MUANDAMO WA MWEZI

MUANDAMO WA MWEZI 0%

MUANDAMO WA MWEZI Mwandishi:
Kundi: Midahalo na majadiliano kielimu

MUANDAMO WA MWEZI

Mwandishi: Juma Muhammad Rashid Al-Mazrui, Al-Zenjibari.
Kundi:

Matembeleo: 59560
Pakua: 4997

Maelezo zaidi:

MUANDAMO WA MWEZI
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 23 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 59560 / Pakua: 4997
Kiwango Kiwango Kiwango
MUANDAMO WA MWEZI

MUANDAMO WA MWEZI

Mwandishi:
Swahili

10

MUANDAMO WA MWEZI

MATN YA HADITHI

Ama kuhusu matn ya Hadithi hii, na kuhusu madai yenu mulioyakariri bila ya kujibu nilioyasema, mimi nilisema hivi: Suala jengine muhimu katika Hadithi hii na ambalo linahusiana zaidi na mizozo na migogoro yetu ya mwezi muandamo katika Afrika ya Mashariki, ni kuwa je Hadithi hii inathibitisha usahihi wa dai la kwamba muandamo wa mji mmoja ni muandamo wa ulimwengu mzima? Katika kitabu chake Sheikh Nassor Abdallah Bachoo, baada ya kuinukuu Hadithi ya bedui, alitoa maelezo haya:

"Pia jambo la kuzingatia hapa ni kwamba ilivyokuwa mtu huyo alikuwa ni Bedui yaani mtu wa Majangwani, Mtume(s.a.w.w) angeweza kumuuliza anatoka wapi, lakini hakumuuliza kabisa suala hili jambo ambalo linathibitisha kuwa suala la umbali gani wa kuonekana mwezi Mtume(s.a.w.w) hakuwa akilizingatia hata kidogo!!!" Mwisho wa kunukuu.

Lakini nadharia hii ya Sheikh Nassor Bachoo, haikutokana na fikra sahihi. Labda tuulize suala ili iwe ndio jawabu ya madai haya ya Sh. Nassor Bachoo. Suala ni kuwa: je Sheikh Bachoo anadhani kwamba bedui huyo alitoka wapi mpaka akaweza kufika kwa Mtume(s.a.w.w) usiku huo huo wa muandamo wa mwezi na akampa habari hio? Je anadhani kuwa bedui huyo alitoka Sham, Misr, Yemen au Oman? Ni wazi kwamba bedui atayeweza kwenda kwa Mtume(s.a.w.w) kumpa habari hio usiku huo huo au hata usiku wa pili na wa tatu, basi atakuwa ni bedui wa jangwa la hapo hapo Madina. Na kwa hivyo Mtume(s.a.w.w) - naye ndiye mkamilifu wetu kwa akili na elimu - hakuwa na haja ya kumuuliza unatoka wapi. Ivo tuseme katika wakati ambao hapakuwa na ndege wala vyombo vyovyote vyenye kwenda kwa kasi akakujia mtu baada ya Isha akakwambia nimeuona mwezi, nawe upo Bumbwini au Mahonda, utahitaji kumuuliza anapotoka? Ni wazi kwamba mtu huyo atakuwa anatoka katika miji hio hio ya Zanzibar. Kwa hivyo, bedui alikuwa ni bedui wa Madina ndio maana akaweza kufika kwa Mtume(s.a.w.w) usiku huo huo. Na kwa hivyo Mtume(s.a.w.w) hakuhitaji kumuuliza anapotoka.

Lakini baada ya maelezo hayo ya kiakili ambayo yako wazi kwa kila mwenye kutafakari, ni bora tuwaachie wapokezi wa Hadithi watueleze bedui huyo alitokea wapi. Ikrima - mwanafunzi wa Ibn Abbas - anaeleza kwamba bedui huyo alikuwa akitokea Al-harrah nayo ni sehemu yenye mawe mawe katika eneo la Madina. Na kwa maelezo haya mafupi, unabainika udhaifu wa dai hilo la Sh. Bachoo la kukufanya kule Mtume(s.a.w.w) kutomuuliza bedui anapotoka, kuwa ni dalili ya kutozingatia masafa, a kitegemea Hadithi hio ya bedui, kwani bedui huyo anajulikana kwamba anatoka Madina: si mahala pengine.

Hayo ndio nilioyasema na yote haya nyinyi hamukuyajibu - si sanad wala si matn, bali mumekariri kitu kile kile ambacho nimeshakijibu, na huu sio mjadala wa kielimu. Mjadala wa kielimu ni kuwa nukta inayojibiwa kwa uwazi huwa haikaririwi tena bali hutazamwa mule ambamo hamukujibiwa. Lakini hayo, ni kwa wale wenye kujua nini maana ya debate. Ama kanuni isemayo: "Kuacha kuuliza pahala ambapo ilikuwa inayumkini kuuliza basi inamaanisha kuwa hii ni hukmu ya jumla ('aam) isiyokuwa na mipaka." Kanuni hii, haihusiani na riwaya hio ya Bedui. Kanuni hii - nayo ni ya Al-Imamu Al-Shafi kwa ninavyokumbuka - inazun gumzia kitu ambacho hakijulikani na hakikuulizwa; si kitu chenye kujulikana. Na asili ya kanuni hii imejengwa katika Hadithi zenye kusimulia Sahaba aliyesilimu naye ana wake wengi zaidi ya wane. Mtume (s.a.w.) akamuamuru awaache abakishe wane. Yule sahaba hakuuliza Mtume(s.a.w.w) je wa kuachwa ni waliolewa mwisho au wowote tu, na Mtume(s.a.w.w) naye hakumbainishia. Kwa hivyo, Maulamaa - nadhani wa mwanzo wao ni Al-Imamu Al-Shafi - ndio wakatoa kanuni hio kutoka katika Hadithi hio. Ama bedui aliyekwenda kwa Mtume(s.a.w.w) usiku wa muandamo au hata siku ya pili na ya tatu, basi ni badui wa jangwa hilo hilo la Madina: si bedui wa Oman, Yemen au Sham. Nadhani hili - ikiwa hamutaki ubishi - basi liko wazi. Juu ya hayo, riwaya yenyewe imesema kwamba huyo bedui alikuwa akitoka wapi. Ikrima - mwanafunzi wa Ibn Abbas - anaeleza kwamba bedui huyo alikuwa akitokea Al-harrah nayo ni sehemu yenye mawe mawe katika eneo la Madina. Sasa uko wapi uhusiano wa kanuni hii na hadithi ya bedui?!!!!!!!!

Ama kanuni isemayo: "Jambo la asli halihitaji (kuletewa) dalili, (lakini dalili inahitajika katika jambo lisilo la asili)" lau muliifahamu kanuni hii, musingeliniambia kuwa nilete ushahidi wa kuwepo kwa matalai ya mwezi, k wani jambo linalojulikana kwamba ndio lilivyo basi halihitaji ushahidi. Lakini nyinyi ndugu zangu hamusemi kitu kwa maarifa sahihi, bali muna msimamo wenu huo hamutaki kuuwacha na anayekupungeni huwa yeye si mtu wa msimamo. Munasema Je nini hukmu ya kadhia hii? Ni vyema tusogeze karibu mezani yetu ya Mustalahul-Hadiyth ili tuone kipimo sahihi na chenye uzito mkubwa kipo upande gani:

"Atakapokwenda kinyume mpokezi (wa Hadiyth) kwa kile alichokipokea; Je hutangulizwa (katika hukmu ya jambo hilo ) njia (madhehebu) ya mpokeaji (namna alivyofanya yeye) au itatangulizwa habari (yaani) kile alichokipokea? Jamhuri ya Wanavyuoni wa Usulul-Fiqhi na Wanavyuoni wa Fiqhi - wakiwemo Imamu Shafi na Abul-Hassan wameonelea kwamba kilicho wajibu kutendewa kazi ni ile habari aliyoipokea mpokeaji sio ile tafsiri (ya tendo) la mpokezi. Kwani chenye kuzingatiwa juu ya kadhia hii ni kile alichokipokea (Swahaba kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) sio kile anachokiona yeye katika rai yake au alichokitenda."

Habari hizi zinapatikana katika vitabu vifuatavyo: 1. Al - Ihkamu Fii Usulil-Ahkam J. 2

2. Irshadul-Fuhul.

3. Khabaril-Waahid Wahujjiyatuh.

4. Al-Fatawa-Swala, Zakka, Swaum wa Hajj - kitabu cha 1 uk 268.

Jawabu

Kanuni hio ni sahihi, lakini wapi Ibn Abbaas kenda kinyume na riwaya yake. Riwaya ya Ibn Abbaas - pamoja na udhaifu wa sanad yake - inasema: ((Kutoka kwa Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) kwamba bedui mmoja alikuja kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Nimeuona mwezi." Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia: "Unashuhudia kwamba hakuna anayepaswa kuabudiwa isipokuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala)?" akasema: "Ndio." Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Ewe Bilal watangazie watu kesho wafunge.")). Haya iko wapi humu kwamba watu wafunge kwa muandamo mmoja, hata iwe Ibn Abbaas kenda kinyume na riwaya hii alipouacha muandamo wa Sham? Naona ndugu zangu munasema tu mambo bila hata ya kufikiri! Ama yale ya Mtume(s.a.w.w) kutokumuuliza bedui atokapo tumeshajibu.

MNASEMA

Baada ya kuona uzito uliopo katika mezani ya Mustalahul-Hadiyth. Ni vyema tuangalie tena mfano mwengine ufuatao:- Kuhusu Sahaba Abu Hurayra (Radhiya Allaahu 'Anhu) alivyopokea hukmu ya chombo kilichorambwa na mbwa. Sahaba huyu ndiye aliyepokea Hadiyth kutoka kwa Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwamba chombo kilichorambwa na mbwa kisafishwe kwa kuoshwa kwa maji mara saba; moja kati ya hizo isafishwe kwa mchanga. Katika mapokezi mengine Abu Hurayra (Radhiya Allaahu 'Anhu) huyu huyu ameshuhudiwa kutoka kwa Sa'iyd bin Musayab kwamba yeye Abu Hurayra alikiosha chombo mara tatu katika sehemu ambayo ilitiwa mdomo na mbwa.

Imeonekana kitendo hicho cha Abu Hurayra (Radhiya Allaahu 'Anhu) kimetofautiana na maneno aliyoyapokea kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Kwa jambo hilo , Wanavyuoni wote wa Kishafi wamesema chombo kilichorambwa na mbwa kioshwe mara saba na wala sio mara tatu. Kwa mantiki hiyo wameona washike yale maneno yake Abu Hurayra aliyoyapokea kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na wameacha kushika kile kitendo chake. Kwa hivyo cha kuzingatia ni yale maneno yaliyopokewa na wala sio kitendo cha aliyepokea. Kwani huenda mpokeaji akaghafilika, lakini maneno yakabaki vile vile na ndiyo yanayostahiki kutendewa kazi. Haya ni kwa mujibu wa misingi ya Shari'ah, Qur-aan na Sunnah. Tokeo hili ni sawa katika hukmu na tokeo la Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) katika kisa cha Kuraib, kama vile Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) alipokea kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikubali habari za mwezi zilizoletwa na bedui asiyetambulika na bila ya kumuuliza anatokea wapi au mwezi aliuona wapi. Halafu Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) huyu huyu hakuukubali mwezi ulioonekana na Kuraib pamoja na watu wengine huko Sham.

JAWABU

Hivyo alivyofanya Abu Huraira ndio mpokezi kwenda kinyume na riwaya yake: sio yale yaliomo katika riwaya ya Ibn Abbaas na Kuraib kwa upande mmoja na riwaya ya Ibn Abbaas na bedui kwa upande wapili. Kule hakuna kwamba katika riwaya moja Ibn Abbaas kaambiwa fungeni kwa muandamo mmoja kisha katika riwaya ya pili akafunga kwa muandamo tafauti. Wala hili halifahamiki katika riwaya hio kamwe kama tulivyobainisha vya kutosha.

MNASEMA

Hapo ndipo tunapowajibika kushika yale maneno aliyoyapokea Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) na kukiacha kitendo chake. Lililo bora ni kushika yale maneno ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) yaliyo wazi kuwa mwezi ukionekana (popote) watu wafunge au wafungue na hivyo ndivyo alivyofanya mwenyewe Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) bila ya kuzingatia wapi umeonekana mwezi. Kauli yake ilikuwa kama ifuatavyo:"Fungeni kwa kuonekana mwezi - muandamo na fungueni kwa kuonekana mwezi - muandamo"

JAWABU

Ama kudai kwamba: "Hapo ndipo tunapowajibika kushika yale maneno aliyoyapokea Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) na kukiacha kitendo chake. Lililo bora ni kushika yale maneno ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) yaliyo wazi".

Hio ni dhana dhaifu sana. Kwa bahati tumekubaliana kwamba twende kwa mujibu wa kanuni. Utakumbuka kwamba riwaya ya Ibn Abbaas na Kuraib inasema: Hivi ndivyo alivyotuamrisha Mtume(s.a.w.w) .. Kwa hivyo, kwa mujibu wa fani ya Hadithi 'Ulumul Hadith hii pia ni Hadithun Marfu'u sawa na Hadithi isemayo:"Fungeni kwa kuonekana mwezi - muandamo na fungueni kwa kuonekana mwezi - muandamo" . Na hivi ndivyo walivykobaliana wajuzi. Anasema Al-Suyuti alipokuwa akizungumzia Hadithun Marfu'u: "Akiwa (sahaba) atasema: 'Mtume s.a.w. katuamuru, basi hakuna khilafu ndani yake (hio ni Hadithun Marfu'u)'.

Kwa hivyo, kuifanya Hadithi (Fungeni kwa kuonekana mwezi - muandamo na fungueni kwa kuonekana mwezi - muandamo.) kuwa ndio Hadithi ya Mtume(s.a.w.w) na Hadithi "Hivi ndivyo alivyotuamrisha Mtume(s.a.w.w) " kuwa ni maneno ya Ibn Abbas ni kosa la kiminhaj (Methodolocal error); hilo halikubaliki katika elimu ya Hadithi. Zote hizo ni Hadithi za Mtume(s.a.w.w) , na kwa hivyo, kilichobaki ni kutafuta hii ina maana gani na hile ina maana gani. Tena nakukumbusheni kauli yenu muliposema: "Isipokuwa Sahaba akisema: "Tumeamrishwa kadha" au "Tumekatazwa kadha." Jambo hilo hupewa hukumu ya "Rafii" yaani hio inazingatiwa kuwa ni Hadithi ya Mtume(s.a.w.w).

Tumesema: ama Hadithi"Fungeni kwa kuuona" ni andiko la wazi juu ya uwajibu wa kufunga kwa kuuona mwezi. Kw a hivyo, lazima tufunge kwa kuuona: si kwa kalenda wala si kufunga siku ya shaka. Hili ndilo linalothibitishwa na Hadithi hio:Fungeni kwa kuuona ." Lamu iliomo katika neno (Liru-uyatihi) ni H arfu Jarri li-tta'alil. Yaani ni harufu yenye kulitia neno kasra na kuonesha sababu ya maneno yaliotangulia au sababu ya hukumu iliotajwa. Kwa hivyo, maana ya haya ni kuwa kuuona mwezi iwe ndio sababu ya kufunga au kwa lugha nyengine sababu ya kufunga iwe ni kuuona mwezi. Hii ndio maana ya meneno"Fungeni kwa kuuona:" Hakuna hapa kinachoonesha mas-ala ya kufunga kwa muandamo mmoja au miandamo tafauti.

Ama Hadithi ya Ibn Abbaas na Kuraib, ambayo ndani yake tunapata kuwa Ibn Abbaas aliukataa kuufata muandamo wa Sham na kusema: Hivi ndivyo alivyotuamrisha Mtume(s.a.w.w ) Hadithi hii ni ushahidi kwamba muandamo wa mbali si hoja kwa walio mbali. Hivi ndivyo, taratibu za kifan i zinavyotutaka: tuyakusanye maandiko madamu inawezekana: sio moja tulitendee kazi jengine tulitupe. Kwa hivyo, natija ni kuwa:

a) Lazima tufunge kwa kuuona: si kwa kalenda wala si kufunga siku ya shaka. Hili linathibiti kwa Hadithi: Fungeni kwa kuuona."

b) Muandamo wa mbali hautendewi kazi mbali. Hili linathibiti kwa kitendo cha Ibn Abbas cha kuukataa muandamo wa Sham na kubainisha kwamba hicho ndicho alichokifunza Mtume(s.a.w.w) . Munasema Suala Jengine: Je masimulizi ya Kuraib na Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) ndio yanakuwa makhsusi katika Hadiyth za Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) zilizotaja habari za kufunga na kufungua? Ni vyema kuweka wazi kwamba Hadiyth zote za Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aali hi wa sallam) ambazo ni nyingi mno (Mutawaatir) zilizotaja habari ya kufunga na kufungua mwezi wa Ramadhaan zote zimekuja kwa ujumla - ('aam) Bila kuhusisha watu wa nchi fulani, masafa au matlai ya aina yoyote. Angalia: Agizo hilo limekuja kwa watu wote. Masimulizi ya Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) na Kuraib yalitokea zaidi ya miaka 30 baada ya kufa kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kwamba Makhalifa wote wanne walikwishaondoka duniani. Kwa hivyo kuyafanya masimulizi hayo ya Kuraib kuwa ndiyo 'Khaas' katika Hadiyth hizo za kufunga na kufungua Swaum ni kinyume na kanuni za kifani. Ni vyema kuwaangalia Wanavyuoni wa fani ya Usulil-Fiqhi wanasema nini katika vitabu vyao kwenye huu mlango wa ('aam) - yaani maana ya ujumla na upamoja kwa watu wote:

JAWABU

1) Naam! Masimulizi ya Kuraib na Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) ndio yanakuwa makhsusi, kwa kuwa yanawahusisha watu wa sehemu pasi na wengine; wakati katika masimulizi mengine hili hulipati.

2) Ama dai kwamba "Hadiyth zote za Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ambazo ni nyingi mno (Mutawaatir) zilizotaja habari ya kufunga na kufungua mwezi wa Ramadhaan zote zimekuja kwa ujumla - ('aam)", si dai sahihi. Sasa riwaya zote zikija kwa uj umla - ('aam), ndio Hadithi ya Ibn Abbaas ishakuwa batili?!!! Au tufate kanuni kwamba andiko mahususi ndilo linalotangulizwa kuliko andiko la ujumla.

3) Pili: Je ujumla huo ni ujmla katika mazingato gani? Ujumla uliomo katika riwaya nyengine ni kama tulivyoeleza ni ujumla kwamba watu wote ni lazima wafunge kwa kuuona: wala hakuna katika Hadithi yoyote ujumla kwamba watu wote wafunge sawa. Suala je tufunge pamoja au tafauti halimo katika riwaya "Fungeni kwa kuuona" wala katika riwaya ziliokurubiana na hii kilafdhi. Bali riwaya hizi zinahimiza kwamba mfungo na mfunguo uwe kwa mujibu wa kuuona mwezi. Ama je muandamo wa mbali unakuwa hoja kwa walio mbali au haui, hilo linabainishwa na riwaya ya Ibn Abbas na Kuraib.

4) Ama dai kwamba: "Masimulizi ya Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) na Kuraib yalitokea zaidi ya miaka 30 baada ya kufa kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kwamba Makhalifa wote wanne walikwishaondoka duniani". Sijui dai hili linathibitisha nini? Kwani masimulizi yakiwa baada ya miaka 30 huwa yanabatilisha riwaya? Na kwani Makhalifa wakiondoka ndio riwaya huwa hazisimuliwi tena?! Masimulizi ya riwaya yana sharti zake zikitimia basi riwaya inazingatiwa.

5) Ama kudai: "Kwa hivyo kuyafanya masimulizi hayo ya Kuraib kuwa ndiyo 'Khaas' katika Hadiyth hizo za kufunga na kufungua Swaum ni kinyume na kanuni za kifani". Tunauliza: ni kinyume na fani gani hio? Tuleteeni hio fani inayoonesha kuwa kutegemea ri waya ya Ibn Abbaas na Kuraib ni kinyume na fani. Fani inasema kwamba "Kauli ya sahaba akisema Mtume s.a.w. katuamuru kadha au katukataza kadha" hio ni Hadithi ya Mtume. Kwa hivyo, hii ni Hadithi ya Mtume (s.a.w.). Sasa wapi umesikia kwamba au ni fani gani isemayo kwamba ni kosa kuuhusisha ujumla wa Hadithi moja kwa Hadithi nyengine?

MNASEMA

Ifuatayo ni tafsiri kwa njia ya maana bila ya kutafsiri neno kwa neno: "Ili khaas ikubalike katika misingi ya Shari'ah kama ni hoja sahihi lazima khaas hiyo iepukane na utata. Kuwepo kwa utata ndani ya khaas kutaifanya kukosa kuwekwa mbele kwenye safu za hoja. Kwa hivyo (kielimu) haitaweza kutegemewa kwa namna yoyote ile. Na badala yake itabakia kuwa ni ya ujumla ('aam) katika kuwajumuisha watu wot e popote walipo. Kwani kuwepo kwa utata ni tuhuma zisizo na ushahidi imara zinazoifanya khaas hiyo kwa mujibu wa kanuni za Usulil-Fiqh kutoweza kuzingatiwa.

JAWABU

Kwanza tafsiri yenu inataka kurekebishwa, pamoja kuwa mumejilinda kwa kusema: "Ifuatayo ni tafsiri kwa njia ya maana bila ya kutafsiri neno kwa neno". Na nadhani pia kuna kosa la chapa. Neno inavyoelekea munakusudia Wallahu A'alam. Na neno Ihtimal halina maana ya utata, bali maana yake ni uwezekano wa tafsiri hii na hile. Ama tafsiri ya maneno hayo ni hivi:

Ama (andiko la ujumla) kuwa lina uwezekano wa kuhusishwa (na andiko khaas specific) bila ya kuwepo dalili ya uwezekano huu, basi hilo ni katika yale yasiozingatiwa wala halitazamwi wala halitendewi kazi. Basi (hapo) ushahidi uliomo katika Aam (andiko la ujumla) unaendelea kubakia katika (ujumla wake wa) kukusanya sehemu zake za yakini. Wala kule kuwa kuna uwezakano tu (kwamba andiko Aam, andiko la ujumla) limehusishwa bila ya dalili hakuliathiri (kitu andiko hilo la Aam ujumla), kwani uwezekano huo ni katika kufikiri kitu kimakosa (illusion), na hakuna kuzingatia fikra ya kimakosa wala kufikiri kimakosa."

Hii ndio tafsiri ya maneno hayo. Sasa mumefahamu nini? Haitoshi mtu kufungua kitabu akatafuta kipande akanukuu ikiwa ile fani hajaisoma yote. Kinachozungumzwa hapa ni kuwa je ndiko Aam ni (la dhana) au ni (la uhakika na yakini)? Mahanafi wanasema ni (la uhakika na yakini); Jumhur wanasema ni (la dhana). Sasa wanaosema kuwa andiko hilo ni (la dhana) - nao ni Jumhur wanasema - wanajega hoja kwamba ndiko Aam linauwezekano wa kuwa limehusishwa kwani imesemwa kwamba hakuna ndiko Aam la ujumla ila huwa limehusishwa isipokuwa andiko kama "Hakika Allah ni Mjuzi wa k ila kitu" na yalio mfano wa hilo. Kwa hivyo, kwa kuzingatia kwamba maandiko Aam ya ujumla yote - taqriban - yamehusishwa, basi huwa hatuna yakini tunapolikuta andiko Aam la ujumla kwamba je ni kweli kila chenye kuhusiana na andiko hilo kimeingia au yameingia baadhi tu. Nikisema Wazanzibari ni wakarimu, je huwa kweli ni Wazanbari wote? Inawezekana ikawa wote na inawezekana ikawa si wote. Lakini kwa vile lafdhi Wazanzibari ni wakarimu inawaingiza wote, basi hapo ndio ikawekwa kanuni nyengine kwamba: "Andiko la ujumla linakwenda katika ujumla wake mpaka lipatikane andiko lenye kuhusisha." Nikikuta andiko jengine kwamba Mzanzibari si karimu, basi yeye huwa kahusiswa na andiko Khaas (specif ic au exceptional). Ama andiko khaas specific ni (la uhakika na yakini) kwa mujibu wa Jumhur. Na kwa hivyo, niksema Ali ni mkarimu, basi hili ni andiko la uhakika kwamba Ali kaingia katika ukarimu.

Ama wanaosema kwamba ndiko Aam la ujumla ni (la uhakika na yakini), nao ni Mahanafi, na kwamba andiko hilo linawaingiza wote wanaoingia katika lafdhi ya andiko hilo, ndio wanaosema hivyo: Ama (andiko la ujumla) kuwa lina uwezekano wa kuhusishwa (na andiko khaas specific) bila ya kuwepo dalili ya uweze kano huu, basi hilo ni katika yale yasiozingatiwa wala halitazamwi wala halitendewi kazi. Basi (hapo) ushahidi uliomo katika Aam (andiko la ujumla) unaendelea kubakia katika (ujumla wake wa) kukusanya sehemu zake za yakini. Wala kule kuwa kuna uwezakan o tu (kwamba andiko Aam, andiko la ujumla) limehusishwa bila ya dalili hakuliathiri (kitu andiko hilo la Aam ujumla), kwani uwezekano huo ni katika kufikiri kitu kimakosa (illusion), na hakuna kuzingatia fikra ya kimakosa wala kufikiri kimakosa." N a hao ni Mahanafi: si Jumhur. Kwa hivyo ni wazi kwamba ndugu zetu:

1) Hawakuyafahamu maana ya maneno walioyanukuu: wameyafasiri sivyo.

2) Hawakufahamu hii ni kauli ya akina nani.

3) Hawakufahamu muradi wake ni nini.

Kwa hivyo, maana ya maneno hayo si kwamba andiko lenye maana nyingi au lenye utata kama munavyoita nyinyi huwa halitumika kuhusisha ujumla. Hii sio maana ya maneno hayo. Bali hata ingelikuwa maana ya maneno hayo ni hivyo mulivyodhani nyinyi, basi hii ingekuwa dhidi yenu kwani Hadithi iliosemwa kuwa ina ihtimal uwezekano huu na hule ni Hadithi "fungeni kwa kuuona".

MNASEMA

Mukhtasari Wa Nukta Muhimu i). Kwa kuwa masimulizi ya Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) na Kuraib yana utatanishi - hayaeleweki kwa maana moja; hayawezi kuchukuliwa kama ni hoja kama walivyoeleza hayo Wanavyuoni wa Usulil-Fiqhi na Mustalahul-Hadiyth.

JAWABU

Tumejibu tayari kwamba hakuna utatanishi: utatanishi munao nyinyi. Bali Hadithi "Fungeni kwa kuuona" ndio yenye utata. Munasema

ii). Kwa kuwa Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) ameonyesha kinyume na vile alivyopokea Hadiyth ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hakiwezi tena kuchukuliwa kitendo chake kama ni hoja.

Jawabu Tumejibu kwa hoja za kielimu kwamba Ibn Abbaas hakwenda kinyume na alichokipokea kutoka kwa Mtume (s.a.w.) bali kilichopo ni Hadithi moja kuifasiri nyengine, kwani zote mbili - kwa mujibu wa fani - ni Hadithi za Mtume(s.a.w.w) .

Munasema iii). Katika Hadiyth iliyopokelewa habari ya kuonekanwa mwezi muandamo na bedui ambapo ingeyumkinika kuulizwa aliuona wapi mwezi muandamo lakini hakuulizwa.

JAWABU

Bedui anajulikana anapotokea. Ikrima - mwanafunzi wa Ibn Abbas - anaeleza kwamba bedui huyo alikuwa akitokea Al-harrah nayo ni sehemu yenye mawe mawe katika eneo la Madina. Na hata pasitajwe anapotokea, inajulikana kuwa anatoka katika jangwa la Madina kwani hakuna uwezekano katika zama hizo mtu kutoka Sham au Misr akafika Madina usiku wa muandamo au hata baada ya wiki nzima.

MNASEMA

Jambo hilo linapewa hukmu ya 'aam ujumla katika fani ya Usulil-Fiqhi. Wanavyuoni wamekuwa wakisema haya yafuatayo: "Hakika chenye kuzingatiwa baina ya njia aliyopita Sahaba (katika kutenda jambo fulani) na kile alichokipokea kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam); jambo la k ufaa kuzingatiwa katika hukmu ni kile alichokipokea (wala sio kile alichokitenda). Hata kama kitendo chake hicho kimepata umaarufu na kujulikana sana ." Hiyo ndio maana ya maneno ya Wanavyuoni wa Shari'ah yasemayo: "Chenye kuzingatiwa ni kile alichokipokea Sahaba kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wala sio kile alichokitenda kutokana na riwaya hiyo."

JAWABU

a) Maneno yenu na dalili mulioitoa ya kiusuli ni vitu viwili tafauti, jambo ambalo linathibitisha kwamba hamujui munasema nini. "Munasema: Jambo hilo linapewa hukmu ya 'aam ujumla katika fani ya Usulil-Fiqhi. Wanavyuoni wamekuwa wakisema haya yafuatayo".: Kisha mukataja kanuni isemayo: "Kikigongana kitendo cha Sahaba na riwaya yake inatangulizwa riwaya yake". Kanuni ina zungumzia mgongano wa rai na riwaya; nyinyi munaitumia kwamba ni dalili ya ujumla!!!

b) Ama ikiwa munakusudia kwamba Ibn Abbaas kenda kinyume na riwaya yake, hili tumelijibu kwamba si kinyume kwani zote ni Hadithi za Mtume(s.a.w.w) .

c) Katika Hadithi ya bedui hakuna kitu ujumla kamwe, ila vile kuwa bedui hakuulizwa atokapo ndiko mulikokudhania nyinyi kuwa hukumu yake ni ya ujumla. Lakini yeye hakuulizwa kwa sababu unajulikana anapotoka. Nimekuulizeni kama mimi niko Bumbwini katika zama za ngamia na punda ukanijia baada ya isha ukaniambia "Mwezi umeonekana", bado nitahitaji kukuuliza ulipoonekana. Si itakuwa umeonekana miji hio hio ya Unguja?

MNASEMA

iv). Ameandika mwanachuoni mmoja anayeitwa Shaykh Aadaud bin Ibrahim bin Umar kitabu cha Kiibadhi cha Usulul-Fiqh kinachosomeshwa mashuleni. Katika J. 2 uk 15 ameandika yafuatayo:

10. Kisha akafupisha kuandika kwenye Khulasa: Tafsiri yake ni kama ifuatavyo:- Atakapoeleza Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) juu ya hukmu ya jambo (fulani) na hukmu hiyo ikawa ina utata (yaani ina tafsiri zaidi ya moja) kisha Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa s allam) akanyamaza bila ya kutoa ufafanuzi mwengine wowote juu ya hukmu ya jambo hilo; itakuwa hukmu ya jambo hilo ni 'aam - yaani ni hukmu ya jambo lenye kuwajumuisha Waumini wote kwa pamoja, pamoja na kuwa jambo hilo lina utata.

JAWABU

Nimeshakufahamisheni nini maana ya kanuni hii. Hii inaeleza kitu ambacho kina uwezekano mwingi na hakijulikani: si kitu chenye kujulikana. Bedui alikuwa akijulikana atoka wapi, kwa hivyo, Mtume (s.a.w.) kutokumuuliza anapotoka haina maana kuwa masafa hayazingatiwi, kwani mtu anajulikana anapotoka. Pili: ni kuwa kilichomuhimu kukifahamu ni kwamba hio yenu ni istimbat; na la Ibn Abbaas ni andiko; na istimbat haina uwezo wa kubomoa andiko. Na kwa hivyo, wamesema katika kawaida za fiq-hi Hakuna kuizingatia dalili (isio wazi) mbele ya andiko lililowazi. Ubainifu wa hili ni kuwa Ibn Abbaas kasema kwa uwazi kwamba "Hivi ndivyo alivyotuamuru Mtume s.a.w." wakati katika hadithi ya bedui hakuna uwazi huu kwamba muandamo ni mmoja, bali hayo munayoyadai nyinyi ni kwa njia ya istimbat na istimbat yunu yote ni makosa kama tulivyobainisha.

11

MUANDAMO WA MWEZI

SEHEMU YA KUMI NA MOJA

MTAZAMO WA MASAHABA (RADHIYA ALLAAHU 'ANHU) JUU YA KADHIA YA KUFUNGA NA KUFUNGUA MTAZAMO WA MASAHABA

MNASEMA

Mtazamo Wa Masahaba (Radhiya Allaahu 'Anhu) Juu Ya Kadhia Ya Kufunga Na Kufungua Ndugu Juma amekuwa na mtazamo wake juu ya yale aliyoyasema Shaykh Naaswir Bachuu kwamba kwa muda wa miaka 30 ya Makhalifa waongofu hapakupatikana utatanishi wowote juu ya suala la muandamo wa mwezi. Haikuthibiti kwamba Masahaba waliwahi kuzingatia suala la masafa au matlai katika suala la kuandama kwa mwezi.

Ndugu Juma anasema: (Kama ilivyokuwa hakuna ushahidi kwamba wao waliwaamrisha watu wasifate miandamo yao, pia hakuna ushahidi kwamba wao waliwakataza wasifate miandamo yao, au kwamba waliwaamrisha kufata muandamo wa Madina.) Kwa upande wetu tunasema hivi: Ni kweli kuna uwezekano kwamba Masahaba hawakuwaamrisha watu wasifuate miandamo yao au waliwakataza watu kufuata miandamo yao.

Bila shaka jambo hilo linawezekana sana, kwani Masahaba hawana mamlaka ya kuwaamrisha au kuwakataza watu kwani wao hawakuwa wakipata Wahyi. Mwenye mamlaka hayo ni mwenyewe Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Isipokuwa Sahaba akisema: "Tumeamrishwa kadha" au "Tumekatazwa kadha." Jambo hilo hupewa hukumu ya "Rafii." Juu yao Masahaba ni kumsikiliza Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anavyowaamuru na kumuuliza pale panapotokea mushkeli wowote. Kwa mantiki hiyo tunapenda kusema kuwa hakuna Riwaya hata moja iliyo Sahihi inayoeleza kuwa labda Masahaba walimuuliza Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuwa tufunge vipi au wenzetu walioko mbali nao wafunge vipi na wafungue namna gani. Hii ina maana kwamba Masahaba walimuelewa vyema Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika maagizo yake hasa katika suala hili la kufunga walielewa vyema kuwa agizo hili ni la Waumini wote, mahala popote walipo.

JAWABU

Dai lenu kwamba: "Kwa mantiki hiyo tunapenda kusema kuwa hakuna Riwaya hata moja iliyo Sahihi inayoeleza kuwa labda Masahaba walimuuliza Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuwa tufunge vipi au wenzetu walioko mbali nao wafunge vipi na wafungue namna gani. Hii ina maana kwamba Masahaba walimuelewa vyema Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika maagizo yake hasa katika suala hili la kufunga walielewa vyema kuwa agizo hili ni la Waumini wote, mahala popote walipo". Hili si dai sahihi. Utaona kwamba tunakariri yayo kwa yao. Tunasema kwamba kutokuwepo kwa riwaya kwamba aliulizwa, hakumaanishi kuwa hakuulizwa, bali kuna maanisha kuwa hakuna riwaya hii wala hile. Kwa hivyo, huenda ikawa aliulizwa huenda ikawa hakuulizwa - hakuna ithbati. Lakini hali hii haina uwezo wa kuibomoa riwaya iliothibiti kwa sanad sahihi kwamba mafunzo yake ni kutokuuzingatia muandamo wa mbali. Nakukumbusheni tena kauli yenu muliposema: "Isipokuwa Sahaba akisema: "Tumeamrishwa kadha" au "Tumekatazwa kadha." Jambo hilo hupewa hukumu ya "Rafii" yaani hio inazingatiwa kuwa ni Hadithi ya Mtume(s.a.w.w) . Kwa hivyo, natija ni kuwa:

1) Hakuna riwaya kwamba Mtume(s.a.w.w) kaulizwa hivi wala vile. Kwa hivyo, hapa hakuna hoja.

2) Kuna Hadithi kwamba Mtume kafunza kutokuuchukua muandamo wa mbali.

MNASEMA

Riwaya itegemewayo juu ya suala hili linalo zingatiwa matlai ni masimulizi ya Kuraib tu. Tukio lililotokea zaidi ya miaka 30 baada ya kufa Bwana Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Pia Makhalifa wote wanne walikwisha ondoka Duniani. Masimulizi ambayo yana utata mkubwa na hayana ufafanuzi wa kina, hususan yanapopimwa katika mezani mbili - mizani ya Usulul Fiqhi na mezani ya Mustalahul- Hadiyth. Baada ya kupimwa vizuri uzito wake katika mezani zote mbili, inabainika kwamba hapana uzito unaostahili kuchukuliwa kama ni hoja sahihi za kutegemewa katika mdahalo huu wa muandamo wa mwezi.

JAWABU

Naona tunaendelea kukariri. Ni mezani gani au ni kanuni gani ya Usulul Fiqhi au ya Mustalahul- Hadiyth muliotumia kubatilisha riwaya ya Kuraib na Ibn Abbaas. Nakukumbusheni tena mulioyasema punde: "Isipokuwa Sahaba akisema: "Tumeamrishwa kadha" au "Tumekatazwa kadha." Jambo hilo hupewa hukumu ya "Rafii" yaani hio inazingatiwa kuwa ni Hadithi ya Mtume(s.a.w.w) . Riwaya ya Ibn Abbaas iko hivyo. Sasa ni elimu gani ya Hadithi mulioitumia? Na kanuni zote za kiusuli kama nilivyobainisha katika kitabu zinaifanya Hadithi ya Kuraib na Ibn Abbaas itangulizwe.

MNASEMA

Ama tukichukua maneno sahihi ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliyoyasema:"Fungeni kwa kuuona mwezi muandamo" katika mezani, tutaona kina cha uzito wa maneno haya ni kikubwa mno. Ndio maana tukasema kushikamana na man eno ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ni bora na ndiyo hasa Sheri'ah inavyotuagiza kuliko kushika maneno yenye utata na yenye khitilafu.

JAWABU

Nakukumbusheni tena maneno yenu: "Isipokuwa Sahaba akisema: "Tumeamrishwa kadha" au "Tumekatazwa kadha." Jambo hilo hupewa hukumu ya "Rafii" yaani hio inazingatiwa kuwa ni Hadithi ya Mtume(s.a.w.w) . Riwaya ya Ibn Abbaas iko hivyo, kwa hivyo nayo ni mafunzo ya Mtume(s.a.w.w) musiyatoe kwenye uzito.

MNASEMA

Kama tukijadili uwezekano wa utekelezaji wa agizo hilo la kufunga na kufungua katika zama ambazo mawasiliano yalikuwa duni na hafifu sana; tungejiuliza, Masahaba wangewezaje kupeana taarifa za kuandama kwa mwezi katika nchi za mbali? Wengewezaje kwa pamoja kuamka wakiwa wamefunga na hasa pakizingatiwa kuwa taarifa zenyewe zinatakiwa ziwafikie wengine kabla ya kupambazukiwa na alfajiri? Bila shaka jambo hilo lilikuwa ni gumu kiutekelazaji hata katika nchi moja pekee. Lakini ni vyema kuelewa kwamba hilo lilikuwa ni jambo la dharura kwa wakati huo.

JAWABU

1) Illa ya kufunga kwa miandamo tafauti ni kutafautina miadamo: si kupatikana kwa teknolojia mpya katika zama zetu na kukosekana kwake hapo zamani. Kama vile ambavyo illa ya kusali katika nyakati tafauti ni kuingia nyakati hizo tafauti kwa mtenguko na mzamo wa jua. Na sharia haibadiliki isipokuwa kitu kiwe kina illa (sababu) fulani iliojulikana katika andiko kwa njia ya tasrih (uwazi) au istimbat, kisha illa (sababu) hiyo iwe haipo tena. Hapo hukumu pia hubadilika. Kama walivyosema wanavyuoni sababu ikiondoka na hukumu huondoka. Sasa nyinyi wenzetu mumepata wapi kwamba kutofika habari ndio sababu ya kufunga kwa miandamo tafauti ili iwe sasa kwa kupatikana teknolojia mpya t ayari illa (sababu) hio imeondoka na sasa hukumu imebadilika?

2) Pili ni kuwa suala hilo nimelijibu kwamba Ibn Abbas alisema: "Hatuachi kufunga mpaka tukamilishe idadi ya siku thalathini au tuuone mwezi." Sasa kama aliukubali muandamo wa Sham, basi asingelisema maneno hayo, kwani kwa hali yoyote ile ikifika siku ya mwezi 29 ya muandamo wa Madina ni lazima watu wa Madina wale idi siku ya pili, ((halafu ikiwa itawathibitikia kwamba Sham mwezi uliandama tarehe thalathini wao watu wa Madina wailipe siku moja)) kwani siku hio ya mwezi 29 wa Madina ni lazima Sham itakuwa ni siku ya tarehe 30 au tarehe mosi. Ikiwa ni tarehe 30 itakuwa Sham wamefunga siku 30, wakati Madina wamefunga siku 29, na Ikiwa Sham ni tarehe mosi siku hio, basi watakuwa wamo ndani ya siku kuu - kwa hali zote mbili, kama Ibn Abbas aliukubali muandamo wa Sham, basi ni lazima watu wa Madina waishie kufunga tarehe 29. Lakini tunamkuta Ibn Abbas anasema "Hatuachi kufunga mpaka tutimize (siku) thalathini au tuuone mwezi." Kusema "Mpaka tutimize (siku) thalathini". Kama ni hivyo, basi utaona hapa kwamba habari ya muandamo wa mwezi ilikwishafika Madana. Suala je ilitendewa kazi? Kwa hivyo, kufika na kutokufika kwa habari si sababu ya kuwepo kwa miandamo tafauti hapo kale, bali sababu ni umbali na kutafautiana kwa matalai. Na lau ilikuwa sababu ni kutofika habari, basi habari ikifika ingetendewa kazi. Lakini hapa habari imefika wala haikutendewa kazi.

MNASEMA

Msisitizo wetu mkubwa ni kuwa katika masimulizi ya Kuraib hapakupatikana maafikiano ya Wanavyuoni kwa hivyo si jambo la kutegemewa. Kama wanavyosema Wanavyuoni wa 'Usulil-fiqhi.' "Dalili ikiwa na maana (nyingi) zaidi ya moja, huporomoka ushahidi wake."

Jawabu Ikiwa kutokuafikiana kwa wanavyuoni ni sababu ya kuachwa kwa andiko, basi itatubidi tuiache Qur-ani yote ila Aya chache kwani Aya zote taqriban wametafautina kuzifasiri. Bismillahi itabidi tuitoe kwenye misahafu kwani wako wanaosema kuwa si Aya kabisa kama vile watu wa Mailk. Bali kwa mantiki hio pia tuiwache Hadithi "Fungeni kwa kuuona musifunge mpaka muuone.." kwani wanavyuoni pia hawakukubaliana juu ya maana yake. Anasema Ibn Hajar (Na wale ambao hawakuchukua kauli hio, wanasema kwa sababu kauli yake Mtume(s.a.w.w) aliposema) "Mpaka muuone" ni agizo kwa watu maalumu." Anasema Al-san'ani: "Na ikasemwa kwamba (Muandamo wa mbali) hauzingatiwi (mbali), kwa sababu kauli yake (Mtume(s.a.w.w) aliposema:"Mukiuona" ni agizo kwa watu maalumu."

Ama kanuni isemayo: "Dalili ikiwa na maana (nyingi) zaidi y a moja, huporomoka ushahidi wake" haihusiani na hapa. Nyinyi hiki kitabu chenu baada ya kukiandika hamukuwapitishia watu wa fani wakakichungulia?! Kanuni hio haina maana kuwa wanachuoni wakitafautiana basi dalili huporomoka. Basi tusisali sala ya safari, maana wametafautina masafa ya safari: wengine kilomita 12; wengine masafa ya siku 3 nk. Na pia muda wa siku ngapi sala ya safari inakwisha: zote hizi ni tafauti, kwa hivyo Waislamu wasisali sala ya safari!!! Maana ya kanuni hio ni kuwa dalili yenyewe (Aya au Hadithi) ikiwa ina uwezekano huu na ule wala hakuna Qarina yenye kuipa uzito maana moja, basi huwa huwezi kutoa ushahidi kwayo ukasema kuwa maana hii ndio ilikusudiwa madamu huna ushahdi.

MNASEMA

Ikumbukwe kuwa Sunnah ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ni (aula) bora kwa hali yoyote iwayo. Kinachotakiwa ni kuifuata sio kuibeza. Shaykh Al-Qanubiy wa Kiibadhi anasema katika kitabu chake kuwa: "Itakapogongana amri ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na amri nyengine yoyote, basi amri ya agizo la Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ni (aula) bora zaidi kutangulizwa (mbele) na ku fuatwa." Shaykh Ahmed Al-Khaliil (Mufti Mkuu wa Omani) naye amesema: "Hakuna kuzingatiwa kauli itakayopingana na Hadiyth sahihi, kwani Sunnah ni hoja juu ya jambo la Kid ini, wala jambo jengine lolote haliwezi kuwa ni hoja dhidi ya Sunnah."

103) Anachokieleza Shaykh Ahmed Al-Khaliil ni kuwa: "Lazima marejeo y a asili (katika misingi ya Kidini) ni kila kilichoelezwa kwa (saraha) uwazi katika Qur-aan Tukufu na kilichoelezwa katika Sunnah Sahihi. "Walikuwa wanavyuoni wema wakionyesha kukereka kwao na hasira zao juu ya yule mtu ambaye anaipuuza (anaibeza) Hadiyth ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa (kuifuata) rai (ya mwanachuoni) au Qiyaas au mapende kezo ya Wanavyuoni au kauli ya mtu yeyote kwa kuipuuza Sunnah ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)" Katika maudhui yetu hayo ya muandamo wa mwezi, katika kadhia ya kufunga na kufungua kwa kuonekana mwezi, ni vyema kuachana na vitu vyenye utata na kusisitiza kushikamana na maneno katika Hadiyth Sahihi ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) isemayo:"Fungeni kwa kuonekana mwezi -muandamo"

Jawabu Munahimiza kufata Hadithi ya Mtume (s.a.w.) kama wanavyohimiza wanavyuoni hao. Hilo hatutafautiani. Lakini tunasema kwamba riwaya zote mbili "Fungeni kwa kuuona" na "Hvi ndivyo alivyotuamu Mtume s.a.w." ni Hadithi. Nakukumbusheni maneno yenu: "Isipokuwa Sahaba akisema: "Tumeamrishwa kadha" au "Tumekatazwa kadha." Jambo hilo hupewa hukumu ya "Rafii" yaani hio inazingatiwa kuwa ni Hadithi ya Mtume (s.a.w.). Kwa hivyo, kinachotakiwa ni kuzijumuisha Hadithi hizo na kuzitazama zina maana gani: sio kuitendea kazi moja na kuiwacha moja: kuitendea kazi moja na kuiwacha moja ni kinyume na Al-Minhaj Al-Sahih (methodology) sahihi.