MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU 13%

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU Mwandishi:
Kundi: Vitabu mbali mbali

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU
  • Anza
  • Iliyopita
  • 22 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 47907 / Pakua: 4683
Kiwango Kiwango Kiwango
MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

Mwandishi:
Swahili

1

2

3

6

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

KUAMINI MALAIKA WA ALLAH (S.W.)

Malaika ni nani? Malaika ni katika waja na viumbe wa Allah(SW) walioumbwa kutokana na nuru. Tunafahamishwa katika hadithi ifuatayo kuwa: Aysha (r.a.) amesimulia kuwa Mtume(s.a.w.w) amesema:

Malaika wameumbwa na nuru na majini wameumbwa kutokana na ndimi za moto na Adamu ameumbwa kwa udongo kama ilivyoelezwa kwenu (katika Qur'an). (Muslim)

Na katika Qur'an tukufu,Allah(SW) anatubainishia kuwa, katika maumbile yao halisi, malaika ni viumbe wenye mbawa.

﴿الْحَمْدُ لِلَّـهِ فَاطِرِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ جَاعِلِ الْمَلَائِكَةِ رُسُلًا أُولِي أَجْنِحَةٍ مَّثْنَىٰ وَثُلَاثَ وَرُبَاعَ يَزِيدُ فِي الْخَلْقِ مَا يَشَاءُ إِنَّ اللَّـهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ﴾

"Sifa zote njema ni za Allah,Muumba wa mbingu na ardhi. Aliyewafanya malaika kuwa wajumbe wenye mbawa mbili-mbili,na tatu tatu, na nne nne.Huzidisha katika kuumba apendavyo.Bila shaka ni mwenye uweza juu ya kila kitu" (35:1)

JE MALAIKA WANAISHI WAPI?

Katika Qur,an tunafahamishwa kuwa Malaika wanayo makazi maalumu lakini si hapa duniani. Allah(SW) anawanukuu malaika wakisema:

﴿وَمَا مِنَّا إِلَّا لَهُ مَقَامٌ مَّعْلُومٌ ﴿١٦٤﴾ وَإِنَّا لَنَحْنُ الصَّافُّونَ ﴿١٦٥﴾ وَإِنَّا لَنَحْنُ الْمُسَبِّحُونَ﴾

Hakuna yoyote miongoni mwetu ila anapo mahali pake mahususi. Na kwa yakini katika sisi wapo wajipangao safu. Na wako katika sisi wamtukuzao (Mwenyezi Mungu) (37:164-166)

Kutokana na kazi zao, Malaika wengi tunaishi nao humu humu duniani na wako nasi muda wote.Kila mtu ana malaika wawili wenye kuandika amali zake. Hakika juu yenu kuna wenye kuwatunza, malaika watukufu wenye kuandika.Wanayajua yote mnayoyatenda (82:10-12) Aidha, tunafahamishwa katika Qur,an kuwa kila mmoja wetu ana kundi la malaika mbele na nyuma yake. Ana (kila mtu) kundi (la malaika) mbele yake na nyuma yake.Wanamlinda kwa amri ya Mwenyezi Mungu. (13:11)

KWANINI HATUWAONI MALAIKA?

Pengine mtu aweza akauliza kuwa kama tumezungukwa na malaika mbele na nyuma, kulia na kushoto, kwanini basi hatuwaoni?

Jibu ni kwamba, mwanadamu yupo kwenye mtihani. Mtihani wenyewe ni kufanya mema kwa kutaraji malipo ya Allah(SW) na kuacha maovu kwa kuogopa adhabu zake.

﴿تَبَارَكَ الَّذِي بِيَدِهِ الْمُلْكُ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿١﴾ الَّذِي خَلَقَ الْمَوْتَ وَالْحَيَاةَ لِيَبْلُوَكُمْ أَيُّكُمْ أَحْسَنُ عَمَلًا وَهُوَ الْعَزِيزُ الْغَفُورُ ﴾

Ametukuka yule ambaye Mkononi mwake umo ufalme(wote); naye ni mwenye uweza juu ya kila kitu. Ambaye ameumba mauti na uhai ili kukujaribuni; ni nani miongoni mwenu mwenye vitendo vizuri zaidi. Naye ni Mwenye nguvu na Mwenye msamaha (67:1-2)

Malaika ndio wasimamizi wa mtihani huu, na wamefanywa wasionekane machoni petu ili kila mtu atumie uhuru wake wa ama kumuogopa Allah(SW) kwa kutenda mema au kumkufuru Allah(SW) kwa kumuasi.

Lau malaika wangelionekana, watu wengi wangelitenda mema kinafiki(ria) badala ya kufanya kwa ikhilaswi. Mfano wake, ingekuwa kama vile watu wenye dhamira za kufanya uhalifu wanavyojidai watu wema pale wanapokuwepo askari waliovalia rasmi. Utendaji kazi wa malaika ni kama mashushushu au askari kanzu. Mtu muovu anapanga na kutenda maovu akidhani yupo peke yake,kumbe malaika wapo wanaandika.Na ndiyo maana muovu atakapoona kila jambo lake limerikodiwa, atashangaa siku ya kiama kuwa alijulikanaje?

﴿وَوُضِعَ الْكِتَابُ فَتَرَى الْمُجْرِمِينَ مُشْفِقِينَ مِمَّا فِيهِ وَيَقُولُونَ يَا وَيْلَتَنَا مَالِ هَـٰذَا الْكِتَابِ لَا يُغَادِرُ صَغِيرَةً وَلَا كَبِيرَةً إِلَّا أَحْصَاهَا وَوَجَدُوا مَا عَمِلُوا حَاضِرًا وَلَا يَظْلِمُ رَبُّكَ أَحَدًا﴾

Na madaftari yatawekwa mbele yao.Utawaona wabaya wanayaogopa kwasababu ya yale yaliyomo; na watasema: "Ole wetu! Namna gani madaftari haya! Haliachi dogo wala kubwa ila yamelidhibiti.Na watakuta yote yale waliyoyafanya yamehudhuria hapo; na Mola wako hamdhulumu yeyote(18:49)

Siku mtu atakapowaona malaika Kuna siku na muda maalumu ambapo kila mtu binafsi ataanza kuwaona malaika katika umbile lao halisi.

(a) Siku ya kukata roho Hii ni siku na saa ambayo dakika chache baada ya hapo mtu hukata roho na kuiaga dunia. Kwa watu wema, watakuja malaika wa kuwaliwaza:

﴿تَتَنَزَّلُ عَلَيْهِمُ الْمَلَائِكَةُ أَلَّا تَخَافُوا وَلَا تَحْزَنُوا وَأَبْشِرُوا بِالْجَنَّةِ الَّتِي كُنتُمْ تُوعَدُونَ﴿٣٠﴾ نَحْنُ أَوْلِيَاؤُكُمْ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَفِي الْآخِرَةِ ﴾

......Hao huwateremkia Malaika "msigope wala msihuzunike, na furahini kwa pepo mliyokuwa mkiahidiwa. Sisi ni vipenzi vyenu katika maisha ya dunia na (huku) katika Akhera......"(41:30-31)

Watu wanaotenda maovu watapata mshituko mkubwa na kujawa na huzuni kubwa mno pale watakapowaona Malaika. Watasikitika sana kwa jinsi walivyokuwa wakijidanganya nafsi zao, wakatenda maovu kwa kudhania kuwa hakuna Malaika wanaorekodi matendo yao waliyokuwa wakiyafanya hadharani na mafichoni. Watafadhaika na kusema:

﴿حَتَّىٰ إِذَا جَاءَ أَحَدَهُمُ الْمَوْتُ قَالَ رَبِّ ارْجِعُونِ ﴿٩٩﴾ لَعَلِّي أَعْمَلُ صَالِحًا فِيمَا تَرَكْتُ كَلَّا إِنَّهَا كَلِمَةٌ هُوَ قَائِلُهَا ﴾

....Mola wangu! Nirudishe(duniani). Ili nifanye mema sasa badala ya yale niliyoyaacha. (Malaika watamwambia): "Hapana! Hakika hili ni neno tu analosema yeye(mtu muovu)....(23:99-100)

(b) Siku ya kiyama Kuanzia pale mtu anapowaona malaika hakutakuwa tena na kizuizi cha kutowaona kama ilivyokuwa hapa duniani. Kuonekana Malaika siku ya kiama itakuwa ni ishara mbaya kwa watu waovu kuwa umeshafika wakati wa wao kuhukumiwa na Allah (s.w) na kuanza kutumikia adhabu za kudumu katika Moto wa Jahannam. Qur'an inatufahamisha kuwa: Siku watakayowaona Malaika haitakuwa furaha siku hiyo kwa wenye makosa; na watasema:

﴿يَوْمَ يَرَوْنَ الْمَلَائِكَةَ لَا بُشْرَىٰ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُجْرِمِينَ وَيَقُولُونَ حِجْرًا مَّحْجُورًا ﴾

"(Mungu) atuepushie mbali adhabu hii iliyotukabili (lakini haitawafaa kitu dua hiyo)(25:22)

(c) Motoni na Peponi Malaika watahudhuria katika uwanja wa hukumu siku ya Kiyama. Kila mtu atawaona wamejipanga safu wakisubiri amri ya Mwenyezi Mungu:

﴿يَوْمَ يَقُومُ الرُّوحُ وَالْمَلَائِكَةُ صَفًّا لَّا يَتَكَلَّمُونَ إِلَّا مَنْ أَذِنَ لَهُ الرَّحْمَـٰنُ وَقَالَ صَوَابًا﴾

Siku ambayo zitasimama Roho na Malaika safu safu; hatasema siku hiyo ila yule ambaye (Allah) Mwingi wa rehema amempa idhini, na atasema yaliyo sawa (78:38)

Wakipewa amri na Allah(s.w) malaika watawakamata waovu na kuwachungachunga kuelekea motoni kuadhibiwa.

﴿وَسِيقَ الَّذِينَ كَفَرُوا إِلَىٰ جَهَنَّمَ زُمَرًا حَتَّىٰ إِذَا جَاءُوهَا فُتِحَتْ أَبْوَابُهَا وَقَالَ لَهُمْ خَزَنَتُهَا أَلَمْ يَأْتِكُمْ رُسُلٌ مِّنكُمْ يَتْلُونَ عَلَيْكُمْ آيَاتِ رَبِّكُمْ وَيُنذِرُونَكُمْ لِقَاءَ يَوْمِكُمْ هَـٰذَا﴾

Na waliokufuru watapelekwa katika Jahannam makundi makundi mpaka watakapoifikia; itafunguliwa milango yake; walinzi wake(malaika) watawaambia: Je! hawakukujieni Mitume miongoni mwenu wakikusomeeni aya za Mola wenu na kukuonyeni juu ya makutano ya siku yenu hii(39: 71)

﴿وَسِيقَ الَّذِينَ اتَّقَوْا رَبَّهُمْ إِلَى الْجَنَّةِ زُمَرًا حَتَّىٰ إِذَا جَاءُوهَا وَفُتِحَتْ أَبْوَابُهَا وَقَالَ لَهُمْ خَزَنَتُهَا سَلَامٌ عَلَيْكُمْ طِبْتُمْ فَادْخُلُوهَا خَالِدِينَ﴾

Watu wema watasindikizwa na malaika mpaka kwenye pepo tukufu, na malaika wa huko watawakaribisha. Na walinzi wake(malaika) watawaambia: Amani juu yenu, furahini, na ingieni humu mkae milele(39:73)

SIFA ZA MALAIKA

Malaika Ni viumbe watiifu wasiomuasi Allah(SW) Malaika ni viumbe watiifu kwa Allah(SW). Wakipewa amri ya kumuadhibu mtu muovu,hawagomi wala kumuonea huruma mtu huyo.

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا قُوا أَنفُسَكُمْ وَأَهْلِيكُمْ نَارًا وَقُودُهَا النَّاسُ وَالْحِجَارَةُ عَلَيْهَا مَلَائِكَةٌ غِلَاظٌ شِدَادٌ لَّا يَعْصُونَ اللَّـهَ مَا أَمَرَهُمْ وَيَفْعَلُونَ مَا يُؤْمَرُونَ﴾

Enyi mlioamini! Ziokoeni nafsi zenu na nafsi za watu wenu na moto ambao kuni zake ni watu na mawe. Juu yake kuna Malaika wakali wenye nguvu.Hawamuasi Allah(SW) katika yale anayowaamuru, na wanatekeleza vile walivyoamrishwa.(66:6)

WANA ELIMU YA KUTOSHA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO

Malaika wana elimu inayowawezesha kutekeleza majukumu yao bila ya kubabaisha. Elimu waliyopewa malaika ni sehemu ndogo sana katika ujuzi wa Allah (SW). Na wenyewe walikiri mbele ya Allah (SW):

﴿قَالُوا سُبْحَانَكَ لَا عِلْمَ لَنَا إِلَّا مَا عَلَّمْتَنَا إِنَّكَ أَنتَ الْعَلِيمُ الْحَكِيمُ﴾

Wakasema: Utukufu ni wako! Hatuna elimu ila ile uliyotufundisha, bila shaka wewe ndiye mjuzi na mwenye hekima (2:32)

HAWANA JINSIA

Malaika hawana jinsia ya kike wala ya kiume.Qur'an inawakosoa watu wanaodhani kuwa malaika ni wanawake. Inahoji:

﴿وَجَعَلُوا الْمَلَائِكَةَ الَّذِينَ هُمْ عِبَادُ الرَّحْمَـٰنِ إِنَاثًا أَشَهِدُوا خَلْقَهُمْ سَتُكْتَبُ شَهَادَتُهُمْ وَيُسْأَلُونَ﴾

Na wamewafanya malaika ambao ni waja wa Mwingi wa Rehma kuwa ni wanawake. Je wameshuhudia kuumbwa kwao (43:19).

NI VIUMBE WENYE MBAWA

﴿الْحَمْدُ لِلَّـهِ فَاطِرِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ جَاعِلِ الْمَلَائِكَةِ رُسُلًا أُولِي أَجْنِحَةٍ مَّثْنَىٰ وَثُلَاثَ وَرُبَاعَ يَزِيدُ فِي الْخَلْقِ مَا يَشَاءُ إِنَّ اللَّـهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ﴾

"Sifa zote njema ni za Allah, Muumba wa mbingu na ardhi.Aliyewafanya malaika kuwa wajumbe wenye mbawa mbili-mbili, na tatu tatu, na nne nne. Huzidisha katika kuumba apendavyo.Bila shaka Allah ni mwenye uweza juu ya kila kitu". (35:1)

HUWEZA KUJIMITHILISHA UMBILE LA MWANADAMU

Malaika huweza kujimithilisha kuwa kama wanadamu. Hufanya hivyo pale wanapotumwa na Allah (SW) kuleta ujumbe kwa watu maalumu. Kwa mfano, Bibi Maryam, mama yake nabii Isa(a.s) , alijiwa na malaika katika umbo mithili ya mwanaume:

﴿وَاذْكُرْ فِي الْكِتَابِ مَرْيَمَ إِذِ انتَبَذَتْ مِنْ أَهْلِهَا مَكَانًا شَرْقِيًّا ﴿١٦﴾ فَاتَّخَذَتْ مِن دُونِهِمْ حِجَابًا فَأَرْسَلْنَا إِلَيْهَا رُوحَنَا فَتَمَثَّلَ لَهَا بَشَرًا سَوِيًّا﴾

Na mtaje katika kitabu, Maryam, alipojitenga na watu wake katika upande wa mashariki. Tukampelekea Muhuisha sharia Yetu (Jibril) akajimithilisha kwake kwa sura ya binaadamu aliye kamilifu. (19:16-17)

LENGO LA KUUMBWA MALAIKA

Lengo la kuumbwa malaika ni kumtumikia Allah(SW). Katika kutekeleza lengo la kuumbwa kwao, malaika hawana hiyari katika kutekeleza amri za Allah(SW), hufanya mambo yote vile anavyotaka Allah(SW).

﴿لَّا يَعْصُونَ اللَّـهَ مَا أَمَرَهُمْ وَيَفْعَلُونَ مَا يُؤْمَرُونَ﴾

..Hawamuasi Allah(SW) katika yale anayowaamuru, na wanatekeleza vile walivyoamrishwa.(66:6)

KAZI ZA MALAIKA

Malaika wamepewa kazi ya kumtumikia Allah(SW) kwa kumtukuza na kumtakasa, kama wanavyosema wenyewe:

﴿وَمَا مِنَّا إِلَّا لَهُ مَقَامٌ مَّعْلُومٌ ﴿١٦٤﴾ وَإِنَّا لَنَحْنُ الصَّافُّونَ ﴿١٦٥﴾ وَإِنَّا لَنَحْنُ الْمُسَبِّحُونَ﴾

Hakuna yoyote miongoni mwetu ila anapo mahali pake mahususi. Na kwa yakini katika sisi wapo wajipangao safu. Na wako katika sisi wamtukuzao (Mwenyezi Mungu) (37:164-166)

MALAIKA PIA HUSHUGHULIKIA MAMBO YA WANADAMU KATIKA MAISHA YA DUNIANI NA AKHERA

Miongoni mwa mambo hayo ni:

(1) KULETA UJUMBE KWA WANAADAMU KUTOKA KWA ALLAH (SW)

Kazi ya kwanza ya malaika ni kuleta ujumbe wa Allah(SW) kwa wanadamu. Ujumbe huo huweza kuwa ni mwongozo wa maisha(Wahy) au habari juu ya jambo fulani. Malaika hupeleka ujumbe wa Allah(SW) kwa mitume au watu wa kawaida. Huteremka Malaika na wahy kwa amri yake juu ya anaowataka katika waja wake kuwa

﴿ أَنْ أَنذِرُوا أَنَّهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا أَنَا فَاتَّقُونِ﴾

"onyeni kuwa hakuna wa kuabudiwa isipokuwa Mimi, basi niogopeni" (16:2)

Jibril, ambaye ndiye mkuu wa Malaika, ndiye mjumbe mkuu aliyekuwa akiwaletea Mitume wote Wahyi. Yeye ni mwalimu mkuu aliyeteuliwa na Allah(SW) kuwafunza mitume namna ya kuwalingania watu Uislamu kwa maneno na matendo.

﴿إِنَّهُ لَقَوْلُ رَسُولٍ كَرِيمٍ ﴿١٩﴾ ذِي قُوَّةٍ عِندَ ذِي الْعَرْشِ مَكِينٍ﴾

Hakika hii Quran ni neno lililoletwa na mjumbe mtukufu, malaika mwenye nguvu na hadhi kubwa kwa Mwenyezi Mungu.(81:19-20)

(2) KUANDIKA AMALI ZA WANAADAMU NJEMA NA MBAYA

Kila mtu ana malaika waandishi wawili, kulia na kushoto kwake. Unaposema au kutenda jema au baya hadharani au umejificha peke yako, malaika hawa wanakuona na kurekodi jambo hilo.

﴿إِذْ يَتَلَقَّى الْمُتَلَقِّيَانِ عَنِ الْيَمِينِ وَعَنِ الشِّمَالِ قَعِيدٌ ﴿١٧﴾ مَّا يَلْفِظُ مِن قَوْلٍ إِلَّا لَدَيْهِ رَقِيبٌ عَتِيدٌ﴾

Wanapopokea wapokeaji wawili, anayekaa kuliani na anayekaa kushotoni. Hatoi (mtu)kauli yoyote isipokuwa karibu naye yupo mngojeaji(malaika) tayari (kuandika.) (50:17-18).

(3) KUWALINDA WANAADAMU

Qur'an inatufahamisha Kazi ya tatu ya malaika ni kumchunga na kumlinda kila mtu na vitu vya hatari vilivyo nje ya uwezo wake.

﴿لَهُ مُعَقِّبَاتٌ مِّن بَيْنِ يَدَيْهِ وَمِنْ خَلْفِهِ يَحْفَظُونَهُ مِنْ أَمْرِ اللَّـهِ إِنَّ اللَّـهَ لَا يُغَيِّرُ مَا بِقَوْمٍ حَتَّىٰ يُغَيِّرُوا مَا بِأَنفُسِهِمْ وَإِذَا أَرَادَ اللَّـهُ بِقَوْمٍ سُوءًا فَلَا مَرَدَّ لَهُ وَمَا لَهُم مِّن دُونِهِ مِن وَالٍ﴾

Ana (kila mtu) kundi (la malaika) mbele yake na nyuma yake. Wanamlinda kwa amri ya Mwenyezi Mungu.Hakika Mwenyezi Mungu habadili yaliyoko nafsini mwa watu mpaka wabadili wao yaliyomo katika nafsi zao. Na Mwenyezi Mungu anapowatakia watu adhabu, hakuna cha kuzuia wala hawana mlinzi yeyote badala yake Mwenyezi Mungu (13:11)

Kwa ulinzi huu wa malaika utokao kwa Allah(SW), mtu hata kama atachukiwa na dunia nzima na kwahiyo wakafanya njama za kutaka kumdhuru, hawataweza mpaka Allah(SW) aondoe ulinzi wake.Vivyo hivyo, kama Allah(SW)atauondoa ulinzi wake huu kwa mtu, hakuna wa kumkinga na shari hata kama atalindwa na mitambo madhubuti ya kisasa pamoja na wataalamu wa ulinzi wa ulimwengu mzima.

(4) KUWAOMBEA WAUMINI MSAMAHA KWA ALLAH (S.W.)

Malaika pia wana kazi ya kumwomba Allah(SW) awasamehe wale watu wanaotubia na kufuatisha vitendo vyema.Humwomba Allah (SW) awasamehe, afute makosa yao, awarehemu kwa kuwalipa pepo na kuwaepusha na adhabu ya Moto.

"Wale wanaokichukua kiti cha enzi (cha Mwenyezi Mungu) na wale wanaokizunguka, wanamtukuza Mola wao na kumsifu na wanamuamini na wanawaombea msamaha waliaomini (Wanasema):

﴿رَبَّنَا وَأَدْخِلْهُمْ جَنَّاتِ عَدْنٍ الَّتِي وَعَدتَّهُمْ وَمَن صَلَحَ مِنْ آبَائِهِمْ وَأَزْوَاجِهِمْ وَذُرِّيَّاتِهِمْ إِنَّكَ أَنتَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ﴾

"Mola wetu! Umekienea kila kitu kwa rehema na Elimu. Basi wasamehe waliotubu na kufuata njia yako na waepushe na adhabu ya Jahannam"(40:8)

Na Mwenyezi Mungu anaahidi kuwa wale wanaotubu kwa kujuta juu ya maovu waliyofanya, wakamuamini Yeye ipasavyo, kwa kujizuia kuyaendea maovu na badala yake wakashikamana na mwenendo mwema; Atabadilisha maovu yao kuwa mema! Qur'an inathibitisha hili katika aya ifuatayo, inasema:

﴿إِلَّا مَن تَابَ وَآمَنَ وَعَمِلَ عَمَلًا صَالِحًا فَأُولَـٰئِكَ يُبَدِّلُ اللَّـهُ سَيِّئَاتِهِمْ حَسَنَاتٍ وَكَانَ اللَّـهُ غَفُورًا رَّحِيمًا﴾

Ila yule atakayetubia na kuamini na kufanya vitendo vizuri; basi hao ndio Mwenyezi Mungu atawabadilishia maovu yao kuwa mema, na mwenyezi Mungu ni mwingi wa kusamehe na Mwingi wa kurehemu.(25:70)

(5) KUWASAIDIA WAUMINI VITANI KATIKA KUPAMBANA NA MADHALIMU

Miongoni mwa kazi tukufu za malaika ni kuwasaidia waislamu kupambana na maadui wenye nguvu kubwa kijeshi katika vita. Qur'an inatueleza kuwa:

﴿بَلَىٰ إِن تَصْبِرُوا وَتَتَّقُوا وَيَأْتُوكُم مِّن فَوْرِهِمْ هَـٰذَا يُمْدِدْكُمْ رَبُّكُم بِخَمْسَةِ آلَافٍ مِّنَ الْمَلَائِكَةِ مُسَوِّمِينَ﴾

Naam.Kama mtasubiri na kujilinda na makatazo yake(Allah) na maadui wakakufikieni kwa ghafla, hapo Mola wenu atakusaidieni kwa Malaika elfu tano washambuliao kwa nguvu(3:125)

(6) KUWAANGAMIZA WATU WAOVU WALIOPINDUKIA MIPAKA

Malaika pia wana kazi ya kuwaangamiza watu waovu waliokubuhu na kupindukia mipaka. Watu wa nabii Lut waliangamizwa na Malaika baada ya kubobea katika maovu na kukataa kwao kujirekebisha. Tunafahamishwa hili pale malaika walipomjibu nabii Ibrahiimu(as) Wakasema:

﴿قَالُوا إِنَّا أُرْسِلْنَا إِلَىٰ قَوْمٍ مُّجْرِمِينَ ﴿٥٨﴾ إِلَّا آلَ لُوطٍ إِنَّا لَمُنَجُّوهُمْ أَجْمَعِينَ﴾

"Hakika sisi tumetumwa kwa wale watu wakosa (tuwaangamize) Isipokuwa waliomfuata Lut.Bila shaka sisi tutawaokoa wote hao (15:58-59)

(7) KUTOA ROHO ZA WATU

Kuna malaika wengi wanaohusika na utoaji wa roho za wanadamu wakati muda wao wa kuishi duniani unapokamilika. Malaika mkuu wa kazi hii ni Malakul-mauti:

﴿قُلْ يَتَوَفَّاكُم مَّلَكُ الْمَوْتِ الَّذِي وُكِّلَ بِكُمْ ثُمَّ إِلَىٰ رَبِّكُمْ تُرْجَعُونَ﴾

Atakufisheni Malaika wa mauti aliyewakilishwa kwenu, kisha mtarejeshwa kwa Mola wenu (32:11)

(8) KUWALIWAZA NA KUWAKARIBISHA WATU WEMA PEPONI KABLA YA KUTOLEWA ROHO

kila mtu aliyetenda mema na kutofanya maovu atashukiwa na malaika wa kumliwaza. Watamwambia:

﴿يَا أَيَّتُهَا النَّفْسُ الْمُطْمَئِنَّةُ ﴿٢٧﴾ ارْجِعِي إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةً مَّرْضِيَّةً ﴿٢٨﴾ فَادْخُلِي فِي عِبَادِي ﴿٢٩﴾ وَادْخُلِي جَنَّتِي﴾

Ewe nafsi yenye kutulia! Rudi kwa Mola wako hali ya kuwa utaridhika Naye amekuridhia. Basi ingia katika kundi la waja (wazuri) uingie katika pepo yangu.(89:27-30).

﴿وَسِيقَ الَّذِينَ اتَّقَوْا رَبَّهُمْ إِلَى الْجَنَّةِ زُمَرًا حَتَّىٰ إِذَا جَاءُوهَا وَفُتِحَتْ أَبْوَابُهَا وَقَالَ لَهُمْ خَزَنَتُهَا سَلَامٌ عَلَيْكُمْ طِبْتُمْ فَادْخُلُوهَا خَالِدِينَ﴾

Na siku ya Kiama watawapokea na kuwakaribisha kwenye pepo ya Allah (SW) yenye neema za kudumu. Watawaambia: Amani juu yenu, furahini, na ingieni humu mkae milele (39:73)

(9) KUWAADHIBU WATU WAOVU MOTONI

Watu wanaotenda maovu watakuwa katika adhabu kali kwenye Moto wa Jahannam. Mwenyezi Mungu amewaweka malaika maalumu kwa ajili ya kuwaadhibu watu waovu wasiotaka kutubia, kujirekebisha wala kutenda mema. Allah (SW) anamtangazia kila mtu mwenya tabia hizi kuwa:

﴿سَأُصْلِيهِ سَقَرَ ﴿٢٦﴾ وَمَا أَدْرَاكَ مَا سَقَرُ ﴿٢٧﴾ لَا تُبْقِي وَلَا تَذَرُ ﴿٢٨﴾ لَوَّاحَةٌ لِّلْبَشَرِ ﴿٢٩﴾ عَلَيْهَا تِسْعَةَ عَشَرَ﴾

Karibuni hivi nitamtia katika Moto.Na ni nini kitakachokujulisha Moto huo? Haubakizi wala hausazi, unababua ngozi mara moja.Juu yake wako malaika (walinzi) kumi na tisa.(74:26-30).

Mkuu wa malaika hawa wa adhabu katika Jahannam ni Malik. Kutokana na machungu ya adhabu watakayopata, watu waovu watalia na kutamani mauti, watamtaka Malik amwombe Allah (SW) awafishe kuliko hiyo adhabu inayowakabili:

﴿ وَنَادَوْا يَا مَالِكُ لِيَقْضِ عَلَيْنَا رَبُّكَ قَالَ إِنَّكُم مَّاكِثُونَ﴾

Nao watapiga kelele: watasema: "Ewe Malik!Na atufishe Mola wako! (Maliki) atasema: "Kwa hakika mtakaa humu humu"(43:77)

Na Mwenyezi Mungu anasifu kuwa adhabu watakayotoa malaika hao kutokana na uwezo aliowapa haitakuwa na mfano wake katika adhabu hizi za duniani.

Siku hiyo mwanadamu atakumbuka, lakini kukumbuka huko kutamfaa nini.Atasema:

﴿وَجِيءَ يَوْمَئِذٍ بِجَهَنَّمَ يَوْمَئِذٍ يَتَذَكَّرُ الْإِنسَانُ وَأَنَّىٰ لَهُ الذِّكْرَىٰ ﴿٢٣﴾يَقُولُ يَا لَيْتَنِي قَدَّمْتُ لِحَيَاتِي ﴿٢٤﴾ فَيَوْمَئِذٍ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُ أَحَدٌ ﴿٢٥﴾ وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُ أَحَدٌ﴾

"Laiti ningalitanguliza(wema) kwa ajili ya uhai wangu (huu wa leo). Basi adhabu ya(Allah) siku hiyo, haitolingana na adhabu aitoayo yeyote (katika wanadamu).Wala hatafunga yeyote jinsi ya kifungo chake (Allah) (89:23-26).

Taathira ya Imani ya Malaika katika maisha ya kila siku Kuamini Malaika ni imani ambayo pindi ikithibiti vema moyoni, huleta taathira kubwa sana katika maisha ya kila siku na hivyo kubadili kabisa tabia na mwenendo wa Muumini. Hii ni kwa sababu:

1. Imani ya kweli juu ya Malaika humuepusha Muumini na kumshirikisha Allah (s.w) na viumbe vyake, hasa vile visivyoonekana, miongoni mwa hivyo ni Malaika na Majini.

2. Muislamu anaamini kuwa Malaika ni viumbe watukufu ambao wametakasika na dhambi na kila aina ya uchafu, lakini binaadamu amepewa daraja ya juu zaidi pindi atakapotimiza wajibu wake kama Khalifa wa Allah (s.w) hapa duniani. Imani hii humpelekea mtu kujitahidi upeo wa uwezo wake kuishi maisha yanayolingana na cheo hiki kikubwa, cheo ambacho Malaika walikitamani (Rejea Qur-an, 2:30)..

3. Muislam anaamini kuwa kila wakati na kila alipo yu pamoja na Malaika watukufu.Imani hii peke yake inatosha kumfanya mtu abadili tabia yake. Hii ni kwa sababu binaadamu ameumbwa na haya, kwa hiyo huhuzunika akifanya mambo maovu mbele ya watu na hasa mbele ya watu anaowaheshimu.

4. Muislamu anaamini kuwa Malaika hao sio tu kuwa wapo naye daima bali wanahudhurisha mbele ya Allah (s.w) kila anachokitenda. Imani hii ikithibiti moyoni humfanya Muislam ajitahidi kufanya mambo mema na ajitahidi kuepuka maovu.

5. Muislamu anajua kuwa Malaika sio tu hupendezwa na mema, bali pia humuombea mtu huyo anayefanya mema, maghfira kwa Allah (s.w) jambo ambalo humzidishia Muislamu hima ya kutenda mema daima na kujiepusha na maovu hata akiwa peke yake.

KUAMINI VITABU VYA ALLAH (S.W)

Mtu hawi Muumini wa kweli mpaka awe na yakini juu ya vitabu vya Allah (s.w). Vitabu vya Allah (s.w) vimeshushwa kupitia kwa Mitume mbali mbali.

﴿لَقَدْ أَرْسَلْنَا رُسُلَنَا بِالْبَيِّنَاتِ وَأَنزَلْنَا مَعَهُمُ الْكِتَابَ وَالْمِيزَانَ لِيَقُومَ النَّاسُ بِالْقِسْطِ﴾

"Kwa hakika tuliwapeleka Mitume wetu kwa dalili wazi wazi na tukaviteremsha Vitabu na uadilifu pamoja nao, ili watu wasimamie uadilifu..." (57:25).

Vitabu vya Allah (s.w) ni vingi lakini tunavyovifahamu ni vile vilivyotajwa katika Qur-an kama ifuatavyo:

(1) Suhufi kwa Ibrahimu(a.s)

(2) Taurati kwa Mussa(a.s)

(3) Zabri kwa Daud(a.s)

(4) Injili kwa Issa(a.s)

(5) Qur-an kwa Muhammad(s.a.w.w)

Lengo la kushushwa Vitabu vya Allah (s.w) Iimebainishwa wazi katika Qur-an kuwa vitabu vya Allah (s.w) vimeshushwa kupitia kwa Mitume wake ili kuwaongoza wanaadamu katika njia iliyonyooka. Njia iliyonyooka ni ile inayomuwezesha mwanaadamu kumuabudu Allah (s.w) katika kila kipengele cha maisha yake kwa kipindi chote cha uhai wake hapa ulimwenguni. Allah (s.w) amechukua ahadi ya kuwaletea watu mwongozo tangu awali pale alipowashusha wazazi wetu, Adamu(a.s) na mkewe (Hawwah) hapa ardhini kama tunavyojifunza katika Qur-an:

﴿قُلْنَا اهْبِطُوا مِنْهَا جَمِيعًا فَإِمَّا يَأْتِيَنَّكُم مِّنِّي هُدًى فَمَن تَبِعَ هُدَايَ فَلَا خَوْفٌ عَلَيْهِمْ وَلَا هُمْ يَحْزَنُونَ ﴿٣٨﴾ وَالَّذِينَ كَفَرُوا وَكَذَّبُوا بِآيَاتِنَا أُولَـٰئِكَ أَصْحَابُ النَّارِ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ﴾

"Tukasema, shukeni humo nyote, na kama ukikufikieni uwongozi utokao kwangu, basi watakaoufuata uwongozi wangu huo haitakuwa hofu juu yao wala hawatahuzunika. Lakini wenye kukufuru na kuyakadhibisha maneno yetu, hao ndio watakaokuwa watu wa Motoni, humo watakaa milele". (2:38-39).

Ahadi hii ameitekeleza Allah (s.w) kwa kuwaleta Mitume mbali mbali baada ya Adamu (a.s) na kuwashushia vitabu vyenye Uongozi na nuru. Qur-an inasisitiza:

﴿إِنَّا أَنزَلْنَا التَّوْرَاةَ فِيهَا هُدًى وَنُورٌ﴾

"Hakika tuliteremsha Taurat yenye Uongozi na Nuru.." (5:44)

﴿وَقَفَّيْنَا عَلَىٰ آثَارِهِم بِعِيسَى ابْنِ مَرْيَمَ مُصَدِّقًا لِّمَا بَيْنَ يَدَيْهِ مِنَ التَّوْرَاةِ وَآتَيْنَاهُ الْإِنجِيلَ فِيهِ هُدًى وَنُورٌ﴾

"Na tukawafuatishia (Mitume hao) Issa bin Maryam kuyahakikisha yaliyokuwa kabla yake katika Taurat, na tukampa Injili iliyomo ndani yake Uongozi na nuru." (5:46)

﴿شَهْرُ رَمَضَانَ الَّذِي أُنزِلَ فِيهِ الْقُرْآنُ هُدًى لِّلنَّاسِ وَبَيِّنَاتٍ مِّنَ الْهُدَىٰ وَالْفُرْقَانِ﴾

"Ni mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa katika (mwezi) huo (hii) Qur-an ili iwe Uongozi kwa watu na hoja zilizo wazi za Uongozi wa upambanuizi..." (2:185)

Haja ya Mwongozo kutoka kwa Allah (s.w) Mwanaadamu pamoja na elimu aliyotunukiwa, hana uwezo pasina msaada wa muumba wake, kupata majibu sahihi ya maswali ya msingi ya maisha yake hapa duniani na huko akhera. Maswali haya ya msingi ni:

1. Nani chanzo cha maumbile yote?

2. Ni lipi lengo la mwanaadamu hapa ulimwenguni?

3. Atalifikiaje lengo hilo?

4. Ni ipi nafasi halisi ya mwanaadamu hapa ulimwenguni?

5. Ni ipi hatma yake baada ya kufa, je kufa ndio mwisho wa maisha yake?

Mwanaadamu bila ya mwongozo kutoka kwa muumba wake hana uwezo wa kutoa majibu sahihi ya maswali haya. Elimu ya mazingira aliyonayo mwanaadamu ni finyu mno kiasi kwamba haimuwezeshi hata kuijua roho yake kama tunavyokumbushwa katika Qur-an:

﴿وَيَسْأَلُونَكَ عَنِ الرُّوحِ قُلِ الرُّوحُ مِنْ أَمْرِ رَبِّي وَمَا أُوتِيتُم مِّنَ الْعِلْمِ إِلَّا قَلِيلًا﴾

"Na wanakuuliza habari ya roho.Sema: "Roho ni jambo lililohusika na Mola wangu. Nanyi hamkupewa katika elimu ila kidogo kabisa" (17:85)

Maana ya Kuamini Vitabu vya Allah Imani ya kweli katika Uislamu haishii moyoni tu bali ni lazima idhihirishwe katika matendo ya kila siku. Hivyo, waumini wa kweli wa vitabu vya Allah (s.w) ni wale wanaoendesha maisha yao ya kila siku katika kila kipengele kwa kufuata bara bara maongozi ya vitabu vya Allah (s.w). Kabla ya Qur-an kushushwa, waumini wa kweli wa vitabu vya Allah vilivyotangulia, vikiwemo Taurat, Injili, Zaburi, n.k. ni wale walioishi kwa mujibu wa maongozi ya vitabu hivyo kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:

﴿إِنَّا أَنزَلْنَا التَّوْرَاةَ فِيهَا هُدًى وَنُورٌ يَحْكُمُ بِهَا النَّبِيُّونَ الَّذِينَ أَسْلَمُوا لِلَّذِينَ هَادُوا وَالرَّبَّانِيُّونَ وَالْأَحْبَارُ بِمَا اسْتُحْفِظُوا مِن كِتَابِ اللَّـهِ وَكَانُوا عَلَيْهِ شُهَدَاءَ فَلَا تَخْشَوُا النَّاسَ وَاخْشَوْنِ وَلَا تَشْتَرُوا بِآيَاتِي ثَمَنًا قَلِيلًا وَمَن لَّمْ يَحْكُم بِمَا أَنزَلَ اللَّـهُ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْكَافِرُونَ﴾

"Hakika tuliteremsha Taurati yenye uwongozi na nuru; ambayo kwayo Manabii waliojisalimisha (kwa Allah) waliwahukumu Mayahudi; Watawa na Maulamaa pia (walihukumu kwa hiyo Taurat); kwa sababu walitakiwa kuhifadhi kitabu hicho cha Allah; Nao walikuwa mashahidi juu yake. Basi, msiwaogope watu, bali niogopeni (Mimi). Wala msibadilishe Aya zangu kwa thamani chache (ya maslahi ya dunia).Na wasiohukumu kwa yale aliyoteremsha Allah, basi Hao ndio makafiri." (5:44)

﴿وَلْيَحْكُمْ أَهْلُ الْإِنجِيلِ بِمَا أَنزَلَ اللَّـهُ فِيهِ وَمَن لَّمْ يَحْكُم بِمَا أَنزَلَ اللَّـهُ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْفَاسِقُونَ﴾

"Watu wa Injili wahukumu kwa yale aliyoteremsha Allah ndani yake.Na wasiohukumu kwa (kufuata) yale aliyoteremsha Allah, basi hao ndio mafasiki (maasi)" (5:47)

Baada ya Qur-an kushushwa kupitia kwa Mtume Muhammad(s.a.w.w) kwa ajili ya walimwengu wote, Waumini wa kweli wa vitabu vya Allah (s.w) ni wale wanaoishi kwa kufuata maongozi ya Qur-an na Sunnah ya Mtume Muhammad(s.a.w.w) katika maisha yao yote. Si muumini yule anayeikataa Qur-an na Mtume aliyeshushiwa hatakama anadai kuwa anaiamini Taurat, Zabur, Injili, n.k. na Mitume walioshushiwa vitabu hivyo kwa mujibu wa aya ifuatayo:

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا آمِنُوا بِاللَّـهِ وَرَسُولِهِ وَالْكِتَابِ الَّذِي نَزَّلَ عَلَىٰ رَسُولِهِ وَالْكِتَابِ الَّذِي أَنزَلَ مِن قَبْلُ وَمَن يَكْفُرْ بِاللَّـهِ وَمَلَائِكَتِهِ وَكُتُبِهِ وَرُسُلِهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ فَقَدْ ضَلَّ ضَلَالًا بَعِيدًا﴾

"Enyi mlioamini! Mwaminini Allah na Mtume wake na kitabu alichokiteremsha juu ya Mtume wake,na vitabu alivyoviteremsha zamani. Na mwenye kumkanusha Allah na Malaika wake na vitabu vyake, na Mitume wake na siku ya mwisho, basi bila shaka amepotea upotofu uliombali (na haki)" (4:136)

Hivi sasa, katika vitabu vya Allah (s.w) vilivyoshushwa hapa ulimwenguni, ni Qur-an pekee iliyobakia katika lugha yake ya asili (Kiarabu fasaha) na katika usahihi wake wa asili. Vitabu vilivyoitangulia Qur-an vinakabiliwa na matatizo makubwa mawili yafuatayo:

1. Lugha zilizotumika katika vitabu hivyo zimekufa (zimetoweka). Kwa mujibu wa Qur-an kila Mtume alilepewa wahay kwa lugha ya watu wake

﴿وَمَا أَرْسَلْنَا مِن رَّسُولٍ إِلَّا بِلِسَانِ قَوْمِهِ لِيُبَيِّنَ لَهُمْ﴾

"Na hatukumpeleka Mtume yeyote isipokuwa kwa lugha ya watu wake ili apate kuwabainishia..." (14:4).

Tunajua kutokana na historia kuwa lugha hukua na kufa. Hivi sasa kwa mfano Allah (s.w) akituletea kitabu alichoshushiwa Nabii Adam(a.s) katika lugha aliyozungumza Adam(a.s) na wanawe wa karibu wa wakati ule, hatuwezi kupata ujumbe wake.

2. Vitabu vilivyoitangulia Qur-an viliingizwa mikono ya watu, vikabadilishwa na kupotoshwa ili kukidhi matashi ya watu waliodai kufuata vitabu hivyo kinyume na Allah (s.w). Taurat, Zabur, Injili, n.k. Vilikumbwa na tatizo hili.

Qur-an imeepukana na matatizo haya kwani hivi leo, Lugha ya Kiarabu, ni miongoni mwa lugha kubwa zinazokua kwa kasi; pia Kiarabu ni lugha fasaha na tajiri kwa maneno kuliko lugha zote duniani. Pia Qur-an tofauti na vitabu vingine vya Allah (s.w), haitaingiliwa na mkono wa mtu, kwani imepewa hifadhi na Allah (s.w) mwenyewe:

﴿نَّا نَحْنُ نَزَّلْنَا الذِّكْرَ وَإِنَّا لَهُ لَحَافِظُونَ﴾

Hakika sisi ndio tulioteremsha mawaidha haya (hii Qur-an) na hakika Sisi ndio tutakao yalinda" (15:9).

﴿لَّا يَأْتِيهِ الْبَاطِلُ مِن بَيْنِ يَدَيْهِ وَلَا مِنْ خَلْفِهِ تَنزِيلٌ مِّنْ حَكِيمٍ حَمِيدٍ﴾

"Haitakifikia batili mbele yake wala nyumba yake; kimeteremshwa na Mwenye Hikma Ahimidiwaye." (41:42).

Hivyo hivi sasa, Muumini wa kweli wa vitabu vya Allah (s.w) ni yule:

1. Anayeamini pasi na tone la shaka kuwa Qur-an yote kama msahafu ulivyo kuanzia sura ya kwanza (Al-Faatiha) mpaka sura ya mwisho (An-Naas) ni maneno kutoka kwa Allah (s.w). Muumini anayakinisha kuwa:

﴿ذَٰلِكَ الْكِتَابُ لَا رَيْبَ فِيهِ هُدًى لِّلْمُتَّقِينَ﴾

"Hiki ni kitabu kisichokuwa na shaka ndani yake, ni uwongozi kwa wamchao Allah" (2:2)

2. Anayaongoza maisha yake ya kila siku kwa kufuata Qur'an na mwenendo au sunnah ya mfasiri wa Qur-an, Mtume Muhammad(s.a.w.w). Qur-an yenyewe inasisitiza:

﴿وَمَا كَانَ لِمُؤْمِنٍ وَلَا مُؤْمِنَةٍ إِذَا قَضَى اللَّـهُ وَرَسُولُهُ أَمْرًا أَن يَكُونَ لَهُمُ الْخِيَرَةُ مِنْ أَمْرِهِمْ وَمَن يَعْصِ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ فَقَدْ ضَلَّ ضَلَالًا مُّبِينًا﴾

"Haiwi kwa mwanamume aliyeamini wala kwa mwanamke aliyeamini, Mwenyezi Mungu na Mtume wake wanapokata shauri, wawe na hiari katika shauri lao. Na mwenye kumuasi Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hakika amepotea upotofu ulio wazi (kabisa)." (33:36)

﴿وَمَن لَّمْ يَحْكُم بِمَا أَنزَلَ اللَّـهُ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْكَافِرُونَ﴾

"...Na wasiohukumu kwa yale aliyoteremsha Mwenyezi Mungu, basi hao ndio makafiri". (5:44)

﴿وَمَن لَّمْ يَحْكُم بِمَا أَنزَلَ اللَّـهُ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ﴾

"... Na wasiohukumu kwa yale aliyoteremsha Mwenyezi Mungu, basi hao ndio madhalimu" (5:45) lengo-2 166 1/18/10, 12:28 PM 167

﴿وَمَن لَّمْ يَحْكُم بِمَا أَنزَلَ اللَّـهُ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْفَاسِقُونَ﴾

"... Na wasiohukumu kwa yale aliyoteremsha Mwenyezi Mungu, basi hao ndio mafasiki (maasi)" (5:47)

KUAMINI MITUME WA ALLAH (S.W)

Mtu hawi Muumini wa kweli mpaka awe na yakini juu ya Mitume wa Allah (s.w) kama tunavyojifunza katika Qur-an: "Semeni nyinyi (Waislamu kuwaambia Mayahudi na Wakristo kuwa):"Tumemwamini Mwenyezi Mungu na yale tuliyoteremshiwa, na yale yaliyoteremshwa kwa Ibrahimu, na Ismail na Is-haqa na Yaaqubu na kizazi (chake Yaaqubu); na waliyopewa Manabii (wengine) kutoka kwa Mola wao; hatutafautishi baina ya yoyote katika hao.(Wote tunawaamini), na sisi tumenyenyekea kwake." (2:136) Kuamini baadhi ya Mitume wa Mwenyezi Mungu na kuwakanusha wengine kama walivyo fanya mayahudi na Wakristo ni Ukafiri kama tunavyojifunza katika Qur-an:

﴿إِنَّ الَّذِينَ يَكْفُرُونَ بِاللَّـهِ وَرُسُلِهِ وَيُرِيدُونَ أَن يُفَرِّقُوا بَيْنَ اللَّـهِ وَرُسُلِهِ وَيَقُولُونَ نُؤْمِنُ بِبَعْضٍ وَنَكْفُرُ بِبَعْضٍ وَيُرِيدُونَ أَن يَتَّخِذُوا بَيْنَ ذَٰلِكَ سَبِيلًا ﴿١٥٠﴾ أُولَـٰئِكَ هُمُ الْكَافِرُونَ حَقًّا وَأَعْتَدْنَا لِلْكَافِرِينَ عَذَابًا مُّهِينًا ﴿١٥١﴾ وَالَّذِينَ آمَنُوا بِاللَّـهِ وَرُسُلِهِ وَلَمْ يُفَرِّقُوا بَيْنَ أَحَدٍ مِّنْهُمْ أُولَـٰئِكَ سَوْفَ يُؤْتِيهِمْ أُجُورَهُمْ وَكَانَ اللَّـهُ غَفُورًا رَّحِيمًا﴾

"Hakika wale wanaomkanusha Mwenyezi Mungu na Mitume yake, na wanataka kutenga baina ya Mwenyezi Mungu na Mitume yake, kwa kusema: "Wengine tunawaamini na wengine tunawakataa," na wanataka kushika njia iliyo kati kati ya haya (si ya Kiislamu khasa wala ya Kikafiri).Hao ndio Makafiri kweli.Na tumewaandalia makafiri adhabu idhalilishayo.Na waliomwamini Mwenyezi Mungu na Mitume yake wala wasimfarikishe yoyote katika wao (bali wamewaamini wote), hao atawapa ujira wao.Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe (na) Mwingi wa kurehemu." (4:150-152).

Mitume wa Allah (s.w) ni wengi sana kama inavyobainishwa katika Qur-an:

﴿وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا رُسُلًا مِّن قَبْلِكَ مِنْهُم مَّن قَصَصْنَا عَلَيْكَ وَمِنْهُم مَّن لَّمْ نَقْصُصْ عَلَيْكَ﴾

"Na kwa yakini tuliwatuma mitume kabla yako (Muhammad).Wengine katika hao tumekusimulia (majina yao na habari zao) na wengine hatukukusimulia..." (40:78)

Mitume waliosimuliwa katika Qur-an ni hawa ishirini na tano (25) wafuatao:

1. Adam(a.s)

2. Idrisa (Enock)(a.s)

3. Nuhu (Noah)(a.s)

4. Hud (Heber)(a.s)

5. Salih (Metheusaleh)(a.s)

6. Ibrahim (Abrahim)(a.s)

7. Lut (Lot) (a.s)

8. Ismail (Ismael)(a.s)

9. Is-haq (Isaac)(a.s)

10. Yaaqub (Jacob)(a.s)

11. Yusuf (Joseph)(a.s)

12. Shu'aib (Jethro)(a.s)

13. Ayyub (Job)(a.s)

14. Mussa (Moses)(a.s)

15. Harun (Aaron)(a.s)

16. Dhul kifl (Ezekiel)(a.s)

17. Daud ( David)(a.s)

18. Sulayman (Solomon)(a.s)

19. Ilyaas (Elias)(a.s)

20. Al - Yassa' (Elisha)(a.s)

21. Yunus (Johah)(a.s)

22. Zakariya (Zechariah)(a.s)

23. Yahya (John the Baptist)(a.s)

24. Isa (Jesus)(a.s)

25. Muhammad(s.a.w.w)

LENGO LA KULETWA MITUME WA ALLAH (S.W)

Mitume wameletwa kuwa Waalimu na viongozi wa kuwafundisha watu Uislamu na kuwaelekeza kuusimamisha Uislamu katika jamii kinadharia na kimatendo kama tunavyojifunza katika Qur-an:

﴿ لَقَدْ أَرْسَلْنَا رُسُلَنَا بِالْبَيِّنَاتِ وَأَنزَلْنَا مَعَهُمُ الْكِتَابَ وَالْمِيزَانَ لِيَقُومَ النَّاسُ بِالْقِسْطِ﴾

"Kwa hakika Tuliwapeleka Mitume wetu kwa dalili wazi wazi na Tukaviteremsha vitabu na Uadilifu (mizani) pamoja nao, ili watu wasimamie uadilifu. (57:25)

﴿ هُوَ الَّذِي أَرْسَلَ رَسُولَهُ بِالْهُدَىٰ وَدِينِ الْحَقِّ لِيُظْهِرَهُ عَلَى الدِّينِ كُلِّهِ وَلَوْ كَرِهَ الْمُشْرِكُونَ﴾

"Yeye ndiye aliyemtuma Mtume wake kwa uongofu na kwa dini ya haki ili kuifanya ishinde dini zote, ijapokuwa washirikina watachukia." (9:33, 61:9)

MWISHO WA UTUME

Maswali ambayo huweza kuulizwa ni: Kwa nini wahyi ukatike?Kwa nini Mitume wasiendelee kuletwa hadi kiyama? Kwa nini Muhammad(s.a.w.w) afunge mlango wa Utume? Ili kulielewa vizuri suala hili la mwisho wa Utume yafaa kwanza tuzingatie kuwa kilicho muhimu na cha msingi kabisa kwa Mtume yeyote si kule kuwepo kimwili bali ni kule kuufikisha kwake ujumbe aliopewa na Mwenyezi Mungu (s.w) ili watu wake wasiwe na hoja tena iwapo watachagua kupotea. Na lau ingekuwa lililo muhimu kwa Mtume ni kule kuwapo kimwili basi Mwenyezi Mungu angelimpeleka Mtume mara tu baada ya kufariki Mtume aliyetangulia.

Kilicho cha msingi ni mafundisho aliyokuja nayo.Maadamu ujumbe aliouleta uko hai basi Mtume huyo yu hai. Hivyo kifo halisi cha Mtume ni kule kupotea kwa mafundisho aliyoyaleta. Mitume wote waliomtangulia Muhammad(s.a.w.w) mafundisho yao yalipotea, kwani yalichanganyika na hekaya mbali mbali. Katika vitabu vilivyoitangulia Qur-an, kwa mfano Taurat, Injil, na Zaburi hakuna hata kimoja ambacho kipo katika hali ya usahihi wake wa asili. Hata wafuasi wa vitabu hivyo wanakiri kuwa nakala walizonazo leo si zile walizopewa Mitume. Si hivyo tu bali hata historia za maisha ya Mitume waliomtangulia Muhammad(s.a.w.w) zimechanganywa na ngano za kushtusha kabisa, hata inakuwa vigumu kupambanua haki na batili.

Kinyume chake mafundisho aliyokuja nayo Muhammad(s.a.w.w) yako hai kabisa na hayajaharibiwa na katu hayawezi kuharibiwa.Qur-an, kitabu alichoteremshiwa kipo tena katika lugha ile ile ya asili bila ya kupunguza wala kuzidisha japo nukta moja. Historia kamili ya maisha yake, maneno yake, maagizo yake, vitendo vyake, vyote vimehifadhiwa kwa usahihi kabisa kiasi ambacho karne 14 zimepita lakini bado historia yake ni ya wazi na kamili kama kwamba tunamuona kwa macho yetu. Katika kila kipengele cha maisha yetu tunaweza kupata muongozo na mafundisho kutoka kwa Muhammad(s.a.w.w) . hii ndio sababu hakuna haja ya kuletwa Mtume mwingine baada yake.

Zaidi ya hayo yapo mambo matatu ambayo husababisha kuhitajika kuja kwa Mtume mwengine baada ya yule aliyetangulia:

(1) Iwapo mafundisho ya Mtume aliyetangulia yamechanganywa na hekaya za nzushi, kuharibiwa na kupotea. Katika hali kama hiyo Mtume anahitajika ili aje aifundishe dini katika usahihi wake wa awali.

(2) Iwapo mafundisho ya Mtume aliyeondoka hayakukamilika na hivyo kukawa na haja ya kuyakamilisha, kuyarekebisha, au kuongeza jambo fulani.

(3) Iwapo Mtume aliyetangulia alipelekwa kwa watu wa taifa fulani maalum au nchi fulani maalum na hivyo kuwepo haja ya kuletwa Mtume kwa watu wa taifa au nchi nyingine. Au pengine Mtume anaweza kuletwa ili amsaidie Mtume mwingine, lakini kwa kuwa hii si kanuni ya kawaida, hatujaita kama sharti la nne. Katika Qur-an ipo mifano miwili ya hali kama hiyo. Nabii Haruni(a.s) alikuwa msaidizi wa Nabii Musa(a.s) . Nabii Lut (a.s) Ismail(a.s) na Is-haq(a.s) walikuwa wasaidizi wa Nabii Ibrahim(a.s).

Haya matatu ndiyo masharti makuu ya kimsingi yanayohitajika ili aletwe Mtume mwingine. Kati ya hayo hakuna hata sharti moja lililopo leo.

Kwanza : mafundisho ya Mtume wa mwisho, Muhammad(s.a.w.w) yako hai, yamehifadhiwa na yatadumu hadi siku ya Kiyama. Mwongozo aliouleta kwa walimwengu wote ni sahihi na kamili na umehifadhiwa katika Qur-an humo kuna ahadi ya ulinzi wa Allah (s.w) kama tunavyofahamishwa:

﴿نَّا نَحْنُ نَزَّلْنَا الذِّكْرَ وَإِنَّا لَهُ لَحَافِظُونَ﴾

"Hakika sisi ndio tulioteremsha mawaidha (haya hii Qur-an); na Hakika sisi ndio tutakaoyalinda." (15:9).

Pia sunnah zake zimehifadhiwa kikamilifu kiasi ambacho mtu anaweza kujua pasi na shaka yoyote nini mafundisho ya Mtume juu ya jambo fulani.Hivyo sharti la kwanza linaondoka.

Pili : Mwenyezi Mungu amekamilisha mwongozo wake kwa Nabii Muhammad(s.a.w.w) na hivyo Uislamu ni dini kamilifu kwa ulimwengu wote. Allah (s.w) anasema katika Qur-an:

﴿الْيَوْمَ أَكْمَلْتُ لَكُمْ دِينَكُمْ وَأَتْمَمْتُ عَلَيْكُمْ نِعْمَتِي وَرَضِيتُ لَكُمُ الْإِسْلَامَ دِينًا ﴾

"Leo nimekukamilishieni dini yenu, na kukutimizieni neema yangu juu yangu na nimekupendeleeni Uislamu uwe dini yenu (5:3)

Na tukiutafiti Uislamu kwa makini kama mfumo kam ili wa maisha tunaona unadhihiri ukweli wa aya hii ya Qur-an. Uislamu unatoa mwongozo wa maisha haya na ya akhera na hakuna jambo lililo muhimu katika kumuongoza mwanaadamu lisilokuwemo katika mwongozo aliokuja nao Muhammad(s.a.w.w) . Hivyo hoja ya kuhitaji Mtume ili aje kukamilisha dini pia inaondoka. Hata hivyo kuna baadhi ya watu wanaosema kwamba kupita tu kwa muda mrefu ni sababu ya kuhitaji Mtume mwingine. Hii ni kwa sababu wanasema mwongozo ulioletwa karne 14 zilizopita ni wa kale mno kiasi kwamba hauwezi kukidhi mahitaji ya watu wa leo. Mawazo haya hayana msingi kabisa, kwa sababu zifuatazo:

(i) Mafunzo ya Uislamu ni ya milele, kwa sababu ni ufunuo utokao kwa Mwenyezi Mungu mjuzi wa yote ya kale, ya sasa na yajayo, tena basi mwenye uhai wa milele. Elimu ya binaadamu ndiyo yenye ukomo, na ni jicho la binaadamu ambalo haliwezi kuona hata kesho achilia mbali miaka milioni mmoja ijayo. Elimu na hikima ya Mwenyezi Mungu imesalimika na upungufu kama huo.

(ii) Uislamu umeegemeza mafundisho yake juu ya umbile la binaadamu. Na umbile la binaadamu limesalia vile vile katika zama zote. Watu wote wamejengwa kwa majengo yale yale yaliyowajenga watu wa kale kabisa na hivyo umbile lao kimsingi ni lilelile.

(iii) Katika maisha ya binaadamu kuna mizani inayoridhisha kabisa baina ya mambo yanayodumu na mambo yanayobadilika. Misingi muhimu na maadili makuu hayabadiliki na sura ya nje ndiyo inayoweza kubadilika kutokana na kupita kwa muda. Qur-an na sunna zinatoa kanuni au misingi ya kudumu na kwa kutumia ijitihadi misingi hiyo inaweza kutekelezwa kadri hali itakavyobadilika. Uislamu ndio dini pekee iliyoweka utaratibu madhubuti unaoweza kuoanisha maendeleo ya binaadamu na misingi ya Kitabu cha Allah (s.w) na Sunnah ya Mtume wake Muhammad(s.a.w.w).

Na tukirudi katika lile sharti letu la tatu kuhitajia kuletwa Mtume mwingine, tunaona kuwa Muhammad(s.a.w.w) hakuletwa kwa taifa au watu maalum bali kwa walimwengu wote. Qur-an inasema:

﴿قُلْ يَا أَيُّهَا النَّاسُ إِنِّي رَسُولُ اللَّـهِ إِلَيْكُمْ جَمِيعًا﴾

"Sema (Ewe Nabii Muhammad): "Enyi watu! Hakika mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu nyinyi nyote". (7:158)

﴿وَمَا أَرْسَلْنَاكَ إِلَّا رَحْمَةً لِّلْعَالَمِينَ﴾

"Nasi hatukukutuma ila uwe rehema kwa walimwengu wote" (21:107)

Labda itaulizwa: Kwanini Mtume Muhammad(s.a.w.w) awe Mtume wa walimwengu wote? Ama kuhusu suali hili, hapana jibu lolote lililotolewa katika Qur-an wala katika hadithi za Mtume(s.a.w.w) . Hivyo ni Allah (s.w) pekee anayejua ni kwanini alimleta kwa ulimwengu mzima. Lakini tunaweza kutumia akili zetu finyu tukajaribu kuona hikima iliyopo kwa Mtume(s.a.w.w) kuwa Mtume wa ulimwengu mzima jambo ambalo halikuwezekana kwa Mitume waliotangulia. Hapo awali, kabla ya Mtume(s.a.w.w) , Mitume walikuwa wakitokea kwa kila nchi au kila taifa. Sababu ya msingi tunayoweza kuona kirahisi ni kwamba katika wakati huo wa historia njia za usafiri na mawasiliano yalikuwa finyu sana kwa kiasi ambacho mawasiliano kati ya watu na nchi moja na nyingine yalikosekana kabisa. Kila nchi au ukanda wa jiografia ulikuwa ni ulimwengu wa peke yake.

Katika hali hii ilikuwa ni vigumu mno kuwa na Mtume mmoja kwa ulimwengu wote. Ndio tunakuta kila nchi au kila ukanda wa jiografia ukatumiwa Mtume wake. Sote tunashuhudia kuwa katika umma huu wa mwisho wa Mtume Muhammad(s.a.w.w) pamekuwa na maendeleo makubwa sana ya mawasiliano kiasi kwamba dunia inakuwa kama kijiji. Suala la "Globalization" (utandawazi) kwa Waislamu sijambo geni. Tunafahamishwa katika Qur-an kuwa umma huu wa Mtume Muhammad(s.a.w.w) ni umma mmoja na unawajibika kuufanya Uislamu utawale ulimwengu mzima.

Kutokana na hoja hizi tatu itaonekana wazi ni kwanini hakuna haja ya Mtume mwingine baada ya Muhammad(s.a.w.w) . Na ndivyo Allah (s.w) anavyotufahamisha katika Qur-an kuwa yeye Muhammad(s.a.w.w) ni "Khataman-Nabiyyina" - yaani mwisho wa Mitume:

﴿مَّا كَانَ مُحَمَّدٌ أَبَا أَحَدٍ مِّن رِّجَالِكُمْ وَلَـٰكِن رَّسُولَ اللَّـهِ وَخَاتَمَ النَّبِيِّينَ وَكَانَ اللَّـهُ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمًا ﴾

Muhammad si baba wa yeyote katika wanaume wenu, bali yeye ni Mtume wa Allah na mwisho wa Mitume na Allah ni mjuzi wa kila kitu. (33:40)

Na Mtume Muhammad(s.a.w.w) mwenyewe pia anasema:

Palikuwa na Mitume waliowaongoza Banii Israil katika njia sahihi. Kila Mtume alipokufa, alifuatiwa na Mtume mwingine. Lakini hapana Mtume atakayekuja baada yangu.Kazi hii (ya kuufundisha Uislamu na kuusimamisha) inaweza kufanywa na makhalifa (viongozi wa Kiislamu). (Bukhari)

Na katika Hadithi nyengine Mtume(s.a.w.w) amesema:

"Uhusiano wangu na (msururu mrefu) wa Mitume unaweza kueleweka vizuri kwa mfano wa nyumba nzuri ya kifalme. Nyumba hii ikawa imejengwa vizuri sana na ikawa inapendeza lakini pakawa na nafasi moja iliyobakia. Watu wakawa wanaizungumza nyumba hii nzuri na wakawa wanauliza kwa mshangao.Kwanini hii sehemu isiwe imejazwa! Nimejaza pengo hili na ni Mtume wa mwisho". (Bukhari)

Mitume wa Uongo Wafuatao ni baadhi ya wale waliodai utume wakati Mtume (s.a.w) akiwepo na baada yake. Aswad Aus: Alijitangazia Utume wakati wa Mtume(s.a.w.w) na aliuawa kwa amri ya Mtume mwenyewe.

Musailama (Al-kadhaab) Alijitangazia Utume wakati wa Abubakari (Khalifa wa kwanza wa Mtume(s.a.w.w) . Waislamu walimpiga vita na kumuua. Bahau'lla Alijitokeza huko Iran katika karne ya 19 na aliuawa na Waisalmu.

Mirza Gulam Ahmed Alizaliwa huko India katika kitongoji cha Kadiani katika karne ya 19. Japo alilindwa na serikali ya Kikoloni ya Kiingereza, alipigwa vita na Waislamu kwa maneno na kalamu mpaka uwongo wake ukawa dhahiri kwa waislamu pamoja na kutumia kwake Qur-an hii wanayoifuata Waislamu. Pia kwa kukosekana mtu aliyekuja na kitabu cha mwongozo kinachofanana na Qur'an angalau kwa mbali, inazidi kutudhibitishia kuwa Mtume Muhammad(s.a.w.w) ni Mtume wa mwisho na Qur'an ni ujumbe wa mwisho wa Allah (s.w) utakaobakia mpaka mwisho wa ulimwengu. Maana ya Kuamini Mitume wa Allah (s.w) katika maisha ya kila siku.

Waumini wa kweli wa Mitume wa Allah (s.w) ni wale wenye tabia ifuatayo:

1. Kuwatii Mitume ipasavyo kwa kufanya yale yote waliyoamrisha na kuacha yale yote waliyoyakataza kama Qur'an inavyosisitiza:

﴿وَمَا آتَاكُمُ الرَّسُولُ فَخُذُوهُ وَمَا نَهَاكُمْ عَنْهُ فَانتَهُوا﴾

"... Na anachokupeni Mtume basi pokeeni, na anachokukatazeni jiepusheni nacho..." (59:7)

﴿قُلْ إِن كُنتُمْ تُحِبُّونَ اللَّـهَ فَاتَّبِعُونِي يُحْبِبْكُمُ اللَّـهُ وَيَغْفِرْ لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ وَاللَّـهُ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿٣١﴾ قُلْ أَطِيعُوا اللَّـهَ وَالرَّسُولَ فَإِن تَوَلَّوْا فَإِنَّ اللَّـهَ لَا يُحِبُّ الْكَافِرِينَ ﴾

Sema: "Ikiwa nyinyi mnampenda Mwenyezi Mungu, basi nifuateni; (hapo)Mwenyezi Mungu atakupendeni na atakughufirieni madhambi yenu.Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye maghufira, mwenye rehema. Sema: "Mtiini Mwenyezi Mungu na Mtume. Na kama mkikengeuka,(Mwenyezi Mungu atakutieni adabu),kwani Mwenyezi Mungu hawapendi Makafiri" (3:31-32)

2. Kuwafanya Mitume vigezo vya maisha yao kibinafsi, kifamilia na kijamii kama inavyosisitizwa katika Qur-an:

﴿ لَّقَدْ كَانَ لَكُمْ فِي رَسُولِ اللَّـهِ أُسْوَةٌ حَسَنَةٌ لِّمَن كَانَ يَرْجُو اللَّـهَ وَالْيَوْمَ الْآخِرَ وَذَكَرَ اللَّـهَ كَثِيرًا﴾

"Bila shaka mnao mfano mwema (wa kuiga) kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu, kwa mwenye kumuogopa Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho, na kumtaja Mwenyezi Mungu sana". (33:21)

3. Kuwapenda Mitume kuliko nafsi zao kama Qur-an inavyosistiza:

﴿قُلْ إِن كَانَ آبَاؤُكُمْ وَأَبْنَاؤُكُمْ وَإِخْوَانُكُمْ وَأَزْوَاجُكُمْ وَعَشِيرَتُكُمْ وَأَمْوَالٌ اقْتَرَفْتُمُوهَا وَتِجَارَةٌ تَخْشَوْنَ كَسَادَهَا وَمَسَاكِنُ تَرْضَوْنَهَا أَحَبَّ إِلَيْكُم مِّنَ اللَّـهِ وَرَسُولِهِ وَجِهَادٍ فِي سَبِيلِهِ فَتَرَبَّصُوا حَتَّىٰ يَأْتِيَ اللَّـهُ بِأَمْرِهِ وَاللَّـهُ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الْفَاسِقِينَ ﴾

"Sema "Kama baba zenu na wana wenu na ndugu zenu na wake zenu na jamaa zenu na mali mlizozichuma na biashara mnazoogopa kuharibikiwa,na majumba mnayoyapenda; (ikiwa vitu hivi) ni vipenzi zaidi kwenu kuliko Mwenyezi Mungu na Mtume wake na kupigania dini yake, basi ngojeni mpaka Mwenyezi Mungu alete amri yake; na Mwenyezi Mungu hawaongozi watu maasi" (9:24)

Kumpenda Mwenyezi Mungu na Mtume si jambo lingine zaidi ya kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake kwa unyenyekevu na upendo.

Muumini wa kweli hatakuwa tayari kuifurahisha nafsi yake au kumfurahisha yeyote awaye kinyume na kumfurahisha Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Ni katika maana hii Mtume(s.a.w.w) anasema:

"Hatakuwa mmoja wenu ni Muumini wa kweli mpaka anipende zaidi kuliko chochote kile ikiwa ni pamoja na familia yake, mali yake na watu wote" .(Sahihi Muslim)

"Yeyote yule anayependa Sunnah yangu ananipenda, na yeyote yule anayenipenda atajikuta yuko ubavuni kwangu huko Peponi" (Tirmidh)

4. Kuwafanya Mitume kuwa Mahakimu wao pale wanapohitilafiana katika jambo lolote lile kama tunavyojifunza katika Qur-an:

﴿فَلَا وَرَبِّكَ لَا يُؤْمِنُونَ حَتَّىٰ يُحَكِّمُوكَ فِيمَا شَجَرَ بَيْنَهُمْ ثُمَّ لَا يَجِدُوا فِي أَنفُسِهِمْ حَرَجًا مِّمَّا قَضَيْتَ وَيُسَلِّمُوا تَسْلِيمًا﴾

"Naapa kwa (haki ya) Mola wako (Ewe Muhammad); wao hawawi wenye kuamini mpaka wakufanye hakimu katika yale wanayokhitalifiana, kisha wasione uzito nyoyoni mwao juu ya hukumu uliyopitisha, na wanyenyekee kabisa." (4:65)

﴿وَمَا كَانَ لِمُؤْمِنٍ وَلَا مُؤْمِنَةٍ إِذَا قَضَى اللَّـهُ وَرَسُولُهُ أَمْرًا أَن يَكُونَ لَهُمُ الْخِيَرَةُ مِنْ أَمْرِهِمْ وَمَن يَعْصِ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ فَقَدْ ضَلَّ ضَلَالًا مُّبِينًا﴾

"Haiwi kwa mwanamume aliyeamini wala kwa mwanamke aliyeamini, Mwenyezi Mungu na Mtume wake wanapokata shauri, wawe na hiyari katika shauri lao. Na mwenye kumuasi Mwenyezi Mungu na Mtume wake hakika amepotea upotofu (upotevu) ulio wazi." (33:36)

5. Kuwa na yakini kuwa Mtume Muhammad(s.a.w.w) ndiye Mtume wa mwisho kama Qur-an inavyosisitiza:

﴿مَّا كَانَ مُحَمَّدٌ أَبَا أَحَدٍ مِّن رِّجَالِكُمْ وَلَـٰكِن رَّسُولَ اللَّـهِ وَخَاتَمَ النَّبِيِّينَ وَكَانَ اللَّـهُ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمًا﴾

"Muhammad si baba wa yeyote katika wanaume wenu, bali yeye ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na mwisho wa Mitume, na Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa kila kitu." (33:40)

6. Kumswalia Mtume(s.a.w.w) mara kwa mara katika swala na kila anapotajwa. Kumswalia Mtume(s.a.w.w) ni amri ya Allah (s.w) kama inavyotuelekeza ifuatavyo:

﴿إِنَّ اللَّـهَ وَمَلَائِكَتَهُ يُصَلُّونَ عَلَى النَّبِيِّ يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا صَلُّوا عَلَيْهِ وَسَلِّمُوا تَسْلِيمًا﴾

Hakika Mwenyezi Mungu anamteremshia Rehema Mtume;na Malaika wake. Basi; Enyi mlioamini, msalieni Mtume na muombeeni amani. (33:56)

ZOEZI 2:2

1. Malaika ni......................................................................

2. Toa tofauti nne (4) zilizopo kati ya Malaika na binaadamu.

3. Orodhesha kazi kumi (10) za malaika zenye mahusiano na binaadamu.

4. Muumini wa kweli wa Malaika ni yule anayefanya yafuatayo:-

(a) ..........................(b) ......................(c) .....................(d) .........................

5. Taja vitabu vinne (4) vya Allah (s.w) vilivyohadithiwa katika Qur-an na Mitume walioshushiwa.

6. Lengo la kushushwa vitabu vya Allah (s.w) ni..................................

7. "Hakika ni juu yetu kutoa mwongozo." (92:12) Pamoja na binaadamu kupewa akili na elimu hana uwezo wa kujiundia njia sahihi ya maisha kwa sababu zifuatazo:

(a)...............................................

(a)..............................................

(b)..............................................

8. Toa tofauti nne (4) zilizopo kati ya Qur-an na vitabu vingine vya Allah (s.w). 9. Muumini wa kweli wa Qur-an ni yule anayefanya yafuatayo:

(a).............................................

(b)..................................................

10. (a) Mitume wa Allah (s.w) ni ..................................................

(b) Mitume wameletwa ili..................................................

(c) Waumini wa kweli wa Mitume wa Allah (s.w) ni wale wenye tabia zifuatayo:

(i)..........................

(ii)..........................

(iii)..........................

(iv)..........................

(v)..........................

4

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

NGUZO ZA IMANI

Tunajifunza katika Qur-an na hadithi sahihi kuwa; Imani ya Kiislamu imejengwa juu ya nguzo sita zifuatazo:

1 Kumuamini Allah (s.w)

2 Kuamini Malaika wake

3 Kuamini Vitabu vyake

4 Kuamini Mitume wake

5 Kuamini Siku ya mwisho

6 Kuamini Qadar yake

Hawi Muumini wa Kiislam yule ambaye amekanusha angalau moja ya nguzo hizi kama inavyobainika katika Qur-an:

﴿وَمَن يَكْفُرْ بِاللَّـهِ وَمَلَائِكَتِهِ وَكُتُبِهِ وَرُسُلِهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ فَقَدْ ضَلَّ ضَلَالًا بَعِيدًا﴾

"... Na mwenye kumkanusha Allah (s.w) na Malaika wake na Vitabu vyake na Mitume wake na siku ya mwisho. basi bila shaka amepotea upotofu ulio mbali (kabisa)" (4:136)

Mtu hatakuwa Muumini kwa kutamka tu hizi nguzo sita, bali pale atakapozijua kwa undani na kuendesha maisha yake yote kwa misingi ya nguzo hizi.

Tunazifahamu nguzo hizi sita kutokana na Hadith ya Mtume (s.a.w) iliyosimuliwa na Umar (r.a) kama ifuatavyo: Siku moja tulipokuwa tumeketi pamoja na Mtume(s.a.w.w) alitutokea mtu mmoja ambaye nguo zake zilikuwa nyeupe kama theluji na nywele zake nyeusi sana, hakuwa na dalili zozote za msafiri, ingawa alikuwa mgeni kwetu sote. Halafu alikaa mbele ya Mtume(s.a.w.w) hali magoti yake yakikabiliana na yale ya Mtume na akaweka mikono yake katika mapaja ya Mtume na akasema:"Ewe Muhammad nifahamishe juu ya Uislamu" na Mtume akasema ;

"Ni kushuhudia ya kuwa hakuna apasaye kuabudiwa kwa haki ila Allah, Kusimamisha swalaa, kutoa Zakat, Kufunga Mwezi wa Ramadhani, Kuhiji Makkat kwa mwenye kuweza"

Halafu yule mgeni akasema "umesema kweli".

Tukastaajabu kwa nini aliuliza halafu akasadikisha. Halafu akasema; "Nifahamishe juu ya Iman".

Mtume akasema :

"Ni kumuamini Mwenyezimungu na, Malaika wake , Vitabu vyake, Mitume wake, Siku ya Mwisho na Qadar, Kheri na shari yake . Kisha akasema nifahamishe juu ya Ihsaan" Akasema"Ni Kumuabudu Allah kama kwamba unamuona, ikiwa wewe humuoni yeye anakuona" Halafu akasema nifahamishe juu ya Kiyama" Akasema:"Hajui mwenye kuulizwa juu ya hilo zaidi ya mwenye kuuliza. Akasema: Nifahamishe dalili zake. Mtume akasema: "sNi wakati ambapo mjakazi atamzaa bibi yake, na utakapowaona wachungaji masikini wanaposhindana kujenga maghorofa. "Yule mgeni alipoondoka, Mtume alikaa kimya kwa muda kisha akasema: "eweUmar, unamfahamu muulizaji?' Sote tukamjibu kuwa Allah na Mtume wake wanajua zaidi. Mtume akasema"Huyo ni Jibriil amekuja kuwafundisheni dini yenu" (MUSLIM)

KUMUAMINI ALLAH ( S.W )

Nafasi ya akili katika kumtambua Allah (s.w) Imani ya kweli juu ya Allah (s.w) itathibitika moyoni baada ya kumjua vyema Allah (s.w) na sifa zake zote tukufu. Allah (s.w) hatumuoni kwa macho bali tunamfahamu kwa akili zetu katika kuchunguza dalili mbali mbali zilizotuzunguka. Tunavyojifunza katika Qur-an, matumizi ya kwanza ya akili tulizotunukiwa ni kuyakinisha kuwepo kwa Allah (s.w) na sifa zake. Msisitizo wa matumizi ya akili na fikra zetu katika kazi hii ya kumjua Allah (s.w) na sifa zake tukufu unabainishwa katika aya zifuatazo:

﴿إِنَّ فِي خَلْقِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَاخْتِلَافِ اللَّيْلِ وَالنَّهَارِ لَآيَاتٍ لِّأُولِي الْأَلْبَابِ﴾

"Katika kuumbwa mbingu na ardhi na mfuatano wa usiku na mchana ziko hoja (za kuonyesha kuwepo Mwenyezi Mungu-Allah) kwa wenye akili" (3:190)

﴿وَمِنْ آيَاتِهِ أَنْ خَلَقَ لَكُم مِّنْ أَنفُسِكُمْ أَزْوَاجًا لِّتَسْكُنُوا إِلَيْهَا وَجَعَلَ بَيْنَكُم مَّوَدَّةً وَرَحْمَةً إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِّقَوْمٍ يَتَفَكَّرُونَ ﴿٢١﴾ وَمِنْ آيَاتِهِ خَلْقُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَاخْتِلَافُ أَلْسِنَتِكُمْ وَأَلْوَانِكُمْ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِّلْعَالِمِينَ ﴿٢٢﴾ وَمِنْ آيَاتِهِ مَنَامُكُم بِاللَّيْلِ وَالنَّهَارِ وَابْتِغَاؤُكُم مِّن فَضْلِهِ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِّقَوْمٍ يَسْمَعُونَ﴿٢٣﴾ وَمِنْ آيَاتِهِ يُرِيكُمُ الْبَرْقَ خَوْفًا وَطَمَعًا وَيُنَزِّلُ مِنَ السَّمَاءِ مَاءً فَيُحْيِي بِهِ الْأَرْضَ بَعْدَ مَوْتِهَا إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِّقَوْمٍ يَعْقِلُونَ﴾

"Na katika ishara zake,(za kuthibitisha kuwepo kwake na uweza wake) ni kuwa amekuumbieni wake zenu katika jinsi yenu ili mpate utulivu kutoka kwao, naye amejaalia mapenzi na huruma baina yenu. Bila shaka katika haya zimo ishara kwa watu wanaofahamu.Na katika ishara zake (za kuonyesha uwezo wake) ni kuumba mbingu na ardhi na kuhitalifiana lugha zenu na rangi zenu na (mengine yenu na hali ya kuwa muumbaji ndiye huyo huyo mmoja). Kwa yakini katika haya zimo ishara kwa wenye ujuzi. Na katika ishara zake ni kulala kwenu usiku na (kuamka) mchana, na kutafuta kwenu fadhila yake. Hakika katika hayo zimo ishara kwa watu wanaosikia.Na katika ishara zake ni kukuonyesheni umeme kwa (kukutieni) hofu na tamaa (ya kuja mvua), na kuyateremsha (hayo) maji kutoka mawinguni. Kwayo huifufua ardhi baada ya kufa kwake.Bila shaka katika haya zimo ishara kwa watu wanaofahamu" (30:21-24)

Aya hizi chache zatosha kuonesha msisitizo wa Qur-an juu ya kutumia akili na fikara zetu katika kumfahamu vyema Allah (s.w). Kila mtu atakavyozama katika utafiti wa mazingira katika fani yoyote ile ndivyo atakavyoweza kumuona Allah (s.w) na utukufu wake kwa upeo mkubwa zaidi. Allah (s.w) mwenyewe anathibitisha hilo katika aya zifuatazo:

﴿أَلَمْ تَرَ أَنَّ اللَّـهَ أَنزَلَ مِنَ السَّمَاءِ مَاءً فَأَخْرَجْنَا بِهِ ثَمَرَاتٍ مُّخْتَلِفًا أَلْوَانُهَا وَمِنَ الْجِبَالِ جُدَدٌ بِيضٌ وَحُمْرٌ مُّخْتَلِفٌ أَلْوَانُهَا وَغَرَابِيبُ سُودٌ ﴿٢٧﴾ وَمِنَ النَّاسِ وَالدَّوَابِّ وَالْأَنْعَامِ مُخْتَلِفٌ أَلْوَانُهُ كَذَٰلِكَ إِنَّمَا يَخْشَى اللَّـهَ مِنْ عِبَادِهِ الْعُلَمَاءُ إِنَّ اللَّـهَ عَزِيزٌ غَفُورٌ﴾

"Je! Huoni kwamba Mwenyezi Mungu Ameteremsha maji mawinguni! Na kwayo Tumeyatoa matunda yenye rangi mbali mbali.Na katika milima imo mistari myeupe na myekundu yenye rangi mbali mbali, na (mengine) myeusi sana.Na katika watu na wanyama wanaotambaa na wanyama (wengine), pia rangi zao ni mbali mbali, kwa hakika wanaomcha Allah miongoni mwa waja Wake ni wale wataalamu (wanazuoni): Bila shaka Mwenyezi Mungu ni Mwenye Nguvu, Msamehevu" (35:27-28)

Wataalamu (wanazuoni) kwa mnasaba wa aya hizi si wale waliobobea kwenye fani ya fiq-h tu na nyinginezo zinazoitwa za "dini" bali ni pamoja na wale walio zama kwenye fani mbali mbali za elimu ya mazingira. Kwa mujibu wa aya hizi, wataalamu waliopigiwa mfano ni wale waliobobea katika taaluma ya hali ya hewa (meteorologists), katika taaluma ya madini (Geologists), katika taaluma ya matunda (horticulturist), katika taaluma ya wanyama (Zoologist) na katika taaluma ya watu na tabia zao (anthropologists).

Wale ambao hawatumii vipawa vyao vya akili katika kumfahamu Mola wao kutokana na mazingira wamefananishwa na wanyama, kama tunavyojifunza katika Qur-an:

﴿وَلَقَدْ ذَرَأْنَا لِجَهَنَّمَ كَثِيرًا مِّنَ الْجِنِّ وَالْإِنسِ لَهُمْ قُلُوبٌ لَّا يَفْقَهُونَ بِهَا وَلَهُمْ أَعْيُنٌ لَّا يُبْصِرُونَ بِهَا وَلَهُمْ آذَانٌ لَّا يَسْمَعُونَ بِهَا أُولَـٰئِكَ كَالْأَنْعَامِ بَلْ هُمْ أَضَلُّ أُولَـٰئِكَ هُمُ الْغَافِلُونَ﴾

"Na bila shaka tumewaumbia moto wa Jahannam wengi katika majini na watu (kwa sababu hii) Nyoyo (akili) wanazo, lakini hawafahamu kwazo, macho wanayo lakini hawaoni kwayo na masikio wanayo lakini hawasikii kwayo Hao ni kama wanyama bali wao ni wapotofu zaidi. Hao ndio walioghafilika" (7:179)

﴿إِنَّ شَرَّ الدَّوَابِّ عِندَ اللَّـهِ الصُّمُّ الْبُكْمُ الَّذِينَ لَا يَعْقِلُونَ﴾

"Hakika vinyama viovu mbele ya Mwenyezi Mungu ni hawa wanaojipa uziwi na ububu ambao hawayatii akilini (wanayoambiwa au wanayoyaona)" (8:22).

Vilevile Alla(s.w) anawashutumu wale wanaobishana kuhusu Yeye pasina kuwa na elimu.

﴿أَلَمْ تَرَوْا أَنَّ اللَّـهَ سَخَّرَ لَكُم مَّا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ وَأَسْبَغَ عَلَيْكُمْ نِعَمَهُ ظَاهِرَةً وَبَاطِنَةً وَمِنَ النَّاسِ مَن يُجَادِلُ فِي اللَّـهِ بِغَيْرِ عِلْمٍ وَلَا هُدًى وَلَا كِتَابٍ مُّنِيرٍ﴾

Je! Huoni ya kwamba Mwenyezi Mungu amekutiishieni vilivyomo mbinguni na ardhini, na Akakukamilishieni neema zake zilizo dhahiri na za siri? Na wako watu wanaobishana katika (mambo) ya Mwenyezi Mungu pasipo elimu wala uwongofu wala Kitabu chenye nuru (31:20)

﴿وَمِنَ النَّاسِ مَن يُجَادِلُ فِي اللَّـهِ بِغَيْرِ عِلْمٍ وَلَا هُدًى وَلَا كِتَابٍ مُّنِيرٍ﴾

Na katika watu wako wanaojadiliana juu ya Mwenyezi Mungu bila ya ilimu wala uwongozi wala kitabu chenye nuru (22:8)

Kutokana na aya hizi tunabainikiwa kwa uwazi kuwa katika Uislamu suala la kumuamini Allah (s.w) si suala la kibubusa (la kufuata mkumbo tu) bali ni suala la kitaaluma linalohitaji utafiti wa kina wa kisayansi. Kuna maeneo matano makubwa ambayo tukiyazamia vizuri kisayansi, yanatupatia dalili mbali mbali za uwazi zinazotuthibitishia kuwepo kwa Allah (s.w) na utukufu wake usio na mfano wake. Maeneo haya ni:

(i) Umbile la mbingu na ardhi na vyote vilivyomo ndani yake

(ii) Nafsi ya mwanaadamu

(iii) Historia ya mwanaadamu

(iv) Maisha ya Mitume

(v) Mafundisho ya Mitume

Umbile la mbingu na ardhi

﴿إِنَّ فِي خَلْقِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَاخْتِلَافِ اللَّيْلِ وَالنَّهَارِ لَآيَاتٍ لِّأُولِي الْأَلْبَابِ﴾

"Katika kuumbwa mbingu na ardhi na mfuatano wa usiku na mchana,ziko alama (hoja) za kuonyesha kuwepo Allah (s.w) kwa wenye akili." (3:190).

Mungu, Muumba wa kila kitu ndiye mmiliki pekee wa viumbe vyote. Ni Yeye anayebadili mielekeo ya upepo, anayekusanya mawingu, anayewasha jua na kuiangazia dunia na kudhibiti sayari zizunguuke katika mihimili yao. Kudai maisha haya ya dunia na ulimwengu mzima yanatokana na bahati nasibu ni kutokitumia kipawa cha busara alichotunukiwa kila mwanaadamu mwenye akili timamu. Mpango bora wa dunia na ulimwengu kwa ujumla unapinga uwezekano wa kutokea kwa bahati nasibu tu, na kinyume chake ni ishara ya wazi ya uwezo wa Allah(s.w)usio na kikomo unaodhihirisha kuwepo kwake.

Wakati ambapo ni muhali hata kwa kitu chepesi kufanya mzunguko wa moja kwa moja katika njia yake bila kwenda kombo, dunia pamoja na ukubwa wake yenye mkusanyiko wa vitu visivyo na idadi hufanya hivyo. Na imekuwa ikifanya hivyo kwa miaka dahari, na dahari, tangu dunia kuumbwa na kuanza mzunguko wake. Allah anasema Yeye ndiye mfanyaji wa mahesabu ya mzunguko huo.

﴿قَدْ جَعَلَ اللَّـهُ لِكُلِّ شَيْءٍ قَدْرًا﴾

Hakika Mwenyezi Mungu amekwishakiwekea kila kitu kipimo chake (65:3)

Utaratibu huo bora wa ulimwengu unaendeshwa kwa mfumo wa ajabu unaokwenda kwa kutegemea mihimili isiyo na mashiko.Wengine hudhani kuwa baada ya kuumba, Allah(s.w)amekiacha kila kitu kijiendeshe chenyewe tu. La hasha kila tukio litokealo mahala popote pale ulimwenguni hutokea kwa idhini ya Allah(s.w) na chini ya udhibiti wake.

Qur'an inatufahamisha:

﴿أَلَمْ تَعْلَمْ أَنَّ اللَّـهَ يَعْلَمُ مَا فِي السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ إِنَّ ذَٰلِكَ فِي كِتَابٍ إِنَّ ذَٰلِكَ عَلَى اللَّـهِ يَسِيرٌ﴾

Je! Hujui ya kwamba Mwenyezi Mungu anajua yaliyoko mbinguni na ardhini? Bila shaka yote yamo kitabuni mwake.Hakika hayo kwa Mwenyezi Mungu ni sahali. (22:70)

Kwa ujumla, umbile la mbingu na ardhi pamoja na vyote vilivyomo - jua, mwezi, nyota, sayari mbali mbali, milima na mabonde, maji ya mvua, bahari, mito na maziwa, mimea ya kila namna, wanyama wa kila namna na kadhalika ni hoja kubwa ya kuthibitisha kuwepo Allah (s.w) na utukufu wake kwa kila mwenye kutumia akili yake vizuri. Kila mtu atakavyobobea katika taaluma zinazohusiana na maumbile ya mbingu na ardhi kama vile Jeografia, Elimu ya anga (Astronomy), Elimu ya mimea (Botany), Elimu ya wanyama (Zoology), n.k. ndivyo Imani yake ya kuwepo Allah (s.w) itakavyopea.

﴿إِنَّمَا يَخْشَى اللَّـهَ مِنْ عِبَادِهِ الْعُلَمَاءُ إِنَّ اللَّـهَ عَزِيزٌ غَفُورٌ﴾

Kwa hakika wanaomuogopa Allah (s.w) miongoni mwa waja wake ni wale wataalam..." (35:28)

NAFSI YA MWANAADAMU

﴿وَفِي الْأَرْضِ آيَاتٌ لِّلْمُوقِنِينَ ﴿٢٠﴾ وَفِي أَنفُسِكُمْ أَفَلَا تُبْصِرُونَ﴾

"Na katika ardhi zipo (alama namna kwa namna za kuonyesha kuwepo Allah (s.w) kwa wenye akili.Na katika nafsi zenu (pia zimo ishara hizo) Je, hamuoni?" (51:20-21)

Ukimtafakari mwanaadamu utapata dalili nyingi zinazothibitisha kuwepo kwa Allah (s.w). Maeneo ya kutafakari ni pamoja na:

(I) CHANZO NA MWISHO WA UHAI WA MWANAADAMU

﴿كَيْفَ تَكْفُرُونَ بِاللَّـهِ وَكُنتُمْ أَمْوَاتًا فَأَحْيَاكُمْ ثُمَّ يُمِيتُكُمْ ثُمَّ يُحْيِيكُمْ ثُمَّ إِلَيْهِ تُرْجَعُونَ﴾

"Vipi mnamkanusha Allah (s.w) na hali mlikuwa wafu, akakuhuisheni, kisha atakufisheni, kisha atakurudisheni (tena) kisha kwake mtarejeshwa" (2:28)

﴿فَلَوْلَا إِذَا بَلَغَتِ الْحُلْقُومَ ﴿٨٣﴾ وَأَنتُمْ حِينَئِذٍ تَنظُرُونَ ﴿٨٤﴾ وَنَحْنُ أَقْرَبُ إِلَيْهِ مِنكُمْ وَلَـٰكِن لَّا تُبْصِرُونَ ﴿٨٥﴾ فَلَوْلَا إِن كُنتُمْ غَيْرَ مَدِينِينَ ﴿٨٦﴾ تَرْجِعُونَهَا إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ﴾

"Basi mbona (roho) ifikapo kooni,na nyinyi wakati ule mnamtazama. Nasi tunakaribiana naye zaidi (huyo anayetoka roho) kuliko nyinyi,wala nyinyi hamuoni.Kama nyinyi hamumo katika mamlaka (yangu), kwanini hamuirudishi (hiyo roho) ikiwa mnasema kweli?" (56:83-87)

(II) ASILI YA MWANAADAMU

﴿وَمِنْ آيَاتِهِ أَنْ خَلَقَكُم مِّن تُرَابٍ ثُمَّ إِذَا أَنتُم بَشَرٌ تَنتَشِرُونَ﴾

"Na katika ishara zake (za kuonyesha kuwepo kwake) ni huku kukuumbeni kwa udongo kisha mnakuwa watu mnaoenea (kila mahali)" (30:20)

(III) KUUMBWA WANAUME NA WANAWAKE

﴿أَيَحْسَبُ الْإِنسَانُ أَن يُتْرَكَ سُدًى ﴿٣٦﴾ أَلَمْ يَكُ نُطْفَةً مِّن مَّنِيٍّ يُمْنَىٰ ﴿٣٧﴾ ثُمَّ كَانَ عَلَقَةً فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ ﴿٣٨﴾ فَجَعَلَ مِنْهُ الزَّوْجَيْنِ الذَّكَرَ وَالْأُنثَىٰ ﴿٣٩﴾ أَلَيْسَ ذَٰلِكَ بِقَادِرٍ عَلَىٰ أَن يُحْيِيَ الْمَوْتَىٰ﴾

"Je! Anafikiri binaadamu kuwa ataachwa bure(asipewa amri za Mwenyezi Mungu wala makatazo yake)? Je, hakuwa tone la manii lililotonwa?.Kisha akawa kidonge cha damu, kisha akamuumba na akamsawazisha,kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.Je!Hakuwa huyo ni muweza wa kuhuisha wafu?" (75:36-40).

﴿وَمِنْ آيَاتِهِ أَنْ خَلَقَ لَكُم مِّنْ أَنفُسِكُمْ أَزْوَاجًا لِّتَسْكُنُوا إِلَيْهَا وَجَعَلَ بَيْنَكُم مَّوَدَّةً وَرَحْمَةً إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِّقَوْمٍ يَتَفَكَّرُونَ﴾

"Na katika ishara zake ni kuwa amekuumbieni wake zenu katika jinsi yenu ili mpate utulivu kwao, naye amejaalia mapenzi na huruma baina yenu. Bila shaka katika haya ziko alama (za kuwepo Allah) kwa watu wanaofikiri" (30:21)

(IV) TOFAUTI YA LUGHA, RANGI, MAKABILA, MATAIFA

﴿وَمِنْ آيَاتِهِ خَلْقُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَاخْتِلَافُ أَلْسِنَتِكُمْ وَأَلْوَانِكُمْ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِّلْعَالِمِينَ﴾

"Na katika ishara zake (za kuonyesha kuwepo kwake na uwezo wake) ni kuumba mbingu na ardhi na kuhitalifiana lugha zenu na rangi zenu.Kwa yakini katika haya zimo ishara kwa wenye ujuzi" (30:22)

﴿يَا أَيُّهَا النَّاسُ إِنَّا خَلَقْنَاكُم مِّن ذَكَرٍ وَأُنثَىٰ وَجَعَلْنَاكُمْ شُعُوبًا وَقَبَائِلَ لِتَعَارَفُوا إِنَّ أَكْرَمَكُمْ عِندَ اللَّـهِ أَتْقَاكُمْ إِنَّ اللَّـهَ عَلِيمٌ خَبِيرٌ ﴾

"Enyi watu! Kwa hakika tumekuumbeni (nyote) kwa (yule) mwanamume (mmoja Adam) na (yule) mwanamke (mmoja Hawwa). Na tumekufanyeni mataifa na makabila (mbali mbali) ili mjuane (tu basi). Hakika aheshimiwaye sana miongoni mwenu mbele ya Allah ni yule amchaye Allah zaidi katika nyinyi. Kwa yakini Allah ni Mjuzi Mwenye habari (za mambo yote)." (49:13)

(V) UMBO NA SURA

﴿ يَا أَيُّهَا الْإِنسَانُ مَا غَرَّكَ بِرَبِّكَ الْكَرِيمِ ﴿٦﴾ الَّذِي خَلَقَكَ فَسَوَّاكَ فَعَدَلَكَ ﴿٧﴾ فِي أَيِّ صُورَةٍ مَّا شَاءَ رَكَّبَكَ﴾

"Ewe mwanaadamu! Nini kikudanganyacho na Mola wako Mtukufu (hata ukamkanusha).Aliyekuumba na akakutengeneza, kisha akakulinganisha sawa sawa. Katika sura yoyote aliyoipenda amekutengeneza" (82: 6-8)

﴿وَفِي خَلْقِكُمْ وَمَا يَبُثُّ مِن دَابَّةٍ آيَاتٌ لِّقَوْمٍ يُوقِنُونَ﴾

Na katika umbo lenu na katika viumbe alivyovitawanya zimo alama kwa watu wenye yakini" (45:4)

(VI) CHAKULA CHA MWANAADAMU

﴿فَلْيَنظُرِ الْإِنسَانُ إِلَىٰ طَعَامِهِ ﴿٢٤﴾ أَنَّا صَبَبْنَا الْمَاءَ صَبًّا ﴿٢٥﴾ ثُمَّ شَقَقْنَا الْأَرْضَ شَقًّا ﴿٢٦﴾ فَأَنبَتْنَا فِيهَا حَبًّا ﴿٢٧﴾ وَعِنَبًا وَقَضْبًا ﴿٢٨﴾ وَزَيْتُونًا وَنَخْلًا ﴿٢٩﴾ وَحَدَائِقَ غُلْبًا ﴿٣٠﴾ وَفَاكِهَةً وَأَبًّا ﴿٣١﴾ مَّتَاعًا لَّكُمْ وَلِأَنْعَامِكُمْ﴾

"Hebu mwanaadam na atazame chakula chake.Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu(kutoka mawinguni). Tena tukaipasuapasua ardhi.Kisha Tukaotesha humo (vyakula vilivyo) chembe chembe.Na mizabibu na mboga.Na mizeituni na mitende. Na mabustani, (mashamba) yenye miti iliyosongamana barabara.Na matunda na malisho.Kwa ajili ya kukustarehesheni nyinyi na wanyama wenu. (80:24-32)

(VII) UFANYAJI KAZI WA VIUNGO VYA NDANI NA NJE YA MWILI WA MWANAADAMU

﴿فَأَقِمْ وَجْهَكَ لِلدِّينِ حَنِيفًا فِطْرَتَ اللَّـهِ الَّتِي فَطَرَ النَّاسَ عَلَيْهَا لَا تَبْدِيلَ لِخَلْقِ اللَّـهِ ذَٰلِكَ الدِّينُ الْقَيِّمُ وَلَـٰكِنَّ أَكْثَرَ النَّاسِ لَا يَعْلَمُونَ﴾

"Basi uelekeze uso wako katika dini iliyo sawasawa - ndilo umbile Mwenyezi Mungu alilowaumbia watu; (yaani dini hii ya Kiislamu inawafikiana barabara na umbo la binaadamu).Hakuna mabadiliko katika maumbile ya viumbe vya Mwenyezi Mungu.Hiyo ndiyo dini iliyo haki, lakini watu wengi hawajui." (30:30)

(VIII) USINGIZI

﴿وَمِنْ آيَاتِهِ مَنَامُكُم بِاللَّيْلِ وَالنَّهَارِ وَابْتِغَاؤُكُم مِّن فَضْلِهِ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِّقَوْمٍ يَسْمَعُونَ﴾

"Na katika ishara zake ni kulala kwenu usiku na kuamka mchana na kutafuta fadhila Yake.Hakika katika hayo zimo ishara kwa wenye kusikia.(30:23)

Mwanadamu japo analala kila siku, hajui chanzo cha usingizi.Mtu anapokuwa usingizini hajui chochote kinachoendelea, Je! ni nani anayeleta usingizi na kuuondoa?

(IX) MWANADAMU KUMKUMBUKA ALLAH (S.W) WAKATI WA MATATIZO

﴿قُلْ مَن يُنَجِّيكُم مِّن ظُلُمَاتِ الْبَرِّ وَالْبَحْرِ تَدْعُونَهُ تَضَرُّعًا وَخُفْيَةً لَّئِنْ أَنجَانَا مِنْ هَـٰذِهِ لَنَكُونَنَّ مِنَ الشَّاكِرِينَ﴾

"Sema: Ni nani anayekuokoeni katika viza (taabu) vya bara na baharini? Mnamuomba kwa unyenyekevu na kwa sauti ndogo (mnasema): Kama akituokoa katika (baa) hii bila shaka tutakuwa miongoni mwa wanaoshukuru (6:63)

Hata Fir'auni, aliyetakabari sana kiasi cha kudai kuwa yeye ni mkubwa kuliko Allah, alimkumbuka Mola wake pale alipokabiliwa barabara na matatizo.

﴿وَجَاوَزْنَا بِبَنِي إِسْرَائِيلَ الْبَحْرَ فَأَتْبَعَهُمْ فِرْعَوْنُ وَجُنُودُهُ بَغْيًا وَعَدْوًا حَتَّىٰ إِذَا أَدْرَكَهُ الْغَرَقُ قَالَ آمَنتُ أَنَّهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا الَّذِي آمَنَتْ بِهِ بَنُو إِسْرَائِيلَ وَأَنَا مِنَ الْمُسْلِمِينَ﴾

"Na tukawapitisha wana wa Israel katika bahari, na Firauni na majeshi yake wakawafuata kwa dhulma na jeuri. Hata kulipomfikia Fir'aun kuzama alisema, "Naamini kwamba hakuna aabudiwaye kwa haki ila yule wanayemuamini wana wa Israel na mimi ni miongoni mwa wanaotii". (10:90)

Historia ya Mwanadamu Historia ya mwanadamu ukiichunguza tangu mwanzo wake utakuta matukio mengi yanayothibitisha kuwepo Allah (s.w) Mmiliki wa kila kitu na mwenye nguvu na uwezo juu ya kila kitu. Mara kwa mara tunatanabahishwa katika Qur-an:

﴿أَفَلَمْ يَهْدِ لَهُمْ كَمْ أَهْلَكْنَا قَبْلَهُم مِّنَ الْقُرُونِ يَمْشُونَ فِي مَسَاكِنِهِمْ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِّأُولِي النُّهَىٰ﴾

"Je! Haikuwabainikia tu kama (kaumu) ngapi tuliziangamiza kabla yao? Na hawa (makafiri wa sasa) wanatembeatembea katika maskani yao, (hawaoni alama za kuangamizwa kwao)?Bila shaka katika hayo zimo ishara kwa wenye akili." (20:128)

﴿أَوَلَمْ يَسِيرُوا فِي الْأَرْضِ فَيَنظُرُوا كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ الَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ كَانُوا أَشَدَّ مِنْهُمْ قُوَّةً وَأَثَارُوا الْأَرْضَ وَعَمَرُوهَا أَكْثَرَ مِمَّا عَمَرُوهَا وَجَاءَتْهُمْ رُسُلُهُم بِالْبَيِّنَاتِ فَمَا كَانَ اللَّـهُ لِيَظْلِمَهُمْ وَلَـٰكِن كَانُوا أَنفُسَهُمْ يَظْلِمُونَ﴾

"Je! Hawatembei katika nchi na kuona jinsi ulivyokuwa mwisho wa wale waliokuwa kabla yao? Walikuwa wenye nguvu zaidi kuliko wao na wakilima ardhi na kuistawisha zaidi kuliko wao walivyostawisha. Na mitume wao waliwajia kwa dalili waziwazi, basi hakuwa Mwenyezi Mungu ni mwenye kuwadhulumu,lakini walikuwa wenyewe wakijidhulumu nafsi zao." (30:9)

﴿أَلَمْ تَرَ كَيْفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِأَصْحَابِ الْفِيلِ ﴿١﴾ أَلَمْ يَجْعَلْ كَيْدَهُمْ فِي تَضْلِيلٍ ﴿٢﴾ وَأَرْسَلَ عَلَيْهِمْ طَيْرًا أَبَابِيلَ ﴿٣﴾ تَرْمِيهِم بِحِجَارَةٍ مِّن سِجِّيلٍ ﴿٤﴾ فَجَعَلَهُمْ كَعَصْفٍ مَّأْكُولٍ﴾

"Je!Huoni Mola wako alivyo wafanya watu wenye ndovu?Hakujaalia vitimbi vyao kuharibika?Na akawapeleka ndege makundi kwa makundi, wakawapiga kwa mawe ya udongo wa kuchoma, Akawafanya kama majani yaliyotafunwa." (105:1-5)

Tukio hili la watu wenye ndovu lilitokea mwaka 570.A.D. miezi michache kabla ya kuzaliwa Mtume Muhammad(s.a.w.w). Mnamo mwaka wa 570 A.D. Abraha, gavana wa Yemen, chini ya himaya ya Kikiristo ya Uhabeshi alikusanya jeshi lenye askari 60,000 na ndovu (tembo) kumi na tatu (13) kwa nia ya kuibomoa na kuisambaratisha Al-Ka'abah, nyumba takatifu ya Allah (s.w) iliyopo Makka. Walinzi wa Ka'abah, kabila la Quraish waliongozwa na Abdul-Muttalib, Babu yake Mtume (s.a.w), walimfahamisha Abraha kuwa wao hawana uwezo wa kupambana na jeshi lake hilo bali mwenye Ka'abah ndiye atakayeilinda. Abraha alipokaidi na kusisitiza kutekeleza azma yake ya kuivunja Ka'abah, Abdul- Muttalib aliwaamuru wakazi wa Makka wampishe na akaingia ndani ya Ka'abah na kumuomba Allah (s.w) kwa unyenyekevu kama ifuatavyo:

"O Allah, mtu hulinda nyumba yake, nawe ilinde nyumba yako. Usiuachie msalaba na hila zao kesho kushinda hila zako. Kama utaamua kuwaachia waifanye watakavyo Qibla yetu, Basi wewe ni muweza wa kufanya upendavyo. Wanusuru leo watumishi wako dhidi ya watumishi wa Msalaba na waabudu wake. Ewe Mola wangu, sina matumaini yoyote toka kwa yeyote dhidi yao isipokuwa kwako. Ewe Mola wangu, ilinde nyumba yako dhidi yao. Adui wa nyumba hii ni adui yako. Wazuie wasiiharibu nyumba yako"

Kesho yake, Abraha na jeshi lake kabla hawajapiga hatua kutoka kwenye kambi yao, kilometa tano (5) tokea Makka, walizingirwa na jeshi la ndege wadogo wadogo walioitwa "Ababil" waliokuwa na silaha ya vijiwe. Kila ndege alimlenga askari wake na kijiwe hicho kilichomchakaza na kumfanya kama majani yaliyotafunwa na kutemwa. Tukio hili la "watu wa ndovu" ni kielelezo tosha kutokana na historia ya binaadamu kuwa Allah (s.w) yupo na anauwezo ulio juu ya hila zote za binaadamu na juu ya kila kitu.

Maisha ya Mitume Ukiyachunguza maisha ya mitume mbalimbali kama yalivyoelezwa katika Qur-an utabaini kuwa wao kweli walikuwa ni wajumbe wa Allah (s.w). Tunayoyaona katika maisha ya Mitume ambayo yanatuhakikishia kuwepo kwa Allah (s.w) ni pamoja na:

(i) Kuwepo kwao na kujieleza kwa watu wao kuwa ni Mitume wa Mwenyezi Mungu (s.w)

(ii) Msimamo wao katika kujieleza kwa jamii zao kuwa wao ni Mitume wa Allah (s.w)

(iii) Mwenendo wao mwema kutoathiriwa na (mazingira) jamii

(iv) Miujiza waliyoionesha katika kuthibitisha utume wao (v) Kuhimili kwao mateso na kujitoa kwao muhanga kwa ajili ya Allah (s.w)

(vi) Ujasiri wao katika kuwakabili viongozi wa jamii zao.

(vii) Ushindi wao dhidi ya maadui wa Mwenyezi Mungu

(viii) Mitume kutohitaji malipo yoyote kwa ajili ya kazi yao.

(i) Kuwepo kwao na kujieleza kwa watu wao kuwa ni Mitume wa Mwenyezi Mungu (s.w) Mitume walijieleza kwa uwazi kuwa wao ni mitume wa Allah (s.w) kama tunavyojifunza katika mifano ifuatayo:

﴿لَقَدْ أَرْسَلْنَا نُوحًا إِلَىٰ قَوْمِهِ فَقَالَ يَا قَوْمِ اعْبُدُوا اللَّـهَ مَا لَكُم مِّنْ إِلَـٰهٍ غَيْرُهُ إِنِّي أَخَافُ عَلَيْكُمْ عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ ﴿٥٩﴾ قَالَ الْمَلَأُ مِن قَوْمِهِ إِنَّا لَنَرَاكَ فِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ ﴿٦٠﴾ قَالَ يَا قَوْمِ لَيْسَ بِي ضَلَالَةٌ وَلَـٰكِنِّي رَسُولٌ مِّن رَّبِّ الْعَالَمِينَ ﴿٦١﴾ أُبَلِّغُكُمْ رِسَالَاتِ رَبِّي وَأَنصَحُ لَكُمْ وَأَعْلَمُ مِنَ اللَّـهِ مَا لَا تَعْلَمُونَ ﴿٦٢﴾ أَوَعَجِبْتُمْ أَن جَاءَكُمْ ذِكْرٌ مِّن رَّبِّكُمْ عَلَىٰ رَجُلٍ مِّنكُمْ لِيُنذِرَكُمْ وَلِتَتَّقُوا وَلَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ ﴿٦٣﴾ فَكَذَّبُوهُ فَأَنجَيْنَاهُ وَالَّذِينَ مَعَهُ فِي الْفُلْكِ وَأَغْرَقْنَا الَّذِينَ كَذَّبُوا بِآيَاتِنَا إِنَّهُمْ كَانُوا قَوْمًا عَمِينَ ﴿٦٤﴾ وَإِلَىٰ عَادٍ أَخَاهُمْ هُودًا قَالَ يَا قَوْمِ اعْبُدُوا اللَّـهَ مَا لَكُم مِّنْ إِلَـٰهٍ غَيْرُهُ أَفَلَا تَتَّقُونَ ﴿٦٥﴾ قَالَ الْمَلَأُ الَّذِينَ كَفَرُوا مِن قَوْمِهِ إِنَّا لَنَرَاكَ فِي سَفَاهَةٍ وَإِنَّا لَنَظُنُّكَ مِنَ الْكَاذِبِينَ ﴿٦٦﴾ قَالَ يَا قَوْمِ لَيْسَ بِي سَفَاهَةٌ وَلَـٰكِنِّي رَسُولٌ مِّن رَّبِّ الْعَالَمِينَ﴾

"Tulimtuma Nuhu kwa watu wake naye akasema: 'Enyi watu wangu! Muabuduni Mwenyezi Mungu. Nyinyi hamna Mungu ila Yeye. Hakika mimi ninakuhofieni adhabu ya siku iliyo Kuu. Wakuu wa watu wake wakasema: "Sisi tunakuona uko katika upotofu uliodhahiri.Akasema (Nuhu):"Enyi kaumu yangu mimi simo katika upotofu lakini mimi ni Mtume nitokaye kwa Mola wa walimwengu wote. Na kwa Adi (tulimpeleka) ndugu yao Hudi akasema: "Ewe kaumu yangu! Muabuduni Mwenyezi Mungu nyinyi hamna Mungu ila Yeye Hamuogopi? Wakasema wakuu waliokufuru katika kaumu yake:"Sisi tunakuona umo katika upumbavu na tunakuona u miongoni mwa waongo.Akasema: "Enyi kaumu yangu! Mimi sina upumbavu.Lakini mimi ni Mtume niliyetoka kwa Mola wa walimwengu.(7:59-67)

Pamoja na Mitume kujieleza kuwa wanatoka kwa Allah (s.w) mwenyewe Allah (s.w) anatufahamisha kuwa ametuma Mitume:

﴿وَلَقَدْ بَعَثْنَا فِي كُلِّ أُمَّةٍ رَّسُولًا أَنِ اعْبُدُوا اللَّـهَ وَاجْتَنِبُوا الطَّاغُوتَ فَمِنْهُم مَّنْ هَدَى اللَّـهُ وَمِنْهُم مَّنْ حَقَّتْ عَلَيْهِ الضَّلَالَةُ فَسِيرُوا فِي الْأَرْضِ فَانظُرُوا كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ الْمُكَذِّبِينَ﴾

Na bila shaka tulimpeleka Mtume katika kila umma ya kwamba,"muadubuni Mwenyezi Mungu na mwepukeni muovu (twaaghuut) (16:36)

﴿إِنَّا أَرْسَلْنَاكَ بِالْحَقِّ بَشِيرًا وَنَذِيرًا وَإِن مِّنْ أُمَّةٍ إِلَّا خَلَا فِيهَا نَذِيرٌ﴾

Bila shaka Sisi tumekutuma (tumekuleta) kwa haki ili ubashirie na uonye. Na hakuna taifa lolote ila alipita humo muonyaji (Mtume kuwaonya). (35:24)

﴿وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا رُسُلًا مِّن قَبْلِكَ مِنْهُم مَّن قَصَصْنَا عَلَيْكَ وَمِنْهُم مَّن لَّمْ نَقْصُصْ عَلَيْكَ وَمَا كَانَ لِرَسُولٍ أَن يَأْتِيَ بِآيَةٍ إِلَّا بِإِذْنِ اللَّـهِ فَإِذَا جَاءَ أَمْرُ اللَّـهِ قُضِيَ بِالْحَقِّ وَخَسِرَ هُنَالِكَ الْمُبْطِلُونَ﴾

Na kwa yakini tuliwatuma Mitume kabla yako.Wengine katika hao tumekusimulia (majina yao na habari zao) na wengine hatukusimulia na haikuwa kwa Mtume yoyote kuleta muujiza wowote ila kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Na itakapokuja hukumu ya Mwenyezi Mungu kutahukumiwa kwa haki, na wafanyao mambo ya batili watapata hasara wakati huo. (40:78).

Hivyo, kuwepo kwa Mitume kunatuthibitishia kuwepo kwa Mwenyezi Mungu (s.a.w) kwa namna mbili, kwanza, kama Mwenyezi Mungu (s.w) asingelikuwepo asingelileta Mitume kwa wanaadamu. Pili, Mitume wote waliotokea katika nyakati mbali mbali za historia wasingelitoa dai moja linalofanana kwa wote kuwa wao ni Mitume wa Mwenyezi Mungu (s.w) kama Mwenyezi Mungu hayupo.

(ii) Mwenendo wao mwema kutoathiriwa na jamii Mitume wote takriban walizaliwa na kulelewa katika jamii za kijahili zilizozama katika kumshirikisha Mwenyezi Mungu (s.w) na miungu chungu nzima. lakini jambo la ajabu na kushangaza ni kwamba, Mitume wote tangu utotoni waliepukana na tabia za kijahili na walijiepusha mbali na kumshirikisha Mwenyezi Mungu (s.w). Walikuwa na mwenendo wa kiutu (wa Kiislamu) uliowavutia watu wote wa jamii zao na walikuwa ni nyota katika jamii. Kwa mfano, Nabii Ibrahim(a.s) alizaliwa na kuhani Mkuu.

Yaani baba yake Nabii Ibrahim alikuwa ni kiongozi au msimamizi wa ibada ya masanamu. Lakini Nabii Ibrahim kamwe hakuvutiwa na ibada hiyo ya masanamu bali akiwa angali kijana mdogo aliona kuwa ni kinyume kabisa na akili ya mwanaadamu kuwaabudu miungu wengine kinyume na kumuabudu Allah (s.w) aliye mpweke. Mfano wa pili ni ule wa Nabii, Musa(a.s) aliyelelewa katika nyumba ya Firaun aliyetakabari na kujiita mungu. Malezi hayo ya kifalme kamwe hayakumuathiri Nabii Musa(a.s) .Aliinukia kuwa na mwenendo mwema wa kumpwekesha Allah (s.w).

Mfano mwingine ni ule wa Mtume Muhammad(s.a.w.w) ambaye alizaliwa katika jamii ya Maquraysh iliyobobea katika ujahili na iliyozama katika ushirikina kiasi kwamba kila kitu kwao kiliweza kufanywa mungu na kuabudiwa. Katika wakati huo masanamu ya watu, ndege na wanyama yaliuzwa sokoni kama miungu wa kuabudiwa na hata tende zilifinyangwa na kuabudiwa. Lakini tunavyojifunza katika historia, Mtume(s.a.w.w) tangu utotoni mwake hakuathiriwa kamwe na ibada za masanamu na mwendo wa ujahili. Bali tunajifunza kuwa aliinukia katika kumtambua na kumpwekesha Allah (s.w) na aliwazidi watu wote kwa tabia njema kiasi kwamba watu wake walimtegemea sana kwa ushauri na kuwatunzia amana zao na walimwita "mkweli", "mwaminifu" na majina mengine kama haya yaliyodhihirisha tabia yake njema katikati ya jamii ya kijahili. Ni kitu gani kilichowafanya Mitume kuwa tofauti na watu wa jamii zao?

Je, hakuna aliyewatayarisha na kuwalea katika mwenendo huo ili wawe viigizo vyema katika jamii zao? Bila shaka Mwenyezi Mungu (s.w) ndiye aliwewaleta Mitume ili wafikishe ujumbe wake na wawe viigizo vyema katika kuutekeleza Uislam kama inavyobainishwa katika Qur-an:

﴿لَقَدْ أَرْسَلْنَا رُسُلَنَا بِالْبَيِّنَاتِ وَأَنزَلْنَا مَعَهُمُ الْكِتَابَ وَالْمِيزَانَ لِيَقُومَ النَّاسُ بِالْقِسْطِ﴾

Kwa hakika tuliwapeleka Mitume wetu kwa dalili wazi wazi na tukaviteremsha Vitabu na uadilifu pamoja nao, ili watu wasimamie uadilifu. (57:25)

(iii) Dalili (miujiza) za kuthibitisha Utume wao Mitume wameletwa pamoja na alama mbali mbali za kuwathibitisha Utume wao kwa watu wao.

﴿لَقَدْ أَرْسَلْنَا رُسُلَنَا بِالْبَيِّنَاتِ﴾

"Kwa hakika tumewapeleka Mitume wetu kwa dalili wazi wazi" (57:25)

Kila Mtume alipewa dalili za kuwathibitishia watu wake kuwa yeye ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu. Alama za Utume wa Nabii Musa(a.s) ni fimbo yake kugeuka kuwa nyoka wa kweli na mkono wake kutoa mwan ga mkali kama tunavyojifunza katika Qur-an. (Rejea 28:29-32)

Dalili za Utume wa Nabii Issa(a.s) zilikuwa ni kuwafufua wafu, kuwaponyesha vipofu na wenye mbaranga, kulifanya sanamu la ndege kuwa ndege wa kweli kama inavyobainishwa katika Quran (5:110).

Dalili aliyopewa Mtume Muhammad(s.a.w.w) ya kuthibitisha kuwa yeye ni Mtume wa Allah (s.w) ambayo itabakia mpaka mwisho wa ulimwengu ni Qur-an. Qur-an tofauti na vitabu vingine vya Allah (s.w) imehifadhiwa na uharibifu wa aina yoyote. Qur-an yenyewe inatukumbusha:

﴿أَفَلَا يَتَدَبَّرُونَ الْقُرْآنَ وَلَوْ كَانَ مِنْ عِندِ غَيْرِ اللَّـهِ لَوَجَدُوا فِيهِ اخْتِلَافًا كَثِيرًا﴾

Hawaizingatii nini,hii Qur-an? Na kama ingelitoka kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu bila shaka wangelikuta ndani yake khitilafu nyingi. (4:82).

(iv) Kuhimili mateso na kujitoa kwao muhanga kwa ajili ya Mwenyezi Mungu (s.w)

Jambo jingine linalopatikana katika historia ya Mitume ni uvumilivu waliokuwa nao dhidi ya mateso mbali mbali waliyofanyiwa na watu wao na bado wakaendelea kufikisha ujumbe wa Mwenyezi Mungu bila ya kukata tama. Tukirejea katika Qur'an tunapata mifano mbali mbali ya mateso waliyofanyiwa na jamaa zao. Kwa mfano tunajifunza katika Qur-an kuwa ilikuwa ni tabia ya Wayahudi (kizazi cha Israil) kuwauwa Mitume yao pasina haki:

﴿إِنَّ الَّذِينَ يَكْفُرُونَ بِآيَاتِ اللَّـهِ وَيَقْتُلُونَ النَّبِيِّينَ بِغَيْرِ حَقٍّ وَيَقْتُلُونَ الَّذِينَ يَأْمُرُونَ بِالْقِسْطِ مِنَ النَّاسِ فَبَشِّرْهُم بِعَذَابٍ أَلِيمٍ﴾

Wale (Mayahudi) wanaozikataa Aya za Mwenyezi Mungu, na wakawaua manabii pasina haki, na wakaua watu wanaoamrisha kusimamisha haki, wapashe habari ya adhabu kali. (3:21)

Nabii Yahya(a.s) (Yohana mbatizaji) ni miongoni mwa Mitume wa Mwenyezi Mungu waliochinjwa na Mayahudi, kwa sababu tu eti walisimama kidete kufikisha neno la Mwenyezi Mungu, kwa watu wao ili wasimamishe haki katika jamii kwa kufanya mema na kuacha maovu.Pia Mayahudi walikula njama za kumuua Nabii Isa(a.s) . Lakini Mwenyezi Mungu (s.w) alimuokoa na kumnyakuwa kwake kama tunavyojifunza katika Qur-an:

﴿وَقَوْلِهِمْ إِنَّا قَتَلْنَا الْمَسِيحَ عِيسَى ابْنَ مَرْيَمَ رَسُولَ اللَّـهِ وَمَا قَتَلُوهُ وَمَا صَلَبُوهُ وَلَـٰكِن شُبِّهَ لَهُمْ وَإِنَّ الَّذِينَ اخْتَلَفُوا فِيهِ لَفِي شَكٍّ مِّنْهُ مَا لَهُم بِهِ مِنْ عِلْمٍ إِلَّا اتِّبَاعَ الظَّنِّ وَمَا قَتَلُوهُ يَقِينًا ﴿١٥٧﴾ بَل رَّفَعَهُ اللَّـهُ إِلَيْهِ وَكَانَ اللَّـهُ عَزِيزًا حَكِيمًا ﴿١٥٨﴾ وَإِن مِّنْ أَهْلِ الْكِتَابِ إِلَّا لَيُؤْمِنَنَّ بِهِ قَبْلَ مَوْتِهِ وَيَوْمَ الْقِيَامَةِ يَكُونُ عَلَيْهِمْ شَهِيدًا﴾

"Na kwa (ajili ya) kusema kwao: Sisi tumemuua Masihi Isa, mwana wa Maryam Mtume wa Mungu", hali hawakumuua wala hawakumsulubu, bali walibadilishiwa (mtu mwingine wakamdhani Nabii Issa). Na kwa hakika wale waliokhitilafiana katika (hakika) hiyo (ya kumuua Nabii Isa) wamo katika shaka nalo (jambo hilo la kusema kauawa).Wao (kabisa) hawana yakini juu ya (jambo) hili (la kuwa kweli wamemua Nabii (Isa). Isipokuwa wanafuata dhana tu. Na kwa yakini hawakumua.Bali Mwenyezi Mungu alimnyanyua kwake, na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu na Mwenye hikima. (4:157-158)

Naye Nabii Ibrahim alitupwa motoni na jamaa zake, Mwenyezi Mungu (s.w) aliuamrisha moto kuwa baridi na salama kwake:

﴿قُلْنَا يَا نَارُ كُونِي بَرْدًا وَسَلَامًا عَلَىٰ إِبْرَاهِيمَ﴾

"Tukasema: 'Ewe moto! Kuwa baridi na salama juu ya Ibrahim". (21:69)

Mitume pia walitiwa vifungoni na vizuizini (kutengwa na jamii) kama ilivyokuwa kwa Nabii Yusufu(a.s) na Nabii Muhammad(s.a.w.w) . Baadhi ya Mitume na wafuasi wao walifukuzwa nchini mwao na kuhamia ugenini kama ilivyokuwa kwa Mtume(s.a.w.w) na Muhajirina:

﴿لِلْفُقَرَاءِ الْمُهَاجِرِينَ الَّذِينَ أُخْرِجُوا مِن دِيَارِهِمْ وَأَمْوَالِهِمْ يَبْتَغُونَ فَضْلًا مِّنَ اللَّـهِ وَرِضْوَانًا وَيَنصُرُونَ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ أُولَـٰئِكَ هُمُ الصَّادِقُونَ﴾

"(Basi) wapewe (mali hayo) mafakiri wa Kimuhajiri ambao walifukuzwa katika nyumba zao na mali zao; (wakakhiari kuyaacha hayo) kwa ajili ya (kutafuta) fadhila za Mwenyezi Mungu na radhi (yake) na kuinusuru (dini ya) Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Basi hao ndio waislamu wa kweli. (59:8).

Mitume pia walinyanyaswa kwa matusi na kejeli. Kwa mfano Mtume Muhammad(s.a.w.w) aliitwa mwendawazimu, mchawi, mtunga mashairi, abtair (mkiwa) na matusi mengineyo. Pamoja na kufanyiwa madhila yote hayo, bado Mitume walisimama kidete kuufikisha ujumbe wa Mwenyezi Mungu (s.w) kwa watu wao na wala hawakukata tamaa.Ni nguvu gani iliyowapa Mitume ustahimilivu kiasi hicho? Je,kuna malipo yoyote ya hapa duniani waliyoyapata ndiyo yakawafanya kuwa wastahamilivu kiasi hicho? Je, Mitume hawakuwa na tegemeo la kulipwa na mwenye uwezo juu ya kila kitu anayestahiki kutegemewa na kuogopwa kuliko yeyote yule? Bila shaka uvumilivu na subira ya hali ya juu waliyokuwa nayo Mitume ni alama kuwa yuko mwenye nguvu na uwezo juu ya kila kitu waliyekuwa wakimtegemea na kutaraji ujira mkubwa kutoka kwake.

(v) Ujasiri wa Mitume mbele ya Viongozi wa jamii ya kishirikina Mitume hawakumchelea yeyote katika kuwafikishia watu ujumbe waliotumwa kuufikisha.Hawakufikisha ujumbe wao kwa watu wa kawaida tu bali waliwaendea Wafalme na watawala wa jamii waliokuwa wapinzani wakubwa wa ujumbe wa Mwenyezi Mungu (s.w). Mitume waliwaelekea wakuu hao wa jamii pamoja na takaburi zao na vitisho vingi walivyovitoa dhidi yao. Kwa mfano Nabii Ibrahiim hakumchelea baba yake katika kumfikishia ujumbe wa kumpwekesha Mwenyezi Mungu (s.w) kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:

﴿إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ يَا أَبَتِ لِمَ تَعْبُدُ مَا لَا يَسْمَعُ وَلَا يُبْصِرُ وَلَا يُغْنِي عَنكَ شَيْئًا ﴿٤٢﴾ يَا أَبَتِ إِنِّي قَدْ جَاءَنِي مِنَ الْعِلْمِ مَا لَمْ يَأْتِكَ فَاتَّبِعْنِي أَهْدِكَ صِرَاطًا سَوِيًّا ﴿٤٣﴾ يَا أَبَتِ لَا تَعْبُدِ الشَّيْطَانَ إِنَّ الشَّيْطَانَ كَانَ لِلرَّحْمَـٰنِ عَصِيًّا ﴿٤٤﴾ يَا أَبَتِ إِنِّي أَخَافُ أَن يَمَسَّكَ عَذَابٌ مِّنَ الرَّحْمَـٰنِ فَتَكُونَ لِلشَّيْطَانِ وَلِيًّا ﴿٤٥﴾ قَالَ أَرَاغِبٌ أَنتَ عَنْ آلِهَتِي يَا إِبْرَاهِيمُ لَئِن لَّمْ تَنتَهِ لَأَرْجُمَنَّكَ وَاهْجُرْنِي مَلِيًّا﴾

(Wakumbushe) alipomwambia baba yake: "Ewe baba yangu! Kwanini unaabudu visivyosikia na visivyoona na visivyo kufaa chochote?Ewe baba yangu!Kwa yakini imenijia ilimu isiyokujia. Basi nifuate nitakuongoza njia iliyosawa.Ewe baba yangu! Usimuabudu shetani, hakika shetani ni mwenye kumuasi (Mwenyezi Mungu) Mwingi wa rehma.Ewe baba yangu! Hakika naogopa kukupata adhabu inayotoka kwa Mwingi wa Rehma (Mwenyezi Mungu), ukifanya hivyo) utakuwa mwenziwe shetani".Akasema (yule baba yake):"Je, unaichukia miungu yangu, ewe Ibahimu? Kama huachi (haya unayoyasema) lazima nitakupiga mawe.Na niondokelee mbali, kwa muda mchache (huu). (19:42-46)

Nabii Ibrahim hakuishia kuufikisha ujumbe kwa baba yake tu, bali aliufikisha pia kwa vitendo kwa jamii nzima kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:

﴿وَتَاللَّـهِ لَأَكِيدَنَّ أَصْنَامَكُم بَعْدَ أَن تُوَلُّوا مُدْبِرِينَ ﴿٥٧﴾فَجَعَلَهُمْ جُذَاذًا إِلَّا كَبِيرًا لَّهُمْ لَعَلَّهُمْ إِلَيْهِ يَرْجِعُونَ ﴿٥٨﴾ قَالُوا مَن فَعَلَ هَـٰذَا بِآلِهَتِنَا إِنَّهُ لَمِنَ الظَّالِمِينَ ﴿٥٩﴾ قَالُوا سَمِعْنَا فَتًى يَذْكُرُهُمْ يُقَالُ لَهُ إِبْرَاهِيمُ ﴿٦٠﴾ قَالُوا فَأْتُوا بِهِ عَلَىٰ أَعْيُنِ النَّاسِ لَعَلَّهُمْ يَشْهَدُونَ ﴿٦١﴾ قَالُوا أَأَنتَ فَعَلْتَ هَـٰذَا بِآلِهَتِنَا يَا إِبْرَاهِيمُ ﴿٦٢﴾ قَالَ بَلْ فَعَلَهُ كَبِيرُهُمْ هَـٰذَا فَاسْأَلُوهُمْ إِن كَانُوا يَنطِقُونَ ﴿٦٣﴾ فَرَجَعُوا إِلَىٰ أَنفُسِهِمْ فَقَالُوا إِنَّكُمْ أَنتُمُ الظَّالِمُونَ ﴿٦٤﴾ ثُمَّ نُكِسُوا عَلَىٰ رُءُوسِهِمْ لَقَدْ عَلِمْتَ مَا هَـٰؤُلَاءِ يَنطِقُونَ ﴿٦٥﴾ قَالَ أَفَتَعْبُدُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ مَا لَا يَنفَعُكُمْ شَيْئًا وَلَا يَضُرُّكُمْ ﴿٦٦﴾ أُفٍّ لَّكُمْ وَلِمَا تَعْبُدُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ أَفَلَا تَعْقِلُونَ ﴿٦٧﴾ قَالُوا حَرِّقُوهُ وَانصُرُوا آلِهَتَكُمْ إِن كُنتُمْ فَاعِلِينَ﴾

"Na wallahi (kwa haki ya Mungu) nitayafanyia mabaya masanamu yenu haya baada ya kunipa mgongo mkenda zenu." Basi akayavunja (masanamu yote yale) vipande vipande isipokuwa lile kubwa lao (aliliacha), ili wao (hao makafiri) walirudie. Wakasema: "Nani aliyeifanya hivi miungu yetu? Hakika huyo yu miongoni mwa madhalimu (wakubwa).Wakasema: "Tulimsikia kijana mmoja akiwataja anayeitwa Ibrahim.Wakasema: Basi mleteni mbele ya macho ya watu, wamshuhudie (kwa ubaya wake huyo)" Wakasema: "Je!Wewe umeifanya hivi miungu yetu, Ee Ibrahim? Akasema: Siyo,bali amefanya (hayo) huyu mkubwa wao, basi (muulizeni na) waulizeni (pia hao waliovunjwa) kama wanaweza kusema! Basi wakajirudi nafsi zao, (wakafikiri udhalilifu wa waungu hao walio nao, wasioweza kujipigania) na wakasema: "Hakika nyinyi mlikuwa madhalimu (wa nafsi zenu kwenda kuwaabudu wasiokuwa na maana)." Kisha wakainamishwa vichwa vyao, (wakarejea ujingani, ukafirini, wakasema): "Hakika umekwishajua ya kwamba hawasemi, (kwa nini unatucheza shere?).Akasema: "Je! Mnaabudu badala ya Mwenyezi Mungu (miungu) isiyokufaeni chochote(mnapowaabudu) wala kukudhuruni (chochote mnapoacha kuwaabudu? Kefule (udhalilifu) yenu na ya hivyo mnavyoviabudu kinyume na Mwenyezi Mungu. Je! hamfikiri? (21:57- 67)

Pia Nabii Ibrahim(a.s) alimkabili mfalme na kuhojiana naye. - Rejea Qur-an (2:258)

(vi) Ushindi wa Mitume dhidi ya maadui Jambo jingine tunalojifunza katika historia ya Mtime ambalo ni miongoni mwa dalili kubwa za kuonyesha kuwepo kwa Mwenyezi Mungu (s.w) ni ushindi waliokuwa wakiupata Mitume na wafuasi wao wachache dhidi ya maadui zao. Mara zote walikuwa wapinzani wakubwa wa ujumbe wa Mwenyezi Mungu (s.w) walikuwa watawala wa walioshikilia dola na matajiri waliokuwa na wafuasi wengi na majeshi yenye nguvu kubwa. Kwa upande mwingine, katika jamii zote, walioamini Mitume walikuwa wachache na wengi wao wakiwa wanyonge wa jamii. Pamoja na hivyo Mitume na waumini wachache wanyonge waliwashinda maadui zao walikuwa na nguvu kwa kiasi kikubwa.

Hebu turejee mifano michache ifuatayo: Nabii Nuhu(a.s) aliwalingania watu wa jamii yake kwa miaka 950. Lakini watu wake pamoja na kutishia kumuua, walimtaka awaletee kutoka kwa Mola wake hiyo adhabu aliyokuwa akiwatahadharisha kwayo ikiwa anasema kweli kuwa yeye ni Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.w). Mwishowe adhabu kweli ililetwa na wakawa ni wenye kugharikishwa kama tunavyojifunza katika Qur-an: Basi kwa ajili ya makosa yao waligharikishwa wakaingizwa motoni wala hawakuwapata wa kuwanusuru mbele ya Mwenyezi Mungu (s.w). (71:25) Nabii Hud(a.s) alitumwa kwa watu wa Ad na kuwafikishia ujumbe wa Mwenyezi Mungu (s.w). Lakini wengi wao wakiongozwa na watawala na matajiri walitakabari na kukataa na kuwa dhidi yake na wafuasi wachache walioamini pamoja naye. Kisha Mwenyezi Mungu (s.w) alimnusuru Mtume wake na walioamini pamoja naye kutokana na madhalimu kama tunavyojifunza katika Qur-an:

﴿٧٢فَأَنجَيْنَاهُ وَالَّذِينَ مَعَهُ بِرَحْمَةٍ مِّنَّا وَقَطَعْنَا دَابِرَ الَّذِينَ كَذَّبُوا بِآيَاتِنَا وَمَا كَانُوا مُؤْمِنِينَ﴾

Basi tukamuokoa yeye na waliokuwa pamoja naye kwa rehema zetu, na tukakata mizizi ya wale waliozikadhibisha aya zetu, na (ambao) hawakuwa wenye kuamini. (7:72).

Nabii Musa(a.s) na wana wa Israil waliokolewa kutokana na makucha ya dhalimu Firaun na majeshi yake kama tunavyojifunza katika Qur-an:

﴿فَأَتْبَعُوهُم مُّشْرِقِينَ ﴿٦٠﴾فَلَمَّا تَرَاءَى الْجَمْعَانِ قَالَ أَصْحَابُ مُوسَىٰ إِنَّا لَمُدْرَكُونَ ﴿٦١﴾ قَالَ كَلَّا إِنَّ مَعِيَ رَبِّي سَيَهْدِينِ ﴿٦٢﴾ فَأَوْحَيْنَا إِلَىٰ مُوسَىٰ أَنِ اضْرِب بِّعَصَاكَ الْبَحْرَ فَانفَلَقَ فَكَانَ كُلُّ فِرْقٍ كَالطَّوْدِ الْعَظِيمِ ﴿٦٣﴾ وَأَزْلَفْنَا ثَمَّ الْآخَرِينَ ﴿٦٤﴾ وَأَنجَيْنَا مُوسَىٰ وَمَن مَّعَهُ أَجْمَعِينَ ﴿٦٥﴾ ثُمَّ أَغْرَقْنَا الْآخَرِينَ ﴿٦٦﴾ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ ﴿٦٧﴾ وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ﴾

Basi (watu wa Firaun na mwenyewe nafsi yake Firaun) wakawafuata (Nabii Mussa na watu wake) lilipotua jua. Na yalipoonana majeshi mawili (haya, watu wa Nabii Musa wanakimbia, na Firauni na watu wake wanawafuatia). Watu wa Musa walisema: "Hakika tutakamatwa. (Musa) akasema: "La, kwa yakini Mola wangu yu pamoja nami, bila shaka ataniongoza (tuokoke sote)". Mara tulimpelekea Wahyi Musa (tukamwambia): "Piga bahari kwa fimbo yako". Basi ikatengana, na kila sehemu ikawa kama jabali kubwa. Na tukawaleta hapo wale wengine (nao ni firauni na watu wake). Na tukamuokoa Musa na wale waliokuwa pamoja naye wote.Kisha tukawagharikisha hao wengine. Hakika katika hayo muna mazingatio: lakini wengi katika wao si wenye kuamini. Na kwa yakini Mola wako ndiye Mwenye Nguvu, mwenye Rehema. (26:60-68)

Mfano wa mwisho ni ule unaopatikana katika historia ya Mtume Muhammad(s.a.w.w) na wafuasi wake. Vita vya kwanza vikubwa alivyopigana Mtume (s.a.w) na wafuasi wake dhidi ya maadui wa Mwenyezi Mungu ni vita vya Badr. Katika vita hivyo jeshi la makafiri wa Kiquraish lililojizatiti barabara lilikuwa na watu 1000 ambapo jeshi la Waislamu lisilojiandaa vizuri kivita lilikuwa na wanajeshi 300 tu hivi. Pamoja na udogo na uduni wa jeshi, Waislamu walipata ushindi mkubwa kwa msaada kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w) kama tunavyojifunza katika Qur-an:

﴿إِذْ تَسْتَغِيثُونَ رَبَّكُمْ فَاسْتَجَابَ لَكُمْ أَنِّي مُمِدُّكُم بِأَلْفٍ مِّنَ الْمَلَائِكَةِ مُرْدِفِينَ ﴿٩﴾ وَمَا جَعَلَهُ اللَّـهُ إِلَّا بُشْرَىٰ وَلِتَطْمَئِنَّ بِهِ قُلُوبُكُمْ وَمَا النَّصْرُ إِلَّا مِنْ عِندِ اللَّـهِ إِنَّ اللَّـهَ عَزِيزٌ حَكِيمٌ﴾

(Kumbukeni) mlipokuwa mkiomba msaada kwa Mola wenu, naye akakujibuni kuwa:"Kwa yakini Mimi nitakusaidieni kwa malaika elfu moja watakaofuatana mfululizo (wanaongezeka tu)". Na mwenyezi Mungu hakufanya haya ila iwe bishara (habari ya furaha) na ili nyoyo zenu zituwe kwayo. Na hakuna msaada (wa kufaa) ila utokao kwa Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu (na) Mwenye hikima. (8:9-10).

Ushindi wa Mitume na wafuasi wao haukupatikana ila kwa msaada kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w). (vii) Mitume kutohitajia malipo kutoka kwa watu wao:

Mitume, tofauti na viongozi wengine waliojitokeza katika jamii mbalimbali, hawakuifanya kazi yao ya kuwaongoza watu katika njia ya Mwenyezi Mungu (s.w) kwa kutarajia maslahi yoyote si ya hali wala ya mali, kutoka kwa watu wao. Waliifanya kazi hiyo kama watumishi wa Mwenyezi Mungu (s.w) na ni yeye pekee waliyemtegemea awalipe kwa kazi hiyo. Daima walikuwa wakiwakumbusha watu wao jambo hili kama tunavyorejea katika Qur-an:

﴿وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ﴾

"Wala sikutakini juu yake ujira, ujira wangu hauko ila kwa (Mwenyezi Mungu) Mola wa walimwengu wote"(26:127)

Mitume wasingelikuwa wajumbe wa Mwenyezi Mungu (s.w) wenye uhakika wa kupata ujira mkubwa kwake kwa kazi yao, kitu gani kingeliwazuia wasitake malipo kutoka kwa watu wao, kama viongozi wa kawaida wa jamii za wanaadamu wanavyotaka malipo kutoka kwa watu wao?


6

7

8

9

10

11

12

13

14

15