TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN12%

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: tafsiri ya Qurani

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN
  • Anza
  • Iliyopita
  • 29 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 42546 / Pakua: 4762
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

Mwandishi:
Swahili

1

2

3

4

5

6

14

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

SURA AL-FAJR (ALFAJIRI) (NA. 89)

INA AYA 30

Kwa jina la Allah, Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu

وَالْفَجْرِ ﴿١﴾

1. Naapa kwa Alfajiri.

وَلَيَالٍ عَشْرٍ ﴿٢﴾

2. Na (kwa) masiku kumi.

وَالشَّفْعِ وَالْوَتْرِ ﴿٣﴾

3. Na (kwa) shufwa na witiri.

وَاللَّيْلِ إِذَا يَسْرِ ﴿٤﴾

4. Na (kwa) usiku unapopita.

هَلْ فِي ذَٰلِكَ قَسَمٌ لِّذِي حِجْرٍ ﴿٥﴾

5. Katika hayo mna kiapo kwa mwenye akili.

أَلَمْ تَرَ كَيْفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍ ﴿٦﴾

6. Je, hujui jinsi Mola alivyoifanya (kabila) ya Aad.

إِرَمَ ذَاتِ الْعِمَادِ ﴿٧﴾

7. Iram wenye nguzo ndefu?

الَّتِي لَمْ يُخْلَقْ مِثْلُهَا فِي الْبِلَادِ ﴿٨﴾

8. Ambayo haikuumbwa mfano wake katika miji.

وَثَمُودَ الَّذِينَ جَابُوا الصَّخْرَ بِالْوَادِ ﴿٩﴾

9. Na (kabila) ya Thamud ambao walikua wakipasua majabali katika (mji wa) waad.

وَفِرْعَوْنَ ذِي الْأَوْتَادِ ﴿١٠﴾

10. Na Firaun mwenye vigingi.

الَّذِينَ طَغَوْا فِي الْبِلَادِ ﴿١١﴾

11. Ambao walipetuka mipaka katika miji.

فَأَكْثَرُوا فِيهَا الْفَسَادَ ﴿١٢﴾

12. Wakazidisha humo mambo maovu.

فَصَبَّ عَلَيْهِمْ رَبُّكَ سَوْطَ عَذَابٍ ﴿١٣﴾

13. Akawateremshia Mola wako namna za adhabu.

إِنَّ رَبَّكَ لَبِالْمِرْصَادِ ﴿١٤﴾

14. Hakika Mola wako ni Mwenye kuotea.

فَأَمَّا الْإِنسَانُ إِذَا مَا ابْتَلَاهُ رَبُّهُ فَأَكْرَمَهُ وَنَعَّمَهُ فَيَقُولُ رَبِّي أَكْرَمَنِ ﴿١٥﴾

15. Ama mwanadamu - Mola wake anapomjaribu, akamtukuza, akamneemesha, husema: Mola wangu amenitukuza.

وَأَمَّا إِذَا مَا ابْتَلَاهُ فَقَدَرَ عَلَيْهِ رِزْقَهُ فَيَقُولُ رَبِّي أَهَانَنِ ﴿١٦﴾

16. Ama anapomjaribu akampunguzia riziki yake husema Mola wangu amenitweza.

كَلَّا بَل لَّا تُكْرِمُونَ الْيَتِيمَ ﴿١٧﴾

17. La, si hayo tu! Bali nyinyi humumtukuzi yatima.

وَلَا تَحَاضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ الْمِسْكِينِ ﴿١٨﴾

18. Wala hamhimizani katika kumlisha maskini.

وَتَأْكُلُونَ التُّرَاثَ أَكْلًا لَّمًّا ﴿١٩﴾

19.Na mnakula mirathi kula kwa pupa.

وَتُحِبُّونَ الْمَالَ حُبًّا جَمًّا ﴿٢٠﴾

20. Na mnapenda mali mapenzi makubwa.

كَلَّا إِذَا دُكَّتِ الْأَرْضُ دَكًّا دَكًّا ﴿٢١﴾

21. Si hivyo! Ardhi itakapo pondwa pondwa!

وَجَاءَ رَبُّكَ وَالْمَلَكُ صَفًّا صَفًّا ﴿٢٢﴾

22. Akaja Mola wako na Malaika (wamejipanga) safu kwa safu.

وَجِيءَ يَوْمَئِذٍ بِجَهَنَّمَ ۚ يَوْمَئِذٍ يَتَذَكَّرُ الْإِنسَانُ وَأَنَّىٰ لَهُ الذِّكْرَىٰ ﴿٢٣﴾

23. Ikaletwa siku hiyo Jahannam! Siku hiyo ndipo mwanadamu atakapokumbuka, lakini kutamfaa nini kukumbuka (kwake)?!

يَقُولُ يَا لَيْتَنِي قَدَّمْتُ لِحَيَاتِي ﴿٢٤﴾

24. Atasema laiti niliyatangulizia (wema) maisha yangu.

فَيَوْمَئِذٍ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُ أَحَدٌ ﴿٢٥﴾

25. Basi siku hiyo hapana yoyote atakayeadhibu kama adhabu yake (Mwenyezi Mungu).

وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُ أَحَدٌ ﴿٢٦﴾

26. Wala hapana yoyote atakayefunga kama kufunga kwake.

يَا أَيَّتُهَا النَّفْسُ الْمُطْمَئِنَّةُ ﴿٢٧﴾

27. Ewe nafsi iliyotua!

ارْجِعِي إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةً مَّرْضِيَّةً ﴿٢٨﴾

28. Rejea kwa Mola wako hali yakuwa uradhi (na) mwenye kuridhiwa.

فَادْخُلِي فِي عِبَادِي ﴿٢٩﴾

29. Kisha ingia katika waja wangu (wema).

وَادْخُلِي جَنَّتِي ﴿٣٠﴾

30. Na uingie katika pepo yangu.

UBAINIFU

Katika Sura hii kuna makemeo juu ya kufungamana na dunia kwenye kufuatiwa na kupetuka mpaka na ukafiri, na kuwaogopesha watu wenye mambo hayo na ukali wa adhabu ya Mwenyezi Mungu katika dunia na akhera. Kwa hiyo Sura inabainisha kuwa mtu kwa ufupi wa mtazamo wake na ubaya wa fikra yake anaona kuwa anayoletewa na Mwenyezi Mungu miongoni mwa neema yake ni katika ukarimu wake Mwenyezi Mungu, na yale anayovaana nayo miongoni mwa ufakiri ni utwezo. Kwa hiyo anapetuka mpaka na kuwa mfisadi katika ardhi anapopata na anakufuru anapokosa. Basi yanayompata katika cheo na utajiri na katika ufakiri na dhiki ya maisha, ni mitihani na balaa za Mungu ili adhihirishe kwayo yale atakayoyatanguliza akhera yake kutoka katika dunia yake.

Basi mambo hayako kama vile anavyofikiri mtu na anavyosema, bali mambo yalivyo kama atakavyoyakumbuka itakapotuka hisabu na kuletwa adhabu, kwamba yaliyompata miongoni mwa ufakiri au utajiri na nguvu au unyonge yalikuwa ni mitihani ya Mungu. Ilikuwa inamuwezekania yeye kutangulizia kesho yake kutokana na leo yake, lakini hakufanya na akaathirika na mateso kuliko thawabu. Basi haitapata maisha mema katika akhera isipokuwa nafsi iliyotua kwa Mola wke, isiyoyumba kwa vimbunga vya balaa wala kupetuka mpaka kwa kipato au kukufuru kwa kukosa. Sura hii imeshuka Makka kwa ushahidi wa mpangilio wa aya zake.

Aya Na 1-4

Aya hizo zote ni kiapo. Huenda dhahiri ya neno Alfajiri, Alfajiri yoyote, lakini sio mbali kuwa makusudio yake ni Alfajiri ya usiku wa Ijumaa. Imesemwa ni swala ya Alfajiri na imesemwa ni mchana wote na imesemwa ni kupasuka chemchem katika miamba na mengineyo. Njia zote hizi ziko mbali. Kuhusu masiku kumi huenda makusudio ni masiku kumi ya mwanzo katika mwezi wa Dhulhijja. Imesemwa makusudio ni siku za mwisho za mwezi wa Ramadhan, na ikasemwa ni za mwanzo wake. Pia imesemwa ni siku kumi za mwanzo za mwezi wa Muharram na ikasemwa kuwa ni ibada ya masiku kumi kuchukulia kuwa makusudio ya Alfajiri ni swala ya Alfajiri. Kuhusu Shufwa wa Witiri maana yanakubali kufungamana na kuwa ni siku wa Tarwiya (tarehe 8 Dhul-hijja) na siku ya Arafa (tarehe 9 Dhul-hijja). Imesemwa kuwa makusudio yake ni swala mbili ( rakaa mbilimbili na rakaa moja) katika mwisho wa usiku. Na imesemwa ni swala yoyote, ziko mbili mbili na moja.

Pia imesemwa kuwa Shufwa ni siku ya Idd ya Dhul-hijja wa Witiri ni siku ya Arafa, na imesemwa Shufwa ni viumbe vyote, kwa sababu Mwenyezi Mungu anasema: "Na tukawaumba wanawake na wanaume " (78:8).

Na Witiri ni Mwenyezi Mungu (s.w.t) Kuna riwaya nyingi zitakazokuja juu ya kauli hizi katika utafiti wa hadith 8 Vile Vile imesemwa makusudio yake ni hisabu ya viwiliviwili na kimojakimoja na kwamba kuapa kwa hisabu, ni kuwa kudhibiti idadi katika kiasi ni katika nema kubwa itokayo kwa Mwenyezi Mungu. Imesemwa kuwa ni viumbe vyote, kwa sababu vitu vyote ama vitakuwa ni jozi au kimoja. Imesemwa kuwa makusudio ya Witiri ni Adam na Shufwa ni kuwa pamoja na mkewe Hawa.

Na imesemwa Shufwa ni mchana, na usiku, na Witiri ni mchana ambao, hauna usiku nao ni siku ya Kiyama. Imesemwa Shufwa ni Safa na Marwa na Witiri ni Al-Ka'aba, na imesemwa ni siku za kabila la Ad na Witiri ni nyusiku zake. Na imesemwa Shufwa ni milango ya motoni saba. Na zaidi ya hayo mengi yaliyosemwa zaidi ya kauli thelethini na sita (36). Kuhusu kauli yake; Na (kwa) usiku unapopita ni kama Aya Na 33, Sura ya 74 inayosoma: "Na (kwa) usiku unapokucha".

Kwa dhahiri herufi Lam ni ya jinsi yaani usiku wowote, lakini wengine wamesema ni usiku wa Muzdalifa (usiku wa kuamkia Idd) ambao mahujaji wanapita kutoka Arafa mpaka Muzdalifa wanakusanyika Mahujaji kwa kumtii Mwenyezi Mungu kisha wanaamkia kwenda Mina kwa hiyo kama unavyoona itakuwa makusudio ya usiku kumi ni usiku kumi za mwanzo katika mwezi wa Hijja (Dhul-Hijja).

Aya Na 5

Ni ishara ya yaliyotangulia katika kiapo na ni swali la kuthibitisha, maana yake kwa ujumla, ni kwamba, katika hayo tuliyoyatanguliza kuyaapia yanatosha kwa mwenye akili ya utambuzi wa maneno inayopambanua haki na batili. Na Mwenyezi Mungu akiapa naye haapi isipokuwa lile lenye utukufu na daraja linakuwa ni neno la haki lenye kutiliwa mkazo ambalo halina shaka katika ukweli wake. Jawabu la kiapo limeondolewa linafahamika kutokana na yatakayotajwa katika adhabu ya watu waliopetuka mipaka na ukafiri katika dunia na akhera na thawabu ya nafsi yenye kutulia na kwamba kuneemesha kwake Mwenyezi Mungu (s.w.t) juu ya aliyomneemesha na kumzuilia, hakika hayo ni majaribio na mitihani. Kuondoa jawabu la kiapo na kulileta kwa njia ya fumbo, ni kutilia mkazo zaidi katika hali ya kuonya na kutoa biashara.

Aya Na 6

Ni kabila la Aad wa kwanza nao ni kaumu ya Mtume Hud(a.s) . Vimekaririka visa vyao katika Qur'an tukufu na imeonyesha kwa wao walikuwa watu wa nchi yenye machunguu ya michanga. Yameelezwa yale yanayopatikana katika visa vyao katika Sur ya Hud (11).

Aya Na 7-8

Neno Imad ni nguzo za nyumba. Kwa dhahiri ya aya mbili hizi, ni kuwa Iram ulikua ni mji uliokuwa wa aina yake wenye majumba marefu na maguzo marefu. Hakika habari zao zimekatika na athari zao zimefutika, kwa hiyo hakuna njia ya ufafanuzi itakayoeleza hali zao kiasi cha kuituliza nafsi isipokuwa yale tu, yaliyohadithiwa na Qur'an tukufu kwa ujumla juu ya kisa chao; kwamba wao walikuwa baada ya kaumu ya Nuh, wakazi wa nchi yenye machuguu ya mchanga, na walikuwa ni wenye umbo kubwa na nguvu kubwa zaidi na walikuwa na maendeleo, miji yenye majengo mengi ardhi za rutuba zenye mabustani ya mitende na mimea na mahali pazuri. Kimeelezewa zaidi kisa chao katika Sura ya Nuh.

Imesemwa kuwa makusudi ya neno Iram ni hao kaumu ya Aad - na sili na neno hilo ni jina la baba yao kwa hiyo wakaitwa kwa jina la baba yao, kama inavyosemwa Quraish kwa kukusudia wanawe au Israil kwa kukusudia wana Israil. Makusudio ya kusema wenye maguzo marefu ni kuwa wao ni watu wenye nguvu, na maana yake ni Je, hujui jinsi Mola wako alivyoifanya (kabila) ya Aad Iram wenye nguvu ambao haukumbwa mfano wao katika miji, au katika dunia nzima, lakini hayo hayaepukani na kuwa mbali na dhahiri ya tamko. Ya umbali zaidi ya yaliyosemwa kwamba makusudio ya kuwa wao ni wenye maguzo marefu, ni vile kuwa wao walikuwa ni watu wa kuazimia kusafiri katika wakati wa maleleji na mimea inaponyauka basi hurudi majumbani mwao. Kisa cha bustani ya Iram kilichopokewa kutoka kwa Wahb bin Manbih na Kaabulahbar, ni katika ngano za watu wakale tu!

Aya Na 9

Yaani walipasua miamba ya milima kwa kuichonga kuwa nyumba. Aya hii iko katika maana ya aya inayosema: "Na mnachonga milimani majumba mkastarehe tu! " (26:149)

Aya Na 11

Huyo ni Firaun wa Musa, ameitwa mwenye vigingi- kutokana na yaliyo katika baadhi ya riwaya - kwamba yeye alikuwa akitaka kumuadhibu mtu humnyoosha juu ya ardhi na kuipingilia mikono yake na miguu yake kwa vigingi vine katika ardhi, au humnyoosha juu ya ubao na kumfanyia hivyo. Hayo yanatiliwa nguvu na yale aliyoyasimulia Mwenyezi Mungu kuhusu kauli yake Firaun akiwatisha wachawi walipomwamini Musa kwa kusema: "Nitawasulubu katika mashina ya mitende ." (20:71).

Hakika wao walikuwa wakiwamba mikono ya msulubiwa na miguu yake juu ya ubao wa kusulubu.

Aya Na 12

Ni sifa wa waliotajwa, Ad, Thamud na Firaun, maana yako wazi.

Aya Na 13

Ametaja kumimina kwa njia ya fumbo kwa maana ya kufuatana, maana yake ni kuwa Mwenyezi Mungu aliteremsha kwa mataghut wote hawa wenye kukithirisha uharibifu mara tu, baada ya kupetuka kwao mipaka na ufisadi wao, adhabu kali ya aina yake yenye kufuatana mfululizo.

Aya Na 14

Kuwa Mwenyezi Mungu yuko katika kuotea, ni istiara ya kufananisha Mwenyezi Mungu anavyochunga matendo ya waja wake na mtu anayeotea mtu apite amchukue, bila ya kutambua. Basi Mwenyezi Mungu anachunga matendo ya waja wake, wakipetuka mipaka na kukithirisha ufisadi tu, huwaadhibu kwa adhabu kali. Aya hiyo ni sababu ya yaliyotangulia katika mazungumzo ya kuadhibu wanaopetuka mipaka wenye kukithirisha ufisadi. Kuongeza dhamira katika neno Mola na kuwa "mola wako", ni kuonyesha kuwa desturi hiyo ya adhabu ilikuwa ni yenye kupita katika umma wake Mtume(s.a.w.w) kama ilivyopita katika umati zilizotangulia.

Aya Na 15

Ni mtiririko wa yaliyotangulia, ndani yake mna ufafanuzi kuhusu hali ya mtu anapopewa neema ya dunia au anapozuiliwa, ni kama vile imesemwa: Hakika mtu yuko chini ya ulinzi wa Mungu, anaotewa na Mola wake kuwa je, atatengenea au ataharibika?. Kwa hiyo anamjaribu na kumtahini katika yale atakayompa katika neema yake au kunyima kwake. Ama mtu yeye akineemeshwa huhisabu kwamba huo ni utukuzo wa Mungu kwa hiyo anaweza kufanya vile anavyotaka. Hivyo anapetuka mipaka na kukithirisha ufisadi. Na akimzuilia na kuifanya chache riziki yake, huhisabu kuwa ametwezwa na Mungu, basi hukufuru na kulalamika Makusudio ya mtu ni jinsi ya mtu. Kusema kwake: akamtukuza akamneemesha ni tafsiri ya majarabio yaani Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemtukuza na akampa nema iliamshukuru na amuabudu, lakini yeye mtu mwenyewe anajaalia ni mateso juu ya nafsi yake yanayofuatiwa na adhabu. Kuhusu neno "husema Mola wangu amenitukuza" yaani amenijaalia juu ya ukarimu unaotokana naye kwa neema ambazo amenipa, kwa hiyo ninaweza kufanya lile ninalo taka.

Kusema "Mola wangu amenitukuza" kuko katika mnasaba wa kumzingatia Mungu - hayo hayasemwi na waabudu masanamu na wanaomkanusha Mungu - na ni kwenye kujengwa juu ya kumkubali Mungu kwa kiasi cha maumbile yalivyo ijapokuwa ulimi unajizuia na hilo, vile vile aya inayofuatia.

Aya Na 16

Yaani akifanya mtihani ikawa dhiki riziki yake, basi husema Mola wangu amenidhalilisha. Kutokana na aya hizi (15 na 16) yanadhihirika mambo yafuatayo:

Kwanza : Kukaririka majaribio na kuthibitika katika sura mbili za neema na kuzuiliwa, ni kwamba kupewa neema na kuzuiliwa vyote ni katika majaribio na mitihani ya Mungu kama alivyosema: "Tutawajaribu kwa (mambo) ya shari na heri " (21:35).

Pili : Kupewa neema kwa kuwa ni fadhila na rehema, ni utukufu iwapo wanadamu hawakukubadilisha kuwa adhabu. Tatu: Mtu anaona wema wake katika maisha ya dunia ni kuneemeshwa katika dunia ka neema za Mwenyezi Mungu, hivyo anaona ndio utukufu na kunyima kunakotokana na Mwenyezi Mungu anakuona kuwa ni uovu. Ilivyo nikuwa, utukufu uko katika kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu kwa imani na amali njema, ni mamoja iwe ni utajiri au ufakiri, kupata au kukosa, yote hayo ni mitihani. Wanayo maana nyengine kuhusu aya hizi mbili lakini tumeacha kuyaonyesha kwa kutokuwa na umuhimu wowote.

Aya Na 17

Na makemeo kwa yale wanayoyasema kwamba utukufu uko katika utajiri na kwamba ufakiri na kukosa ni madhila. Basi si hivyo isipokuwa kutoa kwake Mwenyezi Mungu (s.w.t) neema, na kuizuia yote hayo ni mitihani anayojaribiwa mtu. Kusema kwake Mwenyezi Mungu: Bali nyinyi hamumtukuzi yatima, ni kutilia mkazo makemeo kwa kutaja baadhi ya neema ambayo haikusanyi utukufu kabisa, kama kukosa kumtukuza yatima kwa kula urathi wake na kumzuilia nao na kukosa kuhimizana juu ya kumlisha maskini kwa ajili ya kupenda mali. Kuacha kumtukuza yatima ni kumzuilia na urathi wa mzazi wake kama walivyokuwa wakiwazuilia watoto wadogo na kurithi, kama inavyotia nguvu aya inayofuatia.

Aya Na 18

Yaani hamuhimizani kutoa sadaka. Hayo yanatokana na kupenda mali sana kama ilivyo katika aya inayofuatia.

Aya Na 19

Maana ya neno Lamma ni mtu kula fungu lake na la mwengine, na kula chochote anachokipata kiwe kibaya au kizuri. Aya hii ni tafsiri ya kukosa kumtukuza yatima kama iliyotangulia.

Aya Na 20

Aya hiyo nayo inafasiri kukosa kuhimizana katika kumlisha maskini kama ilivyotangulia.

Aya Na 21

Makusudio yake ni kufika siku ya Kiyama. Hilo ni kemeo la pili kutokana na yale anayoyasema mtu katika hali mbili za utajiri na ufakiri. Aya hii inasimamia sababu za makemeo kwa maana ya kuwa, sio kama anavyosema mtu, kwani yeye atakumbuka kitakaposimama Kiyama kwamba maisha ya dunia na vilivyomo ndani yake miongoni mwa utajiri na ufakiri sio makusudio kwa dhati, bali yamekuwa ni majaribio na mitihani kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) Anapambanua kutokana na mitihani hiyo mwema na mwovu na inamuandalia mtu yale atakayoishi kwayo katika akhera. Hakika mtu ametatizika akadhania kuwa utukufu ndio makusudio kwa dhati akajishughulisha nao na wala asitangulize chochote kwa maisha yake ya Akhera. Kwa hiyo wakati huo atatamani huku akisema: Laiti mimi niliyatanguliza (wema) maisha yangu, lakini matamani hayatatoshelezea lolote na adhabu.

Aya Na 22

Kunasibisha kuja Mungu ni katika mikanganyo ambayo inahukumuliwa na kauli yake Mwenyezi Mungu (s.w.t) "Hakuna chochote mfano wake " (42:11). Na yaliyokuja katika alama za Kiyama, ni katika upambanuzi wa kuondoa sababu na mapazia yaliyowaziba na kushihiri kwamba Mwenyezi Mungu ni haki iliyo wazi. Kwa hiyo yale yaliyopokewa katika hadith yanalirudia hilo kwamba makusudio ya kuja kwake Mwenyezi Mungu (s.w.t) ni kuja amri yake kama alivyosema Mwenyezi Mungu: "Na amri siku hiyo ni ya Allah " (82:19).

Kunatilia nguvu njia hii kusema kwake Mwenyezi Mungu: "Je, kuna jengine wanalongojea ila kuwafikia Allah katika vivuli vya mawingu na kuwafikia malaika na imekwishapitishwa amri ". (2:210).

Kama tukikikutanisha na kusema kwake. "Je, wanangoja jengine (hawa makafiri) ila wawafikie Malaika? Au iwafikie amri ya Mola wako? " (16:33). Kwa hiyo basi kuna neno lililondolewa, kukadiria kwake ni: ikaja amri ya Mola wako. Au kunasibisha kuja Mungu ni kwa majazi (fumbo) ya kiakili.

Aya Na 23

Sio mbali kuwa makusudio ya kuletwa Jahannam ni kudhihirishwa, kama ilivyo katika kauli yake. "Basi tumekuondolea pazia yako kuona kwako leo kumekuwa kukali " (50:22).

Kusema kwake "Siku hiyo atakumbuka mtu" yaani atakumbuka kwa uwazi zaidi kwamba yale yaliyokuwa yakimjia katika maisha ya dunia miongoni mwa heri au shari yalikuwa ni majaribio ya Mwenyezi Mungu na mitihani yake na yeye akapuuza. Hivyo ndivyo unavyofahamisha mpangilio wa maneno. Kusema kwake "wapi kutamfaa kukumbuka" ni fumbo la kukosa kunufaika na kukumbuka isipokuwa kukumbuka kungefaa kama angekuunganisha na kutubia na kutenda amali njema kwa yale aliyoyapuuza, na leo ni siku ya malipo sio siku ya kutubia na kufanya amali.

Aya Na 24

Maisha hapa ni ya akhera au ni maisha ya kihakika ambayo ndiyo hayo maisha ya akhera, kama kulivyozindua kusema kwake: "Na hayakuwa haya maisha ya dunia ila ni upuzi na mchezo; na nyumba ya akhera ndio maisha hasa: Laiti wangalijua ". (29:64) Makusudio ya kuyatanguliza maisha ni kuyatangulizia amali njema.

Aya Na 25-26

Dhamir katika neno adhabu na kufunga inamrudia Mwenyezi Mungu. Yaani siku hiyo hakika adhabu yake na kufunga kwake kutakuwa zaidi ya adhabu ya kiumbe chochote. Wengine wamesoma kwa Fat'ha ya Dhali na Thau. Dhamir kwa kisomo hiki itakuwa inamrudia mtu, yaani hataadhibishwa yoyote siku hiyo mfano wa adhabu ya mtu wala hatafungwa yoyote siku hiyo mfano wa kufunga kwa mtu.

Aya Na 27

Mpangilio wa maneno uonaokubaliana na 'nafsi' hii kutokana na yale yaliyotajwa kabla yake katika sifa zinazofungamana na dunia, upitukaji mipaka, ufisadi na ukafiri na yale yaliyoahidiwa katika mwisho mbaya, unaonyesha kuwa nafsi yenye kutulia ni ile inayotulizana kwa Mola wake na kurudhia kile kinachoridhiwa na Mola wake, inajiona kuwa ni mtumwa asiyejimiliki na chochote katika kheri na inaiona dunia ni nyumba ya kupita, na inayoyakabili katika hiyo dunia miongoni mwa utajiri au ufakiri, manufaa au madhara, ni majaribio na mitihani ya Mungu. Kwa hiyo mtiririko wa neema haumpelekei kupetuka mipaka, kufanya ufisadi mwingi au kujifanya mkubwa wala ufakiri na kukosa kitu hakumuingizi katika ukafiri na kuwacha kushukuru, bali yeye ni mwenye kutulizana, hakosei njia yake yenye kunyooka kwa kupetuka mipaka au kuwapitusha mipaka wengine.

Aya Na 28

Kuisifu nafsi kwa hali yakuwa radhi ni kwamba kutulizana kwale kwa Mola wake kunalazimisha kuridhia kwake yale yaliyokadiriwa na kuhukumiliwa na wala hayamchukizi. Mtu akimridhia Mola wake naye humridhia, kwani Mwenyezi Mungu S.W.T. huchukia sana kutoka mja katika kipambo chake. Basi akilazimiana na njia ya kuwa mja wa Mwenyezi Mungu, litawajibisha hilo radhi ya Mola wake, kwa hiyo ndio maana hali ya kuridhia imefuatishwa na kuridhiwa.

Aya Na 29

Inaungana na aua iliyotangulia inafahamisha kuwa mwenye nafsi yenye kutulia yuko katika kundi la waja wa Mwenyezi Mungu. Hilo ni kwamba alipotulia kwa Mola wake alijiondoa kujiona huru, na akaridhia ile iliyohaki kwa Mola wake, akaona dhati yake, sifa zake na vitendo vyake ni miliki ya Mola wake. Hakupita katika yaliyokadiriwa kuhukumiliwa wala katika yaliyo amrishwa na kukatazwa isipokuwa yale anayoyataka Mola wake. Huko ndiko kudhihiri uja wenye kutimia. Kwa hiyo kusema kwake "ingia katika waja wangu" ni ikrari ya mahali pa uja wake hiyo nafsi. Neno lake "na ingia katika pepo yangu" ni kubainisha kituo chake. Kuitegemeza pepo kwa dhamiri ya mwenye kusema (pepo yangu) ni utukuzo mahsusi wala halipatikani hilo katika maneno yake Mwenyezi Mungu (s.w.t) isipokuwa katika aya hii tu!.

Utafiti Wa Hadithi Katika Majmau kuhusu kusema kwake "na (kwa) Shufwa na Witiri, imesemwa kuwa Shufwa ni kuumba kwa sababu Mwenyezi Mungu amesema: "Na tukawaumba nyinyi wanaume na wanawake (jozi) " (78:8). na Witiri ni Mwenyezi Mungu Mtukufu. Hadithi hiyo imeyoka kwa Atiyal-Aufiy, Abu Saleh, Ibn Abbs na Mujahid, hiyo ni riwAya Na Abu Saad El-Khudriy naye amepokea kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) .

Imesemekana kuwa Shufwa na Witiri ni swala: kuna katika hiyo swala ya Shufwa na ya Witiri. Hiyo ni riwAya Na Ibn Haswin naye amepokea kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) .

Imesemwa kuwa Shufwa ni siku ya kuchinja na Witiri ni siku ya Arafa, kutoka kwa Ibn Abbas Akrama na Adh-Dhah-hak nayo ni riwAya Na Jabir kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) .

Imesemwa kuwa Shufwa ni siku ya Tarwiya (siku ya nane ya mwezi Dhul-Hijja) na Witiri ni siku ya Arafa (siku ya tisa ya Dhul-Hijja), hayo yamepokewa kutoka kwa Abu Jaffar na Abu Abdillah.

Riwaya hizo tatu zimepokewa kwa njia ya Ahli Sunnah. Inawezekana kukusanya kati ya hizo riwaya kwamba makusudio ni Shufwa na Witiri yoyote. Katika Tafsiri ya Qummi kuhusu "Masiku kumi" amesema ni ya mwezi wa Dhul-Hijja na "Shufwa na Witiri" amesema ni rakaa mbili na moja. Katika hadith Shufwa ni Hassan na Hussein na Witiri ni Amiirul Muuminiin(a.s) . Katika riwAya Na Abu Jarud, kutoka kwa Abu Jaffar kuhusu Aya Na tano anasema ni "Mwenye akili". Katika ulal kwa isnadi yake kwa Abana Al-Ahmar amesema: "Nilimuuliza Abu Abdillahi kuhusu kusema kwake Mwenyezi Mungu. Na Firaun mwenye vigingi, kwanini ameitwa hivyo?" Akasema : "Kwa sababu alikuwa anapomwadhibu mtu humtandaza juu ya ardhi na kumnyoosha mikono yake na miguu yake kisha humwamba kwa vigingi vinne. Mara nyengine humtandaza juu ya ubao na kumwamba miguu yake na mikono yake kwa vigingi vine, kisha humwacha mpaka afe, ndio Mwenyezi Mungu akamwita mwenye vigingi."

Katika Majmau kuhusu "Hakika Mola wako ni mwenye kuotea" imepokewa kutoka kwa Ali(a.s) kwamba yeye amesema: Hakika maana yake ni kwamba Mola wako ni muweza wa kuwalipa waasi malipo yao. Katika hiyo hiyo Majmau imepokewa kwa Swadiq amesema maana ya neno Mirswad ni korongo kwenye Swirat halipiti korongo hilo mja ambaye hakujiweka kimja. Kutoka kwa Ghawali naye kutoka kwa Aswadiq(a.s) katika hadithi ya kutafsiri kauli ya Mwenyezi Mungu (s.w.t): "Na dhun-nun (Yunusi) alipoondoka hali amechukiwa na akadhani ya kwamba hatutamdhikisha." (21:87) Amesema: Husikii kauli yake Mwenyezi Mungu. "Ama amjaribupo, akamdhikisha riziki yake, husema: Mola wangu amenitweza"? Katika Tafsiri ya Qummi katika riwAya Na Abu Jarud, kutoka kwa Abu Jaffar(a.s) kuhusu kauli yake "si hivyo ardhi itakapopondwa pondwa' Amesema hilo ni tetemeko.

Katika Durril-Manthur ametoa Ibn Murduwayh kutoka kwa Ali bin Abu Twalib amesema: "Amesema Mtume(s.a.w.w) he, mnajua nini tafsiri ya aya hii! "Si hivyo ardhi Takapondwa pondwa ikaleta siku hiyo Jahannam" akasema: Kitakapokuwa Kiyama Jahannam itaongozwa kwa hatamu elfu sabini kwa mikono ya Malaika elfu sabini itachomoza mchomozo mmoja, lau Mwenyezi Mungu sikuifunga ingeliunguza mbingu na ardhi. Hadith hii pia ni yenye kupokewa kutoka cha Amali Sheikh kwa isnadi yake kutoka kwa Arridha naye kutoka kwa baba yake naye kutoka kwa Ali(a.s) naye kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) .

Katika Uyun katika mlango wa yaliyokuja kutoka kwa Arridha katika Akhbaru Tawhid kwa isnadi yake kutoka kwa Ali bin Fadh-dhal naye kutoka kwa baba yake amesema: Nilimuuliza Arridha(a.s) kuhusu kusema kwake Mwenyezi Mungu "Na akaja Mola wako na Malaika (wamejipanga) safu kwa safu" Akasema: "Hakika Mwenyezi Mungu Mtukufu hasifiwi na kuja na kwenda isipokuwa maana ni, na ikaja amri ya Mola wako."

Katika Kafi kwa isnadi yake kutoka kwa Sadiyr Asswayrafiy amesema: "Nilimwambia Abu Abdillah(a.s) niwe mkombozi wako ewe mtoto wa Mtume wa Mwenyezi Mungu, Je, muumin anachukia anapotolewa roho yake akasema: Hapana, hakika yeye anapojiwa na Malaika wa Mauti kuchukua roho yake hufadhaika, Malaika wa Mauti huwambia: Ewe walii wa Mwenyezi Mungu usifadhaike, ninaapa kwa ambaye amempa utume Muhammad, hakika mimi nitakufanyia wema na upole kuliko mzazi, fungua macho uone.

Hapo atafanishiwa Mtume(s.a.w.w) , Amirul Muminiin, Fatima, Hassan and Hussein na Maimamu katika kizazi chao(a.s) ataambiwa hawa ni marafiki zako. Atafungua macho yake na atanadi mnadi kutoka mbele ya Mwenyezi Mungu atasema; Ewe nafsi iliyotua! Kwa Muhammad na Ahlul Bait wake rudi kwa Mola wako hali ya kuridhia wilaya na hali ya kuridhiwa thawabu, ingia katika waja wangu yaani Muhammad na Ahlul Bait wake na ingia katika pepo yangu. Litakua ni jambo la kupendeza kwake kutolewa roho yake na kumsikia mnadi. Amepokea Qummi riwaya kwa maana haya katika Tafsiri yake na Al-Barqi katika Mahasin.

15

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

SURA BALAD (MJI) (NA. 90)

INA AYA 20

Kwa jina la Allah, Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu

لَا أُقْسِمُ بِهَـٰذَا الْبَلَدِ ﴿١﴾

1. Naapa ka mji huu.

وَأَنتَ حِلٌّ بِهَـٰذَا الْبَلَدِ ﴿٢﴾

2. Na hali yakuwa wewe ni mkazi wa mji huu.

وَوَالِدٍ وَمَا وَلَدَ ﴿٣﴾

3. Na (kwa) mzazi na alichokizaa.

لَقَدْ خَلَقْنَا الْإِنسَانَ فِي كَبَدٍ ﴿٤﴾

4. Hakika tumemuumba mwanadamu, katika mateso.

أَيَحْسَبُ أَن لَّن يَقْدِرَ عَلَيْهِ أَحَدٌ ﴿٥﴾

5.Je anadhani kwamba hatawezekana na yeyote?

يَقُولُ أَهْلَكْتُ مَالًا لُّبَدًا ﴿٦﴾

6. Anasema: Nimepoteza mali mengi!

أَيَحْسَبُ أَن لَّمْ يَرَهُ أَحَدٌ ﴿٧﴾

7. Anadhani kwamba hakuonekana na yeyote?

أَلَمْ نَجْعَل لَّهُ عَيْنَيْنِ ﴿٨﴾

8. Ja hatukumpa macho mawili?

وَلِسَانًا وَشَفَتَيْنِ ﴿٩﴾

9. Na ulimi na midomo miwili?

وَهَدَيْنَاهُ النَّجْدَيْنِ ﴿١٠﴾

10. Tukamuonyesha njia mbili?

فَلَا اقْتَحَمَ الْعَقَبَةَ ﴿١١﴾

11. Basi mbona hakupita njia nzito?

وَمَا أَدْرَاكَ مَا الْعَقَبَةُ ﴿١٢﴾

12. Na umejuaje, ni ipi njia nzito?

فَكُّ رَقَبَةٍ ﴿١٣﴾

13. Ni kumwacha huru mtumwa.

أَوْ إِطْعَامٌ فِي يَوْمٍ ذِي مَسْغَبَةٍ ﴿١٤﴾

14. Au kumlisha siku ya njaa.

يَتِيمًا ذَا مَقْرَبَةٍ ﴿١٥﴾

15. Yatima aliye jamaa.

أَوْ مِسْكِينًا ذَا مَتْرَبَةٍ ﴿١٦﴾

16. Au maskini mwenye haja.

ثُمَّ كَانَ مِنَ الَّذِينَ آمَنُوا وَتَوَاصَوْا بِالصَّبْرِ وَتَوَاصَوْا بِالْمَرْحَمَةِ ﴿١٧﴾

17. Kisha akawa ni katika ambao wameamini, wakausiana kusubiri na wakausiana kuoneana huruma.

أُولَـٰئِكَ أَصْحَابُ الْمَيْمَنَةِ ﴿١٨﴾

18. Hao ndio watu wa heri.

وَالَّذِينَ كَفَرُوا بِآيَاتِنَا هُمْ أَصْحَابُ الْمَشْأَمَةِ ﴿١٩﴾

19. Na ambao wamezikanusha alama zetu, hao ndio wa shari.

عَلَيْهِمْ نَارٌ مُّؤْصَدَةٌ ﴿٢٠﴾

20. Juu yao ni moto uliokomewa.

UBAINIFU

Sura inataja kwamba umbo la mtu ni lenye kujengwa juu ya tabu na mashaka. Huwezi kukuta jambo lolote katika mambo ya maisha isipokuwa litakuwa limekutanishwa na matatizo na tabu, tangu roho inapoingia katika kiwiliwili chake mpaka anapokufa. Hana raha inayoepukana na tabu na mashaka, wala furaha isiyoandamana na misukusuko au huzuni isipokuwa katika nyumba ya akhera tu, mbele ya Mwenyezi Mungu. Basi mtu na avumulie uzito wa taklifa za Mwenyezi Mungu kwa kusubiri juu ya kufanya twaa na kuepukana na maasia. Na ajitahidi kueneza huruma juu ya wale waliopatwa na majaribio na balaa za dunia kama uyatima, ufakiri na maradhi ili awe ni katika watu wa heri. Kama si hivyo, basi akhera yake itakuwa kama dunia yake na atakuwa katika watu waovu juu yao ni moto uliofungiwa.

Mpangilio wa Aya Na Sura nii unafanana na wa Makka, kwa hiyo unatilia nguvu kuwa Sura imeshuka Makka. Baadhi wamedai kuwa hilo (la kushuka Makka) ni kwa Ijmai (mkusanyiko wa makubaliano ya wanazuoni). Imesemekana kwamba Sura hii imeshuka Madina na kwamba mpangilio wa aya za mwanzo hausaidii kusema kuwa imeshula Makka. Na pia imesemwa imeshuka Madina isipokuwa aya nne za mwanzo. Utakuja ufafanuzi katika utafiti wa hadith (Inshallah).

Aya Na 1

Wametaja kuwa makusudio ya mji huu ni Makka na hilo linatilia nguvu kuwa Sura imeshuka Makka.

Aya Na 2

Kuliweka jina dhahiri mahali pa dhamir ni kwa ajili ya kuadhimisha (mji huo) na kushughulika nao ambao ni mji mtukufu. Neno Hillun ni masdar kiarifa chenye kutumika kama jina kwa maana ya kukaa na kuthibiti mahali. Masdar hapa imekuja kwa maana ya (fail) Mtendaji maana yake kwa ujumal: ninaapa kwa mji huu na hali ya kuwa wewe ni mkazi wake. Na hilo uzindushi juu ya utukufu wa Makka kwa sababu ya kukaa kwake Mtume(s.a.w.w) na kuwa ni mahali pake pa kuzaliwa.

Inasemekana jumla hiyo imeingia kati tu; kati ya kiapo na chenye kuapiwa na makusudio yake ni kuhalalishwa. Anasema katika Kash-shaf "Na ameingilia kati ya kiapo na chenye kuapiwa kwa Kusema: "Na hali yakuwa wewe ni mwenye kuhalalishwa katika mji huu" yaani ni katika mateso kwamba mfano wako wewe juu ya ukubwa na utukufu wako unahalalishwa katika mji huu mtukufu, kama linavyohalalishwa windo nje ya haram. Wanaharamishwa kuua windo na kupukusa majani, lakini wanahalalisha kukutoa wewe na kukuua. Hadith hiyo imepokewa katuka kwa Sharhabil. Katika hilo ni uthabiti kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu na uwezekano na mateso aliyokuwa akiyapata kutoka kwa watu kustajaabu kutokana na hali yao ya uadui. Kisha akasema: "au alimfariji Mtume kwa kuapa kwa mji wake kwamba mtu haepukani na shida kisha akaingilia kati kwa kusema kuwa kiaga chake cha ushindi wa Makka kitatimu ili kumpa faraja, kwa hiyo akasema: na hali ya kuwa wewe ni mwenye kuhalalishiwa (yaliyoharamu) katika mji huu yaani na hali wewe utahalilishiwa hapo mbeleni utafanya ndani ya mji huu yale utakayoyataka maka kuua na kuteka".

Kwa hiyo inakuwa tafsiri ya neno Hillum ni kwa maana ya mwenye kuhalilishiwa kinyume chake ni mwenye kuharamishiwa; yaani tutakuhalalishia siku ya ushindi wa kuichukua Makka kwa muda utapigana na utamuua unayemtaka.

Aya Na 3

Ni kulazimisha namna ya kunasibika na kufungamana kati ya kiapo na chenye kuapiwa, kunapelekea kuwa makusudio ya mzazi na alichokizaa, kwamba kuna mnasaba iliowazi kati yake na mji wenye kuapiwa. Hilo linakubaliana na Ibrahim na mtoto wake Ismail(a.s) . Wao ndio chanzo cha kujengwa mji wa Makka na ndio wajenzi wa Al-Ka'aba tukufu: Mwenyezi Mungu anasema; "Na (kumbukeni) alipoinua Ibrahim kuta za nyumba (Al-Ka'aba) na Ismail (pia); (wakaomba wakasema) Ewe Mola wetu tutakabalie (amali yetu). Hakika wewe ndio mwenye kusikia, na mwenye kujua ." (2:127).

Kuleta herufi "Maa" yenye maana ya ambacho badala ya kuleta Man yenye maana ya ambaye, ni kwa ajili ya kulikuza jambo na kulistaajabia jambo lenyewe; kama alivyosema; "na Allah anajua zaidi alichokizaa ." (3:36).

Maana kwa ujumla ni naapa kwa mzazi mwenye jambo kubwa ambaye ni Ibrahim na alichokizaa ambacho ni mtoto wa ajabu wa jambo lake mwenye kubarikiwa; naye ni Ismail. Na wao wawili ndio waliojenga Al-Ka'aba. Ufahamisho wa aya tatu ni kuapa kwa mji mtukufu Makka kwa Mtume ambae amekaa katika mji huo na kwa Ibrahim na Ismail ambao wameujenga. Inasemekana kuwa makusudio ya mzazi ni Ibrahim na alichokizaa ni watoto wake wote Waarabu. Lakini ni umbali kwa Mwenyezi Mungu kuwa Mtume (SAWW) na Nabii Ibrahim(a.s) awakutanishe na watu kama akina Abu Lahab, Abu Jahal na wengineo katika viongozi wa ukafiri na awaapie wote. Na Ibrahim(a.s) alijiepusha na kila asiyemfuata katika watoto wake juu ya Tawhid wakati aliposema: "Na uniepushe mimi na wanangu na kuabudu masanamu. Mola wangu! Hakika (masanamu) hawa wamepoteza watu wengi. Basi aliyenifuata ni wangu mimi na aliyeniasi (unaweza kumsamehe) kwani wewe ni mwingi wa msamaha na Mwingi wa rehema ". (14:35-36).

Basi mwenye kufasiri alichokizaa kuwa ni watoto wa Ibrahim, ni juu yake kuwahusisha waislamu tu, katika kizazi chake, kama ilivyo katika dua ya Ibrahim. "Ewe Mola wetu! Utufanye tuwe wenyenyekevu kwako. Na miongoni mwa kizazi chetu (pia ufanye) umma mnyenyekevu kwako na utuonyeshe njia ya ibada yetu na utusameha ." (2:128).

Inasemekana kuwa makusudio ya mzazi na alichokizaa na Adma(a.s) na kizazi chake chote kwa kuzingatia kuwa kilichoapiwa viapo hivi ni kule kuumbwa mwanadamu katika mateso. Na Mwenyezi Mungu ameweka utaratibu wa kuzaliana ili kuhifadhi jinsi hii. Kwa hiyo ameapia katika aya hizi kwa kupitia utaratibu huu na matokeo yake - nayo ni mzazi na alichokizaa - kuwa mtu yuko katika tabu na mateso kulingana na namna ya kuumbwa kwake kuanzia anapopata uhai mpaka kufa.

Maelezo haya hayana ubaya, lakini kunabakia kubainisha mnasaba uliopo kati ya mji wa Makka na mzazi na kila mwenye kuzaliwa katika kuwakusanya kwenye viapo. Pia imesemwa kuwa makusudio ni Adam na watu wema katika kizazi chake. Maelezo haya ni kama yanamtakasa Mwenyezi Mungu kuapia kwa maadui wake wenye kupetuka mipaka na wafisadi katika makafiri.

Imesemwa kuwa makusudio ni kila mzazi na kila mwenye kuzaliwa na pia imesemwa kuwa ni mwenye kuzaa na asiyezaa kwa kuchukulia herufi Maa kuwa ni ya kukanusha. Vile vile imesemwa makusudio ya mzazi ni Mtume na alichokizaa ni umati wake kwa sababu yeye yuko katika daraja ya baba kwa umati wake; lakini hayo yote ni maelezo yaliyo mbali.

Aya Na 4

Jumla hiyo ni jawabu ya kiapo. Mateso katika umbile la binadamu na tabu katika mambo yake yote ya uhai ni jambo lisilofichika kwa kila mwenye roho. Mwanadamu hakusudii neema yoyote katika neema ya dunia ila huwa na matatizo katika dunia uzuri wako. Wala hawezi kupata kitu chochote katika dunia ila kitakuwa kimechanganyika na usumbufu pamoja na matatizo na mateso kuongozea misiba ya balaa za dunia na matukio ya ghafla.

Aya Na 5

Katika natija ya hoja iliyotangulia, uthibitisho wake ni kuwa; kwa kuwa mtu umbile lake limejengewa tabu, hapati kitu chochote katika anavyovitaka ila hupata asivyotaka, basi yeye ni mwenye kuzungukwa katika umbile lake, mwenye kushindwa katika matakwa yake na ni mwenye kushindwa nguvu katika analoliweza. Anayemshinda katika matakwa yake na kumshinda nguvu kufanya mambo anayoyaweza ni Mwenyezi Mungu (s.w.t) naye ni muweza katika kila upande, yeye anaweza kumfanyia mtu lolote analolitaka na kumchukua wakati anapomtaka.

Kwa hiyo mtu asifikirie kuwa hawezwi na yeyote, kwani fikra hiyo itampelekea kujifanya mkubwa mbele ya Mwenyezi Mungu na kutakabari katika kumwabudu. Au akitoa katika baadhi ya aliyoamrishwa, na kutoa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, basi anajiona ni mwingi wa mali, na husimbulia baada ya kufanya ria, kwa kusema: "Nimepoteza mali mengi!'.

Aya Na 6

Mpangilio wa aya na nyengine zinazofuatia mpaka mwisho wa Sura unaonyesha kuwa kulikuwa na baadhi ya wenye kudhihirisha Uislamu; akitoa baadhi ya mali yake anajifaharisha kuwa ametoa sana kwa kusema: nimepoteza mali mengi! Ndio ikashuka aya kumjibu, kwamba kufuzu kwa kheri za uhai hakutimu ila kwa kupita njia nzito ya kutoa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na kuingia katika kundi la wale ambao wameamini wakausiana kusubiri na kuoneana huruma. Yatatilia nguvu hilo yale yatakayokuja katika utafiti wa hadith (Inshallah).

Aya Na 7

Ni kukanusha hilo neno la mtu kwa njia ya fumbo. Maana yanayopatikana ni kwamba vile mtu anavyolazimika kusema kuwa amepoteza mali mengi, akafikiria kuwa mimi nimeghafilika na sijui, yale aliyotoa? Basi amekosea katika hilo na Mwenyezi Mungu ni mwenye kuona aliyoyatoa, lakini kiasi hicho hakitoshi kumfanya awe ni mwenye kufuzu kwa maisha ya kheri bali hana budi kuvumilia zaidi ya hayo katika mashaka ya kimja, apite njia nzito na awe pamoja na waumini katika yote waliyonayo.

Aya Na 8-10

Yaani tumemtayarisha katika mwili wake kwa yale anayoonea ili apate elimu ya vinavyoonwa kwa kadri ya upana wa elimu hiyo Na je, hatukumpa ulimi na midomo miwili vitakavyomsaidia kutamka yaliyo katika dhamir yake miongoni mwa elimu na aongoke kwa hilo mwenzake kwa kujua mambo yaliyofichika na macho? Na tumemfahamisha njia ya heri na ya shari kwa ilhamu itokayo kwetu, hivyo yeye anujua heri na anapambanua shari. Na aya hii ya tisa iko katika maana ya Aya Na nane ya Sura Shams Na. (91).

Aya hizo tatu ni hoja juu ya kauli yake Mwenyezi Mungu "Anadhani kwamba hakuonekana na yeyote" Yaani Yeye Mwenyezi Mungu anaona matendo ya waja wake na anajua yaliyo katika dhamiri yao kwa njia ya matendo na anapambanua kheri na shari na mema na mabaya. Kwa ujumla ni kuwa hakika Mwenyezi Mungu S.W.T. ndiye ambaye anamfahamisha yenye kuonekana kupitia macho yake mawili na namna anavyoweza kupiga picha kumfahamisha jambo asilolijua, na ni Yeye ambaye anamfahamisha yaliyo katika dhamiri kupitia kusema Je, inaingilika akilini kuwa Mwenyezi Mungu amfunulie mtu mambo ambayo Yeye mwenyewe hayajui?

Na yeye ndiye ambaye anampambanulia mtu heri na shari kwa ilhamu, Je, inawezekana kuwa Yeye hawezi kujua wala kupambanua? Yeye Mwenyezi Mungu anaona aliyoyafanya mtu na najua anayonuia kuyafanya na kuyapambanua kuwa ni kheri au shari.

Aya Na 11

Maana ya neno Iqtahama ni kuingia kwa haraka na kwa shida kujigagamiza na neno Aqaba ni njia nzito yenye vikwazo vya kupanda majabali. Kujigagamiza kuparamia njia nzito ni ishara ya kutoa (mali) ambako kunakuwa vigumu kwa mtoaji, kama itakavyoelezwa. Inasemekana kuwa jumla yote ni dua dhidi ya mtu anayesema nimepoteza mali mengi lakini si hivyo.

Aya Na 12

Ni kulikuza jambo lenyewe, kama ilivyopita katika mtazamo wake.

Aya Na 13

Yaani njia nzito ni kumwachia hutu mtumwa. Makusudio ya njia nzito ndiyo huko kuacha huru ambako ni kitendo chenyewe, na kujigagamiza kunaamanisha kukitenda. Kwa hiyo basi inaharabika kauli ya baadhi ya wanaosema kwa kumwachia huru mtumwa ndiko kupita njia nzito lakini sio njia nzito yenyewe, kwamba kuna mudhafu (neno lenye kutegemezwa) uliondolewa kukisia kwake ni: Na umejuaje ni nini kupita njia nzito, kupita njia nzito ni kumwacha huru mtumwa. Hayo yaliyotajwa katika kubainisha njia nzito ambayo ni kumwacha huru mtumwa au kulisha siku ya njaa, katika kueneza huruma yamehusishwa kutajwa kutokana na umuhimu wake. Na kumetangulizwa kuacha huru mtumwa kwa sababu dini imeshughulikia sana suala hilo.

Aya Na 14-16

Neno Matraba linatoka katika neno Turab (mchanga) na maana yake ni kushikwa na mchanga (vumbi) kutokana na shida ya ufakiri. Maana yake kwa ujumla ni, au kumlisha siku ya njaa. Yatima mwenye udugu au maskini mwenye ufakiri sana.

Aya Na 17

Kuusiana kusubiri ni kuusiana kusubiri juu ya kumtii Mwenyezi Mungu na kuusiana kuoneana huruma ni kuusiana kuwaonea huruma wenye ufakiri na umaskini. Jumla nzima inaungana na jumla ya kupita njia nzito.

Aya Na 18

Neno Maymana limekuja kwa maana ya heri kinyume chake na Mash'ama uovu. Kuleta ishara ya neno (hao) kwa unavyofahamisha mpangilio wa maneno uliotangulia, ni kuwa: Wale ambao wamepita njia nzito na wakawa katika wale ambao wameamini, na wakausiana kusubiri na wakausiana kuoneana huruma ni watu wa heri. Walilolifanya katika imani na amali yao ni njema wataliona ni jambo lenye kubarikiwa, zuri na lenye kurudhiwa. Imesemekana kuwa makusudio ya Maymana ni Yamin upande wa kuume na watu wa upande ya kuume ndio ambao watapewa vitabu vyao kwa upande wao wa kuume, lakini hilo halifuatani na neno Mash'ama (uovu).

Aya Na 19

Alama zetu ni alama za mbinguni na za kinafsi nazo zinafahamisha juu ya umoja katika uungu na kuzikanusha ndio kumkanusha Mwenyezi Mungu, vile vile ni kukanusha Qur'an tukufu na aya zake na yote yaliyoshuka na kufikishwa kwa njia ya ujumbe.

Utafiti Wa Hadith Katika Majmau Aya Na 2 imesemwa kuwa maana yake ni na hali ya kuwa ni halali kwako kumuua unayemwona anastahiki kuuliwa katika makafiri. Hilo ni wakati alipoamrishwa kupigana siku wa kuichukua Makka; Mwenyezi Mungu akamhalalishia hata akaweza kupigana na kuua. AmesemaMtume(s.a.w.w) haikuhalalishiwa kwa yoyote kabla yangu wala haitakuwa halali baada yangu kwa yoyote, na mimi sikuhalalishiwa isipokuwa saa moja katika mchana. Hadith hiyo imepokewa kutoka kwa Ibn Abbas, Mujahid na Ata.

Imepokewa kutoka kwa Abu Abdillah amesema: "Maquraish walikuwa wakiuadhimisha mji na kumuhalalisha Muhammad(s.a.w.w) katika mji huo, akasema: Naapa kwa mji na halo ya kuwa wewe ni mwenye kuhalalishwa katika mji huu anakusudia kusema kuwa wao wamehalalisha kukuudhi kukuadhibisha na kukutukana. Na wao walikuwa hawamwadhibu hata mtu aliyeua baba wa mmoja wao. Na walikuwa wakivaa majani wa mti kumpa amani, lakini wakahalalisha kwa Mtume(s.a.w.w) yale ambayo hawakumuhalalishia mwengine. Katika hiyo Majmau kuhusu Aya Na tatu imesemwa kuwa ni Adam an alichokizaa katika Mitume, mawalii na wafuasi wao. Hadith hiyo imepokewa kutoka kwa Abu Abdillahi.

Maana yaliyotangulia pia yamepokewa katika njia ya Ahli Sunna. Pia amepokea Qummi katika Tafsiri yake. Katika Tafsiri ya Qummi kuhusu Aya Na sita amesema maana ya neno Lubada ni mkusanyiko. Na katika Majmau kuhusu aya hiyo hiyo imesemwa huyo aliyesema hivyo ni Harith bin Naufal bin Abdul Manaf, wakati alipofanya dhambi fulani, akataka fatuwa kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) akamwamrisha kutoa kafara, akasema: Tangu nilipoingia dini ya Muhammad mali yangu imeisha katika makafara na kulisha. Hadith hiyo imepokewa na Muqatil. Katika hiyo hiyo Majmau, imesemwa kuwa, aliulizwa Amirul-Miminin Ali(a.s) kwamba watu wanasema kuhusu neno ya Mwenyezi Mungu "Na tukamuongoza njia mbili" kwamba hizo njia mbili ni matiti? Akasema hapana njia mbili hizo ni heri na shari.

Katika Kafi kwa isnadi yake kutoka kwa Hamza bin Muhammad naye kutoka kwa Abu Abdillahi(a.s) amesema nilimuuliza kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu tukamwongoza njia mbili akasema ni njia ya heri na shari. Imepokewa riwaya hii katika Durril Manthur kwa njia ya Ali(a.s) Anas, Abu Amama na wengineo kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) .

Katika Kafi kutoka kwa Jaffar bin Khilad amesema: Alikuwa Abul-Hassan Ridha(a.s) anapokula, huletewa chano karibu na chakula chake, anaangalia chakula kizuri katika vyakula alivyoletewa na kukiweka katika chano, kisha anaamrisha kipewe masikini kisha anasoma ayah ii: 'Haya naapite hiyo njia nzito 'kisha anasema: "Mungu anajua kuwa sio kila mtu anaweza kuacha huru mtumwa kwa hiyo amewafanyia njia nyengine ya kwenda peponi".

Katika Majmau imepokewa hadith Marfuu kutoka kwa Baraa bin Azib amesema: "Alikuja bedui kwa Mtume(s.a.w.w) akasema: "Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu nijulishe amali itakayonitia peponi" Mtume akasema: "Ukiwa umefupisha hotuba basi umerefusha masuala; muache huru mtu, na uifungulie shingo." Akasema yule bedui "kwani yote hayo sio kitu kimoja?" Akasema Mtume: La! Kuacha huruni kumuacha aende zake na kuifungulia shingo ni kumsaidia katika thamani yake. Kama si hivyo, basi mlishe mwenye njaa, na mnyweshe mwenye kiu na uamrishe mema na ukataze maovu na uzuiye ulimi isipokuwa katika jambo la kheri tu. Katika Tafsiri ya Qummi kuhusu kauli yale Mwenyezi Mungu : "Au maskini mwenye shida" ni yule asiyeweza kujikinga na mchanga (vumbi).

11

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

SURA TARIQ (CHENYE KUJA USIKU) (NA. 86)

INA AYA 17

Kwa Jina la Allah, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu.

وَالسَّمَاءِ وَالطَّارِقِ ﴿١﴾

1. Naapa kwa mbingu na chenye kuja usiku.

وَمَا أَدْرَاكَ مَا الطَّارِقُ ﴿٢﴾

2. Na lipi la kukujulisha ni nini chenye kuja siku.

النَّجْمُ الثَّاقِبُ ﴿٣﴾

3. Ni nyota inayong'ara usiku.

إِن كُلُّ نَفْسٍ لَّمَّا عَلَيْهَا حَافِظٌ ﴿٤﴾

4. Hakuna nafsi isipokuwa kuna mwenye kuitunza.

فَلْيَنظُرِ الْإِنسَانُ مِمَّ خُلِقَ ﴿٥﴾

5. Basi mtu na ajitazame ameumbwa kwa kitu gani..

خُلِقَ مِن مَّاءٍ دَافِقٍ ﴿٦﴾

6. Ameumbwa kwa maji yanayotoka kwa nguvu.

يَخْرُجُ مِن بَيْنِ الصُّلْبِ وَالتَّرَائِبِ ﴿٧﴾

7. Yanayotoka baina ya uti wa mgongo na mifupa ya kifua.

إِنَّهُ عَلَىٰ رَجْعِهِ لَقَادِرٌ ﴿٨﴾

8. Hakika yeye ni mweza wa kumrejeza.

يَوْمَ تُبْلَى السَّرَائِرُ ﴿٩﴾

9. Siku zaitakapofunuliwa siri.

فَمَا لَهُ مِن قُوَّةٍ وَلَا نَاصِرٍ ﴿١٠﴾

10. Basi hatakuwa na nguvu wala wa kumnusuru.

وَالسَّمَاءِ ذَاتِ الرَّجْعِ ﴿١١﴾

11. Naapa kwa mbingu yenye kurudi.

وَالْأَرْضِ ذَاتِ الصَّدْعِ ﴿١٢﴾

12. Na ardhi yenye mipasuko.

إِنَّهُ لَقَوْلٌ فَصْلٌ ﴿١٣﴾

13. Hakika hii (Qur'an) ni kauli yenye kupambanua.

وَمَا هُوَ بِالْهَزْلِ ﴿١٤﴾

14. Wala si upuuzi.

إِنَّهُمْ يَكِيدُونَ كَيْدًا ﴿١٥﴾

15. Hakika wao wanakuchimbia vitimbi.

وَأَكِيدُ كَيْدًا ﴿١٦﴾

16. Nami (pia) ninawachimbia vitimbi.

فَمَهِّلِ الْكَافِرِينَ أَمْهِلْهُمْ رُوَيْدًا ﴿١٧﴾

17. Basi wape muhula makafiri wape muhula kidogo.

UBAINIFU

Katika Sura hii kuna maonyo kwa marejeo ya akhera na kufufuliwa. Na hayo yanafamisha uwezo wake Mwenyezi Mungu. Na inamalizia Sura kwa kueleza kiaga cha makafiri. Sura hii imeshuka Makka bila ya ubishi.

Aya 1-3

Neno Twariq asili yake- kama ilivyosemwa- ni kugonga kiasi cha kutoa sauti, miongoni mwao, ni nyundo na lina maana njia. Njia imeitwa hivyo kwa vile mpita njia anaigonga kwa nyayo zake. Kywa hivyo likaenea neno hilo kutumiwa kwa njia, kisha likahusishwa na kuja usiku, kwa sababu mwenye kuja usiku aghlabu hukuta milango imefungwa, kwa hiyo hugonga, kisha likaenea hilo neno kwa kila chenye kuhidhiri usiku. Makusudio ya neno hilo katika aya ni nyota yenye kutokeza usiku. Neno Thaqb asili yake ni kupasua; kisha likawa ni nuru yenye kuangaza, kwa sababu inapasua giza, na linakuja kwa maana ya kuwa juu kama kusema: imepaa juu ndege, nikama vile inapasua anga kwa kuruka kwake. Kwa hivyo makusudio ya Aya Na kwanza ni kuapa kwa mbingu na nyota inayotokeza usiku. Na Aya Na pili ni kwa ajili ya kulikuza jambo la chenye kuapiwa ambacho ni hicho chenye kutokeza usiku. Aya Na tatu ni ubainifu wa hicho chenye kutokeza usiku. Jumla hiyo ni jawabu ya swali.

Aya Na 4

Ni jawabu la kiapo. Herufi Lamma ni kwa maana ya illa (isipokuwa). Makusidio ya kutunza hapa ni kuandika matendo yake mema na maovu, ili yaweze kuhisabiwa siku ya Kiyama na kulipwa. Kwa hivyo mtunzaji ni malaika na chenye kutunzwa ni matendo, kama alivyosema Mwenyezi Mungu: "Na hakika mna wenye kuwatunza watukufu wenye kuandika ." (82:10-11).

Sio mbali kuwa makusudio ni kutunza nafsi dhati yake na vitendo vyake, kwa hiyo inafahamisha kuwa nafsi ni zenye kutunzwa hazimaliziki kwa mauti wala haziharibiki mpaka Mwenyezi Mungu atakapovifufua viwiliviwili, atavirudisha nafsi na atakuwa mtu kama alivyokuwa mtu wa duniani kwa dhati yake; kisha alipwe kwa mujibu wa vitendo vyake vyenye kuchungwa, vikiwa ni kheri au shari. Hilo linatiliwa nguvu na aya nyingi zinazofahamisha juu ya kutunzwa vitu, kama vile kusema kwake Mwenyezi Mungu: "Sema atawaua Malaika wa mauti aliye wakilishwa kwenu kisha mtarejeshwa kwa Mola wenu. " (32:11).

"Allah huzichukua roha wakati wa mauti yake na zile zisizokufa katika usingizi wao. Basi huzizuwiya zile alizozihukumia mauti. ." (39:42).

Hayo hayakanushi dhahiri ya Aya Na Sura ya (82:10).

kuwa kutunza kwa Malaika ni kuandika, kwa sababu kuitunza nafsi pia kutokana na kuandika kama anavyofahamisha Mwenyezi Mungu kwa kusema: "Hakika sisi tulikuwa tukiandika yale aliyokuwa mkiyatenda ." (45:29).

Kwa njia hii kunabatilika kutia makosa juu ya yale yanayofahamisha juu ya marejeo ya Kiyama katika kuenea Kudura, kwamba kumrusisha mtu kwa dhati yake ni muhali kwa sababu mtu ataumbwa tena mara ya pili mfano wa yule mtu wa duniani aliyeumbwa kwanza, lakini si yule yule na mfano wa kitu sio kitu chenyewe. Njia ya kubatilisha hoja hiyo ni kwamba: utu wa mtu unatokana na mtu kwa nafsi yake sio kwa kiwilikiwili chake na nafsi ni yenye kihifadhiwa kwa hivyo akiumba kiwilikiwili na kukifungamanisha na nafsi atakuwa ndiya yule yule mtu wa duniani kwa utu wake, ijapokuwa sio dhati yake.

Aya Na 5

Yaani aangalie nini mwanzo wa umbile lake? Na ni kitu gani ambacho Mwenyezi Mungu amekifanya kuwa mtu? Jumla hii ni mtiririko wa aya iliyotangulia. Maana yanavyofahamisha kutokana na mpangilio wake, ni kwamba, ikiwa kila nafsi ni yenye kuhifadhiwa kwa dhati yake na vitendo vyake, bila ya kwisha hiyo nafsi na kusahauliwa vitendo vyake basi akubali mtu ukweli kwamba yeye atarudi kwa Mola wake na kulipwa aliyoyatenda, wala hilo asilihisabu kuwa ni mbali. Naangalie ukweli huu kwenye asili ya umbile lake na akumbuke kwamba yeye ameumbwa kwa maji yanayoka kwa nguvu yanayotoka baina ya uti wa mgongo na mifupa ya kifua. Basi yule aliyeanza kumuumba kutokana na maji haya anaweza kumrudisha na kumuhuisha baada ya mauti.

Aya Na 6

Maji yenye kutoka kwa kuruka ni manii. Jumla hiyo iko katika jawabu la swali.

Aya Na 7

Neno Sulb lina maana ya mgongo na Taraib ni mifupa wa kifua. Wamehitalifiana kiajabu kwenye matamko yao katika aya hii na iliyo kabla yake. Kwa dhahiri makusudio yake ni sehemu iliyokatikati ya uti wa mgongo na mifupa ya kifua.

Aya Na 8

Yaani ambaye amemuumba mtu kutokana na maji, sifa yake ni hiyo hiyo, ni mwenye kuweza kumrudisha na kumuhuisha baada ya mauti.

Aya Na 9: Ni siku yatakayofichuka yale alioyoyaficha mtu na kuyafanya siri katika itikadi na matendo ya kheri au ya shari. Aya hii iko katika maana ya aya inayosema "Na mkidhihirisha yaliyomo katika nyoyo zenu au mkiyafichua, Allah atawataka hisabu ya (yote) hayo ." (2:284)

Aya Na 10

Hana uwezo katika nafsi yake utakaomzuia na adhabu ya Mwenyezi Mungu wala hana wa kumnusuru atakayemkinga na adhabu yaani hakutakuwa na uwezo wowote utakaomkinga na shari kutoka kwake au kwa mtu mwengine.

Aya Na 11

Kiapo baadha ya kiapo, ni kwa ajili ya kutilia mkazo jambo la Kiyama na kurejea kwa Mungu. Makusudio ya kurudi ni kuhisi kwenda kwake kwa kuchimbuka nyota na kutua. Imesemwa kuwa makusudio yake ni mvua. Makusudio ya kupasuka ni kupasuka kwa ajili ya mimea.

Aya Na 12-13

Maana ya neno Fasl ni kupambanua kati ya vitu viwili. Aya hizi mbili ni jawabu la kiapo kwa maana; ninaapa kwa hivyo nilivyoviapia hakika Qur'an ni neno lenye kupambanua kati ya haki na batili na sio maneno yasiyokuwa na maana. Yale inayoyahakikisha ni haki isiyokuwa na shaka na yale inayoya batilisha ni batili isiyokuwa na shaka. Kwa hiyo yale iliyoyatolea habari katika ufufuo na marejeo ni haki isiyokuwa na shaka ndani yake. Imesemekana kuwa dhamiri katika neno Innahu ni ya hayo yaliyotangulia kuelezwa katika habari ya marejeo lakini tuliyoyaeleza mwanzo ndiyo yanayoelekea zaidi.

Aya Na 15

Yaani makafiri wanaichimba vitimbi wakikusudia kuizima nuru ya Mwenyezi Mungu na kubatilisha mlingano wako.

Aya Na 16

Ikiwa wao wanavyo vitimbi na mimi ninavyo vitimbi. Na Mwenyezi Mungu ndiye mwenye kushinda juu ya jambo lake, kwa hivyo wangojee tu; wala usifanye haraka, ngoja kidogo tu! Yatawajia yale waliyoahidiwa, na kila linalokuja liko karibu.

Utafiti Wa Hadithi Katika Tafsiri ya Qummi kuhusu kusema kwake Mwenyezi Mungu "Hakika kila nafsi ina mwenye kuichunga" amesema ni Malaika. Na kuhusu "Ameumbwa kwa maji yanayotoka kwa nguvu" amesema ni manii ambayo hutoka kwa nguvu". Kuhusu "yanayotoka kati ya uti wa mgongo na mifupa ya kifua" amesema uti wa mgongo ni mwanaume na mifupa ya kifua ni mwanamke. Katika Majmau imepokewa hadith marfuu kutoka kwa Abu Dardai amesema: "Amesema Mtume(s.a.w.w) :Amedhamini Mwenyezi Mungu kuumba kwake vitu vine: Swala, Zaka, Kufunga Ramdhan na kuoga janaba na hizo ndizo siri alizozisema Mwenyezi Mungu "Siku itakayofunuliwa siri ."

Huenda ikawa maana ya hadithi hiyo ni kutaja baadhi ya mambo ya ukweli, kama inavyotilia nguvu hilo hadithi inayofuata. Katika hiyo hiyo Majmau kutoka kwa Muadh bin Jabal amesema: "Nilimuuliza Mtume wa Mwenyezi Mungu: ni siri zipi ambazo Mwenyezi Mungu atawafunuliwa waja katika akhera? Akasema siri zenu ni matendo yeno ya swala, kufunga, zaka, udhu, kuoga janaba na kila lenye kufaradhiwa, kwa sababu matendo yote ni siri yenye kufichamana, mtu akitaka anaweza kusema ameswali na asiwe ameswali au aseme ametawadha kumbe hakutawadha. Basi ndiyo kusema kwake Mwenyezi Mungu "siku itakayofunuliwa siri."

Katika Tafsiri ya Qummi kuhusu kauli yake Mwenyezi Mungu: "Basi hatakuwa na nguvu wala wa kumnusuru." Amesema: hatakuwa na nguvu yoyote kwa muumba wake wala wa kumnusuru kama Mwenyezi Mungu akimtakia uovu. Katika hiyo Tafsiri ya Qummi amesema kuhusu neno Raj'n amesema ni mvua na ardhi yenye mipasuko ni ardhi yenye mimea. Katika Majmau kuhusu : "hakika hii Qur'an ni kauli ya haki" amesema "Hakika Qur'an inapambanua kati ya haki na batili kwa kuibainisha kila moja. Hayo yamepokewa kutoka kwa Imam Assadiq(a.s) .

Katika Durril Manthur ametoa Ibn Abi Shayba, Addarami, Tirmdhi, Muhammad bin nasr na Ibn el- Ambari katika Masahif kutoka kwa Harith el-Aa'war amesema: Niliingia msikitini mara watu wakaingia katika mazungumzo. Nikamwendea Ali nikampa habari; akasema: "Je wamekwishafanya? Mimemsikia Mtume(s.a.w.w) akisema: "Kutatokea fitna. Nikasema: Ni kitu gani cha kutokea katika fitna hiyo Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, Je ni sawa hapa? Akasema:kitabu cha Mwenyezi Mungu kina habari za kabla yenu baada yenu na kimekwisha wahukumia, ni upambanuzi na sio upuuzi, mwenye kukiacha Mwenyezi Mungu kumuangamiza, mwenye kukusudia pengine Mwenyezi Mungu humpoteza .

Ni kamba madhubuti, mauidha yenye hekima na njia yenye kunyooka. Ni ambachi hakipotezi wala hawashibi nacho wanavyuoni, hazitatiziki nacho ndimi wala haiishi ajabu yake. Ndicha ambacho majini waliposikia walisema: " Hakika tumesikia Qur'an ya ajabu inaongoza kwenye uongofu." Mwenye kusema kwacho huwa mkweli, mwenye kuhukumu kwacho amefanya uadilifu na mwenye kuganya amali kwacho amepata thawabu, na mwenye kulingania kwenye kitabu hicho ameongoka katika njia iliyonyooka. Amepokea karibu na maana hayo Muadh bin Jabal kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) .

12

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

SURA A'ALAA (MTUKUFU) (NA. 87)

INA AYA 19

Kwa jina la Allah, Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu.

سَبِّحِ اسْمَ رَبِّكَ الْأَعْلَى ﴿١﴾

1. Litakase jina la Mola wako aliye Mtukufu.

الَّذِي خَلَقَ فَسَوَّىٰ ﴿٢﴾

2. Ambaye ameumba (kila kitu) akakiweka sawa.

وَالَّذِي قَدَّرَ فَهَدَىٰ ﴿٣﴾

3. Na ambaye amekadiria (kila kitu) na akakiongoza.

وَالَّذِي أَخْرَجَ الْمَرْعَىٰ ﴿٤﴾

4. Na ambaye ameotesha malisho.

فَجَعَلَهُ غُثَاءً أَحْوَىٰ ﴿٥﴾

5. Kisha akayafanya makavu yenye kupiga weusi.

سَنُقْرِئُكَ فَلَا تَنسَىٰ ﴿٦﴾

6. Tutakusomesha wala hutasahau.

إِلَّا مَا شَاءَ اللَّـهُ إِنَّهُ يَعْلَمُ الْجَهْرَ وَمَا يَخْفَىٰ ﴿٧﴾

7. Ila anachopenda Allah. Hakika yeye anayajua yaliyowazi na yaliyofichika.

وَنُيَسِّرُكَ لِلْيُسْرَىٰ ﴿٨﴾

8. Tutakusahilishia njia nyepesi.

فَذَكِّرْ إِن نَّفَعَتِ الذِّكْرَىٰ ﴿٩﴾

9. Basi waidhisha ikiwa utafaa waadhi.

سَيَذَّكَّرُ مَن يَخْشَىٰ ﴿١٠﴾

10. Atawaidhika nao mcha (Mungu).

وَيَتَجَنَّبُهَا الْأَشْقَى ﴿١١﴾

11. Na atajiepusha nao asiyemcha.

الَّذِي يَصْلَى النَّارَ الْكُبْرَىٰ ﴿١٢﴾

12. Ambaye atauingia moto mkubwa..

ثُمَّ لَا يَمُوتُ فِيهَا وَلَا يَحْيَىٰ ﴿١٣﴾

13. Kisha humo hatakufa wala hatokuwa hai.

قَدْ أَفْلَحَ مَن تَزَكَّىٰ ﴿١٤﴾

14. Hakika amekwishafaulu mwenye kujitakasa.

وَذَكَرَ اسْمَ رَبِّهِ فَصَلَّىٰ ﴿١٥﴾

15. Akakumbuka jina la Mola wake na akaswali.

بَلْ تُؤْثِرُونَ الْحَيَاةَ الدُّنْيَا ﴿١٦﴾

16. Lakini nyinyi mnapenda zaidi maisha ya ulimwengu.

وَالْآخِرَةُ خَيْرٌ وَأَبْقَىٰ ﴿١٧﴾

17. Hali akhera ni bora na yenye kubaki.

إِنَّ هَـٰذَا لَفِي الصُّحُفِ الْأُولَىٰ ﴿١٨﴾

18. Hakika hAya Na mo katika vitabu vya kwanza.

صُحُفِ إِبْرَاهِيمَ وَمُوسَىٰ ﴿١٩﴾

19. Vitabu vya Ibrahim na Musa.

UBAINIFU

Ni amri ya kumpwekesha Mwenyezi Mungu juu ya yale yanayoelekeana na upande wake Mtukufu na kuitakasa dhati yake tukufu na kutaja pamoja na jina lake Mtu mwengine au kutegemeza kwa mwengine yale yanayopasa kutegemezwa kwake, kama kuumba kuangalia vizuri mambo na kuruzuku. Na nikiaga chake kwa Mtume kwa kumpa nguvu kwa elmu, hifadhi na kummakinisha katika njia ambayo ni nyepesi kwa tabligh na inayonasibiana zaidi na mlingano. Mpangilio wa aya katika mwanzo wa Sura ni mpangilio wa ki Makka. Ama mwisho wake yaani kuanzia Aya Na 14 mpaka mwisho wa Sura, imepokewa katika njia ya Maimamu wa Ahlul Bait vile vile katika njia ya Ahli Sunnah kwamba, makusudio yake ni zaka ya fitr, na swala ya Idd, na ni maalum kuwa saumu na yanayofuatia saumu miongoni mwa zaka ya fitr na swala ya Idd ilianzishwa Madina baada ya Hijra. Hivyo zitakuwa aya za mwisho zimeshuka Madina. Katika hiyo Sura mwanzo wake ni Makka na mwisho wake ni Madina, wala hayo hayakanushi yale yaliyokuja kuwa Sura imeshuka Makka, kwani ilivyo nikuwa haikataliki kuchukulia hivyo mwanzo wa Sura.

Aya Na 1

Ni amri ya kulitakasa jina lake Mwenyezi Mungu S.W.T. na kulitukuza. Na kwa vile hapa kutakaswa Mwenyezi Mungu kumefungamanishwa na jina yake, basi huko kumtakasha kunamaanisha asitajwe yeyote ambaye yeye Mwenyezi Mungu ametakata naye. Kwa sababu jina linatokea katika kusema. Hivyo isitajwe pamoja na jina lake miungu wengine washirikina, waombozi na kuwanasibishia uungu. Na vile vile kama kutaja baadhi ya yanayohusika naye Mwenyezi Mungu (s.w.t) kama kuumba kupatisha, kuruzuku, kuhuisha na kufisha na mfano wake kwa kuyanasibisha kwa asiyekuwa yeye Mwenyezi Mungu Au kama kutaja baadhi ya yasiyofanana na upande wa utakatifu wake, katika vitendo kama kushindwa, ujinga, dhuluma, mghafala na mfano wake katika sifa za upungufu na aibu kwa kuyanasibisha kwake Mwenyezi Mungu (s.w.t).

Kwa ujumla kulitakasa jina lake ni kuepuka kauli na kutaja yasiyonasibiana kuyataja kwake na jina lake Mwenyezi Mungu (s.w.t), na huko ni kumtakasa katika kiwango cha kauli kwenye kuafikiana na kumtakasa kwake katika kiwango cha kitendo. Hiyo inalazimisha Tawhid (kumpwekesha Mwenyezi Mungu) iliyo kamili kwa kukanusha kumshirikisha Mwenyezi Mungu kuliko waziwazi; kama ilivyo katika kusema kwake Mwenyezi Mungu:

"Na anapotajwa Allah peke yake nyoyo za wale wasioamini akhera, huchukiwa na wanapotajwa wale walio kinyume naye, mara wanafurahi ". (39:45).

Na pia kusema kwake: "Na unapomtaja Mola wako katika Qu'ran peke yake, basi wao hugeuza migongo yao kwa kuchukia ." (17:46).

Kutegemeza jina Mola kwa dhamiri ya mwenye kusemeshwa (jina la Mola wako) ni kutilia nguvu yale tuliyotangulia kuyataja, kwani maana ni litakase jina la Mola wako ambaye umemfanya ni Mola na wewe unalingania kuwa yeye ni Mola wa waungu, basi isitokee katika maneno yako pamoja na kutaja jina lake kwa uungu wake na kutaja mwengine, kwa kiasi ambacho kitakanusha kumwita Mungu kama alivyojijulisha kwako.

Kusemwa kwake: Mtukufu ni ambaye yuko juu ya aliye juu na kushinda kila kitu, hiyo ni sifa ya Mola wako yaani litakase jina lake kwa sababu yeye ni Mtukufu zaidi. Imesemwa kuwa maana ya aya hii ni kusema "Subhana rabial aala" hayo ni kutoka kwa Ibn Abbas, pia amesema, ni kuswali. Imesemwa makusudio ni jina vile, anavyoitwa yaani mtakase Mwenyezi Mungu S.W.T. na kila sifa na vitendo visivyofanana naye. Imesemwa kuwa makusudio ni kuyatakasa majina yake Mwenyezi Mungu (s.w.t) na yale yasiyofanana naye wala haitwi asiyekuwa yeye na jina linalomhusu yeye Mwenyezi Mungu, wala halitamkwi katika mahali pasipo nasibiana naye kama chooni n.k. Yale tuliyotanguliza kuyataja katika maana ndiyo mapana zaidi na yenye kukusanya zaidi maana na ndiyo yanayonasibiana zaidi na aya inayosema "tutakusomesha wala hutasahau" na "tutakusahilishia njia nyepesi". Kwa sababu mpangilio ni wa kupewa utume mpaka kwenye ukumbusho na tabligh. Hivyo ikaanzwa kwa maneno yake Mtume(s.a.w.w) ya kumtakasa na kila linalo tambulisha shirika kwa uwazi au kwa undani. Akamwahidi mara ya pili kumsomesha kiasi ambacho hataweza kusahau chochote katika yale aliyopewa Wahyi na kusahilishiwa njia ya Tabligh.

Aya Na 2

Kuumba kitu ni kukusanya mafungu yake na kuyapanga sawasawa kiasi ambacho huwekwa kila kitu mahali pake panapo nasibiana napo na kukipa haki yake, kama kuweka kila kiungo katika viungo vya binadamu mahali panapo nasibu. Ayah ii mpaka mwisho wa Aya Na nne zinasifu mipangilio mizuri, ya Mungu na hayo ni dalili ya uungu wake Mwenyezi Mungu (s.w.t)

Aya Na 3

Yaani ni kuvifanya vitu alivyoviuumba juu ya kiasi mahususi na mipaka yenye kuonyesha dhati zake na sifa zake na vitendo vyake visivyozidi kipimo chake na akaviandaa na yale yanayonasibiana na yaliyokadiriwa. Kwa hiyo kila mmoja anafuata upande wa yale yaliyokadiriwa kwake, kwa uongozi wa Mungu, kama mtoto kuendea titi la mama yake, kifaranga kutegemea riziki ya mama yake, mwanamume kwa mwanamke na mifano ya hayo. Mwenyezi Mungu anasema:"Na hakuna kitu chcochote ila hazina yake iko kwetu wala hatukukiteremsha ila kwa kipimo maalum ." (15:21).

Amesema tena: "Kisha akamfanyis nyepesi njia " (80:20). Amesema tena: "Kila mmoja ana mwelekeo wake wa kuelekea ." (2:148).

Aya Na 4 -5

Kutoa malisho kwa ajili ya chakula kisha kuyafanya makavu meusi ni katika usadikisho wa mipangilio ya Mungu na dalili zake; kama ilivyo katika kuumba, kulinganisha sawa, kukadiri na uongozi.

Aya Na 6-7

Amesema katika Mufradati: "Kusoma ni kukusanya herufi na matamko pamoja katika kusoma, lakini sio mkusanyiko wowote ni kusoma, huwezi kusema umewasoma watu, kama ukiwakusanya." Hiyo inafahamisha kuwa hakuwezi kuitwa kusoma kwa herufi moja. Katika Majmau anasema kusomesha ni kuchukua kisomo kwa msomaji kwa kumsikiliza ili usahihishe makosa.

Kumsomesha kwake Mtume, sio kama vile tunavyosemeshana sisi kwa kumsikiliza msomaji kisha kumsahihisha anayoyakosa. Haikuwa kwa Mtume kusoma chochote katika Qur'an akakikosea au asahau wahyi kisha asome ndipo arekebishwe la, bali makusudio yake ni kumwezesha Mtume (SAWW) kuisoma Qur'an kama ilivyoteremsha bila ya kuibadilisha, kwa kuzidisha kitu au kupunguza au kuifanya kombo kwa sababu ya kusahau. Kwa hivyo kauli yake Mwenyezi Mungu tutakusomesha hutasahau ni kiaga kitokacho kwake Mwenyezi Mungu kwa Mtume wake kumuwezesha kuijua Qur'an na kuifikisha kama ilivyoteremshwa, kiasi ambacho hataisahau. Huo ni msingi wa kufikisha wahyi (ufunuo) kama iluvyofunuliwa. Kusema kwake "Ila anachopenda Allah, ni kuvua kunakofahamisha uwezo wa Mungu ulio huru na kwamba kipawa hiki cha kutosahau sio kuwa Mungu amelazimika macho. Yeye anao uwezo wa kukusahaulisha kama akitaka.

Ayah ii kwa mpangilio wake, haiepukani kuwa inatilia nguvu yale yaliosemwa kwamba Mitume(s.a.w.w) alipokuwa akiletewa wahyi (ufunuo) na Jibril humsomea kwa kuogopa kusahau, ikawa Jibril akimaliza tu naye huanza. Basi iliposhuka ayah ii hakusahau kitu baadaye. Inakurubia kuzingatia kuwa ayah ii tutakusomesha hutosahau ilishuka kwanza ndipo ikashuka aya inayosema: "Usiutikise ulimi wako kwa (kuufanyia haraka) wahyi kwa hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha. Wakati tunapokusomea, basi fuata kusomwa kwake, kisha ni juu yetu kuubainisha ". (75:17-19).

Kisha aya inayosema: Usiifanyie haraka (hii) Qur'an kabla haujamalizika wahyi (ufunuo) wake, Na (uombe) useme. Mola wangu nizidishie elimu" (20:114).

Kusema kwake "Hakika anajua yaliyowazi na yaliofichika" kuwa wazi ni kwa kuona au kusikia kama Qur'an inavyosema: "Wakasema tuonyeshe Mungu waziwazi ". (4:153).

"Hakika yeye anajua kauli iliyo dhahiri ". (21:110) Jumla ya aya iko katika mahali pa sababu kwa maana tutakufanyia uzuri katika kupokea wahyi (ufunuo) na kuuhifadhi kwa sababu sisi tunajua dhahiri na ndani ya hali yako na vile unavyojihimu katika jambo la wahyi na unavyopupia twaa katika yale uliyoamrishwa.

Aya Na 8

Wepesi ni sifa yenye kusimama mahali pa msifiwa yaani njia nyepesi, kwa maana ya kuwa daima tutakufanyia njia ya tabligh ni nyepesi kwa maneno na vitendo utaongoza watu na itatimia hoja kwa wengine na utafanya subira juu ya maudhi yao.

Aya Na 9

Ni mtiririko wa amri iliyotangulia ya kulitakasa jina la Mola wake kuahidiwa kwake kusomeshwa wahyi kiasi ambacho hatasahau, na kusahilishiwa njia nyepesi, hizo ni sharti za kidharura ambazo zinaweza kuzuwia kufaulu mlinganio wa kidini. Maana ni kuwa ukitimiza amri ya kufuata yale tuliyokuamrisha, kukusomesha hutosahau na kukusahilishia njia ya wepesi, basi waidhisha ikiwa utafaa (huo) waadhi.

Imeshartiwa kuwa waadhi uwe wenye kunufaisha. Na hilo ni sharti juu ya uhakika wake. Kwani ikiwa waadhi hautanufaisha basi itakuwa ni upuuzi, naye Mwenyezi Mungu ametakata na kuamrisha upuuzi. Kwa hiyo kumwadhia mwenye kumcha Mwenyezi Mungu kwanza kunafahamisha kupondokea haki na hayo ndio manufaa yake (huo waadhi), vile vile kuwaidhika kama alivyosema: "Atawaidhika anayemcha (Mungu). Na kumwaidhia muovu ambaye haogopi katika moyo wake, kwanza kunafahamisha kutimia hoja juu yake na ndio manufaa yake (huo waadhi) na kunalazimisha kuejiepusha kwake, na kuikataa kwake haki kama alivyosema Mwenyezi Mungu: "Na atajiepusha nayo muovu". Waadhi baada wa waadhi haunufaishi na chochote kwa hiyo kukaamriwa kuachana naye. Mwenyezi Mungu amesema: "Basi jiepushe na wale wanaoupa mgongo ukumbusho wetu huu na wala hawataki ila maisha ya dunia ." (53:29)

Imesemekana kuwa sharti ni sharti la kisura tu! Sio la kihakika, kwamba ni kutolea habari kuwa waadhi ni wenye kunufaisha katika kuzidisha twaa na kukoma na maasi, kama inavyosemwa: Muulize inafaa kumuuliza, kwa hiyo ndio baadhi yao wakasema: "Herufi In katika aya ni kwa maana ya (Qad) hakika". Na imesemwa kuwa maneno ni ya mkato kwa kuondoa maneno mengine, kukadiria kwake ni "Basi waidhisha ikiwa utafaa waadhi na hata ukitofaa". Hilo ni kwamba yeye Mtume(s.a.w.w) amepelekwa kwa waadhi na kuonya. Kwa hiyo ni juu yake kuonya na kutoa waadhi uwe una manufaa au usiwe na manufaa; Kwa hiyo aya inaelekeana na aya inayosema: "Na amewafanyia kanzu zinazowakinga na joto (na baridi) ". (16:81).

Imesemwa kuna ishara ya kuweka mbali manufaa ya hawa wenye kutajwa; Ni kama vile imesemwa: Fanya unayoamrishwa hata kama hayatanufaisha.

Aya Na 10

Yaani atawaidhika na Qur'an yule ambaye moyoni mwake mna kitu cha kumwogopa Mwenyezi Mungu na kuogopa mateso yake.

Aya Na 11

Dhamiri ni ya mawaidha. Makusudio ya neno Ashqa kwa kulinganisha na aya iliyotangulia, ni yule asiyemwogopa Mwenyezi Mungu.

Aya Na 12

Mto mkubwa ni moto wa Jahanam, ni mkubwa kulinganisha na wa dunia. Imesemwa makusudio yake ni daraja ya chini ya Jahanam ambayo ina adhabu kali zaidi.

Aya Na 13

Makusudio ya kutokufa wala kuwa hai, ni kutookoka kabisa kwa maana ya kuwa adhabu haitakwisha wala maisha hayatabadilika kuwa mazuri. Kwa hiyo makusudio ya uhai ni maisha mema; kama alivyosema katika Ardhi; "Si hai wakutarajiwa wala si maiti wakusahauliwa".

Aya Na 14 -15

Makusudio ya kujitakasa hapa, ni kujitakasa na uchafu wenye kufungamana na dunia kwa dalili ya kusema kwake Mwenyezi Mungu: "Lakini nyinyi mnapendelea zaidi uhai wa kilimwengu." Kurejea kwa Mwenyezi Mungu kwa kumuelekea yeye Mwenyezi Mungu ni kujitakasa. Kutoa katika njia ya Mwenyezi Mungu ni kujitakasa na uchafu unaofungamna na mali. Hata udhu wa swala ni mfano wa kujitakasa na yale yaliyochumwa na nyuso, mikono na miguu. Kusema kwake: Akalikumbuka jina la Mola wake akaswali, makusudio yake kwa dhahiri ni kumtaja Mwenyezi Mungu kwa kutamka, na kuswali ni swala ya kawaida ya Kiislamu. Aya mbili hizi kwa dhahiri ufahamisho wake ni kuenea a kila kitu, lakini imepokewa kutoka kwa Maimamu wa Ahlul Bait(a.s) kuwa aya hizo zinahusu zaka ya fitri na swala ya Idd. Vile vile hayo yamepokewa katika Ahli Sunnah.

Aya Na 16

Msemo huo unaelekezwa kwa watu juu ya tabia yao ya kiutu inayopelekea kufungamana kabisa na dunia na kujishughulisha na kuiamirisha. Imesemwa kuwa msemo unawaelekea makafiri tu. Kwa hali yoyote maneno ni yenye kuelekezwa kwenye lawama.

Aya Na 17

Imehisabiwa akhera ni yenye kubakia kulinganisha na dunia, pamoja na kuwa yenyewe akhera ni yenye kubaki milele, kwa sababu ya kupima kati ya dunia na akhera.

Aya Na 18-19

Neno haya "Linaonyesha yale yaliyobainishwa kuanzia aya 14 mpaka 17. Imesemwa kuwa ni hAya Na kuwa akhera ni bora na ni yenye kubaki. Imesemwa kuwa kusema vitabu vya kwanza tu. Kisha kuvibainisha kuwa ni vitabu vya Ibrahim na Musa ni kwa ajili ya kutukuza na kukuza jambo.

Utafiti Wa Hadith Katika Tafsiri ya Iyashi kutoka kwa Uqba bin Amir El-Jahaniy amesema iliposhuka aya inayosema: "Litakase jina la Mola wako aliye mkuu" Mtume(s.a.w.w) alisema ifanyeni katika kurukui kwenu. Na iliposhuka "Litakase jina la Mola wako aliye Mtukufu akasema": Ifanyeni katika kusujudi kwenu. Hadith hiyo pia imepokewa katika Durril Manthur kutoka kwa Ahmad, Abu Dawud, Ibn Maja Ibn El-Mundhir na Ibn Murdawayh nao wamepokea kutoka ka Uqba naye kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) .

Katika Tafsiri ya Qummi kuhusu Aya Na kwanza amesema: "utakata ni kwa Mola wangu aliye Mtukufu". Kuhusu na ambaye ameumba akakamilisha na ambaye makadirio ya mwanzo kisha akaviongoza.

Katika Durril Manthur ametoa Ibn Murdawayh kutoka kwa Ibn Abbas amesema: "Mtume(s.a.w.w) alikuwa anajikumbusha Qur'an kwa kuhofia kusahau akaambiwa tumekutoshea na hilo", na ikashuka aya Tutakusomesha wala hutasahau. Katika Faqih aliulizwa Imam As Sadiq(a.s) kuhusu kusema kwake Mwenyezi Mungu (s.w.t) "Hakika amefaulu mwenye kuitakasa " Akasema: "Ni mwenye kutoa zaka ya fitr". Akaulizwa: na akamkumbuka Mola wake, akaswali? Akasema ni aliyetoa uwanjani akaswali. Amepokea hadith kwa maana hii Hammad, naye kutoka kwa Jarir naye kutoka kwa Abu Baswir na Zurarah kutoka kwake Imam Jaffar As Sadiq(a.s) . Katika Durril Manthur ametoa Ibn Murdawayh kutoka kwa Abu Said Al-Khudri amesema: Mtume(s.a.w.w) alikuwa akisema: "Hakika amefaulu mwenye kujitakasa na akamkumbuka Mola wake akaswali " Kisha hugawanya zaka ya fitr kabla ya kwenda kwenye mswala siku ya Idd-ul-fitr.

Vile vile kumepokewa kushuka aya mbili hizo katika zaka ya fitri na swala ya Idd kwa njia mbili kutoka kwa Abu Said, vile vile kwa njia mbili kutoka kwa Ibn Umar kwa njia moja kutoka kwa Naila bin Al-Asqa, kwa njia mbili kutoka kwa Abu Aliya na kwa njia moja kutoka kwa Atau. Vile vile kwa njia moja kutoka kwa Muhammad bin Sirin, kwa njia moja kutoka kwa Ibrahim Annakhyi na kutoka kwa Amru bin Awf naye kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) .

Katika Khiswali imepokewa kutoka kwa Utbah bin Amru Allaythi naye kutoka kwa Abu Dharr katika hadith inayosema: "Nilimuuliza Mtume(s.a.w.w) ni kitu gani katika dunia alichokuteremshia Mwenyezi Mungu kilichokuwa katika vitabu vya Ibrahim na Musa? Akasema, Ewe Abu Dharr, soma: hakika amefaulu mwenye kujitakasa akalikumbuka jina la Mola wake akaswali. Lakini nyinyi mnapendelea zaidi uhai wa kilimwengu. Hali akhera ni bora na yenye kubaki. Hakika hayo yamo katika vitabu vya kwanza vitabu vya Ibrahim na Musa. Hadithi inatilia nguvu kuwa ishara na neno "haya" ni mkusanyiko wa aya nne kama ilivyotangulia. Katika Baswir kwa isnadi yake kutoka kwa Abu Baswir amesema Abu Abdillah: Tunazo suhuf alizozitaja Mwenyezi Mungu katika Aya Na 19: Nikamwambia ni mbao? Akasema ndio. Amepokea vile vile kwa njia nyengine Abu Baswir kutoka kwake Abu Abdillah(a.s) . Kwa dhahiri ni kwamba makusudio ya kuwa Suhuf ni mbao nikuwa ni Taurat yenye kuelezewa katika Qur'an kama mbao; kama alivyosema Mwenyezi Mungu (s.w.t): "Na ukamwandikia katika mbao kila kitu ." (7:145).

Na pia kusema kwake Mwenyezi Mungu:'na akazitupa mbao .." (7:150). Na kusema kwake "aliziokota zile mbao " (7:154).

Katika Majmau imepokewa kwa Abu Dharr, yeye amesema: "Nilimuuliza Mtume wa Mwenyezi Mungu ni Mitume wangapi? Akasema: Ni laki moja na ishirini na nne elfu (124,000) nikamuuliza ni wangapi walio Mursaal katika wao? Akasema mia tatu na kumi na tatu (313). Nikasema Adam alikuwa Mtume. Akasema ndio Mwenyezi Mungu alimsemesha na amemuumba kwa mkono wake. Ewe Abu Dharr, Mitume waarabu ni Hud, Saleh, Shuayb na Mtume wako.

Nikasema tena: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu ameteremsha vitabu vingapi? Akasema mia moja na nne (104). Kwa Adam mbao kumi, kwa Shiyth hamsini kwa Ukhnun ambaye ni Idris thelathini naye ndiye wa kwanza kuandika kwa kalamu, Ibrahim kumi na Taurat, Injil, Zabur na Qur'an. Yamepokewa hayo katika Durril Manthur kutoka kwa Abd bin Hamid, Ibn Murdawayh na Ibn Asakir nao kutoka kwa Abu Dharr isipokuwa hazikutajwa mbao za Adam na zimetajwa mbao kumi za Musa kabla ya Taurat.

13

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

SURA GHASHIYA (KIYAMA) (NA. 88)

INA AYA 26

Kwa jina la Allah, Mwingi wa Rehema, Mwnye kurehemu

هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ الْغَاشِيَةِ ﴿١﴾

1. Je, imekujia habari ya Kiyama?

وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ خَاشِعَةٌ ﴿٢﴾

2. Nyuso siku hiyo zitadhalilika.

عَامِلَةٌ نَّاصِبَةٌ ﴿٣﴾

3. Zitatumika na kutaabika.

تَصْلَىٰ نَارًا حَامِيَةً ﴿٤﴾

4. Zitaingia katika moto mkali.

تُسْقَىٰ مِنْ عَيْنٍ آنِيَةٍ ﴿٥﴾

5. Zitanyweshwa maji ya chemshemi ichemkayo.

لَّيْسَ لَهُمْ طَعَامٌ إِلَّا مِن ضَرِيعٍ ﴿٦﴾

6. Hawatakuwa na chakula isipokuwa cha miba.

لَّا يُسْمِنُ وَلَا يُغْنِي مِن جُوعٍ ﴿٧﴾

7. Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.

وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ نَّاعِمَةٌ ﴿٨﴾

8. Nyuso siku hiyo zitanawiri.

لِّسَعْيِهَا رَاضِيَةٌ ﴿٩﴾

9. Zitakuwa radhi kwa amali yake.

فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٍ ﴿١٠﴾

10. (Zitakuwa) katika pepo iliyo tukufu.

لَّا تَسْمَعُ فِيهَا لَاغِيَةً ﴿١١﴾

11. Hazitasikia humo upuuzi.

فِيهَا عَيْنٌ جَارِيَةٌ ﴿١٢﴾

12. Humo mna chemichemi inayotiririka.

فِيهَا سُرُرٌ مَّرْفُوعَةٌ ﴿١٣﴾

13. Mna malili yaliyotukuzwa.

وَأَكْوَابٌ مَّوْضُوعَةٌ ﴿١٤﴾

14. Na vikombe vilivyowekwa.

وَنَمَارِقُ مَصْفُوفَةٌ ﴿١٥﴾

15. Na mito iliyopangwa.

وَزَرَابِيُّ مَبْثُوثَةٌ ﴿١٦﴾

16. Na mazulia yaliyotandikwa.

أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى الْإِبِلِ كَيْفَ خُلِقَتْ ﴿١٧﴾

17. Je, hawamtazami ngamia namna gani alivyoumbwa.

وَإِلَى السَّمَاءِ كَيْفَ رُفِعَتْ ﴿١٨﴾

18. Na mbingu namna gani zilivyoinuliwa?

وَإِلَى الْجِبَالِ كَيْفَ نُصِبَتْ ﴿١٩﴾

19. Na majabali namna gani yalivyo simamishwa.

وَإِلَى الْأَرْضِ كَيْفَ سُطِحَتْ ﴿٢٠﴾

20. Na ardhi namna gani ilivyotandikwa.

فَذَكِّرْ إِنَّمَا أَنتَ مُذَكِّرٌ ﴿٢١﴾

21. Basi kumbusha, hakika wewe ni mkubushaji tu!

لَّسْتَ عَلَيْهِم بِمُصَيْطِرٍ ﴿٢٢﴾

22. Wewe si mtenza nguvu.

إِلَّا مَن تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ ﴿٢٣﴾

23. Lakini mwenye kupa mgongo akakufuru.

فَيُعَذِّبُهُ اللَّـهُ الْعَذَابَ الْأَكْبَرَ ﴿٢٤﴾

24. Allah atamwadhibu adhabu kubwa mno!

إِنَّ إِلَيْنَا إِيَابَهُمْ ﴿٢٥﴾

25. Hakika ni kwetu sisi marejeo yao.

ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا حِسَابَهُم ﴿٢٦﴾

26. Kisha ni juu yetu sisi hesabu yao.

UBAINIFU

Ni Sura ya maonyo na biashara. Inasifu Kiyama kwa hali ambayo watu watakuwa nayo ya kugawanyika makundi mawili: Wema na waovu, na kutua kwao katika sehemu walizoandaliwa miongoni mwa pepo na moto. Inamalizia kwa kumwamrisha Mtume(s.a.w.w) kuwakumbusha watu fani za mazingatio ya Mungu katika ulimwengu zenye kufahamisha juu ya uungu wake, na kurudi kwao kwake kwa ajili ya kuhisabiwa. Sura imeshuka Makka kwa ushahidi wa mpangilio wa aya zake.

Aya Na 1

Ni swali linalopelekea kukuza mambo. Limetumiwa neno kufudikiza (Ghashiya) kwa maana ya Kiyama, kwa sababu kitawafudikiza watu na kitawazingira kama alivyosema Mwenyezi Mungu: "Na tutawafufua wala hatutamwacha hata mmoja katika wao ." (18:47). Au kimeitwa hivyo kwa kuwa kitafudikiza nyuso za makafiri kwa adhabu.

Aya Na 2

Yaani nyuso ni zenye kudhalilika kwa ghamu na adhabu itayozifunika. Kudhalilika kutawapata wenye nyuso, lakini hapa kumenasabishwa kwenye nyuso, kwa sababu kunadhihiri katika uso.

Aya Na 3

Makusudio yake kwa kulinganisha na aya inayokabiliana nayo katika sifa ya watu wa peponi inayosema "Zitakuwa radhi kwa mali yake" ni kuwa kutumika kwake ni katika dunia na kutaabika kwake ni katika akhera. Hakika mtu anafanya anayoyafanya katika dunia ili atengenekewe, na apate matakwa, lakini amali zao ni bure tu; Hazitawafaa na chochote, kama alivyosema Mwenyezi Mungu: "Na tutayaendea yale waliyoyatenda katika amali tuyafanye kama mavumbi yaliyitawanywa ". (25:23).

Kwa hiyo hakirudi chochote katika waliyoyafanya isipokuwa taabu, kinyume cha watu wa peponi, kwani hakika wao mahangaiko yao waliyohangaika katika dunia ni kibali kitakachowapeleka katika pepo siku ya Kiyama. Imesemwa makusudio yake ni kutumika katika dunia kwa maasi na kutaabika katika moto siku ya Kiyama.

Aya Na 4

Yaani ni moto katika ukomo ya joto.

Aya Na 5

Yaani ni yenye joto kali.

Aya Na 6

Dhwarii ni aina ya miba ambayo watu wa Hijazi wanaita hivyo inapokauka. Na chakula kibaya sana, hawawalishi hata wanyama wao. Huenda hiyo ya motoni imeitwa hivyo, kwa kufanana.

Aya Na 7

Kunawiri ni fumbo la furaha inayodhihiri usoni kama ilivyosemwa: "utaona katika nyuso zao mng'ao wa kunawiri ." (83:24). Au itakuwa kwa maana ya kuneemeka. Imesemwa haikuwekwa herufi za kuunganisha kwa kuonyesha ubainifu kamili kati ya hali za makundi mawili.

Aya Na 8

Makusudio ya amali njema yaani imeridhia amali yake njema kwa kulipwa malipo mema.

Aya Na 9-16

Ni utukufu wa daraja yake, kwani katika hiyo pepo kuna maisha yasiyokuwa na kifo, ladha isiyokuwa na machungu yoyote, na furaha isiyokuwa na huzuni. Kusema kwake "Hazitasikia humo upuuzi" yaani hizo nyuso hazitasikia tamko lolote lisilokuwa na faida. Kuhusu chemchemi makusudio yake ni jinsi yake, na amezihesabu Mwenyezi Mungu chemchemi katika hiyo pepo katika maneno kama Salsabil Kinywaji kitakatifu nk.

Aya Na 17

Baada ya kumaliza kukisifu Kiyama na kubainisha hali za makundi mawili wa waumini na makafiri, amefuatishia kuishiria kijumla mipangilio mizuri ya Mungu ambayo inabainisha uungu wake, inayohukumilia kumwabudu kwake, na hilo likafuatiwa na hisabu ya matendo na malipo ya muumin kwa imani yake na kafiri kwa kufuru yake. Wakati wake hayo ni siku ya Kiyama. Kwanza amewaambia kuangalia ngamia vile alivyoumbwa. Vipi alivyoitia sura Mwenyezi Mungu ardhi isiyokuwa na uhai wala hisia, kwa Sura hii ya ajabu katika viungo vyake, nguvu zake na vitendo vyake. Akaitiisha kwao ili wanufaike nayo kwa kuipanda, uchukuzi, nyama yake, maziwa yake, ngozi yake na sufu yake. Na hata mkojo wake na kinyesi chake. Je, yote hAya Na mezuka tu kwa bahati bila ya kupangwa? Kuhusisha kutaja ngamia ni kwa njia kuwa Sura imeshuka Makka na ngamia alikuwa ndio nguzo ya maisha ya waarabu.

Aya Na 18

Imepambwa hiyo mbingu kwa jua, mwezi na sayari nyenginezo kwa manufaa ya watu wa dunia; na amejaalia hewa ambayo wanalazimika wanyama kuivuta.

Aya Na 19

Majabali ndio vigingi vya ardhi vinavyoizuia ardhi isitetemeke na hazina ya maji ambapo mito na chemchem hububujika kutoka huko na ni hifadhi za madini.

Aya Na 20

Yaani imatendikwa ili mwanadamu aweze kukaa na kumsahilikia kuguru hapa na pale na matumizi mengine ya kiufundi. Basi mipangilio yote hii imetegemezwa kwa Mwenyezi Mungu bila ya wasiwasi wowote. Yeye ni Mola wa mbingu ardhi na vilivyo ndani yake. Yeye ni Bwana wa ulimwengu wa kibinadamu, niwajibu kwao kumfanya ndiye Mola, kumpwekesha na kumwabudu na mbele yao kuna Kiyama ndiyo siku ya hesabu ya malipo.

Aya Na 21

Ni sehemu ya yaliotangulia maana yake ikiwa Mwenyezi Mungu ndiye Mola na hakuna Mola asiyekuwa yeye na mbele yao kuna siku ya hesabu na malipo kwa aliyeamini katika wao au aliyekufuru, basi wakumbushe hilo. Kusema kwake "Hakika wewe ni mkumbushaji tu " ni ubainifu wa kuwa kazi ya Mtume ni kukumbusha tu kwa kutarajia kuitikiwa na kuaminiwa bila ya kulazimisha.

Aya Na 22

Ni ubainifu na tafsiri ya aya iliyotangulia.

Aya Na 23

Hapo anavuliwa na ukumbusho yule mwenye kupa mgongo na kukufuru. Ilivyo ni kuwa kukanusha kumekuja baada ya ukumbusho; kukanusha kwa kuvua, ni ukumbusho baada ya ukumbusho. Ni kama vile imesemwa wakumbushe na udumishe ukumbusho isipokuwa yule ambaye umemkumbusha akapa mgongo na kukufuru. Kwa hiyo huna haja ya kudumisha kumkumbusha bali achana naye. Mwenyezi Mungu atamwadhibu adhabu kubwa. Aya Na 21 - 24 katika Sura hii zinalingana na Aya Na 9 -12 ya Sura ya Al-A'laa (87). Imesemekana kuwa sio kuvuliwa na ukumbusho bali nikuvuliwa kutenza nguvu, na maana ni wewe simtenza nguvu isipokuwa juu ya yule mwenye kupa mgongo akakufuru ndio Mwenyezi Mungu anakusaliti naye na kukuamrisha kufanya jihadi; utapigana naye na kumuua. Na imesemwa kuvua hapa ni kwa kukataa tu, Kwa maana; wewe si mtenza nguvu, lakini mwenye kupa mgongo akakufuru katika wao hataachwa bure. Atamwadhibu Mwenyezi Mungu adhabu kubwa. Tuliyoyatanguliza kuyataja yako karibu na yenye nguvu zaidi.

Aya Na 24-25

Imetangulizwa "ni kwetu sisi" kwa sababu ya kutilia mkazo. Na aya hiyo iko katika mahali pa illa (sababu) ya kuadhibu kulikotajwa katika aya iliyotangulia.

Utafiti Wa Hadith Katika Majmau imepokewa kutoka kwa Ibn Abbas amesema: "Amesema Mtume(s.a.w.w) Dhwarii ni kitu katika moto kinafanana na mwiba kichungu kuliko shubiri. Kinanuka uvundo kuliko mzoga na ni kikali kuliko moto. Katika Tafsiri ya Qummi kuhusu kwake Mwenyezi Mungu "Hawatasikia humo upuzi" ni upuuzi na uwongo." Kuhusu Aya Na 22 amesema yaani sio mwenye kuwachunga. Katika Durril Manthur ametoa Ibn Jariyr, Hakim, Ibn Murdawayh na Bayhaqi kutoka kwa Jabir amesema: 'Amesema Mtume(s.a.w.w) : "Nimeamrishwa kupigana na watu mpaka waseme: "La ilaha illa llahu" wakisema, damu yao na mali zao zitakuwa zimesalimika isipokuwa kwa haki yake, na hisabu yao iko juu ya Mwenyezi Mungu, kisha akasoma aya "Basi kumbusha hakika wewe ni mkumbushaji wewe si mtenza nguvu ". Hakuna dalili yoyote kwamba kuvua kunatokana na dhamiri ya wao na hilo ni dhahiri.

Katika hiyo Durril Manthur katika hadith iliyopokewa kutoka kwa Abu Jaffar(a.s) kuhusu kusema kwake Mwenyezi Mungu: "Lakini mwenye kupa mgongo na akakufuru" anakusudia yule asiyewaidhika, na asiyesadiki akakanusha uungu na akakufuru neema. "Atamwadhibu Allah adhabu kubwa mno!" anakusudia adhabu nzito ya milele. "Hakika ni kwetu sisi marejeo yao" anakusudia mwisho wao "kisha hakika ni juu yetu sisi hesabu yao" anakusudia malipo yao. Katika Nahj aliulizwa Ali(a.s) vipi atawahisabu Mwenyezi Mungu watu na wingi wao huo? Akasema: Kama vile anvyowaruzuku na wingi wao. Kukaulizwa vipi atawahisabu na hawamuoni? Akasema kama anavyowaruzuku na hawamwoni.

Katika hiyo hiyo Nahj amesema As Sadiq, kila Umma utahisabiwa na Imam wa zama zake. Na wanawajua maimam marafiki zao na maadui zao kwa alama zao na ndio maana ya kauli yake Mwenyezi Mungu: "Na juu ya mahali hapo palipoinuka watakuaweko watu hao watakaowafahamu wote kwa alama zao ". (7:46). Imepokewa hadith kwa maana haya katika Baswir kutoka kwa Sadiq, katika Kafi kutoka kwa Baqir na Kadhim(a.s) na katika Faqih kutoka kwa Hadi(a.s) .


9

10

11

12

13

14

15

16