿٦﴾

6. Akalisadiki jambo jema.

فَسَنُيَسِّرُهُ لِلْيُسْرَىٰ ﴿٧﴾

7. Tutamsahilishia njia ya wepesi.

وَأَمَّا مَن بَخِلَ وَاسْتَغْنَىٰ ﴿٨﴾

8. Ama mwenye kufanya ubakhili akajiona hana haja.

وَكَذَّبَ بِالْحُسْنَىٰ ﴿٩﴾

9. Akalikadhibisha jambo jema.

فَسَنُيَسِّرُهُ لِلْعُسْرَىٰ ﴿١٠﴾

10. Tutamfanyia nyepesi njia ya uzito.

وَمَا يُغْنِي عَنْهُ مَالُهُ إِذَا تَرَدَّىٰ ﴿١١﴾

11. Hayatamfaa mali yake atakapopomoka.

إِنَّ عَلَيْنَا لَلْـهُدَىٰ ﴿١٢﴾

12. Hakika na juu yetu kuongoza.

وَإِنَّ لَنَا لَلْآخِرَةَ وَالْأُولَىٰ ﴿١٣﴾

13. Na hakika ni yetu sisi akhera na ulimwengu.

فَأَنذَرْتُكُمْ نَارًا تَلَظَّىٰ ﴿١٤﴾

14. Basi ninawahadharisha na moto unaowaka kwa nguvu.

لَا يَصْلَاهَا إِلَّا الْأَشْقَى ﴿١٥﴾

15. Hatauingia ila mwovu mno!

الَّذِي كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ ﴿١٦﴾

16. Ambaye amekadhibisha akapa mgongo.

وَسَيُجَنَّبُهَا الْأَتْقَى ﴿١٧﴾

17. Na ataepushwa nao mwenye kucha (Mungu).

الَّذِي يُؤْتِي مَالَهُ يَتَزَكَّىٰ ﴿١٨﴾

18. Ambaye hutoa mali yake kwa (kutaka) kujitakasa.

وَمَا لِأَحَدٍ عِندَهُ مِن نِّعْمَةٍ تُجْزَىٰ ﴿١٩﴾

19. Na hali ya kuwa hakuna yoyote aliyemfanyia hisani ili awe anamlipa.

إِلَّا ابْتِغَاءَ وَجْهِ رَبِّهِ الْأَعْلَىٰ ﴿٢٠﴾

20. Isipokuwa ni kwa kutaka radhi ya Mola wake aliye Mtukufu mno.

وَلَسَوْفَ يَرْضَىٰ ﴿٢١﴾

21. Basi hapo ataridhia.

UBAINIFU

Lengo la Sura hii ni kuonya. Inaelezea huko kuonya kwa kufuata njia ya kuonyesha tofauti ya matendo ya watu: Kwamba katika wao, mwenye kutoa, akamcha Mwenyezi Mungu na akalisadiki jambo jema, basi Mwenyezi Mungu atammanikisha katika maisha mema ya milele. Na katika wao mwenye kufanya ubakhili, akajiona hana haja na akalikadhibisha jambo jema, basi Mwenyezi Mungu atamwelekeza kwenye uovu. Sura hii inatilia umuhimu zaidi jambo la kutoa mali. Kulingana na mpangilio wake inawezekana kuwa imeshuka Makka au Madina.

Aya Na 1

Mwenyezi Mungu anaapa kwa usiku unapofunika mchana; kama alivyosema: "Huufunika usiku kwa mchana " (7:54). Inawezekana kuwa makusudio yake ni kufunika ardhi au jua.

Aya Na 2

Inaungana na Aya Na (1). Maana ya neno Tajallaa ni kudhihiri kitu baada ya kujificha. Amesema katika Majmau ni kudhihiri huo mchana kutoka katika giza. Hili ni neema kubwa, kwani lau wakati wote ungekuwa ni giza, basi watu wasingeweza kutafuta maisha.

Aya Na 3

Pia inaungana na aya iliyotangulia herufi Maa ni kiwakilishi na makusudio yake ni Mwenyezi Mungu Mtukufu. Imekuja ibara hiyo bila ya kumtaja Mwenyezi Mungu kwa kutambulisha utukufu wake; Maana yake; ninaapa kwa kitu cha ajabu ambacho kimeleta kiume na kike ambavyo ni namna moja, lakini vimetofautina. Imesemwa kuwa herufi Maa ni kiarifa chenye kutumika kama jina; Maana yake ni ninaapa kwa kuumba kiume na kike lakini njia hii ni dhaifu. Mukusudio ya kiume na kike hapa ni aina yoyote ya kiume na kike. Imesemwa kuwa ni mtu mume na mke na pia imesemwa kuwa ni Adam na mkewe Hawa, lakini njia iliyo na nguvu zaidi, ni hiyo ya kwanza.

Aya Na 4

Neno Saa'ya lina maana ya kwenda haraka, na makusudio yake hapa ni ketendo kwa vile mtu anajihimu nacho, nalo liko katika maana ya wingi. Jumla hiyo ni jawabu la kiapo na maana yake; Ninaapa kwa vitu hivi vyenye kutofautiana kwa umbo na athari, hakika matendo yenu ni yenye kutofautiana hayo yenyewe na athari zake. Kuna katika hayo ni ya kutoa, kumcha Mwenyezi Mungu na kusadikisha, yana athari inayohusika nayo. Na kuna katika hayo ni ya ubakhili, kujitosheleza na kukadhibisha nayo yana athari inayohusika nayo.

Aya Na 5-6

Ni ufafanuzi wa kutofautiana matendo yao na kutofautiana athari yake. Makusudio ya kutoa ni kutoa mali kwa ajili ya Mwenyezi Mungu kinyume chake ni ubakhili wa kujizuia kutoa mali. Na kusema kwake: "Hayatamfaa mali yake atakapopomoka." Na kusema kwake : "Na akamcha Allah" ni kama anafasiri kutoa, makusudio yake ni kutoa kwa njia ya (taqwa) uchaji Mungu. "Jambo jema" ni sifa yenye kusimama mahali pa chenye kusufiwa, kwa dhahiri kukadiriya kwake ni maandalizi mema ambayo ameyatolea ahadi Mwenyezi Mungu Katika thawabu ya kutoa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) Na huko kutoa ni kusadikisha ufufuo na kuamini Mwenyezi Mungu na kulazimisha imani kwa umoja wake Mwenyezi Mungu (s.w.t) katika ubwana na kuuamini utume. Hiyo ndiyo njia ya kufikia yale aliyoyatolea ahadi Mwenyezi Mungu kupitia kwenye ulimi wa Mtume wake.

Aya Na 7

Makusudio ya kumsahilishia njia ya wepesi ni kumwafikisha kwa mali njema kwa kuzifanya nyepesi bila ya uzito wowote. Au kumfanya ni mwenye kujiandaa kwa maisha mema mbele ya Mola wake na kuingia peponi kwa sababu ya amali njema anazozifanya. Hii njia ya pili ni karibu na iko wazi zaidi kutokana na yale yaliyotolewa ahadi katika viaga vya Qur'an.

Aya Na 8 -10

Ubakhili ni kunyume cha kutoa. Makusudio ya kukadhibisha jambo jema ni kukanusha mambo mema na thawabu za Mwenyezi Mungu ambazo wamezielezea Mitume. Na hayo yanarudia kukanusha ufufuo. Makusudio ya 'kusahilishiwa uzito' ni kutofanikiwa kwake kwa kukosa kuwafikishwa kwenye amali njema, kwa kuwa nzito na kukosa kukunjuliwa moyo wake na imani au ni kuandaliwa adhabu.

Aya Na 11

Herufi Maa ni swali yaani mali yake itamfaa namna gani atakapokufa na kuangamia. Au ni ya kukanusha, yaani haitamfaa mali yake atakapoangamia.

Aya Na 12-13

Ni sababu ya yaliyotangulia katika kuzungumzia wepesi na uzito Au nikuelezea kwa ufafanuzi zaidi kwamba hakika sisi tunafanya huu wepesi au tunaubainisha ubainifu huu, kwa sababu unatokana na uongofu na ni juu yetu kuongoza na wala hakituzuii kitu chochote. Kwa hivyo kusema kwake "Hakika ni juu yetu kuongoza", kunamaanisha kwamba kuongoza watu alikokupitisha Mwenyezi Mungu (s.w.t) amejiwabisha mwenyewe kwa mujibu wa hekima, na hilo ni kwamba yeye amewaumba ili wamwabudu; kama alivyosema: "Sikuumba majini na watu ila waniabudu ". (51:56).

Kwa hiyo amefanya kumwabudu ndiyo lengo la kuumbwa kwao na akaifanya hiyo ibada ni njia yenye kunyooka ya kumwendea yeye; kama alivyosema: "Hakika Allah ni Mola wangu na ni Mola wenu, basi mwabuduni hii ndiyo njio iliyonyooka " (3:51) "Hakika wewe unaongoza njia iliyonyooka " (42:52).

Mwenyezi Mungu amejihukumilia kuwabainishia watu njia yake na kuwaongoza kwake, kwa maana ya kuwaonyeshea njia, ikiwa wataifuata au wataiwacha, kama alivyosema: "Na Allah ndiye anayesema kweli, naye kuongoa njia (ya uongofu) (33:4). Amesema tena: "Hakika sisi tumemuongoa njia, basi ama atakuwa mwenye kushukuru au kukufuru ". (76:3).

Hayo yote hayapingi kuwa mtu mwengine asiyekuwa Mwenyezi Mungu kuweza kusimamia jambo hili kwa idhini yake Mwenyezi Mungu, kama vile mitume; kama alivyosema Mwenyezi Mungu: "Hakika wewe (Muhammad) unaongoza njia iliyonyooka " (42:52). Amesema tena: "Sema, hii ndiyo njia yangu ninailingania kwa Allah kwa ujuzi wa kweli, mimi (ninafanya hivi) na wanaonifuata " (12:108)

Hayo ni ikiwa uongozi ni kwa maana ya kuonyesha njia. Ama ikiwa uongozi ni kwa maana ya kufikisha kwenye matakwa - na matakwa ni athari nzuri ambazo zinafuatana na kuongoka kwa uongofu wa Mwenyezi Mungu kama maisha mema ya dunia na ya akhera ya milele - basi kwa ubainifu zaidi itakuwa ni kwa upande wa kutengeneza na kupatisha ambako anahusika nako Mwenyezi Mungu (s.w.t) Hayo ni katika yale aliyoyahukumilia Mwenyezi Mungu na kujiwajibishia na kuyasajili kwa kiaga chake cha haki; Mwenyezi Mungu anasema: "Basi atakayeufuata uongofu wangu hatapotea wala hatataabika ." (20:123).

"Mwenye kufanya mema miongoni mwa wanaume au wanawake na hali ya kuwa yeye ni muu'min tutamuhuyisha maisha mema na tutawapa ujira wao mkubwa kwa sababu ya yale mema waliyokuwa wakiyatenda ." (16:97).

Amesema tena: "Na wale waliomaini na wakatenda njema tutawaingiza katika mabustani yapitayo mito chini yake watakaa humo milele. Ndiyo ahadi ya Allah iliyokweli. Na ninani mkweli zaidi kwa usemi kuliko Allah ? (4:122). Kunasibishiwa uongozi mtu mwingine asiyekuwa Mwenyezi Mungu, kwa kuingia kati huyo mtu na hayo yanayonasibishwa kwa Mwenyezi Mungu. Hii ikiwa ni kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Hivyo Mwenyezi Mungu atakuwa ndiyo asili ya uongozi, na mtu huyo ni mfuasi. Maana ya aya, ikiwa makusudio ya uongofu ni kuonyesha njia, ni: hakika sisi tunawabainisha yale tunayoyabainisha, kwa sababu ni juu yetu kuonyesha njia ya kuabudu. Ikiwa ni kwa makusudio ya kufikisha kwenye matakwa, ni: hakika tunawasahilishia hawa wepesi wa amali njema, au na maisha mepesi ya milele na kuingia peponi; kwa sababu hilo ni katika kuvifikisha vitu kwenye lengo lake, na hilo ni juu yetu. Ama kusahilishia njia ya uzito ni kuzuilika na kupata wepesi, "Ili Allah apate kuwapambanua walio wabaya na walio wazuri na kuwaweka wabaya juu ya wabaya wengine na kuwarundika wote pamoja na kuwatupa katika Jahanam ". (8:37).

Mwenyezi Mungu amekwishasema: "Na tunateremsha katika Qur'an (Hayo mafundisho yake) ambayo ni ponyo na rehema kwa wanaoamini wala hayawazidishi (mafundisho hayo) madhalimu ila hasara tu! (kwani hawakubali kufuata) ." (17:82).

Inawezekana kuwa maana ya ungozi hapa - kwa vile tamko 'uongozi' halikutegemezewa sharti yeyote - ni kwamba huu uongozi, pasi na kutajwa katika jambo gani, una maana mapana zaidi kuliko uongozi uliotajwa kama katika mazingatio ya sheria n.k. - kwa hiyo Mwenyezi Mungu ni wake uongozi wa kiuhakika kama alivyosema: "ambaye amekipa kila kitu umbo lake kisha akakiongoza ." (20:50).

Na ni wake uongofu wa kimazingatio, kama alivyosema: "Hakika sisi tumemuongoa (tumembainishia) njia (ya kheri nay a shari) , basi (mwenyewe tena) atakuwa mwenye kushukuru au kukufuru .(76:3).

Kuhusu Aya Na (13) ni ulimwengu wa mwanzo na ulimwengu wa kurudi; kila kinachohisabika ni kitu basi ni milki yake Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwa milki ya uhakika ambayo inasimamia kupatikana kwa kiti hicho, kisha ndipo inakuja milki wa kimazingatio ambayo katika athari zake ni kujuzu kukifanya lolote.

Kwa hiyo yeye Mwenyezi Mungu (s.w.t) anamiliki kila kitu kwa kila upande hakuna mpinzani anayempinga wala mzuwiyaji atakayemzuwiya, wala hakuna kitu kinachomshinda, kama alivyosema: "Na Allah huhukumu hakuna wa kupinga hukumu yake "(13:41).

Na amesema tena: "Na Allah hufanya apendavyo." (14:27).

Na amesema tena: "Na Allah ndiye mwenye kushinda juu ya jambo lake (alitakalo lazima liwe) ." (12:21).

Aya Na 14-16

Ni mtiririko wa yaliyotangulia; yaani ikiwa uongofu ni juu yetu, basi ninawatahadharisha na moto wa Jahannam. Na kwa hilo anauelekeza msemo katika kauli yake (ninawatahadharisha) kutoka katika wenye kusema wengi kwenda kwa mwenye kusema mmoja pekee, yaani ikiwa uongofu ni wenye kupitishwa, basi muhadharishaji wa asili ni Mwenyezi Mungu ijapokuwa ni kupitia kwa ulimi wa Mtume wake. Makusudio ya moto uwakao ni Jahannam kama alivyosema Mwenyezi Mungu: "Lakini wapi! Kwa hakika huo ni moto uwakao ". (70:15).

Makusudio ya mwovu mno ni kafiri yeyote ambaye anakufuru kwa kukadhibisha na kupa mgongo. Kwani yeye ni mwovu zaidi ya waovu wengine. Mwenye kuwa na balaa katika mwili wake amepata uovu, mwenye kupatwa na balaa katika mali yake au mtoto wake pia amepata uovu na mwenye kupata hasara katika mambo yake ya akhera amekuwa mwovu, lakini huyu ni mwovu zaidi ya wengine kwa vile uovu wake ni wa milele hakuna tamaa ya kuepukana nao. Kinyume cha uovu wa mambo ya kidunia, kwa sababu uovu unakatika na ni wenye kutarajiwa kuondoka haraka.

Kwa hiyo makusudio ya mwovu mno hapa ni kafiri mwenye kukadhibisha mlingano wa haki, kama alivyomwelezea Mwenyezi Mungu kwa kusema: "Ambaye amekadhibisha na akapa mgongo." Ama kusema muovu zaidi ni kwa maana ya muovu wa watu wote ni jambo ambalo halisaidiwi kabia na mpangilio wa maneno. Makusudio ya neno Yaswlaaha ni kuufuata huo moto na kulazimiana nao (kuwa nao) kwa hiyo inafahamisha kudumu kwenye huo moto. Hayo ni katika aliyoyahukumilia Mwenyezi Mungu katika haki ya kafiri, kama alivyosema: "Na wale ambao wamekufuru na wakayakadhibisha maneno yetu hao ni watu wa motoni, watakaa milele humo ." (2:39).

Hilo basi linapinga yale yaliyosemwa kwamba maana ya neno: "Hatauingia ila mwovu mno" kwamba mafasiki katika waislamu hawataingia motoni, isipokuwa inaonyesha kuwa asiyekuwa kafiri hatadumu , lakini atauingia.

Aya Na 17-19

Makusudio ya neno Atqaa ni yule mwenye kumcha Mungu zaidi: Wako watu hucha kupotea nafsi kama kwa kifo au kuuawa, na wengine hucha kuharibika mali na wengine hucha ufakiri, kwa hiyo wanajizuia kutoa mali. Na wengine humcha Mwenyezi Mungu tu; kwa hiyo wanatoa mali. Basi huyu ndiye mwenye kucha zaidi ya wote, anatoa mali kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. Ukipenda unaweza kusema: hucha hasara ya akhera , kwa hiyo anajitakasa kwa kutoa. Yule ambaye hachi kwa kutoa mali anashindwa na huyo anayetoa mali, ijapokuwa hucha mambo ya kidunia au humcha Mungu kwa baadhi ya matendo mema.

Ayah ii inaenea kwa wote na sio mahsusi kwa mtu, kulingana na inavyofahamisha, na kunafahamisha hilo, kumsifu mwenye kucha zaidi kwa aya inayofuatia. "Ambayo hutoa mali yake" hiyo ni sifa ya yeyote yule amayetoa, lakini hili halikanushi kuwa aya au Sura yote imeshuka kwa sababu mahsusi kama ilivyopokewa katika sababu za kushuka. Ama kumuhusisha mbora zaidi mmoja tu! Juu ya watu wote, wabaya au wema katika wote au katika kila zama na iwe maana ni "ataepushwa nao mwenye kucha zaidi ya watu wote, na hatauingia ila mwovu zaidi ya watu wote", ni jambo ambalo halisaidiwi na mpangilio wa aya za mwanzo wa Sura vile vile hakuna maana ya kusema "Ninawahadharisha nyote na moto ambao hatadumu ndani yake ila mmoja katika nyinyi na hataokoka ila mmoja katika nyinyi".

Aya Na (18) ni sifa ya yule mwenye kumcha zaidi yaani ambaye anatoa mali yake hali ya kutaka kwa hilo ziada njema.

Aya Na (19) ni ya kuthibitisha madhumuni ya aya iliyotangulia yaani hana yoyote mbele zake ihsani itakayolipa hiyo ihsani yake isipokuwa anatoa kwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu. HAya Na natiliwa nguvu na aya inayofuatia.

Aya Na 20

Maana yake ni lakini yeye anatoa mali yake hali ya kutaka radhi ya Mola wake Mtukufu. Maelezo zaidi ya Mola Mtukufu yako katika Sura ya 87.

Aya Na 21

Yaani huyu mchaji zaidi ataridhia yale anayopewa na Mola wake Mtukufu kutokana na malipo mema yaliyo mazuri. Kutaja sifa mbili za Mola na Utukufu, ni kufahamisha kwamba yale malipo anayopewa ni malipo ya neema zaidi na ya utukufu zaidi (juu zaidi) nayo ni yenye kunasibiana na Uungu na Utukufu.

Utafiti Wa Hadith Katika Kafi kutoka kwa Muhammad bin Muslim amesema: "Nilimuuliza Abu jaffar(a.s) kuhusu maneno ya Mwenyezi Mungu: "Naapa kwa usiku unapofunika, na naapa kwa nyota zinapoanguka (zinapokuchwa) " na mifano ya hayo. Akaniambia: "Hakika Mwenyezi Mungu anaweza kuapia chochote anachotaka katika viumbe vyake, lakini viumbe haviwezi kumwapia asiyekuwa Yeye (Mwenyezi Mungu). Imepokewa katika Faqih kutoka kwa Ali bin Mahziyar kutoka kwa Abu Jaffar wa pili(a.s) na katika Tafsiri ya Qummi kuhusu Aya Na kwanza anasema: Ni wakati unapofunikwa mchana, na hicho ni kiapo. Kutoka kwa Humayri naye kutoka kwa Ahmad bin Muhammad naye kutoka kwa Ahmad bin Muhammad bin Abu nasr naye kutoka kwa Abul-Hassan Arridhaa(a.s) kuhusu tafsiri ya Sura ya Al-layl anasema:

"Hakika mtu mmoja alikuwa na mtende katika ukuta wa Mtu mwengine na huyo mwenye mtende alikuwa akimdhuru huyo mwengine; akamshtakia Mtume akaitwa yule mwenye na Mtume akamwambia nipe mtende wako kwa mtende wa peponi, akakataa. Na kulikuwepo mtu mwengine anayeitwa Abu Dahdaah aliyesikia hayo akamwendea mwenye mtende akamwambia niuzie mtende wako kwa ukuta wangu akamuuzia. Abu Dahdaah akwamwendea Mtume akamwambia nimeununua mtende fulani: kwa ukuta wangu. Mtume akamwambia "utapata badala yake mtende katika peponi ndipo akateremsha Mwenyezi Mungu: "Na mwenye kuumba kike na kiume. Hakika matendo yenu ni mbalimbali. Ama mwenye kutoa (yaani mtende) na akamcha Allah na akalisadiki jambo jema (yaani lililo mbele ya Mtume(s.a.w.w) mpaka Aya Na 11.

Katika Tafsiri ya Qummi mwenye kucha Mwenyezi Mungu zaidi ni Abu Dahdaah. Hayo ni kwa upande wa Shia kutokana na Maimamu wa Ahlul Bait. Kwa upande wa Ahli Sunna amepokea Tabrasi katika Majmau kwamba kisa hicho kimepokewa kwa Wahidi naye kutoka kwa Akrama naye kutoka kwa Ibn Abbas kwamba Ansari mmoja alipiga bei na mwenye mtende akaununua kwa mitende arubaini, kisha akampa Mtume naye Mtume akampa mwenye nyumba. Amepokea Tabrasi kutoka kwa Ata kwamba jina la huyo mtu ni Abu Dahdaah. Na amepokea Assuyuti katika Durril Manthur kisa hicho kutoka kwa Ibn Abu Hatim naye kutoka kwa Ibn Abbas, lakini ameifanya dhaifu riwaya hiyo.

Imepokewa tena, katika njia ya Ahli Sunna kwamba Sura hii ilishuka kwa Abu Bakr. Amesema Arrazi katika Tafsiri Kabir: "Wamekongamana wafasiri katika sisi kwamba makusudio katika aya ni Abu Bakr. Anaendelea kusema Arrazi: "Jua kwamba Mashia wote wanakanusha riwaya hii, wanasema imeshuka katika haki ya Ali bin Abu Twalib na dalili juu ya hilo ni juu ya aya inayosema: "Na hutoa zaka na hali yakua wao wanaswali " (5:55).

Kwa hiyo neno lake Mwenyezi Mungu: "Mwenye kumcha (Mungu) zaidi ambaye hutoa mali yake kwa kujitakasa " linaishiria kwenye aya hiyo (5:55).

Ama yale yaliyonasibishwa kwa Mashia wote, yenye kutegemewa katika njia zao ni Sahihi ya Al-Himyariyy iliyotangulia kueleza yaliyo katika riwAya Na nayofahamisha kushuka aya kwa Abu-Dahdaah El- Ansari.

Ndio, imekuja riwaya dhaifu kutoka kwa Barqi naye kutoka kwa Ismail bin Mahraan naye kutoka kwa Ayman bin Muhriz naye kutoka kwa Abu Basiyr naye kutoka kwa Abu Abdillah amesema: Ama kauli yake: Na ataepushwa nao mwenye kumcha (Mungu) zaidi, mwenye kumcha (Mungu) zaidi ni Mtume(s.a.w.w) na wafuasi wake na Ambaye hutoa mali yake kwa (kutaka) kujitakasa, huyo ni Amiirul-Mui'miniin Ali(a.s) na ndiyo kauli yake Mwenyezi Mungu: "Na wanatoa zaka na hali wao ni wenye kuswali ." (5:55).

Na kuhusu aya "Na hali ya kuwa hakuna yoyote aliyemfanyia hisani ili awe anamlipa " huyo ni Mtume(s.a.w.w) ambaye hana yoyote wa kumlipa hisani na hali hisani zake ni zenye kuenea kwa watu wote.

Riwaya hiyo ni dhaifu kwa upande wa mapitio yake na kufuatilia kwake bila ya kuangalia tafsir. Dalili iliyowazi ya udhaifu wake ni vile kufuatilia kwake kuwa mwenye kusifiwa ni Mtume na sifa iwe juu ya Ali(a.s) kisha aya inayofuatia tena juu ya Mtume. Na kama hilo lingekuwa katika tafsiri ingeliharibika nidhamu yake kabisa. Na huyo Ayman bin Muhriz hajulikani.

Imepokjewa kutoka kwa Al Himyariyy kutoka kwa Ahmad bin Muhammad bin Abu Nasr naye kutoka kwa Abul hassan Arridha(a.s) amesema: Niliulizwa kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: "Hakika Allah humwongoza anayemtaka na kumpoteza anayetaka. Nikamwambia: Mwenyezi Mungu akufanye uwe mwema "Hakika watu katika watu wetu wanadai mwamba maarifa ni yenye kuchumwa na kwamba wao wakiangalia vizuri wanapata heri". Akakanusha hilo na akasema: "Hawa watu hawachumi heri wao wenyewe, hakuna yeyote katika watu isipokuwa ni wajibu kuwa heri inatokana na yule ambaye heri inatoka kwake.

Ama uongofu ambao makusudio yake ni kufikisha kwenye matakwa, huo ni wa Mwenyezi Mungu kwa sababu ni katika mambo ya Mungu. Ama upotevu ambao makusudio yake ni kupoteza kwa upande wa njia na wala sio kupoteza kwa kuanzia ambako hakuegemezwi kwa Mwenyezi Mungu, ni kwa Mwenyezi Mungu pia, kwa kuwa yeye ni mwenye kuzuwiya kushusha rehema na kukosekana uongofu. Ikiwa uongofu unatokana naye basi kuzuilika nako pia kunatokana naye.

18

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

SURA ADHUHAA (DHUHA)(NA. 93)

INA AYA 11

Kwa jina la Allah, Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu.

وَالضُّحَىٰ ﴿١﴾

1. Naapa kwa mwanzo wa mchana.

وَاللَّيْلِ إِذَا سَجَىٰ ﴿٢﴾

2. Na kwa usiku unapotuwa.

مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ ﴿٣﴾

3. Hakukuacha Mola wako wala hakukukasirikia.

وَلَلْآخِرَةُ خَيْرٌ لَّكَ مِنَ الْأُولَىٰ ﴿٤﴾

4. Hakika akhera ni bora kwako kuliko ulimwengu.

وَلَسَوْفَ يُعْطِيكَ رَبُّكَ فَتَرْضَىٰ ﴿٥﴾

5. Na atakupa Mola wako utaridhia.

أَلَمْ يَجِدْكَ يَتِيمًا فَآوَىٰ ﴿٦﴾

6. Je, hakukuta ni yatima akakuhifadhi?

وَوَجَدَكَ ضَالًّا فَهَدَىٰ ﴿٧﴾

7. Akakukuta umedangana akakuongoza?

وَوَجَدَكَ عَائِلًا فَأَغْنَىٰ ﴿٨﴾

8. Akakukuta ufakiri akakutajirisha.

فَأَمَّا الْيَتِيمَ فَلَا تَقْهَرْ ﴿٩﴾

9. Basi yatima usimdhalilishe.

وَأَمَّا السَّائِلَ فَلَا تَنْهَرْ ﴿١٠﴾

10. Na mwenye kuoma usimkaripie.

وَأَمَّا بِنِعْمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثْ ﴿١١﴾

11. Na neema ya Mola wako, izungumze.

UBAINIFU

Inasemekana kuwa Mtume(s.a.w.w) alikatikiwa na wahyi kwa siku kadhaa mpaka watu wakawa wanasema: "Hakika Mola wake amemwachilia mbali". Basi ndio akateremsha Mwenyezi Mungu Sura hii kuituliza nafsi yake. Sura hii inawezekana kuwa imeshuka Makka au Madina.

Aya Na 1-2

Maana ya neno Dhuhaa ni kuangaza jua na kuenea mchana na neno Sajaa nikutulia yaani kuingia giza.

Aya Na 3

Ni jawabu la kiapo. Mnasaba wa nuru ya mchana na giza la usiku kwa kushuka wahyi na kukatika kwake uko dhahiri.

Aya Na 4

Maana yake kutokana na inavyofahamisha aya iliyotangulia ni kama vile anaambiwa Mtume: Yale uliyonayo miongoni mwa fadhila na rehema ni muda wa kuwa uko hai katika dunia na uhai wako wa akhera ni bora kwako kuliko maisha yako ya dunia.

Aya Na 5

Ni uthibitisho wa aya iliyotangulia na imekusanya kiaga cha kutoa kutakakofuatiwa na kuridhia. Imesemwa aya hii inaangalia pande zote mbili (maisha ya dunia na akhera) na wala sio akhera tu!

Aya Na 6

Inaishiria baadhi ya neema zake Mwenyezi Mungu kwa Mtume; alifiwa na baba yake akiwa tumboni mwa mama yake, kisha akafa mama yake akiwa na miaka miwili, tena akafa (mlezi wake) babu yake naye akiwa na miaka minane, basi ndio akachukuliwa na ami yake kumlea. Inasemekana makusudio ya yatima hapa ni yule mtu aliye peke yake. Kwa hiyo maana inakuwa; Je hakukuta peke yako kati ya watu, akawakusanya watu kwako?

Aya Na 7

Makusudio ya neno Dhwallan ni kudangana kukosa ungofu na makusudio ya kudangana kwake Mtume(s.a.w.w) ni ila hali ya kukatikiwa na ungofu wake Mwenyezi Mungu Mtukufu na hapana uongofu kwa Mtume(s.a.w.w) wala kwa yoyote katika viumbe ila kwa msaada wa Mwenyezi Mungu. Kwa hiyo nafsi yake ilikuwa imedangana, ijapokuwa uongofu wa Mwenyezi Mungu ni wenye kulazimiana naye. Aya hii iko katika maana na aya inayosema: "Ulikuwa hujui kitabu nini wala imani " (42:52).

Vile vile iko katika maana ya neno la Musa, kama anavyosimulia Mwenyezi Mungu katika Qur'an. "nimeyafanya hayo nilipokuwa miongoni mwa waliodangana ." (26:20) yaani wakati bado sijapata uongofu wa utume.

Yanakurubia maana hayo na yale yaliyosemwa kuwa makusudio ya Dhwallan ni kuondokewa na elimu (kutokujua) kama ilivyo katika kauli yake Mwenyezi Mungu."..ili kama mmoja wao akipotea, mmoja wao amkumbushe mwengine " (2:282).

Hayo yanatiliwa nguvu na kauli yake Mwenyezi Mungu: "na hakika ulikuwa kabla ya haya ni miongoni mwa wasio na habari hizi ." (12:3).

Imesemwa maana yake ni akakukuta umepotea kati ya watu hawajui haki yako akawaongoza kwako na akawajulisha kuhusu wewe.

Imesemwa ni ishira ya kupotea njia ya Makka alipokuwa mdogo. Pia imesemwa ni ishara ya kupotea kwake ndani ya msafara wa Maysara mtumishi wa Khadija, wakati alipokwenda Sham pamoja na ami yake, Abu Twalib. Na yamesemwa zaidi ya hayo ni hizo zote ni njia dhaifu.

Aya Na 8

Fukara ni yule ambaye hana mali. Alikuwa Mtume(s.a.w.w) ni fukara akatajirishwa na Mwenyezi Mungu baada ya kumuoa Bibi Khadija ambaye alikuwa na mali nyingi akampa Mtume.

Aya Na 9-11

Aya zote hizi tatu zinatokana na aya zilizotangulia na zinataja wema wake Mwenyezi Mungu (s.w.t), ni kama anasema: "Umeyapata yale yanayompata yatima katika udhalili na upweke kwa hiyo basi usimdhalilishe yatima kwa kuidhalilisha nafsi yake au mali yake." Na mara nyingi umeipata haja ya mwenye kupotea vile anavyohitajia uongofu na fakiri anavyohitajia utajiri, basi usimkaripie mwenye kuomba kuondolewa haja yake ya uongofu au maisha. Vile vile umeona kuwa neema ulizonazo amekuneemesha Mola wako kwa ukarimu wake, basi ishukuru neema yake kwa kuizungumza wala usiifiche. Maamrisho yote haya ni kwa watu wote ingawaje yanaelekezwa kwa Mtume.

Utafiti Wa Hadith Katika Tafsiri ya Qummi kuhusu neno la Mwenyezi Mungu Dhuhaa anasema ni wakati wa kupanda jua na Sajaa anasema ni wakati wa giza. Na kuhusu neno la Mwenyezi Mungu Maqalaa anasema ni "hakukukasirikia". Katika Durril Manthur kuhusu Aya Na tano, ametoa Ibn Abu Shayba kutoka kwa Ibn Masud amesema: "Amesema Mtume(s.a.w.w) "Sisi Ahlul Bait Mwenyezi Mungu ametuchagulia akhera kuliko dunia ."

Katika hiyo hiyo Durril Manthur ametoa Askary katika Mawaidh, Ibn Laali na Ibn Najjar kutoka kwa Jabir bin Abdillahi amesema; "Mtume(s.a.w.w) aliingia kwa Fatima akiwa anatwanga kwa jiwe huku amevaa nguo za sufu za ngamia". Alipomwangalia akasema: "Ewe Fatima fanya haraka umeze uchungu wa dunia kwa neema na akhera kesho." Akateremsha Mwenyezi Mungu aya hiyo ya tano. Riwaya hii inachukulia kuwa aya hiyo ilishuka peke yake baada ya kushuka aya zilizo kabla yake katika Sura hii kisha kuunganishwa. Kuna uwezekano wa Aya hiyo kushuka peke yake kwa mara nyingi.

Katika hiyo hiyo Durril Manthur ametoa Ibn El Mundhir,Ibn Murdawayh na Abu naim katika Hilyat kutoka katika njia ya Harb bin Sharih amesema:"Nilimwambia Abu jaffar Muhammad bin Ali bin Hussein(a.s) unaonaje hii Shafaa (uombezi) wanayoizungumzia watu wa Iraq ni kweli? Akasema: "Kabisa Wallah". Alinizungumzia Ami yangu Muhammad bin El-Hanafiya kutoka kwa Ali kwamba Mtume(s.a.w.w) alisema: "nitauombea shafaa umati wangu mpaka Mola wangu anisemeshe: Umeridhika ewe Muhammad? Na nisema: Ndio ewe Mola wangu nimeridhika." Kisha akanikabili na kuniambia: "Hakika nyinyi watu wa Iraq mnasema: Hakika aya yenye kutarajiwa zaidi katika kitabu cha Mwenyezi Mungu ni ile inayosema: "Sema, enyi waja wangu mliojidhulumu nafsi zenu! Msikate tamaa na Rehema ya Allah; Hakika Mwenyezi Mungu husamehe dhambi zote " (39:53). Nikasema ndio sisi tunasema hivyo. Akasema: Basi sote sisi Ahlul Bait tunasema: "Hakika aya inayotarajiwa zaidi katika kitabu cha Mwenyezi Mungu ni ile inayosema: "Na atakupa Mola wako nawe utaridhia". Yaani uombezi. (Aya Na tano katika Sura hii).

Katika Tafsiri ya Burhan kutoka kwa Baabwayh kwa isnadi ya Ibn Jaham kutoka kwa Ridhaa(a.s) katika kikao pamoja ya Maamun alisema huyo Ridhaa; "Anasema Mwenyezi Mungu (s.w.t) kumwambia Mtume wake Muhammad(s.a.w.w) . "Je hakukuta ni yatima akakuhifadhi?" Anasema: "Je hakukuta peke yako akakusanyia watu? Na akakukuta umedangana yaani mbele ya watu wako "akakuongoa" yaani akawongoa watu wakakufahamu. Na akakukuta ufakiri akakutajirisha". Anasema "akakutajirisha kwa kujaalia dua yako ni yenye kutakabaliwa?" Akasema Maamun: "Mwenyezi Mungu akubarikie ewe mtoto wa Mtume wa Mwenyezi Mungu".

Katika hiyo hiyo Tafsiri ya Burhan kutoka kwa Barqi kwa isnadi yake kutoka kwa Amru bin Abu Nasr amesema: Alinizungumzia mtu mmoja katika watu wa Basra akasema: "Nilimuona Hussein bin Ali(a.s) na Abdallah bin Umar wanatufu Al-Kaaba. Nikamuuliza Ibn Umar: Kuhusu neno lake Mwenyezi Mungu "Na neema ya Mola wako izungumze", Akasema : "Ni kuzungumza aliyoneemesha Mwenyezi Mungu." Kisha nikamuuliza Hussein bin Ali(a.s) akasema: "Nikuzungumza aliyoneemesha Mwenyezi Mungu katika dini yake." Katika Durril Manthur kutoka kwa Bayhaqi naye kutoka kwa Hassan bin Ali kuhusu ayay hiyo ya 11 akasema: "Ukipata heri wazungumzie ndugu zako".

Katika hiyo Durril Manthur ametoa Abu Dawud kutoka kwa Jabir bin Abdillahi kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) amesema: "Mwenye kujaribiwa kwa kupewa misukosuko akaizungumza, hakika huyo amemshukuru Mwenyezi Mungu, na mwenye kuficha atakuwa amemkanusha (uweza) wa Mwenyezi Mungu. Na mwenye kujinasibishia asilokuwa nalo, hakika yeye ni kama amevaa nguo za uzushi.


11

12

13

14

15

16