Site ya Al-Imaamaini Al-Hassanaini (A.S) ya usambazaji wa utamaduni wa Kiislamu na mafunzo ya Kidini

VISA VYA KWELI NO.2

0 Voti 00.0 / 5

VISA VYA KWELI NO.2
2) UKARIMU
Allah Mwenye Hikma, amesema:
“KWA HAKIKA ALLAH YUPO PAMOJA NA WANAOJILINDA NA MAOVU NA WANAOFANYA WEMA (KWA WENGINE).”1
MAELEZAO MAFUPI:
Allah humpenda mtu mwenye sifa ya ukarimu, kama ambavyo tu Allah ameonyesha upole kwetu, ni muhimu kwetu kuonyesha ukarimu zaidi kwa wengine. Hata kama mtu ametukosea, tunapaswa kujibu kwa upole na tusilipe uovu kwa uovu, kwani hili litaongeza mafuta kwenye moto na kuzidisha chuki na uadui.
Mwenendo wa wajumbe wa Allah (na Maimam) ulikuwa kwamba wak- isalimiwa, wanaitikia kwa salamu iliyo bora zaidi na kwa ukamilifu zaidi na wakifanyiwa wema, walikuwa wakiulipa, (tena) kwa kuzidisha (walivyofanyiwa wao).
Wale wanaofanya wema na kuonyesha ukarimu kwa wengine, huvuta mioyo ya watu, na wakati huohuo matendo yao yanamuumiza shetani.
Lazima ikumbukwe kwamba wale wanaofanya wema huwa hawamdhalilishi (wanayemfanyia wema) au kuharibu amali zao kwa kuweka aina yoyote ya masharti (kwa huyo waliyemfanyia wema).
Myahudi masikini alipata kukutana na muabudu moto tajiri wakiwa safari- ni. Muabudu moto aliyekuwa anamiliki ngamia na masurufu ya kutosha kwa ajili ya safari, alimuuliza, “Ni nini imani na Itikadi yako?”
Myahudi alijibu, “Ninaamini kwamba ulimwengu huu una aliyeuumba na ninamuabudu yeye na ninaomba hifadhi kwake. Ninaonyesha wema kwa yeyote anayeikiri imani yangu, lakini ninamwaga damu ya yeyote anayeto- fautiana na mimi. Ni nini itikadi yako?”
Muabudu moto alijibu, “Nina wapenda viumbe wote, simdhuru yeyote na ninaonyesha ukarimu na wema kwa marafiki na maadui pia. Mtu yeyote akinikosea, nina jibu kwa wema kwa sababu najua kuwa ulimwengu huu una muumba.”
Aliposikia hivi, Myahudi alisema, “Usidanganye sana. Mimi ni binadamu kama wewe, lakini wakati wewe unasafiri juu ya ngamia na una masurufu ya safari, hunipi chakula chako wala huniruhusu nikae kwenye ngamia wako.”
Muabudu moto aliteremka kutoka kwenye ngamia wake na akatandika kitambaa chini, akaweka chakula chake mbele ya mwenzake, myahudi alikula mkate na kisha akakaa kwenye ngamia ili kuondoa uchovu. Walikuwa wamesafari umbali fulani pamoja. Ghafla myahudi alipompiga ngamia kwa bakora alimlazimisha kukimbia. Yule Mwabudu moto alimwita:
“Ewe mtu! Nilionyesha upole kwako lakini sasa, unalipa ukarimu wangu kwa kuniacha peke yangu jangwani!”
Lakini haikujalisha chochote alichosema, nasaha zake hazikuwa na faida. “Nilikutajia kwamba nina muangamiza yeyote anaye tofautiana na mimi katika imani na itikadi,” Myahudi alimkemea huku akikimbia.
Muabudu moto alitizama juu mbinguni na kuomba: “Ewe Mola wangu! Nimemtendea mtu huyu vyema, lakini amenilipa uovu. Nitendee uadilifu.” Alipokuwa akisema haya, aliendelea na safari yake. Alikuwa amesafiri umbali mfupi tu, ghafla macho yake yalipoangukia kwenye ngamia wake, aliyekuwa amesimama peke yake baada ya kumbwaga myahudi chini. Myahudi, aliyekuwa ameumizwa vibaya, alikuwa akilalama kwa mau- mivu.
Alikuwa na furaha sana, muabudu moto alichukua ngamia wake, akapanda mgongoni mwake na alipokuwa anataka kuondoka Myahudi alilalamika: “Ewe mtu rahimu! Umevuna matunda ya wema wako na nimeshuhudia matokeo ya uovu wangu; sasa kwa kuzingatia imani zako, usiondoke katika njia ya wema; kuwa mpole kwangu na usinitelekeze katika jangwa hili.”
Muabudu moto alijiwa na huruma na akamruhusu kukaa kwenye ngamia na akampeleka mjini.2
1. WEMA WA IMAM HUSEIN (AS) KWA MPANDA NGAMIA
Imam Sadiq (as) alisema: “Mwanaume mmoja alikuwa akimvuta mwanamke alipokuwa (mwanamke) amejishughulisha katika kutufu Kaaba. Mwanamke huyu alikuwa akinyanyua mikono yake mwanaume yule alipoweka mkono wake juu ya mkono wake (mwanamke) wakati huo Allah aligundisha mkono wake katika mkono wa mwanamke.
Watu walimiminika (kwenda) kushuhudia tukio hili la ajabu kwa wingi mkubwa kiasi kwamba utembeaji ulikwama. Mtu mmoja alitumwa kwa Amiri wa Makka kumjulisha juu ya tukio hili. Alikusanya wanazuoni wote na kwa ujumla wakajaribu kutafuta suluhisho la tatizo hili. Watu wengi pia wa kawaida walikusanyika wakitaka kujua hukumu itakayotolewa kwa uhalifu huu. Wote wakiwa wamesimama (huku) wametatizika, hatimaye Amiri alisema: “Je kuna mtu yeyote hapa kutoka katika familia ya Mtukufu Mtume (saw)?”
Wale waliokuwepo wakasema, “Ndio! Husein Ibn Ali (as) yupo hapa” Usiku ule Amiri aliamuru Imam (as) akaletwe mbele yake. Alitaka kujua hukumu ya tukio hili kutoka kwa Imam (as)
Kwanza, Imam (as) aligeukia Ka’aba na kunyoosha mikono yake alisima- ma katika hali hii kwa muda kisha akaomba dua.
Kisha alimfuata mwanaume yule akautenganisha mkono wake kutoka katika mkono wa yule mwanamke kwa nguvu ya Uimam wake. Yule Amiri alimuuliza Imam (as): “Ewe Husein (as) nimuadhibu?” “Hapana,” alijubu Imam (as).
Mtunzi anasema huu ulikuwa ni wema ambao Imam (as) aliuonyesha kwa mpanda ngamia lakini ni mtu huyu huyu aliyelipa kitendo hiki cha wema kwa kukata mikono ya Imam ili akwapue mkanda wake, katika giza la usiku wa 11 Muharram 61H.A.3
2. ABU AYYUB ANSAARI
Abu Ayyub Ansaar alikuwa ni mmoja wa masahaba watukufu wa Mtukufu Mtume (saw). Mtukufu Mtume (saw) alipohama Makka kwenda Madina, makabila yote ya Madina yalimuomba akae lakini alisema:
“Sehemu nitakayokaa inategemea sehemu atakayokaa ngamia wangu.” Msafara ulipofika sehemu karibu na nyumba ya Maalik Ibn Najjar, ambayo baadaye ilikuja kuwa mlango wa msikiti wa Mtume, ngamia alikaa chini kupumzika. Lakini muda mfupi baadaye alisimama tena na akaanza kutembea, kisha akarudi sehemu ile ile aliyokuwa amekaa awali.
Watu wakaanza kumuendea Mtukufu Mtume (saw) na kumuomba akawe mgeni wao. Alipoona hivi, Abu Ayyub alinyanyua mfuko uwekwao kwenye siti ya ngamia wa Mtukufu Mtume (saw) kutoka kwenye mgongo wa ngamia na akaupeleka nyumbani kwake.
Mtukufu Mtume (saw) alipobaini kuwa mfuko wake haupo, aliuza “Nini kimetokea juu ya mfuko wangu?” Wale waliokuwepo walimjulisha kwam- ba Abu Ayyub alikuwa ameupeleka nyumbani kwake.
Mtukufu Mtume (saw) akasema: “Mara nyingi mtu anatakiwa aambatane na mzigo wake” kisha akaelekea kwenye nyumba ya Abu Ayyub na akakaa hapo hadi nyumba katika eneo la msikiti zilipokuwa zimejengwa.
Awali, Mtukufu Mtume (saw), alikuwa akiishi katika chumba cha chini wakati Abu Ayyub aliishi juu ghorofani lakini baadaye aliomba: “Ewe Mjumbe wa Allah! Sio sawa kwamba wewe ukae chini, wakati sisi tunaishi ghorofani juu: itafaa zaidi ikiwa utahamia juu.”
Mtukufu Mtume (saw) alikubali na akaomba vitu vyake vihamishiwe juu. Abu Ayyub alikuwa pamoja na Mtukufu Mtume (saw) na alishiriki katika vita kama Badr na Uhud, akipigana dhidi ya maadui wa Uislam akionye- sha ushujaa na ukakamavu wa kusifika.
Usiku akiwa anarudi nyumbani baada ya vita vya Khaibar, Abu Ayyub alikesha usiku kucha akilinda hema la Mtukufu Mtume (saw). Asubuhi ilipopambazuka, Mtukufu Mtume (saw) aliuliza: “Ni nani yupo nje huko?”
“Ni mimi, Abu Ayyub”, lilitoka jibu.
Mtukufu Mtume (saw) alisema mara mbili, “Allah akurehemu!”
Hivyo, Abu Ayyub kwa kupitia wema wake kwa Mtume, kwa fedha zake na roho yake, alinufaika na dua hii ya Mtukufu Mtume (saw).4
3. MALIPO YA MASHAIRI
Siku moja ya Nawruz, Mansur Dawaaniqi, Khalifa kutoka ukoo wa Bani Abbasi aliyechukua ukhalifa baada ya kaka yake Abu al-Abbas Saffaah, alimuamuru Imam Musa Kadhim (as) kuhudhuria katika Eid ya Nawruz, ilifanywa hivi ili watu waje na kumsalimia na kumpa zawadi ambazo ali- paswa kuzikubali.
Imam (as) alimuambia Mansur, “Nawruz ni Eid ya kimila ya Wairan haku- na kilichotajwa juu yake katika Uislam”
Juu ya hili Mansur alijibu “kitendo hiki kina hamasa za kisiasa na inakusudiwa kuwafurahisha askari wangu. Ninakuweka chini ya Mola mkuu kuwa ukubali ombi langu na uhudhurie katika mkusanyiko huo.” Imam (as) alikubali na akawasili katika hadhara ya Majenerari wa jeshi, Mamwinyi na watu wa kawaida walipita mbele yake wakamsalimia na kumpa zawadi zao.
Wakati huo huo Mansur alikuwa amemuamuru mmoja wa watumwa wake akae karibu na Imam akitunza kumbukumbu ya fedha na zawadi zina- zowasilishwa kwake.
Mtu wa mwisho kuja kumuona Imam (as) alikuwa ni mzee aliyemuambia: “Ewe mtoto wa Mjumbe wa Allah! Mimi ni mtu masikini na sina fedha za kukununulia zawadi, lakini zawadi yangu kwa leo ni aya tatu za shairi la maombolezo, ambazo babu yangu amezitunga kwa ajili ya babu yako, Husein Ibn Ali (as).” Baada ya kusema hayo akasoma aya hizo.
Imam (as) alishukuru kwa kusema; “Nimeikubali zawadi yako” kisha akamsomea dua mtu huyo. Kisha akamgeukua mtumwa na kumuagiza “Nenda kwa Mansur mjulishe juu ya zawadi hizi na muulize zifanyweje.” Mtumwa alifanya kama alivyoagizwa na aliporudi, alimuambia Imam (as): “Khalifa amesema: “Nimekupa wewe (Imam Musa Kadhim) kama zawadi, zitumie utakavyo.”
Imam (as) alimuambia yule mzee: “Chukua utajiri huu na zawadi hizi, kwani ninakupatia vyote hivi kama zawadi.”5
4. YUSUF (AS) NA NDUGUZE
Miaka kadhaa baada ya tukio la nduguze Yusuf (as) kumchukuwa kwa udanganyifu nje ya mji. Kumpiga na kumtupa kisimani na hivyo kumlaz- imisha baba yao kulia mfulululizo na kusonononeka kwa hasara yake, wale ndugu walisikia kuwa Yusuf amekuwa Mfalme wa Misir. Wao na baba yao walienda kuonana naye.
Sentensi ya kwanza kabisa ambayo Yusuf aliitamka alipowaona, ilikuwa:
“Na kwa hakika alikuwa mwema kwangu aliponitoa gerezani…”6
Inavyooneka ni kwa sababu ya tabia njema kwamba Yusuf aliepuka kutaja matatizo aliyoyapata; kwanza kutupwa kisimani, kisha kufanywa kwake mtumwa na kisha matukio yasiyofurahisha, aliyokumbana nayo kutokana na matendo ya nduguze. Hakutaka kufufua kumbukumbu hizo chungu, ambazo zingewasababishia fedheha na mfadhaiko.
Kisha aliongeza, “Ni shetani aliyewashawishi ndugu zangu kunifanyia yale matendo yasiyofaa, kunitupa kisimani na kunitenganisha na baba yangu; hata hivyo Mwenyezi Mungu Mtukufu alinifanyia wema kwani aliyafanya matendo hayo kuwa ni njia ya kuipatia familia yetu utukufu na heshima!”
Kuyahusisha matendo ya kidhalimu na nduguze na shetani na kumuona yeye (shetani) kama mhusika mkuu wa uhalifu wa nduguze, ulikuwa ni mfano mwingine wa ukarimu na moyo wa kusamehe wa Yusuf. Hivyo ali- wakinga dhidi ya mfadhaiko na akawaacha na fursa ya kuomba msamaha kwa matendo yao.
Alisema:
لَا تَثْرِيبَ عَلَيْكُمُ الْيَوْمَ ۖ {92}
“Hakutakuwa lawama dhidi yenu (kuanzia) siku hii (Quran 12:92)
Kaeni kwa amani juu yangu, kwani nimewasamehe na nimeyasahau yote yaliyotokea, na kwa niaba ya Mwenyezi Mungu pia, ninaweza kuwapeni habari njema na tafuteni kutoka kwake ili Allah awasamehe na Yeye ni Mwenye rehema kuliko wenye rehema wote.7
إنَّهُ مَنْ يَتَّقِ وَيَصْبِرْ فَإِنَّ اللَّهَ لَا يُضِيعُ أَجْرَ الْمُحْسِنِين
{90}
“Kwa hakika yule ajichungaye (dhidi ya maovu) na akawa na subira (hulipwa) kwani kwa hakika Allah huwa hapotezi ujira wa wafanyao wema.” (Qur’an 12:90)
Neno la mtunzi: Somo ambalo Hadhrat Yusuf (as) alimfundisha kila mmoja ni lile la kuonyesha wema na ukarimu kama majibu ya tabia mbaya, na tunataraji sisi pia tunaweza kufanya hivyo kwa ndugu zetu katika Iman, Inshaallah!
•    1. Qur’ani Tukufu Suratu’l-Nahl 16:128
•    2. Jawaame al–Hikayaat, uk. 24, Namunah- e ma’arif, Juz. 1, uk. 29
•    3. Raahinama –e- Sa’adat, Juz. 1 uk, 36; Shajarah-e-Tuba, uk 422
•    4. Payghambar Wa yaraan, Juz. 1, uk. 20-27; Bihaar al –Answaar, Juz. 6, uk. 554
•    5. Muntahal Aamal, Juz, 2 uk.187
•    6. Qur’ani Tukufu Suratul Yusuf 12:100
•    7. Qur’ani Suratul Yusuf 12:92
ITAENDELEA KATIKA MAKALA IAJAYO

Toa maoni yako

Maoni ya watumiaji

Hakuna maoni
*
*

Site ya Al-Imaamaini Al-Hassanaini (A.S) ya usambazaji wa utamaduni wa Kiislamu na mafunzo ya Kidini