Site ya Al-Imaamaini Al-Hassanaini (A.S) ya usambazaji wa utamaduni wa Kiislamu na mafunzo ya Kidini

WANAZUONI NI WARITHI WA MITUME

1 Voti 01.0 / 5

WANAZUONI NI WARITHI WA MITUME:"

HADITHI HII INA WAHUSU WANAZUONI WA AHLUBAITI RASUL AS PEKEE AMBAO NI MA'ASUMU

بحث "العلماء ورثة الانبياء"

Utafiti kuhusu hadithi ya Wanazuoni ni warithi wa Mitume".

قال سبحانه ((إنما يخشى الله من عباده العلماء))

Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: Hakika Wanaomuogopa Mwenyezi Mungu zaidi katika waja wake ni Wanazuoni.

فمن الواضح انه ليس كلما ذكرت الروايات كلمة ( العلماء ) فالمقصود بها عامة العلماء بل أكثر الروايات التي تتطرق إلى مدح العلماء وعلو منزلتهم وأنهم أفضل البشر بعد الأنبياء، فالمقصود من هكذا روايات هم علماء آل محمد وهم الأئمة المعصومين (ع) وهم الراسخون في العلم المذكورين في الاية (لَكِنِ الرَّاسِخُونَ فِي الْعِلْمِ مِنْهُمْ وَالْمُؤْمِنُونَ يُؤْمِنُونَ بِمَا أُنْزِلَ إِلَيْكَ وَمَا أُنْزِلَ مِنْ قَبْلِكَ وَالْمُقِيمِينَ الصَّلاةَ وَالْمُؤْتُونَ الزَّكَاةَ وَالْمُؤْمِنُونَ بِاللَّهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ أُولَئِكَ سَنُؤْتِيهِمْ أَجْراً عَظِيماً) (النساء:162

Kwa uwazi kabisa siyo kila linapotajwa neno" "Wanazuoni" basi makusudio yake eti ni kwa Wanazuoni wote, (Hapana) Bali riwaya nyingi ambazo zinapelekea kuwasifu Wanazuoni na daraja lao la juu na hakika wao wanakuwa ni wabora wa viumbe baada ya Mitume, makusudio ya riwaya hizo ni Wanazuoni wa Kizazi cha Mtukufu Mtume Muhammad saww na hao ndiyo Maimamu watakatifu waliohifadhiwa as na wao ndiyo hasa wanaitwa waliozama katika elimu waliotajwa katika Qur-ani Tukufu:

Lakini waliozama katika elimu miongoni mwao na Walioamini yale yaliyoteremshwa kwako na yaliyoteremshwa kabla yako wenye kudumu na kuswali wenye kutoa zaka na wanaomuamini Mwenyezi Mungu na siku ya Kiyamah, hao tutawalipa malipo makubwa.4:162

ومن البديهي انه لا يعقل أن يكون فقيه غير معصوم قابل للخطأ والانحراف أفضل من نبي من أنبياء بني إسرائيل (ع) كنبي الله موسى (ع) أو نبي الله عيسى (ع) روح الله ، فمهما بلغ الإنسان من الكمال دون العصمة لا يفضل على الذي يمتلك

Kwa ujumla haiwezi kuingia akilini kuwa mwanazuoni asiyekuwa Ma'asumu anayefanya madhambi na kugeuza mambo ya haramu kuwa ya halali eti awe mbora zaidi ya Mtume miongoni mwa Mitume wa Bani Israel as kama vile Nabii wa Mwenyezi Mungu Musa as au Nabii wa Mwenyezi Mungu Isa as Roho ya Mwenyezi Mungu, vyovyote vile Mwanadamu atakavyoufikia ukamilifu hawezi kumzidi yule ambaye anaumiliki ubora huo (kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.

وعن الصادق (ع) ( إن علياً كان عالماً وإن العلم يتوارث و لن يهلك عالم إلا بقي من بعده من يعلم مثل علمه أوما شاء الله )) الكافي ج : 1 ص248.

Kutoka kwa Imamu Ja'afar Swadiq as anasema: Hakika Ally Bin Abi Twalib as alikuwa ni mwanazuoni (mkubwa) na Hakika elimu hurithiwa na katu hatoangamia mwanazuoni isipokuwa atakuwa amebaki baada yake anayejua mfano wake au kwa namna atakavyo Mwenyezi Mungu Mtukufu.

ومعنى الحديث إن الإمام علي (ع) هو وارث رسول الله وذريته من بعده هم العلماء يرث بعضهم الأخر (ع) حتى انتهت الوراثة إلى مولانا صاحب العصر والزمان الإمام الحجة بن الحسن (مكن الله له في الأرض) فهو وارث الأنبياء والمرسلين (ع) لا فلان ولا اشباهم كما يدعون.

 

Maana ya hadithi hii ni kwamba: Hakika Imamu Ally as ndiye mrithi wa Mtukufu Mtume Muhammad saww, na kizazi chake kitukufu kilicho kuja baada yake wao ndiyo Wanazuoni waliorithi baadhi yao kuwarithi wengine hadi urithi huo ukakomea kwa Maulana Swahibu Zamani Imamu Hujja wa Mwenyezi Mungu Muhammad bin Hassani (Mwenyezi Mungu ampe umakini katika dunia) yeye ndiye mrithi wa Mitume Ambiyaa na Mitume mursalina as, siyo fulani wala mfano wao kama watu wengi wanavyodai.

 

ومن كلام للإمام الرضا ع مع أحد أصحابه نأخذ منه مقدار الحاجة (( ... أفتدري من السفهاء؟ فقلت : لا يا ابن رسول الله . فقال: هم قصاص من مخالفينا و تدري من العلماء؟ فقلت :لا يا ابن رسول الله. قال: فقال: هم علماء آل محمد (ع) الذين فرض الله عز و جل طاعتهم و أوجب مودتهم))) ... )) معاني الأخبار ص 180)).

Na katika maneno ya Imamu Ally Ridhaa as akiwa pamoja na mmoja wa Maswahaba wake tuchukue maneno Sehemu tu kwa kadir ya mahitaji.

.....Swahaba wa Imamu Ridhaa anasema niliulizwa swali na Imamu Ally Ridhaa as akasema Je unawajua wapumbavu? Swahaba akasema nikasema: Hapana Ewe mtoto wa Mtukufu Mtume saww,. Imamu Ally Ridhaa as akasema: Ni wale wanaolipiza kisasi katika watu wanaotupinga. Imamu Ally Ridhaa as akasema:  Je unawajua Wanazuoni? Swahaba akasema nikasema: Hapana Ewe mtoto wa Mtukufu Mtume saww. Imamu Ally Ridhaa as akasema: Wanazuoni ni kizazi cha Mtukufu Mtume Muhammad saww ambao Mwenyezi Mungu Mtukufu amefaradhisha kuwatii wao na akawajibisha kuwapenda.

 

REJEA:

  1. Alkaafiy Jz 1 UK 248
  2. Maanil Akhbari UK 180

Vilevile ukisoma vitabu hivi hapa chini utapata ufafanuzi zaidi

عن المحقق الخوئي في مصباح الفقاهة ج3 ص289 ،

Miswubahul Fiqaahat Jz 3 UK 289

وقال أيضاً في كتاب الصوم ج2 :

Kitabu saumu Jz 2

 

وعن محمد سعيد الحكيم في كتابه مصباح المنهاج -التقليد-ص199

Kitabu Maswabihul Minhajit Taqlid UK 199

 

وعن السيد أحمد الخونساري في كتابه منية الطالب ج2ص232 -

Kitabu Miswubahul Maniyat Twalib Jz 2 UK 232

الشيخ محمد حسين الأصفهاني في حاشيته على المكاسب ج2 ص385

Katika Hashiyatu Alal Makasibi Jz 2 UK 385

Toa maoni yako

Maoni ya watumiaji

Hakuna maoni
*
*

Site ya Al-Imaamaini Al-Hassanaini (A.S) ya usambazaji wa utamaduni wa Kiislamu na mafunzo ya Kidini