MALEZI YA WATOTO KATIKA UISLAMU

MALEZI YA WATOTO KATIKA UISLAMU Mwandishi:
Kundi: Familia na watoto

  • Anza
  • Iliyopita
  • 9 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 14686 / Pakua: 4750
Kiwango Kiwango Kiwango
MALEZI YA WATOTO KATIKA UISLAMU

MALEZI YA WATOTO KATIKA UISLAMU

Mwandishi:
Swahili

MALEZI YA WATOTO KATIKA UISLAMU

KIMEANDIKWA NA: JOPO LA MAULAMAA (MISRI)

KIMETARJUMIWA NA: USTADH ABDALLAH MOHAMED

KIMEHARIRIWA NA: HEMEDI LUBUMBA SELEMANI

KIMEPANGWA KATIKA KOMPYUTA NA: UKHTI PILI RAJAB

NENO LA MCHAPISHAJI

Kitabu ulichonacho mikononi mwako asili yake kimeandikwa kwa Kiingereza na jopo la maulamaa wa Misri kwa jina la Child Care in Islam. Sisi tumekiita: Malezi ya Watoto katika Uislamu.

Kama inavyofahamika kwamba; Uislamu ni dini na ni mfumo wa maisha, basi mafundisho yake hayakuacha kitu kinachohusiana na maisha ya mwanadamu - kuanzia tumboni mwa mama yake, kuzaliwa kwake, kunyonya na kulikizwa kwake, kufunzwa mambo ya kimsingi na mama yake, mpaka kufikia kimo cha kwenda shuleni. Haya yameelezwa kwa utaratibu mzuri sana kutoka kwenye vyanzo viwili vikubwa vya sheria ya Kiislamu - Qur'ani na Sunna.

Kwa mujibu wa Uislamu kipindi cha mafunzo ya watoto huanza wakati mwanaume na mwanamke wanapoingia katika ushirika wa ndoa, kama wazazi wa baadaye, ni lazima wajihisi kwamba wana wajibu wa kuwalea watoto wao. Hii ni kwa sababu kwa mujibu wa kanuni za kurithi (tabia), mwenendo wote wa tabia nzuri na mbaya wa wazazi hurithiwa na watoto wa wazazi hao. Hivyo, mzazi akiwa na tabia nzuri atawarithisha watoto wake tabia hiyo, na ni kwa sababu hii mafunzo ya watoto huanzia punde tu wakati mume na mke wanapoingia katika ndoa. Ili kufanikisha somo la kitabu hiki, jopo hilo la maulamaa limerejea sana kwenye vyanzo hivyo viwili - Qur'ani na Sunna. Watoto ni taifa la kesho, na ili kuwa na taifa zuri lenye maadili mema, lazima kuwalea watoto katika mazingira mazuri ya kimaadili; na ni mafunzo ya Kiislamu tu, kama yatafundishwa vizuri na kuzingatiwa basi Umma utaondokana na matatizo mengi ya kijamii kama inavyoonekana hivi sasa.

Tumekiona kitabu hiki ni chenye manufaa sana, hususan katika wakati huu ambapo jamii inazidi kudidimia katika maovu kutokana na kumomonyoka kwa maadili mema. Taasisi yetu ya Al-Itrah Foundation imeamua kukichapisha kitabu hiki kwa lugha ya Kiswahili kwa madhumuni yaleyale ya kuwahudumia Waislamu, hususan wazungumzaji wa Kiswahili. Tunamshukuru ndugu yetu A. Mohamed kwa kukubali jukumu hili la kukitarjumi kitabu hiki. Vilevile tunawashukuru wale wote walioshiriki kwa njia moja au nyingine hadi kufanikisha uchapishaji kitabu hiki.

Mchapishaji: Al-Itrah Foundation

S. L. P. 19701

Dar-es-Salaam, Tanzania.

MALEZI YA WATOTO KATIKA UISLAMU

Mwanzo Qur ani tukufu na Hadith, ndivyo vitu viwili vya kimsingi ambavyo vinaunda Sheria za Kiislamu na kuzi hakikisha, na ni kutokana na vitu viwili hivyo ndipo misingi yote ya dini inaporejea. Hata hivyo, ni Qur ani tukufu tu ndiyo marejeo makubwa ambayo Hadith zinategemea. Kwa ajili hiyo, Hadith hazitofautiani au kupingana na Qurani ambayo inaaminiwa kuwa ndi yo asili ya ukweli wote.

Miongoni mwa maudhui yenye maana sana ya Qur ani tukufu, ni kuwa inaeleza kanuni na Sheria zote za mwanzo kusaidia watu ili waweze kupanga vizuri maisha yao, na hivyo kuweza kubadilisha desturi zilizokuwa zikifuatwa.

Kwa maana hiyo Qur ani imehifadhi haki za kila mmoja, na za jamii, imefanya kuenea kwa uadilifu, imewapa watu moyo wa kuishi pamoja kwa ushirikiano na ihsani, na imeweka kipimo cha kumcha Mwenyezi Mungu kuwa ndiyo tofauti pekee baina ya watu. Hadith ni chochote kile ambacho Mtume(s.a.w.w) amekitenda na ambacho si Qurani; au mambo ambayo yamemfikia kupitia kwa ufahamu wake au maono, na kuthibitishwa na Mwenyezi Mungu. Kwa hiyo (Sunnah) inakusanya vitendo na maneno yanayohusika na ufafanuzi wa itikadi, Swala au ibada nyinginezo, pia kulingana na uhusiano mwema baina ya ndugu, kumfundisha mwenendo mzuri, na kuamrisha mambo mema na kukataza maovu.

Kwa hivyo chochote kilichotendwa na Mtume(s.a.w.w) katika hali kama hiyo, huchukuliwa kama sunnah, na watu wanatakiwa kukifuata. Chochote kile ambacho hakihusiani na hayo yaliyotajwa hapo awali, kama vile kula, kunywa, au kuvaa nguo, hakichukuliwi kuwa ni sunnah, na watu hawalazimiki kukifuata.

Mtume(s.a.w.w) amesema:Hakika mimi ni mwanaadamu, pindi nitakapowaamrisha jambo linalohusiana na dini yenu, lifuateni, na nitakapowaamrisha jambo kutokana na maoni yangu, basi kumbukeni kuwa mimi ni mwanaadamu.

Ushahidi wa jambo hili ni ushauri ambao Mtume(s.a.w.w) alizoea kuutoa kuhusiana na kutaf uta tiba ya baadhi ya maradhi. Ushauri ambao hakuletewa wahyi ila ni kutokana na uzoefu alioupata kutokana na kuishi katika mazingira ya kibinaadamu.

Ametaja Abu Daud katika Isnadi yake, kutoka kwa Usama kwamba: Nilikwenda kwa Mtume(s.a.w.w) naye alikuw a ameketi na maswahaba zake, nao walikuwa (wametulia) kama kwamba kuna ndege juu ya vichwa vyao, nikawatolea salaam, kisha nikaketi. Wakaja mabedui kutoka huku na huko wakasema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, je tunaweza kujitibu? Mtume(s.a.w.w) akasema:Mnaweza kujitibu, kwani Mwenyezi Mungu Mtukufu hakuumba ugonjwa pekee ila ameumba na dawa yake, isipokuwa ugonjwa wa aina moja tu, kifo.

Hadith nyingine iliyopokewa kutoka kwa Umar Bin Dinar imetaja jambo hilo (pia).

Siku moja Mtume(s.a.w.w) alimtembelea mgonjwa, akawaambia nduguze, Mwiteni daktari, mmoja wao akasema: hata nawe pia wasema hivyo ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?! Mtume akasema:Ndiyo, kwani Mwenyezi Mungu Mtukufu hakuumba maradhi ila ameumba na dawa yake.

Kitendo cha Mtume(s.a.w.w) cha kuwataka ndugu za wagonjwa kumwita daktari kinaonyesha kwamba utabibu wa madawa si miongoni mwa mambo aliyofunuliwa (wahyi) kutoka kwa Mwenyezi Mungu, na ni kwa sababu hii ndipo akawashauri watu kufuata ushauri wa daktari pale unapohitajika.

Pia hali hiyo inahusiana na jinsi alivyokuwa akivaa na kula, ilivyokuwa ikilingana na tabia za wakati wake na mahali alipoishi. Na lau kama angeishi katika mazingira na wakati tofauti, basi pengine angestawisha desturi zingine.

Kwa hivyo basi, Sunnah (Hadith) inafafanua Qur ani, inachambua hukmu zake, inaikamilisha, inaelezea na kuamua kuhusu mipaka ambayo inatawala kanuni zake kamili, na inafafanua sehemu zenye kutatanisha. Na endapo itaongezea chochote, ziada hiyo haiwezi kupingan a na misingi ya kanuni za Qur ani. Kwa hivyo uhusiano wa Sunnah na Qurani ulivyo ni kama hali ya kiongozi na mfuasi. Kwa ajili hiyo, Hadith inafuata kile kilichokuja katika Qurani na inaambatana nayo moja kwa moja. Inadhihirika wazi sasa, kwa nini Quran i inatangulia Sunnah, na kuchukuliwa kuwa ni msingi wa Uislamu, wakati ambapo Sunnah inaikamilisha Qur ani kwa kanuni.

Mkusanyiko huu (wa kitabu hiki kinachohusu malezi ya mtoto) umetokana na yale yaliyotajwa katika Qur ani yahusuyo malezi ya mtoto, na k atika Sunnah kuhusiana na mambo haya. Ili kutoa mwanga, habari zaidi na ufafanuzi uliyomo katika Qur ani, baadhi ya methali na dondoo maarufu zimeongezwa ili ziwe ni mifano mizuri na yenye nguvu zaidi.

1

MALEZI YA WATOTO KATIKA UISLAMU

SEHEMU YAKWANZA

1.HALI NA HAKI ZA MTOTO KATIKA UISLAMU

Hawa ni watoto wetu kwetu sisi wenye hadhi Ni kama maini yetu yaendayo kwenye ardhi Na tulivyo kati yetu hatuwezi kuwa radhi Tuwaonapo wanetu wanaugua maradhi (Tafsiri ya shairi la kale la kiarabu) Umoja wa mataifa umeanza kuonyesha kuvutiwa na suala la watoto kwa kufanya maadhimisho ya Siku ya Watoto katika mwezi wa Novemba kila mwaka, ambayo inalingana na maadhimisho ya kutangazwa kwa haki za mtoto.

Kwa hali yoyote ile, ipo haja ya kutaja hapa kwamba, mazingatio ya Uislamu kwa watoto yameanza zamani na yanarejea nyuma zaidi ya miaka elfu moja na mia nne.

Uislamu kwa mfululizo unaadhimisha na kuonyesha huruma yake kwa mtoto, si baada ya kuzaliwa tu, bali hata kabla ya kuzaliwa, na umeelezewa kwa makini haki zake. Wakati wa utoto katika Uislamu umepewa picha ya ulimwengu mzuri wa furaha, uzuri, ndoto, mapenzi na ruya njema.

Na aya za Qur ani zinaonyesha mapenzi ya Mwenyezi Mungu kwa watoto, na ndipo akaapa Mwenyezi Mungu:

لَا أُقْسِمُ بِهَـٰذَا الْبَلَدِ ﴿١﴾ وَأَنتَ حِلٌّ بِهَـٰذَا الْبَلَدِ ﴿٢﴾ وَوَالِدٍ وَمَا وَلَدَ ﴿٣﴾

Naapa kwa mji huu, (wa Makkah). Na wewe utahalalishwa katika mji huu. Na (kwa) mzaz i na alichokizaa. (90:1-3).

Watoto wameelezwa katika Qur ani kuwa ni bishara njema. Amesema Mwenyezi Mungu:

يَا زَكَرِيَّا إِنَّا نُبَشِّرُكَ بِغُلَامٍ اسْمُهُ يَحْيَىٰ ﴿٧﴾

Ewe Zakaria tunakupa habari njema ya (kupata) mtoto jina lake ni Yahya (19:7).

Pia watoto ni kiburudisho cha macho yetu. Amesema Mwenyezi Mun gu:

رَبَّنَا هَبْ لَنَا مِنْ أَزْوَاجِنَا وَذُرِّيَّاتِنَا قُرَّةَ أَعْيُنٍ وَاجْعَلْنَا لِلْمُتَّقِينَ إِمَامًا ﴿٧٤﴾

Ewe Mola wetu, tupe katika wake zetu na watoto wetu watakaoyaburudisha macho yetu (25:74).

Na watoto ni pambo la maisha katika ulimwengu huu.

الْمَالُ وَالْبَنُونَ زِينَةُ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا ﴿٤٦﴾

Mali na watoto ni pambo la maisha ya duniani (18:16).

Mtume(s.a.w.w) anatudhihirishia ya kuwa ulimwengu wa utoto ni kama pepo, pale aliposema: Watoto ni vipepeo vya Peponi.

Kuwatunza watoto ni jambo la lazima, na kuwapenda humleta mtu karibu na Mwenyezi Mungu. Mtume(s.a.w.w) amesema:Lau kama si watoto wanyonyeshwao, na wazee wanaorukuu (kwa kuswali) na wanyama walishwao mashambani, basi mngelipatwa na adhabu kali.

Inaonyesha wazi kwamba huruma na uangalifu wa Mwenyezi Mungu kwa watoto ndiyo uliofanya Mwenyezi Mungu kuzuia adhabu juu ya watu wake.

MAPENZI YA MTUME KWA WATOTO

Mapenzi ya Mtume(s.a.w.w) kwa watoto yalijaa ndani ya moyo wake mwema, imeelezwa katika Hadith: Siku moja Mtume(s.a.w.w) alipanda juu ya mimbari akiwahutubia watu, (mara) akawaona Hasan na Husein(a.s) wanakimbia na huku wakijikwaa, akakatiza hotuba yake, akashuka kutoka juu ya mimbari kwenda kuwapokea watoto hao wawili. Akawabeba mikononi mwake, kisha akapanda tena juu ya mimbari akasema:Enyi watu, hakika mali zenu na watoto wenu ni fitina, Wallahi nimewaona wajukuu zangu wawili wakikimbia na kujikwaa, basi sikuweza kujizuia mpaka nimeshuka nikawabeba.

Siku moja Mtume(s.a.w.w) alikuwa anaswali, mara Hasan na Husein(a.s) wakaingia ndani na kumpanda mgongoni kwake wakati alipokuwa amesujudu, Mtume(s.a.w.w) akaendelea kusujudu tu. Alichukia kuwaharakisha washuke, mpaka waliposh uka wao wenyewe. Kisha alipotoa salaam na kumaliza Swala, akaulizwa na maswahaba zake sababu zilizomfanya asujudu kwa kitambo kirefu hivyo; akawajibu:Wajukuu zangu wawili walikuwa wamepanda juu ya mgongo wangu nami nilichukia kuwahimiza washuke kwa haraka.

Mtume(s.a.w.w) alizoea kuharakisha Swala yake pindi asikiapo mtoto analia, na husema:Mimi huchukia kumchosha mama yake . Siku moja alikuwa anapita nyumbani kwa Fatima(a.s) (binti yake), akamsikia mjukuu wake Husein(a.s) akilia, aliingia ndani n a baada ya kumkemea Fatima akasema:Je hujui kwamba nimsikiapo Husein akilia huwa nakereka? Siku moja Mtume(s.a.w.w) alitembelewa na Al-Akraa Ibn Habis, ambaye alimwona Mtume(s.a.w.w) akiwabusu wajukuu zake, Al-Akraa akasema: Unawabusu watoto wa binti y ako? Naapa kwa Mungu nina watoto kumi,

na sijawahi kumbusu hata mmoja. Mtume(s.a.w.w) akamjibu:Je ni kosa langu kama Mwenyezi Mungu ameing’oa rehma kutoka moyoni mwako.

2. UMUHIMU WA MTOTO KATIKA UISLAMU KABLA YA KUZALIWA

Kutilia maanani kwa Uislamu kuhusu malezi ya mtoto hakuanzi baada ya kuzaliwa tu, bali hata kabla hajaanza kupata umbo (tumboni) kwani Uislamu unamuamuru mtu kuoa mke mcha Mungu na mtulivu.

Mtume(s.a.w.w) amesema:Jitahidi umpate mwenye kushikamana na dini, basi furaha zote ni zako.

Uzuri, na utajiri si sifa pekee za kutosha kuchagua mke, sambamba na sifa hizo, pia mke ni lazima awe na sifa zingine, kwa mfano kumpata aliye na dini, na awe ametoka kwenye nyumba yenye mema. Kwa sababu watoto wake atakaow azaa mke huyo watarithi tabia, adabu na mwenendo wake. Mwenyezi Mungu amekataza kuoa mwanamke mzuri tu asiye na tabia nzuri na nidhamu. Mtume(s.a.w.w) amekataza:Jihadharini na wanawake wazuri wenye sifa mbaya.

Mtume(s.a.w.w) ameweka mwongozo kwa mwanamke ambaye yu tayari kuolewa:atafute mume mcha Mungu, mwenye tabia za kidini, atakayeangalia jamii yake kwa ukamilifu, kutekeleza haki za mke, na kusimamia malezi ya watoto.

Mtume(s.a.w.w) amesema:Atakapowajia mtu mtakayeridhishwa na jinsi alivyoshika dini, na tabia yake, basi muozeni, ama msipofanya hivyo, mtaleta fitina na ufisadi mkubwa duniani.

Mtume(s.a.w.w) ameonya pia kuhusu kuoana na ndugu wa karibu, ili watoto wasizaliwe wadhaifu, akasema:Oeni walio nje ya jamii yenu, msiwadhoofishe watoto wenu.

Qur ani imetaja ya kwamba, mwanadamu ameumbwa kutokana na tone la manii lililochanganyika:

إِنَّا خَلَقْنَا الْإِنسَانَ مِن نُّطْفَةٍ أَمْشَاجٍ نَّبْتَلِيهِ فَجَعَلْنَاهُ سَمِيعًا بَصِيرًا ﴿٢﴾

Hakika tumemuumba mwanadamu kutokana na tone la manii lililochanganyika...(76:2).

Hii inaonyesha kwamba, mtoto azali waye na wazazi ambao si ndugu wa karibu atakuwa na uwerevu, utambuzi na mwenye nguvu za kimwili kuliko mtoto aliyezaliwa na wazazi wenye uhusiano wa karibu. Hii inaweza kuonekana kwamba Uislamu umezitangulia (kwa uvumbuzi) kanuni za kisayansi na elimu ya tabia zinazorithishwa (Heredity) kwa kuonyesha umuhimu ulioko katika sehemu ya urithi wa tabia, na namna gani uteuzi mzuri wa watu wawili wanaooana utakavyopelekea kupata watoto ambao ni tuzo la Mwenyezi Mungu na furaha ya maisha.

Kwa kuwa mtoto atachukua mwenendo wa wajomba na shangazi zake, asili ya undani ya baba yake na mama yake, na akajifunza kupitia kwa urathi ambao umepitia kutokana kwa muungano wa baba yake na mama yake, na ndipo Uislamu ukazitengeneza asili hizi kwa njia hiyo ili kumhifadhi mtoto awe ni kiumbe mwenye heshima na nidhamu, na hivyo kuepukana na upungufu wowote. Mara tu mtu anapoanza kufikiria kuoa na kutunza familia, Uislamu unamuongoza kupitia katika njia hizo.

3. FAMILIA KATIKA UISLAMU

Familia katika Uislamu, ina utaratibu mzuri na wa hali ya juu sana, na ni utaratibu unaoheshimiwa sana hata ina mahali panapostahiwa. Ni kwa sababu hii na ndio maana Uislamu huipa nguvu (familia) kuanzia mwanzo wa nguvu yake. Ndoa ni sura mpya katika njia ya kuunda jamii, na uangalifu wa Uislamu katika nguzo hiyo muhimu, hatimaye unaongoza kuelekea katika maisha ya amani na furaha.

4. PENDO LA WAZAZI

Mtoto ni matokeo ya kimaumbile ya uhusiano imara wa wazazi, ubaba na umama ni matamko mawili ambayo Mwenyezi Mungu ameyazatiti kwa ihsani na mapenzi Yake, akayatajirisha na kuyapitia kwa maana ya kuungana watu wawili na kuendelea kuwa pamoja.

Uhusiano wa karibu zaidi baina ya wazazi na watoto wao, ni miongoni mwa uhusiano ulio imara na wenye daraja ya juu zaidi kuliko uhusiano wowote ule wa kibinaadamu. Uhusiano huo umehifadhiwa na Mwenyezi Mungu, naye amehakikisha kuwa unaendelea na kustawi; kwa sababu kufanya hivyo ni kuendelea kwa jamii ya binaadamu na uhai. Upendo wa wazazi kwa watoto wao hauna nafasi yoyote ya kutia shaka, kwani ni alama ya Mwenyezi Mungu na ni neema Yake kubwa kwa walimwengu. Mwenyezi Mungu amesema:

وَمِنْ آيَاتِهِ أَنْ خَلَقَ لَكُم مِّنْ أَنفُسِكُمْ أَزْوَاجًا لِّتَسْكُنُوا إِلَيْهَا وَجَعَلَ بَيْنَكُم مَّوَدَّةً وَرَحْمَةً ﴿٢١﴾

Na katika alama zake, ni huku kuwaumbia wake zenu, kutoka miongoni mwenu ili mpate utulivu kwao, na akajaalia mapenzi na huruma baina yenu (30:21).

Baadhi ya wafasiri wameeleza pen zi na huruma hapa, kwa maana ya mtoto ambaye ameupa nguvu uhusiano baina ya wazazi na ameupa amani na usalama.

Familia ndicho kitu cha kwanza ambacho Uislamu unakichukulia kuwa ni cha kwanza katika jamii ya watu. Familia huunda nyoyoni mwao penzi lisilo na kikomo kwa watoto wao, penzi hili ni nuru waliyopewa na Mwenyezi Mungu. Mtume(s.a.w.w) aliwaambia maswahaba zake na huku akiwaonyesha mwanamke akasema:Je Mnaweza kufikiria kwamba siku moja mwanamke huyu anaweza kumtupa mwanawe motoni? Wao wakasema: La, akasema: Basi Mwenyezi Mungu ni mwenye huruma zaidi kwa waja wake kuliko mama huyu alivyo na huruma kwa mtoto wake.

Basi haya ni maumbile, na ni aina ya pendo la kiasili ambalo hapana yeyote awezaye kulizuia au kushindana nalo, na kwa sababu hii ndipo Mwenyezi Mungu akawausia wazazi kuwaangalia watoto wao, Amesema:

وَوَصَّيْنَا الْإِنسَانَ بِوَالِدَيْهِ حَمَلَتْهُ أُمُّهُ وَهْنًا عَلَىٰ وَهْنٍ وَفِصَالُهُ فِي عَامَيْنِ أَنِ اشْكُرْ لِي وَلِوَالِدَيْكَ إِلَيَّ الْمَصِيرُ ﴿١٤﴾

Na tumemuusia mwanaadamu (kuwafanyia wema) wazazi wake, mama ameichukua mimba yake kwa udhaifu juu ya udhaifu, na kumnyonyesha na kumwachisha kunyonya katika miaka miwili, nishukuru Mi mi na wazazi wako na kwangu ndio marejeo (31:14).

Amesema tena:

وَوَصَّيْنَا الْإِنسَانَ بِوَالِدَيْهِ إِحْسَانًا حَمَلَتْهُ أُمُّهُ كُرْهًا وَوَضَعَتْهُ كُرْهًا وَحَمْلُهُ وَفِصَالُهُ ثَلَاثُونَ شَهْرًا حَتَّىٰ إِذَا بَلَغَ أَشُدَّهُ وَبَلَغَ أَرْبَعِينَ سَنَةً قَالَ رَبِّ أَوْزِعْنِي أَنْ أَشْكُرَ نِعْمَتَكَ الَّتِي أَنْعَمْتَ عَلَيَّ وَعَلَىٰ وَالِدَيَّ وَأَنْ أَعْمَلَ صَالِحًا تَرْضَاهُ وَأَصْلِحْ لِي فِي ذُرِّيَّتِي إِنِّي تُبْتُ إِلَيْكَ وَإِنِّي مِنَ الْمُسْلِمِينَ ﴿١٥﴾

Na tumemuuusia mwanaadamu kuwatendea wema wazazi wake. Mama yake ameichukua mimba yake kwa taabu na akamzaa kwa taabu. Na kubeba mimba yake (mpaka) kumwachisha kunyonya ni miezi thelathini mpaka anapofikia kubaleghe kwake, na akafikia miaka arubaini. Akasema: Ewe Mola wangu niwezeshe nizishukuru neema zako ambazo umenineemesha mimi na wazazi wangu. Na uniwezeshe nifanye amali njema uzipendazo, na unitengenezee watoto wangu. Kwa hakika natu bu kwako, kwa hakika mimi ni miongoni mwa waislamu (46:15).

Mwenyezi Mungu amefanya kuwapenda watoto na kuwahurumia ni sehemu ya maumbile ya kiasili ya kibinaadamu yasioepukika. Pia ameziingiza hisia hizi thabiti ndani ya nyoyo za wazazi. Ni kwa ajili h ii basi ndipo maelezo haya yote pamoja na wasia yameelekezwa moja kwa moja kwa watoto, kwa ajili ya kuwatendea wema na kuwapa heshima wazazi wao. Maelekezo haya amepewa mtoto ili kuzivutia hisia zake.

Ni maelekezo ya hali ya juu ambayo yanategemeza uhusiano wa karibu na hisia ya kibinaadamu ambazo ndio sababu kubwa ya kuwepo kwetu duniani.

5. USAWA BAINA YA WATOTO KATIKA UISLAMU NA MAONI YAKE JUU YA WATOTO WA KIKE

Kadri Uislamu unavyochukulia watoto kuwa ni kiburudisho cha macho yetu, ni lazima hii idhihiri kwa vitendo na kwa njia zake. Usawa baina ya watoto hauna budi kutekelezwa hata katika kuwabusu. Uislamu unataka usawa ufanywe kulingana na maagizo yake matukufu.

Siku moja Mtume(s.a.w.w) alimwona baba ambaye alikuwa na watoto waw- ili, akambusu mmoja na kumwacha mwingine, kisha Mtume mtukufu akamuuliza: Je huwezi kuwafanyia usawa? Tukiangalia mvuto wa kumpendelea mtoto mmoja zaidi ya mwingine au jinsia moja (wa kike au wa kiume) zaidi ya nyingine, hii ni kinyume kabisa na maadili ya kiislamu, mila n a fikra za usawa ambazo Uislamu umejengewa. Uislamu hautofautishi baina ya mwanamume na mwanamke, wala hautofautishi baina ya mvulana na msichana. Wote sawa, hapana yeyote ampitaye mwenzake ila kutokana na baadhi ya sifa alizonazo kitabia alizojipatia yeye mwenyewe, Mwenyezi Mungu amesema:

فَاسْتَجَابَ لَهُمْ رَبُّهُمْ أَنِّي لَا أُضِيعُ عَمَلَ عَامِلٍ مِّنكُم مِّن ذَكَرٍ أَوْ أُنثَىٰ بَعْضُكُم مِّن بَعْضٍ ﴿١٩٥﴾

Mola akawakubalia (maombi yao), ya kwamba mimi sipotezi amali ya mwenye kutenda, awe ni mwanamume au mwanamke, baadhi yenu kwa baadhi nyingine (3:195).

Kwenda kinyume na misingi hii kunafuatia kwenda kinyume na fikra za usawa, maarifa, na haki. Kwa ajili hii, Uislamu unawaamuru Waislamu kuwafanyia usawa watoto wao ili kwamba kusiwe na yeyote yule atakayekuwa na kinyongo au kusononeka. Kwa njia kama hiyo, Uislamu unazuia kuzagaa kwa chuki badala ya mapenzi, na kusema maudhi badala ya amani. Mambo haya iwapo yataendelea, hatimaye yataleta matatizo ya kinafsi, majonzi, na utengano, na haya yote huvunja hisia za moyo. Mtume(s.a.w.w) mara kwa mara alikataza kuwapendelea watoto wa kiume zaidi ya wa kike pasi na sababu yoyote, kwa maana hiyo, ndiyo akaipa daraja la juu heshima ya watoto wa kike na akaipa nguvu thamani na staha yao.

Amesema Mtume(s.a.w.w) : Bora ya watoto wenu ni mabinti. Mtume(s.a.w.w) alipopew a habari ya kuzaliwa bintiye Fatima(a.s) , nyuso za maswahaba zilionekana kuparama, Mtume(s.a.w.w) akawaambia: Mna jambo gani linalowahuzunisha? (kumzaa Fatima) ni kama kupata ua la mrehani niunusao, na riziki yake iko kwa Mwenyezi Mungu. Hapa Mtume(s.a.w.w) kwa ubaba wake mtukufu alijaribu kubadilisha mawazo ya watu ya kuwapendelea watoto wa kiume zaidi ya watoto wa kike, tena hata aliwatanguliza watoto wa kike zaidi kwa kusema: Mwenye kwenda sokoni, na kununua zawadi na kuwapelekea jamii yake, (famili a yake) ni kama mtu aliyewapelekea sadaka wahitaji, basi aanze kuwapatia watoto wa kike kabla ya kiume.

Mtume(s.a.w.w) amejaribu kwa kadri awezavyo kuvutia penzi la watoto wa kike kama vile lilivyo penzi la asili kwa watoto wa kiume. Amesema:Mwenye kuwalisha (kuwalea) watoto watatu wa kike ataingia Peponi. Akaulizwa: Je wakiwa ni wawili?, akajibu:Hata kama wawili, Akaulizwa: Je mmoja, akajibu:Hata kama ni moja.

2

MALEZI YA WATOTO KATIKA UISLAMU

SEHEMU YA PILI

MAISHA NA MAKAZI YA MTOTO

Mtume(s.a.w.w) amesema: Yatosha kwa mtu kupata dhambi kwa kutowaangalia wanaomtegemea. Kuna maagizo kadhaa na misingi ya kanuni iongozayo, ambapo Uislamu unaamuru kwa jinsi gani maisha na maendeleo ya mtoto yalivyo lazima, na kwamba uzembe wowote ama kufanya ajizi katika kutimiza misingi hii ya kanuni ni kosa kubwa. Misingi hii imetolewa mfano kama ifuatavyo:

Amesema Mwenyezi Mungu: Wala msijiue. Amesema tena:

وَلَا تَقْتُلُوا النَّفْسَ الَّتِي حَرَّمَ اللَّـهُ إِلَّا بِالْحَقِّ ﴿١٥١﴾

..wala msiue nafsi ambayo Mwenyezi Mungu ameharamisha kuuawa ila kwa njia ya haki (6:151).

Amesema tena:

مَن قَتَلَ نَفْسًا بِغَيْرِ نَفْسٍ أَوْ فَسَادٍ فِي الْأَرْضِ فَكَأَنَّمَا قَتَلَ النَّاسَ جَمِيعًا وَمَنْ أَحْيَاهَا فَكَأَنَّمَا أَحْيَا النَّاسَ جَمِيعًا ﴿٣٢﴾

Mtu atakayemuua mtu bila ya yeye kuua, au bila ya kufanya ufisadi nchini, basi ni kama amewaua watu wote, na atakayeokoa maisha ya mtu, basi ni kama ameokoa maisha ya watu wote (5:32).

Amesema tena:

وَلَا تَقْتُلُوا أَوْلَادَكُم ﴿١٥١﴾

Wala ms iwaue watoto wenu (6:151). Amesema tena:

يُرِيدُ اللَّـهُ أَن يُخَفِّفَ عَنكُمْ وَخُلِقَ الْإِنسَانُ ضَعِيفًا ﴿٢٨﴾

Mwenyezi Mungu anataka kukurahisishieni (mambo mazito) kwani mwanaadamu ameumbwa dhaifu. (4:28).

Amesema tena:

وَلْيَخْشَ الَّذِينَ لَوْ تَرَكُوا مِنْ خَلْفِهِمْ ذُرِّيَّةً ضِعَافًا خَافُوا عَلَيْهِمْ ﴿٩﴾

Na waogope (mawasii kuwadhulumu yatima, na wakumbuke) kama wao wangeacha nyuma yao watoto dhaifu wangekuwa na khofu juu yao. (4:9).

Amesema tena:

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا قُوا أَنفُسَكُمْ وَأَهْلِيكُمْ نَارًا ﴿٦﴾

Enyi mlioamini! Jiokoeni nafsi zenu na watu wenu kutokana na moto. (66:6)

Amesema tena Mwenyezi Mungu:

وَلَا تُلْقُوا بِأَيْدِيكُمْ إِلَى التَّهْلُكَةِ ﴿١٩٥﴾

Wala msijitie wenyewe katika maangamivu. (2:195).

Amesema Mtume(s.a.w.w) :Yatosha kwa mtu kupata dhambi kwa kumtupa yule anayemtegemea.

1. KUISHI KWA MTOTO

Uislamu unamchukulia mtu kuwa ni khalifa wa Mwenyezi Mungu duniani, imetajwa katika Qurani: Hakika nitaweka katika dunia hii khalifa (2:30).

Kwa hivyo, jambo lolote litakalomtia khalifa huyu kwenye aibu, fedheha, ama kudhoofisha uwezo wake, limekatazwa na sheria ya Kiislamu.

Na hii ni kwa sababu ya kuhifadhi heshima na daraja ya mwanaadamu aliyopati- wa akiwa kama khalifa wake duniani. Mwenyezi Mungu amempa uwezo binaadamu kuwa na fahamu za kujua mambo bila ya kufundishwa, nguvu za ulinzi za kuweza kujihami, na kumwezesha kupata kudumu kwa ulimwengu. Pia Mwenyezi Mungu amempa mwanaadamu undani wa maarifa, na amemtukuza zaidi ya viumbe vyote vilivyosalia. Miongoni mwa uwezo aliopewa mwanaadamu ili kukabiliana na vitisho ni uwezo wa kujihami.

Uangalifu wa Uislamu kuhusiana na maisha ya mtoto na ulinzi wake, tayari wenyewe una mamlaka kwenye jamii ya kiislamu kimwili au kiroho, kwa sababu uangalifu huu unazalisha miili imara yenye siha. Kuwa na miili yenye afya katika Uislamu hakuleti natija ya nguvu ya kiakili tu, bali pia uhakika, mafanikio na matumaini katika kushughulika na maisha na watu. Ni kwa sababu hizi ndipo Uislamu umekusanya taratibu zifaazo za kujikinga, ili kuyahifadhi maisha ya waislamu na kuwaongoza katika njia yenye utaratibu na iliyopangwa katika maisha yao yote. Afya ndiyo neema bora kuliko zote alizotunikiwa mwanaadamu baada ya kuwa muislamu, kwani bila ya kuwa na afya huwezi kufanya kazi na kuweza kumtii Mungu sawasawa, kwa hivyo, hakuna chochote kinachoweza kulinganishwa nayo.

Imetajwa na Tirmidhy, kutokana na Abu Huraira ya kwamba Mtume(s.a.w.w) amesema: Kitu cha kwanza atakachoulizwa mwanaadamu Siku ya Kiyama, kutokana na neema alizopewa ni: Je mwili wako, sikuupa afya? (uliifanyia nini?)

2. JUKUMU LA WAZAZI HUKO AKHERA, NA MATUNZO YA WATOTO

Inasadikiwa ya kwamba, kulingana na maumbile na hisia za binaadamu, anaweza kuepuka hali zinazotishia (maisha yake). Zaidi ya hayo, Mwenyezi Mungu amemuumbia mwanaadamu nguvu ya kiasili inayomlinda kutokana na hatari hizo. Licha ya hivyo, Uislamu umeipa uwezo nguvu hiyo, na umemkumbusha mwanaadamu aitumie kwa kujihami na kwa kuongozea mikakati ya ulinzi kwa ajili ya maisha yake. Kwa hivyo inaonyesha wazi namna gani Uislamu ulivyoupa daraja ulinzi na kuuimarisha. Ulinzi kwa maana hiyo (ilivyotajwa hapa) ungeweza kuwa na maana ya ulinzi wa mwanaadamu hapo Akhera, ambao utamwokoa kutokana na moto na vitisho vya Siku ya Kiyama. Au ungeweza kuwa ni kujilinda kwa mtu kutokana na moto ambako kunamaanisha wakati huo huo, kuilinda familia yake.

Imetajwa katika Qur ani:

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا قُوا أَنفُسَكُمْ وَأَهْلِيكُمْ نَارًا وَقُودُهَا النَّاسُ وَالْحِجَارَةُ ﴿٦﴾

Enyi mlioamini! Jiokoeni nafsi zenu na watu (jamii) yenu kutokana na Moto ambao kuni zake ni watu na mawe (66:6).

Aya hizo zilizotangulia zinawataka wacha Mungu waumini kujilinda na kujihami wao na jamii zao pia kutokana na Moto ambao kuni zake zitakuwa ni watu waovu. Kujilinda maana yake (hapa) inarejea kwenye kutenda amali njema, na kuwa na mwenendo mzuri, kumtii Mwenyezi Mungu na kujizuia na makatazo yake. Miongoni mwa matendo ya kujilinda kwa Akhera, ni kujizuia na maamrisho yote ya Mwenyezi Mungu, kuhusiana na chakula, kinywaji, mavazi, n.k.

Imetajwa katika Qur ani:

يَا أَيُّهَا الرُّسُلُ كُلُوا مِنَ الطَّيِّبَاتِ وَاعْمَلُوا صَالِحًا إِنِّي بِمَا تَعْمَلُونَ عَلِيمٌ ﴿٥١﴾

Enyi Mitume! Kuleni vyakula vilivyo vizuri (halali) na tendeni mambo mema, hakika Mimi najua yote myafanyayo. (23:51).

3. JUKUMU LA WAZAZI MAISHANI NA MATUNZO YA MTOTO

Matunzo ya mtoto wakati wa maisha yake yanahusiana na kumkinga kutokana na magonjwa na maradhi yaambukizayo na yote yale yawezayo kumpata mtu kutokana na uzembe, na kutojihusisha. Imesema Qur ani:

Wala msijitie wenyewe katika maangamivu (2:1 95).

Katika Aya iliyotangulia hapo juu, Mwenyezi Mungu amemkataza mwanaadamu kuchangia maangamivu yake mwenyewe kupitia kwenye vitendo ambavyo angevitenda kulingana na mwenyewe. Ijapokuwa mtu kujidhuru au kujiangamiza kunaonekana kwamba kunapingana na fikra zilizo timamu (yaani haiwezekani), lakini yaelekea kuwa kunaweza kutokea kutokana na uzembe ama kutojihusisha na kuchukua kinga zifaazo ili kuyachunga maisha yake mwenyewe.

Kujiangamiza hapa, haina maana tu ya maangamivu yanayosababishwa na kiu, nja a, au mtu mwenyewe kujitoa mhanga kwa njia moja au nyingine kutokana na madhambi ayatendayo. Kuangamia kwa maana hiyo, kunamaanisha kwamba kufanya ajizi kidogo tu, au kuzembea katika kujikinga, ndiko kujiangamiza. Kwa hivyo hii ni pamoja na mtu kujihatar isha na magonjwa, maradhi yaambukizayo, ukosefu wa chanjo kutokana na maradhi yauwayo, na ukosefu wa uangalifu wakati wa shida na hatari. Vitendo hivyo vyote vilivyotangulia kutajwa vinachukuliwa kuwa ni kumchangia mtu katika maangamivu yake mwenyewe.

Kwa sababu hiyo ndipo Uislamu ukaamuru kuchukua kinga zifaazo, na kutafuta matibabu kwa ajili ya magonjwa yote. Mtume(s.a.w.w) amesema: Mwenyezi Mungu hakuweka maradhi ila ameleta na dawa ya kuyatibu.

4. JUKUMU LA WAZAZI NA MAKUZI YA MTOTO

Sheria ya Kiislamu imewaamuru wazazi kuwa ni dhamana kwa maisha ya mtoto na makuzi yake. Kwa msingi wa kwamba, mtoto huchukuliwa kuwa ni dhamana waliyopewa, ambayo inapaswa kutunzwa nao kwani watakujaeleza mbele ya Mwenyezi Mungu (jinsi walivyoitunza amana waliyopewa). Mtoto mwanzoni mwa maisha yake huwa hajui hatari hasa ambazo zingehatarisha maisha yake. Kwa kuongezea ni kwamba yeye hawezi kujilisha na kuchunga maisha yake, kwa hivyo basi, ndipo Mwenyezi Mungu akawafanya wazazi kuwa ni dhamana kwa ajili ya kuwalinda watoto wao kutokana na magonjwa mbalimbali na hatari ambazo zingetishia maisha na makuzi yao.

Imetajwa katika Hadith:Kila mmoja wenu ni mchungaji na kila mmoja ataulizwa juu ya kile akichungacho.

Baba ni mlezi wa jamii yake. Mke ni mchungaji wa mali ya mu mewe na watoto wake, na ndiye atakayeulizwa kuhusu akitunzacho. Mtumishi ni mtunzaji wa mali ya tajiri yake na ndiye atakayeulizwa kuhusu mali aitunzayo. Ndiyo, kila mmoja wenu ni mchungaji na ndiye atakayeulizwa juu ya anachokiangalia. Mbali na kuwa ni d hamana, ni wajibu wao pia kuwalisha watoto wao na kuwatosheleza mahitaji yao, hii inaweza kuwa kwa kuwachagulia kwa njia nzuri chakula chao, na kuwalinda kutokana na maradhi yote yatakayowadhuru.

Miongoni mwa hatari zinazoweza kutishia maisha ya mtoto katika miaka yake ya mwanzoni ni uwezekano wa kupatwa na mojawapo ya maradhi yauwayo watoto kama: Ugonjwa wa kupooza (Polio), Surua (Ukambi), dondakoo (DPT au Diphtheria) n.k. Au upungufu wa maji mwilini uletwao na magonjwa ya kuharisha n.k. Magonjwa hayo yote yanaweza kumshambulia mtoto, kumlemaza na kumhuzunisha maisha yake na ya wazazi wake. Uislamu unatuonya vikali sana tusipuuze matunzo na matibabu ya watoto wetu kutokana na maradhi yauwayo watoto au mengineo. Kwa ajili hiyo, Uislamu unaamrisha waumini wake kuwa wenye nguvu na afya. Mtume(s.a.w.w) amesema: Muislamu mwenye nguvu ni bora na ndiye apendezaye zaidi kwa Mwenyezi Mungu kuliko Muislamu mnyonge.

Kwa kuwa upendo wa wazazi kwa watoto ni sehemu ya maumbile yao (wazazi) ya kiasili, ndipo ikawa hapana haja ya kuagizwa juu ya jambo hilo, kwa hivyo Uislamu umetilia mkazo zaidi umuhimu wa matunzo ya watoto na ukaonya vikali wazazi wasizembee katika jambo hilo, ili familia na jamii ziweze kuishi kwa raha na furaha. Na hii hatimaye huleta muundo wa kizazi ambacho kitategemewa kuweza kubeba mzigo wake barabara na katika hali ya kujitegemea. Imetajwa katika Qur ani:

Wala msijitie wenyewe katika maangamivu. (2:145).

Na je ni maangamivu gani maovu zaidi ambayo mtu anaweza akajifanyia mwenyewe kuliko kuingiza kiwiliwili chake na damu (watoto) wake kwenye hatari ya kifo na adhabu? Imetajwa tena katika Qur ani:

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا قُوا أَنفُسَكُمْ وَأَهْلِيكُمْ نَارًا وَقُودُهَا النَّاسُ وَالْحِجَارَةُ ﴿٦﴾

Enyi mlioamini! Jiokoeni nafsi zenu na watu (jamii) wenu kut okana na moto, ambao kuni zake ni watu na mawe (66:6).

Kujilinda na maangamivu (ya ugonjwa n.k.) kuna maana sawa na kuna daraja moja na kuilinda jamii kutokana na maangamivu ya motoni. Ikiwa kujilinda kunahitajika kwa ajili ya maisha ya akhera, basi kujilinda huko kunahitajika zaidi wakati wa maisha ya duniani kwani kile ukipendacho katika maisha yako duniani ndicho utakachokivuna akhera. Kujilinda kwa maana hiyo, hakumaanishi kujizuia kutokana na kutenda maovu, madhambi na mambo ya fedheha tu, bali ina maana ya ndani zaidi kuhusiana na usawa baina ya mahitaji ya nafsi, kiwiliwili, roho, na kujilinda na maneno ya Mtume(s.a.w.w) aliposema:Yatosha kwa mtu kupata dhambi kwa kutomjali yule anaemtegemea.

Pia:Nyote ni wachungaji na kila mmoja wenu ataulizwa kutokana na kile anachokichunga.

Tukizingatia, inatudhihirikia wazi kwamba kuwakinga watu wetu kutokana na maradhi ni amri ya kidini na ni wajibu wa jamii na pia ni wajibu wa taifa zima. Mtume(s.a.w.w) amesema: Mwenye kuitunza jamii na hakuipa nasaha (maonyo), basi mtu huyo atanyimwa pepo. Kuwapatia watoto huduma za chanjo dhidi ya maradhi yauwayo na yalemazayo, humwokoa mtunzaji wa jamii kutokana na kosa la kupuuza jamii yake. Na mwishowe ataokoka Siku ya Kiyama kutokana na vitisho ambavyo vingempat a wakati Mwenyezi Mungu atapomuuliza kuhusu hali ya wafuasi wake (wenye kumtegemea) na sababu ya kuwa mzembe katika jambo hilo. Kwa hivyo basi, iwapo wazazi hawatachukua hatua zifaazo ili kulinda maisha ya watoto wao kuwakinga kutokana na maradhi, kuna uwezekano mkubwa wa kunyimwa pepo akhera.

Chanjo na huduma za O.R.S. (Maji ya dawa ya kurudisha maji mwilini kutokana na maradhi ya kuharisha) hutolewa bure na serikali. Wazazi wanachotakiwa kufanya ni kuzitumia huduma hizi, ili kuwakinga watoto wao kutokana na madhara na hatari ziletwazo na magonjwa. Hata kama watalazimika kulipa ili watoto wao wachanjwe, Uislamu unawapa moyo kufanya hivyo, kwani Mtume(s.a.w.w) amesema: Bora ya matumizi, ni kutumia (japo) senti kwa ajili ya familia yako.

5. KUWALINDA WATOTO NI HURUMA, NA HURUMA NI KINGA

Mtume(s.a.w.w) ametueleza mpango maalum wa kutuwezesha tuwe na huruma na upendo kwa watoto wetu. Ametaja Bukhari katika kitabu chake cha Al-Adab, katika mlango maalum kwamba wahurumieni watoto na pale Mtume(s.a.w.w) ali posema: Si katika sisi yule mtu asiyemhurumia mdogo, na asiyejua haki ya mkubwa (asiye mheshimu). Akasema tena: Rehemuni (sikitikieni) wenzenu, nanyi mtarehemewa. Ni dhahiri kutokana na Hadith zilizotajwa hapo juu kwamba Mtume(s.a.w.w) ameeleza jinsi wa le watu ambao hawana huruma kwa wadogo zao wanavyochukuliwa kuwa si waislamu wa kweli na hawako pamoja na Mtume(s.a.w.w) na ujumbe wake Mtukufu. Inasemekana kuwa hapana yeyote awezaye kuwa na huruma kwa mtoto kama ilivyo wazazi wake (mtoto).

Ikiwa Mtume(s.a.w.w) amewataka watu wote kwa pamoja kuwa na huruma kwa watoto, basi ni jambo lililo muhimu zaidi kwanza kwa wazazi kuwaonea huruma watoto wao kuliko watu wengine. Sehemu ya huruma yao kwa watoto wao ni kuwapeleka wakapatiwe chanjo na kinga kutokana na magonjwa na maradhi yote yenye kuenea yawezayo kuwashambulia.

Wazazi watakapokuwa na huruma kwa watoto wao, basi huruma hiyo hiyo huwarudia (wazazi) wakati wa uzeeni kwa sababu upendo ni kitu cha kulipana. Mtume(s.a.w.w) ameeleza kwa ubainifu kuhusiana na suala hili la huruma na kinga, na akaeleza jinsi huruma ilivyokuwa sehemu ya kinga na kinga ni sehemu ya huruma. Amesema: Harehemiwi (haonewi huruma) yule mtu asiyemrehemu mwingine, na hasemehewi yule asiyemsamehe mwingine, wala hapewi toba (na Mwenyez i Mungu) mtu asiyetubu, na wala halindwi yule asiyejilinda.

Katika Hadith hii Mtume(s.a.w.w) ametilia mkazo ya kuwa huruma ndilo jambo la msingi na akaeleza ya kwamba, yeyote asiyejilinda, basi Mwenyezi Mungu hatamlinda kutokana na maradhi. Ijapokuwa jambo hilo limeelezwa, lakini Mtume(s.a.w.w) amelielezea kimantiki kwa njia ya maombi. Amesisitiza Mtume(s.a.w.w) kwamba, yeyote asiyejilinda ama kulinda wengine kutokana na kitakachowadhuru au kuwaingiza hatarini au kwenye ugonjwa, basi Mwenyezi Mungu naye hawezi kumlinda kutokana na mambo hayo. Kwa hivyo basi Mtume(s.a.w.w) katika maelezo yake hapa anakusudia kuifanya huruma isambae miongoni mwa watu, na anaazimia kuwapa moyo watu kujaribu kupata huduma za kinga zifaazo dhidi ya hii ikiwa ni kukamilisha sehemu ya huruma.

6. UISLAMU NA UZAZI WA MPANGO

Qur ani imefafanua waziwazi kuhusu muda maalum ufaao kwa kutenganisha baina ya kuzaliwa mtoto mmoja hadi kupata mwingine. Imetajwa ndani ya Qurani kuwa kubeba mimba ya mtoto hadi kumwachisha kunyonya ni kipin di cha miezi thelathini; Amesema Mwenyezi Mungu:

Kubeba mimba ya mtoto hadi kumwachisha ni miezi thelathini (46:15) Pamoja na hayo, Uislamu unaunga mkono kunyonyesha kwa maziwa ya mama kunakodumu kwa miaka miwili kamili kwa wale wanaotaka kutimiza muda huo kamili. Kwa kufanya hivi, kunamwezesha mama (aliyezaa) kurekebisha afya yake, na kumrudisha nguvu zake za mwilini alizozipoteza katika kipindi cha uja uzito hadi kujifungua.

Muda huu maalum pia utamwezesha mtoto kupata muda wa kutosha wa kunyonya matiti ambapo utaalamu wa utabibu (wa kisasa) umekuja kuunga mkono baada ya kutofaulu kwa muda mrefu, kwa kutumia chupa ya kunyonyea.

Kwa hivyo hapa ni dhahiri namna gani Uislamu unavyopigania uzazi wa mpango ili kuwapatia afya bora mama na mtoto.

Imetajwa katika Qur ani:

وَوَصَّيْنَا الْإِنسَانَ بِوَالِدَيْهِ إِحْسَانًا حَمَلَتْهُ أُمُّهُ كُرْهًا وَوَضَعَتْهُ كُرْهًا وَحَمْلُهُ وَفِصَالُهُ ثَلَاثُونَ شَهْرًا ﴿١٥﴾

Na tumemwusia mwanaadamu kuwatendea wema wazazi wake, mama yake amechukua mimba yake kwa taabu, na akamzaa kwa taabu, kubeba mimba yake mpaka kumwachisha kunyonya ni (kipindi cha) miezi thelathini (46:15).

Imetajwa pia katika Qurani:

وَوَصَّيْنَا الْإِنسَانَ بِوَالِدَيْهِ حَمَلَتْهُ أُمُّهُ وَهْنًا عَلَىٰ وَهْنٍ وَفِصَالُهُ فِي عَامَيْنِ ﴿١٤﴾

Na tumemuusia mwanaadamu kuwafanyia mema wazazi wake, mama yake amebeba mimba yake kwa unyonge juu ya unyonge, na (kumnyonyesha na) kumwachisha kunyonya katika miaka miwili.

7. UISLAMU NA KARANTINI ZA AFYA

Uislamu unaonya sana tuwe macho kutokana na maradhi yaambukizayo na unatusihi tujikinge na maradhi hayo. Imepokewa Hadith ya kwamba Mtume(s.a.w.w) alibaiwa (kuungwa mkono wa uongozi) na mtu mwenye ugonjwa wa ukoma pasi na kupeana naye mkono[1] , ama kumruhusu kutangamana na watu. Imepokewa kutoka kwa Umar bin Shareed, kutoka kwa baba yake amesema:

Katika ujumbe wa Thaqif uliokuja kum bai (kumtambua kama kiongozi) kulikuwa na mtu mwenye ugonjwa wa ukoma, basi Mtume(s.a.w.w) alimrejesha (bila ya kumpa mkono) kwa kusema: Hakika tumekutambua. Na katika Sahih Bukhari, Mtume(s.a.w.w) amesema: Kaa mbali na mwenye ukoma kama unavyokaa mbali na simba. Mtume(s.a.w.w) ameeleza wazi wazi kwamba wakati yatapoingia maradhi ya tauni, watu ni lazima wawe macho sana, na wachukue hadhari zote za lazima ili kujikinga na kujiepusha na mtu aliyeambukizwa.

Imetajwa katika Hadith:Tauni (ugonjwa ueneao) ni alama ya adhabu ambayo Mwenyezi Mungu Mtukufu huwajaribu nayo watu miongoni mwa waja wake. Mtakaposikia kuwa umeingia nchini, basi msiingie nchini humo na iwapo utatokea nanyi mko ndani ya nchi hiyo basi msitoke.

Hapa Mtume(s.a.w.w) anaamuru Karantini na anatukataza kuingia katika nchi iliyokumbwa na ugonjwa wa tauni, ili tujilinde kutokana na kifo, vile vile tumeonywa tusitoke nje ya nchi ambayo tayari imekumbwa na ugonjwa huo, ili tusisambaze maradhi. Na hii pia ni aina nyingine ya kujilinda. Aina hizi mbili za maonyo (zilizotangulia hapo juu) zinachukuliwa kuwa ni aina za hasi (Negative) za kujikinga. Wakati ambapo kuchanja kwa ajili ya kinga za magonjwa na maradhi ya kuambukiza ni aina ya chanya (Positive). Kwa hivyo Uislamu unapigania sana aina hii ya chanjo kwani ndiyo iliyo bora na ni yenye gharama ndogo zaidi kuliko matibabu.

11

UCHUNGUZI JUU YA UWAHABI

KUTABARUKU KWA ATHARI ZA MAWALLI WA MWENYEZI MUNGU NA KUOMBA UPONYO

Mawahabi wanaitikadi kwamba kutaka baraka kwenye Athari za Mawalii wa Mwenyezi Mungu ni kumshirikisha Mwenyezi Mungu. Mawahabi pia wanamuona kuwa ni mshirkina mtu ambaye ataibusu mihrabu ya Mtume[s.a.w.w] na mimbari yake, japo hatafanya hivyo kwa nia ya ibada, isipokuwa ni kwa ajili tu ya mapenzi yake kwa Mtume[s.a.w.w] ndiyo maana katabaruku na kutaka uponyo kwenye Athari zake. Kukataza kutabaruku kwa athari za Mtume[s.a.w.w] na kulibusu kaburi lake na mimbari yake tukufu ni katika mambo ambayo Mawahabi wametilia nguvu kuyapinga dhidi ya Waislamu, na wamekuwa wakitumia makundi ya askari wa kigaidi waliopewa jina la waamrishaji mema na kukataza maovu, na wamewasambaza (askari) hao katika Msikiti wa Mtume[s.a.w.w] ili wazuwiye kulibusu kaburi lake tukufu na mimbari yake tukufu, pamoja na mihrab ya Msikiti wa Mtume[s.a.w.w] . Mawahabi hawa wanawahujumu mahujaji hapo Madina kwa kila aina ya mateso na kuwazuwiya kutabaruku na kulibusu kaburi la Mtume[s.a.w.w] na utawaona kila mara wameshika fimbo, na mikononi mwao mna nyaya ngumu tayari kumshambulia kila Hujaj atakayethubutu kutabaruku au kulibusu kaburi la Mtume[s.a.w.w] . Na kutokana na hali hii basi, mara kwa mara wamekuwa wakimwaga damu za mahujaji wasio na makosa na kuudhalilisha utu wao katika Msikiti wa Mtume[s.a.w.w] , kwa madai kwamba kutabaruku na kulibusu kaburi ni kumuabudu huyo aliyezikwa hapo.

Kwa hakika watu hawa hawaujuwi Uislamu, na wamekosea kufahamu maana ya Ibada na Maf-humu yake, na kwa sababu hii basi wamepotea njia na wanatangatanga ndani ya upotevu. Wamekuwa wanaona eti kila anapoheshimiwa mtu aliyekwisha kufa ni kumuabudu mtu huyo, pamoja na kufahamu kwamba kubusu kaburi tukufu na kutabaruku kwa athari za Utume siyo kwa ajili nyingine isiyokuwa ya Mwenyezi Mungu, kwa kuwa Waislami hawamtukuzi Mtume Mtukufu wala hawatabaruku kwa athari zake ila ni kwa kuwa yeye ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na ni Nabii wake mteule ambaye Mwenyezi Mungu amemtukuza kuliko Manabii wote na viumbe wote. Basi na ifahamike kwamba kila wanapoheshimiwa na kutukuzwa Mawalii wa Mwenyezi Mungu tendo hilo (kwa asili) ni kumtukuza Mwenyezi Mungu. Na hauthibitiki ukweli wa Tauhidi ila pale kila kitu kitakapotendwa kiwe ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na katika njia yake, na hapo ndipo itakapokuwa kila kitu kinaanzia kwa Mwenyezi Mungu na kila kitu kinaishia kwake.

Tutazungumzia maana ya Ibada katika sehemu ifuatayo kwa undani, ama sasa hivi utafiti wetu utahusu kutabaruku kwa athari za Mawalii, na utafiti huu tutalazimika kuulekeza kwenye kipimo cha Qur'an na Sunna ya Mtume[s.a.w.w] ili haki iweze kubainika.

MTAZAMO WA QUR'AN JUU YA KUTABARUKU

Katika Qur'an tunatosheka na aya moja tu, nayo ni ile inayomnukuu Nabii Yusuf[a.s] akisema: "Nendeni na kanzu yangu hii mukaiweke usoni kwa baba yangu (macho yake yatarudi) ataona". Qur'an, 12.93. Nabii Yusuf aliituma kanzu yake kwenda kwa baba yake na akawaambia ndugu zake "Nendeni na kanzu yangu hii na muiweke usoni kwa baba yangu ili macho yake yarudi apate kuona. Mwenyezi Mungu anasema: "Na alipokuja mtoaji habari njema, aliiweka kanzu ile usoni kwake na macho yalirudi akaona". Qur'an, 12:96. Aya hii iko wazi kutoa ruhusa ya kutabaruku kwa athari za Manabii na Mawalii kiasi kwamba hata Nabii anatabaruku kwa Nabii mwenziwe kama hivi Nabii Yaqub[a.s] anatabaruku kwa kanzu ya Nabii Yusuf[a.s] .

Na ni wazi kabisa kwamba kuponya kunatoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, na yeye ndiye mtendaji halisi, isipokuwa kutabaruku kwa kanzu ya Nabii kumekuwa ni wasila wa kuponya kama tunavyotumia dawa kuwa ni wasila wa kupona kwa idhini ya Mwenyezi Mungu Mtukufu. Ewe msomaji ingekuwaje kama kutabaruku kwa Nabii Yaqub kwa kanzu ya mwanawe Yusuf kungelitokea mbele ya watu wa Najdi na wafuasi wa Muhammad Ibn Abdul-Wahab, wangelihukumu namna gani jambo hili? Je, wangehukumu kuwa ni kafiri au mshirikina au mwenye dhambi? Wakati yeye ni Nabii na ni maasum? Kutabaruku kwa Waislamu kwenye kaburi la Mtume[s.a.w.w] na makaburi ya watu wa nyumba yake na pia athari zao hakuna tofauti na kutabaruku alikotabaruku Nabii Yaqub[a.s] kwa kanzu ya mwanawe Yusuf[a.s] .

KUTABARUKU NA SERA YA WAISLAMU

Mtazamo wa haraka katika sera ya Waislamu kuanzia kwa Masahaba mpaka leo, unatuonyesha wazi sunna inayofuatwa kuhusu kutabaruku kwa Mtume[s.a.w.w] yeye mwenyewe na athari zake tukufu katika kpindi chote cha historia ya Uislamu. Na katika maelezo yafuatayo tutaeleza mifano michache inayohusu kutabaruku:

1. Bibi Fatma Az-Zahra ambaye ndiye mwanamke bora ulimwenguni na ni binti ya Mtume[s.a.w.w] , alifika kwenye kaburi la baba yake na akachukua gao Ia udongo wa kaburi akawa anaunusa na kulia huku akisema: "Mtu aliyenusa udongo wa kaburi la Ahmad, halaumiwi iwapo hatanusa mafuta mazuri ya ghaliya." Yamenipata milele masaibu ambayo lau yangeliupata mchana ungegeuka na kuwa usiku. Wameitaja Qadhiya hii wanahistoria wengi miongoni mwao ni As-Samhudi.[151] Kwa hakika kitendo hiki cha Bibi Fatma Az-Zahra ambaye ni maasum kinajulisha kwamba kutabaruku kwenye kaburi la Mtume[s.a.w.w] ni jambo linalofaa na pia kutabaruku kwa udongo wa kaburi lake.

2. Bilal ambaye alikuwa ni muadhini wa Mtume[s.a.w.w] alipata kuishi Shamu katika kipindi cha utawala wa Omar Ibn Khattab. Siku moja alimuona Mtume[s.a.w.w] katika ndoto anamwambia:

"Ewe Bilal mbona umenitupa kiasi hiki, je haujakufikia wakati wa kunizuru ewe Bilal?" Basi Bilal alizindukana usingizini akiwa na huzuni na khofu nyingi na alipanda kipando chake kuelekea Madina na akafika kwenye kaburi la Mtume[s.a.w.w] akawa analia pale kaburini huku anausugua uso wake kwenye kaburi, mara Hasan[a.s] na Husein[a.s] wakafika, Bilal akawakumbatia na kuwabusu....[152]

3. Ibn Hajar anasema: "Kila mtoto aliyezaliwa katika zama za uhai wa Mtume[s.a.w.w] huhukumiwa kwamba alimuona Mtume[s.a.w.w] , na hii ni kwa sababu Ansar wote walikuwa wakiwaleta watoto wao kwa Mtume[s.a.w.w] kwa ajili ya Tahnik [153] na kupata baraka kiasi kwamba imesemwa kuwa: Wakati Makka ilipotekwa na (Waislamu), watu wa Makka wakawa wanakuja kwa Mtume[s.a.w.w] wakiwa na watoto wao ili awaguse vichwa vyao na awaombee baraka".[154] Na kuhusu jambo la kutabaruku, mwandishi wa kitabu kiitwacho, "Tabar-rukus Sahabah" amesema: "Hapana shaka kwamba athari za Mjumbe wa Mwenyezi Mungu (ambaye ni) mbora kuliko viumbe wote na mbora kuliko mitume wote, kuwepo kwake ni jambo lenye kuthibiti na ni mashuhuri mno. Basi kwa hiyo athari hizo ndiyo bora kutabaruku kwazo, na idadi kubwa ya Masahaba wameziona na wakaafikiana kutabaruku kwazo na kuzipa umuhimu wa kuzikusanya nao Masahaba ndiyo watu waongofu na ni kiigizo kizuri, kwani walitabaruku kwa nywele zake na maji aliyotawadhia na jasho lake na nguo zake na pia kuugusa mwili wake na mengineyo yanayofahamika katika athari zake tukufu ambazo zimesihi khabari zake toka kwa watu wema.[155] Yanatosheleza maelezo aliyoyataja Muslim katika Sahih yake kuhusu kutabaruku aliposema: "Hakika Mtume[s.a.w.w] alikuwa akiletewa watoto naye huwafanyia tahnik.[156]

4. Masahaba walikuwa wakitabaruku kwa maji ya udhu aliyotawadha na aliyokoga Mtume[s.a.w.w] : Bukhari amopokea hadithi isemayo: "Mtume[s.a.w.w] alitutokea katika kipindi cha jua kali, akaletewa maji ya kutawadha na akatawadha, basi watu wakawa wanachukua maji ya udhu atawadhayo Mtume[s.a.w.w] wanajipangusia". [157] Kuhusu jambo hilo kuna riwaya nyingi zilizojaa katika vitabu vya hadithi.

5. Masahaba walikuwa wakitabaruku kwa nywele za Mtume[s.a.w.w] kama alivyopokea Anas kwamba: "Mtume[s.a.w.w] aliponyoa kichwa chake, Abu Tal-ha alikuwa ni mtu wa kwanza kuchukuwa nywele za Mtume[s.a.w.w] . [158] Anas anaposema "Abu Tal-ha ndiyo mtu wa kwanza kuchukua nywele za Mtume[s.a.w.w] " inaonyesha wazi kuwa Masahaba walishindana katika kutabaruku kwa nywele za Mtume[s.a.w.w] lakini Abu Tal-ha alikuwa wa kwanza kuzichukua. Na imepokewa tena kwamba: "Mtume[s.a.w.w] alifika Mina akaenda kwenye Jamrah akalipiga, kisha akaenda kwenye makazi yake hapo Mina, kisha akamwambia kinyozi, "ninyowe," na akaashiria upande wa kulia kisha kushoto kisha akaendelea kuwapa watu (nywele zake)". [159]

6. Masahaba vile vile walikuwa wakitabaruku kwa chombo alichokuwa amenyewea Mtume[s.a.w.w] : Abu Bar-da amesema: "Abdullah bin Salaam aliniambia, "Je, nisikunyweshe kwenye chombo alichonywea Mtume?"[160] Riwaya hii inaonyesha kwamba, Abdallah bin Salaam alikuwa amekihifadhi chombo hicho kwa kuwa kilikuwa kimepata baraka kwa sababu mjumbe wa Mwenyezi Mungu alinywea chombo hicho.

7. Pia Masahaba walikuwa wakitabaruku kwa mikono yake Mitukufu: "Imepokewa toka kwa Abu Juhaifah amesema, "Mtume alitoka katika siku yenye joto kali akaenda mpaka Bat-haa akatawadha kisha akaswali Adhuhuri rakaa mbili na Al-asr rakaa mbili.... watu wakasimama wakaishika mikono yake wakawa wanajipangusia nyuso zao. Anasema Abu Juhaifah, "Nikauchukua mkono wake nikauweka usoni kwangu, basi niliuona ubaridi mno kuliko theluji na una harufu nzuri kuliko miski".[161]

8. Pia wakitabaruku kwenye mimbari yake tukufu:

Imepokewa toka kwa Ibrahim bin Abdur-Rahman bin Abdil-Qari kwamba yeye alimuona Ibn Omar ameweka mkono wake kwenye Mimbar mahala ambapo Mtume[s.a.w.w] alikuwa akikaa, kisha akauweka nikono wake usoni kwake.[162]

9. Vile vile walikuwa wakitaka uponyo kwenye kaburi lake tukufu: Imepokewa toka kwa Imam Ali[a.s] kwamba yeye amesema, "Kuna bedui alikuja kwetu baada ya kuwa tumemzika Mtume[s.a.w.w] kiasi cha siku tatu zimepita, akajitupa kwenye kaburi Ia Mtume[s.a.w.w] , akajipaka kichwani udongo wa kaburi Ia Mtume[s.a.w.w] na akasema, ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, ulisema tukasikia usemi wako na uliyapokea toka kwa Mwenyezi Mungu, nasi tulipokea toka kwako na miongoni mwa yale ulioteremshiwa na Mwenyezi Mungu ilikuwa, lau wao watazidhulumu nafsi zao wangekujia... nami nimedhulumu (nafsi yangu) na nimekujia unitakie msamaha". Basi palisemwa kutoka kaburini "Hakika umesamehewa." [163] Kwa kifupi, iwapo mtu atavirjea vitabu vya historia (As-sihah na As-Sunan na Masanid) ataona ni jinsi gani Masahaba na Tabiina walivyokuwa wakitabaruku kwa kila kitu ambacho kinamafungamano na Mtume[s.a.w.w] , na walikuwa wakitaka kuponywa kwenye kaburi lake kwa kuweka mashavu yao juu ya kaburi na kuunusa udongo wa mahali hapo na kulia kwenye kaburi la Mtume[s.a.w.w] .

Zaidi ya hapo, walikuwa pia wakitabaruku kwa fimbo ya Mtume[s.a.w.w] na mavazi yake na kuswali sehemu alizokuwa akiswali au alimopita. Na masimulizi yanayozungumzia jambo la kutabaruku ni mengi mno na haiwezekani kwa mtu mwenye akili kusema eti masimulizi haya ni ya kutungwa tu. Basi yatakuwaje ni ya kutunga wakati Bukhari na Muslim pamoja na wanachuoni wengine wa hadithi wameyapokea? Isitoshe hali hii, bali wanachuoni wawili wakubwa wamesimamia ukusanyaji wa riwaya hizi na kuzifafanua pamoja na kutaja rejea zake. Wa kwanza ni, Al-Ustadh Sheikh Muhammad Tahir Makki katika kitabu chake kiitwacho "Tabar-rukus-Sahabah Bia'thari Rasulillah". Wa pili ni, Al-Ustadh Sheikh Ali Ahmadi katika kitabu chake madhubuti kiitwacho "At-Tabar-ruk". Yeye amefafanua kwa undani habari zote zilizokuja kuhusu Tabar-ruk; na kitabu hiki kinahesabiwa kuwa bora cha zama hizi. Basi watasemaje Mawahabi juu ya hadithi hizi ambazo ni mutawatiri kimatamko na kimaana? Na ni upi msimamo wao kutokana na ukweli huu ulio wazi?

Basi ni za nini kelele hizi wazipigazo dhidi ya kutabaruku kwenye kaburi la Mtume[s.a.w.w] jambo ambalo Masahaba na Tabiina wamekuwa wakilifanya bila ubaya wowote wala kulipinga au kuliharamisha, wakati hatuoni popote kwamba Mtume au Masahaba wake waliharamisha jambo hili. Na ni kwa nini Mawahabi hawawaachi Waislamu walibusu kaburi la Mtume[s.a.w.w] na wapate baraka zake na waonyeshe hisiya zao na mapenzi yao kwa Mtume[s.a.w.w] ? Je, Mawahabi hawajuwi kuwa, kukataza kutabaruku kwenye kaburi la Mtume na athari zake ilikuwa tabia na kazi ya Bani Ummayya hasa Mar-wani aliyelaaniwa na Mtume[s.a.w.w] ? Hebu soma mapokezi aliyoyapokea Al-Hakim ndani ya Mustad-rak yake kutoka kwa Dawuud bin Salih amesema: "Sika moja Mar-wan alikuja akamkuta mtu ameweka uso wake juu ya kaburi (la Mtume[s.a.w.w] ) akamshika shingoni kisha akamwambia, "Je unafahamu unachokifanya"? Kumbe mtu yule alikuwa Abu Ayyubul-Ansari, akamjibu, "Ndiyo mimi sikulijia jiwe hapa nimemjia Mjumbe wa Mwenyezi Mungu". Nimemsikia mjumbe wa Mwenyezi[s.a.w.w] akisema: "Msiililie dini (msiihuzunikie) kama watawala wake ni watu wanaostahiki lakini ililieni dini watakapoitawalia wasiostahiki". [164] Mar-hum Sheikh Al-Amini amesema:

"Hadithi hii inatufahamisha kwamba kuzuwiya kutawas-sal kwenye makaburi matakatifu ni miongoni mwa Bid'a za Banu Ummayya na upotevu wao tangu zama za Masahaba na hakuna hata sikio moja kabisa lililopata kumsikia Sahaba akipinga tawas-sul hiyo isipokuwa Mar-wan mdhalimu aliyetokana na kizazi cha Umayya". Ni kweli "Ng'ombe huilinda pua yake kwa pembe zake". Ni kweli pia kwamba "Kwa kisingizio cha kumtafuta njiwa, muwindaji hula tende (za shamba la mitende aliloingia). Ukweli ulivyo ni kwamba Banu Ummayya na hasa Mar-wan, wanayo chuki dhidi ya Mtume[s.a.w.w] tangu siku ile Mtume[s.a.w.w] alipokuwa hakubakisha heshima yoyote ya Banu Ummayya, ila aliivunja wala cheo chochote ila alikiharibu na wala nguzo yao yoyote isipokuwa aliivunja na hayo yametokea kutokana na maneno makali ya Mtume[s.a.w.w] kuhusu Bani Ummayya ile siku ya Badri alipowapiga. Mtume[s.a.w.w] hasemi lolote kwa matamanio ya nafsi yake ila ni wahyi aliyopewa (aliyemfundisha Bwana Mtume ndiye mwenye nguvu zote) kwani imepokewa hadithi sahihi kuwa Mtume[s.a.w.w] amesema, "Itakapofika idadi ya Banu Ummayya watu arobaini watawafanya waja wa Mwenyezi Mungu kuwa ni watumwa, na mali ya Mwenyezi Mungu wataipora na kuifanya knwa ni mali yao na watakitumia vibaya kitabu cha Mwenyezi Mungu". [165]

Umeona jibu la Abu Ayyubul-Ansari kwa Mar-wan pale alipomuuliza unafanya nini? Akawa amejibu, sikujia jiwe bali nimemjia mjumbe wa Mwenyezi Mungu. Hapa tunamuona Abu Ayyubul-Ansari anaeleza kwamba: "Makusudio ya kutawas-sal na kutabaruku ni kwa Mtume[s.a.w.w] ambaye tunaitakidi kuwa hapana tofauti baina ya kuwa yu hai au amekufa katika suala hili, lakini udongo na jiwe havina umuhimu wowote, isipokuwa udongo na jiwe vilivyopo kwenye kaburi la Mtume[s.a.w.w] vimepata heshima na utukufu kwa sababu ya Mtume[s.a.w.w] . Ewe msomaji mpendwa, Bukhari ambaye kitabu chake kinazingatiwa na Masunni kuwa ndiyo kitabu sahihi mno kuliko vingine, yeye ameweka mlango aliouita "Babu Ma-dhukira Min Dir-in-nabi wa asahu wa Saifahu wa qadahahu wa khatamahu wa mas-ta-amalal-khulafan baadahu. Yaani mlango unaozungumzia habari za deraya ya Mtume, panga lake na fimbo yake, kikombe chake, pete yake na vitu walivyovitumia makhalifa waliokuja baada yake katika vitu ambavyo havikugawanywa na nywele zake, na viatu vyake na vyombo vyake ambavyo Masahaba wa Mtume na wengineo walikuwa wakitabaruku kwa vitu hivyo baada ya kufa Mtume[s.a.w.w] . [166]

Kama Mawahabi watazifuatilia hadithi hizi nyingi zaidi ya mia hawatakuwa na njia isipokuwa kukubali ukweli na kukiri iwapo tu watakuwa miongoni mwa wale wanaosikiliza maneno na kufuata yaliyo bora, vinginevyo: "Siku ya Hukumu imewekewa wakati maalum".

TAUHIDI KATIKA IBADA

Msingi wa wito wa Manabii[a.s] siku zote umekuwa ni kulingania kumuabudu Mwenyezi Mungu peke yake na siyo kumuabudu mwingine peke yake, au kumshirikisha na Mwenyezi Mungu. Na msingi wa hukmu za mbinguni tangu mwanzo wa kutumwa ujumbe wa Manabii ilikuwa ni kumpwekesha Mwenyezi Mungu na kukata mizizi ya shirki. Ukweli halisi ulivyo ni kwamba, lengo la kutumwa kwa Manabii ni kulingania (watu) kwenye ibada ya Mwenyezi Mungu peke yake, na kupiga vita ushirikina wa aina zote na khususan kupinga shirki katika ibada. Qur'an Tukufu inaashiria ukweli huu wazi wazi na inasema:

وَلَقَدْ بَعَثْنَا فِي كُلِّ أُمَّةٍ رَّسُولًا أَنِ اعْبُدُوا اللَّـهَ وَاجْتَنِبُوا الطَّاغُوتَ ﴿٣٦﴾

"Na bila shaka tulimpeleka Mjumbe kwa kila umma (akawambie umma wake) muabuduni Mwenyezi Mungu na muyaepuke masanamu. (Qur'an, 16:36)

وَمَا أَرْسَلْنَا مِن قَبْلِكَ مِن رَّسُولٍ إِلَّا نُوحِي إِلَيْهِ أَنَّهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا أَنَا فَاعْبُدُونِ ﴿٢٥﴾

Na hatukumtuma kabla yako Mjumbe yeyote ila tulimfunulia ya kwamba hakuna apasiwaye kuabudiwa ila mimi, basi niabuduni." (Qur'an, 21:25) Qur'an imeizingatia ibada ya Mwenyezi Mungu kuwa ni jambo linalokusanya na kushirikisha sheria zote za mbinguni na inasema:

قُلْ يَا أَهْلَ الْكِتَابِ تَعَالَوْا إِلَىٰ كَلِمَةٍ سَوَاءٍ بَيْنَنَا وَبَيْنَكُمْ أَلَّا نَعْبُدَ إِلَّا اللَّـهَ وَلَا نُشْرِكَ بِهِ شَيْئًا ﴿٦٤﴾

"Waambie, Enyi mliopewa Kitabu cha Mwenyezi Mungu njooni katika neno lililo sawa baina yetu na baina yenu, ya kwamba tusimuabudu yeyote ila Mwenyezi Mungu na wala tusimshirikishe na chochote." (Qur 'an, 3:64)

Tauhidi katika ibada ni msingi imara kwa Waislamu wote, na hapana yeyote aipingaye Tauhidi au kuwa na tofauti ndani yake miongoni mwa vikundi vyote vya Kiislamu, ijapokuwa Mutazilah mtazamo wao juu ya Tauhid ya matendo ya Mwenyezi Mungu unatofauti, na vile vile Ashaira nao wanayo tofauti juu ya Tauhid katika sifa za Mwenyezi Mungu, lakini madhehebu zote za Kiislamu zinaafikiana kuhusu Tauhid ndani ya ibada na hakuna nafasi ya kupinga hilo. Kama kutakuwa na khitilafu, basi ikhtilafu hiyo haiko katika msingi wa Tauhidi ya ibada bali iko katika Misdaaq za Tauhidi ya Ibada. Hii inamaanisha kwamba, baadhi ya Waislamu wanaona kuwa baadhi ya matendo ni ibada na Waislamu wengine wanaona kuwa (matendo hayo) ni Takrima na Taadhima tu na siyo ibada. Na kwa mujibu wa Istilahi ya Elimu ya "Mantik" Tofauti kama hii iko ndani ya 'As-Sughraa" ambayo ni Je, kitendo hiki ni ibada au hapana? Wakati ambapo hakuna tofauti katika 'Al-Kubraa" ambayo ni je, inafaa kumuabudu asiyekuwa Mwenyezi Mungu au hapana? Na hii wameafikiana (Waislamu wote) kwamba haijuzu kumuabudu asiyekuwa Mwenyezi Mungu.

Kwa maneno mengine (Tunaweza kusema) tofauti iliyopo inatokana na Mawahabi kuyazingatia matendo fulani kuwa ni ibada wakati ambapo wasiokuwa wao miongoni mwa Waislamu ulimwenguni kote hawayazingatii kamwe matendo hayo kuwa ni ibada. Hapana budi tuifafanue maana ya "Ibada" kwa mujibu wa lugha na vile vile kwa mjibu wa Qur'an, na hapo ndipo yatakapofahamika matawi ambayo ndani yake imekuja tofauti kuyahusu mwenyewe kwa dhati yake, na ndipo utakapotudhihirikia uhakika na ukweli wa ibada.

TAARIFU KAMILI YA MAANA YA IBADA

Bila shaka maana na Maf-humu ya Ibada iko wazi katika lugha ya Kiarabu, na lau tutakwa hatuwezi kuiarifisha "Ibada" kwa Taarifu ya kimantik kwa kutumia neon moja, basi ni kama mbingu na ardhi ambazo zina maana mbili zilizowazi, wakati ambapo wengi katika sisi hawawezi kutoa taarifu kamili kwa kutumia neon moja lakini hali hii haizuwii kujengeka maana ya ardhi na mbingu katika akili zetu tunapoyasikia matamko hayo. Bila shaka basi, maana ya Ibada ni kama maana ya ardhi na mbingu ambayo inafahamika kwetu sote, pamoja na kutokuweza kuziarifisha mbingu na ardhi kwa taarifu ya kimantiki: Kwa hiyo basi "Ibada" na "Kutukuza" na "Kuheshimu" na "Kukirimu" ni matamko mbali mbali yenye matawi yanayofahamika, na kuyachambua ni jambo rahisi tena jepesi.

Kwa hakika mtu ambaye anampenda yeyote yule kwa mapenzi ya kweli kabisa, utamuona akibusu kutaza nyumba ya mpenzi wake na kunusa mavazi yake na kuyakumbatia kifuani, na atapokufa (mpenzi wake huyu) atalibusu kaburi lake na udongo wa kaburi hilo.... Pamoja na matendo yote haya, hapana yeyote atakayeona kuwa matendo yake huyu mwenye kupenda ni ibada amfanyiayo yule mpenzi wake. Hali hii ni kama ile ya watu kukimbilia kwena kuona miili ya viongozi iliyomo ndani ya majeneza, au kuona kumbukumbu zao na majumba walioyokuwa wakiishi na kusimama dakika chache kuonyesha huzuni kwa ajili ya rohozao yote haya hayazingatiwi kuwa ni ibada katika Taifa lolote miongoni mwa mataifa ulimwenguni, japokuwa mapenzi yao na unyenyekevu wao kwa wato hao uko katika kiwango cha unyenyekevu wa waumini kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu. Hivyo basi, watu wenye maarifa na wachambuzi wa mambo ndiyo ambao wanaweza kupambanua baina ya kuheshimu na ibada. Ewe msomaji mtukufu iwapo tutataka kutoa taarifu ya ibada kimantik, basi ibada itakuwa na taarifu za aina tatu na zote hizi zitalenga maana moja. Ama Mawahabi wao wamechagua Taarifu mbili nyingine na wakazitegemea, lakini zinaupungufu hazikukamilika. Katika maelezo yafuatayo tunazileta hizo Taarifu zao ili tuzijadili.

TAARIFU MBILI PUNGUFU KUHUSU IBADA

Ibada ni kunyenyekea na kudhalilika. Ndani ya vitabu vya lugha Taarifu ya ibada imekuja kwa maana ya kunyenyekea na kudhalilika. Na maana hii imekuja katika Qur'an tukufu lakini Taarifu hii ya Ibada haitoi maana ya ibada kwa undani, na hiyo ni kwa sababu zifuatazo: Ikiwa ibada inakubaliana katika maana na kuwa ni kunyenyekea na kudhalilika, basi haitawezekana kwa mtu yeyote kumzingatia kuwa anampwekesha Mwenyezi Mungu, kwani mtu kwa maumbile yake humnyenyekea Mwalimu wake na mtoto naye huwanyenyekea wazazi wake wawili na kila mpenzi kwa ampendaye. Bila shaka Qur'an Takufu inamuamuru mtu adhalilike kwa wazazi wawili inasema:

وَاخْفِضْ لَهُمَا جَنَاحَ الذُّلِّ مِنَ الرَّحْمَةِ وَقُل رَّبِّ ارْحَمْهُمَا كَمَا رَبَّيَانِي صَغِيرًا ﴿٢٤﴾

"Na wainamishie Bawa Ia udhalili kwa kuwaonea huruma na useme, Mola wangu wahurumie (wazazi) wangu kama walivyonihurumia mimi nilipokuwa mdogo". (Qur'an, 17:24)

Basi iwapo unyenyekevu na udhalili maana yake ni kumfanyia ibada uliyemdhalilikia, basi italazimu kumhukumu ukafiri yeyote anayelea wazazi wake wawili na kinyume chake itakuwa ni lazima kumhukumu kuwa ni mtu wa Tauhidi yule anayewatelekeza wazazi wake na kutowafanyia wema. B: Ibada ni ukomo wa kunyenyekea. Baadhi ya wafasiri walijaribu kuitengeneza na kuirekesbisha Taarifu ya ibada ya kilugha pale walipogundua kuwa inaupungufu wakasema:

"Ibada ni ukomo wa kunyenyekea kwa yule ambaye utukufu wake na ukamilifu wake unafahamika." Taarifu hii inashirikiana na ile ya kwanza katika upungufu na utata. Mwenyezi Mungu anawaamuru Malaika wamsujudie Adam anasema:

وَإِذْ قُلْنَا لِلْمَلَائِكَةِ اسْجُدُوا لِآدَمَ فَسَجَدُوا إِلَّا إِبْلِيسَ أَبَىٰ وَاسْتَكْبَرَ وَكَانَ مِنَ الْكَافِرِينَ ﴿٣٤﴾

"Na kumbuka tulipowaambia Malaika, msujudieni Adam, wakasujudu wote isipokuwa Iblisi". Qur'an, 2:34

Bila shaka kusujudu ndiyo ukomo wa kadhalilika na kunyenyekea kwa yule unayemsujudia, basi ikiwa maana ya ibada ni ukomo wa kunyenyekea italazimu kuwakufurisha Malaika waliotekeleza amri ya Mwenyezi Mungu, na Iblisi kwa kupinga kwake amri ya Mwenyezi Mungu atakuwa ndiyo mwenye imani. Hakika ndugu wa Nabii Yusuf na wazazi wake Nabii Yusuf wote walimsujudia Yusuf kama asemavyo Mwenyezi Mungu Mtukufu:

وَرَفَعَ أَبَوَيْهِ عَلَى الْعَرْشِ وَخَرُّوا لَهُ سُجَّدًا وَقَالَ يَا أَبَتِ هَـٰذَا تَأْوِيلُ رُؤْيَايَ مِن قَبْلُ قَدْ جَعَلَهَا رَبِّي حَقًّا ﴿١٠٠﴾

"Na waliporomoka wote kumsujudia, (Naye Yusuf) akasema: Ewe Baba yangu hii ndiyo Tafsiri ya ndoto yangu ya zamani bila shaka Mwenyezi Mungu ameithibitisha". Qur'an, 12:100

Ndoto aliyoiashiria Nabii Yusuf katika Aya hii, hi ile iliyoko katika kauli ya Mwenyezi Mungu aliposema:

إِذْ قَالَ يُوسُفُ لِأَبِيهِ يَا أَبَتِ إِنِّي رَأَيْتُ أَحَدَ عَشَرَ كَوْكَبًا وَالشَّمْسَ وَالْقَمَرَ رَأَيْتُهُمْ لِي سَاجِدِينَ ﴿٤﴾

"(Kumbuka) Yusuf aliopomwambia Baba yake, Ewe baba yangu hakika nimeona (ndotoni) nyota kumi na moja na jua na mwezi vinanisujudia" (Qur'an, 12:4)

Ni hakika (isiyopingika) kwamba Waislamu wote kwa kufuata mwendo wa Mtume[s.a.w.w] huwa wanalibusu "Hajarul-As-wad". Jiwe jensi lililoko kwenye kona ya Kaaba Tukufu na pia hutaka baraka kwenye jiwe hilo. Kitendo kile kile hufanywa na waabuduo sanamu kwenye masanamu yao jambo ambalo moja kwa moja ni shirki, lakini tendo la Waislamu kwenye Hajarul-As-wad ni tendo la Tauhidi bila shaka yoyote. Kwa hiyo, maana ya ibada siyo ukomo wa kunyenyekea na kudhalilika ingawaje (kunyenyekea na kudhalilika) hakika ni miongoni mwa nguzo za Ibada lakini siyo kwamba hizo ndiyo nguzo pekee za ibada. Hivyo basi, hapana budi pasemwe kuwa, Ibada maana yake ni kunyenyekea na kudhalilika kunakoambatanishwa na itikadi maalum, kitu ambacho kitaifanya ibada iwe imeundika katika misingi miwili.

1. Kunyenyekea na kudhalilika.

2. Itikadi maalum.

Na hii itikadi maalum ndiyo ambayo inaweka msimamo wa kufafanua Qadhiya ya ibada, kwani kunyenyekea japo si sana, ikiwa kutaambatanishwa na itikadi maalum, basi itakuwa ibada. Kwa hakika "Itikadi Maalum" ndiyo inayokivalisha kitendo vazi Ia Ibada, na bila itikadi hiyo maalum ibada haithibitiki japo itadhihirika katika hali ya Ibada.

Na sasa baada ya kuwa tumethibitisha ubatili wa Taarifu mbili ambazo Mawahabi wamezitegemea, na umedhihiri upungufu wake na udhaifu wake, umefika wakati wa kuzungumzia zile Taarifu tatu. Sasa suali ni je, ni nini hiyo "Itikadi maalum" ambayo inaitenganisha ibada na visivyokuwa ibada? Jawabu lake: Kwa hakika ukweli na usahihi, hapa ndipo mahali pa uchambuzi na uhakiki, na jawabu lake litaonekana ndani ya Taarifu tatu zifuatazo:

Taarifu ya Kwanza: Ibada ni kunyenyekea kimatendo au kimatamko, ambako kunatoka ndani ya itikadi ya mtu kwa ajili ya Uluhiyyah (Uungu). Nini maana ya Uluhiyyah nukta hii ni muhimu sana kwa hiyo ni lazima kuieleza.

Jibu: "Uluhiyyah" ni tamko litakanalo na neno "Al-Ilahu" na hilo neno "Al-Ilahu" ndiyo Allah kwa tamko la nakira, (naye ndiyo muumba mtukufu). Na ilivyokuwa neno "Al-llahu" hupata likafasiriwa kwa maana ya mwenye kuabudiwa, basi tafsiri hiyo hiyo ni tafsiri ya kulazimiana, yaani Uluhiyyah unalazimu kuabudiwa siyo kwamba Ilahu maana yake ni mwenye kuabudiwa.

Bila shaka watu wanaoitakidi Ilahu vile vile wanaitakidi kuwepo ulazima wa kumuabudia, sawa sawa ikiwa ni Ilahu wa haki kama alivyo Mwenyezi Mungu au akawa siyo wa haki kama illvyo miungu isiyokuwa Mwenyezi Mungu. Kwa hiyo neno Al-Ilahu hufasiriwa kwa maana ya chenye kuabudiwa kutokana na hali hii tu basi. Dalili iliyowazi kuhusu taarifu hii ni Aya za Qur'an zilizokuja kuzungumzia nyanja hii. Katika mazingatio ndani ya aya hizo inatudhihirikia kwamba "Ibada" na matendo na maneno yanayotokana na Itikadi za Uungu, na kwamba Itikadi hii inapokosekana, basi maana ya Ibada haithibitiki, na ndiyo maana utaiona Qur'an wakati inapoamuru ibada ya Mwenyezi Mungu, basi haraka sana hutoa maelekezo kwamba, hapana mungu asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Kwa mfano isema:

"Enyi watu wangu, muabuduni Mwenyezi Mungu ninyi hamna Mungu ila yeye." Madhumuni ya aya hii yamekuja katika sehemu tisa ndani ya Qur'an au zaidi, nawe msomaji mpendwa unaweza kuzirjea aya hizi katika Surat A'araf aya ya 65, 73 na 58. Pia Surat Huud aya ya 5, 61 na 84, vile vile Surat Anbiyyah aya ya 25, kadhalika Surat Muuminnuna aya ya 23 na 32 na Surat Taha aya ya 14. Ibada zote hizi zinajulisha kwamba, ibada ni kule kunyenyekea na kudhalilika kunakotokana na itikadi ya kuitakidi Uluhiyyah na bila itikadi hii tendo hilo halitaitwa Ibada. Hebu angalia aya zaidi zinazojulisha makusudio hayo. Anasema Mwenyezi Mungu:

إِنَّهُمْ كَانُوا إِذَا قِيلَ لَهُمْ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا اللَّـهُ يَسْتَكْبِرُونَ ﴿٣٥﴾

"Hakika wao walipokuwa wakiambiwa, hapana Mungu (Mwingine) ila Mwenyezi Mungu wao Hupinga." Qur'an, 37:35

Ni kwa nini walikuwa wakipinga? Ni kwa sababu wanaitakidi waungu wasio Mwenyezi Mungu na wanawaabudu. Na anasema Mwenyezi Mungu:

أَمْ لَهُمْ إِلَـٰهٌ غَيْرُ اللَّـهِ سُبْحَانَ اللَّـهِ عَمَّا يُشْرِكُونَ ﴿٤٣﴾

"Au wanaye Mungu mwingine asiye Mwenyezi Mungu, ametakasika Mwenyezi Mungu kutokana na hao washirikina hao wanaowashirikisha." Qur'an, 52:43.

Qur'an inawazingatia watu hawa kuwa ni washirikina kwa kuwa wanaitakidi uungu kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu. Anasema tena Mwenyezi Mungu:

الَّذِينَ يَجْعَلُونَ مَعَ اللَّـهِ إِلَـٰهًا آخَرَ فَسَوْفَ يَعْلَمُونَ ﴿٩٦﴾

"Wale ambao wanafanya pamoja na Mwenyezi Mungu; Mungu Mwingine basi hivi karibuni watajua." Qur'an , 15:96

وَالَّذِينَ لَا يَدْعُونَ مَعَ اللَّـهِ إِلَـٰهًا آخَرَ ﴿٦٨﴾

"Na wale ambao hawamuombi mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu..... (Qur'an, 25:68).

Na miongoni mwa aya zinazojulisha kwamba maombi ya Washirikina yalikuwa yakiambatana na itikadi ya uungu kwa masanamu yao ni hizi zifuatazo:

وَاتَّخَذُوا مِن دُونِ اللَّـهِ آلِهَةً لِّيَكُونُوا لَهُمْ عِزًّا ﴿٨١﴾

"Waliwafanya waungu wengine badala ya Mwenyezi Mungu ili wawe wenye nguvu." Qur'an, 19:81.

"Je, ninyi mnashuhudia kwamba kuna waungu wengine pamoja na Mwenyezi Mungu." Qur'an, 6:19

وَإِذْ قَالَ إِبْرَاهِيمُ لِأَبِيهِ آزَرَ أَتَتَّخِذُ أَصْنَامًا آلِهَةً إِنِّي أَرَاكَ وَقَوْمَكَ فِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ ﴿٧٤﴾

"Na (kumbukeni) Ibrahimu alipomwambia Baba yake Azar. 'Unawafanya Masanamu kuwa ni waungu.'" Qur'an, 6:74

Mazingatio katika aya zinazozungumzia shirki yawatu wanaoabudu sanamu yatatudhihirishia ukweli huu, nao ni kuwa ushirikina wa watu hawa umekuja kwa sababu ya kuitakidi kwao uungu wa masanamu yao waliyokuwa wakiyaabudu, na kwamba masanamu hayo ni miungu wadogo ambao Mungu mkubwa amewapa baadhi ya mambo yanayomstahiki, basi (masanamu hayo) yameumbwa na wakati huo huo yanaabudiwa. Na kwa ajili hii basi walikuwa wakiikataa Tauhidi. Qur'an inasema:

ذَٰلِكُم بِأَنَّهُ إِذَا دُعِيَ اللَّـهُ وَحْدَهُ كَفَرْتُمْ وَإِن يُشْرَكْ بِهِ تُؤْمِنُوا فَالْحُكْمُ لِلَّـهِ الْعَلِيِّ الْكَبِيرِ ﴿١٢﴾

"Hii ni kwa sababu mlikuwa akitajwa Mwenyezi Mungu peke yake mnakanusha, na akishirikishwa mnaamini, basi (leo) hukumu ni yake Mwenyezi Mungu Mtukufu aliye mkuu." Qur'an, 40:12

Na kwa ajili hii mfasiri mkubwa mar-hum Ayatullah Sheikh Muhammad Jawad Al-Balaghi ametoa Taarifu nzuri ya "Ibada" katika tafsiri yake madhubuti iitwayo Aalaur-Rahman anasema: "Ibada: Ni hisia ya unyenyekevu wanayoifanya kwa ajili ya yule wanayemfikiria kuwa ni Mungu wake ili atimize haki yake makususi ya uungu.[167]

Bila shaka marehemu Al-Balaghi ametoa mtazamo wake wa kielimu kutokana na ufahamu wa kimaumbile juu ya neno "Ibada" katika msingi wa tamko, ndipo ilipokuja Taarifu hii inayokubaliana na aya za Qur'an. Taarifu ya Pili ya Ibada: Hakika Ibada ni kunyenyekea mbele ya yule ambaye (Mwenye kunyenyekea) humzingatia kuwa ndiyo Rabbi (Mola). Na tunaweza kuiarifisha ibada kama ifuatavyo; Ibada ni kunyenyekea kimatendo au kimaneno kwa yule anayeitakidiwa kuwa Mola basi kuabudiwa kunalazimiana na kuwa Mola na ikiwa mtu atajiona yeye mwenyewe kuwa ni mja kwa yule anayemuitakidi kuwa ni Mola wake kwa kuumba; sawa sawa Mola huyo akiwa ni kwa hakika au hapana, na akamnyenyekea pamoja na itikadi hii basi atakuwa amemuabudia. Na katika Qur'an Tukufu kuna aya zinazofahamisha kuwa ibada ni miongoni mwa mambo ya umola yaani "Ar-rububiyyah". Hebu ziangalie baadhi ya hizo aya:

وَقَالَ الْمَسِيحُ يَا بَنِي إِسْرَائِيلَ اعْبُدُوا اللَّـهَ رَبِّي وَرَبَّكُمْ ﴿٧٢﴾

"Naye Masihi alisema, Enyi wana wa Israeli, mwabuduni Mwenyezi Mungu, Mola wangu na Mola wenu". Qur'an, 5:72

إِنَّ اللَّـهَ رَبِّي وَرَبُّكُمْ فَاعْبُدُوهُ هَـٰذَا صِرَاطٌ مُّسْتَقِيمٌ ﴿٥١﴾

"Bila shaka Mwenyezi Mungu ni Mola wangu na ni Mola wenu. Basi muabuduni hii ndiyo njia iliyonyooka" Qur'an 3.51

Na aya nyinginezo zaidi ya hizi. Na kuna aya nyingine zinazoizingatia Ibada kuwa ni miongoni mwa mambo ya muumba kama ilivyo katika kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu aliposema:

ذَٰلِكُمُ اللَّـهُ رَبُّكُمْ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ خَالِقُ كُلِّ شَيْءٍ فَاعْبُدُوهُ ﴿١٠٢﴾

"Huyo ndiye Mwenyezi Mungu Mola wenu, hakuna anayeabudiwa kwa haki ila yeye muumba wa kila kitu, basi muabuduni." Qur'an 6:102

Ni maana ya neno (Ar-Rabbu)? Neno Rabbu hutumika katika lugha ya Kiarabu kwa yule aliyetegemezewa uangalizi wa kitu fulani na yakaachwa mikononi mwake matokeo au ukomo wa kitu hicho. Basi iwapo neno hili litatumika kwa mtu anayemiliki nyumba na au anayemiliki ngamia au mlezi wa mtoto na mkulima na wengineo, basi hiyo ni kwa sababu wanamiliki kuendesha kitu hicho na kusimamia majukumu yake. Nasi tunapomzingatia Mwenyezi Mungu kuwa ni "Ar- Rabbu" ni kwa sababu mambo yetu na mwisho wetu kama vile mauti, uhai, rizki, afya na uwekaji wa sheria pia msamaha na mambo mengineyo, yote yako mikononi mwake Mwenyezi Mungu Mtukufu. Sasa basi Iau kuna mtu ataitakidi kwamba, moja katika mambo haya au yote, Mwenyezi Mungu amempa mtu fulani (Ayasimamie), basi maana ya itikadi hii ni kwamba kumzingatia huyo mtu kuwa ni "Rabbu" na kumuamini Rabbi huyu na kumnyenyekea itakuwa ni kumuabudia. Kwa maneno mengine tunasema, "Bila shaka ibada inatokana na hisiya za mtu kujiona kuwa yeye ni mja (mtumwa) na hii ndiyo hakika ya ubudiyah, ni ni mtu kuizingatia nafsi yake kuwa amemilikiwa na yuko juu yake aliyemmiliki, kuwepo kwake na kifo chake na uhai na rizki yake na mengineyo. Au kwa uchache akamfanya huyo aliye juu yake kuwa ni mwenye kumiliki uwezo wa kusamehe:

(1) Mwenyezi Mungu Anasema:Nani anayesamehe madhambi isipokuwa ni Mwenyezi Mungu ; 3:135

(2) Mwenyezi Mungu Anasema:Waambie Shafaa ni ya Mwenyezi Mungu ; Az-zumar: 44

(3) Mwenyezi Mungu Anasema:Waliwafanya Makasisi wao na watawa wao kuwa ni Mola badala ya Mwenyezi Mungu, 9:31 Na Shafaa, na kumuwekea Kanuni (za maisha yake) na wajibu mwingineo, basi kwa ajili hiyo atakuwa amemfanya kuwa ni "RABBU" mlezi wake. Kwa hiyo yeyote ambaye atakayeamini na kuitakidi katika nafsi yake (kama tulivyoeleza hapo kabla) na akaifasiri itikadi hiyo kwa maneno na matendo, basi hapana shaka kwamba anamuabudu huyo aliyemzingatia kuwa ni "Rabbu".

TAARIFU YA TATU YA IBADA

Hapa tunaweza kutoa Taarifu hii ya tatu ya ibada inayopatikana kutokana na maumbile na nguvu ya nafsi. Tunasema: "Ibada ni kumnyenyekea yule ambaye tunamzingatia kuwa Mungu na ndiyo asili ya matendo ya kiungu". Hapana shaka kwamba matendo ambayo yanahusiana na ulimwengu, kama vile kusimamia uendeshaji wa ulimwengu na kuhuisha na kufisha na kugawa rizki baina ya viumbe na kusamehe madhambi yote haya yanamuhusu Mwenyezi Mungu Mtukufu. Nawe (msomaji) lau utazizingatia vyema aya za Qur'an zinazozungumzia maelezo tuliyotangulia kuyataja, katika Aya ya 35 Surat Al- Qasa, Aya ya 60 mpaka Aya ya 64 Surat An-Namli Aya ya 5 na ya 6 Sura Az-Zummar. Utaona kwamba Qur'an inasisitiza kwa nguvu sana kuwa matendo haya yanamuhusu Mwenyezi Mungu tu na wala hayamuhusu mwingine asiyekuwa yeye. Hii ni kwa upande mmoja, ama kwa upande wa pili: Sote tunafahamu kwamba ulimwengu wa viumbe ni ulimwengu uliopangwa vyema kabisa, na hakiwezi kutokea kitu isipokuwa sababu ya kutokea kwake itarejea kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Qur'an Tukufu inaonyesha (ukweli) wa jambo hili. Mwenyezi Mungu anasema:

وَهُوَ الَّذِي يُحْيِي وَيُمِيتُ وَلَهُ اخْتِلَافُ اللَّيْلِ وَالنَّهَارِ أَفَلَا تَعْقِلُونَ ﴿٨٠﴾

"Na ni yeye (Mwenyezi Mungu) ndiye anayehuisha na kufisha, na mabadiliko ya usiku na mchana yamo katika milki yake." Qur'an, 23:80.

Katika mahala pengine Mwenyezi Mungu anasema kwamba miongoni mwa Malaika wapo wanaosimamia utoaji wa Roho. Nayo ni kauli yake isemayo:

حَتَّىٰ إِذَا جَاءَ أَحَدَكُمُ الْمَوْتُ تَوَفَّتْهُ رُسُلُنَا وَهُمْ لَا يُفَرِّطُونَ ﴿٦١﴾

"Hata pale mmoja wenu anapofikiwa na mauti wajumbe wetu humfisha." Qur'an, 6:61

Kwa kuijengea hali hii, inawezekana kuzikusanya aya hizi mbili na tukasema kama ifuatavyo: "Bila shaka hizi sababu zinazosababisha pia matendo ya ulimwenguni, kama yatakuwa ni ya kimaumbile ya kawaida au kimaana kama vile Malaika, basi iwe iwavyo yanathibitika kwa idhini ya Mwenyezi Mungu Mtukufu naye ndiye mtendaji halisi." Kwa maneno mengine ni kwamba, kitendo cha watendaji hawa wawili (Mwenyezi Mungu na Malaika) ni kitendo kimoja tu na si vitendo viwili lakini mtendaji wa kwanza anafanya kwa uwe wake na yule wa pili anamfuatia yule wa kwanza (kutekeleza maamrisho yake).

Maana hii ni miongoni mwa maarifa ya juu katika Qur'an ambayo hufahamika kwa kuzirejea aya za Qur'an zinazozungumzia matendo ya Mwenyezi Mungu Mtukufu. Sasa basi ikiwa mtu ataitakidi kwamba Mwenyezi Mungu amewapa baadhi ya viumbe wake kama vile, Malaika na Mawalii matendo yake ya kuruzuku, na kuhuisha na yasiyokuwa hayo, na akaammi pia kuwa viumbe hao ndiyo wanaoendesha mambo ya ulimwengu na kuyasimamia mambo yake na akaona kuwa Mwenyezi Mungu hahusiki tena kwenye matendo hayo kiasi kwamba itikadi hiyo ikampelekea kuwanyenyekea viumbe hawa, basi hapana shaka yoyote kwamba unyenyekevu wake huu ni ibada na tendo hili ni kumshirikisha Mwenyezi Mungu Mtukufu. Kwa maneno mengine tunasema: "Lau mtu ataitakidi kwamba Mwenyezi Mungu ameukabidhi ustahiki wa kutekeleza matendo kwa Malaika na Mawalii, na Mwenyezi Mungu akawa amebaki hana ustahiki wote wote (katika matendo hayo) na hao Malaika na Mawalii wanayafanya matendo hayo bila kumtegemea Mwenyezi Mungu na bila idhini yake, basi mtu huyu aliyeitakidi itikadi hii, hakika amemfanyia Mwenyezi Mungu mshirika na amemfananisha (Na viumbe vyake). Hapana shaka kwamba itikadi kama hii ndiyo kuishirikisha dhati ya Mwenyezi Mungu na kutawas-sal na kunyenyekea kunakotokana na itikadi hii ni ibada kama ilivyokuja katika Qur'an Tukufu.

Anasema Mwenyezi Mungu:

وَمِنَ النَّاسِ مَن يَتَّخِذُ مِن دُونِ اللَّـهِ أَندَادًا يُحِبُّونَهُمْ كَحُبِّ اللَّـهِ ﴿١٦٥﴾

"Na miongoni mwa watu wako wanaofanya waungu badala ya Mwenyezi Mungu, na wanawapenda kama (anavyostahiki) kupendwa Mwenyezi Mungu". Qur'an, 2:165

Kwa hakika chochote chenye kuwa na kuwepo hakiwezi kuwa mfano wa Mwenyezi Mungu au mshiriki isipokuwa kitakapokuwa na uwezo wa kuuendesha ulimwengu kwa matakwa yake binafsi bila ya matakwa ya Mwenyezi Mungu lakini hakuna yeyote mwenye uweza huo. Bali kila kilichopo ni chenye kunyenyekea mbele ya matakwa ya Mwenyezi Mungu Mtukufu kitake au kisitake basi kwa hiyo hakiwezi kuwa mshirika wa Mwenyezi Mungu bali kitakuwa kitiifu kwake kutenda kama atakavyo yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu. Ukweli halisi in kuwa, washirikina walikuwa wakiitakidi kwamba, masanamu yao waliyokuwa wakiyaabudu yanajitegemea katika kunendesha ulimwengu huu na pia katika mambo ya uungu.

Na katika zama za Jahiliya (kabla kuja Uislamu) kulikuwa na ushirikina wa namna mbali mbali na ushirikina wa daraja ya chini kabisa ilikuwa ni itikadi ya Mayahudi na Wakristo kwamba mapadri na Makasisi wao wanayo madaraka ya uwekaji wa kanuni na sheria kama alivyosema Mwenyezi Mungu:

وَعَلَّمَ آدَمَ الْأَسْمَاءَ كُلَّهَا ثُمَّ عَرَضَهُمْ عَلَى الْمَلَائِكَةِ فَقَالَ أَنبِئُونِي بِأَسْمَاءِ هَـٰؤُلَاءِ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ﴿٣١﴾

"Waliwafanya wanachuoni wao na watawa wao kuwa ni waungu wao kinyume cha Mwenyezi Mungu". Qur 'an, 2:31

Kadhalika washirikina walikuwa wakiitakidi kwamba, ustahiki wa Shafaa na Maghfira (mambo ambayo yanamstahiki Mwenyezi Mungu tu) vimekabidhiwa kwa Masanamu yao wanayoyaabudu, na masanamu hayo yanafanya mambo hayo yenyewe kikamilifu kwa kujitegemea katika ustahiki huo. Na kwa ajili hii utaona aya nyingi za Qur'an zinazozungumzia Shafaa zinasisitiza kwamba Shafaa haithibitiki ila kwa idhini ya Mwenyezi Mungu asemavyo ndani ya Qur'an:

مَن ذَا الَّذِي يَشْفَعُ عِندَهُ إِلَّا بِإِذْنِهِ ﴿٢٥٥﴾

"Na ni nani huyo awezaye kushufaiya (kuombea) mbele ya Mwenyezi Mungu isipokuwa kwa idhini yake." Qur 'an, 2:255

Na lau washirikina wangekuwa wanaitakidi kwamba, masanamu yao waliyokuwa wakiyaabudu yanauwezo wa kushufaiya kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, basi usingeona Qur'an inakanusha moja kwa moja Shafaa bila ya idhini ya Mwenyezi Mungu. Baadhi ya wanafalsafa wa Kiyunani walikuwa wamejenga ndani ya fikra zao Miungu wengi kwa kila jambo miongoni mwa mambo ya ulimwenguni. (Kwa mfano) mvua ina Mungu wake, mimea ina mungu wake, mtu ana Mungu wake na mambo mengine (kila moja lina mungu wake). Na walikuwa wakidai kwamba utendaji wa kuendesha mambo ya ulimwengu ambao unamuhusu Mwenyezi Mungu peke yake, umekabidhiwa kwa miungu hawa. Na katika zama za Jahiliya, baadhi ya Waarabu walikuwa wakiabudu Malaika na nyota zitembeazo na zile zisizotembea hali ya kuwa wakidhani kwamba usimamizi wa mambo ya ulimwengu na watu umekabidhiwa kwa vitu hivyo, navyo ndivyo vinavyotenda kikamilifu kwa kujitegemea na hiyari kamili, na kuwa Mwenyezi Mungu ameuzuliwa na hana uwezo wowote juu ya mambo haya kabisa (ametakasika Mwenyezi Mungu na fikra hizi sana sana).[168]

Na kwa hiyo basi kila aina ya unyenyekevu utaofanywa kwa Malaika na nyota utazingatiwa kuwa ni ibada kwa kuwa unatokana na itikadi hii yenye makosa. Kuna baadhi ya Waarabu wengine wa zama za Jahiliyyah, hawakuyaitakidi masanamu yaliyochongwa kwa miti na madini kuwa ni Miungu na kwamba ndiyo yaliyowaumba wala kusimamia mambo ya ulimwengu na watu, bali wao walikuwa wakiyaamini kuwa yanao uwezo wa kuwaombea na walikuwa wakisema: "Masanamu haya ni waombezi wetu mbele ya Mwenyezi Mungu".[169] Na kwa msingi wa mtazamo huu batili, walikuwa wakiyaabudu Masanamu haya kwa lengo la kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu na walikuwa wakisema wamasema:

مَا نَعْبُدُهُمْ إِلَّا لِيُقَرِّبُونَا إِلَى اللَّـهِ زُلْفَىٰ ﴿٣﴾

"Sisi hatuyaabudu (Masanamu) isipokuwa kwa ajili ya kutukurubisha kwa Mwenyezi Mungu." Qur 'an, 39:3

Kwa kifupi tunasema: "Bila shaka tendo lolote litokanalo na itikadi hii na likajulisha kufuata na kunyenyekea basi ni ibada, na kinyume chake ni kuwa tendo lolote ambalo halikutegemezewa itikadi kama hii haliwezi kuzingatiwa kuwa ni ibada wala shirki."

Lau mtu atanyenyekea mbele ya mtu na akamuheshimu na kumtukuza bila ya kuamini itikadi kama hii, basi tendo hili halitachukuliwa kuwa ni shirki wala ibada hata kama tendo hilo litakakadiriwa kuwa ni haramu.

Kwa mfano: Haitazingatiwa kuwa ni ibada sijda ya mpenzi kwa mpenzi wake, wala mwenye kuamriwa kumsujudia aliyemuamuru na mke kumsujudia mume pamoja na kwamba Sijda kumsujudia asiye Mwenyezi Mungu ni haramu kisheria, kwani Sijda ni Makhsusi kwa Mwenyezi Mungu peke yake wala hairuhisiwi kwa yeyote yule kafanyiwa japo itakuwa ni kwa sura ya dhahiri isiyokuwa na itikaadi isipokuwa kama Mwenyezi Mungu ataamuru kufanywa kwa sijida hiyo (kwa asiye Mwenyezi Mungu).

11

UCHUNGUZI JUU YA UWAHABI

KUTABARUKU KWA ATHARI ZA MAWALLI WA MWENYEZI MUNGU NA KUOMBA UPONYO

Mawahabi wanaitikadi kwamba kutaka baraka kwenye Athari za Mawalii wa Mwenyezi Mungu ni kumshirikisha Mwenyezi Mungu. Mawahabi pia wanamuona kuwa ni mshirkina mtu ambaye ataibusu mihrabu ya Mtume[s.a.w.w] na mimbari yake, japo hatafanya hivyo kwa nia ya ibada, isipokuwa ni kwa ajili tu ya mapenzi yake kwa Mtume[s.a.w.w] ndiyo maana katabaruku na kutaka uponyo kwenye Athari zake. Kukataza kutabaruku kwa athari za Mtume[s.a.w.w] na kulibusu kaburi lake na mimbari yake tukufu ni katika mambo ambayo Mawahabi wametilia nguvu kuyapinga dhidi ya Waislamu, na wamekuwa wakitumia makundi ya askari wa kigaidi waliopewa jina la waamrishaji mema na kukataza maovu, na wamewasambaza (askari) hao katika Msikiti wa Mtume[s.a.w.w] ili wazuwiye kulibusu kaburi lake tukufu na mimbari yake tukufu, pamoja na mihrab ya Msikiti wa Mtume[s.a.w.w] . Mawahabi hawa wanawahujumu mahujaji hapo Madina kwa kila aina ya mateso na kuwazuwiya kutabaruku na kulibusu kaburi la Mtume[s.a.w.w] na utawaona kila mara wameshika fimbo, na mikononi mwao mna nyaya ngumu tayari kumshambulia kila Hujaj atakayethubutu kutabaruku au kulibusu kaburi la Mtume[s.a.w.w] . Na kutokana na hali hii basi, mara kwa mara wamekuwa wakimwaga damu za mahujaji wasio na makosa na kuudhalilisha utu wao katika Msikiti wa Mtume[s.a.w.w] , kwa madai kwamba kutabaruku na kulibusu kaburi ni kumuabudu huyo aliyezikwa hapo.

Kwa hakika watu hawa hawaujuwi Uislamu, na wamekosea kufahamu maana ya Ibada na Maf-humu yake, na kwa sababu hii basi wamepotea njia na wanatangatanga ndani ya upotevu. Wamekuwa wanaona eti kila anapoheshimiwa mtu aliyekwisha kufa ni kumuabudu mtu huyo, pamoja na kufahamu kwamba kubusu kaburi tukufu na kutabaruku kwa athari za Utume siyo kwa ajili nyingine isiyokuwa ya Mwenyezi Mungu, kwa kuwa Waislami hawamtukuzi Mtume Mtukufu wala hawatabaruku kwa athari zake ila ni kwa kuwa yeye ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na ni Nabii wake mteule ambaye Mwenyezi Mungu amemtukuza kuliko Manabii wote na viumbe wote. Basi na ifahamike kwamba kila wanapoheshimiwa na kutukuzwa Mawalii wa Mwenyezi Mungu tendo hilo (kwa asili) ni kumtukuza Mwenyezi Mungu. Na hauthibitiki ukweli wa Tauhidi ila pale kila kitu kitakapotendwa kiwe ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na katika njia yake, na hapo ndipo itakapokuwa kila kitu kinaanzia kwa Mwenyezi Mungu na kila kitu kinaishia kwake.

Tutazungumzia maana ya Ibada katika sehemu ifuatayo kwa undani, ama sasa hivi utafiti wetu utahusu kutabaruku kwa athari za Mawalii, na utafiti huu tutalazimika kuulekeza kwenye kipimo cha Qur'an na Sunna ya Mtume[s.a.w.w] ili haki iweze kubainika.

MTAZAMO WA QUR'AN JUU YA KUTABARUKU

Katika Qur'an tunatosheka na aya moja tu, nayo ni ile inayomnukuu Nabii Yusuf[a.s] akisema: "Nendeni na kanzu yangu hii mukaiweke usoni kwa baba yangu (macho yake yatarudi) ataona". Qur'an, 12.93. Nabii Yusuf aliituma kanzu yake kwenda kwa baba yake na akawaambia ndugu zake "Nendeni na kanzu yangu hii na muiweke usoni kwa baba yangu ili macho yake yarudi apate kuona. Mwenyezi Mungu anasema: "Na alipokuja mtoaji habari njema, aliiweka kanzu ile usoni kwake na macho yalirudi akaona". Qur'an, 12:96. Aya hii iko wazi kutoa ruhusa ya kutabaruku kwa athari za Manabii na Mawalii kiasi kwamba hata Nabii anatabaruku kwa Nabii mwenziwe kama hivi Nabii Yaqub[a.s] anatabaruku kwa kanzu ya Nabii Yusuf[a.s] .

Na ni wazi kabisa kwamba kuponya kunatoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, na yeye ndiye mtendaji halisi, isipokuwa kutabaruku kwa kanzu ya Nabii kumekuwa ni wasila wa kuponya kama tunavyotumia dawa kuwa ni wasila wa kupona kwa idhini ya Mwenyezi Mungu Mtukufu. Ewe msomaji ingekuwaje kama kutabaruku kwa Nabii Yaqub kwa kanzu ya mwanawe Yusuf kungelitokea mbele ya watu wa Najdi na wafuasi wa Muhammad Ibn Abdul-Wahab, wangelihukumu namna gani jambo hili? Je, wangehukumu kuwa ni kafiri au mshirikina au mwenye dhambi? Wakati yeye ni Nabii na ni maasum? Kutabaruku kwa Waislamu kwenye kaburi la Mtume[s.a.w.w] na makaburi ya watu wa nyumba yake na pia athari zao hakuna tofauti na kutabaruku alikotabaruku Nabii Yaqub[a.s] kwa kanzu ya mwanawe Yusuf[a.s] .

KUTABARUKU NA SERA YA WAISLAMU

Mtazamo wa haraka katika sera ya Waislamu kuanzia kwa Masahaba mpaka leo, unatuonyesha wazi sunna inayofuatwa kuhusu kutabaruku kwa Mtume[s.a.w.w] yeye mwenyewe na athari zake tukufu katika kpindi chote cha historia ya Uislamu. Na katika maelezo yafuatayo tutaeleza mifano michache inayohusu kutabaruku:

1. Bibi Fatma Az-Zahra ambaye ndiye mwanamke bora ulimwenguni na ni binti ya Mtume[s.a.w.w] , alifika kwenye kaburi la baba yake na akachukua gao Ia udongo wa kaburi akawa anaunusa na kulia huku akisema: "Mtu aliyenusa udongo wa kaburi la Ahmad, halaumiwi iwapo hatanusa mafuta mazuri ya ghaliya." Yamenipata milele masaibu ambayo lau yangeliupata mchana ungegeuka na kuwa usiku. Wameitaja Qadhiya hii wanahistoria wengi miongoni mwao ni As-Samhudi.[151] Kwa hakika kitendo hiki cha Bibi Fatma Az-Zahra ambaye ni maasum kinajulisha kwamba kutabaruku kwenye kaburi la Mtume[s.a.w.w] ni jambo linalofaa na pia kutabaruku kwa udongo wa kaburi lake.

2. Bilal ambaye alikuwa ni muadhini wa Mtume[s.a.w.w] alipata kuishi Shamu katika kipindi cha utawala wa Omar Ibn Khattab. Siku moja alimuona Mtume[s.a.w.w] katika ndoto anamwambia:

"Ewe Bilal mbona umenitupa kiasi hiki, je haujakufikia wakati wa kunizuru ewe Bilal?" Basi Bilal alizindukana usingizini akiwa na huzuni na khofu nyingi na alipanda kipando chake kuelekea Madina na akafika kwenye kaburi la Mtume[s.a.w.w] akawa analia pale kaburini huku anausugua uso wake kwenye kaburi, mara Hasan[a.s] na Husein[a.s] wakafika, Bilal akawakumbatia na kuwabusu....[152]

3. Ibn Hajar anasema: "Kila mtoto aliyezaliwa katika zama za uhai wa Mtume[s.a.w.w] huhukumiwa kwamba alimuona Mtume[s.a.w.w] , na hii ni kwa sababu Ansar wote walikuwa wakiwaleta watoto wao kwa Mtume[s.a.w.w] kwa ajili ya Tahnik [153] na kupata baraka kiasi kwamba imesemwa kuwa: Wakati Makka ilipotekwa na (Waislamu), watu wa Makka wakawa wanakuja kwa Mtume[s.a.w.w] wakiwa na watoto wao ili awaguse vichwa vyao na awaombee baraka".[154] Na kuhusu jambo la kutabaruku, mwandishi wa kitabu kiitwacho, "Tabar-rukus Sahabah" amesema: "Hapana shaka kwamba athari za Mjumbe wa Mwenyezi Mungu (ambaye ni) mbora kuliko viumbe wote na mbora kuliko mitume wote, kuwepo kwake ni jambo lenye kuthibiti na ni mashuhuri mno. Basi kwa hiyo athari hizo ndiyo bora kutabaruku kwazo, na idadi kubwa ya Masahaba wameziona na wakaafikiana kutabaruku kwazo na kuzipa umuhimu wa kuzikusanya nao Masahaba ndiyo watu waongofu na ni kiigizo kizuri, kwani walitabaruku kwa nywele zake na maji aliyotawadhia na jasho lake na nguo zake na pia kuugusa mwili wake na mengineyo yanayofahamika katika athari zake tukufu ambazo zimesihi khabari zake toka kwa watu wema.[155] Yanatosheleza maelezo aliyoyataja Muslim katika Sahih yake kuhusu kutabaruku aliposema: "Hakika Mtume[s.a.w.w] alikuwa akiletewa watoto naye huwafanyia tahnik.[156]

4. Masahaba walikuwa wakitabaruku kwa maji ya udhu aliyotawadha na aliyokoga Mtume[s.a.w.w] : Bukhari amopokea hadithi isemayo: "Mtume[s.a.w.w] alitutokea katika kipindi cha jua kali, akaletewa maji ya kutawadha na akatawadha, basi watu wakawa wanachukua maji ya udhu atawadhayo Mtume[s.a.w.w] wanajipangusia". [157] Kuhusu jambo hilo kuna riwaya nyingi zilizojaa katika vitabu vya hadithi.

5. Masahaba walikuwa wakitabaruku kwa nywele za Mtume[s.a.w.w] kama alivyopokea Anas kwamba: "Mtume[s.a.w.w] aliponyoa kichwa chake, Abu Tal-ha alikuwa ni mtu wa kwanza kuchukuwa nywele za Mtume[s.a.w.w] . [158] Anas anaposema "Abu Tal-ha ndiyo mtu wa kwanza kuchukua nywele za Mtume[s.a.w.w] " inaonyesha wazi kuwa Masahaba walishindana katika kutabaruku kwa nywele za Mtume[s.a.w.w] lakini Abu Tal-ha alikuwa wa kwanza kuzichukua. Na imepokewa tena kwamba: "Mtume[s.a.w.w] alifika Mina akaenda kwenye Jamrah akalipiga, kisha akaenda kwenye makazi yake hapo Mina, kisha akamwambia kinyozi, "ninyowe," na akaashiria upande wa kulia kisha kushoto kisha akaendelea kuwapa watu (nywele zake)". [159]

6. Masahaba vile vile walikuwa wakitabaruku kwa chombo alichokuwa amenyewea Mtume[s.a.w.w] : Abu Bar-da amesema: "Abdullah bin Salaam aliniambia, "Je, nisikunyweshe kwenye chombo alichonywea Mtume?"[160] Riwaya hii inaonyesha kwamba, Abdallah bin Salaam alikuwa amekihifadhi chombo hicho kwa kuwa kilikuwa kimepata baraka kwa sababu mjumbe wa Mwenyezi Mungu alinywea chombo hicho.

7. Pia Masahaba walikuwa wakitabaruku kwa mikono yake Mitukufu: "Imepokewa toka kwa Abu Juhaifah amesema, "Mtume alitoka katika siku yenye joto kali akaenda mpaka Bat-haa akatawadha kisha akaswali Adhuhuri rakaa mbili na Al-asr rakaa mbili.... watu wakasimama wakaishika mikono yake wakawa wanajipangusia nyuso zao. Anasema Abu Juhaifah, "Nikauchukua mkono wake nikauweka usoni kwangu, basi niliuona ubaridi mno kuliko theluji na una harufu nzuri kuliko miski".[161]

8. Pia wakitabaruku kwenye mimbari yake tukufu:

Imepokewa toka kwa Ibrahim bin Abdur-Rahman bin Abdil-Qari kwamba yeye alimuona Ibn Omar ameweka mkono wake kwenye Mimbar mahala ambapo Mtume[s.a.w.w] alikuwa akikaa, kisha akauweka nikono wake usoni kwake.[162]

9. Vile vile walikuwa wakitaka uponyo kwenye kaburi lake tukufu: Imepokewa toka kwa Imam Ali[a.s] kwamba yeye amesema, "Kuna bedui alikuja kwetu baada ya kuwa tumemzika Mtume[s.a.w.w] kiasi cha siku tatu zimepita, akajitupa kwenye kaburi Ia Mtume[s.a.w.w] , akajipaka kichwani udongo wa kaburi Ia Mtume[s.a.w.w] na akasema, ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, ulisema tukasikia usemi wako na uliyapokea toka kwa Mwenyezi Mungu, nasi tulipokea toka kwako na miongoni mwa yale ulioteremshiwa na Mwenyezi Mungu ilikuwa, lau wao watazidhulumu nafsi zao wangekujia... nami nimedhulumu (nafsi yangu) na nimekujia unitakie msamaha". Basi palisemwa kutoka kaburini "Hakika umesamehewa." [163] Kwa kifupi, iwapo mtu atavirjea vitabu vya historia (As-sihah na As-Sunan na Masanid) ataona ni jinsi gani Masahaba na Tabiina walivyokuwa wakitabaruku kwa kila kitu ambacho kinamafungamano na Mtume[s.a.w.w] , na walikuwa wakitaka kuponywa kwenye kaburi lake kwa kuweka mashavu yao juu ya kaburi na kuunusa udongo wa mahali hapo na kulia kwenye kaburi la Mtume[s.a.w.w] .

Zaidi ya hapo, walikuwa pia wakitabaruku kwa fimbo ya Mtume[s.a.w.w] na mavazi yake na kuswali sehemu alizokuwa akiswali au alimopita. Na masimulizi yanayozungumzia jambo la kutabaruku ni mengi mno na haiwezekani kwa mtu mwenye akili kusema eti masimulizi haya ni ya kutungwa tu. Basi yatakuwaje ni ya kutunga wakati Bukhari na Muslim pamoja na wanachuoni wengine wa hadithi wameyapokea? Isitoshe hali hii, bali wanachuoni wawili wakubwa wamesimamia ukusanyaji wa riwaya hizi na kuzifafanua pamoja na kutaja rejea zake. Wa kwanza ni, Al-Ustadh Sheikh Muhammad Tahir Makki katika kitabu chake kiitwacho "Tabar-rukus-Sahabah Bia'thari Rasulillah". Wa pili ni, Al-Ustadh Sheikh Ali Ahmadi katika kitabu chake madhubuti kiitwacho "At-Tabar-ruk". Yeye amefafanua kwa undani habari zote zilizokuja kuhusu Tabar-ruk; na kitabu hiki kinahesabiwa kuwa bora cha zama hizi. Basi watasemaje Mawahabi juu ya hadithi hizi ambazo ni mutawatiri kimatamko na kimaana? Na ni upi msimamo wao kutokana na ukweli huu ulio wazi?

Basi ni za nini kelele hizi wazipigazo dhidi ya kutabaruku kwenye kaburi la Mtume[s.a.w.w] jambo ambalo Masahaba na Tabiina wamekuwa wakilifanya bila ubaya wowote wala kulipinga au kuliharamisha, wakati hatuoni popote kwamba Mtume au Masahaba wake waliharamisha jambo hili. Na ni kwa nini Mawahabi hawawaachi Waislamu walibusu kaburi la Mtume[s.a.w.w] na wapate baraka zake na waonyeshe hisiya zao na mapenzi yao kwa Mtume[s.a.w.w] ? Je, Mawahabi hawajuwi kuwa, kukataza kutabaruku kwenye kaburi la Mtume na athari zake ilikuwa tabia na kazi ya Bani Ummayya hasa Mar-wani aliyelaaniwa na Mtume[s.a.w.w] ? Hebu soma mapokezi aliyoyapokea Al-Hakim ndani ya Mustad-rak yake kutoka kwa Dawuud bin Salih amesema: "Sika moja Mar-wan alikuja akamkuta mtu ameweka uso wake juu ya kaburi (la Mtume[s.a.w.w] ) akamshika shingoni kisha akamwambia, "Je unafahamu unachokifanya"? Kumbe mtu yule alikuwa Abu Ayyubul-Ansari, akamjibu, "Ndiyo mimi sikulijia jiwe hapa nimemjia Mjumbe wa Mwenyezi Mungu". Nimemsikia mjumbe wa Mwenyezi[s.a.w.w] akisema: "Msiililie dini (msiihuzunikie) kama watawala wake ni watu wanaostahiki lakini ililieni dini watakapoitawalia wasiostahiki". [164] Mar-hum Sheikh Al-Amini amesema:

"Hadithi hii inatufahamisha kwamba kuzuwiya kutawas-sal kwenye makaburi matakatifu ni miongoni mwa Bid'a za Banu Ummayya na upotevu wao tangu zama za Masahaba na hakuna hata sikio moja kabisa lililopata kumsikia Sahaba akipinga tawas-sul hiyo isipokuwa Mar-wan mdhalimu aliyetokana na kizazi cha Umayya". Ni kweli "Ng'ombe huilinda pua yake kwa pembe zake". Ni kweli pia kwamba "Kwa kisingizio cha kumtafuta njiwa, muwindaji hula tende (za shamba la mitende aliloingia). Ukweli ulivyo ni kwamba Banu Ummayya na hasa Mar-wan, wanayo chuki dhidi ya Mtume[s.a.w.w] tangu siku ile Mtume[s.a.w.w] alipokuwa hakubakisha heshima yoyote ya Banu Ummayya, ila aliivunja wala cheo chochote ila alikiharibu na wala nguzo yao yoyote isipokuwa aliivunja na hayo yametokea kutokana na maneno makali ya Mtume[s.a.w.w] kuhusu Bani Ummayya ile siku ya Badri alipowapiga. Mtume[s.a.w.w] hasemi lolote kwa matamanio ya nafsi yake ila ni wahyi aliyopewa (aliyemfundisha Bwana Mtume ndiye mwenye nguvu zote) kwani imepokewa hadithi sahihi kuwa Mtume[s.a.w.w] amesema, "Itakapofika idadi ya Banu Ummayya watu arobaini watawafanya waja wa Mwenyezi Mungu kuwa ni watumwa, na mali ya Mwenyezi Mungu wataipora na kuifanya knwa ni mali yao na watakitumia vibaya kitabu cha Mwenyezi Mungu". [165]

Umeona jibu la Abu Ayyubul-Ansari kwa Mar-wan pale alipomuuliza unafanya nini? Akawa amejibu, sikujia jiwe bali nimemjia mjumbe wa Mwenyezi Mungu. Hapa tunamuona Abu Ayyubul-Ansari anaeleza kwamba: "Makusudio ya kutawas-sal na kutabaruku ni kwa Mtume[s.a.w.w] ambaye tunaitakidi kuwa hapana tofauti baina ya kuwa yu hai au amekufa katika suala hili, lakini udongo na jiwe havina umuhimu wowote, isipokuwa udongo na jiwe vilivyopo kwenye kaburi la Mtume[s.a.w.w] vimepata heshima na utukufu kwa sababu ya Mtume[s.a.w.w] . Ewe msomaji mpendwa, Bukhari ambaye kitabu chake kinazingatiwa na Masunni kuwa ndiyo kitabu sahihi mno kuliko vingine, yeye ameweka mlango aliouita "Babu Ma-dhukira Min Dir-in-nabi wa asahu wa Saifahu wa qadahahu wa khatamahu wa mas-ta-amalal-khulafan baadahu. Yaani mlango unaozungumzia habari za deraya ya Mtume, panga lake na fimbo yake, kikombe chake, pete yake na vitu walivyovitumia makhalifa waliokuja baada yake katika vitu ambavyo havikugawanywa na nywele zake, na viatu vyake na vyombo vyake ambavyo Masahaba wa Mtume na wengineo walikuwa wakitabaruku kwa vitu hivyo baada ya kufa Mtume[s.a.w.w] . [166]

Kama Mawahabi watazifuatilia hadithi hizi nyingi zaidi ya mia hawatakuwa na njia isipokuwa kukubali ukweli na kukiri iwapo tu watakuwa miongoni mwa wale wanaosikiliza maneno na kufuata yaliyo bora, vinginevyo: "Siku ya Hukumu imewekewa wakati maalum".

TAUHIDI KATIKA IBADA

Msingi wa wito wa Manabii[a.s] siku zote umekuwa ni kulingania kumuabudu Mwenyezi Mungu peke yake na siyo kumuabudu mwingine peke yake, au kumshirikisha na Mwenyezi Mungu. Na msingi wa hukmu za mbinguni tangu mwanzo wa kutumwa ujumbe wa Manabii ilikuwa ni kumpwekesha Mwenyezi Mungu na kukata mizizi ya shirki. Ukweli halisi ulivyo ni kwamba, lengo la kutumwa kwa Manabii ni kulingania (watu) kwenye ibada ya Mwenyezi Mungu peke yake, na kupiga vita ushirikina wa aina zote na khususan kupinga shirki katika ibada. Qur'an Tukufu inaashiria ukweli huu wazi wazi na inasema:

وَلَقَدْ بَعَثْنَا فِي كُلِّ أُمَّةٍ رَّسُولًا أَنِ اعْبُدُوا اللَّـهَ وَاجْتَنِبُوا الطَّاغُوتَ ﴿٣٦﴾

"Na bila shaka tulimpeleka Mjumbe kwa kila umma (akawambie umma wake) muabuduni Mwenyezi Mungu na muyaepuke masanamu. (Qur'an, 16:36)

وَمَا أَرْسَلْنَا مِن قَبْلِكَ مِن رَّسُولٍ إِلَّا نُوحِي إِلَيْهِ أَنَّهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا أَنَا فَاعْبُدُونِ ﴿٢٥﴾

Na hatukumtuma kabla yako Mjumbe yeyote ila tulimfunulia ya kwamba hakuna apasiwaye kuabudiwa ila mimi, basi niabuduni." (Qur'an, 21:25) Qur'an imeizingatia ibada ya Mwenyezi Mungu kuwa ni jambo linalokusanya na kushirikisha sheria zote za mbinguni na inasema:

قُلْ يَا أَهْلَ الْكِتَابِ تَعَالَوْا إِلَىٰ كَلِمَةٍ سَوَاءٍ بَيْنَنَا وَبَيْنَكُمْ أَلَّا نَعْبُدَ إِلَّا اللَّـهَ وَلَا نُشْرِكَ بِهِ شَيْئًا ﴿٦٤﴾

"Waambie, Enyi mliopewa Kitabu cha Mwenyezi Mungu njooni katika neno lililo sawa baina yetu na baina yenu, ya kwamba tusimuabudu yeyote ila Mwenyezi Mungu na wala tusimshirikishe na chochote." (Qur 'an, 3:64)

Tauhidi katika ibada ni msingi imara kwa Waislamu wote, na hapana yeyote aipingaye Tauhidi au kuwa na tofauti ndani yake miongoni mwa vikundi vyote vya Kiislamu, ijapokuwa Mutazilah mtazamo wao juu ya Tauhid ya matendo ya Mwenyezi Mungu unatofauti, na vile vile Ashaira nao wanayo tofauti juu ya Tauhid katika sifa za Mwenyezi Mungu, lakini madhehebu zote za Kiislamu zinaafikiana kuhusu Tauhid ndani ya ibada na hakuna nafasi ya kupinga hilo. Kama kutakuwa na khitilafu, basi ikhtilafu hiyo haiko katika msingi wa Tauhidi ya ibada bali iko katika Misdaaq za Tauhidi ya Ibada. Hii inamaanisha kwamba, baadhi ya Waislamu wanaona kuwa baadhi ya matendo ni ibada na Waislamu wengine wanaona kuwa (matendo hayo) ni Takrima na Taadhima tu na siyo ibada. Na kwa mujibu wa Istilahi ya Elimu ya "Mantik" Tofauti kama hii iko ndani ya 'As-Sughraa" ambayo ni Je, kitendo hiki ni ibada au hapana? Wakati ambapo hakuna tofauti katika 'Al-Kubraa" ambayo ni je, inafaa kumuabudu asiyekuwa Mwenyezi Mungu au hapana? Na hii wameafikiana (Waislamu wote) kwamba haijuzu kumuabudu asiyekuwa Mwenyezi Mungu.

Kwa maneno mengine (Tunaweza kusema) tofauti iliyopo inatokana na Mawahabi kuyazingatia matendo fulani kuwa ni ibada wakati ambapo wasiokuwa wao miongoni mwa Waislamu ulimwenguni kote hawayazingatii kamwe matendo hayo kuwa ni ibada. Hapana budi tuifafanue maana ya "Ibada" kwa mujibu wa lugha na vile vile kwa mjibu wa Qur'an, na hapo ndipo yatakapofahamika matawi ambayo ndani yake imekuja tofauti kuyahusu mwenyewe kwa dhati yake, na ndipo utakapotudhihirikia uhakika na ukweli wa ibada.

TAARIFU KAMILI YA MAANA YA IBADA

Bila shaka maana na Maf-humu ya Ibada iko wazi katika lugha ya Kiarabu, na lau tutakwa hatuwezi kuiarifisha "Ibada" kwa Taarifu ya kimantik kwa kutumia neon moja, basi ni kama mbingu na ardhi ambazo zina maana mbili zilizowazi, wakati ambapo wengi katika sisi hawawezi kutoa taarifu kamili kwa kutumia neon moja lakini hali hii haizuwii kujengeka maana ya ardhi na mbingu katika akili zetu tunapoyasikia matamko hayo. Bila shaka basi, maana ya Ibada ni kama maana ya ardhi na mbingu ambayo inafahamika kwetu sote, pamoja na kutokuweza kuziarifisha mbingu na ardhi kwa taarifu ya kimantiki: Kwa hiyo basi "Ibada" na "Kutukuza" na "Kuheshimu" na "Kukirimu" ni matamko mbali mbali yenye matawi yanayofahamika, na kuyachambua ni jambo rahisi tena jepesi.

Kwa hakika mtu ambaye anampenda yeyote yule kwa mapenzi ya kweli kabisa, utamuona akibusu kutaza nyumba ya mpenzi wake na kunusa mavazi yake na kuyakumbatia kifuani, na atapokufa (mpenzi wake huyu) atalibusu kaburi lake na udongo wa kaburi hilo.... Pamoja na matendo yote haya, hapana yeyote atakayeona kuwa matendo yake huyu mwenye kupenda ni ibada amfanyiayo yule mpenzi wake. Hali hii ni kama ile ya watu kukimbilia kwena kuona miili ya viongozi iliyomo ndani ya majeneza, au kuona kumbukumbu zao na majumba walioyokuwa wakiishi na kusimama dakika chache kuonyesha huzuni kwa ajili ya rohozao yote haya hayazingatiwi kuwa ni ibada katika Taifa lolote miongoni mwa mataifa ulimwenguni, japokuwa mapenzi yao na unyenyekevu wao kwa wato hao uko katika kiwango cha unyenyekevu wa waumini kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu. Hivyo basi, watu wenye maarifa na wachambuzi wa mambo ndiyo ambao wanaweza kupambanua baina ya kuheshimu na ibada. Ewe msomaji mtukufu iwapo tutataka kutoa taarifu ya ibada kimantik, basi ibada itakuwa na taarifu za aina tatu na zote hizi zitalenga maana moja. Ama Mawahabi wao wamechagua Taarifu mbili nyingine na wakazitegemea, lakini zinaupungufu hazikukamilika. Katika maelezo yafuatayo tunazileta hizo Taarifu zao ili tuzijadili.

TAARIFU MBILI PUNGUFU KUHUSU IBADA

Ibada ni kunyenyekea na kudhalilika. Ndani ya vitabu vya lugha Taarifu ya ibada imekuja kwa maana ya kunyenyekea na kudhalilika. Na maana hii imekuja katika Qur'an tukufu lakini Taarifu hii ya Ibada haitoi maana ya ibada kwa undani, na hiyo ni kwa sababu zifuatazo: Ikiwa ibada inakubaliana katika maana na kuwa ni kunyenyekea na kudhalilika, basi haitawezekana kwa mtu yeyote kumzingatia kuwa anampwekesha Mwenyezi Mungu, kwani mtu kwa maumbile yake humnyenyekea Mwalimu wake na mtoto naye huwanyenyekea wazazi wake wawili na kila mpenzi kwa ampendaye. Bila shaka Qur'an Takufu inamuamuru mtu adhalilike kwa wazazi wawili inasema:

وَاخْفِضْ لَهُمَا جَنَاحَ الذُّلِّ مِنَ الرَّحْمَةِ وَقُل رَّبِّ ارْحَمْهُمَا كَمَا رَبَّيَانِي صَغِيرًا ﴿٢٤﴾

"Na wainamishie Bawa Ia udhalili kwa kuwaonea huruma na useme, Mola wangu wahurumie (wazazi) wangu kama walivyonihurumia mimi nilipokuwa mdogo". (Qur'an, 17:24)

Basi iwapo unyenyekevu na udhalili maana yake ni kumfanyia ibada uliyemdhalilikia, basi italazimu kumhukumu ukafiri yeyote anayelea wazazi wake wawili na kinyume chake itakuwa ni lazima kumhukumu kuwa ni mtu wa Tauhidi yule anayewatelekeza wazazi wake na kutowafanyia wema. B: Ibada ni ukomo wa kunyenyekea. Baadhi ya wafasiri walijaribu kuitengeneza na kuirekesbisha Taarifu ya ibada ya kilugha pale walipogundua kuwa inaupungufu wakasema:

"Ibada ni ukomo wa kunyenyekea kwa yule ambaye utukufu wake na ukamilifu wake unafahamika." Taarifu hii inashirikiana na ile ya kwanza katika upungufu na utata. Mwenyezi Mungu anawaamuru Malaika wamsujudie Adam anasema:

وَإِذْ قُلْنَا لِلْمَلَائِكَةِ اسْجُدُوا لِآدَمَ فَسَجَدُوا إِلَّا إِبْلِيسَ أَبَىٰ وَاسْتَكْبَرَ وَكَانَ مِنَ الْكَافِرِينَ ﴿٣٤﴾

"Na kumbuka tulipowaambia Malaika, msujudieni Adam, wakasujudu wote isipokuwa Iblisi". Qur'an, 2:34

Bila shaka kusujudu ndiyo ukomo wa kadhalilika na kunyenyekea kwa yule unayemsujudia, basi ikiwa maana ya ibada ni ukomo wa kunyenyekea italazimu kuwakufurisha Malaika waliotekeleza amri ya Mwenyezi Mungu, na Iblisi kwa kupinga kwake amri ya Mwenyezi Mungu atakuwa ndiyo mwenye imani. Hakika ndugu wa Nabii Yusuf na wazazi wake Nabii Yusuf wote walimsujudia Yusuf kama asemavyo Mwenyezi Mungu Mtukufu:

وَرَفَعَ أَبَوَيْهِ عَلَى الْعَرْشِ وَخَرُّوا لَهُ سُجَّدًا وَقَالَ يَا أَبَتِ هَـٰذَا تَأْوِيلُ رُؤْيَايَ مِن قَبْلُ قَدْ جَعَلَهَا رَبِّي حَقًّا ﴿١٠٠﴾

"Na waliporomoka wote kumsujudia, (Naye Yusuf) akasema: Ewe Baba yangu hii ndiyo Tafsiri ya ndoto yangu ya zamani bila shaka Mwenyezi Mungu ameithibitisha". Qur'an, 12:100

Ndoto aliyoiashiria Nabii Yusuf katika Aya hii, hi ile iliyoko katika kauli ya Mwenyezi Mungu aliposema:

إِذْ قَالَ يُوسُفُ لِأَبِيهِ يَا أَبَتِ إِنِّي رَأَيْتُ أَحَدَ عَشَرَ كَوْكَبًا وَالشَّمْسَ وَالْقَمَرَ رَأَيْتُهُمْ لِي سَاجِدِينَ ﴿٤﴾

"(Kumbuka) Yusuf aliopomwambia Baba yake, Ewe baba yangu hakika nimeona (ndotoni) nyota kumi na moja na jua na mwezi vinanisujudia" (Qur'an, 12:4)

Ni hakika (isiyopingika) kwamba Waislamu wote kwa kufuata mwendo wa Mtume[s.a.w.w] huwa wanalibusu "Hajarul-As-wad". Jiwe jensi lililoko kwenye kona ya Kaaba Tukufu na pia hutaka baraka kwenye jiwe hilo. Kitendo kile kile hufanywa na waabuduo sanamu kwenye masanamu yao jambo ambalo moja kwa moja ni shirki, lakini tendo la Waislamu kwenye Hajarul-As-wad ni tendo la Tauhidi bila shaka yoyote. Kwa hiyo, maana ya ibada siyo ukomo wa kunyenyekea na kudhalilika ingawaje (kunyenyekea na kudhalilika) hakika ni miongoni mwa nguzo za Ibada lakini siyo kwamba hizo ndiyo nguzo pekee za ibada. Hivyo basi, hapana budi pasemwe kuwa, Ibada maana yake ni kunyenyekea na kudhalilika kunakoambatanishwa na itikadi maalum, kitu ambacho kitaifanya ibada iwe imeundika katika misingi miwili.

1. Kunyenyekea na kudhalilika.

2. Itikadi maalum.

Na hii itikadi maalum ndiyo ambayo inaweka msimamo wa kufafanua Qadhiya ya ibada, kwani kunyenyekea japo si sana, ikiwa kutaambatanishwa na itikadi maalum, basi itakuwa ibada. Kwa hakika "Itikadi Maalum" ndiyo inayokivalisha kitendo vazi Ia Ibada, na bila itikadi hiyo maalum ibada haithibitiki japo itadhihirika katika hali ya Ibada.

Na sasa baada ya kuwa tumethibitisha ubatili wa Taarifu mbili ambazo Mawahabi wamezitegemea, na umedhihiri upungufu wake na udhaifu wake, umefika wakati wa kuzungumzia zile Taarifu tatu. Sasa suali ni je, ni nini hiyo "Itikadi maalum" ambayo inaitenganisha ibada na visivyokuwa ibada? Jawabu lake: Kwa hakika ukweli na usahihi, hapa ndipo mahali pa uchambuzi na uhakiki, na jawabu lake litaonekana ndani ya Taarifu tatu zifuatazo:

Taarifu ya Kwanza: Ibada ni kunyenyekea kimatendo au kimatamko, ambako kunatoka ndani ya itikadi ya mtu kwa ajili ya Uluhiyyah (Uungu). Nini maana ya Uluhiyyah nukta hii ni muhimu sana kwa hiyo ni lazima kuieleza.

Jibu: "Uluhiyyah" ni tamko litakanalo na neno "Al-Ilahu" na hilo neno "Al-Ilahu" ndiyo Allah kwa tamko la nakira, (naye ndiyo muumba mtukufu). Na ilivyokuwa neno "Al-llahu" hupata likafasiriwa kwa maana ya mwenye kuabudiwa, basi tafsiri hiyo hiyo ni tafsiri ya kulazimiana, yaani Uluhiyyah unalazimu kuabudiwa siyo kwamba Ilahu maana yake ni mwenye kuabudiwa.

Bila shaka watu wanaoitakidi Ilahu vile vile wanaitakidi kuwepo ulazima wa kumuabudia, sawa sawa ikiwa ni Ilahu wa haki kama alivyo Mwenyezi Mungu au akawa siyo wa haki kama illvyo miungu isiyokuwa Mwenyezi Mungu. Kwa hiyo neno Al-Ilahu hufasiriwa kwa maana ya chenye kuabudiwa kutokana na hali hii tu basi. Dalili iliyowazi kuhusu taarifu hii ni Aya za Qur'an zilizokuja kuzungumzia nyanja hii. Katika mazingatio ndani ya aya hizo inatudhihirikia kwamba "Ibada" na matendo na maneno yanayotokana na Itikadi za Uungu, na kwamba Itikadi hii inapokosekana, basi maana ya Ibada haithibitiki, na ndiyo maana utaiona Qur'an wakati inapoamuru ibada ya Mwenyezi Mungu, basi haraka sana hutoa maelekezo kwamba, hapana mungu asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Kwa mfano isema:

"Enyi watu wangu, muabuduni Mwenyezi Mungu ninyi hamna Mungu ila yeye." Madhumuni ya aya hii yamekuja katika sehemu tisa ndani ya Qur'an au zaidi, nawe msomaji mpendwa unaweza kuzirjea aya hizi katika Surat A'araf aya ya 65, 73 na 58. Pia Surat Huud aya ya 5, 61 na 84, vile vile Surat Anbiyyah aya ya 25, kadhalika Surat Muuminnuna aya ya 23 na 32 na Surat Taha aya ya 14. Ibada zote hizi zinajulisha kwamba, ibada ni kule kunyenyekea na kudhalilika kunakotokana na itikadi ya kuitakidi Uluhiyyah na bila itikadi hii tendo hilo halitaitwa Ibada. Hebu angalia aya zaidi zinazojulisha makusudio hayo. Anasema Mwenyezi Mungu:

إِنَّهُمْ كَانُوا إِذَا قِيلَ لَهُمْ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا اللَّـهُ يَسْتَكْبِرُونَ ﴿٣٥﴾

"Hakika wao walipokuwa wakiambiwa, hapana Mungu (Mwingine) ila Mwenyezi Mungu wao Hupinga." Qur'an, 37:35

Ni kwa nini walikuwa wakipinga? Ni kwa sababu wanaitakidi waungu wasio Mwenyezi Mungu na wanawaabudu. Na anasema Mwenyezi Mungu:

أَمْ لَهُمْ إِلَـٰهٌ غَيْرُ اللَّـهِ سُبْحَانَ اللَّـهِ عَمَّا يُشْرِكُونَ ﴿٤٣﴾

"Au wanaye Mungu mwingine asiye Mwenyezi Mungu, ametakasika Mwenyezi Mungu kutokana na hao washirikina hao wanaowashirikisha." Qur'an, 52:43.

Qur'an inawazingatia watu hawa kuwa ni washirikina kwa kuwa wanaitakidi uungu kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu. Anasema tena Mwenyezi Mungu:

الَّذِينَ يَجْعَلُونَ مَعَ اللَّـهِ إِلَـٰهًا آخَرَ فَسَوْفَ يَعْلَمُونَ ﴿٩٦﴾

"Wale ambao wanafanya pamoja na Mwenyezi Mungu; Mungu Mwingine basi hivi karibuni watajua." Qur'an , 15:96

وَالَّذِينَ لَا يَدْعُونَ مَعَ اللَّـهِ إِلَـٰهًا آخَرَ ﴿٦٨﴾

"Na wale ambao hawamuombi mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu..... (Qur'an, 25:68).

Na miongoni mwa aya zinazojulisha kwamba maombi ya Washirikina yalikuwa yakiambatana na itikadi ya uungu kwa masanamu yao ni hizi zifuatazo:

وَاتَّخَذُوا مِن دُونِ اللَّـهِ آلِهَةً لِّيَكُونُوا لَهُمْ عِزًّا ﴿٨١﴾

"Waliwafanya waungu wengine badala ya Mwenyezi Mungu ili wawe wenye nguvu." Qur'an, 19:81.

"Je, ninyi mnashuhudia kwamba kuna waungu wengine pamoja na Mwenyezi Mungu." Qur'an, 6:19

وَإِذْ قَالَ إِبْرَاهِيمُ لِأَبِيهِ آزَرَ أَتَتَّخِذُ أَصْنَامًا آلِهَةً إِنِّي أَرَاكَ وَقَوْمَكَ فِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ ﴿٧٤﴾

"Na (kumbukeni) Ibrahimu alipomwambia Baba yake Azar. 'Unawafanya Masanamu kuwa ni waungu.'" Qur'an, 6:74

Mazingatio katika aya zinazozungumzia shirki yawatu wanaoabudu sanamu yatatudhihirishia ukweli huu, nao ni kuwa ushirikina wa watu hawa umekuja kwa sababu ya kuitakidi kwao uungu wa masanamu yao waliyokuwa wakiyaabudu, na kwamba masanamu hayo ni miungu wadogo ambao Mungu mkubwa amewapa baadhi ya mambo yanayomstahiki, basi (masanamu hayo) yameumbwa na wakati huo huo yanaabudiwa. Na kwa ajili hii basi walikuwa wakiikataa Tauhidi. Qur'an inasema:

ذَٰلِكُم بِأَنَّهُ إِذَا دُعِيَ اللَّـهُ وَحْدَهُ كَفَرْتُمْ وَإِن يُشْرَكْ بِهِ تُؤْمِنُوا فَالْحُكْمُ لِلَّـهِ الْعَلِيِّ الْكَبِيرِ ﴿١٢﴾

"Hii ni kwa sababu mlikuwa akitajwa Mwenyezi Mungu peke yake mnakanusha, na akishirikishwa mnaamini, basi (leo) hukumu ni yake Mwenyezi Mungu Mtukufu aliye mkuu." Qur'an, 40:12

Na kwa ajili hii mfasiri mkubwa mar-hum Ayatullah Sheikh Muhammad Jawad Al-Balaghi ametoa Taarifu nzuri ya "Ibada" katika tafsiri yake madhubuti iitwayo Aalaur-Rahman anasema: "Ibada: Ni hisia ya unyenyekevu wanayoifanya kwa ajili ya yule wanayemfikiria kuwa ni Mungu wake ili atimize haki yake makususi ya uungu.[167]

Bila shaka marehemu Al-Balaghi ametoa mtazamo wake wa kielimu kutokana na ufahamu wa kimaumbile juu ya neno "Ibada" katika msingi wa tamko, ndipo ilipokuja Taarifu hii inayokubaliana na aya za Qur'an. Taarifu ya Pili ya Ibada: Hakika Ibada ni kunyenyekea mbele ya yule ambaye (Mwenye kunyenyekea) humzingatia kuwa ndiyo Rabbi (Mola). Na tunaweza kuiarifisha ibada kama ifuatavyo; Ibada ni kunyenyekea kimatendo au kimaneno kwa yule anayeitakidiwa kuwa Mola basi kuabudiwa kunalazimiana na kuwa Mola na ikiwa mtu atajiona yeye mwenyewe kuwa ni mja kwa yule anayemuitakidi kuwa ni Mola wake kwa kuumba; sawa sawa Mola huyo akiwa ni kwa hakika au hapana, na akamnyenyekea pamoja na itikadi hii basi atakuwa amemuabudia. Na katika Qur'an Tukufu kuna aya zinazofahamisha kuwa ibada ni miongoni mwa mambo ya umola yaani "Ar-rububiyyah". Hebu ziangalie baadhi ya hizo aya:

وَقَالَ الْمَسِيحُ يَا بَنِي إِسْرَائِيلَ اعْبُدُوا اللَّـهَ رَبِّي وَرَبَّكُمْ ﴿٧٢﴾

"Naye Masihi alisema, Enyi wana wa Israeli, mwabuduni Mwenyezi Mungu, Mola wangu na Mola wenu". Qur'an, 5:72

إِنَّ اللَّـهَ رَبِّي وَرَبُّكُمْ فَاعْبُدُوهُ هَـٰذَا صِرَاطٌ مُّسْتَقِيمٌ ﴿٥١﴾

"Bila shaka Mwenyezi Mungu ni Mola wangu na ni Mola wenu. Basi muabuduni hii ndiyo njia iliyonyooka" Qur'an 3.51

Na aya nyinginezo zaidi ya hizi. Na kuna aya nyingine zinazoizingatia Ibada kuwa ni miongoni mwa mambo ya muumba kama ilivyo katika kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu aliposema:

ذَٰلِكُمُ اللَّـهُ رَبُّكُمْ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ خَالِقُ كُلِّ شَيْءٍ فَاعْبُدُوهُ ﴿١٠٢﴾

"Huyo ndiye Mwenyezi Mungu Mola wenu, hakuna anayeabudiwa kwa haki ila yeye muumba wa kila kitu, basi muabuduni." Qur'an 6:102

Ni maana ya neno (Ar-Rabbu)? Neno Rabbu hutumika katika lugha ya Kiarabu kwa yule aliyetegemezewa uangalizi wa kitu fulani na yakaachwa mikononi mwake matokeo au ukomo wa kitu hicho. Basi iwapo neno hili litatumika kwa mtu anayemiliki nyumba na au anayemiliki ngamia au mlezi wa mtoto na mkulima na wengineo, basi hiyo ni kwa sababu wanamiliki kuendesha kitu hicho na kusimamia majukumu yake. Nasi tunapomzingatia Mwenyezi Mungu kuwa ni "Ar- Rabbu" ni kwa sababu mambo yetu na mwisho wetu kama vile mauti, uhai, rizki, afya na uwekaji wa sheria pia msamaha na mambo mengineyo, yote yako mikononi mwake Mwenyezi Mungu Mtukufu. Sasa basi Iau kuna mtu ataitakidi kwamba, moja katika mambo haya au yote, Mwenyezi Mungu amempa mtu fulani (Ayasimamie), basi maana ya itikadi hii ni kwamba kumzingatia huyo mtu kuwa ni "Rabbu" na kumuamini Rabbi huyu na kumnyenyekea itakuwa ni kumuabudia. Kwa maneno mengine tunasema, "Bila shaka ibada inatokana na hisiya za mtu kujiona kuwa yeye ni mja (mtumwa) na hii ndiyo hakika ya ubudiyah, ni ni mtu kuizingatia nafsi yake kuwa amemilikiwa na yuko juu yake aliyemmiliki, kuwepo kwake na kifo chake na uhai na rizki yake na mengineyo. Au kwa uchache akamfanya huyo aliye juu yake kuwa ni mwenye kumiliki uwezo wa kusamehe:

(1) Mwenyezi Mungu Anasema:Nani anayesamehe madhambi isipokuwa ni Mwenyezi Mungu ; 3:135

(2) Mwenyezi Mungu Anasema:Waambie Shafaa ni ya Mwenyezi Mungu ; Az-zumar: 44

(3) Mwenyezi Mungu Anasema:Waliwafanya Makasisi wao na watawa wao kuwa ni Mola badala ya Mwenyezi Mungu, 9:31 Na Shafaa, na kumuwekea Kanuni (za maisha yake) na wajibu mwingineo, basi kwa ajili hiyo atakuwa amemfanya kuwa ni "RABBU" mlezi wake. Kwa hiyo yeyote ambaye atakayeamini na kuitakidi katika nafsi yake (kama tulivyoeleza hapo kabla) na akaifasiri itikadi hiyo kwa maneno na matendo, basi hapana shaka kwamba anamuabudu huyo aliyemzingatia kuwa ni "Rabbu".

TAARIFU YA TATU YA IBADA

Hapa tunaweza kutoa Taarifu hii ya tatu ya ibada inayopatikana kutokana na maumbile na nguvu ya nafsi. Tunasema: "Ibada ni kumnyenyekea yule ambaye tunamzingatia kuwa Mungu na ndiyo asili ya matendo ya kiungu". Hapana shaka kwamba matendo ambayo yanahusiana na ulimwengu, kama vile kusimamia uendeshaji wa ulimwengu na kuhuisha na kufisha na kugawa rizki baina ya viumbe na kusamehe madhambi yote haya yanamuhusu Mwenyezi Mungu Mtukufu. Nawe (msomaji) lau utazizingatia vyema aya za Qur'an zinazozungumzia maelezo tuliyotangulia kuyataja, katika Aya ya 35 Surat Al- Qasa, Aya ya 60 mpaka Aya ya 64 Surat An-Namli Aya ya 5 na ya 6 Sura Az-Zummar. Utaona kwamba Qur'an inasisitiza kwa nguvu sana kuwa matendo haya yanamuhusu Mwenyezi Mungu tu na wala hayamuhusu mwingine asiyekuwa yeye. Hii ni kwa upande mmoja, ama kwa upande wa pili: Sote tunafahamu kwamba ulimwengu wa viumbe ni ulimwengu uliopangwa vyema kabisa, na hakiwezi kutokea kitu isipokuwa sababu ya kutokea kwake itarejea kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Qur'an Tukufu inaonyesha (ukweli) wa jambo hili. Mwenyezi Mungu anasema:

وَهُوَ الَّذِي يُحْيِي وَيُمِيتُ وَلَهُ اخْتِلَافُ اللَّيْلِ وَالنَّهَارِ أَفَلَا تَعْقِلُونَ ﴿٨٠﴾

"Na ni yeye (Mwenyezi Mungu) ndiye anayehuisha na kufisha, na mabadiliko ya usiku na mchana yamo katika milki yake." Qur'an, 23:80.

Katika mahala pengine Mwenyezi Mungu anasema kwamba miongoni mwa Malaika wapo wanaosimamia utoaji wa Roho. Nayo ni kauli yake isemayo:

حَتَّىٰ إِذَا جَاءَ أَحَدَكُمُ الْمَوْتُ تَوَفَّتْهُ رُسُلُنَا وَهُمْ لَا يُفَرِّطُونَ ﴿٦١﴾

"Hata pale mmoja wenu anapofikiwa na mauti wajumbe wetu humfisha." Qur'an, 6:61

Kwa kuijengea hali hii, inawezekana kuzikusanya aya hizi mbili na tukasema kama ifuatavyo: "Bila shaka hizi sababu zinazosababisha pia matendo ya ulimwenguni, kama yatakuwa ni ya kimaumbile ya kawaida au kimaana kama vile Malaika, basi iwe iwavyo yanathibitika kwa idhini ya Mwenyezi Mungu Mtukufu naye ndiye mtendaji halisi." Kwa maneno mengine ni kwamba, kitendo cha watendaji hawa wawili (Mwenyezi Mungu na Malaika) ni kitendo kimoja tu na si vitendo viwili lakini mtendaji wa kwanza anafanya kwa uwe wake na yule wa pili anamfuatia yule wa kwanza (kutekeleza maamrisho yake).

Maana hii ni miongoni mwa maarifa ya juu katika Qur'an ambayo hufahamika kwa kuzirejea aya za Qur'an zinazozungumzia matendo ya Mwenyezi Mungu Mtukufu. Sasa basi ikiwa mtu ataitakidi kwamba Mwenyezi Mungu amewapa baadhi ya viumbe wake kama vile, Malaika na Mawalii matendo yake ya kuruzuku, na kuhuisha na yasiyokuwa hayo, na akaammi pia kuwa viumbe hao ndiyo wanaoendesha mambo ya ulimwengu na kuyasimamia mambo yake na akaona kuwa Mwenyezi Mungu hahusiki tena kwenye matendo hayo kiasi kwamba itikadi hiyo ikampelekea kuwanyenyekea viumbe hawa, basi hapana shaka yoyote kwamba unyenyekevu wake huu ni ibada na tendo hili ni kumshirikisha Mwenyezi Mungu Mtukufu. Kwa maneno mengine tunasema: "Lau mtu ataitakidi kwamba Mwenyezi Mungu ameukabidhi ustahiki wa kutekeleza matendo kwa Malaika na Mawalii, na Mwenyezi Mungu akawa amebaki hana ustahiki wote wote (katika matendo hayo) na hao Malaika na Mawalii wanayafanya matendo hayo bila kumtegemea Mwenyezi Mungu na bila idhini yake, basi mtu huyu aliyeitakidi itikadi hii, hakika amemfanyia Mwenyezi Mungu mshirika na amemfananisha (Na viumbe vyake). Hapana shaka kwamba itikadi kama hii ndiyo kuishirikisha dhati ya Mwenyezi Mungu na kutawas-sal na kunyenyekea kunakotokana na itikadi hii ni ibada kama ilivyokuja katika Qur'an Tukufu.

Anasema Mwenyezi Mungu:

وَمِنَ النَّاسِ مَن يَتَّخِذُ مِن دُونِ اللَّـهِ أَندَادًا يُحِبُّونَهُمْ كَحُبِّ اللَّـهِ ﴿١٦٥﴾

"Na miongoni mwa watu wako wanaofanya waungu badala ya Mwenyezi Mungu, na wanawapenda kama (anavyostahiki) kupendwa Mwenyezi Mungu". Qur'an, 2:165

Kwa hakika chochote chenye kuwa na kuwepo hakiwezi kuwa mfano wa Mwenyezi Mungu au mshiriki isipokuwa kitakapokuwa na uwezo wa kuuendesha ulimwengu kwa matakwa yake binafsi bila ya matakwa ya Mwenyezi Mungu lakini hakuna yeyote mwenye uweza huo. Bali kila kilichopo ni chenye kunyenyekea mbele ya matakwa ya Mwenyezi Mungu Mtukufu kitake au kisitake basi kwa hiyo hakiwezi kuwa mshirika wa Mwenyezi Mungu bali kitakuwa kitiifu kwake kutenda kama atakavyo yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu. Ukweli halisi in kuwa, washirikina walikuwa wakiitakidi kwamba, masanamu yao waliyokuwa wakiyaabudu yanajitegemea katika kunendesha ulimwengu huu na pia katika mambo ya uungu.

Na katika zama za Jahiliya (kabla kuja Uislamu) kulikuwa na ushirikina wa namna mbali mbali na ushirikina wa daraja ya chini kabisa ilikuwa ni itikadi ya Mayahudi na Wakristo kwamba mapadri na Makasisi wao wanayo madaraka ya uwekaji wa kanuni na sheria kama alivyosema Mwenyezi Mungu:

وَعَلَّمَ آدَمَ الْأَسْمَاءَ كُلَّهَا ثُمَّ عَرَضَهُمْ عَلَى الْمَلَائِكَةِ فَقَالَ أَنبِئُونِي بِأَسْمَاءِ هَـٰؤُلَاءِ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ﴿٣١﴾

"Waliwafanya wanachuoni wao na watawa wao kuwa ni waungu wao kinyume cha Mwenyezi Mungu". Qur 'an, 2:31

Kadhalika washirikina walikuwa wakiitakidi kwamba, ustahiki wa Shafaa na Maghfira (mambo ambayo yanamstahiki Mwenyezi Mungu tu) vimekabidhiwa kwa Masanamu yao wanayoyaabudu, na masanamu hayo yanafanya mambo hayo yenyewe kikamilifu kwa kujitegemea katika ustahiki huo. Na kwa ajili hii utaona aya nyingi za Qur'an zinazozungumzia Shafaa zinasisitiza kwamba Shafaa haithibitiki ila kwa idhini ya Mwenyezi Mungu asemavyo ndani ya Qur'an:

مَن ذَا الَّذِي يَشْفَعُ عِندَهُ إِلَّا بِإِذْنِهِ ﴿٢٥٥﴾

"Na ni nani huyo awezaye kushufaiya (kuombea) mbele ya Mwenyezi Mungu isipokuwa kwa idhini yake." Qur 'an, 2:255

Na lau washirikina wangekuwa wanaitakidi kwamba, masanamu yao waliyokuwa wakiyaabudu yanauwezo wa kushufaiya kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, basi usingeona Qur'an inakanusha moja kwa moja Shafaa bila ya idhini ya Mwenyezi Mungu. Baadhi ya wanafalsafa wa Kiyunani walikuwa wamejenga ndani ya fikra zao Miungu wengi kwa kila jambo miongoni mwa mambo ya ulimwenguni. (Kwa mfano) mvua ina Mungu wake, mimea ina mungu wake, mtu ana Mungu wake na mambo mengine (kila moja lina mungu wake). Na walikuwa wakidai kwamba utendaji wa kuendesha mambo ya ulimwengu ambao unamuhusu Mwenyezi Mungu peke yake, umekabidhiwa kwa miungu hawa. Na katika zama za Jahiliya, baadhi ya Waarabu walikuwa wakiabudu Malaika na nyota zitembeazo na zile zisizotembea hali ya kuwa wakidhani kwamba usimamizi wa mambo ya ulimwengu na watu umekabidhiwa kwa vitu hivyo, navyo ndivyo vinavyotenda kikamilifu kwa kujitegemea na hiyari kamili, na kuwa Mwenyezi Mungu ameuzuliwa na hana uwezo wowote juu ya mambo haya kabisa (ametakasika Mwenyezi Mungu na fikra hizi sana sana).[168]

Na kwa hiyo basi kila aina ya unyenyekevu utaofanywa kwa Malaika na nyota utazingatiwa kuwa ni ibada kwa kuwa unatokana na itikadi hii yenye makosa. Kuna baadhi ya Waarabu wengine wa zama za Jahiliyyah, hawakuyaitakidi masanamu yaliyochongwa kwa miti na madini kuwa ni Miungu na kwamba ndiyo yaliyowaumba wala kusimamia mambo ya ulimwengu na watu, bali wao walikuwa wakiyaamini kuwa yanao uwezo wa kuwaombea na walikuwa wakisema: "Masanamu haya ni waombezi wetu mbele ya Mwenyezi Mungu".[169] Na kwa msingi wa mtazamo huu batili, walikuwa wakiyaabudu Masanamu haya kwa lengo la kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu na walikuwa wakisema wamasema:

مَا نَعْبُدُهُمْ إِلَّا لِيُقَرِّبُونَا إِلَى اللَّـهِ زُلْفَىٰ ﴿٣﴾

"Sisi hatuyaabudu (Masanamu) isipokuwa kwa ajili ya kutukurubisha kwa Mwenyezi Mungu." Qur 'an, 39:3

Kwa kifupi tunasema: "Bila shaka tendo lolote litokanalo na itikadi hii na likajulisha kufuata na kunyenyekea basi ni ibada, na kinyume chake ni kuwa tendo lolote ambalo halikutegemezewa itikadi kama hii haliwezi kuzingatiwa kuwa ni ibada wala shirki."

Lau mtu atanyenyekea mbele ya mtu na akamuheshimu na kumtukuza bila ya kuamini itikadi kama hii, basi tendo hili halitachukuliwa kuwa ni shirki wala ibada hata kama tendo hilo litakakadiriwa kuwa ni haramu.

Kwa mfano: Haitazingatiwa kuwa ni ibada sijda ya mpenzi kwa mpenzi wake, wala mwenye kuamriwa kumsujudia aliyemuamuru na mke kumsujudia mume pamoja na kwamba Sijda kumsujudia asiye Mwenyezi Mungu ni haramu kisheria, kwani Sijda ni Makhsusi kwa Mwenyezi Mungu peke yake wala hairuhisiwi kwa yeyote yule kafanyiwa japo itakuwa ni kwa sura ya dhahiri isiyokuwa na itikaadi isipokuwa kama Mwenyezi Mungu ataamuru kufanywa kwa sijida hiyo (kwa asiye Mwenyezi Mungu).