MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU 13%

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU Mwandishi:
Kundi: Vitabu mbali mbali

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU
  • Anza
  • Iliyopita
  • 22 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 47910 / Pakua: 4688
Kiwango Kiwango Kiwango
MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

Mwandishi:
Swahili

1

2

3

4

5

6

7

8

12

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

KUAMINI QADAR YA ALLA

Kwa mujibu wa Hadith iliyosimuliwa na Umar (r.a), kuamini Qadar ni nguzo ya sita ya Imani ya Kiislamu. Katika hadithi hii ndefu, Umar (r.a) anasimulia: Siku moja tulipokuwa tumeketi pamoja na Mtume(s.a.w.w) alitutokea mtu mmoja ambaye nguo zake zilikuwa nyeupe kama theluji na nywele zake nyeusi sana, hakuwa na dalili zozote za msafiri, ingawa alikuwa mgeni kwetu sote. Halafu alikaa mbele ya Mtume hali magoti yake yakikabiliana na yale ya Mtume na akaweka mikono yake katika mapaja ya Mtume halafu akasema:

"Ewe Muhammad nifahamishe juu ya Uislamu" na Mtume akasema: "Ni kushuhudia kuwa hakuna apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allah na kwamba Muhammad ni Mtume wa Allah, kusimamisha Swala, Kutoa Zakat, Kufunga mwezi wa Ramadhani na Kuhiji Makkah kwa mwenye kuweza" Halafu yule mgeni akasema:

"Umesema kweli.Tulistajaabu kwa nini aliuliza halafu akasadikisha. Halafu akasema: "Nifahamishe juu ya Imani". Mtume akasema: "Ni Kumuamini Allah, Malaika Wake, Vitabu vyake, Mitume Wake, Siku ya Mwisho na Qadar, Kheri yake na Shari yake". Kisha akasema: "Nifahamishe juu ya Ihsan". Na Mtume akamjibu:"Ni kumuabudu Allah kama kwamba unamuona, kwani ingawa humuoni, Yeye anakuona". Halafu akasema: "Nifahamishe juu ya Siku ya Kiyama". Mtume akamjibu kwamba hajui mwenye kuulizwa zaidi ya mwenye kuuliza Akasema:

"Nifahamishe dalili zake" Mtume.Akasema: "Ni wakati ambao mjakazi atamzaa bibi yake, na utakapoona wachungaji maskini, wenye nguo zilizoraruka na wasio na viatu wanashindana kujenga maghorofa".Yule mgeni alipoondoka, Mtume alikaa kimya kwa muda halafu akasema: "Ee Umar, unamfahamu muulizaji?" Sote tukajibu kuwa Allah na Mtume wake ndio wajuao. Mtume akasema: "Huyo ni Jibril, amekuja kuwafundisheni dini yenu". (Muslim)

Maana ya Qadar Neno "Al-Qadar" limetumika katika Qur-an kwa maana ya "kiasi", kipimo", kukadiria kipimo maalumu". Hebu turejee aya zifuatazo ambamo neno Qadar limetumiwa:

﴿إِنَّا كُلَّ شَيْءٍ خَلَقْنَاهُ بِقَدَرٍ ﴾

"Kwa hakika Sisi tumekiumba kila kitu kwa kiasi (chake makhsusi)" (54:49)"...

﴿وَخَلَقَ كُلَّ شَيْءٍ فَقَدَّرَهُ تَقْدِيرًا﴾

Na (Mwenyezi Mungu) Ameumba kila kitu na Akakikadiria kipimo (chake)" (25:2)

﴿وَالْقَمَرَ قَدَّرْنَاهُ مَنَازِلَ حَتَّىٰ عَادَ كَالْعُرْجُونِ الْقَدِيمِ﴾

"Na mwezi tumeupimia vituo, mpaka unakuwa (mwembamba) kama chaparare la mtende kuu kuu". (36:39).

Tukizingatia aya hizi, tunajifunza kuwa Allah(s.w) ameumba ulimwengu huu na vyote vilivyomo kwa mujibu wa kanuni zinazotawala mzunguko wa jua, mwezi, nyota, dunia na sayari nyingine. Kutokana na mizunguko ya jua, mwezi na dunia tunapata urefu wa mchana na usiku, hesabu ya miezi, majira, n.k. Kuna kanuni zinazotawala ukuaji wa mimea. Kutokana na kanuni hizo, mimea huzaa matunda yenye rangi na ladha mbali mbali.Kwa ujumla Allah (s.w) ameumba kila kitu kwa lengo, maalumu na ameweka kanuni madhubuti zinazokiwezesha kila kiumbe kifikie lengo lake kama anavyotukumbusha katika Qur-an:

﴿سَبِّحِ اسْمَ رَبِّكَ الْأَعْلَى ﴿١﴾ الَّذِي خَلَقَ فَسَوَّىٰ ﴿٢﴾ وَالَّذِي قَدَّرَ فَهَدَىٰ﴾

"Litukuze jina la Mola wako aliye Mtukufu.Aliyeumba (kila kitu) akakitengeneza.Na akakikadiria (kila kimoja jambo lake) na akakiongoza (kufanya jambo hilo). (87:1-3)

Pia matukio yote yako katika Qadar ya Allah (s.w).Hapana tukio lolote linalotokea liwe la kheri au la shari kwa mwanaadamu, ila limo katika Qadar ya Allah (s.w) kama tunavyojifunza katika Qur-an:

﴿ وَاللَّـهُ خَلَقَكُم مِّن تُرَابٍ ثُمَّ مِن نُّطْفَةٍ ثُمَّ جَعَلَكُمْ أَزْوَاجًا وَمَا تَحْمِلُ مِنْ أُنثَىٰ وَلَا تَضَعُ إِلَّا بِعِلْمِهِ وَمَا يُعَمَّرُ مِن مُّعَمَّرٍ وَلَا يُنقَصُ مِنْ عُمُرِهِ إِلَّا فِي كِتَابٍ إِنَّ ذَٰلِكَ عَلَى اللَّـهِ يَسِيرٌ﴾

Na Mwenyezi Mungu amekuumbeni kwa udongo, kisha kwa tone la manii, kisha akakufanyeni wanaume na wanawake. Na mwanamke yoyote hachukui mimba wala hazai ila kwa ilimu Yake (Mwenyezi Mungu). Na mwenye kupewa umri hapewi umri (zaidi) wala hapunguziwi umri wake ila yamo hayo katika Kitabu (cha Mwenyezi Mungu). Bila shaka (kuyapitisha) haya ni sahali kwa Mwenyezi Mungu. (35:11)

﴿مَا أَصَابَ مِن مُّصِيبَةٍ فِي الْأَرْضِ وَلَا فِي أَنفُسِكُمْ إِلَّا فِي كِتَابٍ مِّن قَبْلِ أَن نَّبْرَأَهَا إِنَّ ذَٰلِكَ عَلَى اللَّـهِ يَسِيرٌ﴾

Hautokei msiba katika ardhi wala katika nafsi zenu ila umekwishaandikwa katika Kitabu (cha Mwenyezi Mungu) kabla Hatujauumba. Kwa yakini hilo ni sahali kwa Mwenyezi Mungu. (57:22)

Mtazamo wa Uislamu juu ya Qadar Kwa mujibu wa mafundisho ya Uislamu, ni makosa makubwa kudhani kuwa mtu anaweza kufanya jambo lolote lile kinyume na Qadar ya Allah (s.w). Na ni makosa makubwa pia kudhani kuwa mtu anaweza kumlaumu Allah (s.w) kwa maovu anayotenda. Utatanishi wote wanaoupata watu juu ya suala hili unaondoka kwa sababu Uislamu umegawanya maisha ya binaadamu katika maeneo makuu mawili:

(a) Eneo ambalo binaadamu hana hiari, na

(b) Eneo ambalo binaadamu anao uchaguzi. Binaadamu hana hiari kabisa katika baadhi ya mambo katika maisha yake. Mambo hayo humtokea atake asitake. Hana uwezo wa kuyachagua wala kuyabadilisha.Kwa mfano mtu hana hiari ya kuwachagua wazazi wake.Hawezi kuchagua tarehe ya kuzaliwa wala nchi atakayozaliwa.Hawezi kuchagua rangi ya ngozi yake wala aina ya nywele, rangi ya macho, kimo au vipawa vingine.

Damu itazunguka mwilini bila kuipangia yeye safari hiyo, moyo wake utadunda bila yeye kuuamrisha.Mwili mzima wa binaadamu unafanya kazi bila yeye kuupigia kura. Kwa mujibu wa mafundisho ya Uislamu binaadamu hataulizwa au kuhisabiwa juu ya jambo lolote ambalo yeye hakuwa na hiari nalo.Yaani hakuna mtu atakayeulizwa kwanini wewe ulizaliwa siku ya Jumanne badala ya Jumatano? Au kwa nini ulifariki mwezi wa Shaabani badala ya kusubiri hadi mwezi wa Ramadhani? Au kwanini ulikuwa mrefu namna hii badala ya kuwa na kimo cha wastani? Kwa hakika ni rehema kubwa ya Allah (s.w) kwamba mambo hayo hatuyadhibiti sisi wenyewe.

Hebu fikiria kama moyo ungelikuwa unapiga kwa amri yetu, tungeliwazaje kulihakikisha hilo tunapolala usingizini au tunaposahau? Matatizo yangekuwa hayo hayo lau myeyusho wa chakula (digestion) ungelikuwa uko chini ya udhibiti wetu, n.k.

Kuna eneo ambalo binaadamu anao uhuru wa kuchagua hili au lile. Mtu anaweza kwa mfano kuchukua bastola na kumuulia mtu mwingine na kupora mali yake au anaweza kuchukua chakula na kumpa mwenye njaa. Mtu anaweza kutumia pesa zake kwa kuwanunulia nguo wazazi wake, au anaweza kwenda nazo kilabuni kunywea pombe. Mtu anaweza kumuamini Allah (s.w) na kumtii na anaweza kukataa kumuamini na akaamua kumuasi. Mtu anaweza kusema kweli au akiamua anaweza kusema uwongo.Anaweza kumtendea mwenziwe haki au anaweza kumdhulumu.Katika eneo hili binaadamu ni Mas-uli, yaani atahisabiwa na Allah (s.w) kwa yote aliyoyafanya kwani ni mambo ambayo binaadamu amepewa uhuru wa kuchagua kutenda hili au lile.

﴿إِنَّا هَدَيْنَاهُ السَّبِيلَ إِمَّا شَاكِرًا وَإِمَّا كَفُورًا﴾

"Hakika Sisi Tumemuongoa, (tumembainishia) njia. Basi atakuwa mwenye shukurani au mwenye kukufuru" (76:3)

﴿وَقُلِ الْحَقُّ مِن رَّبِّكُمْ فَمَن شَاءَ فَلْيُؤْمِن وَمَن شَاءَ فَلْيَكْفُرْ﴾

"Na sema: Huu ni ukweli uliotoka kwa Mola wenu, basi anayetaka naamini na anayetaka na akufuru." (18:29)

﴿ أَلَمْ نَجْعَل لَّهُ عَيْنَيْنِ ﴿٨﴾ وَلِسَانًا وَشَفَتَيْنِ ﴿٩﴾ وَهَدَيْنَاهُ النَّجْدَيْنِ﴾

"Je, hatukumpa(binaadamu) macho mawili? Na ulimi na midomo miwili?Na tukambainishia zote njia mbili?" (90:8-10)

Hivyo ni dhahiri kuwa katika eneo hili binaadamu hajapangiwa na Allah (s.w) lipi aje kulifanya atake asitake. Allah (s.w) amempa mwongozo wa kuufuata lakini kampa na hiari ya kuufuata au kuuacha. Na ndio maana ataulizwa.Ukweli kuwa watu wanaweza kumuasi Allah (s.w) ni ushahidi tosha kuwa watu wanao uhuru wa kuchagua kutenda mema au maovu, kwani lau si hivyo watu wote wangekuwa kama Malaika.

Hata hivyo, kwanza, isidhaniwe kuwa maadamu watu wanao uhuru wa kuchagua kutenda lolote basi Allah (s.w) hajui mpaka jambo hilo litokee.Yeye anayajua yote atakayofanya mja hadi hatima yake ya mwisho siku ya kiyama hata kabla mtu huyo hajazaliwa.

﴿وَمَا مِن دَابَّةٍ فِي الْأَرْضِ إِلَّا عَلَى اللَّـهِ رِزْقُهَا وَيَعْلَمُ مُسْتَقَرَّهَا وَمُسْتَوْدَعَهَا كُلٌّ فِي كِتَابٍ مُّبِينٍ﴾

"Na hakuna mnyama yeyote (kiumbe chochote) katika ardhi ila riziki yake iko juu ya Mwenyezi Mungu. Na anajua makao yake ya milele na mahali pake pa kupita tu (hapa duniani). Yote yamo katika kitabu kinachodhihirisha (kila kitu)" (11:6)

Allah (s.w) anayajua atakayoyachagua mtu kuyafanya lakini hakumshurutisha kuyafanya

Pili, isidhaniwe pia kuwa maadamu mtu amechagua kumuasi Allah (s.w), basi mtu huyo anapotenda uovu huo Allah (s.w) huchukia lakini hana uwezo wa kumzuia. Mtu hawezi kufanya lolote ila kwa idhini ya Allah (s.w). Yaani mtu anaweza tu kutenda jema au ovu kwa sababu ya kutumia vizuri au vibaya neema alizopewa na Allah (s.w).

Kwa mfano tusema mtu amekusudia kwenda kuswali Ijumaa lakini kabla hajaondoka Allah (s.w) akamnyang'anya mtu huyo neema ya akili au fahamu, au akakosa nguvu hata za kukaa, ni dhahiri kuwa hataweza kuswali Ijumaa. Na hivyo hivyo kwa mtu aliyekusudia kwenda kuvunja duka na kupora mali kabla ya kufanya hivyo akavunjika mgongo au akatiwa upofu machoni, ni dhahiri kuwa hawezi kutenda lile alilolikusudia. Hivyo mema au maovu hayatendeki kinyume na uwezo wa Allah (s.w).

13

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

SUALA LA UONGOFU

Badhi ya watu hujiuliza: Kama sote tuna fursa sawa sawa ya kuchagua kutenda mema au maovu mbona Qur-an yasema Mwenyezi Mungu humuongoza amtakaye na humuacha kupotea amtakaye? Uongofu utokao kwa Mwenyezi Mungu uko wa namna mbili: Kwanza uongofu kwa maana ya kumfahamisha mtu njia sahihi ya kufuata. Na pili uongofu kwa maana ya msaada utokao kwa Mwenyezi Mungu.

Uongofu kwa maana ya kwanza, yaani kujulishwa njia ya heri na ya shari, na kujulishwa jambo lipi mtu atende na lipi aliwache, ni uongofu ambao kila mtu anaupata. Na uongofu huo ni wa namna tatu kwanza ni: fitra, yaani kupandikizwa uongofu katika nafsi yake mtu:

﴿وَنَفْسٍ وَمَا سَوَّاهَا ﴿٧﴾ فَأَلْهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقْوَاهَا﴾

Na kwa nafsi na aliyeitengeneza.Kisha akaifahamisha uovu wake na wema. (91:7-8)

Na uongofu wa namna ya pili ni kipawa cha akili, ambacho kinaweza kutumika kuisadikisha imani. Na namna ya tatu ni uongofu aliopewa binaadamu kwa kupitia Mitume na Vitabu vya Mwenyezi Mungu. Hivyo kila mtu amepata uongofu kutoka kwa Mwenyezi Mungu angalau kwa njia mbili za mwanzo.

Uongofu kwa maana ya msaada wanaupata wale tu wanaoamua kuufuata kikweli kweli ule uongofu waliopewa. Tuseme mathalan mtu fulani amepotea mjini au hajui njia ya kwenda mahali fulani akaamua kumuuliza askari: Baada ya kumuelekeza mtu yule aliyepotea aseme: Sikuamini, mwongo mkubwa wee!! Askari atamwambia: Sawa fuata njia unayoijua. Lakini iwapo mtu aliyepotea baada ya kuelekezwa atasema: Ahsante sana kwa kunielekeza nafikiri nitafika ninakokusudia, askari anaweza kumwambia: Subiri kidogo mimi nakwenda huko huko nitakupeleka hadi unapokwenda. Huu ni mfano tu, na Mwenyezi Mungu hawezi kufananishwa na askari au kiumbe yeyote.Kusudio hapa ni kuonesha kuwa watu wanaofuata muongozo wa Mwenyezi Mungu huzidishiwa uongofu:

﴿وَالَّذِينَ اهْتَدَوْا زَادَهُمْ هُدًى وَآتَاهُمْ تَقْوَاهُمْ﴾

Na wale wanaokubali kuongoka anawazidishia uongofu na anawapa (jaza) ya ucha Mungu wao. (47:17)

﴿نَّحْنُ نَقُصُّ عَلَيْكَ نَبَأَهُم بِالْحَقِّ إِنَّهُمْ فِتْيَةٌ آمَنُوا بِرَبِّهِمْ وَزِدْنَاهُمْ هُدًى﴾

Sisi tunakusimulia habari zao kwa kweli. Hakika wao walikuwa ni vijana waliomuamini Mola wao Nasi tukawazidisha uongofu.(18:13)

Ili kuweka wazi zaidi uongofu wa aina hii ya pili hebu tuizingatie kwa makini aya aifuatayo:

﴿إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ يَهْدِيهِمْ رَبُّهُم بِإِيمَانِهِمْ تَجْرِي مِن تَحْتِهِمُ الْأَنْهَارُ فِي جَنَّاتِ النَّعِيمِ﴾

Hakika wale walioamini na kufanya vitendo vizuri, Mola wao atawaongoza kwa sababu ya imani yao (wende katika Pepo) Itakuwa inapita mito mbele yao katika mabustani yenye neema. (10:9).

"Allah (s.w) humwingiza katika rahma zake amtakaye na kumwacha kupotea amtakaye" Muradi wa aya zenye melekeo huu ni kuwa Allah(s.w) ametoa sifa za waumini kama zilivyoaminishwa katika Qur'an mf.( 23: 1-11), (25: 63-77), (8:2-4), (49: 1-13,15), (70:19-35), n.k.

Hawa ndiyo "anaowataka" basi anayetaka awepo katika kundi hilo hana budi ajipambe kwazo. lakini pia ametoa sifa za wafiki, washirikina, makafiri, .n.k kama zilivyoanishwa katika qur'an (33:12-20), (2:8-20), (3:166-171), (4:135-152), n.k. Watu watakojipamba na sifa hizi basi Allah huwaacha ( akawaelekezea huko) kupotea, Allah (s.w) ni mwadilifu, humrahisishia mja kila akitakacho cha kheri au cha shari, ndiyo maana pia anasema, "Haakhirishi ya watu mpaka watu wabadilishe yayokuwa katika nafsi zao....." Mbona kuna Uovu na Mateso Duniani? Kuna baadhi ya watu ambao huuliza hivi: Iwapo Mwenyezi Mungu anawapenda waja wake mbona anaacha maovu na mateso yaendelee duniani?Kwa nini asiyazuie?

Kwanza : ni makosa kumhukumu Mwenyezi Mungu ambaye ni Mjuzi wa kila kitu kwa vipimo vya kibinaadamu. Hii ni kwa sababu binaadamu mara nyingi anaathiriwa na hisia zake binafsi na maslahi yake katika kufanya maamuzi yake. Kwa mfano tunaamuaje kuwa kitu fulani ni chema au kibaya? Tuchukue mifano rahisi.Mvua ikinyesha mkulima aliyepanda mazao anamshukuru Mwenyezi Mungu lakini mtu anayekwenda pikiniki au anayefanya sherehe ya harusi, mvua hasa ikinyesha kutwa nzima ni nuksi kubwa kwake!Au tuseme mtu amekodi teksi anawahi ndege uwanjani kwenda kumzika mama yake.

Kwa sababu ya msongamano wa magari barabarani amechelewa kufika uwanjani na hivyo ndege imemwacha na safari kaikosa. Atalaani mtu huyo na kudai kuwa huo ni mkosi mkubwa. Baada ya nusu saa akisikia kuwa ndege ile imeanguka na watu wote wamekufa utamsikia anamshukuru Mungu kwa bahati njema aliyoipata! Binaadamu hawana haki ya kumuuliza Mwenyezi Mungu kama tunavyofahamishwa katika Qur-an:

﴿لَا يُسْأَلُ عَمَّا يَفْعَلُ وَهُمْ يُسْأَلُونَ﴾

Haulizwi (Mwenyezi Mungu) anayoyafanya lakini wao (viumbe wataulizwa).(21:23)

Hii haina maana kuwa binaadamu wanakatazwa kujaribu kutafuta hikima ya Mwenyezi Mungu katika kuamrisha au kukataza kwake mambo, La!Kinyume chake wanahimizwa kufanya hivyo. Wanachokatazwa ni kujaribu kumhukumu Mwenyezi Mungu au kuyakataa na kuyapinga yale ambayo hikima yake hawaijui. Hivyo katika hizo jitihada za kujaribu kubahatisha kuona hikima ya kuyaacha maovu na mateso yawepo baadhi ya watu wanasema kuwa lau si kuwepo kwa uovu watu wasingejua nini wema, bila kuwepo maradhi watu wasingejua thamani ya afya na bila ya mauti watu wasingeyathamini maisha. Wengine wanasema hata wadudu wabaya tunaodhani wanawabughudhi binaadamu, tunadhani hivyo kwa sababu tu hatujajua thamani yao kwetu.

Jambo la kukumbuka ni kuwa kwa mujibu wa Qur-an binaadamu katika kipindi chote cha maisha yake hapa duniani yupo katika majaribio. Na majaribio hayo yatachukua sura mbali mbali za heri na shari. Na jingine ni kwamba ili mtihani huo uwe na maana yoyote watu lazima wawe na hiari ya uchaguzi. Hii ina maana kuwa watu wanaweza kuchagua uovu pia. Hivyo iwapo Mwenyezi Mungu atawapa watu hiari ya uchaguzi lakini atahakikisha hawachagui kufanya ufisadi na uovu nini maana ya kutoa mtihani? Hii haina maana kuwa baada ya kuumbwa ulimwengu Mwenyezi Mungu ameususa na kuuacha uende vyovyote utakavyokwenda, La!Bali kila kitu kipo katika Qadar yake.

Maana ya Kuamini Qadar katika Maisha ya Kila Siku Kwanza, Kwa kujua kuwa fursa, bahati, vipaji na neema zote alizonazo hakuzipata kwa uwezo wake, hanabudi kuvitumia vitu hivi kama amana aliyokabidhiwa na Mola wake. Hanabudi kuitumia amana hii vizuri ili kumuwezesha kufikia lengo la kuumbwa kwake. Muumini wa kweli ana yakini kabisa kuwa atakapo khini amana aliyokabidhiwa na Mola wake, atakuwa ni mwenye kukosa shukrani na atastahiki kuadhibiwa.

﴿ثُمَّ لَتُسْأَلُنَّ يَوْمَئِذٍ عَنِ النَّعِيمِ﴾

Kisha kwa hakika mtaulizwa siku hiyo juu ya neema (mlizopewa mlizitumiaje)" (102:8)

Pili : Kwa kujua pia kuwa fursa, bahati, vipaji na neema zote zinatoka kwa Allah (s.w), halalami pale atakapokuwa amekadiriwa vitu hivi kwa uchache. Yaani hatalalama na kukata tamaa pale atakapokosa fursa mbali mbali, atakapofikiwa na bahati mbaya, atakapodhikishwa vipaji na neema mbali mbali. Bali ataridhika na alichokadiriwa na Mola wake na pia atamshukuru Mola wake kwa kumpangia amana ndogo anayoiweza kuitunza, kwani huenda kama angelikabidhiwa amana kubwa zaidi ya hiyo aliyonayo, angelishindwa kuitunza na kuwa miongoni mwa waliofeli mtihani.

Tatu : atajitahidi kutumia fursa, bahati, vipaji na neema zote alizotunukiwa na Mola wake kwa kadiri ya uwezo wake, kisha matunda ya jitihada hizo huyategemeza kwa Mola wake. Akipata matunda mazuri yaliyotarajiwa hafurahi kupita kiasi, bali atakuwa na furaha ya kawaida ikiambatana na kumshukuru Mola wake kwa kuzidisha kutenda wema kwa kuswali Sunnat-shukra, kutoa sadaqa, kufunga sunnah, n.k. Akipata matunda dhaifu asiyoyategemea, hatakata tamaa na kusononeka, bali ataridhika na matokeo hayo, na ataona ndio makadirio ya Allah (s.w) na ndiyo yenye manufaa naye. Atashukuru na kusema "Al-hamdulillah 'Alaa kullihaali"

Nne : anapotokewa na misuko suko mbali mbali iliyo nje ya uwezo na jitihada za binaadamu, huwa ni mwenye kutulizana na kusubiri akijua kuwa:

﴿مَا أَصَابَ مِن مُّصِيبَةٍ فِي الْأَرْضِ وَلَا فِي أَنفُسِكُمْ إِلَّا فِي كِتَابٍ مِّن قَبْلِ أَن نَّبْرَأَهَا إِنَّ ذَٰلِكَ عَلَى اللَّـهِ يَسِيرٌ ﴿٢٢﴾ لِّكَيْلَا تَأْسَوْا عَلَىٰ مَا فَاتَكُمْ وَلَا تَفْرَحُوا بِمَا آتَاكُمْ وَاللَّـهُ لَا يُحِبُّ كُلَّ مُخْتَالٍ فَخُورٍ﴾

"Hautokei msiba katika ardhi wala katika nafsi zenu ila umekwisha andikwa katika kitabu kabla hatujaumba.Kwa yakini hilo ni sahali kwa Allah, Ili msihuzunike sana juu ya kitu kilichokupateni. Na Allah hampendi kila ajivunaye, ajifaharishaye" (57:22-23)

Muumini wa kweli anajua kuwa misiba na misuko suko mbali mbali ni katika qadar ya Allah (s.w) kama tunavyojifunza katika aya ifuatayo:

﴿وَلَنَبْلُوَنَّكُم بِشَيْءٍ مِّنَ الْخَوْفِ وَالْجُوعِ وَنَقْصٍ مِّنَ الْأَمْوَالِ وَالْأَنفُسِ وَالثَّمَرَاتِ وَبَشِّرِ الصَّابِرِينَ﴾

"Na tutakutieni katika misuko suko na hofu, njaa, upungufu wa mali na watu na matunda.Na wapashe habari njema wale wanaosubiri. (2:155)

Tano : Mtu anayeamini Qadar ya Allah (s.w), siku zote huyaweka mategemeo yake yote kwa Allah (s.w) ambaye ndiye mdhibiti wa kila jambo. Huendelea kutimiza wajibu wake kwa ujasiri na subira hata anapokuwa katika mazingira magumu kwa kuwa anayakini kuwa:

﴿قُل لَّن يُصِيبَنَا إِلَّا مَا كَتَبَ اللَّـهُ لَنَا هُوَ مَوْلَانَا وَعَلَى اللَّـهِ فَلْيَتَوَكَّلِ الْمُؤْمِنُونَ﴾

"... Halitatusibu ila alilotuandikia Mwenyezi Mungu, Yeye ni Mola wetu. Basi waislamu na wamtegemee Mwenyezi Mungu tu" (9:51)

SURA YA NNE

LENGO LA MAISHA YA MWANADAMU

Lengo la maisha Ili mwanaadamu aweze kuishi maisha yenye maana hapa ulimwenguni hanabudi kuwa na ujuzi wa yakini juu ya Lengo, Hadhi na Dhima aliyonayo hapa ulimwenguni.Lengo la kuumbwa watu limebainishwa katika Qur-an kama ifuatavyo:

﴿وَمَا خَلَقْتُ الْجِنَّ وَالْإِنسَ إِلَّا لِيَعْبُدُونِ ﴾

Sikuwaumba majini na watu ila wapate kuniabudu. (51:56)

Aya hii inabainisha wazi kuwa watu hawakuletwa hapa ulimwenguni kwa lengo lingine ila kumuabudu Allah (s.w) tu. Kumuabudu Allah (s.w) ni kufanya Ibada kwa ajili ya Allah (s.w). Maana ya Ibada kwa Mnasaba wa Lengo la Kuumbwa Ibada ni neno la Kiarabu linalotokana na neno "Abd" lenye maana ya Mtumwa au mtumishi. Hivyo kumuabudu Allah (s.w) ni kumtumikia Allah (s.w) kitumwa au kumtumikia Allah (s.w) kikweli kweli bila ya kuwa na hiari katika utumishi huo. Kwa maana hii, lengo la kuumbwa mwanaadamu ni kumtumikia Allah (s.w) kwa unyenyekevu bila ya kumtumikia mwingine yeyote kinyume na mwongozo wake.

Kwa hiyo, ili mwanaadamu aishi kulingana na lengo la kuumbwa kwake, hanabudi kumuabudu Allah (s.w) katika kila hatua na kila pumzi ya maisha yake kwa kuzingatia na kufuata maamrisho yake yote na kuacha makatazo yake yote na kuchunga bara bara mipaka yake kwa kila atakalolifanya. Kwa maana nyingine kila kitendo atakachokifanya mtu kwa lengo la kupata radhi ya Allah (s.w) kitakuwa ni Ibada. Kwa mfano kuchuma mali kwa kuzingatia mipaka ya Allah (s.w) ili kupata riziki ya halali na mahitajio muhimu ya maisha ni Ibada. Kula chakula kizuri na halali ili upate afya nzuri itakayokuwezesha kutekeleza majukumu yako ya kifamilia na ya kijamii kwa ujumla ni Ibada Kulala au kujipumzisha ili uweze kupata nguvu mpya ya kiakili na kimwili itakayokuwezesha kutekeleza majukumu yako kwa jamii ni Ibada. Kwa ujumla kila kitendo kizuri cha halali kilichotendwa kwa kuchunga mipaka ya Allah (s.w) kwa nia ya kumuwezesha mtu kuwa katika hali nzuri ya kutekeleza wajibu wake kwa Allah (s.w) na kwa jamii kwa ujumla ni Ibada.

Mtazamo Potofu Juu ya Maana ya Ibada Baadhi ya watu wameifinya ibada ya Allah (s.w) kwa kuinasibisha na matendo maalumu tu kama vile kuswali, kutoa zakat na sadaqa, kufunga, kuhiji, na ibada nyingine za sunnah zilizoambatana na hizi. Kwa mtazamo huu, matendo yaliyo nje ya Swala, Zakat, Swaum,na kadhalika. si ibada. Je, tutakuwa tumefikia lengo la kuumbwa kwetu kwa kutekeleza tu hizi ibada maalumu? Ukichunguza utaona kuwa muda wanaotumia Waislamu katika kutekeleza ibada hizi maalum ni mdogo sana. Kwa mfano muda tunaotumia kuswali swala tano za siku, ibada ambayo Waislamu wanaitekeleza kwa wingi kuliko ibada nyingine yoyote katika nguzo za Uislamu, ni mdogo sana. Jaalia tunachukua dakika 20 kwa kila swala; hivyo tutahitaji dakika 100 tu katika sa 24 za siku. Hii ni na asilimia 7 (7%) tu ya muda wa siku.

Kuhusu Zakat, kiasi kinachotakiwa kutolewa na tajiri aliye na mali iliyofikia nisaabu ni asilimia 2.5 (2.5%) tu. Vile vile tukichukua mfano wa funga ya Ramadhani, tutaona ni muda mfupi tu tunaotumia katika funga. Jalia tunafunga mwezi mzima wenye siku 30 na kila siku tunafunga kwa saa 14 katika nyakati za kiangazi, ambapo mchana ni mrefu kuliko usiku. Kwa mfano huu kiasi tunachofunga ni sawa na asilimia 5 (5%) ya muda wa mwaka.

Kwa mifano hii michache utaona kuwa lengo la kuumbwa kwetu halitatimia kwa kutekeleza tu hizi ibada za Swala, Zakat, Funga, Hija, n.k. bali tunatakiwa tumuabudu Allah (s.w) muda wote wa saa 24 kwa maisha yetu yote. Hivi ndivyo Allah (s.w) anatuamrisha katika aya zifuatazo:

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا ادْخُلُوا فِي السِّلْمِ كَافَّةً وَلَا تَتَّبِعُوا خُطُوَاتِ الشَّيْطَانِ إِنَّهُ لَكُمْ عَدُوٌّ مُّبِينٌ﴾

"Enyi mlioamini! Ingieni katika Uislamu wote, wala msifuate nyayo za shetani, kwa hakika yeye kwenu ni adui dhahiri" (2:208)

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّـهَ حَقَّ تُقَاتِهِ وَلَا تَمُوتُنَّ إِلَّا وَأَنتُم مُّسْلِمُونَ﴾

"Enyi mlioamini! Mcheni-Mwenyezi Mungu kama ipasavyo kumcha,wala msife isipokuwa mmekwisha kuwa Waislamu kamili." (3:102)

Aidha, Allah (s.w) anatufahamisha kuwa wale wenye akili miongoni mwa wanaadamu ni wale wanaomuamini Allah (s.w) na kumuabudu katika kila kipengele cha maisha yao kama tunavyojifunza katika aya ifuatayo:

﴿إِنَّ فِي خَلْقِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَاخْتِلَافِ اللَّيْلِ وَالنَّهَارِ لَآيَاتٍ لِّأُولِي الْأَلْبَابِ ﴿١٩٠﴾ الَّذِينَ يَذْكُرُونَ اللَّـهَ قِيَامًا وَقُعُودًا وَعَلَىٰ جُنُوبِهِمْ وَيَتَفَكَّرُونَ فِي خَلْقِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ رَبَّنَا مَا خَلَقْتَ هَـٰذَا بَاطِلًا سُبْحَانَكَ فَقِنَا عَذَابَ النَّارِ﴾

Katika kuumbwa mbingu na ardhi na mfuatano wa usiku na mchana ziko hoja (za kuonyesha kuwepo kwa Allah (s.w) kwa wenye akili.Ambao humkumbuka Allah wakiwa wima, wakiwa wamekaa na wakiwa wamelala. Na hufikiri umbile la mbingu na ardhi (tena na tena kisha wanasema), Mola wetu! Hukuviumba hivi bure (pasina lengo).Utukufu ni wako. Basi tuepushe na adhabu ya Moto (3:190-191).

Aya hizi zinatuusia kuwa tumuabudu Allah (s.w) katika shughuli zetu zote tunazozifanya tukiwa tumesimama, tukiwa tumekaa na tukiwa tumelala. Tutahesabika kuwa katika ibada katika kila sekunde ya maisha yetu pale tutakapofanya kila jambo au kila shughuli ya kibinafsi au kijamii kwa kuzingatia mwongozo wa Allah (s.w) na kuchunga bara bara mipaka aliyotuwekea.

Vinginevyo kumuabudu Allah (s.w) kwa baadhi ya wakati, haikubaliki kabisa kama tunavyojifunza katika aya ifuatayo:

﴿أَفَتُؤْمِنُونَ بِبَعْضِ الْكِتَابِ وَتَكْفُرُونَ بِبَعْضٍ فَمَا جَزَاءُ مَن يَفْعَلُ ذَٰلِكَ مِنكُمْ إِلَّا خِزْيٌ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَيَوْمَ الْقِيَامَةِ يُرَدُّونَ إِلَىٰ أَشَدِّ الْعَذَابِ وَمَا اللَّـهُ بِغَافِلٍ عَمَّا تَعْمَلُونَ﴾

"...Je! Mnaamini baadhi ya kitabu na kukataa baadhi (yake)? Basi hakuna malipo kwa mwenye kufanya haya katika nyinyi ila fedheha katika maisha ya dunia; na siku ya kiyama watapelekwa katika adhabu kali. Na Mwenyezi Mungu si mwenye kughafilika na yale mnayoyatenda" (2:85).

8

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

(iv) SIKU YA KUFUFULIWA

Baada ya kipindi cha Barzakh watu watafufuliwa na kuelekea kwenye uwanja wa Hisabu - kama tunavyojifunza katika Qur'an:

﴿ وَنُفِخَ فِي الصُّورِ فَإِذَا هُم مِّنَ الْأَجْدَاثِ إِلَىٰ رَبِّهِمْ يَنسِلُونَ ﴿٥١﴾ قَالُوا يَا وَيْلَنَا مَن بَعَثَنَا مِن مَّرْقَدِنَا هَـٰذَا مَا وَعَدَ الرَّحْمَـٰنُ وَصَدَقَ الْمُرْسَلُونَ ﴿٥٢﴾ إِن كَانَتْ إِلَّا صَيْحَةً وَاحِدَةً فَإِذَا هُمْ جَمِيعٌ لَّدَيْنَا مُحْضَرُونَ ﴿٥٣﴾ فَالْيَوْمَ لَا تُظْلَمُ نَفْسٌ شَيْئًا وَلَا تُجْزَوْنَ إِلَّا مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ﴾

Na kisha litapigwa baragumu (la kufufuliwa), tahamaki hao wanatoka makaburini kwenda mbio mbio kwa Mola wao. (Na huku) wanasema: Ole wetu, (Eee adhabu yetu)!Nani aliyetufufua malaloni petu?" (Waambiwe): "Haya ndiyo yale aliyoahidi (Mwenyezi Mungu) Mwingi wa rehema na waliyoyasema kwa haki Mitume". Haitakuwa ila ukelele mmoja tu, tahamaki wote wamehudhurishwa mbele yetu. (Waambiwe) "Basi leo nafsi yoyote haitadhulumiwa chochote kile wala hamtalipwa ila yale mliyokuwa mkiyatenda".[36:51-54]

Aya hizi zinatufahamisha kuwa hali ya siku hiyo itakuwa ni tofauti kabisa na hali ya hapa ulimwenguni na kwa ujumla itakuwa ni hali ya kutisha na ngumu kwa wanadamu (na majini). Muelekeo wa watu wote baada ya kufufuliwa utakuwa kwa Mola wao katika uwanja wa Hisabu. Japo katika aya nyingi za Qur'an siku ya kufufuliwa imeunganishwa moja kwa moja na siku ya hisabu, bado katika Hadith tunawekwa wazi kuwa patapita muda mrefu wa taabu na mashaka kabla ya kufikia katika hisabu. Patakuwa na jua kali na joto kali sana. Ardhi na mbingu vitakuwa vya shaba kama tunavyofahamishwa katika aya hii:

﴿ يَوْمَ تَكُونُ السَّمَاءُ كَالْمُهْلِ﴾

"Siku mbingu zitakapokuwa kama shaba iliyoyeyuka". [70:8].

Katika hali hii joto na jua kali watu watabubujikwa na jasho litakalofurika kama tunavyofahamishwa katika hadithi zifuatazo:

Abu Hurairah amesimulia kuwa Mtume(s.a.w.w) amesema:Siku ya kufufuliwa (Siku ya Kiyama) watu watatokwa na jasho kwa kiasi ambacho jasho lao litafurika juu (litakuwa na kina) kiasi cha dhiraa sabini na litawazamisha watu mpaka kufikia masikioni. [Bukhari na Muslim]

Mbubujiko na mafuriko haya ya jasho yatategemeana na matendo waliyoyatanguliza waja. Kama tunavyopata ufafanuzi katika Hadith ifuatayo: Miqdad amesimulia: Nimemsikia Mtume(s.a.w.w) akisema: Siku ya Kiyama jua litashushwa karibu na viumbe kiasi cha umbali wa maili moja. Watu watatokwa na jasho kulingana na matendo yao. Kwa watu wengine litafika kwenye fundo za miguu, wengine litafika mpaka magotini na katika watu kuna wale watakaozamishwa mzamisho mkubwa na jasho lao, akiashiria mdomoni mwake kwa mkono wake" [Muslim]

Watu wataangalia mbinguni juu kwa juu kwa muda wa miaka arobaini. Matumbo yataungua kwa njaa na midomo itapasuka kwa kiu. Kila mmoja siku hiyo atahakikisha kuwa siku aliyoahidi Allah (s.w.) na kuikariri mara nyingi katika ujumbe wake, ndio hiyo iliyowadia na hapana popote pa kukimbilia isipokuwa kwa Mola wako.Kila mmoja ataona matendo yake yamehudhurishwa. Na katika hali hii Qur'an inauliza:

﴿ وَمَا أَدْرَاكَ مَا يَوْمُ الدِّينِ ﴿١٧﴾ ثُمَّ مَا أَدْرَاكَ مَا يَوْمُ الدِّينِ ﴿١٨﴾ يَوْمَ لَا تَمْلِكُ نَفْسٌ لِّنَفْسٍ شَيْئًا وَالْأَمْرُ يَوْمَئِذٍ لِّلَّـهِ﴾

Ni nini kitakachokujulisha siku ya malipo ni siku gani hiyo. Tena nini kitakachojulisha siku ya malipo ni siku gani hiyo?Ni siku ambayo nafsi hitamilikia nafsi (nyingine) chochote. Na amri siku hiyo itakuwa ya Mwenyezi Mungu tu" [82:17-19]

Kwa ujumla kipindi kati ya kufufuliwa na kufikia hisabu, kitakuwa kigumu sana na kila mtu atahisi ugumu wake na kiasi ambacho hata Mitume wa Allah (s.w.) ambao ni vipenzi vyake watahisi. Hapana nafsi itakayojiamini, kama tunavyofahamishwa katika Hadith ifuatayo:

Aysha amesimulia kuwa alikumbuka moto na akaangusha kilio. Mtume(s.a.w.w) akauliza:Ni kitu gani kinachokuliza? Akajibu: "Nimekumbuka moto na nikaanza kulia. Je utawakumbuka wake zak siku ya Kiyama?" Mtume (s.a.w.) akasema: "Sikiliza: Katika sehemu tatu (zifuatazo) hakuna atakayemkumbuka yeyote yule - karibu na mizani (hisabu) mpaka ajue kuwa mizani yake itakuwa nyepesi au nzito, na karibu na kupewa kitabu kilichorikodiwa matendo mpaka utakapoitwa: Njoo, soma kitabu chako, na mpaka atakapopewa kitabu chake kwa mkono wa kulia au kushoto au nyuma ya mgongo wake, na karibu na njia nyembamba (siratwa) inakayowekwa baina ya ncha mbili za moto wa Jahannam". [Abuu Daud]

Hata hivyo, tunafahamishwa katika Hadith kuwa katika hicho kipindi kigumu cha baina ya kufufuliwa na kuhukumiwa, waumini waliotenda matendo mema watawekewa kivuli cha Allah (s.w.) na kila Mtume atapewa kisima au haudhi ya maji ya kuwanywesha watu wa ummah wake walioamini pamoja naye. Mtume(s.a.w.w) ameahidiwa Kauthar katika Qur'an:

﴿ إِنَّا أَعْطَيْنَاكَ الْكَوْثَرَ ﴾

"Hakika Tumekupa kheri nyingi" [108:1]

Kutokana na Hadith, Kauthar ni Birika (haudhi) aliloahidiwa Mtume(s.a.w.w) ambalo maji yake ni matamu kuliko asali na meupe kuliko maziwa na yanakata kiu milele - yaani kila mwenye kunywa maji hayo hasikii kiu tena.

Hadith ifuatayo inatufahamisha Kauthar ni nini: Abdullah bin Amr amesimulia kuwa Mtume wa Allah (s.w.) amesema: "Haudhi yangu ina urefu wa safari ya mwezi mmoja na ni pembe mraba na maji yake ni meupe kuliko maziwa, na harufu yake ni nzuri kuliko misk na vikombe vyake vinang'ara kama nyota angani. Yeyote yule anywaye maji yake hasikii kiu daima . [Bukhari na Muslim]

Watakaonyweshwa maji haya na Mtume(s.a.w.w) katika kipindi hicho kigumu cha joto kali lisilo kifani, njaa inayounguza matumbo na kiu kikali kisicho kifani, ni wale tu katika waumini waliomfuata Mtume(s.a.w.w) bila ya kumzumulia lolote. Waliozusha jambo lolote katika dini, Mtume(s.a.w.w) atawafukuza na kuwanyima maji yake kama tunavyofahamishwa katika Hadith ifautayo:

Sahl bin Sa'ad amesimulia kuwa Mtume(s.a.w.w) amesema: Hakika nitawatangulia katika Haudhi. Yeyote atakayepita kwangu atakunywa, na yeyote atakayekunywa hatasikia kiu daima. Watu wale nitakaowajua na watakaonijua hapana shaka watakuja kwangu kunywa lakini patakuwa na kizuizi kati yangu na wao, kisha nitasema: "Hakika hawa ni wangu". Patasemwa: Hakika hujui ni uzushi gani waliokuzulia baada yako. Kisha nitasema: Ondokeni, ondokeni nyinyi mlionizulia (mliozua mambo na kuyaingiza kwenye dini) baada ya yangu. [Bukhari na Muslim]

(V) SIKU YA HUKUMU

Siku ya Hukumu ndio Siku Kuu ambapo Ufalme wa Allah (s.w.) utaonekana kwa wazi kwa kila mtu. Kila mtu atayakinisha kuwa Ufalme ni wa Allah (s.w.) Peke Yake hata kwa wale waliokanusha hapo awali katika maisha ya dunia. Hata hivyo Allah (s.w.) atauliza: Leo Ufalme ni wa nani? Wote watakuwa kimya, halafu atajibu Mwenyewe swali hili kama ilivyo katika aya ifuatayo:

﴿ يَوْمَ هُم بَارِزُونَ لَا يَخْفَىٰ عَلَى اللَّـهِ مِنْهُمْ شَيْءٌ لِّمَنِ الْمُلْكُ الْيَوْمَ لِلَّـهِ الْوَاحِدِ الْقَهَّارِ﴾

Siku watakayodhihiri (mbele ya Mwenyezi Mungu), na haitafichika habari yao yoyote kwa Mwenyezi Mungu. Leo Ufalme ni wa nani? Ni wa Mwenyezi Mungu Mmoja, Mwenye Nguvu (za kufanya Atakalo). [40:16]

Hukumu itatolewa katika ardhi iliyotambarare kabisa ambapo viumbe vyote vitahudhurishwa.Malaika wote watasimama katika safu:

﴿ يَوْمَ يَقُومُ الرُّوحُ وَالْمَلَائِكَةُ صَفًّا لَّا يَتَكَلَّمُونَ إِلَّا مَنْ أَذِنَ لَهُ الرَّحْمَـٰنُ وَقَالَ صَوَابًا﴾

"Siku ambayo zitasimama Roho (za viumbe wote) na Malaika safu safu; hatasema siku hiyo ila yule ambaye (Mwenyezi Mungu) Mwingi wa rehema amempa idhini ( ya kusema) na atasema yaliyo sawa". [78:38]

Kisha kiti cha Enzi cha Allah (s.w.) cha kutolea Hukumu kitahudhurishwa pale na Nuru Yake itazagaa kila mahali na kila mmoja atakuwa na uhakika kuwa Allah (s.w.) yupo kwa kuchukua Hisabu. Qur'an tukufu inatupa picha ya Siku hiyo kuwa:

﴿ وَأَشْرَقَتِ الْأَرْضُ بِنُورِ رَبِّهَا وَوُضِعَ الْكِتَابُ وَجِيءَ بِالنَّبِيِّينَ وَالشُّهَدَاءِ وَقُضِيَ بَيْنَهُم بِالْحَقِّ وَهُمْ لَا يُظْلَمُونَ﴾

Na ardhi (siku hiyo) itang'ara kwa nuru ya Mola wake, na madaftari (ya vitendo) yatawekwa, na wataletwa Manabii na mashahidi na kutahukumiwa baina yao kwa haki wala hawatadhulumiwa". [39:69]

Kila mmoja atapita katika hisabu, japo wengine hisabu zao zitakuwa ngumu sana na wengine nyepesi sana. Hebu tuzingatie Hadith zifuatazo: Aysha amesimulia kuwa Mtume wa Allah (s.w.) amesema: Yeyote atakayehisabiwa (atakayeulizwa) katika siku ya Hukumu, ataangamia. Nikauliza (Aysha) Je, Allah hakusema:

﴿ فَسَوْفَ يُحَاسَبُ حِسَابًا يَسِيرًا ﴾

"Basi Yeye Atahisabiwa hisabu nyepesi?" [84:8]

Akajibu: Hayo kwa hakika ni maelezo ya ujumla lakini atakayehisabiwa kila kitu kwa undani wake, ataangamia. [Bukhari na Muslim] Hadith inatufundisha kuwa kila mmoja atahisabiwa, lakini yule ambaye hisabu yake haitafanywa nyepesi, hataweza kufaulu kutokana na maelezo yake na bila shaka atakuwa ni mtu wa motoni. Pia Hadith ifuatayo inasisitiza juu ya kila mtu kuulizwa na Allah (s.w.):

Ad bin Haatim amesimulia kuwa Mtume(s.a.w.w) amesema:Hapana yeyote kati yenu ambaye hataongea na Mola wake. Hapatakuwa na mkalimani yeyote kati ya Allah na yeye na hapatakuwa na pazia ya kumzuia Allah asionekane. Mja ataangalia kuliani kwake,lakini hatoona chochote isipokuwa matendo yake aliyoyatanguliza.Ataangalia mbele yake, lakini hataona chochote isipokuwa moto unaomjia usoni mwake. Kwa hiyo jikinge na moto (na kutoa sadaka) angalau kipande cha tende. [Bukhari na Muslim] Vile vile tunafahamishwa katika Hadith kuwa hapana yeyote atakayetoka kwenye uwanja wa Hisabu bila ya kuulizwa mambo matano yafuatayo:

1. Ujana wako umeutumiaje?

2. Umri wako umeutumiaje?

3. Mwili wako na vipaji vyako umevitumiaje?

4. Mali yako umeipataje na umeitumiaje?

5. Elimu yako umeitumiaje ?

Maswali haya yataulizwa mbele ya viumbe vyote vilivyoumbwa tangu mwanzo wa ulimwengu mpaka mwisho wake.Kila mchunga (kila kiongozi katika ngazi yoyote ile) ataulizwa juu ya uchungaji (uongozi) wake. Mitume ndio watakaokuwa wa kwanza kuulizwa. Allah (s.w.) atawauliza Mitume: Ni lipi jibu lenu. Watajibu: Hatuna ujuzi.Hakika Wewe Ndiye Mjuzi wa siri (ghaibu)". Mitume watapumbaa kwa woga baada ya kuulizwa swali hili: Kisha Mtume Nuhu(a.s.) ataitwa na kuulizwa kama tunavyofahamishwa katika Hadith ifuatayo: Abu Sayyid amesimulia kuwa Mtume(s.a.w.w) amesema: Nuhu(a.s.) atahudhurishwa katika siku ya hukumu. Ataulizwa: Je, umefikisha (ujumbe wangu)? "Ndiyo" atajibu.Kisha wafuasi wake wataulizwa: Aliwafikishia (ujumbe wangu)? Watajibu: "Hapana mwonyaji aliyetujia". Ataulizwa (Nuhu ni nani mashahidi wako? Atajibu: Muhammad na Umma wake. Mtume(s.a.w.w) amesema: Kisha mtaitwa (mtahudhurishwa) na mtatoa ushahidi kuwa kwa hakika alifikisha ujumbe (wa Allah kwa watu wake).

Kisha Mtume(s.a.w.w) akasoma (aya ifuatayo): Na hivyo ndivyo Tumekufanyeni umati bora (kama Kibla chenu tulivyokifanya bora) ili muwe mashahidi juu ya watu, na Mtume(s.a.w.w) awe shahidi juu yenu. Na hatukukifanya Kibla ulichokuwa nacho (mara ya kwanza kuwa ndio Kibla chako sasa na mwisho wa ulimwengu) ili tupate anayegeuka akarejea nyuma. Na kwa yakini ilikuwa jambo gumu isipokuwa kwa wale aliowaongoza Mwenyezi Mungu. Kwani Mwenyezi Mungu. Kwa watu ni mpole sana (na) mwenye rehma. (2:143) [Bukhari]

Habari juu ya kuulizwa kwa Nabii Issa(a.s.) inatolewa katika Qur'an: Na (kumbukeni) Mwenyezi Mungu atakaposema: Ewe Issa bin Maryam Je, wewe uliwaambia watu 'Nifanyeni mimi na mama yangu kuwa waungu badala ya Mwenyezi Mungu? Aseme (Nabii Issa): "Wewe umetakasika na kuwa na mshirika. Hainijuzii mimi kusema ambayo si haki yangu (kuyasema, kwa kuwa ni ya uwongo).Kama ningalisema bila shaka ungalijua; unayajua yaliyomo nafsini mwangu, lakini siyajui yaliyo nafsini mwako; hakika Wewe ndiye ujuaye mambo ya ghaibu".

﴿ ن يَدْعُونَ مِن دُونِهِ إِلَّا إِنَاثًا وَإِن يَدْعُونَ إِلَّا شَيْطَانًا مَّرِيدًا ﴿١١٧﴾ لَّعَنَهُ اللَّـهُ وَقَالَ لَأَتَّخِذَنَّ مِنْ عِبَادِكَ نَصِيبًا مَّفْرُوضًا ﴿١١٨﴾ وَلَأُضِلَّنَّهُمْ وَلَأُمَنِّيَنَّهُمْ وَلَآمُرَنَّهُمْ فَلَيُبَتِّكُنَّ آذَانَ الْأَنْعَامِ وَلَآمُرَنَّهُمْ فَلَيُغَيِّرُنَّ خَلْقَ اللَّـهِ وَمَن يَتَّخِذِ الشَّيْطَانَ وَلِيًّا مِّن دُونِ اللَّـهِ فَقَدْ خَسِرَ خُسْرَانًا مُّبِينًا﴾

"Sikuwaambia lolote ila yale uliyoniamrisha: Ya kwamba mwabuduni Mwenyezi Mungu, Mola wangu na Mola wenu'. Na nilikuwa shahidi juu yao nilipokuwa nao, na uliponikamilisha muda wangu, wewe ukawa mchungaji juu yao, na wewe shahidi juu ya kila kitu. "Ikiwa utawaadhibu basi bila shaka hao ni waja wako, na ukiwasamehe basi kwa hakika wewe ndiye mwenye nguvu na mwenye hikima; (hutaambiwa kuwa wamekushinda kuwatia adabu).Mwenyezi Mungu atasema: Hii ndiyo siku ambayo wakweli utawafaa ukweli wao. Wao watapata Bustani zipitazo mbele yake mito. Humo watakaa milele.Mwenyezi Mungu amewawia (amewapa) radhi,nao wawe radhi naye.Huku ndiko kufaulu kukubwa. [4:117-119)

Waovu na madhalimu watapiga kelele na kila mmoja katika waumini (wa kweli) atasema:

"Nafsi yangu Nafsi yangu" Watakapokuwa katika hali hii moto utalisambaza tena joto lake mara ya pili, na watarudi katika hali ya kuogopa na kutetemeka. Katika mara ya tatu, watu wataanguka kifudifudi na hapo baba atamkimbia mtoto, ndugu atamkimbia ndugu yake na mume atamkimbia mkewe.

﴿ وَلَا يَسْأَلُ حَمِيمٌ حَمِيمًا﴾

"Wala jamaa hatamuuliza jamaa (yake)" [70:10]

Kisha watu watahudhurishwa mmoja mmoja mbele ya Mola wao kuulizwa. Hapana yeyote atakayeongea bila ya kuulizwa. Hapatakuwa na ndugu wala rafiki wa kumsaidia au kumuonea huruma mtu mwingine. Mahojiano na Allah (s.w.) itakuwa kama tunavyofahamishwa katika Hadith ifuatayo: Abu Hurairah amehadithia: Ewe Mtume(s.a.w.w) Tutamuona Bwana wetu Siku ya Kiyama? Akauliza (Mtume(s.a.w.w) Je, mnaona ugumu kuona mwanga wa jua katikati ya mchana wakati halikufunikwa na mawingu?" Hapana" walijibu. Akauliza (tena): Mnaona vigumu kuona mwanga wa mwezi katikati ya mbalamwezi kali wakati ambapo hamna mawingu? Wakajibu: Hapana. Akasema: Naapa kwa yule ambaye maisha yangu yamo mikononi mwake, hamtapata shida katika kumuona Bwana wenu bali mtamuona kama msivyoona shida kuona jua katikati ya mchana na mwezi wakati wa mbalamwezi kali. Kisha (Allah) atakutana na mja na kumuuliza: Ewe fulani sikukutukuza na nikakupa nguvu, na nikakuozesha, na nikakutiishia farasi na ngamia, na sikukupa uongozi na bora (ya ngawira)? Ulifikiria kuwa utakutana na Mimi. 'Hapana'. Atajibu. Atasema Allah (s.w.) Sasa nimekusahau kama ulivyonisahau. Qur'an inatueleza:

﴿ وَقِيلَ الْيَوْمَ نَنسَاكُمْ كَمَا نَسِيتُمْ لِقَاءَ يَوْمِكُمْ هَـٰذَا وَمَأْوَاكُمُ النَّارُ وَمَا لَكُم مِّن نَّاصِرِينَ﴾

Na itasemwa:"Leo tunakusahauni kama nyinyi mlivyotusahau siku yenu hii, na mahali penu ni motoni, wala hamna wa kukunusuruni". [45:34]

Kisha Allah atakutana na mtu wa pili. (Mtume(s.a.w.w) akatekeleza habari zake kama yule wa kwanza. Kisha Allah (s.w.) akakutana na mtu wa tatu atamuuliza maswali yale yale: Mja huyo atajibu: Ee Bwana, nilikuamini na nikaamini kitabu chako, na Mitume wako, na niliswali, nikafunga na kutoa zaka. Atataja matendo mema aliyoyafanya kwa kiasi atakachoweza.

Allah atamwambia: Njoo hapa (kama unavyosema ndivyo).Sasa tunakuletea mashahidi. Atajiuliza ni nani atakayetoa ushahidi dhidi yangu? Kisha mdomo wake utafungwa na makalio yake yatapewa amri: Sema. Makalio yake, nyama yake na mifupa yake itaongea juu ya vitendo vyake na kwa hivyo ataomba msamaha na huyo atakuwa ni mnafiki ambaye amekasirikiwa na Allah (s.w.). [Muslim]

Kwa ujumla kabla ya kuulizwa na kisha kujitetea kote huku, kila mja atapewa uwezo wa kuona matendo yake aliyoyatanguliza ambayo yamehifadhiwa katika kitabu maalum ambacho atapewa aambiwe akisome mwenyewe kama tunavyofahamishwa katika Qur'an:

﴿وَكُلَّ إِنسَانٍ أَلْزَمْنَاهُ طَائِرَهُ فِي عُنُقِهِ وَنُخْرِجُ لَهُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ كِتَابًا يَلْقَاهُ مَنشُورًا ﴿١٣﴾ اقْرَأْ كِتَابَكَ كَفَىٰ بِنَفْسِكَ الْيَوْمَ عَلَيْكَ حَسِيبًا﴾

"Na kila mwanadamu tumemfungia (jaza ya) vitendo vyake shingoni mwake, tutamtolea siku ya kiyama daftari (iliyoandikwa ndani yake kila alilolifanya) atakayoikuta imekunjuliwa (aambiwe): Soma daftari yako.Nafsi yako inatosha leo kukuhisabu" [17:13-14]

Daftari hili ni daftari la ajabu, litakuwa limenukuu kila kitu mja alichokitenda katika maisha yake. Tunaweza kukiangalia kitabu hiki zaidi ya mfano wa televisheni ya matendo ya mtu ya kila siku kutokea kwenye baleghe yake mpaka kufariki kwake dunia. Televisheni hii itaonesha hata fikra zilizofichikana akilini na siri zilizohifadhiwa vifuani. Kila kitu kitaonekana kwa uwazi katika kitabu hicho. Kitabu hiki kinatolewa picha yake na Qur'an katika aya ifuatayo:

﴿ وَوُضِعَ الْكِتَابُ فَتَرَى الْمُجْرِمِينَ مُشْفِقِينَ مِمَّا فِيهِ وَيَقُولُونَ يَا وَيْلَتَنَا مَالِ هَـٰذَا الْكِتَابِ لَا يُغَادِرُ صَغِيرَةً وَلَا كَبِيرَةً إِلَّا أَحْصَاهَا وَوَجَدُوا مَا عَمِلُوا حَاضِرًا وَلَا يَظْلِمُ رَبُّكَ أَحَدًا ﴾

Na madaftari yatawekwa (mbele yao). Utaona wabaya wanavyoogopa kwa sababu ya yale yaliyomo (madaftarini) na watasema: "Ole wetu, (Ee kuangamia kweli leo). Namna gani madaftari haya!Haliachi dogo wala kubwa ila yamelidhibiti (yameliandika)!"Na watakuta yote yale waliyoyafanya yamehudhuria hapo, na Mola wako hamdhulumu yeyote. [18:49]

Pia tumefahamishwa katika Qur'an:

﴿فَمَن يَعْمَلْ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ خَيْرًا يَرَهُ ﴿٧﴾ وَمَن يَعْمَلْ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ شَرًّا يَرَهُ﴾

Basi anayefanya wema (hata) kwa kiasi cha uzito wa mdudu chungu (atom's weight) ataona jaza yake. Na anayefanya uovu (hata) wa uzito wa mdudu chungu (atom's weight) ataona jaza yake" [99:7-9]

Pia tunafahamishwa katika Qur'an kuwa dalili ya kufaulu au kufeli kwa mtu itaonekana hata kabla mja hajasoma kitabu chake. Atakayekabidhiwa kitabu chake kwa mkono wa kulia atakuwa ni miongoni mwa wenye kufaulu na atakayekabidhiwa kitabu chake kwa mkono wa kushoto atakuwa miongoni mwa waliofeli kama tunavyofahamishwa katika Qur'an:

﴿فَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ بِيَمِينِهِ فَيَقُولُ هَاؤُمُ اقْرَءُوا كِتَابِيَهْ ﴿١٩﴾ إِنِّي ظَنَنتُ أَنِّي مُلَاقٍ حِسَابِيَهْ ﴿٢٠﴾ فَهُوَ فِي عِيشَةٍ رَّاضِيَةٍ ﴿٢١﴾ فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٍ ﴿٢٢﴾ قُطُوفُهَا دَانِيَةٌ ﴿٢٣﴾ كُلُوا وَاشْرَبُوا هَنِيئًا بِمَا أَسْلَفْتُمْ فِي الْأَيَّامِ الْخَالِيَةِ ﴿٢٤﴾ وَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ بِشِمَالِهِ فَيَقُولُ يَا لَيْتَنِي لَمْ أُوتَ كِتَابِيَهْ ﴿٢٥﴾ وَلَمْ أَدْرِ مَا حِسَابِيَهْ ﴿٢٦﴾ يَا لَيْتَهَا كَانَتِ الْقَاضِيَةَ ﴿٢٧﴾ مَا أَغْنَىٰ عَنِّي مَالِيَهْ ﴿٢٨﴾ هَلَكَ عَنِّي سُلْطَانِيَهْ ﴿٢٩﴾ خُذُوهُ فَغُلُّوهُ ﴿٣٠﴾ ثُمَّ الْجَحِيمَ صَلُّوهُ ﴿٣١﴾ ثُمَّ فِي سِلْسِلَةٍ ذَرْعُهَا سَبْعُونَ ذِرَاعًا فَاسْلُكُوهُ ﴿٣٢﴾ إِنَّهُ كَانَ لَا يُؤْمِنُ بِاللَّـهِ الْعَظِيمِ﴾

Basi ama yule atakayepewa daftari lake kwa mkono wake wa kuume (kulia) atasema (kwa furaha) "haya someni daftari langu (nililopewa sasa hivi). Hakika nilijua ya kuwa nitapokea hisabu yangu (kwa vizuri)". Basi yeye atakuwa katika maisha ya raha katika pepo tukufu.Vishada vya matunda yake vitakuwa karibu;(vinachumika bila tabu). (Waambiwe) "Kuleni na mnywe kwa furaha kwa sababu ya vitendo mlivyofanya katika siku zilizopita".Walakini atakayepewa daftari lake katika mkono wake wa kushoto basi yeye atasema: "Oh Laiti nisingalipewa daftari langu.Wala nisingelijua nini hisabu yangu.Laiti (mauti) yangemaliza (kila kitu changu). Mali yangu haikunifaa.Usultani (ukubwa) wangu umenipotea.(Kusemwe): "Mkamateni na mtieni makongwa.Kisha mtupeni motoni. Tena katika mnyororo wenye urefu wa dhiraa sabini muingizeni, (mtatizeni). Hakika yeye alikuwa hamuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu" [69:19-33]

Baada ya kupewa daftari, tukio kubwa litakalofuata ni kupimwa amali katika mizani. Jambo ambalo litakuwa pia ni lenye kutisha sana kwa waja kama tulivyofahamishwa katika Hadith. Patakuwa na makundi matatu ya watu. Kuna watakaoingia peponi moja kwa moja bila hesabu. Hili litakuwa kundi la watu wachache waliojizatiti katika kutenda mema kwa ajili ya kupata radhi ya Allah (s.w.). Atawakaribisha moja kwa moja baada ya kuwafanyia wepesi katika hesabu yao kwa kuwaita:

﴿يَا أَيَّتُهَا النَّفْسُ الْمُطْمَئِنَّةُ ﴿٢٧﴾ ارْجِعِي إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةً مَّرْضِيَّةً ﴿٢٨﴾ فَادْخُلِي فِي عِبَادِي ﴿٢٩﴾ وَادْخُلِي جَنَّتِي﴾

"Ewe nafsi yenye kutua: Rudi kwa Mola wako, hali ya kuwa umeridhika (kwa utakayoyapata), na (Mwenyezi Mungu) aridhike na wewe. Basi ingia katika (kundi la) waja wangu (wazuri) uingie katika Pepo Yangu" [89:27-30]

Kundi la pili la wale ambao hawakumuamini Allah (s.w.) hata chembe, hawa wataingizwa motoni moja kwa moja bila ya amali zao kupimwa katika mizani kwani chochote atakachokifanya kafiri au mushriki, au kitakachofanywa kwa ria au kwa unafiki hakitakuwa na malipo yoyote kutoka kwa Allah (s.w.). Hivyo kafiri, mushriki na mnafiki hawatakuwa na lao mbele ya Allah (s.w.) kama tunavyofahamishwa katika Qur'an:

﴿أَفَحَسِبَ الَّذِينَ كَفَرُوا أَن يَتَّخِذُوا عِبَادِي مِن دُونِي أَوْلِيَاءَ إِنَّا أَعْتَدْنَا جَهَنَّمَ لِلْكَافِرِينَ نُزُلًا ﴿١٠٢﴾ قُلْ هَلْ نُنَبِّئُكُم بِالْأَخْسَرِينَ أَعْمَالًا ﴿١٠٣﴾ الَّذِينَ ضَلَّ سَعْيُهُمْ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَهُمْ يَحْسَبُونَ أَنَّهُمْ يُحْسِنُونَ صُنْعًا ﴿١٠٤﴾ أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ كَفَرُوا بِآيَاتِ رَبِّهِمْ وَلِقَائِهِ فَحَبِطَتْ أَعْمَالُهُمْ فَلَا نُقِيمُ لَهُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَزْنًا ﴿١٠٥﴾ ذَٰلِكَ جَزَاؤُهُمْ جَهَنَّمُ بِمَا كَفَرُوا وَاتَّخَذُوا آيَاتِي وَرُسُلِي هُزُوًا﴾

Je,wale waliokufuru wanadhani ya kwamba kule kuwafanya waja wangu kuwa walinzi (wao) badala Yangu (kutawafaa kitu kufanya hivyo)?Hakika Sisi Tumeiandaa Jahannamu iwe ndio mahala pa kuteremkia makafiri. Sema:Je!Tukujulisheni wenye hasara katika vitendo (vyao)? Hao ambao bidii yao hapa duniani imepotea bure katika maisha ya dunia, nao wanafikiri kwamba wanafanya amali njema? Hao ni wale waliozikataa (waliozikanusha) ishara za Mola wao na (wakakataa) naye.Kwa hiyo vitendo vya vimeruka patupu, wala hatutawasimamishia mizani siku ya kiyama. Hivyo Jahannamu ni malipo yao kwa sababu walikufuru na kuzifanyia mzaha aya zangu na Mitume wangu. [18:102-106]

﴿ وَلَقَدْ أُوحِيَ إِلَيْكَ وَإِلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكَ لَئِنْ أَشْرَكْتَ لَيَحْبَطَنَّ عَمَلُكَ وَلَتَكُونَنَّ مِنَ الْخَاسِرِينَ﴾

"Na kwa yakini imefunuliwa kwako na kwa wale waliokuwa kabla yako (maneno haya): "Kama ulimshirikisha (Mwenyezi Mungu) bila shaka amali zako zitaruka patupu (hatazipatia thawabu japo ni amali njema), na lazima utakuwa miongoni mwa wenye hasara". [39:65]

Kundi la tatu ni lile la watu walimuamini Allah (s.w.) lakini katika utendaji wakawa wamechanganya mema na maovu. Mema yao na maovu yao itabidi yapimwe katika mizani ya haki ili kila mmoja alipwe kwa haki kutokana na matendo yake aliyoyatanguliza. Qur'an inatufahamisha juu ya hili:

﴿وَنَضَعُ الْمَوَازِينَ الْقِسْطَ لِيَوْمِ الْقِيَامَةِ فَلَا تُظْلَمُ نَفْسٌ شَيْئًا وَإِن كَانَ مِثْقَالَ حَبَّةٍ مِّنْ خَرْدَلٍ أَتَيْنَا بِهَا وَكَفَىٰ بِنَا حَاسِبِينَ﴾

Nasi tutaweka mizani za uadilifu siku ya Kiyama na nafsi yeyote haitadhulumiwa hata kidogo. Na hata kama ikiwa (jambo hilo lina) uzito mdogo wa chembe ya hardali nalo tutalileta. Nasi tunatosha kuwa wajuzi (wazuri kabisa) wa hisabu. [21:47]

Wale watakaokuwa na mizani nzito upande wa wema au wale ambao uzito wa mema yao utazidi uzito wa uovu wao, hawa watakuwa ni wenye kufaulu watastahiki pepo. Na wale ambao mizani itaonyesha kinyume chake, utakapokuwa umezidi uzito wa mema yao, hao watakuwa ni watu wa motoni kama tunavyofahamishwa katika Qur'an:

﴿ فَمَن ثَقُلَتْ مَوَازِينُهُ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُفْلِحُونَ ﴿١٠٢﴾ وَمَنْ خَفَّتْ مَوَازِينُهُ فَأُولَـٰئِكَ الَّذِينَ خَسِرُوا أَنفُسَهُمْ فِي جَهَنَّمَ خَالِدُونَ﴾

Ama wale ambao mizani ya amali zao (nzuri) itakuwa nzito,hao ndio wenye kufaulu. Na wale ambao mizani yao itakuwa nyepesi, hao ndio waliozitia hasarani nafsi zao, na katika Jahannamu watakaa muda mrefu. [23:102-103]

Ukweli wa mambo ni kwamba, mizani anayo mtu katika maisha yake yote ya hapa ulimwenguni. Kila mja ameshajulishwa ni tabia ipi au mwenendo upi wa maisha akiufuata atafaulu hapa duniani na akhera, na ni tabia ipi au mwenendo upi wa maisha atakapoufuata mja utamhilikisha hapa duniani na huko akhera. Hivyo kila mja anao uwezo wa kukisia kuwa mizani yake itakuwaje kwa kuiangalia tabia yake jinsi anavyolandana na inavyopingana na utaratibu wa Sharia aliyoiweka Allah (s.w.). Makisio haya tutayafanya kwa kutumia mizani aliyotuletea Allah (s.w.) kama Qur'an inavyofufahamisha:

﴿لَقَدْ أَرْسَلْنَا رُسُلَنَا بِالْبَيِّنَاتِ وَأَنزَلْنَا مَعَهُمُ الْكِتَابَ وَالْمِيزَانَ لِيَقُومَ النَّاسُ بِالْقِسْطِ﴾

Kwa hakika Tuliwapeleka Mituma wetu kwa dalili wazi wazi na tukaviteremsha vitabu na mizani (ya mema na maovu) ili watu wasimamie uadilifu [57:25]

Hivyo kila mmoja anao uwezo wa kuiweka mizani yake ikaelemea upande unastahili kwa kulipima kila jambo analolifanya katik a maisha yake kwa mizani aliyoiweka Allah (s.w.) ya kuyaweka bayana mabaya na mazuri kisha mtu akajihukumu. Mafundisho tunayoyapata kutokana na Hadith ifuatayo:

Aysha amesimulia kuwa, alikuja mtu mmoja na kukaa mbele ya Mtume(s.a.w.w) na kuuliza: "Ewe Mtume(s.a.w.w) wa Allah nimeweka mkataba wa watumwa ambao wananikadhibisha na wananifanyia hila na kunidanganya na hawanitii, ninawakemea na kuwapiga.Niwafanyeje? Mtume(s.a.w.w) akasema: "Siku ya malipo itakapofika, hisabu itachukuliwa dhidi yao kiasi walichokuhadaa kwa hila, kiasi walichokataa kukutii na kiasi walichokughadhibisha. Kama adhabu uliyowapa (ya kuwakemea na kuwapiga) itakuwa ni sawa na makosa yao, sawa kwako na kwao, na kama adhabu uliyowapa itakuwa ni ndogo kuliko makosa yao, utaongezewa ufidie sehemu iliyobaki, na kama adhabu uliyowapa itazidi makosa yao basi itabidi fidia itoke (kwenye amali yako) kwkao uwape.". Yule mtu aligeuka pembeni na akaanza kusikitika na kulia. Kisha Mtume(s.a.w.w) akasema:" Hujasoma aya za Allah (s.w.):

﴿وَنَضَعُ الْمَوَازِينَ الْقِسْطَ لِيَوْمِ الْقِيَامَةِ فَلَا تُظْلَمُ نَفْسٌ شَيْئًا وَإِن كَانَ مِثْقَالَ حَبَّةٍ مِّنْ خَرْدَلٍ أَتَيْنَا بِهَا وَكَفَىٰ بِنَا حَاسِبِينَ﴾

"Tutaweka mizani kwa uadilifu siku ya Kiyama na nafsi yoyote haitadhulumiwa hata kidogo na hata kama likiwa na uzito ndogo wa chembe yardali nalo tutalileta, Nasi tutatosha kuwa wajuzi wa kuhisabu". [21:47].

Yule mtu akasema: "Ewe Mtume wa Allah: Ninaona kuwa hapana jambo lililo bora zaidi kwangu mimi na kwa hawa watumwa, isipokuwa kuachana nao.Ninashuhudia mbele yako kuwa wote sasa wako huru". [Tirmidh]

Hadith inatupa fundisho kubwa kuwa, pamoja na mtu kukosewa, si vema kutoa hukumu kwani anaweza kutoa hukumu isiyolingana na kosa. Kwa ujumla Mtume (s.a.w.w) ametuusia kuwa tujihisabu wenyewe kabla hatujahisabiwa. Huku kujihesabu si lingine bali ni kutubu kikweli kweli kwa moyo mkunjufu kwa makosa yote mtu aliyoyafanya na kwa yale yote aliyoacha kuyatekeleza katika yale aliyoamrishwa. Na kurudisha haki ya aliyedhulumiwa hata kama ni punje moja iliyochukuliwa kwa makosa au kinyume na idhini yake, kumtaka msamaha kwa haki iliyochukuliwa, na wale walioumizwa kwa uonevu kwa ulimi au mkono. Kama mtu aliyefanya makosa haya atafariki bila ya kutubia na kuwaomba msamaha wale aliowakosea au kuwarudishia haki zao kama zinarudishika, atawakuta karibu na mizani katika siku ya hisabu wakidai haki zao na kushitaki: "Ulinigombeza (ulinikemea) bila ya sababu yoyote, ulinitukana, uliniteta, ulinifanyia ubaya ukiwa kama jirani, mtumishi, Rais, hukunihudumia ipasavyo nilipokuwa mgonjwa, ulinikuta nina njaa na hukunilisha na ilihali ulikuwa na uwezo, unilikuta nina kiu hukuninyeshwa, ulinikuta ni uchi hukunivisha, hukuondoa dhulma na ili hali ulikuwa na madaraka na kadhalika. Hapa Allah (s.w.) atasema:

﴿الْيَوْمَ تُجْزَىٰ كُلُّ نَفْسٍ بِمَا كَسَبَتْ لَا ظُلْمَ الْيَوْمَ إِنَّ اللَّـهَ سَرِيعُ الْحِسَابِ﴾

"Leo kila nafsi italipwa kwa kila ilichokitanguliza.Hapana atakayedhulumiwa leo".[40:17]

Kwa muhtasari kutokana na haya tuliyojifunza juu ya Siku ya Kiyama mambo matano yafuatayo yamejitokeza:

Kwanza : hukumu itakuwa ya haki na kwamba hakuna mtu hata mmoja atakayedhulumiwa chochote kama Qur'an inavyosisitiza:

﴿الْيَوْمَ تُجْزَىٰ كُلُّ نَفْسٍ بِمَا كَسَبَتْ لَا ظُلْمَ الْيَوْمَ إِنَّ اللَّـهَ سَرِيعُ الْحِسَابِ﴾

Leo kila mtu atapewa malipo ya yale aliyoyatenda, hakuna dhulma leo, bila shaka Allah ni Mwepesi kuhisabu. [40:17]

﴿إِنَّ اللَّـهَ لَا يَظْلِمُ النَّاسَ شَيْئًا وَلَـٰكِنَّ النَّاسَ أَنفُسَهُمْ يَظْلِمُونَ﴾

Hakika Allah hawadhulumu watu chochote, lakini watu wanajidhulumu nafsi zao [10:44]

Pili : mambo yote siku hiyo yatakuwa wazi kiasi cha kuweza mtu kujihesabu mwenyewe

Tatu : kabla ya hukumu kwa kawaida hutakikana ushahidi. Ushahidi wa siku hiyo ni daftari la amali za mtu ambalo limedhibitiwa vyema na malaika waandishi hodari wa amali za waja kama tunavyofahamishwa katika Qur'an:

﴿مَّا يَلْفِظُ مِن قَوْلٍ إِلَّا لَدَيْهِ رَقِيبٌ عَتِيدٌ﴾

Hatoi kauli yoyote isipokuwa karibu naye yuko mngojeaji tayari (kuandika) [50:18]

﴿وَإِنَّ عَلَيْكُمْ لَحَافِظِينَ ﴿١٠﴾ كِرَامًا كَاتِبِينَ ﴿١١﴾ يَعْلَمُونَ مَا تَفْعَلُونَ﴾

Na hakika juu yenu kuna wenye kuwatunza (Malaika) watukufu wenye kuandika.Wanayajua yote mnayoyatenda.[82:10-12].

Nne : mashahidi siku hiyo ni viungo vyake mtu. Macho yatasema yalichokitazama kinyume na sheria ya Allah (s.w.), mikono itachoiba, miguu iliko kwenda na kadhalika. Maadam mtu hatendi jema wala ovu ila atatumia kiungo fulani cha mwili wake basi ajue hao ni mashahidi waadilifu ambao hawapokei rushwa, na ataitoa wapi rushwa siku hiyo? Tunafahamishwa katika Qur'an:

﴿يَوْمَ تَشْهَدُ عَلَيْهِمْ أَلْسِنَتُهُمْ وَأَيْدِيهِمْ وَأَرْجُلُهُم بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ﴾

Siku ambayo zitawashuhudia ndimi zao na mikono yao na miguu yao kwa yale waliyokuwa wakifanya. [24:24]

﴿لْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَىٰ أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُم بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ﴾

Siku hiyo tutaviziba vinywa vyao, itazungumza mikono yao, na itoe ushahidi miguu yao kwa yale waliyokuwa wakiyachuma. [36:65]

﴿وَمَا كُنتُمْ تَسْتَتِرُونَ أَن يَشْهَدَ عَلَيْكُمْ سَمْعُكُمْ وَلَا أَبْصَارُكُمْ وَلَا جُلُودُكُمْ وَلَـٰكِن ظَنَنتُمْ أَنَّ اللَّـهَ لَا يَعْلَمُ كَثِيرًا مِّمَّا تَعْمَلُونَ﴾

Na hamkuwa mkijificha hata masikio yenu na macho yenu na ngozi zenu zisiweze kutoa ushahidi juu yenu, bali mlidhani ya kwamba Allah hayajui mengi katika (hayo) mnayoyafanya. [41:22]

Tano : kutakuwa na mizani ya kupimia amali za waja. Mizani hii haitapima amali zenyewe bali thamani ya amali. Uzito siku hiyo utakuwa ni kweli na haki. Yaani kweli au haki ndivyo vitakavyokuwa na uzito. Allah (s.w.) amesema:

﴿وَالْوَزْنُ يَوْمَئِذٍ الْحَقُّ فَمَن ثَقُلَتْ مَوَازِينُهُ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُفْلِحُونَ ﴿٨﴾ وَمَنْ خَفَّتْ مَوَازِينُهُ فَأُولَـٰئِكَ الَّذِينَ خَسِرُوا أَنفُسَهُم بِمَا كَانُوا بِآيَاتِنَا يَظْلِمُونَ﴾

Na siku hiyo kipimo (uzito) kitakuwa ni haki. Basi watakaokuwa na uzani mzito, hao ndio watakaofaulu. Na watakaokuwa na uzani hafifu, basi hao ndio waliozitia hasarani nafsi zao kwa sababu ya kuzifanyia jeuri Aya zetu. [7:8-9]

"Na siku hiyo uzito utakuwa ni haki Msemo huu wa Allah (s.w.) una maana kuwa, siku ya Hukumu katika mizani ya haki, hakuna chochote isipokuwa Haki na Ukweli ndivyo vitakavyokuwa na uzito. Uzito utazidi au kupungua kulingana na ukweli utakaokuwa nao mja juu ya nafsi yake na atahukumiwa kwa kipimo cha ukweli huo na si kwa kitu kingine chochote. Maisha ya kinafiki na uasi hata kama yatakuwa marefu na hata kama mtu atakuwa amefanya mambo mengi ambayo yeye atadhani kuwa ni makubwa katika mizani ya Allah (s.w.) hayatakuwa na uzito wowote.


11

12

13

14

15