MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA 40%

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA Mwandishi:
: AMIRALY M.H.DATOO
Kundi: Vitabu mbali mbali

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA
  • Anza
  • Iliyopita
  • 21 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 17268 / Pakua: 3438
Kiwango Kiwango Kiwango
MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA

Mwandishi:
Swahili

12

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA

SOMO LA 111: QURAN TUKUFU NI YA KILA ZAMA

Al-Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) amesema:

Allah swt hakuifanya Qur'an Tukufu kuwa kwa ajili ya zama fulani tu, wala si kwa ajili ya taifa fulani, hivyo daima huwa ni mpya na kwa ajili ya kila taifa ulimwenguni humu hadi siku ya Qiyama. 116

Maelezo mafupi: Al-Imam 'Ali ar-ridha a.s. alimjibu mtu mmoja ambaye alitaka kujua ni kwa nini Qur'an Tukufu haizeeki kwa kusomwa kila mara au kuchapwa ? Katika kusema huku kwa Al- Imam 'Ali ar-ridha a.s. amezungumzia kwa maana kamilifu kwa uhakika huu kuwa Qur'an Tukufu haikuumbwa na vitu vya dunia hii au haikutengenezwa na mwanadamu ambaye mwenyewe ataangamia na kuisha pamoja na mawazo yake yanayokaa yakibadilika. Hivyo vumbi hilo la kuzeeka haufuniki Qur'an Tukufu kwa kupita muda. Kwa hakika Qur'an Tukufu imetokea kutokana na sayansi na elimu ya Allah swt, ambaye kuwapo kwake kumekuwapo tangia mwanzoni na utakuwepo milele. Kila itakavyosomwa zaidi, ndivyo hivyo itakavyokuwa mpya na yenye kuvutia, na kwa hakika huu ndio mojawapo wa muujiza wa Qur'an Tukufu.

SOMO LA 112: JITAHADHARISHE NA MATAMANIO

Al-Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema:

Ole wako kwa matamanio ya nafsi yako kama vile unavyojihadhari na maadui zako kwa sababu hakuna adui wako mkubwa kuliko matamanio yako na yale yanayotokana na ndimi zao. 117

Maelezo mafupi: Bila shaka maadui wa ndani ni hatari zaidi kuliko maadui wa nje. Kwa hivyo, matamanio ambayo humwathiri mwanadamu kwa undani, kwani huchukuliwa ni adui hatari kabisa wa mwanadamu. Upofu wa matamanio humfanya mtu akawa kiziwi na kipofu wa macho. Huondoa nuru ya busara, hugeuza nyuso za ukweli na hatimaye humwongoza katika maovu.

SOMO LA 113: NJIA MOJA TU YA KUWA SHI'A

Al-Imam Muhammad al-Baqir(a.s) alimwambia to jaber jofi:

Wafikishie salaam zangu kwa Mashi'a wetu na uwaambie kuwa wao hawatakuwa na uhusiano pamoja nasi na Allah swt ambapo njia moja tu iliyopo ni ya kujisalimisha kwa amri za Allah swt. 118

Maelezo mafupi: Kwa hakika wapo watu wengi ambao wanadai kuwa wao ni Mashi'a na mapenzi yao pamoja na Ahlul Bayt a.s. ndiyo yanayotosheleza kwa ajili ya uokovu wao Siku ya Qiyamah. Ati kwa kudhania kwao hivyo, wao wataingizwa katika ndugu na jamaa za Ahlul Bayt a.s., na kwamba watakuwa na uhusiano maalumu pamja na Allah swt, na hivyo kila kitu chao kitakuwa sawasawa kwa kuomba kwao. Kwa hakika uhusiano wa mwanadamu na Allah swt ni ule tu unaotokana na utiifu na kutimiza wajibu wake mtu. Yeyote yule anayejisalimisha mbele ya amri za Allah swt ndiye mtu wa karibu kabisa, na kwa hakika yeyote yule asiyemtii Allah swt kwa hakika amejiweka mbali mno na Allah swt, yeyote yule awaye.

SOMO LA 114: UHUSIANO WA MALI NA MATUMIZI!

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Yeyote yule anayechuma mali kwa njia ya haraam, ataitumia kwa njia ambayo haina baraka za Allah swt. 119

Maelezo mafupi: Inaaminiwa kwa kawaida kuwa si kila mali au milki inayopaswa kutumiwa kwa ajili ya wema wa jamii au njia nzuri na zilizo bora. Kwa hakika Hadith ya hapo juu ni uthibitisho mzuri kwa imani hii ya kawaida. Ni ukweli ulioonekana kwamba baadhi ya watu wamenuia kushiriki katika jambo jema kwa kutumia mali na milki yao, lakini ama wamesitisha wakiwa wamefikia katikati, au iwapo watakuwa wamekamilisha basi juhudi zao hizo hazitakuwa na ufanisi wa kutosha au itaonekana yenye matokeo yaliyogeuka. Kwa hakika wapo watu wengi mno ambao watoa huduma kubwa mno kwa moyo msafi na kwa mitaji yao midogo.

SOMO LA 115: MKWELI KABISA NA MWENYE BUSARA

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

Kila Ummah unao mtu aliye mkweli na mbainifu, na hivyo mkweli na mbainifu wa Ummah wangu ni Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib (a.s) 120

Maelezo mafupi: Kwa ajili yakutaka kukamilisha Dini halisi, Dini ya kudumu milele kama Islam, basi kunatakiwa kuwepo na mtu ambaye ni mzoefu na mwenye kujua masuala yote na undani wa Dini hiyo ili aweze kubainisha tofauti iliyopo baina ya ukweli na uwongo ( mstahikiwa jina la mbainishaji) baada ya kifo cha Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w., sehemu kubwa ya Misheni yake ilipita katika magomvi mbalimbali pamoja na maadui wake. Inabidi yeye awe mkweli, mwaminifu, msemaji bora na msema ukweli ili aweze kuondoa kero zozote zinazowakera watu baada ya kiongozi wa kwanza. Kwa hakika wadhifa huu, kama ilivyo bayana hapo juu, ulikuwa umepewa Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) tu.

SOMO LA 116: MAISHA NA KUENDESHA NYUMBA

Al-Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema:

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. alikuwa akikusanya na kuzichana kuni (kwa ajili ya nyumbani kwake) kutokea jangwani na kuchota maji na kufanya usafi kwa kufagia, na Bi. Fatimah az-Zahra a.s. alitayarisha unga na alikanda unga na kupika mikate. 121

Maelezo mafupi: Ukuu na utukufu wa ulimwengu mzima wa moyo na daraja kuu umefichika katika Hadith hii fupi kwa kuhusiana na Kiongozi Adhimu wa Islam, Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) na mfano mkubwa wa wanawake, Bi.Fatimah az-Zahra(a.s) kwani maisha yao kwa hakika yalikuwa ya kawaida na yenye kujaa uaminifu, uhalisi, kusaidiana na kushirikiana. Kufanya kazi haikuwa kudhalilika, na ushirikiano na kuelewana yalikuwa yakichukuliwa kuwa ni kipaumbele ya kimsingi, na kisichopendeza kulichukuliwa kama ndicho kipa umbele. Kwa hakika masuala haya hayapatikani tena majumbani mwetu na matokeo yake ni kwamba udugu na amani na mapenzi ndiyo maana yametoweka.

SOMO LA 117: SAA NZIMA YA UADILIFU

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

Saa moja ya uadilifu ni bora kuliko ibada ya mwaka mzima. 122

Maelezo mafupi: 'Ibada ni uhusianao sawa wa viumbe pamoja na Muumba wao na 'uwezekano' pamoja na lazima na kuzingatia kwa uhusiano na muungano huu. Kwa hakika 'Ibada hizo ndizo zilizo mafunzo muhimu ambazo kwa hakika yanaathiri mno katika kurekebisha nafsi na akili ya mtu. Hata hivyo, sisi tunasoma katika Hadith hiyo hapo juu kuwa saa moja ya uadilifu ni bora na afadhali kuliko 'Ibada ya Sunnah ya mwaka mzima.

Na mahala pengine tunasoma kuwa saa moja ipitishwayo katika kufikiria na kutafakari, basi ni bora kuliko usiku mmoja ( au mwaka mmoja) upitishwao katika 'Ibada. Kwa hakika maneno haya yanaonyesha muhimu wa uadilifu ulivyo na fikara, kwani yote yana asili sawa. Popote pale ambapo hapatakuwa na uadilifu, basi hakutakuwa na ufikiriaji sahihi na busara.

SOMO LA 118: MGANGA WA KWELI

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

Kwa hakika mgamnga halisi ni Allah swt, na vitu ambavyo vikufaavyo vinaweza kuwa vyenye kumdhuru mtu mwingine. 123

Maelezo mafupi: Matukio yanayotokea katika maisha ya mwanadamu kwa mara nyingi hutokana na sera zake mbaya, uchaguaji au moyo wake na kwa hakika yapo matukio mengi mno kama haya yanayoumiza. Lakini mara nyingine matukio yasiyo mazuri hutokea si kwa kutokana na sababu hizo za juu, lakini kwa hakika hutokana na amri za Allah swt kama ndizo dawa kwa ajili ya waja wake. Dawa hizo mara nyingi huwa ni chungu, lakini huwa ni kama kengele ya kumwamsha na kumzindua mwanadamu, au kumtanabahisha juu ya udhaifu wake na au kuondoa kiburi na upotofu wake.

SOMO LA 119: MAKHALIFA WA MTUME S.A.W.W.

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

Dini hii ya Allah swt daima itaheshimiwa na kuhifadhiwa kutokea maadui hadi hapo Makhalifa kumi na wawili (12) watakapoiongoza, na wote watatokana na Maqureish. 124

Maelezo mafupi: Hadith na Riwaya zilizo wazi na kujieleza zenyewe zimetolewa katika kuzungumzia Makhalifa 12 halisi wa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) katika vitabu vinavyoheshimiwa na kuaminiwa katika Ahl as-Sunnah kama vile Sahih Bukhari, Sahih Muslim, Sahih Tirmidhi, Sahih Abu Dawud, Masud Ahmad na vitabu vingi vinginevyo, na jumla ya Hadith hizi zilizotolewa na Mashi'a na Masunni zinafikia idadi ya Ahadith 271! Ni jambo la kuvutia kuwa Ahadith hizo hazikubaliani na hata mmojawapo wa Waislamu waliongoza au kutawala baada ya Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) isipokuwa Maimamu 12 wa Mashi'a tu kwani makhalifa 4 wa kwanza, au wa-Bani Umayyah or Bani 'Abbas si wanaozungumziwa katika Hadith hii.

Kwa hivyo Masunni wameingia katika hali ngumu ya kutafsiri Hadith hii iliyo sahihi lakini kwa hakika tafsiri ya Hadith hii ipo wazi kabisa katika Ushi'a wa Ahlul bayt a.s. ya wananyumba wa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w)

SOMO LA 120: FURAHA YENEY MADHAMBI

Al-Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema:

Si haki kwa Waumini kushiriki katika hafla na sherehe ambamo kunatendwa maasi ambayo wao hawawezi kuzibadilisha. 125

Maelezo mafupi: Kushiriki katika karamu au sherehe zenye madhambi ni dhambi lenyewe, ingawaje mtu mwenyewe hatendi dhambi wala kushirikiana na washiriki katika karamu au sherehe hiyo. Kwa sababu kushiriki katika karamu au sherehe kama hizo kunachukuliwa ni kusaini dhambi, isipokuwa tu iwapo hatima ya mtu itakuwa ni kubadilisha hali hiyo na kutekeleza jukumu gumu kabisa la kuhubiri uwema na kukataza ubaya na maovu. Zaidi ya hayo, kujishughulisha na hali za madhambi, wakati kuwa tofauti na wao, kunaitia kiza nafsi ya mtu na kupunguza hali ya kujiepusha na madhambi na kumfanya mtu kuzoea madhambi.

13

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA

SOMO LA 121: UFANYE KAZI ZINAZOZALISHA

Al-Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema:

Lima na panda mti. Kwa kiapo cha Allah swt , watu hawajafanya tendo lolote lililo halisi zaidi ya hili. 126

Maelezo mafupi: Maisha ya mwanadamu yapo juu ya kazi zinazo zalisha, ikiwemo kilimo, na biashara mbalimbali, na hata wingi wa viwanda havitakuwa na maana bila ya kilimo kwani kwayo hujipatia mali ghafi. Kwa kuongezea, uovu na uzushi hauwezekani katika kilimo kama vile ilivyo kawaida katika mambo mengine. Kwani misingi yake ipo ni kawaida na kwa hakika faida yake ni kwa kutokana na jitihada za mtu. Kwa misingi hii, kilimo na upandaji wa miti kumeitwa kuwa ni kazi njema na halisi katika Hadith ya hapo juu.

SOMO LA 122: UREFU NA UFUPI WA MAISHA

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Kifo kinamwijia mtu mapema kuliko kawaida kwa kutokana na madhambi, na urefu wa maisha unatokana na uchamungu wake zaidi ya maisha ya kawaida. 127

Maelezo mafupi: Hakuna shaka kuwa wingi wa madhambi na tabia mbaya zinafupisha maisha moja kwa moja ( kama vile kulewa, kamari, husuda, wivu na shari na kutaka kulipiza kisasi) na nyingi zinafupisha maisha vinginevyo kwa kuathiri mivurugano ya kijamii na kuondoa amani na usalama wa kijamii na kuzuka kwa vita na mapigano ( kama vile riba, dhuluma na ukandamizaji).

Kwa upande wa pili, uchamungu ndio unaweza kuwa ndiyo sababu ya kurefuka kwa umri mrefu kwa kutokana na athari za utulivu wa nafsi na nyoyo na dhamira. Hivyo, madhambi, kutokujali athari zake mbaya, ni kichocheo kikubwa katika kufupisha maisha ya mwanadamu, ambapo kwa hakika uchamungu ni sababu kubwa katika kurefusha maisha pamoja mema yake yote.

SOMO LA 123: URAFIKI NA SHETANI!

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Usimlaani Shetani kidhahiri, wakati wewe ni rafiki yake kwa undani mwako. 128

Maelezo mafupi: Baadhi ya watu wanijiepusha na kuogopa kutokea maneno, maneno ya umasikini, unafiki, sheitani na kama hayo, wakati ambapo kimatendo wao wanakuwa wametumbukia ndani mwao. Sisi tunawajua baadhi ya matajiri ambao huishi maisha ya kimasikini kwa kuhofia umasikini. Sisi vile vile tunawajua wanafiki ambao kwa kurudia huwalaani wanafiki, lakini kwa hakika maisha yao yanakuwa yamejaa kwa unafiki.

Sisi vie vile tunawajua watu waovu ambao kwa udhahiri kabisa wanajiingiza katika kujinusuru kwa Allah swt dhidi ya Shetani, kwa maneno yao ya ulimini, lakini wao ni marafiki wa Shetani kwa undani mwao na hutilia mkazo na usisitizo juu ya mipango ya kishetani. Kwa hakika wao ni maadui kwa maneno na wala si kwa wa kweli kwa hisia au ukweli.

SOMO LA 124: POKEA USHAURI ILI UONGOZWE !

Al-Imam Hasan ibn 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Hakuna mataifa yanayoshauriana miongoni mwao hadi pale wanapokuwa wameongozwa kwa mema na faida zao. 129

Maelezo mafupi: Kwa umoja daima imeilipa jamii neema, maendeleo na uboreshaji wao, hususan katika masuala ya kiakili na mipango ya maendeleo na utatuaji wa matatizo yao, kwa hakika kutekelezeka ushauriano na majadiliano kwa kimaajabu. Wale ambao wamezoea kujitolea mawazo yao wenyewe na kujitenga, mara nyingi kudhurika kwa makosa na hasara. Akili yoyote inayo mchocheo ambao haupo katika akili nyingineyo. Wakati vichocheo hivi vinapokutana na nyenzao, basi kutatokea mwanga ambao utang'arisha kiza wowote utakao kuwapo. Inatubidi sisi sote tuamue kuwa tutashauriana pamoja na watu walioelimika na wale walio makini.

SOMO LA 125: SALAAM, KUSALIMIANA KIISLAMU

Al-Imam Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Salaam (kusalimiana) zina thawabu 70, sehemu 69 za Salamu hiyo ni kwa ajili ya yule anayetoa Salaam na sehemu moja ni kwa ajili ya yule anayejibu Salaam hiyo. 130

Maelezo mafupi: Miongoni mwa kusalimiana katika mataifa ya ulimwenguni, Salaam, usalimio wa Kiislamu na kuamkiana, kwa hakika unao nuru ya ajabu, kwa sababu hiyo inamaanisha ukaribisho na amani, furaha na urafiki, na vile vile Dua ya amani na usalama na kheri kutokea Allah swt kwa mtu anayesalimiwa. Kwa sababu hizi, maamkizi ya wakazi wa Jannat ni Salaam, na Malaika wa Rahma huwapokea wachamungu na watendao mema kwa Salaam. Lakini kwa bahati mbaya, baadhi ya Waislamu wanaikataa amri hii ya Dini ya Islam kwa kujifakharisha kuwa kwa kutokusalimiana ndiko kunakoonyesha heshima zao na kwa kusalimiana hivyo kunawadhalilisha wao na kwa hakika wao ndio wenye hasara ya kukosa baraka, amani na Dua iliyopo katika Salaam kwa mujibu wa hadith hiyo ya hapo juu !

SOMO LA 126: KUTOKUKUBALIANA KWA IMANI NA MATENDO

Al-Imam Zainul 'Abidiin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Wale watu wanaochukiwa na Allah swt ni wale ambao wameukubalia uongozi wa Imamu, lakini hawafuati matendo yake. 131

Maelezo mafupi: Mojawapo ya makosa makuu ya mwanadamu ni kutokukubaliana kwa imani yake pamoja na matendo yake. Yeye huamini kitu kingine, lakini hakuna ufuatio wa imani yake hiyo unaopatikana katika matendo yake. Yeye huamini katika Allah swt, lakini hukana katika matendo yake. Yeye huamini katika Mahakama Kuu ya Allah swt, lakini haonyeshi kujitayarisha kwayo. Yeye huamini kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ni Mtume Mkuu na kwamba Al- Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) kuwa ni kiongozi Mkuu, lakini utaona hawana sifa yoyote katika matendo yake yoyote. Hivyo tunasema kuwa matendo yake yapo upande mmoja na matendo yake yapo upande wa pili

SOMO LA 127: ADHABU ZA ALLAH SWT !

Al-Imam Muhammad al-Baqir(a.s) amesema:

Allah swt ameweka adhabu (kwa ajili ya madhambi na uasi) katika nyoyo na miili: 132 " Umasikini katika kipato " Uvivu katika 'Ibada Lakini Allah swt hajamwadhibu mja wake yeyote yule aliye na kitu kiovu kuliko moyo mgumu."

Maelezo mafupi: Adhabu za Allah swt kwa hakika ni matokeo ya matendo na matokeo ya madhambi ya mwanadamu mwenyewe. Kwa hakika baadhi ya nyakati hatima hizi mbaya huonekana kama nyakati mbaya katika maisha ya kidunia na nyakati zinginezo kama kunyimwa uhalisi katika 'Ibada na Dua pamoja na Muumba wetu. Lakini jambo lililo la muhimu na hatari kabisa ni kule kwa mwanadamu kudhihirisha maasi na makosa na matendo maovu kabisa kwa nyonyo ngumu na ukatili wa mwanadamu, kuondokana kutokea moyo wa mwandamu kwa hisia za kibinadamu na ukarimu, mapenzi na huruma, na kwa hakika moyo wa mwanadamu unaweza kuwa ndio chanzo kikuu cha madhambi na maasi mengi mno.

SOMO LA 128: UHAKIKA ULIO SAHAULIKA

Al-Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema:

Allah swt ameumba yakini bila shaka kama mauti, lakini inaonekana kuwa shaka ndimo kamwe hakuna yakini. 133

Maelezo mafupi: Kwa hakika msemo huo ni wa kustaajabisha, na tafsiri bayana ya kutokujua kwa mwanadamu kuhusu hatima ya maisha na mauti. Mtu anaweza kusita katika kitu chochote kile na asiamini katika dini yoyote, lakini hasiti kwa kukiri kuwa maisha yatafikia mwisho wake tu na kuisha. Lakini yeye anaonekana hajui katika suala hili kama kwamba hakutakuwa na kifo ambacho ndicho kitakacho malizia maisha yake ! Hivyo, yeye hajitayarishi kwa kuikaribisha mauti na mwisho wake kwa imani, matendo mema, uhalisi na uchamungu. Hata hivyo, inatubidi sisi kwa lazima tuwe watu wenye uhakika na uhalisi katika kila hali na umri ili tusije tukajuta na kuaibika wakati wowote pale maisha yetu yatakapo malizika.

SOMO LA 129: NAFASI YA ELIMU NA BUSARA

Al-Imam Musa al-Kadhim(a.s) amesema:

Uoteshaji unakuwa katika ardhi laini, na wala si juu ya majiwe ! Na vile vile elimu na busra vinachomoza katika nyoyo za wachamungu, na kamwe si katika nyoyo za wadhalimu. 134

Maelezo mafupi: Hatua ya kwanza katika kutafuta elimu ni unyenyekevu, unyenyekevu kuelekea ukweli, unyenyekevu kuelekea mwalimu, na mtu yeyote anayejua zaidi kuliko sisi, na ambaye anaweza kutufundisha chochote. Kwa sababu hizi, ujahili na kiburi na ufidhuli yanakuwa yameambatana pamoja. Mfedhuli na mjauri kamwe hawezi kukubali kukiri kwa ujinga, na hata kama iwapo ukweli hautakuwa kwa mujibu wa nafsi yake ya kiburi na ufedhuli, si kwamba ati kuwa wao hukanusha hayo, bali hupinga pia. Wao hawakubali ukweli kutokea wale walio chini yao na mara nyingi hubakia kuwa wapumbavu kwa ukamilifu.

SOMO LA 130: MAJUKUMU MAZITO YA IMAM

Al-Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) amesema:

Imam ni Mwakilishi wa Allah swt juu ya ardhi hii na miongoni mwa waja wa Allah swt, na ni ushahidi kwa waja wake na mwenye kuwalingania watu kwake na mwenye mlinzi wa mipaka ya Allah swt dhidi ya yale yaliyoharamishwa. 135

Maelezo mafupi: Katika Hadith hii, ambayo ni sehemu ya Hadith ndefu katika kuzungumzia nafasi ya Uimamu, inazungumzia sehemu tano zilizo nzito za majukumu ya Imam(a.s)

1- Imam(a.s) ni mweka hazina na wakala wa Ufunuo na mhifadhi wa sayanzi zote, maamrisho na elimu za Dini.

2- Imam(a.s) ni sababu iliyohai na udhihirisho na mtambulishaji na mwendelezaji wa Dini ya Islam

3- Imam(a.s) ni mwakilishi mtakatifu wa Allah swt na mamlaka yake miongoni mwa watu

4- Imam(a.s) , hualika katika mema na kuzuia mabaya na ni Mjumbe mkuu wa Dini

5- Imam(a.s) ni mhifadhi wa mipaka ya Dini ya Islam dhidi ya uvamizi wa maadui wake. Na mtu kma huyo ndiye awenayo elimu ya Allah swt na daraja la utoharifu na hakuna mtu yeyote mwingine anayeweza kuwachagua hao Maimamu(a.s) isipokuwa ni Allah swt tu.

14

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA

SOMO LA 131: MILANGO ILIYOFUNGWA ITAFUNGULIWA

Al-Imam Muhammad at-Taqi(a.s) amesema:

Iwapo milango ya Jannat na ardhini zimefungwa kwa ajili ya mtu, na achaguapo uchamungu, Allah swt atamtoa humo. 136

Maelezo mafupi: Baadhi ya nyakati katika maisha, milango yote huwa inafungwa kwa ajili ya mwanadamu na popote pale anapogeukia, hukumbana na matatizo na magumu. Kwa hakika matukio kama hayo ni majukumu kwa ajili ya kumwamsha mwanadamu na kumfanya arejee kwa Allah swt, urejeo ulio sahihi na kubadilisha maisha na bahati yake. Wakati huu, iwapo yeye atajipatia usisitizo unaostahili kwa moyo wake wote, na kuomba msaada kutokea Allah swt, basi hakuna shaka kuwa msaada huo ataupata kutokea kwa Allah swt na upepo murua za baraka na rehema za Allah swt zitamkumba yeye na kwa hakika utakua ni muujiza mkubwa kwani milango yote iliyokuwa imefungwa itafunguka !

SOMO LA 132: JITAHADHARISHE NA WAOVU!

Al-Imam Muhammad at-Taqi (a.s) amesema:

Jitahadharishe na ugonjwa wa mtu yule ambaye hajistahi mwenyewe! 137

Maelezo mafupi: Kwa hakika, mojawapo ya hoja muhimu katika kuzuia ufisadi na uovu ni heshima au kuwa na hisia za heshima. Watu walioheshimika au wale wanaochukua heshima kwa ajili yao wenyewe, ingawaje wao inawezekana wasihesabike miongoni mwa walioheshimika katika mtazamo wa kijamii, wanajiepusha na mengi ya maovu na matendo mabaya kwa ajili ya kujitunzia nafasi yao. Lakini pale wao wanapohisi kuwa hawana heshima yoyote, jina au , basi wao hawatajali chochote. Hivyo Imam a.s. ametuonya tujitahadharishe na watu kama hao ! Na kwa misingi hiyo, mojawapo ya jambo lililo muhimu ni kuwaelimisha watoto au watu kwa ujumla ni kutengeneza heshima ndani mwao ili wao wawe na hisia ya kuwa na heshima maalum. Ama kwa upande mwingine, kinyume na hayo, kuwapunguzia watu heshima kwa hakika inayo athari mbaya kwa mtazamo wa kielimu na kuelimishana.

SOMO LA 133: VITA VIKUU

Al-Imam Hasan al-Askari(a.s) amesema:

Mtu aliye shupavu kabisa ni yule ambaye anaacha madhambi. 138

Maelezo mafupi: Sisi tunajua kuwa harakati dhidi ya matamanio ya maasi na za nafsi ndizo chanzo kikuu cha madhambi na inaitwa 'vita vikuu' katika Dini ya Islam, ikiwa kwa hakika harakati na vita vikali na vigumu hata kuzidi vita dhidi ya maadui. Kwa sababu vita hivi ni kwa ajili ya kujitakasisha kwa nafsi na hakutakuwa na ushindi wowote kwani kushindwa hutokea mara nyingi kwa sababu ya mipango na mikakati dhaifu. Katika jamii ambazo zilizojaa kwa madhambi, thamani ya vita hivi vinakuwa lazima na umuhimu wake katika kuboresha malengo na matakwa yake ya kijamii huwa yako wazi. Ushindi wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika mji mtukufu wa Madinah kwa hakika ulikuwa ndio uhitimisho wa utakasishaji wa nafsi na nyoyo, na harakati tukufu za Masahaba wake katika mji mtukufu wa Makkah.

SOMO LA 134: GHAIBU IMAM MUHAMMAD MAHDI A.S.

Al-Imam Muhammad Mahdi Sahib az-Zamaan(a.s)

amesema:

Katika matukio mengi yatakakayotokea katika kipindi hiki cha kuwa- ghaibu, rejea kwa wanaohadithia Hadith na Riwaya zetu. 139

Maelezo mafupi: Jamii za kibinadamu hazina mpangilio bila ya kuwa na kiongozi sawasawa. Na kwa sababu hizi, Allah swt kamwe hakuwaachia waja wake bila ya kiongozi na daima kumekuwapo viongozi wa Allah swt miongoni mwao. Hata katika kipindi cha kuwepo Ghaibu kwa Al-Imam Muhammad Mahdi Sahib az-Zamaan(a.s) kumekuwapo na wawakilishi wake mahsusi, na baada ya kusita kwa kipindi chao, aliwachagua wawakilishi wake wa kawaida kwa ajili ya kuwaongoza watu. Watu waliojitolea, waaminifu na watu walio makini ambao kwa hakika wanakuwa wameelimika vya kutosha kuhusu Kitabu Kitakatifu cha Waislamu, yaani Qur'an Tukufu, na vile vile Sunnah za Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) na Ahlul Bayt(a.s) tu ndio wanaopewa jukumu hili na yeyote yule mwingine ambaye anajidhania kuwa anaweza kulibeba jukumu hili, kwa hakika hukataliwa!

SOMO LA 135: CHANZO CHA MAOVU

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

Jiepushe na pombe kwani hiyo ndiyo ufunguo (chanzo) cha maovu yote. 140

Maelezo mafupi: Ingawaje kunaandikwa vitabu na makala mbalimbali kuhusu athari na matokeo mabaya ya pombe na vileo, juu ya mishipa yetu ya fahamu, na mpangilio mzima wa kuivisha chakula tumboni na moyo, mishipa ya damu, maini na mafigo na kwa kifupi, sehemu zote za mwili zinatajwa na kwa hakika athari zake mbaya zinazozikumba jamii zimefanyiwa utafiti wa hali ya juu na wanasayansi na matokeo yao yanatisha, lakini sentenso hiyo fupi ya Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) haiwezi kupatikana popote kwani imeelezea uhakika wote katika sentenso (Hadith) moja tu. Naam, pombe kama maovu yote mengineyo, ni chanzo cha magomvi na balaa na shida za kila aina.

SOMO LA 136: KUTIMIZA WAJIBU NDIYO IBADA KUU

Yeyote yule atimizaye wajibu wake, basi atakuwa miongoni mwa wachamungu. 141

Maelezo mafupi: 'Ibada haijawekwa tu kwa ajili ya kuwahudumia watu, wala kusali na kufunga. Ambapo kwa hakika 'ibada kuu ni kule ambapo kila mmoja atatimiza wajibu wake sehemu yake. Je ni 'ibada ipi iliyo juu na bayana kuliko hiyo? Kwa hakika ni 'ibada ambayo inaweza kubadilisha jamii katika bustani ya maua na ambapo kunawza kupatikana mema na maendeleo. Kutimiza wajibu kuna imani kubwa ikiwemo wajibu wa kuabudu, zaidi ya wajibu wa kibinadamu na kijamii na hata huduma za kiuchumi, na hapo ndipo ubainisho sahihi wa wale walioacha wajibu zao zilizo za lazima na kujivunia na kuchunguza and kujidhania wao kuwa ni wafuasi wa Dini ya Islam, imebainishwa wazi.

SOMO LA 137: MAKAZI KATIKA SAYARI

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Nyota hizi angani ni kama miji ilivyo juu ya ardhi, kila mji unakuwa umeunganishwa (na miji mingine) kwa kupitia mihimili ya mwanga. 142

Maelezo mafupi: NI jambo la ubinafsi kwa kuchukulia dunia yetu hii kuwa ni mahala pa kuishi tu na ambapo mamilioni ya sayari hazitumiki, zikiwa ati ni kimya bila ya viumbe vyenye uhai vinavyoishi humo. Leo wanasayansi wamepiga mahisabu yao kuhusiana na kuwapo maisha katika sayari zinginezo na wanao uhakika kuwa mamilioni ya sayari hizi zinazo viumbe vyenye uhai vinavyoishi humo, na kuna uwezekano mkubwa kuwa nyingi za sayari hizo zinamaendeleo makubwa hata kuliko sisi wakaazi wa sayari hii ya dunia kwa sababu maisha ya huko yameanza miaka maelfu ya mamilioni kabla dunia yetu hii. Hadith hiyo ya juu ni mojawapo ya muujiza wa kisayansi wa Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. ambayo yeye ameizungumzia karne 14 zilizopita.

SOMO LA 138: QUR'AN TUKUFU NA KANUNI YA UZITO

Al-Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) amemwambia mmoja wa marafiki zake:

Je Allah swt hasemi kuwa ameumba Jannat juu ya nguzo isiyoonekana ? Mimi nilimjibu : "Naam!" Naye (a.s) alinijibu : "Kwa hakika kuna nguzo ambayo nyinyi hamuioni." 143

Maelezo mafupi: Siku hizi, imethibitishwa kuwa sayari zimewekwa kwatika mizunguko yao, kwa hakika shukrani kwa uwiano sahihi wa uzito wa mvutano na nguvu zinazorudisha. Kwa hakika uvutio huo huvutiana kwa mfano wa mnyororo mkubwa, na nguvu za kurejesha huondoka kutokea nyenzake na uwiano wao upo sawasawa ambao umesababisha kubakia katika mzunguko wao bila ya kutokea badiliko au kulemea upande wowote, na kubakia imara katika nafasini mwao juu ya nguzo zao zisizoonekana. Je kuna maelezo yaliyo na nguvu kama ya hapo juu katika kuelezea ukweli huu katika zama hizo ambapo maajabu haya yalikuwa bado hayajavumbuliwa ? Je huu si muujiza mojawapo wa Viongozi wetu Wakuu?

SOMO LA 139: MAAJABU YA MILIMA!

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Mitikisiko na mienendo ya ardhi inadhibitiwa na milima. 144

Maelezo mafupi: Siku hizi, imethibitishwa kuwa mvuto wa Mwezi unaathari katika mwenendo wa maji ya mabahari na maji kujaa na kupwa kwa mara mbili kwa siku, kwa utofautisho wa mita 1 na hata zaidi ya mita 15 katika baadhi ya sehemu, vile vile inayo athari zake juu ya uso wa dunia (ardhi) na huiinua kwa zaidi ya sentimeta 30 na tena kuirudisha chini. Lakini kwa kutokana na ugumu halisi wa uso wa dunia kwa kutokana na kuwepo kwa milima, mizizi ambayo imeshikamana na nyenzake na kufanya mtandao kuuzunguka dunia ndio unaouponyesha athari zake zaidi. Kwa hakika, iwapo kusingalikuwapo na milima na gamba gumu la dunia lisingekuwa gumu kabisa, na kama kungalikuwapo na daima mwongezeko wa maji na kupwa, je kungalikuwapo na amani na usalama wetu ? Kwa hakika viongozi wetu wa Kiislamu wameyaelezea ukweli na uhakika huu karne 14 zilizopita.

SOMO LA 140: WANYAMA WADOGO KABISA

Al-Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) amesema:

Sisi tunamwita Allah swt kuwa ni Mwerevu na Mwenye ustadi mwingi kwa sababu ameumba viumbe vidogo mno ambavyo sisi hatuwezi kuviona kwa sababu ya udogo wao, na wala mikono yetu haziwahisi hao. 145

Maelezo mafupi: Kile ukionacho hapo juu ni sehemu tu ya Hadith ndefu ambayo Fat'h Ibn yazid Gurgani ameihadithia kutokea Al-Imam 'Ali ar-ridha(a.s) , ambamo imeelezwa kuwa, 'wanyama hawa ni wadogo mno kiasi kwamba hawawezi kuhisiwa, na wapo wametawanyika katika mawimbi ya baharini na magamba ya miti, na majangwani na ardhi tambarare'. Hadith hii ambayo imeandikwa kiasi cha miaka elfu moja iliyopita imebakia kama ndiyo ukumbusho wa Al-Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) na imetaja masuala haya miaka elfu zilizopita hata kabla ya kuvumbuliwa vifaa vya kuchunguzia na kukuzia viumbe vidogo kiasi hicho, na kwa hakika huu ni muujiza wa kisayansi.

15

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA

SOMO LA 14 1: LITABAKIA JINA TU KUTOKEA ISLAM

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Itawafikia watu zama ambapo herufi na maandishi kutokea Qur'an Tukufu na jina kutokea Islam yatakuwa yamebakia miongoni mwao. Misikiti ya Waislamu itakuwa ikiimarishwa kimajengo lakini yatakuwa yameteketea kwa mtazamo wa mwongozo na hidaya. 146

Maelezo mafupi: Sisi hatuwezi kusema kuhusu ubashiri huu wa kiajabu iwapo umekwisha dhihirika siku hizi au itahusika maishani mbele, lakini kwa hakika sisi tunashuhudia baadhi ya mifano yake hapa na pale na inashangaza kuwa Waislamu wanalalamikia kurudi nyuma kama kwamba kwao jina la Islam na mapicha ya Qur'an Tukufu tu vinatosha. Wao kamwe hawakuitumia Qur'an Tukufu kama ni Kitabu kifundishacho kwa ajili ya kumwelimisha mwanadamu na wala hawakuichukulia Islam kama ni shule yenye mpango wa kufundishia kiakili na kimatendo. Je wewe umeshashuhudia jamii halisi ya Kiislamu ambayo imerudi au kubakia nyuma au jamii ambayo haikutukuzwa au kuheshimiwa ulimwenguni ?

SOMO LA 14 2: KUTAMBUA UWEREVU NA UJAHILI

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Ulimi ni utambulisho wa kukadiria kiasi cha ujahili na kupima uwerevu na busara. 147

Maelezo mafupi: Kwa hakika ulimi ni dirisha muhimu la nafsi na utu wake na kupima upeo wa fahamu za kila mtu. Ulimi ambao hufunua pazia kwa kupitia mizunguko yake ya kawaida na hivyo hudhihirisha vile ilipo na ilivyo nafsi ya mtu. Kwa misingi hii, mafunzo mengi mno ya Dini ya Islam yanazungumzia na kusisitiza usahihishwaji wa ulimi na maonyo na tahadhari zinakaa zikitolewa na hata viongozi wetu na ingawaje kusahihishwa kwa kikamilifu kwa ulimi hauwezekani bila ya kuirekebisha nafsi na akili na fahamu, lakini sisi tunaweza kudhibiti matokeo yanayoumiza kwa kutokwenda kwa ulimi katika mkondo sahihi kwa kukaa kimya au kujidhibiti na hiyo ndiyo njia ya kujiepusha na maovu yatokanayo na ulimi.

SOMO LA 14 3: ZAIDI YA NEEMA

imam hadi(a.s.) amesema:

"Yeyote yule anayeshukuru msaada, kuneemeka kwake kwa kushukuru kwake ni zaidi ya neema kwa ajili ya msaada, kwa sababu misaada ni mambo ya maisha ya humu duniani na shukurani ni mtaji wa humu duniani na Aakhera." 148

Maelezo mafupi: Tukichukulia ukweli huu kuwa shukrani si shukrani kwa mdomo tu, bali ni shukrani kwa uhakika na vile vile kwa kutumia msaada mahala panapostahiki, basi hapo ndipo inasemwa kuwa shukrani kwa msaada ina matokeo katika neema na mali yake kiasi kwamba msaada wenyewe si jambo kubwa kwa kulinganishwa nayo. Kwa kutumia misaada kwa uridhisho wa Allah swt na mahitaji ya waja Wake kwa hakika ni rasilimali na mtaji mkubwa kwa kuheshimika humu duniani na vile vile kwa neema kubwa huko Aakhera, wakati ambapo msaada unaweza kuwa ni neema cha kitu tu. Hivyo, shukurani ina thamani zaidi na zaidi ya msaada wenyewe.

SOMO LA 14 4: KUHUISHA SIRA ZA MA'ASUMIIN A.S.

Al-Imam 'Ali ar-Ridha (a.s) amesema:

Yeyote yule akaaye katika kikao au mkusanyiko ambapo huisha sira zetu, basi moyo wake hautakufa pale patakapo kufa nyoyo zingine. 149

Maelezo mafupi: Inafahamika wazi wazi kutokana na kauli ya hapo juu kuwa wajibu mkuu wa lazima juu ya wafuasi wa Ahlul Bayt(a.s) ya wananyumba ya Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ni kuhuisha katika mikutano na mikusanyiko yao, kwa kujua imani na akida zao, kuelewa maana na ujumbe halisi kutokana na kauli na semi zao na kujizoesha na kufuata maamrisho yao na ni kusema kwamba mikutano na mikusanyiko yao iwe daima ni mikutano ya kusahihishana na kuwa tayari kwa maisha vile ipasavyo, na wala isiwe mikutano na mikusanyiko yao kwa ajili ya kuupoteza muda kwa starehe tu, kujiombea maslahi yao ya kibinafsi na kujifikiria mwenyewe na matatizo yake mwenyewe na matakwa yake mwenyewe bila kujali maslahi ya binadamu wengineo, imani na jamii kwa ujumla. Kwa hakika iwapo mikutano na mikusanyiko itakapokuwa vile tulivyofundishwa na Ahlul Bayt(a.s) basi nyoyo zetu zitahuika na vile vile fikara zetu zitakuwa njema zenye kuzaa matunda.

SOMO LA 14 5: SIRI NI AMANA

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

Wakati mtu asemapo jambo lolote na kujitazama mwenyewe, basi mazungumzo yake hayo ni amana na siri kwetu (na inatubidi sisi kuitunza). 150

Maelezo mafupi: Kuamini katika Dini ya Islam ina sura nyingi, ikiwemo uaminifu katika kuweka na kutunza siri za watu. Jambo ili lina umuhimu mno katika Dini ya Islam kiasi kwamba kutoa siri za watu kumesemwa kuwa ni mojawapo ya Madhambi Makuu. Kwa ajili ya kutaka kuthibitisha jambo fulani kuwa siri, si lazima kwa msemaji kusema na kuomba na kusisitiza kuwapo kwa siri na kuitunza kwake. Na badala yake, ishara ndogo inatosheleza kuelewa uhakika huu. Iwapo mtu akijitazama mwenyewe na kujichambua mbele ya mtu mwingine basi inatosheleza kwake yeye kuweka mazungumzo ya ndugu yake Mwislamu kama siri yake.

SOMO LA 14 6: ALAMA ZA IMANI YA DINI YA ISLAM

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

Wakati matendo yako mema yanapokufurahisha na matendo yako maovu yanapokuhuzunisha, basi wewe ni Mumin. 151

Maelezo mafupi: Dini ya Islam inasema kuwa kila mtu huzaliwa akiwa katika maumbile yaliyo halisi na safi, imani halisi na mapenzi ya mema. Maovu na maasi ndiyo yanayokuja kuathiri nafsi yake na kuibadilisha na kuigeuza kabisa. Hata hivyo, hadi pale mwanadamu anapokuwa akipenda mema na kuchukia mabaya, nafsi yake ya imani na hali ya uhalisi wake bado unakuwapo hai ndani mwake. Watu walio waovu ambao wanakuwa wamekerwa kwa matendo yao maovu, na hujisikia fahari katika hali hiyo na au wanapojitolea mhanga, uwema, usamehevu na uadilifu huwa ni kero kwao, kwa hakika wao ni makafiri.

SOMO LA 14 7: SHARTI LA KWANZA KWA AJILI YA KILA KAZI

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amemwambia Kumail ibn Ziyad:

Hakuna harakati wala kazi hadi pale utakapohitaji maarifa yake, uzoefu na elimu ya kutekeleza hivyo. 152

Maelezo mafupi: Iwapo sisi tutatafakari juu ya 'harakati zozote' zile, ndipo hapo sisi tutakuwa na uzoefu kwa mikakati na mipango ya Kiislamu na tutatambua hapo kuwa Dini ya Islam si mfuatilio wa 'ibada na dua tu na au inakosa mipango ya kimatendo. Badala yake inayo mipango na mikakati ya maisha ya mtu binafsi na vie vile masuala ya kijamii na vile vile hatua za maendeleo ya kibinadamu, jambo la kwanza ni akili na elimu ya uhakika. Islam inachukulia harakati na jitihada zote zisizo na matunda, ambazo zina elimu kidogo au mwongozo mdogo.

SOMO LA 14 8: UMUHIMU WA WAGENI

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

Wakati Allah swt anapowatakia watu kheri na ukarimu, basi huwazawadia. Wao waliuliza: "Je ni zawadi ipi hiyo?" Kwa hayo Mtume (s.a.w.w) alijibu: "Mgeni." 153

Maelezo mafupi: Hayo ni ya kweli kabisa. Kwa hakika mgeni ni zawadi kutoka Allah swt , zawadi yenye heshima na thamani kubwa mno. Lakini katika ulimwengu ambamo mapenzi yote yameshapotea, mgeni hathaminiwi. Na badala yake ngeni anachukuliwa kusumbua na kutokupendwa. Hivyo, ni kwa nadra tu hutokea kwa mtu kumwalika mtu mwingine au kutembelewa isipokuwa kwa maada tu, kibiashara na uhusiano wa kisiasa. Wakati ambapo katika nchi za Kiislamu na familia ambazo bado utamaduni wa Kiislam upo hai, basi kwao mgeni huheshimiwa na kutukuzwa kama ni zawadi kutokea Allah swt hata kama hatakuwa na uhusiano wowote wa kijamaa pamoja nao.

SOMO LA 1 4 9: HESHIMA NA MAPENZI

Al-Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema:

Yeyote asiyewaheshimu wakubwa na wala kuwahurumia na kuwapenda wadogo, basi huyo si miongoni mwetu. 154

Maelezo mafupi: Jamii za binadamu ni kama msafara mkubwa ambao daima upo katika mwendo. Watoto wachanga huzaliwa na mama zao, na watoto hao hukua na wakubwa huwa wazee na wazee hufa na hakuna mtu ambaye asiyepitia msafara huu. Humu ndani, watu wazima ndio kwa kawaida wanakuwa na uzoefu zaidi na kuwa na mtazamo wa undani zaidi na wamekuwa ndio vianzio vya huduma mbalimbali katika maisha yao lau wao wangalikuwa watu wenye kutuonya kuhusu matendo yetu iwapo ni mema au mabaya, na mahisabu yote yanaonyesha kuwa wao waheshimiwe na vijana na mabarobaro waelewe heshima zao.

Na kwa kuwa watoto bado ni wapya na mwazoni mwa maisha yao, lazima wapendwe na misingi ya ukuaji wao lazima ijengwe na wakubwa kwa moyo halisi, na kwa hakika hivyo ndivyo ilivyo njia na utamaduni wa kibinadamu na jamii inayoendelea kimaendeleo.

SOMO LA 150: JICHUKULIE NJIA HII KWA AJILI YAKO

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Chochote kile kutokea kheri utakachokituma, kitahifadhiwa kwa ajili yako, na chochote kile utakachokiahirisha wewe, kitawafaidia wengineo ( na uwajibisho huo utakuwa mzigo juu yako). 155

Maelezo mafupi: Mali na utajiri unapatikana katika ulimwengu wetu wa leo kuliko kabla ilivyokuwapo bila ya kujali madhumuni muhimu na falsafa ya mali. Wale ambao hulimibikiza mali kama vichaa, na ambao hawajali ni njia zipi za halali, haraamu, haki au kudhulumu, kamwe hawafikirii kuwa wao kamwe hawataambatana pamoja na mali yao, na wala kuila yote kwa pamoja. Kwa hakika mzigo mzito upo juu ya mabega ya wenye kuimiliki mali hiyo; kulimbikiza, kuiacha na kuondoka na hatimaye kubeba wajibu wote juu yao.

VITABU VILIVYOKUSANYWA NA KUTARJUMIWA NA AMIRALY M. H. DATOO

BUKOBA - TANZANIA

Anwani ya pepe: datooam@hotmail.com

Hazina kubwa ya elimu inapatikana katika mtandao:

"www.alitrah.org

"www.dartabligh.org

"www.al-islam.org/kiswahili

VITABU VILIVYOTAYARI

1. AHADITH 2500 ZA MTUME S.A.W.W. NA MA-IMAMU A.S.

2. BWANA ABU TALIB (a.s) MADHULUMU WA HISTORIA

3. DALILI ZA QIYAMA NA KUDHIHIRI KWA IMAM MAHDI a.s.

4. DHAMBI KUU LA ISRAAF (UFUJAJI)

5. DHAMBI KUU LA KHIANA

6. DHAMBI KUU LA KUFICHA UKWELI

7. DHAMBI KUU LA KULA VIAPO VYA UONGO

8. DHAMBI KUU LA KUTOA USHAHIDI WA UONGO

9. DHAMBI KUU LA KUTOKUTIMIZA AHADI

10. DHAMBI KUU LA UCHAWI

11. DHAMBI KUU LA ULAWITI

12. DHAMBI KUU LA ULEVI

13. DHAMBI KUU LA KUTOKULIPA ZAKA, KHUMS NA SADAQAH

14. ELIMU KWA MADRASSAH : KITABU CHA KWANZA

15. FUNGUO ZA PEPONI - DUA MBALIMBALI

16. HADITHI ZA WATOTO ( PAMOJA NA PICHA )

17. HISTORIA YA ISLAM

18. HUKUMU ZILIZOTOLEWA NA IMAM 'ALI IBN ABI TALIB a.s.

19. IMAM ALI IBN ABI TALIB a.s. : FADHAIL NA HUKUMU

20. JANNAT NA JAHANNAM

21. JE MAKHARIJI NI NANI ?

22. KANUNI ZA SAUM

23. KESI YA FADAK

24. SADAKA : KUTOA NA KUPOKEA

25. MAANDISHI YA NAWHA 200 ZA 14 MASUMIIN a.s. (KATIKA LUGHA YA URDU )

26. MAELEZO NA KANUNI YA HAJJ

27. MAFUNZO 150 YA MAISHA

28. MAKALA MCHANGANYIKO No. 1

29. MAKALA MCHANGANYIKO No. 2

30. MAKHALIFA 4 BAADA YA MTUME MUHAMMAD MUSTAFA S.A.W.W.

31. MASIMULIZI KUTOKA QUR'AN TUKUFU

32. MKUSANYIKO WA FAHIRISTI YA AYAH ZA QUR'AN

33. MSAFARA WA IMAM HUSAYN IBN Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. MADINA - KARBALA

34. MWONGOZO KATIKA KUTENGENEZA USIA.

35. NAWHA, MARTHIYYAH 3100 ZA 14 MASUMIIN a.s. (SAUTI KATIKA LUGHA YA URDU)

36. TADHWIN AL-HADITH

37. TAJWID ILIYORAHISISHWA

38. TAWBA

39. USAMEHEVU KATIKA ISLAM

40. UWAHHABI - ASILI NA KUENEA KWAKE

41. VITA VILIVYOPIGANWA KATIKA ISLAM

42. WAANDISHI MASHI'A KATIKA SAHIH NA SUNAN ZA AHL SUNNA

43. WANYAMA WALIOTAJWA KATIKA QUR'AN TUKUFU

VITABU VILIVYOCHAPWA 44. DHAMBI KUU LA KAMARI

45. DHAMBI KUU LA RIBA

46. DHAMBI KUU LA UWONGO (juzuu ya kwanza )

47. DHAMBI KUU LA UWONGO (juzuu ya pili )

48. HEKAYA ZA BAHLUL

49. KITABU CHA TAJWID

50. NDOA KATIKA ISLAM

VITABU VINAVYOTAYARISHWA

1. DHAMBI KUU LA KUDHULUMU HAKI ZA WENGINE AU KUTOZITIMIZA

2. DHAMBI KUU LA KUDHULUMU MALI YA MAYATIMA

3. DHAMBI KUU LA KUIBIA UZITO

4. DHAMBI KUU LA KUKWEPA JIHAD

5. DHAMBI KUU LA KURUDIA UKAFIRI BAADA YA KUSILIMU

6. DHAMBI KUU LA KUTOKUJALI ADHABU ZA ALLAH swt

7. DHAMBI KUU LA KUTOKUWATII WAZAZI

8. DHAMBI KUU LA KUVUNJA UHUSIANO NA NDUGU NA JAMAA

9. DHAMBI KUU LA KUWASAIDI MADHALIMU

10. DHAMBI KUU LA KUWATUHUMU WATU KWA ULAWITI

11. DHAMBI KUU LA MAUAJI

12. DHAMBI KUU LA MUZIKI

13. DHAMBI KUU LA SHIRK

14. DHAMBI KUU LA UTUMIAJI WA KILICHO HARAMISHWA

15. DHAMBI KUU LA UWIZI

16. DHAMBI KUU LA ZINAA

17. DHAMBI KUU LA KUTOWASAIDIA WANYONGE

18. HIARI NA SHURUTISHO KATIKA ISLAM

19. MADHAMBI MAKUBWA NA MADHAMBI MADOGO

20. MAJINA YA WATOTO WAISLAMU

21. MASWALI NA MAJIBU MBALIMBALI

22. QUNUT

23. QURBAA-MAPENZI YA WANANYUMBA YA MTUME MUHAMMAD MUSTAFA S.A.W.W.

24. TAFSIRI YA JUZUU' 'AMMA

25. TAFSIRI YA SURAH AL-YA-SIIN

26. TAQWA

27. TUSIUPOTEZE WAKATI

28. USINGIZI NA NDOTO

29. YAAS

3

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA

SOMO LA 21 : UKAMILISHO WA KAZI

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema :

Kukamilisha na kuendeleza matendo mema ni bora kuliko kuanzisha hivyo. 21

Maelezo mafupi: Mara nyingi sisi tunakumbana na kazi zilizo zenye faida na matendo yetu na majukumu ya maisha ya jamii ambazo zinabakia hazikukamilika. Watendaji wake wameanzisha kwa sababu mbalimbali za kuathiriwa, lakini wakaja kupoteza moyo wa kuendeleza na hivyo kuacha bila ya kukamilika. Islam inapendelea watu walio waaminifu na wenye moyo wa kujitolea ambao hukamilisha kazi yoyote ile wanayoianza.

SOMO LA 22: MIKAKATI YA KUDUMU

Al-Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema:

Allah swt amewaamrisha Mitume yote kuwausia watu kuhusu uaminifu na amana. 22

Maelezo mafupi: Jamii bora ni ile ambayo inayo mambo mema mbalimbali, na muhimu mojawapo ni kwa watu kuwa na uaminifu na amana, kuaminiwa kwa kauli na matendo na tutambue wazi kuwa adui mkubwa wa mtaji huu ni uwongo, udanganyifu na hila. Jamii ambamo uwongo na udanganyifu na hila yanakuwa mambo ya kawaida, basi watu wote wataogopana, watajikuta wamekuwa pekee, hivyo kila mmoja itambidi aubebe mzigo mzito wa majukumu ya maisha peke yake na kwa hakika jamii hii itakuwa ni ya kipekee bila ya ushirikiano na wengineo. Na kwa misingi hii hii ndiyo maana Mitume a.s. yote imekuwa na mikakati ya kuhubiri na kuwalingania watu katika ukweli, uaminifu na kutimiza amana.

SOMO LA 23: ADHABU KALI KABISA

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

Mtu yeyote yule ambaye anajua jambo na wala hakifuati, basi siku ya Qiyamah atakuwa na adhabu kali mno. 23

Maelezo mafupi Katika mantiki ya Dini ya Kiislam, elimu imekuwa daima ni chombo cha kutumika na vile vile kuboresha maisha ya jamii. Ama sivyo elimu hiyo haitakuwa na manufaa wala faida yoyote. Wale watendao madhambi kwa kutokujua, wana wajibika kidogo, lakini wale wanapotenda dhambi huku wakitambua wazi wazi, wao watakuwa na mzigo mzito na mkubwa wa kubeba na wale ambao wanapuuzia kuwahudumia jamii katika nyanja mbalimbali, na yeyote yule aliye na hata kiasi kidogo au kikubwa cha elimu, basi watabebeshwa wajibu huo huo.

SOMO LA 24: MAOVU YA MADENI

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

Jiepusheni kukopa kwa kiasi muwezacho, kwani huleta majonzi usiku na udhalilisho wakati wa siku. 24

Maelezo mafupi: Urembo na mavutio ya maisha haya ya vitu na mashindano ya anasa katika zama zetu hizi zinawafanya watu wengi watumbukie katika gharama wasizoziweza kwa kuchukua mikopo na madeni yasiyolipika au kwa kufanya malipo kwa awamu. Kwa kuwa mdaiwa si mtu huru, hivyo tunaelekezwa kutokutumbukia katika madeni isipokuwa katika nyakati za shida kubwa tu. Hatari na athari za madeni yanakuwa makubwa na hatari kwa mujibu wa kanuni za nchi mbalimbali, na kwa hakika inaumiza uhuru na uhuru wa kiroho wa mataifa.

SOMO LA 25: MAISHA BORA YA KIJAMII

Al-Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema:

Iwapo watu watalipana haki zao miongoni mwao, na kutimiza mahitaji ya wahitaji, wote wataishi maisha yaliyo mema na kutosheleza. 25

Maelezo mafupi: Katika Hadith iliyotajwa hapo juu, ambayo inazungumzia sadaka, kodi juu ya mali na milki na kuwasaidia mahitaji wale waliomuhtaji katika jamii zetu, inawaonya watu kuwa kwa kutimiza haki za watu wengine si jambo la hisani au la kibinadamu tu, bali ni kanuni iliyo muhimu mno ya kijamii ambapo amani na uhai wa jamii unapotegemea. Matokeo ya hatari yanayotokana na kutokuwapo na haki na vile vile ubaguzi wa watu ambayo yanahatarisha jamii za siku hizi na kwa hakika zinahatarisha na kuvuruga amani hivyo tunatambua umuhimu wa amri adhimu hii ya Dini ya Islam. Jamii zote za Wanaadamu zinahatarishwa na watu wa ulimwengu huu ambao wanachukulia haki ya kulazimisha na watu wenye uwezo mkubwa hujiepusha na haki zilizo faradhi juu yao kulipa.

SOMO LA 26: UFUNGUO WA MAAFA

Al-Imam Hasan al-Askari(a.s) amesema:

Allah swt ametuma kufuli za baadhi ya maovu na maradhi, ufunguo wao ni pombe, na uwongo ni mbaya zaidi kuliko pombe. 26

Maelezo mafupi: Jambo kubwa ambalo linaudhi maovu na magonjwa ni busara na akili, na kwa hakika haya ndiyo makufuli madhubuti yaliyowekea haya. Iwapo kufuli la busara litafunguliwa kwa ufunguo wa pombe, basi maovu na machafu yote yatakuwa huru na vile vile mlevi anaweza kutenda kosa, dhambi na ufisadi wowote ule.

Lakini iwapo mlevi atatenda kosa lolote lile akiwa katika hali ya ulevi, na mwongo huku akitambua wazi kwa fahamu zake, iwapo ataidanganya na kuihadaa taasisi ya maisha ya jamii, na akaua moyo wa kujitolea na akawa ndie chanzo cha madhambi na ufisadi wote katika jamii, hivyo uwongo ni hatari na uovu mkubwa hata kuliko pombe.

SOMO LA 27: ALAMA ZA WATU WA JANNAT ( PEPONI )

Al-Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema:

Watu wa Jannat ( Peponi) wanakuwa na alama nne:Uso wazi, ndimi zao zinazungumza kwa nguvu na mambo yaliyo wazi, moyo wa huruma na mikono ya kheri .27

Maelezo mafupi: Shule bora kabisa ya wanaadamu ni ile ambayo inamchukulia mtu ndani ya jamii na jamii kama mkufunzi wa watu bora kwa sababu jamii ndiyo chanzo cha baraka zote za maada na kiroho. Hadith ya hapo juu inazungumzia alama za watu walioneemeka na wa Jannat ( Peponi), masuala hayo manne yamejihusisha na ukakamavu wa mfungamano wa kijamii na kupandikiza mbegu ya mapenzi na upendo wa kibinadamu katika jamii. Nyuso zilizo wazi na za kuvutia, na ndimi zilizo nyororo na zilizojaa huruma, mipigo ya moyo kwa ajili ya kuwahurumia watu, na mikono isiyositisha misaada, naam, hizi ndizo alama za watu wa Jannat.

SOMO LA 28: ALAMA ZA MNAFIKI

Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) amesema kuwa: Luqman, mwenye busara alimwambia mwanake:

Zipo alama 3 za wanafiki: Ndimi zao hazioani wala nyoyo zao, Ndivyo zilivyo nyoyo zao ambazo hazioani na matendo yao, Yale yaliyo dhahiri hayaoani na yale yaliyo ndani mwao. 28

Maelezo mafupi: Unafiki ni maumivu makubwa yanayotokana na mtu mwovu na asiye na hima. Wale ambao wanajaribu kujionyesha kile ambacho sivyo walivyo, ndimi na nyoyo zao, udhahiri na undani wao, na vile vile kauli na matendo yao yanatofautiana. Kwa hakika watu kama hao huwa ni dhaifu na wala si mashupavu kwa kuelezea walivyo wao wenyewe kwa uhakika, na wala hawana mori na wla hawana maamuzi sahihi ya kufanya.

Wao wanaonekana katika sura mbalimbali na kwa hakika ni waovu kwa kila mtu hata wao wenyewe. Hata jamii ambazo zinajionyesha wema kwa nje wakati ni waovu kwa ndani. Ndimi zao ambazo ni vyombo vya kupasha habari kwa hakika yanapingana na kile kinachoendelea mioyoni mwa jamii hizi.

SOMO LA 29: USHAURI

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Wachukulie ushauri na mawaida vizazi zinavyokuja kutokea waliokutangulia na ushauri na mawaidha hayo yawe ni kwa ajili ya maisha na mustakbal wako. 29

Maelezo mafupi: Tarikh (historia) imejaa kwa ushauri na mawaidha na mafunzo tunayotakiwa kuyapata, na hatima za kukosa haki, udhalimu, utofauti na ubaguzi, vilio na kugeuka jiwe (wagumu), kutokujua na kutokujali hali ya mazingira na nyakati hizo, na kwa hakika yote hayo yapo bayana katika historia. Lakini Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s., mtu bora kabisa katika historia ya wanaadamu, anatuonya sisi tuchukue fundisho kwa ajili ya maisha yetu kutokea historia na hatima ya wale waliotutangulia ili isitokee sisi tukawa ndio mfano wa maovu na kasoro zetu zikawa ndizo mifano kwa vizazi vijavyo. Kwa hakika mawimbi haya ya muda yanawakumba watu wote na kuwachukua pamoja nao. Kwa hakika mataifa ambayo yanayamulika yale yaliyopita na kujenga utajiri na maendeleo yao ya mustakbal ndiyo yaliyobahatika na wenye ufanisi.

SOMO LA 30: KUONGEA NA UKIMYA

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema :

Hakuna wema wala faida katika ukimya wa mtu mwenye busara, na vile vile hakuna wema wala faida katika mazungumzo ya jahili. 30

Maelezo mafupi Allah swt amefanya ahadi pamoja na wale ambao wamejulishwa na waliosoma kuwa kamwe hawatabakia kimya pale patokeapo upotofu, tabia mbaya, kutokuwapo na haki na usawa na njama za maadui na hueneza kote nuru ya hidaya, haki, usawa na uadilifu katika nyoyo kwa kutokana na maelezo na maneno yao yaliyo ya unyenyekevu na kwa mantiki sahihi (na kila mtu anachukuliwa kuwa amejulishwa na kuwajibika kwa kile ajuacho, hata kama kitakuwa kidogo kiasi gani).

Ama kwa upande wa pili, wale wasio na habari au taarifa za kutosha, wasiwapotoshe watu kwa kutokana na kutokujua kwao vya kutosha. Kwa hakika ukimya ule na mazungumzo haya yanaweza kuleta maafa na upotoshi. Yaani anayejua vya kutosha asikae kimya na yule asiyejua vya kutosha asizungumze kwa sababu ya kutokujua.

4

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA

SOMO LA 31: FURAHA YA USAMEHEVU

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

Wewe utakapomzidi adui wako, basi mjaalie msamaha na kumwachia kama ni kuonyesha shukurani za ushindi wako . 31

Maelezo mafupi: Katika mtizamo wa Kiislamu, aina yoyote ya msaada na hisani, bila ya suala lolote, yanahitaji kushukuriwa, na shukurani ya uwezo ni usamehevu. Ushindi dhidi ya adui utaonekana pale tu ambapo moyo wa adui utakapo takasika dhidi ya maovu, na pale ambapo mizizi ya uadui utakapotokomea. Kwa kutoa sadaqa ya uwezo na nguvu ni usamehevu, kwa hakika ndicho kilicho jambo hilo kwa ajili ya sababu hizi. Kwa njia hii, adui atakuwa ameguswa moyoni mwake na hivyo adui wa jana atakuwa ndiye rafiki wa leo, na ni dhahiri kuwa ushindi utakuwa umepatikana wa undani na nje mwa mtu. Lakini, kinyume na hayo, wale ambao wanakuwa wamejitumbukiza katika kulipiza kisasi baada ya ushindi, si kwamba wanakuwa wamejinyima ubindamu, bali wanakuwa wanahatarisha ushindi wao vile vile.

SOMO LA 32: ZAHID KATIKA MAANA SAHIHI

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Kwa hakika, Zahid duniani humu ni yule ambaye haghalibiwi na yale yaliyo haramu, bali hufanya as-Sabr na wala hapotoshwi na yale yaliyo halali latika kumshukuru Allah swt na kutimiza wajibu wake kumkumbuka Allah swt. 33

Maelezo mafupi: Baadhi ya watu wasioelimika vya kutosha wameigeuza u-Zohdi katika sura ya kupotosha. Wao wameichukuliwa u-Zohdi kama ni kuachalia neema za Allah swt na kujinyima mambo yote ya maisha na badala yake kuamua kuishi kama masikini na mafukara. Wakati ambavyo sivyo hivyo ilivyo ukweli. U-Zohdi kwa hakika ni kama vile ilivyoelezwa na Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. hapo juu na inaweza kuelezwa kwa kusema :Subira na kujizuia dhidi ya yale yaliyo haram na kutokuachilia au kusahau wajibu wetu kwa ajili ya yale yaliyo halali.

Iwapo sisi kwa hakika tutaitafsiri hivyo U-Zohdi, basi kwa hakika itakuwa ni kujitengezea kwetu upya, kuboresha na kuwa fundisho kwa jamii nzima kuliko kuchukulia msimamo wa upotofu na kujinyima yaliyo halalishwa.

SOMO LA 33: KULINGANA NA MASHAHIDI 34

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Yeyote yule awaye katika jitihada katika njia ya Allah swt na akiuawa, hatakuwa katika daraja la juu kuliko yule ambaye anajiepusha na kutenda dhambi ingawaje angeliweza kulitenda hilo. 35

Maelezo mafupi: Katika msimamo wa mantiki ya Dini ya Islam, vita vikuu vitakatifu ni kupigana dhidi ya matamanio ya nafsi hususan katika mazingira yaliyochafuka. Kwa hakika vita dhidi ya maadui yatapewa ushindi iwapo yatapiganwa kwa uhalisi na moyo msafi, nia halisi isiyojipendelea na tamaa za kibinafsi. Kwa hakika haya hayatawezekana kupatikana hadi hapo mtu awe amepata elimu ya kutosha ya maadili na mapambano ya nafsi. Hivyo Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema kuwa wale ambao wanafanikiwa kushinda katika uwanja wa vita dhidi ya nafsi, na wanabakia watu halisi katika mazingira yaliyo machafu, kwa hakika hawapo katika daraja la chini kuliko mashahidi wanaouawa katika njia ya Allah swt. Kwa kufuata Hadith hii, sisi twasoma katika Nahjul Balagha kuwa watu kama hao wanakuwa katika daraja la Malaika huko Jannat (Peponi).

SOMO LA 34: WATU WALIO BORA

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Bora ya watu ni wale ambao hufanya maamuzi kwa haki na uadilifu . 36

Maelezo mafupi: Uamuzi wa haki katika Shariah, jamii na kimaadili itawezekana pale tu ambapo mtu anapochukulia maslahi yake na ya wengine kuwa sawa na mapenzi yake na chuki zake hazimshawishi wala kumzuia yeye asiweze kufanya haki na uadilifu. Na kwa hakika haya yatawezekana pale tu ambapo maisha ya mtu yatakuwa yameingiwa na nuru ya imani, uthamini wa kibinadamu, na mapenzi ya jamii kiasi kwamba mawingu ya ubinafsi, kutaka faida na uasherati hayawezi kupoteza fahamu na dhamira zake. Kwa hakika watu kama hawa inabidi waitwe watu bora kabisa.

SOMO LA 35: IBADA ZA WATU WALIO HURU

Al-Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema:

Waumini wapo wa makundi 3 :

Wale wanaomwabudu Allah swt kwa kuiogopa Jahannam; ibada hii ni ya watumwa Wale wanaomwabudu Allah swt kwa kutarajia malipo Yake; hii ni ibada ya mamluki; Wale wanaomwabudu Allah swt kwa mapenzi na huruma zake; kwa hakika hii ndiyo ibada ya mtu aliye huru. 37

Maelezo mafupi: Ingawaje ahadi ya kulipwa mema kwa matendo mema na adhabu kwa kutenda maasi na madhambi, basi tutambue kuwa thawabu za Allah swt huwa bora kabisa papo hapo Adhabu za Allah swt huwa ni kali na zenye kuumiza kabisa, lakini wale waja wake halisi hawaoni chochote isipokuwa Allah swt tu na wala hawamwombi yeyote mwingine isipokuwa Allah swt tu na nyoyo zao zimeja kwa mapenzi ya Allah swt na huruma tu, wao daima huangalia kile kilicho zaidi ya thawabu na adhabu. Na nia yao huwa ni kuzitii amri za Allah swt ambayo huwa imejaa kwa mapenzi yaliyochanganyikana na kumtambua na kumjua Allah swt .

SOMO LA 36: KILE KIVUNJACHO MGONGO WA MTU

Al-Imam Muhammad al-Baqir(a.s) amesema:

Mambo 3 yanamwangamiza mtu : Yule ambaye anayejigamba kwa mema yake Yule ambaye anayasahau madhambi yake Yule ambaye ni mbishi. 38

Maelezo mafupi: Wale ambao hukuza matendo yako, kwa hakika wanaridhika kwayo, na kwa hakika tabia hii huwadhuru kwa kupatikana maendeleo na ufanisi. Na wale ambao huyasahau madhambi yao, basi kila siku hupakwa kwa madhambi mapya badala ya kufidia madhambi yao yaliyopita na hatima yao itakuwa ni kuanguka kwa ghafla.

Ama wale ambao hubakia katika maoni yao tu, wanakuwa wameepukana na msaada wa fikara za kijamii na akili zilizojaa na elimu na maarifa na uzoefu wa wengineo. Kwa hakika watu kama hao hutumbukia katika makosa, na hatimaye migongo yao huvunjika kwa kulemewa na uzito mkubwa wa matatizo na shida za kila aina.

SOMO LA 37: KUWA MSAFI

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

Mdomo wako ni njia mojawapo ya Allah swt. Mdomo ulio bora kabisa mbele ya Allah swt ni ule wenye harufu nzuri. Hivyo uweke mdomo wako unukie harufu nzuri kiasi uwezacho. 39

Maelezo mafupi: Katika Hadith hii ambayo imetolewa kutokea Al Wasa'il as-Shi'a kwa kuhusiana na kanuni za kupiga mswaki ambayo yanayo maana mbili za kidhahiri na batini. Kidhahiri inamaanisha kwa kuwa mwanadamu hufanya dhikiri ya Allah swt, husoma Ayah za Qur'an Tukufu na kumwabudu Allah swt kwa midomo yenu, basi yeye atazifanya midomo yao kuwa safi na kunukia manukato mazuri.

Na maana yake ya kibatini (kindani) inathibitisha mdomo ule ambao unao uhusiano pamoja na njia takatifu za Allah swt na waja wake, ndiyo iliyopendelewa zaidi mbele ya Allah swt wakati pale inapokuwa na manukato kwa wema, usafi na mazungumzo mema na inapokuwa huru bila ya kuzungumza chochote kibaya, kashfa, uwongo na ukali au ufokaji.

SOMO LA 38: HATIMA YA UJAHILI

Al-Imam Jawad(a.s.) amesema:

Yeyote yule atendaye chochote bila ya kuwa na elimu na maarifa ya kutosha, basi atakuwa mharibifu zaidi kuliko kutengeneza au kurekebisha. 40

Maelezo mafupi: Hasara za ujahili haipo tu kufikia kiasi ambacho mtu kwa hakika hawezi kufikia uthamini wake wa maisha halisi. Bali, ubaya na maangamizi yanayotokana na makosa ni kubwa kwa wale wanaotenda mambo bila ya kuwa na elimu.

Hivyo, ni kwamba mtu jahili anajaribu kufanya jambo jema kwa ajili ya mtoto wake, lakini humtumbukiza katika mabaya na bahati mbaya; anajaribu kuisaidia Islam, lakini anaiaibisha Dini; anajaribu kudumisha amani miongoni mwa watu, lakini yeye ndiye huwa mchochezi wa utenganisho na unafiki; kwa kifupi, maovu yake na maangamizo yake katika nyanja zote yatakuwa makubwa na hatari zaidi kuliko matengenezo yake.

SOMO LA 39: MISINGI YA MUONGOZO

Al-Imam Muhammad at-Taqi(a.s) amesema :

Mumin anahitaji kuwa na sifa 3 : Ufanisi kutokea kwa Allah swt Mhubiri halisi anayehubiri kutokea moyoni mwake Kukubali kutokea yale anayoshauriwa. 41

Maelezo mafupi: Katika njia hii, pamoja na wingi wa mipando na miteremko ambayo mwanadamu hupitia maishani mwake kwa ajili ya kuokolewa kutokana na wingi wa hatari ambazo zinahatarisha ukuaji na yenye manufaa na kuwa mtu wenye manufaa katika jamii, kwanza kabisa yeye anahitaji uhusiano wa kiroho pamoja na Allah swt ikisaidiwa na uasili wake, na baadaye kuwa na dhamira ambayo huwa makini na ile ambayo inamwongoza undani mwake, baadaye masikio yasikiayo kwa kutumia mawazo yake, miongozo, nasiha na mashauriano pamoja na wengineo.

SOMO LA 40: MASIKITIKO NI TABIA ZA UJAHILIYYAH

Al-Imam Muhammad al-Baqir (a.s) amesema kuwa; katika mojawapo ya hotuba fupi ya Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) , ambayo haijawahi kusemwa na mtu yeyote kabla yake :Masikitiko ni mojawapo na tabia ya zama za ujahiliyyah (haimbidi mtu kulalamikia matatizo na magumu, na badala yake inambidi ajitahidi kuyatatua). 42

Maelezo mafupi: Hadith hii fupi iliyojaa maana inayo maana ya kidhahiri na kibatini. Udhahiri wake unazungumzia matendo yasiyo sahihi ambayo yamekuwapo mashuhuri katika zama za ujahiliyya. Wakati mtu alipokufa, waombolezaji wanawake walikuwa wakiitwa kuimba nyimbo, mashairi mahsusi yasiyokuwa na maadili.

Na maana nyingineyo ambayo Al-Imam Muhammad al-Baqir a.s. labda atakuwa akimaanisha ni, uombelezaji na masikitiko kwa nyakati ngumu na yenye shida na matatizo ya kibinafsi na kijamii, kwa hakika haya yote ni bure na upuuzi kwa kupoteza nguvu na wakati. Kwa hakika inambidi mtu ayatatue hayo kwa kuyatafutia utatuzi kwa kutumia uwezo wa akili na kufikiria njia endelevu na uvumilivu (subira).

5

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA

SOMO LA 4 1: KUJIPIMA MWENYEWE KILA SIKU

Al-Imam Musa al-Kadhim(a.s) amesema:

Yeyote yule asiyejipima kila siku, hana uhusiano wowote pamoja nasi. 43

Maelezo mafupi: Kuepukana na hasara na kujaribu kupata faida kubwa, katika taasisi yoyote ile iliyo kubwa au ndogo katika ulimwengu huu, haitawezekana bila ya kuwa na ukaguzi wa kila mara, majaribio na mahisabu kamili. Kwa hakika jambo la kushangaza ni kamba watu wapo waangalifu mno katika kuweka mahisabu yao ya mali na milki zao, na vile vile huwa waangalifu katika kupunguza au kuongeza uzito wao kwa gramu chache, lakini baadhi ya nyakati wao hata hawajali kuchunguza ubinadamu wao, maadili na masuala ya kiroho hata mara moja maishani mwao. Kwa hakika hili ndilo janga kubwa!

Lakini Mwislamu ambaye ni makini na halisi ni yule ambaye, kwa mujibu wa kauli ya Al- Imam Musa al-Kadhim a.s. katika hadith ya hapo juu, anachambua na kupitia mahisabu yake ya siku nzima bila kukosa. Iwapo atakuwa ametenda mema, basi hujaribu kuendeleza, na iwapo ametenda maovu, hujuta na kutubu.

SOMO LA 4 2: NISHANI ZA IMANI NI NGUMU KULIKO CHUMA

Al-Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema:

Waumini ni madhubuti kuliko chuma kwa sababu chuma kinapowekwa motoni, hubadilika, lakini Waumini wanapouawa na kuhuishwa tena, basi hakutakuwapo na mabadiliko yoyote katika nyoyo na imani zao. 44

Maelezo mafupi: Maisha ni mlolongo wa matatizo na masuala magumu. Wale walio dhaifu hujisalimisha kwa urahisi, na hujitoa kutoka uwanja wa mapambano, lakini wale walio madhubuti kwa baraka za imani zao, kamwe hawajisalimishi kwa idadi yoyote ya matatizo. Wao wanajua kuwa daima vizuizi huwa vingi katika amri na njia ya Allah swt, kujiepusha na madhambi, na kujipatia heshima na sifa, na kwa ajili ya kutaka kujipatia utukuzo haya, kujidhibiti mtu mwenyewe,moyo wa kujitolea na kujizuia dhidi ya nguvu za matamanio na matatizo mengineyo. Hivyo, wao hawasiti kuendelea na juhudi zao katika njia ya dini, na wala hawaogopi chochote cha matukio haya.

SOMO LA 4 3: UHAKIKA WA UMOJA NA UADILIFU WA ALLAH SWT

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Uhakika wa upweke wa Allah swt unaonyesha kuwa mtu asijaribu kufikia kuhusu uasili wa Allah swt, na imani juu ya uadilifu Wake unamfanya mtu asimtuhumu Allah swt kwa jambo lake lolote lile. 45

Maelezo mafupi: Kwa kiwango ambacho kanuni ya kuwapo kwa Allah swt ilivyo wazi na ushahidi kwa ajili yetu na kitu chochote kile kutokea duniani humu ni sababu za Ukuu Wake, nguvu, maarifa na uwezo, uhakika wa uasili wake upo umejificha mbele yetu. Kwa asababu Yeye si kitu cha kuonekana na yupo nje ya uwezo wetu wa kumjua. Hivyo tunachukulia uhalisi wake upo zaidi ya mtu yeyote yule anavyomdhania na huu ndio uhakika wa umoja. Ama kwa upande wa pili, baadhi ya matukio ya humu duniani hutokea kiasi kwamba sisi hatuelewi maajabu na majibu yao. Kwa kuzingatia uadilifu wa Allah swt unatuambia kuwa matukio haya yote ni wastani, na shaka yoyote ile inayojitokeza si kwa mujibu wa uadilifu na busara Zake.

SOMO LA 4 4: BAADHI Y ALAMA ZA IMANI

Al-Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema:

Mumini anao msaada mkubwa kabisa, na kwa gharama ndogo, na yenye busara maishani, na kamwe haipigwi mara dufu kutokea tundu moja ( haipatwi na madhara kwa mara nyingine kutokea mahala moja). 46

Maelezo mafupi: Imani inayo udhihirisho wa kisayansi, kimaadili na kijamii na dalili, ambapo bila ya hayo litakuwa ni jina tupu lisilo na maana. Hivyo Hadith ya hapo juu inazungumzia dalili zake nne :

1- Waumini wanawapatia misaada muhimu ndugu zao Waislamu kwa sababu misaada yao hiyo inakuwa pamoja na mapenzi, uadilifu na kutambua wazi.

2- Wao hawana maisha ya anasa na ghali na wala hawatendi makosa kwa ajili ya kujipatia vitu vyao.

3- Wao wanakuwa makini na kutambua katika maisha hususan katika masuali ya kiuchumi.

4- Wao wanajifunza somo kutokea kila tukio litokeapo na hivyo wao hawapatwi na majanga kwa suala hilo hilo moja.

SOMO LA 4 5: ULIMWENGU SI MWISHO WETU BALI NI NJIA YA KUPITIA

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Ulimwengu umeumbwa kwa makusudi mengineyo, na kamwe haikuumbwa kwa ajili yake mwenyewe. 47

Maelezo mafupi: Kwa hakika inakuwa vigumu kwa watu kuelewa tafsiri za Ayah za Qur'an Tukufu na hotuba mbalimbali zinazoisifu dunia, yaliyomo duniani, kwa kuitambulisha dunia kama ni jumba la biashara au ni shamba la Waja wa Allah swt upande mmoja na kwa upande wa pili, kwa Ayah za Qur'an Tukufu na hotuba ambazo zinazoilaumu dunia hii na kwa kuiita kuwa ni hatari, danganyifu na chanzo cha movu.

Lakini, Hadith ya hapo juu inazitafsiri hayo kwa uwema kabisa, kwani inabainisha waziwazi kuwa iwapo dunia na yale yaliyomo yatatumiwa vyema na ipasavyo kwa ajili ya kujipatia maendeleo ya binadamu na upanuzi wa uadilifu na vile vile kama neema kwa ajili ya wanaadamu, basi kwa hakika itakuwa ni jambo la thamani na njema kabisa. Lakini iwapo mtu atadhania kuwa huu ndio mwisho wake tu na kuipendelea kupita kiasi, na kufanya uasi, maovu na madhambi, basi hakuna shaka kuwa itakuwa kuchukiwa na hatari mno.

SOMO LA 4 6: THAMANI YA MTU

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Ole wako ! Hakuna thamani yako isipokuwa ufanisi na Jannat, hivyo usibadilishane nacho kwa thamani ya kitu kingine. 48

Maelezo mafupi: Kwa kawaida iwapo mtu ataulizwa thamani ya maisha yake, basi hawezi kukisia au kukadiria. Hata hivyo, tunaona kuwa siku baada ya siku mtu huyu huyu anabadalisha thamani ya maisha yake kwa vitu ambavyo hatimaye anajikuta kuwa amepata hasara kubwa kwani amejibadilisha kwa vitu ambavyo havina thamani wala havitabakia (ni vitu vyenye kwisha na kuangamia) kama vile nyumba au jengo, au gari.

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. anasema kuwa hakuna kitu chochote cha humu duniani kinachoweza kubadilishwa kwa maisha yako matakatifu! Jambo ambalo unaweza kubadilisha nacho ni ridhaa ya Allah swt, uendelevu wa kibinadamu na kiroho na vile vile neema isiyokwisha na yenye kudumu milele. Kwa hakika inastahili kujaribu na kujipatia na vile vile hata kama itabidi kujitolea mhanga kwa ajili ya kujipatia kiasi kiwezekanacho.

SOMO LA 4 7: UKWELI NA UWONGO

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Ukweli ni nzito ipendezayo, na uwongo ni nyepesi na rahisi, lakini ni yenye maumivu na hatari mno. 49

Maelezo mafupi: Tunaona vile Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. alivyoweza kuelezea kwa uzuri kabisa kuhusu ukweli na uwongo katika sentenso fupi ya hapo juu! Kwa hakika ukweli unaonekana mkali na mara nyingi huwa chungu lakini hatima yake ni yenye kufurahisha na njema. Inafyonzwa kwa urahisi na jamii na hivyo huimarika kuwa madhubuti.

Lakini uwongo ni kitu kilicho rahisi na mara nyingi huwa tamu ipendezayo, lakini athari zake huwa maangamizi kama ilivyo chakula kitamu ambacho kwa hakika ni chakula chenye sumu ambacho kinadhuru moyo, tumbo, na matumbo ambayo yanatokezea hivyo iwapo vitaliwa na kumezwa. Na vivyo hivyo ndivyo ulivyo uwongo kama chakula hicho chenye sumu, ambapo kwa hakika uwongo huo huangamiza sehemu zote za jamii.

SOMO LA 4 8: URITHI WENYE THAMANI MKUBWA WA WAARABU

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

Sentenso iliyo sahihi na yenye nguvu ni ile iliyotolewa na Waarabu katika msemo wa Lubaid (mshairi maarufu) pale asemapo: Ole wenu ! Kitu chochote mbali na Allah swt ni batili na uwongo na hatimaye kupotezwa kwa neema. 50

Maelezo mafupi: Tukitilia maanani kuteketea na kuangamia kwa mali na wadhifa au cheo na kuondolewa kwa baraka, kwa hakika yote yanam tanabahisha mtu kushikilia ukweli na haki katika kujipatia hayo na vile vile awe mtumiaji wa kiasi, yaani asiwe mfujaji 51 Kudumu na umilele ni mfano wa nguo ambayo inafaa kwa ajili ya kimo adhimu, kusimoingia uharibifu wa aina yoyote na kwa hakika heshima na adabu ndiyo yanayonasibishwa na uhalisi Wake. Inambidi mtu atambue uhakika huu katika kila hali ya maisha yake na kamwe asiwe mjeuri au mwenye kiburi.

SOMO LA 4 9: NINAWACHUKIA

Al-Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) amesema:Yule ambaye anaghushi au kumlaghai na kumfikishia hasara Mwislamu mwenzake, basi huyo hayupo pamoja nasi . 52

Maelezo mafupi: Wale ambao huchukulia furaha yao katika hali mbaya ya wengineo na faida zao kwa hasara za wengineo, basi watu kama hao kamwe hawatahesabiwa kuwa ni binadamu kwa hakika wala Wasilamu waaminiwao. Fadhila za mtu juu ya viumbe vinginevyo ni tabia na desturi zake katika jamii na yeyote yule anayejipatia faida kwa hasara za wengineo, kwa hakika anakuwa amekosa hadhi hiyo.

Mara nyingine tunaona kuwa sababu za hasara zinakuwa wazi na kutegemewa ambapo mara nyinginezo sababu hizo zinakuwa zimefichika kwa sababu ya kughushi na kukandamiza ama kwa njama au kukosa uaminifu. Kwa hakika haya yameharamishwa wazi wazi katika dini ya Islam katika sura yoyote ile, na hivyo ndivyo maana Al-Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) amesema:"Mimi huwachukia wale watu wafanyao maovu na madhambi haya."

SOMO LA 50: JITIHADA ZA WALIO WAOVU NA DHAIFU

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Kusengenya ni jitihada za mwisho za wale waliodhaifu 53

Maelezo mafupi: Baadhi ya madhambi yanapatikana kuwa ni miongoni mwa Madhambi Makuu (kabair dhamb) 54 ambayo machache ni Uchoyo au Ubahili, Udhaifu, Udhalilisho, na pasi na ushujaa kama Uwongo na Uzushi. Wale ambao wana tabia za kutafuta aibu na kasoro za wengine na hivyo kuzitoboa huku wakiwavunjia adabu na heshima za watu hao, na kwamba tunaona kuwa wingi wa watu wanakuwa wamejihusisha na moja wapo ya maovu kama hayo na hivyo ndivyo utawaona wanajiridhisha kwa mioto yao ya husuda na maovu na uwongo wao kwa njia hii, kwa hakika watu kama hawa ni dhaifu na ni watu waovu ambao hawaonyeshi uhodari wao kwa kujitokeza mbele bali utaona wao wanalengea kutokea nyuma ya migongo. Imeelezwa katika Hadith kuwa mtu yeyote anayezua uwongo, akatubu, basi atakuwa wa mwisho kuingia Jannat (Peponi). Ama sivyo, atakuwa ndiye mtu wa kwanza kuingia Jahannam (Motoni).

6

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA

SOMO LA 5 1: ALAMA ZA UKANDAMIZAJI

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Dhalimu anazo alama 3 :

Kuwadhulumu wale walio zaidi yake kwa upinzani na kutokutii Kuwadhulumu wale walio chini yake kwa kuwakandamiza na kuwanyanyasa Na kushirikiana pamoja na wadhalimu. 55

Maelezo mafupi: Yeyote yule ambaye hutawaliwa na kasumba ya ukandamizaji akilin mwake, na kuathiriwa na ukosefu na maadili, hujidhihirisha tu vyovyote vile. Yeye hujiepusha na kutekeleza wajibu wake mbele ya wale ambao yeye atakuja kuwatii, na hufikia mwisho wa ukandamizaji, kutumia nguvu, vitisho na kudhulumu mbele ya wale walio dhaifu kwake, na huwachagua marafiki na wenzake miongoni mwa wale walio dhalimu. Yeye huwa daima dhalimu.

SOMO LA 5 2: HAKUNA UGONJWA USIOTIBIKA

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

Allah swt hakujaalia ugonjwa wowote hadi pale ameumba dawa yake. 56

Maelezo mafupi: Katika ulimwengu huu tunaoishi kuna matukio na athari zake. Zipo nguvu sahihi na zile zilizo pingamizi ambazo zinahitajiwa kutafutwa ili ziweze kutumiwa vile ipasavyo. Si kwamba hakuna magonjwa yoyote yasiyotibika na vile vile hakuna tatizo la kijamii lisiloweza kusuluhishwa. Wale ambao huchukulia msimamo kuwa matatizo hayawezi kutafutiwa ufumbuzi na popote pale wanapokumbana na masuala magumu husema kuwa hayo ni magonjwa sugu yasiyoweza kupatiwa ufumbuzi, kwa hakika wao hukiuka uhakika huu wa kusema kuwa hakuna ugonjwa usiotibika. Hivyo inatubidi sisi tujihusishe katika uwanja wenye matukio magumu maishani kwa subira na ustahimilivu na tujaribu kutafuta ufumbuzi wake.

SOMO LA 5 3: KWA NINI UPENDELEO HUTOKOMEA ?

Al-Imam Muhammad al-Baqir(a.s) amesema:

Allah swt amefanya Sharia ya kudumu kuwa Yeye kamwe hazichukui neema alizowajaalia watu, hadi pale wao watakapotenda dhambi litakalosababisha kuondolewa kwao kwa neema hizo. 57

Maelezo mafupi: Neema za Allah swt zipo chungu nzima bali si bila sababu. Allah swt kamwe hagawi wala kuzichukua neema Zake bila sababu. Wakati wanaadamu wanapozitumia neema zake kwa maovu, madhambi, maangamizo na uharibifu na pasi na haki, basi neema hizo hizo zinabadilishwa katika maangamizo yao wenyewe. Neema hizo walizojaaliwa zinachukuliwa tena na kubadilishwa kwa maafa na misiba. Viwanda na teknolojia yao yanageuka kuwa maangamizo na jamii zao zinakuwa ndizo vianzio vya kutokuwa na amani na usalama, na vie vile vyombo vya upesi vinageukia kuanguka kwao, na yote hayo ni kwa sababu wao wametumia vibaya neema za Allah swt alizowajaalia.

SOMO LA 5 4: SHAHADA NA UHALISI

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

Ukifa katika hali ya utohara, utakuwa miongoni mwa Mashahidi. 58

Maelezo mafupi: Hadith ya hapo juu ya Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ni sehemu ya maagizo kwa mmoja wa Masahaba wake; "Iwapo itawezekana kwako, fanya wudhuu usiku na mchana, kwani iwapo utafariki ukiwa tohara katika hali ya wudhuu, basi wewe utahesabiwa kuwa Shahidi." Hivyo tunaona kuwa amri ya kwanza ni kufanya wudhuu, na papo hapo ujumbe mkubwa ni kutuambia sisi kuwa ni umuhimu mno kuishi maisha na kufa tukiwa bila madhambi. Wale ambao ni watoharifu wasio na madhambi, nyoyo zao huwa safi na maisha halisi na akili zao, na hufa kutokea humu duniani katika hali hiyo, na hivyo kwa hakika wao watahesabiwa miongoni mwa Mashahidi kwani ushahidi si tu kuuawa vitani tu. Zipo Ahadith sahihi zinginezo za Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ambazo zinathibitisha ukweli huu.

SOMO LA 5 5: WAJIPENDEAO KUJITOA MHANGA WENYEWE

Al-Imam Muhammad al-Baqir(a.s) amesema:

Babu yangu (Al-Imam Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. ) kwa sababu ya Masahaba wake, hakusikia maumivu ya dharuba za mapanga wala mikuki ya maadui (Jeshi la Muawiyah bin Abi Sufian ). 59

Maelezo mafupi: Wakati uvutio wa mtu unapokuwa katika hatua ya mapenzi, kwa hakika mapenzi mahsusi, basi hisia zake zote zinakuwa zikilenga mahala hapo, hivyo chochote kile kitakachomwia basi kitavumiliwa nae. Si kuvumilia tu, bali hatajisikia vibaya. Wakati ambapo wanawake wa Kimisri, kwa kuuona uso wa Mtume Yusuf a.s., wakiwa wameghalibiwa na mapenzi, walipoteza fahamu zao na wakajikata vidole vyao badala ya matunda, hivyo hatushangai kuwa wale walio na mapenzi halisi katika njia ya Allah swt hawaoni ugumu wala maumivu katika kujitolea mhanga katika njia ya haki na ukweli ya Allah swt. Kwanza kabisa inambidi mtu awe mfanya mapenzi, ndipo hapo kutakapokuja kufikiwa hatua ya kuweza kujitolea mhanga na kuweza kuvumilia.

SOMO LA 5 6: MWENYE BUSARA NA MPUMBAVU

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Mtu mwenye busara hutegemea akili yake, wakati ambao mpumbavu hutegemea matakwa yake tu. 60

Maelezo mafupi: Watu wenye busara huwa ni watu wanyoofu na wenye kutaka ukweli na haki. Hivyo utawaona daima wao wakitafuta malengo yao makuu katika msaada wa Watakatifu ambao kuwafikia wao haiwezekani bila jitihada na matendo, kwani wao hulenga jitihada zao katika malengo, wakati ambapo wapumbavu wasiojua wanakuwa wametumbukia katika bahari la matakwa na fikara, na hujitafutia katika ulimwengu wa kubuni na ndoto, na kwa kuwa kutumbukia katika ndoto hakuhitaji jitihada wala matendo basi fikara potofu zinakuwa zikiwepo katika kila sehemu ya maisha yao. Wao daima hubakia katika ndoto zao kuwa kweli kesho, ambavyo haitakuja na kamwe isije, hivyo wao hawana msaada wowote ule katika maisha yao isipokuwa ndoto na matakwa yao tu.

SOMO LA 5 7: WAPO WACHAMUNGU WACHACHE

Al-Imam Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Wingi wa watu ni watumwa wa ulimwengu wa vitu, na kwa hakika Dini ipo katika ndimi zao tu. Maisha yao ilimradi yapo sawa chini ya dini yao, wao wanaiunga mkono. Lakini pale wanapojaribiwa na matukio magumu, basi hubakia wachamungu wachache. 61

Maelezo mafupi: Dini, hususan Dini ya Islam, inahifadhi haki za watu katika jamii na kusaidia na kuunga mkono matakwa yao yaliyohaki na sawa. Lakini mara nyingine Dini inakuwa kizuizi kwa ajili ya matakwa ya mtu binafsi. Kwa hakika hapa ndipo watu wanapoweza kutambuliwa iwapo kweli ni watu wa Dini kama vile wanavyojiita.

Watu wengi huangalia kila kitu kwa mtazamo wa maslahi yao na kuitangaza Dini pale wanapoona kuwa inalinda maslahi na haki zao, lakini pale Dini inatenganishwa na maslahi yao ya kibinafsi, wao wanaiacha moja kwa moja na wanashuhudia kuwa sisi twaamini katika baadhi na hatuamini katika baadhi. Ama kwa hakika wale walio katika Dini huwa daima waaminifu na waumini halisi katika kila hali, na kwamba Dini ndiyo inayokuwa kila kitu kwao, na kamwe hawajali wala kupotoshwa na maslahi yao ya kibinafsi.

SOMO LA 5 8: UADILIFU MIONGONI MWA WATOTO

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:Fanya uadilifu mingoni ma watoto wako kama vile utakavyopenda wewe utendewe uadilifu miongoni mwenu. 62

Maelezo mafupi: Mojawapo ya makosa makuu ni kufanya upendeleo miongoni mwa watoto. Baadhi ya wazazi huwapendelea watoto wao wakubwa na ambapo wengine huwapendelea watoto wao walio wadogo. Kwa hakika utaona kuwa katika baadhi ya nyakati wazazi hao hupita mipaka na kwamba humpendelea mmoja wao kwa kupita kiasi kwa kumwonea huruma, mali na milki na mapenzi na hivyo kuwanyima kabisa watoto wake wengine haki kama hizo.

Kwa hakika hali hii inaibua moto wa uchoyo na husuda mioyoni mwao, na kwenda mbele, wao watakuwa maadui miongoni mwao na kugombana na kutengana na wazazi wao na hata wataweza kuthubutu kutaka kulipiza visasi katika jamii. Hivyo tujiepushe na tabia hii, kwani inatubidi tuwe waadilifu miongoni mwa watoto wetu.

SOMO LA 5 9: WEWE UPO DAIMA UKIDHIBITIWA

Al-Imam Muhammad at-Taqi(a.s) amesema :

Uelewe wazi wazi kuwa wewe hauwezi kutoka nje ya jicho la Allah swt. Sasa jitazame utakuwaje ? 63

Maelezo mafupi: Chapa ya kwanza ya Imani katika Allah swt ni daima kuwa na hisia na kujidhibiti vyema kwa maarifa ya Allah swt. Utambue wazi kuwa hakuna mwanya wowote ule ambao unakuwapo wewe nje ya elimu Yake, kwani walinzi wake wapo daima wametuzunguka pande zote.

Kiwango cha juu cha Imani kinamfanya mtu awe daima akijihisi akiwa mbele ya Allah swt. Kwa hakika kuwa na hisia kama hizi ni kipeo cha juu kwa ajili ya mwanadamu na jamii kwa ajili ya kujirekebisha na kujiongoza katika ubora kabisa wa Imani, na kwa hakika hutengeneza na kurekebisha kasoro zote za kijamii.

SOMO LA 60: SI KUSIFU KWA KUDANGANYA, WALA SI WIVU

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Kusifu na kutukuza zaidi ya ustahiki na haki ni udanganyifu na kusifu na kutukuza kasoro ya ustahiki ni udhaifu katika kuelezea au wivu. 64

Maelezo mafupi: Hakuna shaka kuwa mtu anayepaswa na mwenye sifa za kusifiwa ni lazima asifiwe na kushukuriwa, kwa njia hii sisi tutampa hima na nguvu katika mwelekeo wanaoelekea mbele. Lakini haya yanatakiwa lazima yawe sawa kabisa na sifa za mtu mwenyewe anavyostahiki. Ama sivyo, kutakuwa na matokeo na madhara mabaya. Iwapo yatakuwa zaidi ya mema, basi hapo tunasema kuwa ni udanganyifu ambayo kwa hakika huumiza sifa za msemaji na kusababisha kujiona na kujipenda kwa mtendaji. Na iwapo kwa hakika itakuwa kasoro ya sifa za mtu, basi itamvunja moyo mteda mema na huonyesha wivu au kuthibitisha udhaifu wa msemaji.


3

4

5